19.02.2015 Views

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

93. Mheshimiwa Spika, Tume ikishirikiana na Benki ya Dunia, kupitia mradi wa Info Dev,<br />

imeanzisha Atamizi ya TEHAMA (ICT Incubator) kwa ajili ya kukuza ujasiriamali katika<br />

Teknolojia ya Habari na Mawasiliano. Atamizi hii itatoa ushauri wa teknolojia, mafunzo<br />

ya biashara kwa wajasiriamali wanaokusudia kuanzisha kampuni za biashara ya<br />

TEHAMA ili waweze kujiajri wenyewe na pia wale wenye kampuni hizo kuweza<br />

kuongeza ufanisi na kupata teknolojia mpya.<br />

94. Mheshimiwa Spika, Tume kwa kushirikiana na Shirika la Misaada la Sweden imeanza<br />

kuratibu shughuli za Kongano (Clusters) 19 katika mikoa 12. Kongano zinazoratibiwa<br />

kwa utaratibu huu, zinajishughulisha na mambo ya uhandisi, usindikaji wa mazao na<br />

matunda, utalii, uchimbaji wa madini chini ya wachimbaji wadogo wadogo, kilimo cha<br />

mwani, uyoga, mihogo na wabunifu wa sanaa za mikono.Kongano zinawezesha<br />

wataalamu (wa vyuo vikuu na vituo vya utafiti) kufanya kazi karibu na wajasiriamali<br />

katika kutoa mafunzo na katika upatikanaji wa teknolojia zinazoongeza ufanisi na<br />

uzalishaji wa wajasiriamali walio kwenye kongano hizo.<br />

TUME <strong>YA</strong> NGUVU ZA ATOMIKI<br />

95. Mheshimiwa Spika, Tume ya Nguvu za Atomiki (TAEC) katika kutekeleza moja ya<br />

jukumu lake kuu, ilipima jumla ya sampuli 19,921 za vyakula na mbolea ambapo hakuna<br />

sampuli iliyoonekana kuwa na kiwango kikubwa cha mionzi. Vile vile, kaguzi 39<br />

zilifanywa bandarini, mipakani na kwenye viwanja vya ndege katika sehemu za<br />

kuingia/kutoka (entry/exit points) nchini ili kuhakikisha kuwa waingizaji wote wa bidhaa<br />

za vyakula wanazingatia sheria na kanuni za kinga ya mionzi. Aidha, Upimaji wa mionzi<br />

(personal Dosimetry) ulifanywa kwa wafanyakazi 1,032 ambao ni sawa na asilimia 86 ya<br />

wafanyakazi waliolengwa kupimwa katika vituo 119 vilivyokaguliwa. Pia, mabaki 45 ya<br />

vyanzo vya mionzi yamekusanywa kwa kipindi cha miaka mitano kati ya 2005 na 2010 na<br />

kufanya jumla ya mabaki yote yaliyokusanywa na kuhifadhiwa na Tume kufikia 70.<br />

Katika mwaka wa fedha 2010/2011, chanzo kimoja kilikusanywa kutoka Dodoma.<br />

[30]

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!