19.02.2015 Views

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

kurefusha maisha kwa waishio na virusi vya UKIMWI na kupunguza maambukizi ya<br />

UKIMWI kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. Aidha, Wizara imeendelea kuelimisha<br />

watumishi ili wale waliopata maambukizi waweze kujitokeza na kupatiwa huduma kwa<br />

mujibu wa Waraka wa Utumishi wa Serikali Na. 2 wa mwaka 2006.<br />

71. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuratibu na kufanya ukaguzi wa matumizi ya<br />

fedha za Wizara na Taasisi zilizo chini yake kwa lengo la kuongeza ufanisi wa utendaji<br />

kazi na kuwa na matokeo mazuri na yenye tija kwa Taifa. Aidha, Wizara imeendelea<br />

kushirikiana na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika masuala yote yanayohitaji<br />

ushauri wa kisheria ikijumuisha masuala ya mikataba, miswada, sheria ndogo ndogo,<br />

kanuni na mashauri mbalimbali yanayohusu Wizara au Taasisi zake. Vile vile, Wizara<br />

imeandaa taarifa ya mashauri yanayohusu Wizara au Taasisi zilizo chini ya Wizara kwa<br />

lengo la kuzifuatilia kwa karibu.<br />

72. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuelimisha umma na wadau mbalimbali kuhusu<br />

utekelezaji wa majukumu ya Wizara, ambapo nakala 5,000 za vipeperushi kuhusu sera za<br />

Wizara, Ujenzi wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano, Ujenzi wa Taasisi ya Sayansi na<br />

Teknolojia ya Nelson Mandela-Arusha, uanzishwaji wa Mfuko wa Mawasiliano kwa<br />

Wote, Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania, Vituo vya Mawasiliano pamoja na elimu<br />

kuhusu Dira, Dhima na Majukumu ya Wizara vimeandaliwa na kusambazwa kwa wadau<br />

mbalimbali.<br />

73. Mheshimiwa Spika, katika kuwapata wazabuni wa kutoa huduma mbalimbali kwa<br />

mujibu wa Sheria ya Ununuzi namba 21 ya mwaka 2004 kifungu namba 35, shughuli zote<br />

za Ununuzi na Ugavi zimesimamiwa kwa kushirikiana na Wakala wa Ununuzi na Ugavi<br />

wa Serikali (GPSA). Aidha, Ununuzi wa bidhaa na huduma umezingatia taratibu hizo.<br />

TAASISI <strong>YA</strong> TEKNOLOJIA DAR ES SALAAM<br />

[24]

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!