19.02.2015 Views

MAELEZO MAFUPI YA MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO MHE ...

MAELEZO MAFUPI YA MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO MHE ...

MAELEZO MAFUPI YA MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO MHE ...

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

<strong>MAELEZO</strong> <strong>MAFUPI</strong> <strong>YA</strong> <strong>MKUU</strong> <strong>WA</strong> <strong>MKOA</strong> <strong>WA</strong> <strong>KILIMANJARO</strong><br />

<strong>MHE</strong>: MOHAMMED A. BABU K<strong>WA</strong> <strong>MHE</strong>: <strong>WA</strong>ZIRI <strong>MKUU</strong> KWENYE<br />

UZINDUZI <strong>WA</strong> TOVUTI <strong>YA</strong> OFISI <strong>YA</strong> <strong>MKUU</strong> <strong>WA</strong> <strong>MKOA</strong> <strong>WA</strong><br />

<strong>KILIMANJARO</strong> – TAREHE 19 FEBRUARI 2009:<br />

• Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda (Mb) - Waziri Mkuu wa<br />

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,<br />

• Mhe. Katibu Tawala wa Mkoa Kilimanjaro,<br />

• Wahe. Wakuu wa Wilaya,<br />

• Mhe. Mstahiki Meya Manispaa ya Moshi,<br />

• Wenyeviti wa Halmashauri za Wilaya,<br />

• Wakurugenzi Watendaji, Halmashauri za Wilaya na<br />

Manispaa,<br />

• Makatibu Tawala wasaidizi Sekretarieti ya Mkoa,<br />

• Wataalam na washauri wa Sekretarieti ya Mkoa,<br />

• Wageni waalikwa,<br />

• Mabibi na Mabwana.<br />

Awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia<br />

sote kuona mwaka huu wa 2009. Napenda kukukaribisha sana katika<br />

Makao Makuu ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro kutuzindulia<br />

TOVUTI ya mkoa na kuongea na watumishi.<br />

Mhe. Waziri Mkuu, Mkoa wa Kilimanjaro kwa ushirikiano na Wizara<br />

yako, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa<br />

tumekuwa katika mchakato wa kuweka mfumo wa habari na<br />

mawasiliano (TEKNOHAMA) katika ngazi ya mkoa na halmashauri za<br />

wilaya kwa lengo la kutekeleza azma ya kuwa na serikali mtandao (e-<br />

1


government). Kuimarika kwa matumizi haya ya (TEKNOHAMA)<br />

kutasaidia sana kurahisisha utendaji kazi na kuongeza ufanisi katika<br />

shughuli mbalimbali za kila siku ndani ya serikali, mkoa, halmashauri<br />

za wilaya na wadau wengine.<br />

Ili kukuza serikali-mtandao, mkoa umejiwekea malengo yafuatayo ya<br />

utekelezaji;-<br />

i) Utengenezaji na uboreshaji wa miundombinu ya mawasiliano<br />

na vitendea kazi;<br />

ii) Kuboresha na kuhimiza matumizi ya mifumo ya kompyuta<br />

iliyopo pamoja na kutengeneza mifumo mingine kwa ajili ya<br />

kurahisha kazi. Hii inakwenda sambamba na utoaji wa<br />

mafunzo ya kompyuta kwa watumiaji wa mifumo katika ngazi<br />

ya mkoa na halmashauri;<br />

iii) Kufanya mawasiliano kwa kutumia mtandao;<br />

iv) Kutuma na kupokea habari kwa kupitia mtandao.<br />

Mhe. Waziri Mkuu, nafurahi kukujulisha kuwa hivi sasa mkoa<br />

umefanikiwa kuwa na chumba cha darasa kwa ajili ya kutolea mafunzo<br />

mbalimbali ya kompyuta na mifumo tuliyonayo, na tayari Wilaya ya<br />

Moshi imeanza kupata mafunzo hayo. Mafunzo kwa wataalamu wa<br />

sekretarieti ya mkoa na halmashauri zilizobaki yatafanyika baadaye.<br />

Pia mkoa umefanikiwa kuboresha mitandao ya mawasiliano ya sauti<br />

na data katika jengo la Mkuu wa Mkoa na kusimika mifumo mbalimbali<br />

ya kurahisisha utendaji kazi wa ofisi. Gharama ya uanzishaji ni<br />

shs.65,000,000/=.<br />

2


Tovuti ya Mkoa wa Kilimanjaro inapatikana kwa anwani ya<br />

www.kilimanjaro.go.tz. Anuani za tovuti za mikoa mingine ni<br />

katika muundo huo na kwa jina la mkoa husika.<br />

Katika TOVUTI ya mkoa wa Kilimanjaro taarifa mbalimbali za kisiasa,<br />

kiuchumi na kijamii zinazohusu mkoa zitakuwa zinapatikana.<br />

Taarifa hizi zinawezesha wadau ndani na nje ya Tanzania kupata<br />

taarifa za mkoa na halmashauri ambazo ni muhimu sana katika<br />

kupanga na kutoa maamuzi, kuhusiana na mipango ya maendeleo.<br />

Mhe. Waziri Mkuu, uzinduzi wa TOVUTI hii unatupa changamoto ya<br />

kuhakikisha kuwa teknolojia hii inawafikia wananchi wa kawaida .<br />

Changamoto hizo ni pamoja na kutokamilika kwa mfumo wa kujenga<br />

serikali mtandao (e-overment) katika halmashauri zote. Ninatoa wito<br />

kwa kila halmashauri kuharakisha ufungaji, uboreshaji na utumiaji wa<br />

teknolojia hizi kwa lengo la kuharakisha maendeleo kwa mkoa wetu<br />

wa Kilimanjaro.<br />

Mhe. Waziri Mkuu, baada ya maelezo hayo mafupi ya utangulizi, kwa<br />

heshima na taadhima kubwa ninakuomba sasa utuzindulie TOVUTI<br />

yetu ya mkoa yenye anwani www.kilimanjaro.go.tz na kuongea<br />

na watumishi wa Sekretarieti ya mkoa na halmashauri.<br />

KARIBU SANA.<br />

3

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!