19.02.2015 Views

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

kuongeza msongo wa umeme kutoka 11 kV na kuwa 33 kV kukidhi mahitaji ya Taasisi<br />

inashughulikiwa na TANESCO.<br />

TUME <strong>YA</strong> TAIFA <strong>YA</strong> SA<strong>YA</strong>NSI <strong>NA</strong> TEKNOLOJIA<br />

86. Mheshimiwa Spika, Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), ikishirikiana<br />

na wadau wa utafiti ilibainisha maeneo matano (5) ya kipaumbele ya fedha za utafiti ili<br />

kuendeleza mikakati ya Kilimo Kwanza kama ifuatavyo: (a) Utafiti utakaosaidia kupata<br />

njia bora ya kuhamasisha matumizi ya pembejeo za kilimo kwa watu wengi zaidi, (b)<br />

Utafiti utakaosaidia kuongeza thamani ya mazao ya Kilimo, (c) Utafiti wa kupata taarifa<br />

juu ya mnyororo wa thamani (value chain) wa mazao ya kilimo, (d) Kuhawilisha<br />

teknolojia zilizofanyiwa utafiti ili ziweze kutumika na watu wengi zaidi na (e) Tafiti<br />

zitakazosaidia kujua ubora wa teknolojia.<br />

87. Mheshimiwa Spika, Tume ilikaribisha mapendekezo ya tafiti ya awali (research concept<br />

notes) katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi kutoka katika Taasisi na Vyuo Vikuu<br />

nchini. Kupitia mwito huo, Concept Notes 360 zilipokelewa na baada ya kuchambuliwa<br />

na wataalamu, 106 zilipitishwa kwa ajili ya kutengeneza maandiko kamili ya tafiti (Full<br />

Proposals). Mchakato wa kupitia maandiko ya tafiti hizi umekamilika na kuingia hatua ya<br />

kuchagua tafiti zilizo bora kwa ajili ya kupatiwa mwega. Matokeo ya mchakato huu<br />

yatatangazwa kwa wanasayansi na watafiti kwenye vyombo vya habari hivi karibuni ili<br />

shughuli za utafiti ziweze kuanza.<br />

88. Mheshimiwa Spika, Tume imetengeneza Mwongozo wa Kutoa Mwega (Grants Manual)<br />

na kuusambaza kwenye taasisi za utafiti, vyuo vikuu na wadau wengine. Pia, Tume<br />

imenunua programu ya kompyuta ili kuimarisha mfumo wa kupokea maombi kupitia<br />

mtandao wa kompyuta (internet). Aidha, Tume imeingiza kwenye Daftari la Hati Miliki<br />

aina ishirini (20) za mazao mbalimbali yalizozalishwa na taasisi za utafiti wa kilimo na<br />

[28]

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!