19.02.2015 Views

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

114. Mheshimiwa Spika, changamoto moja kubwa kwenye sekta hii ni shughuli za Utafiti na<br />

Maendeleo (Research and Development – R&D) kutotengewa fedha za kutosha.<br />

Upungufu huu wa fedha umeendelea kuathiri ufanisi wa shughuli za utafiti na maendeleo.<br />

Katika Bajeti ya Mwaka wa fedha wa 2010-2011 zilitengwa Sh. bilioni 30 kwa ajili ya<br />

shughuli za utafiti. Hata hivyo, hadi kufikia tarehe 30 Juni, 2011 Wizara imepokea kiasi<br />

cha Sh. bilioni 19. Ili kukabiliana na changamoto hii, Serikali na Asasi za Utafiti<br />

zimeendelea kutumia njia nyingine kufadhili utafiti ikiwa ni pamoja na kushirikiana na<br />

mashirika ya nje na sekta binafsi kuchangia shughuli za utafiti. Aidha, Sera ya Taifa ya<br />

Utafiti na Maendeleo iliyoanza kutumika inabainisha vivutio kwa sekta binafsi kwenye<br />

utafiti ikiwa ni pamoja na Sekta hiyo kuthamini na kutumia matokeo ya utafiti.<br />

115. Mheshimiwa Spika, uhaba wa wataalam katika nyanja mbalimbali umeathiri mafanikio<br />

ya sekta. Aidha, changamoto kubwa katika eneo hili ni pamoja na kuwa na idadi ndogo ya<br />

wataalam wa TEHAMA ikilinganishwa na mahitaji, wataalam wengi watafiti kuwa wa<br />

umri mkubwa, wataalam kutokuwa na uelewa wa teknolojia mpya, na uwiano baina ya<br />

wataalam mbalimbali (kama vile uwiano wa wahandisi na mafundi wa ngazi ya cheti na<br />

diploma) kutokuwa mzuri. Wizara, kupitia Sera ya Utafiti na Maendeleo inaandaa<br />

mikakati ya muda mfupi na mrefu ili kupata ufumbuzi wa kudumu kukabiliana na<br />

changamoto hii.<br />

116. Mheshimiwa Spika, Taasisi zinazohudumia Sekta ya Mawasiliano, Sayansi na<br />

Teknolojia ziko katika hatua ya kujijenga ama katika hatua za kuanzishwa (kama vile<br />

Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Taasisi ya Nelson Mandela na Taaluma za Ngozi cha<br />

Mwanza), au kuwa katika hatua ya kujipanua kukidhi mahitaji ya soko kama ilivyo kwa<br />

MIST na DIT ambazo zinaongeza michepuo na udahili na hivyo kuwa na mahitaji ya<br />

miundombinu mipya na kuongezewa bajeti zao. Aidha, bado lipo hitaji la kuzijenga taasisi<br />

hizi kuwa imara na kujenga nyingine ili kuharakisha maendeleo ya sayansi na teknolojia<br />

nchini. Kama ilivyo kwa shughuli za utafiti, njia ambayo Wizara imeendelea kutumia<br />

kukabiliana na changamoto hii ni pamoja na kubuni njia mbadala za kupata fedha ikiwa ni<br />

[36]

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!