<strong>Aprili</strong> - Juni, 2011WAHARIRI/MAONI/PICHA YA JARIDABodi ya WahaririWashauriAffan O. MaalimJuma Ali JumaDk. Bakar S. AsseidMhariri MkuuDk. Juma M. AkilMsanifu na MhaririMtendajiHashim H. ChandeWahariri WasaidiziMakame M. AbdulrahmanNassor S. MkarafuuOthman A. MaulidNassor S. MohammedMpiga chapaFatma A. JumaMpiga pichaKhamis A. BakariANUWANIWizara ya <strong>Kilimo</strong>,Maliasili - ZanzibarS.L.P. 159Simu: +255 24 2230986Fax: +255 24 2234650E-mail: kilimo@zanlink.comTovuti: kilimoznz.or.tzMAONI YA MHARIRINdugu Wakulima, umuhimu wa kilimo cha mpunga unaonekana wazina viongozi wakuu wa Serikali Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti waBaraza <strong>la</strong> Mapinduzi Mhe. Ali Mohamed Shein, Makamo wa kwanzawa Rais Mhe. Seif Sharif Hamad na Makamo wa pili wa Rais Mhe.Seif Ali Iddi katika siku tofauti walipotembelea mabonde ya mpungayaliyopo katika wi<strong>la</strong>ya na mikoa ya visiwa vya Unguja na Pemba nakujionea wenyewe jinsi kilimo hicho kinavyoendelezwa. Wakati waziara zao viongozi hao walipata fursa ya kuzungumza na wakulimana wafanyakazi wa Wizara ya <strong>Kilimo</strong> na Maliasili na kuweza kujua halihalisi ya kilimo hicho muhimu cha chaku<strong>la</strong> kwa wazanzibari wengi. Nijambo <strong>la</strong> fahari kwetu kuona kuwa viongozi wetu hao licha ya kazi zaowana nyingi wameweza kutembelea sekta ya kilimo na kutilia mkazokilimo hicho na zaidi walifurahishwa na juhudi zinazochukuliwa katikakuimarisha kilimo hicho.Ndugu Wakulima, hata hivyo ni juu yetu kuongeza bidii katikakuimarisha ukulima wa mpunga kwa kuongeza kasi kwa kutumiambegu bora, mbolea na kuhakikisha tunapalilia kwa wakati ili mpungauote vizuri bi<strong>la</strong> ya kuzongwa na magugu. Mara nyingi uzalishaji mpungahuwa duni iwapo hatutotumia mbegu bora, mbolea na kufanya palizikwa wakati kama inavyoshauriwa na wataa<strong>la</strong>mu.Ndugu Wakulima, wakati wote wa kuvuna mpunga tunashauriwakuhakikisha mavuno yetu yanakuwa bora hatuna budi kufuata kanunibora za uvunaji, uanikaji na uhifadhi wa mpunga wetu. Tukiwa badokatika sua<strong>la</strong> hilo <strong>la</strong> kilimo cha mpunga inabidi wakulima wa mpungahivi sasa tufi kirie nini cha kupanda baada ya kuvuna mpunga ili tuwezekuongeza kipato chetu, tuhifadhi mashamba yetu kutokana na maguguna kuirutubisha ardhi kwa ajili ya msimu ujao.Ndugu Wakulima, utafi ti uliofanywa unaonesha kuwa katika mabondeya mpunga wa kutegemea mvua inashauriwa na inandekezwa sanawakulima kupanda kunde baada ya kuvuna mpunga. Kwa mpangohuu mkulima anafaidika kwa kupata kunde, kuzuia magugu kuota kwawingi na kurutubisha ardhi kutokana na zao hilo, hivyo kupanda kundekunamwezesha mkulima kutengeneza konde yake kwa msimu ujao.Ndugu Wakulima, mara nyingi baada ya kuvunwa mpunga kondezinaachiwa bi<strong>la</strong> ya kupandwa kitu chochote kunakosababisha kuotakwa magugu na inapofi ka musimu wa mpunga kazi huwa kubwa zaidiya kuchimbua na kuburuga.Ndugu Wakulima, kwa kumalizia ni vizuri tukumbushane kwambatusijaribu kuuza mpunga wetu wote baada ya kuvuna bi<strong>la</strong> ya kujiwekeaakiba, kwanza tuhakikishe tunajiwekea chaku<strong>la</strong> cha kutosha na ziadandiyo tunaiuza.PICHA YA JALADAKatika picha anaonekana Waziri wa <strong>Kilimo</strong> na Maliasili Mhe. MansoorYussuf Himid akipata maelekezo kuhusu kilimo cha zao <strong>la</strong> vani<strong>la</strong> kutokakwa mkulima mzoefu wa zao hilo huko Kizimbani wakati alipofanyaziara za kuwatembelea wakulima na taasisi zilizomo katika Wizara ya<strong>Kilimo</strong> na Maliasili.2
ZIARA YA RAIS KATIKA MAENEO YA KILIMO <strong>Aprili</strong> - Juni, 2011MAENEO YA KILIMO YA UNGUJA NA PEMBANa Mzee M. MzeeRais wa Zanzibar na Mwenyekitiwa Baraza <strong>la</strong> Mapinduzi Mhe. Dk.Ali Mohamed Shein alifanya ziara yakutembelea sekta ya kilimo na maliasilikatika visiwa vya Unguja kuanziatarehe 23 hadi 28/5/2011 na Pembatarehe 30/5 hadi 4/6/2011. Ziara hiyoilikuwa na lengo <strong>la</strong> kujua mafanikio,changamoto na hatua za kuwasaidiawananchi kufi kia malengo ya Serikaliya kujitosheleza kwa chaku<strong>la</strong>, lishe nakupunguza umasikini nchini. Katikaziara hiyo Mhe. Rais aliongozanana Mhe. Mansoor Yussuf HimidWaziri wa <strong>Kilimo</strong> na Maliasili, KatibuMkuu, Manaibu Makatibu Wakuu,Wakurugenzi na Maofi sa wa Wizarahiyo.Ziara hiyo ilianza kwa kukagua kilimocha mpunga wa umwagiliaji maji katikabonde <strong>la</strong> Mtwango ambapo aliwaahidiwakulima kuwapatia pembejeo kwabei nafuu na kwa wakati na kuimarishamiundombinu ya umwagiliaji maji nakusisitiza kuwa kilimo bi<strong>la</strong> maji, mboleana mbegu bora hakiwezi kuwa na tija.Akiwa katika Bonde <strong>la</strong> BumbwisudiMhe. Rais alipata maelezo yamafanikio, changamoto na malengoya uzalishaji wa mpunga na aliahidikuzipatia ufumbuzi changamotozilizopo na kusema Serikali ina nia yakumkomboa mkulima ili aondokane nakilimo duni na kufi kia kilimo chenye tijakwa faida yake na kwa taifa.Katika Kituo cha <strong>Kilimo</strong> KizimbaniMhe. Rais alitembelea sehemu yautafi ti wa mbegu za mpunga, muhogona migomba na kupata maelezo yauzalishaji wa mbegu na utafi ti waudhibiti wa wadudu na maradhi,ambapo aliombwa kusaidia vitendeakazi na kaboresha mas<strong>la</strong>hi ya watafi tiwaliopo ili wasikimbie kutokana namas<strong>la</strong>hi duni.Akiwa katika sehemu ya utibabu wamimea na ukaguzi wa mazao,Mhe. Raisalipata maelezo kuhusu udhibiti wa nziwa matunda, kuangalia maabara yauzalishaji wa miche kwa kutumia Chupa(Tissue culture) na maabara ya udongoambapo alionyeshwa aina tofauti zaudongo zilizopo Zanzibar na kupatamaelezo juu ya utafi ti wa udongo nafaida zake kwa mazao. Pia alitembeleakituo cha usarifu wa mazao na kushaurijambo hili lipewe kipaumbele naRaisi wa Zanzibar, Mhe: Dkt. Ali Mohamed Shein wa kwanza kulia akiwa na KatibuMkuu wa Wizara ya <strong>Kilimo</strong> na Maliasili ndugu Affan O. Maalim na wafanyakazi wengineakipata maelezo kuhusu kilimo cha umwagiliaji maji kutoka kwa mtaaamu ndugu Kadirikuwashajiisha wawekezaji wa ndanikuwekeza katika sekta hiyo. Aidha,aliwataka wafanyakazi na wanafunziwa Chuo cha <strong>Kilimo</strong> Kizimbani kusomazaidi na kwa bidii na kuahidi kukisaidiachuo hicho kiweze kutoa Diploma hadiDigirii.Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein katikaMkoa wa kusini Unguja, alimtembeleandugu Ahmed Saleh mkulima mwekezajiwa shamba <strong>la</strong> viungo na matunda hapoKidimni, Kituo cha Uzalisha mbeguza kilimo Bambi kuangalia uzalishajina utayarishaji wa mbegu mpya zampunga aina ya NERICA, pia alifi kabonde <strong>la</strong> mpunga Cheju na kukaguaukulima wa mpunga wa kutegemeamvua. Aidha, Rais aliwatembeleawakulima wa migomba pamoja nashamba <strong>la</strong> migomba <strong>la</strong> Mwakilishi waJimbo <strong>la</strong> Makunduchi, Mhe. Haroun AliSuleiman na alimalizia ziara yake kwakufanya majumuisho katika ukumbi waChuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu.Mhe. Rais akiongozana na Waziri wa<strong>Kilimo</strong> na Maliasili Mhe. Mansoor YussufHimid pamoja na mawaziri wengine,wakuu wa mikoa, makatibu wakuu naviongozi wa vyama vya siasa alifanyaziara kama hiyo kisiwani Pemba. Akiwakatika Wi<strong>la</strong>ya ya Wete alitembeleaKituo cha kilimo cha mpunga wa3umwagiliaji maji Mangwena na kupatamaelezo ya utekelezaji wa kilimo hicho.Katika shamba <strong>la</strong> ushirika <strong>la</strong> MabiboJunguni Mhe. Rais alipata fursa yakuangalia kilimo cha mikarafuu,muhogo na mda<strong>la</strong>sini ambapo alielezakuwa Serikali ina mpango maalum wakuimarisha zao <strong>la</strong> karafuu na kupunguzabei za pembejeo, pia aliiagiza Wizara ya<strong>Kilimo</strong> na Maliasili kuandaa ziara zawakulima kutoka maeneo mbali mbaliya Zanzibar kwenda huko kujifunzakilimo cha mikarafuu.Ziara iliendelea katika Wi<strong>la</strong>ya yaMicheweni kwa kutembelea bonde <strong>la</strong>Kanambe kwa kukagua ukulima wampunga, kupata maelezo ya ukulimahuu na changamoto zilizopo ikiwa nipamoja na kutotumia mbegu bora,matumizi madogo ya mbolea naupungufu wa mvua katika kipindi chakuchanua mpunga. Mhe. Rais alihimizakulima kilimo chenye tija na kuwatakawakulima waongeze juhudi ili kuzalishaanga<strong>la</strong>u gunia 30 hadi 40 za mpungakwa eka na Serikali itajitahidi kuwekezakatika kilimo cha umwagiliaji maji.Katika bonde <strong>la</strong> Mpunga <strong>la</strong> Mziwandaambalo linategemewa na watu wengiwa Micheweni kwa kilimo hicho,kuingiliwa na maji chumvi Raisalishuhudia. Mhe. Rais akiangalia