19.02.2015 Views

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

23. Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza mabadiliko ya teknolojia za utangazaji kutoka<br />

Analogia kwenda Digitali, hadi sasa kampuni tatu (3) zimepewa leseni ya kutoa huduma<br />

hiyo. Kampuni hizo ni Agape Associates Ltd, Basic Transmission Ltd na StarMedia (T)<br />

Ltd,. Makubaliano ya kuzima mitambo ya Analogia kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki<br />

(EAC) ni mwaka 2012 na kwa Jumuia ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika<br />

(SADC) ni mwaka 2013. Tanzania ni mwanachama kwa Jumuiya zote mbili na hivyo<br />

inapaswa kuzingatia muda uliowekwa wa kufanya mabadiliko hayo.<br />

24. Mheshimiwa Spika, ni muhimu Taifa kufanya mabadiliko haya kutokana na maendeleo<br />

ya kiteknolojia yasiyokwepeka yaliyofikiwa katika sekta ya utangazaji kote Ulimwenguni.<br />

Mabadiliko ya teknolojia ya utangazaji yatalipatia Taifa mafanikio mengi. Miongoni mwa<br />

hayo ni pamoja na:<br />

a) Fursa ya masafa ya ziada katika teknolojia ya digitali ikilinganishwa na ile ya<br />

analogia. Hivyo, kwa masafa yaliyolengwa kwa ajili ya Tanzania Kimataifa,<br />

wawekezaji wengi zaidi wataweza kuhudumiwa kwa masafa yaliyopo; hivyo<br />

kuongeza faida kiuchumi kwa kutoa fursa zaidi kwa wawekezaji na ajira zaidi;<br />

b) Huduma inayotumia teknolojia ya digitali ina ubora wa juu ikilinganishwa na ile ya<br />

analogia. Vile vile, teknolojia ya digitali ni ya kisasa ikilinganishwa na analogia<br />

ambayo inakaribia kufutika, hivyo mabadiliko hayakwepeki,<br />

c) Kurahisishwa zaidi kwa mfumo wa mawasiliano na hivyo kuwawezesha wananchi<br />

wengi zaidi kupata taarifa mbalimbali mahali popote walipo na kwa kutumia vyanzo<br />

vingi zaidi vya habari na mawasiliano kama vile simu za mkononi na kompyuta; na<br />

d) Kutenganishwa kwa shughuli za utayarishaji wa vipindi vya Televisheni na shughuli<br />

za urushaji wa Matangazo hivyo kuongeza utaalamu katika utayarishaji vipindi na<br />

kuongeza nafasi za ajira.<br />

Sayansi na Teknolojia<br />

[8]

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!