19.02.2015 Views

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

(1); leseni ya utangazaji (Content Services) leseni 13; leseni ya usafirishaji wa vifurushi<br />

katika miji ndani ya nchi (Intercity Courier) leseni mbili (2); leseni ya ufungaji na<br />

matengenezo ya vifaa vya mawasiliano (Installation and Maintenance) leseni 21; leseni ya<br />

uagizaji na usambazaji wa vifaa vya mawasiliano (Importation and Distribution) leseni<br />

15; na leseni ya huduma za satelaiti (V-SAT licences) leseni 14.<br />

108. Mheshimiwa Spika, Mamlaka imeendelea kuelimisha watumiaji wa huduma za<br />

mawasiliano kuhusu taratibu za kuwasilisha malalamiko yao kwa mamlaka pale ambapo<br />

hawakuridhika na huduma. Katika kutekeleza azma hii, jumla ya vipindi 18 vya<br />

televisheni na 26 vya radio vimerushwa hewani. Aidha, Mamlaka imeendesha semina za<br />

kuelimisha watumiaji wa huduma za mawasiliano katika wilaya 14 (Rufiji, Kisarawe,<br />

Mkuranga, Kibaha, Bagamoyo, Namtumbo, Songea Mjini, Songea vijijini, Nyassa,<br />

Lushoto, Mbinga, Karatu, Kiteto na Lushoto); Vyuo 5 (Ukutubi Bagamoyo, Maendeleo<br />

ya Wananchi Kisarawe, Maendeleo ya Wananchi Rufiji, VETA Songea na TEHAMA<br />

Ruhuwiko) na Shule za Sekondari 4 za Makita (Namtumbo), Pamoja - Namtumbo,<br />

Namabengo na Sekondari ya Wavulana Songea).<br />

Vile vile, Mamlaka imetoa vipeperushi na machapisho mbalimbali yenye kuelimisha<br />

watumiaji. Kutokana na uelimishaji huu na milango kuwa wazi, Mamlaka imepokea na<br />

kuyashughulikia kikamilifu malalamiko 79 na kuyatolea maamuzi. Kati ya hayo,<br />

malalamiko matatu (3) yamekatiwa rufaa.<br />

109. Mheshimiwa Spika, Mamlaka inaendelea kusimamia mradi wa anuani mpya za makazi<br />

na simbo za posta (Postcode Project) ambao umeanza kutekelezwa katika Manispaa ya<br />

Arusha na Dodoma. Utekelezaji huu pia umehusisha utoaji wa mafunzo ya kutekeleza<br />

mradi huu yaliyofanyika katika Majiji, Manispaa na Halmashauri za Mwanza, Tanga,<br />

Arusha, Dodoma, Moshi, Morogoro, Kigoma Ujiji, Lindi, Ukerewe na Tandahimba.<br />

Utoaji wa mafunzo hayo na uhamasishaji umefanyika pia Zanzibar. Mafunzo haya<br />

yalilenga kuwezesha Mamlaka za Serikali za Mitaa kutekeleza Mradi huu kupitia bajeti<br />

[34]

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!