20.01.2013 Views

Uk. 1 Uk. 17 Uk. 20 - MVIWATA

Uk. 1 Uk. 17 Uk. 20 - MVIWATA

Uk. 1 Uk. 17 Uk. 20 - MVIWATA

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Toleo NO. 040 Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11 Bei Shs. 500/= ISSN 0856-5937<br />

<strong>Uk</strong>. 1<br />

Je wakulima wadogo wamefaidi<br />

matunda ya uhuru<br />

<strong>Uk</strong>. <strong>17</strong><br />

Bodi mpya ya <strong>MVIWATA</strong><br />

yachaguliwa<br />

<strong>Uk</strong>. <strong>20</strong><br />

Wakulima, matrekta waandamana<br />

kupinga uporwaji ardhi


Toleo NO. 040<br />

Oktoba Disemba <strong>20</strong>11<br />

Bei Shs. 500/=<br />

ISSN 0856-5937<br />

WAHARIRI<br />

Susuma Msikula Susuma<br />

Stephen Ruvuga<br />

MHARIRI MSAIDIZI<br />

TOLEO NO.040<br />

BODI YA <strong>MVIWATA</strong><br />

Mwenyekiti – Habibu Simbamkuti<br />

Makamu Mwenyekiti –<br />

Veronica Sophu<br />

Katibu - Stephen Ruvuga-<br />

(Mkurugenzi Mtendaji)<br />

Mweka Hazina – Esther Mallya<br />

WAJUMBE<br />

Joseph Kilowoko<br />

Prisca John<br />

Amina Kazibure<br />

Projestus Ishekanyoro<br />

Haji Ussi Haji<br />

Paul Joseph<br />

MSHAURI WA <strong>MVIWATA</strong><br />

Prof. Amon Mattee<br />

LINATOLEWA NA<br />

KUSAMBAZWA NA<br />

Mtandao wa Vikundi vya<br />

Wakulima Tanzania (<strong>MVIWATA</strong>)<br />

S.L.P 32<strong>20</strong> Morogoro, Tanzania<br />

Simu: 023 261 41 84<br />

Faksi: 023 261 41 84<br />

Barua pepe: info@mviwata.org,<br />

mviwata@morogoro.net<br />

Tovuti: www.mviwata.org<br />

MICHORO<br />

Godwin Chipenya<br />

USANIFU NA<br />

UCHAPISHAJI<br />

PENplus Ltd – 022 218<strong>20</strong>59<br />

Toleo NO. 040 Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11 Bei Shs. 500/= ISSN 0856-5937<br />

Je wakulima wadogo wamefaidi<br />

matunda ya uhuru<br />

Picha ya Jalada:<br />

Mkazi wa kijiji cha Msowero wilayani<br />

Kilosa mkoani Morogoro akiwa na<br />

uso wenye tafakari nzito, Je, baada<br />

ya miaka 50 amefaidi matunda ya<br />

uhuru? b<br />

<strong>Uk</strong>. 1<br />

<strong>Uk</strong>. <strong>17</strong><br />

Bodi mpya ya <strong>MVIWATA</strong><br />

yachaguliwa<br />

<strong>Uk</strong>. <strong>20</strong><br />

Wakulima, matrekta waandamana<br />

kupinga uporwaji ardhi<br />

Tahariri<br />

Serikali iwasaidie wakulima<br />

kujikwamua na umasikini<br />

Moja ya kauli iliyotolewa<br />

na mkulima aliyechangia<br />

mawazo kwenye toleo hili<br />

ni ile isemayo “Kuna maana gani ya<br />

kusheherekea uhuru ili hali umasikini<br />

kama adui namba moja wa uhuru<br />

huo ametamalaki na kushamiri ndani<br />

ya familia za watanzania?”<br />

Kila msomaji wetu ana uhuru wa<br />

kuipa tafsiri na uzito tofauti kauli hii<br />

kadri ya mtizamo wake.<br />

Kwetu sisi kauli hii inaibua<br />

tafakari na msukumo wa kutafuta<br />

kuona kuna mafanikio gani ya msingi<br />

katika kupambana na umasikini<br />

nchini tokea tupate uhuru ambayo<br />

yanaweza kutufariji na kusheherekea<br />

miaka 50 ya uhuru?<br />

Ripoti ya Shirika la<br />

Maendeleo la Umoja wa Mataifa<br />

(UNDP) iliyozinduliwa mwaka jana<br />

jijini Dar es salaam inonyesha jinsi<br />

umasikini ulivyozidi kushika kasi<br />

kwa mtu mmoja mmoja na taifa<br />

kwa ujumla. Kwa mujibu wa ripoti<br />

hiyo, katika kila watanzania 100,<br />

watanzania 97 wanaishi kwenye<br />

umasikini wa kipato cha chini ya<br />

dola 2 kwa siku huku kila watanzania<br />

89 kati ya 100 wakiishi chini ya dola<br />

moja kwa siku. Kwa taswira hii na<br />

katika ulimwengu huu ambapo kila<br />

kitu kinapatikana kwa pesa, ni wazi<br />

kuwa wimbi la watanzania wengi<br />

hawamudu maisha yao kwa kukosa<br />

kipato cha kufanya hivyo.<br />

Kwa kukosa kipato, watanzania<br />

hasa vijijini bado wanaishi kwenye<br />

nyumba za nyasi na tembe mpaka hivi<br />

leo kwa kuwa hawamudu kununua<br />

bati, saruji na vifaa vingine vya ujenzi<br />

kutokana na kukosa kipato, pia<br />

watanzania wengi hususani vijijini<br />

hawamudu gharama hafifu za afya<br />

zilizopo na hivyo kuishia kufa au<br />

kujikita zaidi katika kupiga ramli na<br />

imani za kishirikina.<br />

Inasikitisha kuona kuwa ndani ya<br />

miaka 50 bado tunaishi kwa wasiwasi<br />

wa kukumbwa na njaa kila mwaka.<br />

Tokea uhuru mpaka sasa, watanzania<br />

zaidi ya asilimia 89 wanaishi kwa<br />

mwanga wa vibatari kwa kukosa<br />

nishati ya umeme, ingawa tuna mito,<br />

mabwawa na maziwa kila upande<br />

wa nchi.<br />

Ni vigumu wakulima kufurahia<br />

kuwa wana uhuru wakati ujinga<br />

miongoni mwao umeota mizizi<br />

huku kukiwa na porojo nyingi za<br />

kisiasa za kuwapumbaza hasa wakati<br />

wa kupiga kura. Ni wakulima hao<br />

hao wanaoliingizia kipato taifa hili,<br />

watoto wao wanasoma wakiwa<br />

wamekaa kwenye vumbi chini ya<br />

vivuli vya miti. Je, ndani ya mika 50<br />

ya uhuru na katika mazingira haya,<br />

wakulima wanaelimika ama idadi<br />

ya wajinga inaongezeka miongoni<br />

mwao?<br />

Kuwa huru maana yake ni<br />

kukomboka kifikra kunatokana<br />

na misingi ya elimu ambayo taifa<br />

limejiwekea kwa watu wake.<br />

Elimu ya kumkomboa mtanzania<br />

ni ile ya kumfanya mtanzania<br />

huyu ajisimamie mwenyewe na<br />

kuendesha maisha yake kwa<br />

umakini na ufanisi wa hali ya juu<br />

bila kuwepo na utofauti wowote na<br />

binadamu wengine wanaosemekana<br />

kupiga hatua kimaisha. Je, jamii yetu<br />

wakulima tunayo elimu kweli au<br />

ni ile elimu ya kuzalisha manamba<br />

wanaopaswa kuwahudumia wageni<br />

wanaomiminika nchini kwa kivuli<br />

cha uwekezaji. Ni uhuru upi huo<br />

tunaousherehekea katika hali kama<br />

hii?<br />

<strong>Uk</strong>o wapi uhuru wa mkulima<br />

kijijini wakati bado maelfu ya<br />

wanawake wanajifugulia nyumbani<br />

kwa sababu katika vijiji wanavyoishi<br />

hakuna zahanati, vituo vya afya wala<br />

hospitali? Hii ni huduma ya msingi<br />

inayopaswa kupatikana kiurahisi<br />

na kwa ubora wa hali ya juu kwa<br />

wananchi ndani ya taifa linalojinasibu<br />

kuwa huru kwa takribani miaka 50<br />

sasa. Katika hali halisi ya kitanzania,<br />

je, uhuru maana yake ni kutembea<br />

kilometa zaidi ya 50 kufuata huduma<br />

muhimu? Kwa ujumla serikali<br />

inapaswa kuwekeza nguvu nyingi<br />

katika hili.<br />

Umasikini umeota mizizi kwa<br />

kuwa rushwa nayo imeota mizizi.<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 3<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11


Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania<br />

Bara; Je, Wakulima Wadogo<br />

wamefaidi matunda ya Uhuru?<br />

Na Susuma Susuma, Morogoro<br />

Tanzania Bara imeadhimisha<br />

miaka 50 ya uhuru wake<br />

tangu mkoloni Mwingereza<br />

alipokabidhi utawala mnamo<br />

tarehe 9 Disemba 1961. Uhuru<br />

huu ulipatikana baada ya juhudi<br />

za dhati za vijana wa wakati huo<br />

wakiongozwa na Hayati Baba wa<br />

Taifa Mwalimu Julius Kambarage<br />

Nyerere kupambana kwa njia<br />

ya amani pasipo umwagaji damu<br />

kama yalivyofanya mataifa mengine<br />

Mafanikio<br />

yangekuwa ni uzalishaji<br />

kwa mashamba ya wakulima<br />

umeongezeka kwa kiasi gani, watu<br />

wanaolala njaa wamepungua kwa kiasi<br />

gani, watu wanaoishi chini ya dola<br />

moja kwa siku wamepungua kwa<br />

kiasi gani?<br />

ya Afrika.<br />

Miaka 50 ya kujitawala,<br />

tumeshuhudia awamu nne za<br />

uongozi wa Taifa letu, huku awamu ya<br />

kwanza ikiongozwa na Baba wa Taifa,<br />

Mwalimu Nyerere, awamu ya pili<br />

Mzee Ali Hassan Mwinyi, awamu ya<br />

tatu iliongozwa na Mzee Benjamini<br />

Mkapa na awamu hii ya nne usukani<br />

umeshikwa na Rais Jakaya Mrisho<br />

Kikwete. Katika awamu zote nne,<br />

serikali imepambana na changamoto<br />

nyingi za maendeleo, pia imetumia<br />

fursa nyingi za maendeleo ili<br />

kuwezesha maendeleo ya kiuchumi,<br />

kisiasa na ustawi wa jamii. Makala<br />

hii ambayo imejumuisha maoni na<br />

mitizamo ya makundi mbalimbali,<br />

itaangalia yatokanayo na jitihada za<br />

kuendeleza kilimo na changamoto<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />

zake katika awamu zote hizo<br />

Miongoni mwa maswali ya tafakari<br />

yaliyochochea kuandaa makala hii,<br />

ni:- Je ndani ya miaka 50 ya uhuru,<br />

wakulima wadogo wamefaidi<br />

matunda ya uhuru, nini mustakabali<br />

wao kwa miaka 50 ijayo? Na Jitihada<br />

zilizofanywa na awamu zote nne<br />

za serikali, zimefanikiwa kiasi gani<br />

kutatua matatizo yanayokabili ustawi<br />

wa jamii ya wakulima wadogo?<br />

Je wakulima wadogo wamefaidi<br />

matunda ya uhuru?<br />

Baadhi ya wadau wa kilimo,<br />

walipokuwa wakijibu swali hili, wengi<br />

wao majibu yao yalikuwa ni HAPANA<br />

na kusema kuna kila sababu<br />

ya msingi ya wakulima<br />

kuwa na maombolezo<br />

yanayoashiria kudai<br />

uhuru wa kweli na<br />

kuacha kudanganyika<br />

na uhuru wa bandia<br />

kutokana na dosari<br />

nyingi walizoziainisha.<br />

Msomi wa Chuo<br />

Kikuu cha Kilimo cha<br />

Sokoine (SUA) kilichopo<br />

mkoani Morogoro Dkt Damian<br />

Gabagambi aliyebobea katika<br />

masuala ya Uchumi Kilimo katika<br />

mada aliyoitoa kwenye Kongamano<br />

la miaka 50 ya Uhuru lililoandaliwa<br />

na <strong>MVIWATA</strong> Disemba 6, <strong>20</strong>11<br />

mjini Morogoro alisema tunatakiwa<br />

kujitathmini kwa kina ili kujua<br />

tumekosea wapi na tujipange vipi ili<br />

kukwepa kurudia makosa tuliyofanya<br />

huko nyuma na tunayofanya sasa.<br />

“Kwa haraka haraka wananchi<br />

wanaweza kushawishika na kuridhika<br />

kuwa nchi yetu imeendelea sana<br />

tangu tupate uhuru. <strong>Uk</strong>weli ambao<br />

wananchi hawaelezwi ni kwamba,<br />

tutoke ndani ya boksi kabisa, tuache<br />

tabia ya kujilinganisha na wachovu<br />

ambao hawana hata robo ya utajiri<br />

wa maliasili za Tanzania, tujilinganishe<br />

na walio mbele yetu kama vile<br />

MADA MAALUM<br />

Malaysia” alisema Dkt Gabagambi.<br />

Alisema serikali inatumia fedha<br />

nyingi kwenye sekta ya kilimo bila<br />

mafanikio ya maana, zaidi ya yale<br />

yanayoripotiwa kwenye makaratasi;<br />

tena kwa kiwango cha raslimali<br />

fedha zilizoingizwa kwenye sekta<br />

na wala sio mabadiliko chanya kwa<br />

mkulima.<br />

Alisema mafanikio yanayotajwa<br />

na serikali siyo mafanikio halisi bali<br />

ni maandalizi ya kwenda kwenye<br />

mafanikio. Mafanikio yangekuwa ni<br />

uzalishaji kwa mashamba ya wakulima<br />

umeongezeka kwa kiasi gani, watu<br />

wanaolala njaa wamepungua kwa<br />

kiasi gani, watu wanaoishi chini ya<br />

dola moja kwa siku wamepungua<br />

kwa kiasi gani?<br />

“Kwa ufupi, kinachofanyika nchi<br />

hii katika kuhudumia kilimo ni kwa<br />

miradi kufukuzana na milestones<br />

zilizo katika maandiko ya miradi<br />

basi,” alisema na kuitaka serikali iteue<br />

maeneo machache na kuwekeza kwa<br />

tija badala ya kutawanya raslimali<br />

kwenye miradi mingi isiyoleta tija.<br />

Aliongeza kuwa pamoja na bidii<br />

zote hizi sekta ya kilimo bado<br />

inakabiliwa na matatizo yale yale<br />

ya miaka yote ambayo ni tija duni,<br />

ukosefu wa mikopo, miundo mbinu<br />

duni, kilimo cha kutegemea mvua,<br />

ukosefu wa masoko, usindikaji<br />

mdogo, teknolojia duni, kutotumia<br />

matokeo ya tafiti katika mipango na<br />

huduma duni za ughani.<br />

Mtaalamu huyu anaitaka serikali<br />

iache kujilinganisha na nchi masikini<br />

zenye raslimali chache kuliko Tanzania.<br />

“Tulenge kupata mafanikio makubwa<br />

bila kujali jirani zetu wamefanikiwa<br />

kiasi gani. Kulenga mbali kuna maana<br />

kubwa sana katika saikolojia ya<br />

matumizi ya raslimali za mtu au nchi.<br />

Nchi ikijiwekea malengo makubwa<br />

italazimika kuwa mwangalifu sana<br />

katika kila senti inayopatikana, na<br />

haitakuwa na mchezo kwa yeyote<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 2<br />

1


MADA MAALUM<br />

Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara...<br />

Inatoka uk. wa 1<br />

anayekwamisha mipango kwa<br />

kusimamia vibaya rasilimali za nchi.<br />

Kinyume chake, nchi isipokuwa<br />

na malengo ya juu sana inaweza<br />

kujikuta ikiwa na matumizi ya anasa<br />

kama tunavyoshuhudia hapa nchini.”<br />

Anasema katika miaka hamsini<br />

ijayo Tanzania inatakiwa ilenge mbali.<br />

Ikilenga kuwa kama Afrika Kusini<br />

inaweza kuishia kuwa kama Kenya.<br />

Lakini ikilenga kuwa kama Marekani,<br />

inaweza kuishia kuwa kama Malaysia<br />

au Singapore, ambapo tayari<br />

yatakuwa ni mafanikio makubwa.<br />

Akamalizia ameshauri kwamba ni<br />

vyema itumike kauli mbiu mpya<br />

yenye ujumbe usemao “Miaka<br />

50: Tumethubutu, Tumeshindwa,<br />

Tujipange Upya”.<br />

Mwalimu Nyerere aliposhika<br />

madaraka alibainisha maradhi, ujinga<br />

na umasikini kama matatizo ya msingi<br />

ya nchi yaliyopaswa kushughulikiwa,<br />

ambayo kwa mtizamo wa Bibi<br />

Marcelina Charles Kibena<br />

mkulima kutoka tarafa ya Mgeta<br />

wilayani Mvomero, anahoji “kuna<br />

maana gani ya kusheherekea uhuru<br />

ili hali umasikini kama adui namba<br />

moja wa uhuru huo ametamalaki<br />

na kushamiri ndani ya familia zetu?<br />

Kuna mafanikio gani ya msingi katika<br />

kupambana na umasikini katika<br />

kipindi hiki ambacho wakulima<br />

tunyanyaswa na kunyimwa haki za<br />

msingi?”<br />

Bibi Marcelina Charles Kibena<br />

Bibi Kibena aliyekuwa akiwasilisha<br />

mada ya uzoefu wa mkulima mdogo<br />

kwenye Kongamano la miaka<br />

hamsini ya maendeleo ya kilimo<br />

lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha<br />

Sokoine cha Kilimo (SUA), alisema<br />

tunapoangalia uzoefu wa miaka<br />

50 iliyopita ni lazima kulinganisha<br />

2<br />

maisha ya mkulima mdogo kijijini<br />

na shughuli zake za kilimo kama<br />

mhimili wa maisha yake na wananchi<br />

wengine ambao wanategemea aina<br />

nyingine ya kipato, na hasa watu<br />

waishio mijini.<br />

“Kwa kipindi cha miaka hamsini<br />

ya uhuru kumekuwepo na<br />

matamko mbalimbali<br />

yenye nia thabiti ya<br />

kuboresha kilimo na<br />

wakulima wadogo<br />

kama Siasa ni Kilimo,<br />

Kilimo ni uti wa mgongo<br />

wa nchi, Chakula ni uhai,<br />

Kilimo cha kufa na kupona na sasa<br />

Kilimo Kwanza. Pamoja na matamko<br />

yote hayo, kwa ujumla tunaweza<br />

kusema kuwa katika kipindi hiki<br />

cha miaka hamsini ya uhuru kundi<br />

hili la wazalishaji wadogo limebaki<br />

katika hali duni ya maisha. Hali hii<br />

imetokana na sera ambazo kwa kiasi<br />

kikubwa hazimjali mkulima mdogo.”<br />

Alisema katika miaka 50 hii,<br />

wakulima wadogo wanaishi kwa<br />

hofu kubwa ya kuporwa ardhi na<br />

akakumbuka maneno ya hayati<br />

baba wa Taifa mwaka 1958 ambayo<br />

sasa yanatimia, nukuu: “Katika<br />

nchi kama yetu ambayo<br />

Waafrika ni maskini na<br />

wageni ni matajiri, kuna<br />

uwezekano mkubwa kwamba<br />

Mwafrika akiruhusiwa<br />

kuuza ardhi, katika miaka<br />

themanini au miaka ijayo,<br />

ardhi yote ya Watanganyika<br />

itamilikiwa na matajiri<br />

wageni, na wenyeji watakuwa<br />

watwana. Lakini hata<br />

kama wageni wasingekuwa<br />

matajiri, litaibuka tabaka<br />

la watanganyika matajiri<br />

wajanja. Tukiiruhusu ardhi<br />

iuzwe kama kanzu, katika<br />

muda mchache, kutakuwa<br />

na kundi dogo la waafrika<br />

wakiwa na ardhi na walio<br />

wengi watakuwa watwana.”<br />

Uwezeshaji na Uzalishaji<br />

Akizungumzia kiwango cha uzalishaji,<br />

Bibi Kibena alisema, wakulima<br />

wamekuwa wakitumia kwa kiasi<br />

kikubwa mbegu za asili na ndizo<br />

ambazo zimewezesha kulisha taifa<br />

kwa kipindi chote cha miaka hamsini<br />

ya uhuru. Hata hivyo akasema<br />

wameibuka watu wachache wa<br />

kuzibeza wakishinikiza kuleta mbegu<br />

za viini tete (GMOs) ili kutupotezea<br />

“Sisi<br />

tunaona kuwa hali<br />

hii itamfanya mkulima mdogo<br />

kuwa mtumwa wa mbegu na<br />

kumzidishia umaskini.”<br />

mbegu zetu za asili na wao kumiliki<br />

soko lote la mbegu. “Sisi tunaona<br />

kuwa hali hii itamfanya mkulima<br />

mdogo kuwa mtumwa wa mbegu na<br />

kumzidishia umaskini.”<br />

Mkulima huyo, anashangazwa<br />

na kitendo cha serikali kushindwa<br />

kumuwezesha mkulima mdogo kuwa<br />

mwekezaji ambaye anawezeshwa<br />

kwa kila hali ili azalishe na mazao<br />

yake yanunuliwe kwa bei nzuri<br />

ambayo itamuwezesha kurudisha<br />

gharama zote na akapata faida<br />

stahiki, kwani hii ingekuwa ndiyo<br />

njia pekee ya kuboresha maisha<br />

ya wananchi wa vijijini badala ya<br />

kuwaachia wajitafutie kama kuku<br />

wa kienyeji.<br />

Alisema changamoto nyingine<br />

inayowakabili wakulima ni ushuru<br />

na kodi. Akasema pamoja na<br />

serikali kuondoa kodi ndogo ndogo<br />

zilizokuwa kero kwa wananchi,<br />

lakini bado Halmashauri nyingi<br />

zimezirudisha kodi hizi ambazo<br />

hatima yake ni kumbebesha mzigo<br />

mkulima na kuzidi kumpunja mapato<br />

yake. “Kwenye maeneo mengi<br />

hivi sasa kusafirisha mazao kutoka<br />

kijiji au kata moja kwenda nyingine<br />

inabidi kulipa ushuru kwenye mageti.<br />

Kadri unavyosafirisha mbali ndivyo<br />

unavyokutana na mageti mengi<br />

ambayo inabidi kulipa ushuru. Pamoja<br />

ya kwamba ushuru unalipwa na<br />

msafirishaji, lakini hatimaye mkulima<br />

atapewa bei ndogo ili kufidia ushuru<br />

anaotozwa msafirishaji, na hivyo<br />

mkulima kuzidi kudidimia.”<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 3<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11


Inatoka uk. wa 2<br />

“Kodi hizi haziishii kwenye<br />

mazao peke yake. Hata pale ambapo<br />

wakulima wadogo tumejitahidi<br />

kuanzisha vyombo vyetu vya<br />

fedha kama SACCOS, Mamlaka ya<br />

Mapato Tanzania (TRA) wanakuja<br />

na kuchukua kodi kutoka katika<br />

vyombo hivyo japokuwa SACCOS<br />

hulipa ada kwenye mamlaka<br />

zinazosimamia ushirika nchini. Kwa<br />

nini vyombo vyetu hivi visipewe<br />

msamaha wa kodi kama tunavyosikia<br />

na kushuhudia wawekezaji wa<br />

nje wakipewa misamaha ya kodi<br />

kwa vipindi maalumu?” alihoji Bibi<br />

Kibena.<br />

Kilimo na Muundo wa<br />

Uchumi<br />

Mhadhiri Msaidizi katika Chuo<br />

Kikuu cha Dar es Salaam katika<br />

Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala<br />

wa Umma Bw. Bashiru Ally<br />

anasema kwa asilimia kubwa kilimo<br />

kimechangia maendeleo makubwa<br />

nchini.<br />

“Mambo mengi ya maendeleo<br />

yaliyofanyika hapa nchini ndani ya<br />

miaka 50 ni matunda ya kilimo<br />

kwa sababu nchi yetu ni ya kilimo<br />

na kilimo ndio kinachochangia<br />

maendeleo kwa asilimia kubwa<br />

kwani kinatupatia chakula pamoja<br />

na fedha za kigeni.”<br />

Hata hivyo akichambua historia ya<br />

kilimo hapa nchini Bw. Ally anasema<br />

kuanzia miaka ya 1961-1985 dola<br />

ilimiliki shughuli zote ikiwemo Vyama<br />

vya Ushirika vilivyoanzishwa kwa<br />

malengo ya kuwasaidia wakulima<br />

ambavyo vilimilikishwa kwenye dola<br />

na hivyo kupoteza nguvu yake na<br />

kufanya hali ya mkulima kuendelea<br />

kuwa duni.<br />

Anataja kuwa jambo ambalo<br />

halikutokea katika miaka hii 25 ya<br />

mwanzo ni kutovamiwa kwa ardhi<br />

ya wakulima ingawaje kilimo chetu<br />

kiliendelea kuwa cha kawaida. “Katika<br />

kipindi hicho serikali haikufungua<br />

milango kwa wawekezaji wakubwa<br />

badala yake yenyewe ilianzisha<br />

mashamba na kuyaendesha,<br />

lakini kutokana na kukosa ufanisi<br />

wa kuyatunza mashamba hayo<br />

yalipoteza thamani yake.”<br />

Amesema katika muundo wa<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />

uchumi wa sasa, msukumo mkubwa<br />

upo katika uwekezaji, ambapo ardhi<br />

inayomilikiwa na wakulima wadogo<br />

serikali imeigawa kwa wawekezaji<br />

wakubwa kitendo ambacho kimeleta<br />

athari kubwa kwa wakulima wadogo<br />

kutokana na mfumo wao wa<br />

uzalishaji kuvurugwa.<br />

Bw. Ally akazungumzia jinsi<br />

ambavyo katika miaka ya hivi<br />

karibuni serikali imeshindwa<br />

kuweka muunganiko baina ya<br />

sekta ya uzalishaji (kilimo) na<br />

sekta ya viwanda, kwani wakulima<br />

wanazalisha malighafi lakini viwanda<br />

vya kumalizia kutengeneza bidhaa<br />

za kupeleka sokoni havipo. Viwanda<br />

vingi vilivyokuwepo awali vimefia<br />

mikononi mwa walafi wachache,<br />

mfano kiwanda cha magunia, ngozi<br />

na nguo.<br />

Anasema mwelekeo wa uzalishaji<br />

umekuwa ni wa kuuza nje na si<br />

ndani ya nchi kwani bidhaa nyingi<br />

zinazopatikana katika maduka mengi<br />

nchini si mazao yanayolimwa hapa<br />

nchini bali yanayotoka nje kitendo<br />

ambacho kinachangia kuua soko la<br />

ndani na kuacha mazao ya wakulima<br />

wadogo yakiozea shambani na<br />

kushuka thamani.<br />

“Hivi sasa tunajiandaa kuruhusu<br />

wakulima wakubwa kutoka nje<br />

kuzalisha mazao ya chakula ili<br />

kukidhi mahitaji ya ndani na nje<br />

ya nchi badala ya kuwawezesha<br />

wakulima wetu kuzalisha mazao<br />

hayo ili waweze kuwa na kilimo<br />

endelevu, jambo ambalo linaweka<br />

hatarini mustakabali wa wakulima<br />

wadogo. Mfano halisi ni wa maeneo<br />

makubwa ambayo ni vyanzo vizuri<br />

vya uzalishaji kama vile bonde la<br />

Rufiji na mikoa ya Rukwa na Kigoma,<br />

huku kote ni kwamba sauti za<br />

wakulima wadogo hazisikiki na wala<br />

hazionekani kuwa ni za muhimu.<br />

Suala la sauti za wakulima<br />

kutosikika lilimgusa pia Mtendaji<br />

Mkuu wa Mfuko wa Mwalimu<br />

Nyerere Bw. Joseph Butiku<br />

wakati akifungua Kongamano la<br />

Miaka 50 ya Uhuru na Mustakabali<br />

wa Wakulima Wadogo lililoandaliwa<br />

na <strong>MVIWATA</strong> Disemba 6, <strong>20</strong>11 mjini<br />

Morogoro, alisema wakulima sauti<br />

zao hazisikiki kwa sababu ya uoga<br />

na ujinga walionao. Alisema ujinga ni<br />

MADA MAALUM<br />

kigezo kikubwa kinachowakwamisha<br />

wasifanikiwe. Akashauri chombo cha<br />

<strong>MVIWATA</strong> kilenge kuwapa wakulima<br />

nguvu ili waew na vitendo vya pamoja<br />

na si sauti ya pamoja tu. “<strong>MVIWATA</strong><br />

muwajengee wakulima uwezo wawe<br />

na nguvu na vitendo vya pamoja<br />

vitakavyowezesha kuwaita viongozi<br />

wa Serikali ili kuongea nao na kutoa<br />

mapendekezo yao na wakulima<br />

msiwe waoga wala wanyonge kwani<br />

huwezi kuwa mwoga na ukatafuta<br />

ukweli au kutoa ushauri na kujenga<br />

taifa linalojiamini.”<br />

Aliwahimiza wakulima kwamba<br />

watafanikiwa tu iwapo wataunda<br />

umoja na mshikamano thabiti ili<br />

kwamba wakisema jambo linasikika<br />

na serikali inajibu haraka.<br />

Aliwasihi wajumbe wa kongamano<br />

hilo wanapotafakari miaka 50 ya<br />

uhuru na mustakabali wa mkulima<br />

warejee historia ambapo alisema<br />

kuwa nchi ya Tanzania ni ya makundi<br />

makuu mawili yaani wakulima na<br />

wafugaji na kundi la wafanyakazi,<br />

ambapo kundi la wakulima na<br />

wafugaji linabeba idadi kubwa ya<br />

Inatoka uk. wa Tahariri<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 4<br />

Serikali iwasaidie<br />

wakulima...<br />

Kwa sababu hakuna juhudi zenye<br />

dhamira ya kweli za kupambana<br />

na rushwa zaidi ya maigizo<br />

tunayoyaona sasa basi ni dhahiri<br />

kuwa kuna juhudi hafifu mno za<br />

kupambana na maadui wa uhuru<br />

wa kweli ambao ni umasikini,<br />

maradhi na ujinga.<br />

Kwa kuwa rushwa imekua injini<br />

ya kuchochea ujinga na maradhi<br />

ambayo nayo yamechangia<br />

kukuza umasikini kwa taifa hili,<br />

basi ni ukweli ulio wazi kuwa<br />

rushwa pia ni kihunzi cha uhuru<br />

wa kweli na maendeleo ya kweli<br />

kwa Tanzania.<br />

Wakati tunasherehekea<br />

miaka 50 ya uhuru wa Tanzania<br />

Bara, tunaitaka serikali ionyeshe<br />

dhamira kubwa ya kusukuma<br />

zaidi maedeleo ya kilimo nchini ili<br />

kwenda sambamba na matarajio ya<br />

kujikwamua kiuchumi na kuliletea<br />

taifa maendeleo ya kweli.<br />

3


MADA MAALUM<br />

Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara...<br />

Inatoka uk. wa 3<br />

wananchi wanaolijenga Taifa la<br />

Tanzania. “Serikali inatoka miongoni<br />

mwa makundi hayo mawili kwa hiyo<br />

inabidi kupanga pamoja ili kujua<br />

tuendako baada ya miaka hii 50 ya<br />

uhuru.”<br />

Bw. Butiku alienda mbali zaidi<br />

na kushauri wakulima watumie<br />

mamlaka waliyonayo kwa kuinyima<br />

kura kwenye uchaguzi mkuu ujao<br />

wa <strong>20</strong>15 serikali ya chama tawala<br />

kilichopo madarakani iwapo<br />

itaendelea kutowasikiliza.<br />

“Ninyi nyote ni wapiga kura,<br />

madaraka na mamlaka ya nchi hii<br />

yanatoka kwenu, iambieni CCM<br />

chama changu mimi kwamba kama<br />

sheria ya vijiji na mambo mengine<br />

yanayotukera hayatekelezwi, <strong>20</strong>15<br />

hatuwapigii kura,… mimi sitaki kufa<br />

katika fujo tumekulia katika amani…<br />

kauli yangu ni kauli ya demokrasi na<br />

si uchochezi, ” alisisitiza Bw. Butiku.<br />

Je bado wakulima ni sehemu<br />

ya wamiliki wa uchumi wa<br />

taifa letu?<br />

Akizungumza kwenye Kongamano<br />

hilo lililoandaliwa na <strong>MVIWATA</strong> Dkt.<br />

Azavieli Lwaitama wa Chuo Kikuu<br />

cha Dar Es Saalam, alisema kuwa<br />

katika kipindi cha mwaka 1961 hadi<br />

1985 ni kweli tulithubutu, tuliweza<br />

na kusonga mbele kwa kuwasaidia<br />

wakulima kwa kuanzisha Azimio<br />

la Arusha na viwanda mbalimbali<br />

vilivyotumia malighafi za wakulima.<br />

Lakini kuanzia mwaka 1985 hadi<br />

<strong>20</strong>11 nchi imekuwa na juhudi kubwa<br />

katika kuwakaba koo wakulima na<br />

kuwapora ardhi yao.<br />

Alisema wakulima wadogo<br />

wametupwa kando katika kumiliki<br />

uchumi na kuonekana kama ni<br />

wasumbufu. “Kwa kipindi hiki<br />

kauli mbiu inatakiwa isomeke<br />

“tumethubutu, tumeweza<br />

na tunasonga mbele katika<br />

kuwakaba koo wakulima.”<br />

Alieleza kuwa Uhuru wa nchi yoyote<br />

unatokana na umiliki wa ardhi na<br />

ndio maana watu wanapigana kila<br />

siku kudai ardhi na kuongeza kuwa<br />

kwa sasa wakulima ndio wanapaswa<br />

kujitafakari Je, wamethubutu,<br />

wameweza na kusonga mbele katika<br />

4<br />

kutetea haki zao?<br />

Alishauri kuwa ili kuweza<br />

kukabiliana na hali hii na kuzidi<br />

kusonga mbele inabidi wakulima<br />

waimarishe umoja wao, wapate<br />

elimu ya kujitegemea na sera za ardhi<br />

zifundishwe kuanzia mashuleni.<br />

Kwa upande wake Kanali<br />

(Mst) Anatory Tarimo, Mkuu<br />

wa mkoa mstaafu aliwaambia<br />

washiriki wa Kongamano hilo<br />

kuwa Katiba ya nchi haifuatwi<br />

ndiyo maana hawafaidi matunda ya<br />

uhuru na ni jukumu la wakulima<br />

kuhakikisha inafuatwa na hatua hizo<br />

zinaweza kuwa hata za kisheria.<br />

Aliwashauri wakulima kujiendeleza,<br />

kuwa wabunifu na kujenga uwezo<br />

wa kujiamini huku akisisitiza kuwa<br />

jukumu la kumuendeleza mkulima<br />

mdogo ni la mkulima mwenyewe<br />

na wasitegemee watu kutoka nje au<br />

viongozi waliopo madarakani.<br />

Alisema wakulima wanapaswa<br />

kujipanga katika vikundi na mitandao,<br />

kuwa wabunifu, wazifahamu sheria za<br />

ardhi na wawe na mfumo imara wa<br />

masoko utakaowezesha kumuuzia<br />

mlaji wa mwisho na kuwaondoa<br />

madalali ambao ndio wamekuwa<br />

wakifaidi jasho la wakulima.<br />

Bibi Veronica Sophu ni<br />

Makamu Mwenyekiti wa <strong>MVIWATA</strong><br />

taifa na mkulima mdogo kutoka kijiji<br />

cha Madibila wilaya ya Mbarali yeye<br />

anasema pamoja na kubaki masikini<br />

na kutotambuliwa na serikali katika<br />

kipindi cha miaka hii 50 ya uhuru<br />

wakulima wameendelea kulisha nchi<br />

yetu.<br />

Katika mawasilisho yake kwenye<br />

kongamano hilo Bibi Sophu alisema<br />

anasikitishwa na jinsi ambavyo<br />

wakulima hawathaminiwi na<br />

wanadharauliwa wakati wao ndio<br />

wanalisha taifa. Alisema wakulima<br />

hivi sasa wananyanyasika wanaishi<br />

kwa hofu katika nchi yao kama<br />

wakimbizi kutokana na vitendo<br />

wanavyofanyiwa na serikali.<br />

Bw.Thomas Laizer ambaye<br />

ni Afisa Ushawishi na Utetezi wa<br />

<strong>MVIWATA</strong> yeye anasema kutokana<br />

na historia ya nchi yetu wakulima<br />

wamenufaika kwa uchache sana na<br />

matunda ya uhuru.<br />

Anasema kufa kwa viwanda<br />

vilivyojengwa katika awamu ya<br />

kwanza ya utawala, kumepoteza<br />

fursa nzuri ya masoko kwa mazao<br />

ya wakulima. Jambo jingine anasema<br />

ni kushuka kwa suala la elimu na<br />

huduma muhimu za kijamii. “Kila<br />

mahali wananchi wanashuhudia hilo<br />

na ni vigumu kwa mkulima mdogo<br />

kuakisi faida za uhuru huo katika<br />

maisha yake ya kawaida.”<br />

Bw. Ladslaus Bigambo,<br />

Mratibu wa <strong>MVIWATA</strong> Ruvuma<br />

anasema “kuna ukweli usiopingika<br />

sasa kuwa Tanzania imepoteza<br />

mwelekeo wa karama ya uongozi<br />

wenye utashi wa kisiasa unaoweza<br />

kuwaelekeza watu kwenye<br />

mafanikio.<br />

Kwa upande mwingine watanzania<br />

wengi hawaoni uchungu wa dhuluma<br />

wanayofanyiwa katika nchi yao,<br />

hawapo tayari kuuliza ama kufuatilia<br />

jambo lolote, hata kama lina athiri<br />

maisha yao. Mfano wakazi Loborsoit<br />

na Ngage wilaya ya Simanjiro mkoani<br />

Manyara wamezungukwa na mbuga<br />

ya wanyama inayotumiwa kwa<br />

uwindaji wa kitalii, lakini wakazi wa<br />

vijiji hivyo hawafuatilii kudai mapato<br />

ambayo yangestahili kurejeshwa<br />

kwao ili wao kama walinzi wa<br />

wanyama hao wafaidi matunda.”<br />

Bibi. Mary Nsemwa, mkuu<br />

wa Idara ya Ushawishi na Ujenzi wa<br />

Nguvu za Pamoja katika Mtandao<br />

wa Jinsia Tanzania (TGNP), anasema<br />

asilimia kubwa ya wananchi<br />

wanaojishughulisha na kilimo hiki<br />

ni wanawake ambao hawashirikishi<br />

katika maamuzi ngazi ya kaya<br />

hususani kiasi gani kizalishwe, kiasi<br />

gani kiuzwe, na kwa bei gani na kiasi<br />

gani kinaitosha familia kwa chakula,<br />

vitendo ambavyo vinamfanya<br />

mwanamke huyu kukosa thamani<br />

katika jamii.<br />

Katika miaka hii 50 baada ya uhuru<br />

wanawake wakulima hawawezi<br />

kujivunia kuwa wamenufaika na<br />

lolote kutokana na kasoro mbalimbali<br />

zinazojitokeza katika utaratibu wa<br />

uongozi uliopo kwani hawashiriki<br />

katika kutunga sera na sheria za<br />

nchi, kushiriki katika vyombo vya<br />

maamuzi na kupewa uhuru wa kutoa<br />

maoni na mapendekezo yao katika<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 5<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11


Inatoka uk. wa 4<br />

kupanga mikakati ya maendeleo<br />

itakayowasaidia.<br />

Ametaja mambo kadhaa ya<br />

kufanyiwa marekebisho kuwa ni<br />

pamoja na kuongeza ushiriki wa<br />

wanawake katika vikao vya maamuzi<br />

“wanaume waliobadilika na kuelewa<br />

vyema suala hili la usawa huwasaidia<br />

wanawake katika kutekeleza<br />

majukumu yao.”<br />

Akizungumzia suala la Bajaji<br />

kutumika kusafirisha wajawazito<br />

katika kipindi hiki huku kukiwa<br />

hakuna miundombinu ni kuwafanyia<br />

dhihaka kundi hili la wanawake.<br />

Bw. Marcossy Albanie wa<br />

Kituo cha Msaada wa Sheria na Haki<br />

za Binadamu na pia mchambuzi<br />

wa masuala ya kisiasa na uchumi<br />

yeye alianza kwa kushangazwa na<br />

kitendo cha mkulima kuwekewa<br />

masharti lakini biashara na viwanda<br />

vimeendelea kuwa huru vitendo<br />

ambavyo vimezuia wakulima wadogo<br />

kuwa washindani katika soko huria.<br />

Kwa sasa wakulima wanawekewa<br />

vizingiti kuhusu nini cha kuzalisha, na<br />

wauze wapi na cha kushangaza zaidi<br />

ni kwamba wakuu wa wilaya wana<br />

sauti ya kuwaamrisha wakulima<br />

kuzalisha kwa kiwango fulani lakini<br />

hawasemi kiwanda gani kiwekwe<br />

hapo kitumie mazao yanayozalishwa<br />

kitendo ambacho kinampa hasara<br />

mkulima. Kwa ujumla wakulima ni<br />

kundi lililoachwa nyuma na hata<br />

akizungumza watu wanampuuzia.<br />

Anasema ili wakulima wafaidi<br />

matunda ya uhuru wanahitaji uhuru<br />

wa pili ambao utamkomboa mkulima<br />

na changamoto hizi zinazomkabili<br />

na haya yote yanawezekana endapo<br />

tutabadilisha mfumo wa uongozi<br />

uliopo hapa nchini ambao utatoa<br />

fursa sawa, utalenga huduma sawa<br />

na kutambua kwamba kuishi vijijini<br />

ni changamoto kubwa.<br />

Anasema “Mkulima anapaswa<br />

kupewa kiinua mgongo kama<br />

mfanyakazi wa kawaida kwani hata<br />

yeye anachangia katika maendeleo<br />

ya taifa na mfumo huu uliopo ni<br />

kandamizi, ni sawa na wizi wa nguvu<br />

za wakulima.”<br />

Nini kifanyike kumrejesha<br />

mkulima mdogo katikati ya<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />

mfumo wa uzalisaji<br />

Mkuu wa Mkoa Mstaafu wa Morogoro<br />

Bw. Stephen Mashishanga,<br />

yeye alipendekeza kilimo cha<br />

mkataba kipigwe marufuku nchini<br />

kwa kuwa ni utumwa mpya na<br />

ukoloni mambo leo unaotunyemelea<br />

watanzania.<br />

Akapendekeza pia kila mwananchi<br />

amilikishwe ardhi kisheria, kuongeza<br />

uzalishaji katika kila maeneo na<br />

kuimarisha soko la ndani na nje<br />

ya nchi, kuimarisha huduma za<br />

ugani vijijini na wakulima washiriki<br />

kikamilifu katika kuandaa katiba<br />

mpya na <strong>MVIWATA</strong> iendelee kuwa<br />

mtetezi wa kweli wa mkulima<br />

mdogo.<br />

Mwanasiasa Mkongwe nchini<br />

Dkt Chrisant Mzindakaya<br />

yeye anashauri serikali kuweka<br />

kipaumbele katika kufanya utafiti<br />

wa kilimo na mifugo na kuzitumia<br />

tafiti hizo na akasisitiza watumie<br />

wataalamu walioko vyuoni ili<br />

kuhakikisha wanafanikisha tafiti hizo<br />

zinazochochea maendeleo.<br />

Kwa upande wake Profesa<br />

Dominic Kambarage wa Chuo<br />

Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA)<br />

anasema ili sekta ya kilimo na mifugo<br />

iendelee lazima turudishe mifumo<br />

ya uwajibikaji na serikali iandae<br />

mikakati ya kudhibiti magonjwa<br />

kwa mifugo na mimea. “Kwenye<br />

tasnia ya ugani, ugani umeharibika<br />

inabidi serikali ijiulize tufanye nini<br />

ili kuwe na tasnia nzuri, njia pekee<br />

ni kuajiri wataalamu toka vyuoni<br />

na kutumia rasilimali vizuri waende<br />

vijijini kufanya kazi bila hivyo kilimo<br />

kwanza hakitafanikiwa.”<br />

Profesa Dominic Kambarage - SUA<br />

“Sekta ya mifugo itakwenda<br />

kama kutakuwa na programu<br />

MADA MAALUM<br />

zinazoonyesha sera na nini<br />

kimefanyika pia ndani yake kuwe<br />

na mgawanyiko wa programu<br />

ndogondogo kwa kila tasinia ya<br />

mifugo kama za kuku, ngombe,<br />

maziwa, kwani hivi sasa serikali<br />

ukiiuliza kuhusu programu za<br />

mifugo wanasema bado ziko jikoni<br />

zinapikwa, huu si mwenendo mzuri,”<br />

alisema Profesa Kambarage kwenye<br />

Kongamano la Maendeleo ya Kilimo<br />

chuoni hapo.<br />

Akizungumzia mwelekeo wa<br />

Chuo Kikuu pekee cha Kilimo (SUA)<br />

juu ya kuleta maendeleo ya kilimo<br />

katika miaka 50 ijayo Profesa<br />

Amon Mattee anasema ni lazima<br />

kuangalia mitaala na mbinu za<br />

ufundishaji ili mafunzo yashabihiane<br />

na uhalisia wa watakachokifanya<br />

wahitimu wamalizapo masomo ili<br />

kuweza kutoa mchango wa haraka<br />

na wa moja kwa moja katika<br />

maendeleo ya sekta ya kilimo.<br />

Pili akashauri utafiti ulenge wadau<br />

katika ngazi mbalimbali za maamuzi<br />

toka kwa mkulima hadi ngazi za<br />

juu kabisa za watunga sera kwani<br />

maendeleo ya kilimo ni matokeo ya<br />

maamuzi katika ngazi mbalimbali.<br />

Dkt. Gabagambi wa SUA<br />

anashauri iwepo programu kabambe<br />

ya kitaifa ya kupima ardhi yote ya<br />

nchi ili kuwa na ramani ya kanda za<br />

matumizi bora ya ardhi. Ramani hiyo<br />

ionyeshe eneo gani litatumika kwa<br />

kazi gani hususan katika shughuli za<br />

binadamu kwa uhai wa nchi hii.<br />

Kadhalika anashauri iundwe<br />

bodi ya nafaka (National Cereal<br />

Board) kushughulikia mazao hayo<br />

nchini. Jukumu kuu la bodi liwe<br />

ni kuhamasisha uzalishaji wa<br />

mazao haya kwa lengo la kuwa na<br />

mlipuko wa nafaka (cereal boom)<br />

utakaosaidia taifa kujitosheleza kwa<br />

chakula (Tanzania kuwa ghala la<br />

nafaka la nchi za mashariki na kusini<br />

mwa Afrika), kupata fedha ya kigeni,<br />

na kuchochea kasi ya kukua kwa<br />

uchumi. Na akashauri pia liundwe<br />

baraza la ushauri la kitaifa katika<br />

sekta ya kilimo lenye jukumu la<br />

kufanya tafakuri ya kina juu ya nini<br />

kifanyike, kwanini kifanyike, wapi<br />

kifanyike, namna gani kifanyike, lini<br />

na kwa muda gani kifanyike, na kwa<br />

matokeo gani.<br />

5


MADA MAALUM<br />

6<br />

Maoni ya wakulima<br />

Kwa sehemu kubwa maoni<br />

yaliyotolewa na wakulima<br />

kuhusiana na mustakabali<br />

wao kwenye miaka 50 ijayo<br />

yameakisi hofu kubwa waliyonayo<br />

ya kusukumwa kando kwa<br />

kuporwa ardhi na changamoto ya<br />

masoko ya mazao.<br />

Wengi wao wameonyesha jinsi<br />

ambavyo mifumo ya uzalishaji<br />

inavurugwa pale wakulima<br />

wanapoondolewa kwenye ardhi<br />

waliyokuwa wakilima tangu enzi<br />

za mababu zao na kugawiwa kwa<br />

wawekezaji. Baadhi ya wakulima<br />

wamepigwa, kujeruwiwa na hata<br />

kufungwa gerezani pale walipoendelea<br />

kudai haki yao. Wakati mwingine mazao<br />

ya wakulima kung’olewa shambani,<br />

mifugo kuuawa, kuchomwa moto<br />

nyumba zao au mifereji ya maji hasa<br />

maeneo ya umwagiliaji kufukiwa na<br />

hivyo wakulima kushindwa kuendelea<br />

na kilimo. Wakulima wafuatao<br />

wanashuhudia haya kuhusiana na hali<br />

halisi ya mkulima kiuchumi, kielimu,<br />

kisiasa na hata kijamii.<br />

Bibi.Lydia Ruliho ni mkulima<br />

mdogo kutoka mkoani Rukwa<br />

anasema kuwa katika miaka 50 ya<br />

uhuru elimu vijijini bado ni kitendawili<br />

kutokana na serikali kutotilia mkazo<br />

katika suala la elimu kwa wananchi wa<br />

maeneo ya pembezoni, huku akitolea<br />

mfano wa mkoa wa Rukwa kwamba<br />

mwaka huu wa <strong>20</strong>11 wanafunzi<br />

wa darasa la saba katika vijiji 14<br />

vya mwambao wa ziwa Tanganyika<br />

hawakufanya mitihani ya darasa la<br />

saba kutokana na miundombinu<br />

ya maeneo hayo kuwa mibovu<br />

na wakati mwingine kutokuwepo<br />

kabisa, miundombinu hiyo ni pamoja<br />

na ukosefu wa madaraja ambao<br />

uliwafanya wasimamizi wa mitihani<br />

hiyo kuogopa kuvuka ziwani kwa<br />

kutumia mitumbwi kuelekea katika<br />

vijiji hivyo kutokana na jografia ya<br />

maeneo hayo ilivyo.<br />

“Tatizo hili tumeliona hapa<br />

Rukwa kwa viijiji hivyo lakini Je hali<br />

ikoje kwa mikoa yote ya Tanzania, na<br />

ni vijijii vingapi vinakosa elimu nchini<br />

kila mwaka? Hii bado ni changamoto<br />

kubwa inayoikabili nchi yetu, hivyo<br />

mkulima mdogo bado hajafaidika na<br />

uhuru uliopo kwani yeye anaonekana<br />

kama vile si Mtanzania na wala hana<br />

haki yoyote,” anasema Bibi Ruliho<br />

ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti<br />

Mstaafu wa <strong>MVIWATA</strong>.<br />

Bibi. Kesia Laiser kutoka<br />

Monduli anasema kwamba pamoja na<br />

wao kuwa miongoni mwa Watanzania<br />

ambao wako huru, wakulima wadogo<br />

bado wanakabiliwa na changamoto<br />

zinazowakwamisha katika harakati<br />

zao za kujikomboa na umasikini na<br />

miongoni mwa changamoto hizo ni<br />

suala la gharama kubwa za pembejeo<br />

ambazo ni vigumu kwa mkulima<br />

mdogo kuzimudu.<br />

Bibi. Kesia Laiser<br />

Akizungumzia suala la elimu<br />

Bibi. Laiser amesema kuwa watoto<br />

wa wakulima ndio wanaosoma<br />

katika shule za kata ambazo bado<br />

ni duni kutokana na shule hizo<br />

kukosa walimu wa kutosha na zana<br />

za kufundishia ikiwemo vitabu na<br />

maabara. “Kinachotuumiza zaidi ni<br />

kuona watoto wa viongozi na matajiri<br />

hawasomeshwi katika shule hizi hali<br />

ambayo inawafanya wakulima wadogo<br />

wahisi kuwa bado wako katika utawala<br />

wa kikoloni kwani bado hawajafaidi<br />

matunda ya uhuru wa nchi hii”.<br />

Bibi. Fatuma Kimolo toka<br />

kijiji cha Gidoma, kata ya Galapo,<br />

Babati mkoa wa Manyara anasema<br />

Wakulima wadogo hawajapata bado<br />

matunda ya uhuru wa nchi hii kwa<br />

sababu linapokuja suala la uwekezaji<br />

wakulima wadogo hatushirikishwi<br />

na wawekezaji huongea na serikali<br />

kuu na kisha utekelezaji unafanyika<br />

ambapo mara nyingi wakulima<br />

wadogo huhamishwa bila ya kuwa na<br />

uhakika wa mahali wanapopelekwa.<br />

Kutoka Arusha Bibi. Ruth<br />

Paul anaeleza kwamba katika<br />

miaka 50 ya uhuru wakulima na<br />

wafugaji wanazidi kunyanyasika<br />

badala ya kusaidiwa, mifugo yao<br />

haina dhamana na hakuna masoko<br />

yanayoeleweka ya kuuzia mifugo<br />

hiyo jambo linalozidi kuzorotesha<br />

hali zao kiuchumi.<br />

Ameeleza kwamba ili wakulima<br />

wafaidi matunda ya uhuru ni<br />

lazima katiba ya nchi iwatambue<br />

na kuwalinda wakulima wadogo na<br />

maslahi yao ndipo hata wawekezaji<br />

watawaheshimu wakulima na wafugaji<br />

wadogo tofauti na sasa ambapo<br />

wanawaona kama vile manamba.<br />

Ameongeza kuwa wazawa<br />

wanaoishi jirani na hifadhi za taifa<br />

za wanyama hawafaidiki na raslimali<br />

hizo licha ya kuwalinda wanyama hao<br />

ambao huliingizia pato kubwa taifa.<br />

Bibi. Anna Mesoloi ni mfugaji<br />

kutoka Monduli na anaeleza kwamba<br />

wakulima wadogo hawajafaidi kitu<br />

chochote zaidi ya kusikiliza kauli<br />

mbiu mbalimbali zinazotangazwa<br />

kila siku kwenye vyombo vya habari<br />

ikiwemo hii ya Kilimo kwanza<br />

ambayo hawaielewi na hawafahamu<br />

inafanya nini licha ya kwamba wao<br />

ndio walengwa wakuu wa kauli hiyo.<br />

Amesema haya ni matokeo ya<br />

mfumo wa uongozi uliopo kuanzia<br />

ngazi za chini hadi za juu ambao siyo<br />

shirikishi. Kwa kipindi hiki anasema<br />

anachojivunia yeye ni kubahatika<br />

kuwa mwanachama wa <strong>MVIWATA</strong><br />

ambayo imemwezesha kupata elimu<br />

na mwanga wa kudai haki.<br />

Amesema hali ya upatikanaji<br />

wa mikopo ya elimu ya juu kwa<br />

mtoto wa mkulima ni tatizo kwani<br />

wengi wao huwa hawalewi nini cha<br />

kufanya ili waweze kupata nafasi<br />

hiyo ambayo kwao ni nafasi kubwa<br />

na ya kipekee ya kujiendeleza<br />

kielimu lakini cha kusikitisha ni<br />

kwamba wakati mwingine fomu<br />

zao huwa hazihangaikiwi kitendo<br />

kinachowafanya wazidi kurudi nyyma<br />

kielimu na kuachwa kimaendeleo.<br />

Bibi. Mwanaidi Ally kutoka<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 7<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11


Inatoka uk. wa 6<br />

wilaya ya Uyui mkoani Tabora<br />

aneleza kwamba katika kipindi hiki<br />

wakulima wadogo bado wana uhuru<br />

bandia unaowanufaisha wachache<br />

ambao hufaidi jasho la wakulima<br />

na kuwaacha wenyewe bila kitu.<br />

Amefafanua kwamba umasikini<br />

unaowakabili wakulima wengi ndiyo<br />

chanzo cha watoto wao kupata<br />

elimu duni na kukuza kundi la<br />

wajinga miongoni mwao.<br />

Bibi. Hidaya Chikawe kutoka<br />

Lindi anasema wakulima katika<br />

miaka hamsini iliyopita wamepata<br />

maendeleo kidogo ingawaje bado<br />

wanakabiliwa na changamoto<br />

mbalimbali katika shughuli yao<br />

ya kilimo. Changamoto kubwa<br />

inayowakabili wakulima ni ukiritimba<br />

wa baadhi ya viongozi katika vyama<br />

vya ushirika hasa vya zao la korosho<br />

huko kwao ambao hukwamisha<br />

maendeleo ya wakulima kwa sababu<br />

wao pia hufanya kazi zao kama<br />

madalali na hivyo kunufaika na jasho<br />

la wakulima badala ya kuwasaidia<br />

kuuza mazao yao kwa bei nzuri ili<br />

waweze kupata faida.<br />

Bw. Ponsian Ngaiza kutoka<br />

Kagera anasema katika kipindi<br />

cha miaka 50 ya Uhuru maisha ya<br />

wakulima wengi yamezidi kuwa duni<br />

kutokana na hali halisi ya uchumi<br />

ilivyo hivi sasa ambapo bidhaa nyingi<br />

zinapanda bei siku hadi siku huku<br />

uchumi wa wakulima wengi ukizidi<br />

kudorora kutokana na wao kukosa<br />

masoko ya uhakika ya mazao yao<br />

huku akitolea mfano wa bei ya kilo<br />

ya kahawa katika mkoa wa Kagera<br />

kuwa shilingi 1300 ukilinganisha na<br />

kilo moja ya sukari shilingi <strong>20</strong>00.<br />

“Katika miaka hii 50 wananchi<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />

wengi wa vijijini hawakupata fursa<br />

ya elimu kuhusu masuala mbalimbali<br />

yanayogusa maisha yao kila siku<br />

kama vile siasa, uchumi na hata haki<br />

zao, nashauri katika awamu ijayo<br />

mambo haya yapewe kipaumbele,”<br />

anasema Bw. Ngaiza ambaye pia ni<br />

Mwenyekiti wa <strong>MVIWATA</strong> Kagera.<br />

Bw. Paulo Mossama<br />

kutoka Tarime mkoani Mara<br />

anasema anachoweza kujivunia ni<br />

kwamba katika miaka 50 wakulima<br />

wamenufaika kwa kujifunza mambo<br />

mbalimbali kama vile kilimo cha<br />

kisasa lakini ni kwa asilimia ndogo<br />

sana ukilinganisha na idadi ya<br />

wakulima waliopo hapa nchini.<br />

Bw. Paul Mossama<br />

Bw. Andrew Chalangwa<br />

kutoka Kasulu, Kigoma anasema<br />

kuwa mkulima amenufaika kidogo<br />

sana kwani bado anatumia nyenzo<br />

duni ya jembe la mkono ilihali katika<br />

nchi nyingine wakulima wanatumia<br />

mitambo ya kisasa ya kilimo.<br />

Changamoto nyingine inayowakabili<br />

ni mabadiliko ya hali ya hewa<br />

ambayo katika miaka 50 ijayo serikali<br />

inapaswa kuweka mikakati madhubuti<br />

kukabiliana na mabadiliko hayo.<br />

Bibi. Deodata Katunga<br />

toka Ruvuma anasema “mkulima<br />

mdogo yuko katikati bado kwani<br />

MADA MAALUM<br />

hajapata faida ya kuridhisha ingawaje<br />

amefunguka macho tatizo kubwa ni<br />

watendaji na viongozi wa serikali<br />

wanaoshindwa kutimiza wajibu wao<br />

na kutaka kujinufaisha kwa jasho la<br />

wakulima.<br />

Bw. Hamad Abdalah<br />

Salimini toka Zanzibar anasema<br />

mkulima mdogo katika kipindi<br />

cha miaka 50 kwa kiasi amefaidika<br />

kwani kwa sasa ana sauti ya kusema<br />

matatizo yake kupitia vyombo kama<br />

<strong>MVIWATA</strong>, ingawa bado anakabiliwa<br />

na changamoto nyingi kama vile<br />

kutokushirikishwa katika vyombo<br />

vya maamuzi.<br />

Miongoni mwa maswali<br />

tuliyokuwa tukijadili kwenye makala<br />

hii ni Je ndani ya miaka 50 ya uhuru,<br />

wakulima wadogo wamefaidi<br />

matunda ya uhuru?<br />

Kimsingi kusema kwamba<br />

hakuna kilichofanyika katika miaka<br />

50 ya uhuru si sawa, kwa sababu<br />

yapo mengi ya maana yaliyofanyika.<br />

Itoshe tu kusema kwamba kwa<br />

yale tuliyopiga hatua tunashukuru<br />

tumefanikiwa kufika hapo. Lakini<br />

ziko changamoto kadhaa ambazo<br />

wadau wameziainisha ambazo<br />

zinadhihirisha ukweli kwamba<br />

hawajafaidi matunda.<br />

Kwa bahati mbaya sana<br />

tunapoadhimisha miaka 50 baada<br />

ya uhuru, taifa letu linashuhudia<br />

matumizi ya ujuzi na utaalamu wa<br />

baadhi ya viongozi na watendaji<br />

wenye tamaa, ulafi na ubinafsi<br />

vikitumika kuzidisha umaskini<br />

miongoni mwa jamii kubwa ya<br />

watanzania ambao ni wakulima.<br />

Katika awamu ya kwanza,<br />

Mwalimu Nyerere hakuishia<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 8<br />

Hawa ndiyo watoto wa wakulima ambao kwa miaka 50 ya uhuru bado wanasoma kwenye mazingira duni na ya dhiki kama ambavyo wengi<br />

wao wanaonekana hawana viatu, hivyo kuhatarisha afya zao<br />

7


MAKALA<br />

MAAZIMIO YA KONGAMANO<br />

Miaka 50 ya Uhuru: Nini Mstakabali<br />

Utangulizi<br />

Ili kuwawezesha wakulima<br />

kutafakari kwa pamoja mabadiliko<br />

katika shughuli za kilimo kwa<br />

kipindi cha miaka 50 tangu uhuru,<br />

<strong>MVIWATA</strong> iliandaa Kongamano<br />

lililowakusanya pamoja wajumbe<br />

zaidi ya <strong>17</strong>0 wakiwemo wakulima<br />

wadogo kutoka mikoa mbalimbali<br />

ya Tanzania, viongozi wa serikali na<br />

wakuu wa mikoa wastaafu, wataalam,<br />

wachambuzi wa sera na wanahabari.<br />

Kongamano hilo lilifanyika<br />

Disemba 6, <strong>20</strong>11 mjini Morogoro,<br />

likiwa na ujumbe usemao “Miaka<br />

50 ya Uhuru: Nini mstakabali wa<br />

wakulima wadogo?”<br />

Malengo ya Kongamano<br />

Malengo yalikuwa yafuatayo:<br />

· Kutafakari mabadiliko katika<br />

kipindi cha miaka 50 tangu<br />

Uhuru na Mustakabali wa<br />

mzalishaji mdogo.<br />

· Kuishauri serikali yetu njia<br />

ya kuendelea kiuchumi bila<br />

kuwasukuma kando wazalishaji<br />

wadogo.<br />

Akizungumza kwenye kongamano<br />

hilo Mkurugenzi Mtendaji wa<br />

<strong>MVIWATA</strong> Bw. Stephen Ruvuga,<br />

alisisitiza kuwa tunapoangalia<br />

mstakabali wa wakulima wadogo<br />

baada ya miaka 50 tusiangalie mbegu,<br />

pembejeo na soko la mazao ya kilimo<br />

tu , bali tuzungumzie mstakabali wa<br />

taifa ikiwemo upatikanaji wa elimu,<br />

huduma za afya, haki ya mkulima,<br />

umiliki wa ardhi pamoja na suala<br />

zima la ulinzi wa mkulima.<br />

Bw. Ruvuga alisema shuhuda<br />

zilizotolewa na washiriki wa kongamano<br />

zinadhihirisha kuwa mfumo wa serikali<br />

unaotumika hivi sasa kuhudumia jamii<br />

kiuchumi umefeli.<br />

Alisema “ni ajabu sana kuona<br />

kuwa ndio aina ya mfumo<br />

tunaoukimbilia, kuushangilia na<br />

kuupigia vigelegele, kwa mfano<br />

tunashangilia na kutunga nyimbo<br />

kuhusu Kilimo Kwanza, wakati ni<br />

mfumo ulioletwa kutubomoa sisi<br />

wakulima, tunashangilia kwa kutojua<br />

na ndiyo maana naunga mkono kauli<br />

ya Mzee Butiku kwamba ujinga ni<br />

8<br />

wa wakulima wadogo?<br />

adui yetu nambari moja.”<br />

Alisema ni wajibu wa wakulima<br />

kutumia fursa ya kusanyiko kama<br />

hilo kujifunza, kutafakari na kuchukua<br />

hatua na kuongeza kuwa <strong>MVIWATA</strong><br />

isingependa kuendelea kusikia<br />

wakulima wakisubiri ama kutegemea<br />

zaidi nguvu za nje kuliko kuthamini<br />

nguvu na uwezo walio nao wenyewe<br />

kwanza katika kupigania haki zao.<br />

Alisema kuwepo kwa watu<br />

mashuhuri kama mgeni rasmi Bw.<br />

Maoni ya wakulima...<br />

Inatoka uk. wa 7<br />

kukemea mataifa makubwa pekee<br />

yaliyotunyonya, bali alikemea pia<br />

viongozi wa ndani ya Tanganyika<br />

ambao nia zao binafsi zilikuwa<br />

zinakinzana na maendeleo ya nchi<br />

yetu. Mwalimu hakusita kuanika<br />

udhaifu, uchafu na tamaa za viongozi<br />

wasio waadilifu na akasisitiza kuwa<br />

watu hawa wasipewe uongozi.<br />

Mwalimu alipata kusema kwamba<br />

wasomi wachache waliobahatika<br />

kupata fursa hiyo kwa kutumia kodi<br />

za wananchi ni lazima wajue wana<br />

wajibu wa kwenda kuwatumikia<br />

wananchi kwa moyo.<br />

Mwalimu Nyerere pia alikuwa<br />

mtu wa mfano, alikuwa na shamba<br />

lake kule Butiama, shamba la<br />

Mwalimu lilikuwa mfano kwa<br />

wanakijiji wenzake, ukubwa wa<br />

shamba hili la mwalimu haukuwa<br />

nusu ya ardhi ya kijiji, bali alichukua<br />

sehemu kidogo ili kila mwanakijiji<br />

mwenye nia ya kufanya kilimo naye<br />

apate ardhi.<br />

Hapa utaona fahari ya Mwalimu<br />

Nyerere haikuwa kujilimbikizia<br />

mali, ndio maana uwepo wa<br />

Tanzania ulimhitaji sana Baba wa<br />

Taifa Mwalimu Nyerere.<br />

Kila tunapotazama tulipotoka,<br />

hasa baada ya miaka 50 ya uhuru wa<br />

Tanzania Bara, vema tukijua kuwa<br />

mambo yaliyofanywa na waasisi<br />

wa Taifa letu ni mfano hai wa hiki<br />

kinachotokea. Serikali imeshindwa<br />

kusimamia sheria zake ili wajanja<br />

wachache wasitumie maarifa<br />

Joseph Butiku kwenye kongamano<br />

hilo ni kudhihirisha ni jinsi gani<br />

wanawathamini na kuwaunga<br />

mkono wakulima wadogo na hivyo<br />

kuwataka wakulima kujiona kuwa<br />

hawako pekee bali kuna wasomi na<br />

viongozi wa kuwaunga mkono.<br />

Maazimio ya Kongamano<br />

Baada ya mawasilisho na majadiliano<br />

ya kina washiriki kwa kauli moja<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 19<br />

waliyoyapata kuihujumu serikali.<br />

Wataalamu hawa waliofaidi matunda<br />

ya uhuru kwa kusomeshwa, hivi sasa<br />

wanatumika kukandamiza uhuru wa<br />

watanzania wenzao.<br />

Swali linabakia, je baadhi ya<br />

viongozi tulionao ambao fahari<br />

yao ni kujilimbikizia ardhi na<br />

mali wanazowapora wakulima,<br />

wanawatumikia wananchi kwa<br />

moyo?<br />

Bw. Lohay Langay, mkulima<br />

wa Babati mkoani Manyara<br />

anasema “tunaadhimisha miaka<br />

hamsini ya uhuru wa Tanganyika,<br />

tukiwa na matatizo makubwa ya<br />

kiuchumi. Nchi ikiwa haina umeme<br />

wa uhakika, gharama za maisha<br />

zikipanda kila uchao, huku viongozi<br />

tulionao wakiwa wamefumba<br />

macho na masikio, kwa ufupi<br />

wananchi wametelekezwa.”<br />

“Tabia hii ya viongozi wetu<br />

kuishi maisha ya kifahari, bila kujali<br />

kuwa kuna watoto wa wapiga<br />

kura wao hawana madawati,<br />

wazazi wao wanaishi kwa mlo<br />

moja tu, wakulima hawana soko la<br />

mazao yao, wafugaji na wakulima<br />

wanauana kwa kugombea ardhi<br />

ya malisho inasikitisha mno. Binfsi<br />

niseme huku ambako viongozi<br />

wetu wanataka kutupeleka siko<br />

tulikokusudia kwenda, na hii<br />

itakuwa ni hatari tupu tunaifumbia<br />

macho, lakini naamini itatugharimu<br />

sana,” anaonya Bw Langay.<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11


Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />

MAKALA<br />

Wanawake wasifanywe wahanga<br />

wa kila tatizo kwenye jamii<br />

Na Gratian Cronery, MUCCoBS<br />

Shinyanga<br />

Asilimia 80 ya watanzania<br />

waishio vijijini, maisha yao<br />

hutegemea shughuli za<br />

kilimo, ufugaji, uvuvi na uwindaji.<br />

Shughuli hizo hufanywa kwa lengo<br />

la kupata pato la kujikimu kwenye<br />

kaya na kwa sehemu kidogo sana<br />

hutumika kwa biashara.<br />

Idadi kubwa ya kundi linalotekeleza<br />

shughuli hizo katika maeneo mengi<br />

ni la wanawake, ingawa mpaka sasa<br />

kundi hili halinufaiki na matokeo ya<br />

shughuli hizo.<br />

Hali hii ya kazi nyingi kuachwa<br />

mikononi mwa wanawake na<br />

manufaa yake kusimamiwa na<br />

wanaume, inatokana na mifumo<br />

iliyopo ambayo imejengwa miaka<br />

ya hivi karibuni licha ya kuwa kuna<br />

watu wanaodai kuwa chimbuko lake<br />

ni mila na desturi zilizorithiwa enzi<br />

za mababu.<br />

Hata hivyo, wanaojenga hoja<br />

kuwa utumikishwaji wa wanawake<br />

vijijini umerithiwa enzi za mababu<br />

wanashindwa kubainisha kuwa enzi<br />

hizo wanawake walifanya kazi zote<br />

za nyumbani na mashambani lakini<br />

wanaume nao walitimiza wajibu<br />

wa kulinda na kutunza familia kwa<br />

mahitaji yote tofauti na ilivyo sasa.<br />

Historia inatuelekeza kuwa babu<br />

zetu walikwenda porini kuwinda na<br />

kuwaletea bibi zetu vitoweo vya<br />

wanyamapori, lakini pia walihakikisha<br />

maghala yanahifadhi chakula cha<br />

kutosha na hifadhi hiyo inalindwa na<br />

kutumika kwa nidhamu.<br />

Bibi zetu majukumu yao yaliishia<br />

kwenye kuchota maji, kukusanya kuni<br />

(ambazo zilikuwa karibu) na kupika<br />

tu huku mahitaji mengine kama ya<br />

unga, mboga yakiwa yametekelezwa<br />

na wazee.<br />

Lakini leo ni wanaume wangapi<br />

wanaoshinda vilabuni na baadaye<br />

kurejea nyumbani kudai chakula<br />

na wanapokikosa wanawadhalilisha<br />

wanawake kwa matusi na vipigo?<br />

Ni wanaume wangapi wanaoshiriki<br />

kuwabaka watoto wa kike wengine<br />

wakiwa ni mabinti zao wa kuwazaa?<br />

Babu zetu hao ambao leo<br />

tunawasingizia kuwa walituachia<br />

mfumo kandamizi kwa wanawake,<br />

hawakuruhusu bibi zetu<br />

wadhalilishwe kwa vitendo vya<br />

ubakaji kama inavyotokea kwenye<br />

jamii yetu leo na yeyote aliyepatikana<br />

na kosa hilo aliadhibiwa vikali.<br />

Tunapoliangalia kundi hili la<br />

wanawake hivi sasa, jambo la<br />

kusikitisha ni kuona lilivyoachwa<br />

nyuma kimaendeleo na kwamba<br />

katika baadhi ya maeneo hata<br />

mchango wao wanaoutoa katika<br />

kuleta maendeleo, jamii haiutambui<br />

kutokana na mifumo mibovu iliyopo<br />

hasa ya kutothamini kazi zao.<br />

Mwanamke anachukuliwa kuwa<br />

ni mtu dhaifu wa kufikiri asiyeweza<br />

kutoa mchango makini hata wa<br />

mawazo katika shughuli yoyote<br />

ile ya maendeleo na kwamba yeye<br />

kazi yake ni kutekeleza tu masuala<br />

yaliyojadiliwa na kuamuliwa.<br />

Hali hiyo ya wanawake kupuuzwa<br />

iko kwenye kila sekta ikiwemo hii ya<br />

kilimo ambapo mwanamke hapewi<br />

fursa ya kutoa ushauri nini kilimwe,<br />

lini na kwa kiasi gani na hata mapato<br />

ya familia yanayotokana na kilimo<br />

matumizi yake yanaamuliwa na<br />

wanaume.<br />

Kutokana na kuwepo kwa<br />

ukandamizwaji huu mwanamke<br />

amejikuta akiwa ni mhanga kwenye<br />

familia na jamii inayoishi kijijini.<br />

Tunapoangalia matatizo kama<br />

ya njaa kwenye familia, anayeteseka<br />

zaidi ni mwanamke ambaye ni mlezi<br />

mkuu wa watoto. Matatizo mengine<br />

yanayoikabili jamii kama vile ukosefu<br />

wa huduma bora za afya, maji, nishati,<br />

elimu na miundombinu hususan<br />

ya barabara mwathirika mkuu ni<br />

mwanamke.<br />

Licha ya serikali kutangaza<br />

kuwa imeboresha huduma za afya<br />

vijijini, lakini bado tunasikia na<br />

kushuhudia matukio ya wajawazito<br />

wakisafirishwa kwenye mikokoteni<br />

ya ng’ombe na baiskeli na serikali<br />

nayo kwa kuwapuuza ikawaletea<br />

usafiri wa bajaji.<br />

Suala la uhaba wa pembejeo za<br />

kilimo, kadhalika nalo ni mzigo kwa<br />

wazalishaji hawa ambao ni wanawake<br />

na wengi wao wanashindwa kumudu<br />

gharama za nyongeza ili waweze<br />

kupata pembejeo hizo.<br />

Hata hivyo, kwa upande mwingine<br />

zipo taasisi na mashirika ambayo<br />

kwa kutambua nafasi ya mwanamke<br />

kwenye jamii yameanza kampeni<br />

kuielimisha jamii, juu ya umuhimu<br />

wa makundi yote kwenye jamii<br />

kushirikiana na kuthaminiana.<br />

Jamii nyingi vijijini zimewaachia wanawake kazi za kulima,kuhudumia mifugo, watoto, kupika,<br />

kuchota maji, kukusanya kuni (ambazo zinapatikana umbali mrefu), afya zao kudhoofu.<br />

9


MAKALA<br />

Kilimo kina nafasi ya kimkakati<br />

ya kukuza uchumi<br />

Na Susuma Susuma<br />

Miaka hamsini ni kipindi<br />

kirefu kwa hali na<br />

mazingira yoyote yale<br />

hasa tunapoihusisha na maendeleo<br />

ya binadamu, jamii viumbe au<br />

jambo lolote lile linaloendelea<br />

kuendana na wakati.<br />

Mwaka huu wa <strong>20</strong>11<br />

tunaposherehekea na kufurahia<br />

kufikia miongo mitano tangu taifa letu<br />

la Tanzania Bara lijipatie Uhuru wake<br />

kutoka kwa wakoloni wa Kiingereza<br />

mwaka 1961, tuna kila sababu ya<br />

kujipima katika nyanja tofauti hasa<br />

zile zinazohusisha maendeleo ya<br />

kiuchumi, kijamii na kisiasa kwa<br />

taifa letu. Yatupasa kujiuliza na<br />

kujitathmini wapi tumetoka, wapi<br />

tulipo na ni wapi tunaelekea.<br />

Kwa<br />

wastani wakulima bado<br />

wanalima vishamba vidogo vidogo, pia<br />

bado wakulima wetu wanatumia zana duni<br />

za jadi kama vile jembe la mkono.<br />

Msingi mkubwa k a t i k a<br />

hili ni kuyaangalia mafanikio<br />

yetu katika harakati za kujiletea<br />

maendeleo tangu tumepata Uhuru<br />

na kuweza kuwa na sababu nzuri ya<br />

kujipongeza kwa hilo. Halikadhalika<br />

ili tuzitendee haki dhamira zetu ni<br />

vyema tukaziangalia changamoto<br />

zilizotukwaza katika kipindi chote<br />

hiki cha miaka hamsini ya Uhuru,<br />

ili basi, tuweze kupangilia mikakati<br />

ya kukabiliana na changamoto hizo<br />

na kuzifanya kuwa ndio sehemu ya<br />

chachu ya kutuletea mafanikio kwa<br />

ukubwa na kiwango cha hali ya juu<br />

zaidi kwa kipindi kijacho cha miaka<br />

hamsini.<br />

Kilimo ndio msingi wa uchumi<br />

wetu na kina nafasi ya kimkakati<br />

katika kuboresha uchumi wa<br />

Tanzania. Sekta ya kilimo ndiyo<br />

10<br />

inayotegemewa na asilimia kubwa<br />

ya Watanzania katika harakati za<br />

kujiletea maendeleo ya kiuchumi na<br />

kijamii na kwa maendeleo ya taifa<br />

letu. Kwa maana hiyo kilimo ndiyo<br />

mhimili wa maisha ya watanzania<br />

wengi.<br />

Lakini kilimo cha Tanzania ndani<br />

ya miaka 50 ya uhuru bado ni duni<br />

na wakulima wenyewe wamesongwa<br />

na matatizo mengi. Walio wengi<br />

hawazijui na hawazitekelezi Kanuni za<br />

Kilimo Bora kwa mazao wanayolima,<br />

hivyo kilimo chao hakina tija na<br />

mavuno yao ni kidogo. Kwa wastani<br />

wakulima bado wanalima vishamba<br />

vidogo vidogo, pia bado wakulima<br />

wetu wanatumia zana duni za jadi<br />

kama vile jembe la mkono. Hapa<br />

mwelekeo chanya ni kwamba kilimo<br />

cha kisasa kinapaswa kuwa sharti<br />

muhimu katika kuchangia ujenzi wa<br />

uchumi wa kisasa.<br />

Heshima ya mkulima/mfugaji<br />

mdogo<br />

Toka wakati wa uhuru<br />

hadi miaka ya 70 na 80<br />

mwanzoni, wakulima<br />

wadogo walikuwa<br />

wanaheshimiwa na kazi yao<br />

ilikuwa inathaminiwa na makundi<br />

mbalimbali katika jamii. Hata wasanii<br />

wa muziki walitunga na kuimba<br />

nyimbo mbalimbali zilizowasifu,<br />

kuwapongeza na kuwatia moyo<br />

wakulima wadogo ili waweze<br />

kuendelea na kazi ya kulisha taifa na<br />

kuongeza pato la taifa kupitia katika<br />

kilimo.<br />

Kwa sasa hali imebadilika<br />

kabisa, miaka hamsini ya uhuru<br />

tunashuhudia kilimo kinaonekana<br />

kama mbadala wa mwisho. Mambo<br />

yote yakikushinda unaenda kwenye<br />

kilimo na ukimaliza muda wako wa<br />

kutumikia taifa kwa njia ya ajira rasmi<br />

ndipo unarudi katika kilimo ukafie<br />

huko. Ingawa kauli mbiu ya Kilimo<br />

ni Uti wa Mgongo bado inatumika<br />

sana na makundi mbalimbali katika<br />

jamii yetu, lakini uhalisia ni kwamba<br />

kilimo kinaonekana kuwa ni mateso<br />

au adhabu au shughuli isiyokuwa na<br />

heshima mbele ya jamii. Ni jambo<br />

la kawaida kusikia mtu akisema:<br />

‘Kama mjini pamekushinda rudi kijijini<br />

ukalime’; ‘Kama sanaa imekushinda,<br />

nenda ukalime’; Kama huwezi siasa<br />

nenda kalime’; sio lazima kuwa na<br />

digrii, ukiona unashindwa, rudi kijijini<br />

ukawasaidie wazazi kulima’.<br />

Kejeli hizi zinachangia vijana<br />

wetu wengi kukimbia kilimo na<br />

kwenda mjini kwani kuwa mkulima<br />

ni aibu mbele za watu. Hata<br />

mkulima akivaaa vizuri, akinawiri<br />

au akitoa maoni yake ya maana,<br />

utasikia minong’ono inayoonesha<br />

mashaka kama hayo ni mawazo ya<br />

mkulima. Hapo ndipo wakulima<br />

wadogo wanajiuliza, hivi kweli sifa<br />

zetu ni kuwa mchafu, mchovu, mtu<br />

asiyeweza kutoa mawazo na maoni<br />

ya maana mbele ya jamii au asiye na<br />

mbele wala nyuma?<br />

Kwa ujumla unaweza kuipa<br />

tafsiri Sekta ya Kilimo kwa semi<br />

mbalimbali, mojawapo ikiwa ni<br />

‘sekta iliyotelekezwa ama sekta ya<br />

watu wanaoganga maisha.’ Hata<br />

hivyo, upana na unyeti wa shughuli<br />

zinazofanywa na Sekta ya kilimo ndio<br />

kigezo dhahiri kinachoipa umuhimu<br />

kuweza kuingizwa katika mchakato<br />

huu wa kujitathmini na kuelezea<br />

mafanikio yake katika mwaka huu<br />

<strong>20</strong>11.<br />

Watanzania tunapoadhimisha<br />

na kusherehekea kwa shangwe na<br />

nderemo kutimiza miaka hamsini ya<br />

Uhuru, tunapaswa kujiuliza je, kilimo<br />

ambacho kinaelezwa kuwa kinatoa<br />

mchango mkubwa katika pato la<br />

taifa, kinatoa tafsiri ama mchango<br />

gani wa maendeleo ya mkulima<br />

mmoja mmoja?<br />

Ni ukweli ulio wazi kuwa<br />

wakulima wadogo ni wachangiaji<br />

wakubwa katika pato na maendeleo<br />

ya taifa, ingawa wao wenyewe<br />

hawanufaiki na pato hilo.<br />

Kodi zinazotozwa na<br />

kukusanywa na serikali kwa njia<br />

mbalimbali zinalipwa na kundi<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 11<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11


Inatoka uk. wa 10<br />

kubwa la wale walio katika Sekta ya<br />

Kilimo (wakulima ama wazalishaji<br />

wadogo). Hawa ndiyo tunaambiwa<br />

wanachangia pato la taifa kwa kuwa<br />

shughuli zao kuu ni kilimo. Wanalipa<br />

kodi hizo ama kupitia shughuli<br />

zao za uzalishaji na biashara, ama<br />

kupitia bidhaa wanazonunua kama<br />

vile mafuta ya taa, sukari na nguo.<br />

Lakini hoja inayoweza kuibuka hapa<br />

Hifadhi<br />

ya chakula ni eneo ambalo<br />

linapaswa kuchukuliwa kwa uzito ili<br />

mazao yasiendelee kupungua bali Tanzania<br />

igeuke kuwa ghala ya chakula katika kanda<br />

huu wa Afrika Mashariki.<br />

ni je, kodi<br />

hizo zimetumikaje kusaidia kutatua<br />

kero na matatizo mengi yanayogusa<br />

maisha yao ya kila siku?<br />

Zipo changamoto nyingi<br />

zinazowakabili wakulima nchini<br />

kwetu hivi sasa ambazo zingeweza<br />

kutatuliwa kwa kodi wanazolipa na<br />

nyingine zingetatuliwa na uwepo<br />

wa sera zinazomwezesha mkulima<br />

kupiga hatua za maendeleo.<br />

Kwa mfano changamoto za<br />

masoko na bei nzuri ya mazao ni<br />

suala la kisera, changamoto ya mitaji<br />

inaweza tatuliwa na sera nzuri na<br />

changamoto ya matumizi ya zana<br />

duni, ubaha wa pembejeo na umiliki<br />

wa ardhi ni masuala ya kimkakati<br />

ambayo kama juhudi za makusudi<br />

zikichukuliwa na kutekelezwa kwa<br />

ushirikiano thabiti kati Serikali na<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />

Sekta Binafsi, shughuli ya kilimo<br />

itawanufaisha wakulima na wao<br />

kuona wanafaidi matunda ya uhuru<br />

sawa na wazalishaji kwenye sekta<br />

nyingine. Tukifanya hivi tutaifanya<br />

nchi yetu kufikia mafanikio ya<br />

nchi kama vile Malaysia, Indonesia,<br />

Singapore na Vietnam ambazo katika<br />

miaka ya mwanzo wa sitini sekta za<br />

kilimo zilikuwa katika viwango sawa<br />

na nchi yetu.<br />

Jambo jingine tunalopaswa<br />

kulitumia vyema ni<br />

kiwango kikubwa cha<br />

rasilimali ambazo<br />

Mungu ameijalia<br />

ardhi yetu ya<br />

Tanzania iliyojaa<br />

rutuba na hali ya<br />

hewa inayoruhusu<br />

mazao aina mbalimbali<br />

kustawi, jambo la msingi ni<br />

kuwa na utashi wa kisiasa.<br />

Juhudi kubwa inabidi zielekezwe<br />

kwenye Kilimo cha Kibiashara na<br />

hapa ushirikiano wa serikali na sekta<br />

binafsi ndio utakaofanikisha azma hii.<br />

Mbali na kuongeza wigo katika sekta<br />

ya kilimo, mkazo inabidi uwekwe<br />

kwenye uongezaji thamani kwa<br />

kutilia mkazo usindikaji wa mazao.<br />

Hifadhi ya chakula ni eneo ambalo<br />

linapaswa kuchukuliwa kwa uzito<br />

ili mazao yasiendelee kupungua<br />

bali Tanzania igeuke kuwa ghala ya<br />

chakula katika kanda huu wa Afrika<br />

Mashariki.<br />

Taarifa za ushindani katika uchumi<br />

wa soko huria na urahisi wa kufanya<br />

biashara zinahitajika ili kuchochea<br />

juhudi za kujikwamua kiuchumi.<br />

Vyombo husika vinapaswa kutoa<br />

uwanja sawa na mazingira wezeshi<br />

Kilimo ni Uti wa Mgongo?<br />

MAKALA<br />

kwa wadau wote. Haipendezi<br />

kuendelea kuwabagua wakulima<br />

kwa kuwazuia kuuza mazao huku<br />

nchi ikinadi sera za soko huria.<br />

Mafanikio makubwa ya maendeleo<br />

katika sekta zote yanategemea<br />

sana uwekezaji katika sayansi na<br />

teknolojia. Matumizi ya teknolojia ya<br />

habari (ICT) yatasaidia sana harakati<br />

za biashara ya ushindani, kwa hiyo<br />

uwekezaji katika eneo hili upewe<br />

kipaumbele. Teknolojia hii ya habari<br />

hivi sasa imeonyesha mafanikio<br />

kwenye baadhi ya maeneo, mfano<br />

dhahiri ukiwa ni Mfumo wa Taarifa za<br />

Masoko (MAMIS) unaotekelezwa na<br />

<strong>MVIWATA</strong>, ambao umepongezwa<br />

na wadau wengi kwamba umesaidia<br />

kuimarisha biashara ya mazao.<br />

Kero kubwa katika utendaji wa<br />

biashara ni miundombinu mibovu<br />

hususan barabara ambazo ni<br />

vyema zikaboreshwa ili kurahisisha<br />

usafirishaji wa mazao toka vijijini<br />

ambako ndipo uzalishaji unapofanyika<br />

hadi maeneo ya masoko ya walaji<br />

ambao mara zote ni wakazi wa<br />

mijini.<br />

Tuimarishe na kuwa na mfumo<br />

wa uhakika wa upatikanaji wa<br />

mbegu bora na mbolea na kueneza<br />

matumizi yake kwa wakulima wengi<br />

zaidi.<br />

Uwezeshwaji wa wananchi kwa<br />

ujumla ni jukumu ambalo serikali<br />

inapaswa kulitekeleza kwa dhati. Sera<br />

hii imebuniwa ili kuwapa mamilioni<br />

ya Watanzania fursa ya kujikwamua<br />

kiuchumi. Kilimo kina nafasi ya<br />

kimkakati ya kukuza uchumi, ikiwa<br />

juhudi zaidi zitawekwa kwenye<br />

kupanua uwigo wa utekelezaji wa<br />

mipango inayowekwa.<br />

11


KAMERA<br />

12<br />

KAMERA YA <strong>MVIWATA</strong> MITANDAONI<br />

Wana-<strong>MVIWATA</strong> Zanzibar walioshiriki mkutano mkuu oktoba <strong>20</strong>11<br />

mjini Morogoro<br />

Wana-<strong>MVIWATA</strong> Chunya wakiwa katika ziara ya mafunzo kwa<br />

wakulima wenzao wa wilaya ya Mkuranga Pwani<br />

Bw. Hasira Zahoro Mwezeshaji wa <strong>MVIWATA</strong> akizungumza na wadau<br />

wa soko la Matai Sumbawanga Vijijini, linalojengwa na <strong>MVIWATA</strong><br />

Wana-<strong>MVIWATA</strong> Mara walioshiriki mkutano mkuu Oktoba <strong>20</strong>11<br />

Viongozi wa <strong>MVIWATA</strong> Shinyanga kutoka kulia ni Bw. Masumbuko<br />

Bunzali (Mwenyekiti <strong>MVIWATA</strong> Bariadi), Bw. Charles Ndugulile<br />

(Mwenyekiti Mkoa) Bibi. Justa Charles (Mjumbe kamati ya uongozi<br />

<strong>MVIWATA</strong> Kahama), Bw. Goma Boya (Katibu <strong>MVIWATA</strong> Shinyanga<br />

Vijijini) na Bw. Yusuph Mboje (Katibu <strong>MVIWATA</strong> Kishapu) wakiwa<br />

wameshika majarida ya Pambazuko baada ya kuyapokea kupitia<br />

mfumo wa malipo kabla.<br />

Bibi Atufuage Mgimba mkulima toka kikundi cha Amani, kijiji cha<br />

Mapogoro kata ya Milo wilayani Ludewa, akizungumza kwenye<br />

mafunzo ya uimarishaji vikundi, yaliyofanyika Mlangali<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11


KAMERA YA <strong>MVIWATA</strong> MITANDAONI<br />

Picha ya pamoja ya wakazi wa kijiji cha Itwangi Shinyanga Vijijini, baada<br />

ya kikao cha ufuatiliaji wa Mradi wa Chukua Hatua unaotekelezwa na<br />

<strong>MVIWATA</strong> kwa ushirikiano na shirika la Oxfam.<br />

Mwenyekiti wa Mfuko wa Mwalimu Nyerere Mzee Joseph Butiku<br />

akisisitiza jambo kwenye Kongamano la <strong>MVIWATA</strong> la Kuadhimisha<br />

Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Disemba 6, <strong>20</strong>11 Morogoro mjini<br />

Picha ya pamoja ya washiriki wa Kongamano la <strong>MVIWATA</strong> la Miaka<br />

50 ya Uhuru lililofanyika Morogoro Disemba 6, <strong>20</strong>11<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />

KAMERA<br />

Picha ya pamoja ya wana-<strong>MVIWATA</strong> Shinyanga Vijijini na waheshimiwa<br />

madiwani wa halsmahauri ya wilaya hiyo, baadaya kikao chenye lengo<br />

la kuimarisha mahusiano<br />

Washiriki wa Kongamano la miaka 50 wakimsikiliza mgeni rasmi<br />

Mzee Joseph Butiku anayeonekana picha ya kushoto<br />

Bw.Anno Lwilo mkulima wa kijiji cha Mangalanyene wilaya ya Ludewa<br />

mkoa wa Njombe akichangia mada kwenye Kongamano la <strong>MVIWATA</strong><br />

la miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania<br />

13


KUTOKA MITANDAONI<br />

WARSHA YA KITAIFA<br />

Soko la uhakika kichocheo cha uzalishaji<br />

kwa wakulima Tanzania<br />

Na Jacueline Massawe, Morogoro<br />

<strong>Uk</strong>osefu wa soko la uhakika<br />

kwa mazao ya wakulima<br />

ni miongoni mwa<br />

changamoto zinazomkwamisha<br />

mkulima mdogo kunufaika na<br />

shughuli hiyo ya kilimo na hivyo<br />

kuendelea kuwa masikini.<br />

Kwa kuiona changamoto hiyo,<br />

<strong>MVIWATA</strong> ambayo ni chombo<br />

kinachowaunganisha wakulima<br />

wadogo iliandaa warsha ya kitaifa<br />

iliyowakutanisha wakulima zaidi<br />

250 kutoka mikoa yote ya Tanzania<br />

bara na Visiwani. Warsha hiyo pia<br />

ilihudhuriwa na viongozi wa serikali<br />

na wataalamu kutoka taasisi za<br />

kiserikali na zisizo za kiserikali,<br />

wasomi na wachambuzi wa masuala<br />

ya sera na siasa nchini.<br />

Lengo la warsha hiyo ya siku<br />

moja, ambayo ilibeba maudhui<br />

yasemayo, Soko la Uhakika Kichocheo<br />

cha Uzalishaji! lilikuwa ni kuwapa<br />

fursa wadau wa kilimo kujadili na<br />

kuzitafutia ufumbuzi changamoto za<br />

masoko ya mazao ya wakulima.<br />

Warsha hiyo ilifanyika Oktoba<br />

14<br />

24, <strong>20</strong>11 katika ukumbi wa Kituo<br />

cha Mafunzo ya Wanawake CCT cha<br />

Mjini Morogoro ikiwa ni utangulizi<br />

wa Mkutano Mkuu wa 16 wa shirika<br />

la <strong>MVIWATA</strong> uliofanyika Oktoba 25,<br />

<strong>20</strong>11.<br />

Warsha hiyo ilifunguliwa na<br />

Mkuu wa Mkoa Mstaafu Bw. Stephen<br />

Mashishanga, ambaye katika hotuba<br />

yake, alipongeza utaratibu shirikishi<br />

unaotumiwa na <strong>MVIWATA</strong> kwa<br />

kuwashirikisha wakulima kuibua<br />

kero kwa kuwakutanisha na wadau<br />

mbalimbali na kuhimiza utaratibu<br />

huo uimarishwe kwenye ngazi zote<br />

na siyo ngazi ya taifa tu.<br />

Bw. Mashishanga aliwataka<br />

wakulima kuungana kwa pamoja kwa<br />

kupaza sauti za kukataa makandamizo<br />

na manyanyaso wanayofanyiwa<br />

na serikali na wahisani mbalimbali<br />

wasio na mapenzi mema.<br />

“Ni vizuri wakulima tukahakikisha<br />

kuwa tunajitetea mwenyewe kwa<br />

umoja na nguvu zote badala ya<br />

kutegemea kutetewa na mashirika<br />

yanayokuja kwa mgongo wa<br />

uwekezaji kwa maslahi ya nchi zao,<br />

ama serikali ambayo haituungu<br />

mkono,” alisema Bw. Mashishanga<br />

Washiriki wa warsha ya kitaifa ya <strong>MVIWATA</strong> <strong>20</strong>11<br />

Aidha alihimiza vyama vya<br />

wakulima vijenge mahusiano<br />

imara na halmashauri za wilaya<br />

katika kutekeleza majukumu yake<br />

na kuongeza kuwa kwa kufanya<br />

kazi pamoja wataweza kutatua<br />

changamoto za masoko na<br />

nyinginezo ambazo ni kero kwa<br />

wakulima.<br />

Aliitaka serikali iache kuwapuuza<br />

wakulima na badala yake isikilize<br />

kilio chao na kuzitafutia ufumbuzi<br />

changamoto zinazowakabili.<br />

Kwa upande wake Mwenyekiti<br />

wa <strong>MVIWATA</strong> Taifa aliyemalizamuda<br />

wake Bw. Yazid Makame alisema kuwa<br />

wakulima bado wanakabiliwa na<br />

changamoto nyingi hasa za masoko,<br />

ambazo zinapaswa kutatuliwa ili<br />

kuwezesha maendeleo ya haraka<br />

kwa wakulima wadogo nchini.<br />

Kwa upande wake Mkurugenzi<br />

Mtendaji wa <strong>MVIWATA</strong> Bw. Stephen<br />

Ruvuga alisema tatizo la vikwazo<br />

vya kibiashara kwa wakulima<br />

wadogo limekuwa likiwakatisha<br />

tama na matokeo yake yamekuwa ni<br />

uzalishaji mdogo na duni.<br />

“Wakulima wadogo wakiwa<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 15<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11


Inatoka uk. wa 14<br />

na uhakika wa soko itakuwa ni<br />

motisha kwao klima kwa bidii na<br />

kibishara zaidi. Wakulima wadogo<br />

wakiuza, mapato yao yanarudi tena<br />

mashambani kuimarisha kilimo na<br />

kuongeza uzaishaji. Wakizalisha bila<br />

soko wanakata tamaa ya kuzalisha,”<br />

alisema Bw. Ruvuga.<br />

Akitoa maoni yake juu ya mpango<br />

huo wa uwekezaji, Bw. Ruvuga,<br />

alitahadharisha kuwa kitendo cha<br />

kuwabagua wakulima wadogo katika<br />

umilikaji wa ardhi kinaweza kujenga<br />

tabaka la chuki na kuibua migogoro<br />

ya ardhi isiyokoma.<br />

“Tumeshuhudia nchi nyingine<br />

wakulima waliondolewa katika ardhi<br />

yao kimabavu, baadaye wameungana<br />

na kuifatuta haki yao kwa nguvu”<br />

alisema Bw. Ruvuga.<br />

Bw. Ruvuga alisema, nchi lazima<br />

ihakikishe kunakuwa na usalama<br />

wa chakula kwa tahadhari kwani<br />

wawekezaji wanaweza kuzalisha<br />

mazao ya chakula kwa soko la nje<br />

na kuiacha nchi bila chakula na pia<br />

kushindwa kununua mazao hayo<br />

kwa kuwa mengi yanauzwa kwa bei<br />

kubwa.<br />

Alishauri kuwa ni vyema serikali<br />

ikawekeza zaidi kwa wazalishaji<br />

wadogo kwa kuwajengea uwezo ili<br />

waendelee kulisha Taifa bila kuwa<br />

na kikwazo chochote cha kuingiliwa<br />

katika ardhi yao.<br />

Michango iliyotolewa na<br />

wakulima walioshiriki warsha hiyo,<br />

kwa sehemu kubwa ilionyesha<br />

mashaka makubwa juu ya mkakati<br />

huo wa serikali wa kuwafanya<br />

wakulima kulima kibiashara kutokana<br />

na kero nyingi huku wakitolea<br />

mfano wa kero wanayokumbana<br />

nayo mipakani wanapotaka kuvusha<br />

mazao kwenda nchi jirani na kuitaka<br />

Jumuiya ya Afrika Mashariki kuingilia<br />

kati suala hilo.<br />

“Tunahamasishwa kulima<br />

kibiashara kwa sababu ya soko<br />

huria na soko la pamoja la Afrika<br />

Mashariki, lakini tunapofika mipakani<br />

tunakumbana na vizuizi na kwa kweli<br />

tunanyanyasika mno, tunadaiwa<br />

malipo ambayo hayapo kisheria,”<br />

alisema Bibi Fatuma Kimolo Makamu<br />

Mwenyekiti wa <strong>MVIWATA</strong> Manyara.<br />

Bibi. Kimolo alisema wanasikia<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />

nchi hizo zimesaini Makubaliano ya<br />

Soko la Pamoja la Kibiashara, lakini<br />

akashangazwa na vikwazo hivyo<br />

kuendelea kuwepo.<br />

Mkulima mwingine Bw. Joseph<br />

Mshangama kutoka mkoani Tanga<br />

mbali na kutaka kuondolewa kwa<br />

vikwazo vya kuuza mazao nje ya nchi,<br />

alisema wakulima bado wanahitaji<br />

kuelimishwa vya kutosha kuhusiana<br />

makubaliano ya Soko la Pamoja ili<br />

kuondoa mkanganyiko unaojitokeza<br />

hivi sasa.<br />

Bw. Joseph Mshangama<br />

Bw. Hamad Salmin, mkulima<br />

kutoka Zanzibar alisema<br />

changamoto kubwa inayowakabili<br />

wakulima visiwani humo ni suala<br />

la usindikaji. Alisema wakulima<br />

wengi wanazalisha mbogamboga<br />

na matunda, lakini hawana vifaa<br />

vya kuhifadhi na usindikaji na hivyo<br />

wakulima kulazimika kuuza mazao<br />

kwa bei ndogo kwa madalali.<br />

Wakulima hao walisema licha<br />

ya kuwawekea masharti ya kuuza<br />

mazao yao nje ya nchi kwenye bei<br />

nzuri, serikali hiyo hiyo imekuwa<br />

ikishirikiana na wawekezaji kuwapora<br />

wakulima ardhi.<br />

Bw.Levi Mlengule kutoka wilaya<br />

ya Mufindi alisema katika eneo lake<br />

wawekezaji wanafaidi misitu kuliko<br />

ilivyo kwa wenyeji. Alisema wakulima<br />

wamenyimwa fursa ya kuvuna misitu<br />

hiyo ambayo wao ndiyo watunzaji<br />

wakuu.<br />

Bw. Ahmedi Simba mkulima toka<br />

wilaya ya Kigoma alilalamikia Serikali<br />

wilayani humo kwa kuchukua ardhi<br />

kubwa na kuwapa wawekezaji<br />

na kushindwa kutoa ardhi hiyo<br />

hiyo kwa makundi madogo ya<br />

wakulima ambao kwa muda mrefu<br />

wamewasilisha maombi ya ardhi<br />

hiyo.<br />

“Nahofia tutaishia kuwa<br />

manamba katika mashamba<br />

KUTOKA MITANDAONI<br />

makubwa, tunajiuliza kwa nini<br />

Serikali inawapendelea wawekezaji<br />

wageni na kuwaacha wazawa?”<br />

alihoji kwa uchungu Bw. Simba.<br />

Afrika Mashariki watakiwa<br />

kutekeleza soko huria kwa<br />

vitendo<br />

Mkurugenzi Msaidizi katikaWizara<br />

ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki<br />

anayeshughulikia kitengo cha<br />

Uzalishaji Dkt. Abdullah Makame,<br />

akiwasilisha mada kwenye warsha<br />

hiyo alisema Jumuiya ya nchi za<br />

Afrika Mashariki inatakiwa kuchukua<br />

hatua za makusudi za kuwasaidia<br />

wakulima kunufaika na kilimo kwa<br />

kuwaondolea vizuizi vya kusafirisha<br />

mazao mpakani na vikwazo<br />

vinginevyo kwenye soko la mazao.<br />

Dkt. Makame ambaye mada<br />

yake ilizungumzia Fursa na Vikwazo<br />

katika Biashara ya Mazao ndani ya<br />

Jumuiya ya Afrika Mashariki, alisema<br />

vizuizi hivyo ni moja ya sababu<br />

zinazochangia kudumaza uchumi wa<br />

nchi hizo ambazo asilimia kubwa ya<br />

wananchi wake wanajishughulisha<br />

na kilimo. Jumuiya ya Afrika<br />

Mashariki inaundwa na nchi tano za<br />

Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na<br />

Tanzania.<br />

Akizungumzia maendeleo ya<br />

sekta ya kilimo nchini, Dkt Makame<br />

alisema tatizo kubwa linaloikabili<br />

nchi yetu ni miundombinu mibovu<br />

ambapo asilimia 80 ya usafirishaji<br />

wa mizigo ikiwemo mazao ya kilimo,<br />

inategemea barabara, ilihali katika<br />

nchi zilizoendelea bidhaa nyingi<br />

zinasafirishwa kwa reli, meli na<br />

ndege na hivyo kufikisha mapema<br />

sokoni bidhaa zikiwa na ubora na<br />

thamani inayokidhi soko.<br />

Alisema tatizo jingine<br />

linalowakabili wazalishaji wadogo<br />

nchini ni kukosa umiliki wa ardhi<br />

jambo ambalo alisema serikali<br />

inapaswa kulipa kipaumbele ili<br />

kuchochea uzalishaji na maendeleo<br />

ya kiuchumi kwa ujumla hasa wakati<br />

huu tunapozungumzia kuwa na<br />

shirikisho la Afrika Mashariki.<br />

Aliitaka serikali kuangalia upya<br />

iwapo sera zinazotungwa na zilizopo<br />

kama zinakidhi mahitaji ya kumsaidia<br />

mzalishaji kujiletea maendeleo<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 16<br />

15


KUTOKA MITANDAONI<br />

Inatoka uk. wa 15<br />

badala ya kumkandamiza.<br />

Akiwasilisha uzoefu wa <strong>MVIWATA</strong><br />

kuhusu Ubia wa vyama vya<br />

wakulima na Halmashauri za<br />

wilaya katika uendeshaji wa<br />

masoko, Mratibu wa Kitengo cha<br />

Masoko Bw. Nickson Elly <strong>MVIWATA</strong><br />

mpaka sasa imefanikiwa kujenga<br />

masoko tisa ya mazao ya wakulima<br />

vijijini.<br />

Alisema masoko hayo yako<br />

kwenye vijiji vya Kibaigwa<br />

Kongwa, Nyandira Mvomero,<br />

Tandai na Tawa Morogoro Vijijini,<br />

Mkata Handeni,Igagala Njombe,<br />

Igurusi Mbarali, Matai na Kasanga<br />

Sumbawanga Vijijini.<br />

Alisema masoko hayo<br />

kwa kawaida huendeshwa na<br />

kusimamiwa na bodi za masoko<br />

ambazo mundo wake unajumuisha<br />

uwakilishi wa wadau mbalimbali<br />

wa soko wakiwemo wawakilishi wa<br />

halmashauri za wilaya.<br />

Hata hivyo katika siku za hivi<br />

karibuni uendeshaji wa masoko<br />

hayo umekuwa na changamoto<br />

nyingi ikiwemo kiwango kikubwa<br />

cha ushuru ambao halmashauri<br />

za wilaya zinalazimisha kulipwa,<br />

ambazo hakilingani na makusanyo<br />

halisi ya ushuru wa sokoni kwa<br />

mwezi. Aliongeza kuwa hali hiyo<br />

inahatarisha uendelevu wa masoko<br />

hayo ambayo yamechangia kwa<br />

kiwango kikubwa ukuaji wa uchumi<br />

wa wakulima wa maeneo husika.<br />

Bw. Elly alisema hali hiyo ni<br />

mojawapo ya sababu zilizoisukuma<br />

<strong>MVIWATA</strong> kandaa warsha hiyo ili<br />

kupata fursa ya kujadiliana na wadau<br />

mbalimbali wanahusika kwenye<br />

mfumo wa masoko ya mazao ya<br />

wakulima. kiwangoambah<br />

Umiliki wa ardhi<br />

Akiwasilisha mada kuhusu Nafasi<br />

ya Wazalishaji Wadogo kwenye<br />

mchakato wa kuandikwa Katiba<br />

Mpya, Mhadhiri Msaidizi Kitivo cha<br />

Sayansi ya Siasa ya Jamii chuo kikuu<br />

cha Dar es Salaam Bw. Bashiru<br />

Ally alisema kwamba, mambo yote<br />

yanayohusiana na ardhi ni lazima<br />

yapewe kipaumbele kuzungumziwa<br />

katika katiba mpya ili kuzuia uadui<br />

unaoweza kutokea baina ya wamiliki<br />

16<br />

ardhi na watawala.<br />

“Ni lazima kuangalia sheria<br />

zetu za ardhi na kuziimarisha ili<br />

ziweze kulinda haki za wazawa wa<br />

Kitanzania” alisisitiza Bw. Ally<br />

Alisema hadi mwaka <strong>20</strong>10,<br />

Serikali ilikwishagawa hekta<br />

610,000 za ardhi kwa makampuni<br />

13 ya uwekezaji ya kigeni na wengi<br />

wamepewa na kuhodhi maeneo<br />

hayo pasipo kuyaendeleza na<br />

wengine wamelalamikiwa kwa<br />

kujiingiza katika biashara ya mbao<br />

na hivyo kuharibu mazingira badala<br />

ya kuyatunza.<br />

Alisema serikali imekuwa<br />

ikitangaza kuwa, Tanzania ina hekta<br />

milioni 44 za ardhi inayofaa ka kilimo<br />

na kwamba kati yake ni hakta 10.8<br />

milioni tu zinazotumika.<br />

“Lakini baadhi ya wataalamu na<br />

wanaharakati watetezi wa haki ya<br />

ardhi wamesema huu ni udanganyifu<br />

kwani ardhi ambayo haitumiki ni ile<br />

iliyopo kwenye mbuga za wanyama,<br />

hifadhi ya misitu na kwenye hifadhi<br />

za asili. Wakulima na wafugaji wote<br />

wanatumia ardhi waliyotengewa na<br />

katika maeneo mengi haiwatoshi<br />

ndiyo maana kunatokea migogoro<br />

ya ardhi,” alisema msomi huyo.<br />

Aliwashauri wakulima kushiriki<br />

kikamilifu katika mchakato wa<br />

uandikaji wa katiba mpya pindi<br />

utakapoanza, ili washawishi kuingizwa<br />

kwa vipengele muhimu vinavyotetea<br />

umiliki wa ardhi kwa wazawa.<br />

Alisema mataifa tajiri ambayo<br />

sasa yanaongoza kwa kuvamia ardhi<br />

katika bara la Afrika ni pamoja na<br />

Korea ya Kusini, China Saudi Arabia na<br />

Umoja wa Nchi za Kiarabu, ambapo<br />

nchi za Afrika zilizokwishavamiwa ni<br />

Zambia, Ethiopia, Kenya na Sudani.<br />

“Uwekezaji huo unalenga kuzalisha<br />

mazao ya nishati mmea pamoja<br />

na mazao ya chakula ambacho<br />

kinasafirishwa pasipo nchi husika<br />

kunufaika.”<br />

Ingawa wanaounga mkono<br />

uwekezaji huo wanatetea kuwa<br />

hoja kwa maelezo kuwa utasaidia<br />

kuimarisha kilimo kwenye nchi<br />

zinazoendelea, lakini ukweli unabaki<br />

wazi kuwa uwekezaji huo unafanyika<br />

kwa malengo ya faida binafsi za<br />

kibiashara ama faida za mataifa hayo<br />

tajiri.<br />

Mapema Mkurugenzi Mtendaji<br />

wa wilaya ya Chunya, Bw. Maurice<br />

Sapanjo katika maeneo aliyofanyakazi<br />

na vikundi vya wakulima hasa vya<br />

<strong>MVIWATA</strong>, vimekuwa msaada<br />

mkubwa wakuchochea kazi ya<br />

maendeleo vijijini.<br />

Alishauri <strong>MVIWATA</strong> kujieneza<br />

zaidi vijijini waliko wakulima wengi<br />

ili waweze kunufaika na utetezi na<br />

maarifa inayotolewa kupitia mtandao<br />

huo.<br />

Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya ya Chunya, Bw. Maurice Sapanjo<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11


Bodi mpya ya <strong>MVIWATA</strong><br />

Na Goodness Mrema, Morogoro<br />

Wajumbe wa Mkutano<br />

Mkuu wa 16 wa<br />

<strong>MVIWATA</strong> uliofanyika<br />

Oktoba 25, <strong>20</strong>11 mjini Morogoro<br />

wamechagua Bodi mpya ya<br />

wakurugenzi wa shirika hilo<br />

watakaokaa madarakani kwa miaka<br />

mitatu <strong>20</strong>11-<strong>20</strong>14.<br />

Bodi mpya iliyochaguliwa<br />

inaongozwa na Bw. Habibu<br />

Simbamkuti mkulima mdogo kutoka<br />

Kikundi cha Sanje kijiji cha Msolwa<br />

Ujamaa, tarafa ya Kidatu wilaya ya<br />

Kilombero mkoani Morogoro. Bw.<br />

Simbamkuti anawakilisha kanda<br />

namba 2 (Morogoro,Pwani na Dar<br />

es Salaam).<br />

Msaidizi wake ni Bibi. Veronica<br />

Sophu mkulima mdogo wa kijiji cha<br />

Madibila wilaya ya Mbarali mkoani<br />

Mbeya anayewakilisha kanda namba<br />

7 (Mbeya, Rukwa na Kigoma). Bibi<br />

Esther Mallya mkulima kutoka<br />

wilaya ya Hai,mkoani Kilimanjaro<br />

amechaguliwa kuwa Mwekahazina<br />

akiwakilisha kanda namba 3<br />

(Kilimanjaro na Tanga).<br />

Wajumbe wa bodi wengine ni Bw.<br />

Bodi ya zamani <strong>20</strong>08-11<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />

Joseph Kilowoko kutoka Namtumbo<br />

Ruvuma akiwakilisha kanda namba<br />

8(Iringa na Ruvuma), Paulo Joseph<br />

kutoka Babati Manyara akiwakilisha<br />

kanda namba 4(Manyara, Arusha<br />

na Mara), Haji Ussi Haji kutoka<br />

Bodi mpya <strong>20</strong>11-14<br />

KUTOKA MITANDAONI<br />

Zanzibar akiwakilisha kanda namba<br />

1 (Zanzibar).<br />

Wengine ni Bw. Projestus<br />

Ishekanyoro kutoka Kagera<br />

akiwakilisha kanda namba 6<br />

(Mwanza, Kagera na Shinyanga),<br />

Bibi Amina Kazibure kutoka Masasi<br />

Mtwara akiwakilisha kanda namba 9<br />

(Mtwara na Lindi) na Bibi Prisca John<br />

kutoka Igunga Tabora akiwakilisha<br />

kanda namba 5 (Tabora, Singida na<br />

Dodoma).<br />

Mkurugenzi Mtendaji wa<br />

<strong>MVIWATA</strong> Bw. Stephen Ruvuga<br />

anaingia kwenye vikao vya bodi<br />

kama katibu.<br />

Wajumbe wa bodi iliyomaliza<br />

muda wake walikuwa ni Bw. Yazid<br />

Makame (mwenyekiti), Bibi Lydia<br />

Ruliho (makamu), Bibi Grace<br />

Runkulatire (Mwekahazina).<br />

Wajumbe wengine walikuwa<br />

ni Bw. Julius Mbago, Bw. Joseph<br />

Kilowoko, Bw. Samwel Maseke,<br />

Bibi Cosma Bullu, Bw. Habibu<br />

Simbamkuti, Bw. Sylivester Yatuba.<br />

<strong>17</strong>


KUTOKA MITANDAONI<br />

SIKU YA WANAMTANDAO MKURANGA<br />

Mkuu wa wilaya ahimiza mahusiano<br />

baina ya wadau wa kilimo<br />

Na Abdalla Idd, Mkuranga<br />

Mkuu wa wilaya ya Mkuranga<br />

mkoani Pwani Bw. Henry<br />

Clemence, amewahimiza<br />

wadau wa sekta ya kilimo wilayani<br />

humo kuimarisha mahusiano yenye<br />

lengo la kumsaidia mkulima kupiga<br />

hatua za kimaendeleo.<br />

Wito huo aliutoa wakati<br />

akifungua maadhimisho ya SIKU YA<br />

WANAMTANDAO MKURANGA,<br />

iliyofanyika Disemba 6, <strong>20</strong>11<br />

Mkuranga mjini.<br />

Mkuu huyo wa wilaya alisema, hivi<br />

sasa katika wilaya hiyo na maeneo<br />

mengine nchini yapo mashirika na<br />

taasisi zinazofanya kazi na wakulima,<br />

lakini taasisi hizo hazifahamiani<br />

ingawa zinatekeleza shughuli kwenye<br />

eneo moja.<br />

Alisema kuimarishwa kwa<br />

mahusiano hayo kutasaidia<br />

Wanawake wa kijiji cha Kizapala wilayani Mkuranga wakionyesha usindikaji wa muhogo kwa<br />

wageni toka nje ya nchi waliowatembelea kujifunza shughuli zao<br />

18<br />

kuunganisha nguvu na kuondoa<br />

mtawanyiko wa raslimali ambazo<br />

zikitumika vyema zitaongeza ufanisi.<br />

Siku ya Wanamtandao Mkuranga<br />

ambayo imefanyika kwa mara ya<br />

kwanza, iliandaliwa na <strong>MVIWATA</strong><br />

Mkuranga kwa lengo la kuwakutanisha<br />

wadau mbalimbali kuimarisha<br />

mahusiano na kubadilishana taarifa.<br />

Aidha siku hiyo ilitoa fursa kwa<br />

wakulima kuonesha matokeo ya<br />

shughuli za uzalishaji wanazofanya<br />

na kuhamasisha matumizi ya bidhaa<br />

zitokanazo na zao la Mhogo kama<br />

mbadala wa mazao mengine ya<br />

chakula.<br />

Wakizungumza kwenye<br />

maadhimisho hayo, baadhi ya<br />

wanachama wa <strong>MVIWATA</strong><br />

walisema miongoni mwa mafanikio<br />

waliyoyapata kupitia mtandao wa<br />

wakulima wilayani humo ni pamoja<br />

na kuimarisha mahusiano baina ya<br />

wakulima na wadau wengine wa<br />

kilimo zikiwemo asasi za fedha na<br />

kushirikiana na Jeshi la polisi kupitia<br />

ulinzi wa Polisi Jamii.<br />

Walitolea mfano wa mfumo wa<br />

ulinzi shirikishi ulioanzishwa na<br />

mtandao wa wakulima wa kijiji cha<br />

Kolagwa ili kutatua changamoto<br />

ya usalama wa mali na maisha<br />

ya wananchi hasa baada ya tukio<br />

la kuvamiwa na kujeruhiwa kwa<br />

wakulima waliokuwa wamepata<br />

mkopo.<br />

Wakielezea kuhusiana na<br />

changamoto walizokabiliana<br />

nazo katika kufanikisha siku hiyo<br />

wamesema kuwa ni pamoja na<br />

uhaba wa rasilimali fedha na kwa<br />

kuwa tukio hili lilikuwa la linafanyika<br />

kwa mara ya kwanza ilichukua muda<br />

mrefu kuwashawishi wadau na<br />

kukubali kushiriki.<br />

Mojawapo ya dosari zilizojitokeza<br />

kwenye maadhimisho hayo ni<br />

pamoja na baadhi ya wakuu wa<br />

idara za halmashauri ya wilaya<br />

kutohuhiria na hivyo changamoto<br />

kadhaa zilizoibuliwa na wakulima<br />

zilikosa majibu sahihi.<br />

Mfano kukosekana kwa wataalamu<br />

wa idara ya Afya kulikuwa ni kikwazo<br />

kwa shughuli muhimu ya upimaji<br />

wa hiari wa VVU kwa washiriki<br />

waliokuwa tayari kufanya hivyo.<br />

Siku hii maalum ya wanamtandao<br />

ilihudhuriwa na wadau kutoka asasi<br />

mbalimbali yakiwemo mabenki,<br />

kampuni za simu za mkonini, Jeshi<br />

la polisi, viongozi wa halmashauri<br />

ya wilaya ya Mkuranga, viongozi wa<br />

mtandao wa wilaya na watumishi<br />

wa <strong>MVIWATA</strong> pamoja na wakulima<br />

kutoka vijiji 16 vya wilaya hiyo.<br />

Na maadhimisho ya siku hiyo<br />

yalisindikizwa na burudani za aina<br />

mbalimbali ikiwemo vikundi vya<br />

ngoma na baadaye mashindano<br />

ya mpira wa kikapu kwa timu za<br />

wanawake.<br />

Wakati huo huo, Mtandao<br />

wa kati wa <strong>MVIWATA</strong> Mkuranga<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 19<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11


Maazimio ya Kongamano...<br />

Inatoka uk. wa 8<br />

waliazimia mambo yafuatayo:<br />

1. Sisi wakulima wadogo tunasikitika<br />

kuona kwamba maadili na misingi<br />

ya Azimio la Arusha vimewekwa<br />

kando kama msingi wa mfumo<br />

wa uzalishaji na hivyo kukuza<br />

matabaka ambapo matajiri<br />

wachache ndiyo wanothaminiwa<br />

na watawala wakati sisi tulio<br />

wengi tukiwa tunapuuzwa katika<br />

mfumo wa uzalishaji.<br />

2. Sisi wakulima wadogo tunapinga<br />

kwa nguvu zote na kwa kauli moja<br />

mifumo yote ambayo kwa namna<br />

moja au nyingine inapelekea<br />

kumkandamiza mkulima mdogo na<br />

kumsukuma kando katika mfumo<br />

wa umilikaji ardhi na uzalishaji.<br />

Mifumo hiyo inahusisha uporaji<br />

wa rasilimali za ardhi ili kupisha<br />

wawekezaji wakubwa wa ndani<br />

na nje kwa kisingizio kwamba<br />

wakulima wadogo hawana ufanisi<br />

wa kuendeleza kilimo.<br />

3. Pamoja na kushukuru juhudi za<br />

serikali za kutoa huduma kwa<br />

wakulima, sisi wakulima wadogo<br />

tumekubaliana kwamba kuna<br />

kasi ndogo sana ya maendeleo<br />

ya mkulima mdogo na maisha<br />

ya mkulima mdogo kwa ujumla<br />

yameendelea kuwa duni hata<br />

baada ya miaka 50 ya uhuru.<br />

Tunaazimia kujipanga kuhakikisha<br />

kuwa katika miaka 50 ijayo<br />

wakulima wadogo wawe mhimili<br />

wa uchumi wetu.<br />

4. Wakulima wadogo tumekerwa na<br />

kuchoshwa na migogoro mingi ya<br />

ardhi isiyo na kikomo kila kukicha<br />

katika maeneo mbalimbali ya nchi<br />

hii, ambayo inasababishwa na<br />

usimamizi mbovu na utekelezaji<br />

hafifu wa sheria zetu ikiwemo<br />

sera ya Ardhi ya Taifa pamoja<br />

na sheria za ardhi za 1999 na<br />

kanuni zake. Aidha, tunaitaka<br />

serikali ichukue hatua dhidi ya<br />

wawekezaji ambao wamekiuka<br />

masharti ya kupewa ardhi kwa<br />

ajili ya matumizi waliyoombea.<br />

Vile vile, tunaitaka serikali ichukue<br />

hatua za haraka katika kutatua<br />

migogoro inayohatarisha amani<br />

katika maeneo mbalimbali ya nchi;<br />

kwa mfano mgogoro wa ardhi<br />

Kibaigwa, Mbalali, Kiteto n.k<br />

5. Tunasikitishwa na kuhuzunishwa na<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />

kukua kwa matabaka kati ya matajiri<br />

na masikini wengi wao tukiwa<br />

sisi wakulima wadogo ambapo<br />

hatuna uhakika hata wa upatikanaji<br />

wa huduma za msingi ikiwemo<br />

upatikanaji wa huduma muhimu<br />

za kijamii hususan elimu ya watoto<br />

wetu, huduma za afya kwa familia<br />

zetu, miundombinu ya barabara na<br />

maji safi na salama. Kwa sababu hiyo<br />

tunaitahadharisha serikali kuchukua<br />

hatua thabiti za kupunguza pengo<br />

kati ya walionacho na wasionacho<br />

ili kulinda amani na mshikamano wa<br />

nchi yetu<br />

6. Sisi wakulima wadogo tunaazimia<br />

kuwawajibisha viongozi wote<br />

ambao hawasimamii maslahi<br />

ya wakulima wadogo, ikiwemo<br />

kujipanga kutowapigia kura viongozi<br />

wanaosaliti wakulima wadogo<br />

katika uchaguzi mkuu wa <strong>20</strong>15.<br />

Wakulima wadogo tusiburuzwe<br />

na wanasiasa: tunapaswa kujenga<br />

uwezo wetu wa kutofautisha<br />

kauli za wanasiasa na ahadi zao za<br />

majukwaani ili kuwabaini wanasiasa<br />

wenye dhamira thabiti na wale<br />

ambao kauli zao ni za kutetea<br />

maslahi yao binafsi.<br />

7. Sisi wakulima wadogo tumeazimia<br />

kujenga mshikamano miongoni<br />

mwetu ili tuweze kudai haki zetu<br />

kwa nguvu ya hoja na bila woga.<br />

Tutatumia fursa ya mchakato<br />

wa utungaji wa katiba ili katiba<br />

itakayotungwa ilinde vyema zaidi<br />

maslahi ya wakulima wadogo<br />

8. Sisi wakulima wadogo tumegundua<br />

kwamba kudai haki kwa kupiga<br />

kelele tu haitoshi. Kwa mfano<br />

serikali imeziba masikio kuhusu<br />

kilio chetu cha kuwa na uhuru wa<br />

kuuza mazao yetu kwa mnunuzi<br />

tunayetaka ndani na nje ya nchi.<br />

Kwa hiyo tumedhamiria kutumia<br />

sera, sheria na kanuni zilizopo<br />

kudai haki zetu bila woga katika<br />

vyombo vya sheria vilivyopo na<br />

njia nyinginezo halali.<br />

9. Ili kuongeza nguvu ya <strong>MVIWATA</strong>,<br />

sisi ambao ni wanachama takriban<br />

elfu sabini (70,000), tunaazimia<br />

kuongeza idadi ya wanachama<br />

wetu nchi nzima na shughuli<br />

zetu za kiharakati pamoja na<br />

kuelimishana kuhusu haki na<br />

wajibu wa mkulima mdogo.<br />

KUTOKA MITANDAONI<br />

Mkuu wa wilaya<br />

ahimiza...<br />

Inatoka uk. wa 18<br />

umefanya mkutano wake Mkuu<br />

wa mwaka Disemba 5,<strong>20</strong>11<br />

huku ukitanguliwa na warsha ya<br />

siku moja kwa ajili ya kujifunza<br />

na kujadili changamoto kadhaa<br />

zinazowakabili wakulima wilayani<br />

humo.<br />

Mada kuu iliyojadiliwa kwenye<br />

warsha ni mafunzo ya hatua za<br />

mchakato wa uanzishwaji wa<br />

Chama cha Akiba na Mikopo<br />

(SACCOS) cha wakulima wa<br />

zao la muhogo somo ambalo<br />

lilifundishwa na Afisa kutoka Ofisi<br />

ya Ushirika wilayani hapo.<br />

Washiriki walitafakari zaidi<br />

faida za kuwa na chombo hicho<br />

ambacho kitarahisisha upatikanaji<br />

wa mitaji na kuwasaidia kupanua<br />

shughuli zao.<br />

Baada ya mafunzo hayo,<br />

washiriki walichagua kamati ya<br />

muda iliyopewa jukumu la kuandaa<br />

rasimu ya katiba ya SACCOS<br />

na kukusanya michango kama<br />

kiingilio na hisa kutoka katika vijiji<br />

16 ambavyo ni Dundani, Mkuranga,<br />

Mwanambaya, Mwanadilatu,<br />

Sotele, Mavunje, Njopeka, Misasa,<br />

Kerezange, Kizapara, Tungi, Tunda,<br />

Mamdimpela, Mamdikongo,<br />

Lupondo na Kolangwa.<br />

Aidha siku ya mkutano<br />

mkuu wa mtandao, wajumbe<br />

walijadiliana juu ya uendelevu<br />

wa mitandao ikiwa ni pamoja na<br />

kutafuta mbinu itakayotumika<br />

katika kuongeza wanachama<br />

ambapo viongozi walikumbushwa<br />

kuwahamasisha wakulima<br />

kujiunga na <strong>MVIWATA</strong> na kuwa<br />

na kadi za uanachama, kuweka<br />

mfumo mzuri wa ukusanyaji wa<br />

michango na pia kuweka mfumo<br />

wa utunzaji wa kumbukumbu za<br />

wanachama.<br />

Mkutano huo pia ulipokea<br />

taarifa ya utekelezaji wa shughuli,<br />

taarifa ya mapato na matumizi ya<br />

shughuli za mtandao kwa mwaka<br />

<strong>20</strong>11 na kujadili mpango mkakati<br />

wa mwaka <strong>20</strong>12.<br />

19


MAKALA<br />

Wakulima, matrekta <strong>20</strong>0 waandamana<br />

kudai haki<br />

Na Goodness Mrema, Kibaigwa<br />

Wakulima wilayani<br />

Kongwa mkoani<br />

Dodoma wakiwa<br />

na matrekta yao zaidi ya <strong>20</strong>0<br />

mnamo Disemba 1, <strong>20</strong>11, walifanya<br />

maandamano makubwa na kufunga<br />

kwa muda barabara kuu ya Dodoma<br />

– Dar es Salaam katika eneo la<br />

Kibaigwa wakipinga maamuzi ya<br />

serikali ya kuwazuia kulima kwenye<br />

mashamba yao yaliyoko wilaya jirani<br />

ya Kiteto mkoani Manyara.<br />

Wakulima hao wana mashamba<br />

yao makubwa kwenye vijiji tisa<br />

vya wilaya ya Kiteto ambavyo ni<br />

Lendolai, Mlimahamba, Laitini, Mbigiri,<br />

Kutelimeinyi, Seseni, Laipela, Kimarai<br />

na Kisima, ambavyo vimeingizwa<br />

kwenye eneo la hifadhi ya taifa na<br />

kuzuia shughuli zozote za kilimo.<br />

Maandamano hayo yalifanyika<br />

katika mji mdogo wa Kibaigwa<br />

wilayani Kongwa mahali ambako<br />

kuna soko la kimataifa la Mahindi<br />

ambalo zaidi ya asilimia 60 ya mazao<br />

yanayopokelewa sokoni hapo,<br />

yanatoka kwenye vijiji hivyo.<br />

Wakizungumza kwa nyakati<br />

tofauti wakulima hao walisema kuwa<br />

walianza kulima mashamba hayo tangu<br />

mwaka 1990 lakini cha kushangaza<br />

mwaka <strong>20</strong>06 walitaarifiwa kuwa<br />

eneo hilo limegeuzwa kuwa hifadhi<br />

ya mbuga ya wanyama.<br />

Bw. Clement Petro, mmoja wa<br />

wakulima walioathiriwa na maamuzi<br />

hayo anaeleza kuwa baada ya<br />

kuzuiwa walifungua kesi mahakama<br />

<strong>20</strong><br />

Mmoja wa wakulima walionyang’anywa ardhi akizungumza siku ya maandamano ya<br />

Kibaigwa Disemba 1, <strong>20</strong>11<br />

kuu kupinga uamzi huo na kushinda.<br />

Hata hivyo halmashauri ya<br />

Kiteto ilikata rufaa mahakama ya<br />

rufaa kupinga hukumu hiyo ambapo<br />

ilishinda na wakulima wakaamriwa<br />

kuondoka katika eneo hilo.<br />

Hata hivyo, wakulima hao<br />

wanasikitishwa na maamuzi hayo<br />

huku wakisema serikali haiwatakii<br />

mema kwa kuwa ni hivi karibuni tu<br />

serikali imewahamasisha kuchukua<br />

mikopo ya matrekta na kwamba<br />

wanatarajia mavuno kutoka kwenye<br />

mashamba hayo ili kulipa mikopo.<br />

“Ni hivi majuzi tu serikali<br />

imetuhamasisha kuchukua mikopo<br />

ya matrekta nasi tumeitikia kwa<br />

wingi tukifahamu kuwa tunayo ardhi<br />

ya kutosha na tukivuna tutarejesha<br />

mkopo, sasa leo tunazuiwa kulima, huu<br />

ni sawa na uuaji,” alisema Bw. Petro.<br />

Bw. Omary Athuman ni mkulima<br />

na anamiliki matrekta zaidi ya 10<br />

wilayani humo na anasema “kutokana<br />

na halmashauri kutufukuza kutoka<br />

katika eneo hili nina wasiwasi kama<br />

nitaweza kurejesha mkopo wa<br />

matrekta niliyokopa kutoka katika<br />

Shirika la Uchumi la Jeshi la Kujenga<br />

taifa(Suma JKT) tawi la Dodoma.”<br />

“Mimi sijui hii dhana ya kilimo<br />

kwanza inatekelezwaje kwani mwanzo<br />

tulidhani kuwa ni sera nzuri lakini hivi<br />

sasa tunaona haitekelezwi kwa vitendo<br />

na kuongeza kuwa yeye anazo hekari<br />

300 ambazo huwa analima mahindi na<br />

kupata mavuno mengi.”<br />

Naye mkulima Bw. Ali Khalifan<br />

Said, alisema kuwa wakati amri hiyo<br />

inaanza kutekelezwa tayari walikuwa<br />

wameshaandaa mashamba na hivyo<br />

kuondoka katika eneo hilo ni hasara<br />

kubwa sana kwake.<br />

“Wanataka tuondoke katika eneo<br />

hili lakini cha ajabu hawatuambii<br />

twende wapi wala nani atalipa madeni<br />

ya matrekta yetu tuliyokopa na nyumba<br />

tulizojenga kwa mkopo” alisema Said.<br />

Wakulima hao walielekeza kilio<br />

chao kwa Rais Jakaya Kikwete<br />

wakimuomba kuingilia kati suala<br />

hilo ili waweze kurudishiwa ardhi na<br />

kuendelea na uzalishaji, kwa sababu<br />

viongozi wengine ngazi ya wilaya na<br />

mkoa wameshindwa kuwasaidia.<br />

Kwa upande wake, meneja wa soko<br />

la wakulima la Kibaigwa Bw. Kusekwa<br />

Dalali alisema kuwa wamekuwa<br />

wakipokea mazao kutoka katika<br />

mikoa mitano ambayo ni Dodoma,<br />

Morogoro, Manyara, Iringa na Tanga.<br />

Endelea <strong>Uk</strong> wa 21<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11


Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />

KUTOKA MITANDAONI<br />

Nani mchawi wa maendeleo ya<br />

wakulima nchini?<br />

Na Goodness Mrema<br />

Uchumi wa wakulima<br />

wadogo kabla na baada<br />

ya uhuru uliendelea kuwa<br />

mikononi mwa wakulima wenyewe<br />

kupitia vyama vya ushirika.<br />

Chanzo cha kuanzishwa kwa<br />

vyama vya ushirika, ilikuwa ni<br />

baada ya serikali ya kikoloni kuanza<br />

kudhibiti faida ya mauzo ya mazao<br />

ya wakulima bila kuwashirikisha.<br />

Ni kweli mkoloni ndiye alianzisha<br />

kilimo cha mazao ya biashara ili<br />

kupata fedha za kigeni. Kabla ya hapo<br />

wakulima walijishughulisha na kilimo<br />

cha mazao ya chakula tu na ilipobidi<br />

walibadilishana bidhaa pasipo kutumia<br />

fedha kama ilivyo sasa.<br />

Madhumini ya wakoloni ya<br />

kuanzisha kilimo cha mazao ya<br />

biashara na kuwaingiza wenyeji<br />

kwenye mfumo wa biashara yalikuwa<br />

ni pamoja na kupata malighafi kwa ajili<br />

ya viwanda huko ulaya, lakini pia kwa<br />

minajili ya kupata fedha za kugharamia<br />

uendeshaji wa makolini yao.<br />

Kwa kuwaingiza wakulima<br />

kwenye kilimo cha biashara mkoloni<br />

aliweza kutoza kodi na makato<br />

mengine ambayo ndiyo yaliyotumika<br />

kuendesha serikali.<br />

Ili kupata fedha zaidi mkoloni<br />

aliwanyonya wakulima kwa njia<br />

mbalimbali, kwanza kununua mazao<br />

kwa bei ndogo kuliko gharama<br />

za uzalishaji, na pili kwa kuwauzia<br />

pembejeo za kilimo kwa bei<br />

waliyojipangia mwenyewe.<br />

Na kama hiyo haitoshi, akaanza<br />

kuwalazimisha kulima mazao<br />

aliyoyataka yeye kwa manufaa yake<br />

kitu ambacho kilitafsiriwa kuwa ni<br />

utumwa.<br />

Mtindo huu wa manunuzi<br />

kujipangia bei ya kuuzia pembejeo<br />

na kisha kujipangia ile ya kununulia<br />

mavuno pasipo majadiliano, ndiyo<br />

uliwazindua wakulima na kuanzisha<br />

vyama vya ushirika.<br />

Vyama hivyo vilisaidia siyo tu kuwa<br />

na sauti ya pamoja lakini pia katika<br />

kupigania bei nzuri inayoendana na<br />

gharama halisi za uzalishaji. Vyama<br />

hivi pia vilijiingiza katika kusambaza<br />

pembejeo na huduma nyingine kwa<br />

mkulima.<br />

Wakulima wakajihamasisha na<br />

kuanzisha vyama vya ushirika katika<br />

sehemu mbalimbali za nchi.<br />

TANU ilivyoanzishwa haikusita<br />

kuziunganisha nguvu za vyama vya<br />

ushirika na vyama vya wafanyakazi<br />

na makundi mengine katika harakati<br />

za uhuru. Lakini uhuru ulipopatikana,<br />

serikali ya TANU iliendelea na<br />

staili ile ya mkoloni ya kuwapunja<br />

wakulima kwa kudhibiti faida ya<br />

mauzo bila kuwashirikisha ili ipate<br />

fedha za kugharamia uendeshaji wa<br />

kazi za serikali.<br />

Na ili kuhakikisha wakulima<br />

hawafurukuti, mwaka 1967 serikali<br />

iliviunganisha vyama vyote vya<br />

ushirika nchini chini ya mwavuli<br />

ulioitwa Muungano wa Vyama vya<br />

Ushirika Nchini.<br />

Serikali pia ilianzisha Bodi za Mazao<br />

mbalimbali kuisaidia kudhibiti faida ya<br />

mauzo kwa lengo lile lile la kupata<br />

fedha za uendeshaji wa serikali.<br />

Hata hivyo ilipofika mwaka 1976,<br />

serikali iliuvunjilia mbali ushirika<br />

na badala yake kukaanzishwa bodi<br />

mbalimbali za mazao hasa mazao ya<br />

biashara.<br />

Bodi zilizoanzishwa ni pamoja na<br />

za kahawa, pareto, tumbaku, chai na<br />

korosho bila kusahau mkonge kwani<br />

lilikuwa ndilo zao lenye kuingiza<br />

fedha nyingi za kigeni hadi wakati<br />

huo.<br />

Baadaye tena baadhi ya bodi za<br />

mazao zikabadilishwa kwa sheria<br />

ya bunge kuwa mamlaka za mazao.<br />

Hivyo kuwa na mamlaka ya mkonge,<br />

mamlaka ya pamba na kadhalika.<br />

Kazi kubwa ya mamlaka hizi ikiwa<br />

ni kuimarisha udhibiti wa mfumo wa<br />

uzalishaji, usafirishaji na uuzaji wa<br />

mazao ndani na nje ya nchi.<br />

Na kwa kuwa mamlaka hizo<br />

zilianzishwa kwa sheria ya bunge<br />

kukawa na udhibiti zaidi wa mazao<br />

husika katika kila hatua. Kwa lugha<br />

nyingine, mamlaka hizi ziligeuka<br />

polisi wa wakulima.<br />

Ni bodi za mazao ndizo zilizopanga<br />

kima cha chini ambacho mkulima<br />

alitakuwa kulima, utunzaji wa mazao<br />

shambani, utaratibu na hata tarehe<br />

ya kuvuna na bila kusahau zikipanga<br />

bei ya kununulia mazao kutoka kwa<br />

wakulima na pia bei ya pembejeo<br />

walizouziwa wakulima.<br />

Chini ya mamlaka za mazao<br />

mkulima akageuka kuwa mfungwa<br />

anayepaswa tu kutekeleza kile<br />

alichoambiwa. Uhuru na demokrasia<br />

waliyokuwa wameizoea kwenye<br />

vyama vya ushirika vikapotea.<br />

Badala yake sheria za kikoloni<br />

zinazolazimisha mkulima kulima zao<br />

fulani pasipo hiari yake na ambazo<br />

ndizo zilikuwa zimewakasirisha watu<br />

hadi kuupigania uhuru zikaimarishwa<br />

ndani ya Tanzania huru.<br />

Wakulima, matrekta <strong>20</strong>0 waandamana...<br />

Inatoka uk. wa <strong>20</strong><br />

Alisema kwa mwaka soko linauza<br />

zaidi ya tani 1000 za mazao. “Tunauza<br />

zaidi kwenye maeneo ya Dar es<br />

Salaam, Kilimanjaro, MorogoroTanga,<br />

Iringa na Mbeya na mikoa ya kanda ya<br />

ziwa katika mikoa ya Mara, Mwanza<br />

na Shinyanga ambako tumeanza<br />

mwaka jana, pia kabla ya kufungwa<br />

kwa mipaka tulikuwa tunapata<br />

wateja kutoka Mombasa na Nairobi<br />

lakini pia Zanzíbar ni wanunuzi<br />

wazuri wa mazao yetu.”<br />

Mazao wanayoyapokea katika<br />

soko hilo ni pamoja na mahindi,<br />

mbaazi, tetere, alzeti, nyonyo na<br />

maharagwe na kwamba asilimia 60<br />

ya mazao hayo hutoka katika wilaya<br />

ya Kiteto.<br />

“Kitendo hiki cha wakulima<br />

kuzuiwa kulima mashamba<br />

yao kwenye vijiji hivyo tisa<br />

kinaashiria kufa kwa soko letu<br />

kwa sababu asilimia 60 ya mazao<br />

yanayopokelewa hapa hutoka<br />

wilayani Kiteto hasa kwenye vijiji<br />

hivyo,” alisema Bw. Kusekwa.<br />

21


KATUNI<br />

22<br />

SASA<br />

AFANYAJE NA<br />

MAISHA HAYA MAGUMU<br />

TUNAZALISHA KWA<br />

NGUVU ZOTE LAKINI<br />

FAIDA NI KIDOGO.<br />

LAKINI MAMA CHUNGU HATA NCHI ZA<br />

WENZETU MAJIRANI HAWAJAPIGA<br />

HATUA SANA KATIKA MIPANGO YA<br />

KUWAWEZESHA WAKULIMA<br />

WADOGO.<br />

MIAKA 50 YOTE<br />

TUMESHINDWA KUFIKIA<br />

MALENGO YA KUMUINUA<br />

MKULIMA MDOGO, MIMI NAONA<br />

TUSEME MIAKA 50 YA UHURU<br />

TUMETHUBUTU, TUMESHINDWA,<br />

TUJIPANGE UPYA.<br />

MZEE<br />

KUJIKO HAKATI<br />

TAMAA MWAKA WA<br />

PILI AMEKOSA MAHINDI<br />

LAKINI BADO ANAENDA<br />

KUPANDA TENA.<br />

LAKINI<br />

BABA CHUNGU<br />

SERIKALI SI NDIO<br />

INATAKIWA KUMSIMAMIA<br />

MKULIMA?<br />

‘EHE, EHE EHE!<br />

NDIO<br />

LAKINI SI NDIO<br />

TUNASHEHEREKEA<br />

MIAKA 50 YA UHURU SASA<br />

ANGALIA MIAKA YOTE SERIKALI<br />

IMEMSAIDIA VIPI MKULIMA<br />

KUJIKWAMUA na KILIMO CHA<br />

JEMBE LA MKONO<br />

MH<br />

TUSIJILIN-<br />

GANISHE NA NCHI<br />

MASIKINI ZENYE<br />

RASILIMALI CHACHE<br />

KULIKO TANZANIA<br />

AAH<br />

JEMBE<br />

LENYEWE LA<br />

MKONO?<br />

MIMI SIONI<br />

SABABU YA KUSHEHEREKEA<br />

MIAKA 50 YA UHURU KAMA<br />

MATATIZO YA MSINGI YANA-<br />

TAKIWA KUSHUGHULIKIWA<br />

HAYAJASHUGHULIKWA<br />

LAKINI<br />

ACHA AJARIBU<br />

TENA ANAWEZA<br />

KUPATA.<br />

WAKATI<br />

MKULIMA HUYO<br />

HUYO NDIO ANAZAL-<br />

ISHA CHAKULA CHA<br />

KULISHA TAIFA<br />

TULENGE MA-<br />

FANIKIO MAKUBWA BILA<br />

KUJALI MAJIRANI ZETU, SISI<br />

TUNA RASILIMALI NA ARDHI YA<br />

KUTOSHA AMBAZO HATUTUMII<br />

IPASAVYO MFANO ARDHI, MITO<br />

NA MAZIWA.<br />

MATATIZO<br />

GANI HAYO?<br />

MARADHI,<br />

UJINGA NA UMASKINI,<br />

NA UMASKINI NDIO ADUI<br />

No. 1 NA BADO WAKULIMA<br />

HATUPEWI KIPAUMBELE<br />

JAMANI!<br />

AAH<br />

KILIMO<br />

CHENYEWE<br />

CHA MVUA ZA<br />

KUBAHATISHA?<br />

TENA<br />

NA KIJEMBE<br />

KIMOJA CHA<br />

MKONO!?<br />

ILA MANENO YAKO<br />

MAMA CHUNGU NI YA<br />

BUSARA<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11


MWAKA<br />

1961 - 1985 ILIWEZA<br />

KUWASAIDIA WAKULIMA<br />

KWA KUANZISHA AZIMIO LA<br />

ARUSHA, VIWANDA VILITUMIA<br />

MALI GHAFI ZA WAKULIMA LAKINI<br />

BAADA YA 1985 - <strong>20</strong>11 MKULIMA<br />

HANA THAMANI TENA.<br />

MIAKA 50 YA<br />

UHURU WAKULIMA WENGI<br />

WANAONDOLEWA KWENYE<br />

ARDHI YA MABABU. WAKULIMA<br />

WANAPIGWA WANAFUNGWA,<br />

WAKITETEA ARDHI YAO<br />

NA KUUWAWA.<br />

KWELI<br />

TUMEKUWA<br />

TUKIISHI KWA MATAMKO<br />

MBALIMBALI KAMA KILIMO<br />

NI UTI WA MGONGO, CHAKULA<br />

NI UHAI, NA SASA KILIMO<br />

KWANZA PAMOJA NA HAYO<br />

WAKULIMA WAMEBAKI<br />

DUNI.<br />

HOFU<br />

GANI TENA?<br />

WANAHOFU<br />

KUPORWA ARDHI<br />

YAO.<br />

MIMI<br />

NAFIKIRI IMEFI-<br />

KA WAKATI WAKULIMA<br />

WAUNGANE WAIMARISHE<br />

UMOJA WAO.<br />

NA ARDHI<br />

YENYEWE WANA-<br />

PEWA WAWEKEZAJI<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />

SIO UMOJA TU SASA HIVI<br />

TUNATAKIWA TUJIPANGE NA<br />

KUZIFAHAMU SHERIA ZA<br />

ARDHI ILI TUITETEE HAKI<br />

YETU<br />

SASA<br />

HAPO THAMANI<br />

YA MKULIMA<br />

MDOGO IKO WAPI?<br />

NDIO<br />

MAANA BABA WA<br />

TAIFA ALISEMA MWAF-<br />

RIKA AKIRUHUSIWA KUUZA<br />

ARDHI BAADAE ARDHI YOTE<br />

ITAMILIKIWA NA WAGENI<br />

SABABU YA UMASKINI.<br />

HUWEZI<br />

KUJIZUIA KUUZA<br />

ARDHI WAKATI<br />

WEWE NI MAS-<br />

KINI<br />

HII IMESABA-<br />

BISHWA NA SERA<br />

AMBAZO HAZIMJALI<br />

SANA MKULIMA<br />

MDOGO<br />

SAWA<br />

KABISA SISI<br />

NDIO WAZALISHAJI<br />

WAKUBWA WA CHAKULA<br />

CHA NCHI SIO HAO<br />

WAWEKEZAJI WA-<br />

NAOPELEKA CHAKULA<br />

NJE YA NCHI<br />

NDIO<br />

KATUNI<br />

JAMANI EH TUACHE<br />

KULALAMIKA SI MMESIKIA<br />

KAMATI YA KUKUSANYA MAONI<br />

TUITUMIE VIZURI FURSA HII TUTOE<br />

MAONI ILI KATIBA MPYA IMLINDE<br />

MKULIMA MDOGO JUU YA DHULUMA<br />

TUNAZOFANYIWA BASI!!<br />

EEH NDIO<br />

MAANA MIAKA 50<br />

WANAISHI KWA HOFU!<br />

SASA<br />

IMEFIKA WAKA-<br />

TI SERIKALI IFANYIE<br />

KAZI MADHAIFU YOTE<br />

YANAYO MKANDAMIZA<br />

MKULIMA<br />

23


KUTOKA MITANDAONI<br />

Wakulima 30 wahitimu mafunzo ya<br />

uwezeshaji na usimamizi vikundi<br />

Na Goodness Mrema, Nyandira<br />

Mvomero<br />

Wakulima nchini<br />

wamehimizwa kutumia<br />

vyema ujuzi na elimu<br />

wanayopewa wanaposhiriki<br />

mafunzo mbalimbali kwa ajili ya<br />

maendeleo ya wakulima wote<br />

nchini.<br />

Wito huo umetolewa Novemba<br />

7, <strong>20</strong>11 na Afisa Ushawishi na<br />

Utetezi wa <strong>MVIWATA</strong> Bw<br />

Thomas Laiser, alipokuwa akifunga<br />

mafunzo ya Wakulima Wawezeshaji<br />

30 (Mapromota) waliokuwa<br />

wakihudhuria mafunzo ya wiki<br />

mbili ya usimamizi na uendeshaji wa<br />

vikundi katika kituo cha mafunzo ya<br />

Wakulima cha Nyandira wilaya ya<br />

Mvomero mkoani Morogoro.<br />

Wawezeshaji hao walitoka<br />

kwenye masoko matatu<br />

yanayojengwa na <strong>MVIWATA</strong> katika<br />

vijiji vya Igurusi Mbarali Mbeya, Matai<br />

24<br />

na Kasanga wilaya ya Sumbawanga<br />

Vijijini.<br />

Bw. Laiser alisema <strong>MVIWATA</strong><br />

imekuwa ikitoa mafunzo ya aina<br />

mbalimbali kwa lengo la kuwajengea<br />

uwezo wakulima wachache<br />

(wakulima wakufunzi) ambao<br />

wanatarajiwa kwenda kusambaza<br />

ujuzi huo kwa wakulima wengine.<br />

Mbali na mafunzo hayo <strong>MVIWATA</strong><br />

imekuwa ikiwezesha wakulima<br />

kushiriki semina, mikutano na ziara<br />

za mafunzo nje ya nchi na kwamba<br />

wahusika wanaporudi kwenye<br />

maeneo yao wanapaswa kuwa<br />

chachu ya mabadiliko ya kusaidia<br />

kusukuma mbele maendeleo.<br />

“Tusiwe wachoyo wa kuwagawia<br />

wenzetu maarifa tuliyopewa,<br />

tumieni vyema maarifa mliyoyapata,<br />

mkawasaidie viongozi na wakulima<br />

wenzenu kuleta mabadiliko ya<br />

kiuchumi na kuondokana na maisha<br />

ya kimasikini,” alisema Bw. Laiser.<br />

Aidha aliwataka washiriki<br />

wa mafunzo hayo kuimarisha<br />

Wahitimu wa mafunzo wakifurahia baada ya kukabidhiwa vyeti vya mafunzo hayo<br />

mshikamano na mawasiliano katika<br />

vikundi na mitandao ya wakulima<br />

nchini ili kuwa na sauti yenye nguvu<br />

itakayotimiza lengo la utetezi wa<br />

maslahi yao.<br />

“Mnatakiwa kuwasaidia wakulima<br />

waweze kujipanga,kujisimamia na<br />

kutetea maslahi yao na kuwezesha<br />

vikundi kushirikiana na wadau<br />

wengine,” alisema Bw. Laiser.<br />

Aliwahimiza wakulima hao pia<br />

kujenga utamaduni wa kutafuta<br />

habari mbalimbali kupitia vyombo<br />

vya habari na kuzitumia vyema habari<br />

wanazozipata kujiletea maendeleo.<br />

Katika risala yao wahitimu wa<br />

mafunzo hayo walisema watatumia<br />

vyema elimu waliyoipata kwa<br />

kuielimisha jamii na kuahidi kutimiza<br />

wajibu wao na kufanya kazi kwa<br />

kujituma.<br />

Wawezeshaji hao waliohitimu<br />

mafunzo pia waliomba kupewa<br />

ushirikiano na viongozi wa serikali<br />

ngazi za vijiji na kata ili kurahisisha<br />

utekelezaji wa majukumu yao.<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11


Jipatie nakala ya Jarida la Pambazuko katika ofisi<br />

za <strong>MVIWATA</strong> ngazi za kati zifuatazo<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Morogoro<br />

S.L.P 32<strong>20</strong> Morogoro<br />

Mahali: Uwanja wa Maonyesho NaneNane mkabala na<br />

ofisi za TASO<br />

Simu/Faksi: 023 261 41 84<br />

Barua Pepe: morogoro@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Rukwa<br />

S.L.P 468 Sumbawanga<br />

Mahali: Jengo la Bethlehem Center – Barabara ya Msakila<br />

Faksi: +255 25 280 25 58<br />

Simu: +255 764 232 747, +255 784 940 606<br />

Barua pepe: rukwa@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Mbeya<br />

S.L.P 3015 Mbeya<br />

Mahali: Jengo la Bima na CRDB Bank (Ghorofa ya<br />

mwisho<br />

Simu: +255 784 979 397, +255 652 835 568<br />

Barua pepe: mbeya@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Chunya<br />

Mahali: Jengo la Halmashauri, chumba Na.3<br />

Barua pepe: chunya@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Iringa<br />

S.L.P 918 Njombe<br />

Mahali: Jengo la Njoluma, Njombe mjini<br />

Simu: 0782 241 224, +255 767 241 224<br />

Barua pepe: iringa@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Kilimanjaro<br />

S.L.P 7389 Moshi<br />

Mahali: Mbuyuni sokoni- ghorofa ya GOLDEN GROWN<br />

LODGE<br />

Simu: +255 27 275 16 39, +255 784 7<strong>20</strong> 3<strong>20</strong><br />

Barua pepe: kilimanjaro@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Kagera<br />

S.L.P <strong>17</strong>53 Bukoba Mjini<br />

Mahali: Ofisi za Mayawa-Mtaa wa Rwamishenyi, Barabara<br />

ya Uganda<br />

Simu: +255 788 685818, +255 782 154961, +255 755 522 447<br />

Barua pepe: kagera@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Dodoma<br />

S.L.P 3293 Dodoma<br />

Mahali:Area C Dodoma eneo la INADES Formation<br />

Tz,mkabala na msikiti wa Area C<br />

Simu:255-26-2350013, +255 782 257 783,<br />

+255 767 881 352<br />

Faksi: +255 26 2350744<br />

Barua pepe: dodoma@mviwata.org<br />

Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />

Mwenyekiti<br />

<strong>MVIWATA</strong> Monduli (MVIWAMO)<br />

S.L.P 47 Monduli<br />

Mahali: Barabara ya Boma-Moringe Sekondari, Monduli<br />

Mjini<br />

Simu: 255-27-253 8029, +255 27 253 8337<br />

Faksi: +255 27 253 8338<br />

Barua pepe: monduli@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Manyara<br />

S. L. P. 446,<br />

Babati Manyara<br />

Mahali: Barabara ya Nyerere<br />

SIMU: +255 27 253 0385 Faksi: +255 27 253 0707<br />

Baruapepe: manyara@mviwata.org<br />

Mwenyekiti<br />

<strong>MVIWATA</strong> Tabora<br />

S.L.P <strong>17</strong>5 Igunga<br />

Mahali: Mtaa wa Uarabuni<br />

Simu: +255 784 398 414, +255 782 219 551<br />

Barua pepe: tabora@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Zanzibar<br />

S.L.P 149 Zanzibar<br />

Mahali: Mwana kwerekwe- mkabala na shule ya sekondari<br />

M’kwerekwe A<br />

Simu: +255 773 926 955, +255 777 470 518<br />

+255 783 651 135<br />

Barua pepe: zanzibar@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Ruvuma<br />

S.L.P 696 Songea Manispaa<br />

Mahali: Jengo la TTCL ghorofa ya 2<br />

Simu: +255-25-2600626, +255 756 096 291<br />

Barua pepe: ruvuma@mviwata.org<br />

Mratibu<br />

<strong>MVIWATA</strong> Mkuranga<br />

S.L.P 56 Mkuranga<br />

Mahali: Karibu na Stendi ya Kimanzichana<br />

Simu: 0786 158 646<br />

Barua pepe: mkuranga@mviwata.org<br />

MAWAKALA<br />

Mwenyekiti:<br />

<strong>MVIWATA</strong> Shinyanga<br />

S.L.P 1024 Shinyanga<br />

Mahali: Chuo cha Ushirika Moshi tawi la Shinyanga<br />

(Kizumbi)<br />

Simu: +255 763 740 675, +255 755 546 311<br />

Barua Pepe: shinyanga@mviwata.org<br />

Mwenyekiti<br />

<strong>MVIWATA</strong> Kigoma<br />

S.L.P 1144 Kigoma<br />

Mahali: Ndani ya ofisi ya KIKANGONET, Lumumba road<br />

jengo la NHC chumba <strong>20</strong>5<br />

Simu: 0713 565 252, 0762 565 252<br />

Barua pepe: aisimba@yahoo.co.uk<br />

25


IJUE <strong>MVIWATA</strong><br />

Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania- <strong>MVIWATA</strong><br />

Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (<strong>MVIWATA</strong>) ni chombo cha kuunganisha wakulima wadogo ili kuwa na sauti moja katika utetezi wa<br />

maslahi yao ya kiuchumi, kijamii, kiutamaduni na kisiasa.<br />

Mtandao huu ulianzishwa mwaka 1993 na wakulima wadogo. Kauli mbiu ya <strong>MVIWATA</strong> ni ‘Mtetezi wa Mkulima ni Mkulima<br />

Mwenyewe’.<br />

Falsafa, utume na dira ya <strong>MVIWATA</strong><br />

Falsafa ya <strong>MVIWATA</strong> inajengwa katika ya misingi ya ushawishi na utetezi wa maendeleo ya wakulima wadogo katika nyanja za kiuchumi na<br />

kijamii; kuwezesha mawasiliano na kujifunza kwa kubadilishana uzoefu miongoni mwa wakulima.<br />

Utume wetu:<br />

Kuimarisha mawasiliano na kuwaunganisha wakulima wadogo kupitia vikundi na mitandao yao katika ngazi mbali mbali ili kujenga mtandao wa<br />

kitaifa wenye nguvu ya kuwezesha ushiriki na uwakilishi wa kweli wa maslahi ya wakulima wadogo katika ngazi zote za maamuzi.<br />

Dira yetu:<br />

<strong>MVIWATA</strong> ni kuwa chombo imara chenye nguvu za ushiriki na uwakilishi wa mawazo ya mkulima katika mchakato wa maamuzi ya kiuchumi,<br />

kijamii na kisiasa. Kuwa na uwezo wa kutekeleza na kufuatilia michakato na shughuli za maendeleo ya kiuchumi na kijamii yanayogusa maslahi ya<br />

wakulima wadogo.<br />

Malengo ya <strong>MVIWATA</strong><br />

1. Kuwezesha mawasiliano miongoni mwa wakulima wadogo ili kujenga kwa pamoja mbinu na mikakati ya ushawishi na utetezi kwa maslahi ya<br />

wakulima wadogo, kiuchumi na kijamii.<br />

2. Kubadilishana mawazo, ujuzi na uzoefu juu ya kilimo na shughuli mbalimbali za wakulima ili kuboresha maisha na kuinua hali yao kiuchumi na<br />

kijamii.<br />

3. Kuwakilisha wakulima wadogo katika mashauriano na serikali juu ya masuala mbalimbali yanayohusu au yanayoathiri ufanisi na maslahi ya<br />

wakulima wadogo wa Tanzania.<br />

Maeneo makuu ya mpango mkakati<br />

1. Ushawishi na Utetezi: Kuwezesha wakulima wadogo kuwa na uwezo wa kutetea maslahi yao.<br />

2. Uwezo wa kiuchumi: kuwezesha wakulima wadogo kuwa na uwezo wa kiuchumi kupitia njia za akiba na mikopo, kuunganisha wakulima na<br />

masoko na elimu ya ujasiliamali<br />

3. Kuimarisha vikundi na mitandao ya wakulima kwa lengo la kujipanga na kujitetea.<br />

4. Masuala mtambuka: Kujenga uelewa wa wakulima juu ya <strong>Uk</strong>imwi, Jinsia, Mabadiliko ya Tabia ya nchi.<br />

5. Ujenzi wa kitaaasisi kwa lengo la kuimarisha shirika<br />

Muundo<br />

Muundo wa <strong>MVIWATA</strong> una ngazi tatu ambazo ni Ngazi ya Taifa, Ngazi ya Kati na Ngazi ya Msingi. Ngazi ya Kati inaundwa na mitandao ya<br />

kimkoa na kiwilaya wakati Ngazi ya Msingi inaundwa na mitandao ya Kata na Vijiji.<br />

Shughuli kuu<br />

1. Kujenga uwezo wa wakulima wadogo kwa kupitia mafunzo shirikishi juu ya mbinu za ushawishi na utetezi, mbinu za kuimarisha uchumi wa<br />

wakulima wadogo na uendelevu wa rasilimali kwa njia za warsha, mafunzo, mikutano na ziara za mafunzo.<br />

2.<br />

3.<br />

4.<br />

Kuhamasisha wakulima wadogo kujiunga katika vikundi vya kijamii na kiuchumi, mitandao ya msingi (kata na vijiji) na mitandao ya kati (mikoa<br />

na wilaya). Mpaka sasa <strong>MVIWATA</strong> imeanzisha mitandao ya kimkoa katika Mikoa ya Dodoma, Iringa, Kagera, Kilimanjaro, Manyara, Mbeya,<br />

Morogoro, Rukwa, Ruvuma, Shinyanga, Tabora na Tanga kwa Tanzania Bara. <strong>MVIWATA</strong> pia imeanzisha mitandao ya kiwilaya katika Wilaya<br />

za Monduli (Arusha) na Chunya (Mbeya). Tanzania Visiwani, <strong>MVIWATA</strong> Zanzibar imeanzishwa na kusajiliwa (Usajili namba 401). Mkakati<br />

unaendelea wa kuimarisha mitandao iliyopo na kuanzisha mitandao mipya.<br />

Kukusanya, kuweka katika kumbukumbu na kusambaza habari zinazohusu ujuzi na uzoefu wa wakulima, sera za kitaifa na kimataifa kwa<br />

kupitia jarida la Pambazuko Sauti ya Wakulima, vipindi vya radio, vipeperushi, vijitabu na machapisho mengine.<br />

Kuhamasisha na kuwezesha wakulima kubuni na kuendesha miradi shirikishi ya kiuchumi na uzalishaji kwa lengo la kuboresha uchumi wa<br />

wakulima wadogo kama vile vyama vya mazao, vyama vya kuweka na kukopa na masoko ya mazao.<br />

5. Kuandaa mikutano na warsha kuhusiana na mada zinazowagusa au kuathiri maslahi ya wakulima wadogo.<br />

Uanachama na jinsi ya kujiunga na shirika<br />

<strong>MVIWATA</strong> ina wanachama wa aina tatu (3).<br />

Aina ya kwanza ni Wanachama wa Kawaida ambao wamegawanyika katika makundi mawili;<br />

a) Kikundi cha wakulima wadogo au<br />

b)<br />

Mkulima mdogo binafsi aliye mwanachama katika Kikundi au Mtandao. Mkulima atakuwa mwanachama wa kawaida wa <strong>MVIWATA</strong> mara<br />

tu Kikundi au Mtandao wake utakapokubaliwa kuwa mwanachama. Atapewa kadi ya uanachama na kikundi au mtandao utapewa cheti cha<br />

utambulisho.<br />

Aina ya pili ni Vyama, Mashirika na Mitandao ya Wakulima Wadogo.<br />

Vyama, Mashirika na Mitandao ya Wakulima Wadogo vinavyojishughulisha na utetezi na ushawishi wa maslahi ya wakulima wadogo vilivyosajiliwa<br />

chini ya sheria yoyote ya Tanzania katika Ngazi za Wilaya, Mkoa au Taifa vinaweza kuomba kuwa mwanachama wa <strong>MVIWATA</strong> iwapo vinakubaliana<br />

kwa dhati na malengo na madhumuni ya Shirika.<br />

Aina ya tatu ni Wanachama Washiriki<br />

Ni mtu yeyote, taasisi au kikundi cha watu ambacho kinaunga mkono malengo na madhumuni ya Shirika. Mwanachama mshiriki anatamkwa na<br />

Mkutano Mkuu wa <strong>MVIWATA</strong>.<br />

Kila mwanachama, isipokuwa mwanachama mshiriki atalipa kiingilio na ada ya kila mwaka. Maelezo zaidi juu ya utaratibu wa kujiunga na ada<br />

yanapatikana kutoka kwa kiongozi au ofisi ya <strong>MVIWATA</strong>.<br />

Kwa mawasiliano zaidi<br />

Ofisi Kuu ya <strong>MVIWATA</strong><br />

Mkurugenzi Mtendaji<br />

<strong>MVIWATA</strong><br />

S.L.P 32<strong>20</strong> Morogoro<br />

Simu: 023 261 41 84<br />

Faksi: 023 261 41 84<br />

Barua pepe: info@mviwata.org, mviwata@morogoro.net

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!