19.02.2015 Views

i MIAKA 50 YA UHURU MKOA WA KILIMANJARO UJUMBE WA ...

i MIAKA 50 YA UHURU MKOA WA KILIMANJARO UJUMBE WA ...

i MIAKA 50 YA UHURU MKOA WA KILIMANJARO UJUMBE WA ...

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

<strong>MIAKA</strong> <strong>50</strong> <strong>YA</strong> <strong>UHURU</strong> <strong>MKOA</strong> <strong>WA</strong> <strong>KILIMANJARO</strong><br />

<strong>UJUMBE</strong> <strong>WA</strong> MKUU <strong>WA</strong> <strong>MKOA</strong><br />

Mhe. Meja Jenerali (Mst.) Said S. Kalembo<br />

Mkoa wa Kilimanjaro ni kati ya mikoa 21 ya Tanzania Bara, ambao ulioanzishwa<br />

rasmi kwa Tangazo la Serikali Na.4<strong>50</strong> la mwaka 1963 ukiwa na Wilaya za<br />

Kilimanjaro na Pare. Kabla ya hapo eneo hilo linaloitwa Mkoa wa Kilimanjaro<br />

lilikuwa sehemu ya Jimbo la Kaskazini (Northern Province) lililokuwa linaundwa<br />

pia na wilaya za Arusha na Mbulu; wakati wilaya ya Pare ilikuwa sehemu ya<br />

Jimbo la Tanga (Tanga Province). Wakati nchi yetu inapata Uhuru tarehe<br />

09.12.1961 Mkuu wa Jimbo la Kaskazini (Provisional Commissioner) alikuwa<br />

Mheshimiwa PC Edward Barongo ambaye alitawala hadi 1963, na alipokelewa na<br />

Mheshimiwa Peter Kisumo, Mkuu wa Mkoa wa kwanza wa Mkoa wa Kilimanjaro.<br />

Kwa mantiki hiyo Mkoa umetimiza miaka 38 tangu kuanzishwa kwake ukiwa<br />

umeongozwa na Wakuu wa Mkoa 18 hadi hivi sasa.<br />

Mkoa wa Kilimanjaro una eneo dogo la utawala lenye kilomita za mraba 13,209,<br />

lakini ukiwa na msongamano mkubwa wa watu, vivutio vingi vya utalii mojawapo<br />

ukiwa mlima Kilimanjaro, wasomi wengi, miundombinu mizuri na ya uhakika,<br />

wachapa kazi ambao wanajituma katika kazi za kitaalamu na ujasiriamali, vyote<br />

hivi vikiwa ni vichocheo vikubwa vya maendeleo yake.<br />

i


Napenda kuwapongeza viongozi wakuu wa mkoa huu 18 waliotangulia hadi<br />

kufikia mwaka huu 2011; kwani ndio walioweka misingi bora na imara ya<br />

maendeleo yaliyofikiwa hivi sasa, kama inavyoonyeshwa kwenye mafanikio kwa<br />

kila sekta katika taarifa ya mkoa.<br />

Shukrani za dhati kwa serikali katika jitihada zake za kufikisha huduma na<br />

maendeleo kwa wananchi wa mkoa huu kupitia ngazi mbali mbali za kiutawala<br />

kuanzia ngazi ya Mtaa/Kitongoji, Kijiji, Kata na Halmashauri/Wilaya.<br />

Mkoa wa Kilimanjaro una fursa nyingi za kimaendeleo ambazo zinawezesha<br />

uwekezaji unaotokana mazingira mazuri yaliyopo sasa hivi kama vile:-<br />

(i) Miundombinu ya kuaminika na mawasiliano kama vile mtandao<br />

mzuri wa barabara za lami na changarawe zinazopitika kwa vipindi<br />

vyote vya mwaka;<br />

(ii) Njia za mawasiliano ya Simu, Viwanja vya Ndege kikiwepo kiwanja<br />

cha Kimataifa KIA na viwanja vidogo vya Moshi Mjini na kile cha<br />

Utalii Same na njia ya Reli ya Moshi - Arusha – Dar es Salaam;<br />

(iii) Upatikanaji wa kuridhisha wa huduma za tiba, maji, umeme na<br />

elimu;<br />

(iv) Upatikanaji wa huduma na vivutio vya utalii kama vile Mlima<br />

Kilimanjaro, Hifadhi za Wanyamapori za Kilimanjaro na Mkomazi,<br />

misitu ya asili, mazingira yanayovutia tamaduni za asili na<br />

mapango ya kale;<br />

(v) Uwepo wa vyombo vya kifedha kukidhi haja kama vile benki 13,<br />

SACCOS 217, mifuko ya hifadhi ya jamii na asasi nyingine ndogo<br />

ndogo za fedha kama vile vikoba;<br />

(vi) Ulinzi na usalama wa kuridhisha.<br />

ii


Nina uhakika tukiweza kuimarisha mazingira haya mazuri ya uwekezaji na<br />

kuboresha miundombinu iliyopo sasa, Mkoa unayo nafasi nzuri ya kupiga<br />

hatua kubwa zaidi ya kimaendeleo katika miaka <strong>50</strong> ijayo. Hii ikiwa ni<br />

pamoja na kutumia ardhi ndogo tuliyo nayo kikamilifu kwa kujenga majengo<br />

kwa kwenda juu (vertical expansion) badala ya ujenzi wa kusambaa<br />

(horizontal development);<br />

Mafanikio haya yamepatikana kutokana na ushirikiano na mshikamano kati<br />

ya viongozi mbali mbali wakiwemo viongozi wa serikali, chama, dini na<br />

wananchi wa mkoa wetu wa Kilimanjaro. Tutaendelea kuwategemea kwa<br />

miaka <strong>50</strong> ijayo Inshaalah Mwenyenzi Mungu akitujalia.<br />

“TUMETHUBUTU, TUMEWEZA, TUNAZIDI KUSONGA MBELE”<br />

Said S. Kalembo<br />

Meja Jenerali (Mst)<br />

Kaimu MKUU <strong>WA</strong> <strong>MKOA</strong><br />

<strong>KILIMANJARO</strong><br />

iii


NENO LA SHUKRANI KUTOKA K<strong>WA</strong><br />

KATIBU TA<strong>WA</strong>LA <strong>MKOA</strong> <strong>KILIMANJARO</strong><br />

Taarifa hii ya mafanikio ya Miaka <strong>50</strong> (Jubilee) ya Uhuru ya Mkoa wa<br />

Kilimanjaro imetayarishwa/andaliwa na kamati maalum ya wataalam kutoka<br />

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Ofisi za Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa<br />

Halmashauri za Mkoa wa Kilimanjaro. Licha ya kuandaa taarifa hii, kamati<br />

imejihusisha kikamilifu na maandalizi ya maadhimisho ya miaka <strong>50</strong> ya Uhuru<br />

wa Tanzania Bara ambapo mkoa wa Kilimanjaro umepangiwa tarehe 21/8 –<br />

24/8/2011. Kazi hii imefanyika katika mazingira ya kujituma na kujitolea<br />

kwa hali ya juu na hivyo sina budi kuwashukuru wote kwa bidii na moyo<br />

wao wa kujituma ambao kwa pamoja umewezesha kukamilika kwa taarifa<br />

hizi na maadhimisho katika mkoa wetu na wilaya zake zote sita.<br />

Napenda kuunga mkono ujumbe wa Mkuu wa Mkoa, katika maadhimisho<br />

haya kwamba japo mkoa wa Kilimanjaro una eneo dogo la ardhi, mkoa una<br />

fursa nyingi za kuwezesha kuinua hali ya uchumi kwa wakazi wake. Fursa<br />

hizo ni pamoja na mlima Kilimanjaro, barabara zinazopitika wakati wote wa<br />

mwaka, hifadhi za wanyama na miundombinu ya kutolea elimu kuanzia<br />

elimu ya awali hadi chuo kikuu. Uwezo wa wakazi wake kielimu pamoja na<br />

miundombinu iliyowekezwa katika eneo hili dogo tangu kupatikana kwa<br />

Uhuru, fursa na rasilimali muhimu sana katika kupiga hatua ya kimaendeleo<br />

kwa kuwekeza zaidi katika ardhi ndogo iliyoko ili iweze kuzalisha zaidi<br />

(intensive agriculture), kuwekeza zaidi katika viwanda kwani hakuna<br />

uwezekano wa kupanua ardhi iliyoko kwa kilimo na mwisho kuwekeza zaidi<br />

katika elimu na kuufanya mkoa kuwa “centre for excelency” katika Elimu.<br />

Yote haya yatawezekana endapo kila mwananchi atatimiza wajibu wake<br />

pale alipo kwa kutumia fursa na rasilimali zilizopo.<br />

iv


Napenda kuzishukuru Taasisi za Dini Mkoani Kilimanjaro na wananchi kwa<br />

ujumla kwa michango mikubwa waliyotoa na wanayoendelea kutoa katika<br />

maendeleo ya mkoa wa Kilimanjaro hususan katika huduma za kijamii.<br />

Mafanikio na changamoto zilizojitokeza katika miaka hii <strong>50</strong> ya Uhuru wa<br />

Tanzania Bara katika mkoa wetu ziwe ni chachu ya kutafuta maendeleo<br />

zaidi katika miaka <strong>50</strong> ijayo katika mkoa wetu wa Kilimanjaro.<br />

“TUMETHUBUTU, TUMEWEZA NA TUNAZIDI KUSONGA MBELE”<br />

Hassan M. Bendeyeko<br />

KAIMU KATIBU TA<strong>WA</strong>LA <strong>WA</strong> <strong>MKOA</strong><br />

<strong>KILIMANJARO</strong><br />

v

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!