You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Toleo NO. 040 Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11 Bei Shs. 500/= ISSN 0856-5937<br />
<strong>Uk</strong>. 1<br />
Je wakulima wadogo wamefaidi<br />
matunda ya uhuru<br />
<strong>Uk</strong>. <strong>17</strong><br />
Bodi mpya ya <strong>MVIWATA</strong><br />
yachaguliwa<br />
<strong>Uk</strong>. <strong>20</strong><br />
Wakulima, matrekta waandamana<br />
kupinga uporwaji ardhi
Toleo NO. 040<br />
Oktoba Disemba <strong>20</strong>11<br />
Bei Shs. 500/=<br />
ISSN 0856-5937<br />
WAHARIRI<br />
Susuma Msikula Susuma<br />
Stephen Ruvuga<br />
MHARIRI MSAIDIZI<br />
TOLEO NO.040<br />
BODI YA <strong>MVIWATA</strong><br />
Mwenyekiti – Habibu Simbamkuti<br />
Makamu Mwenyekiti –<br />
Veronica Sophu<br />
Katibu - Stephen Ruvuga-<br />
(Mkurugenzi Mtendaji)<br />
Mweka Hazina – Esther Mallya<br />
WAJUMBE<br />
Joseph Kilowoko<br />
Prisca John<br />
Amina Kazibure<br />
Projestus Ishekanyoro<br />
Haji Ussi Haji<br />
Paul Joseph<br />
MSHAURI WA <strong>MVIWATA</strong><br />
Prof. Amon Mattee<br />
LINATOLEWA NA<br />
KUSAMBAZWA NA<br />
Mtandao wa Vikundi vya<br />
Wakulima Tanzania (<strong>MVIWATA</strong>)<br />
S.L.P 32<strong>20</strong> Morogoro, Tanzania<br />
Simu: 023 261 41 84<br />
Faksi: 023 261 41 84<br />
Barua pepe: info@mviwata.org,<br />
mviwata@morogoro.net<br />
Tovuti: www.mviwata.org<br />
MICHORO<br />
Godwin Chipenya<br />
USANIFU NA<br />
UCHAPISHAJI<br />
PENplus Ltd – 022 218<strong>20</strong>59<br />
Toleo NO. 040 Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11 Bei Shs. 500/= ISSN 0856-5937<br />
Je wakulima wadogo wamefaidi<br />
matunda ya uhuru<br />
Picha ya Jalada:<br />
Mkazi wa kijiji cha Msowero wilayani<br />
Kilosa mkoani Morogoro akiwa na<br />
uso wenye tafakari nzito, Je, baada<br />
ya miaka 50 amefaidi matunda ya<br />
uhuru? b<br />
<strong>Uk</strong>. 1<br />
<strong>Uk</strong>. <strong>17</strong><br />
Bodi mpya ya <strong>MVIWATA</strong><br />
yachaguliwa<br />
<strong>Uk</strong>. <strong>20</strong><br />
Wakulima, matrekta waandamana<br />
kupinga uporwaji ardhi<br />
Tahariri<br />
Serikali iwasaidie wakulima<br />
kujikwamua na umasikini<br />
Moja ya kauli iliyotolewa<br />
na mkulima aliyechangia<br />
mawazo kwenye toleo hili<br />
ni ile isemayo “Kuna maana gani ya<br />
kusheherekea uhuru ili hali umasikini<br />
kama adui namba moja wa uhuru<br />
huo ametamalaki na kushamiri ndani<br />
ya familia za watanzania?”<br />
Kila msomaji wetu ana uhuru wa<br />
kuipa tafsiri na uzito tofauti kauli hii<br />
kadri ya mtizamo wake.<br />
Kwetu sisi kauli hii inaibua<br />
tafakari na msukumo wa kutafuta<br />
kuona kuna mafanikio gani ya msingi<br />
katika kupambana na umasikini<br />
nchini tokea tupate uhuru ambayo<br />
yanaweza kutufariji na kusheherekea<br />
miaka 50 ya uhuru?<br />
Ripoti ya Shirika la<br />
Maendeleo la Umoja wa Mataifa<br />
(UNDP) iliyozinduliwa mwaka jana<br />
jijini Dar es salaam inonyesha jinsi<br />
umasikini ulivyozidi kushika kasi<br />
kwa mtu mmoja mmoja na taifa<br />
kwa ujumla. Kwa mujibu wa ripoti<br />
hiyo, katika kila watanzania 100,<br />
watanzania 97 wanaishi kwenye<br />
umasikini wa kipato cha chini ya<br />
dola 2 kwa siku huku kila watanzania<br />
89 kati ya 100 wakiishi chini ya dola<br />
moja kwa siku. Kwa taswira hii na<br />
katika ulimwengu huu ambapo kila<br />
kitu kinapatikana kwa pesa, ni wazi<br />
kuwa wimbi la watanzania wengi<br />
hawamudu maisha yao kwa kukosa<br />
kipato cha kufanya hivyo.<br />
Kwa kukosa kipato, watanzania<br />
hasa vijijini bado wanaishi kwenye<br />
nyumba za nyasi na tembe mpaka hivi<br />
leo kwa kuwa hawamudu kununua<br />
bati, saruji na vifaa vingine vya ujenzi<br />
kutokana na kukosa kipato, pia<br />
watanzania wengi hususani vijijini<br />
hawamudu gharama hafifu za afya<br />
zilizopo na hivyo kuishia kufa au<br />
kujikita zaidi katika kupiga ramli na<br />
imani za kishirikina.<br />
Inasikitisha kuona kuwa ndani ya<br />
miaka 50 bado tunaishi kwa wasiwasi<br />
wa kukumbwa na njaa kila mwaka.<br />
Tokea uhuru mpaka sasa, watanzania<br />
zaidi ya asilimia 89 wanaishi kwa<br />
mwanga wa vibatari kwa kukosa<br />
nishati ya umeme, ingawa tuna mito,<br />
mabwawa na maziwa kila upande<br />
wa nchi.<br />
Ni vigumu wakulima kufurahia<br />
kuwa wana uhuru wakati ujinga<br />
miongoni mwao umeota mizizi<br />
huku kukiwa na porojo nyingi za<br />
kisiasa za kuwapumbaza hasa wakati<br />
wa kupiga kura. Ni wakulima hao<br />
hao wanaoliingizia kipato taifa hili,<br />
watoto wao wanasoma wakiwa<br />
wamekaa kwenye vumbi chini ya<br />
vivuli vya miti. Je, ndani ya mika 50<br />
ya uhuru na katika mazingira haya,<br />
wakulima wanaelimika ama idadi<br />
ya wajinga inaongezeka miongoni<br />
mwao?<br />
Kuwa huru maana yake ni<br />
kukomboka kifikra kunatokana<br />
na misingi ya elimu ambayo taifa<br />
limejiwekea kwa watu wake.<br />
Elimu ya kumkomboa mtanzania<br />
ni ile ya kumfanya mtanzania<br />
huyu ajisimamie mwenyewe na<br />
kuendesha maisha yake kwa<br />
umakini na ufanisi wa hali ya juu<br />
bila kuwepo na utofauti wowote na<br />
binadamu wengine wanaosemekana<br />
kupiga hatua kimaisha. Je, jamii yetu<br />
wakulima tunayo elimu kweli au<br />
ni ile elimu ya kuzalisha manamba<br />
wanaopaswa kuwahudumia wageni<br />
wanaomiminika nchini kwa kivuli<br />
cha uwekezaji. Ni uhuru upi huo<br />
tunaousherehekea katika hali kama<br />
hii?<br />
<strong>Uk</strong>o wapi uhuru wa mkulima<br />
kijijini wakati bado maelfu ya<br />
wanawake wanajifugulia nyumbani<br />
kwa sababu katika vijiji wanavyoishi<br />
hakuna zahanati, vituo vya afya wala<br />
hospitali? Hii ni huduma ya msingi<br />
inayopaswa kupatikana kiurahisi<br />
na kwa ubora wa hali ya juu kwa<br />
wananchi ndani ya taifa linalojinasibu<br />
kuwa huru kwa takribani miaka 50<br />
sasa. Katika hali halisi ya kitanzania,<br />
je, uhuru maana yake ni kutembea<br />
kilometa zaidi ya 50 kufuata huduma<br />
muhimu? Kwa ujumla serikali<br />
inapaswa kuwekeza nguvu nyingi<br />
katika hili.<br />
Umasikini umeota mizizi kwa<br />
kuwa rushwa nayo imeota mizizi.<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 3<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11
Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania<br />
Bara; Je, Wakulima Wadogo<br />
wamefaidi matunda ya Uhuru?<br />
Na Susuma Susuma, Morogoro<br />
Tanzania Bara imeadhimisha<br />
miaka 50 ya uhuru wake<br />
tangu mkoloni Mwingereza<br />
alipokabidhi utawala mnamo<br />
tarehe 9 Disemba 1961. Uhuru<br />
huu ulipatikana baada ya juhudi<br />
za dhati za vijana wa wakati huo<br />
wakiongozwa na Hayati Baba wa<br />
Taifa Mwalimu Julius Kambarage<br />
Nyerere kupambana kwa njia<br />
ya amani pasipo umwagaji damu<br />
kama yalivyofanya mataifa mengine<br />
Mafanikio<br />
yangekuwa ni uzalishaji<br />
kwa mashamba ya wakulima<br />
umeongezeka kwa kiasi gani, watu<br />
wanaolala njaa wamepungua kwa kiasi<br />
gani, watu wanaoishi chini ya dola<br />
moja kwa siku wamepungua kwa<br />
kiasi gani?<br />
ya Afrika.<br />
Miaka 50 ya kujitawala,<br />
tumeshuhudia awamu nne za<br />
uongozi wa Taifa letu, huku awamu ya<br />
kwanza ikiongozwa na Baba wa Taifa,<br />
Mwalimu Nyerere, awamu ya pili<br />
Mzee Ali Hassan Mwinyi, awamu ya<br />
tatu iliongozwa na Mzee Benjamini<br />
Mkapa na awamu hii ya nne usukani<br />
umeshikwa na Rais Jakaya Mrisho<br />
Kikwete. Katika awamu zote nne,<br />
serikali imepambana na changamoto<br />
nyingi za maendeleo, pia imetumia<br />
fursa nyingi za maendeleo ili<br />
kuwezesha maendeleo ya kiuchumi,<br />
kisiasa na ustawi wa jamii. Makala<br />
hii ambayo imejumuisha maoni na<br />
mitizamo ya makundi mbalimbali,<br />
itaangalia yatokanayo na jitihada za<br />
kuendeleza kilimo na changamoto<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />
zake katika awamu zote hizo<br />
Miongoni mwa maswali ya tafakari<br />
yaliyochochea kuandaa makala hii,<br />
ni:- Je ndani ya miaka 50 ya uhuru,<br />
wakulima wadogo wamefaidi<br />
matunda ya uhuru, nini mustakabali<br />
wao kwa miaka 50 ijayo? Na Jitihada<br />
zilizofanywa na awamu zote nne<br />
za serikali, zimefanikiwa kiasi gani<br />
kutatua matatizo yanayokabili ustawi<br />
wa jamii ya wakulima wadogo?<br />
Je wakulima wadogo wamefaidi<br />
matunda ya uhuru?<br />
Baadhi ya wadau wa kilimo,<br />
walipokuwa wakijibu swali hili, wengi<br />
wao majibu yao yalikuwa ni HAPANA<br />
na kusema kuna kila sababu<br />
ya msingi ya wakulima<br />
kuwa na maombolezo<br />
yanayoashiria kudai<br />
uhuru wa kweli na<br />
kuacha kudanganyika<br />
na uhuru wa bandia<br />
kutokana na dosari<br />
nyingi walizoziainisha.<br />
Msomi wa Chuo<br />
Kikuu cha Kilimo cha<br />
Sokoine (SUA) kilichopo<br />
mkoani Morogoro Dkt Damian<br />
Gabagambi aliyebobea katika<br />
masuala ya Uchumi Kilimo katika<br />
mada aliyoitoa kwenye Kongamano<br />
la miaka 50 ya Uhuru lililoandaliwa<br />
na <strong>MVIWATA</strong> Disemba 6, <strong>20</strong>11<br />
mjini Morogoro alisema tunatakiwa<br />
kujitathmini kwa kina ili kujua<br />
tumekosea wapi na tujipange vipi ili<br />
kukwepa kurudia makosa tuliyofanya<br />
huko nyuma na tunayofanya sasa.<br />
“Kwa haraka haraka wananchi<br />
wanaweza kushawishika na kuridhika<br />
kuwa nchi yetu imeendelea sana<br />
tangu tupate uhuru. <strong>Uk</strong>weli ambao<br />
wananchi hawaelezwi ni kwamba,<br />
tutoke ndani ya boksi kabisa, tuache<br />
tabia ya kujilinganisha na wachovu<br />
ambao hawana hata robo ya utajiri<br />
wa maliasili za Tanzania, tujilinganishe<br />
na walio mbele yetu kama vile<br />
MADA MAALUM<br />
Malaysia” alisema Dkt Gabagambi.<br />
Alisema serikali inatumia fedha<br />
nyingi kwenye sekta ya kilimo bila<br />
mafanikio ya maana, zaidi ya yale<br />
yanayoripotiwa kwenye makaratasi;<br />
tena kwa kiwango cha raslimali<br />
fedha zilizoingizwa kwenye sekta<br />
na wala sio mabadiliko chanya kwa<br />
mkulima.<br />
Alisema mafanikio yanayotajwa<br />
na serikali siyo mafanikio halisi bali<br />
ni maandalizi ya kwenda kwenye<br />
mafanikio. Mafanikio yangekuwa ni<br />
uzalishaji kwa mashamba ya wakulima<br />
umeongezeka kwa kiasi gani, watu<br />
wanaolala njaa wamepungua kwa<br />
kiasi gani, watu wanaoishi chini ya<br />
dola moja kwa siku wamepungua<br />
kwa kiasi gani?<br />
“Kwa ufupi, kinachofanyika nchi<br />
hii katika kuhudumia kilimo ni kwa<br />
miradi kufukuzana na milestones<br />
zilizo katika maandiko ya miradi<br />
basi,” alisema na kuitaka serikali iteue<br />
maeneo machache na kuwekeza kwa<br />
tija badala ya kutawanya raslimali<br />
kwenye miradi mingi isiyoleta tija.<br />
Aliongeza kuwa pamoja na bidii<br />
zote hizi sekta ya kilimo bado<br />
inakabiliwa na matatizo yale yale<br />
ya miaka yote ambayo ni tija duni,<br />
ukosefu wa mikopo, miundo mbinu<br />
duni, kilimo cha kutegemea mvua,<br />
ukosefu wa masoko, usindikaji<br />
mdogo, teknolojia duni, kutotumia<br />
matokeo ya tafiti katika mipango na<br />
huduma duni za ughani.<br />
Mtaalamu huyu anaitaka serikali<br />
iache kujilinganisha na nchi masikini<br />
zenye raslimali chache kuliko Tanzania.<br />
“Tulenge kupata mafanikio makubwa<br />
bila kujali jirani zetu wamefanikiwa<br />
kiasi gani. Kulenga mbali kuna maana<br />
kubwa sana katika saikolojia ya<br />
matumizi ya raslimali za mtu au nchi.<br />
Nchi ikijiwekea malengo makubwa<br />
italazimika kuwa mwangalifu sana<br />
katika kila senti inayopatikana, na<br />
haitakuwa na mchezo kwa yeyote<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 2<br />
1
MADA MAALUM<br />
Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara...<br />
Inatoka uk. wa 1<br />
anayekwamisha mipango kwa<br />
kusimamia vibaya rasilimali za nchi.<br />
Kinyume chake, nchi isipokuwa<br />
na malengo ya juu sana inaweza<br />
kujikuta ikiwa na matumizi ya anasa<br />
kama tunavyoshuhudia hapa nchini.”<br />
Anasema katika miaka hamsini<br />
ijayo Tanzania inatakiwa ilenge mbali.<br />
Ikilenga kuwa kama Afrika Kusini<br />
inaweza kuishia kuwa kama Kenya.<br />
Lakini ikilenga kuwa kama Marekani,<br />
inaweza kuishia kuwa kama Malaysia<br />
au Singapore, ambapo tayari<br />
yatakuwa ni mafanikio makubwa.<br />
Akamalizia ameshauri kwamba ni<br />
vyema itumike kauli mbiu mpya<br />
yenye ujumbe usemao “Miaka<br />
50: Tumethubutu, Tumeshindwa,<br />
Tujipange Upya”.<br />
Mwalimu Nyerere aliposhika<br />
madaraka alibainisha maradhi, ujinga<br />
na umasikini kama matatizo ya msingi<br />
ya nchi yaliyopaswa kushughulikiwa,<br />
ambayo kwa mtizamo wa Bibi<br />
Marcelina Charles Kibena<br />
mkulima kutoka tarafa ya Mgeta<br />
wilayani Mvomero, anahoji “kuna<br />
maana gani ya kusheherekea uhuru<br />
ili hali umasikini kama adui namba<br />
moja wa uhuru huo ametamalaki<br />
na kushamiri ndani ya familia zetu?<br />
Kuna mafanikio gani ya msingi katika<br />
kupambana na umasikini katika<br />
kipindi hiki ambacho wakulima<br />
tunyanyaswa na kunyimwa haki za<br />
msingi?”<br />
Bibi Marcelina Charles Kibena<br />
Bibi Kibena aliyekuwa akiwasilisha<br />
mada ya uzoefu wa mkulima mdogo<br />
kwenye Kongamano la miaka<br />
hamsini ya maendeleo ya kilimo<br />
lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha<br />
Sokoine cha Kilimo (SUA), alisema<br />
tunapoangalia uzoefu wa miaka<br />
50 iliyopita ni lazima kulinganisha<br />
2<br />
maisha ya mkulima mdogo kijijini<br />
na shughuli zake za kilimo kama<br />
mhimili wa maisha yake na wananchi<br />
wengine ambao wanategemea aina<br />
nyingine ya kipato, na hasa watu<br />
waishio mijini.<br />
“Kwa kipindi cha miaka hamsini<br />
ya uhuru kumekuwepo na<br />
matamko mbalimbali<br />
yenye nia thabiti ya<br />
kuboresha kilimo na<br />
wakulima wadogo<br />
kama Siasa ni Kilimo,<br />
Kilimo ni uti wa mgongo<br />
wa nchi, Chakula ni uhai,<br />
Kilimo cha kufa na kupona na sasa<br />
Kilimo Kwanza. Pamoja na matamko<br />
yote hayo, kwa ujumla tunaweza<br />
kusema kuwa katika kipindi hiki<br />
cha miaka hamsini ya uhuru kundi<br />
hili la wazalishaji wadogo limebaki<br />
katika hali duni ya maisha. Hali hii<br />
imetokana na sera ambazo kwa kiasi<br />
kikubwa hazimjali mkulima mdogo.”<br />
Alisema katika miaka 50 hii,<br />
wakulima wadogo wanaishi kwa<br />
hofu kubwa ya kuporwa ardhi na<br />
akakumbuka maneno ya hayati<br />
baba wa Taifa mwaka 1958 ambayo<br />
sasa yanatimia, nukuu: “Katika<br />
nchi kama yetu ambayo<br />
Waafrika ni maskini na<br />
wageni ni matajiri, kuna<br />
uwezekano mkubwa kwamba<br />
Mwafrika akiruhusiwa<br />
kuuza ardhi, katika miaka<br />
themanini au miaka ijayo,<br />
ardhi yote ya Watanganyika<br />
itamilikiwa na matajiri<br />
wageni, na wenyeji watakuwa<br />
watwana. Lakini hata<br />
kama wageni wasingekuwa<br />
matajiri, litaibuka tabaka<br />
la watanganyika matajiri<br />
wajanja. Tukiiruhusu ardhi<br />
iuzwe kama kanzu, katika<br />
muda mchache, kutakuwa<br />
na kundi dogo la waafrika<br />
wakiwa na ardhi na walio<br />
wengi watakuwa watwana.”<br />
Uwezeshaji na Uzalishaji<br />
Akizungumzia kiwango cha uzalishaji,<br />
Bibi Kibena alisema, wakulima<br />
wamekuwa wakitumia kwa kiasi<br />
kikubwa mbegu za asili na ndizo<br />
ambazo zimewezesha kulisha taifa<br />
kwa kipindi chote cha miaka hamsini<br />
ya uhuru. Hata hivyo akasema<br />
wameibuka watu wachache wa<br />
kuzibeza wakishinikiza kuleta mbegu<br />
za viini tete (GMOs) ili kutupotezea<br />
“Sisi<br />
tunaona kuwa hali<br />
hii itamfanya mkulima mdogo<br />
kuwa mtumwa wa mbegu na<br />
kumzidishia umaskini.”<br />
mbegu zetu za asili na wao kumiliki<br />
soko lote la mbegu. “Sisi tunaona<br />
kuwa hali hii itamfanya mkulima<br />
mdogo kuwa mtumwa wa mbegu na<br />
kumzidishia umaskini.”<br />
Mkulima huyo, anashangazwa<br />
na kitendo cha serikali kushindwa<br />
kumuwezesha mkulima mdogo kuwa<br />
mwekezaji ambaye anawezeshwa<br />
kwa kila hali ili azalishe na mazao<br />
yake yanunuliwe kwa bei nzuri<br />
ambayo itamuwezesha kurudisha<br />
gharama zote na akapata faida<br />
stahiki, kwani hii ingekuwa ndiyo<br />
njia pekee ya kuboresha maisha<br />
ya wananchi wa vijijini badala ya<br />
kuwaachia wajitafutie kama kuku<br />
wa kienyeji.<br />
Alisema changamoto nyingine<br />
inayowakabili wakulima ni ushuru<br />
na kodi. Akasema pamoja na<br />
serikali kuondoa kodi ndogo ndogo<br />
zilizokuwa kero kwa wananchi,<br />
lakini bado Halmashauri nyingi<br />
zimezirudisha kodi hizi ambazo<br />
hatima yake ni kumbebesha mzigo<br />
mkulima na kuzidi kumpunja mapato<br />
yake. “Kwenye maeneo mengi<br />
hivi sasa kusafirisha mazao kutoka<br />
kijiji au kata moja kwenda nyingine<br />
inabidi kulipa ushuru kwenye mageti.<br />
Kadri unavyosafirisha mbali ndivyo<br />
unavyokutana na mageti mengi<br />
ambayo inabidi kulipa ushuru. Pamoja<br />
ya kwamba ushuru unalipwa na<br />
msafirishaji, lakini hatimaye mkulima<br />
atapewa bei ndogo ili kufidia ushuru<br />
anaotozwa msafirishaji, na hivyo<br />
mkulima kuzidi kudidimia.”<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 3<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11
Inatoka uk. wa 2<br />
“Kodi hizi haziishii kwenye<br />
mazao peke yake. Hata pale ambapo<br />
wakulima wadogo tumejitahidi<br />
kuanzisha vyombo vyetu vya<br />
fedha kama SACCOS, Mamlaka ya<br />
Mapato Tanzania (TRA) wanakuja<br />
na kuchukua kodi kutoka katika<br />
vyombo hivyo japokuwa SACCOS<br />
hulipa ada kwenye mamlaka<br />
zinazosimamia ushirika nchini. Kwa<br />
nini vyombo vyetu hivi visipewe<br />
msamaha wa kodi kama tunavyosikia<br />
na kushuhudia wawekezaji wa<br />
nje wakipewa misamaha ya kodi<br />
kwa vipindi maalumu?” alihoji Bibi<br />
Kibena.<br />
Kilimo na Muundo wa<br />
Uchumi<br />
Mhadhiri Msaidizi katika Chuo<br />
Kikuu cha Dar es Salaam katika<br />
Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala<br />
wa Umma Bw. Bashiru Ally<br />
anasema kwa asilimia kubwa kilimo<br />
kimechangia maendeleo makubwa<br />
nchini.<br />
“Mambo mengi ya maendeleo<br />
yaliyofanyika hapa nchini ndani ya<br />
miaka 50 ni matunda ya kilimo<br />
kwa sababu nchi yetu ni ya kilimo<br />
na kilimo ndio kinachochangia<br />
maendeleo kwa asilimia kubwa<br />
kwani kinatupatia chakula pamoja<br />
na fedha za kigeni.”<br />
Hata hivyo akichambua historia ya<br />
kilimo hapa nchini Bw. Ally anasema<br />
kuanzia miaka ya 1961-1985 dola<br />
ilimiliki shughuli zote ikiwemo Vyama<br />
vya Ushirika vilivyoanzishwa kwa<br />
malengo ya kuwasaidia wakulima<br />
ambavyo vilimilikishwa kwenye dola<br />
na hivyo kupoteza nguvu yake na<br />
kufanya hali ya mkulima kuendelea<br />
kuwa duni.<br />
Anataja kuwa jambo ambalo<br />
halikutokea katika miaka hii 25 ya<br />
mwanzo ni kutovamiwa kwa ardhi<br />
ya wakulima ingawaje kilimo chetu<br />
kiliendelea kuwa cha kawaida. “Katika<br />
kipindi hicho serikali haikufungua<br />
milango kwa wawekezaji wakubwa<br />
badala yake yenyewe ilianzisha<br />
mashamba na kuyaendesha,<br />
lakini kutokana na kukosa ufanisi<br />
wa kuyatunza mashamba hayo<br />
yalipoteza thamani yake.”<br />
Amesema katika muundo wa<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />
uchumi wa sasa, msukumo mkubwa<br />
upo katika uwekezaji, ambapo ardhi<br />
inayomilikiwa na wakulima wadogo<br />
serikali imeigawa kwa wawekezaji<br />
wakubwa kitendo ambacho kimeleta<br />
athari kubwa kwa wakulima wadogo<br />
kutokana na mfumo wao wa<br />
uzalishaji kuvurugwa.<br />
Bw. Ally akazungumzia jinsi<br />
ambavyo katika miaka ya hivi<br />
karibuni serikali imeshindwa<br />
kuweka muunganiko baina ya<br />
sekta ya uzalishaji (kilimo) na<br />
sekta ya viwanda, kwani wakulima<br />
wanazalisha malighafi lakini viwanda<br />
vya kumalizia kutengeneza bidhaa<br />
za kupeleka sokoni havipo. Viwanda<br />
vingi vilivyokuwepo awali vimefia<br />
mikononi mwa walafi wachache,<br />
mfano kiwanda cha magunia, ngozi<br />
na nguo.<br />
Anasema mwelekeo wa uzalishaji<br />
umekuwa ni wa kuuza nje na si<br />
ndani ya nchi kwani bidhaa nyingi<br />
zinazopatikana katika maduka mengi<br />
nchini si mazao yanayolimwa hapa<br />
nchini bali yanayotoka nje kitendo<br />
ambacho kinachangia kuua soko la<br />
ndani na kuacha mazao ya wakulima<br />
wadogo yakiozea shambani na<br />
kushuka thamani.<br />
“Hivi sasa tunajiandaa kuruhusu<br />
wakulima wakubwa kutoka nje<br />
kuzalisha mazao ya chakula ili<br />
kukidhi mahitaji ya ndani na nje<br />
ya nchi badala ya kuwawezesha<br />
wakulima wetu kuzalisha mazao<br />
hayo ili waweze kuwa na kilimo<br />
endelevu, jambo ambalo linaweka<br />
hatarini mustakabali wa wakulima<br />
wadogo. Mfano halisi ni wa maeneo<br />
makubwa ambayo ni vyanzo vizuri<br />
vya uzalishaji kama vile bonde la<br />
Rufiji na mikoa ya Rukwa na Kigoma,<br />
huku kote ni kwamba sauti za<br />
wakulima wadogo hazisikiki na wala<br />
hazionekani kuwa ni za muhimu.<br />
Suala la sauti za wakulima<br />
kutosikika lilimgusa pia Mtendaji<br />
Mkuu wa Mfuko wa Mwalimu<br />
Nyerere Bw. Joseph Butiku<br />
wakati akifungua Kongamano la<br />
Miaka 50 ya Uhuru na Mustakabali<br />
wa Wakulima Wadogo lililoandaliwa<br />
na <strong>MVIWATA</strong> Disemba 6, <strong>20</strong>11 mjini<br />
Morogoro, alisema wakulima sauti<br />
zao hazisikiki kwa sababu ya uoga<br />
na ujinga walionao. Alisema ujinga ni<br />
MADA MAALUM<br />
kigezo kikubwa kinachowakwamisha<br />
wasifanikiwe. Akashauri chombo cha<br />
<strong>MVIWATA</strong> kilenge kuwapa wakulima<br />
nguvu ili waew na vitendo vya pamoja<br />
na si sauti ya pamoja tu. “<strong>MVIWATA</strong><br />
muwajengee wakulima uwezo wawe<br />
na nguvu na vitendo vya pamoja<br />
vitakavyowezesha kuwaita viongozi<br />
wa Serikali ili kuongea nao na kutoa<br />
mapendekezo yao na wakulima<br />
msiwe waoga wala wanyonge kwani<br />
huwezi kuwa mwoga na ukatafuta<br />
ukweli au kutoa ushauri na kujenga<br />
taifa linalojiamini.”<br />
Aliwahimiza wakulima kwamba<br />
watafanikiwa tu iwapo wataunda<br />
umoja na mshikamano thabiti ili<br />
kwamba wakisema jambo linasikika<br />
na serikali inajibu haraka.<br />
Aliwasihi wajumbe wa kongamano<br />
hilo wanapotafakari miaka 50 ya<br />
uhuru na mustakabali wa mkulima<br />
warejee historia ambapo alisema<br />
kuwa nchi ya Tanzania ni ya makundi<br />
makuu mawili yaani wakulima na<br />
wafugaji na kundi la wafanyakazi,<br />
ambapo kundi la wakulima na<br />
wafugaji linabeba idadi kubwa ya<br />
Inatoka uk. wa Tahariri<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 4<br />
Serikali iwasaidie<br />
wakulima...<br />
Kwa sababu hakuna juhudi zenye<br />
dhamira ya kweli za kupambana<br />
na rushwa zaidi ya maigizo<br />
tunayoyaona sasa basi ni dhahiri<br />
kuwa kuna juhudi hafifu mno za<br />
kupambana na maadui wa uhuru<br />
wa kweli ambao ni umasikini,<br />
maradhi na ujinga.<br />
Kwa kuwa rushwa imekua injini<br />
ya kuchochea ujinga na maradhi<br />
ambayo nayo yamechangia<br />
kukuza umasikini kwa taifa hili,<br />
basi ni ukweli ulio wazi kuwa<br />
rushwa pia ni kihunzi cha uhuru<br />
wa kweli na maendeleo ya kweli<br />
kwa Tanzania.<br />
Wakati tunasherehekea<br />
miaka 50 ya uhuru wa Tanzania<br />
Bara, tunaitaka serikali ionyeshe<br />
dhamira kubwa ya kusukuma<br />
zaidi maedeleo ya kilimo nchini ili<br />
kwenda sambamba na matarajio ya<br />
kujikwamua kiuchumi na kuliletea<br />
taifa maendeleo ya kweli.<br />
3
MADA MAALUM<br />
Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara...<br />
Inatoka uk. wa 3<br />
wananchi wanaolijenga Taifa la<br />
Tanzania. “Serikali inatoka miongoni<br />
mwa makundi hayo mawili kwa hiyo<br />
inabidi kupanga pamoja ili kujua<br />
tuendako baada ya miaka hii 50 ya<br />
uhuru.”<br />
Bw. Butiku alienda mbali zaidi<br />
na kushauri wakulima watumie<br />
mamlaka waliyonayo kwa kuinyima<br />
kura kwenye uchaguzi mkuu ujao<br />
wa <strong>20</strong>15 serikali ya chama tawala<br />
kilichopo madarakani iwapo<br />
itaendelea kutowasikiliza.<br />
“Ninyi nyote ni wapiga kura,<br />
madaraka na mamlaka ya nchi hii<br />
yanatoka kwenu, iambieni CCM<br />
chama changu mimi kwamba kama<br />
sheria ya vijiji na mambo mengine<br />
yanayotukera hayatekelezwi, <strong>20</strong>15<br />
hatuwapigii kura,… mimi sitaki kufa<br />
katika fujo tumekulia katika amani…<br />
kauli yangu ni kauli ya demokrasi na<br />
si uchochezi, ” alisisitiza Bw. Butiku.<br />
Je bado wakulima ni sehemu<br />
ya wamiliki wa uchumi wa<br />
taifa letu?<br />
Akizungumza kwenye Kongamano<br />
hilo lililoandaliwa na <strong>MVIWATA</strong> Dkt.<br />
Azavieli Lwaitama wa Chuo Kikuu<br />
cha Dar Es Saalam, alisema kuwa<br />
katika kipindi cha mwaka 1961 hadi<br />
1985 ni kweli tulithubutu, tuliweza<br />
na kusonga mbele kwa kuwasaidia<br />
wakulima kwa kuanzisha Azimio<br />
la Arusha na viwanda mbalimbali<br />
vilivyotumia malighafi za wakulima.<br />
Lakini kuanzia mwaka 1985 hadi<br />
<strong>20</strong>11 nchi imekuwa na juhudi kubwa<br />
katika kuwakaba koo wakulima na<br />
kuwapora ardhi yao.<br />
Alisema wakulima wadogo<br />
wametupwa kando katika kumiliki<br />
uchumi na kuonekana kama ni<br />
wasumbufu. “Kwa kipindi hiki<br />
kauli mbiu inatakiwa isomeke<br />
“tumethubutu, tumeweza<br />
na tunasonga mbele katika<br />
kuwakaba koo wakulima.”<br />
Alieleza kuwa Uhuru wa nchi yoyote<br />
unatokana na umiliki wa ardhi na<br />
ndio maana watu wanapigana kila<br />
siku kudai ardhi na kuongeza kuwa<br />
kwa sasa wakulima ndio wanapaswa<br />
kujitafakari Je, wamethubutu,<br />
wameweza na kusonga mbele katika<br />
4<br />
kutetea haki zao?<br />
Alishauri kuwa ili kuweza<br />
kukabiliana na hali hii na kuzidi<br />
kusonga mbele inabidi wakulima<br />
waimarishe umoja wao, wapate<br />
elimu ya kujitegemea na sera za ardhi<br />
zifundishwe kuanzia mashuleni.<br />
Kwa upande wake Kanali<br />
(Mst) Anatory Tarimo, Mkuu<br />
wa mkoa mstaafu aliwaambia<br />
washiriki wa Kongamano hilo<br />
kuwa Katiba ya nchi haifuatwi<br />
ndiyo maana hawafaidi matunda ya<br />
uhuru na ni jukumu la wakulima<br />
kuhakikisha inafuatwa na hatua hizo<br />
zinaweza kuwa hata za kisheria.<br />
Aliwashauri wakulima kujiendeleza,<br />
kuwa wabunifu na kujenga uwezo<br />
wa kujiamini huku akisisitiza kuwa<br />
jukumu la kumuendeleza mkulima<br />
mdogo ni la mkulima mwenyewe<br />
na wasitegemee watu kutoka nje au<br />
viongozi waliopo madarakani.<br />
Alisema wakulima wanapaswa<br />
kujipanga katika vikundi na mitandao,<br />
kuwa wabunifu, wazifahamu sheria za<br />
ardhi na wawe na mfumo imara wa<br />
masoko utakaowezesha kumuuzia<br />
mlaji wa mwisho na kuwaondoa<br />
madalali ambao ndio wamekuwa<br />
wakifaidi jasho la wakulima.<br />
Bibi Veronica Sophu ni<br />
Makamu Mwenyekiti wa <strong>MVIWATA</strong><br />
taifa na mkulima mdogo kutoka kijiji<br />
cha Madibila wilaya ya Mbarali yeye<br />
anasema pamoja na kubaki masikini<br />
na kutotambuliwa na serikali katika<br />
kipindi cha miaka hii 50 ya uhuru<br />
wakulima wameendelea kulisha nchi<br />
yetu.<br />
Katika mawasilisho yake kwenye<br />
kongamano hilo Bibi Sophu alisema<br />
anasikitishwa na jinsi ambavyo<br />
wakulima hawathaminiwi na<br />
wanadharauliwa wakati wao ndio<br />
wanalisha taifa. Alisema wakulima<br />
hivi sasa wananyanyasika wanaishi<br />
kwa hofu katika nchi yao kama<br />
wakimbizi kutokana na vitendo<br />
wanavyofanyiwa na serikali.<br />
Bw.Thomas Laizer ambaye<br />
ni Afisa Ushawishi na Utetezi wa<br />
<strong>MVIWATA</strong> yeye anasema kutokana<br />
na historia ya nchi yetu wakulima<br />
wamenufaika kwa uchache sana na<br />
matunda ya uhuru.<br />
Anasema kufa kwa viwanda<br />
vilivyojengwa katika awamu ya<br />
kwanza ya utawala, kumepoteza<br />
fursa nzuri ya masoko kwa mazao<br />
ya wakulima. Jambo jingine anasema<br />
ni kushuka kwa suala la elimu na<br />
huduma muhimu za kijamii. “Kila<br />
mahali wananchi wanashuhudia hilo<br />
na ni vigumu kwa mkulima mdogo<br />
kuakisi faida za uhuru huo katika<br />
maisha yake ya kawaida.”<br />
Bw. Ladslaus Bigambo,<br />
Mratibu wa <strong>MVIWATA</strong> Ruvuma<br />
anasema “kuna ukweli usiopingika<br />
sasa kuwa Tanzania imepoteza<br />
mwelekeo wa karama ya uongozi<br />
wenye utashi wa kisiasa unaoweza<br />
kuwaelekeza watu kwenye<br />
mafanikio.<br />
Kwa upande mwingine watanzania<br />
wengi hawaoni uchungu wa dhuluma<br />
wanayofanyiwa katika nchi yao,<br />
hawapo tayari kuuliza ama kufuatilia<br />
jambo lolote, hata kama lina athiri<br />
maisha yao. Mfano wakazi Loborsoit<br />
na Ngage wilaya ya Simanjiro mkoani<br />
Manyara wamezungukwa na mbuga<br />
ya wanyama inayotumiwa kwa<br />
uwindaji wa kitalii, lakini wakazi wa<br />
vijiji hivyo hawafuatilii kudai mapato<br />
ambayo yangestahili kurejeshwa<br />
kwao ili wao kama walinzi wa<br />
wanyama hao wafaidi matunda.”<br />
Bibi. Mary Nsemwa, mkuu<br />
wa Idara ya Ushawishi na Ujenzi wa<br />
Nguvu za Pamoja katika Mtandao<br />
wa Jinsia Tanzania (TGNP), anasema<br />
asilimia kubwa ya wananchi<br />
wanaojishughulisha na kilimo hiki<br />
ni wanawake ambao hawashirikishi<br />
katika maamuzi ngazi ya kaya<br />
hususani kiasi gani kizalishwe, kiasi<br />
gani kiuzwe, na kwa bei gani na kiasi<br />
gani kinaitosha familia kwa chakula,<br />
vitendo ambavyo vinamfanya<br />
mwanamke huyu kukosa thamani<br />
katika jamii.<br />
Katika miaka hii 50 baada ya uhuru<br />
wanawake wakulima hawawezi<br />
kujivunia kuwa wamenufaika na<br />
lolote kutokana na kasoro mbalimbali<br />
zinazojitokeza katika utaratibu wa<br />
uongozi uliopo kwani hawashiriki<br />
katika kutunga sera na sheria za<br />
nchi, kushiriki katika vyombo vya<br />
maamuzi na kupewa uhuru wa kutoa<br />
maoni na mapendekezo yao katika<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 5<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11
Inatoka uk. wa 4<br />
kupanga mikakati ya maendeleo<br />
itakayowasaidia.<br />
Ametaja mambo kadhaa ya<br />
kufanyiwa marekebisho kuwa ni<br />
pamoja na kuongeza ushiriki wa<br />
wanawake katika vikao vya maamuzi<br />
“wanaume waliobadilika na kuelewa<br />
vyema suala hili la usawa huwasaidia<br />
wanawake katika kutekeleza<br />
majukumu yao.”<br />
Akizungumzia suala la Bajaji<br />
kutumika kusafirisha wajawazito<br />
katika kipindi hiki huku kukiwa<br />
hakuna miundombinu ni kuwafanyia<br />
dhihaka kundi hili la wanawake.<br />
Bw. Marcossy Albanie wa<br />
Kituo cha Msaada wa Sheria na Haki<br />
za Binadamu na pia mchambuzi<br />
wa masuala ya kisiasa na uchumi<br />
yeye alianza kwa kushangazwa na<br />
kitendo cha mkulima kuwekewa<br />
masharti lakini biashara na viwanda<br />
vimeendelea kuwa huru vitendo<br />
ambavyo vimezuia wakulima wadogo<br />
kuwa washindani katika soko huria.<br />
Kwa sasa wakulima wanawekewa<br />
vizingiti kuhusu nini cha kuzalisha, na<br />
wauze wapi na cha kushangaza zaidi<br />
ni kwamba wakuu wa wilaya wana<br />
sauti ya kuwaamrisha wakulima<br />
kuzalisha kwa kiwango fulani lakini<br />
hawasemi kiwanda gani kiwekwe<br />
hapo kitumie mazao yanayozalishwa<br />
kitendo ambacho kinampa hasara<br />
mkulima. Kwa ujumla wakulima ni<br />
kundi lililoachwa nyuma na hata<br />
akizungumza watu wanampuuzia.<br />
Anasema ili wakulima wafaidi<br />
matunda ya uhuru wanahitaji uhuru<br />
wa pili ambao utamkomboa mkulima<br />
na changamoto hizi zinazomkabili<br />
na haya yote yanawezekana endapo<br />
tutabadilisha mfumo wa uongozi<br />
uliopo hapa nchini ambao utatoa<br />
fursa sawa, utalenga huduma sawa<br />
na kutambua kwamba kuishi vijijini<br />
ni changamoto kubwa.<br />
Anasema “Mkulima anapaswa<br />
kupewa kiinua mgongo kama<br />
mfanyakazi wa kawaida kwani hata<br />
yeye anachangia katika maendeleo<br />
ya taifa na mfumo huu uliopo ni<br />
kandamizi, ni sawa na wizi wa nguvu<br />
za wakulima.”<br />
Nini kifanyike kumrejesha<br />
mkulima mdogo katikati ya<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />
mfumo wa uzalisaji<br />
Mkuu wa Mkoa Mstaafu wa Morogoro<br />
Bw. Stephen Mashishanga,<br />
yeye alipendekeza kilimo cha<br />
mkataba kipigwe marufuku nchini<br />
kwa kuwa ni utumwa mpya na<br />
ukoloni mambo leo unaotunyemelea<br />
watanzania.<br />
Akapendekeza pia kila mwananchi<br />
amilikishwe ardhi kisheria, kuongeza<br />
uzalishaji katika kila maeneo na<br />
kuimarisha soko la ndani na nje<br />
ya nchi, kuimarisha huduma za<br />
ugani vijijini na wakulima washiriki<br />
kikamilifu katika kuandaa katiba<br />
mpya na <strong>MVIWATA</strong> iendelee kuwa<br />
mtetezi wa kweli wa mkulima<br />
mdogo.<br />
Mwanasiasa Mkongwe nchini<br />
Dkt Chrisant Mzindakaya<br />
yeye anashauri serikali kuweka<br />
kipaumbele katika kufanya utafiti<br />
wa kilimo na mifugo na kuzitumia<br />
tafiti hizo na akasisitiza watumie<br />
wataalamu walioko vyuoni ili<br />
kuhakikisha wanafanikisha tafiti hizo<br />
zinazochochea maendeleo.<br />
Kwa upande wake Profesa<br />
Dominic Kambarage wa Chuo<br />
Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA)<br />
anasema ili sekta ya kilimo na mifugo<br />
iendelee lazima turudishe mifumo<br />
ya uwajibikaji na serikali iandae<br />
mikakati ya kudhibiti magonjwa<br />
kwa mifugo na mimea. “Kwenye<br />
tasnia ya ugani, ugani umeharibika<br />
inabidi serikali ijiulize tufanye nini<br />
ili kuwe na tasnia nzuri, njia pekee<br />
ni kuajiri wataalamu toka vyuoni<br />
na kutumia rasilimali vizuri waende<br />
vijijini kufanya kazi bila hivyo kilimo<br />
kwanza hakitafanikiwa.”<br />
Profesa Dominic Kambarage - SUA<br />
“Sekta ya mifugo itakwenda<br />
kama kutakuwa na programu<br />
MADA MAALUM<br />
zinazoonyesha sera na nini<br />
kimefanyika pia ndani yake kuwe<br />
na mgawanyiko wa programu<br />
ndogondogo kwa kila tasinia ya<br />
mifugo kama za kuku, ngombe,<br />
maziwa, kwani hivi sasa serikali<br />
ukiiuliza kuhusu programu za<br />
mifugo wanasema bado ziko jikoni<br />
zinapikwa, huu si mwenendo mzuri,”<br />
alisema Profesa Kambarage kwenye<br />
Kongamano la Maendeleo ya Kilimo<br />
chuoni hapo.<br />
Akizungumzia mwelekeo wa<br />
Chuo Kikuu pekee cha Kilimo (SUA)<br />
juu ya kuleta maendeleo ya kilimo<br />
katika miaka 50 ijayo Profesa<br />
Amon Mattee anasema ni lazima<br />
kuangalia mitaala na mbinu za<br />
ufundishaji ili mafunzo yashabihiane<br />
na uhalisia wa watakachokifanya<br />
wahitimu wamalizapo masomo ili<br />
kuweza kutoa mchango wa haraka<br />
na wa moja kwa moja katika<br />
maendeleo ya sekta ya kilimo.<br />
Pili akashauri utafiti ulenge wadau<br />
katika ngazi mbalimbali za maamuzi<br />
toka kwa mkulima hadi ngazi za<br />
juu kabisa za watunga sera kwani<br />
maendeleo ya kilimo ni matokeo ya<br />
maamuzi katika ngazi mbalimbali.<br />
Dkt. Gabagambi wa SUA<br />
anashauri iwepo programu kabambe<br />
ya kitaifa ya kupima ardhi yote ya<br />
nchi ili kuwa na ramani ya kanda za<br />
matumizi bora ya ardhi. Ramani hiyo<br />
ionyeshe eneo gani litatumika kwa<br />
kazi gani hususan katika shughuli za<br />
binadamu kwa uhai wa nchi hii.<br />
Kadhalika anashauri iundwe<br />
bodi ya nafaka (National Cereal<br />
Board) kushughulikia mazao hayo<br />
nchini. Jukumu kuu la bodi liwe<br />
ni kuhamasisha uzalishaji wa<br />
mazao haya kwa lengo la kuwa na<br />
mlipuko wa nafaka (cereal boom)<br />
utakaosaidia taifa kujitosheleza kwa<br />
chakula (Tanzania kuwa ghala la<br />
nafaka la nchi za mashariki na kusini<br />
mwa Afrika), kupata fedha ya kigeni,<br />
na kuchochea kasi ya kukua kwa<br />
uchumi. Na akashauri pia liundwe<br />
baraza la ushauri la kitaifa katika<br />
sekta ya kilimo lenye jukumu la<br />
kufanya tafakuri ya kina juu ya nini<br />
kifanyike, kwanini kifanyike, wapi<br />
kifanyike, namna gani kifanyike, lini<br />
na kwa muda gani kifanyike, na kwa<br />
matokeo gani.<br />
5
MADA MAALUM<br />
6<br />
Maoni ya wakulima<br />
Kwa sehemu kubwa maoni<br />
yaliyotolewa na wakulima<br />
kuhusiana na mustakabali<br />
wao kwenye miaka 50 ijayo<br />
yameakisi hofu kubwa waliyonayo<br />
ya kusukumwa kando kwa<br />
kuporwa ardhi na changamoto ya<br />
masoko ya mazao.<br />
Wengi wao wameonyesha jinsi<br />
ambavyo mifumo ya uzalishaji<br />
inavurugwa pale wakulima<br />
wanapoondolewa kwenye ardhi<br />
waliyokuwa wakilima tangu enzi<br />
za mababu zao na kugawiwa kwa<br />
wawekezaji. Baadhi ya wakulima<br />
wamepigwa, kujeruwiwa na hata<br />
kufungwa gerezani pale walipoendelea<br />
kudai haki yao. Wakati mwingine mazao<br />
ya wakulima kung’olewa shambani,<br />
mifugo kuuawa, kuchomwa moto<br />
nyumba zao au mifereji ya maji hasa<br />
maeneo ya umwagiliaji kufukiwa na<br />
hivyo wakulima kushindwa kuendelea<br />
na kilimo. Wakulima wafuatao<br />
wanashuhudia haya kuhusiana na hali<br />
halisi ya mkulima kiuchumi, kielimu,<br />
kisiasa na hata kijamii.<br />
Bibi.Lydia Ruliho ni mkulima<br />
mdogo kutoka mkoani Rukwa<br />
anasema kuwa katika miaka 50 ya<br />
uhuru elimu vijijini bado ni kitendawili<br />
kutokana na serikali kutotilia mkazo<br />
katika suala la elimu kwa wananchi wa<br />
maeneo ya pembezoni, huku akitolea<br />
mfano wa mkoa wa Rukwa kwamba<br />
mwaka huu wa <strong>20</strong>11 wanafunzi<br />
wa darasa la saba katika vijiji 14<br />
vya mwambao wa ziwa Tanganyika<br />
hawakufanya mitihani ya darasa la<br />
saba kutokana na miundombinu<br />
ya maeneo hayo kuwa mibovu<br />
na wakati mwingine kutokuwepo<br />
kabisa, miundombinu hiyo ni pamoja<br />
na ukosefu wa madaraja ambao<br />
uliwafanya wasimamizi wa mitihani<br />
hiyo kuogopa kuvuka ziwani kwa<br />
kutumia mitumbwi kuelekea katika<br />
vijiji hivyo kutokana na jografia ya<br />
maeneo hayo ilivyo.<br />
“Tatizo hili tumeliona hapa<br />
Rukwa kwa viijiji hivyo lakini Je hali<br />
ikoje kwa mikoa yote ya Tanzania, na<br />
ni vijijii vingapi vinakosa elimu nchini<br />
kila mwaka? Hii bado ni changamoto<br />
kubwa inayoikabili nchi yetu, hivyo<br />
mkulima mdogo bado hajafaidika na<br />
uhuru uliopo kwani yeye anaonekana<br />
kama vile si Mtanzania na wala hana<br />
haki yoyote,” anasema Bibi Ruliho<br />
ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti<br />
Mstaafu wa <strong>MVIWATA</strong>.<br />
Bibi. Kesia Laiser kutoka<br />
Monduli anasema kwamba pamoja na<br />
wao kuwa miongoni mwa Watanzania<br />
ambao wako huru, wakulima wadogo<br />
bado wanakabiliwa na changamoto<br />
zinazowakwamisha katika harakati<br />
zao za kujikomboa na umasikini na<br />
miongoni mwa changamoto hizo ni<br />
suala la gharama kubwa za pembejeo<br />
ambazo ni vigumu kwa mkulima<br />
mdogo kuzimudu.<br />
Bibi. Kesia Laiser<br />
Akizungumzia suala la elimu<br />
Bibi. Laiser amesema kuwa watoto<br />
wa wakulima ndio wanaosoma<br />
katika shule za kata ambazo bado<br />
ni duni kutokana na shule hizo<br />
kukosa walimu wa kutosha na zana<br />
za kufundishia ikiwemo vitabu na<br />
maabara. “Kinachotuumiza zaidi ni<br />
kuona watoto wa viongozi na matajiri<br />
hawasomeshwi katika shule hizi hali<br />
ambayo inawafanya wakulima wadogo<br />
wahisi kuwa bado wako katika utawala<br />
wa kikoloni kwani bado hawajafaidi<br />
matunda ya uhuru wa nchi hii”.<br />
Bibi. Fatuma Kimolo toka<br />
kijiji cha Gidoma, kata ya Galapo,<br />
Babati mkoa wa Manyara anasema<br />
Wakulima wadogo hawajapata bado<br />
matunda ya uhuru wa nchi hii kwa<br />
sababu linapokuja suala la uwekezaji<br />
wakulima wadogo hatushirikishwi<br />
na wawekezaji huongea na serikali<br />
kuu na kisha utekelezaji unafanyika<br />
ambapo mara nyingi wakulima<br />
wadogo huhamishwa bila ya kuwa na<br />
uhakika wa mahali wanapopelekwa.<br />
Kutoka Arusha Bibi. Ruth<br />
Paul anaeleza kwamba katika<br />
miaka 50 ya uhuru wakulima na<br />
wafugaji wanazidi kunyanyasika<br />
badala ya kusaidiwa, mifugo yao<br />
haina dhamana na hakuna masoko<br />
yanayoeleweka ya kuuzia mifugo<br />
hiyo jambo linalozidi kuzorotesha<br />
hali zao kiuchumi.<br />
Ameeleza kwamba ili wakulima<br />
wafaidi matunda ya uhuru ni<br />
lazima katiba ya nchi iwatambue<br />
na kuwalinda wakulima wadogo na<br />
maslahi yao ndipo hata wawekezaji<br />
watawaheshimu wakulima na wafugaji<br />
wadogo tofauti na sasa ambapo<br />
wanawaona kama vile manamba.<br />
Ameongeza kuwa wazawa<br />
wanaoishi jirani na hifadhi za taifa<br />
za wanyama hawafaidiki na raslimali<br />
hizo licha ya kuwalinda wanyama hao<br />
ambao huliingizia pato kubwa taifa.<br />
Bibi. Anna Mesoloi ni mfugaji<br />
kutoka Monduli na anaeleza kwamba<br />
wakulima wadogo hawajafaidi kitu<br />
chochote zaidi ya kusikiliza kauli<br />
mbiu mbalimbali zinazotangazwa<br />
kila siku kwenye vyombo vya habari<br />
ikiwemo hii ya Kilimo kwanza<br />
ambayo hawaielewi na hawafahamu<br />
inafanya nini licha ya kwamba wao<br />
ndio walengwa wakuu wa kauli hiyo.<br />
Amesema haya ni matokeo ya<br />
mfumo wa uongozi uliopo kuanzia<br />
ngazi za chini hadi za juu ambao siyo<br />
shirikishi. Kwa kipindi hiki anasema<br />
anachojivunia yeye ni kubahatika<br />
kuwa mwanachama wa <strong>MVIWATA</strong><br />
ambayo imemwezesha kupata elimu<br />
na mwanga wa kudai haki.<br />
Amesema hali ya upatikanaji<br />
wa mikopo ya elimu ya juu kwa<br />
mtoto wa mkulima ni tatizo kwani<br />
wengi wao huwa hawalewi nini cha<br />
kufanya ili waweze kupata nafasi<br />
hiyo ambayo kwao ni nafasi kubwa<br />
na ya kipekee ya kujiendeleza<br />
kielimu lakini cha kusikitisha ni<br />
kwamba wakati mwingine fomu<br />
zao huwa hazihangaikiwi kitendo<br />
kinachowafanya wazidi kurudi nyyma<br />
kielimu na kuachwa kimaendeleo.<br />
Bibi. Mwanaidi Ally kutoka<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 7<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11
Inatoka uk. wa 6<br />
wilaya ya Uyui mkoani Tabora<br />
aneleza kwamba katika kipindi hiki<br />
wakulima wadogo bado wana uhuru<br />
bandia unaowanufaisha wachache<br />
ambao hufaidi jasho la wakulima<br />
na kuwaacha wenyewe bila kitu.<br />
Amefafanua kwamba umasikini<br />
unaowakabili wakulima wengi ndiyo<br />
chanzo cha watoto wao kupata<br />
elimu duni na kukuza kundi la<br />
wajinga miongoni mwao.<br />
Bibi. Hidaya Chikawe kutoka<br />
Lindi anasema wakulima katika<br />
miaka hamsini iliyopita wamepata<br />
maendeleo kidogo ingawaje bado<br />
wanakabiliwa na changamoto<br />
mbalimbali katika shughuli yao<br />
ya kilimo. Changamoto kubwa<br />
inayowakabili wakulima ni ukiritimba<br />
wa baadhi ya viongozi katika vyama<br />
vya ushirika hasa vya zao la korosho<br />
huko kwao ambao hukwamisha<br />
maendeleo ya wakulima kwa sababu<br />
wao pia hufanya kazi zao kama<br />
madalali na hivyo kunufaika na jasho<br />
la wakulima badala ya kuwasaidia<br />
kuuza mazao yao kwa bei nzuri ili<br />
waweze kupata faida.<br />
Bw. Ponsian Ngaiza kutoka<br />
Kagera anasema katika kipindi<br />
cha miaka 50 ya Uhuru maisha ya<br />
wakulima wengi yamezidi kuwa duni<br />
kutokana na hali halisi ya uchumi<br />
ilivyo hivi sasa ambapo bidhaa nyingi<br />
zinapanda bei siku hadi siku huku<br />
uchumi wa wakulima wengi ukizidi<br />
kudorora kutokana na wao kukosa<br />
masoko ya uhakika ya mazao yao<br />
huku akitolea mfano wa bei ya kilo<br />
ya kahawa katika mkoa wa Kagera<br />
kuwa shilingi 1300 ukilinganisha na<br />
kilo moja ya sukari shilingi <strong>20</strong>00.<br />
“Katika miaka hii 50 wananchi<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />
wengi wa vijijini hawakupata fursa<br />
ya elimu kuhusu masuala mbalimbali<br />
yanayogusa maisha yao kila siku<br />
kama vile siasa, uchumi na hata haki<br />
zao, nashauri katika awamu ijayo<br />
mambo haya yapewe kipaumbele,”<br />
anasema Bw. Ngaiza ambaye pia ni<br />
Mwenyekiti wa <strong>MVIWATA</strong> Kagera.<br />
Bw. Paulo Mossama<br />
kutoka Tarime mkoani Mara<br />
anasema anachoweza kujivunia ni<br />
kwamba katika miaka 50 wakulima<br />
wamenufaika kwa kujifunza mambo<br />
mbalimbali kama vile kilimo cha<br />
kisasa lakini ni kwa asilimia ndogo<br />
sana ukilinganisha na idadi ya<br />
wakulima waliopo hapa nchini.<br />
Bw. Paul Mossama<br />
Bw. Andrew Chalangwa<br />
kutoka Kasulu, Kigoma anasema<br />
kuwa mkulima amenufaika kidogo<br />
sana kwani bado anatumia nyenzo<br />
duni ya jembe la mkono ilihali katika<br />
nchi nyingine wakulima wanatumia<br />
mitambo ya kisasa ya kilimo.<br />
Changamoto nyingine inayowakabili<br />
ni mabadiliko ya hali ya hewa<br />
ambayo katika miaka 50 ijayo serikali<br />
inapaswa kuweka mikakati madhubuti<br />
kukabiliana na mabadiliko hayo.<br />
Bibi. Deodata Katunga<br />
toka Ruvuma anasema “mkulima<br />
mdogo yuko katikati bado kwani<br />
MADA MAALUM<br />
hajapata faida ya kuridhisha ingawaje<br />
amefunguka macho tatizo kubwa ni<br />
watendaji na viongozi wa serikali<br />
wanaoshindwa kutimiza wajibu wao<br />
na kutaka kujinufaisha kwa jasho la<br />
wakulima.<br />
Bw. Hamad Abdalah<br />
Salimini toka Zanzibar anasema<br />
mkulima mdogo katika kipindi<br />
cha miaka 50 kwa kiasi amefaidika<br />
kwani kwa sasa ana sauti ya kusema<br />
matatizo yake kupitia vyombo kama<br />
<strong>MVIWATA</strong>, ingawa bado anakabiliwa<br />
na changamoto nyingi kama vile<br />
kutokushirikishwa katika vyombo<br />
vya maamuzi.<br />
Miongoni mwa maswali<br />
tuliyokuwa tukijadili kwenye makala<br />
hii ni Je ndani ya miaka 50 ya uhuru,<br />
wakulima wadogo wamefaidi<br />
matunda ya uhuru?<br />
Kimsingi kusema kwamba<br />
hakuna kilichofanyika katika miaka<br />
50 ya uhuru si sawa, kwa sababu<br />
yapo mengi ya maana yaliyofanyika.<br />
Itoshe tu kusema kwamba kwa<br />
yale tuliyopiga hatua tunashukuru<br />
tumefanikiwa kufika hapo. Lakini<br />
ziko changamoto kadhaa ambazo<br />
wadau wameziainisha ambazo<br />
zinadhihirisha ukweli kwamba<br />
hawajafaidi matunda.<br />
Kwa bahati mbaya sana<br />
tunapoadhimisha miaka 50 baada<br />
ya uhuru, taifa letu linashuhudia<br />
matumizi ya ujuzi na utaalamu wa<br />
baadhi ya viongozi na watendaji<br />
wenye tamaa, ulafi na ubinafsi<br />
vikitumika kuzidisha umaskini<br />
miongoni mwa jamii kubwa ya<br />
watanzania ambao ni wakulima.<br />
Katika awamu ya kwanza,<br />
Mwalimu Nyerere hakuishia<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 8<br />
Hawa ndiyo watoto wa wakulima ambao kwa miaka 50 ya uhuru bado wanasoma kwenye mazingira duni na ya dhiki kama ambavyo wengi<br />
wao wanaonekana hawana viatu, hivyo kuhatarisha afya zao<br />
7
MAKALA<br />
MAAZIMIO YA KONGAMANO<br />
Miaka 50 ya Uhuru: Nini Mstakabali<br />
Utangulizi<br />
Ili kuwawezesha wakulima<br />
kutafakari kwa pamoja mabadiliko<br />
katika shughuli za kilimo kwa<br />
kipindi cha miaka 50 tangu uhuru,<br />
<strong>MVIWATA</strong> iliandaa Kongamano<br />
lililowakusanya pamoja wajumbe<br />
zaidi ya <strong>17</strong>0 wakiwemo wakulima<br />
wadogo kutoka mikoa mbalimbali<br />
ya Tanzania, viongozi wa serikali na<br />
wakuu wa mikoa wastaafu, wataalam,<br />
wachambuzi wa sera na wanahabari.<br />
Kongamano hilo lilifanyika<br />
Disemba 6, <strong>20</strong>11 mjini Morogoro,<br />
likiwa na ujumbe usemao “Miaka<br />
50 ya Uhuru: Nini mstakabali wa<br />
wakulima wadogo?”<br />
Malengo ya Kongamano<br />
Malengo yalikuwa yafuatayo:<br />
· Kutafakari mabadiliko katika<br />
kipindi cha miaka 50 tangu<br />
Uhuru na Mustakabali wa<br />
mzalishaji mdogo.<br />
· Kuishauri serikali yetu njia<br />
ya kuendelea kiuchumi bila<br />
kuwasukuma kando wazalishaji<br />
wadogo.<br />
Akizungumza kwenye kongamano<br />
hilo Mkurugenzi Mtendaji wa<br />
<strong>MVIWATA</strong> Bw. Stephen Ruvuga,<br />
alisisitiza kuwa tunapoangalia<br />
mstakabali wa wakulima wadogo<br />
baada ya miaka 50 tusiangalie mbegu,<br />
pembejeo na soko la mazao ya kilimo<br />
tu , bali tuzungumzie mstakabali wa<br />
taifa ikiwemo upatikanaji wa elimu,<br />
huduma za afya, haki ya mkulima,<br />
umiliki wa ardhi pamoja na suala<br />
zima la ulinzi wa mkulima.<br />
Bw. Ruvuga alisema shuhuda<br />
zilizotolewa na washiriki wa kongamano<br />
zinadhihirisha kuwa mfumo wa serikali<br />
unaotumika hivi sasa kuhudumia jamii<br />
kiuchumi umefeli.<br />
Alisema “ni ajabu sana kuona<br />
kuwa ndio aina ya mfumo<br />
tunaoukimbilia, kuushangilia na<br />
kuupigia vigelegele, kwa mfano<br />
tunashangilia na kutunga nyimbo<br />
kuhusu Kilimo Kwanza, wakati ni<br />
mfumo ulioletwa kutubomoa sisi<br />
wakulima, tunashangilia kwa kutojua<br />
na ndiyo maana naunga mkono kauli<br />
ya Mzee Butiku kwamba ujinga ni<br />
8<br />
wa wakulima wadogo?<br />
adui yetu nambari moja.”<br />
Alisema ni wajibu wa wakulima<br />
kutumia fursa ya kusanyiko kama<br />
hilo kujifunza, kutafakari na kuchukua<br />
hatua na kuongeza kuwa <strong>MVIWATA</strong><br />
isingependa kuendelea kusikia<br />
wakulima wakisubiri ama kutegemea<br />
zaidi nguvu za nje kuliko kuthamini<br />
nguvu na uwezo walio nao wenyewe<br />
kwanza katika kupigania haki zao.<br />
Alisema kuwepo kwa watu<br />
mashuhuri kama mgeni rasmi Bw.<br />
Maoni ya wakulima...<br />
Inatoka uk. wa 7<br />
kukemea mataifa makubwa pekee<br />
yaliyotunyonya, bali alikemea pia<br />
viongozi wa ndani ya Tanganyika<br />
ambao nia zao binafsi zilikuwa<br />
zinakinzana na maendeleo ya nchi<br />
yetu. Mwalimu hakusita kuanika<br />
udhaifu, uchafu na tamaa za viongozi<br />
wasio waadilifu na akasisitiza kuwa<br />
watu hawa wasipewe uongozi.<br />
Mwalimu alipata kusema kwamba<br />
wasomi wachache waliobahatika<br />
kupata fursa hiyo kwa kutumia kodi<br />
za wananchi ni lazima wajue wana<br />
wajibu wa kwenda kuwatumikia<br />
wananchi kwa moyo.<br />
Mwalimu Nyerere pia alikuwa<br />
mtu wa mfano, alikuwa na shamba<br />
lake kule Butiama, shamba la<br />
Mwalimu lilikuwa mfano kwa<br />
wanakijiji wenzake, ukubwa wa<br />
shamba hili la mwalimu haukuwa<br />
nusu ya ardhi ya kijiji, bali alichukua<br />
sehemu kidogo ili kila mwanakijiji<br />
mwenye nia ya kufanya kilimo naye<br />
apate ardhi.<br />
Hapa utaona fahari ya Mwalimu<br />
Nyerere haikuwa kujilimbikizia<br />
mali, ndio maana uwepo wa<br />
Tanzania ulimhitaji sana Baba wa<br />
Taifa Mwalimu Nyerere.<br />
Kila tunapotazama tulipotoka,<br />
hasa baada ya miaka 50 ya uhuru wa<br />
Tanzania Bara, vema tukijua kuwa<br />
mambo yaliyofanywa na waasisi<br />
wa Taifa letu ni mfano hai wa hiki<br />
kinachotokea. Serikali imeshindwa<br />
kusimamia sheria zake ili wajanja<br />
wachache wasitumie maarifa<br />
Joseph Butiku kwenye kongamano<br />
hilo ni kudhihirisha ni jinsi gani<br />
wanawathamini na kuwaunga<br />
mkono wakulima wadogo na hivyo<br />
kuwataka wakulima kujiona kuwa<br />
hawako pekee bali kuna wasomi na<br />
viongozi wa kuwaunga mkono.<br />
Maazimio ya Kongamano<br />
Baada ya mawasilisho na majadiliano<br />
ya kina washiriki kwa kauli moja<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 19<br />
waliyoyapata kuihujumu serikali.<br />
Wataalamu hawa waliofaidi matunda<br />
ya uhuru kwa kusomeshwa, hivi sasa<br />
wanatumika kukandamiza uhuru wa<br />
watanzania wenzao.<br />
Swali linabakia, je baadhi ya<br />
viongozi tulionao ambao fahari<br />
yao ni kujilimbikizia ardhi na<br />
mali wanazowapora wakulima,<br />
wanawatumikia wananchi kwa<br />
moyo?<br />
Bw. Lohay Langay, mkulima<br />
wa Babati mkoani Manyara<br />
anasema “tunaadhimisha miaka<br />
hamsini ya uhuru wa Tanganyika,<br />
tukiwa na matatizo makubwa ya<br />
kiuchumi. Nchi ikiwa haina umeme<br />
wa uhakika, gharama za maisha<br />
zikipanda kila uchao, huku viongozi<br />
tulionao wakiwa wamefumba<br />
macho na masikio, kwa ufupi<br />
wananchi wametelekezwa.”<br />
“Tabia hii ya viongozi wetu<br />
kuishi maisha ya kifahari, bila kujali<br />
kuwa kuna watoto wa wapiga<br />
kura wao hawana madawati,<br />
wazazi wao wanaishi kwa mlo<br />
moja tu, wakulima hawana soko la<br />
mazao yao, wafugaji na wakulima<br />
wanauana kwa kugombea ardhi<br />
ya malisho inasikitisha mno. Binfsi<br />
niseme huku ambako viongozi<br />
wetu wanataka kutupeleka siko<br />
tulikokusudia kwenda, na hii<br />
itakuwa ni hatari tupu tunaifumbia<br />
macho, lakini naamini itatugharimu<br />
sana,” anaonya Bw Langay.<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />
MAKALA<br />
Wanawake wasifanywe wahanga<br />
wa kila tatizo kwenye jamii<br />
Na Gratian Cronery, MUCCoBS<br />
Shinyanga<br />
Asilimia 80 ya watanzania<br />
waishio vijijini, maisha yao<br />
hutegemea shughuli za<br />
kilimo, ufugaji, uvuvi na uwindaji.<br />
Shughuli hizo hufanywa kwa lengo<br />
la kupata pato la kujikimu kwenye<br />
kaya na kwa sehemu kidogo sana<br />
hutumika kwa biashara.<br />
Idadi kubwa ya kundi linalotekeleza<br />
shughuli hizo katika maeneo mengi<br />
ni la wanawake, ingawa mpaka sasa<br />
kundi hili halinufaiki na matokeo ya<br />
shughuli hizo.<br />
Hali hii ya kazi nyingi kuachwa<br />
mikononi mwa wanawake na<br />
manufaa yake kusimamiwa na<br />
wanaume, inatokana na mifumo<br />
iliyopo ambayo imejengwa miaka<br />
ya hivi karibuni licha ya kuwa kuna<br />
watu wanaodai kuwa chimbuko lake<br />
ni mila na desturi zilizorithiwa enzi<br />
za mababu.<br />
Hata hivyo, wanaojenga hoja<br />
kuwa utumikishwaji wa wanawake<br />
vijijini umerithiwa enzi za mababu<br />
wanashindwa kubainisha kuwa enzi<br />
hizo wanawake walifanya kazi zote<br />
za nyumbani na mashambani lakini<br />
wanaume nao walitimiza wajibu<br />
wa kulinda na kutunza familia kwa<br />
mahitaji yote tofauti na ilivyo sasa.<br />
Historia inatuelekeza kuwa babu<br />
zetu walikwenda porini kuwinda na<br />
kuwaletea bibi zetu vitoweo vya<br />
wanyamapori, lakini pia walihakikisha<br />
maghala yanahifadhi chakula cha<br />
kutosha na hifadhi hiyo inalindwa na<br />
kutumika kwa nidhamu.<br />
Bibi zetu majukumu yao yaliishia<br />
kwenye kuchota maji, kukusanya kuni<br />
(ambazo zilikuwa karibu) na kupika<br />
tu huku mahitaji mengine kama ya<br />
unga, mboga yakiwa yametekelezwa<br />
na wazee.<br />
Lakini leo ni wanaume wangapi<br />
wanaoshinda vilabuni na baadaye<br />
kurejea nyumbani kudai chakula<br />
na wanapokikosa wanawadhalilisha<br />
wanawake kwa matusi na vipigo?<br />
Ni wanaume wangapi wanaoshiriki<br />
kuwabaka watoto wa kike wengine<br />
wakiwa ni mabinti zao wa kuwazaa?<br />
Babu zetu hao ambao leo<br />
tunawasingizia kuwa walituachia<br />
mfumo kandamizi kwa wanawake,<br />
hawakuruhusu bibi zetu<br />
wadhalilishwe kwa vitendo vya<br />
ubakaji kama inavyotokea kwenye<br />
jamii yetu leo na yeyote aliyepatikana<br />
na kosa hilo aliadhibiwa vikali.<br />
Tunapoliangalia kundi hili la<br />
wanawake hivi sasa, jambo la<br />
kusikitisha ni kuona lilivyoachwa<br />
nyuma kimaendeleo na kwamba<br />
katika baadhi ya maeneo hata<br />
mchango wao wanaoutoa katika<br />
kuleta maendeleo, jamii haiutambui<br />
kutokana na mifumo mibovu iliyopo<br />
hasa ya kutothamini kazi zao.<br />
Mwanamke anachukuliwa kuwa<br />
ni mtu dhaifu wa kufikiri asiyeweza<br />
kutoa mchango makini hata wa<br />
mawazo katika shughuli yoyote<br />
ile ya maendeleo na kwamba yeye<br />
kazi yake ni kutekeleza tu masuala<br />
yaliyojadiliwa na kuamuliwa.<br />
Hali hiyo ya wanawake kupuuzwa<br />
iko kwenye kila sekta ikiwemo hii ya<br />
kilimo ambapo mwanamke hapewi<br />
fursa ya kutoa ushauri nini kilimwe,<br />
lini na kwa kiasi gani na hata mapato<br />
ya familia yanayotokana na kilimo<br />
matumizi yake yanaamuliwa na<br />
wanaume.<br />
Kutokana na kuwepo kwa<br />
ukandamizwaji huu mwanamke<br />
amejikuta akiwa ni mhanga kwenye<br />
familia na jamii inayoishi kijijini.<br />
Tunapoangalia matatizo kama<br />
ya njaa kwenye familia, anayeteseka<br />
zaidi ni mwanamke ambaye ni mlezi<br />
mkuu wa watoto. Matatizo mengine<br />
yanayoikabili jamii kama vile ukosefu<br />
wa huduma bora za afya, maji, nishati,<br />
elimu na miundombinu hususan<br />
ya barabara mwathirika mkuu ni<br />
mwanamke.<br />
Licha ya serikali kutangaza<br />
kuwa imeboresha huduma za afya<br />
vijijini, lakini bado tunasikia na<br />
kushuhudia matukio ya wajawazito<br />
wakisafirishwa kwenye mikokoteni<br />
ya ng’ombe na baiskeli na serikali<br />
nayo kwa kuwapuuza ikawaletea<br />
usafiri wa bajaji.<br />
Suala la uhaba wa pembejeo za<br />
kilimo, kadhalika nalo ni mzigo kwa<br />
wazalishaji hawa ambao ni wanawake<br />
na wengi wao wanashindwa kumudu<br />
gharama za nyongeza ili waweze<br />
kupata pembejeo hizo.<br />
Hata hivyo, kwa upande mwingine<br />
zipo taasisi na mashirika ambayo<br />
kwa kutambua nafasi ya mwanamke<br />
kwenye jamii yameanza kampeni<br />
kuielimisha jamii, juu ya umuhimu<br />
wa makundi yote kwenye jamii<br />
kushirikiana na kuthaminiana.<br />
Jamii nyingi vijijini zimewaachia wanawake kazi za kulima,kuhudumia mifugo, watoto, kupika,<br />
kuchota maji, kukusanya kuni (ambazo zinapatikana umbali mrefu), afya zao kudhoofu.<br />
9
MAKALA<br />
Kilimo kina nafasi ya kimkakati<br />
ya kukuza uchumi<br />
Na Susuma Susuma<br />
Miaka hamsini ni kipindi<br />
kirefu kwa hali na<br />
mazingira yoyote yale<br />
hasa tunapoihusisha na maendeleo<br />
ya binadamu, jamii viumbe au<br />
jambo lolote lile linaloendelea<br />
kuendana na wakati.<br />
Mwaka huu wa <strong>20</strong>11<br />
tunaposherehekea na kufurahia<br />
kufikia miongo mitano tangu taifa letu<br />
la Tanzania Bara lijipatie Uhuru wake<br />
kutoka kwa wakoloni wa Kiingereza<br />
mwaka 1961, tuna kila sababu ya<br />
kujipima katika nyanja tofauti hasa<br />
zile zinazohusisha maendeleo ya<br />
kiuchumi, kijamii na kisiasa kwa<br />
taifa letu. Yatupasa kujiuliza na<br />
kujitathmini wapi tumetoka, wapi<br />
tulipo na ni wapi tunaelekea.<br />
Kwa<br />
wastani wakulima bado<br />
wanalima vishamba vidogo vidogo, pia<br />
bado wakulima wetu wanatumia zana duni<br />
za jadi kama vile jembe la mkono.<br />
Msingi mkubwa k a t i k a<br />
hili ni kuyaangalia mafanikio<br />
yetu katika harakati za kujiletea<br />
maendeleo tangu tumepata Uhuru<br />
na kuweza kuwa na sababu nzuri ya<br />
kujipongeza kwa hilo. Halikadhalika<br />
ili tuzitendee haki dhamira zetu ni<br />
vyema tukaziangalia changamoto<br />
zilizotukwaza katika kipindi chote<br />
hiki cha miaka hamsini ya Uhuru,<br />
ili basi, tuweze kupangilia mikakati<br />
ya kukabiliana na changamoto hizo<br />
na kuzifanya kuwa ndio sehemu ya<br />
chachu ya kutuletea mafanikio kwa<br />
ukubwa na kiwango cha hali ya juu<br />
zaidi kwa kipindi kijacho cha miaka<br />
hamsini.<br />
Kilimo ndio msingi wa uchumi<br />
wetu na kina nafasi ya kimkakati<br />
katika kuboresha uchumi wa<br />
Tanzania. Sekta ya kilimo ndiyo<br />
10<br />
inayotegemewa na asilimia kubwa<br />
ya Watanzania katika harakati za<br />
kujiletea maendeleo ya kiuchumi na<br />
kijamii na kwa maendeleo ya taifa<br />
letu. Kwa maana hiyo kilimo ndiyo<br />
mhimili wa maisha ya watanzania<br />
wengi.<br />
Lakini kilimo cha Tanzania ndani<br />
ya miaka 50 ya uhuru bado ni duni<br />
na wakulima wenyewe wamesongwa<br />
na matatizo mengi. Walio wengi<br />
hawazijui na hawazitekelezi Kanuni za<br />
Kilimo Bora kwa mazao wanayolima,<br />
hivyo kilimo chao hakina tija na<br />
mavuno yao ni kidogo. Kwa wastani<br />
wakulima bado wanalima vishamba<br />
vidogo vidogo, pia bado wakulima<br />
wetu wanatumia zana duni za jadi<br />
kama vile jembe la mkono. Hapa<br />
mwelekeo chanya ni kwamba kilimo<br />
cha kisasa kinapaswa kuwa sharti<br />
muhimu katika kuchangia ujenzi wa<br />
uchumi wa kisasa.<br />
Heshima ya mkulima/mfugaji<br />
mdogo<br />
Toka wakati wa uhuru<br />
hadi miaka ya 70 na 80<br />
mwanzoni, wakulima<br />
wadogo walikuwa<br />
wanaheshimiwa na kazi yao<br />
ilikuwa inathaminiwa na makundi<br />
mbalimbali katika jamii. Hata wasanii<br />
wa muziki walitunga na kuimba<br />
nyimbo mbalimbali zilizowasifu,<br />
kuwapongeza na kuwatia moyo<br />
wakulima wadogo ili waweze<br />
kuendelea na kazi ya kulisha taifa na<br />
kuongeza pato la taifa kupitia katika<br />
kilimo.<br />
Kwa sasa hali imebadilika<br />
kabisa, miaka hamsini ya uhuru<br />
tunashuhudia kilimo kinaonekana<br />
kama mbadala wa mwisho. Mambo<br />
yote yakikushinda unaenda kwenye<br />
kilimo na ukimaliza muda wako wa<br />
kutumikia taifa kwa njia ya ajira rasmi<br />
ndipo unarudi katika kilimo ukafie<br />
huko. Ingawa kauli mbiu ya Kilimo<br />
ni Uti wa Mgongo bado inatumika<br />
sana na makundi mbalimbali katika<br />
jamii yetu, lakini uhalisia ni kwamba<br />
kilimo kinaonekana kuwa ni mateso<br />
au adhabu au shughuli isiyokuwa na<br />
heshima mbele ya jamii. Ni jambo<br />
la kawaida kusikia mtu akisema:<br />
‘Kama mjini pamekushinda rudi kijijini<br />
ukalime’; ‘Kama sanaa imekushinda,<br />
nenda ukalime’; Kama huwezi siasa<br />
nenda kalime’; sio lazima kuwa na<br />
digrii, ukiona unashindwa, rudi kijijini<br />
ukawasaidie wazazi kulima’.<br />
Kejeli hizi zinachangia vijana<br />
wetu wengi kukimbia kilimo na<br />
kwenda mjini kwani kuwa mkulima<br />
ni aibu mbele za watu. Hata<br />
mkulima akivaaa vizuri, akinawiri<br />
au akitoa maoni yake ya maana,<br />
utasikia minong’ono inayoonesha<br />
mashaka kama hayo ni mawazo ya<br />
mkulima. Hapo ndipo wakulima<br />
wadogo wanajiuliza, hivi kweli sifa<br />
zetu ni kuwa mchafu, mchovu, mtu<br />
asiyeweza kutoa mawazo na maoni<br />
ya maana mbele ya jamii au asiye na<br />
mbele wala nyuma?<br />
Kwa ujumla unaweza kuipa<br />
tafsiri Sekta ya Kilimo kwa semi<br />
mbalimbali, mojawapo ikiwa ni<br />
‘sekta iliyotelekezwa ama sekta ya<br />
watu wanaoganga maisha.’ Hata<br />
hivyo, upana na unyeti wa shughuli<br />
zinazofanywa na Sekta ya kilimo ndio<br />
kigezo dhahiri kinachoipa umuhimu<br />
kuweza kuingizwa katika mchakato<br />
huu wa kujitathmini na kuelezea<br />
mafanikio yake katika mwaka huu<br />
<strong>20</strong>11.<br />
Watanzania tunapoadhimisha<br />
na kusherehekea kwa shangwe na<br />
nderemo kutimiza miaka hamsini ya<br />
Uhuru, tunapaswa kujiuliza je, kilimo<br />
ambacho kinaelezwa kuwa kinatoa<br />
mchango mkubwa katika pato la<br />
taifa, kinatoa tafsiri ama mchango<br />
gani wa maendeleo ya mkulima<br />
mmoja mmoja?<br />
Ni ukweli ulio wazi kuwa<br />
wakulima wadogo ni wachangiaji<br />
wakubwa katika pato na maendeleo<br />
ya taifa, ingawa wao wenyewe<br />
hawanufaiki na pato hilo.<br />
Kodi zinazotozwa na<br />
kukusanywa na serikali kwa njia<br />
mbalimbali zinalipwa na kundi<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 11<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11
Inatoka uk. wa 10<br />
kubwa la wale walio katika Sekta ya<br />
Kilimo (wakulima ama wazalishaji<br />
wadogo). Hawa ndiyo tunaambiwa<br />
wanachangia pato la taifa kwa kuwa<br />
shughuli zao kuu ni kilimo. Wanalipa<br />
kodi hizo ama kupitia shughuli<br />
zao za uzalishaji na biashara, ama<br />
kupitia bidhaa wanazonunua kama<br />
vile mafuta ya taa, sukari na nguo.<br />
Lakini hoja inayoweza kuibuka hapa<br />
Hifadhi<br />
ya chakula ni eneo ambalo<br />
linapaswa kuchukuliwa kwa uzito ili<br />
mazao yasiendelee kupungua bali Tanzania<br />
igeuke kuwa ghala ya chakula katika kanda<br />
huu wa Afrika Mashariki.<br />
ni je, kodi<br />
hizo zimetumikaje kusaidia kutatua<br />
kero na matatizo mengi yanayogusa<br />
maisha yao ya kila siku?<br />
Zipo changamoto nyingi<br />
zinazowakabili wakulima nchini<br />
kwetu hivi sasa ambazo zingeweza<br />
kutatuliwa kwa kodi wanazolipa na<br />
nyingine zingetatuliwa na uwepo<br />
wa sera zinazomwezesha mkulima<br />
kupiga hatua za maendeleo.<br />
Kwa mfano changamoto za<br />
masoko na bei nzuri ya mazao ni<br />
suala la kisera, changamoto ya mitaji<br />
inaweza tatuliwa na sera nzuri na<br />
changamoto ya matumizi ya zana<br />
duni, ubaha wa pembejeo na umiliki<br />
wa ardhi ni masuala ya kimkakati<br />
ambayo kama juhudi za makusudi<br />
zikichukuliwa na kutekelezwa kwa<br />
ushirikiano thabiti kati Serikali na<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />
Sekta Binafsi, shughuli ya kilimo<br />
itawanufaisha wakulima na wao<br />
kuona wanafaidi matunda ya uhuru<br />
sawa na wazalishaji kwenye sekta<br />
nyingine. Tukifanya hivi tutaifanya<br />
nchi yetu kufikia mafanikio ya<br />
nchi kama vile Malaysia, Indonesia,<br />
Singapore na Vietnam ambazo katika<br />
miaka ya mwanzo wa sitini sekta za<br />
kilimo zilikuwa katika viwango sawa<br />
na nchi yetu.<br />
Jambo jingine tunalopaswa<br />
kulitumia vyema ni<br />
kiwango kikubwa cha<br />
rasilimali ambazo<br />
Mungu ameijalia<br />
ardhi yetu ya<br />
Tanzania iliyojaa<br />
rutuba na hali ya<br />
hewa inayoruhusu<br />
mazao aina mbalimbali<br />
kustawi, jambo la msingi ni<br />
kuwa na utashi wa kisiasa.<br />
Juhudi kubwa inabidi zielekezwe<br />
kwenye Kilimo cha Kibiashara na<br />
hapa ushirikiano wa serikali na sekta<br />
binafsi ndio utakaofanikisha azma hii.<br />
Mbali na kuongeza wigo katika sekta<br />
ya kilimo, mkazo inabidi uwekwe<br />
kwenye uongezaji thamani kwa<br />
kutilia mkazo usindikaji wa mazao.<br />
Hifadhi ya chakula ni eneo ambalo<br />
linapaswa kuchukuliwa kwa uzito<br />
ili mazao yasiendelee kupungua<br />
bali Tanzania igeuke kuwa ghala ya<br />
chakula katika kanda huu wa Afrika<br />
Mashariki.<br />
Taarifa za ushindani katika uchumi<br />
wa soko huria na urahisi wa kufanya<br />
biashara zinahitajika ili kuchochea<br />
juhudi za kujikwamua kiuchumi.<br />
Vyombo husika vinapaswa kutoa<br />
uwanja sawa na mazingira wezeshi<br />
Kilimo ni Uti wa Mgongo?<br />
MAKALA<br />
kwa wadau wote. Haipendezi<br />
kuendelea kuwabagua wakulima<br />
kwa kuwazuia kuuza mazao huku<br />
nchi ikinadi sera za soko huria.<br />
Mafanikio makubwa ya maendeleo<br />
katika sekta zote yanategemea<br />
sana uwekezaji katika sayansi na<br />
teknolojia. Matumizi ya teknolojia ya<br />
habari (ICT) yatasaidia sana harakati<br />
za biashara ya ushindani, kwa hiyo<br />
uwekezaji katika eneo hili upewe<br />
kipaumbele. Teknolojia hii ya habari<br />
hivi sasa imeonyesha mafanikio<br />
kwenye baadhi ya maeneo, mfano<br />
dhahiri ukiwa ni Mfumo wa Taarifa za<br />
Masoko (MAMIS) unaotekelezwa na<br />
<strong>MVIWATA</strong>, ambao umepongezwa<br />
na wadau wengi kwamba umesaidia<br />
kuimarisha biashara ya mazao.<br />
Kero kubwa katika utendaji wa<br />
biashara ni miundombinu mibovu<br />
hususan barabara ambazo ni<br />
vyema zikaboreshwa ili kurahisisha<br />
usafirishaji wa mazao toka vijijini<br />
ambako ndipo uzalishaji unapofanyika<br />
hadi maeneo ya masoko ya walaji<br />
ambao mara zote ni wakazi wa<br />
mijini.<br />
Tuimarishe na kuwa na mfumo<br />
wa uhakika wa upatikanaji wa<br />
mbegu bora na mbolea na kueneza<br />
matumizi yake kwa wakulima wengi<br />
zaidi.<br />
Uwezeshwaji wa wananchi kwa<br />
ujumla ni jukumu ambalo serikali<br />
inapaswa kulitekeleza kwa dhati. Sera<br />
hii imebuniwa ili kuwapa mamilioni<br />
ya Watanzania fursa ya kujikwamua<br />
kiuchumi. Kilimo kina nafasi ya<br />
kimkakati ya kukuza uchumi, ikiwa<br />
juhudi zaidi zitawekwa kwenye<br />
kupanua uwigo wa utekelezaji wa<br />
mipango inayowekwa.<br />
11
KAMERA<br />
12<br />
KAMERA YA <strong>MVIWATA</strong> MITANDAONI<br />
Wana-<strong>MVIWATA</strong> Zanzibar walioshiriki mkutano mkuu oktoba <strong>20</strong>11<br />
mjini Morogoro<br />
Wana-<strong>MVIWATA</strong> Chunya wakiwa katika ziara ya mafunzo kwa<br />
wakulima wenzao wa wilaya ya Mkuranga Pwani<br />
Bw. Hasira Zahoro Mwezeshaji wa <strong>MVIWATA</strong> akizungumza na wadau<br />
wa soko la Matai Sumbawanga Vijijini, linalojengwa na <strong>MVIWATA</strong><br />
Wana-<strong>MVIWATA</strong> Mara walioshiriki mkutano mkuu Oktoba <strong>20</strong>11<br />
Viongozi wa <strong>MVIWATA</strong> Shinyanga kutoka kulia ni Bw. Masumbuko<br />
Bunzali (Mwenyekiti <strong>MVIWATA</strong> Bariadi), Bw. Charles Ndugulile<br />
(Mwenyekiti Mkoa) Bibi. Justa Charles (Mjumbe kamati ya uongozi<br />
<strong>MVIWATA</strong> Kahama), Bw. Goma Boya (Katibu <strong>MVIWATA</strong> Shinyanga<br />
Vijijini) na Bw. Yusuph Mboje (Katibu <strong>MVIWATA</strong> Kishapu) wakiwa<br />
wameshika majarida ya Pambazuko baada ya kuyapokea kupitia<br />
mfumo wa malipo kabla.<br />
Bibi Atufuage Mgimba mkulima toka kikundi cha Amani, kijiji cha<br />
Mapogoro kata ya Milo wilayani Ludewa, akizungumza kwenye<br />
mafunzo ya uimarishaji vikundi, yaliyofanyika Mlangali<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11
KAMERA YA <strong>MVIWATA</strong> MITANDAONI<br />
Picha ya pamoja ya wakazi wa kijiji cha Itwangi Shinyanga Vijijini, baada<br />
ya kikao cha ufuatiliaji wa Mradi wa Chukua Hatua unaotekelezwa na<br />
<strong>MVIWATA</strong> kwa ushirikiano na shirika la Oxfam.<br />
Mwenyekiti wa Mfuko wa Mwalimu Nyerere Mzee Joseph Butiku<br />
akisisitiza jambo kwenye Kongamano la <strong>MVIWATA</strong> la Kuadhimisha<br />
Miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Disemba 6, <strong>20</strong>11 Morogoro mjini<br />
Picha ya pamoja ya washiriki wa Kongamano la <strong>MVIWATA</strong> la Miaka<br />
50 ya Uhuru lililofanyika Morogoro Disemba 6, <strong>20</strong>11<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />
KAMERA<br />
Picha ya pamoja ya wana-<strong>MVIWATA</strong> Shinyanga Vijijini na waheshimiwa<br />
madiwani wa halsmahauri ya wilaya hiyo, baadaya kikao chenye lengo<br />
la kuimarisha mahusiano<br />
Washiriki wa Kongamano la miaka 50 wakimsikiliza mgeni rasmi<br />
Mzee Joseph Butiku anayeonekana picha ya kushoto<br />
Bw.Anno Lwilo mkulima wa kijiji cha Mangalanyene wilaya ya Ludewa<br />
mkoa wa Njombe akichangia mada kwenye Kongamano la <strong>MVIWATA</strong><br />
la miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania<br />
13
KUTOKA MITANDAONI<br />
WARSHA YA KITAIFA<br />
Soko la uhakika kichocheo cha uzalishaji<br />
kwa wakulima Tanzania<br />
Na Jacueline Massawe, Morogoro<br />
<strong>Uk</strong>osefu wa soko la uhakika<br />
kwa mazao ya wakulima<br />
ni miongoni mwa<br />
changamoto zinazomkwamisha<br />
mkulima mdogo kunufaika na<br />
shughuli hiyo ya kilimo na hivyo<br />
kuendelea kuwa masikini.<br />
Kwa kuiona changamoto hiyo,<br />
<strong>MVIWATA</strong> ambayo ni chombo<br />
kinachowaunganisha wakulima<br />
wadogo iliandaa warsha ya kitaifa<br />
iliyowakutanisha wakulima zaidi<br />
250 kutoka mikoa yote ya Tanzania<br />
bara na Visiwani. Warsha hiyo pia<br />
ilihudhuriwa na viongozi wa serikali<br />
na wataalamu kutoka taasisi za<br />
kiserikali na zisizo za kiserikali,<br />
wasomi na wachambuzi wa masuala<br />
ya sera na siasa nchini.<br />
Lengo la warsha hiyo ya siku<br />
moja, ambayo ilibeba maudhui<br />
yasemayo, Soko la Uhakika Kichocheo<br />
cha Uzalishaji! lilikuwa ni kuwapa<br />
fursa wadau wa kilimo kujadili na<br />
kuzitafutia ufumbuzi changamoto za<br />
masoko ya mazao ya wakulima.<br />
Warsha hiyo ilifanyika Oktoba<br />
14<br />
24, <strong>20</strong>11 katika ukumbi wa Kituo<br />
cha Mafunzo ya Wanawake CCT cha<br />
Mjini Morogoro ikiwa ni utangulizi<br />
wa Mkutano Mkuu wa 16 wa shirika<br />
la <strong>MVIWATA</strong> uliofanyika Oktoba 25,<br />
<strong>20</strong>11.<br />
Warsha hiyo ilifunguliwa na<br />
Mkuu wa Mkoa Mstaafu Bw. Stephen<br />
Mashishanga, ambaye katika hotuba<br />
yake, alipongeza utaratibu shirikishi<br />
unaotumiwa na <strong>MVIWATA</strong> kwa<br />
kuwashirikisha wakulima kuibua<br />
kero kwa kuwakutanisha na wadau<br />
mbalimbali na kuhimiza utaratibu<br />
huo uimarishwe kwenye ngazi zote<br />
na siyo ngazi ya taifa tu.<br />
Bw. Mashishanga aliwataka<br />
wakulima kuungana kwa pamoja kwa<br />
kupaza sauti za kukataa makandamizo<br />
na manyanyaso wanayofanyiwa<br />
na serikali na wahisani mbalimbali<br />
wasio na mapenzi mema.<br />
“Ni vizuri wakulima tukahakikisha<br />
kuwa tunajitetea mwenyewe kwa<br />
umoja na nguvu zote badala ya<br />
kutegemea kutetewa na mashirika<br />
yanayokuja kwa mgongo wa<br />
uwekezaji kwa maslahi ya nchi zao,<br />
ama serikali ambayo haituungu<br />
mkono,” alisema Bw. Mashishanga<br />
Washiriki wa warsha ya kitaifa ya <strong>MVIWATA</strong> <strong>20</strong>11<br />
Aidha alihimiza vyama vya<br />
wakulima vijenge mahusiano<br />
imara na halmashauri za wilaya<br />
katika kutekeleza majukumu yake<br />
na kuongeza kuwa kwa kufanya<br />
kazi pamoja wataweza kutatua<br />
changamoto za masoko na<br />
nyinginezo ambazo ni kero kwa<br />
wakulima.<br />
Aliitaka serikali iache kuwapuuza<br />
wakulima na badala yake isikilize<br />
kilio chao na kuzitafutia ufumbuzi<br />
changamoto zinazowakabili.<br />
Kwa upande wake Mwenyekiti<br />
wa <strong>MVIWATA</strong> Taifa aliyemalizamuda<br />
wake Bw. Yazid Makame alisema kuwa<br />
wakulima bado wanakabiliwa na<br />
changamoto nyingi hasa za masoko,<br />
ambazo zinapaswa kutatuliwa ili<br />
kuwezesha maendeleo ya haraka<br />
kwa wakulima wadogo nchini.<br />
Kwa upande wake Mkurugenzi<br />
Mtendaji wa <strong>MVIWATA</strong> Bw. Stephen<br />
Ruvuga alisema tatizo la vikwazo<br />
vya kibiashara kwa wakulima<br />
wadogo limekuwa likiwakatisha<br />
tama na matokeo yake yamekuwa ni<br />
uzalishaji mdogo na duni.<br />
“Wakulima wadogo wakiwa<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 15<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11
Inatoka uk. wa 14<br />
na uhakika wa soko itakuwa ni<br />
motisha kwao klima kwa bidii na<br />
kibishara zaidi. Wakulima wadogo<br />
wakiuza, mapato yao yanarudi tena<br />
mashambani kuimarisha kilimo na<br />
kuongeza uzaishaji. Wakizalisha bila<br />
soko wanakata tamaa ya kuzalisha,”<br />
alisema Bw. Ruvuga.<br />
Akitoa maoni yake juu ya mpango<br />
huo wa uwekezaji, Bw. Ruvuga,<br />
alitahadharisha kuwa kitendo cha<br />
kuwabagua wakulima wadogo katika<br />
umilikaji wa ardhi kinaweza kujenga<br />
tabaka la chuki na kuibua migogoro<br />
ya ardhi isiyokoma.<br />
“Tumeshuhudia nchi nyingine<br />
wakulima waliondolewa katika ardhi<br />
yao kimabavu, baadaye wameungana<br />
na kuifatuta haki yao kwa nguvu”<br />
alisema Bw. Ruvuga.<br />
Bw. Ruvuga alisema, nchi lazima<br />
ihakikishe kunakuwa na usalama<br />
wa chakula kwa tahadhari kwani<br />
wawekezaji wanaweza kuzalisha<br />
mazao ya chakula kwa soko la nje<br />
na kuiacha nchi bila chakula na pia<br />
kushindwa kununua mazao hayo<br />
kwa kuwa mengi yanauzwa kwa bei<br />
kubwa.<br />
Alishauri kuwa ni vyema serikali<br />
ikawekeza zaidi kwa wazalishaji<br />
wadogo kwa kuwajengea uwezo ili<br />
waendelee kulisha Taifa bila kuwa<br />
na kikwazo chochote cha kuingiliwa<br />
katika ardhi yao.<br />
Michango iliyotolewa na<br />
wakulima walioshiriki warsha hiyo,<br />
kwa sehemu kubwa ilionyesha<br />
mashaka makubwa juu ya mkakati<br />
huo wa serikali wa kuwafanya<br />
wakulima kulima kibiashara kutokana<br />
na kero nyingi huku wakitolea<br />
mfano wa kero wanayokumbana<br />
nayo mipakani wanapotaka kuvusha<br />
mazao kwenda nchi jirani na kuitaka<br />
Jumuiya ya Afrika Mashariki kuingilia<br />
kati suala hilo.<br />
“Tunahamasishwa kulima<br />
kibiashara kwa sababu ya soko<br />
huria na soko la pamoja la Afrika<br />
Mashariki, lakini tunapofika mipakani<br />
tunakumbana na vizuizi na kwa kweli<br />
tunanyanyasika mno, tunadaiwa<br />
malipo ambayo hayapo kisheria,”<br />
alisema Bibi Fatuma Kimolo Makamu<br />
Mwenyekiti wa <strong>MVIWATA</strong> Manyara.<br />
Bibi. Kimolo alisema wanasikia<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />
nchi hizo zimesaini Makubaliano ya<br />
Soko la Pamoja la Kibiashara, lakini<br />
akashangazwa na vikwazo hivyo<br />
kuendelea kuwepo.<br />
Mkulima mwingine Bw. Joseph<br />
Mshangama kutoka mkoani Tanga<br />
mbali na kutaka kuondolewa kwa<br />
vikwazo vya kuuza mazao nje ya nchi,<br />
alisema wakulima bado wanahitaji<br />
kuelimishwa vya kutosha kuhusiana<br />
makubaliano ya Soko la Pamoja ili<br />
kuondoa mkanganyiko unaojitokeza<br />
hivi sasa.<br />
Bw. Joseph Mshangama<br />
Bw. Hamad Salmin, mkulima<br />
kutoka Zanzibar alisema<br />
changamoto kubwa inayowakabili<br />
wakulima visiwani humo ni suala<br />
la usindikaji. Alisema wakulima<br />
wengi wanazalisha mbogamboga<br />
na matunda, lakini hawana vifaa<br />
vya kuhifadhi na usindikaji na hivyo<br />
wakulima kulazimika kuuza mazao<br />
kwa bei ndogo kwa madalali.<br />
Wakulima hao walisema licha<br />
ya kuwawekea masharti ya kuuza<br />
mazao yao nje ya nchi kwenye bei<br />
nzuri, serikali hiyo hiyo imekuwa<br />
ikishirikiana na wawekezaji kuwapora<br />
wakulima ardhi.<br />
Bw.Levi Mlengule kutoka wilaya<br />
ya Mufindi alisema katika eneo lake<br />
wawekezaji wanafaidi misitu kuliko<br />
ilivyo kwa wenyeji. Alisema wakulima<br />
wamenyimwa fursa ya kuvuna misitu<br />
hiyo ambayo wao ndiyo watunzaji<br />
wakuu.<br />
Bw. Ahmedi Simba mkulima toka<br />
wilaya ya Kigoma alilalamikia Serikali<br />
wilayani humo kwa kuchukua ardhi<br />
kubwa na kuwapa wawekezaji<br />
na kushindwa kutoa ardhi hiyo<br />
hiyo kwa makundi madogo ya<br />
wakulima ambao kwa muda mrefu<br />
wamewasilisha maombi ya ardhi<br />
hiyo.<br />
“Nahofia tutaishia kuwa<br />
manamba katika mashamba<br />
KUTOKA MITANDAONI<br />
makubwa, tunajiuliza kwa nini<br />
Serikali inawapendelea wawekezaji<br />
wageni na kuwaacha wazawa?”<br />
alihoji kwa uchungu Bw. Simba.<br />
Afrika Mashariki watakiwa<br />
kutekeleza soko huria kwa<br />
vitendo<br />
Mkurugenzi Msaidizi katikaWizara<br />
ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki<br />
anayeshughulikia kitengo cha<br />
Uzalishaji Dkt. Abdullah Makame,<br />
akiwasilisha mada kwenye warsha<br />
hiyo alisema Jumuiya ya nchi za<br />
Afrika Mashariki inatakiwa kuchukua<br />
hatua za makusudi za kuwasaidia<br />
wakulima kunufaika na kilimo kwa<br />
kuwaondolea vizuizi vya kusafirisha<br />
mazao mpakani na vikwazo<br />
vinginevyo kwenye soko la mazao.<br />
Dkt. Makame ambaye mada<br />
yake ilizungumzia Fursa na Vikwazo<br />
katika Biashara ya Mazao ndani ya<br />
Jumuiya ya Afrika Mashariki, alisema<br />
vizuizi hivyo ni moja ya sababu<br />
zinazochangia kudumaza uchumi wa<br />
nchi hizo ambazo asilimia kubwa ya<br />
wananchi wake wanajishughulisha<br />
na kilimo. Jumuiya ya Afrika<br />
Mashariki inaundwa na nchi tano za<br />
Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na<br />
Tanzania.<br />
Akizungumzia maendeleo ya<br />
sekta ya kilimo nchini, Dkt Makame<br />
alisema tatizo kubwa linaloikabili<br />
nchi yetu ni miundombinu mibovu<br />
ambapo asilimia 80 ya usafirishaji<br />
wa mizigo ikiwemo mazao ya kilimo,<br />
inategemea barabara, ilihali katika<br />
nchi zilizoendelea bidhaa nyingi<br />
zinasafirishwa kwa reli, meli na<br />
ndege na hivyo kufikisha mapema<br />
sokoni bidhaa zikiwa na ubora na<br />
thamani inayokidhi soko.<br />
Alisema tatizo jingine<br />
linalowakabili wazalishaji wadogo<br />
nchini ni kukosa umiliki wa ardhi<br />
jambo ambalo alisema serikali<br />
inapaswa kulipa kipaumbele ili<br />
kuchochea uzalishaji na maendeleo<br />
ya kiuchumi kwa ujumla hasa wakati<br />
huu tunapozungumzia kuwa na<br />
shirikisho la Afrika Mashariki.<br />
Aliitaka serikali kuangalia upya<br />
iwapo sera zinazotungwa na zilizopo<br />
kama zinakidhi mahitaji ya kumsaidia<br />
mzalishaji kujiletea maendeleo<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 16<br />
15
KUTOKA MITANDAONI<br />
Inatoka uk. wa 15<br />
badala ya kumkandamiza.<br />
Akiwasilisha uzoefu wa <strong>MVIWATA</strong><br />
kuhusu Ubia wa vyama vya<br />
wakulima na Halmashauri za<br />
wilaya katika uendeshaji wa<br />
masoko, Mratibu wa Kitengo cha<br />
Masoko Bw. Nickson Elly <strong>MVIWATA</strong><br />
mpaka sasa imefanikiwa kujenga<br />
masoko tisa ya mazao ya wakulima<br />
vijijini.<br />
Alisema masoko hayo yako<br />
kwenye vijiji vya Kibaigwa<br />
Kongwa, Nyandira Mvomero,<br />
Tandai na Tawa Morogoro Vijijini,<br />
Mkata Handeni,Igagala Njombe,<br />
Igurusi Mbarali, Matai na Kasanga<br />
Sumbawanga Vijijini.<br />
Alisema masoko hayo<br />
kwa kawaida huendeshwa na<br />
kusimamiwa na bodi za masoko<br />
ambazo mundo wake unajumuisha<br />
uwakilishi wa wadau mbalimbali<br />
wa soko wakiwemo wawakilishi wa<br />
halmashauri za wilaya.<br />
Hata hivyo katika siku za hivi<br />
karibuni uendeshaji wa masoko<br />
hayo umekuwa na changamoto<br />
nyingi ikiwemo kiwango kikubwa<br />
cha ushuru ambao halmashauri<br />
za wilaya zinalazimisha kulipwa,<br />
ambazo hakilingani na makusanyo<br />
halisi ya ushuru wa sokoni kwa<br />
mwezi. Aliongeza kuwa hali hiyo<br />
inahatarisha uendelevu wa masoko<br />
hayo ambayo yamechangia kwa<br />
kiwango kikubwa ukuaji wa uchumi<br />
wa wakulima wa maeneo husika.<br />
Bw. Elly alisema hali hiyo ni<br />
mojawapo ya sababu zilizoisukuma<br />
<strong>MVIWATA</strong> kandaa warsha hiyo ili<br />
kupata fursa ya kujadiliana na wadau<br />
mbalimbali wanahusika kwenye<br />
mfumo wa masoko ya mazao ya<br />
wakulima. kiwangoambah<br />
Umiliki wa ardhi<br />
Akiwasilisha mada kuhusu Nafasi<br />
ya Wazalishaji Wadogo kwenye<br />
mchakato wa kuandikwa Katiba<br />
Mpya, Mhadhiri Msaidizi Kitivo cha<br />
Sayansi ya Siasa ya Jamii chuo kikuu<br />
cha Dar es Salaam Bw. Bashiru<br />
Ally alisema kwamba, mambo yote<br />
yanayohusiana na ardhi ni lazima<br />
yapewe kipaumbele kuzungumziwa<br />
katika katiba mpya ili kuzuia uadui<br />
unaoweza kutokea baina ya wamiliki<br />
16<br />
ardhi na watawala.<br />
“Ni lazima kuangalia sheria<br />
zetu za ardhi na kuziimarisha ili<br />
ziweze kulinda haki za wazawa wa<br />
Kitanzania” alisisitiza Bw. Ally<br />
Alisema hadi mwaka <strong>20</strong>10,<br />
Serikali ilikwishagawa hekta<br />
610,000 za ardhi kwa makampuni<br />
13 ya uwekezaji ya kigeni na wengi<br />
wamepewa na kuhodhi maeneo<br />
hayo pasipo kuyaendeleza na<br />
wengine wamelalamikiwa kwa<br />
kujiingiza katika biashara ya mbao<br />
na hivyo kuharibu mazingira badala<br />
ya kuyatunza.<br />
Alisema serikali imekuwa<br />
ikitangaza kuwa, Tanzania ina hekta<br />
milioni 44 za ardhi inayofaa ka kilimo<br />
na kwamba kati yake ni hakta 10.8<br />
milioni tu zinazotumika.<br />
“Lakini baadhi ya wataalamu na<br />
wanaharakati watetezi wa haki ya<br />
ardhi wamesema huu ni udanganyifu<br />
kwani ardhi ambayo haitumiki ni ile<br />
iliyopo kwenye mbuga za wanyama,<br />
hifadhi ya misitu na kwenye hifadhi<br />
za asili. Wakulima na wafugaji wote<br />
wanatumia ardhi waliyotengewa na<br />
katika maeneo mengi haiwatoshi<br />
ndiyo maana kunatokea migogoro<br />
ya ardhi,” alisema msomi huyo.<br />
Aliwashauri wakulima kushiriki<br />
kikamilifu katika mchakato wa<br />
uandikaji wa katiba mpya pindi<br />
utakapoanza, ili washawishi kuingizwa<br />
kwa vipengele muhimu vinavyotetea<br />
umiliki wa ardhi kwa wazawa.<br />
Alisema mataifa tajiri ambayo<br />
sasa yanaongoza kwa kuvamia ardhi<br />
katika bara la Afrika ni pamoja na<br />
Korea ya Kusini, China Saudi Arabia na<br />
Umoja wa Nchi za Kiarabu, ambapo<br />
nchi za Afrika zilizokwishavamiwa ni<br />
Zambia, Ethiopia, Kenya na Sudani.<br />
“Uwekezaji huo unalenga kuzalisha<br />
mazao ya nishati mmea pamoja<br />
na mazao ya chakula ambacho<br />
kinasafirishwa pasipo nchi husika<br />
kunufaika.”<br />
Ingawa wanaounga mkono<br />
uwekezaji huo wanatetea kuwa<br />
hoja kwa maelezo kuwa utasaidia<br />
kuimarisha kilimo kwenye nchi<br />
zinazoendelea, lakini ukweli unabaki<br />
wazi kuwa uwekezaji huo unafanyika<br />
kwa malengo ya faida binafsi za<br />
kibiashara ama faida za mataifa hayo<br />
tajiri.<br />
Mapema Mkurugenzi Mtendaji<br />
wa wilaya ya Chunya, Bw. Maurice<br />
Sapanjo katika maeneo aliyofanyakazi<br />
na vikundi vya wakulima hasa vya<br />
<strong>MVIWATA</strong>, vimekuwa msaada<br />
mkubwa wakuchochea kazi ya<br />
maendeleo vijijini.<br />
Alishauri <strong>MVIWATA</strong> kujieneza<br />
zaidi vijijini waliko wakulima wengi<br />
ili waweze kunufaika na utetezi na<br />
maarifa inayotolewa kupitia mtandao<br />
huo.<br />
Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya ya Chunya, Bw. Maurice Sapanjo<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11
Bodi mpya ya <strong>MVIWATA</strong><br />
Na Goodness Mrema, Morogoro<br />
Wajumbe wa Mkutano<br />
Mkuu wa 16 wa<br />
<strong>MVIWATA</strong> uliofanyika<br />
Oktoba 25, <strong>20</strong>11 mjini Morogoro<br />
wamechagua Bodi mpya ya<br />
wakurugenzi wa shirika hilo<br />
watakaokaa madarakani kwa miaka<br />
mitatu <strong>20</strong>11-<strong>20</strong>14.<br />
Bodi mpya iliyochaguliwa<br />
inaongozwa na Bw. Habibu<br />
Simbamkuti mkulima mdogo kutoka<br />
Kikundi cha Sanje kijiji cha Msolwa<br />
Ujamaa, tarafa ya Kidatu wilaya ya<br />
Kilombero mkoani Morogoro. Bw.<br />
Simbamkuti anawakilisha kanda<br />
namba 2 (Morogoro,Pwani na Dar<br />
es Salaam).<br />
Msaidizi wake ni Bibi. Veronica<br />
Sophu mkulima mdogo wa kijiji cha<br />
Madibila wilaya ya Mbarali mkoani<br />
Mbeya anayewakilisha kanda namba<br />
7 (Mbeya, Rukwa na Kigoma). Bibi<br />
Esther Mallya mkulima kutoka<br />
wilaya ya Hai,mkoani Kilimanjaro<br />
amechaguliwa kuwa Mwekahazina<br />
akiwakilisha kanda namba 3<br />
(Kilimanjaro na Tanga).<br />
Wajumbe wa bodi wengine ni Bw.<br />
Bodi ya zamani <strong>20</strong>08-11<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />
Joseph Kilowoko kutoka Namtumbo<br />
Ruvuma akiwakilisha kanda namba<br />
8(Iringa na Ruvuma), Paulo Joseph<br />
kutoka Babati Manyara akiwakilisha<br />
kanda namba 4(Manyara, Arusha<br />
na Mara), Haji Ussi Haji kutoka<br />
Bodi mpya <strong>20</strong>11-14<br />
KUTOKA MITANDAONI<br />
Zanzibar akiwakilisha kanda namba<br />
1 (Zanzibar).<br />
Wengine ni Bw. Projestus<br />
Ishekanyoro kutoka Kagera<br />
akiwakilisha kanda namba 6<br />
(Mwanza, Kagera na Shinyanga),<br />
Bibi Amina Kazibure kutoka Masasi<br />
Mtwara akiwakilisha kanda namba 9<br />
(Mtwara na Lindi) na Bibi Prisca John<br />
kutoka Igunga Tabora akiwakilisha<br />
kanda namba 5 (Tabora, Singida na<br />
Dodoma).<br />
Mkurugenzi Mtendaji wa<br />
<strong>MVIWATA</strong> Bw. Stephen Ruvuga<br />
anaingia kwenye vikao vya bodi<br />
kama katibu.<br />
Wajumbe wa bodi iliyomaliza<br />
muda wake walikuwa ni Bw. Yazid<br />
Makame (mwenyekiti), Bibi Lydia<br />
Ruliho (makamu), Bibi Grace<br />
Runkulatire (Mwekahazina).<br />
Wajumbe wengine walikuwa<br />
ni Bw. Julius Mbago, Bw. Joseph<br />
Kilowoko, Bw. Samwel Maseke,<br />
Bibi Cosma Bullu, Bw. Habibu<br />
Simbamkuti, Bw. Sylivester Yatuba.<br />
<strong>17</strong>
KUTOKA MITANDAONI<br />
SIKU YA WANAMTANDAO MKURANGA<br />
Mkuu wa wilaya ahimiza mahusiano<br />
baina ya wadau wa kilimo<br />
Na Abdalla Idd, Mkuranga<br />
Mkuu wa wilaya ya Mkuranga<br />
mkoani Pwani Bw. Henry<br />
Clemence, amewahimiza<br />
wadau wa sekta ya kilimo wilayani<br />
humo kuimarisha mahusiano yenye<br />
lengo la kumsaidia mkulima kupiga<br />
hatua za kimaendeleo.<br />
Wito huo aliutoa wakati<br />
akifungua maadhimisho ya SIKU YA<br />
WANAMTANDAO MKURANGA,<br />
iliyofanyika Disemba 6, <strong>20</strong>11<br />
Mkuranga mjini.<br />
Mkuu huyo wa wilaya alisema, hivi<br />
sasa katika wilaya hiyo na maeneo<br />
mengine nchini yapo mashirika na<br />
taasisi zinazofanya kazi na wakulima,<br />
lakini taasisi hizo hazifahamiani<br />
ingawa zinatekeleza shughuli kwenye<br />
eneo moja.<br />
Alisema kuimarishwa kwa<br />
mahusiano hayo kutasaidia<br />
Wanawake wa kijiji cha Kizapala wilayani Mkuranga wakionyesha usindikaji wa muhogo kwa<br />
wageni toka nje ya nchi waliowatembelea kujifunza shughuli zao<br />
18<br />
kuunganisha nguvu na kuondoa<br />
mtawanyiko wa raslimali ambazo<br />
zikitumika vyema zitaongeza ufanisi.<br />
Siku ya Wanamtandao Mkuranga<br />
ambayo imefanyika kwa mara ya<br />
kwanza, iliandaliwa na <strong>MVIWATA</strong><br />
Mkuranga kwa lengo la kuwakutanisha<br />
wadau mbalimbali kuimarisha<br />
mahusiano na kubadilishana taarifa.<br />
Aidha siku hiyo ilitoa fursa kwa<br />
wakulima kuonesha matokeo ya<br />
shughuli za uzalishaji wanazofanya<br />
na kuhamasisha matumizi ya bidhaa<br />
zitokanazo na zao la Mhogo kama<br />
mbadala wa mazao mengine ya<br />
chakula.<br />
Wakizungumza kwenye<br />
maadhimisho hayo, baadhi ya<br />
wanachama wa <strong>MVIWATA</strong><br />
walisema miongoni mwa mafanikio<br />
waliyoyapata kupitia mtandao wa<br />
wakulima wilayani humo ni pamoja<br />
na kuimarisha mahusiano baina ya<br />
wakulima na wadau wengine wa<br />
kilimo zikiwemo asasi za fedha na<br />
kushirikiana na Jeshi la polisi kupitia<br />
ulinzi wa Polisi Jamii.<br />
Walitolea mfano wa mfumo wa<br />
ulinzi shirikishi ulioanzishwa na<br />
mtandao wa wakulima wa kijiji cha<br />
Kolagwa ili kutatua changamoto<br />
ya usalama wa mali na maisha<br />
ya wananchi hasa baada ya tukio<br />
la kuvamiwa na kujeruhiwa kwa<br />
wakulima waliokuwa wamepata<br />
mkopo.<br />
Wakielezea kuhusiana na<br />
changamoto walizokabiliana<br />
nazo katika kufanikisha siku hiyo<br />
wamesema kuwa ni pamoja na<br />
uhaba wa rasilimali fedha na kwa<br />
kuwa tukio hili lilikuwa la linafanyika<br />
kwa mara ya kwanza ilichukua muda<br />
mrefu kuwashawishi wadau na<br />
kukubali kushiriki.<br />
Mojawapo ya dosari zilizojitokeza<br />
kwenye maadhimisho hayo ni<br />
pamoja na baadhi ya wakuu wa<br />
idara za halmashauri ya wilaya<br />
kutohuhiria na hivyo changamoto<br />
kadhaa zilizoibuliwa na wakulima<br />
zilikosa majibu sahihi.<br />
Mfano kukosekana kwa wataalamu<br />
wa idara ya Afya kulikuwa ni kikwazo<br />
kwa shughuli muhimu ya upimaji<br />
wa hiari wa VVU kwa washiriki<br />
waliokuwa tayari kufanya hivyo.<br />
Siku hii maalum ya wanamtandao<br />
ilihudhuriwa na wadau kutoka asasi<br />
mbalimbali yakiwemo mabenki,<br />
kampuni za simu za mkonini, Jeshi<br />
la polisi, viongozi wa halmashauri<br />
ya wilaya ya Mkuranga, viongozi wa<br />
mtandao wa wilaya na watumishi<br />
wa <strong>MVIWATA</strong> pamoja na wakulima<br />
kutoka vijiji 16 vya wilaya hiyo.<br />
Na maadhimisho ya siku hiyo<br />
yalisindikizwa na burudani za aina<br />
mbalimbali ikiwemo vikundi vya<br />
ngoma na baadaye mashindano<br />
ya mpira wa kikapu kwa timu za<br />
wanawake.<br />
Wakati huo huo, Mtandao<br />
wa kati wa <strong>MVIWATA</strong> Mkuranga<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 19<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11
Maazimio ya Kongamano...<br />
Inatoka uk. wa 8<br />
waliazimia mambo yafuatayo:<br />
1. Sisi wakulima wadogo tunasikitika<br />
kuona kwamba maadili na misingi<br />
ya Azimio la Arusha vimewekwa<br />
kando kama msingi wa mfumo<br />
wa uzalishaji na hivyo kukuza<br />
matabaka ambapo matajiri<br />
wachache ndiyo wanothaminiwa<br />
na watawala wakati sisi tulio<br />
wengi tukiwa tunapuuzwa katika<br />
mfumo wa uzalishaji.<br />
2. Sisi wakulima wadogo tunapinga<br />
kwa nguvu zote na kwa kauli moja<br />
mifumo yote ambayo kwa namna<br />
moja au nyingine inapelekea<br />
kumkandamiza mkulima mdogo na<br />
kumsukuma kando katika mfumo<br />
wa umilikaji ardhi na uzalishaji.<br />
Mifumo hiyo inahusisha uporaji<br />
wa rasilimali za ardhi ili kupisha<br />
wawekezaji wakubwa wa ndani<br />
na nje kwa kisingizio kwamba<br />
wakulima wadogo hawana ufanisi<br />
wa kuendeleza kilimo.<br />
3. Pamoja na kushukuru juhudi za<br />
serikali za kutoa huduma kwa<br />
wakulima, sisi wakulima wadogo<br />
tumekubaliana kwamba kuna<br />
kasi ndogo sana ya maendeleo<br />
ya mkulima mdogo na maisha<br />
ya mkulima mdogo kwa ujumla<br />
yameendelea kuwa duni hata<br />
baada ya miaka 50 ya uhuru.<br />
Tunaazimia kujipanga kuhakikisha<br />
kuwa katika miaka 50 ijayo<br />
wakulima wadogo wawe mhimili<br />
wa uchumi wetu.<br />
4. Wakulima wadogo tumekerwa na<br />
kuchoshwa na migogoro mingi ya<br />
ardhi isiyo na kikomo kila kukicha<br />
katika maeneo mbalimbali ya nchi<br />
hii, ambayo inasababishwa na<br />
usimamizi mbovu na utekelezaji<br />
hafifu wa sheria zetu ikiwemo<br />
sera ya Ardhi ya Taifa pamoja<br />
na sheria za ardhi za 1999 na<br />
kanuni zake. Aidha, tunaitaka<br />
serikali ichukue hatua dhidi ya<br />
wawekezaji ambao wamekiuka<br />
masharti ya kupewa ardhi kwa<br />
ajili ya matumizi waliyoombea.<br />
Vile vile, tunaitaka serikali ichukue<br />
hatua za haraka katika kutatua<br />
migogoro inayohatarisha amani<br />
katika maeneo mbalimbali ya nchi;<br />
kwa mfano mgogoro wa ardhi<br />
Kibaigwa, Mbalali, Kiteto n.k<br />
5. Tunasikitishwa na kuhuzunishwa na<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />
kukua kwa matabaka kati ya matajiri<br />
na masikini wengi wao tukiwa<br />
sisi wakulima wadogo ambapo<br />
hatuna uhakika hata wa upatikanaji<br />
wa huduma za msingi ikiwemo<br />
upatikanaji wa huduma muhimu<br />
za kijamii hususan elimu ya watoto<br />
wetu, huduma za afya kwa familia<br />
zetu, miundombinu ya barabara na<br />
maji safi na salama. Kwa sababu hiyo<br />
tunaitahadharisha serikali kuchukua<br />
hatua thabiti za kupunguza pengo<br />
kati ya walionacho na wasionacho<br />
ili kulinda amani na mshikamano wa<br />
nchi yetu<br />
6. Sisi wakulima wadogo tunaazimia<br />
kuwawajibisha viongozi wote<br />
ambao hawasimamii maslahi<br />
ya wakulima wadogo, ikiwemo<br />
kujipanga kutowapigia kura viongozi<br />
wanaosaliti wakulima wadogo<br />
katika uchaguzi mkuu wa <strong>20</strong>15.<br />
Wakulima wadogo tusiburuzwe<br />
na wanasiasa: tunapaswa kujenga<br />
uwezo wetu wa kutofautisha<br />
kauli za wanasiasa na ahadi zao za<br />
majukwaani ili kuwabaini wanasiasa<br />
wenye dhamira thabiti na wale<br />
ambao kauli zao ni za kutetea<br />
maslahi yao binafsi.<br />
7. Sisi wakulima wadogo tumeazimia<br />
kujenga mshikamano miongoni<br />
mwetu ili tuweze kudai haki zetu<br />
kwa nguvu ya hoja na bila woga.<br />
Tutatumia fursa ya mchakato<br />
wa utungaji wa katiba ili katiba<br />
itakayotungwa ilinde vyema zaidi<br />
maslahi ya wakulima wadogo<br />
8. Sisi wakulima wadogo tumegundua<br />
kwamba kudai haki kwa kupiga<br />
kelele tu haitoshi. Kwa mfano<br />
serikali imeziba masikio kuhusu<br />
kilio chetu cha kuwa na uhuru wa<br />
kuuza mazao yetu kwa mnunuzi<br />
tunayetaka ndani na nje ya nchi.<br />
Kwa hiyo tumedhamiria kutumia<br />
sera, sheria na kanuni zilizopo<br />
kudai haki zetu bila woga katika<br />
vyombo vya sheria vilivyopo na<br />
njia nyinginezo halali.<br />
9. Ili kuongeza nguvu ya <strong>MVIWATA</strong>,<br />
sisi ambao ni wanachama takriban<br />
elfu sabini (70,000), tunaazimia<br />
kuongeza idadi ya wanachama<br />
wetu nchi nzima na shughuli<br />
zetu za kiharakati pamoja na<br />
kuelimishana kuhusu haki na<br />
wajibu wa mkulima mdogo.<br />
KUTOKA MITANDAONI<br />
Mkuu wa wilaya<br />
ahimiza...<br />
Inatoka uk. wa 18<br />
umefanya mkutano wake Mkuu<br />
wa mwaka Disemba 5,<strong>20</strong>11<br />
huku ukitanguliwa na warsha ya<br />
siku moja kwa ajili ya kujifunza<br />
na kujadili changamoto kadhaa<br />
zinazowakabili wakulima wilayani<br />
humo.<br />
Mada kuu iliyojadiliwa kwenye<br />
warsha ni mafunzo ya hatua za<br />
mchakato wa uanzishwaji wa<br />
Chama cha Akiba na Mikopo<br />
(SACCOS) cha wakulima wa<br />
zao la muhogo somo ambalo<br />
lilifundishwa na Afisa kutoka Ofisi<br />
ya Ushirika wilayani hapo.<br />
Washiriki walitafakari zaidi<br />
faida za kuwa na chombo hicho<br />
ambacho kitarahisisha upatikanaji<br />
wa mitaji na kuwasaidia kupanua<br />
shughuli zao.<br />
Baada ya mafunzo hayo,<br />
washiriki walichagua kamati ya<br />
muda iliyopewa jukumu la kuandaa<br />
rasimu ya katiba ya SACCOS<br />
na kukusanya michango kama<br />
kiingilio na hisa kutoka katika vijiji<br />
16 ambavyo ni Dundani, Mkuranga,<br />
Mwanambaya, Mwanadilatu,<br />
Sotele, Mavunje, Njopeka, Misasa,<br />
Kerezange, Kizapara, Tungi, Tunda,<br />
Mamdimpela, Mamdikongo,<br />
Lupondo na Kolangwa.<br />
Aidha siku ya mkutano<br />
mkuu wa mtandao, wajumbe<br />
walijadiliana juu ya uendelevu<br />
wa mitandao ikiwa ni pamoja na<br />
kutafuta mbinu itakayotumika<br />
katika kuongeza wanachama<br />
ambapo viongozi walikumbushwa<br />
kuwahamasisha wakulima<br />
kujiunga na <strong>MVIWATA</strong> na kuwa<br />
na kadi za uanachama, kuweka<br />
mfumo mzuri wa ukusanyaji wa<br />
michango na pia kuweka mfumo<br />
wa utunzaji wa kumbukumbu za<br />
wanachama.<br />
Mkutano huo pia ulipokea<br />
taarifa ya utekelezaji wa shughuli,<br />
taarifa ya mapato na matumizi ya<br />
shughuli za mtandao kwa mwaka<br />
<strong>20</strong>11 na kujadili mpango mkakati<br />
wa mwaka <strong>20</strong>12.<br />
19
MAKALA<br />
Wakulima, matrekta <strong>20</strong>0 waandamana<br />
kudai haki<br />
Na Goodness Mrema, Kibaigwa<br />
Wakulima wilayani<br />
Kongwa mkoani<br />
Dodoma wakiwa<br />
na matrekta yao zaidi ya <strong>20</strong>0<br />
mnamo Disemba 1, <strong>20</strong>11, walifanya<br />
maandamano makubwa na kufunga<br />
kwa muda barabara kuu ya Dodoma<br />
– Dar es Salaam katika eneo la<br />
Kibaigwa wakipinga maamuzi ya<br />
serikali ya kuwazuia kulima kwenye<br />
mashamba yao yaliyoko wilaya jirani<br />
ya Kiteto mkoani Manyara.<br />
Wakulima hao wana mashamba<br />
yao makubwa kwenye vijiji tisa<br />
vya wilaya ya Kiteto ambavyo ni<br />
Lendolai, Mlimahamba, Laitini, Mbigiri,<br />
Kutelimeinyi, Seseni, Laipela, Kimarai<br />
na Kisima, ambavyo vimeingizwa<br />
kwenye eneo la hifadhi ya taifa na<br />
kuzuia shughuli zozote za kilimo.<br />
Maandamano hayo yalifanyika<br />
katika mji mdogo wa Kibaigwa<br />
wilayani Kongwa mahali ambako<br />
kuna soko la kimataifa la Mahindi<br />
ambalo zaidi ya asilimia 60 ya mazao<br />
yanayopokelewa sokoni hapo,<br />
yanatoka kwenye vijiji hivyo.<br />
Wakizungumza kwa nyakati<br />
tofauti wakulima hao walisema kuwa<br />
walianza kulima mashamba hayo tangu<br />
mwaka 1990 lakini cha kushangaza<br />
mwaka <strong>20</strong>06 walitaarifiwa kuwa<br />
eneo hilo limegeuzwa kuwa hifadhi<br />
ya mbuga ya wanyama.<br />
Bw. Clement Petro, mmoja wa<br />
wakulima walioathiriwa na maamuzi<br />
hayo anaeleza kuwa baada ya<br />
kuzuiwa walifungua kesi mahakama<br />
<strong>20</strong><br />
Mmoja wa wakulima walionyang’anywa ardhi akizungumza siku ya maandamano ya<br />
Kibaigwa Disemba 1, <strong>20</strong>11<br />
kuu kupinga uamzi huo na kushinda.<br />
Hata hivyo halmashauri ya<br />
Kiteto ilikata rufaa mahakama ya<br />
rufaa kupinga hukumu hiyo ambapo<br />
ilishinda na wakulima wakaamriwa<br />
kuondoka katika eneo hilo.<br />
Hata hivyo, wakulima hao<br />
wanasikitishwa na maamuzi hayo<br />
huku wakisema serikali haiwatakii<br />
mema kwa kuwa ni hivi karibuni tu<br />
serikali imewahamasisha kuchukua<br />
mikopo ya matrekta na kwamba<br />
wanatarajia mavuno kutoka kwenye<br />
mashamba hayo ili kulipa mikopo.<br />
“Ni hivi majuzi tu serikali<br />
imetuhamasisha kuchukua mikopo<br />
ya matrekta nasi tumeitikia kwa<br />
wingi tukifahamu kuwa tunayo ardhi<br />
ya kutosha na tukivuna tutarejesha<br />
mkopo, sasa leo tunazuiwa kulima, huu<br />
ni sawa na uuaji,” alisema Bw. Petro.<br />
Bw. Omary Athuman ni mkulima<br />
na anamiliki matrekta zaidi ya 10<br />
wilayani humo na anasema “kutokana<br />
na halmashauri kutufukuza kutoka<br />
katika eneo hili nina wasiwasi kama<br />
nitaweza kurejesha mkopo wa<br />
matrekta niliyokopa kutoka katika<br />
Shirika la Uchumi la Jeshi la Kujenga<br />
taifa(Suma JKT) tawi la Dodoma.”<br />
“Mimi sijui hii dhana ya kilimo<br />
kwanza inatekelezwaje kwani mwanzo<br />
tulidhani kuwa ni sera nzuri lakini hivi<br />
sasa tunaona haitekelezwi kwa vitendo<br />
na kuongeza kuwa yeye anazo hekari<br />
300 ambazo huwa analima mahindi na<br />
kupata mavuno mengi.”<br />
Naye mkulima Bw. Ali Khalifan<br />
Said, alisema kuwa wakati amri hiyo<br />
inaanza kutekelezwa tayari walikuwa<br />
wameshaandaa mashamba na hivyo<br />
kuondoka katika eneo hilo ni hasara<br />
kubwa sana kwake.<br />
“Wanataka tuondoke katika eneo<br />
hili lakini cha ajabu hawatuambii<br />
twende wapi wala nani atalipa madeni<br />
ya matrekta yetu tuliyokopa na nyumba<br />
tulizojenga kwa mkopo” alisema Said.<br />
Wakulima hao walielekeza kilio<br />
chao kwa Rais Jakaya Kikwete<br />
wakimuomba kuingilia kati suala<br />
hilo ili waweze kurudishiwa ardhi na<br />
kuendelea na uzalishaji, kwa sababu<br />
viongozi wengine ngazi ya wilaya na<br />
mkoa wameshindwa kuwasaidia.<br />
Kwa upande wake, meneja wa soko<br />
la wakulima la Kibaigwa Bw. Kusekwa<br />
Dalali alisema kuwa wamekuwa<br />
wakipokea mazao kutoka katika<br />
mikoa mitano ambayo ni Dodoma,<br />
Morogoro, Manyara, Iringa na Tanga.<br />
Endelea <strong>Uk</strong> wa 21<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />
KUTOKA MITANDAONI<br />
Nani mchawi wa maendeleo ya<br />
wakulima nchini?<br />
Na Goodness Mrema<br />
Uchumi wa wakulima<br />
wadogo kabla na baada<br />
ya uhuru uliendelea kuwa<br />
mikononi mwa wakulima wenyewe<br />
kupitia vyama vya ushirika.<br />
Chanzo cha kuanzishwa kwa<br />
vyama vya ushirika, ilikuwa ni<br />
baada ya serikali ya kikoloni kuanza<br />
kudhibiti faida ya mauzo ya mazao<br />
ya wakulima bila kuwashirikisha.<br />
Ni kweli mkoloni ndiye alianzisha<br />
kilimo cha mazao ya biashara ili<br />
kupata fedha za kigeni. Kabla ya hapo<br />
wakulima walijishughulisha na kilimo<br />
cha mazao ya chakula tu na ilipobidi<br />
walibadilishana bidhaa pasipo kutumia<br />
fedha kama ilivyo sasa.<br />
Madhumini ya wakoloni ya<br />
kuanzisha kilimo cha mazao ya<br />
biashara na kuwaingiza wenyeji<br />
kwenye mfumo wa biashara yalikuwa<br />
ni pamoja na kupata malighafi kwa ajili<br />
ya viwanda huko ulaya, lakini pia kwa<br />
minajili ya kupata fedha za kugharamia<br />
uendeshaji wa makolini yao.<br />
Kwa kuwaingiza wakulima<br />
kwenye kilimo cha biashara mkoloni<br />
aliweza kutoza kodi na makato<br />
mengine ambayo ndiyo yaliyotumika<br />
kuendesha serikali.<br />
Ili kupata fedha zaidi mkoloni<br />
aliwanyonya wakulima kwa njia<br />
mbalimbali, kwanza kununua mazao<br />
kwa bei ndogo kuliko gharama<br />
za uzalishaji, na pili kwa kuwauzia<br />
pembejeo za kilimo kwa bei<br />
waliyojipangia mwenyewe.<br />
Na kama hiyo haitoshi, akaanza<br />
kuwalazimisha kulima mazao<br />
aliyoyataka yeye kwa manufaa yake<br />
kitu ambacho kilitafsiriwa kuwa ni<br />
utumwa.<br />
Mtindo huu wa manunuzi<br />
kujipangia bei ya kuuzia pembejeo<br />
na kisha kujipangia ile ya kununulia<br />
mavuno pasipo majadiliano, ndiyo<br />
uliwazindua wakulima na kuanzisha<br />
vyama vya ushirika.<br />
Vyama hivyo vilisaidia siyo tu kuwa<br />
na sauti ya pamoja lakini pia katika<br />
kupigania bei nzuri inayoendana na<br />
gharama halisi za uzalishaji. Vyama<br />
hivi pia vilijiingiza katika kusambaza<br />
pembejeo na huduma nyingine kwa<br />
mkulima.<br />
Wakulima wakajihamasisha na<br />
kuanzisha vyama vya ushirika katika<br />
sehemu mbalimbali za nchi.<br />
TANU ilivyoanzishwa haikusita<br />
kuziunganisha nguvu za vyama vya<br />
ushirika na vyama vya wafanyakazi<br />
na makundi mengine katika harakati<br />
za uhuru. Lakini uhuru ulipopatikana,<br />
serikali ya TANU iliendelea na<br />
staili ile ya mkoloni ya kuwapunja<br />
wakulima kwa kudhibiti faida ya<br />
mauzo bila kuwashirikisha ili ipate<br />
fedha za kugharamia uendeshaji wa<br />
kazi za serikali.<br />
Na ili kuhakikisha wakulima<br />
hawafurukuti, mwaka 1967 serikali<br />
iliviunganisha vyama vyote vya<br />
ushirika nchini chini ya mwavuli<br />
ulioitwa Muungano wa Vyama vya<br />
Ushirika Nchini.<br />
Serikali pia ilianzisha Bodi za Mazao<br />
mbalimbali kuisaidia kudhibiti faida ya<br />
mauzo kwa lengo lile lile la kupata<br />
fedha za uendeshaji wa serikali.<br />
Hata hivyo ilipofika mwaka 1976,<br />
serikali iliuvunjilia mbali ushirika<br />
na badala yake kukaanzishwa bodi<br />
mbalimbali za mazao hasa mazao ya<br />
biashara.<br />
Bodi zilizoanzishwa ni pamoja na<br />
za kahawa, pareto, tumbaku, chai na<br />
korosho bila kusahau mkonge kwani<br />
lilikuwa ndilo zao lenye kuingiza<br />
fedha nyingi za kigeni hadi wakati<br />
huo.<br />
Baadaye tena baadhi ya bodi za<br />
mazao zikabadilishwa kwa sheria<br />
ya bunge kuwa mamlaka za mazao.<br />
Hivyo kuwa na mamlaka ya mkonge,<br />
mamlaka ya pamba na kadhalika.<br />
Kazi kubwa ya mamlaka hizi ikiwa<br />
ni kuimarisha udhibiti wa mfumo wa<br />
uzalishaji, usafirishaji na uuzaji wa<br />
mazao ndani na nje ya nchi.<br />
Na kwa kuwa mamlaka hizo<br />
zilianzishwa kwa sheria ya bunge<br />
kukawa na udhibiti zaidi wa mazao<br />
husika katika kila hatua. Kwa lugha<br />
nyingine, mamlaka hizi ziligeuka<br />
polisi wa wakulima.<br />
Ni bodi za mazao ndizo zilizopanga<br />
kima cha chini ambacho mkulima<br />
alitakuwa kulima, utunzaji wa mazao<br />
shambani, utaratibu na hata tarehe<br />
ya kuvuna na bila kusahau zikipanga<br />
bei ya kununulia mazao kutoka kwa<br />
wakulima na pia bei ya pembejeo<br />
walizouziwa wakulima.<br />
Chini ya mamlaka za mazao<br />
mkulima akageuka kuwa mfungwa<br />
anayepaswa tu kutekeleza kile<br />
alichoambiwa. Uhuru na demokrasia<br />
waliyokuwa wameizoea kwenye<br />
vyama vya ushirika vikapotea.<br />
Badala yake sheria za kikoloni<br />
zinazolazimisha mkulima kulima zao<br />
fulani pasipo hiari yake na ambazo<br />
ndizo zilikuwa zimewakasirisha watu<br />
hadi kuupigania uhuru zikaimarishwa<br />
ndani ya Tanzania huru.<br />
Wakulima, matrekta <strong>20</strong>0 waandamana...<br />
Inatoka uk. wa <strong>20</strong><br />
Alisema kwa mwaka soko linauza<br />
zaidi ya tani 1000 za mazao. “Tunauza<br />
zaidi kwenye maeneo ya Dar es<br />
Salaam, Kilimanjaro, MorogoroTanga,<br />
Iringa na Mbeya na mikoa ya kanda ya<br />
ziwa katika mikoa ya Mara, Mwanza<br />
na Shinyanga ambako tumeanza<br />
mwaka jana, pia kabla ya kufungwa<br />
kwa mipaka tulikuwa tunapata<br />
wateja kutoka Mombasa na Nairobi<br />
lakini pia Zanzíbar ni wanunuzi<br />
wazuri wa mazao yetu.”<br />
Mazao wanayoyapokea katika<br />
soko hilo ni pamoja na mahindi,<br />
mbaazi, tetere, alzeti, nyonyo na<br />
maharagwe na kwamba asilimia 60<br />
ya mazao hayo hutoka katika wilaya<br />
ya Kiteto.<br />
“Kitendo hiki cha wakulima<br />
kuzuiwa kulima mashamba<br />
yao kwenye vijiji hivyo tisa<br />
kinaashiria kufa kwa soko letu<br />
kwa sababu asilimia 60 ya mazao<br />
yanayopokelewa hapa hutoka<br />
wilayani Kiteto hasa kwenye vijiji<br />
hivyo,” alisema Bw. Kusekwa.<br />
21
KATUNI<br />
22<br />
SASA<br />
AFANYAJE NA<br />
MAISHA HAYA MAGUMU<br />
TUNAZALISHA KWA<br />
NGUVU ZOTE LAKINI<br />
FAIDA NI KIDOGO.<br />
LAKINI MAMA CHUNGU HATA NCHI ZA<br />
WENZETU MAJIRANI HAWAJAPIGA<br />
HATUA SANA KATIKA MIPANGO YA<br />
KUWAWEZESHA WAKULIMA<br />
WADOGO.<br />
MIAKA 50 YOTE<br />
TUMESHINDWA KUFIKIA<br />
MALENGO YA KUMUINUA<br />
MKULIMA MDOGO, MIMI NAONA<br />
TUSEME MIAKA 50 YA UHURU<br />
TUMETHUBUTU, TUMESHINDWA,<br />
TUJIPANGE UPYA.<br />
MZEE<br />
KUJIKO HAKATI<br />
TAMAA MWAKA WA<br />
PILI AMEKOSA MAHINDI<br />
LAKINI BADO ANAENDA<br />
KUPANDA TENA.<br />
LAKINI<br />
BABA CHUNGU<br />
SERIKALI SI NDIO<br />
INATAKIWA KUMSIMAMIA<br />
MKULIMA?<br />
‘EHE, EHE EHE!<br />
NDIO<br />
LAKINI SI NDIO<br />
TUNASHEHEREKEA<br />
MIAKA 50 YA UHURU SASA<br />
ANGALIA MIAKA YOTE SERIKALI<br />
IMEMSAIDIA VIPI MKULIMA<br />
KUJIKWAMUA na KILIMO CHA<br />
JEMBE LA MKONO<br />
MH<br />
TUSIJILIN-<br />
GANISHE NA NCHI<br />
MASIKINI ZENYE<br />
RASILIMALI CHACHE<br />
KULIKO TANZANIA<br />
AAH<br />
JEMBE<br />
LENYEWE LA<br />
MKONO?<br />
MIMI SIONI<br />
SABABU YA KUSHEHEREKEA<br />
MIAKA 50 YA UHURU KAMA<br />
MATATIZO YA MSINGI YANA-<br />
TAKIWA KUSHUGHULIKIWA<br />
HAYAJASHUGHULIKWA<br />
LAKINI<br />
ACHA AJARIBU<br />
TENA ANAWEZA<br />
KUPATA.<br />
WAKATI<br />
MKULIMA HUYO<br />
HUYO NDIO ANAZAL-<br />
ISHA CHAKULA CHA<br />
KULISHA TAIFA<br />
TULENGE MA-<br />
FANIKIO MAKUBWA BILA<br />
KUJALI MAJIRANI ZETU, SISI<br />
TUNA RASILIMALI NA ARDHI YA<br />
KUTOSHA AMBAZO HATUTUMII<br />
IPASAVYO MFANO ARDHI, MITO<br />
NA MAZIWA.<br />
MATATIZO<br />
GANI HAYO?<br />
MARADHI,<br />
UJINGA NA UMASKINI,<br />
NA UMASKINI NDIO ADUI<br />
No. 1 NA BADO WAKULIMA<br />
HATUPEWI KIPAUMBELE<br />
JAMANI!<br />
AAH<br />
KILIMO<br />
CHENYEWE<br />
CHA MVUA ZA<br />
KUBAHATISHA?<br />
TENA<br />
NA KIJEMBE<br />
KIMOJA CHA<br />
MKONO!?<br />
ILA MANENO YAKO<br />
MAMA CHUNGU NI YA<br />
BUSARA<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11
MWAKA<br />
1961 - 1985 ILIWEZA<br />
KUWASAIDIA WAKULIMA<br />
KWA KUANZISHA AZIMIO LA<br />
ARUSHA, VIWANDA VILITUMIA<br />
MALI GHAFI ZA WAKULIMA LAKINI<br />
BAADA YA 1985 - <strong>20</strong>11 MKULIMA<br />
HANA THAMANI TENA.<br />
MIAKA 50 YA<br />
UHURU WAKULIMA WENGI<br />
WANAONDOLEWA KWENYE<br />
ARDHI YA MABABU. WAKULIMA<br />
WANAPIGWA WANAFUNGWA,<br />
WAKITETEA ARDHI YAO<br />
NA KUUWAWA.<br />
KWELI<br />
TUMEKUWA<br />
TUKIISHI KWA MATAMKO<br />
MBALIMBALI KAMA KILIMO<br />
NI UTI WA MGONGO, CHAKULA<br />
NI UHAI, NA SASA KILIMO<br />
KWANZA PAMOJA NA HAYO<br />
WAKULIMA WAMEBAKI<br />
DUNI.<br />
HOFU<br />
GANI TENA?<br />
WANAHOFU<br />
KUPORWA ARDHI<br />
YAO.<br />
MIMI<br />
NAFIKIRI IMEFI-<br />
KA WAKATI WAKULIMA<br />
WAUNGANE WAIMARISHE<br />
UMOJA WAO.<br />
NA ARDHI<br />
YENYEWE WANA-<br />
PEWA WAWEKEZAJI<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />
SIO UMOJA TU SASA HIVI<br />
TUNATAKIWA TUJIPANGE NA<br />
KUZIFAHAMU SHERIA ZA<br />
ARDHI ILI TUITETEE HAKI<br />
YETU<br />
SASA<br />
HAPO THAMANI<br />
YA MKULIMA<br />
MDOGO IKO WAPI?<br />
NDIO<br />
MAANA BABA WA<br />
TAIFA ALISEMA MWAF-<br />
RIKA AKIRUHUSIWA KUUZA<br />
ARDHI BAADAE ARDHI YOTE<br />
ITAMILIKIWA NA WAGENI<br />
SABABU YA UMASKINI.<br />
HUWEZI<br />
KUJIZUIA KUUZA<br />
ARDHI WAKATI<br />
WEWE NI MAS-<br />
KINI<br />
HII IMESABA-<br />
BISHWA NA SERA<br />
AMBAZO HAZIMJALI<br />
SANA MKULIMA<br />
MDOGO<br />
SAWA<br />
KABISA SISI<br />
NDIO WAZALISHAJI<br />
WAKUBWA WA CHAKULA<br />
CHA NCHI SIO HAO<br />
WAWEKEZAJI WA-<br />
NAOPELEKA CHAKULA<br />
NJE YA NCHI<br />
NDIO<br />
KATUNI<br />
JAMANI EH TUACHE<br />
KULALAMIKA SI MMESIKIA<br />
KAMATI YA KUKUSANYA MAONI<br />
TUITUMIE VIZURI FURSA HII TUTOE<br />
MAONI ILI KATIBA MPYA IMLINDE<br />
MKULIMA MDOGO JUU YA DHULUMA<br />
TUNAZOFANYIWA BASI!!<br />
EEH NDIO<br />
MAANA MIAKA 50<br />
WANAISHI KWA HOFU!<br />
SASA<br />
IMEFIKA WAKA-<br />
TI SERIKALI IFANYIE<br />
KAZI MADHAIFU YOTE<br />
YANAYO MKANDAMIZA<br />
MKULIMA<br />
23
KUTOKA MITANDAONI<br />
Wakulima 30 wahitimu mafunzo ya<br />
uwezeshaji na usimamizi vikundi<br />
Na Goodness Mrema, Nyandira<br />
Mvomero<br />
Wakulima nchini<br />
wamehimizwa kutumia<br />
vyema ujuzi na elimu<br />
wanayopewa wanaposhiriki<br />
mafunzo mbalimbali kwa ajili ya<br />
maendeleo ya wakulima wote<br />
nchini.<br />
Wito huo umetolewa Novemba<br />
7, <strong>20</strong>11 na Afisa Ushawishi na<br />
Utetezi wa <strong>MVIWATA</strong> Bw<br />
Thomas Laiser, alipokuwa akifunga<br />
mafunzo ya Wakulima Wawezeshaji<br />
30 (Mapromota) waliokuwa<br />
wakihudhuria mafunzo ya wiki<br />
mbili ya usimamizi na uendeshaji wa<br />
vikundi katika kituo cha mafunzo ya<br />
Wakulima cha Nyandira wilaya ya<br />
Mvomero mkoani Morogoro.<br />
Wawezeshaji hao walitoka<br />
kwenye masoko matatu<br />
yanayojengwa na <strong>MVIWATA</strong> katika<br />
vijiji vya Igurusi Mbarali Mbeya, Matai<br />
24<br />
na Kasanga wilaya ya Sumbawanga<br />
Vijijini.<br />
Bw. Laiser alisema <strong>MVIWATA</strong><br />
imekuwa ikitoa mafunzo ya aina<br />
mbalimbali kwa lengo la kuwajengea<br />
uwezo wakulima wachache<br />
(wakulima wakufunzi) ambao<br />
wanatarajiwa kwenda kusambaza<br />
ujuzi huo kwa wakulima wengine.<br />
Mbali na mafunzo hayo <strong>MVIWATA</strong><br />
imekuwa ikiwezesha wakulima<br />
kushiriki semina, mikutano na ziara<br />
za mafunzo nje ya nchi na kwamba<br />
wahusika wanaporudi kwenye<br />
maeneo yao wanapaswa kuwa<br />
chachu ya mabadiliko ya kusaidia<br />
kusukuma mbele maendeleo.<br />
“Tusiwe wachoyo wa kuwagawia<br />
wenzetu maarifa tuliyopewa,<br />
tumieni vyema maarifa mliyoyapata,<br />
mkawasaidie viongozi na wakulima<br />
wenzenu kuleta mabadiliko ya<br />
kiuchumi na kuondokana na maisha<br />
ya kimasikini,” alisema Bw. Laiser.<br />
Aidha aliwataka washiriki<br />
wa mafunzo hayo kuimarisha<br />
Wahitimu wa mafunzo wakifurahia baada ya kukabidhiwa vyeti vya mafunzo hayo<br />
mshikamano na mawasiliano katika<br />
vikundi na mitandao ya wakulima<br />
nchini ili kuwa na sauti yenye nguvu<br />
itakayotimiza lengo la utetezi wa<br />
maslahi yao.<br />
“Mnatakiwa kuwasaidia wakulima<br />
waweze kujipanga,kujisimamia na<br />
kutetea maslahi yao na kuwezesha<br />
vikundi kushirikiana na wadau<br />
wengine,” alisema Bw. Laiser.<br />
Aliwahimiza wakulima hao pia<br />
kujenga utamaduni wa kutafuta<br />
habari mbalimbali kupitia vyombo<br />
vya habari na kuzitumia vyema habari<br />
wanazozipata kujiletea maendeleo.<br />
Katika risala yao wahitimu wa<br />
mafunzo hayo walisema watatumia<br />
vyema elimu waliyoipata kwa<br />
kuielimisha jamii na kuahidi kutimiza<br />
wajibu wao na kufanya kazi kwa<br />
kujituma.<br />
Wawezeshaji hao waliohitimu<br />
mafunzo pia waliomba kupewa<br />
ushirikiano na viongozi wa serikali<br />
ngazi za vijiji na kata ili kurahisisha<br />
utekelezaji wa majukumu yao.<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11
Jipatie nakala ya Jarida la Pambazuko katika ofisi<br />
za <strong>MVIWATA</strong> ngazi za kati zifuatazo<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Morogoro<br />
S.L.P 32<strong>20</strong> Morogoro<br />
Mahali: Uwanja wa Maonyesho NaneNane mkabala na<br />
ofisi za TASO<br />
Simu/Faksi: 023 261 41 84<br />
Barua Pepe: morogoro@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Rukwa<br />
S.L.P 468 Sumbawanga<br />
Mahali: Jengo la Bethlehem Center – Barabara ya Msakila<br />
Faksi: +255 25 280 25 58<br />
Simu: +255 764 232 747, +255 784 940 606<br />
Barua pepe: rukwa@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Mbeya<br />
S.L.P 3015 Mbeya<br />
Mahali: Jengo la Bima na CRDB Bank (Ghorofa ya<br />
mwisho<br />
Simu: +255 784 979 397, +255 652 835 568<br />
Barua pepe: mbeya@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Chunya<br />
Mahali: Jengo la Halmashauri, chumba Na.3<br />
Barua pepe: chunya@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Iringa<br />
S.L.P 918 Njombe<br />
Mahali: Jengo la Njoluma, Njombe mjini<br />
Simu: 0782 241 224, +255 767 241 224<br />
Barua pepe: iringa@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Kilimanjaro<br />
S.L.P 7389 Moshi<br />
Mahali: Mbuyuni sokoni- ghorofa ya GOLDEN GROWN<br />
LODGE<br />
Simu: +255 27 275 16 39, +255 784 7<strong>20</strong> 3<strong>20</strong><br />
Barua pepe: kilimanjaro@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Kagera<br />
S.L.P <strong>17</strong>53 Bukoba Mjini<br />
Mahali: Ofisi za Mayawa-Mtaa wa Rwamishenyi, Barabara<br />
ya Uganda<br />
Simu: +255 788 685818, +255 782 154961, +255 755 522 447<br />
Barua pepe: kagera@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Dodoma<br />
S.L.P 3293 Dodoma<br />
Mahali:Area C Dodoma eneo la INADES Formation<br />
Tz,mkabala na msikiti wa Area C<br />
Simu:255-26-2350013, +255 782 257 783,<br />
+255 767 881 352<br />
Faksi: +255 26 2350744<br />
Barua pepe: dodoma@mviwata.org<br />
Pambazuko Na. 40 Toleo la Oktoba – Disemba <strong>20</strong>11<br />
Mwenyekiti<br />
<strong>MVIWATA</strong> Monduli (MVIWAMO)<br />
S.L.P 47 Monduli<br />
Mahali: Barabara ya Boma-Moringe Sekondari, Monduli<br />
Mjini<br />
Simu: 255-27-253 8029, +255 27 253 8337<br />
Faksi: +255 27 253 8338<br />
Barua pepe: monduli@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Manyara<br />
S. L. P. 446,<br />
Babati Manyara<br />
Mahali: Barabara ya Nyerere<br />
SIMU: +255 27 253 0385 Faksi: +255 27 253 0707<br />
Baruapepe: manyara@mviwata.org<br />
Mwenyekiti<br />
<strong>MVIWATA</strong> Tabora<br />
S.L.P <strong>17</strong>5 Igunga<br />
Mahali: Mtaa wa Uarabuni<br />
Simu: +255 784 398 414, +255 782 219 551<br />
Barua pepe: tabora@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Zanzibar<br />
S.L.P 149 Zanzibar<br />
Mahali: Mwana kwerekwe- mkabala na shule ya sekondari<br />
M’kwerekwe A<br />
Simu: +255 773 926 955, +255 777 470 518<br />
+255 783 651 135<br />
Barua pepe: zanzibar@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Ruvuma<br />
S.L.P 696 Songea Manispaa<br />
Mahali: Jengo la TTCL ghorofa ya 2<br />
Simu: +255-25-2600626, +255 756 096 291<br />
Barua pepe: ruvuma@mviwata.org<br />
Mratibu<br />
<strong>MVIWATA</strong> Mkuranga<br />
S.L.P 56 Mkuranga<br />
Mahali: Karibu na Stendi ya Kimanzichana<br />
Simu: 0786 158 646<br />
Barua pepe: mkuranga@mviwata.org<br />
MAWAKALA<br />
Mwenyekiti:<br />
<strong>MVIWATA</strong> Shinyanga<br />
S.L.P 1024 Shinyanga<br />
Mahali: Chuo cha Ushirika Moshi tawi la Shinyanga<br />
(Kizumbi)<br />
Simu: +255 763 740 675, +255 755 546 311<br />
Barua Pepe: shinyanga@mviwata.org<br />
Mwenyekiti<br />
<strong>MVIWATA</strong> Kigoma<br />
S.L.P 1144 Kigoma<br />
Mahali: Ndani ya ofisi ya KIKANGONET, Lumumba road<br />
jengo la NHC chumba <strong>20</strong>5<br />
Simu: 0713 565 252, 0762 565 252<br />
Barua pepe: aisimba@yahoo.co.uk<br />
25
IJUE <strong>MVIWATA</strong><br />
Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania- <strong>MVIWATA</strong><br />
Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (<strong>MVIWATA</strong>) ni chombo cha kuunganisha wakulima wadogo ili kuwa na sauti moja katika utetezi wa<br />
maslahi yao ya kiuchumi, kijamii, kiutamaduni na kisiasa.<br />
Mtandao huu ulianzishwa mwaka 1993 na wakulima wadogo. Kauli mbiu ya <strong>MVIWATA</strong> ni ‘Mtetezi wa Mkulima ni Mkulima<br />
Mwenyewe’.<br />
Falsafa, utume na dira ya <strong>MVIWATA</strong><br />
Falsafa ya <strong>MVIWATA</strong> inajengwa katika ya misingi ya ushawishi na utetezi wa maendeleo ya wakulima wadogo katika nyanja za kiuchumi na<br />
kijamii; kuwezesha mawasiliano na kujifunza kwa kubadilishana uzoefu miongoni mwa wakulima.<br />
Utume wetu:<br />
Kuimarisha mawasiliano na kuwaunganisha wakulima wadogo kupitia vikundi na mitandao yao katika ngazi mbali mbali ili kujenga mtandao wa<br />
kitaifa wenye nguvu ya kuwezesha ushiriki na uwakilishi wa kweli wa maslahi ya wakulima wadogo katika ngazi zote za maamuzi.<br />
Dira yetu:<br />
<strong>MVIWATA</strong> ni kuwa chombo imara chenye nguvu za ushiriki na uwakilishi wa mawazo ya mkulima katika mchakato wa maamuzi ya kiuchumi,<br />
kijamii na kisiasa. Kuwa na uwezo wa kutekeleza na kufuatilia michakato na shughuli za maendeleo ya kiuchumi na kijamii yanayogusa maslahi ya<br />
wakulima wadogo.<br />
Malengo ya <strong>MVIWATA</strong><br />
1. Kuwezesha mawasiliano miongoni mwa wakulima wadogo ili kujenga kwa pamoja mbinu na mikakati ya ushawishi na utetezi kwa maslahi ya<br />
wakulima wadogo, kiuchumi na kijamii.<br />
2. Kubadilishana mawazo, ujuzi na uzoefu juu ya kilimo na shughuli mbalimbali za wakulima ili kuboresha maisha na kuinua hali yao kiuchumi na<br />
kijamii.<br />
3. Kuwakilisha wakulima wadogo katika mashauriano na serikali juu ya masuala mbalimbali yanayohusu au yanayoathiri ufanisi na maslahi ya<br />
wakulima wadogo wa Tanzania.<br />
Maeneo makuu ya mpango mkakati<br />
1. Ushawishi na Utetezi: Kuwezesha wakulima wadogo kuwa na uwezo wa kutetea maslahi yao.<br />
2. Uwezo wa kiuchumi: kuwezesha wakulima wadogo kuwa na uwezo wa kiuchumi kupitia njia za akiba na mikopo, kuunganisha wakulima na<br />
masoko na elimu ya ujasiliamali<br />
3. Kuimarisha vikundi na mitandao ya wakulima kwa lengo la kujipanga na kujitetea.<br />
4. Masuala mtambuka: Kujenga uelewa wa wakulima juu ya <strong>Uk</strong>imwi, Jinsia, Mabadiliko ya Tabia ya nchi.<br />
5. Ujenzi wa kitaaasisi kwa lengo la kuimarisha shirika<br />
Muundo<br />
Muundo wa <strong>MVIWATA</strong> una ngazi tatu ambazo ni Ngazi ya Taifa, Ngazi ya Kati na Ngazi ya Msingi. Ngazi ya Kati inaundwa na mitandao ya<br />
kimkoa na kiwilaya wakati Ngazi ya Msingi inaundwa na mitandao ya Kata na Vijiji.<br />
Shughuli kuu<br />
1. Kujenga uwezo wa wakulima wadogo kwa kupitia mafunzo shirikishi juu ya mbinu za ushawishi na utetezi, mbinu za kuimarisha uchumi wa<br />
wakulima wadogo na uendelevu wa rasilimali kwa njia za warsha, mafunzo, mikutano na ziara za mafunzo.<br />
2.<br />
3.<br />
4.<br />
Kuhamasisha wakulima wadogo kujiunga katika vikundi vya kijamii na kiuchumi, mitandao ya msingi (kata na vijiji) na mitandao ya kati (mikoa<br />
na wilaya). Mpaka sasa <strong>MVIWATA</strong> imeanzisha mitandao ya kimkoa katika Mikoa ya Dodoma, Iringa, Kagera, Kilimanjaro, Manyara, Mbeya,<br />
Morogoro, Rukwa, Ruvuma, Shinyanga, Tabora na Tanga kwa Tanzania Bara. <strong>MVIWATA</strong> pia imeanzisha mitandao ya kiwilaya katika Wilaya<br />
za Monduli (Arusha) na Chunya (Mbeya). Tanzania Visiwani, <strong>MVIWATA</strong> Zanzibar imeanzishwa na kusajiliwa (Usajili namba 401). Mkakati<br />
unaendelea wa kuimarisha mitandao iliyopo na kuanzisha mitandao mipya.<br />
Kukusanya, kuweka katika kumbukumbu na kusambaza habari zinazohusu ujuzi na uzoefu wa wakulima, sera za kitaifa na kimataifa kwa<br />
kupitia jarida la Pambazuko Sauti ya Wakulima, vipindi vya radio, vipeperushi, vijitabu na machapisho mengine.<br />
Kuhamasisha na kuwezesha wakulima kubuni na kuendesha miradi shirikishi ya kiuchumi na uzalishaji kwa lengo la kuboresha uchumi wa<br />
wakulima wadogo kama vile vyama vya mazao, vyama vya kuweka na kukopa na masoko ya mazao.<br />
5. Kuandaa mikutano na warsha kuhusiana na mada zinazowagusa au kuathiri maslahi ya wakulima wadogo.<br />
Uanachama na jinsi ya kujiunga na shirika<br />
<strong>MVIWATA</strong> ina wanachama wa aina tatu (3).<br />
Aina ya kwanza ni Wanachama wa Kawaida ambao wamegawanyika katika makundi mawili;<br />
a) Kikundi cha wakulima wadogo au<br />
b)<br />
Mkulima mdogo binafsi aliye mwanachama katika Kikundi au Mtandao. Mkulima atakuwa mwanachama wa kawaida wa <strong>MVIWATA</strong> mara<br />
tu Kikundi au Mtandao wake utakapokubaliwa kuwa mwanachama. Atapewa kadi ya uanachama na kikundi au mtandao utapewa cheti cha<br />
utambulisho.<br />
Aina ya pili ni Vyama, Mashirika na Mitandao ya Wakulima Wadogo.<br />
Vyama, Mashirika na Mitandao ya Wakulima Wadogo vinavyojishughulisha na utetezi na ushawishi wa maslahi ya wakulima wadogo vilivyosajiliwa<br />
chini ya sheria yoyote ya Tanzania katika Ngazi za Wilaya, Mkoa au Taifa vinaweza kuomba kuwa mwanachama wa <strong>MVIWATA</strong> iwapo vinakubaliana<br />
kwa dhati na malengo na madhumuni ya Shirika.<br />
Aina ya tatu ni Wanachama Washiriki<br />
Ni mtu yeyote, taasisi au kikundi cha watu ambacho kinaunga mkono malengo na madhumuni ya Shirika. Mwanachama mshiriki anatamkwa na<br />
Mkutano Mkuu wa <strong>MVIWATA</strong>.<br />
Kila mwanachama, isipokuwa mwanachama mshiriki atalipa kiingilio na ada ya kila mwaka. Maelezo zaidi juu ya utaratibu wa kujiunga na ada<br />
yanapatikana kutoka kwa kiongozi au ofisi ya <strong>MVIWATA</strong>.<br />
Kwa mawasiliano zaidi<br />
Ofisi Kuu ya <strong>MVIWATA</strong><br />
Mkurugenzi Mtendaji<br />
<strong>MVIWATA</strong><br />
S.L.P 32<strong>20</strong> Morogoro<br />
Simu: 023 261 41 84<br />
Faksi: 023 261 41 84<br />
Barua pepe: info@mviwata.org, mviwata@morogoro.net