HOTUBA RC MWANZA-BMU.pdf - karibu kwenye tovuti rasmi ya ...
HOTUBA RC MWANZA-BMU.pdf - karibu kwenye tovuti rasmi ya ...
HOTUBA RC MWANZA-BMU.pdf - karibu kwenye tovuti rasmi ya ...
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
<strong>HOTUBA</strong> YA MKUU WA MKOA WA <strong>MWANZA</strong> MHESHIMIWA<br />
DR. JAMES ALEX MSEKELA (MB) KATIKA WARSHA YA VIONGOZI<br />
WA SERIKALI ZA MITAA MKOA WA <strong>MWANZA</strong> JUU YA<br />
USHIRIKISHWAJI WA JAMII KUPITIA VIKUNDI VYA ULINZI WA<br />
RASLIMALI YA UVUVI (<strong>BMU</strong>s) KATIKA UKUMBI WA BENKI KUU<br />
<strong>MWANZA</strong> TAREHE 17 MACHI 2006<br />
MHESHIMIWA MSTAHIKI MEYA WA JIJI LA<strong>MWANZA</strong><br />
WAHESHIMIWA WENYEVITI WA HALMASHAURI ZA WILAYA<br />
WAKURUGENZI WATENDAJI WA HALMASHAURI ZA WILAYA<br />
MABIBI NA MABWANA<br />
Awali <strong>ya</strong> yote ninapenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa waandaaji wa<br />
warsha hii kwa kunipa heshima <strong>ya</strong> kuwa mgeni <strong>rasmi</strong> katika ufunguzi wa<br />
warsha hii muhimu kuhusu Ushirikishwaji wa jamii katika ulinzi wa raslimali<br />
<strong>ya</strong> Uvuvi hususani katika Ziwa Victoria. Nachukua nafasi hii kuwapa pole<br />
<strong>ya</strong> safari wale wote waliotoka nje <strong>ya</strong> Jiji la Mwanza kuja kuhudhuria<br />
warsha hii.<br />
Ndugu Mwenyekiti, Nimejulishwa kuwa warsha hii imejumuisha Mstahiki<br />
Me<strong>ya</strong> wa Jiji la Mwanza, Wenyeviti wa Halmashauri za Wila<strong>ya</strong>,<br />
Waheshimiwa Madiwani wa Kata zinazopakana na Ziwa Victoria na<br />
Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Wila<strong>ya</strong>.Warsha ina lengo la<br />
kujenga uelewa wa Waheshimiwa Madiwani juu <strong>ya</strong> dhana <strong>ya</strong> ushirikishwaji<br />
wa jamii katika kupanga, kusimamia na kuendeleza raslimali <strong>ya</strong> Uvuvi<br />
pamoja na mabadiliko <strong>ya</strong> muundo na utendaji wa vikundi v<strong>ya</strong> ulinzi wa<br />
raslimali <strong>ya</strong> uvuvi (Beach Management Units). Warsha hii imekuja wakati<br />
mwafaka baada <strong>ya</strong> Halmashauri zetu katika Mkoa wa Mwanza kupata<br />
Madiwani wap<strong>ya</strong> baada <strong>ya</strong> Uchaguzi Mkuu uliofanyika Tarehe 14<br />
Desemba 2005.<br />
Ndugu Mwenyekiti, kama mnavyofahamu, mchango wa sekta <strong>ya</strong> uvuvi<br />
katika uchumi wa taifa na wananchi katika halmashauri zetu<br />
zinazozunguka Ziwa Victoria ni mkubwa sana.Ni ukweli uliowazi kwamba<br />
maendeleo <strong>ya</strong> kiuchumi na kijamii <strong>ya</strong> Wananchi katika Mkoa wa Mwanza<br />
1
<strong>ya</strong>nategemea sana shughuli za Uvuvi.Sekta <strong>ya</strong> Uvuvi inatoa ajira kwa<br />
Wananchi na hususani vijana ambao ni nguvu kazi inayopaswa kutumika<br />
ipasavyo kuleta maendeleo <strong>ya</strong> taifa kiuchumi na kijamii katika taifa letu.<br />
Takwimu zinaonyesha kuwa Sekta <strong>ya</strong> Uvuvi inatoa ajira kwa wavuvi<br />
80,053 (Frame Survey 2002). Pia sekta <strong>ya</strong> uvuvi huongeza kipato na kutoa<br />
lishe bora <strong>ya</strong> protini kwa wananchi na kuchangia pato la taifa la fedha za<br />
ndani na fedha za kigeni. Kwa mfano mwaka 2005 mauzo <strong>ya</strong> tani<br />
53392.20 za samaki nchi za nje <strong>ya</strong>lilipatia Taifa Tsh. 182 bilioni sawa na<br />
Dola za Marekani 16,561,981.46. Kupanuka kwa sekta <strong>ya</strong> uvuvi<br />
kumechochea mzunguko mkubwa wa fedha na kusababisha upanukaji wa<br />
shughuli zingine za kiuchumi na kijamii mfano upanukaji wa shughuli za<br />
viwanda, ujenzi wa mahoteli, maduka, biashara na ujenzi wa nyumba bora<br />
mijini na vijijini miongoni mwa jamii za wavuvi. Hivyo raslimali <strong>ya</strong> uvuvi <strong>ya</strong><br />
Ziwa Victoria inapaswa kulindwa,kuhifadhiwa, kuendelezwa na kuvunwa<br />
kwa busara ili iendelee kutoa mchango endelevu wa maisha <strong>ya</strong> wananchi<br />
kwa kizazi kilichopo na vizazi vijavyo.<br />
Ndugu Mwenyekiti, licha <strong>ya</strong> manufaa niliyo<strong>ya</strong>taja; raslimali <strong>ya</strong> Uvuvi<br />
katika Ziwa Victoria inakabiliwa na matatizo kadhaa: uharibifu wa<br />
mazingira unaotokana na uchafuzi wa maji taka toka viwandani na<br />
majumbani, katika sehemu za mijini, kuendelea kuwepo kwa uvuvi usio<br />
endelevu wa kutumia mbinu na zana haramu za uvuvi kama vile<br />
• Makokoro <strong>ya</strong> kuvutia nchi kavu(beach seines)<br />
• Makokoro <strong>ya</strong> dagaa chini <strong>ya</strong> milimita 10<br />
• N<strong>ya</strong>vu za makila za chini <strong>ya</strong> inchi 5. kwa samaki aina <strong>ya</strong><br />
Sato(Tilapia) na inchi 6 kwa kuvulia samaki aina <strong>ya</strong> Sangara na<br />
Katuli.<br />
• Hali duni <strong>ya</strong> usafi wa mazingira <strong>ya</strong> mialo, pia kumekuwepo na<br />
upotevu mkubwa wa samaki baada <strong>ya</strong> kuvuliwa kutokana na mbinu<br />
duni za uchakataji(processing) na uhifadhi wa samaki baada <strong>ya</strong><br />
kuvuliwa.<br />
Aidha ushirikiswaji duni wa wadau wa sekta <strong>ya</strong> Uvuvi na jamii <strong>ya</strong> wavuvi<br />
katika Ziwa Victoria umechangia kwa kiasi kikubwa kwa jamii kutowajibika<br />
2
katika kulinda raslimali <strong>ya</strong> uvuvi kutokana na jamii kufikiri kuwa raslimali <strong>ya</strong><br />
uvuvi ni mali <strong>ya</strong> Serikali na sio <strong>ya</strong>o. Kutokana na matatizo niliyo<strong>ya</strong>taja hapo<br />
juu, ni wazi kuwa hivi sasa samaki wamepungua na aina nyingi za samaki<br />
zimeelekea kutoweka katika Ziwa Victoria na kubakiwa na samaki aina<br />
tatu tu zinazovuliwa kibiashara ambazo ni Sangara, Sato, Dagaa na Furu<br />
katika baadhi <strong>ya</strong> maeneo.<br />
Wote mnafahamu kuwa uwezo wa serikali pekee kusimamia raslimali <strong>ya</strong><br />
uvuvi ni mdogo kutokana na kuwa na watumishi wachache na uwezo<br />
mdogo wa kugharamia usimamizi wa raslimali. Njia pekee <strong>ya</strong> kusimamia<br />
kikamilifu raslimali hii ni kwa kuwashirikisha wadau wote wa sekta hii<br />
hususan jamii <strong>ya</strong> wavuvi katika kupanga, kutekeleza, kusimamia na<br />
kuendeleza raslimali <strong>ya</strong> uvuvi.<br />
Ndugu Mwenyekiti, Kwa kutambua umuhimu wa jamii kushiriki katika<br />
menejimenti <strong>ya</strong> uvuvi Serikali mwaka 1997 ilitunga sera <strong>ya</strong> uvuvi ambayo<br />
inatamka ba<strong>ya</strong>na umuhimu wa ushirikishwaji wa jamii katika kuhakikisha<br />
usimamizi madhubuti wa raslimali za uvuvi katika nchi yetu.<br />
Kulingana na sera hii <strong>ya</strong> sekta <strong>ya</strong> Uvuvi vikundi v<strong>ya</strong> ulinzi wa<br />
raslimali(<strong>BMU</strong>s) vipatavyo 511 vilianzishwa katika mialo <strong>ya</strong> Ziwa<br />
Victoria.Kutokana na matatizo mbalimbali vikundi hivyo vimepungua sana.<br />
Baadhi <strong>ya</strong> matatizo ni kutokuwa na nguvu <strong>ya</strong> kisheria <strong>ya</strong> uwepo wa<br />
vikundi, kutoshirikishwa kwa makundi yote <strong>ya</strong>liyopo mialoni, kukosekana<br />
kwa wajibu uliowazi wa vikundi hivi na kukosa ushirikiano wa kutosha na<br />
msaada toka kwa viongozi katika ngazi za vijiji na wila<strong>ya</strong> katika kutekeleza<br />
majukumu <strong>ya</strong>o. Ili kutekeleza sera Serikali imetunga Sheria mp<strong>ya</strong> <strong>ya</strong> Uvuvi<br />
na. 22 <strong>ya</strong> Mwaka 2003 ambayo imefuta ile iliyokuwepo awali sheria Na.6<br />
<strong>ya</strong> 1970.Hivi sasa ushirikishwaji wa jamii katika usimamizi wa raslimali <strong>ya</strong><br />
uvuvi una nguvu <strong>ya</strong> kisheria ukilinganisha na hali ilivyokuwa kabla <strong>ya</strong><br />
kutungwa kwa sheria mp<strong>ya</strong> ambayo imeanza kutumika mwezi Agosti 2005.<br />
Sheria hii pia inahalalisha uwepo wa vikundi v<strong>ya</strong> ulinzi wa rasilimali <strong>ya</strong><br />
Uvuvi katika Ziwa Victoria (<strong>BMU</strong>s).<br />
3
Ziwa Victoria linamilikiwa na nchi zote tatu za Afrika <strong>ya</strong> Mashariki, hivyo<br />
usimamaizi wake unahitaji mtazamo na mbinu za pamoja.Kwa kutambua<br />
hilo nchi hizi zimekubaliana kuwa ushirikishwaji wa jamii katika ulinzi wa<br />
raslimali <strong>ya</strong> uvuvi ni njia pekee itakayowezesha kuwa na usimamizi<br />
endelevu na mkamilifu wa sekta <strong>ya</strong> Uvuvi katika Ziwa Victoria. Nchi hizi<br />
zimekubaliana juu <strong>ya</strong> mfumo wa uanzishaji na uendeshaji wa vikundi v<strong>ya</strong><br />
Ulinzi wa raslimali(<strong>BMU</strong>s) ambao ni tofauti kidogo na mfumo tulioutumia<br />
Tanzania katika kuanzisha vikundi hivi. Kutokana na mabadiliko hayo<br />
inalazimu kufan<strong>ya</strong> mabadiliko katika mfumo wa <strong>BMU</strong> tulionao. Hivyo<br />
Tanzania imetoa muongozo wa kitaifa wa ushirikishwaji wa jamii katika<br />
Menejimenti <strong>ya</strong> Uvuvi Ziwa Victoria (National <strong>BMU</strong> Guideline) ambao<br />
umekidhi matakwa <strong>ya</strong> kikanda.<br />
Nimeelezwa baadhi <strong>ya</strong> mabadiliko ni kuwa <strong>BMU</strong> katika mfumo mp<strong>ya</strong><br />
zitajumuisha makundi yote <strong>ya</strong> wadau waliopo mwaloni, Uwakilishi<br />
unaowiana wa makundi hayo katika Kamati <strong>ya</strong> Utendaji na kuwa ili mwalo<br />
ustahili kuunda <strong>BMU</strong> unapaswa kuwa na mitumbwi kuanzia thelathini na<br />
kuendelea.<br />
Kwa kuzingatia mabadiliko hayo, nimefahamishwa kuwa katika warsha hii,<br />
jumla <strong>ya</strong> mada sita zitatolewa ambazo zinalenga kuwaelewesha<br />
Waheshimiwa madiwani kuhusu mradi wa IFMP unaofadhili utekelezaji wa<br />
Mpango wa menejimenti <strong>ya</strong> Uvuvi katika Ziwa Victoria ambao<br />
utajishughulisha na mambo <strong>ya</strong>fuatayo:<br />
• Kuimarisha usimamizi wa jamii wa raslimali;<br />
• Hali <strong>ya</strong> uwingi na aina za samaki katika Ziwa Victoria;<br />
• Sheria zinazohusu usimamizi wa raslimali <strong>ya</strong> uvuvi Tanzania<br />
hususani Ziwa Victoria;<br />
• Usimamizi wa serikali pekee na matatizo <strong>ya</strong>ke katika menejimenti <strong>ya</strong><br />
uvuvi na njia mbadala <strong>ya</strong> usimamizi shirikishi wa jamii;<br />
• Ushirikishwaji wa jamii katika Menejimenti <strong>ya</strong> Uvuvi kupitia <strong>BMU</strong>;<br />
• Mada juu <strong>ya</strong> Muundo, uanzishwaji na uendeshaji wa taasisi <strong>ya</strong> <strong>BMU</strong><br />
na<br />
4
• Mada juu <strong>ya</strong> wajibu wa serikali za mitaa katika kusimamia raslimali<br />
<strong>ya</strong> uvuvi hapa nchini.<br />
Nimefahamishwa kuwa baada <strong>ya</strong> kila mada kutolewa majadiliano <strong>ya</strong> kina<br />
<strong>ya</strong>tafanyika, mikakati <strong>ya</strong> pamoja na maazimio <strong>ya</strong>tawekwa <strong>ya</strong>nayolenga<br />
kuboresha ushiriki wa jamii katika menejimenti <strong>ya</strong> Uvuvi katika Ziwa<br />
Victoria.<br />
Napenda kusisitiza kuwa raslimali <strong>ya</strong> Ziwa Victoria ni muhimu kwa<br />
maendeleo <strong>ya</strong> kiuchumi na kijamii kwa wananchi wetu, kitaifa, kikanda na<br />
kimataifa. Tumieni vizuri muda wa warsha hii katika kujadili matatizo <strong>ya</strong><br />
uvuvi usio endelevu na kupata uelewa juu <strong>ya</strong> umuhimu wa kushirikisha<br />
jamii. Aidha kwa kuwa ninyi ni viongozi ni muhimu kupata uelewa wa kina<br />
juu muundo mp<strong>ya</strong> wajibu na utendaji wa <strong>BMU</strong>s ili muweze kutoa msukumo<br />
katika kuziunda, kuratibu na kusimamia shughuli zake, kikamilifu kwa<br />
lengo la kuwa na uvunaji endelevu wa raslimali <strong>ya</strong> samaki.<br />
Mafanikio <strong>ya</strong> ushirikiswaji wa jamii katika ulinzi wa raslimali <strong>ya</strong> Uvuvi<br />
<strong>ya</strong>nahitaji sana msaada wa viongozi katika ngazi zote toka ngazi <strong>ya</strong> kijijini,<br />
Wila<strong>ya</strong>(madiwani na uongozi wa wila<strong>ya</strong>) na Serikali kuu katika kujenga<br />
uwezo wa jamii kushiriki kikamilifu katika menejimenti <strong>ya</strong> uvuvi. Pia jamii<br />
inahitaji kujengewa uwezo katika katika uongozi, menejimenti <strong>ya</strong> uvuvi na<br />
menejimenti <strong>ya</strong> fedha n.k. Nimeelezwa kuwa Mradi wa IFMP utagharamia<br />
uundaji wa <strong>BMU</strong> katika mfumo mp<strong>ya</strong>, kujenga uwezo wa vikundi katika<br />
kusimamia raslimali kwa kutoa mafunzo kwa kamati za <strong>BMU</strong> katika n<strong>ya</strong>nja<br />
za uongozi, menejimenti <strong>ya</strong> uvuvi na menejimenti <strong>ya</strong> fedha. Pia Serikali <strong>ya</strong><br />
Tanzania imenunua injini 27 za boti ambazo zitagawiwa vikundi v<strong>ya</strong><br />
jamii(<strong>BMU</strong>) vinavyohusika na ulinzi na usimamizi wa raslimali <strong>ya</strong> uvuvi.<br />
Uendeshaji na usimamizi wa raslimali <strong>ya</strong> Uvuvi kupitia jamii(<strong>BMU</strong>) una<br />
gharama zake. Jamii kupitia vikundi v<strong>ya</strong> ulinzi wa raslimali inahitaji kuwa<br />
na v<strong>ya</strong>nzo v<strong>ya</strong> mapato endelevu kugharamia usimamizi wa raslimali katika<br />
ngazi <strong>ya</strong> jamii. Jambo muhimu na la msingi ambalo Halmashauri<br />
zinapaswa kusaidia ni kuvipa upendeleo wa pekee vikundi hivi kwa kuvipa<br />
uwakala wa kukusan<strong>ya</strong> ushuru wa mapato <strong>ya</strong> samaki na mazao <strong>ya</strong>ke ili<br />
5
mapato <strong>ya</strong> ziada baada <strong>ya</strong> kulipa kiwango kilichowekwa na halmashauri,<br />
itumike katika kugharamia shughuli za usimamizi wa raslimali unaofanywa<br />
na vikundi kwa manufaa yetu sote na pia kuwa motisha kwa ushiriki wao<br />
katika usimamizi wa raslimali.<br />
Ni mategemeo <strong>ya</strong>ngu kuwa baada <strong>ya</strong> warsha hii na mrudipo katika<br />
halmashauri zenu mtakuwa katika mstari wa mbele kutekeleza na<br />
kusimamia ushirikishwaji wa jamii kwa kuvipa vikundi v<strong>ya</strong> <strong>BMU</strong> kila<br />
msaada ili kuhakikisha jamii inatekeleza majukumu <strong>ya</strong> ulinzi wa raslimali<br />
katika mialo wanayoisimamia. Mkumbuke kuwa ilani <strong>ya</strong> Chama Cha<br />
Mapinduzi inatamka ba<strong>ya</strong>na kuhusu uvuvi endelevu hivyo hatuna budi<br />
kuitekeleza kwa vitendo.<br />
Baada <strong>ya</strong> kusema ha<strong>ya</strong>, sasa napenda kutamka kuwa warsha hii juu <strong>ya</strong><br />
ushirikishwaji wa jamii katika menejimenti <strong>ya</strong> Uvuvi katika Ziwa Victoria<br />
kupitia vikundi v<strong>ya</strong> jamii v<strong>ya</strong> ulinzi wa raslimali(<strong>BMU</strong>) imefunguliwa <strong>rasmi</strong>.<br />
AHSANTENI KWA KUNISIKILIZA<br />
6