Maelezo zaidi - Kilimoznz.or.tz
Maelezo zaidi - Kilimoznz.or.tz
Maelezo zaidi - Kilimoznz.or.tz
- TAGS
- maelezo
- zaidi
- kilimoznz.or.tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
UZINDUZI WA KILIMO CHA MPUNGA KWA MSIMU<br />
WA MWAKA 2011/2012 CHEJU<br />
Mpunga ni miongoni mwa mazao yanayolimwa sana hapa visiwani, mpunga ukiwa tayari shamban,<br />
huvunwa, huanikwa, hupigwa/hupukuchuliwa, hupetwa na kukubolewa ili kupatikana mchele ambao<br />
tumika kwa mapishi ya vyakula aina mbali mbali kama vile wali, pilau, biriani, mikate na chila. Wakaazi<br />
wengi wa visiwa vya Unguja na Pemba hupoendelea kula wali ambao unatokana na mpunga.<br />
Licha ya kua na mazao mengi ya kibiashara pamoja na chakula lakini moja ya chakula ambacho<br />
kinawavutia wakaazi wengi wa visiwa hivi ni wali.<br />
Wakulima wa visiwa vya Unguja na Pemba wanajishughulisha na kilimo cha mpunga kwa miaka mingi kwa<br />
lengo la kujipatia chakula chao, ni dhana ambayo ilijengeka miongoni mwa wakulima wengi<br />
waliojishughulisha na kilimo hicho.<br />
Katika kukiinua kilimo hicho cha mpunga Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeamua kufanya mabadiliko<br />
makubwa kwa kukifanya kilimo cha mpunga<br />
kiwe cha kibiashara kwa kuwaekea<br />
miiundombinu b<strong>or</strong>a katika maeneo ya<br />
uzalishaji, kutoa ruzuku kwa pembejeo<br />
muhimu za kilimo na kuwapatia wakulima<br />
taaluma b<strong>or</strong>a za uzalishaji ili kufikia lengo<br />
lililokusudiwa.<br />
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza<br />
la Mapinduzi Mhe. Dr. ALI MOHAMMED<br />
SHEIN aliyabainisha hayo huko Cheju,<br />
Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja<br />
wakati wa uzinduzi wa msimu wa mpunga<br />
kwa mwaka 2011‐2012.<br />
Shughuli ambayo ilihudhuriwa na viongozi<br />
wengine wa Serikali wakiwemo Wakuu wa<br />
Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Waziri wa<br />
Miudombinu, Kaimu Waziri wa Kilimo,<br />
Katibu Mkuu, Manaibu Katibu Mkuu,<br />
Wakurugenzi na maafisa kutoka Wizara ya<br />
Kilimo pamoja na wakulima mbalimbali wa
kilimo cha Mpunga.<br />
Amesema kuwa Serikali imeamua kufanya mabadiliko ya kilimo hicho kuwa cha kibiashara kutokana na<br />
matumizi b<strong>or</strong>a ya nyenzo za kilimo zitakazotumiwa na wakulima wake.<br />
Amafahamisha kua kilimo ndio njia pekee ya kuwapatia wananchi chakula cha uhakika pia ndio jambo<br />
ambalo Ulimwengu mzima hivi sasa unalitilia mkazo, hivyo hatuna budi kuongeza nguvu <strong>zaidi</strong> katika kilimo<br />
chetu ili tuweze kulima kwa tija na kilimo chetu kiwe cha kisasa.<br />
Amesema kupitia Shirika la Chakula Duniani (FAO) pamoja na mashirika mengine ya maendeleo likiwemo<br />
IFAD yanaendelea kuzishajiisha nchi zote duniani ziweze kuzalisha mazao ya chakula kwa wingi na<br />
kujitosheleza kwa chakula.<br />
Dr. Shein alieleza kua hali ya dunia hivi sasa imebadilika kutokana na matatizo ya kiuchumi jambo ambalo<br />
linasababisha kupanda kwa bei za vyakula mara kwa mara na kufanya hali ya thamani ya fedha<br />
kutotabirika.<br />
Dr. Shein alisema kua matarajio ya Serikali ni kukibadilisha kilimo cha mpunga na kulifanya bonde la<br />
mpunga la Cheju kuwa la kisasa katika kilimo cha mpunga kwa kuzilima hekta zote 3000 zilizopo ili liweze<br />
kuchangia upatikanaji wa chakula kwa Zanzibar yote. Hali ambayo itaweza kulibadilisha bonde hilo na<br />
kuwa tofauti na ile ya zamani.<br />
Amefahamisha kua kutokana na hatua hiyo lengo na matarajio kwa msimu wa 2011/1212 ni kupata tani<br />
5000 za mpunga katika bonde hilo linaweza kufikiwa kutokana na juhudi zinazochukuliwa na Serikali<br />
kupitia Wizara ya Kilimo na Maliasili kwani mipango yote ya kuwapatia wakulima wake huduma b<strong>or</strong>a za<br />
kilimo imeshapangwa.<br />
Dr Shein amewataka wakulima wa bonde la Cheju kupanda mbegu ya aina moja ili iwe rahisi wakati wa<br />
mavuno sambamba na utumiaji wa mbegu b<strong>or</strong>a, mbolea na taaluma b<strong>or</strong>a za uzalishaji.<br />
Pamoja na uzinduzi huo Dr. Shein alitoa pongezi za dhati kutokana na juhudi kubwa zilizochukuliwa na<br />
mafundi wa matrekta wa Unguja na Pemba za kufanya matengenezo kwa wakati. Jumla ya matrekta 21<br />
yalifanyiwa matengenezo yakiwemo 14 Unguja na 7 Pemba.<br />
DR. Shein pia alivipongeza vikundi vya wakulima vya bonde la Cheju kwa kuchangia asilimia 80 ya gharama<br />
na kupelekea kuanza kulimiwa katika bonde lao kwa wakati.
Akielezea juu ya mikakati iliopo ya barabara ya Jendele‐Cheju‐Unguja ukuu kaibona, Waziri wa<br />
Miundombinu na Mawasliano Mhe. Hamad Masoud alieleza kua utaratibu wa ujenzi huo unafanyiwa kazi<br />
na hivi karibuni watapatikana makandarasi wa kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami.<br />
Nae Kaimu Waziri wa Kilimo na Maliasili Mhe. Ramadhan Abdalla Shaaban aliwataka wakulima wa bonde<br />
hilo kuiunga mkono Wizara ya Kilimo na Maliasili kutokana na jitihada zake inazozichukua katika kuwasidia<br />
wakulima hao.<br />
Akitoa ufafanuzi juu ya maendeleo ya kilimo kwa msimu huu Naibu Katibu Mkuu (Kilimo) ndugu Juma Ali<br />
Juma alisema kuwa wizara imeshafanya maandalizi ya kuagiza mbegu ya kutosha kutoka Tanzania Bara<br />
kwa msimu huu kwa ajili ya kugaiwa kwa wakulima kwa sasa tayari imeshanunua tani 141 za mbegu<br />
sambamba na kufanya maandalizi ya mbegu ya NERICA.<br />
Amaefahamisha kua kwa mwaka ujao 2012 eneo lote la bonde hilo litakua la kilimo cha umwagiliaji maji<br />
ambapo tayari wataaalamu kutoka K<strong>or</strong>ea washawasili.<br />
Nd. Juma amesema kua<br />
katika kukiimarisha kilmo<br />
hicho Wizara imeamua<br />
shughuli zote za kilimo<br />
zitasimamiwa na wakulima<br />
wakulima wenyewe kupitia<br />
Jumuiya zao. Jumla ya vituo<br />
20 vimetegwa Unguja na<br />
Pemba. Aliendelea kueleza<br />
kuwa Wizara imesamua<br />
kuliteua bonde la cheju kuwa<br />
eneo tengefu la mbegu ili<br />
liweze kuleta tija na manufaa<br />
kwa Taifa.<br />
Nao wakulima wa Zanzibar<br />
katika risala yao walieleza<br />
kufarijika kwao na<br />
kumpongeza Dr.Shein<br />
kutokana na jitihada anazozichukua katika kukipa kipaumbele kilimo cha mpunga na kuweza kushiriki<br />
katika shughuli mbalimbali za kilimo.<br />
Aidha walitoa pongezi kutokana na bajeti ya Wizara ya Kilimo ya mwaka 2011/2012 ilivyowaona wakulima<br />
kwa kuwapatia ruzuku ya pembejeo kwa asilimia 50.<br />
Wakieleza changamoto zinazowakabili katika ukulima wa mpunga ni pamoja na tatizo la ujenzi kwenye<br />
mabonde ya mpunga na wanaiomba Serikali kufuatilia kwa kina suala hilo ikiwa ni pamoja na kutunga<br />
sheria itakoyozuia ujenzi katika mabonde ya mpunga.