12.12.2012 Views

1` 2` UBORA NA UPANGAJI WA KOROSHO KATIKA MADARAJA ...

1` 2` UBORA NA UPANGAJI WA KOROSHO KATIKA MADARAJA ...

1` 2` UBORA NA UPANGAJI WA KOROSHO KATIKA MADARAJA ...

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

<strong>1`</strong> <strong>2`</strong><br />

<strong>UBORA</strong> <strong>NA</strong> <strong>UPANGAJI</strong> <strong>WA</strong> <strong>KOROSHO</strong><br />

<strong>KATIKA</strong> <strong>MADARAJA</strong><br />

_____________________________________<br />

Utangulizi<br />

Kwa kipindi kirefu ubora wa zao la korosho<br />

umekuwa ukididimia siku hadi siku kwa<br />

sababu mbalimbali. Baadhi ya sababu hizo ni<br />

ndani ya uwezo wa wakulima na zingine<br />

zimesababishwa na wanunuzi chini ya mfumo<br />

wa soko.huria ulioanza msimu 1992/93.<br />

Kipeperushi hiki kinaelezea namna ya kulinda<br />

na kudumisha ubora wa korosho toka<br />

shambani hadi gulioni ili kuinua kipato cha<br />

mkulima.<br />

Ubora wa Korosho.<br />

Ubora wa korosho unaanza shambani. Ili<br />

mkulima apate korosho nying na zilizo bora ni<br />

budi azingatie kanuni za kilimo bora cha<br />

korosho ikiwa ni pamoja na:-<br />

• Kuweka shamba katika hali ya usafi ili<br />

wadudu na magonjwa yasipate nafasi<br />

ya kujificha na kuzaliana.\<br />

Picha ya shamba<br />

• Kupanda mazao ya msimu kama<br />

mtama, mahindi na jamii ya kunde<br />

katika shamba la korosho kama sehemu<br />

ya matumizi bora ya ardhi na<br />

kupunguza gharama za uendeshaji.<br />

• Kutumia njia za asili ama madawa ili<br />

kudhibiti Magonjwa yanayoathiri<br />

ubora na uwingi wa korosho.<br />

3`<br />

• Kuokota korosho zilizoanguka<br />

zenyewe na sio kuzitikisa pamoja na<br />

kutoa kikonyo chake chote.<br />

• Hakikisha kuwa nyama ya bibo<br />

inayobakia kwenye korosho imetolewa<br />

na kifaa kikali kuzuia uharibifu dhidi<br />

ya maonjwa na wadudu.<br />

• Kuanika korosho juani katika sehemu<br />

iliyosafi na kavu kwa muda wa siku<br />

mbili hadi tatu ili kuhakikisha kwamba<br />

zimekauka inavyotakiwa. Korosho<br />

zilizokauka vizuri hutoa mlio wa sauti<br />

kali ukiziangusha chini.<br />

• Sehemu ya kuanikia korosho sharti iwe<br />

safi ili korosho zisipate uchafu.<br />

• Kuzipanga korosho kimadaraja na<br />

kuzihifadhi ndani ya magunia<br />

kimadaraja.<br />

• Kuhifadhi magunia ya korosho juu ya<br />

chaga kwenye chumba kikavu na sio<br />

sakafuni.


• Magunia ya mkonge au jute huruhusu<br />

hewa kupita kwa urahisi wakati wa<br />

kuhifadhi korosho.<br />

• Kagua ghala lako ili kubaini kuwepo<br />

kwa wadudu waharibifu kama mchwa.<br />

KUPANGA <strong>MADARAJA</strong> YA <strong>KOROSHO</strong>.<br />

Korosho zipangwe kwenye madaraja mawili.<br />

Kwa kuzingatia sifa zifuatazo:-<br />

Daraja la Kwanza (Standard Grade- SG)<br />

• Korosho za daraja la kwanza zitakuwa<br />

na sifa zifuatazo.<br />

• Zitatoa mlio wa sauti kali ukiziangusha<br />

chini.<br />

• Zina rangi ya kijivu au kikahawia<br />

kilichofifia.<br />

• Hazina makunyanzi.<br />

• Hazina madoadoa kwenye ganda la nje.<br />

• Zina umbile safi.<br />

• Zimekomaa vizuri, unyevu asilimia 12.<br />

Picha ya korosho SG<br />

Daraja la Pili (Under Grade – UG)<br />

• Zimekomaa.<br />

• Zimekauka unyevu asilimia 12, lakini<br />

ganda lake la nje lina madoa doa.<br />

• Zina makunyanzi.<br />

Korosho za daraja la kwanza na la pili zote ni<br />

budi ziwe na sifa za msingi za kukauka vizuri<br />

na ujazo wa kutosha ndani karanga)<br />

Picha ya korosho UG<br />

Korosho zisizotakiwa.<br />

• Hazikukomaa vizuri.<br />

• Hazikauka au mbichi.<br />

• Zimeota.<br />

• Zina makunyazi.<br />

Hazina rangi ya kijivu au kikahawia<br />

kilichofifia.<br />

Picha ya korosho Chafu<br />

UTAFITI <strong>NA</strong> MAENDELEO<br />

KANDA YA KUSINI<br />

<strong>UBORA</strong> <strong>NA</strong> <strong>UPANGAJI</strong> <strong>WA</strong><br />

<strong>KOROSHO</strong> <strong>KATIKA</strong> <strong>MADARAJA</strong><br />

Imetolewa na<br />

KITUO CHA UTAFITI,<br />

<strong>NA</strong>LIENDELE,<br />

S. L. P. 509,<br />

MT<strong>WA</strong>RA

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!