19.02.2015 Views

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

43. Mheshimiwa Spika, kupitia ushirikishwaji wa Sekta Binafsi katika kutoa huduma za<br />

TEHAMA, Kampuni za Simu za mkononi za Airtel, Tigo na Zantel zimeanzisha umoja<br />

(Consortium of Operators) kwa nia ya kujenga miundombinu ya TEHAMA yenye uwezo<br />

mkubwa wa Kimawasiliano (Broadband) katika maeneo ya miji (Metro Networks) ili<br />

kufikisha huduma za Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano kwa watumiaji wa mwisho (Last<br />

Mile Connectivity). Kampuni hizo zitaanza kujenga miundombinu hiyo katika miji ya Dar<br />

es Salaam, Arusha, Mwanza na Dodoma.<br />

44. Mheshimiwa Spika, katika kuongeza matumizi ya Mkongo na miundombinu mingine ya<br />

mawasiliano, Serikali imeamua kuunda Tume ya Kuendeleza TEHAMA. Andiko la<br />

kuanzisha chombo hiki lipo katika hatua za kufanyiwa maamuzi na Serikali baada ya<br />

kupata maoni kutoka kwa wadau wa sekta ya teknolojia ya habari na mawasiliano.<br />

Shirika la Posta Tanzania (TPC)<br />

45. Mheshimiwa Spika, Shirika linaendesha ofisi 253 zinazotoa huduma kamili za Posta<br />

ikiwa ni pamoja na utumaji na ulipaji wa fedha na shughuli za uwakala kwa niaba ya<br />

taasisi nyingine. Aidha, ofisi 145 kati ya hizo zinatoa huduma ya usafirishaji wa nyaraka,<br />

vifurushi na vipeto vya haraka ndani na nje ya nchi (EMS courier). Pia, huduma za<br />

intaneti zinatolewa katika ofisi 26 za posta nchini ikilinganishwa na kituo kimoja (1)<br />

kilichokuwepo mwaka 2000. Vile vile Shirika limeanzisha huduma mpya ya kusambaza<br />

kwa haraka nyaraka, vifurushi na vipeto kwa Ofisi za Serikali, Kampuni binafsi na taasisi<br />

kupitia huduma inayoitwa City Urgent Mail.<br />

46. Mheshimiwa Spika, Vituo vya Posta 104 vinavyotoa huduma za kawaida za Posta<br />

vinaendeshwa na wakala katika juhudi za kushirikisha sekta binafsi katika kutoa huduma<br />

za posta. Aidha, vibali 2,878 vimetolewa kwa wafanyabiashara kuwa wakala wa Shirika<br />

katika kuuza stempu na shajala za posta.<br />

[16]

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!