19.02.2015 Views

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

wanafunzi 3,028 ikiwa ni ongezeko la asilimia 19. Aidha, Taasisi itaendeleza wafanyakazi<br />

15 katika masomo ya juu, wakufunzi 8 na maafisa waendeshaji 7. Pia, Taasisi itaendelea<br />

kuhudumia wafanyakazi 48, wakufunzi 41 na maafisa waendeshaji 7 walioko masomoni.<br />

Vile vile, Taasisi itaendesha masomo ya awali (Pre-entry training) ili kupata wanafunzi<br />

wa kike katika kozi ya ufundi sanifu (30) na uhandisi (25).<br />

137. Mheshimwa Spika, Taasisi itaanza kufundisha kozi mpya za Diploma za Biomedical<br />

Equipment Engineering (35), Communication Systems Engineering (35), Multimedia<br />

Technology (35) na Information Technology (35). Aidha, Taasisi itakamilisha taratibu za<br />

kuidhinishwa na kozi mpya za Diploma za Electronic Equipment Maintenance,<br />

Geographical Information System na Mechatronics. Kozi hizi huidhinishwa na Baraza la<br />

Elimu Tanzania (<strong>NA</strong>CTE).<br />

138. Mheshimiwa Spika, Taasisi itakarabati na kufunga mitambo katika vituo vitatu (3) vya<br />

Habari Jamii vya mradi wa Super Computer vilivyoko Morogoro, Mtwara na Dodoma ili<br />

kukamilisha mradi wa Super Computer. Pia, Taasisi itaendelea kuhudumia kituo cha<br />

TEHAMA (IT Centre of Excellence) kwa kutoa mafunzo ya TEHAMA, kuhamasisha<br />

matumizi ya Super Computer na kutoa huduma za Tiba Mtandao (Tele-medicine). Aidha,<br />

Taasisi itakamilisha awamu ya pili ya ujenzi wa jengo la DIT Teaching Tower kwa ajili ya<br />

madarasa, maabara na ofisi za wafanyakazi.<br />

139. Mheshimiwa Spika, Taasisi itakarabati majengo na miundombinu ya Taasisi ya<br />

Teknolojia ya Ngozi Mwanza ili iweze kutoa mafunzo ya Diploma ya Teknolojia katika<br />

mwaka wa masomo 2011/2012. Aidha, Taasisi itafanya matengenezo ya nyumba 5 za<br />

wafanyakazi wa Taasisi zilizoko Mbezi Kilongawima, Dar es Salaam.<br />

[42]

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!