19.02.2015 Views

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

HOTUBA YA WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA ...

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

32. Mheshimiwa Spika, ili kuimarisha Tume ya Sayansi na Teknolojia, Serikali imeanza<br />

mchakato wa kutunga sheria itakayosimamia masuala yote ya sayansi, teknolojia na<br />

ubunifu nchini (Science, Technology and Innovation Act). Kupitia mchakato huu, Sheria<br />

Na. 7 ya mwaka 1986 iliyounda Tume ya Sayansi na Teknolojia itarejewa ili kuhakikisha<br />

majukumu ya Tume yanakidhi mahitaji ya sasa ya sayansi, teknolojia na ubunifu ndani ya<br />

mfumo wa kisheria.<br />

Kuishirikisha sekta binafsi katika kuchangia maendeleo na matumizi ya sayansi na<br />

teknolojia kwenye uzalishaji mali na utoaji wa huduma<br />

33. Mheshimiwa Spika, kulingana na Sera ya Ushirikishwaji wa Sekta Binafsi, Wizara<br />

imeandaa na kuainisha maeneo ya sayansi na teknolojia ambayo sekta binafsi inaweza<br />

kuwekeza. Maeneo hayo ni pamoja na eneo la usindikaji mazao ya kilimo na uzalishaji wa<br />

bidhaa za bayoteknolojia. Aidha, mfumo mpya wa sayansi, teknolojia na ubunifu<br />

unaoandaliwa utawezesha uanzishwaji wa taasisi za utafiti zisizo za serikali katika sekta<br />

mbalimbali za sayansi na teknolojia kama ilivyo kwenye mazao ya chai na kahawa,<br />

ambapo taasisi za jinsi hii zimeonyesha kuwa na manufaa makubwa kwa wananchi.<br />

Kuandaa programu mahsusi ya wataalamu wa kada mbalimbali kama vile uhandisi,<br />

uganga wa binadamu na wanyama, madini, jiolojia na kilimo n.k. watakaojaza nafasi<br />

ambazo ni muhimu na za lazima katika kuyafikia malengo hayo ya dira<br />

34. Mheshimiwa Spika, ili kukabiliana na uhaba wa wataalam katika fani mbalimbali za<br />

sayansi nchini, Serikali imeendelea kupanua taasisi zinazotoa mafunzo katika fani<br />

mbalimbali za sayansi na teknolojia na kuanzisha taasisi mpya ikiwemo Taasisi ya<br />

Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Arusha ambayo imeanzishwa mahsusi ili<br />

kupambana na uhaba wa wataalam katika fani za sayansi na teknolojia. Taasisi ya<br />

Teknolojia Dar es Salaam (DIT) na Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Mbeya (MIST)<br />

zimeendelea kuongeza udahili wa wanafunzi, uanzishwaji wa programu mpya na kupanua<br />

zilizopo katika taaluma za uhandisi TEHAMA, Mazingira na nyinginezo. Aidha, Wizara<br />

[12]

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!