30.01.2013 Views

Maelezo zaidi - Kilimoznz.or.tz

Maelezo zaidi - Kilimoznz.or.tz

Maelezo zaidi - Kilimoznz.or.tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

UZINDUZI WA KILIMO CHA MPUNGA KWA MSIMU<br />

WA MWAKA 2011/2012 CHEJU<br />

Mpunga ni miongoni mwa mazao yanayolimwa sana hapa visiwani, mpunga ukiwa tayari shamban,<br />

huvunwa, huanikwa, hupigwa/hupukuchuliwa, hupetwa na kukubolewa ili kupatikana mchele ambao<br />

tumika kwa mapishi ya vyakula aina mbali mbali kama vile wali, pilau, biriani, mikate na chila. Wakaazi<br />

wengi wa visiwa vya Unguja na Pemba hupoendelea kula wali ambao unatokana na mpunga.<br />

Licha ya kua na mazao mengi ya kibiashara pamoja na chakula lakini moja ya chakula ambacho<br />

kinawavutia wakaazi wengi wa visiwa hivi ni wali.<br />

Wakulima wa visiwa vya Unguja na Pemba wanajishughulisha na kilimo cha mpunga kwa miaka mingi kwa<br />

lengo la kujipatia chakula chao, ni dhana ambayo ilijengeka miongoni mwa wakulima wengi<br />

waliojishughulisha na kilimo hicho.<br />

Katika kukiinua kilimo hicho cha mpunga Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeamua kufanya mabadiliko<br />

makubwa kwa kukifanya kilimo cha mpunga<br />

kiwe cha kibiashara kwa kuwaekea<br />

miiundombinu b<strong>or</strong>a katika maeneo ya<br />

uzalishaji, kutoa ruzuku kwa pembejeo<br />

muhimu za kilimo na kuwapatia wakulima<br />

taaluma b<strong>or</strong>a za uzalishaji ili kufikia lengo<br />

lililokusudiwa.<br />

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza<br />

la Mapinduzi Mhe. Dr. ALI MOHAMMED<br />

SHEIN aliyabainisha hayo huko Cheju,<br />

Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja<br />

wakati wa uzinduzi wa msimu wa mpunga<br />

kwa mwaka 2011‐2012.<br />

Shughuli ambayo ilihudhuriwa na viongozi<br />

wengine wa Serikali wakiwemo Wakuu wa<br />

Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Waziri wa<br />

Miudombinu, Kaimu Waziri wa Kilimo,<br />

Katibu Mkuu, Manaibu Katibu Mkuu,<br />

Wakurugenzi na maafisa kutoka Wizara ya<br />

Kilimo pamoja na wakulima mbalimbali wa


kilimo cha Mpunga.<br />

Amesema kuwa Serikali imeamua kufanya mabadiliko ya kilimo hicho kuwa cha kibiashara kutokana na<br />

matumizi b<strong>or</strong>a ya nyenzo za kilimo zitakazotumiwa na wakulima wake.<br />

Amafahamisha kua kilimo ndio njia pekee ya kuwapatia wananchi chakula cha uhakika pia ndio jambo<br />

ambalo Ulimwengu mzima hivi sasa unalitilia mkazo, hivyo hatuna budi kuongeza nguvu <strong>zaidi</strong> katika kilimo<br />

chetu ili tuweze kulima kwa tija na kilimo chetu kiwe cha kisasa.<br />

Amesema kupitia Shirika la Chakula Duniani (FAO) pamoja na mashirika mengine ya maendeleo likiwemo<br />

IFAD yanaendelea kuzishajiisha nchi zote duniani ziweze kuzalisha mazao ya chakula kwa wingi na<br />

kujitosheleza kwa chakula.<br />

Dr. Shein alieleza kua hali ya dunia hivi sasa imebadilika kutokana na matatizo ya kiuchumi jambo ambalo<br />

linasababisha kupanda kwa bei za vyakula mara kwa mara na kufanya hali ya thamani ya fedha<br />

kutotabirika.<br />

Dr. Shein alisema kua matarajio ya Serikali ni kukibadilisha kilimo cha mpunga na kulifanya bonde la<br />

mpunga la Cheju kuwa la kisasa katika kilimo cha mpunga kwa kuzilima hekta zote 3000 zilizopo ili liweze<br />

kuchangia upatikanaji wa chakula kwa Zanzibar yote. Hali ambayo itaweza kulibadilisha bonde hilo na<br />

kuwa tofauti na ile ya zamani.<br />

Amefahamisha kua kutokana na hatua hiyo lengo na matarajio kwa msimu wa 2011/1212 ni kupata tani<br />

5000 za mpunga katika bonde hilo linaweza kufikiwa kutokana na juhudi zinazochukuliwa na Serikali<br />

kupitia Wizara ya Kilimo na Maliasili kwani mipango yote ya kuwapatia wakulima wake huduma b<strong>or</strong>a za<br />

kilimo imeshapangwa.<br />

Dr Shein amewataka wakulima wa bonde la Cheju kupanda mbegu ya aina moja ili iwe rahisi wakati wa<br />

mavuno sambamba na utumiaji wa mbegu b<strong>or</strong>a, mbolea na taaluma b<strong>or</strong>a za uzalishaji.<br />

Pamoja na uzinduzi huo Dr. Shein alitoa pongezi za dhati kutokana na juhudi kubwa zilizochukuliwa na<br />

mafundi wa matrekta wa Unguja na Pemba za kufanya matengenezo kwa wakati. Jumla ya matrekta 21<br />

yalifanyiwa matengenezo yakiwemo 14 Unguja na 7 Pemba.<br />

DR. Shein pia alivipongeza vikundi vya wakulima vya bonde la Cheju kwa kuchangia asilimia 80 ya gharama<br />

na kupelekea kuanza kulimiwa katika bonde lao kwa wakati.


Akielezea juu ya mikakati iliopo ya barabara ya Jendele‐Cheju‐Unguja ukuu kaibona, Waziri wa<br />

Miundombinu na Mawasliano Mhe. Hamad Masoud alieleza kua utaratibu wa ujenzi huo unafanyiwa kazi<br />

na hivi karibuni watapatikana makandarasi wa kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami.<br />

Nae Kaimu Waziri wa Kilimo na Maliasili Mhe. Ramadhan Abdalla Shaaban aliwataka wakulima wa bonde<br />

hilo kuiunga mkono Wizara ya Kilimo na Maliasili kutokana na jitihada zake inazozichukua katika kuwasidia<br />

wakulima hao.<br />

Akitoa ufafanuzi juu ya maendeleo ya kilimo kwa msimu huu Naibu Katibu Mkuu (Kilimo) ndugu Juma Ali<br />

Juma alisema kuwa wizara imeshafanya maandalizi ya kuagiza mbegu ya kutosha kutoka Tanzania Bara<br />

kwa msimu huu kwa ajili ya kugaiwa kwa wakulima kwa sasa tayari imeshanunua tani 141 za mbegu<br />

sambamba na kufanya maandalizi ya mbegu ya NERICA.<br />

Amaefahamisha kua kwa mwaka ujao 2012 eneo lote la bonde hilo litakua la kilimo cha umwagiliaji maji<br />

ambapo tayari wataaalamu kutoka K<strong>or</strong>ea washawasili.<br />

Nd. Juma amesema kua<br />

katika kukiimarisha kilmo<br />

hicho Wizara imeamua<br />

shughuli zote za kilimo<br />

zitasimamiwa na wakulima<br />

wakulima wenyewe kupitia<br />

Jumuiya zao. Jumla ya vituo<br />

20 vimetegwa Unguja na<br />

Pemba. Aliendelea kueleza<br />

kuwa Wizara imesamua<br />

kuliteua bonde la cheju kuwa<br />

eneo tengefu la mbegu ili<br />

liweze kuleta tija na manufaa<br />

kwa Taifa.<br />

Nao wakulima wa Zanzibar<br />

katika risala yao walieleza<br />

kufarijika kwao na<br />

kumpongeza Dr.Shein<br />

kutokana na jitihada anazozichukua katika kukipa kipaumbele kilimo cha mpunga na kuweza kushiriki<br />

katika shughuli mbalimbali za kilimo.<br />

Aidha walitoa pongezi kutokana na bajeti ya Wizara ya Kilimo ya mwaka 2011/2012 ilivyowaona wakulima<br />

kwa kuwapatia ruzuku ya pembejeo kwa asilimia 50.<br />

Wakieleza changamoto zinazowakabili katika ukulima wa mpunga ni pamoja na tatizo la ujenzi kwenye<br />

mabonde ya mpunga na wanaiomba Serikali kufuatilia kwa kina suala hilo ikiwa ni pamoja na kutunga<br />

sheria itakoyozuia ujenzi katika mabonde ya mpunga.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!