Mheshimiwa Naibu Spika, haya ninayoyasema yana mantiki yake. Tulipokwenda Marekanimwezi wa Tisa, tumekutana na Mshauri wa Rais Bush kwa masuala ya Kiafrika. Tukamwuliza ninyimnawapa watu wenu subsidy na ndio Mheshimiwa Waziri wa Viwanda mlikuwa kule Cancun akasemalook here, wanaolima hapa sio asilimia hata kumi. Sasa kama mtu anaweza akawa na ng’ombe wa maziwakule kwangu kikombe kimoja, halafu lita moja Sh.40/=, lakini mashudu kununua zege, kununua dawa zakuoshea, sijui kununua chumvi, sijui kumwosha, yule anayekata nyasi, kwa mwaka gharama nzima niSh.200,000/= na akaja kuuza hayo maziwa yake gharama akatoa Sh.40,000/=, anasema ni kitu ambachohata wewe mwenyewe unaona mahesabu haya hayaingii kichwani. Kwa sababu kwanza yale maziwayamenywewa na watoto ambao wangeugua unyafuzi, mwingine kesho atakuwa Rais.Hayo maziwa yameuzwa kwenye mahoteli na watu wakapata ajira kwenye mahoteli, nyama yahuyo ng’ombe imeuzwa kwenye hoteli na mwingine akinyimwa nyama shin<strong>go</strong> yote inarefuka. N<strong>go</strong>zi yang’ombe yule amekwenda kwenye kiwanda watu wakapata ajira, wenye vishikizo wakapata ajira, wenyekutengeneza guru wakapata ajira, sasa huyu katika mzunguko mzima ameweka ajira huyu lazima afikemahali tum-subsidize. That is why tunawa-subsidize, wakajibu hivyo. Ni hoja ambayo huwezi ukaipingakwa mantiki hiyo. Kwa misingi hiyo tukiendelea ku<strong>go</strong>mbana na tusipoliangalia tukadhani kwamba kusubsidizewakulima ni kitu kibaya, nadhani tutakuwa tunajipeleka mahali ambapo tutashindwa kwa sababukwa vyovyote vile hatutawalazimisha na wao kisiasa hawatakubali. Kwa mfano hivi sasa tunaWamachinga pale, mtu mmoja alikuwa anasema waulizwe hizo bidhaa mnatoa wapi? Lakini watakwendawapi? Kwa sababu elimu yao ni Darasa la Saba! Sasa wakija pale wakati mwingine hata sisi tuliopokwenye Upinzani tunasema wanawafukuza pale Kariakoo, sasa pale Kariakoo wakijazana kama uyogahuoni ni shida? Sasa haya mambo sisi tunayaona hivi hivi tu. Lakini kama ukiboresha ile Sekta, kuwasubsidizehali inakwenda vizuri.Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kuyasema hayo, nilikuwa nasema kwamba sheria hiitumeitunga, iko hoja ilitolewa na Mheshimiwa Waziri kwamba kwa mfano lile gunia la katani linadumu.Ndiyo! Lakini gharama yake ni Shilingi ngapi? Sh.1,500/=. Kama mkulima wa kahawa anataka kununuamagunia 100, unazungumza akatumie Shilingi laki moja nadhani na zaidi, kama mahesabu yanguhayajazeeka; kuna yale magunia ya jute ni Sh.200/= na yeye shida yake ni kupakia mzi<strong>go</strong> wake iliusiende unamwagika akauze pale na wakishapima wala kale kagunia ka-jute wala hakana hata robo kilolakini akisema lile la katani wanasema tunakukata na kilo mbili. Sasa hata mahesabu yenyewe yanakuwahayawezi kuingia. Kwa hiyo, hoja ya msingi tunapoliangalia hili Mheshimiwa Waziri wa Biashara naViwanda, yapo mambo mengi ya kufanya katika kupiga hatua ili Muswada wetu uweze kufanya kazivizuri. Sisi wala tusiseme kwa sababu tuna sheria, atakaye-dump hapa tunamrukia, sasa unamrukia ndiyolakini tunajiandaa vipi ili kuweza kuhakikisha kwamba na sisi tunachukua kile kitu kinaitwa comparativeadvantage? Ni bahati mbaya kwamba mimi sikusoma uchumi lakini nadhani yapo mambo mengineambayo unaweza kuyaona kwa mantiki hiyo. Kwa hiyo, hilo ningeomba tulione.Mheshimiwa Naibu Spika, maana yake sisi ndio umesema tutenganishe na kilimo. Kama nichuma, kiko pale sijui liganga; tena ni mlima wala sisi hatupashwi kuchimba ardhini, kiko juu.Wamekwenda pale na vijana mnapeleka pale wanakatakata hivi mnakwenda kuuza. Sasa sijuituzungumzie nini kwa sababu hawata-subsidize hizi chuma kule nadhani. Kama ni mkaa wa mawe, sisitunao, hawawezi kuchimba, hawata-subsidize hiyo. Nadhani our base need kwa sababu huwezikuzungumzia industrial revolution kwa nchi kama hii bila kuzungumzia Agrarian Revolution na kuviconnect.Mheshimiwa Naibu Spika, sasa cha msingi hiyo nadhani Mheshimiwa Waziri wa Viwanda naBiashara lazima aliangalie hilo kwa sababu hilo suala la subsidy haliko kwenye vyuma, halipo kwenyeuranium, halipo kwenye petroleum wala halipo kwenye mambo mengine yale. Liko kwenye bidhaa hiziambazo ni za kilimo na ambazo tunazipigia kelele na ndizo hizo wakishaziongeza value wanapokujakushindana na sisi, kwa sababu wao wangeliacha vile maana kama bei ya kilo moja ya pamba ama yakorosho ambazo ndizo zinapigiwa kelele kwenye soko la dunia tuseme kilo ya pamba ni Sh.1,200/=,Wazungu wana mahesabu. Kama ardhi yao imechoka, ameweka trekta, ameweka mafuta, amewekavibarua, amewaajiri na mishahara mikubwa kufuatana na standard ya maisha, sasa wao hawawezi kukubalikama sisi tunavyopeana Sh.2,000/= au Sh.200/= au Sh.500/= halafu unamwambia nyamaza kwa sababustandard ya maisha yetu ni kutumia kwa Sh.200/= au Sh.500/=.
Baada ya kuyasema hayo, nilikuwa nasema sheria hii mimi sina tatizo nayo, lakini tunawaombawaende ili iweze kutekelezeka vizuri na tuweze kufaidi, tuseme tuna sheria basi mambo yetu yamenyookahakuna atakayefanya dumping. Maana kuna vitu vingine mtavizuia, sisi wenyewe tutaanza kupiga kelele.Maana yake mwingine atachukulia kwa sababu kuna advanced technology watu wanazalisha kwa wingina kwa sababu ya volume ya business halafu ndio wanauza vitu vyao huku chini sasa inatafsiriwa kwambahawa wanataka kufanya dumping katika nchi yetu. Baada ya kuyasema hayo, nadhani ujumbe umefika.Niwashukuruni wote kwa kunisikiliza, lakini nitaendelea kuchangia na kujenga hoja inapobidi nakuzisimamia kwa msimamo thabiti. Ahsante sana. (Kicheko/Makofi)MHE. ABDULLATIF HUSSEIN ESMAIL: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Miminakushukuru kwa kunipa fursa hii ya kuchangia Muswada huu wa Anti-Dumping.Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri amesema kwamba Muswada wa Anti-Dampingunatumiwa sana na nchi zilizoendelea. Nakubali sana. Nchi maskini hazina uwezo wa kutoa subsidies nazenye uwezo ni hizo hizo nchi tajiri tu, isipokuwa nchi maskini zina uwezo wa kutoa incentive kwa mfanoIndia wana zero tax katika all kinds of export. Adhabu ya kuongezewa ushuru, suspended duty, hofu yanguisije ikatumiwa vibaya sheria hii kuwabana waagizaji wa bidhaa mbalimbali ambao TRA leo ndioinawatazama kwa ajili ya mapato. Umoja wenye viwanda CTI watafanya kila njia kwa kushawishiwa nabaadhi ya wenye viwanda kuwabana waagizaji kwa kutumia ile policy inayoitwa live and let die. Serikaliyetu inatakiwa iwe kama buibui na spider, itembee juu ya maji. Spider can walk over the surface of wateriwapatie maendeleo wananchi wa nchi hii na inafanya hivyo, naipongeza Serikali yetu. Wahengawanasema bora uaminiwe kuliko kupendwa (Kicheko/Makofi)Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu ukosefu wa soko la ndani, mimi nasema soko la ndani lipo.Kuna alphabeti tatu, AID wenye viwanda washughulikie AID. A - Advatize, I - Initiative and D - Dynamic.Supply what the market wants. Binadamu hanunui anachokitaka, ananunua anachokihitaji. Walewanaopenda sana hawazeeki. Serikali yetu iwapende wafanyabiashara waagizaji bidhaa, wenye viwanda nakadhalika. (Kicheko)Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, naunga mkono hoja kwa asilimia mia. Ahsante.(Kicheko/Makofi)MHE. OMAR MJAKA ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii.Lakini kwanza nataka nitumie nafasi hii kuwapongeza Wa<strong>bunge</strong> wote wale ambao wameshinda katikaBunge la Afrika. Tunawatakia mafanikio na kazi njema ya Taifa hili kwa misingi na Katiba ya nchi yetuna Katiba watakayoikuta katika Bunge la Afrika.Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kuwapongeza wenzangu hao, nataka nichukue nafasi hii namimi kuunga mkono Muswada huu wa Anti-Dumping and Countervailing Measures asilimia mia kwa mia.Mfumo wa uchumi wa ushindani hivi sasa ndio msingi wa uchumi wa nchi yoyote ile duniani. Nikinukuuzile mada ambazo ziliwasilishwa jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda pamoja na hotuba ya MgeniRasmi ambaye ni Waziri Mkuu, kwa kweli nataka niipongeze Serikali kwa kuleta Muswada huu nakutunga sheria hii kwa maslahi ya Taifa letu hili la Tanzania. Nikimnukuu Mheshimiwa Waziri Mkuukatika hotuba yake ya ufunguzi alisema, “Kuingia kwa bidhaa kutoka nje na kuuzwa kwa bei ya chinikunaweza kuua viwanda vyetu nchini.” Sasa kama tumeshaanza kuwa na hofu kama hii ni lazima sheriahizi ambazo tutakuwa tumezitunga ziondoe hofu hii ambayo tayari inaonekana imeshaingia ndani yaSerikali na hata jamii inaweza ikapata mshtuko mkubwa sana. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziritunamwomba kwamba aisimamie Muswada huu kwa nguvu zote mara tu itakapokamilika na kupitishwa.Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri Mkuu alisema ni rahisi sana nchi yetu kugeuzwasoko na nchi nyingine. Kwa hiyo, vile vile tuitake Wizara hii isimamie juu ya bidhaa ambazo zinaingiakatika nchi yetu kwamba ziwe ni bidhaa sahihi na zenye viwan<strong>go</strong> vinavyohitajika. Kama tutaruhusubidhaa ziingie tu na tukija tukabaini baadaye kwamba zina madhara kama ambavyo tunazungumzia sasahivi mifuko hii ya Rambo, kuitoa itakuja kuwa ni tatizo. Kwa hiyo, sheria hii iweze ku-cover yale maeneo
- Page 1 and 2: BUNGE LA TANZANIA_______________MAJ
- Page 3: jana tarehe 5 Februari, 2004, suala
- Page 6 and 7: La pili ni kwamba, Mkandarasi huyu
- Page 9 and 10: (a) Je, Serikali ina mpango gani wa
- Page 11 and 12: mambo mengine, umebainisha kwamba S
- Page 13 and 14: La pili, kama itakuwa Chuo Kikuu je
- Page 15 and 16: Na. 54Mikoa isiyo na Viwanda Nchini
- Page 17 and 18: (c) Mheshimiwa Spika, napenda kumha
- Page 19 and 20: kutumia dawa ya kujipaka mwilini, k
- Page 22 and 23: Napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mb
- Page 24 and 25: HON. AMBASSADOR GETRUDE I. MONGELLA
- Page 26 and 27: DEPUTY SPEAKER: Honorable Omar Mjak
- Page 28 and 29: DEPUTY SPEAKER: Honorable Kidawa Ha
- Page 30 and 31: DEPUTY SPEAKER: Honorable Dr. Amani
- Page 32 and 33: I think the issue is stipulated cle
- Page 34 and 35: I do feel that the experience and e
- Page 36 and 37: DEPUTY SPEAKER: Don’t...HON. GEOR
- Page 38 and 39: I come to you with considerable exp
- Page 40 and 41: Mheshimiwa Spika, baada ya kusema h
- Page 42 and 43: Kwa hiyo, sisi hatujawahi kuona suk
- Page 44 and 45: Vile vile Mheshimiwa Dr. Juma Ngaso
- Page 46 and 47: Kundi la Wanawake walikuwa wagombea
- Page 48 and 49: vikaweza kuingia katika soko jipya
- Page 52 and 53: ambayo tunaona yanaweza kuleta atha
- Page 54 and 55: kweli waweze kuchambua ili tusije t
- Page 56 and 57: Nikaona hii labda hii Kiswahili cha
- Page 58 and 59: Naomba nichukue nafasi hii kumponge
- Page 60 and 61: kwa sheria ya Bunge hili kwamba Mak
- Page 62 and 63: General Tyre kinaendelea kufanya ka
- Page 64 and 65: Mheshimiwa Naibu Spika, juzi niliku
- Page 66 and 67: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo na
- Page 68: Sasa kutokana na hayo mimi nafikiri