KILIMO CHA VITUNGUU MAJI - The 4-H Global Knowledge Center
KILIMO CHA VITUNGUU MAJI - The 4-H Global Knowledge Center
KILIMO CHA VITUNGUU MAJI - The 4-H Global Knowledge Center
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Mbinu za kudhibiti ugonjwa huu ni kuendesha mzunguko (crop<br />
rotation) wa muda mrefu wa mazao pamoja na kuzuia kutuama kwa<br />
maji shambani. Kupunguza msongamano wa mazao shambani na<br />
matumizi ya mbolea zenye calcium, phosphate and potassium<br />
hupunguza kuenea kwa ugonjwa huu. Kwa upande mwingine,<br />
matumizi ya mbolea ya nitrojeni kwa wingi au kwa kiasi pungufu<br />
uongeza mlipuko wa magonjwa. Viatilifu kama vile Mancozeb<br />
hutumika kuzuia mashmbulizi ya ugonjwa huu.<br />
2. Ukungu wa unga (powdery mildew) na wa chini (Downy<br />
mildew)<br />
Magonjwa haya hushambulia majani ya mimea shamabani na hata<br />
miche michanga. Kwenye majani kunaonekana vidoa vyeupe hasa<br />
kwenye majani makuu ya mimea michanga. Ukungu mweupe<br />
unatokea na kuongezeka kwa haraka kwenye sehemu au nyakati za<br />
baridi. Viini huishi kwenye mabaki ya mimea ya vitunguu na huweza<br />
kupeperushwa mbali na upepo. Kwenye mimea michanga ugonjwa<br />
unaweza kudhibitiwa na madawa kama mancozeb.<br />
3. Kuoza kwa vitunguu (bulb rots)<br />
Hali hii inaweza kutokea shambani au wakati wa hifadhi ghalani.<br />
Ugonjwa huu ni hatari zaidi kwenye sehemu za joto na zenye<br />
kutuamisha maji. Ni vyema kuhakikisha kwamba shambani hakuna<br />
hali ya kutuamisha maji na pia kwenye ghala kunakuwa na hali nzuri<br />
ya mzuunguko wa hewa.<br />
Udhibiti wa wadudu<br />
Utitiri wa vitunguu (Onion thrips), Funza wa vitunguu (Onion<br />
maggots) na Minyoo wa vitunguu (Onion wireworms) ni miongoni<br />
mwa wadudu wasumbufu kwenye zao la kitunguu.<br />
1. Utitiri wa vitunguu (Onion thrips)<br />
Hawa ni wadudu wadogodogo sana ambao hula kwa kukwaruza juu<br />
ya jani na kunyonya majimaji ya kwenye mmea. Hali husababisha<br />
kutoka kwa mikwaruzo meupe kwenye majani ya vitunguu.<br />
Mashambulizi yakizidi majani huanguka na kunyauka. Ukubwa wa<br />
vitunguu hupungua. Hili ni tatizo kubwa zaidi hasa wakati wa ukame<br />
kuliko wakati wa unyevu.<br />
Utitiri wa vitunguu Madhara ya utitiri<br />
2. Bungua weupe (White grub)<br />
Huyu ni aina ya funza mkubwa. Hutaga mayai yake kwenye uozo wa<br />
majani na samadi na hivyo mashamba ya vitunguu yaliyoko karibu<br />
au kwenye maeneo ya jinsi hiyo huwa kwenye hatari zaidi.<br />
Hushambulia mizizi na kusababisha kukauka kwa mimea. Kutifulia<br />
shamba na kuwaweka wazi wadudu hawa kunapunguza idadi yao.