17.12.2012 Views

KILIMO CHA VITUNGUU MAJI - The 4-H Global Knowledge Center

KILIMO CHA VITUNGUU MAJI - The 4-H Global Knowledge Center

KILIMO CHA VITUNGUU MAJI - The 4-H Global Knowledge Center

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Mbinu za kudhibiti ugonjwa huu ni kuendesha mzunguko (crop<br />

rotation) wa muda mrefu wa mazao pamoja na kuzuia kutuama kwa<br />

maji shambani. Kupunguza msongamano wa mazao shambani na<br />

matumizi ya mbolea zenye calcium, phosphate and potassium<br />

hupunguza kuenea kwa ugonjwa huu. Kwa upande mwingine,<br />

matumizi ya mbolea ya nitrojeni kwa wingi au kwa kiasi pungufu<br />

uongeza mlipuko wa magonjwa. Viatilifu kama vile Mancozeb<br />

hutumika kuzuia mashmbulizi ya ugonjwa huu.<br />

2. Ukungu wa unga (powdery mildew) na wa chini (Downy<br />

mildew)<br />

Magonjwa haya hushambulia majani ya mimea shamabani na hata<br />

miche michanga. Kwenye majani kunaonekana vidoa vyeupe hasa<br />

kwenye majani makuu ya mimea michanga. Ukungu mweupe<br />

unatokea na kuongezeka kwa haraka kwenye sehemu au nyakati za<br />

baridi. Viini huishi kwenye mabaki ya mimea ya vitunguu na huweza<br />

kupeperushwa mbali na upepo. Kwenye mimea michanga ugonjwa<br />

unaweza kudhibitiwa na madawa kama mancozeb.<br />

3. Kuoza kwa vitunguu (bulb rots)<br />

Hali hii inaweza kutokea shambani au wakati wa hifadhi ghalani.<br />

Ugonjwa huu ni hatari zaidi kwenye sehemu za joto na zenye<br />

kutuamisha maji. Ni vyema kuhakikisha kwamba shambani hakuna<br />

hali ya kutuamisha maji na pia kwenye ghala kunakuwa na hali nzuri<br />

ya mzuunguko wa hewa.<br />

Udhibiti wa wadudu<br />

Utitiri wa vitunguu (Onion thrips), Funza wa vitunguu (Onion<br />

maggots) na Minyoo wa vitunguu (Onion wireworms) ni miongoni<br />

mwa wadudu wasumbufu kwenye zao la kitunguu.<br />

1. Utitiri wa vitunguu (Onion thrips)<br />

Hawa ni wadudu wadogodogo sana ambao hula kwa kukwaruza juu<br />

ya jani na kunyonya majimaji ya kwenye mmea. Hali husababisha<br />

kutoka kwa mikwaruzo meupe kwenye majani ya vitunguu.<br />

Mashambulizi yakizidi majani huanguka na kunyauka. Ukubwa wa<br />

vitunguu hupungua. Hili ni tatizo kubwa zaidi hasa wakati wa ukame<br />

kuliko wakati wa unyevu.<br />

Utitiri wa vitunguu Madhara ya utitiri<br />

2. Bungua weupe (White grub)<br />

Huyu ni aina ya funza mkubwa. Hutaga mayai yake kwenye uozo wa<br />

majani na samadi na hivyo mashamba ya vitunguu yaliyoko karibu<br />

au kwenye maeneo ya jinsi hiyo huwa kwenye hatari zaidi.<br />

Hushambulia mizizi na kusababisha kukauka kwa mimea. Kutifulia<br />

shamba na kuwaweka wazi wadudu hawa kunapunguza idadi yao.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!