12.12.2012 Views

Leaflet Mpunga.p65 - Kilimo

Leaflet Mpunga.p65 - Kilimo

Leaflet Mpunga.p65 - Kilimo

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

MBINU BORA ZA UZALISHAJI MPUNGA<br />

WA KUTEGEMEA MVUA<br />

Utangulizi:<br />

<strong>Mpunga</strong> ni zao maarufu sana duniani na hapa<br />

Zanzibar. Ni la tatu kulimwa likitanguliwa na<br />

muhogo na ndizi. Hata hivyo ni la kwanza<br />

kupendwa kuliwa na wananchi wote wa hapa<br />

Unguja na Pemba.<br />

Wakulima wa visiwani hulima mpunga wa aina<br />

mbili, wakutegemea mvua ambao hulimwa katika<br />

msimu wa mwaka na wa umwagiliaji maji ambao<br />

unalimwa mara mbili kutegemea na uwezo<br />

pamoja na mbegu zinazotumika.<br />

Katika <strong>Kilimo</strong> cha aina zote mbili hutumia mbegu<br />

kubwa za miezi sita au mbegu ndogo za miezi<br />

mitatu. Hata hivyo mpunga wakutegea mvua<br />

hupitia katika hatua saba muhimu nazo ni:<br />

1. Utayarishaji wa ardhi.<br />

2. Uchaguzi wa mbegu, usiaji na utiaji wa mbolea<br />

za kupandia.<br />

3. Palizi kwa jembe, mkono au kwa dawa.<br />

4. Udhibiti wa wadudu<br />

5. Ukaguzi wa shamba<br />

6. Upatikanaji wa wataalam.<br />

7. Mavuno<br />

Utayarishaji wa ardhi:<br />

Matayarisho ya ardhi kwa ajili ya kilimo cha<br />

mpunga huanza kwa kufyekwa majani, na<br />

kuwekwa pembeni kama mipaka katika shamba<br />

kwani yanapooza hutoa mbolea nzuri kutokana<br />

na kupelekwa na maji ya mvua shambani.<br />

Kwa wakulima waliowengi huchoma moto majani,<br />

mbinu hii kitaalam haikubaliki kwani ni chanzo<br />

kikuu cha uharibifu wa mazingira kutokana na<br />

moto kuua viumbe hai wa udongo.<br />

Kabla ya kupanda ni vyema kuweka mbolea za<br />

awali kama Samadi au TSP ili kupata mimea bora<br />

na yenye afya inayokua vizuri. Hata hivyo mbolea<br />

za asili zinapendekezwa zaidi kwani hizi ni nzuri<br />

kwa kuhifadhi mazingira na kupunguza gharama<br />

za ununuzi<br />

Uchaguzi wa mbegu:<br />

Mkulima inampasa kuwa makini katika kutafuta<br />

mbegu zenye sifa nzuri ili ataposia ziweze kuota<br />

na kukua vizuri. Mbegu hizo ziwe na uwezo wa<br />

kustahamili wadudu, magonjwa, maradhi na<br />

upepo, sambamba na mbegu bora, kusia kwa<br />

wakati pamoja na kutumia mbolea za kupandia<br />

ni jambo la msingi ili mpunga uchipue na ukue<br />

vizuri.<br />

Aina nne ya mbegu za mpunga<br />

Palizi kwa kutumia mkono, jembe au dawa:<br />

Wakati wa palizi utakapofika mkulima anatakiwa<br />

asichelewe kuifanya kazi hiyo,<br />

Kwa sababu magugu yaliyoota na mpunga mara<br />

nyingi huhitaji virutubisho vingi zaidi ili kukua<br />

vizuri na kuuacha mpunga kukosa virutubisho vya<br />

kutosha kutokana na magugu ardhini. Hali hiyo<br />

ikitokea mpunga hautakuwa vizuri.<br />

<strong>Mpunga</strong> ukipaliliwa unakuwa vizuri<br />

Baada ya palizi majani laini yote yanayoweza<br />

kuoza kwa haraka yawachwe huko shambani na<br />

yale magugu yawekwe kwenye mipaka kwani<br />

nayo baada ya muda itakuwa mbolea ambayo<br />

itasambazwa na maji ya mvua.<br />

Baada ya palizi ya kwanza unatakiwa kuweka<br />

mbolea ya pili ya kukuzia na mbolea ya tatu<br />

huwekwa baada ya palizi ya pili au mpunga ukiwa<br />

na mimba.<br />

Udhibiti wa wadudu:<br />

<strong>Mpunga</strong> huwa unashambuliwa sana na wadudu<br />

mbalimbali ukiwa katika hatua tofauti za ukuaji,


lakini mashambulizi makubwa yanatokea mpunga<br />

ukiwa mchanga. Wadudu wanaoshambulia sana<br />

mpunga ni pamoja na kunguni mgunda na funza<br />

wa kigogo. Ili kudhibiti uharibifu hou hapana budi<br />

kutayarisha shamba<br />

vizuri na kwa wakati<br />

pamoja na ukaguzi<br />

wa shamba mara<br />

kwa mara, ni mbinu<br />

bora ya kupunguza<br />

maradhi na wadudu<br />

kwa kiasi kikubwa<br />

sambamba na<br />

utumiaji wa dawa za<br />

viwandani kama vile<br />

Dawa ya unga aina<br />

ya Marshal ambayo huchanganywa na mbegu<br />

kabla ya kupandwa, Dawa za mafuta za Rogo,<br />

Attakan, C344SE, na nyenginezo. Dawa hizi<br />

hutumika zaidi mara tu mashambulizi yanapoanza<br />

baada ya mpunga kuota/kuchipua.<br />

Ukaguzi wa shamba:<br />

Kwa kipindi chote hicho inashauriwa kukagua<br />

shamba lako mara kwa mara ili kuweza kugundua<br />

tatizo lolote mapema na kulichukulia hatua<br />

inayofaa kwa haraka.<br />

Upatikanaji wa Wataalam:<br />

Wakulima ili wafanikiwe wanahitaji kupata ushauri<br />

wa kitaalam na miongozo mbalimbali ili uzalishaji<br />

uweze kukuwa. Ni vizuri kwa wakulima kuwa<br />

karibu na mabwana shamba wa maeneo yao, ili<br />

kubadilishana uzoefu na kupata taaluma zaidi.<br />

Mavuno:<br />

Uvunaji hufanyika mapema mpunga unapokauka<br />

na kugeuka rangi ya kahawia kabla majani<br />

hayajakauka kabisa. Unapochelewa kuvunwa<br />

mpunga hukauka shambani na hupukutika na<br />

kupungua uzito.<br />

Baada ya kuvunwa mpunga husafishwa kwa<br />

kupeta na huhifadhiwa kwenye mapolo na<br />

magunia kwa matumizi ya baadae.<br />

Kimetayarishwa na<br />

Kamisheni ya <strong>Kilimo</strong>, Utafiti na Elimu kwaWakulima<br />

(Kitengo cha habari na Vielelezo)<br />

Wizara ya <strong>Kilimo</strong>, Mifugo na Mazingira<br />

S. L. P 159, ZANZIBAR<br />

Juni, 2008<br />

WIZARA YA KILIMO, MIFUGO NA<br />

MAZINGIRA - ZANZIBZAR<br />

MBINU MBINU BORA BORA ZA<br />

ZA<br />

UZALISHAJI<br />

UZALISHAJI<br />

MPUNGA MPUNGA WA<br />

KUTEGEMEA KUTEGEMEA MVU MVUA MVU

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!