20.01.2013 Views

Uk. 4 Uk. 18 Uk. 14 - MVIWATA

Uk. 4 Uk. 18 Uk. 14 - MVIWATA

Uk. 4 Uk. 18 Uk. 14 - MVIWATA

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

<strong>Uk</strong>. 4<br />

Toleo NO. 039 Julai –Septemba 2011 Bei Shs. 500/= ISSN 0856-5937<br />

Wakulima wapongeza <strong>MVIWATA</strong> kwa<br />

kuhabarisha wakazi wa vijijini<br />

<strong>Uk</strong>. <strong>14</strong><br />

Maonesho ya NaneNane 2011<br />

<strong>Uk</strong>. <strong>18</strong><br />

Kijana mbunifu atengeneza mitambo ya radio<br />

kunufaisha wanakijiji


Toleo NO. 039<br />

Julai Septemba 2011<br />

Bei Shs. 500/=<br />

ISSN 0856-5937<br />

WAHARIRI<br />

Susuma Msikula Susuma<br />

Stephen Ruvuga<br />

BODI YA <strong>MVIWATA</strong><br />

Mwenyekiti – Yazid Makame<br />

Makamu Mwenyekiti – Lydia Ruliho<br />

Katibu - Stephen Ruvuga-<br />

(Mkurugenzi Mtendaji)<br />

Mweka Hazina - Grace Runkulatile<br />

WAJUMBE<br />

Cosma Bulu<br />

Sylvester Yatuba<br />

Joseph Kilowoko<br />

Samweli Maseke<br />

Julius Mbago<br />

Habibu Simbamkuti<br />

MSHAURI WA <strong>MVIWATA</strong><br />

Prof. Amon Mattee<br />

LINATOLEWA NA<br />

KUSAMBAZWA NA<br />

Mtandao wa Vikundi vya<br />

Wakulima Tanzania (<strong>MVIWATA</strong>)<br />

S.L.P 3220 Morogoro, Tanzania<br />

Simu: 023 261 41 84<br />

Faksi: 023 261 41 84<br />

Barua pepe: info@mviwata.org,<br />

mviwata@morogoro.net<br />

Tovuti: www.mviwata.org<br />

MICHORO<br />

Godwin Chipenya<br />

USANIFU NA<br />

UCHAPISHAJI<br />

PENplus Ltd – 022 2<strong>18</strong>2059<br />

<strong>Uk</strong>. 4<br />

Toleo NO. 039 Julai –Septemba 2011 Bei Shs. 500/= ISSN 0856-5937<br />

Wakulima wapongeza <strong>MVIWATA</strong> kwa<br />

kuhabarisha wakazi wa vijijini<br />

<strong>Uk</strong>. <strong>14</strong><br />

Maonesho ya NaneNane 2011<br />

<strong>Uk</strong>. <strong>18</strong><br />

Kijana mbunifu atengeneza mitambo ya radio<br />

kunufaisha wanakijiji<br />

Picha ya Jalada:<br />

Bw. Benjamini Nziku mkulima wa<br />

kijiji cha Lusala kata ya Lupanga<br />

wilayani Ludewa akipata habari<br />

kupitia gazeti la wakulima la<br />

Pambazuko. b<br />

Tahariri<br />

Habari za vijijini zipewe<br />

kipaumbele<br />

Ingawa juhudi na mchango wa jamii za vijijini nchini Tanzania<br />

ndiyo vinavyoiendeleza Taifa, habari za vijijini haziandikwi kwa<br />

umuhimu huo.<br />

Mara nyingi, habari za vijijini zinazopewa nafasi kwenye<br />

vyombo vya habari ni zinazohusu maafa, kesi, vimbwanga na hotuba<br />

za viongozi wanapotembelea maeneo hayo.<br />

Wanahabari wanafanya kazi kubwa ya kuuelimisha umma, hata<br />

hivyo kwa sehemu kubwa habari hizo zimekuwa ni zile zinazohusu<br />

watu wa mijini.<br />

Toleo hili linalozungumzia habari za vijijini ni sehemu ya<br />

utekelezaji wa ajenda ya upashanaji habari inayotekelezwa na<br />

<strong>MVIWATA</strong> kwa muda mrefu sasa.<br />

Tunafahamu kwamba pamoja haya umuhimu wa upatikanaji wa<br />

habari kwa watu wa vijijini, ziko changamoto kadhaa zinazokwamisha<br />

ufanisi wake.<br />

Miongoni mwa changamoto hizo ni ukosefu wa vitendea<br />

kazi ikiwemo usafiri, kamera na vinasa sauti ambapo hata<br />

waandishi wachache wenye nia ya kwenda kukusanya habari vijijini<br />

wameshindwa kufanya hivyo kwa kukosa usafiri na wengine kuishia<br />

kutegemea usafiri wa viongozi wanapotembelea maeneo ya vijijini.<br />

Kulingana na kubanwa na ratiba za viongozi hao, waandishi hawawezi<br />

kukusanya habari nzuri zenye kuchochea maendeleo ya vijijini zaidi<br />

ya kuishia kuandika hotuba na maagizo ya viongozi.<br />

Changamoto nyingine ni ya waandishi wa habari kukosa<br />

taaluma ya kutosha yenye kuwawezesha kudadisi na kuibua kero na<br />

changamoto halisia za vijijini na siyo vimbwanga.<br />

Tunaamini ziko changamoto nyingi na lengo letu siyo kuziainisha<br />

zote isipokuwa tunawakumbusha wadau wa sekta ya habari kuwa<br />

vijijini ndiko kwenye chimbuko la wazalishaji na kwamba hatupaswi<br />

kuwatenga.<br />

Tunashauri kuwepo na jitihada za makusudi za kutatua<br />

changamoto hizi na vilevile kuwe na juhudi za kuhimiza vyombo<br />

vya habari kuzipa kipaumbele habari za vijijini. Ni wakati muafaka<br />

ambapo<br />

Tunawakumbusha wana habari juu ya umuhimu wa kuzingatia<br />

maadili ya taaluma ya uandishi wa habari kwa kuandika habari<br />

zilizofanyiwa utafiti wa kina na kuhakikisha jamii zote vijijini na<br />

mijini wananufaika na huduma hii muhimu.<br />

Tusaidie kuchochea maendeleo vijijini kwa kuhakikisha<br />

tunawapatia habari za kutosha na zilizofanyiwa utafiti.<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011


Upatikanaji wa habari vijijini,<br />

kichocheo cha maendeleo?<br />

Na Goodness Mrema, Morogoro<br />

Kutokana na kupiga hatua<br />

za kimaendeleo katika<br />

teknolojia hasa ya habari,<br />

wigo wa upatikanaji wa habari<br />

hivi sasa umepanuka ukilinganisha<br />

na miaka ya nyuma hasa wakati<br />

tunapata uhuru.<br />

Hivi sasa watu wanauwezo<br />

wa kutumia kompyuta na<br />

simu za mkononi zenye<br />

huduma ya intaneti na<br />

kuweza kupata taarifa<br />

mbalimbali zinazotokea<br />

ulimwenguni kwa wakati<br />

huo huo ama kulipia huduma<br />

mbalimbali kama vile matibabu,<br />

maji na umeme. Lakini pia wanaweza<br />

hata kufanya manunuzi ya bidhaa<br />

mbalimbali kupitia intaneti na hivyo<br />

kupunguza gharama na muda na<br />

kurahisisha biashara.<br />

Hata hivyo mbali na kukua kwa<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />

teknolojia ya habari, nchi za Kusini<br />

mwa Afrika bado zinakabiliwa na<br />

tatizo kubwa la kukosekana kwa<br />

habari za umma hasa kwenye maeneo<br />

ya vijijini ambazo ni muhimu kwa<br />

wananchi kutoa maamuzi mbalimbali<br />

ambayo ni sahihi kwa maisha yao.<br />

Hata<br />

radio za kijamii<br />

zilizoanzishwa kwa lengo<br />

la kuhudumia wakazi wa vijijini,<br />

zimeacha misingi ya kuanzishwa<br />

kwake na kuegemea zaidi<br />

kutangaza mambo ya<br />

mijini.<br />

Bado<br />

kuna changamoto zinazoikumba<br />

sekta hii ya habari ikiwemo uhaba<br />

wa upatikanaji wa habari sahihi<br />

na zenye manufaa kwa baadhi ya<br />

MADA MAALUM<br />

maeneo hasa ya vijijini. Mfumo wa<br />

upashanaji habari uliopo sasa siyo<br />

wa kuridhisha kwani haumfikii kila<br />

mwananchi wa kijijini mahali alipo.<br />

Kwa mfano magazeti yanayofika<br />

kwa nadra vijijini ndani yake yanakuwa<br />

yamejaa habari zinazohusu vuguvugu<br />

la maisha ya mjini. Habari hizo nyingi<br />

ni zile zinazohusu malumbano na<br />

siasa za chuki baina ya viongozi<br />

wa vyama, foleni za barabarani,<br />

michezo ambayo pengine mtu<br />

wa kijijini hajawahi kuiona na<br />

burudani kama vile miziki<br />

na picha kubwa kubwa za<br />

wasanii ambazo ki uhalisia<br />

hazimuongezei tija mtu wa<br />

kijijini katika harakati zake za<br />

kupambana na umasikini kupitia<br />

kilimo, ufugaji ama uvuvi.<br />

Tunashuhudia ongezeko la<br />

vyombo vya habari vya kielektroniki<br />

kama vile radio na televisheni na<br />

ukuaji wake kutoka kwenye mfumo<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 2<br />

Mwekahazina wa <strong>MVIWATA</strong> Ruvuma Bibi Immaculata John akitekeleza shughuli za <strong>MVIWATA</strong> za kusambaza habari za wakulima kwa<br />

wadau<br />

1


MADA MAALUM<br />

Upatikanaji wa habari vijijini<br />

Inatoka uk. wa 1<br />

wa analogia kwenda digitali.<br />

Ongezeko na ukuaji wa<br />

teknolojia bado hauwanufaishi<br />

vya kutosha wakazi wa vijijini.<br />

Kilichobadilika ni kuwepo kwa<br />

usikivu mzuri wa matangazo ya<br />

radio kwenye baadhi ya vijiji tofauti<br />

na ilivyokuwa awali. Habari zenye<br />

mlengo wa kuchochea maendeleo<br />

vijijini bado hazipewi kipaumbele.<br />

Hata radio za kijamii<br />

zilizoanzishwa kwa lengo la<br />

kuhudumia wakazi wa vijijini,<br />

zimeacha misingi ya kuanzishwa<br />

kwake na kuegemea zaidi kutangaza<br />

mambo ya mijini.<br />

Japokuwa televisheni na redio<br />

zinajitahidi kurusha matangazo<br />

yake na kuwafikia kwa wakati watu<br />

wa vijijini, lakini bado habari zake<br />

zinakosa mguso kwao, ingawa serikali<br />

inajinadi kuwa matumizi ya mfumo<br />

wa digitali yameongeza upatikanaji<br />

wa habari maeneo ya vijijini.<br />

Kwa ujumla habari zinazohusu<br />

mafundisho ama mafanikio ya<br />

wananchi vijijini haziandikwi wala<br />

kusikika vya kutosha na kwamba<br />

kuna haja ya kubadili mfumo<br />

ili waandishi wa habari wapate<br />

msukumo wa kuwafikia wananchi<br />

vijijini na kuandika habari zao.<br />

Siku hizi umekuja utaratibu<br />

mpya wa upashanaji habari kupitia<br />

mitandao mbalimbali ya kijamii<br />

(tovuti, blogs, facebook, twitter)<br />

ambayo kwa hakika mkulima au<br />

mfugaji mdogo anayeishi kijijini<br />

hafahamu hata jinsi ya kuitumia na<br />

wachache wenye uelewa hawawezi<br />

kuitumia kwa kukosa nishati ya<br />

umeme.<br />

Changamoto ya<br />

miundombinu<br />

Ziko sababu nyingi zinazotajwa<br />

kuchangia habari kutowafikia watu<br />

wa vijijini. Sababu mojawapo ni ubovu<br />

wa miundombinu ya barabara katika<br />

maeneo mengi ya vijijini ambako<br />

kuna asilimia 80 ya Watanzania<br />

wazalishaji wanaochangia pato la<br />

taifa.<br />

Kulingana na miundombinu<br />

duni ya barabara zetu hasa maeneo<br />

2<br />

ya vijijini, ni vigumu kwa mwananchi<br />

wa kijijini kupata gazeti kwa wakati<br />

na kulisoma.<br />

Wauzaji na wasambazaji wa<br />

magazeti ya kila siku wanajikuta<br />

wakishindwa kuyafikia maeneo hayo<br />

kwa wakati. Kwa mfano gazeti la<br />

kila siku linalosambazwa asubuhi<br />

katika maeneo ya mijini huchukua<br />

wakati mwingine siku mbili kufika<br />

eneo la Mrimba Kilombero mkoani<br />

Morogoro kutokana na barabara ya<br />

kuelekea sehemu hiyo kuwa mbaya.<br />

Huu ni mfano wa sehemu moja<br />

iliyo katika mkoa jirani na mji ambapo<br />

magazeti mengi huchapishiwa, swali<br />

ni je vipi kwa watu waishio Kigoma<br />

vijijini, Karagwe ama Murugwanza<br />

huko Ngara, wao hulipata gazeti hilo<br />

siku ngapi baada ya kuchapishwa?<br />

<strong>Uk</strong>osefu wa nishati nalo ni tatizo<br />

kubwa kwa wakazi wa maeneo ya<br />

vijijini ambalo linazuia wananchi<br />

wa vijijini kununua televisheni<br />

au radio kwa sababu ya kukosa<br />

nishati itakayowawezesha kuvitumia<br />

vyombo hivyo.<br />

Maisha magumu ya vijijini<br />

yanayosababishwa na ukosefu wa<br />

huduma muhimu za kijamii pia<br />

yanadhoofisha kasi ya upatikanaji<br />

wa habari vijijini. Kwa mfano<br />

mtu anayesumbuliwa<br />

na maradhi kwa<br />

kukosa huduma<br />

sahihi za<br />

matibabu,<br />

hawezi kukaa<br />

na kusikiliza<br />

radio huku<br />

a k i g u g u m i a<br />

kwa maumivu<br />

makali. Mtu huyu<br />

pia hawezi kutenga<br />

fedha ya kununua gazeti<br />

linalomfikia baada ya siku mbili<br />

Akina mama wengi vijijini<br />

wanakosa muda wa kusikiliza taarifa<br />

za habari ama matangazo mengine<br />

muhimu kwa kuwa muda ambao<br />

radio na televisheni zinatangaza<br />

taarifa za habari wao wanakuwa<br />

kwenye shughuli za kupika, kutafuta<br />

maji na kuni na shughuli za shamba.<br />

<strong>Uk</strong>iachana na tatizo la<br />

miundombinu duni, iko sababu<br />

nyingine ya baadhi ya wananchi kukosa<br />

mwamko wa kutafuta ama kutoa<br />

habari. Wananchi kwenye baadhi ya<br />

maeneo ya vijijini hawajaelimishwa<br />

vya kutosha juu ya umuhimu wa<br />

kutoa na kupokea habari kuhusiana<br />

na masuala mbalimbali hivyo baadhi<br />

yao kuona kwamba kununua gazeti<br />

ama kununua televisheni ni kuwa na<br />

matumizi ya anasa.<br />

Habari zinachochea<br />

maendeleo?<br />

Wakazi wa vijijini wengi wao wakiwa<br />

ni wakulima waliopata fursa ya<br />

kuzungumzia hoja hii, walikiri kuwa<br />

upatikanaji wa habari sahihi vijijini<br />

umesaidia kuchochea maendeleo,<br />

japokuwa kiwango cha upatikanaji<br />

wake siyo cha kuridhisha.<br />

Walieleza kuwa habari chache<br />

zilizowafikia ziliwasaidia kupata<br />

elimu ya kilimo bora, taarifa za<br />

upatikanaji wa pembejeo, masoko,<br />

mwelekeo wa hali ya hewa na<br />

mwenendo wa uchumi na hali ya<br />

kisiasa nchini pamoja na kufahamu<br />

jitihada za maendeleo zinazofanywa<br />

na makundi mbalimbali.<br />

Mbali na<br />

vyombo vya habari,<br />

ziko njia nyingine za asili<br />

zinazotumika kufikisha habari kwa<br />

jamii kwenye maeneo ya vijijini ikiwemo<br />

mikutano ya vijiji, kwenye nyumba<br />

za ibada na kwenye mikusanyiko<br />

kama vile sokoni na kwenye<br />

minada.<br />

Walisema habari hizo pia<br />

zinawapatia uwanja mpana wa<br />

mjadala na kubadilishana uzoefu<br />

kuhusiana na masuala mbalimbali<br />

yanayowakabili ikiwemo uwezo wa<br />

kudai haki zao za msingi. Wanafahamu<br />

mahali pa kupata mahitaji muhimu na<br />

fursa zinazopatikana kwa ajili yao na<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 3<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011


Inatoka uk. wa 2<br />

njia muafaka za kufikia suluhu kwa<br />

changamoto zinazowakabili katika<br />

shughuli zao.<br />

“Suala la upatikanaji wa habari<br />

linahusika zaidi na maisha ya kila<br />

siku ya mwananchi. Ni suala la<br />

maendeleo ya kila mwanadamu hapa<br />

ulimwenguni, endapo wananchi hawa<br />

wa vijijini watapata habari sahihi na<br />

kwa wakati zitachochea bidii katika<br />

kujiletea maendeleo,” alisema Bw<br />

Andrew Hepelwa, Katibu Mkuu<br />

Mstaafu wa <strong>MVIWATA</strong> taifa.<br />

Aliongeza kuwa maendeleo<br />

ni jambo la muhimu ambalo kila<br />

mwanadamu analitegemea katika<br />

maisha yake kuanzia ngazi ya familia<br />

hadi ngazi za kitaifa. Kama hupati<br />

taarifa kamili kuhusu kitu fulani,<br />

huwezi kujua uzito wake na huwezi<br />

kuchukua hatua za kimaendeleo na<br />

kwa upande mwingine jamii ikipata<br />

taarifa na habari sahihi inaweza<br />

kuchukua hatua ya kujikwamua<br />

katika matatizo.<br />

Matumizi ya habari<br />

Kwa ujumla jamii ya vijijini kutokana<br />

na kutengwa kwa muda mrefu na<br />

mfumo wa habari, nayo kwa namna<br />

fulani imekuwa kama imejiengua na<br />

kuyaona masuala ya habari kama<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />

siyo sehemu yao.<br />

Jamii hii inahitaji kujengewa<br />

ufahamu wa kutosha kuhusu<br />

umuhimu wa kupashana habari<br />

na matumizi sahihi ya vyombo vya<br />

habari katika kujiletea maendeleo.<br />

Vyombo vya habari katika hili vina<br />

mchango mkubwa wa kuwafumbua<br />

macho wakazi wa kijijini ili wafahamu<br />

umuhimu wa matumizi sahihi ya<br />

habari katika mchakato wa kujiletea<br />

maendeleo.<br />

Mbali na vyombo vya habari, ziko<br />

njia nyingine za asili zinazotumika<br />

kufikisha habari kwa jamii kwenye<br />

maeneo ya vijijini ikiwemo mikutano<br />

ya vijiji, kwenye nyumba za ibada<br />

na kwenye mikusanyiko kama vile<br />

sokoni na kwenye minada.<br />

Hata hivyo taarifa nyingi muhimu<br />

hutolewa katika mikutano ya vijiji,<br />

lakini kutokana na kukosa mwamko<br />

huko nako mahudhurio ni madogo<br />

na hivyo kukosesha wananchi habari<br />

muhimu.<br />

Miongoni mwa wakulima<br />

waliohojiwa wamekiri wazi kuwa<br />

hawajawahi kuhudhuria mkutano<br />

wa kijiji kwa zaidi ya miaka miwili.<br />

Hili ni tatizo na ni tabia inayopaswa<br />

kuachwa kwa sababu inadidimiza<br />

maendeleo.<br />

Miongoni mwa wakulima hao<br />

pia wamekiri mapungufu kwamba<br />

Upatikanaji wa habari sahihi unapanua wigo wa mijadala kama hii ya wakulima<br />

MADA MAALUM<br />

walipata habari lakini hawakuzitumia<br />

ipasavyo jambo ambalo wamelijutia<br />

na baadaye kujirekebisha. Kwa<br />

mfano Bw. Charles Ndugulile<br />

mkulima wa kijiji cha Mwamala Kata<br />

ya Mwamala wilaya ya Shinyanga<br />

Vijijini alisema “mwaka 2008 kupitia<br />

matangazo ya radio nilipata taarifa za<br />

kutokea mabadiliko ya tabia ambayo<br />

yatasababisha ukame na mlipuko wa<br />

wadudu lakini nilipuuzia na baadaye<br />

msimu wa kilimo uliofuata nililima<br />

shamba kubwa kama kawaida,<br />

nikapata hasara baada ya mazao<br />

kukauka kwa ukame.”<br />

Bw. Ndugulile akafafanua<br />

kwamba kutokana na hali hiyo<br />

amekuwa mhamasishaji mkubwa<br />

kwenye mkoa wa Shinyanga<br />

akiwahimiza wakulima umuhimu<br />

wa kutafuta habari na kuzitumia,<br />

lakini pia wawe wamezipata kutoka<br />

katika vyanzo vya uhakika na<br />

vinavyoaminika ila wasipotoshwe<br />

kwa kupata habari ambazo si sahihi.<br />

Hitimisho<br />

Ili kuboresha upatikanaji wa habari<br />

vijijini, serikali na wadau wa habari<br />

kwa ujumla wanapaswa kushirikiana<br />

kuondoa kasoro zilizopo na kuweka<br />

mfumo wa usawa wa utoaji taarifa<br />

na upatikanaji wa habari kwenye<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 5<br />

3


MADA MAALUM<br />

4<br />

Maoni ya wakulima na<br />

Na Goodness Mrema<br />

Changamoto kubwa<br />

inayowakabili wakulima<br />

vijijini kwa kukosa habari<br />

ni kuachwa nyuma kimaendeleo,<br />

kuibuka kwa migogoro mingi baina<br />

yao na viongozi wao ama makundi<br />

mengine katika jamii.<br />

Baadhi ya wakulima na wataalam<br />

wamekuwa na maoni tofauti<br />

kuhusiana na suala hili la upatikanaji<br />

wa habari vijijini. Wakulima kutoka<br />

mikoa mbalimbali walieleza jinsi<br />

wanavyokabiliwa na changamoto<br />

katika kupokea na kutoa habari<br />

katika maeneo mengi ya vijijini<br />

kutokana na miundombinu mibovu.<br />

Yafuatayo ni maoni waliyoyatoa<br />

wataalam<br />

baada ya kuulizwa swali lililosema<br />

hali ya upatikanaji wa habari kijijini<br />

ukoje?<br />

Bibi. Mariam Mmanga<br />

kutoka kijiji cha Kivulini wilayani<br />

Mwanga mkoani Kilimanjaro alieleza<br />

kwamba japokuwa kijijini kwake<br />

hawatembelewi na waandishi wa<br />

habari mara kwa mara wala kufikiwa<br />

na magazeti, lakini wanawake<br />

kijijini kwake wamejiunga katika<br />

vikundi wanavyovitumia kupashana<br />

habari kupitia mikutano na vikao<br />

mbalimbali na sasa wamehamasika<br />

na wanaelewa umuhimu wa kupata<br />

habari, jambo ambalo linawatia moyo<br />

na wanaimani kwamba hawataweza<br />

kubaki nyuma kwani wanafahamu na<br />

wanaelewa nini kinaendelea katika<br />

nchi yao. Hata hivyo akaongeza<br />

kuwa wanaomba kutembelewa na<br />

wanahaabari ili habari za vikundi<br />

vyao pia zitangazwe.<br />

Bibi. Mariam Hassan<br />

kutoka kijiji cha Magamba, wilayani<br />

Kibondo mkoani Kigoma anaeleza<br />

kwamba magazeti kijijini Magamba<br />

yanawafikia baada ya siku tatu ama<br />

nne, tena lazima awepo mtu ametoka<br />

mjini siku hiyo. Kwa upande wa radio<br />

wanakamata zaidi radio za Burundi<br />

na kwamba hupokea matangazo ya<br />

radio moja tu ya Tanzania ambayo<br />

nayo husikika usiku tu, jambo ambalo<br />

linawafanya washindwe kupiga hatua<br />

kimaendeleo.<br />

Ameiomba serikali kuwakumbuka<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 5<br />

Miongoni mwa machapisho yanayotolewa na <strong>MVIWATA</strong> ambayo yamewanufaisha wakulima wengi kwa kuwapata habari sahihi za kilimo<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011


Inatoka uk. wa 4<br />

na kuhakikisha kwamba nao pia<br />

wanapata huduma hii muhimu kwani<br />

wanaonekana wamesahaulika kama<br />

vile wako nje ya Tanzania kutokana<br />

na kijiji chao kuwa mpakani mwa<br />

nchi ya Burundi. “Kuhusu habari za<br />

kijijini kwetu zinaandikwa pale tu<br />

kiongozi anapokuja kututembelea<br />

ama wakati mwingine waandishi<br />

hufika kijijini hapo kunapokuwa<br />

na matukio ya maafa kama vile<br />

mauaji. Tatizo hili linatuathiri zaidi<br />

sisi wanawake kwani muda mwingi<br />

tuko ndani, afadhali wenzetu<br />

wanaume wanakutana kwenye<br />

vikao na kuhabarishana na wengine<br />

wanamiliki simu za mkononi.”<br />

Bw. Hamad Abdallah<br />

Salimin kutoka Zanzibar yeye<br />

alieleza kukerwa na waandishi wa<br />

habari wanaokurupuka na kutangaza<br />

mambo yasiyo sahihi na kuupotosha<br />

umma. Akashauri ni vyema<br />

wanataaluma hawa kuthibitisha<br />

habari wanazozikusanya kabla ya<br />

kuzitangaza kwa umma.<br />

Hata hivyo aliwashauri wakulima<br />

wenzake wakabiliane na changamoto<br />

ya upatikanaji wa habari katika<br />

maeneo ya vijijini kwa kutosubiri<br />

tu hadi magazeti yawafikie ndipo<br />

wajue wamepata habari kumili kujua<br />

nini kinaendelea, bali wanaweza pia<br />

kupata habari zinazowahusu kwa<br />

kupitia majarida yanayochapishwa<br />

na mashirika yanayojihusisha<br />

na shughuli za kilimo kama vile<br />

<strong>MVIWATA</strong> ili kutambua fursa walizo<br />

nazo.<br />

Lakini akasema kwamba wakulima<br />

wasiishie kusoma habari na kuziacha<br />

tu katika makaratasi bali wazifanyie<br />

kazi na pia wasiogope kutumia<br />

vyombo vya habari kuwasilisha kero<br />

na kufichua maovu.<br />

Bw. Joseph Msagama kutoka<br />

Tanga alikiri kuwa changamoto<br />

kubwa ipo katika upokeaji wa habari<br />

kutokana na uhaba wa rasilimali<br />

fedha ambayo inamwathiri kila<br />

mkulima.<br />

“Jambo la kusikitisha ni kwamba<br />

wananchi wa vijijini wanaonekana<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />

kuwa tabaka la watu waliosahaulika<br />

katika kila kitu kuanzia kipato, elimu<br />

na hata haki zao mbalimbali ikiwemo<br />

hii ya kupata habari” alisema Bw.<br />

Msagama.<br />

Alishauri Halmashauri za wilaya<br />

ziweke utaratibu wa kutenga<br />

mafungu ya kuwawezesha usafiri<br />

maaalum waandishi wa habari<br />

ili wafike maeneo ya vijijini na<br />

kuwasaidia wananchi kufahamu<br />

nini kinaendelea na kwa kiasi gani<br />

kinaathiri uchumi wa wakulima.<br />

Kwa upande wake Bw. Abdala<br />

Ramadhani kutoka wilaya ya<br />

Misungwi, Mwanza alisema wakulima<br />

wengi vijijini wanakabiliwa na uhaba<br />

wa habari na kushauri vituo vya<br />

taarifa vijijini viimarishwe ili kuziba<br />

pengo lililopo.<br />

“Kupitia vituo hivyo vichache<br />

vilivyopo sasa wakulima na<br />

wajasiriamali wanapata habari<br />

kuhusiana na bei za mazao na wapi<br />

wanaweza kuuza lakini habari hizo<br />

haziwafikii wengi kutokana na uhaba<br />

wa rasilimali fedha unaozikabili,”<br />

alisema Ramadhani.<br />

“Tunashukuru kuwapo kwa<br />

gazeti letu wakulima la Pambazuko,<br />

linatuwezesha kufahamu wenzetu<br />

katika maeneo mengine wanafanya<br />

nini na ni njia gani wanazozitumia<br />

kutatua changamoto zao, jambo<br />

ambalo linatupa ari ya kufanya kazi<br />

kwa bidii ili kuzalisha kwa tija.”<br />

Bw. Ramadhani alisema kupitia<br />

mtandao wa wakulima wanajipanga<br />

ili kuweka utaratibu mzuri wa<br />

kuwezesha habari za wakulima<br />

wa Mwanza zinamfikia mhariri wa<br />

Pambazuko kwa wakati.<br />

Bw. Paul Mossama kutoka<br />

Serengeti mkoani Mara, anaeleza<br />

kuwa mfumo wa upashanaji habari<br />

uliopo nchini hivi sasa ni mzuri<br />

kuliko miaka ya nyuma, japokuwa una<br />

kasoro ya kutotangaza habari nyingi<br />

za kuwasaidia wakulima kuboresha<br />

shughuli zao na akashauri vituo vya<br />

radio na televisheni vinavyoanzishwa<br />

na halmashauri za wilaya vitangaze<br />

zaidi habari hizo badala ya kuwa na<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 6<br />

Inatoka uk. wa 3<br />

MADA MAALUM<br />

Upatikanaji wa<br />

habari vijijini<br />

maeneo ya vijijini na mijini.<br />

Kwa upande wa radio<br />

matangazo yaboreshwe yasikike<br />

vizuri vijijini ili wananchi wetu<br />

walioko mipakani kama vile<br />

Kigoma pia waweze kunufaika<br />

na matangazo ya radio za nchini<br />

mwao badala ya radio za nchi jirani<br />

ya Burundi na Kongo ambazo<br />

kila kukicha zinatangaza vita na<br />

mauaji kutokana na mapigano<br />

yanayoendelea nchini mwao.<br />

Kadhalika waandishi<br />

wenyewe wanakabiliwa na<br />

changamoto ya kujiendeleza<br />

kitaaluma ili kuweza kuwa<br />

na upeo zaidi wa kuandika<br />

na kuchanganua habari zao<br />

kwa weledi hasa zinazohusu<br />

maendeleo vijijini badala ya kuwa<br />

mawakala ama mashabiki wa<br />

siasa tu.<br />

Kuna matatizo mengi vijijini<br />

ambayo kimsingi yanahitaji nguvu<br />

ya wanahabari kuyatatua. Kwa<br />

mfano wanahabari wanapaswa<br />

kuijengea uwezo jamii kuhusu<br />

elimu ya afya vijijini, elimu ya<br />

ukatili wa wanawake na vitendo<br />

vya unyanyasaji, elimu juu ya<br />

umiliki na matumizi bora ya ardhi,<br />

elimu ya kilimo bora na ufugaji,<br />

ujasiriamali, masoko na umuhimu<br />

wa elimu kwa watoto wao.<br />

Ipo haja kubwa ya tasnia<br />

ya habari kutilia mkazo suala la<br />

kuielimisha jamii ili iepukane na<br />

imani potofu za kwenda kwa<br />

waganga wa kienyeji kupiga ramli<br />

badala ya kuwapeleka wagojwa<br />

kutibiwa kwenye zahanati na<br />

vituo vya afya.<br />

Wanakijiji ambao kwa sehemu<br />

kubwa ni wakulima wanapaswa<br />

kujengewa uelewa wa masoko<br />

ya mazao yao, taarifa za bei na<br />

mbinu bora za kuongeza tija katika<br />

uzalishaji na kuboresha uchumi.<br />

Maendeleo vijijini<br />

yanachelewa kwa sababu<br />

wananchi hawapati habari sahihi<br />

kwa wakati muafaka. Hivyo<br />

yanapaswa kuchochewa kwa<br />

kuwapatia habari za kina.<br />

5


MADA MAALUM<br />

Maoni ya wakulima...<br />

Inatoka uk. wa 5<br />

vipindi vingi vya miziki na salamu.<br />

Akashauri pia magazeti kutenga<br />

kurasa maalumu zitakazoandika<br />

habari za wakulima wadogo angalau<br />

mara moja kwa wiki. “Magazeti<br />

mengi sasa yamefungua kurasa za<br />

udaku, urembo na muziki, hivyo hata<br />

kwa habari za wakulima jambo hili<br />

linawezekana.”<br />

Aliwashauri wakulima wadogo<br />

kutumia mitandao ya wakulima<br />

waliyonayo katika maeneo yao<br />

kwa ajili ya kupashana habari<br />

hadi pale wanapokuwa wanaona<br />

wameshindwa kufanya hivyo<br />

wenyewe ndipo waweze kumtafuta<br />

mwandishi ambaye atawasaidia<br />

kutangaza taarifa zao ili nao<br />

wapate nafasi ya kupaza sauti zao<br />

na kusaidiwa pale wanapohitaji<br />

msaada.<br />

Bw. Benardi Maiko kutoka<br />

Kasanga, wilayani Sumbawanga<br />

mkoani Rukwa alisema wakulima<br />

wanayo mambo mengi ambayo ni<br />

vyema wakayatangaza ikiwemo<br />

mazao yao na bidhaa zingine<br />

wanazozalisha, changamoto ya uhaba<br />

wa pembejeo na zana bora za kilimo<br />

pamoja na mahitaji ya masoko ya<br />

kuuzia mazao yao.<br />

Aliongeza pia, wakulima<br />

wanahitaji kuwezeshwa kuwasiliana<br />

wao kwa wao kupitia vyombo vya<br />

habari ili kurahisisha mawasiliano<br />

kwani badala ya wao kufunga<br />

safari kwenda maeneo mengine<br />

kuwatembelea wenzao wataweza<br />

kusoma tu kwenye magazeti ama<br />

kusikiliza radioni na kujifunza.<br />

“Endapo habari zingekuwa zinafika<br />

maeneo ya vijijini kama ilivyo kwa<br />

maeneo ya mijini hakika wakulima<br />

leo tungekuwa kundi lenye nguvu<br />

kiuchumi na tusingekandamizwa<br />

wala kunyanyaswa” alisema Bw.<br />

Maiko<br />

Bw. Charles Ndugulile<br />

mkulima wa kijiji cha Mwamala<br />

Kata ya Mwamala wilaya ya<br />

Shinyanga Vijijini alieleza kwamba<br />

6<br />

upatikanaji wa habari unategemeana<br />

na watafutaji wa habari kwamba<br />

wanataka habari za namna gani na<br />

zinazohusu nini na kutolea mfano<br />

wa jarida la Pambazuko kwamba kila<br />

anayetaka kupata habari kuhusiana<br />

na wakulima anaweza kuzipata<br />

kutoka ndani ya jarida hilo.<br />

Akizungumzia matumizi sahihi<br />

ya habari Bw. Ndugulile alisema<br />

“mwaka 2008 kupitia matangazo<br />

ya radio nilipata taarifa za kutokea<br />

mabadiliko ya tabia ambayo<br />

yatasababisha ukame na mlipuko wa<br />

wadudu lakini nilipuuzia na baadaye<br />

msimu wa kilimo uliofuata nililima<br />

shamba kubwa kama kawaida,<br />

nikapata hasara baada ya mazao<br />

kukauka kwa ukame.”<br />

Bw. Ndugulile alifafanua kwamba<br />

kutokana na hali hiyo amekuwa<br />

mhamasishaji mkubwa kwenye katika<br />

mkoa wa Shinyanga akiwahimiza<br />

wakulima umuhimu wa kutafuta<br />

habari na kuzitumia, lakini pia wawe<br />

wamezipata kutoka katika vyanzo<br />

vya uhakika na vinavyoaminika ila<br />

wasipotoshwe kwa kupata habari<br />

ambazo si sahihi.<br />

Alifafanua kwamba katika mkoa<br />

wa Shinyanga wamewahamasisha<br />

wakulima umuhimu wa kutafuta<br />

habari kutoka katika vyanzo vya<br />

uhakika na vinavyoaminika ili<br />

wasipotoshwe kwa kupata habari<br />

ambazo si sahihi.<br />

Alisema kuwa wakulima wanaumia<br />

waonapo habari mara kwa mara<br />

zinazoeleza kuwa wameshindwa<br />

kufanya jambo ama wana mgogoro<br />

fulani wakati habari za mafanikio<br />

waliyopata kupitia kilimo ikiwemo<br />

kuongeza uzalishaji na kuweza<br />

kulipa ada za watoto wao, kujenga<br />

nyumba, kuongeza idadi ya mifugo<br />

na hata kufanikiwa kununua zana za<br />

kilimo, haziandikwi. “Kwa msingi huu<br />

ndiyo maana mara nyingi nimekuwa<br />

nikishauri kwamba ni muhimu<br />

wakulima tuimarishe chombo<br />

chetu cha habari kama Pambazuko<br />

kinachoweza kutusemea habari<br />

zetu.”<br />

Bw. Ndugulile ambaye pia<br />

ni mwenyekiti wa <strong>MVIWATA</strong><br />

Shinyanga, alisema vyombo vingi<br />

vya habari nchini hivi sasa vinafanya<br />

shughuli zake kibiashara na hivyo<br />

kujikita katika matukio yenye<br />

habari zinazouzika na kutupa kando<br />

jukumu la kuwaelimisha wakulima<br />

kilimo biashara ama ufugaji na uvuvi<br />

wa kisasa.<br />

Maoni ya wataalam<br />

Bibi Mary Nsemwa, ni mkuu<br />

wa Idara ya Ushawishi na Ujenzi wa<br />

Nguvu za Pamoja katika Mtandao<br />

wa Jinsia Tanzania (TGNP), anasema<br />

asilimia kubwa ya wananchi wa<br />

vijijini wanaoathirika na upatikanaji<br />

wa habari ni wanawake.<br />

Bibi Nsemwa alisema wanawake<br />

wanahitaji kuhabarishwa kuhusiana<br />

na kilimo, ujasiriamali, sheria<br />

ya ardhi na mambo mbalimbali<br />

yanayoendelea mijini na duniani,<br />

lakini haki hiyo wanaikosa kutokana<br />

na kutokuwepo kwa miundo mbinu<br />

inayofika maeneo ya vijijini hususan<br />

barabara kwa ajili ya magazeti.<br />

“Hata kwa familia zenye radio<br />

nyingi zinamilikiwa na wanaume,<br />

hivyo wanawake kukosa taarifa<br />

muhimu ndiyo maana wanazidi<br />

kukandamizwa”.<br />

Bw. Marcossy Albanie wa<br />

Kituo cha Msaada wa Sheria na Haki<br />

za Binadamu yeye anasema “kwa<br />

ujumla wakulima ni kundi lililoachwa<br />

nyuma na hata wakizungumza watu<br />

wanawapuuza na ndiyo maana hata<br />

vyombo vingi vya habari vimeegemea<br />

zaidi mjini, ingawa kisingizio kikubwa<br />

kimekuwa ni miundombinu mibovu<br />

vijijini.<br />

“Suala hili linamfanya mkulima<br />

mdogo abaki kwenye kiza na watu<br />

wachache waendelee kunufaika na<br />

rasilimali za nchi.<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011


Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />

MAKALA<br />

Soko huria lilivyoathiri upatikanaji<br />

wa habari vijijini<br />

Na Rashid Kejo<br />

Tulikotoka<br />

Nchi ya Tanzania tangu ilipopata<br />

uhuru wake mwaka 1961, ilikuwa<br />

ikitumia mfumo wa vyama vingi hadi<br />

mwaka 1965 ilipoamua kuachana<br />

nao. Hata hivyo mwaka 1992,<br />

Tanzania iliridhia mageuzi makubwa<br />

ya kurejea katika mfumo wa vyama<br />

vingi vya siasa.<br />

Sababu iliyotolewa mwaka 1965<br />

wakati wa kuachana na vyama vingi<br />

ni kwamba pamoja na mambo<br />

mengine, vyama vya upinzani<br />

ambavyo vilikuwapo kama vile<br />

African Independence Movement<br />

(AIM) na People’s Democratic<br />

(PDP), havikuwa na nguvu.<br />

Lakini pia wakati ule, kulikuwa na<br />

vuguvugu kubwa la mataifa mengi<br />

ya Afrika kuendeshwa chini ya<br />

utawala wa chama kimoja kutokana<br />

na kile kilichoelezwa kwamba ni<br />

kuleta umoja wa kitaifa na kuondoa<br />

mifarakano na migogoro kwa lengo<br />

la kujiletea maendeleo.<br />

Licha ya kuwa na chama kimoja<br />

kilichokuwa kimeshika hatamu, hata<br />

nyanja nyingine kuu na muhimu za<br />

kiuchumi na kijamii, kwa kiwango<br />

kikubwa zilikuwa chini ya umma.<br />

Vyombo vya habari kadhalika,<br />

vilikuwa katika mfumo dola. Redio,<br />

televisheni (kwa Zanzibar) na<br />

magazeti, ama vilimilikiwa moja<br />

kwa moja na Serikali, taasisi zake au<br />

chama na jumuiya zake.<br />

Tunakumbuka vyombo kama<br />

Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD),<br />

Sauti ya Tanzania Zanzibar (STZ),<br />

Magazeti ya Daily News/Sunday<br />

News, Uhuru/Mzalendo, Mfanyakazi<br />

na Mkulima wa Kisasa.<br />

Kutokana na uchache na umiliki<br />

wake, maudhui ya vyombo hivi<br />

yaliratibiwa na dola yakilenga<br />

masuala kadhaa ambayo Serikali<br />

ilikuwa imeyapa kipaumbele.<br />

Pamoja na changamoto zake,<br />

habari za wakulima zilipata fursa<br />

katika vyombo hivyo. Achilia mbali<br />

gazeti, kulikuwa na vipindi vya redio<br />

vya Mkulima wa Kisasa ambavyo<br />

vilitoa mafunzo na maelekezo<br />

mbalimbali ya kilimo bora.<br />

Kulikuwa pia na mkakati maalumu<br />

kupitia Taasisi ya Vielelezo wa<br />

kupeleka sinema vijijini kuelimisha<br />

wakulima juu ya ukulima na<br />

ufugaji bora. Kimsingi, kulikuwa na<br />

upatikanaji wa taarifa hasa zile za<br />

msingi kwa umma wa vijijini.<br />

Wahenga walisema, kila masika<br />

yana mbu wake. Katika mabadiliko<br />

ya mwaka 1992 yaliyoruhusu mfumo<br />

wa vyama vingi na soko huria,<br />

Serikali ilijitoa katika biashara na<br />

kulegeza masharti hivyo kuiwezesha<br />

sekta binafsi kushiriki moja kwa<br />

moja katika masuala ya kiuchumi<br />

na kijamii. Mabadiliko yalichochea<br />

kuanzishwa kwa Sera ya Habari na<br />

Utangazaji ya mwaka 1993.<br />

Hata hivyo, haikujitoa katika<br />

usimamizi na uendeshaji wa vyombo<br />

vyake vya habari, bali iliruhusu sekta<br />

binafsi nayo kuingia katika biashara<br />

hiyo. Hivyo, kuanzia mwaka 1992,<br />

magazeti, vituo vya televisheni<br />

na redio na baadaye mitandao ya<br />

mawasiliano vilianza kwa kasi.<br />

Tofauti na awali ambako<br />

mwelekeo wa habari ulilenga zaidi<br />

propaganda, safari hii mtazamo<br />

ulikuwa wa kibiashara zaidi na hali<br />

hiyo imekuwa na athari kubwa katika<br />

upatikanaji wa habari za vijijini.<br />

Kutokana na msukumo huo wa<br />

nguvu ya soko, vyombo ambavyo<br />

vilishindwa kujiendesha kibiashara<br />

vilikufa na hivyo ndivyo ilivyotokea<br />

kwa Gazeti la Mkulima wa Kisasa.<br />

Vipindi vingi vilivyoanzishwa katika<br />

redio na televisheni vililenga zaidi<br />

kuwavutia watangazaji (advertisers).<br />

Kwa upande mwingine, asilimia<br />

kubwa ya magazeti na machapisho<br />

husomwa zaidi mijini ambako<br />

usambazaji ni rahisi na kiwango cha<br />

kujua kusoma na kuandika ni kikubwa<br />

na hilo likawa na athari kubwa kwa<br />

upatikanaji wa habari za vijijini.<br />

Hiyo ilimaanisha kwamba<br />

wakulima na wananchi wengine<br />

waishio vijijini walianza kupewa<br />

habari ambazo hazikuwa na uwiano<br />

wa moja kwa moja na matatizo au<br />

vipaumbele vyao.<br />

Kwa mfano, mwaka 1995<br />

wakati taifa likiwa katika kampeni<br />

za kwanza tangu kurejeshwa kwa<br />

mfumo wa vyama vingi, baadhi ya<br />

vituo vya televisheni vilitumia fursa<br />

hiyo vibaya kwa kuonyesha picha za<br />

mauaji hivyo kuwatishia wananchi.<br />

Mabadiliko makubwa<br />

Hata hivyo, kadri miaka inavyosonga<br />

kumekuwa na mabadiliko makubwa.<br />

Kukua kwa teknolojia ya mawasiliano<br />

na dhana ileile ya soko kumevifanya<br />

vyombo vya habari kuanza kubaini<br />

umuhimu wa kulitazama soko la vijijini<br />

waliko asilimia 80 ya Watanzania.<br />

Halmashauri za wilaya na<br />

wawekezaji wengine wa ndani<br />

wameanzisha redio za jamii<br />

(community radio) ambazo zinatoa<br />

huduma ya habari katika maeneo<br />

yao. Hili limekuwa na mchango<br />

mkubwa kwa wananchi wa vijijini<br />

kwani taarifa, kero na shida zao<br />

zimekuwa zikipata fursa ya kusikika.<br />

Lakini siyo kusikika tu, kumekuwa<br />

na fursa kubwa zaidi ya kupata<br />

habari zinazokidhi mahitaji yao<br />

kwa kiwango kikubwa na hivyo<br />

kuchochea maendeleo yao.<br />

Ingawa wilaya zilizoanzisha radio<br />

hizi za jamii ni chache mno, lakini<br />

wilaya zilizobahatika kuwa na redio<br />

hizi, zimekuwa zikitumia fursa hiyo<br />

kufikisha ujumbe muhimu katika<br />

maeneo husika kama vile bei ya<br />

bidhaa na huduma nyingine muhimu.<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 11<br />

7


ANA KWA MFUMO ANA/MAKALA WA TAARIFA ZA MASOKO WA <strong>MVIWATA</strong><br />

(MAMIS)<br />

PATA BEI ZA MAZAO KWENYE SIMU YAKO POPOTE ULIPO!!<br />

Jinsi ya kupata taarifa kwenye simu yako:<br />

Masoko yaliyopo mpaka sasa:<br />

MOROGORO, TAWA, TANDAI, NYANDIRA, KIBAIGWA, DODOMA, IGUNGA, TABORA, SHINYANGA,<br />

MASWA, BARIADI, BUKOMBE, KAHAMA, KILOMBERO (ARUSHA), KARIAKOO, BUGURUNI, TEMEKE,<br />

IGURUSI (MBEYA), MKURANGA, MAKAMBAKO, SIMANJIRO, TAVETA, MKATA, IGAGALA, MATAI<br />

(RUKWA), KASANGA, HIMO, HOLILI, n.k<br />

Mazao yaliyo kwenye mfumo huu:<br />

MAHINDI, MCHELE, MAHARAGE, CHOROKO, KUNDE, MBAAZI, NJEGERE, MTAMA, UWELE, ULEZI,<br />

UFUTA, ALIZETI, NDIZI MBIVU, NDIZI MBICHI, MAGIMBI, MUHOGO, NANASI, CHUNGWA, PAPAI,<br />

EMBE, PARACHICHI, NYANYA, VITUNGUU MAJI, VITUNGUU SAUMU, TANGO, KAROTI, KABICHI,<br />

HOHO, LUBABU, SELELI, BITRUTI, ZUKINI, SALADI, KOLIFLAWA, TANGAWIZI, PILIPILI MTAMA,<br />

MDALASINI, ILIKI.<br />

...meseji moja kwa kila zao moja<br />

8<br />

imedhaminiwa na;<br />

Taarifa ya BEI ZA MAZAO<br />

1. Andika neno BEI acha nafasi<br />

2. Andika zao unalotaka bei yake mfano; MAHINDI<br />

3. Kisha tuma kwenda namba 0654 555 884<br />

Taarifa ya WAUZAJI<br />

1. Andika neno NANUNUA acha nafasi<br />

2. Andika zao unalotaka kununua mfano; MAHINDI<br />

3. Kisha tuma kwenda namba 0654 555 884<br />

Taarifa ya WANUNUZI:<br />

1. Andika neno NAUZA acha nafasi<br />

2. Andika zao unalotaka kuuza mfano; MAHINDI<br />

3. Kisha tuma kwenda namba 0654 555 884<br />

Kwa Mawasiliano zaidi piga SIMU NAMBA 0659250317<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011


Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />

MAKALA<br />

Taaluma ya habari ni wito<br />

Na Susuma Susuma<br />

Vyombo vya habari ni jina<br />

la jumla la mfumo wa<br />

mawasiliano unaojumuisha<br />

utangazaji wa redio, televisheni,<br />

majarida na magazeti. Vyombo<br />

hivi vina wajibu mkubwa wa<br />

kuhudumia matakwa ya jamii katika<br />

maisha yao ya kila siku. Vyombo<br />

vya habari vinaelimisha, vinatoa<br />

burudani na kutoa changamoto<br />

kwa wananchi na viongozi kuhusu<br />

mambo mbalimbali.<br />

Kadhalika taaluma ya habari ni<br />

tasnia nyeti inayoheshimika katika<br />

jamii yoyote inayothamini ustaarabu,<br />

umoja na utangamano wa kitaifa.<br />

Kuandika makala kwenye<br />

magazeti, kusoma taarifa ya habari<br />

au utayarishaji wa vipindi vya siasa,<br />

jamii, utamaduni, dini, burudani ama<br />

matukio yanayohitaji jamii kupewa<br />

taarifa, ni shughuli zinazohitaji<br />

ushirikiano wa kutosha baina ya<br />

wadau yaani waandishi, watoa habari<br />

na walaji (wasikilizaji/wasomaji).<br />

Kwa mantiki hiyo, ushirikiano<br />

madhubuti kati ya wadau wa habari<br />

na waandishi wa habari ni nguzo ya<br />

maendeleo katika jamii.<br />

Aidha, kufanikisha masuala<br />

haya kunahitaji umakini, weledi,<br />

mazingatio ya kufuata miiko, maadili<br />

na heshima kwa mwandishi ama<br />

mtangazaji husika.<br />

Utendaji kazi wa vyombo<br />

vya habari<br />

<strong>Uk</strong>ilinganisha miaka 50 iliyopita hali<br />

ya utendaji kazi wa vyombo vya<br />

habari na hali ilivyo hivi sasa nchini<br />

kwetu ni tofauti kabisa.<br />

Uandikaji wa habari, makala,<br />

utangazaji na utayarishaji wa vipindi<br />

hivi sasa hauzingatii ujuzi, taaluma na<br />

kuheshimu miiko, kama ilivyokuwa<br />

miaka ya awali.<br />

Fani hii imeshuhudia watu<br />

wanahitimu uandishi wa habari ngazi<br />

ya shahada ya kwanza au ya uzamili,<br />

lakini bado wakashindwa kuandika<br />

habari kwa usahihi.<br />

Kwa mfano eneo moja<br />

linalowashinda ni jinsi ya kufahamu<br />

mahitaji halisi ya wasomaji,<br />

wasikilizaji ama watazamaji wao,<br />

kushindwa kufahamu habari ilipo<br />

ama kushindwa kutofautisha habari,<br />

uzushi na fitina.<br />

Wapo wanaosema fani hii ni<br />

rahisi kuliko zote na hawa ndiyo<br />

wanaovamia fani hii na kudhani<br />

kwamba wanafanya vizuri bila<br />

kufahamu kuwa wanachangia kuua<br />

taaluma.<br />

Fani hii siyo rahisi kama<br />

inavyodhaniwa na wengi, na pengine<br />

ndiyo maana kila kukicha vyombo<br />

vya habari vinalaumiwa kwa kukiuka<br />

miiko na maadili kwa kuwa wengi<br />

wanaamua kujiunga wakidhani<br />

ni kuandika tu, matokeo yake<br />

wanafanya upotoshaji.<br />

Tumeshuhudia pia utitiri wa<br />

vyombo vya habari vinavyoanzishwa<br />

kila leo, lakini cha kushangaza vingi<br />

vinaanzishwa mijini na kuhudumia<br />

watu wa mijini tu na kuwaacha<br />

kando watu waishio vijijini.<br />

Kwa mujibu wa takwimu za<br />

Msajili wa Magazeti mpaka sasa<br />

amekwishasajili zaidi ya magazeti<br />

na majarida 350 ingawa ni asilimia<br />

15 tu ya machapisho hayo ambayo<br />

yanaonekana mitaani kwa wakati huu<br />

na asilimia kubwa yakiwa mijini. Idadi<br />

kubwa ya magazeti yaliyosajiliwa<br />

yanamilikiwa na watu au makampuni<br />

binafsi isipokuwa magazeti ya ”Daily<br />

News, Sunday News na Habari leo”<br />

ambayo yanamilikiwa na Serikali na<br />

gazeti la Uhuru linalomilikiwa na<br />

chama tawala CCM. <strong>Uk</strong>ipekuwa<br />

kwa undani utendaji kazi wa<br />

magazeti haya sasa yako kibiashara<br />

zaidi kinyume na matarajio ya kutoa<br />

huduma ya kuhabarisha umma.<br />

Vyombo vya habari<br />

vinapoanzishwa vikiwa na mlengo<br />

wa kibiashara zaidi, ni moja ya<br />

sababu inayochangia vyombo vingi<br />

virundikane mjini ambako wamiliki<br />

wanaamini watauza na kupata<br />

matangazo ya kutosha. Na hoja hapa<br />

ni Je, jamii ya huko vijijini ambako<br />

biashara ya radio, televisheni na<br />

magazeti hazilipi, itafikiwaje na habari<br />

zenye kuchochea maendeleo?<br />

Kufanya hivi vyombo vya habari<br />

vinakiuka sheria na kuwanyima haki<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 10<br />

<strong>MVIWATA</strong> katika kusaidia wakulima kupaza sauti zao, imekuwa ikiwawezesha wanahabari<br />

kuyafikia maeneo ya vijijini na kuchukua habari za kero zao<br />

9


MAKALA<br />

Taaluma ya habari ni wito...<br />

Inatoka uk. wa 9<br />

ya msingi wananchi wa vijijini.<br />

Katiba ya Jamhuri ya Muungano<br />

wa Tanzania (1977) ambayo ilifanyiwa<br />

marekebisho mwaka 1984, imeweka<br />

kifungu maalum kinachotaja wazi<br />

kuwa habari ni haki ya msingi ya raia.<br />

Kifungu hicho cha <strong>18</strong> cha Katiba<br />

kinasema:<br />

(1) Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila<br />

mtu yuko huru kuwa na maoni<br />

yoyote na kutoa nje mawazo<br />

yake, na kutafuta, kupokea na<br />

kutoa habari na dhana zozote<br />

kupitia chombo chochote bila<br />

ya kujali mipaka ya nchi, na<br />

pia uhuru wa mawasiliano yake<br />

kutoingiliwa kati.<br />

(2) Kila raia anayo haki ya kupewa<br />

taarifa wakati wowote kuhusu<br />

matukio mbalimbali nchini na<br />

duniani kote, ambayo ni muhimu<br />

kwa maisha na shughuli za<br />

wananchi; na pia juu ya masuala<br />

muhimu kwa jamii.<br />

Wajibu wa vyombo vya<br />

habari<br />

Njia muhimu za kuwezesha<br />

wananchi kufurahia haki ya kupasha<br />

na kupashwa habari na kujieleza<br />

kwa kutoa maoni hadharani bila<br />

bughudha,vitisho na ukandamizwaji<br />

ni kupitia vyombo vya habari.<br />

Kutokana na umuhimu wa kipekee<br />

wa haki hii ya msingi, nafasi ya<br />

vyombo vya habari katika utekelezaji<br />

wake pia ni ya kipekee. Kwa kuwa<br />

vyombo vya habari vinawawezesha<br />

wananchi kutumia haki hii ili isibaki<br />

nadharia au kwenye maandishi tu,<br />

hakuna budi wamiliki wa vyombo vya<br />

habari pamoja na serikali, watambue<br />

na kukiri kwamba nafasi yao ni ya<br />

kutoa huduma au mahitaji ya lazima<br />

kwa jamii, huduma kwa umma.<br />

Hadhi ya huduma ya kijamii<br />

inazidi sana ile ya bidhaa ambazo<br />

huuzwa kuingiza faida. Ndiyo maana<br />

wajibu wa wamiliki wa vyombo vya<br />

habari kwa jamii ni mkubwa kuliko<br />

wa mfanyabiashara ama mwekezaji<br />

ambao msukumo wao mkubwa ni<br />

10<br />

kutengeneza faida.<br />

Hata vyombo vya habari vya<br />

serikali vinapaswa kuwajibika kwa<br />

umma na sio utashi wa kisiasa wa<br />

wanasiasa na watawala.<br />

Wanahabari pamoja na kwamba<br />

huajiriwa na wamiliki wa vyombo,<br />

bado huwajibika kwa umma. Na<br />

ndiyo maana ili vyombo vya habari<br />

viweze kutekeleza majukumu<br />

yao, hakuna budi kwa wahariri na<br />

wanahabari kuwa na uhuru wa<br />

kutosha kukusanya, kuchambua<br />

na kusambaza habari bila woga,<br />

shinikizo au ushawishi wa wamiliki<br />

na washiriki wao kibiashara.<br />

Habari ni huduma<br />

Kazi ya uandishi wa habari ni fani<br />

ambayo pamoja na kuwa na ujuzi<br />

lakini inahitaji zaidi wito. Ni fani<br />

ambayo inahitaji zaidi mtu kutanguliza<br />

utu na upendo ama dhana ya kutoa<br />

huduma kuliko malipo ama kufanya<br />

biashara. Ni fani isiyojali sana malipo<br />

yenye kulingana na kadhia, ugumu<br />

wala masuala mengine kwa kuwa<br />

kuna wakati unakuwa unashughulikia<br />

tatizo la kijamii iliyo masikini ambayo<br />

malipo yake ni asante.<br />

Kinachosikitisha zaidi ni kuona<br />

baadhi ya waandishi wa habari<br />

wakishabikia zaidi kuandika habari<br />

za migogoro na kuwachafua watu,<br />

wakati mwingine wakiishia kudai<br />

posho bila hata kuandika chochote.<br />

Hali hii inaonesha walivyokosa<br />

ushirikiano na jamii.<br />

Pia zipo sheria ambazo<br />

zinaonekana kukandamiza uhuru wa<br />

vyombo vya habari nchini, ambazo<br />

wanahabari wamekuwa wakizipigia<br />

kelele kwa kuitaka serikali<br />

kuzirekebisha ama kuzifuta kabisa.<br />

Hizi ni pamoja na sheria ya magazeti<br />

ya Tanzania ya mwaka 1976 ambayo<br />

inampatia uwezo waziri anayehusika<br />

na habari wa kulifungia gazeti lolote<br />

lile kama ataridhika kuwa limekiuka<br />

kwa kiasi kikubwa matakwa ya sheria<br />

hiyo. Sheria hizi pia zinakwamisha<br />

upatikanaji wa habari sahihi zenye<br />

maslahi umma.<br />

Mfano halisi ni wa taarifa<br />

zinazohusiana na kashfa kwenye<br />

migodi ya madini na kwenye sekta ya<br />

uwindaji wanyama kwenye mbuga za<br />

wanyama ambazo zinaakisi uchumi<br />

wa nchi.<br />

Serikali inapaswa kupitisha sheria<br />

rafiki kwa vyombo vya habari na<br />

ambazo zinaweka mazingira huru ya<br />

upatikanaji wa habari, kwani kuvifunga<br />

minyororo vyombo vya habari ni<br />

kuwafunga minyororo wananchi.<br />

Kwa upande mwingine wapo<br />

waandishi wa habari wanaotishiwa<br />

maisha pale wanapofuatilia ili kupata<br />

habari za kina kuhusiana na jambo<br />

fulani lenye maslahi kwa jamii. Lakini<br />

hiyo siyo sababu ya wao kufanya<br />

shughuli zao kinyume cha sheria na<br />

maadili ya taaluma yao kama vile<br />

kutoa na kupokea rushwa, upotoshaji<br />

na udanyanyifu, uchochezi, ushabiki,<br />

kutunga ama kutia chumvi habari.<br />

Hata hivyo changamoto ni sehemu<br />

ya maisha, ni chachu kwa maendeleo<br />

yoyote, wanahabari ni vyema<br />

tukajenga tamaduni ya kwenda<br />

vijijini kuzungumza na kutangaza<br />

habari za mafanikio, ubunifu, uzoefu<br />

na mbinu wanazotumia wanavijiji<br />

kutatua changamoto za maisha yao<br />

ya kila siku.<br />

Kwa kuwa tumeamua<br />

kuwatumikia wananchi wenye<br />

uhitaji wa huduma yetu, hatuna<br />

budi kuzikabili changamoto zote<br />

za kutafuta, kuandaa na kuzifikisha<br />

habari kwa wadau bila kujali<br />

zinapatikana kutoka mazingira yenye<br />

changamoto nyingi.<br />

Kwa upande mwingine liko kundi<br />

dogo la wanahabari nchini ambao<br />

wamepungukiwa utu na upendo,<br />

wametanguliza zaidi maslahi binafsi,<br />

ndiyo maana wameigeuza fani hii<br />

kuwa biashara badala ya huduma<br />

kwa jamii. Kundi hili japokuwa ni<br />

dogo lakini laweza kuwa na madhara<br />

makubwa kwa jamii hasa kipindi hiki<br />

ambao vitendo vya ufisadi vinazidi<br />

kushika kasi ndani ya nchi yetu.<br />

Wakialikwa kwenda kuchukua habari<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 11<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011


Soko huria lilivyoathiri...<br />

Inatoka uk. wa 7<br />

Inawezekana bado kuna vikwazo<br />

vya hapa na pale katika kuwafikia<br />

wananchi wa vijijini walio wengi, lakini<br />

muhimu ni kuviimarisha zaidi vyombo<br />

hivi ili walau viweze kuziba pengo<br />

lililosababishwa na kutoweka kwa<br />

majarida kama ya mkulima wa kisasa.<br />

Mamlaka za miji na wilaya nchini<br />

ni mali ya wananchi kupitia mabaraza<br />

ya madiwani ambao wanatokana na<br />

kura za watu katika ngazi za kata.<br />

Kwa maana hiyo basi ni fursa kwa<br />

viongozi hawa wawakilishi wa umma<br />

(madiwani), kuimarisha usimamizi<br />

wa vituo vya redio na televisheni<br />

vinavyomilikiwa na halmashauri zao<br />

ili viweze kukidhi matakwa ya jamii<br />

husika, ziwe za wakulima, wafugaji,<br />

wavuvi, wachuuzi au wengineo.<br />

Hii ni moja ya hatua muhimu<br />

zinazoweza kuwarejesha wazalishaji<br />

wadogo wa sekta mbalimbali nchini<br />

katika dunia ya mawasiliano.<br />

Intaneti na simu za mkononi<br />

Tunapozungumzia habari, hatuwezi<br />

kuacha kuzungumzia njia nyingine<br />

za kisasa za mawasiliano kama vile<br />

intaneti na simu za mkononi. Hizi kwa<br />

ujumla wake zimekuwa na mchango<br />

mkubwa kwa wananchi wa vijijini<br />

katika mambo mbalimbali.<br />

Intaneti kwa mfano, imewawezesha<br />

wananchi kutafuta masoko, masomo<br />

na kuwasiliana kwa sababu mbalimbali<br />

na taasisi, ndugu, jamaa na marafiki zao<br />

walio mbali.<br />

Zamani ilikuwa ni gharama kubwa<br />

na usumbufu kuwasiliana kwa njia ya<br />

barua na ndugu walio mbali. Lakini<br />

sasa, katika baadhi ya maeneo ya<br />

vijijini kuna vituo vya mawasiliano<br />

ambako wananchi huenda na kupata<br />

huduma hizo za mtandao (simu/<br />

intaneti) na hivyo kupata taarifa<br />

mbalimbali za shughuli zao na pia<br />

kuwasiliana na watu mbalimbali.<br />

Magazeti mengi ya ndani na<br />

nje na hata redio zimeunganishwa<br />

pia katika mitandao hii ya intaneti,<br />

hivyo wananchi popote walipo<br />

wanaweza kusoma habari za leoleo<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />

hivyo kujiweka katika nafasi nzuri ya<br />

kuujua ulimwengu na yanayoendelea<br />

na kutumia taarifa hizo kujiongezea<br />

maarifa na kujiendeleza.<br />

Njia hii ya simu ndiyo imekuwa<br />

na athari chanya kubwa. Idadi kubwa<br />

ya Watanzania mijini na vijijini hivi<br />

sasa wanafaidika kwa huduma hii<br />

iwe moja kwa moja au kupitia kwa<br />

ndugu na jamaa zao.<br />

Upashanaji wa habari ulikwaza<br />

mambo mengi ya watu waishio<br />

vijijini lakini baada ya mapinduzi ya<br />

teknolojia hii, si ajabu hivi sasa kwa<br />

mfano, mtu aliye kijijini kumweleza<br />

au kumpa taarifa aliye mjini juu ya<br />

tukio lililotokea huko huko mjini.<br />

Mara ngapi tumesikia watu<br />

waishio Dar es Salaam wakipewa<br />

taarifa za msiba uliotokea hukohuko<br />

Dar es Salaam na mtu aishie<br />

kijijini? Kimsingi mawasiliano<br />

hayo yamevunja umbali baina ya<br />

watu wa maeneo haya. Japokuwa<br />

haya yanatokea kwenye maeneo<br />

machache mno ya vijijini ambayo<br />

yamebahatika kuunganishwa na<br />

huduma za simu za mkononi.<br />

Mapinduzi mengine chanya<br />

yaliyotokana na uwepo wa mawasiliano<br />

haya ya simu ni utumaji na upokeaji wa<br />

fedha kupitia mitandao ya simu.<br />

Usumbufu wa kuwatumia wazazi<br />

kijijini fedha au kuwalazimu wakulima<br />

na wafanyabiashara kusafiri kwenda<br />

mjini au kijijini kununua au kuuza<br />

bidhaa siku hizi hauna ulazima. Baada<br />

ya kuingia makubaliano, mkulima<br />

anaweza kufungasha mazao yake na<br />

kuyatuma mjini na kutumiwa fedha<br />

kwa njia ya simu na hayo hufanyika<br />

ndani ya muda mfupi mno. Zaidi ya<br />

hayo huduma za mawasiliano ya simu<br />

zimepanua wigo wa ajira kwa vijana<br />

vijijini na kuongeza kipato, hivyo<br />

basi wananchi wanapaswa kuitumia<br />

vyema fursa hiyo kwa kuifanya kuwa<br />

kichochocheo cha maendeleo yao.<br />

Mwandishi wa Makala hii ni<br />

Mhariri wa Habari wa Gazeti<br />

la Mwananchi<br />

Taaluma ya habari<br />

ni wito...<br />

Inatoka uk. wa 10<br />

MAKALA<br />

kijijini, swali la kwanza wanalouliza ni<br />

watalipwa? nani atawalipa? kiasi gani<br />

watalipwa? Wakishapewa majibu<br />

kuwa hakuna malipo kwa kuwa<br />

kazi hiyo ni sehemu ya utekelezaji<br />

wa majukumu yao, wanaishia kutoa<br />

visingizio vya kutoenda kufanya kazi<br />

hiyo.<br />

Wanahabari tunapaswa<br />

kujitambua kuwa sisi ni nguzo<br />

muhimu ya maendeleo katika<br />

jamii hivyo tunatakiwa kujenga<br />

ushirikiano madhubuti baina yetu<br />

na wadau wa habari wakati wa<br />

kutekeleza majukumu ya kuipasha<br />

habari jamii kwa uaminifu na<br />

kudhihirisha kuwa tulioko kwenye<br />

taaluma hii tuna wito.<br />

Aidha ni muhimu kwa umma<br />

kuwa na imani na wanahabari<br />

kuwa wanachofanya ni sehemu<br />

ya utekelezaji wa majukumu<br />

kama ilivyo kwa watumishi<br />

wa sekta nyingine na kwamba<br />

hawana sababu ya kuwaogopa,<br />

kujenga chuki ama kuwapa taarifa<br />

za uongo na uchochezi, bali<br />

washirikiane nao kwa ukaribu.<br />

Ni vyema kila kundi likajali na<br />

kuheshimu uhuru wa kutoa na<br />

kupata habari kama ilivyo ndani<br />

ya katiba ya nchi.<br />

Jihadhari na<br />

maambukizo ya<br />

UKIMWI<br />

jikinga na umlinde<br />

mwenzako<br />

11


KAMERA<br />

12<br />

KAMERA YA <strong>MVIWATA</strong> MITANDAONI<br />

Wakulima wa kata ya Mlangali wilayani Ludewa wakioneshana<br />

jambo lililowavutia kwenye gazeti la Pambazuko linaloandika habari<br />

za wakulima na kusambazwa vijijini<br />

Moja ya mikutano ya mitandao ya wakulima ambayo imekuwa<br />

ikitumika kupashana habari vijijini<br />

Picha ya pamoja ya baadhi ya viongozi na watumishi wa <strong>MVIWATA</strong><br />

na wawakilishi wa ubalozi wa Ireland nchini Bibi Aileen D’donovan,<br />

Dkt Sizya Lugeye na Bw. Vicent Akuluyuka (wa nne hadi wa sita<br />

kutoka kushoto waliosimama), baada ya ujumbe huo kutembelea<br />

makao makuu ya <strong>MVIWATA</strong> yaliyoko Morogoro Julai 5, 2011.<br />

Bibi HotensiaThomas, mwenyekiti wa Bodi ya Soko la Wakulima<br />

Nyandira akisikiliza swali kwa mmoja wa wadau wa masoko ya<br />

Igurusi, Matai na Kasanga walipofanya ziara sokoni hapo Julai 21,<br />

2011<br />

Wana-<strong>MVIWATA</strong> walioshiriki Tamasha la Jinsia Septemba 2011<br />

wakimsikiliza mwenzao wakati wa majadiliano<br />

Wana-<strong>MVIWATA</strong> Kiteto Manyara walioshiriki mafunzo ya kujengea<br />

uwezo viongozi Julai 28-29, 2011, wakiwa na baadhi ya watumishi<br />

wa <strong>MVIWATA</strong> taifa waliowezesha mafunzo hayo<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011


KAMERA YA <strong>MVIWATA</strong> MITANDAONI<br />

<strong>Uk</strong>osefu wa habari sahihi za masoko vijijini unasababisha bidhaa za<br />

wajasiliamali kama hawa wa Kwekanga Lushoto kukosa soko<br />

Wakulima wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kushiriki<br />

Jukwaa la Wakulima mkoani Ruvuma<br />

Wanawake jamii ya wafugaji wilayani Monduli, wakishiriki kazi ya<br />

kuchimba msingi na kuweka mawe ya msingi ya jengo la kukusanyia<br />

la kituo cha kibiashara<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />

KAMERA<br />

‘Natangaza kazi za mikono’, ndivyo anavyoelekea kusema mama<br />

huyu mkazi wa kijiji cha Kwalei wilayani Lushoto<br />

Bibi Elizabeth Lagwen (kulia) Mwenyekiti wa mtandao wa msingi<br />

Mamire Babati Vijijini akiwasikiliza wageni kutoka shirika la TRIAS<br />

Ubeligiji waliomtembelea kujifunza shughuli anazozifanya<br />

Licha ya kuwa na historia ya ufugaji pekee, jamii ya Wamasai sasa<br />

wamebadlika na kuanza kushiriki kilimo kama wanawake hawa<br />

walivyokutwa na kamera yetu wakipanda mazao shambani<br />

13


KUTOKA MITANDAONI<br />

Maonesho ya NaneNane 2011<br />

Wakulima wazungumzia matumizi na faida<br />

za bidhaa walizoonesha<br />

Na Goodness Mrema, Morogoro<br />

Mtandao wa vikundi<br />

vya wakulima Tanzania<br />

(<strong>MVIWATA</strong>) katika<br />

kuhakikisha kwamba unatekeleza<br />

vyema majukumu yake umekuwa<br />

na utaratibu wa kuwawezesha<br />

wakulima toka mikoa mbalimbali<br />

kushiriki kuonesha bidhaa zao<br />

kwenye maonesho ya kilimo<br />

maarufu kama NaneNane.<br />

Mwaka 2011 katika maonesho<br />

hayo ya wakulima <strong>MVIWATA</strong><br />

iliwawezesha wakulima zaidi ya 40<br />

kushiriki maonesho hayo kwenye<br />

viwanja vya Mwalimu Nyerere<br />

Morogoro na Themi Arusha, kwa<br />

lengo la kuwapatia fursa ya kujifunza,<br />

kubadilishana uzoefu na kutangaza<br />

bidhaa zao. Katika maonesho hayo<br />

<strong>MVIWATA</strong> ilipata ushindi wa kwanza<br />

kwa upande wa vyama na mashirika<br />

yasiyo ya kiserikali kwenye uwanja<br />

wa maonesho ya NaneNane kanda<br />

ya Mashariki wa Mwalimu Nyerere<br />

Morogoro na katika kanda ya<br />

Kaskazini kwenye viwanja vya Themi<br />

<strong>14</strong><br />

Arusha na kukabidhiwa zawadi ya<br />

Kombe na Cheti vilivyotolewa na<br />

Waziri Mkuu Bw. Mizengo Pinda.<br />

Aidha kwenye viwanja vya Themi<br />

Arusha mkulima Bw. Richard Kipara<br />

ambaye ni katibu wa Mtandao wa<br />

Vikundi vya Wakulima Ekenywa<br />

(MVIWAEKE) alishinda kuwa<br />

‘Mkulima Bora’ wa wilaya mpya ya<br />

Arusha Vijijini.<br />

Katika maonesho hayo mfugaji<br />

Bw. Moses Ndoipo kutoka wilaya ya<br />

Longido, alileta mbuzi bora aina ya<br />

Isiolo wa uzito wa kilo 240 aliyekuwa<br />

anauzwa Sh. 300,000 na kuwa<br />

kivutio kwa wageni waliotembelea<br />

maonesho.<br />

Miongoni mwa wakulima waliopata<br />

fursa ya kushiriki maonesho haya<br />

ya NaneNane kwenye viwanja<br />

vya Mwalimu Nyerere Morogoro,<br />

walielezea umuhimu wa bidhaa<br />

walizoonesha na faida ya maonesho<br />

kwa ujumla.<br />

Kakao na Mawese<br />

Bibi Lain Mwakatundu kutoka<br />

Kyela, Mbeya alikuwa na zao la<br />

mawese na kakao ambapo<br />

alisema usindikaji wa mawese<br />

unawezesha utengenezaji wa bidhaa<br />

mbalimbali muhimu kama vile sabuni<br />

ya kufulia na kuogea.<br />

Lain Mwakatundu<br />

“Vile vile kutokana na mawese<br />

unaweza kupata mbosa ambayo<br />

hutengeneza mafuta ya kupikia<br />

na kupaka. Mafuta haya ya kupaka<br />

yanafaida kubwa ikiwemo ya<br />

kuponya mba wa ngozi katika mwili<br />

wa binadamu. Aidha magamba ya<br />

mawese hutumika kwa ajili ya kuni.<br />

Kwa upande wa zao la kakao<br />

alisema lina matumizi mengi<br />

ingawaje matumizi yanayofahamika<br />

zaidi kwa watu ni utengenezaji<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 15<br />

Mwenyekiti wa <strong>MVIWATA</strong> Morogoro Bw. Stanford Chabonga aliyenyanyua juu kikombe, akiungwa mkono na wana-<strong>MVIWATA</strong> wenzake<br />

kusherehekea ushindi<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011


Inatoka uk. wa <strong>14</strong><br />

wa kinywaji na kitafunwa aina ya<br />

chocolate. Akaongeza kuwa “ndani<br />

ya tunda la kakao kuna mbegu zenye<br />

ladha ya sukari ambazo hutumika<br />

kutengeneza juisi lakini pia juisi hiyo<br />

waweza kuichachusha na kupata<br />

kilevi baada ya kuiweka kwa muda<br />

wa siku tatu hadi nne.”<br />

“Mbegu hizi za kakao pia<br />

zikikaushwa na kusagwa hupatikana<br />

unga laini ambao unafaa kwa<br />

matumizi mengi ikiwemo kuweka<br />

kama kiungo kwenye mboga na<br />

wengine hutafuna unga pekee maan<br />

unaradha nzuri,” anafafanua.<br />

Bibi. Mwakatundu anafafanua zaidi<br />

kuwa zao la kakao ni dawa nzuri<br />

ya kupunguza kasi ya ugonjwa wa<br />

kisukari mwilini na pia hupunguza<br />

mafuta ndani ya mwili wa binadamu,<br />

hivyo anawahimiza watanzania<br />

kulitumia zaidi.<br />

Anaeleza kuwa katika mkoa wa<br />

Mbeya hususan wilaya ya Kyela mazao<br />

ya Kakao na Mawese hulimwa kwa<br />

ajili ya chakula na biashara japokuwa<br />

soko lake kwa sasa siyo zuri. Hata<br />

hivyo anaongeza kuwa maonesho ya<br />

mwaka huu yamemsaidia kupanua<br />

wigo wa soko kwani hivi sasa<br />

amepokea maombi ya wateja wengi<br />

wanaohitaji bidhaa na wengine<br />

wameomba aende kuwafundisha<br />

kilimo cha mazao hayo.<br />

Tiba asili<br />

Mzee Hassan Nundu kutoka<br />

kijiji cha Chamkoroma wilaya ya<br />

Kongwa - Dodoma, yeye alionesha<br />

dawa za asili zinazotokana na<br />

magome na mizizi ya miti ambazo<br />

zinaaminika kutibu magonjwa<br />

mbalimbali ya binadamu kama vile<br />

meno, tumbo, athma pamoja na<br />

kideri cha kuku.<br />

Akielezea matibabu ya ugonjwa<br />

wa vidonda vya tumbo, anasema<br />

mgonjwa anayetumia dawa hiyo<br />

anapona kwa muda mfupi hata kama<br />

vidonda ni vya muda mrefu. “Dawa<br />

hii ambayo ni mchanganyiko wa<br />

mizizi ya miti mbalimbali, mtumiaji<br />

huchanganya na maziwa mabichi<br />

kwa kuweka kijiko kimoja cha<br />

dawa katika kikombe cha maziwa<br />

na kunywa mara tatu kwa siku kwa<br />

muda wa siku kumi na tano tu.”<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />

“Dawa nyingine ni ya fangasi<br />

ambapo fangasi hawa huwa tumboni<br />

na kwenye mapacha ya vidole vya<br />

miguu kutokana na joto linalokuwepo<br />

ndani ya kiatu kufuatia msuguano<br />

wa miguu ya mtu anapotembea.<br />

Dawa hii ya unga inampasa mgonjwa<br />

kuiweka kwenye maji baridi na kisha<br />

kuichuja ili kupata mabaki ambayo<br />

atayapaka sehemu zilizoathirika na<br />

baadaye kunywa dawa iliyochujwa<br />

mara tatu kwa siku kwa muda wa<br />

siku tatu na atapona kabisa.”<br />

Bw. Nundu anafafanua kuwa<br />

athma ni ugonjwa ambao hauna tiba<br />

hospitalini bali hutulizwa lakini yeye<br />

anayo dawa ya kutibu ugonjwa huu<br />

ambayo inapatikana kwenye vipaketi<br />

vitatu. Mgonjwa anapaswa kuiloweka<br />

na kuichuja kisha kunywa mara mbili<br />

kwa siku asubuhi na jioni.<br />

“Ninawashauri Watanzania<br />

kurudia dawa zao za asili<br />

zinazotokana na mizizi na magome<br />

ya miti kwani hazina kemikali<br />

zitakazowadhuru kiafya tofauti na<br />

dawa za hospitalini ambazo nyingi<br />

sasa ni bandia na kuongeza kuwa<br />

anazo dawa nyingi za asili zinazotibu<br />

maradhi ambayo hayawezi kutibiwa<br />

hospitalini kama vile kukojoa<br />

kitandani pamoja na meno ambayo<br />

mara nyingi hung’olewa badala ya<br />

kutibiwa.<br />

Mzee Nundu anasema maonesho<br />

ya NaneNane ambayo amekuwa<br />

akishiriki yanamsaidia kupata wateja<br />

wapya na kukutana na wagonjwa<br />

aliowatibu miaka ya nyuma ambao<br />

wanashuhudia kuponywa na dawa<br />

zake.<br />

Bibi Hortenzia Thomas kutoka<br />

kijiji cha Nyandira Mvomero, mkoani<br />

Morogoro alifika katika maonesho<br />

hayo kutangaza tiba asili itokanayo<br />

na matunda na mbogamboga<br />

zikiwemo njegere, sereri, cornflower,<br />

maharagwe, redishi, boga, nzukini,<br />

pasili na kabichi.<br />

Anaeleza kuwa kabichi huponya<br />

ugonjwa wa kisukari. Hii ni baada ya<br />

mgonjwa kuchukua mti wa katikati ya<br />

kabichi kuukatakata na kuuchemsha,<br />

kisha kunywa maji yake mara tatu<br />

kwa siku. Pia mboga mboga kama<br />

Radishi na tenepsi hutumika kutibu<br />

vidonda vya tumbo na shinikizo la<br />

damu.<br />

KUTOKA MITANDAONI<br />

Bibi Mwajuma Mwiyoha,<br />

ni mkulima kutoka Chamkoroma<br />

ambaye alifika kwenye maonesho<br />

haya akiwa na zao la Alizeti ambalo<br />

ni maarufu kwa kutengeneza mafuta<br />

ya kupikia. Hata hivyo, kwa mkulima<br />

huyo zao la Alizeti siyo kwa ajili<br />

ya kukamua mafuta pekee bali pia<br />

hulitumia kutengeneza dawa ya<br />

kuhifadhia mazao galán, dawa ambayo<br />

haina madhara kwa watumiaji.<br />

Mwajuma Mwiyoha<br />

“Dawa hii ya kuhifadhia mazao<br />

hutokana na masuke ya alzeti<br />

hutengenezwa kwa teknolojia<br />

rahisi tu ambayo mkulima yeyote<br />

anaweza kumudu kwani cha kufanya<br />

ni kuyachoma masuke ya alizeti<br />

kwenye chombo kisafi, yakishaungua<br />

vizuri hutwangwa na kuchekechwa<br />

ili kupata majivu laini ambayo<br />

ndio dawa yenyewe. Dawa hii<br />

hunyunyizwa juu ya magunia yenye<br />

mazao na ina uwezo wa kuzuia<br />

mazao yasishambiliwe na wadudu<br />

kwa muda wa miaka miwili hadi<br />

mitatu.<br />

Bibi. Mwiyoha anasema dawa hii<br />

ni nafuu kwani haimwingizii mkulima<br />

gharama na ni salama kwa afya ya<br />

binadamu.<br />

Ufugaji wa nyuki wadogo<br />

Bw. Hassan Haji kutoka Zanzíbar<br />

ni mkulima mdogo anayefuga nyuki<br />

wadogo wasiouma.<br />

Mkulima huyu ameanza ufugaji wa<br />

nyuki wasiouma miaka 15 iliyopita.<br />

Alianza ufugaji wa nyuki hao kama<br />

mradi wa kiuchumi lakini pia kwa<br />

lengo la kuwahifadhi baada ya kuona<br />

kwamba wako hatarini kutoweka<br />

kutokana ukataji wa miti katika<br />

maeneo ya misitu vitendo ambavyo<br />

vinawafanya viumbe hao kukimbia<br />

na hivyo kizazi hicho kupotea.<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 17<br />

15


KUTOKA MITANDAONI<br />

16<br />

Ludewa wahimizwa kuwekeza<br />

kwenye kilimo cha miti<br />

Na Susuma Susuma, Ludewa<br />

Wakulima wilayani<br />

Ludewa na nchini kote<br />

wametakiwa kuwekeza<br />

zaidi katika upandaji wa miti<br />

kibiashara ili kuhifadhi mazingira<br />

na kujiongezea kipato kutokana<br />

na soko la miti kuongezeka kila<br />

mwaka.<br />

Wito huo umetolewa na Naibu<br />

Mkurugenzi wa Shirika la Swedish<br />

Cooperative Center (SCC) Kanda<br />

ya Mashariki mwa Afrika Bw. George<br />

Onyango alipokuwa akizungumza na<br />

wakulima wa kata za Mlangali na<br />

Milo wilayani Ludewa katika mkoa<br />

mpya wa Njombe.<br />

Bw. Onyango alikuwa kwenye<br />

ziara ya kukagua maendeleo ya<br />

mradi wenye lengo la kuwawezesha<br />

wakulima wadogo kuwa na uzalishaji<br />

wenye kukuza na kuongeza kipato<br />

na uhifadhi wa mazingira na bioanuai<br />

Uharibifu<br />

huu tuliufanya sisi katika<br />

harakati za kujitafutia riziki, na<br />

tunaoathirika na uharibifu huu ni sisi, hivyo<br />

ni sisi wenyewe ndiyo tunapaswa kurejesha<br />

uhai wa mazingira yetu kwa kuwekeza kwenye<br />

upandaji miti na kwa kufanya hivi tutasaidia<br />

kupunguza athari za mabadiliko ya<br />

tabia ya nchi<br />

k a t i k a<br />

Ziwa Nyasa unaotekelezwa na<br />

Mtandao wa Vikundi vya Wakulima<br />

Wadogo Tanzania (<strong>MVIWATA</strong>) kwa<br />

kushirikiana na SCC.<br />

Bw. Onyango alisema biashara ya<br />

miti na mazao yake, inakuwa kila siku<br />

na kupanda bei, hivyo kwa kuwekeza<br />

zaidi kwenye upandaji miti wakulima<br />

hao watapata mapato mazuri kuliko<br />

hata wanayoyapata kwenye mazao<br />

Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Swedish Cooperative Center (SCC) Kanda ya Mashariki mwa<br />

Afrika Bw. George Onyango (aliyenyosha mkono) akizungumza na wakulima wa kata ya Mlangali<br />

ya chakula wanayolima.<br />

Aidha aliwataka wakulima hao<br />

kuunda mitandao imara itakayofanya<br />

kazi ya kutafuta na kusimamia soko<br />

la mazao ya miti ili kuondokana na<br />

walanguzi ambao sasa wananeemeka<br />

kwenye biashara ya mazao ya chakula<br />

ya wakulima.<br />

Naibu mkurugenzi<br />

huyo alisema licha ya<br />

kuwaingizia utajiri,<br />

kilimo cha miti<br />

kitasaidia kwa<br />

kiwango kikubwa<br />

katika utunzaji<br />

wa mazingira ya<br />

wilaya hiyo ambayo<br />

yameharibiwa kutokana<br />

na shughuli za kibinadamu<br />

zikiwemo ukataji miti kwa ajili ya<br />

kupata nishati ya mkaa na kuni.<br />

“Uharibifu huu tuliufanya sisi<br />

katika harakati za kujitafutia riziki,<br />

na tunaoathirika na uharibifu<br />

huu ni sisi, hivyo ni sisi wenyewe<br />

ndiyo tunapaswa kurejesha uhai<br />

wa mazingira yetu kwa kuwekeza<br />

kwenye upandaji miti na kwa kufanya<br />

hivi tutasaidia kupunguza athari za<br />

mabadiliko ya tabia ya nchi,” alisema<br />

Bw. Onyango.<br />

Aliwahimiza wakulima hao<br />

kutumia vyema elimu ya uhifadhi wa<br />

mazingira, ujasiriamali na usimamizi<br />

wa vikundi inayotolewa kupitia<br />

mradi huo.<br />

Kwa upande wake afisa<br />

anayesimamia mradi huo wilayani<br />

Ludewa Bw.Remmy Urio alisema<br />

matokeo ya mafunzo yaliyotolewa<br />

kwa wakulima yameanza kuonekana<br />

baada ya wengi wao kuanza kupanda<br />

miti kwenye maeneo ya wazi na<br />

wameimarisha usimamizi wa sheria<br />

zinazolinda mazingira.<br />

Bw. Urio alisema wakulima wengi<br />

pia wameibua miradi ya kiuchumi<br />

ikiwemo uanzishaji wa SACCOS<br />

ili kuwawezesha kuboresha kipato<br />

badala ya kutegemea kipato kutoka<br />

kwenye kazi zinazochangia uharibifu<br />

wa mazingira.<br />

Afisa Programu wa <strong>MVIWATA</strong><br />

Bw. Laurent Kaburire alisema, utafiti<br />

uliofanywa na <strong>MVIWATA</strong> kwenye<br />

wilaya zinazounganishwa na Ziwa<br />

Nyasa kwa upande wa Tanzania,<br />

umebaini kwa shughuli nyingi<br />

zinazoathiri ziwa zinatekelezwa<br />

na wavuvi, wafugaji na wakulima<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 17<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011


Maonesho ya NaneNane 201...<br />

Inatoka uk. wa 15<br />

Miongoni mwa faida anazozipata<br />

Bw. Haji ni pamoja na kujipatia kipato<br />

kwa ajili ya familia yake kwani kwa<br />

sasa anao wateja wengi wanaotumia<br />

asali ya nyuki hawa wasiouma na<br />

kwamba asali yake ina soko zuri. Kwa<br />

sasa ana jumla ya mizinga 20 ya nyuki<br />

ingawaje changamoto anayokutana<br />

nayo katika kupanua ufugaji huo ni<br />

ugumu kuwapata kutoka msituni<br />

kwani huwa wanajificha sana.<br />

“Ninawashauri watanzania<br />

kupenda kutumia zaidi asali kwani ni<br />

kinga ya maradhi mengi kwenye mwili<br />

wa binadamu. Hiki ni chakula kizuri<br />

mno hasa kwa watoto, nawaambia<br />

wazazi wasiwape watoto pia badala<br />

yake wawape asali,” anasisitiza.<br />

<strong>Uk</strong>aushaji matunda na<br />

mbogamboga<br />

Bw. Zuberi Sultani kutoka<br />

Korogwe Tanga kwenye maonesho<br />

haya yeye alionesha utaalamu<br />

wa kuhifadhi matunda na<br />

mboga mboga kwa njia<br />

ya ukaushaji. Miongoni mwa<br />

matunda yanayosindikwa ndizi,<br />

mananasi, maembe pamoja na<br />

zikiwemo mbogamboga kama vile<br />

mchunga na kisamvu.<br />

Anafafanua kuwa usindikaji wa<br />

matunda na mboga unafanyika ili<br />

kuyahifadhi na kutumika kwa msimu<br />

wote wa mwaka, wakulima wengi<br />

wa matunda hawanufaiki na kilimo<br />

hicho kwa sababu msimu wa mavuno<br />

matunda hushuka bei na mengine<br />

kuoza kwa kuwa wakulima hawana<br />

ujuzi wa kuyahifadhi.<br />

Anasema ukaushaji huu hutumia<br />

teknolojia rahisi, ambayo yeye<br />

amekuwa akiwafundisha wakulima<br />

wenzake bure ili nao wanufaike.<br />

“Tunakausha kwa kutumia chombo<br />

maalum ambacho hufunikwa na<br />

turubali jeusi juu kwa lengo la<br />

kupunguza ukali wa mionzi ya jua<br />

na kuhakikisha kwamba haileti<br />

madhara kwa watumiaji. Matunda<br />

haya yanapokaushwa huzidishiwa<br />

ubora kwani sukari yake huongezeka<br />

mara dufu ukilinganisha na tunda<br />

linavyokuwa katika hali ya kawaida.”<br />

“Mtanzania yeyote anaweza<br />

kusindika matunda na hata mboga<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />

kwani si kazi ngumu bali inahitaji<br />

usafi na uangalifu wa karibu ili<br />

kuhakikisha bidhaa inakuwa katika<br />

kiwango cha juu cha ubora ili isilete<br />

madhara kwa binadamu,” anaeleza.<br />

Bw. Sultani anasema kwamba<br />

utaratibu wa kusindika matunda<br />

huanzia katika utafutaji wa matunda<br />

mazuri yaliyoiva kiasi, unayaosha<br />

kuyakata vipande vidogo vinavyoweza<br />

kukauka upesi, kisha kuyaweka<br />

kwenye chombo kinachotumia<br />

mwanga wa jua kukaushia na<br />

baada ya hapo huhifadhiwa kwenye<br />

vifungashio maalum tayari kwa<br />

kuuzwa.<br />

Utaratibu huu unafanana vile vile<br />

katika mboga za majani ambapo<br />

huoshwa na kuchemshwa kidogo<br />

jikoni kisha huanikwa katika<br />

chombo kinachotumia mwanga wa<br />

jua kukaushia mazao na baada ya<br />

kukauka huwa tayari kufangashwa<br />

kwa ajili ya kuuzwa ama kuliwa.<br />

Usindikaji zao la Muhogo<br />

Bw. Juma Nyamgunda kutoka<br />

Mkuranga Pwani anasema katika<br />

kuhakikisha kwamba zao hili la<br />

muhogo linaongezewa thamani<br />

wakulima wa Mkuranga wameanza<br />

kusindika muhogo na kupata unga<br />

ambao huutumia katika kutengeneza<br />

Watazamaji wakitoka kwenye banda la <strong>MVIWATA</strong><br />

KUTOKA MITANDAONI<br />

vitu mbalimbali ikiwemo keki, biscuti,<br />

tambi, chinchin, chapati na maandazi<br />

kazi ambayo hufanywa kwa wingi na<br />

kina mama kwa lengo la kuongeza<br />

kipato cha familia.<br />

Bw. Nyamgunda anasema<br />

usindikaji unawapa faida kubwa<br />

wakulima ukilinganisha na<br />

walivyokuwa wakiuza muhogo ghafi<br />

kwa walanguzi na katika maonesho<br />

ya NaneNane amepata wateja wengi<br />

wanaohitaji kiwango kikubwa cha<br />

unga wa muhogo.<br />

Ludewa<br />

wahimizwa...<br />

Inatoka uk. wa 16<br />

wadogo ambao kipato chao ni<br />

kidogo ama cha wastani.<br />

Alisema katika hatua ya awali ya<br />

miaka mitatu ya majaribio, mradi<br />

unatekelezwa kwenye wilaya mbili<br />

ambazo ni Kyela mkoani Mbeya na<br />

Ludewa mkoani Njombe. Katika<br />

hatua ya pili ya mradi utajumuisha<br />

wilaya za Mbinga mkoani Ruvuma<br />

na Makete mkoani Njombe.<br />

Kwa ujumla mradi unalenga<br />

kuwafikia na kuwanufaisha<br />

wakulima,wafugaji na wavuvi<br />

wapatao 15,000 wa hapa nchini.<br />

17


MAKALA<br />

Mtweve: Ubunifu wangu wa redio<br />

umenufaisha wengi<br />

Anamiliki Mlangali Coconut FM<br />

Hatimaye ndoto ya siku<br />

nyingi ya Bw. Ditrick<br />

Mtweve (<strong>18</strong>) mkazi wa<br />

Kata ya Mlangali wilayani Ludewa<br />

mkoa mpya wa Njombe imeweza<br />

kutimia baada ya kutumia ubunifu<br />

wake kutengeneza mtambo wa<br />

redio unaowanufaisha wakazi<br />

wengi wa wilaya hiyo.<br />

Mtambo huo uliotokana na<br />

kuunganishwa kwa vifaa mbalimbali<br />

kutoka katika redio mbovu na vifaa<br />

vinginevyo kama miti ya mianzi,<br />

boksi na vyuma vya baiskeli, ulianza<br />

kurusha matangazo yake mwaka jana<br />

katika kijiji cha Lufumbu na kwa sasa<br />

matangazo hayo yanawafikia wakazi<br />

wa vijiji sita katika Kata ya Mlangali.<br />

Kwa sasa redio hii ambayo ameipa<br />

jina la ‘Mlangali Coconut FM’ imekuwa<br />

ikitumiwa na viongozi wa vijiji vya<br />

kata ya Mlangali kutangaza taarifa<br />

muhimu kama vile mikutano ya<br />

vijiji, kampeni ya chanjo pia shughuli<br />

muhimu za kijamii.<br />

Vile vile imekuwa kichocheo<br />

kikubwa cha biashara na burudani<br />

kwani watu binafsi hutumia redio<br />

hiyo kutangaza biashara na huduma<br />

wanazotoa bila kusahau wapenzi wa<br />

muziki wa kisasa na nyimbo za injili<br />

ambao pia hupata fursa ya kupiga simu<br />

Mwanachama na mhamasishaji wa <strong>MVIWATA</strong> Mlangali akizungumza kwenye kipindi cha<br />

karibu mgeni<br />

<strong>18</strong><br />

na kuchagua wimbo waupendao.<br />

Bw. Mtweve ambaye ni mtoto<br />

pekee kwenye familia na yatima<br />

(aliyefiwa na baba) alisema kuwa<br />

alitamani siku moja katika maisha<br />

yake awe mtangazaji maarufu<br />

wa redio kubwa hapa nchini na<br />

ikiwezekana aweze kumiliki redio<br />

yake mwenyewe na mapema mwaka<br />

2009 akiwa kidato cha tatu katika<br />

Shule ya Sekondari ya Lufumbu<br />

ndoto yake ilianza kutimia ambapo<br />

kwa kutumia maarifa madogo<br />

aliyoyapata shuleni alianza kubuni na<br />

kutengeneza mtambo huo wa redio.<br />

“Wakati naanza ilikuwa kama<br />

mchezo, kwanza nilichukua muda<br />

nikitafakari kwanini ‘Microphone’<br />

zisizo na waya zinasafirisha sauti<br />

na kuupeleka katika mitambo.<br />

Baadaye nilichukua kifaa ‘transistor’<br />

kilichotumika katika ‘Microphone’<br />

hizo na vifaa vingine nilivichukua<br />

katika redio mbovu na kuviunganisha,”<br />

alisema Bw. Mtweve.<br />

Baada ya kukusanya vifaa<br />

mbalimbali kutoka kwenye redio<br />

mbovu na maeneo mengine pia<br />

alitumia betri za kawaida hatimaye<br />

kufanikiwa kuwasha mtambo wake<br />

na redio yake kuanza kusikilizwa na<br />

wananchi waishio jirani.<br />

Uwezo huu wa redio kusikilizwa<br />

na watu wa jirani ulianza baada ya<br />

kuboresha baadhi ya vifaa vyenye<br />

uwezo mkubwa zaidi ili kuwezesha<br />

mawimbi ya sauti kufika mbali zaidi na<br />

hatimaye alifanikiwa kufunga mnara<br />

wa mlingoti wa miti iliyounganishwa<br />

wenye antena ya waya wa kawaida<br />

juu yake na kuutundika juu ya<br />

kilele cha mlima uliokuwa jirani na<br />

nyumbani kwao.<br />

“Haikuwa kazi ndogo kwani<br />

mwanzoni niliweka mtambo huu<br />

nyumbani kwetu ambako ni bondeni<br />

ikawa inasikika nyumba kadhaa za<br />

jirani tu. Ilibidi kutumia muda mwingi<br />

na kuumiza akili ili kuweza kufikia<br />

mafanikio, baadaye nikapata wazo<br />

la kuhamia hapa mlimani kwenye<br />

nyumba ya rafiki yangu ambaye<br />

amenipangishia chumba kimoja,”<br />

alisema Bw. Mtweve alipozungumza<br />

na Pambazuko ndani ya studio yake<br />

kijijini Lufumbu.<br />

Bw. Mtweve alisema anafurahia<br />

ubunifu wake lakini bado anakabiliwa<br />

na changamoto nyingi sana ikiwemo<br />

kutokujua sheria “mpaka sasa redio<br />

hii naimiliki kienyeji kwa lengo la<br />

kukuza kipaji changu na kuiwezesha<br />

jamii inayonizunguka kunufaika na<br />

kipaji hicho, sijui taratibu za kuisajili<br />

zikoje,” alisema Bw. Mtweve.<br />

Tatizo jingine ni kukosa mtaji wa<br />

kuweza kununua vifaa vya kisasa na<br />

kuwa na jengo maalumu la studio ya<br />

utangazaji.<br />

Kwa hivi sasa Bw. Mtweve anaishi<br />

na mama yake baada ya baba yake<br />

kufariki wakati yeyé akiwa na umri<br />

wa miaka 10 na alikuwa akisoma<br />

darasa la tatu wakati huo.<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 19<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011


Inatoka uk. wa <strong>18</strong><br />

Alisema hali hiyo ya kubakia na<br />

mzazi mmoja imechangia kwa kiasi<br />

kikubwa umasikini katika familia<br />

yao baada ya mama yake kutokuwa<br />

na uwezo wa kifedha na hata afya<br />

yake kutokuwa thabiti kutokana<br />

na maradhi yanayomsumbua na<br />

hivyo wakati mwingine hulazimika<br />

kusimamisha kazi za redio ili<br />

kumsaidia mama yake shughuli za<br />

shamba.<br />

“Redio hii huwa hewani kwa<br />

masaa 24 kila siku kwa kurusha<br />

muziki hewani na salamu, short<br />

time za muziki wa bongo flava na<br />

chaguo la msikilizaji, na inapofika<br />

4.00 usiku hurudi nyumbani na<br />

kuuacha mtambo ukipiga muziki<br />

mpaka alfajiri ninapoingia kuendelea<br />

na vipindi,” alisema Bw. Mtweve.<br />

Awali kabla ya kufikia kiwango<br />

cha kurusha matangazo saa 24,<br />

alikuwa akitumia redio inayotumia<br />

kanda za kawaida na baadaye alipata<br />

redio yenye kutumia ‘memory card’<br />

ambayo imekuwa ikimwezesha<br />

kupiga muziki muda wote.<br />

Hata hivyo eneo hili la Mlangali<br />

bado halijafikwia na huduma ya<br />

umeme wa Tanesco hali inayomlazimu<br />

kutumia betri za kawaida za<br />

redio kuendeshea mtambo wake.<br />

“Nimekuwa nikiwategemea watu<br />

mmoja mmoja ambao wanavutiwa<br />

na huduma hii, kuninunulia betri,<br />

kuna wakati zinapoisha na hakuna<br />

mtu wa kununua ninalazimika kuzima<br />

matangazo kwa siku kadhaa, hadi<br />

ninapoenda kufanya kibarua mahali<br />

Afisa programu wa <strong>MVIWATA</strong> Bw. Laurent Kaburire akimtambulisha Bw.Ditrick Mtweve kwa<br />

wajumbe wa Mkutano Mkuu wa 16 wa <strong>MVIWATA</strong> Oktoba 24, 2011 mjini Morogoro<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />

Hii ndiyo mitambo ya kurusha matangazo<br />

ya COCONUT FM<br />

na kupata fedha, nitafurahi kama<br />

kijijini kwetu tutapata umeme.”<br />

Wakazi wa vijiji vya kata hiyo<br />

ambao hawakuwa wakimiliki<br />

redio majumbani mwao kwa sasa<br />

wameanza kumiliki redio na kusikia<br />

matangazo na burudani kutoka<br />

katika mtambo wa redio ya kijana<br />

huyo.<br />

Wafanyabiashara wa Mlangali nao<br />

kwa uchache wameanza kuitumia<br />

fursa ya redio hii kujitangaza na<br />

humlipa kati ya Sh 500 na 1,000 ili<br />

kuweza kurushiwa matangazo yao<br />

redioni kwa siku kiwango ambacho<br />

kijana huyo anasema kuwa kimekuwa<br />

kikimsaidia kwa mahitaji binafsi yeye<br />

na mama yake.<br />

Anasema hata hivyo kuwa kwa<br />

sasa yeye ndiye mtangazaji na fundi<br />

mitambo wa redio hiyo. Anawaomba<br />

wananchi wenye uwezo na ambao<br />

wanaguswa na kipaji chake kumsaidia<br />

kuweza kwenda kusoma katika chuo<br />

cha ufundi stadi (Veta) ili kuongeza<br />

maarifa.<br />

Sambamba na hilo, kijana huyu<br />

anaeleza kuwa kamwe ndoto zake<br />

MAKALA<br />

hazitaishia hapo, bali ataendelea<br />

kubuni mbinu mbalimbali na<br />

kuboresha kazi yake hiyo na kiu<br />

yake ni kuona siku moja redio hiyo<br />

inasikika katika wilaya nzima ya<br />

Ludewa.<br />

Bw. Mtweve anaishukuru jamii<br />

inayomzunguka kwani pamoja na<br />

kukosa fedha sambamba na ufinyu wa<br />

elimu ya ufundi alionayo, bado jamii<br />

hiyo imekuwa msaada mkubwa sana<br />

kwake kwani wameweza kutambua<br />

umuhimu wake katika jamii kwa<br />

kumpati redio mbovu ili aweze kutoa<br />

vifaa muhimu kwa kazi yake.<br />

Hii ndiyo studio ya COCONUT FM<br />

Kwa kutambua mchango mkubwa<br />

anaoutoa katika kuhakikisha jamii ya<br />

vijijini inafikiwa na habari, Mtandao<br />

wa Vikundi vya Wakulima Tanzania<br />

(<strong>MVIWATA</strong>), ulimwalika Bw. Mtweve<br />

na kuwezesha kushiriki kwenye<br />

Warsha ya Kitaifa na Mkutano Mkuu<br />

wa 16 wa <strong>MVIWATA</strong> uliofanyika<br />

Oktoba 24 na 25, 2011 mjini<br />

Morogoro.<br />

Mojawapo ya mada iliyojadiliwa<br />

kwenye warsha hiyo na kugusa hisia<br />

ni “haki ya upatikanaji wa<br />

habari vijijini” ambapo wakulima<br />

kutoka vijiji mbalimbali walieleza<br />

jinsi ambavyo wanakabiliwa na<br />

changamoto katika kupokea na<br />

kutoa habari katika kutokana na<br />

vyombo vingi vya habari kuegemea<br />

zaidi mijini.<br />

Hivyo washiriki hao walipongeza<br />

ubunifu wa kijana huyo na kuomba<br />

<strong>MVIWATA</strong> kama taasisi kuendelea<br />

kumuunga mkono na kumtumia<br />

kutangaza zaidi habari za wakulima.<br />

Jambo hilo limetekeleza na hivi sasa<br />

baadhi ya vipindi vya SAUTI YA<br />

<strong>MVIWATA</strong> vinarushwa kupitia redio<br />

hiyo Mlangali Coconut FM.<br />

19


KUTOKA MITANDAONI<br />

Viongozi wa masoko ya wakulima<br />

wapewa ushauri<br />

Na Susuma Susuma, Morogoro<br />

Viongozi wa masoko ya<br />

wakulima wametakiwa<br />

kutojenga uhasama na<br />

viongozi wa awamu zilizopita bali<br />

wawatumie kujifunza na kupata<br />

mbinu za kuyafanya masoko hayo<br />

kuwa endelevu.<br />

Wito huo umetolewa Julai<br />

30,2011 mjini Morogoro na<br />

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi<br />

wa Soko la Wakulima la Kibaigwa<br />

Kongwa mkoani Dodoma Bw.<br />

Richard Kapinye kwenye kikao cha<br />

pamoja cha wakurugenzi wa bodi<br />

za masoko sita yaliyojengwa na<br />

<strong>MVIWATA</strong> kwenye vijiji mbalimbali<br />

hapa nchini.<br />

Bw. Kapinye alisema “tuepuke<br />

uhasama unaofanywa na wanasiasa<br />

kwamba akishamuondoa mwenzake<br />

madarakani wanakuwa maadui<br />

wanaotafuta kuharibiana kila wakati,<br />

sisi tuwe tofauti tuwatumieni<br />

wenzetu waliotutangulia ili tuweze<br />

kufanikiwa.”<br />

Kadhalika Bw. Kapinye ambaye<br />

pia ni mkulima mdogo na Diwani<br />

wa Kata ya Kibaigwa, aliwataka<br />

wajumbe wenzake kutumie<br />

vyema dhamana waliyopewa kwa<br />

20<br />

kusimamia haki na maslahi ya<br />

wakulima huku akitahadharisha<br />

tabia inayojitokeza ya baadhi ya<br />

wakulima wanaopata nyadhifa za<br />

kisiasa, kusahau walikotoka na<br />

kuanza kuwakandamiza wenzao.<br />

Akawahimiza pia wakulima ili<br />

kupanua uelewa wawe na hamasa<br />

ya kujifunza mambo mapya kwa<br />

kusoma magazeti na machapisho<br />

mengine likiwemo jarida la wakulima<br />

la Pambazuko (Sauti ya Wakulima)<br />

linalochapishwa na <strong>MVIWATA</strong>.<br />

Kwa upande wake mratibu wa<br />

kikao hicho ambaye pia ni Afisa<br />

Masoko wa <strong>MVIWATA</strong> Bw. Jimmy<br />

Mongi aliwahimiza wakurugenzi hao<br />

wa bodi, wawatumie wajumbe wenye<br />

uzoefu walioko masoko ya jirani ili<br />

kuwafundisha na kuwajengea uwezo<br />

wajumbe wapya wanaochaguliwa.<br />

“Tunaamini kuwa wajumbe<br />

wa mwanzo kwenye bodi hizi,<br />

walijengewa uwezo mkubwa kielimu<br />

kwa kupelekwa ziara mbalimbali<br />

za mafunzo, hivyo tunapofikiria<br />

kupata mafunzo kwa wajumbe<br />

wapya tuwafikirie kwanza hawa,<br />

ni wenzetu watatupatia elimu<br />

hiyo kwa gharama ndogo na pale<br />

panapohitajika utaalamu zaidi ndipo<br />

tuombe msaada wa <strong>MVIWATA</strong> ofisi<br />

Kufunga mipaka ya kuuza mazao nje ya nchi<br />

kunamsababishia hasara mkulima<br />

Na Martin Pius, Babati<br />

Serikali imetakiwa kutotoa<br />

amri za kuzuia mazao ya<br />

chakula yakiwamo mahindi<br />

kuuzwa nje ya nchi kwani kufanya<br />

hivyo inawasababishia hasara<br />

wakulima na kuwakatisha tamaa<br />

ya kuongeza uzalishaji.<br />

Rai hiyo imetolewa Julai<br />

13, 2011 na Mjumbe wa Bodi<br />

ya Mtandao wa Jinsia Tanzania<br />

(TGNP), Bibi Rehema Mwateba<br />

wakati akifungua Mkutano Mkuu<br />

wa nne wa <strong>MVIWATA</strong> Manyara<br />

uliowashirikisha wanachama wa<br />

wilaya tano za mkoani Manyara.<br />

Bibi Mwateba alisema Serikali<br />

itambue kwamba inatumia mfumo<br />

kandamizi kwa mkulima kwa kufunga<br />

mipaka ya kuuza mazao ndani na nje<br />

ya nchi bila ya kujali kuwa hilo ni<br />

hitaji la mkulima la kuendesha maisha<br />

yake yanayotegemea hasa bei nzuri<br />

ya mazao. Alisema kuzuia biashara<br />

ya mazao kwa kutumia kisingizio cha<br />

kinga ya njaa hakitavumilika kwani<br />

wakati utafika wakulima watachukua<br />

kuu,” alisema Bw. Mongi<br />

Kwa upande wake Bibi.<br />

Honolata Blass, mjumbe wa bodi<br />

ya Soko la Nyandira alisema bodi<br />

za wakurugenzi zinapaswa kuwa<br />

na ubunifu ili kuongeza ufanisi wa<br />

masoko. “Kwa upande wetu ubunifu<br />

wa bodi umesaidia kuongeza mapato<br />

ya soko kila mwaka na kulifanya soko<br />

kuwanufaisha wakulima wengi,”<br />

alisema Bibi Blass.<br />

Bodi hizo za wakurugenzi wa<br />

masoko hukutana mara kwa mara<br />

kwa lengo la kuwapa wadau hao<br />

fursa ya kushirikishana uzoefu wa<br />

mafanikio, changamoto na kuweka<br />

mikakati ya uendelevu wa masoko<br />

hayo ya wakulima.<br />

Kikao hiki kilikutanisha<br />

wakurugenzi 25 wa bodi za masoko<br />

ya Kibaigwa wilaya ya Kongwa,<br />

Nyandira wilayani Mvomero, Tandai<br />

na Tawa Morogoro Vijijini, Mkata<br />

wilaya ya Handeni na Igagala wilayani<br />

Njombe.<br />

Masoko hayo yalijengwa na<br />

<strong>MVIWATA</strong> tangu mwaka 2004 na<br />

kukabidhiwa kwa halmashauri za<br />

wilaya na uendeshaji wake kubakia<br />

mikononi mwa bodi za wakurugenzi<br />

ambazo zinaundwa na wakulima na<br />

wawakilishi wa halmashauri.<br />

hatua ambazo huenda zikawa na<br />

madhara makubwa kwa taifa.<br />

“Serikali inatakiwa kufanya<br />

utafiti wa haraka kubaini maeneo<br />

yaliyoathirika na njaa na kupeleka<br />

chakula cha msaada na kwa maeneo<br />

mengine yasiyokuwa na uhaba wa<br />

chakula wakulima waruhusiwe<br />

kuuza mazao yao nje ya nchi ili<br />

kuweza kupata faida,” alisema.<br />

Makamu Mwenyekiti wa<br />

<strong>MVIWATA</strong> Manyara, Bibi Fatuma<br />

Kimolo, akizungumza kwenye<br />

mkutano huo alisema kama serikali<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 21<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011


Wakulima washauriwa wasidai<br />

posho za mafunzo<br />

Na Ledis Kigala, Kyela<br />

Baadhi ya wakulima wilayani<br />

Kyela mkoani Mbeya<br />

wamewaasa wenzao<br />

kutanguliza mbele manufaa ya<br />

elimu wanayopata katika kshiriki<br />

kwao kwenye mafunzo badala ya<br />

kudai posho.<br />

Wamesema mtindo wa kudai<br />

posho kwanza, unawafanya wakulima<br />

kushindwa kupata elimu muhimu<br />

kwa ustawi wa maisha yao.<br />

Walitoa wito huo wakati wa<br />

kufunga mafunzo ya kuwajengea<br />

uwezo katika uzalishaji bora wa<br />

mazao ya mpunga, mahindi, kokoa<br />

na ufugaji wa wanyama.<br />

Mmoja wa wakulima hao Bw.<br />

Goden Mwantimwa wa kijiji cha<br />

Lutusyo kata ya Muungano wilayani<br />

Kyela alieleza kufurahishwa na<br />

elimu na mafunzo yanayoendelea<br />

kutolewa na Mtandao wa Vikundi<br />

vya Wakulima Tanzania (<strong>MVIWATA</strong>)<br />

na kuahidi kuwa ataendelea kushiriki<br />

kwa sababu kwake elimu ni muhimu<br />

kuliko posho.<br />

“Mimi niko tayari kujitolea<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />

kushiriki mafunzo mengine hata kama<br />

itakuwa nje ya hapa, nawaombeni<br />

wenzangu tuithamini sana elimu hii<br />

ili itusaidie katika kuboresha kilimo<br />

chetu,” alisema Bw. Mwantimwa.<br />

Kwa upande wake Bw. Musa<br />

Mwangongolo mkulima wa kijiji<br />

cha Makwale kata ya Makwale,<br />

alisema tabia ya kudai posho<br />

kutoka kwa waandaaji wa mafunzo<br />

imesababbisha wadau mbalimbali wa<br />

maendeleo kuwakimbia wakulima<br />

wa eneo hilo.<br />

Alisema matokeo yake ni<br />

waandaaji kuhamishia mafunzo hayo<br />

katika maeneo mengine na kuwaacha<br />

wakulima wa Kyela wakiwa hawana<br />

la kufanya.<br />

Alisema kimsingi wakulima siyo<br />

masikini wa kipato, na kwamba<br />

umasikini wao ni maarifa ambayo<br />

<strong>MVIWATA</strong> imeonyesha njia ili<br />

kufikia azma ya kuboresha kilimo ili<br />

kiwe chenye tija zaidi.<br />

Mafunzo hayo yaliyofanyika kuanzia<br />

tarehe Septemba 21 hadi Oktoba 11,<br />

2011 kwenye vijiji <strong>18</strong> vilivyoko kwenye<br />

kata 10 za wilaya ya Kyela yalilenga<br />

kuwapa elimu wakulima ya kuongeza<br />

Bibi Edina Mwakipesile mkulima wa kijiji cha Mwiyonde wilayani Kyela akielezea dhana<br />

ya <strong>MVIWATA</strong> kwa wakulima wenzake walioshiriki mafunzo ya kujengea uwezo vikundi,<br />

yaliyoandaliwa na <strong>MVIWATA</strong> mjini Kyela.<br />

KUTOKA MITANDAONI<br />

uzalishaji pamoja na ubora wa mazao<br />

na mifugo.<br />

Mafunzo hayo ni sehemu ya<br />

utekelezaji wa mradi wa Uhifadhi<br />

Mazingira na Kukuza kipato<br />

kwa wakulima wadogo waishio<br />

kandokando ya ziwa Nyasa,<br />

unaotekelezwa na <strong>MVIWATA</strong><br />

kwa ufadhili wa Shirika la Swedish<br />

Cooperative Center (SCC).<br />

Afisa Mradi huo Bw. Ledis Kigala,<br />

alisema, mradi huo unatekelezwa<br />

kwenye kata 10 kati ya kata 20<br />

za wilaya ya Kyela ambazo ni<br />

Bujonde, Ikolo, Ngonga, Ikimba,<br />

Katumbasongwe, Ipande, Mwaya,<br />

Ipinda, Muungano na Makwale.<br />

Kufunga mipaka ya kuuza<br />

mazao nje ya nchi...<br />

Inatoka uk. wa 20<br />

imeamua kufunga mipaka ya kuuza<br />

chakula inatakiwa sasa ijipange<br />

kununua mazao hayo ya wakulima<br />

kwa bei yenye tija badala ya<br />

kupanga bei yake isiyokuwa na<br />

maslahi kwa mkulima.<br />

Bibi Kimolo alisema kufungwa<br />

mipaka kipindi hiki kumesababisha<br />

bei ya mahindi kushuka kutoka<br />

Sh. 45,000 na kufikia Sh 30,000<br />

kwa gunia, hali ambayo inarudisha<br />

nyuma maendeleo ya mkulima.<br />

Alihoji kuwa iweje watumishi<br />

wa Serikali wapandishiwe<br />

mishahara kila mwaka kutokana<br />

na kupanda kwa gharama ya<br />

maisha, huku mkulima akiwekewa<br />

masharti ya kupata ujira stahiki ili<br />

aweze kukabiliana na hali ngumu ya<br />

maisha magumu kwa kuuza mazao<br />

kwenye soko lenye bei nzuri?<br />

Alisema umefika wakati sasa,<br />

serikali iache kutumia raslimali<br />

nyingi kwenye kutoa na kusimamia<br />

matamko ambayo hayana tija kwa<br />

ustawi wa wakulima badala yake<br />

nguvu na raslimali hizo zitumike<br />

kuimarisha miundombinu ya<br />

kilimo ili kiweze kuwa na uzalishaji<br />

wa kutosheleza mahitaji ya chakula<br />

na ziada ya biashara.<br />

21


KATUNI<br />

MUDA<br />

MREFU NAONA<br />

UNASOMA HILO<br />

GAZETI LINA<br />

HABARI GANI?<br />

WEWE UTAZI-<br />

PATA VIPI HABARI ZA<br />

MJINI WAKATI GAZETI<br />

LINACHUKUA SIKU 4<br />

KUFIKA HAPA<br />

22<br />

OH! KWELI NDIO<br />

SABABU<br />

AHA<br />

HAHA SIO HIVYO,<br />

NI MFUMO WA TAARIFA<br />

YA MASOKO <strong>MVIWATA</strong>.<br />

NAPATA TAARIFA KUPI-<br />

TIA SIMU YANGU YA<br />

MKONONI TU.<br />

AH! GAZETI<br />

LENYEWE LINA<br />

HABARI ZA MJINI TU,<br />

SIONI HATA HABARI<br />

INAYOGUSIA KERO<br />

ZETU.<br />

WAANDISHI<br />

WENGI WANAJI-<br />

SHUGHULISHA NA<br />

MAMBO YA MJINI<br />

TU.<br />

SI<br />

NINATUMIA<br />

SIMU YANGU YA<br />

MKONONI<br />

ONA<br />

SASA MIMI<br />

SIJUI HATA KUTUMIA<br />

HUO MTANDAO, HEBU<br />

FIKIRIA NI WATU WAN-<br />

GAPI HAWAPATI HIZO<br />

HABARI?<br />

HIVI KWANINI SISI<br />

WATU WA VIJIJNI<br />

HABARI ZETU<br />

HAZIANDIKWI?<br />

NDIO MAANA<br />

HAKUNA HABARI ZA<br />

KILIMO KWENYE<br />

MAGAZETI<br />

MENGI!<br />

YAANI<br />

UNAWAULIZA<br />

WATU WA MJINI KWA<br />

SIMU!?<br />

LAKINI MIMI NAONA BADO<br />

HIZO HABARI UNAZOPATA<br />

KWENYE SIMU HAZIZUN-<br />

GUMZII KILIMO<br />

NANI ATAKUJUA<br />

HUKU KIJIJINI<br />

HUKU<br />

HABARI ZI-<br />

TAFIKAJE<br />

HAPANA<br />

NATUMIA<br />

MTANDAO<br />

AH!<br />

MBONA<br />

MWAKA JANA<br />

WAANDISHI WALI-<br />

KUJA WENGI TU<br />

LAKINI<br />

MIMI NAPATA<br />

TAARIFA NYINGI ZA<br />

MASOKO YA MJINI<br />

KILA SIKU.<br />

HAWA<br />

WAANDISHI<br />

WANAUPENDELEO<br />

BWANA!<br />

WE UM-<br />

ESAHAU!? SI KWA<br />

SABABU WALILETWA<br />

NA WAHESHIMIWA<br />

KWENYE KAMPE-<br />

NI<br />

MTANDAO<br />

WA WAKULIMA<br />

<strong>MVIWATA</strong>?<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011


HUKU<br />

HABARI ZA<br />

KILIMO HAZIANDIKWI<br />

NA WAKIANDIKA GAZETI<br />

LINACHELEWA KUFIKA<br />

AU LISIFIKE KABISA.<br />

SASA HUKU KWETU<br />

BARABARA NI TATIZO<br />

LABDA TUTAPATA HIZO<br />

HABARI KWENYE RA-<br />

DIO NA TV<br />

KWELI TUTAPATAJE<br />

MAENDELEO KAMA HATUJUI<br />

TAARIFA YA KILA SIKU YA<br />

MASOKO, UCHUMI NA<br />

SIASA?!<br />

WATU WENGI WANAKUFA KWA KUKOSA<br />

ELIMU YA AFYA NA KUAMINI IMANI PO-<br />

TOFU ZA KWENDA KWA WAGANGA.<br />

LAKINI TUSIWALAUMU SANA<br />

WAANDISHI, MIMI NAFIKIRI<br />

SERIKALI YETU IANGALIE NA<br />

MIUNDO MBINU YETU<br />

HATA KAMA ZIPO KU-<br />

TOKANA NA HALI YA UCHU-<br />

MI JE, TUTAWEZA KUNUNUA<br />

HIZI TV NA UMEME<br />

TUTAPATA WAPI?<br />

HAPO<br />

MAENDELEO<br />

YATACHELEWA<br />

SANA<br />

EH<br />

HAYO YOTE<br />

YANATOKEA SABABU<br />

HATUPATI HABARI<br />

SAHIHI!<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />

ACHA UCHUMI<br />

TU, IDADI KUBWA YA<br />

WATANZANIA WANAISHI<br />

VIJIJINI NA UMEME<br />

HAKUNA HAYO MATAN-<br />

GAZO WATAYAONA<br />

VIPI?<br />

WANAHABARI<br />

WANA NAFASI KUBWA<br />

SANA YA KUELIMISHA<br />

WATU KUHUSU MATUMIZI<br />

BORA YA ARDHI, UFU-<br />

GAJI BORA, BEI KATIKA<br />

MASOKO<br />

KWA-<br />

HERINI<br />

NDIO, BARABARA SIYO<br />

NZURI KUWEZA KUSA-<br />

FIRISHA MAGAZETI<br />

YAFIKE HARAKA<br />

SASA<br />

NAFIKIRI MUDA<br />

MUAFAKA KWA WAHUSIKA KU-<br />

LIANGALIA HILI, SABABU VYOMBO<br />

VYA HABARI NDIO VINAWEZA KU-<br />

WAELIMISHA WATU NA KULETA<br />

MAENDELEO HARAKA.<br />

ITA-<br />

TUSAIDIA KUPA-<br />

TA ELIMU SAHIHI YA<br />

AFYA, UKATILI DHIDI<br />

YA WANAWAKE<br />

HILI TATIZO LIFANYIWE KAZI, SABABU HATA RADIO ZENYEWE<br />

HAZIFIKI VIJIJINI NA ZINATANGAZA UDHAIFU TU WA WATU WA<br />

KIJIJINI INGAWA KUNA MAFANIKIO NA UBUNIFU WANAOUFANYA.<br />

KATUNI<br />

KWELI<br />

BARABARA NI<br />

TATIZO KWA SABABU<br />

HATA MTOTO WA MZEE<br />

KIPARA ALIFARIKI KWENYE<br />

GARI KWA UBOVU WA<br />

BARABARA.<br />

WASAL-<br />

IMIE RAFIKI<br />

ZANGU’<br />

JUZI NILIKUWA MJINI<br />

NIMEONA MATANGAZO MENGI<br />

YANAYOONESHA UDHAIFU<br />

WA WATU WA KIJIJINI TU<br />

INA MAANA HUKU HATUNA<br />

MAMBO MAZURI YA KU-<br />

TANGAZA NA TV?<br />

23


KUTOKA MITANDAONI<br />

Mfumo shirikishi unaharakisha<br />

maendeleo<br />

Na Gratian Cronery, MUCCoBS<br />

Shinyanga<br />

Maendeleo na ustawi<br />

wa miradi ya kijamii<br />

yanategemea zaidi<br />

ushirikishwaji wa jamii husika<br />

katika hatua zote.<br />

Katika nchi yetu hali ni<br />

tofauti ambapo miradi mingi<br />

wanayopelekewa wananchi<br />

hawakushirikishwa kikamilifu na<br />

kwamba kinachofanyika ni wao<br />

kupokea amri ya bwana mkubwa na<br />

kutekeleza wasichokijua.<br />

Hali hii ya kuwapelekea<br />

wananchi maamuzi badala ya wao<br />

kushiriki kuibua wazo na kuamua,<br />

imesababisha miradi mingi kutotoa<br />

matokeo chanya licha ya kugharimu<br />

fedha nyingi.<br />

Serikali katika kuwasaidia<br />

wananchi kutekeleza mipango ya<br />

maendeleo imekuwa ikianzisha<br />

miradi ikiwemo ya kujenga majengo<br />

kwa lengo la kuwasaidia wananchi, ila<br />

ukweli ni kwamba fedha na raslimali<br />

nyingi zimekuwa zikipotea bure.<br />

Iko mifano mingi ya miradi ya<br />

aina hii ambayo wananchi wanaipa<br />

jina la ‘miradi ya serikali’ kwa kuwa<br />

hawakushirikishwa na haikuwa<br />

kipaumbele chao. Miradi hii ni kama<br />

vile ya majengo ya masoko kwenye<br />

vijiji vya Ruvu Darajani mkoani<br />

Pwani, Buigiri wilaya ya Chamwino,<br />

Ruaha mkoa wa Iringa na kwingineko<br />

ambayo yametelekezwa na kuwa<br />

vichaka vya wezi ama nyumba ya<br />

wanyama na wadudu, baada ya<br />

wananchi kususa kuyatumia kwa<br />

kuwa haikuwa kipaumbele chao<br />

na kwingineko uchaguzi wa eneo<br />

haukuwa sahihi.<br />

Huu ni mmoja wa mifano ya<br />

24<br />

miradi mingi ambayo imeanzishwa<br />

na serikali pasipo kuwashirikisha<br />

wananchi katika kutoa mawazo yao<br />

na kupendekeza nini wanahitaji na ni<br />

kwa matumizi gani, na kama ni jengo<br />

likae sehemu gani.<br />

Mfumo uliotumika kuanzisha<br />

na kutekeleza kauli mbiu ya “kilimo<br />

kwanza” ni ule ule wa amri kutoka<br />

kwa bwana mkubwa, mkulima hana<br />

hiari cha kuchagua kukataa hata<br />

kama kilicholetwa ni mwiba kwake.<br />

Vile vile serikali imekuja na<br />

mpango wa zana bora za kilimo<br />

ikiwemo matrekta madogo (power<br />

tiller) na ambapo kwenye maeneo<br />

mengi hazihitajiki kutokana na<br />

aina ya udongo na mazingira.<br />

Baada ya wakulima kulazimishwa<br />

kuzinunua wamezigeuza matumizi<br />

na kuwa mashine za kufua umeme,<br />

kusukuma maji, kulanda mbao na<br />

kusaga unga.<br />

Hii ni changamoto kwa serikali na<br />

wadau wengine ambao wanatazamia<br />

kupeleka miradi kwa wananchi,<br />

kwamba ni vyema kuzingatia<br />

ushirikishwaji wa wananchi na<br />

mawazo yao yakaheshimiwa<br />

ili baadaye wakithamini<br />

wanachopelekewa.<br />

Watanzania wanakabiliwa na kero<br />

nyingi ambazo wangetarajia serikali<br />

kuwekeza nguvu zake zaidi kwa<br />

kutumia mfumo wa ushirikishwaji<br />

katika kuzitatua. Kwa mfano<br />

kuondoa kero ya ushuru mkubwa<br />

wa mazao unaotozwa kwenye<br />

vizuizi vya kila barabara ya nchi hii<br />

inayoelekea mjini. Kuna maana gani<br />

kumpa ruzuku ya pembejeo mkulima<br />

na baadaye kumkamua faida yote<br />

inayotokana na mavuno hayo?<br />

Kama ushuru unatozwa ili kufidia<br />

fedha za ruzuku, ni bora ruzuku<br />

hiyo ifutwe wakulima wajitafutie<br />

pembejeo na wawe huru kusafirisha<br />

mazao yao. Hili linaweza kutatuliwa<br />

kwa njia shirikishi ya majadiliano.<br />

Kwa kufanya hivyo tunaweza<br />

kutengeneza mipango na miradi<br />

endelevu kwa vizazi na vizazi ambayo<br />

italeta tija katika nyanja zote za<br />

maisha kisiasa, kiuchumi na kijamii.<br />

Kwa upande mwingine tumeona<br />

mfano wa miradi ya ujenzi wa masoko<br />

inayotekelezwa na <strong>MVIWATA</strong><br />

kwa mfumo shirikishi imefanya<br />

vyema na wakulima wanathibitisha<br />

matokeo yake. Mwenyekiti wa<br />

<strong>MVIWATA</strong> Shinyanga Bw. Charles<br />

Ndugulile anasema siri kubwa ya<br />

mafanikio ya masoko ya <strong>MVIWATA</strong><br />

ni kuzingatiwa kwa dhana ya<br />

ushirikishwaji.<br />

“<strong>MVIWATA</strong> imefanikiwa kufanya<br />

hivyo kwa hutoa mafunzo mazuri<br />

ya jinsi ya kushirikisha jamii kuanzia<br />

ngazi ya kaya hadi taifa ambayo<br />

huambatana na mafunzo ya andiko<br />

la mradi, uendeshaji na usimamizi<br />

wa miradi, uhasibu wa vikundi na<br />

mashirika pamoja na taasisi pamoja<br />

na mifumo ya masoko na biashara,”<br />

anasema Bw. Ndugulile.<br />

Endapo serikali na wadau<br />

wengine wa maendeleo watatumia<br />

dhana hii ya ushirikishwaji wa jamii<br />

kwa mapana na kuiona kama fursa<br />

ya kuleta mabadiliko chanya kwa<br />

jamii ya Watanzania, hakika taifa<br />

litapiga hatua ya ukuaji wa kasi wa<br />

maendeleo.<br />

Jamii kwa upande wao pia<br />

wanapaswa kujipanga vyema<br />

kushiriki katika mradi kwa kuibua<br />

wazo, kupanga, kutekeleza na<br />

kusimamia na baadaye kujipima<br />

kiwango cha uwajibikaji wao kwenye<br />

miradi husika.<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011


Jipatie nakala ya Jarida la Pambazuko katika ofisi<br />

za <strong>MVIWATA</strong> ngazi za kati zifuatazo<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Morogoro<br />

S.L.P 3220 Morogoro<br />

Mahali: Uwanja wa Maonyesho NaneNane mkabala na<br />

ofisi za TASO<br />

Simu/Faksi: 023 261 41 84<br />

Barua Pepe: morogoro@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Rukwa<br />

S.L.P 468 Sumbawanga<br />

Mahali: Jengo la Bethlehem Center – Barabara ya Msakila<br />

Faksi: +255 25 280 25 58<br />

Simu: +255 764 232 747, +255 784 940 606<br />

Barua pepe: rukwa@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Mbeya<br />

S.L.P 3015 Mbeya<br />

Mahali: Jengo la Bima na CRDB Bank (Ghorofa ya<br />

mwisho<br />

Simu: +255 784 979 397, +255 652 835 568<br />

Barua pepe: mbeya@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Chunya<br />

Mahali: Jengo la Halmashauri, chumba Na.3<br />

Barua pepe: chunya@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Iringa<br />

S.L.P 9<strong>18</strong> Njombe<br />

Mahali: Jengo la Njoluma, Njombe mjini<br />

Simu: 0782 241 224, +255 767 241 224<br />

Barua pepe: iringa@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Kilimanjaro<br />

S.L.P 7389 Moshi<br />

Mahali: Mbuyuni sokoni- ghorofa ya GOLDEN GROWN<br />

LODGE<br />

Simu: +255 27 275 16 39, +255 784 720 320<br />

Barua pepe: kilimanjaro@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Kagera<br />

S.L.P 1753 Bukoba Mjini<br />

Mahali: Ofisi za Mayawa-Mtaa wa Rwamishenyi, Barabara<br />

ya Uganda<br />

Simu: +255 788 6858<strong>18</strong>, +255 782 154961, +255 755 522 447<br />

Barua pepe: kagera@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Dodoma<br />

S.L.P 3293 Dodoma<br />

Mahali:Area C Dodoma eneo la INADES Formation<br />

Tz,mkabala na msikiti wa Area C<br />

Simu:255-26-2350013, +255 782 257 783,<br />

+255 767 881 352<br />

Faksi: +255 26 2350744<br />

Barua pepe: dodoma@mviwata.org<br />

Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />

Mwenyekiti<br />

<strong>MVIWATA</strong> Monduli (MVIWAMO)<br />

S.L.P 47 Monduli<br />

Mahali: Barabara ya Boma-Moringe Sekondari, Monduli<br />

Mjini<br />

Simu: 255-27-253 8029, +255 27 253 8337<br />

Faksi: +255 27 253 8338<br />

Barua pepe: monduli@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Manyara<br />

S. L. P. 446,<br />

Babati Manyara<br />

Mahali: Barabara ya Nyerere<br />

SIMU: +255 27 253 0385 Faksi: +255 27 253 0707<br />

Baruapepe: manyara@mviwata.org<br />

Mwenyekiti<br />

<strong>MVIWATA</strong> Tabora<br />

S.L.P 175 Igunga<br />

Mahali: Mtaa wa Uarabuni<br />

Simu: +255 784 398 4<strong>14</strong>, +255 782 219 551<br />

Barua pepe: tabora@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Zanzibar<br />

S.L.P <strong>14</strong>9 Zanzibar<br />

Mahali: Mwana kwerekwe- mkabala na shule ya sekondari<br />

M’kwerekwe A<br />

Simu: +255 773 926 955, +255 777 470 5<strong>18</strong><br />

+255 783 651 135<br />

Barua pepe: zanzibar@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Ruvuma<br />

S.L.P 696 Songea Manispaa<br />

Mahali: Jengo la TTCL ghorofa ya 2<br />

Simu: +255-25-2600626, +255 756 096 291<br />

Barua pepe: ruvuma@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Mkuranga<br />

S.L.P 56 Mkuranga<br />

Mahali: Karibu na Stendi ya Kimanzichana<br />

Simu: 0786 158 646<br />

Barua pepe: mkuranga@mviwata.org<br />

MAWAKALA<br />

Mwenyekiti:<br />

<strong>MVIWATA</strong> Shinyanga<br />

S.L.P 1024 Shinyanga<br />

Mahali: Chuo cha Ushirika Moshi tawi la Shinyanga<br />

(Kizumbi)<br />

Simu: +255 763 740 675, +255 755 546 311<br />

Barua Pepe: shinyanga@mviwata.org<br />

Mwenyekiti<br />

<strong>MVIWATA</strong> Kigoma<br />

S.L.P 1<strong>14</strong>4 Kigoma<br />

Mahali: Ndani ya ofisi ya KIKANGONET, Lumumba road<br />

jengo la NHC chumba 205<br />

Simu: 0713 565 252, 0762 565 252<br />

Barua pepe: aisimba@yahoo.co.uk<br />

25


IJUE <strong>MVIWATA</strong><br />

Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania- <strong>MVIWATA</strong><br />

Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (<strong>MVIWATA</strong>) ni chombo cha kuunganisha wakulima wadogo ili kuwa na sauti moja katika utetezi wa<br />

maslahi yao ya kiuchumi, kijamii, kiutamaduni na kisiasa.<br />

Mtandao huu ulianzishwa mwaka 1993 na wakulima wadogo. Kauli mbiu ya <strong>MVIWATA</strong> ni ‘Mtetezi wa Mkulima ni Mkulima<br />

Mwenyewe’.<br />

Falsafa, utume na dira ya <strong>MVIWATA</strong><br />

Falsafa ya <strong>MVIWATA</strong> inajengwa katika ya misingi ya ushawishi na utetezi wa maendeleo ya wakulima wadogo katika nyanja za kiuchumi na<br />

kijamii; kuwezesha mawasiliano na kujifunza kwa kubadilishana uzoefu miongoni mwa wakulima.<br />

Utume wetu:<br />

Kuimarisha mawasiliano na kuwaunganisha wakulima wadogo kupitia vikundi na mitandao yao katika ngazi mbali mbali ili kujenga mtandao wa<br />

kitaifa wenye nguvu ya kuwezesha ushiriki na uwakilishi wa kweli wa maslahi ya wakulima wadogo katika ngazi zote za maamuzi.<br />

Dira yetu:<br />

<strong>MVIWATA</strong> ni kuwa chombo imara chenye nguvu za ushiriki na uwakilishi wa mawazo ya mkulima katika mchakato wa maamuzi ya kiuchumi,<br />

kijamii na kisiasa. Kuwa na uwezo wa kutekeleza na kufuatilia michakato na shughuli za maendeleo ya kiuchumi na kijamii yanayogusa maslahi ya<br />

wakulima wadogo.<br />

Malengo ya <strong>MVIWATA</strong><br />

1. Kuwezesha mawasiliano miongoni mwa wakulima wadogo ili kujenga kwa pamoja mbinu na mikakati ya ushawishi na utetezi kwa maslahi ya<br />

wakulima wadogo, kiuchumi na kijamii.<br />

2. Kubadilishana mawazo, ujuzi na uzoefu juu ya kilimo na shughuli mbalimbali za wakulima ili kuboresha maisha na kuinua hali yao kiuchumi na<br />

kijamii.<br />

3. Kuwakilisha wakulima wadogo katika mashauriano na serikali juu ya masuala mbalimbali yanayohusu au yanayoathiri ufanisi na maslahi ya<br />

wakulima wadogo wa Tanzania.<br />

Maeneo makuu ya mpango mkakati<br />

1. Ushawishi na Utetezi: Kuwezesha wakulima wadogo kuwa na uwezo wa kutetea maslahi yao.<br />

2. Uwezo wa kiuchumi: kuwezesha wakulima wadogo kuwa na uwezo wa kiuchumi kupitia njia za akiba na mikopo, kuunganisha wakulima na<br />

masoko na elimu ya ujasiliamali<br />

3. Kuimarisha vikundi na mitandao ya wakulima kwa lengo la kujipanga na kujitetea.<br />

4. Masuala mtambuka: Kujenga uelewa wa wakulima juu ya <strong>Uk</strong>imwi, Jinsia, Mabadiliko ya Tabia ya nchi.<br />

5. Ujenzi wa kitaaasisi kwa lengo la kuimarisha shirika<br />

Muundo<br />

Muundo wa <strong>MVIWATA</strong> una ngazi tatu ambazo ni Ngazi ya Taifa, Ngazi ya Kati na Ngazi ya Msingi. Ngazi ya Kati inaundwa na mitandao ya<br />

kimkoa na kiwilaya wakati Ngazi ya Msingi inaundwa na mitandao ya Kata na Vijiji.<br />

Shughuli kuu<br />

1. Kujenga uwezo wa wakulima wadogo kwa kupitia mafunzo shirikishi juu ya mbinu za ushawishi na utetezi, mbinu za kuimarisha uchumi wa<br />

wakulima wadogo na uendelevu wa rasilimali kwa njia za warsha, mafunzo, mikutano na ziara za mafunzo.<br />

2.<br />

3.<br />

4.<br />

Kuhamasisha wakulima wadogo kujiunga katika vikundi vya kijamii na kiuchumi, mitandao ya msingi (kata na vijiji) na mitandao ya kati (mikoa<br />

na wilaya). Mpaka sasa <strong>MVIWATA</strong> imeanzisha mitandao ya kimkoa katika Mikoa ya Dodoma, Iringa, Kagera, Kilimanjaro, Manyara, Mbeya,<br />

Morogoro, Rukwa, Ruvuma, Shinyanga, Tabora na Tanga kwa Tanzania Bara. <strong>MVIWATA</strong> pia imeanzisha mitandao ya kiwilaya katika Wilaya<br />

za Monduli (Arusha) na Chunya (Mbeya). Tanzania Visiwani, <strong>MVIWATA</strong> Zanzibar imeanzishwa na kusajiliwa (Usajili namba 401). Mkakati<br />

unaendelea wa kuimarisha mitandao iliyopo na kuanzisha mitandao mipya.<br />

Kukusanya, kuweka katika kumbukumbu na kusambaza habari zinazohusu ujuzi na uzoefu wa wakulima, sera za kitaifa na kimataifa kwa<br />

kupitia jarida la Pambazuko Sauti ya Wakulima, vipindi vya radio, vipeperushi, vijitabu na machapisho mengine.<br />

Kuhamasisha na kuwezesha wakulima kubuni na kuendesha miradi shirikishi ya kiuchumi na uzalishaji kwa lengo la kuboresha uchumi wa<br />

wakulima wadogo kama vile vyama vya mazao, vyama vya kuweka na kukopa na masoko ya mazao.<br />

5. Kuandaa mikutano na warsha kuhusiana na mada zinazowagusa au kuathiri maslahi ya wakulima wadogo.<br />

Uanachama na jinsi ya kujiunga na shirika<br />

<strong>MVIWATA</strong> ina wanachama wa aina tatu (3).<br />

Aina ya kwanza ni Wanachama wa Kawaida ambao wamegawanyika katika makundi mawili;<br />

a) Kikundi cha wakulima wadogo au<br />

b)<br />

Mkulima mdogo binafsi aliye mwanachama katika Kikundi au Mtandao. Mkulima atakuwa mwanachama wa kawaida wa <strong>MVIWATA</strong> mara<br />

tu Kikundi au Mtandao wake utakapokubaliwa kuwa mwanachama. Atapewa kadi ya uanachama na kikundi au mtandao utapewa cheti cha<br />

utambulisho.<br />

Aina ya pili ni Vyama, Mashirika na Mitandao ya Wakulima Wadogo.<br />

Vyama, Mashirika na Mitandao ya Wakulima Wadogo vinavyojishughulisha na utetezi na ushawishi wa maslahi ya wakulima wadogo vilivyosajiliwa<br />

chini ya sheria yoyote ya Tanzania katika Ngazi za Wilaya, Mkoa au Taifa vinaweza kuomba kuwa mwanachama wa <strong>MVIWATA</strong> iwapo vinakubaliana<br />

kwa dhati na malengo na madhumuni ya Shirika.<br />

Aina ya tatu ni Wanachama Washiriki<br />

Ni mtu yeyote, taasisi au kikundi cha watu ambacho kinaunga mkono malengo na madhumuni ya Shirika. Mwanachama mshiriki anatamkwa na<br />

Mkutano Mkuu wa <strong>MVIWATA</strong>.<br />

Kila mwanachama, isipokuwa mwanachama mshiriki atalipa kiingilio na ada ya kila mwaka. Maelezo zaidi juu ya utaratibu wa kujiunga na ada<br />

yanapatikana kutoka kwa kiongozi au ofisi ya <strong>MVIWATA</strong>.<br />

Kwa mawasiliano zaidi<br />

Ofisi Kuu ya <strong>MVIWATA</strong><br />

Mkurugenzi Mtendaji<br />

<strong>MVIWATA</strong><br />

S.L.P 3220 Morogoro<br />

Simu: 023 261 41 84<br />

Faksi: 023 261 41 84<br />

Barua pepe: info@mviwata.org, mviwata@morogoro.net

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!