NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA UCHUKUZI alijibu:-Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Omar Juma Omar, M<strong>bunge</strong> wa Pandani,kama ifuatavyo:-Mheshimiwa Spika, kimsingi ZANTEL haijakatazwa kutoa huduma Tanzania Bara. Inaweza nainaruhusiwa kutumia minara ya TTCL na ya Kampuni za simu nyingine za mikononi. Sababu pekee na yamsingi inayosababisha ZANTEL isiweze kutumia mfumo wake kutoa huduma za simu Tanzania Bara niMuda Maalum wa miaka minne uliopewa Kampuni ya Simu ya TTCL kutoa huduma zake hapa nchinihususan kwa huduma za simu za kawaida.Mheshimiwa Spika, napenda kutoa taarifa kuwa muda maalum wa TTCL kutoa huduma peke yakeutakwisha mwezi Februari, 2005 na Serikali imekwishatamka wazi kuwa baada ya muda huo kumalizika,TTCL hawataongezewa muda tena. Kuanzia hapo Kampuni zote ikiwa ni pamoja na ZANTEL zitaruhusiwakutoa huduma hizo kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania.Tayari ZANTEL na Mamlaka ya Mawasiliano, wameanza majadiliano kuhusu suala hili na taarifatulizonazo ni kuwa majadiliano yanaendelea vizuri.Na. 56Kuangamiza Mazalio ya MbuMHE. DR. CHRISANT M. MZINDAKAYA aliuliza:-Kwa kuwa katika miaka kama 30 hivi ya nyuma mbu hawakuwa wanazaliana kwa kiwan<strong>go</strong>kikubwa kama ilivyo sasa; na kwa kuwa kwenye maeneo ya baridi kama vile Ufipa ya Juu, Mbeya, Iringa,Ruvuma, Arusha na sehemu zenye miinuko mikubwa hapakuwa na mbu na kwamba wakati ule MabwanaAfya walikuwa na zana na dawa za kuua vyanzo vya mazalio ya mbu:-(a)(b)(c)Je, kwa nini maeneo ambayo hayakuwa na mbu sasa yana mbu?Je, isingekuwa vyema kukinga malaria kwa kuweka mipan<strong>go</strong> ya usafi na kuangamizamazalio ya mbu?Je, Serikali inafahamu kuwa u<strong>go</strong>njwa wa malaria ndio unaoua watu wengi zaidi kulikomaradhi mengine wakati uwezekano wa kutokomeza u<strong>go</strong>njwa huo upo?NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, napenda kujibu swali la Mheshimiwa ChrisantMajiyatanga Mzindakaya, M<strong>bunge</strong> wa Kwela, lenye sehemu ya (a), (b) na (c) kama ifuatavyo:-(a) Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa kuna baadhi ya maeneo hususan yale ya baridiambayo hayakuwa na mbu hapo zamani na sasa yana mbu wanaoambukiza u<strong>go</strong>njwa wa malaria. Hali hiiimejitokeza kutokana na shughuli kadhaa za kibinadamu katika kilimo, ujenzi na uharibifu wa mazingira.Shughuli hizi zimetengeneza mazingira muafaka ya mazalio ya mbu. Aidha, ongezeko la joto Duniani(Global Warming) kutokana na kuongezeka kwa joto na kupungua kwa tabaka la ozone (Ozone Layer),kumetengeneza mazingira mazuri kwa mbu kuweza kuzaliana.(b) Mheshimiwa Spika, Wizara ya Afya bado inazingatia kuwa usafi wa mazingira ni njiakubwa na muhimu katika kupambana na u<strong>go</strong>njwa wa malaria pamoja na ma<strong>go</strong>njwa mengineyanayoambukiza. Mikakati ya usafi wa mazingira inafanywa katika ngazi ya Halmashauri ambapowanashughulikia ukusanyaji na utupaji wa taka na usafishaji wa mifereji ya maji ya mvua. Aidha, elimukwa wananchi inatolewa kwa ajili ya kujikinga na malaria ikiwa ni pamoja na kuhimizwa kuweka usafi wamazingira wanamoishi na kufukia madimbwi ya maji.
(c) Mheshimiwa Spika, napenda kumhakikishia Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> kuwa, Serikaliinafahamu kwamba u<strong>go</strong>njwa wa malaria ndio unaoua watu wengi zaidi kuliko ma<strong>go</strong>njwa mengine. Aidha,takwimu zetu zinaonyesha kuwa asilimia 30 - 40 ya wa<strong>go</strong>njwa wa nje husumbuliwa na malaria na asilimia20 - 25 ya vifo vya watoto hospitalini husababishwa na malaria.Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mkakati wa kutokomeza u<strong>go</strong>njwa wa malaria ni mgumu kwamaana unahitaji fedha nyingi na kutokana na hali ya uchumi wa nchi, jambo hili haliwezekani.Kutokomeza malaria kunategemea zaidi maendeleo ya jumla ya wananchi. Kutokana na ufahamu huo,mwaka 1998 Tanzania kwa kushirikiana na Mashirika ya Kimataifa ya Shirika la Afya Duniani (WHO),Shirika la Kuhudumia Watoto (UNICEF) na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP),yalianzisha mkakati maalum wa kupambana na malaria. Mkakati huo unaitwa Roll Back Malaria. Mkakatihuu ulilenga kupunguza vifo vinavyotokana na u<strong>go</strong>njwa wa malaria kwa kiwan<strong>go</strong> cha asilimia 50ikilinganishwa na hali ilivyo sasa ifikapo mwaka 2010. Katika kipindi hicho, tumepanga kuboresha nyenzoza kupambana na malaria ambazo ni tiba bora na sahihi ya malaria, matumizi ya vyandarua vilivyotiwadawa na kuongeza juhudi za utafiti na ushirikishwaji wa wananchi.MHE. DR. CHRISANT M. MZINDAKAYA: Mheshimiwa Spika, nina maswali mawili yanyongeza.(i) Kwa kuwa Waziri amethibitisha hapa kwamba mojawapo ya mambo yanayofanya kazihii isifanyike vizuri ni gharama kwa sababu pesa nyingi zinahitajika lakini atakubaliana na mimi kwambakwa sasa hivi fedha zinazotolewa kwa ajili ya kuzuia au kuhangaika na u<strong>go</strong>njwa wa HIV ni nyingi sanakuliko za mbu ambapo tungeweza kufanya vizuri zaidi?(ii) Kwa kuwa Waziri amekiri kwamba kweli mbu wanazaliana hata katika maeneo ambapozamani hawakuwepo maana yake ni kusema mbu wanaongezeka kuliko kupungua, atakubaliana na mimikwamba iko dawa ambayo ikitumika katika maeneo wanakozaliwa mbu inaweza kuua mbu kabisa nawasizaliane tena kwa wingi?NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa kwamba, fedha zinazotumikakupambana na u<strong>go</strong>njwa wa UKIMWI ni nyingi ukilinganisha na zile za malaria. Lakini natakanimkumbushe Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> kwamba, fedha hizi nyingi zinatoka kwa wahisani au tuseme donorcountries na mara nyingi fedha hizo zinakuwa zimepangiwa wao wenyewe wanaelekeza kwamba fedhahizi zitumike kwa u<strong>go</strong>njwa fulani. Kwa hiyo, sio rahisi kubadilisha fedha za matumizi ya kupambana naUKIMWI kuzipeleka kwenye malaria.Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la kupulizia dawa kwenye maeneo ya mazalio ya mbu, jambohili linaeleweka lakini nilishawahi kusema kabla katika Bunge hili kwamba, tatizo tunalokabiliana nalohapa ni mambo mawili. Kwanza, gharama za kupulizia dawa katika maeneo ya eradication ya malaria,ilishashindikana kutokana na gharama kuwa kubwa. Pili, dawa iliyokuwa inatumika wakati ule (DDT)ilionekana ina athari kwa mazingira na kwa hiyo wahisani hawako tayari kuendelea kutoa fedha kwamatumizi ya dawa hiyo.MHE. ISMAIL J.R. IWVATTA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasiniulize swali la nyongeza.Inasemekana kwamba kati ya maeneo yanayochangia mbu kuzaliana ni makaro na vyoo, sasa sijuikama kuna ukweli wowote juu ya suala hilo. Kama ni kweli je, Serikali kwa utaratibu wa kupunguzagharama haiwezi kuweka utaratibu wa wananchi kuchangia gharama kwa kununua hiyo dawa ili na waowaweze kuchangia kuweka katika hizo sehemu ambapo mbu wanazaliana?NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, maeneo ambapo mbu wanazaliana ni maeneoyoyote yenye maji yaliyotuama. Kwa maana nyingine sehemu yoyote ambayo ina maji ambayo hayatembeibasi hapo inakuwa ni eneo la mazalio ya mbu. Sasa vyoo na makaro ni sehemu moja lakini madimbwiyaliyoko mbele ya nyumba zetu na kadhalika vile vile ni maeneo yanayosababisha tatizo hili.
- Page 1 and 2: BUNGE LA TANZANIA_______________MAJ
- Page 3: jana tarehe 5 Februari, 2004, suala
- Page 6 and 7: La pili ni kwamba, Mkandarasi huyu
- Page 9 and 10: (a) Je, Serikali ina mpango gani wa
- Page 11 and 12: mambo mengine, umebainisha kwamba S
- Page 13 and 14: La pili, kama itakuwa Chuo Kikuu je
- Page 15: Na. 54Mikoa isiyo na Viwanda Nchini
- Page 19 and 20: kutumia dawa ya kujipaka mwilini, k
- Page 22 and 23: Napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mb
- Page 24 and 25: HON. AMBASSADOR GETRUDE I. MONGELLA
- Page 26 and 27: DEPUTY SPEAKER: Honorable Omar Mjak
- Page 28 and 29: DEPUTY SPEAKER: Honorable Kidawa Ha
- Page 30 and 31: DEPUTY SPEAKER: Honorable Dr. Amani
- Page 32 and 33: I think the issue is stipulated cle
- Page 34 and 35: I do feel that the experience and e
- Page 36 and 37: DEPUTY SPEAKER: Don’t...HON. GEOR
- Page 38 and 39: I come to you with considerable exp
- Page 40 and 41: Mheshimiwa Spika, baada ya kusema h
- Page 42 and 43: Kwa hiyo, sisi hatujawahi kuona suk
- Page 44 and 45: Vile vile Mheshimiwa Dr. Juma Ngaso
- Page 46 and 47: Kundi la Wanawake walikuwa wagombea
- Page 48 and 49: vikaweza kuingia katika soko jipya
- Page 50 and 51: Mheshimiwa Naibu Spika, haya ninayo
- Page 52 and 53: ambayo tunaona yanaweza kuleta atha
- Page 54 and 55: kweli waweze kuchambua ili tusije t
- Page 56 and 57: Nikaona hii labda hii Kiswahili cha
- Page 58 and 59: Naomba nichukue nafasi hii kumponge
- Page 60 and 61: kwa sheria ya Bunge hili kwamba Mak
- Page 62 and 63: General Tyre kinaendelea kufanya ka
- Page 64 and 65: Mheshimiwa Naibu Spika, juzi niliku
- Page 66 and 67:
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo na
- Page 68:
Sasa kutokana na hayo mimi nafikiri