Vile vile Mheshimiwa Dr. Juma Ngasongwa, najua mimi namtambua ni mion<strong>go</strong>ni mwa wachumiwazuri ni msomi mzuri halafu ni mtendaji wa kazi. Huyu alishafanya kazi mpaka kwenye vijiji alishakuwaDDD na mimi nataka kumsifu kabisa Mheshimiwa Dr. Juma Ngasongwa, mimi nilipokuwa Mkuu waMkoa wa Moro<strong>go</strong>ro ndiye alikuwa Mwenyekiti wa wasomi na watalaam wa University mbili SUA na IDM,walinishauri na kusaidiana na wananchi kuandaa mpan<strong>go</strong> wa maendeleo ya mkoa wa Moro<strong>go</strong>ro. Kwa hiyo,ana utaalam na utalaam mkubwa sana. (Makofi)Jambo ambalo nilikuwa nataka kushauri na tukubaliane pia wakati nilipouliza swali juzi akajibukwamba hakuna nchi inayoweza kujitegemea mia kwa mia. Kitalaam, kiuchumi ni sawa, lakini halisinilikuwa mimi nazungumzia halisi ya Tanzania kwamba mipan<strong>go</strong> yetu lazima tujitegemee.Kwa hiyo, mimi nilikuwa naomba Waziri mwenyewe anisaidie atakapokuwa anajibu sasa asemeni katika sekta gani Tanzania na hususan kwenye viwanda ambako tumeanza kujitegemea?Mimi ninavyojua ni kuwa sehemu nyingi sana kwa mfano chukua textures tulikuwa tumefikambali wakati ule, lakini baada ya kuporomoka tunaanza upya. Kwa hiyo, nguo zinazoingia kutoka nje ninyingi kuliko tunazozalisha sisi. Mahali ambapo tumekazana tumefanya vizuri mpaka sasa ni sukari nakwenye sukari tumeanza kufanya vizuri kwa sababu tulishakubaliana na hatukubadilika. Tumekuwa namsimamo mmoja kuhusu mambo ya kodi na kubana uingizaji wa sukari kutoka nje ambayo ikiangiainabaki inapigwa kodi kubwa, tumevipa viwanda vyetu nguvu na sasa hivi uzalishaji umeongezeka kwakiasi kikubwa sana.Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, mimi nilikuwa nataka kusema kwamba sera yetu ni kujitegemea,narudia tena Mheshimiwa Spika, tunahitaji kuwa na programu ya kujitegemea kwa mfano tuchukue sisi niwazalishaji wa pamba, lakini sehemu kubwa ya pamba inauzwa nje wala haiuzwi nyuzi, tunauza pambayenyewe hatuuzi nyuzi ambazo zingeongeza thamani, zingeleta faida.Mheshimiwa Spika, hivi sasa mimi ninao ushahidi pia kwamba baadhi ya watu wanaotengenezanguo viwandani wana-import kutoka nje, wengine wanaagiza nguo ambazo zimekwisha kutengenezwakama Marekani halafu wanakuja wanazipiga mihuli. Hii iko hapa nchini. (Makofi)Sasa nilipokuwa nazungumza kujitegemea nilikuwa na maana hiyo kwamba kazana ujitegemee iliuwe na cha kuuza. Sasa hivi vile vile kama kwa mfano wafanyabiashara wasipoingiza bidhaa hapa nchinimapato ya Serikali yatashuka kwa sababu kodi kubwa tunaotegemea ni ya imported <strong>go</strong>ods siyo za kwetuwenyewe tulizozalisha wenyewe.Kwa hiyo, nataka niseme kwamba mimi bado, lazima tutengeneze mpan<strong>go</strong> wa kujitegemeakiviwanda na tutaje maeneo ambayo uwezo tunao. Moja ni Textile Industries, ya pili mafuta ya kupikiakama tulivyofanya kwenye sukari. Bila mafuta ya kupikia naomba niseme kwa tahadhari kwa Wizara naSerikali kwa ujumla. Mwaka jana tulipokutana Wizara ya Fedha ilileta na ikapitishwa kodi zinazolindaviwanda vyetu vya mafuta ya kupikia na sabuni. Lakini hivi ninavyozungumza wafanyabiashara wa sektahiyo ya mafuta na sabuni wamekwishazua bado ubishi na wanakwenda kila ofisi wanayoweza kukampeniawatu wa Serikali wakubali sisi turudi nyuma tubadilishe maamuzi tuliyofanya katika mwaka wa fedha.Sasa mimi nawatahadharisheni msije mkafungua pandola nyingine, kwa sababu habari nilizokuwanazo humu, nikizileta humu Bungeni kuna watu wataumia hapa kuhusu jambo hili la mafuta. Sasa mnatakaturudie kule kule tulikotoka? Maana yake watu wazima mnakutana leo mnasema tulinde viwanda vyetu,kesho mnaanza kampeni ya kuhama tena. Hivi nazungumza kuna watu wanafanya mikutano Dar es Salaamwa viwanda vya sabuni, wako wakubwa wanataka kuwala wado<strong>go</strong>. Viwanda vya kutengeneza mafutanchini vipo.Vile viwanda ambavyo wakubwa wamekuwa wakienda maandamanoni kwa Musa zile ni packingfactories, wana-pack raw materials 100% kutoka Malaysia wanaingiza kwenye makopo ndiyo watu wotetunaandamana kwenda kule na kushangilia kwamba nchi ina capacity. Lakini capacity iliyopo nchiniambayo ni 120 tones inakufa siku hadi siku kwa ku-pack mafuta kwenye makopo siyo kusindika mafuta.Kusindika mafuta unaweza ukaenda ukakuta oil na viwanda vingine vipo mimi nina rekodi ya mapato.
Kama tunaka Watanzania wote, Serikali tunataka kutoka sasa tuanze tujenge umoja, yako mambotutawanong’oneza pembeni msifanye ili tusiyalete hapa Bungeni na hili acheni la sabuni na mafutalitawaumiza watu. (Makofi)Pili, nataka tusiabudu sana Jumuiya ya Afrika ya Mashariki. Kuna vitu tunataka tukakatae kwenyevikao, ukiambia kila kitu kiwe zero tarrif, tunakuwa watumwa wa Kenya pale pale. Hata wanaokampeniamafuta kutafuta mara zero tarrif mara sabuni ni makampuni ya Kenya wana branches za wenzaowanaowatumia.Kwa hiyo, mimi natoa tahadhari hiyo, kwa Serikali muwe very careful juu ya jambo hilo. Mimisiwezi kwenda Sumbawanga nikaona wananchi wanaolima sunflower wanaacha kulima kwa sababuhawawezi kusindika kwa kuwa tunakumbatia wakubwa wanaosindika mafuta kwenye makopo. Kwa hiyo,nataka niseme hiyo, msije mkakosea, msifanye kosa hilo. (Makofi)Mheshimiwa Spika, la mwisho ambalo ningependa kushauri hapa nakubaliana na MheshimiwaEliachim Simpasa na Mheshimiwa Leonard Derefa, mimi nchi nyingi ambazo nimekwenda na wengitunaokwenda nchi nyingi mkienda shopping siyo ubaguzi mnakuta ubora wa vitu vinavyofanana lakini kwatofauti kido<strong>go</strong> kwamba mnatengeneza vitu lakini viwe bora lakini vinaweza kununuliwa na aina fulani yawatu na aina ya pili ya watu na ya tatu. Ukienda unajua kabisa mimi nakwenda huku tofauti kwa mfano sisiDar es Salaam bei ya vitu haitegemei ilivyozalishwa, inategemea mpangaji, mfanyabiashara amepangawapi duka lake. Shati unalokuta Kariakoo, ukilikuta Independence ya Samora lina bei tofauti na lile.Kwa hiyo, anachofanya bei iwe tofauti ni kwa kuwa yeye amepanga biashara Mtaa wa Samorasiyo quality ya bidhaa ile iliyo Kariakoo na kwenye duka lake. Lakini nchi zingine ukifika wanakuonyeshakabisa kwamba mtakaye shati hili bei yake ni hii kwa sababu tunataka kila mtu avae. Ukienda hukukwingine utakuta hata ukishika utaona kweli nimevamia ni nzuri kwa thamani na quality. Sasa sisi kwetu nitofauti. Kwa hiyo, mimi ningependa tufike hapo. (Makofi)Hata hili la kanga kwa vijijini kwetu kanga ni vazi, Mijini kanga siyo vazi. Naomba radhiakinamama wanisamehe. Naweza kusema ni kama anasa kido<strong>go</strong>, lakini anasa nzuri inavaliwa wakatimzuri. Kwa hiyo, kwa Mijini kanga inayokuwa transparent si mbaya sana, ni vazi la raha kwa wakati ule.Kwa hiyo, ikiwa transparent ni nzuri zaidi kuliko ile nzito, kumbe Sumbawanga ni vazi kanga,watu wanavaa wanakwenda hata kwenye sherehe wanavaa kanga. Kwa hiyo, wasingependa kuonekana.Kwa hiyo, nataka tuelewane vile vile kwamba tunapozungumza habari ya ubora tuzungumzie nguo maanayetu ni hiyo. (Makofi/Kicheko)Mheshimiwa Spika, baada ya hapo naunga mkono Muswada huu.SPIKA: Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong>, nimehakikishiwa na wahesabu kura kwamba karibuwanamaliza, kwa hiyo, sitaahirisha Bunge mpaka niwatangazie matokeo. (Makofi)MATOKEO YA UCHAGUZI WA WABUNGE LA AFRIKA(PAN-AFRICAN PARLIAMENT)SPIKA: Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong>, kazi ya kuhesabu kura zilizopigwa leo asubuhi imekamilika nanimeshakabidhiwa matokeo.Kanuni inasema kwamba: “Spika, akishakabidhiwa matokeo, he will report to the Assembly theresult of the election together with a number of votes recorded for each candidate in each of the groupsspecified above.”Katika kila kundi kila m<strong>go</strong>mbea amepata kura ngapi hatua ya kwanza. Hatua ya pili ndiyotunatangaza waliochaguliwa kuwa Wa<strong>bunge</strong> wa Bunge la Afrika. Sasa sehemu ya kwanza ya kilam<strong>go</strong>mbea amepata kura ngapi ni kama ifuatavyo:-
- Page 1 and 2: BUNGE LA TANZANIA_______________MAJ
- Page 3: jana tarehe 5 Februari, 2004, suala
- Page 6 and 7: La pili ni kwamba, Mkandarasi huyu
- Page 9 and 10: (a) Je, Serikali ina mpango gani wa
- Page 11 and 12: mambo mengine, umebainisha kwamba S
- Page 13 and 14: La pili, kama itakuwa Chuo Kikuu je
- Page 15 and 16: Na. 54Mikoa isiyo na Viwanda Nchini
- Page 17 and 18: (c) Mheshimiwa Spika, napenda kumha
- Page 19 and 20: kutumia dawa ya kujipaka mwilini, k
- Page 22 and 23: Napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mb
- Page 24 and 25: HON. AMBASSADOR GETRUDE I. MONGELLA
- Page 26 and 27: DEPUTY SPEAKER: Honorable Omar Mjak
- Page 28 and 29: DEPUTY SPEAKER: Honorable Kidawa Ha
- Page 30 and 31: DEPUTY SPEAKER: Honorable Dr. Amani
- Page 32 and 33: I think the issue is stipulated cle
- Page 34 and 35: I do feel that the experience and e
- Page 36 and 37: DEPUTY SPEAKER: Don’t...HON. GEOR
- Page 38 and 39: I come to you with considerable exp
- Page 40 and 41: Mheshimiwa Spika, baada ya kusema h
- Page 42 and 43: Kwa hiyo, sisi hatujawahi kuona suk
- Page 46 and 47: Kundi la Wanawake walikuwa wagombea
- Page 48 and 49: vikaweza kuingia katika soko jipya
- Page 50 and 51: Mheshimiwa Naibu Spika, haya ninayo
- Page 52 and 53: ambayo tunaona yanaweza kuleta atha
- Page 54 and 55: kweli waweze kuchambua ili tusije t
- Page 56 and 57: Nikaona hii labda hii Kiswahili cha
- Page 58 and 59: Naomba nichukue nafasi hii kumponge
- Page 60 and 61: kwa sheria ya Bunge hili kwamba Mak
- Page 62 and 63: General Tyre kinaendelea kufanya ka
- Page 64 and 65: Mheshimiwa Naibu Spika, juzi niliku
- Page 66 and 67: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo na
- Page 68: Sasa kutokana na hayo mimi nafikiri