19.02.2015 Views

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

KAMPUNI <strong>YA</strong> SIMU TANZANIA<br />

160. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2011/2012, Kampuni ya Simu Tanzania<br />

inatarajia kuongeza tija na ufanisi wa Kampuni hivyo kuongeza mapato kutoka Sh. bilioni<br />

80 mwaka 2010 hadi Sh. bilioni 113 mwaka 2011. Aidha, Kampuni itaboresha makusanyo<br />

yanayotokana na huduma za simu zilizotolewa kwa wateja wake, ikiwemo Serikali kuu na<br />

taasisi zake. Lengo ni kukusanya angalau asilimia 94 ya mauzo ya kila mwezi husika.<br />

161. Mheshimiwa Spika, Kampuni itaboresha huduma kwa wateja kwa kuweka mitambo<br />

(switches) ya Kisasa inayotumia teknolojia ya Next Generation Network kwa kuondoa<br />

mitambo ya simu ya zamani aina ya NEAX, AXE10, DTS na GX 5000 iliyobakia. Pia,<br />

Kampuni itarekebisha njia za simu zilizoharibika pamoja na kuboresha huduma kwa<br />

wateja ili kukidhi mahitaji halisi ya kibiashara ya simu na data. Aidha, Kampuni<br />

itaendelea kupanua mtandao wa intaneti (Fixed and wireless Broadband) kwenye Makao<br />

Makuu ya Mikoa na miji mikubwa yote Tanzania bara na Visiwani kwa kujenga minara<br />

mipya.<br />

MAMLAKA <strong>YA</strong> MA<strong>WA</strong>SILIANO TANZANIA<br />

162. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2011/2012, Mamlaka ya Mawasiliano<br />

Tanzania itaanzisha rejesta (Central Equipment Identification Register) ili kudhibiti<br />

matumizi mabaya ya simu za viganjani nchini na nchi za Afrika Mashariki.<br />

163. Mheshimiwa Spika, Mamlaka itaendelea kuratibu utekelezaji wa kuhamia katika mfumo<br />

mpya wa utangazaji wa digitali (Migration from Analogue to Digital Broadcasting), kwa<br />

kutoa elimu kwa umma na kwa watoa huduma za utangazaji kwa mujibu wa kanuni na<br />

sheria husika. Pia, Mamlaka itaendelea kuratibu ushiriki wa watoa huduma za<br />

mawasiliano katika ujenzi wa mitambo ya intaneti (Internet Exchange Points) na<br />

kuunganisha mitandao yao kwenye mtambo huo. Aidha, Mamlaka itashirikiana na Umoja<br />

[48]

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!