19.02.2015 Views

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

G. MAAZIMIO <strong>NA</strong> MWELEKEO <strong>WA</strong> BAJETI K<strong>WA</strong> M<strong>WA</strong>KA <strong>WA</strong> FEDHA<br />

2011/2012<br />

167. Mheshimiwa Spika, Sekta ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia inaazimia kutekeleza<br />

Mpango wa Muda wa Kati na Muda Mrefu ambao umetilia mkazo programu ya kufanya<br />

mabadiliko ya mfumo wa mawasiliano, habari na utangazaji kutoka analogia kwenda<br />

digitali.<br />

168. Mheshimiwa Spika, Wizara itaendelea kusimamia uanzishwaji wa mfumo mpya wa<br />

Anuani za Makazi na Simbo za Posta ambao una lengo la kurahisisha upatikanaji wa<br />

anuani kamili za makazi zinazoonyesha mitaa, majina ya majengo na uwekaji wa namba<br />

za nyumba. Mambo haya kwa pamoja yatawezesha upatikanaji wa anuani ya mwananchi<br />

na mfumo huu wa anuani za makazi na simbo za posta utarahisisha utoaji wa huduma<br />

mbalimbali za kibiashara na kijamii kama vile wakati wa dharura na uokoaji kama zima<br />

moto, magari ya wagonjwa, maji, umeme, mawasiliano, ugawaji misaada, bima,<br />

ukusanyaji wa kodi mbalimbali za Serikali na ushirikishwaji wa wananchi katika shughuli<br />

za maendeleo. Mambo mengine yatakayoweza kufanywa kwa urahisi kupitia utekelezwaji<br />

wa mradi huu ni pamoja na utambuaji wananchi kupitia Wakala wa Vizazi, Vifo na Ufilisi<br />

(RITA), uandikishaji wapiga kura, na utoaji wa vitambulisho vya mkazi kupitia Mamlaka<br />

ya Vitambulisho Tanzania (NIDA).<br />

169. Mheshimiwa Spika, Wizara itaendelea kuimarisha usimamizi wa masuala ya<br />

mawasiliano na haki za watumiaji wa huduma na kuboresha mtandao wa simu za mezani<br />

na viganjani hadi vijijini. Aidha, Wizara itaendelea kukamilisha ujenzi wa Mkongo wa<br />

Taifa wa Mawasiliano (National ICT Broadband Backbone Infrastructure). Pia, Wizara<br />

itaratibu na kusimamia uanzishwaji wa vituo vikuu vya kumbukumbu (Mega Data<br />

Centers) pamoja na kuandaa Sera ya Usalama wa TEHAMA.<br />

[50]

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!