kulea vifaranga ulishaji vifaranga/chanjo/dawa
Ufugaji wa kuku wa Asili3.0 Shughuli za vikundi3.1. Kikundi cha watotoleshaji vifarangaHiki kitakuwa na jukumu la kulea kuku wazazi wenye sifa inayopendwana kikundi na wanaweza kuchanganya mbegu ili kupata kuku bora. Kwakuanzia, kikundi kitatumia njia za asili za kutotolesha na baadaye kulinganana uhitaji kuongezeka waweza kuamua kutumia viatamizi. RLDC kupitiawatendaji wake vijijini itakusanya habari muhimu kuhusu viatamizi nakuhakikisha habari hizi zinawafikia wahusika wa kikundi.3.2 . Kikundi cha Walezi wa vifarangaHiki kinahusisha vifaranga wa siku moja hadi wiki tano. Wanakikundiwatawajibika kuchukua vifaranga toka kwa watotoleshaji na kuvilea hadikufikia umri tajwa. Wanakikundi watawajibika kuwapa chanjo na madawamuhimu kulingana na magonjwa yanayojulikana katika eneo husika.Wanachama wa kikundi hiki watahitajika kuwekeza katika chanjo namahitaji mengine mengi yatakayohitajika kwa ajili ya afya bora ya kuku.Pia watahitajika kuwekeza katika mabanda mazuri yenye kutunza vifarangambali na maadui mbalimbali na uambukizo wa magonjwa. Baada ya wikitano, vifaranga watauzwa kwa wanavikundi wengine watakaowatunza hadiumri wa kuuzwa au kutunzwa kama kuku wa mbegu. Hata hivyo, wakati wotewa utunzaji, wanachama watahitaji huduma toka kwa kundi linaloshughulikana afya ya kuku pamoja na watengenzaji wa chakula.3.3. Kikundi kinachohusika na afya ya kuku.Wanachama wa kikundi hiki watafundishwa namna bora ya kutambuamagonjwa, kuchanja kuku na kutibu magonjwa mbalimbali ya kuku.Wanachama wa kundi hili watafanya kazi kwa karibu na wataalamu waserikali waliopo katika eneo lao ili kuboresha huduma yao pale wanapoonawanahitaji utaalamu zaidi. Wanachama wa kikundi hiki watalazimikakuwekeza katika kununua madawa, chanjo na vifaa vya kutunza baridi.4
Ufugaji wa kuku wa AsiliChombo cha asili cha kutunza joto – vifaranga3.4. Kikundi cha watengenezaji chakulaHiki kitahusika na kuchanganya chakula na kusaga kulingana na mahitajiyaliyopo. Kikundi kitazingatia aina ya vyanzo vya vyakula vinavyopatikanakatika maeneo yao. Chakula kinachochanganywa kitaalamu husaidiakupunguza muda wa kuku kufikia muda wa kuchinjwa. Wanachama wakikundi hiki watahitajika kuwekeza katika kununua vifaa vya kusagia nakuchanganya chakula.3.5. Kikundi cha masokoKikundi kitahusika na kutafuta habari za masoko ndani na nje ya kikundi nakuwaunganisha wafugaji na wanunuzi mbali mbali toka masoko menginekwa bei nzuri. Wanachama wa kikundi hiki watahitajika kuwekeza katikagharama za usafiri kwa ajili ya kutafuta masoko.5
- Page 1 and 2: Ufugaji Mwongozo wa kuku kwa wa mfu
- Page 3 and 4: Ufugaji wa kuku wa AsiliSehemu ya K
- Page 5: Ufugaji wa kuku wa AsiliKutokana na
- Page 9 and 10: Ufugaji wa kuku wa Asili4.0 Uongozi
- Page 11 and 12: 9Ufugaji wa kuku wa Asili
Ufugaji wa kuku wa Asili
Chombo cha asili cha kutunza joto – vifaranga
3.4. Kikundi cha watengenezaji chakula
Hiki kitahusika na kuchanganya chakula na kusaga kulingana na mahitaji
yaliyopo. Kikundi kitazingatia aina ya vyanzo vya vyakula vinavyopatikana
katika maeneo yao. Chakula kinachochanganywa kitaalamu husaidia
kupunguza muda wa kuku kufikia muda wa kuchinjwa. Wanachama wa
kikundi hiki watahitajika kuwekeza katika kununua vifaa vya kusagia na
kuchanganya chakula.
3.5. Kikundi cha masoko
Kikundi kitahusika na kutafuta habari za masoko ndani na nje ya kikundi na
kuwaunganisha wafugaji na wanunuzi mbali mbali toka masoko mengine
kwa bei nzuri. Wanachama wa kikundi hiki watahitajika kuwekeza katika
gharama za usafiri kwa ajili ya kutafuta masoko.
5