Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
<strong>Uk</strong>. 4<br />
Toleo NO. 039 Julai –Septemba 2011 Bei Shs. 500/= ISSN 0856-5937<br />
Wakulima wapongeza <strong>MVIWATA</strong> kwa<br />
kuhabarisha wakazi wa vijijini<br />
<strong>Uk</strong>. <strong>14</strong><br />
Maonesho ya NaneNane 2011<br />
<strong>Uk</strong>. <strong>18</strong><br />
Kijana mbunifu atengeneza mitambo ya radio<br />
kunufaisha wanakijiji
Toleo NO. 039<br />
Julai Septemba 2011<br />
Bei Shs. 500/=<br />
ISSN 0856-5937<br />
WAHARIRI<br />
Susuma Msikula Susuma<br />
Stephen Ruvuga<br />
BODI YA <strong>MVIWATA</strong><br />
Mwenyekiti – Yazid Makame<br />
Makamu Mwenyekiti – Lydia Ruliho<br />
Katibu - Stephen Ruvuga-<br />
(Mkurugenzi Mtendaji)<br />
Mweka Hazina - Grace Runkulatile<br />
WAJUMBE<br />
Cosma Bulu<br />
Sylvester Yatuba<br />
Joseph Kilowoko<br />
Samweli Maseke<br />
Julius Mbago<br />
Habibu Simbamkuti<br />
MSHAURI WA <strong>MVIWATA</strong><br />
Prof. Amon Mattee<br />
LINATOLEWA NA<br />
KUSAMBAZWA NA<br />
Mtandao wa Vikundi vya<br />
Wakulima Tanzania (<strong>MVIWATA</strong>)<br />
S.L.P 3220 Morogoro, Tanzania<br />
Simu: 023 261 41 84<br />
Faksi: 023 261 41 84<br />
Barua pepe: info@mviwata.org,<br />
mviwata@morogoro.net<br />
Tovuti: www.mviwata.org<br />
MICHORO<br />
Godwin Chipenya<br />
USANIFU NA<br />
UCHAPISHAJI<br />
PENplus Ltd – 022 2<strong>18</strong>2059<br />
<strong>Uk</strong>. 4<br />
Toleo NO. 039 Julai –Septemba 2011 Bei Shs. 500/= ISSN 0856-5937<br />
Wakulima wapongeza <strong>MVIWATA</strong> kwa<br />
kuhabarisha wakazi wa vijijini<br />
<strong>Uk</strong>. <strong>14</strong><br />
Maonesho ya NaneNane 2011<br />
<strong>Uk</strong>. <strong>18</strong><br />
Kijana mbunifu atengeneza mitambo ya radio<br />
kunufaisha wanakijiji<br />
Picha ya Jalada:<br />
Bw. Benjamini Nziku mkulima wa<br />
kijiji cha Lusala kata ya Lupanga<br />
wilayani Ludewa akipata habari<br />
kupitia gazeti la wakulima la<br />
Pambazuko. b<br />
Tahariri<br />
Habari za vijijini zipewe<br />
kipaumbele<br />
Ingawa juhudi na mchango wa jamii za vijijini nchini Tanzania<br />
ndiyo vinavyoiendeleza Taifa, habari za vijijini haziandikwi kwa<br />
umuhimu huo.<br />
Mara nyingi, habari za vijijini zinazopewa nafasi kwenye<br />
vyombo vya habari ni zinazohusu maafa, kesi, vimbwanga na hotuba<br />
za viongozi wanapotembelea maeneo hayo.<br />
Wanahabari wanafanya kazi kubwa ya kuuelimisha umma, hata<br />
hivyo kwa sehemu kubwa habari hizo zimekuwa ni zile zinazohusu<br />
watu wa mijini.<br />
Toleo hili linalozungumzia habari za vijijini ni sehemu ya<br />
utekelezaji wa ajenda ya upashanaji habari inayotekelezwa na<br />
<strong>MVIWATA</strong> kwa muda mrefu sasa.<br />
Tunafahamu kwamba pamoja haya umuhimu wa upatikanaji wa<br />
habari kwa watu wa vijijini, ziko changamoto kadhaa zinazokwamisha<br />
ufanisi wake.<br />
Miongoni mwa changamoto hizo ni ukosefu wa vitendea<br />
kazi ikiwemo usafiri, kamera na vinasa sauti ambapo hata<br />
waandishi wachache wenye nia ya kwenda kukusanya habari vijijini<br />
wameshindwa kufanya hivyo kwa kukosa usafiri na wengine kuishia<br />
kutegemea usafiri wa viongozi wanapotembelea maeneo ya vijijini.<br />
Kulingana na kubanwa na ratiba za viongozi hao, waandishi hawawezi<br />
kukusanya habari nzuri zenye kuchochea maendeleo ya vijijini zaidi<br />
ya kuishia kuandika hotuba na maagizo ya viongozi.<br />
Changamoto nyingine ni ya waandishi wa habari kukosa<br />
taaluma ya kutosha yenye kuwawezesha kudadisi na kuibua kero na<br />
changamoto halisia za vijijini na siyo vimbwanga.<br />
Tunaamini ziko changamoto nyingi na lengo letu siyo kuziainisha<br />
zote isipokuwa tunawakumbusha wadau wa sekta ya habari kuwa<br />
vijijini ndiko kwenye chimbuko la wazalishaji na kwamba hatupaswi<br />
kuwatenga.<br />
Tunashauri kuwepo na jitihada za makusudi za kutatua<br />
changamoto hizi na vilevile kuwe na juhudi za kuhimiza vyombo<br />
vya habari kuzipa kipaumbele habari za vijijini. Ni wakati muafaka<br />
ambapo<br />
Tunawakumbusha wana habari juu ya umuhimu wa kuzingatia<br />
maadili ya taaluma ya uandishi wa habari kwa kuandika habari<br />
zilizofanyiwa utafiti wa kina na kuhakikisha jamii zote vijijini na<br />
mijini wananufaika na huduma hii muhimu.<br />
Tusaidie kuchochea maendeleo vijijini kwa kuhakikisha<br />
tunawapatia habari za kutosha na zilizofanyiwa utafiti.<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
Upatikanaji wa habari vijijini,<br />
kichocheo cha maendeleo?<br />
Na Goodness Mrema, Morogoro<br />
Kutokana na kupiga hatua<br />
za kimaendeleo katika<br />
teknolojia hasa ya habari,<br />
wigo wa upatikanaji wa habari<br />
hivi sasa umepanuka ukilinganisha<br />
na miaka ya nyuma hasa wakati<br />
tunapata uhuru.<br />
Hivi sasa watu wanauwezo<br />
wa kutumia kompyuta na<br />
simu za mkononi zenye<br />
huduma ya intaneti na<br />
kuweza kupata taarifa<br />
mbalimbali zinazotokea<br />
ulimwenguni kwa wakati<br />
huo huo ama kulipia huduma<br />
mbalimbali kama vile matibabu,<br />
maji na umeme. Lakini pia wanaweza<br />
hata kufanya manunuzi ya bidhaa<br />
mbalimbali kupitia intaneti na hivyo<br />
kupunguza gharama na muda na<br />
kurahisisha biashara.<br />
Hata hivyo mbali na kukua kwa<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />
teknolojia ya habari, nchi za Kusini<br />
mwa Afrika bado zinakabiliwa na<br />
tatizo kubwa la kukosekana kwa<br />
habari za umma hasa kwenye maeneo<br />
ya vijijini ambazo ni muhimu kwa<br />
wananchi kutoa maamuzi mbalimbali<br />
ambayo ni sahihi kwa maisha yao.<br />
Hata<br />
radio za kijamii<br />
zilizoanzishwa kwa lengo<br />
la kuhudumia wakazi wa vijijini,<br />
zimeacha misingi ya kuanzishwa<br />
kwake na kuegemea zaidi<br />
kutangaza mambo ya<br />
mijini.<br />
Bado<br />
kuna changamoto zinazoikumba<br />
sekta hii ya habari ikiwemo uhaba<br />
wa upatikanaji wa habari sahihi<br />
na zenye manufaa kwa baadhi ya<br />
MADA MAALUM<br />
maeneo hasa ya vijijini. Mfumo wa<br />
upashanaji habari uliopo sasa siyo<br />
wa kuridhisha kwani haumfikii kila<br />
mwananchi wa kijijini mahali alipo.<br />
Kwa mfano magazeti yanayofika<br />
kwa nadra vijijini ndani yake yanakuwa<br />
yamejaa habari zinazohusu vuguvugu<br />
la maisha ya mjini. Habari hizo nyingi<br />
ni zile zinazohusu malumbano na<br />
siasa za chuki baina ya viongozi<br />
wa vyama, foleni za barabarani,<br />
michezo ambayo pengine mtu<br />
wa kijijini hajawahi kuiona na<br />
burudani kama vile miziki<br />
na picha kubwa kubwa za<br />
wasanii ambazo ki uhalisia<br />
hazimuongezei tija mtu wa<br />
kijijini katika harakati zake za<br />
kupambana na umasikini kupitia<br />
kilimo, ufugaji ama uvuvi.<br />
Tunashuhudia ongezeko la<br />
vyombo vya habari vya kielektroniki<br />
kama vile radio na televisheni na<br />
ukuaji wake kutoka kwenye mfumo<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 2<br />
Mwekahazina wa <strong>MVIWATA</strong> Ruvuma Bibi Immaculata John akitekeleza shughuli za <strong>MVIWATA</strong> za kusambaza habari za wakulima kwa<br />
wadau<br />
1
MADA MAALUM<br />
Upatikanaji wa habari vijijini<br />
Inatoka uk. wa 1<br />
wa analogia kwenda digitali.<br />
Ongezeko na ukuaji wa<br />
teknolojia bado hauwanufaishi<br />
vya kutosha wakazi wa vijijini.<br />
Kilichobadilika ni kuwepo kwa<br />
usikivu mzuri wa matangazo ya<br />
radio kwenye baadhi ya vijiji tofauti<br />
na ilivyokuwa awali. Habari zenye<br />
mlengo wa kuchochea maendeleo<br />
vijijini bado hazipewi kipaumbele.<br />
Hata radio za kijamii<br />
zilizoanzishwa kwa lengo la<br />
kuhudumia wakazi wa vijijini,<br />
zimeacha misingi ya kuanzishwa<br />
kwake na kuegemea zaidi kutangaza<br />
mambo ya mijini.<br />
Japokuwa televisheni na redio<br />
zinajitahidi kurusha matangazo<br />
yake na kuwafikia kwa wakati watu<br />
wa vijijini, lakini bado habari zake<br />
zinakosa mguso kwao, ingawa serikali<br />
inajinadi kuwa matumizi ya mfumo<br />
wa digitali yameongeza upatikanaji<br />
wa habari maeneo ya vijijini.<br />
Kwa ujumla habari zinazohusu<br />
mafundisho ama mafanikio ya<br />
wananchi vijijini haziandikwi wala<br />
kusikika vya kutosha na kwamba<br />
kuna haja ya kubadili mfumo<br />
ili waandishi wa habari wapate<br />
msukumo wa kuwafikia wananchi<br />
vijijini na kuandika habari zao.<br />
Siku hizi umekuja utaratibu<br />
mpya wa upashanaji habari kupitia<br />
mitandao mbalimbali ya kijamii<br />
(tovuti, blogs, facebook, twitter)<br />
ambayo kwa hakika mkulima au<br />
mfugaji mdogo anayeishi kijijini<br />
hafahamu hata jinsi ya kuitumia na<br />
wachache wenye uelewa hawawezi<br />
kuitumia kwa kukosa nishati ya<br />
umeme.<br />
Changamoto ya<br />
miundombinu<br />
Ziko sababu nyingi zinazotajwa<br />
kuchangia habari kutowafikia watu<br />
wa vijijini. Sababu mojawapo ni ubovu<br />
wa miundombinu ya barabara katika<br />
maeneo mengi ya vijijini ambako<br />
kuna asilimia 80 ya Watanzania<br />
wazalishaji wanaochangia pato la<br />
taifa.<br />
Kulingana na miundombinu<br />
duni ya barabara zetu hasa maeneo<br />
2<br />
ya vijijini, ni vigumu kwa mwananchi<br />
wa kijijini kupata gazeti kwa wakati<br />
na kulisoma.<br />
Wauzaji na wasambazaji wa<br />
magazeti ya kila siku wanajikuta<br />
wakishindwa kuyafikia maeneo hayo<br />
kwa wakati. Kwa mfano gazeti la<br />
kila siku linalosambazwa asubuhi<br />
katika maeneo ya mijini huchukua<br />
wakati mwingine siku mbili kufika<br />
eneo la Mrimba Kilombero mkoani<br />
Morogoro kutokana na barabara ya<br />
kuelekea sehemu hiyo kuwa mbaya.<br />
Huu ni mfano wa sehemu moja<br />
iliyo katika mkoa jirani na mji ambapo<br />
magazeti mengi huchapishiwa, swali<br />
ni je vipi kwa watu waishio Kigoma<br />
vijijini, Karagwe ama Murugwanza<br />
huko Ngara, wao hulipata gazeti hilo<br />
siku ngapi baada ya kuchapishwa?<br />
<strong>Uk</strong>osefu wa nishati nalo ni tatizo<br />
kubwa kwa wakazi wa maeneo ya<br />
vijijini ambalo linazuia wananchi<br />
wa vijijini kununua televisheni<br />
au radio kwa sababu ya kukosa<br />
nishati itakayowawezesha kuvitumia<br />
vyombo hivyo.<br />
Maisha magumu ya vijijini<br />
yanayosababishwa na ukosefu wa<br />
huduma muhimu za kijamii pia<br />
yanadhoofisha kasi ya upatikanaji<br />
wa habari vijijini. Kwa mfano<br />
mtu anayesumbuliwa<br />
na maradhi kwa<br />
kukosa huduma<br />
sahihi za<br />
matibabu,<br />
hawezi kukaa<br />
na kusikiliza<br />
radio huku<br />
a k i g u g u m i a<br />
kwa maumivu<br />
makali. Mtu huyu<br />
pia hawezi kutenga<br />
fedha ya kununua gazeti<br />
linalomfikia baada ya siku mbili<br />
Akina mama wengi vijijini<br />
wanakosa muda wa kusikiliza taarifa<br />
za habari ama matangazo mengine<br />
muhimu kwa kuwa muda ambao<br />
radio na televisheni zinatangaza<br />
taarifa za habari wao wanakuwa<br />
kwenye shughuli za kupika, kutafuta<br />
maji na kuni na shughuli za shamba.<br />
<strong>Uk</strong>iachana na tatizo la<br />
miundombinu duni, iko sababu<br />
nyingine ya baadhi ya wananchi kukosa<br />
mwamko wa kutafuta ama kutoa<br />
habari. Wananchi kwenye baadhi ya<br />
maeneo ya vijijini hawajaelimishwa<br />
vya kutosha juu ya umuhimu wa<br />
kutoa na kupokea habari kuhusiana<br />
na masuala mbalimbali hivyo baadhi<br />
yao kuona kwamba kununua gazeti<br />
ama kununua televisheni ni kuwa na<br />
matumizi ya anasa.<br />
Habari zinachochea<br />
maendeleo?<br />
Wakazi wa vijijini wengi wao wakiwa<br />
ni wakulima waliopata fursa ya<br />
kuzungumzia hoja hii, walikiri kuwa<br />
upatikanaji wa habari sahihi vijijini<br />
umesaidia kuchochea maendeleo,<br />
japokuwa kiwango cha upatikanaji<br />
wake siyo cha kuridhisha.<br />
Walieleza kuwa habari chache<br />
zilizowafikia ziliwasaidia kupata<br />
elimu ya kilimo bora, taarifa za<br />
upatikanaji wa pembejeo, masoko,<br />
mwelekeo wa hali ya hewa na<br />
mwenendo wa uchumi na hali ya<br />
kisiasa nchini pamoja na kufahamu<br />
jitihada za maendeleo zinazofanywa<br />
na makundi mbalimbali.<br />
Mbali na<br />
vyombo vya habari,<br />
ziko njia nyingine za asili<br />
zinazotumika kufikisha habari kwa<br />
jamii kwenye maeneo ya vijijini ikiwemo<br />
mikutano ya vijiji, kwenye nyumba<br />
za ibada na kwenye mikusanyiko<br />
kama vile sokoni na kwenye<br />
minada.<br />
Walisema habari hizo pia<br />
zinawapatia uwanja mpana wa<br />
mjadala na kubadilishana uzoefu<br />
kuhusiana na masuala mbalimbali<br />
yanayowakabili ikiwemo uwezo wa<br />
kudai haki zao za msingi. Wanafahamu<br />
mahali pa kupata mahitaji muhimu na<br />
fursa zinazopatikana kwa ajili yao na<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 3<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
Inatoka uk. wa 2<br />
njia muafaka za kufikia suluhu kwa<br />
changamoto zinazowakabili katika<br />
shughuli zao.<br />
“Suala la upatikanaji wa habari<br />
linahusika zaidi na maisha ya kila<br />
siku ya mwananchi. Ni suala la<br />
maendeleo ya kila mwanadamu hapa<br />
ulimwenguni, endapo wananchi hawa<br />
wa vijijini watapata habari sahihi na<br />
kwa wakati zitachochea bidii katika<br />
kujiletea maendeleo,” alisema Bw<br />
Andrew Hepelwa, Katibu Mkuu<br />
Mstaafu wa <strong>MVIWATA</strong> taifa.<br />
Aliongeza kuwa maendeleo<br />
ni jambo la muhimu ambalo kila<br />
mwanadamu analitegemea katika<br />
maisha yake kuanzia ngazi ya familia<br />
hadi ngazi za kitaifa. Kama hupati<br />
taarifa kamili kuhusu kitu fulani,<br />
huwezi kujua uzito wake na huwezi<br />
kuchukua hatua za kimaendeleo na<br />
kwa upande mwingine jamii ikipata<br />
taarifa na habari sahihi inaweza<br />
kuchukua hatua ya kujikwamua<br />
katika matatizo.<br />
Matumizi ya habari<br />
Kwa ujumla jamii ya vijijini kutokana<br />
na kutengwa kwa muda mrefu na<br />
mfumo wa habari, nayo kwa namna<br />
fulani imekuwa kama imejiengua na<br />
kuyaona masuala ya habari kama<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />
siyo sehemu yao.<br />
Jamii hii inahitaji kujengewa<br />
ufahamu wa kutosha kuhusu<br />
umuhimu wa kupashana habari<br />
na matumizi sahihi ya vyombo vya<br />
habari katika kujiletea maendeleo.<br />
Vyombo vya habari katika hili vina<br />
mchango mkubwa wa kuwafumbua<br />
macho wakazi wa kijijini ili wafahamu<br />
umuhimu wa matumizi sahihi ya<br />
habari katika mchakato wa kujiletea<br />
maendeleo.<br />
Mbali na vyombo vya habari, ziko<br />
njia nyingine za asili zinazotumika<br />
kufikisha habari kwa jamii kwenye<br />
maeneo ya vijijini ikiwemo mikutano<br />
ya vijiji, kwenye nyumba za ibada<br />
na kwenye mikusanyiko kama vile<br />
sokoni na kwenye minada.<br />
Hata hivyo taarifa nyingi muhimu<br />
hutolewa katika mikutano ya vijiji,<br />
lakini kutokana na kukosa mwamko<br />
huko nako mahudhurio ni madogo<br />
na hivyo kukosesha wananchi habari<br />
muhimu.<br />
Miongoni mwa wakulima<br />
waliohojiwa wamekiri wazi kuwa<br />
hawajawahi kuhudhuria mkutano<br />
wa kijiji kwa zaidi ya miaka miwili.<br />
Hili ni tatizo na ni tabia inayopaswa<br />
kuachwa kwa sababu inadidimiza<br />
maendeleo.<br />
Miongoni mwa wakulima hao<br />
pia wamekiri mapungufu kwamba<br />
Upatikanaji wa habari sahihi unapanua wigo wa mijadala kama hii ya wakulima<br />
MADA MAALUM<br />
walipata habari lakini hawakuzitumia<br />
ipasavyo jambo ambalo wamelijutia<br />
na baadaye kujirekebisha. Kwa<br />
mfano Bw. Charles Ndugulile<br />
mkulima wa kijiji cha Mwamala Kata<br />
ya Mwamala wilaya ya Shinyanga<br />
Vijijini alisema “mwaka 2008 kupitia<br />
matangazo ya radio nilipata taarifa za<br />
kutokea mabadiliko ya tabia ambayo<br />
yatasababisha ukame na mlipuko wa<br />
wadudu lakini nilipuuzia na baadaye<br />
msimu wa kilimo uliofuata nililima<br />
shamba kubwa kama kawaida,<br />
nikapata hasara baada ya mazao<br />
kukauka kwa ukame.”<br />
Bw. Ndugulile akafafanua<br />
kwamba kutokana na hali hiyo<br />
amekuwa mhamasishaji mkubwa<br />
kwenye mkoa wa Shinyanga<br />
akiwahimiza wakulima umuhimu<br />
wa kutafuta habari na kuzitumia,<br />
lakini pia wawe wamezipata kutoka<br />
katika vyanzo vya uhakika na<br />
vinavyoaminika ila wasipotoshwe<br />
kwa kupata habari ambazo si sahihi.<br />
Hitimisho<br />
Ili kuboresha upatikanaji wa habari<br />
vijijini, serikali na wadau wa habari<br />
kwa ujumla wanapaswa kushirikiana<br />
kuondoa kasoro zilizopo na kuweka<br />
mfumo wa usawa wa utoaji taarifa<br />
na upatikanaji wa habari kwenye<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 5<br />
3
MADA MAALUM<br />
4<br />
Maoni ya wakulima na<br />
Na Goodness Mrema<br />
Changamoto kubwa<br />
inayowakabili wakulima<br />
vijijini kwa kukosa habari<br />
ni kuachwa nyuma kimaendeleo,<br />
kuibuka kwa migogoro mingi baina<br />
yao na viongozi wao ama makundi<br />
mengine katika jamii.<br />
Baadhi ya wakulima na wataalam<br />
wamekuwa na maoni tofauti<br />
kuhusiana na suala hili la upatikanaji<br />
wa habari vijijini. Wakulima kutoka<br />
mikoa mbalimbali walieleza jinsi<br />
wanavyokabiliwa na changamoto<br />
katika kupokea na kutoa habari<br />
katika maeneo mengi ya vijijini<br />
kutokana na miundombinu mibovu.<br />
Yafuatayo ni maoni waliyoyatoa<br />
wataalam<br />
baada ya kuulizwa swali lililosema<br />
hali ya upatikanaji wa habari kijijini<br />
ukoje?<br />
Bibi. Mariam Mmanga<br />
kutoka kijiji cha Kivulini wilayani<br />
Mwanga mkoani Kilimanjaro alieleza<br />
kwamba japokuwa kijijini kwake<br />
hawatembelewi na waandishi wa<br />
habari mara kwa mara wala kufikiwa<br />
na magazeti, lakini wanawake<br />
kijijini kwake wamejiunga katika<br />
vikundi wanavyovitumia kupashana<br />
habari kupitia mikutano na vikao<br />
mbalimbali na sasa wamehamasika<br />
na wanaelewa umuhimu wa kupata<br />
habari, jambo ambalo linawatia moyo<br />
na wanaimani kwamba hawataweza<br />
kubaki nyuma kwani wanafahamu na<br />
wanaelewa nini kinaendelea katika<br />
nchi yao. Hata hivyo akaongeza<br />
kuwa wanaomba kutembelewa na<br />
wanahaabari ili habari za vikundi<br />
vyao pia zitangazwe.<br />
Bibi. Mariam Hassan<br />
kutoka kijiji cha Magamba, wilayani<br />
Kibondo mkoani Kigoma anaeleza<br />
kwamba magazeti kijijini Magamba<br />
yanawafikia baada ya siku tatu ama<br />
nne, tena lazima awepo mtu ametoka<br />
mjini siku hiyo. Kwa upande wa radio<br />
wanakamata zaidi radio za Burundi<br />
na kwamba hupokea matangazo ya<br />
radio moja tu ya Tanzania ambayo<br />
nayo husikika usiku tu, jambo ambalo<br />
linawafanya washindwe kupiga hatua<br />
kimaendeleo.<br />
Ameiomba serikali kuwakumbuka<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 5<br />
Miongoni mwa machapisho yanayotolewa na <strong>MVIWATA</strong> ambayo yamewanufaisha wakulima wengi kwa kuwapata habari sahihi za kilimo<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
Inatoka uk. wa 4<br />
na kuhakikisha kwamba nao pia<br />
wanapata huduma hii muhimu kwani<br />
wanaonekana wamesahaulika kama<br />
vile wako nje ya Tanzania kutokana<br />
na kijiji chao kuwa mpakani mwa<br />
nchi ya Burundi. “Kuhusu habari za<br />
kijijini kwetu zinaandikwa pale tu<br />
kiongozi anapokuja kututembelea<br />
ama wakati mwingine waandishi<br />
hufika kijijini hapo kunapokuwa<br />
na matukio ya maafa kama vile<br />
mauaji. Tatizo hili linatuathiri zaidi<br />
sisi wanawake kwani muda mwingi<br />
tuko ndani, afadhali wenzetu<br />
wanaume wanakutana kwenye<br />
vikao na kuhabarishana na wengine<br />
wanamiliki simu za mkononi.”<br />
Bw. Hamad Abdallah<br />
Salimin kutoka Zanzibar yeye<br />
alieleza kukerwa na waandishi wa<br />
habari wanaokurupuka na kutangaza<br />
mambo yasiyo sahihi na kuupotosha<br />
umma. Akashauri ni vyema<br />
wanataaluma hawa kuthibitisha<br />
habari wanazozikusanya kabla ya<br />
kuzitangaza kwa umma.<br />
Hata hivyo aliwashauri wakulima<br />
wenzake wakabiliane na changamoto<br />
ya upatikanaji wa habari katika<br />
maeneo ya vijijini kwa kutosubiri<br />
tu hadi magazeti yawafikie ndipo<br />
wajue wamepata habari kumili kujua<br />
nini kinaendelea, bali wanaweza pia<br />
kupata habari zinazowahusu kwa<br />
kupitia majarida yanayochapishwa<br />
na mashirika yanayojihusisha<br />
na shughuli za kilimo kama vile<br />
<strong>MVIWATA</strong> ili kutambua fursa walizo<br />
nazo.<br />
Lakini akasema kwamba wakulima<br />
wasiishie kusoma habari na kuziacha<br />
tu katika makaratasi bali wazifanyie<br />
kazi na pia wasiogope kutumia<br />
vyombo vya habari kuwasilisha kero<br />
na kufichua maovu.<br />
Bw. Joseph Msagama kutoka<br />
Tanga alikiri kuwa changamoto<br />
kubwa ipo katika upokeaji wa habari<br />
kutokana na uhaba wa rasilimali<br />
fedha ambayo inamwathiri kila<br />
mkulima.<br />
“Jambo la kusikitisha ni kwamba<br />
wananchi wa vijijini wanaonekana<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />
kuwa tabaka la watu waliosahaulika<br />
katika kila kitu kuanzia kipato, elimu<br />
na hata haki zao mbalimbali ikiwemo<br />
hii ya kupata habari” alisema Bw.<br />
Msagama.<br />
Alishauri Halmashauri za wilaya<br />
ziweke utaratibu wa kutenga<br />
mafungu ya kuwawezesha usafiri<br />
maaalum waandishi wa habari<br />
ili wafike maeneo ya vijijini na<br />
kuwasaidia wananchi kufahamu<br />
nini kinaendelea na kwa kiasi gani<br />
kinaathiri uchumi wa wakulima.<br />
Kwa upande wake Bw. Abdala<br />
Ramadhani kutoka wilaya ya<br />
Misungwi, Mwanza alisema wakulima<br />
wengi vijijini wanakabiliwa na uhaba<br />
wa habari na kushauri vituo vya<br />
taarifa vijijini viimarishwe ili kuziba<br />
pengo lililopo.<br />
“Kupitia vituo hivyo vichache<br />
vilivyopo sasa wakulima na<br />
wajasiriamali wanapata habari<br />
kuhusiana na bei za mazao na wapi<br />
wanaweza kuuza lakini habari hizo<br />
haziwafikii wengi kutokana na uhaba<br />
wa rasilimali fedha unaozikabili,”<br />
alisema Ramadhani.<br />
“Tunashukuru kuwapo kwa<br />
gazeti letu wakulima la Pambazuko,<br />
linatuwezesha kufahamu wenzetu<br />
katika maeneo mengine wanafanya<br />
nini na ni njia gani wanazozitumia<br />
kutatua changamoto zao, jambo<br />
ambalo linatupa ari ya kufanya kazi<br />
kwa bidii ili kuzalisha kwa tija.”<br />
Bw. Ramadhani alisema kupitia<br />
mtandao wa wakulima wanajipanga<br />
ili kuweka utaratibu mzuri wa<br />
kuwezesha habari za wakulima<br />
wa Mwanza zinamfikia mhariri wa<br />
Pambazuko kwa wakati.<br />
Bw. Paul Mossama kutoka<br />
Serengeti mkoani Mara, anaeleza<br />
kuwa mfumo wa upashanaji habari<br />
uliopo nchini hivi sasa ni mzuri<br />
kuliko miaka ya nyuma, japokuwa una<br />
kasoro ya kutotangaza habari nyingi<br />
za kuwasaidia wakulima kuboresha<br />
shughuli zao na akashauri vituo vya<br />
radio na televisheni vinavyoanzishwa<br />
na halmashauri za wilaya vitangaze<br />
zaidi habari hizo badala ya kuwa na<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 6<br />
Inatoka uk. wa 3<br />
MADA MAALUM<br />
Upatikanaji wa<br />
habari vijijini<br />
maeneo ya vijijini na mijini.<br />
Kwa upande wa radio<br />
matangazo yaboreshwe yasikike<br />
vizuri vijijini ili wananchi wetu<br />
walioko mipakani kama vile<br />
Kigoma pia waweze kunufaika<br />
na matangazo ya radio za nchini<br />
mwao badala ya radio za nchi jirani<br />
ya Burundi na Kongo ambazo<br />
kila kukicha zinatangaza vita na<br />
mauaji kutokana na mapigano<br />
yanayoendelea nchini mwao.<br />
Kadhalika waandishi<br />
wenyewe wanakabiliwa na<br />
changamoto ya kujiendeleza<br />
kitaaluma ili kuweza kuwa<br />
na upeo zaidi wa kuandika<br />
na kuchanganua habari zao<br />
kwa weledi hasa zinazohusu<br />
maendeleo vijijini badala ya kuwa<br />
mawakala ama mashabiki wa<br />
siasa tu.<br />
Kuna matatizo mengi vijijini<br />
ambayo kimsingi yanahitaji nguvu<br />
ya wanahabari kuyatatua. Kwa<br />
mfano wanahabari wanapaswa<br />
kuijengea uwezo jamii kuhusu<br />
elimu ya afya vijijini, elimu ya<br />
ukatili wa wanawake na vitendo<br />
vya unyanyasaji, elimu juu ya<br />
umiliki na matumizi bora ya ardhi,<br />
elimu ya kilimo bora na ufugaji,<br />
ujasiriamali, masoko na umuhimu<br />
wa elimu kwa watoto wao.<br />
Ipo haja kubwa ya tasnia<br />
ya habari kutilia mkazo suala la<br />
kuielimisha jamii ili iepukane na<br />
imani potofu za kwenda kwa<br />
waganga wa kienyeji kupiga ramli<br />
badala ya kuwapeleka wagojwa<br />
kutibiwa kwenye zahanati na<br />
vituo vya afya.<br />
Wanakijiji ambao kwa sehemu<br />
kubwa ni wakulima wanapaswa<br />
kujengewa uelewa wa masoko<br />
ya mazao yao, taarifa za bei na<br />
mbinu bora za kuongeza tija katika<br />
uzalishaji na kuboresha uchumi.<br />
Maendeleo vijijini<br />
yanachelewa kwa sababu<br />
wananchi hawapati habari sahihi<br />
kwa wakati muafaka. Hivyo<br />
yanapaswa kuchochewa kwa<br />
kuwapatia habari za kina.<br />
5
MADA MAALUM<br />
Maoni ya wakulima...<br />
Inatoka uk. wa 5<br />
vipindi vingi vya miziki na salamu.<br />
Akashauri pia magazeti kutenga<br />
kurasa maalumu zitakazoandika<br />
habari za wakulima wadogo angalau<br />
mara moja kwa wiki. “Magazeti<br />
mengi sasa yamefungua kurasa za<br />
udaku, urembo na muziki, hivyo hata<br />
kwa habari za wakulima jambo hili<br />
linawezekana.”<br />
Aliwashauri wakulima wadogo<br />
kutumia mitandao ya wakulima<br />
waliyonayo katika maeneo yao<br />
kwa ajili ya kupashana habari<br />
hadi pale wanapokuwa wanaona<br />
wameshindwa kufanya hivyo<br />
wenyewe ndipo waweze kumtafuta<br />
mwandishi ambaye atawasaidia<br />
kutangaza taarifa zao ili nao<br />
wapate nafasi ya kupaza sauti zao<br />
na kusaidiwa pale wanapohitaji<br />
msaada.<br />
Bw. Benardi Maiko kutoka<br />
Kasanga, wilayani Sumbawanga<br />
mkoani Rukwa alisema wakulima<br />
wanayo mambo mengi ambayo ni<br />
vyema wakayatangaza ikiwemo<br />
mazao yao na bidhaa zingine<br />
wanazozalisha, changamoto ya uhaba<br />
wa pembejeo na zana bora za kilimo<br />
pamoja na mahitaji ya masoko ya<br />
kuuzia mazao yao.<br />
Aliongeza pia, wakulima<br />
wanahitaji kuwezeshwa kuwasiliana<br />
wao kwa wao kupitia vyombo vya<br />
habari ili kurahisisha mawasiliano<br />
kwani badala ya wao kufunga<br />
safari kwenda maeneo mengine<br />
kuwatembelea wenzao wataweza<br />
kusoma tu kwenye magazeti ama<br />
kusikiliza radioni na kujifunza.<br />
“Endapo habari zingekuwa zinafika<br />
maeneo ya vijijini kama ilivyo kwa<br />
maeneo ya mijini hakika wakulima<br />
leo tungekuwa kundi lenye nguvu<br />
kiuchumi na tusingekandamizwa<br />
wala kunyanyaswa” alisema Bw.<br />
Maiko<br />
Bw. Charles Ndugulile<br />
mkulima wa kijiji cha Mwamala<br />
Kata ya Mwamala wilaya ya<br />
Shinyanga Vijijini alieleza kwamba<br />
6<br />
upatikanaji wa habari unategemeana<br />
na watafutaji wa habari kwamba<br />
wanataka habari za namna gani na<br />
zinazohusu nini na kutolea mfano<br />
wa jarida la Pambazuko kwamba kila<br />
anayetaka kupata habari kuhusiana<br />
na wakulima anaweza kuzipata<br />
kutoka ndani ya jarida hilo.<br />
Akizungumzia matumizi sahihi<br />
ya habari Bw. Ndugulile alisema<br />
“mwaka 2008 kupitia matangazo<br />
ya radio nilipata taarifa za kutokea<br />
mabadiliko ya tabia ambayo<br />
yatasababisha ukame na mlipuko wa<br />
wadudu lakini nilipuuzia na baadaye<br />
msimu wa kilimo uliofuata nililima<br />
shamba kubwa kama kawaida,<br />
nikapata hasara baada ya mazao<br />
kukauka kwa ukame.”<br />
Bw. Ndugulile alifafanua kwamba<br />
kutokana na hali hiyo amekuwa<br />
mhamasishaji mkubwa kwenye katika<br />
mkoa wa Shinyanga akiwahimiza<br />
wakulima umuhimu wa kutafuta<br />
habari na kuzitumia, lakini pia wawe<br />
wamezipata kutoka katika vyanzo<br />
vya uhakika na vinavyoaminika ila<br />
wasipotoshwe kwa kupata habari<br />
ambazo si sahihi.<br />
Alifafanua kwamba katika mkoa<br />
wa Shinyanga wamewahamasisha<br />
wakulima umuhimu wa kutafuta<br />
habari kutoka katika vyanzo vya<br />
uhakika na vinavyoaminika ili<br />
wasipotoshwe kwa kupata habari<br />
ambazo si sahihi.<br />
Alisema kuwa wakulima wanaumia<br />
waonapo habari mara kwa mara<br />
zinazoeleza kuwa wameshindwa<br />
kufanya jambo ama wana mgogoro<br />
fulani wakati habari za mafanikio<br />
waliyopata kupitia kilimo ikiwemo<br />
kuongeza uzalishaji na kuweza<br />
kulipa ada za watoto wao, kujenga<br />
nyumba, kuongeza idadi ya mifugo<br />
na hata kufanikiwa kununua zana za<br />
kilimo, haziandikwi. “Kwa msingi huu<br />
ndiyo maana mara nyingi nimekuwa<br />
nikishauri kwamba ni muhimu<br />
wakulima tuimarishe chombo<br />
chetu cha habari kama Pambazuko<br />
kinachoweza kutusemea habari<br />
zetu.”<br />
Bw. Ndugulile ambaye pia<br />
ni mwenyekiti wa <strong>MVIWATA</strong><br />
Shinyanga, alisema vyombo vingi<br />
vya habari nchini hivi sasa vinafanya<br />
shughuli zake kibiashara na hivyo<br />
kujikita katika matukio yenye<br />
habari zinazouzika na kutupa kando<br />
jukumu la kuwaelimisha wakulima<br />
kilimo biashara ama ufugaji na uvuvi<br />
wa kisasa.<br />
Maoni ya wataalam<br />
Bibi Mary Nsemwa, ni mkuu<br />
wa Idara ya Ushawishi na Ujenzi wa<br />
Nguvu za Pamoja katika Mtandao<br />
wa Jinsia Tanzania (TGNP), anasema<br />
asilimia kubwa ya wananchi wa<br />
vijijini wanaoathirika na upatikanaji<br />
wa habari ni wanawake.<br />
Bibi Nsemwa alisema wanawake<br />
wanahitaji kuhabarishwa kuhusiana<br />
na kilimo, ujasiriamali, sheria<br />
ya ardhi na mambo mbalimbali<br />
yanayoendelea mijini na duniani,<br />
lakini haki hiyo wanaikosa kutokana<br />
na kutokuwepo kwa miundo mbinu<br />
inayofika maeneo ya vijijini hususan<br />
barabara kwa ajili ya magazeti.<br />
“Hata kwa familia zenye radio<br />
nyingi zinamilikiwa na wanaume,<br />
hivyo wanawake kukosa taarifa<br />
muhimu ndiyo maana wanazidi<br />
kukandamizwa”.<br />
Bw. Marcossy Albanie wa<br />
Kituo cha Msaada wa Sheria na Haki<br />
za Binadamu yeye anasema “kwa<br />
ujumla wakulima ni kundi lililoachwa<br />
nyuma na hata wakizungumza watu<br />
wanawapuuza na ndiyo maana hata<br />
vyombo vingi vya habari vimeegemea<br />
zaidi mjini, ingawa kisingizio kikubwa<br />
kimekuwa ni miundombinu mibovu<br />
vijijini.<br />
“Suala hili linamfanya mkulima<br />
mdogo abaki kwenye kiza na watu<br />
wachache waendelee kunufaika na<br />
rasilimali za nchi.<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />
MAKALA<br />
Soko huria lilivyoathiri upatikanaji<br />
wa habari vijijini<br />
Na Rashid Kejo<br />
Tulikotoka<br />
Nchi ya Tanzania tangu ilipopata<br />
uhuru wake mwaka 1961, ilikuwa<br />
ikitumia mfumo wa vyama vingi hadi<br />
mwaka 1965 ilipoamua kuachana<br />
nao. Hata hivyo mwaka 1992,<br />
Tanzania iliridhia mageuzi makubwa<br />
ya kurejea katika mfumo wa vyama<br />
vingi vya siasa.<br />
Sababu iliyotolewa mwaka 1965<br />
wakati wa kuachana na vyama vingi<br />
ni kwamba pamoja na mambo<br />
mengine, vyama vya upinzani<br />
ambavyo vilikuwapo kama vile<br />
African Independence Movement<br />
(AIM) na People’s Democratic<br />
(PDP), havikuwa na nguvu.<br />
Lakini pia wakati ule, kulikuwa na<br />
vuguvugu kubwa la mataifa mengi<br />
ya Afrika kuendeshwa chini ya<br />
utawala wa chama kimoja kutokana<br />
na kile kilichoelezwa kwamba ni<br />
kuleta umoja wa kitaifa na kuondoa<br />
mifarakano na migogoro kwa lengo<br />
la kujiletea maendeleo.<br />
Licha ya kuwa na chama kimoja<br />
kilichokuwa kimeshika hatamu, hata<br />
nyanja nyingine kuu na muhimu za<br />
kiuchumi na kijamii, kwa kiwango<br />
kikubwa zilikuwa chini ya umma.<br />
Vyombo vya habari kadhalika,<br />
vilikuwa katika mfumo dola. Redio,<br />
televisheni (kwa Zanzibar) na<br />
magazeti, ama vilimilikiwa moja<br />
kwa moja na Serikali, taasisi zake au<br />
chama na jumuiya zake.<br />
Tunakumbuka vyombo kama<br />
Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD),<br />
Sauti ya Tanzania Zanzibar (STZ),<br />
Magazeti ya Daily News/Sunday<br />
News, Uhuru/Mzalendo, Mfanyakazi<br />
na Mkulima wa Kisasa.<br />
Kutokana na uchache na umiliki<br />
wake, maudhui ya vyombo hivi<br />
yaliratibiwa na dola yakilenga<br />
masuala kadhaa ambayo Serikali<br />
ilikuwa imeyapa kipaumbele.<br />
Pamoja na changamoto zake,<br />
habari za wakulima zilipata fursa<br />
katika vyombo hivyo. Achilia mbali<br />
gazeti, kulikuwa na vipindi vya redio<br />
vya Mkulima wa Kisasa ambavyo<br />
vilitoa mafunzo na maelekezo<br />
mbalimbali ya kilimo bora.<br />
Kulikuwa pia na mkakati maalumu<br />
kupitia Taasisi ya Vielelezo wa<br />
kupeleka sinema vijijini kuelimisha<br />
wakulima juu ya ukulima na<br />
ufugaji bora. Kimsingi, kulikuwa na<br />
upatikanaji wa taarifa hasa zile za<br />
msingi kwa umma wa vijijini.<br />
Wahenga walisema, kila masika<br />
yana mbu wake. Katika mabadiliko<br />
ya mwaka 1992 yaliyoruhusu mfumo<br />
wa vyama vingi na soko huria,<br />
Serikali ilijitoa katika biashara na<br />
kulegeza masharti hivyo kuiwezesha<br />
sekta binafsi kushiriki moja kwa<br />
moja katika masuala ya kiuchumi<br />
na kijamii. Mabadiliko yalichochea<br />
kuanzishwa kwa Sera ya Habari na<br />
Utangazaji ya mwaka 1993.<br />
Hata hivyo, haikujitoa katika<br />
usimamizi na uendeshaji wa vyombo<br />
vyake vya habari, bali iliruhusu sekta<br />
binafsi nayo kuingia katika biashara<br />
hiyo. Hivyo, kuanzia mwaka 1992,<br />
magazeti, vituo vya televisheni<br />
na redio na baadaye mitandao ya<br />
mawasiliano vilianza kwa kasi.<br />
Tofauti na awali ambako<br />
mwelekeo wa habari ulilenga zaidi<br />
propaganda, safari hii mtazamo<br />
ulikuwa wa kibiashara zaidi na hali<br />
hiyo imekuwa na athari kubwa katika<br />
upatikanaji wa habari za vijijini.<br />
Kutokana na msukumo huo wa<br />
nguvu ya soko, vyombo ambavyo<br />
vilishindwa kujiendesha kibiashara<br />
vilikufa na hivyo ndivyo ilivyotokea<br />
kwa Gazeti la Mkulima wa Kisasa.<br />
Vipindi vingi vilivyoanzishwa katika<br />
redio na televisheni vililenga zaidi<br />
kuwavutia watangazaji (advertisers).<br />
Kwa upande mwingine, asilimia<br />
kubwa ya magazeti na machapisho<br />
husomwa zaidi mijini ambako<br />
usambazaji ni rahisi na kiwango cha<br />
kujua kusoma na kuandika ni kikubwa<br />
na hilo likawa na athari kubwa kwa<br />
upatikanaji wa habari za vijijini.<br />
Hiyo ilimaanisha kwamba<br />
wakulima na wananchi wengine<br />
waishio vijijini walianza kupewa<br />
habari ambazo hazikuwa na uwiano<br />
wa moja kwa moja na matatizo au<br />
vipaumbele vyao.<br />
Kwa mfano, mwaka 1995<br />
wakati taifa likiwa katika kampeni<br />
za kwanza tangu kurejeshwa kwa<br />
mfumo wa vyama vingi, baadhi ya<br />
vituo vya televisheni vilitumia fursa<br />
hiyo vibaya kwa kuonyesha picha za<br />
mauaji hivyo kuwatishia wananchi.<br />
Mabadiliko makubwa<br />
Hata hivyo, kadri miaka inavyosonga<br />
kumekuwa na mabadiliko makubwa.<br />
Kukua kwa teknolojia ya mawasiliano<br />
na dhana ileile ya soko kumevifanya<br />
vyombo vya habari kuanza kubaini<br />
umuhimu wa kulitazama soko la vijijini<br />
waliko asilimia 80 ya Watanzania.<br />
Halmashauri za wilaya na<br />
wawekezaji wengine wa ndani<br />
wameanzisha redio za jamii<br />
(community radio) ambazo zinatoa<br />
huduma ya habari katika maeneo<br />
yao. Hili limekuwa na mchango<br />
mkubwa kwa wananchi wa vijijini<br />
kwani taarifa, kero na shida zao<br />
zimekuwa zikipata fursa ya kusikika.<br />
Lakini siyo kusikika tu, kumekuwa<br />
na fursa kubwa zaidi ya kupata<br />
habari zinazokidhi mahitaji yao<br />
kwa kiwango kikubwa na hivyo<br />
kuchochea maendeleo yao.<br />
Ingawa wilaya zilizoanzisha radio<br />
hizi za jamii ni chache mno, lakini<br />
wilaya zilizobahatika kuwa na redio<br />
hizi, zimekuwa zikitumia fursa hiyo<br />
kufikisha ujumbe muhimu katika<br />
maeneo husika kama vile bei ya<br />
bidhaa na huduma nyingine muhimu.<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 11<br />
7
ANA KWA MFUMO ANA/MAKALA WA TAARIFA ZA MASOKO WA <strong>MVIWATA</strong><br />
(MAMIS)<br />
PATA BEI ZA MAZAO KWENYE SIMU YAKO POPOTE ULIPO!!<br />
Jinsi ya kupata taarifa kwenye simu yako:<br />
Masoko yaliyopo mpaka sasa:<br />
MOROGORO, TAWA, TANDAI, NYANDIRA, KIBAIGWA, DODOMA, IGUNGA, TABORA, SHINYANGA,<br />
MASWA, BARIADI, BUKOMBE, KAHAMA, KILOMBERO (ARUSHA), KARIAKOO, BUGURUNI, TEMEKE,<br />
IGURUSI (MBEYA), MKURANGA, MAKAMBAKO, SIMANJIRO, TAVETA, MKATA, IGAGALA, MATAI<br />
(RUKWA), KASANGA, HIMO, HOLILI, n.k<br />
Mazao yaliyo kwenye mfumo huu:<br />
MAHINDI, MCHELE, MAHARAGE, CHOROKO, KUNDE, MBAAZI, NJEGERE, MTAMA, UWELE, ULEZI,<br />
UFUTA, ALIZETI, NDIZI MBIVU, NDIZI MBICHI, MAGIMBI, MUHOGO, NANASI, CHUNGWA, PAPAI,<br />
EMBE, PARACHICHI, NYANYA, VITUNGUU MAJI, VITUNGUU SAUMU, TANGO, KAROTI, KABICHI,<br />
HOHO, LUBABU, SELELI, BITRUTI, ZUKINI, SALADI, KOLIFLAWA, TANGAWIZI, PILIPILI MTAMA,<br />
MDALASINI, ILIKI.<br />
...meseji moja kwa kila zao moja<br />
8<br />
imedhaminiwa na;<br />
Taarifa ya BEI ZA MAZAO<br />
1. Andika neno BEI acha nafasi<br />
2. Andika zao unalotaka bei yake mfano; MAHINDI<br />
3. Kisha tuma kwenda namba 0654 555 884<br />
Taarifa ya WAUZAJI<br />
1. Andika neno NANUNUA acha nafasi<br />
2. Andika zao unalotaka kununua mfano; MAHINDI<br />
3. Kisha tuma kwenda namba 0654 555 884<br />
Taarifa ya WANUNUZI:<br />
1. Andika neno NAUZA acha nafasi<br />
2. Andika zao unalotaka kuuza mfano; MAHINDI<br />
3. Kisha tuma kwenda namba 0654 555 884<br />
Kwa Mawasiliano zaidi piga SIMU NAMBA 0659250317<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />
MAKALA<br />
Taaluma ya habari ni wito<br />
Na Susuma Susuma<br />
Vyombo vya habari ni jina<br />
la jumla la mfumo wa<br />
mawasiliano unaojumuisha<br />
utangazaji wa redio, televisheni,<br />
majarida na magazeti. Vyombo<br />
hivi vina wajibu mkubwa wa<br />
kuhudumia matakwa ya jamii katika<br />
maisha yao ya kila siku. Vyombo<br />
vya habari vinaelimisha, vinatoa<br />
burudani na kutoa changamoto<br />
kwa wananchi na viongozi kuhusu<br />
mambo mbalimbali.<br />
Kadhalika taaluma ya habari ni<br />
tasnia nyeti inayoheshimika katika<br />
jamii yoyote inayothamini ustaarabu,<br />
umoja na utangamano wa kitaifa.<br />
Kuandika makala kwenye<br />
magazeti, kusoma taarifa ya habari<br />
au utayarishaji wa vipindi vya siasa,<br />
jamii, utamaduni, dini, burudani ama<br />
matukio yanayohitaji jamii kupewa<br />
taarifa, ni shughuli zinazohitaji<br />
ushirikiano wa kutosha baina ya<br />
wadau yaani waandishi, watoa habari<br />
na walaji (wasikilizaji/wasomaji).<br />
Kwa mantiki hiyo, ushirikiano<br />
madhubuti kati ya wadau wa habari<br />
na waandishi wa habari ni nguzo ya<br />
maendeleo katika jamii.<br />
Aidha, kufanikisha masuala<br />
haya kunahitaji umakini, weledi,<br />
mazingatio ya kufuata miiko, maadili<br />
na heshima kwa mwandishi ama<br />
mtangazaji husika.<br />
Utendaji kazi wa vyombo<br />
vya habari<br />
<strong>Uk</strong>ilinganisha miaka 50 iliyopita hali<br />
ya utendaji kazi wa vyombo vya<br />
habari na hali ilivyo hivi sasa nchini<br />
kwetu ni tofauti kabisa.<br />
Uandikaji wa habari, makala,<br />
utangazaji na utayarishaji wa vipindi<br />
hivi sasa hauzingatii ujuzi, taaluma na<br />
kuheshimu miiko, kama ilivyokuwa<br />
miaka ya awali.<br />
Fani hii imeshuhudia watu<br />
wanahitimu uandishi wa habari ngazi<br />
ya shahada ya kwanza au ya uzamili,<br />
lakini bado wakashindwa kuandika<br />
habari kwa usahihi.<br />
Kwa mfano eneo moja<br />
linalowashinda ni jinsi ya kufahamu<br />
mahitaji halisi ya wasomaji,<br />
wasikilizaji ama watazamaji wao,<br />
kushindwa kufahamu habari ilipo<br />
ama kushindwa kutofautisha habari,<br />
uzushi na fitina.<br />
Wapo wanaosema fani hii ni<br />
rahisi kuliko zote na hawa ndiyo<br />
wanaovamia fani hii na kudhani<br />
kwamba wanafanya vizuri bila<br />
kufahamu kuwa wanachangia kuua<br />
taaluma.<br />
Fani hii siyo rahisi kama<br />
inavyodhaniwa na wengi, na pengine<br />
ndiyo maana kila kukicha vyombo<br />
vya habari vinalaumiwa kwa kukiuka<br />
miiko na maadili kwa kuwa wengi<br />
wanaamua kujiunga wakidhani<br />
ni kuandika tu, matokeo yake<br />
wanafanya upotoshaji.<br />
Tumeshuhudia pia utitiri wa<br />
vyombo vya habari vinavyoanzishwa<br />
kila leo, lakini cha kushangaza vingi<br />
vinaanzishwa mijini na kuhudumia<br />
watu wa mijini tu na kuwaacha<br />
kando watu waishio vijijini.<br />
Kwa mujibu wa takwimu za<br />
Msajili wa Magazeti mpaka sasa<br />
amekwishasajili zaidi ya magazeti<br />
na majarida 350 ingawa ni asilimia<br />
15 tu ya machapisho hayo ambayo<br />
yanaonekana mitaani kwa wakati huu<br />
na asilimia kubwa yakiwa mijini. Idadi<br />
kubwa ya magazeti yaliyosajiliwa<br />
yanamilikiwa na watu au makampuni<br />
binafsi isipokuwa magazeti ya ”Daily<br />
News, Sunday News na Habari leo”<br />
ambayo yanamilikiwa na Serikali na<br />
gazeti la Uhuru linalomilikiwa na<br />
chama tawala CCM. <strong>Uk</strong>ipekuwa<br />
kwa undani utendaji kazi wa<br />
magazeti haya sasa yako kibiashara<br />
zaidi kinyume na matarajio ya kutoa<br />
huduma ya kuhabarisha umma.<br />
Vyombo vya habari<br />
vinapoanzishwa vikiwa na mlengo<br />
wa kibiashara zaidi, ni moja ya<br />
sababu inayochangia vyombo vingi<br />
virundikane mjini ambako wamiliki<br />
wanaamini watauza na kupata<br />
matangazo ya kutosha. Na hoja hapa<br />
ni Je, jamii ya huko vijijini ambako<br />
biashara ya radio, televisheni na<br />
magazeti hazilipi, itafikiwaje na habari<br />
zenye kuchochea maendeleo?<br />
Kufanya hivi vyombo vya habari<br />
vinakiuka sheria na kuwanyima haki<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 10<br />
<strong>MVIWATA</strong> katika kusaidia wakulima kupaza sauti zao, imekuwa ikiwawezesha wanahabari<br />
kuyafikia maeneo ya vijijini na kuchukua habari za kero zao<br />
9
MAKALA<br />
Taaluma ya habari ni wito...<br />
Inatoka uk. wa 9<br />
ya msingi wananchi wa vijijini.<br />
Katiba ya Jamhuri ya Muungano<br />
wa Tanzania (1977) ambayo ilifanyiwa<br />
marekebisho mwaka 1984, imeweka<br />
kifungu maalum kinachotaja wazi<br />
kuwa habari ni haki ya msingi ya raia.<br />
Kifungu hicho cha <strong>18</strong> cha Katiba<br />
kinasema:<br />
(1) Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila<br />
mtu yuko huru kuwa na maoni<br />
yoyote na kutoa nje mawazo<br />
yake, na kutafuta, kupokea na<br />
kutoa habari na dhana zozote<br />
kupitia chombo chochote bila<br />
ya kujali mipaka ya nchi, na<br />
pia uhuru wa mawasiliano yake<br />
kutoingiliwa kati.<br />
(2) Kila raia anayo haki ya kupewa<br />
taarifa wakati wowote kuhusu<br />
matukio mbalimbali nchini na<br />
duniani kote, ambayo ni muhimu<br />
kwa maisha na shughuli za<br />
wananchi; na pia juu ya masuala<br />
muhimu kwa jamii.<br />
Wajibu wa vyombo vya<br />
habari<br />
Njia muhimu za kuwezesha<br />
wananchi kufurahia haki ya kupasha<br />
na kupashwa habari na kujieleza<br />
kwa kutoa maoni hadharani bila<br />
bughudha,vitisho na ukandamizwaji<br />
ni kupitia vyombo vya habari.<br />
Kutokana na umuhimu wa kipekee<br />
wa haki hii ya msingi, nafasi ya<br />
vyombo vya habari katika utekelezaji<br />
wake pia ni ya kipekee. Kwa kuwa<br />
vyombo vya habari vinawawezesha<br />
wananchi kutumia haki hii ili isibaki<br />
nadharia au kwenye maandishi tu,<br />
hakuna budi wamiliki wa vyombo vya<br />
habari pamoja na serikali, watambue<br />
na kukiri kwamba nafasi yao ni ya<br />
kutoa huduma au mahitaji ya lazima<br />
kwa jamii, huduma kwa umma.<br />
Hadhi ya huduma ya kijamii<br />
inazidi sana ile ya bidhaa ambazo<br />
huuzwa kuingiza faida. Ndiyo maana<br />
wajibu wa wamiliki wa vyombo vya<br />
habari kwa jamii ni mkubwa kuliko<br />
wa mfanyabiashara ama mwekezaji<br />
ambao msukumo wao mkubwa ni<br />
10<br />
kutengeneza faida.<br />
Hata vyombo vya habari vya<br />
serikali vinapaswa kuwajibika kwa<br />
umma na sio utashi wa kisiasa wa<br />
wanasiasa na watawala.<br />
Wanahabari pamoja na kwamba<br />
huajiriwa na wamiliki wa vyombo,<br />
bado huwajibika kwa umma. Na<br />
ndiyo maana ili vyombo vya habari<br />
viweze kutekeleza majukumu<br />
yao, hakuna budi kwa wahariri na<br />
wanahabari kuwa na uhuru wa<br />
kutosha kukusanya, kuchambua<br />
na kusambaza habari bila woga,<br />
shinikizo au ushawishi wa wamiliki<br />
na washiriki wao kibiashara.<br />
Habari ni huduma<br />
Kazi ya uandishi wa habari ni fani<br />
ambayo pamoja na kuwa na ujuzi<br />
lakini inahitaji zaidi wito. Ni fani<br />
ambayo inahitaji zaidi mtu kutanguliza<br />
utu na upendo ama dhana ya kutoa<br />
huduma kuliko malipo ama kufanya<br />
biashara. Ni fani isiyojali sana malipo<br />
yenye kulingana na kadhia, ugumu<br />
wala masuala mengine kwa kuwa<br />
kuna wakati unakuwa unashughulikia<br />
tatizo la kijamii iliyo masikini ambayo<br />
malipo yake ni asante.<br />
Kinachosikitisha zaidi ni kuona<br />
baadhi ya waandishi wa habari<br />
wakishabikia zaidi kuandika habari<br />
za migogoro na kuwachafua watu,<br />
wakati mwingine wakiishia kudai<br />
posho bila hata kuandika chochote.<br />
Hali hii inaonesha walivyokosa<br />
ushirikiano na jamii.<br />
Pia zipo sheria ambazo<br />
zinaonekana kukandamiza uhuru wa<br />
vyombo vya habari nchini, ambazo<br />
wanahabari wamekuwa wakizipigia<br />
kelele kwa kuitaka serikali<br />
kuzirekebisha ama kuzifuta kabisa.<br />
Hizi ni pamoja na sheria ya magazeti<br />
ya Tanzania ya mwaka 1976 ambayo<br />
inampatia uwezo waziri anayehusika<br />
na habari wa kulifungia gazeti lolote<br />
lile kama ataridhika kuwa limekiuka<br />
kwa kiasi kikubwa matakwa ya sheria<br />
hiyo. Sheria hizi pia zinakwamisha<br />
upatikanaji wa habari sahihi zenye<br />
maslahi umma.<br />
Mfano halisi ni wa taarifa<br />
zinazohusiana na kashfa kwenye<br />
migodi ya madini na kwenye sekta ya<br />
uwindaji wanyama kwenye mbuga za<br />
wanyama ambazo zinaakisi uchumi<br />
wa nchi.<br />
Serikali inapaswa kupitisha sheria<br />
rafiki kwa vyombo vya habari na<br />
ambazo zinaweka mazingira huru ya<br />
upatikanaji wa habari, kwani kuvifunga<br />
minyororo vyombo vya habari ni<br />
kuwafunga minyororo wananchi.<br />
Kwa upande mwingine wapo<br />
waandishi wa habari wanaotishiwa<br />
maisha pale wanapofuatilia ili kupata<br />
habari za kina kuhusiana na jambo<br />
fulani lenye maslahi kwa jamii. Lakini<br />
hiyo siyo sababu ya wao kufanya<br />
shughuli zao kinyume cha sheria na<br />
maadili ya taaluma yao kama vile<br />
kutoa na kupokea rushwa, upotoshaji<br />
na udanyanyifu, uchochezi, ushabiki,<br />
kutunga ama kutia chumvi habari.<br />
Hata hivyo changamoto ni sehemu<br />
ya maisha, ni chachu kwa maendeleo<br />
yoyote, wanahabari ni vyema<br />
tukajenga tamaduni ya kwenda<br />
vijijini kuzungumza na kutangaza<br />
habari za mafanikio, ubunifu, uzoefu<br />
na mbinu wanazotumia wanavijiji<br />
kutatua changamoto za maisha yao<br />
ya kila siku.<br />
Kwa kuwa tumeamua<br />
kuwatumikia wananchi wenye<br />
uhitaji wa huduma yetu, hatuna<br />
budi kuzikabili changamoto zote<br />
za kutafuta, kuandaa na kuzifikisha<br />
habari kwa wadau bila kujali<br />
zinapatikana kutoka mazingira yenye<br />
changamoto nyingi.<br />
Kwa upande mwingine liko kundi<br />
dogo la wanahabari nchini ambao<br />
wamepungukiwa utu na upendo,<br />
wametanguliza zaidi maslahi binafsi,<br />
ndiyo maana wameigeuza fani hii<br />
kuwa biashara badala ya huduma<br />
kwa jamii. Kundi hili japokuwa ni<br />
dogo lakini laweza kuwa na madhara<br />
makubwa kwa jamii hasa kipindi hiki<br />
ambao vitendo vya ufisadi vinazidi<br />
kushika kasi ndani ya nchi yetu.<br />
Wakialikwa kwenda kuchukua habari<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 11<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
Soko huria lilivyoathiri...<br />
Inatoka uk. wa 7<br />
Inawezekana bado kuna vikwazo<br />
vya hapa na pale katika kuwafikia<br />
wananchi wa vijijini walio wengi, lakini<br />
muhimu ni kuviimarisha zaidi vyombo<br />
hivi ili walau viweze kuziba pengo<br />
lililosababishwa na kutoweka kwa<br />
majarida kama ya mkulima wa kisasa.<br />
Mamlaka za miji na wilaya nchini<br />
ni mali ya wananchi kupitia mabaraza<br />
ya madiwani ambao wanatokana na<br />
kura za watu katika ngazi za kata.<br />
Kwa maana hiyo basi ni fursa kwa<br />
viongozi hawa wawakilishi wa umma<br />
(madiwani), kuimarisha usimamizi<br />
wa vituo vya redio na televisheni<br />
vinavyomilikiwa na halmashauri zao<br />
ili viweze kukidhi matakwa ya jamii<br />
husika, ziwe za wakulima, wafugaji,<br />
wavuvi, wachuuzi au wengineo.<br />
Hii ni moja ya hatua muhimu<br />
zinazoweza kuwarejesha wazalishaji<br />
wadogo wa sekta mbalimbali nchini<br />
katika dunia ya mawasiliano.<br />
Intaneti na simu za mkononi<br />
Tunapozungumzia habari, hatuwezi<br />
kuacha kuzungumzia njia nyingine<br />
za kisasa za mawasiliano kama vile<br />
intaneti na simu za mkononi. Hizi kwa<br />
ujumla wake zimekuwa na mchango<br />
mkubwa kwa wananchi wa vijijini<br />
katika mambo mbalimbali.<br />
Intaneti kwa mfano, imewawezesha<br />
wananchi kutafuta masoko, masomo<br />
na kuwasiliana kwa sababu mbalimbali<br />
na taasisi, ndugu, jamaa na marafiki zao<br />
walio mbali.<br />
Zamani ilikuwa ni gharama kubwa<br />
na usumbufu kuwasiliana kwa njia ya<br />
barua na ndugu walio mbali. Lakini<br />
sasa, katika baadhi ya maeneo ya<br />
vijijini kuna vituo vya mawasiliano<br />
ambako wananchi huenda na kupata<br />
huduma hizo za mtandao (simu/<br />
intaneti) na hivyo kupata taarifa<br />
mbalimbali za shughuli zao na pia<br />
kuwasiliana na watu mbalimbali.<br />
Magazeti mengi ya ndani na<br />
nje na hata redio zimeunganishwa<br />
pia katika mitandao hii ya intaneti,<br />
hivyo wananchi popote walipo<br />
wanaweza kusoma habari za leoleo<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />
hivyo kujiweka katika nafasi nzuri ya<br />
kuujua ulimwengu na yanayoendelea<br />
na kutumia taarifa hizo kujiongezea<br />
maarifa na kujiendeleza.<br />
Njia hii ya simu ndiyo imekuwa<br />
na athari chanya kubwa. Idadi kubwa<br />
ya Watanzania mijini na vijijini hivi<br />
sasa wanafaidika kwa huduma hii<br />
iwe moja kwa moja au kupitia kwa<br />
ndugu na jamaa zao.<br />
Upashanaji wa habari ulikwaza<br />
mambo mengi ya watu waishio<br />
vijijini lakini baada ya mapinduzi ya<br />
teknolojia hii, si ajabu hivi sasa kwa<br />
mfano, mtu aliye kijijini kumweleza<br />
au kumpa taarifa aliye mjini juu ya<br />
tukio lililotokea huko huko mjini.<br />
Mara ngapi tumesikia watu<br />
waishio Dar es Salaam wakipewa<br />
taarifa za msiba uliotokea hukohuko<br />
Dar es Salaam na mtu aishie<br />
kijijini? Kimsingi mawasiliano<br />
hayo yamevunja umbali baina ya<br />
watu wa maeneo haya. Japokuwa<br />
haya yanatokea kwenye maeneo<br />
machache mno ya vijijini ambayo<br />
yamebahatika kuunganishwa na<br />
huduma za simu za mkononi.<br />
Mapinduzi mengine chanya<br />
yaliyotokana na uwepo wa mawasiliano<br />
haya ya simu ni utumaji na upokeaji wa<br />
fedha kupitia mitandao ya simu.<br />
Usumbufu wa kuwatumia wazazi<br />
kijijini fedha au kuwalazimu wakulima<br />
na wafanyabiashara kusafiri kwenda<br />
mjini au kijijini kununua au kuuza<br />
bidhaa siku hizi hauna ulazima. Baada<br />
ya kuingia makubaliano, mkulima<br />
anaweza kufungasha mazao yake na<br />
kuyatuma mjini na kutumiwa fedha<br />
kwa njia ya simu na hayo hufanyika<br />
ndani ya muda mfupi mno. Zaidi ya<br />
hayo huduma za mawasiliano ya simu<br />
zimepanua wigo wa ajira kwa vijana<br />
vijijini na kuongeza kipato, hivyo<br />
basi wananchi wanapaswa kuitumia<br />
vyema fursa hiyo kwa kuifanya kuwa<br />
kichochocheo cha maendeleo yao.<br />
Mwandishi wa Makala hii ni<br />
Mhariri wa Habari wa Gazeti<br />
la Mwananchi<br />
Taaluma ya habari<br />
ni wito...<br />
Inatoka uk. wa 10<br />
MAKALA<br />
kijijini, swali la kwanza wanalouliza ni<br />
watalipwa? nani atawalipa? kiasi gani<br />
watalipwa? Wakishapewa majibu<br />
kuwa hakuna malipo kwa kuwa<br />
kazi hiyo ni sehemu ya utekelezaji<br />
wa majukumu yao, wanaishia kutoa<br />
visingizio vya kutoenda kufanya kazi<br />
hiyo.<br />
Wanahabari tunapaswa<br />
kujitambua kuwa sisi ni nguzo<br />
muhimu ya maendeleo katika<br />
jamii hivyo tunatakiwa kujenga<br />
ushirikiano madhubuti baina yetu<br />
na wadau wa habari wakati wa<br />
kutekeleza majukumu ya kuipasha<br />
habari jamii kwa uaminifu na<br />
kudhihirisha kuwa tulioko kwenye<br />
taaluma hii tuna wito.<br />
Aidha ni muhimu kwa umma<br />
kuwa na imani na wanahabari<br />
kuwa wanachofanya ni sehemu<br />
ya utekelezaji wa majukumu<br />
kama ilivyo kwa watumishi<br />
wa sekta nyingine na kwamba<br />
hawana sababu ya kuwaogopa,<br />
kujenga chuki ama kuwapa taarifa<br />
za uongo na uchochezi, bali<br />
washirikiane nao kwa ukaribu.<br />
Ni vyema kila kundi likajali na<br />
kuheshimu uhuru wa kutoa na<br />
kupata habari kama ilivyo ndani<br />
ya katiba ya nchi.<br />
Jihadhari na<br />
maambukizo ya<br />
UKIMWI<br />
jikinga na umlinde<br />
mwenzako<br />
11
KAMERA<br />
12<br />
KAMERA YA <strong>MVIWATA</strong> MITANDAONI<br />
Wakulima wa kata ya Mlangali wilayani Ludewa wakioneshana<br />
jambo lililowavutia kwenye gazeti la Pambazuko linaloandika habari<br />
za wakulima na kusambazwa vijijini<br />
Moja ya mikutano ya mitandao ya wakulima ambayo imekuwa<br />
ikitumika kupashana habari vijijini<br />
Picha ya pamoja ya baadhi ya viongozi na watumishi wa <strong>MVIWATA</strong><br />
na wawakilishi wa ubalozi wa Ireland nchini Bibi Aileen D’donovan,<br />
Dkt Sizya Lugeye na Bw. Vicent Akuluyuka (wa nne hadi wa sita<br />
kutoka kushoto waliosimama), baada ya ujumbe huo kutembelea<br />
makao makuu ya <strong>MVIWATA</strong> yaliyoko Morogoro Julai 5, 2011.<br />
Bibi HotensiaThomas, mwenyekiti wa Bodi ya Soko la Wakulima<br />
Nyandira akisikiliza swali kwa mmoja wa wadau wa masoko ya<br />
Igurusi, Matai na Kasanga walipofanya ziara sokoni hapo Julai 21,<br />
2011<br />
Wana-<strong>MVIWATA</strong> walioshiriki Tamasha la Jinsia Septemba 2011<br />
wakimsikiliza mwenzao wakati wa majadiliano<br />
Wana-<strong>MVIWATA</strong> Kiteto Manyara walioshiriki mafunzo ya kujengea<br />
uwezo viongozi Julai 28-29, 2011, wakiwa na baadhi ya watumishi<br />
wa <strong>MVIWATA</strong> taifa waliowezesha mafunzo hayo<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
KAMERA YA <strong>MVIWATA</strong> MITANDAONI<br />
<strong>Uk</strong>osefu wa habari sahihi za masoko vijijini unasababisha bidhaa za<br />
wajasiliamali kama hawa wa Kwekanga Lushoto kukosa soko<br />
Wakulima wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kushiriki<br />
Jukwaa la Wakulima mkoani Ruvuma<br />
Wanawake jamii ya wafugaji wilayani Monduli, wakishiriki kazi ya<br />
kuchimba msingi na kuweka mawe ya msingi ya jengo la kukusanyia<br />
la kituo cha kibiashara<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />
KAMERA<br />
‘Natangaza kazi za mikono’, ndivyo anavyoelekea kusema mama<br />
huyu mkazi wa kijiji cha Kwalei wilayani Lushoto<br />
Bibi Elizabeth Lagwen (kulia) Mwenyekiti wa mtandao wa msingi<br />
Mamire Babati Vijijini akiwasikiliza wageni kutoka shirika la TRIAS<br />
Ubeligiji waliomtembelea kujifunza shughuli anazozifanya<br />
Licha ya kuwa na historia ya ufugaji pekee, jamii ya Wamasai sasa<br />
wamebadlika na kuanza kushiriki kilimo kama wanawake hawa<br />
walivyokutwa na kamera yetu wakipanda mazao shambani<br />
13
KUTOKA MITANDAONI<br />
Maonesho ya NaneNane 2011<br />
Wakulima wazungumzia matumizi na faida<br />
za bidhaa walizoonesha<br />
Na Goodness Mrema, Morogoro<br />
Mtandao wa vikundi<br />
vya wakulima Tanzania<br />
(<strong>MVIWATA</strong>) katika<br />
kuhakikisha kwamba unatekeleza<br />
vyema majukumu yake umekuwa<br />
na utaratibu wa kuwawezesha<br />
wakulima toka mikoa mbalimbali<br />
kushiriki kuonesha bidhaa zao<br />
kwenye maonesho ya kilimo<br />
maarufu kama NaneNane.<br />
Mwaka 2011 katika maonesho<br />
hayo ya wakulima <strong>MVIWATA</strong><br />
iliwawezesha wakulima zaidi ya 40<br />
kushiriki maonesho hayo kwenye<br />
viwanja vya Mwalimu Nyerere<br />
Morogoro na Themi Arusha, kwa<br />
lengo la kuwapatia fursa ya kujifunza,<br />
kubadilishana uzoefu na kutangaza<br />
bidhaa zao. Katika maonesho hayo<br />
<strong>MVIWATA</strong> ilipata ushindi wa kwanza<br />
kwa upande wa vyama na mashirika<br />
yasiyo ya kiserikali kwenye uwanja<br />
wa maonesho ya NaneNane kanda<br />
ya Mashariki wa Mwalimu Nyerere<br />
Morogoro na katika kanda ya<br />
Kaskazini kwenye viwanja vya Themi<br />
<strong>14</strong><br />
Arusha na kukabidhiwa zawadi ya<br />
Kombe na Cheti vilivyotolewa na<br />
Waziri Mkuu Bw. Mizengo Pinda.<br />
Aidha kwenye viwanja vya Themi<br />
Arusha mkulima Bw. Richard Kipara<br />
ambaye ni katibu wa Mtandao wa<br />
Vikundi vya Wakulima Ekenywa<br />
(MVIWAEKE) alishinda kuwa<br />
‘Mkulima Bora’ wa wilaya mpya ya<br />
Arusha Vijijini.<br />
Katika maonesho hayo mfugaji<br />
Bw. Moses Ndoipo kutoka wilaya ya<br />
Longido, alileta mbuzi bora aina ya<br />
Isiolo wa uzito wa kilo 240 aliyekuwa<br />
anauzwa Sh. 300,000 na kuwa<br />
kivutio kwa wageni waliotembelea<br />
maonesho.<br />
Miongoni mwa wakulima waliopata<br />
fursa ya kushiriki maonesho haya<br />
ya NaneNane kwenye viwanja<br />
vya Mwalimu Nyerere Morogoro,<br />
walielezea umuhimu wa bidhaa<br />
walizoonesha na faida ya maonesho<br />
kwa ujumla.<br />
Kakao na Mawese<br />
Bibi Lain Mwakatundu kutoka<br />
Kyela, Mbeya alikuwa na zao la<br />
mawese na kakao ambapo<br />
alisema usindikaji wa mawese<br />
unawezesha utengenezaji wa bidhaa<br />
mbalimbali muhimu kama vile sabuni<br />
ya kufulia na kuogea.<br />
Lain Mwakatundu<br />
“Vile vile kutokana na mawese<br />
unaweza kupata mbosa ambayo<br />
hutengeneza mafuta ya kupikia<br />
na kupaka. Mafuta haya ya kupaka<br />
yanafaida kubwa ikiwemo ya<br />
kuponya mba wa ngozi katika mwili<br />
wa binadamu. Aidha magamba ya<br />
mawese hutumika kwa ajili ya kuni.<br />
Kwa upande wa zao la kakao<br />
alisema lina matumizi mengi<br />
ingawaje matumizi yanayofahamika<br />
zaidi kwa watu ni utengenezaji<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 15<br />
Mwenyekiti wa <strong>MVIWATA</strong> Morogoro Bw. Stanford Chabonga aliyenyanyua juu kikombe, akiungwa mkono na wana-<strong>MVIWATA</strong> wenzake<br />
kusherehekea ushindi<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
Inatoka uk. wa <strong>14</strong><br />
wa kinywaji na kitafunwa aina ya<br />
chocolate. Akaongeza kuwa “ndani<br />
ya tunda la kakao kuna mbegu zenye<br />
ladha ya sukari ambazo hutumika<br />
kutengeneza juisi lakini pia juisi hiyo<br />
waweza kuichachusha na kupata<br />
kilevi baada ya kuiweka kwa muda<br />
wa siku tatu hadi nne.”<br />
“Mbegu hizi za kakao pia<br />
zikikaushwa na kusagwa hupatikana<br />
unga laini ambao unafaa kwa<br />
matumizi mengi ikiwemo kuweka<br />
kama kiungo kwenye mboga na<br />
wengine hutafuna unga pekee maan<br />
unaradha nzuri,” anafafanua.<br />
Bibi. Mwakatundu anafafanua zaidi<br />
kuwa zao la kakao ni dawa nzuri<br />
ya kupunguza kasi ya ugonjwa wa<br />
kisukari mwilini na pia hupunguza<br />
mafuta ndani ya mwili wa binadamu,<br />
hivyo anawahimiza watanzania<br />
kulitumia zaidi.<br />
Anaeleza kuwa katika mkoa wa<br />
Mbeya hususan wilaya ya Kyela mazao<br />
ya Kakao na Mawese hulimwa kwa<br />
ajili ya chakula na biashara japokuwa<br />
soko lake kwa sasa siyo zuri. Hata<br />
hivyo anaongeza kuwa maonesho ya<br />
mwaka huu yamemsaidia kupanua<br />
wigo wa soko kwani hivi sasa<br />
amepokea maombi ya wateja wengi<br />
wanaohitaji bidhaa na wengine<br />
wameomba aende kuwafundisha<br />
kilimo cha mazao hayo.<br />
Tiba asili<br />
Mzee Hassan Nundu kutoka<br />
kijiji cha Chamkoroma wilaya ya<br />
Kongwa - Dodoma, yeye alionesha<br />
dawa za asili zinazotokana na<br />
magome na mizizi ya miti ambazo<br />
zinaaminika kutibu magonjwa<br />
mbalimbali ya binadamu kama vile<br />
meno, tumbo, athma pamoja na<br />
kideri cha kuku.<br />
Akielezea matibabu ya ugonjwa<br />
wa vidonda vya tumbo, anasema<br />
mgonjwa anayetumia dawa hiyo<br />
anapona kwa muda mfupi hata kama<br />
vidonda ni vya muda mrefu. “Dawa<br />
hii ambayo ni mchanganyiko wa<br />
mizizi ya miti mbalimbali, mtumiaji<br />
huchanganya na maziwa mabichi<br />
kwa kuweka kijiko kimoja cha<br />
dawa katika kikombe cha maziwa<br />
na kunywa mara tatu kwa siku kwa<br />
muda wa siku kumi na tano tu.”<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />
“Dawa nyingine ni ya fangasi<br />
ambapo fangasi hawa huwa tumboni<br />
na kwenye mapacha ya vidole vya<br />
miguu kutokana na joto linalokuwepo<br />
ndani ya kiatu kufuatia msuguano<br />
wa miguu ya mtu anapotembea.<br />
Dawa hii ya unga inampasa mgonjwa<br />
kuiweka kwenye maji baridi na kisha<br />
kuichuja ili kupata mabaki ambayo<br />
atayapaka sehemu zilizoathirika na<br />
baadaye kunywa dawa iliyochujwa<br />
mara tatu kwa siku kwa muda wa<br />
siku tatu na atapona kabisa.”<br />
Bw. Nundu anafafanua kuwa<br />
athma ni ugonjwa ambao hauna tiba<br />
hospitalini bali hutulizwa lakini yeye<br />
anayo dawa ya kutibu ugonjwa huu<br />
ambayo inapatikana kwenye vipaketi<br />
vitatu. Mgonjwa anapaswa kuiloweka<br />
na kuichuja kisha kunywa mara mbili<br />
kwa siku asubuhi na jioni.<br />
“Ninawashauri Watanzania<br />
kurudia dawa zao za asili<br />
zinazotokana na mizizi na magome<br />
ya miti kwani hazina kemikali<br />
zitakazowadhuru kiafya tofauti na<br />
dawa za hospitalini ambazo nyingi<br />
sasa ni bandia na kuongeza kuwa<br />
anazo dawa nyingi za asili zinazotibu<br />
maradhi ambayo hayawezi kutibiwa<br />
hospitalini kama vile kukojoa<br />
kitandani pamoja na meno ambayo<br />
mara nyingi hung’olewa badala ya<br />
kutibiwa.<br />
Mzee Nundu anasema maonesho<br />
ya NaneNane ambayo amekuwa<br />
akishiriki yanamsaidia kupata wateja<br />
wapya na kukutana na wagonjwa<br />
aliowatibu miaka ya nyuma ambao<br />
wanashuhudia kuponywa na dawa<br />
zake.<br />
Bibi Hortenzia Thomas kutoka<br />
kijiji cha Nyandira Mvomero, mkoani<br />
Morogoro alifika katika maonesho<br />
hayo kutangaza tiba asili itokanayo<br />
na matunda na mbogamboga<br />
zikiwemo njegere, sereri, cornflower,<br />
maharagwe, redishi, boga, nzukini,<br />
pasili na kabichi.<br />
Anaeleza kuwa kabichi huponya<br />
ugonjwa wa kisukari. Hii ni baada ya<br />
mgonjwa kuchukua mti wa katikati ya<br />
kabichi kuukatakata na kuuchemsha,<br />
kisha kunywa maji yake mara tatu<br />
kwa siku. Pia mboga mboga kama<br />
Radishi na tenepsi hutumika kutibu<br />
vidonda vya tumbo na shinikizo la<br />
damu.<br />
KUTOKA MITANDAONI<br />
Bibi Mwajuma Mwiyoha,<br />
ni mkulima kutoka Chamkoroma<br />
ambaye alifika kwenye maonesho<br />
haya akiwa na zao la Alizeti ambalo<br />
ni maarufu kwa kutengeneza mafuta<br />
ya kupikia. Hata hivyo, kwa mkulima<br />
huyo zao la Alizeti siyo kwa ajili<br />
ya kukamua mafuta pekee bali pia<br />
hulitumia kutengeneza dawa ya<br />
kuhifadhia mazao galán, dawa ambayo<br />
haina madhara kwa watumiaji.<br />
Mwajuma Mwiyoha<br />
“Dawa hii ya kuhifadhia mazao<br />
hutokana na masuke ya alzeti<br />
hutengenezwa kwa teknolojia<br />
rahisi tu ambayo mkulima yeyote<br />
anaweza kumudu kwani cha kufanya<br />
ni kuyachoma masuke ya alizeti<br />
kwenye chombo kisafi, yakishaungua<br />
vizuri hutwangwa na kuchekechwa<br />
ili kupata majivu laini ambayo<br />
ndio dawa yenyewe. Dawa hii<br />
hunyunyizwa juu ya magunia yenye<br />
mazao na ina uwezo wa kuzuia<br />
mazao yasishambiliwe na wadudu<br />
kwa muda wa miaka miwili hadi<br />
mitatu.<br />
Bibi. Mwiyoha anasema dawa hii<br />
ni nafuu kwani haimwingizii mkulima<br />
gharama na ni salama kwa afya ya<br />
binadamu.<br />
Ufugaji wa nyuki wadogo<br />
Bw. Hassan Haji kutoka Zanzíbar<br />
ni mkulima mdogo anayefuga nyuki<br />
wadogo wasiouma.<br />
Mkulima huyu ameanza ufugaji wa<br />
nyuki wasiouma miaka 15 iliyopita.<br />
Alianza ufugaji wa nyuki hao kama<br />
mradi wa kiuchumi lakini pia kwa<br />
lengo la kuwahifadhi baada ya kuona<br />
kwamba wako hatarini kutoweka<br />
kutokana ukataji wa miti katika<br />
maeneo ya misitu vitendo ambavyo<br />
vinawafanya viumbe hao kukimbia<br />
na hivyo kizazi hicho kupotea.<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 17<br />
15
KUTOKA MITANDAONI<br />
16<br />
Ludewa wahimizwa kuwekeza<br />
kwenye kilimo cha miti<br />
Na Susuma Susuma, Ludewa<br />
Wakulima wilayani<br />
Ludewa na nchini kote<br />
wametakiwa kuwekeza<br />
zaidi katika upandaji wa miti<br />
kibiashara ili kuhifadhi mazingira<br />
na kujiongezea kipato kutokana<br />
na soko la miti kuongezeka kila<br />
mwaka.<br />
Wito huo umetolewa na Naibu<br />
Mkurugenzi wa Shirika la Swedish<br />
Cooperative Center (SCC) Kanda<br />
ya Mashariki mwa Afrika Bw. George<br />
Onyango alipokuwa akizungumza na<br />
wakulima wa kata za Mlangali na<br />
Milo wilayani Ludewa katika mkoa<br />
mpya wa Njombe.<br />
Bw. Onyango alikuwa kwenye<br />
ziara ya kukagua maendeleo ya<br />
mradi wenye lengo la kuwawezesha<br />
wakulima wadogo kuwa na uzalishaji<br />
wenye kukuza na kuongeza kipato<br />
na uhifadhi wa mazingira na bioanuai<br />
Uharibifu<br />
huu tuliufanya sisi katika<br />
harakati za kujitafutia riziki, na<br />
tunaoathirika na uharibifu huu ni sisi, hivyo<br />
ni sisi wenyewe ndiyo tunapaswa kurejesha<br />
uhai wa mazingira yetu kwa kuwekeza kwenye<br />
upandaji miti na kwa kufanya hivi tutasaidia<br />
kupunguza athari za mabadiliko ya<br />
tabia ya nchi<br />
k a t i k a<br />
Ziwa Nyasa unaotekelezwa na<br />
Mtandao wa Vikundi vya Wakulima<br />
Wadogo Tanzania (<strong>MVIWATA</strong>) kwa<br />
kushirikiana na SCC.<br />
Bw. Onyango alisema biashara ya<br />
miti na mazao yake, inakuwa kila siku<br />
na kupanda bei, hivyo kwa kuwekeza<br />
zaidi kwenye upandaji miti wakulima<br />
hao watapata mapato mazuri kuliko<br />
hata wanayoyapata kwenye mazao<br />
Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Swedish Cooperative Center (SCC) Kanda ya Mashariki mwa<br />
Afrika Bw. George Onyango (aliyenyosha mkono) akizungumza na wakulima wa kata ya Mlangali<br />
ya chakula wanayolima.<br />
Aidha aliwataka wakulima hao<br />
kuunda mitandao imara itakayofanya<br />
kazi ya kutafuta na kusimamia soko<br />
la mazao ya miti ili kuondokana na<br />
walanguzi ambao sasa wananeemeka<br />
kwenye biashara ya mazao ya chakula<br />
ya wakulima.<br />
Naibu mkurugenzi<br />
huyo alisema licha ya<br />
kuwaingizia utajiri,<br />
kilimo cha miti<br />
kitasaidia kwa<br />
kiwango kikubwa<br />
katika utunzaji<br />
wa mazingira ya<br />
wilaya hiyo ambayo<br />
yameharibiwa kutokana<br />
na shughuli za kibinadamu<br />
zikiwemo ukataji miti kwa ajili ya<br />
kupata nishati ya mkaa na kuni.<br />
“Uharibifu huu tuliufanya sisi<br />
katika harakati za kujitafutia riziki,<br />
na tunaoathirika na uharibifu<br />
huu ni sisi, hivyo ni sisi wenyewe<br />
ndiyo tunapaswa kurejesha uhai<br />
wa mazingira yetu kwa kuwekeza<br />
kwenye upandaji miti na kwa kufanya<br />
hivi tutasaidia kupunguza athari za<br />
mabadiliko ya tabia ya nchi,” alisema<br />
Bw. Onyango.<br />
Aliwahimiza wakulima hao<br />
kutumia vyema elimu ya uhifadhi wa<br />
mazingira, ujasiriamali na usimamizi<br />
wa vikundi inayotolewa kupitia<br />
mradi huo.<br />
Kwa upande wake afisa<br />
anayesimamia mradi huo wilayani<br />
Ludewa Bw.Remmy Urio alisema<br />
matokeo ya mafunzo yaliyotolewa<br />
kwa wakulima yameanza kuonekana<br />
baada ya wengi wao kuanza kupanda<br />
miti kwenye maeneo ya wazi na<br />
wameimarisha usimamizi wa sheria<br />
zinazolinda mazingira.<br />
Bw. Urio alisema wakulima wengi<br />
pia wameibua miradi ya kiuchumi<br />
ikiwemo uanzishaji wa SACCOS<br />
ili kuwawezesha kuboresha kipato<br />
badala ya kutegemea kipato kutoka<br />
kwenye kazi zinazochangia uharibifu<br />
wa mazingira.<br />
Afisa Programu wa <strong>MVIWATA</strong><br />
Bw. Laurent Kaburire alisema, utafiti<br />
uliofanywa na <strong>MVIWATA</strong> kwenye<br />
wilaya zinazounganishwa na Ziwa<br />
Nyasa kwa upande wa Tanzania,<br />
umebaini kwa shughuli nyingi<br />
zinazoathiri ziwa zinatekelezwa<br />
na wavuvi, wafugaji na wakulima<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 17<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
Maonesho ya NaneNane 201...<br />
Inatoka uk. wa 15<br />
Miongoni mwa faida anazozipata<br />
Bw. Haji ni pamoja na kujipatia kipato<br />
kwa ajili ya familia yake kwani kwa<br />
sasa anao wateja wengi wanaotumia<br />
asali ya nyuki hawa wasiouma na<br />
kwamba asali yake ina soko zuri. Kwa<br />
sasa ana jumla ya mizinga 20 ya nyuki<br />
ingawaje changamoto anayokutana<br />
nayo katika kupanua ufugaji huo ni<br />
ugumu kuwapata kutoka msituni<br />
kwani huwa wanajificha sana.<br />
“Ninawashauri watanzania<br />
kupenda kutumia zaidi asali kwani ni<br />
kinga ya maradhi mengi kwenye mwili<br />
wa binadamu. Hiki ni chakula kizuri<br />
mno hasa kwa watoto, nawaambia<br />
wazazi wasiwape watoto pia badala<br />
yake wawape asali,” anasisitiza.<br />
<strong>Uk</strong>aushaji matunda na<br />
mbogamboga<br />
Bw. Zuberi Sultani kutoka<br />
Korogwe Tanga kwenye maonesho<br />
haya yeye alionesha utaalamu<br />
wa kuhifadhi matunda na<br />
mboga mboga kwa njia<br />
ya ukaushaji. Miongoni mwa<br />
matunda yanayosindikwa ndizi,<br />
mananasi, maembe pamoja na<br />
zikiwemo mbogamboga kama vile<br />
mchunga na kisamvu.<br />
Anafafanua kuwa usindikaji wa<br />
matunda na mboga unafanyika ili<br />
kuyahifadhi na kutumika kwa msimu<br />
wote wa mwaka, wakulima wengi<br />
wa matunda hawanufaiki na kilimo<br />
hicho kwa sababu msimu wa mavuno<br />
matunda hushuka bei na mengine<br />
kuoza kwa kuwa wakulima hawana<br />
ujuzi wa kuyahifadhi.<br />
Anasema ukaushaji huu hutumia<br />
teknolojia rahisi, ambayo yeye<br />
amekuwa akiwafundisha wakulima<br />
wenzake bure ili nao wanufaike.<br />
“Tunakausha kwa kutumia chombo<br />
maalum ambacho hufunikwa na<br />
turubali jeusi juu kwa lengo la<br />
kupunguza ukali wa mionzi ya jua<br />
na kuhakikisha kwamba haileti<br />
madhara kwa watumiaji. Matunda<br />
haya yanapokaushwa huzidishiwa<br />
ubora kwani sukari yake huongezeka<br />
mara dufu ukilinganisha na tunda<br />
linavyokuwa katika hali ya kawaida.”<br />
“Mtanzania yeyote anaweza<br />
kusindika matunda na hata mboga<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />
kwani si kazi ngumu bali inahitaji<br />
usafi na uangalifu wa karibu ili<br />
kuhakikisha bidhaa inakuwa katika<br />
kiwango cha juu cha ubora ili isilete<br />
madhara kwa binadamu,” anaeleza.<br />
Bw. Sultani anasema kwamba<br />
utaratibu wa kusindika matunda<br />
huanzia katika utafutaji wa matunda<br />
mazuri yaliyoiva kiasi, unayaosha<br />
kuyakata vipande vidogo vinavyoweza<br />
kukauka upesi, kisha kuyaweka<br />
kwenye chombo kinachotumia<br />
mwanga wa jua kukaushia na<br />
baada ya hapo huhifadhiwa kwenye<br />
vifungashio maalum tayari kwa<br />
kuuzwa.<br />
Utaratibu huu unafanana vile vile<br />
katika mboga za majani ambapo<br />
huoshwa na kuchemshwa kidogo<br />
jikoni kisha huanikwa katika<br />
chombo kinachotumia mwanga wa<br />
jua kukaushia mazao na baada ya<br />
kukauka huwa tayari kufangashwa<br />
kwa ajili ya kuuzwa ama kuliwa.<br />
Usindikaji zao la Muhogo<br />
Bw. Juma Nyamgunda kutoka<br />
Mkuranga Pwani anasema katika<br />
kuhakikisha kwamba zao hili la<br />
muhogo linaongezewa thamani<br />
wakulima wa Mkuranga wameanza<br />
kusindika muhogo na kupata unga<br />
ambao huutumia katika kutengeneza<br />
Watazamaji wakitoka kwenye banda la <strong>MVIWATA</strong><br />
KUTOKA MITANDAONI<br />
vitu mbalimbali ikiwemo keki, biscuti,<br />
tambi, chinchin, chapati na maandazi<br />
kazi ambayo hufanywa kwa wingi na<br />
kina mama kwa lengo la kuongeza<br />
kipato cha familia.<br />
Bw. Nyamgunda anasema<br />
usindikaji unawapa faida kubwa<br />
wakulima ukilinganisha na<br />
walivyokuwa wakiuza muhogo ghafi<br />
kwa walanguzi na katika maonesho<br />
ya NaneNane amepata wateja wengi<br />
wanaohitaji kiwango kikubwa cha<br />
unga wa muhogo.<br />
Ludewa<br />
wahimizwa...<br />
Inatoka uk. wa 16<br />
wadogo ambao kipato chao ni<br />
kidogo ama cha wastani.<br />
Alisema katika hatua ya awali ya<br />
miaka mitatu ya majaribio, mradi<br />
unatekelezwa kwenye wilaya mbili<br />
ambazo ni Kyela mkoani Mbeya na<br />
Ludewa mkoani Njombe. Katika<br />
hatua ya pili ya mradi utajumuisha<br />
wilaya za Mbinga mkoani Ruvuma<br />
na Makete mkoani Njombe.<br />
Kwa ujumla mradi unalenga<br />
kuwafikia na kuwanufaisha<br />
wakulima,wafugaji na wavuvi<br />
wapatao 15,000 wa hapa nchini.<br />
17
MAKALA<br />
Mtweve: Ubunifu wangu wa redio<br />
umenufaisha wengi<br />
Anamiliki Mlangali Coconut FM<br />
Hatimaye ndoto ya siku<br />
nyingi ya Bw. Ditrick<br />
Mtweve (<strong>18</strong>) mkazi wa<br />
Kata ya Mlangali wilayani Ludewa<br />
mkoa mpya wa Njombe imeweza<br />
kutimia baada ya kutumia ubunifu<br />
wake kutengeneza mtambo wa<br />
redio unaowanufaisha wakazi<br />
wengi wa wilaya hiyo.<br />
Mtambo huo uliotokana na<br />
kuunganishwa kwa vifaa mbalimbali<br />
kutoka katika redio mbovu na vifaa<br />
vinginevyo kama miti ya mianzi,<br />
boksi na vyuma vya baiskeli, ulianza<br />
kurusha matangazo yake mwaka jana<br />
katika kijiji cha Lufumbu na kwa sasa<br />
matangazo hayo yanawafikia wakazi<br />
wa vijiji sita katika Kata ya Mlangali.<br />
Kwa sasa redio hii ambayo ameipa<br />
jina la ‘Mlangali Coconut FM’ imekuwa<br />
ikitumiwa na viongozi wa vijiji vya<br />
kata ya Mlangali kutangaza taarifa<br />
muhimu kama vile mikutano ya<br />
vijiji, kampeni ya chanjo pia shughuli<br />
muhimu za kijamii.<br />
Vile vile imekuwa kichocheo<br />
kikubwa cha biashara na burudani<br />
kwani watu binafsi hutumia redio<br />
hiyo kutangaza biashara na huduma<br />
wanazotoa bila kusahau wapenzi wa<br />
muziki wa kisasa na nyimbo za injili<br />
ambao pia hupata fursa ya kupiga simu<br />
Mwanachama na mhamasishaji wa <strong>MVIWATA</strong> Mlangali akizungumza kwenye kipindi cha<br />
karibu mgeni<br />
<strong>18</strong><br />
na kuchagua wimbo waupendao.<br />
Bw. Mtweve ambaye ni mtoto<br />
pekee kwenye familia na yatima<br />
(aliyefiwa na baba) alisema kuwa<br />
alitamani siku moja katika maisha<br />
yake awe mtangazaji maarufu<br />
wa redio kubwa hapa nchini na<br />
ikiwezekana aweze kumiliki redio<br />
yake mwenyewe na mapema mwaka<br />
2009 akiwa kidato cha tatu katika<br />
Shule ya Sekondari ya Lufumbu<br />
ndoto yake ilianza kutimia ambapo<br />
kwa kutumia maarifa madogo<br />
aliyoyapata shuleni alianza kubuni na<br />
kutengeneza mtambo huo wa redio.<br />
“Wakati naanza ilikuwa kama<br />
mchezo, kwanza nilichukua muda<br />
nikitafakari kwanini ‘Microphone’<br />
zisizo na waya zinasafirisha sauti<br />
na kuupeleka katika mitambo.<br />
Baadaye nilichukua kifaa ‘transistor’<br />
kilichotumika katika ‘Microphone’<br />
hizo na vifaa vingine nilivichukua<br />
katika redio mbovu na kuviunganisha,”<br />
alisema Bw. Mtweve.<br />
Baada ya kukusanya vifaa<br />
mbalimbali kutoka kwenye redio<br />
mbovu na maeneo mengine pia<br />
alitumia betri za kawaida hatimaye<br />
kufanikiwa kuwasha mtambo wake<br />
na redio yake kuanza kusikilizwa na<br />
wananchi waishio jirani.<br />
Uwezo huu wa redio kusikilizwa<br />
na watu wa jirani ulianza baada ya<br />
kuboresha baadhi ya vifaa vyenye<br />
uwezo mkubwa zaidi ili kuwezesha<br />
mawimbi ya sauti kufika mbali zaidi na<br />
hatimaye alifanikiwa kufunga mnara<br />
wa mlingoti wa miti iliyounganishwa<br />
wenye antena ya waya wa kawaida<br />
juu yake na kuutundika juu ya<br />
kilele cha mlima uliokuwa jirani na<br />
nyumbani kwao.<br />
“Haikuwa kazi ndogo kwani<br />
mwanzoni niliweka mtambo huu<br />
nyumbani kwetu ambako ni bondeni<br />
ikawa inasikika nyumba kadhaa za<br />
jirani tu. Ilibidi kutumia muda mwingi<br />
na kuumiza akili ili kuweza kufikia<br />
mafanikio, baadaye nikapata wazo<br />
la kuhamia hapa mlimani kwenye<br />
nyumba ya rafiki yangu ambaye<br />
amenipangishia chumba kimoja,”<br />
alisema Bw. Mtweve alipozungumza<br />
na Pambazuko ndani ya studio yake<br />
kijijini Lufumbu.<br />
Bw. Mtweve alisema anafurahia<br />
ubunifu wake lakini bado anakabiliwa<br />
na changamoto nyingi sana ikiwemo<br />
kutokujua sheria “mpaka sasa redio<br />
hii naimiliki kienyeji kwa lengo la<br />
kukuza kipaji changu na kuiwezesha<br />
jamii inayonizunguka kunufaika na<br />
kipaji hicho, sijui taratibu za kuisajili<br />
zikoje,” alisema Bw. Mtweve.<br />
Tatizo jingine ni kukosa mtaji wa<br />
kuweza kununua vifaa vya kisasa na<br />
kuwa na jengo maalumu la studio ya<br />
utangazaji.<br />
Kwa hivi sasa Bw. Mtweve anaishi<br />
na mama yake baada ya baba yake<br />
kufariki wakati yeyé akiwa na umri<br />
wa miaka 10 na alikuwa akisoma<br />
darasa la tatu wakati huo.<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 19<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
Inatoka uk. wa <strong>18</strong><br />
Alisema hali hiyo ya kubakia na<br />
mzazi mmoja imechangia kwa kiasi<br />
kikubwa umasikini katika familia<br />
yao baada ya mama yake kutokuwa<br />
na uwezo wa kifedha na hata afya<br />
yake kutokuwa thabiti kutokana<br />
na maradhi yanayomsumbua na<br />
hivyo wakati mwingine hulazimika<br />
kusimamisha kazi za redio ili<br />
kumsaidia mama yake shughuli za<br />
shamba.<br />
“Redio hii huwa hewani kwa<br />
masaa 24 kila siku kwa kurusha<br />
muziki hewani na salamu, short<br />
time za muziki wa bongo flava na<br />
chaguo la msikilizaji, na inapofika<br />
4.00 usiku hurudi nyumbani na<br />
kuuacha mtambo ukipiga muziki<br />
mpaka alfajiri ninapoingia kuendelea<br />
na vipindi,” alisema Bw. Mtweve.<br />
Awali kabla ya kufikia kiwango<br />
cha kurusha matangazo saa 24,<br />
alikuwa akitumia redio inayotumia<br />
kanda za kawaida na baadaye alipata<br />
redio yenye kutumia ‘memory card’<br />
ambayo imekuwa ikimwezesha<br />
kupiga muziki muda wote.<br />
Hata hivyo eneo hili la Mlangali<br />
bado halijafikwia na huduma ya<br />
umeme wa Tanesco hali inayomlazimu<br />
kutumia betri za kawaida za<br />
redio kuendeshea mtambo wake.<br />
“Nimekuwa nikiwategemea watu<br />
mmoja mmoja ambao wanavutiwa<br />
na huduma hii, kuninunulia betri,<br />
kuna wakati zinapoisha na hakuna<br />
mtu wa kununua ninalazimika kuzima<br />
matangazo kwa siku kadhaa, hadi<br />
ninapoenda kufanya kibarua mahali<br />
Afisa programu wa <strong>MVIWATA</strong> Bw. Laurent Kaburire akimtambulisha Bw.Ditrick Mtweve kwa<br />
wajumbe wa Mkutano Mkuu wa 16 wa <strong>MVIWATA</strong> Oktoba 24, 2011 mjini Morogoro<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />
Hii ndiyo mitambo ya kurusha matangazo<br />
ya COCONUT FM<br />
na kupata fedha, nitafurahi kama<br />
kijijini kwetu tutapata umeme.”<br />
Wakazi wa vijiji vya kata hiyo<br />
ambao hawakuwa wakimiliki<br />
redio majumbani mwao kwa sasa<br />
wameanza kumiliki redio na kusikia<br />
matangazo na burudani kutoka<br />
katika mtambo wa redio ya kijana<br />
huyo.<br />
Wafanyabiashara wa Mlangali nao<br />
kwa uchache wameanza kuitumia<br />
fursa ya redio hii kujitangaza na<br />
humlipa kati ya Sh 500 na 1,000 ili<br />
kuweza kurushiwa matangazo yao<br />
redioni kwa siku kiwango ambacho<br />
kijana huyo anasema kuwa kimekuwa<br />
kikimsaidia kwa mahitaji binafsi yeye<br />
na mama yake.<br />
Anasema hata hivyo kuwa kwa<br />
sasa yeye ndiye mtangazaji na fundi<br />
mitambo wa redio hiyo. Anawaomba<br />
wananchi wenye uwezo na ambao<br />
wanaguswa na kipaji chake kumsaidia<br />
kuweza kwenda kusoma katika chuo<br />
cha ufundi stadi (Veta) ili kuongeza<br />
maarifa.<br />
Sambamba na hilo, kijana huyu<br />
anaeleza kuwa kamwe ndoto zake<br />
MAKALA<br />
hazitaishia hapo, bali ataendelea<br />
kubuni mbinu mbalimbali na<br />
kuboresha kazi yake hiyo na kiu<br />
yake ni kuona siku moja redio hiyo<br />
inasikika katika wilaya nzima ya<br />
Ludewa.<br />
Bw. Mtweve anaishukuru jamii<br />
inayomzunguka kwani pamoja na<br />
kukosa fedha sambamba na ufinyu wa<br />
elimu ya ufundi alionayo, bado jamii<br />
hiyo imekuwa msaada mkubwa sana<br />
kwake kwani wameweza kutambua<br />
umuhimu wake katika jamii kwa<br />
kumpati redio mbovu ili aweze kutoa<br />
vifaa muhimu kwa kazi yake.<br />
Hii ndiyo studio ya COCONUT FM<br />
Kwa kutambua mchango mkubwa<br />
anaoutoa katika kuhakikisha jamii ya<br />
vijijini inafikiwa na habari, Mtandao<br />
wa Vikundi vya Wakulima Tanzania<br />
(<strong>MVIWATA</strong>), ulimwalika Bw. Mtweve<br />
na kuwezesha kushiriki kwenye<br />
Warsha ya Kitaifa na Mkutano Mkuu<br />
wa 16 wa <strong>MVIWATA</strong> uliofanyika<br />
Oktoba 24 na 25, 2011 mjini<br />
Morogoro.<br />
Mojawapo ya mada iliyojadiliwa<br />
kwenye warsha hiyo na kugusa hisia<br />
ni “haki ya upatikanaji wa<br />
habari vijijini” ambapo wakulima<br />
kutoka vijiji mbalimbali walieleza<br />
jinsi ambavyo wanakabiliwa na<br />
changamoto katika kupokea na<br />
kutoa habari katika kutokana na<br />
vyombo vingi vya habari kuegemea<br />
zaidi mijini.<br />
Hivyo washiriki hao walipongeza<br />
ubunifu wa kijana huyo na kuomba<br />
<strong>MVIWATA</strong> kama taasisi kuendelea<br />
kumuunga mkono na kumtumia<br />
kutangaza zaidi habari za wakulima.<br />
Jambo hilo limetekeleza na hivi sasa<br />
baadhi ya vipindi vya SAUTI YA<br />
<strong>MVIWATA</strong> vinarushwa kupitia redio<br />
hiyo Mlangali Coconut FM.<br />
19
KUTOKA MITANDAONI<br />
Viongozi wa masoko ya wakulima<br />
wapewa ushauri<br />
Na Susuma Susuma, Morogoro<br />
Viongozi wa masoko ya<br />
wakulima wametakiwa<br />
kutojenga uhasama na<br />
viongozi wa awamu zilizopita bali<br />
wawatumie kujifunza na kupata<br />
mbinu za kuyafanya masoko hayo<br />
kuwa endelevu.<br />
Wito huo umetolewa Julai<br />
30,2011 mjini Morogoro na<br />
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi<br />
wa Soko la Wakulima la Kibaigwa<br />
Kongwa mkoani Dodoma Bw.<br />
Richard Kapinye kwenye kikao cha<br />
pamoja cha wakurugenzi wa bodi<br />
za masoko sita yaliyojengwa na<br />
<strong>MVIWATA</strong> kwenye vijiji mbalimbali<br />
hapa nchini.<br />
Bw. Kapinye alisema “tuepuke<br />
uhasama unaofanywa na wanasiasa<br />
kwamba akishamuondoa mwenzake<br />
madarakani wanakuwa maadui<br />
wanaotafuta kuharibiana kila wakati,<br />
sisi tuwe tofauti tuwatumieni<br />
wenzetu waliotutangulia ili tuweze<br />
kufanikiwa.”<br />
Kadhalika Bw. Kapinye ambaye<br />
pia ni mkulima mdogo na Diwani<br />
wa Kata ya Kibaigwa, aliwataka<br />
wajumbe wenzake kutumie<br />
vyema dhamana waliyopewa kwa<br />
20<br />
kusimamia haki na maslahi ya<br />
wakulima huku akitahadharisha<br />
tabia inayojitokeza ya baadhi ya<br />
wakulima wanaopata nyadhifa za<br />
kisiasa, kusahau walikotoka na<br />
kuanza kuwakandamiza wenzao.<br />
Akawahimiza pia wakulima ili<br />
kupanua uelewa wawe na hamasa<br />
ya kujifunza mambo mapya kwa<br />
kusoma magazeti na machapisho<br />
mengine likiwemo jarida la wakulima<br />
la Pambazuko (Sauti ya Wakulima)<br />
linalochapishwa na <strong>MVIWATA</strong>.<br />
Kwa upande wake mratibu wa<br />
kikao hicho ambaye pia ni Afisa<br />
Masoko wa <strong>MVIWATA</strong> Bw. Jimmy<br />
Mongi aliwahimiza wakurugenzi hao<br />
wa bodi, wawatumie wajumbe wenye<br />
uzoefu walioko masoko ya jirani ili<br />
kuwafundisha na kuwajengea uwezo<br />
wajumbe wapya wanaochaguliwa.<br />
“Tunaamini kuwa wajumbe<br />
wa mwanzo kwenye bodi hizi,<br />
walijengewa uwezo mkubwa kielimu<br />
kwa kupelekwa ziara mbalimbali<br />
za mafunzo, hivyo tunapofikiria<br />
kupata mafunzo kwa wajumbe<br />
wapya tuwafikirie kwanza hawa,<br />
ni wenzetu watatupatia elimu<br />
hiyo kwa gharama ndogo na pale<br />
panapohitajika utaalamu zaidi ndipo<br />
tuombe msaada wa <strong>MVIWATA</strong> ofisi<br />
Kufunga mipaka ya kuuza mazao nje ya nchi<br />
kunamsababishia hasara mkulima<br />
Na Martin Pius, Babati<br />
Serikali imetakiwa kutotoa<br />
amri za kuzuia mazao ya<br />
chakula yakiwamo mahindi<br />
kuuzwa nje ya nchi kwani kufanya<br />
hivyo inawasababishia hasara<br />
wakulima na kuwakatisha tamaa<br />
ya kuongeza uzalishaji.<br />
Rai hiyo imetolewa Julai<br />
13, 2011 na Mjumbe wa Bodi<br />
ya Mtandao wa Jinsia Tanzania<br />
(TGNP), Bibi Rehema Mwateba<br />
wakati akifungua Mkutano Mkuu<br />
wa nne wa <strong>MVIWATA</strong> Manyara<br />
uliowashirikisha wanachama wa<br />
wilaya tano za mkoani Manyara.<br />
Bibi Mwateba alisema Serikali<br />
itambue kwamba inatumia mfumo<br />
kandamizi kwa mkulima kwa kufunga<br />
mipaka ya kuuza mazao ndani na nje<br />
ya nchi bila ya kujali kuwa hilo ni<br />
hitaji la mkulima la kuendesha maisha<br />
yake yanayotegemea hasa bei nzuri<br />
ya mazao. Alisema kuzuia biashara<br />
ya mazao kwa kutumia kisingizio cha<br />
kinga ya njaa hakitavumilika kwani<br />
wakati utafika wakulima watachukua<br />
kuu,” alisema Bw. Mongi<br />
Kwa upande wake Bibi.<br />
Honolata Blass, mjumbe wa bodi<br />
ya Soko la Nyandira alisema bodi<br />
za wakurugenzi zinapaswa kuwa<br />
na ubunifu ili kuongeza ufanisi wa<br />
masoko. “Kwa upande wetu ubunifu<br />
wa bodi umesaidia kuongeza mapato<br />
ya soko kila mwaka na kulifanya soko<br />
kuwanufaisha wakulima wengi,”<br />
alisema Bibi Blass.<br />
Bodi hizo za wakurugenzi wa<br />
masoko hukutana mara kwa mara<br />
kwa lengo la kuwapa wadau hao<br />
fursa ya kushirikishana uzoefu wa<br />
mafanikio, changamoto na kuweka<br />
mikakati ya uendelevu wa masoko<br />
hayo ya wakulima.<br />
Kikao hiki kilikutanisha<br />
wakurugenzi 25 wa bodi za masoko<br />
ya Kibaigwa wilaya ya Kongwa,<br />
Nyandira wilayani Mvomero, Tandai<br />
na Tawa Morogoro Vijijini, Mkata<br />
wilaya ya Handeni na Igagala wilayani<br />
Njombe.<br />
Masoko hayo yalijengwa na<br />
<strong>MVIWATA</strong> tangu mwaka 2004 na<br />
kukabidhiwa kwa halmashauri za<br />
wilaya na uendeshaji wake kubakia<br />
mikononi mwa bodi za wakurugenzi<br />
ambazo zinaundwa na wakulima na<br />
wawakilishi wa halmashauri.<br />
hatua ambazo huenda zikawa na<br />
madhara makubwa kwa taifa.<br />
“Serikali inatakiwa kufanya<br />
utafiti wa haraka kubaini maeneo<br />
yaliyoathirika na njaa na kupeleka<br />
chakula cha msaada na kwa maeneo<br />
mengine yasiyokuwa na uhaba wa<br />
chakula wakulima waruhusiwe<br />
kuuza mazao yao nje ya nchi ili<br />
kuweza kupata faida,” alisema.<br />
Makamu Mwenyekiti wa<br />
<strong>MVIWATA</strong> Manyara, Bibi Fatuma<br />
Kimolo, akizungumza kwenye<br />
mkutano huo alisema kama serikali<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 21<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
Wakulima washauriwa wasidai<br />
posho za mafunzo<br />
Na Ledis Kigala, Kyela<br />
Baadhi ya wakulima wilayani<br />
Kyela mkoani Mbeya<br />
wamewaasa wenzao<br />
kutanguliza mbele manufaa ya<br />
elimu wanayopata katika kshiriki<br />
kwao kwenye mafunzo badala ya<br />
kudai posho.<br />
Wamesema mtindo wa kudai<br />
posho kwanza, unawafanya wakulima<br />
kushindwa kupata elimu muhimu<br />
kwa ustawi wa maisha yao.<br />
Walitoa wito huo wakati wa<br />
kufunga mafunzo ya kuwajengea<br />
uwezo katika uzalishaji bora wa<br />
mazao ya mpunga, mahindi, kokoa<br />
na ufugaji wa wanyama.<br />
Mmoja wa wakulima hao Bw.<br />
Goden Mwantimwa wa kijiji cha<br />
Lutusyo kata ya Muungano wilayani<br />
Kyela alieleza kufurahishwa na<br />
elimu na mafunzo yanayoendelea<br />
kutolewa na Mtandao wa Vikundi<br />
vya Wakulima Tanzania (<strong>MVIWATA</strong>)<br />
na kuahidi kuwa ataendelea kushiriki<br />
kwa sababu kwake elimu ni muhimu<br />
kuliko posho.<br />
“Mimi niko tayari kujitolea<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />
kushiriki mafunzo mengine hata kama<br />
itakuwa nje ya hapa, nawaombeni<br />
wenzangu tuithamini sana elimu hii<br />
ili itusaidie katika kuboresha kilimo<br />
chetu,” alisema Bw. Mwantimwa.<br />
Kwa upande wake Bw. Musa<br />
Mwangongolo mkulima wa kijiji<br />
cha Makwale kata ya Makwale,<br />
alisema tabia ya kudai posho<br />
kutoka kwa waandaaji wa mafunzo<br />
imesababbisha wadau mbalimbali wa<br />
maendeleo kuwakimbia wakulima<br />
wa eneo hilo.<br />
Alisema matokeo yake ni<br />
waandaaji kuhamishia mafunzo hayo<br />
katika maeneo mengine na kuwaacha<br />
wakulima wa Kyela wakiwa hawana<br />
la kufanya.<br />
Alisema kimsingi wakulima siyo<br />
masikini wa kipato, na kwamba<br />
umasikini wao ni maarifa ambayo<br />
<strong>MVIWATA</strong> imeonyesha njia ili<br />
kufikia azma ya kuboresha kilimo ili<br />
kiwe chenye tija zaidi.<br />
Mafunzo hayo yaliyofanyika kuanzia<br />
tarehe Septemba 21 hadi Oktoba 11,<br />
2011 kwenye vijiji <strong>18</strong> vilivyoko kwenye<br />
kata 10 za wilaya ya Kyela yalilenga<br />
kuwapa elimu wakulima ya kuongeza<br />
Bibi Edina Mwakipesile mkulima wa kijiji cha Mwiyonde wilayani Kyela akielezea dhana<br />
ya <strong>MVIWATA</strong> kwa wakulima wenzake walioshiriki mafunzo ya kujengea uwezo vikundi,<br />
yaliyoandaliwa na <strong>MVIWATA</strong> mjini Kyela.<br />
KUTOKA MITANDAONI<br />
uzalishaji pamoja na ubora wa mazao<br />
na mifugo.<br />
Mafunzo hayo ni sehemu ya<br />
utekelezaji wa mradi wa Uhifadhi<br />
Mazingira na Kukuza kipato<br />
kwa wakulima wadogo waishio<br />
kandokando ya ziwa Nyasa,<br />
unaotekelezwa na <strong>MVIWATA</strong><br />
kwa ufadhili wa Shirika la Swedish<br />
Cooperative Center (SCC).<br />
Afisa Mradi huo Bw. Ledis Kigala,<br />
alisema, mradi huo unatekelezwa<br />
kwenye kata 10 kati ya kata 20<br />
za wilaya ya Kyela ambazo ni<br />
Bujonde, Ikolo, Ngonga, Ikimba,<br />
Katumbasongwe, Ipande, Mwaya,<br />
Ipinda, Muungano na Makwale.<br />
Kufunga mipaka ya kuuza<br />
mazao nje ya nchi...<br />
Inatoka uk. wa 20<br />
imeamua kufunga mipaka ya kuuza<br />
chakula inatakiwa sasa ijipange<br />
kununua mazao hayo ya wakulima<br />
kwa bei yenye tija badala ya<br />
kupanga bei yake isiyokuwa na<br />
maslahi kwa mkulima.<br />
Bibi Kimolo alisema kufungwa<br />
mipaka kipindi hiki kumesababisha<br />
bei ya mahindi kushuka kutoka<br />
Sh. 45,000 na kufikia Sh 30,000<br />
kwa gunia, hali ambayo inarudisha<br />
nyuma maendeleo ya mkulima.<br />
Alihoji kuwa iweje watumishi<br />
wa Serikali wapandishiwe<br />
mishahara kila mwaka kutokana<br />
na kupanda kwa gharama ya<br />
maisha, huku mkulima akiwekewa<br />
masharti ya kupata ujira stahiki ili<br />
aweze kukabiliana na hali ngumu ya<br />
maisha magumu kwa kuuza mazao<br />
kwenye soko lenye bei nzuri?<br />
Alisema umefika wakati sasa,<br />
serikali iache kutumia raslimali<br />
nyingi kwenye kutoa na kusimamia<br />
matamko ambayo hayana tija kwa<br />
ustawi wa wakulima badala yake<br />
nguvu na raslimali hizo zitumike<br />
kuimarisha miundombinu ya<br />
kilimo ili kiweze kuwa na uzalishaji<br />
wa kutosheleza mahitaji ya chakula<br />
na ziada ya biashara.<br />
21
KATUNI<br />
MUDA<br />
MREFU NAONA<br />
UNASOMA HILO<br />
GAZETI LINA<br />
HABARI GANI?<br />
WEWE UTAZI-<br />
PATA VIPI HABARI ZA<br />
MJINI WAKATI GAZETI<br />
LINACHUKUA SIKU 4<br />
KUFIKA HAPA<br />
22<br />
OH! KWELI NDIO<br />
SABABU<br />
AHA<br />
HAHA SIO HIVYO,<br />
NI MFUMO WA TAARIFA<br />
YA MASOKO <strong>MVIWATA</strong>.<br />
NAPATA TAARIFA KUPI-<br />
TIA SIMU YANGU YA<br />
MKONONI TU.<br />
AH! GAZETI<br />
LENYEWE LINA<br />
HABARI ZA MJINI TU,<br />
SIONI HATA HABARI<br />
INAYOGUSIA KERO<br />
ZETU.<br />
WAANDISHI<br />
WENGI WANAJI-<br />
SHUGHULISHA NA<br />
MAMBO YA MJINI<br />
TU.<br />
SI<br />
NINATUMIA<br />
SIMU YANGU YA<br />
MKONONI<br />
ONA<br />
SASA MIMI<br />
SIJUI HATA KUTUMIA<br />
HUO MTANDAO, HEBU<br />
FIKIRIA NI WATU WAN-<br />
GAPI HAWAPATI HIZO<br />
HABARI?<br />
HIVI KWANINI SISI<br />
WATU WA VIJIJNI<br />
HABARI ZETU<br />
HAZIANDIKWI?<br />
NDIO MAANA<br />
HAKUNA HABARI ZA<br />
KILIMO KWENYE<br />
MAGAZETI<br />
MENGI!<br />
YAANI<br />
UNAWAULIZA<br />
WATU WA MJINI KWA<br />
SIMU!?<br />
LAKINI MIMI NAONA BADO<br />
HIZO HABARI UNAZOPATA<br />
KWENYE SIMU HAZIZUN-<br />
GUMZII KILIMO<br />
NANI ATAKUJUA<br />
HUKU KIJIJINI<br />
HUKU<br />
HABARI ZI-<br />
TAFIKAJE<br />
HAPANA<br />
NATUMIA<br />
MTANDAO<br />
AH!<br />
MBONA<br />
MWAKA JANA<br />
WAANDISHI WALI-<br />
KUJA WENGI TU<br />
LAKINI<br />
MIMI NAPATA<br />
TAARIFA NYINGI ZA<br />
MASOKO YA MJINI<br />
KILA SIKU.<br />
HAWA<br />
WAANDISHI<br />
WANAUPENDELEO<br />
BWANA!<br />
WE UM-<br />
ESAHAU!? SI KWA<br />
SABABU WALILETWA<br />
NA WAHESHIMIWA<br />
KWENYE KAMPE-<br />
NI<br />
MTANDAO<br />
WA WAKULIMA<br />
<strong>MVIWATA</strong>?<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
HUKU<br />
HABARI ZA<br />
KILIMO HAZIANDIKWI<br />
NA WAKIANDIKA GAZETI<br />
LINACHELEWA KUFIKA<br />
AU LISIFIKE KABISA.<br />
SASA HUKU KWETU<br />
BARABARA NI TATIZO<br />
LABDA TUTAPATA HIZO<br />
HABARI KWENYE RA-<br />
DIO NA TV<br />
KWELI TUTAPATAJE<br />
MAENDELEO KAMA HATUJUI<br />
TAARIFA YA KILA SIKU YA<br />
MASOKO, UCHUMI NA<br />
SIASA?!<br />
WATU WENGI WANAKUFA KWA KUKOSA<br />
ELIMU YA AFYA NA KUAMINI IMANI PO-<br />
TOFU ZA KWENDA KWA WAGANGA.<br />
LAKINI TUSIWALAUMU SANA<br />
WAANDISHI, MIMI NAFIKIRI<br />
SERIKALI YETU IANGALIE NA<br />
MIUNDO MBINU YETU<br />
HATA KAMA ZIPO KU-<br />
TOKANA NA HALI YA UCHU-<br />
MI JE, TUTAWEZA KUNUNUA<br />
HIZI TV NA UMEME<br />
TUTAPATA WAPI?<br />
HAPO<br />
MAENDELEO<br />
YATACHELEWA<br />
SANA<br />
EH<br />
HAYO YOTE<br />
YANATOKEA SABABU<br />
HATUPATI HABARI<br />
SAHIHI!<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />
ACHA UCHUMI<br />
TU, IDADI KUBWA YA<br />
WATANZANIA WANAISHI<br />
VIJIJINI NA UMEME<br />
HAKUNA HAYO MATAN-<br />
GAZO WATAYAONA<br />
VIPI?<br />
WANAHABARI<br />
WANA NAFASI KUBWA<br />
SANA YA KUELIMISHA<br />
WATU KUHUSU MATUMIZI<br />
BORA YA ARDHI, UFU-<br />
GAJI BORA, BEI KATIKA<br />
MASOKO<br />
KWA-<br />
HERINI<br />
NDIO, BARABARA SIYO<br />
NZURI KUWEZA KUSA-<br />
FIRISHA MAGAZETI<br />
YAFIKE HARAKA<br />
SASA<br />
NAFIKIRI MUDA<br />
MUAFAKA KWA WAHUSIKA KU-<br />
LIANGALIA HILI, SABABU VYOMBO<br />
VYA HABARI NDIO VINAWEZA KU-<br />
WAELIMISHA WATU NA KULETA<br />
MAENDELEO HARAKA.<br />
ITA-<br />
TUSAIDIA KUPA-<br />
TA ELIMU SAHIHI YA<br />
AFYA, UKATILI DHIDI<br />
YA WANAWAKE<br />
HILI TATIZO LIFANYIWE KAZI, SABABU HATA RADIO ZENYEWE<br />
HAZIFIKI VIJIJINI NA ZINATANGAZA UDHAIFU TU WA WATU WA<br />
KIJIJINI INGAWA KUNA MAFANIKIO NA UBUNIFU WANAOUFANYA.<br />
KATUNI<br />
KWELI<br />
BARABARA NI<br />
TATIZO KWA SABABU<br />
HATA MTOTO WA MZEE<br />
KIPARA ALIFARIKI KWENYE<br />
GARI KWA UBOVU WA<br />
BARABARA.<br />
WASAL-<br />
IMIE RAFIKI<br />
ZANGU’<br />
JUZI NILIKUWA MJINI<br />
NIMEONA MATANGAZO MENGI<br />
YANAYOONESHA UDHAIFU<br />
WA WATU WA KIJIJINI TU<br />
INA MAANA HUKU HATUNA<br />
MAMBO MAZURI YA KU-<br />
TANGAZA NA TV?<br />
23
KUTOKA MITANDAONI<br />
Mfumo shirikishi unaharakisha<br />
maendeleo<br />
Na Gratian Cronery, MUCCoBS<br />
Shinyanga<br />
Maendeleo na ustawi<br />
wa miradi ya kijamii<br />
yanategemea zaidi<br />
ushirikishwaji wa jamii husika<br />
katika hatua zote.<br />
Katika nchi yetu hali ni<br />
tofauti ambapo miradi mingi<br />
wanayopelekewa wananchi<br />
hawakushirikishwa kikamilifu na<br />
kwamba kinachofanyika ni wao<br />
kupokea amri ya bwana mkubwa na<br />
kutekeleza wasichokijua.<br />
Hali hii ya kuwapelekea<br />
wananchi maamuzi badala ya wao<br />
kushiriki kuibua wazo na kuamua,<br />
imesababisha miradi mingi kutotoa<br />
matokeo chanya licha ya kugharimu<br />
fedha nyingi.<br />
Serikali katika kuwasaidia<br />
wananchi kutekeleza mipango ya<br />
maendeleo imekuwa ikianzisha<br />
miradi ikiwemo ya kujenga majengo<br />
kwa lengo la kuwasaidia wananchi, ila<br />
ukweli ni kwamba fedha na raslimali<br />
nyingi zimekuwa zikipotea bure.<br />
Iko mifano mingi ya miradi ya<br />
aina hii ambayo wananchi wanaipa<br />
jina la ‘miradi ya serikali’ kwa kuwa<br />
hawakushirikishwa na haikuwa<br />
kipaumbele chao. Miradi hii ni kama<br />
vile ya majengo ya masoko kwenye<br />
vijiji vya Ruvu Darajani mkoani<br />
Pwani, Buigiri wilaya ya Chamwino,<br />
Ruaha mkoa wa Iringa na kwingineko<br />
ambayo yametelekezwa na kuwa<br />
vichaka vya wezi ama nyumba ya<br />
wanyama na wadudu, baada ya<br />
wananchi kususa kuyatumia kwa<br />
kuwa haikuwa kipaumbele chao<br />
na kwingineko uchaguzi wa eneo<br />
haukuwa sahihi.<br />
Huu ni mmoja wa mifano ya<br />
24<br />
miradi mingi ambayo imeanzishwa<br />
na serikali pasipo kuwashirikisha<br />
wananchi katika kutoa mawazo yao<br />
na kupendekeza nini wanahitaji na ni<br />
kwa matumizi gani, na kama ni jengo<br />
likae sehemu gani.<br />
Mfumo uliotumika kuanzisha<br />
na kutekeleza kauli mbiu ya “kilimo<br />
kwanza” ni ule ule wa amri kutoka<br />
kwa bwana mkubwa, mkulima hana<br />
hiari cha kuchagua kukataa hata<br />
kama kilicholetwa ni mwiba kwake.<br />
Vile vile serikali imekuja na<br />
mpango wa zana bora za kilimo<br />
ikiwemo matrekta madogo (power<br />
tiller) na ambapo kwenye maeneo<br />
mengi hazihitajiki kutokana na<br />
aina ya udongo na mazingira.<br />
Baada ya wakulima kulazimishwa<br />
kuzinunua wamezigeuza matumizi<br />
na kuwa mashine za kufua umeme,<br />
kusukuma maji, kulanda mbao na<br />
kusaga unga.<br />
Hii ni changamoto kwa serikali na<br />
wadau wengine ambao wanatazamia<br />
kupeleka miradi kwa wananchi,<br />
kwamba ni vyema kuzingatia<br />
ushirikishwaji wa wananchi na<br />
mawazo yao yakaheshimiwa<br />
ili baadaye wakithamini<br />
wanachopelekewa.<br />
Watanzania wanakabiliwa na kero<br />
nyingi ambazo wangetarajia serikali<br />
kuwekeza nguvu zake zaidi kwa<br />
kutumia mfumo wa ushirikishwaji<br />
katika kuzitatua. Kwa mfano<br />
kuondoa kero ya ushuru mkubwa<br />
wa mazao unaotozwa kwenye<br />
vizuizi vya kila barabara ya nchi hii<br />
inayoelekea mjini. Kuna maana gani<br />
kumpa ruzuku ya pembejeo mkulima<br />
na baadaye kumkamua faida yote<br />
inayotokana na mavuno hayo?<br />
Kama ushuru unatozwa ili kufidia<br />
fedha za ruzuku, ni bora ruzuku<br />
hiyo ifutwe wakulima wajitafutie<br />
pembejeo na wawe huru kusafirisha<br />
mazao yao. Hili linaweza kutatuliwa<br />
kwa njia shirikishi ya majadiliano.<br />
Kwa kufanya hivyo tunaweza<br />
kutengeneza mipango na miradi<br />
endelevu kwa vizazi na vizazi ambayo<br />
italeta tija katika nyanja zote za<br />
maisha kisiasa, kiuchumi na kijamii.<br />
Kwa upande mwingine tumeona<br />
mfano wa miradi ya ujenzi wa masoko<br />
inayotekelezwa na <strong>MVIWATA</strong><br />
kwa mfumo shirikishi imefanya<br />
vyema na wakulima wanathibitisha<br />
matokeo yake. Mwenyekiti wa<br />
<strong>MVIWATA</strong> Shinyanga Bw. Charles<br />
Ndugulile anasema siri kubwa ya<br />
mafanikio ya masoko ya <strong>MVIWATA</strong><br />
ni kuzingatiwa kwa dhana ya<br />
ushirikishwaji.<br />
“<strong>MVIWATA</strong> imefanikiwa kufanya<br />
hivyo kwa hutoa mafunzo mazuri<br />
ya jinsi ya kushirikisha jamii kuanzia<br />
ngazi ya kaya hadi taifa ambayo<br />
huambatana na mafunzo ya andiko<br />
la mradi, uendeshaji na usimamizi<br />
wa miradi, uhasibu wa vikundi na<br />
mashirika pamoja na taasisi pamoja<br />
na mifumo ya masoko na biashara,”<br />
anasema Bw. Ndugulile.<br />
Endapo serikali na wadau<br />
wengine wa maendeleo watatumia<br />
dhana hii ya ushirikishwaji wa jamii<br />
kwa mapana na kuiona kama fursa<br />
ya kuleta mabadiliko chanya kwa<br />
jamii ya Watanzania, hakika taifa<br />
litapiga hatua ya ukuaji wa kasi wa<br />
maendeleo.<br />
Jamii kwa upande wao pia<br />
wanapaswa kujipanga vyema<br />
kushiriki katika mradi kwa kuibua<br />
wazo, kupanga, kutekeleza na<br />
kusimamia na baadaye kujipima<br />
kiwango cha uwajibikaji wao kwenye<br />
miradi husika.<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011
Jipatie nakala ya Jarida la Pambazuko katika ofisi<br />
za <strong>MVIWATA</strong> ngazi za kati zifuatazo<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Morogoro<br />
S.L.P 3220 Morogoro<br />
Mahali: Uwanja wa Maonyesho NaneNane mkabala na<br />
ofisi za TASO<br />
Simu/Faksi: 023 261 41 84<br />
Barua Pepe: morogoro@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Rukwa<br />
S.L.P 468 Sumbawanga<br />
Mahali: Jengo la Bethlehem Center – Barabara ya Msakila<br />
Faksi: +255 25 280 25 58<br />
Simu: +255 764 232 747, +255 784 940 606<br />
Barua pepe: rukwa@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Mbeya<br />
S.L.P 3015 Mbeya<br />
Mahali: Jengo la Bima na CRDB Bank (Ghorofa ya<br />
mwisho<br />
Simu: +255 784 979 397, +255 652 835 568<br />
Barua pepe: mbeya@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Chunya<br />
Mahali: Jengo la Halmashauri, chumba Na.3<br />
Barua pepe: chunya@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Iringa<br />
S.L.P 9<strong>18</strong> Njombe<br />
Mahali: Jengo la Njoluma, Njombe mjini<br />
Simu: 0782 241 224, +255 767 241 224<br />
Barua pepe: iringa@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Kilimanjaro<br />
S.L.P 7389 Moshi<br />
Mahali: Mbuyuni sokoni- ghorofa ya GOLDEN GROWN<br />
LODGE<br />
Simu: +255 27 275 16 39, +255 784 720 320<br />
Barua pepe: kilimanjaro@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Kagera<br />
S.L.P 1753 Bukoba Mjini<br />
Mahali: Ofisi za Mayawa-Mtaa wa Rwamishenyi, Barabara<br />
ya Uganda<br />
Simu: +255 788 6858<strong>18</strong>, +255 782 154961, +255 755 522 447<br />
Barua pepe: kagera@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Dodoma<br />
S.L.P 3293 Dodoma<br />
Mahali:Area C Dodoma eneo la INADES Formation<br />
Tz,mkabala na msikiti wa Area C<br />
Simu:255-26-2350013, +255 782 257 783,<br />
+255 767 881 352<br />
Faksi: +255 26 2350744<br />
Barua pepe: dodoma@mviwata.org<br />
Pambazuko Na. 39 Toleo la Julai – Septemba 2011<br />
Mwenyekiti<br />
<strong>MVIWATA</strong> Monduli (MVIWAMO)<br />
S.L.P 47 Monduli<br />
Mahali: Barabara ya Boma-Moringe Sekondari, Monduli<br />
Mjini<br />
Simu: 255-27-253 8029, +255 27 253 8337<br />
Faksi: +255 27 253 8338<br />
Barua pepe: monduli@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Manyara<br />
S. L. P. 446,<br />
Babati Manyara<br />
Mahali: Barabara ya Nyerere<br />
SIMU: +255 27 253 0385 Faksi: +255 27 253 0707<br />
Baruapepe: manyara@mviwata.org<br />
Mwenyekiti<br />
<strong>MVIWATA</strong> Tabora<br />
S.L.P 175 Igunga<br />
Mahali: Mtaa wa Uarabuni<br />
Simu: +255 784 398 4<strong>14</strong>, +255 782 219 551<br />
Barua pepe: tabora@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Zanzibar<br />
S.L.P <strong>14</strong>9 Zanzibar<br />
Mahali: Mwana kwerekwe- mkabala na shule ya sekondari<br />
M’kwerekwe A<br />
Simu: +255 773 926 955, +255 777 470 5<strong>18</strong><br />
+255 783 651 135<br />
Barua pepe: zanzibar@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Ruvuma<br />
S.L.P 696 Songea Manispaa<br />
Mahali: Jengo la TTCL ghorofa ya 2<br />
Simu: +255-25-2600626, +255 756 096 291<br />
Barua pepe: ruvuma@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Mkuranga<br />
S.L.P 56 Mkuranga<br />
Mahali: Karibu na Stendi ya Kimanzichana<br />
Simu: 0786 158 646<br />
Barua pepe: mkuranga@mviwata.org<br />
MAWAKALA<br />
Mwenyekiti:<br />
<strong>MVIWATA</strong> Shinyanga<br />
S.L.P 1024 Shinyanga<br />
Mahali: Chuo cha Ushirika Moshi tawi la Shinyanga<br />
(Kizumbi)<br />
Simu: +255 763 740 675, +255 755 546 311<br />
Barua Pepe: shinyanga@mviwata.org<br />
Mwenyekiti<br />
<strong>MVIWATA</strong> Kigoma<br />
S.L.P 1<strong>14</strong>4 Kigoma<br />
Mahali: Ndani ya ofisi ya KIKANGONET, Lumumba road<br />
jengo la NHC chumba 205<br />
Simu: 0713 565 252, 0762 565 252<br />
Barua pepe: aisimba@yahoo.co.uk<br />
25
IJUE <strong>MVIWATA</strong><br />
Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania- <strong>MVIWATA</strong><br />
Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (<strong>MVIWATA</strong>) ni chombo cha kuunganisha wakulima wadogo ili kuwa na sauti moja katika utetezi wa<br />
maslahi yao ya kiuchumi, kijamii, kiutamaduni na kisiasa.<br />
Mtandao huu ulianzishwa mwaka 1993 na wakulima wadogo. Kauli mbiu ya <strong>MVIWATA</strong> ni ‘Mtetezi wa Mkulima ni Mkulima<br />
Mwenyewe’.<br />
Falsafa, utume na dira ya <strong>MVIWATA</strong><br />
Falsafa ya <strong>MVIWATA</strong> inajengwa katika ya misingi ya ushawishi na utetezi wa maendeleo ya wakulima wadogo katika nyanja za kiuchumi na<br />
kijamii; kuwezesha mawasiliano na kujifunza kwa kubadilishana uzoefu miongoni mwa wakulima.<br />
Utume wetu:<br />
Kuimarisha mawasiliano na kuwaunganisha wakulima wadogo kupitia vikundi na mitandao yao katika ngazi mbali mbali ili kujenga mtandao wa<br />
kitaifa wenye nguvu ya kuwezesha ushiriki na uwakilishi wa kweli wa maslahi ya wakulima wadogo katika ngazi zote za maamuzi.<br />
Dira yetu:<br />
<strong>MVIWATA</strong> ni kuwa chombo imara chenye nguvu za ushiriki na uwakilishi wa mawazo ya mkulima katika mchakato wa maamuzi ya kiuchumi,<br />
kijamii na kisiasa. Kuwa na uwezo wa kutekeleza na kufuatilia michakato na shughuli za maendeleo ya kiuchumi na kijamii yanayogusa maslahi ya<br />
wakulima wadogo.<br />
Malengo ya <strong>MVIWATA</strong><br />
1. Kuwezesha mawasiliano miongoni mwa wakulima wadogo ili kujenga kwa pamoja mbinu na mikakati ya ushawishi na utetezi kwa maslahi ya<br />
wakulima wadogo, kiuchumi na kijamii.<br />
2. Kubadilishana mawazo, ujuzi na uzoefu juu ya kilimo na shughuli mbalimbali za wakulima ili kuboresha maisha na kuinua hali yao kiuchumi na<br />
kijamii.<br />
3. Kuwakilisha wakulima wadogo katika mashauriano na serikali juu ya masuala mbalimbali yanayohusu au yanayoathiri ufanisi na maslahi ya<br />
wakulima wadogo wa Tanzania.<br />
Maeneo makuu ya mpango mkakati<br />
1. Ushawishi na Utetezi: Kuwezesha wakulima wadogo kuwa na uwezo wa kutetea maslahi yao.<br />
2. Uwezo wa kiuchumi: kuwezesha wakulima wadogo kuwa na uwezo wa kiuchumi kupitia njia za akiba na mikopo, kuunganisha wakulima na<br />
masoko na elimu ya ujasiliamali<br />
3. Kuimarisha vikundi na mitandao ya wakulima kwa lengo la kujipanga na kujitetea.<br />
4. Masuala mtambuka: Kujenga uelewa wa wakulima juu ya <strong>Uk</strong>imwi, Jinsia, Mabadiliko ya Tabia ya nchi.<br />
5. Ujenzi wa kitaaasisi kwa lengo la kuimarisha shirika<br />
Muundo<br />
Muundo wa <strong>MVIWATA</strong> una ngazi tatu ambazo ni Ngazi ya Taifa, Ngazi ya Kati na Ngazi ya Msingi. Ngazi ya Kati inaundwa na mitandao ya<br />
kimkoa na kiwilaya wakati Ngazi ya Msingi inaundwa na mitandao ya Kata na Vijiji.<br />
Shughuli kuu<br />
1. Kujenga uwezo wa wakulima wadogo kwa kupitia mafunzo shirikishi juu ya mbinu za ushawishi na utetezi, mbinu za kuimarisha uchumi wa<br />
wakulima wadogo na uendelevu wa rasilimali kwa njia za warsha, mafunzo, mikutano na ziara za mafunzo.<br />
2.<br />
3.<br />
4.<br />
Kuhamasisha wakulima wadogo kujiunga katika vikundi vya kijamii na kiuchumi, mitandao ya msingi (kata na vijiji) na mitandao ya kati (mikoa<br />
na wilaya). Mpaka sasa <strong>MVIWATA</strong> imeanzisha mitandao ya kimkoa katika Mikoa ya Dodoma, Iringa, Kagera, Kilimanjaro, Manyara, Mbeya,<br />
Morogoro, Rukwa, Ruvuma, Shinyanga, Tabora na Tanga kwa Tanzania Bara. <strong>MVIWATA</strong> pia imeanzisha mitandao ya kiwilaya katika Wilaya<br />
za Monduli (Arusha) na Chunya (Mbeya). Tanzania Visiwani, <strong>MVIWATA</strong> Zanzibar imeanzishwa na kusajiliwa (Usajili namba 401). Mkakati<br />
unaendelea wa kuimarisha mitandao iliyopo na kuanzisha mitandao mipya.<br />
Kukusanya, kuweka katika kumbukumbu na kusambaza habari zinazohusu ujuzi na uzoefu wa wakulima, sera za kitaifa na kimataifa kwa<br />
kupitia jarida la Pambazuko Sauti ya Wakulima, vipindi vya radio, vipeperushi, vijitabu na machapisho mengine.<br />
Kuhamasisha na kuwezesha wakulima kubuni na kuendesha miradi shirikishi ya kiuchumi na uzalishaji kwa lengo la kuboresha uchumi wa<br />
wakulima wadogo kama vile vyama vya mazao, vyama vya kuweka na kukopa na masoko ya mazao.<br />
5. Kuandaa mikutano na warsha kuhusiana na mada zinazowagusa au kuathiri maslahi ya wakulima wadogo.<br />
Uanachama na jinsi ya kujiunga na shirika<br />
<strong>MVIWATA</strong> ina wanachama wa aina tatu (3).<br />
Aina ya kwanza ni Wanachama wa Kawaida ambao wamegawanyika katika makundi mawili;<br />
a) Kikundi cha wakulima wadogo au<br />
b)<br />
Mkulima mdogo binafsi aliye mwanachama katika Kikundi au Mtandao. Mkulima atakuwa mwanachama wa kawaida wa <strong>MVIWATA</strong> mara<br />
tu Kikundi au Mtandao wake utakapokubaliwa kuwa mwanachama. Atapewa kadi ya uanachama na kikundi au mtandao utapewa cheti cha<br />
utambulisho.<br />
Aina ya pili ni Vyama, Mashirika na Mitandao ya Wakulima Wadogo.<br />
Vyama, Mashirika na Mitandao ya Wakulima Wadogo vinavyojishughulisha na utetezi na ushawishi wa maslahi ya wakulima wadogo vilivyosajiliwa<br />
chini ya sheria yoyote ya Tanzania katika Ngazi za Wilaya, Mkoa au Taifa vinaweza kuomba kuwa mwanachama wa <strong>MVIWATA</strong> iwapo vinakubaliana<br />
kwa dhati na malengo na madhumuni ya Shirika.<br />
Aina ya tatu ni Wanachama Washiriki<br />
Ni mtu yeyote, taasisi au kikundi cha watu ambacho kinaunga mkono malengo na madhumuni ya Shirika. Mwanachama mshiriki anatamkwa na<br />
Mkutano Mkuu wa <strong>MVIWATA</strong>.<br />
Kila mwanachama, isipokuwa mwanachama mshiriki atalipa kiingilio na ada ya kila mwaka. Maelezo zaidi juu ya utaratibu wa kujiunga na ada<br />
yanapatikana kutoka kwa kiongozi au ofisi ya <strong>MVIWATA</strong>.<br />
Kwa mawasiliano zaidi<br />
Ofisi Kuu ya <strong>MVIWATA</strong><br />
Mkurugenzi Mtendaji<br />
<strong>MVIWATA</strong><br />
S.L.P 3220 Morogoro<br />
Simu: 023 261 41 84<br />
Faksi: 023 261 41 84<br />
Barua pepe: info@mviwata.org, mviwata@morogoro.net