You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
MBINU BORA ZA UZALISHAJI MPUNGA<br />
WA KUTEGEMEA MVUA<br />
Utangulizi:<br />
<strong>Mpunga</strong> ni zao maarufu sana duniani na hapa<br />
Zanzibar. Ni la tatu kulimwa likitanguliwa na<br />
muhogo na ndizi. Hata hivyo ni la kwanza<br />
kupendwa kuliwa na wananchi wote wa hapa<br />
Unguja na Pemba.<br />
Wakulima wa visiwani hulima mpunga wa aina<br />
mbili, wakutegemea mvua ambao hulimwa katika<br />
msimu wa mwaka na wa umwagiliaji maji ambao<br />
unalimwa mara mbili kutegemea na uwezo<br />
pamoja na mbegu zinazotumika.<br />
Katika <strong>Kilimo</strong> cha aina zote mbili hutumia mbegu<br />
kubwa za miezi sita au mbegu ndogo za miezi<br />
mitatu. Hata hivyo mpunga wakutegea mvua<br />
hupitia katika hatua saba muhimu nazo ni:<br />
1. Utayarishaji wa ardhi.<br />
2. Uchaguzi wa mbegu, usiaji na utiaji wa mbolea<br />
za kupandia.<br />
3. Palizi kwa jembe, mkono au kwa dawa.<br />
4. Udhibiti wa wadudu<br />
5. Ukaguzi wa shamba<br />
6. Upatikanaji wa wataalam.<br />
7. Mavuno<br />
Utayarishaji wa ardhi:<br />
Matayarisho ya ardhi kwa ajili ya kilimo cha<br />
mpunga huanza kwa kufyekwa majani, na<br />
kuwekwa pembeni kama mipaka katika shamba<br />
kwani yanapooza hutoa mbolea nzuri kutokana<br />
na kupelekwa na maji ya mvua shambani.<br />
Kwa wakulima waliowengi huchoma moto majani,<br />
mbinu hii kitaalam haikubaliki kwani ni chanzo<br />
kikuu cha uharibifu wa mazingira kutokana na<br />
moto kuua viumbe hai wa udongo.<br />
Kabla ya kupanda ni vyema kuweka mbolea za<br />
awali kama Samadi au TSP ili kupata mimea bora<br />
na yenye afya inayokua vizuri. Hata hivyo mbolea<br />
za asili zinapendekezwa zaidi kwani hizi ni nzuri<br />
kwa kuhifadhi mazingira na kupunguza gharama<br />
za ununuzi<br />
Uchaguzi wa mbegu:<br />
Mkulima inampasa kuwa makini katika kutafuta<br />
mbegu zenye sifa nzuri ili ataposia ziweze kuota<br />
na kukua vizuri. Mbegu hizo ziwe na uwezo wa<br />
kustahamili wadudu, magonjwa, maradhi na<br />
upepo, sambamba na mbegu bora, kusia kwa<br />
wakati pamoja na kutumia mbolea za kupandia<br />
ni jambo la msingi ili mpunga uchipue na ukue<br />
vizuri.<br />
Aina nne ya mbegu za mpunga<br />
Palizi kwa kutumia mkono, jembe au dawa:<br />
Wakati wa palizi utakapofika mkulima anatakiwa<br />
asichelewe kuifanya kazi hiyo,<br />
Kwa sababu magugu yaliyoota na mpunga mara<br />
nyingi huhitaji virutubisho vingi zaidi ili kukua<br />
vizuri na kuuacha mpunga kukosa virutubisho vya<br />
kutosha kutokana na magugu ardhini. Hali hiyo<br />
ikitokea mpunga hautakuwa vizuri.<br />
<strong>Mpunga</strong> ukipaliliwa unakuwa vizuri<br />
Baada ya palizi majani laini yote yanayoweza<br />
kuoza kwa haraka yawachwe huko shambani na<br />
yale magugu yawekwe kwenye mipaka kwani<br />
nayo baada ya muda itakuwa mbolea ambayo<br />
itasambazwa na maji ya mvua.<br />
Baada ya palizi ya kwanza unatakiwa kuweka<br />
mbolea ya pili ya kukuzia na mbolea ya tatu<br />
huwekwa baada ya palizi ya pili au mpunga ukiwa<br />
na mimba.<br />
Udhibiti wa wadudu:<br />
<strong>Mpunga</strong> huwa unashambuliwa sana na wadudu<br />
mbalimbali ukiwa katika hatua tofauti za ukuaji,
lakini mashambulizi makubwa yanatokea mpunga<br />
ukiwa mchanga. Wadudu wanaoshambulia sana<br />
mpunga ni pamoja na kunguni mgunda na funza<br />
wa kigogo. Ili kudhibiti uharibifu hou hapana budi<br />
kutayarisha shamba<br />
vizuri na kwa wakati<br />
pamoja na ukaguzi<br />
wa shamba mara<br />
kwa mara, ni mbinu<br />
bora ya kupunguza<br />
maradhi na wadudu<br />
kwa kiasi kikubwa<br />
sambamba na<br />
utumiaji wa dawa za<br />
viwandani kama vile<br />
Dawa ya unga aina<br />
ya Marshal ambayo huchanganywa na mbegu<br />
kabla ya kupandwa, Dawa za mafuta za Rogo,<br />
Attakan, C344SE, na nyenginezo. Dawa hizi<br />
hutumika zaidi mara tu mashambulizi yanapoanza<br />
baada ya mpunga kuota/kuchipua.<br />
Ukaguzi wa shamba:<br />
Kwa kipindi chote hicho inashauriwa kukagua<br />
shamba lako mara kwa mara ili kuweza kugundua<br />
tatizo lolote mapema na kulichukulia hatua<br />
inayofaa kwa haraka.<br />
Upatikanaji wa Wataalam:<br />
Wakulima ili wafanikiwe wanahitaji kupata ushauri<br />
wa kitaalam na miongozo mbalimbali ili uzalishaji<br />
uweze kukuwa. Ni vizuri kwa wakulima kuwa<br />
karibu na mabwana shamba wa maeneo yao, ili<br />
kubadilishana uzoefu na kupata taaluma zaidi.<br />
Mavuno:<br />
Uvunaji hufanyika mapema mpunga unapokauka<br />
na kugeuka rangi ya kahawia kabla majani<br />
hayajakauka kabisa. Unapochelewa kuvunwa<br />
mpunga hukauka shambani na hupukutika na<br />
kupungua uzito.<br />
Baada ya kuvunwa mpunga husafishwa kwa<br />
kupeta na huhifadhiwa kwenye mapolo na<br />
magunia kwa matumizi ya baadae.<br />
Kimetayarishwa na<br />
Kamisheni ya <strong>Kilimo</strong>, Utafiti na Elimu kwaWakulima<br />
(Kitengo cha habari na Vielelezo)<br />
Wizara ya <strong>Kilimo</strong>, Mifugo na Mazingira<br />
S. L. P 159, ZANZIBAR<br />
Juni, 2008<br />
WIZARA YA KILIMO, MIFUGO NA<br />
MAZINGIRA - ZANZIBZAR<br />
MBINU MBINU BORA BORA ZA<br />
ZA<br />
UZALISHAJI<br />
UZALISHAJI<br />
MPUNGA MPUNGA WA<br />
KUTEGEMEA KUTEGEMEA MVU MVUA MVU