19.02.2015 Views

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

128. Mheshimiwa Spika, Wizara itaendelea kuhamasisha watumishi kujikinga na kuepuka<br />

maambukizi mapya ya UKIMWI, upimaji wa UKIMWI kwa hiari, matumizi ya dawa za<br />

kurefusha maisha kwa waishio na virusi vya UKIMWI na kupunguza maambukizo ya<br />

UKIMWI kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Aidha, Wizara imeendelea kuhamasisha<br />

watumishi waliopata maambukizi kujitokeza ili waweze kupatiwa huduma kwa mujibu wa<br />

Waraka wa Utumishi wa Serikali Na. 2 wa Mwaka 2006.<br />

129. Mheshimiwa Spika, Wizara itarejea Mpango Mkakati (Strategic Plan) ya mwaka<br />

2008/2009 – 2011/2012 na kusimamia Mpango wa Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya<br />

Chama cha Mapinduzi (CCM) 2010-2015 katika sekta ya mawasiliano, sayansi na<br />

teknolojia. Aidha, itasimamia utekelezaji na ufuatiliaji wa miradi mbalimbali<br />

inayotekelezwa ikiwa ni pamoja na ile iliyoko kwenye taasisi zilizo chini yake.<br />

130. Mheshimiwa Spika, Wizara itaandaa chapisho la takwimu mbalimbali zinazotoa taarifa<br />

ya maendeleo ya sekta ya mawasiliano, sayansi na teknolojia. Pia, Wizara itaratibu na<br />

kuendesha zoezi la kupitia matumizi ya fedha za sekta ya mawasiliano, sayansi na<br />

teknolojia kwa kulingana na majukumu ya Wizara.<br />

131. Mheshimiwa Spika, ili kuendeleza na kuimarisha sekta ya mawasiliano, sayansi na<br />

teknolojia, Wizara itaendelea kuimarisha ushirikiano wa kikanda na kimataifa ili<br />

kuchochea ukuaji wa sekta hizi nchini. Katika kutekeleza jukumu hilo, Wizara<br />

itakamilisha uridhiwaji wa mikataba mbalimbali ya kikanda na kimataifa inayohusu sekta<br />

ya mawasiliano, sayansi na teknolojia.<br />

132. Mheshimiwa Spika, Wizara itaendelea kutoa huduma za malipo kupitia mtandao wa<br />

malipo wa Serikali ambao unasimamiwa na Katibu Mkuu Hazina kupitia Mhasibu Mkuu<br />

wa Serikali kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za usimamizi wa fedha. Aidha,<br />

Wizara itaendelea kutoa taarifa za mwaka za hesabu za Wizara na kwa ajili ya ukaguzi na<br />

tathmini za wadau mbalimbali kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu zilizopo.<br />

[40]

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!