19.02.2015 Views

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

57. Mheshimiwa Spika, Wizara inaendelea kuhamasisha uanzishwaji na utumiaji endelevu<br />

wa vituo hivi ili viwe chachu ya kuwaendeleza wananchi kiuchumi, kielimu na katika<br />

upatikanaji wa huduma nyingine za maendeleo. Aidha, rasimu ya mwongozo wa<br />

uanzishaji na uendeshaji wa vituo hivi imeandaliwa. Mwongozo huu unalenga kuvifanya<br />

vituo hivi kuwa vituo vya taarifa mbalimbali zikiwemo za elimu, kilimo, afya na serikali<br />

na hivyo kuvifanya viwe gurudumu la kuchochea kasi ya maendeleo ya kijamii, kiuchumi<br />

na kiutawala. Ili kufanikisha mkakati huu, vituo hivi 10 vya mfano vimepangwa<br />

kujengwa katika maeneo mbalimbali ili viweze kutumika kwa kuigwa katika maeneo<br />

mengine.<br />

58. Mheshimiwa Spika, Mfumo wa Anuani za Makazi na Simbo za Posta ni moja ya<br />

utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Posta ya mwaka 2003. Kukamilika kwa mradi huu<br />

kutafanya kila mwanachi, biashara, kampuni na taasisi itambulike kulingana na jengo na<br />

eneo ilipo. Mfumo huu utarahisisha ufikishaji wa huduma na utendaji wa shughuli<br />

mbalimbali za kijamii, kiuchumi na kiusalama ikiwa ni pamoja na zoezi zima la utoaji wa<br />

vitambulisho vya Taifa. Utekelezaji wa mradi huu chini ya uratibu wa Mamlaka ya<br />

Mawasiliano Tanzania ulianza kwa majaribio katika Kata 7 za Manispaa ya Arusha<br />

(Kaloleni, Kati, Sekei, Lovolosi, Orelioni, Unga Limited na Themi) na kuendelea katika<br />

Kata 7 za Manispaa ya Dodoma (Kiwanja cha Ndege, Uhuru, Makole, Viwandani,<br />

Uhindini, Tambukareli na Kilimani).<br />

59. Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI<br />

inawasiliana na wadau mbalimbali ili kuwezesha upatikanaji wa fedha kwa ajili ya<br />

utekelezaji wa mradi huu nchini. Aidha, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania inaendelea<br />

kutoa mafunzo kuhusu mfumo huu mpya wa anuani kwa watendaji wa Serikali za Mitaa<br />

na wadau mbalimbali kwa ajili ya kuutekeleza mradi huu kitaifa.<br />

60. Mheshimiwa Spika, Wizara kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania inasimamia<br />

Sheria na Kanuni mbalimbali za Mawasiliano ili kuhakikisha kuwa watumiaji wa huduma<br />

[20]

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!