15.01.2013 Views

HOTUBA RC MWANZA-BMU.pdf - karibu kwenye tovuti rasmi ya ...

HOTUBA RC MWANZA-BMU.pdf - karibu kwenye tovuti rasmi ya ...

HOTUBA RC MWANZA-BMU.pdf - karibu kwenye tovuti rasmi ya ...

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

<strong>HOTUBA</strong> YA MKUU WA MKOA WA <strong>MWANZA</strong> MHESHIMIWA<br />

DR. JAMES ALEX MSEKELA (MB) KATIKA WARSHA YA VIONGOZI<br />

WA SERIKALI ZA MITAA MKOA WA <strong>MWANZA</strong> JUU YA<br />

USHIRIKISHWAJI WA JAMII KUPITIA VIKUNDI VYA ULINZI WA<br />

RASLIMALI YA UVUVI (<strong>BMU</strong>s) KATIKA UKUMBI WA BENKI KUU<br />

<strong>MWANZA</strong> TAREHE 17 MACHI 2006<br />

MHESHIMIWA MSTAHIKI MEYA WA JIJI LA<strong>MWANZA</strong><br />

WAHESHIMIWA WENYEVITI WA HALMASHAURI ZA WILAYA<br />

WAKURUGENZI WATENDAJI WA HALMASHAURI ZA WILAYA<br />

MABIBI NA MABWANA<br />

Awali <strong>ya</strong> yote ninapenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa waandaaji wa<br />

warsha hii kwa kunipa heshima <strong>ya</strong> kuwa mgeni <strong>rasmi</strong> katika ufunguzi wa<br />

warsha hii muhimu kuhusu Ushirikishwaji wa jamii katika ulinzi wa raslimali<br />

<strong>ya</strong> Uvuvi hususani katika Ziwa Victoria. Nachukua nafasi hii kuwapa pole<br />

<strong>ya</strong> safari wale wote waliotoka nje <strong>ya</strong> Jiji la Mwanza kuja kuhudhuria<br />

warsha hii.<br />

Ndugu Mwenyekiti, Nimejulishwa kuwa warsha hii imejumuisha Mstahiki<br />

Me<strong>ya</strong> wa Jiji la Mwanza, Wenyeviti wa Halmashauri za Wila<strong>ya</strong>,<br />

Waheshimiwa Madiwani wa Kata zinazopakana na Ziwa Victoria na<br />

Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Wila<strong>ya</strong>.Warsha ina lengo la<br />

kujenga uelewa wa Waheshimiwa Madiwani juu <strong>ya</strong> dhana <strong>ya</strong> ushirikishwaji<br />

wa jamii katika kupanga, kusimamia na kuendeleza raslimali <strong>ya</strong> Uvuvi<br />

pamoja na mabadiliko <strong>ya</strong> muundo na utendaji wa vikundi v<strong>ya</strong> ulinzi wa<br />

raslimali <strong>ya</strong> uvuvi (Beach Management Units). Warsha hii imekuja wakati<br />

mwafaka baada <strong>ya</strong> Halmashauri zetu katika Mkoa wa Mwanza kupata<br />

Madiwani wap<strong>ya</strong> baada <strong>ya</strong> Uchaguzi Mkuu uliofanyika Tarehe 14<br />

Desemba 2005.<br />

Ndugu Mwenyekiti, kama mnavyofahamu, mchango wa sekta <strong>ya</strong> uvuvi<br />

katika uchumi wa taifa na wananchi katika halmashauri zetu<br />

zinazozunguka Ziwa Victoria ni mkubwa sana.Ni ukweli uliowazi kwamba<br />

maendeleo <strong>ya</strong> kiuchumi na kijamii <strong>ya</strong> Wananchi katika Mkoa wa Mwanza<br />

1


<strong>ya</strong>nategemea sana shughuli za Uvuvi.Sekta <strong>ya</strong> Uvuvi inatoa ajira kwa<br />

Wananchi na hususani vijana ambao ni nguvu kazi inayopaswa kutumika<br />

ipasavyo kuleta maendeleo <strong>ya</strong> taifa kiuchumi na kijamii katika taifa letu.<br />

Takwimu zinaonyesha kuwa Sekta <strong>ya</strong> Uvuvi inatoa ajira kwa wavuvi<br />

80,053 (Frame Survey 2002). Pia sekta <strong>ya</strong> uvuvi huongeza kipato na kutoa<br />

lishe bora <strong>ya</strong> protini kwa wananchi na kuchangia pato la taifa la fedha za<br />

ndani na fedha za kigeni. Kwa mfano mwaka 2005 mauzo <strong>ya</strong> tani<br />

53392.20 za samaki nchi za nje <strong>ya</strong>lilipatia Taifa Tsh. 182 bilioni sawa na<br />

Dola za Marekani 16,561,981.46. Kupanuka kwa sekta <strong>ya</strong> uvuvi<br />

kumechochea mzunguko mkubwa wa fedha na kusababisha upanukaji wa<br />

shughuli zingine za kiuchumi na kijamii mfano upanukaji wa shughuli za<br />

viwanda, ujenzi wa mahoteli, maduka, biashara na ujenzi wa nyumba bora<br />

mijini na vijijini miongoni mwa jamii za wavuvi. Hivyo raslimali <strong>ya</strong> uvuvi <strong>ya</strong><br />

Ziwa Victoria inapaswa kulindwa,kuhifadhiwa, kuendelezwa na kuvunwa<br />

kwa busara ili iendelee kutoa mchango endelevu wa maisha <strong>ya</strong> wananchi<br />

kwa kizazi kilichopo na vizazi vijavyo.<br />

Ndugu Mwenyekiti, licha <strong>ya</strong> manufaa niliyo<strong>ya</strong>taja; raslimali <strong>ya</strong> Uvuvi<br />

katika Ziwa Victoria inakabiliwa na matatizo kadhaa: uharibifu wa<br />

mazingira unaotokana na uchafuzi wa maji taka toka viwandani na<br />

majumbani, katika sehemu za mijini, kuendelea kuwepo kwa uvuvi usio<br />

endelevu wa kutumia mbinu na zana haramu za uvuvi kama vile<br />

• Makokoro <strong>ya</strong> kuvutia nchi kavu(beach seines)<br />

• Makokoro <strong>ya</strong> dagaa chini <strong>ya</strong> milimita 10<br />

• N<strong>ya</strong>vu za makila za chini <strong>ya</strong> inchi 5. kwa samaki aina <strong>ya</strong><br />

Sato(Tilapia) na inchi 6 kwa kuvulia samaki aina <strong>ya</strong> Sangara na<br />

Katuli.<br />

• Hali duni <strong>ya</strong> usafi wa mazingira <strong>ya</strong> mialo, pia kumekuwepo na<br />

upotevu mkubwa wa samaki baada <strong>ya</strong> kuvuliwa kutokana na mbinu<br />

duni za uchakataji(processing) na uhifadhi wa samaki baada <strong>ya</strong><br />

kuvuliwa.<br />

Aidha ushirikiswaji duni wa wadau wa sekta <strong>ya</strong> Uvuvi na jamii <strong>ya</strong> wavuvi<br />

katika Ziwa Victoria umechangia kwa kiasi kikubwa kwa jamii kutowajibika<br />

2


katika kulinda raslimali <strong>ya</strong> uvuvi kutokana na jamii kufikiri kuwa raslimali <strong>ya</strong><br />

uvuvi ni mali <strong>ya</strong> Serikali na sio <strong>ya</strong>o. Kutokana na matatizo niliyo<strong>ya</strong>taja hapo<br />

juu, ni wazi kuwa hivi sasa samaki wamepungua na aina nyingi za samaki<br />

zimeelekea kutoweka katika Ziwa Victoria na kubakiwa na samaki aina<br />

tatu tu zinazovuliwa kibiashara ambazo ni Sangara, Sato, Dagaa na Furu<br />

katika baadhi <strong>ya</strong> maeneo.<br />

Wote mnafahamu kuwa uwezo wa serikali pekee kusimamia raslimali <strong>ya</strong><br />

uvuvi ni mdogo kutokana na kuwa na watumishi wachache na uwezo<br />

mdogo wa kugharamia usimamizi wa raslimali. Njia pekee <strong>ya</strong> kusimamia<br />

kikamilifu raslimali hii ni kwa kuwashirikisha wadau wote wa sekta hii<br />

hususan jamii <strong>ya</strong> wavuvi katika kupanga, kutekeleza, kusimamia na<br />

kuendeleza raslimali <strong>ya</strong> uvuvi.<br />

Ndugu Mwenyekiti, Kwa kutambua umuhimu wa jamii kushiriki katika<br />

menejimenti <strong>ya</strong> uvuvi Serikali mwaka 1997 ilitunga sera <strong>ya</strong> uvuvi ambayo<br />

inatamka ba<strong>ya</strong>na umuhimu wa ushirikishwaji wa jamii katika kuhakikisha<br />

usimamizi madhubuti wa raslimali za uvuvi katika nchi yetu.<br />

Kulingana na sera hii <strong>ya</strong> sekta <strong>ya</strong> Uvuvi vikundi v<strong>ya</strong> ulinzi wa<br />

raslimali(<strong>BMU</strong>s) vipatavyo 511 vilianzishwa katika mialo <strong>ya</strong> Ziwa<br />

Victoria.Kutokana na matatizo mbalimbali vikundi hivyo vimepungua sana.<br />

Baadhi <strong>ya</strong> matatizo ni kutokuwa na nguvu <strong>ya</strong> kisheria <strong>ya</strong> uwepo wa<br />

vikundi, kutoshirikishwa kwa makundi yote <strong>ya</strong>liyopo mialoni, kukosekana<br />

kwa wajibu uliowazi wa vikundi hivi na kukosa ushirikiano wa kutosha na<br />

msaada toka kwa viongozi katika ngazi za vijiji na wila<strong>ya</strong> katika kutekeleza<br />

majukumu <strong>ya</strong>o. Ili kutekeleza sera Serikali imetunga Sheria mp<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> Uvuvi<br />

na. 22 <strong>ya</strong> Mwaka 2003 ambayo imefuta ile iliyokuwepo awali sheria Na.6<br />

<strong>ya</strong> 1970.Hivi sasa ushirikishwaji wa jamii katika usimamizi wa raslimali <strong>ya</strong><br />

uvuvi una nguvu <strong>ya</strong> kisheria ukilinganisha na hali ilivyokuwa kabla <strong>ya</strong><br />

kutungwa kwa sheria mp<strong>ya</strong> ambayo imeanza kutumika mwezi Agosti 2005.<br />

Sheria hii pia inahalalisha uwepo wa vikundi v<strong>ya</strong> ulinzi wa rasilimali <strong>ya</strong><br />

Uvuvi katika Ziwa Victoria (<strong>BMU</strong>s).<br />

3


Ziwa Victoria linamilikiwa na nchi zote tatu za Afrika <strong>ya</strong> Mashariki, hivyo<br />

usimamaizi wake unahitaji mtazamo na mbinu za pamoja.Kwa kutambua<br />

hilo nchi hizi zimekubaliana kuwa ushirikishwaji wa jamii katika ulinzi wa<br />

raslimali <strong>ya</strong> uvuvi ni njia pekee itakayowezesha kuwa na usimamizi<br />

endelevu na mkamilifu wa sekta <strong>ya</strong> Uvuvi katika Ziwa Victoria. Nchi hizi<br />

zimekubaliana juu <strong>ya</strong> mfumo wa uanzishaji na uendeshaji wa vikundi v<strong>ya</strong><br />

Ulinzi wa raslimali(<strong>BMU</strong>s) ambao ni tofauti kidogo na mfumo tulioutumia<br />

Tanzania katika kuanzisha vikundi hivi. Kutokana na mabadiliko hayo<br />

inalazimu kufan<strong>ya</strong> mabadiliko katika mfumo wa <strong>BMU</strong> tulionao. Hivyo<br />

Tanzania imetoa muongozo wa kitaifa wa ushirikishwaji wa jamii katika<br />

Menejimenti <strong>ya</strong> Uvuvi Ziwa Victoria (National <strong>BMU</strong> Guideline) ambao<br />

umekidhi matakwa <strong>ya</strong> kikanda.<br />

Nimeelezwa baadhi <strong>ya</strong> mabadiliko ni kuwa <strong>BMU</strong> katika mfumo mp<strong>ya</strong><br />

zitajumuisha makundi yote <strong>ya</strong> wadau waliopo mwaloni, Uwakilishi<br />

unaowiana wa makundi hayo katika Kamati <strong>ya</strong> Utendaji na kuwa ili mwalo<br />

ustahili kuunda <strong>BMU</strong> unapaswa kuwa na mitumbwi kuanzia thelathini na<br />

kuendelea.<br />

Kwa kuzingatia mabadiliko hayo, nimefahamishwa kuwa katika warsha hii,<br />

jumla <strong>ya</strong> mada sita zitatolewa ambazo zinalenga kuwaelewesha<br />

Waheshimiwa madiwani kuhusu mradi wa IFMP unaofadhili utekelezaji wa<br />

Mpango wa menejimenti <strong>ya</strong> Uvuvi katika Ziwa Victoria ambao<br />

utajishughulisha na mambo <strong>ya</strong>fuatayo:<br />

• Kuimarisha usimamizi wa jamii wa raslimali;<br />

• Hali <strong>ya</strong> uwingi na aina za samaki katika Ziwa Victoria;<br />

• Sheria zinazohusu usimamizi wa raslimali <strong>ya</strong> uvuvi Tanzania<br />

hususani Ziwa Victoria;<br />

• Usimamizi wa serikali pekee na matatizo <strong>ya</strong>ke katika menejimenti <strong>ya</strong><br />

uvuvi na njia mbadala <strong>ya</strong> usimamizi shirikishi wa jamii;<br />

• Ushirikishwaji wa jamii katika Menejimenti <strong>ya</strong> Uvuvi kupitia <strong>BMU</strong>;<br />

• Mada juu <strong>ya</strong> Muundo, uanzishwaji na uendeshaji wa taasisi <strong>ya</strong> <strong>BMU</strong><br />

na<br />

4


• Mada juu <strong>ya</strong> wajibu wa serikali za mitaa katika kusimamia raslimali<br />

<strong>ya</strong> uvuvi hapa nchini.<br />

Nimefahamishwa kuwa baada <strong>ya</strong> kila mada kutolewa majadiliano <strong>ya</strong> kina<br />

<strong>ya</strong>tafanyika, mikakati <strong>ya</strong> pamoja na maazimio <strong>ya</strong>tawekwa <strong>ya</strong>nayolenga<br />

kuboresha ushiriki wa jamii katika menejimenti <strong>ya</strong> Uvuvi katika Ziwa<br />

Victoria.<br />

Napenda kusisitiza kuwa raslimali <strong>ya</strong> Ziwa Victoria ni muhimu kwa<br />

maendeleo <strong>ya</strong> kiuchumi na kijamii kwa wananchi wetu, kitaifa, kikanda na<br />

kimataifa. Tumieni vizuri muda wa warsha hii katika kujadili matatizo <strong>ya</strong><br />

uvuvi usio endelevu na kupata uelewa juu <strong>ya</strong> umuhimu wa kushirikisha<br />

jamii. Aidha kwa kuwa ninyi ni viongozi ni muhimu kupata uelewa wa kina<br />

juu muundo mp<strong>ya</strong> wajibu na utendaji wa <strong>BMU</strong>s ili muweze kutoa msukumo<br />

katika kuziunda, kuratibu na kusimamia shughuli zake, kikamilifu kwa<br />

lengo la kuwa na uvunaji endelevu wa raslimali <strong>ya</strong> samaki.<br />

Mafanikio <strong>ya</strong> ushirikiswaji wa jamii katika ulinzi wa raslimali <strong>ya</strong> Uvuvi<br />

<strong>ya</strong>nahitaji sana msaada wa viongozi katika ngazi zote toka ngazi <strong>ya</strong> kijijini,<br />

Wila<strong>ya</strong>(madiwani na uongozi wa wila<strong>ya</strong>) na Serikali kuu katika kujenga<br />

uwezo wa jamii kushiriki kikamilifu katika menejimenti <strong>ya</strong> uvuvi. Pia jamii<br />

inahitaji kujengewa uwezo katika katika uongozi, menejimenti <strong>ya</strong> uvuvi na<br />

menejimenti <strong>ya</strong> fedha n.k. Nimeelezwa kuwa Mradi wa IFMP utagharamia<br />

uundaji wa <strong>BMU</strong> katika mfumo mp<strong>ya</strong>, kujenga uwezo wa vikundi katika<br />

kusimamia raslimali kwa kutoa mafunzo kwa kamati za <strong>BMU</strong> katika n<strong>ya</strong>nja<br />

za uongozi, menejimenti <strong>ya</strong> uvuvi na menejimenti <strong>ya</strong> fedha. Pia Serikali <strong>ya</strong><br />

Tanzania imenunua injini 27 za boti ambazo zitagawiwa vikundi v<strong>ya</strong><br />

jamii(<strong>BMU</strong>) vinavyohusika na ulinzi na usimamizi wa raslimali <strong>ya</strong> uvuvi.<br />

Uendeshaji na usimamizi wa raslimali <strong>ya</strong> Uvuvi kupitia jamii(<strong>BMU</strong>) una<br />

gharama zake. Jamii kupitia vikundi v<strong>ya</strong> ulinzi wa raslimali inahitaji kuwa<br />

na v<strong>ya</strong>nzo v<strong>ya</strong> mapato endelevu kugharamia usimamizi wa raslimali katika<br />

ngazi <strong>ya</strong> jamii. Jambo muhimu na la msingi ambalo Halmashauri<br />

zinapaswa kusaidia ni kuvipa upendeleo wa pekee vikundi hivi kwa kuvipa<br />

uwakala wa kukusan<strong>ya</strong> ushuru wa mapato <strong>ya</strong> samaki na mazao <strong>ya</strong>ke ili<br />

5


mapato <strong>ya</strong> ziada baada <strong>ya</strong> kulipa kiwango kilichowekwa na halmashauri,<br />

itumike katika kugharamia shughuli za usimamizi wa raslimali unaofanywa<br />

na vikundi kwa manufaa yetu sote na pia kuwa motisha kwa ushiriki wao<br />

katika usimamizi wa raslimali.<br />

Ni mategemeo <strong>ya</strong>ngu kuwa baada <strong>ya</strong> warsha hii na mrudipo katika<br />

halmashauri zenu mtakuwa katika mstari wa mbele kutekeleza na<br />

kusimamia ushirikishwaji wa jamii kwa kuvipa vikundi v<strong>ya</strong> <strong>BMU</strong> kila<br />

msaada ili kuhakikisha jamii inatekeleza majukumu <strong>ya</strong> ulinzi wa raslimali<br />

katika mialo wanayoisimamia. Mkumbuke kuwa ilani <strong>ya</strong> Chama Cha<br />

Mapinduzi inatamka ba<strong>ya</strong>na kuhusu uvuvi endelevu hivyo hatuna budi<br />

kuitekeleza kwa vitendo.<br />

Baada <strong>ya</strong> kusema ha<strong>ya</strong>, sasa napenda kutamka kuwa warsha hii juu <strong>ya</strong><br />

ushirikishwaji wa jamii katika menejimenti <strong>ya</strong> Uvuvi katika Ziwa Victoria<br />

kupitia vikundi v<strong>ya</strong> jamii v<strong>ya</strong> ulinzi wa raslimali(<strong>BMU</strong>) imefunguliwa <strong>rasmi</strong>.<br />

AHSANTENI KWA KUNISIKILIZA<br />

6

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!