Elimu bora bila mafunzo endelevu kwa walimu.pdf - HakiElimu
Elimu bora bila mafunzo endelevu kwa walimu.pdf - HakiElimu
Elimu bora bila mafunzo endelevu kwa walimu.pdf - HakiElimu
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
ELIMU BORA<br />
Bila Mafunzo Endelevu<br />
<strong>kwa</strong> Walimu Kazini?
Mwandishi wa hadithi:<br />
Richard Mziray<br />
Mchoraji:<br />
Ismael Abdoulkarym.<br />
Wahariri:<br />
Elizabeth Missokia<br />
Robert Mihayo<br />
Wachangiaji: Benedicta Mrema, Edwin Mashasi, Honoratus Swai,<br />
Wambura Wasira, Agnes Mangweha<br />
© Haki<strong>Elimu</strong> 2010<br />
SLP 79401, Dar es Salaam, Tanzania<br />
Simu: (25522) 2151852 au 3<br />
Nukushi: (255 22) 2152449<br />
Barua pepe: info@hakielimu.org<br />
Tovuti: www.hakielimu.org<br />
ISBN: 9987-9331-3-6<br />
Unaruhusiwa kunakili sehemu yoyote ya kijitabu hiki <strong>kwa</strong> minajili isiyo ya kibiashara. Unachotakiwa<br />
kufanya ni kunukuu chanzo cha sehemu iliyonakiliwa na kutuma nakala mbili Haki<strong>Elimu</strong>.<br />
2
Utangulizi<br />
Ni ukweli uliodhahiri <strong>kwa</strong>mba maendeleo ya jamii yoyote yanahitaji elimu iliyo <strong>bora</strong>. <strong>Elimu</strong> hii ni ile<br />
itakayowawezesha wanafunzi kushiriki kikamilifu katika kutatua matatizo na kupambana na changamoto<br />
mbalimbali katika maisha yao ya kila siku. <strong>Elimu</strong> <strong>bora</strong> ni zaidi ya uwepo wa vifaa na mazingira mazuri<br />
ya kufundishia.<br />
<strong>Elimu</strong> <strong>bora</strong> lazima imwezeshe mwanafunzi kuwa na uwezo katika nyanja mbalimbali ili aweze kufanya<br />
vizuri katika ulimwengu wa maendeleo. <strong>Elimu</strong> <strong>bora</strong> ni ile inayompa mwanafunzi ujuzi kutokana na<br />
masomo mbalimbali anayofundishwa sambamba na kumwezesha kuwa mdadisi wa mambo na kuwa<br />
mbunifu. Pia elimu <strong>bora</strong> humjengea mwanafunzi tabia ya kujiamini na hatimaye kuwa na ujasiri katika<br />
kukabiliana na kutatua changamoto mbalimbali katika maisha.<br />
Walimu ndio watendaji wakuu katika mchakato wa kujifunza na kufundisha. Hii ina maana <strong>kwa</strong>mba<br />
matarajio ya elimu <strong>bora</strong> ndani ya jamii yanatokana na <strong>mafunzo</strong> <strong>bora</strong> ya <strong>walimu</strong>. Walimu wakiwa na elimu<br />
<strong>bora</strong> watakuwa na uwezo wa kutoa elimu <strong>bora</strong> <strong>kwa</strong> wanafunzi wanaowafundisha. Ili mtu aweze kuwa<br />
m<strong>walimu</strong> anahitaji kupata <strong>mafunzo</strong> ya kutosha na yanayoendana na masomo anayotarajia kufundisha.<br />
Mafunzo ya <strong>walimu</strong> ni mchakato maalum wa kumwandaa mtu kwenda kufundisha. Mafunzo haya<br />
huendeshwa <strong>kwa</strong> muda maalum, mazingira maalum, nadharia na vitendo maalumu. Mafunzo haya<br />
ni lazima yamjenge m<strong>walimu</strong> mtarajiwa kwenye maeneo matatu muhimu: Kwanza, ni lazima apate<br />
taaluma na maarifa ya kutosha ya somo analofundisha ili aweze kulimudu somo hilo. Pili, ajue mbinu<br />
za kutosha kufundishia na nadharia zinazoambatana na mbinu hizo.Tatu, sharti aifahamu falsafa na dira<br />
ya taifa ya elimu ili awasaidie watoto kuitafsiri falsafa ya nchi na malengo ya elimu<br />
3
Ili kuenda sambamba na mabadiliko ya kimaisha na mitaala yanayotokea kila kukicha katika ulimwengu<br />
wa leo, <strong>walimu</strong> wanahitaji fursa ya kupata <strong>mafunzo</strong> kazini ili waweze kufundisha kulingana na mabadiliko<br />
hayo na hatimaye kuwajengea wanafunzi uwezo na mbinu <strong>endelevu</strong> za kupambana na changamaoto<br />
zinazotokana na mabadiliko hayo. Mafunzo ya <strong>walimu</strong> kazini ni <strong>mafunzo</strong> yanayotolewa <strong>kwa</strong> <strong>walimu</strong><br />
wakiwa kazini <strong>kwa</strong> lengo la kuamsha na kuongeza ujuzi na maarifa kwenye utaalam na taaluma ya<br />
ualimu katika nadharia na vitendo vya kufundishia. Vilevile <strong>mafunzo</strong> haya yanalenga kuchagiza maadili<br />
na hisia za kufundisha, kuchochea ari ya kufundisha na kusimamia mchakato wa kufundisha.<br />
Kitabu hiki <strong>kwa</strong> kutumia katuni ambazo ni rahisi kuzisoma, zinazofurahisha na kuburudisha, kinalenga<br />
kuonesha athari zinazotokana na <strong>walimu</strong> kutopata <strong>mafunzo</strong> kazini. Athari hizo ni pamoja na kushuka<br />
<strong>kwa</strong> kiwango cha elimu kutokana na wanafunzi kutokuwa na uelewa wa kutosha katika masomo, na<br />
hatimaye kumaliza elimu ya msingi <strong>bila</strong> maarifa wala ujuzi wa kuwawezesha kukabiliana na changamoto<br />
mbalimbali za maisha.<br />
Hadithi hii yenye kichwa cha habari “<strong>Elimu</strong> Bora Bila Mafunzo Endelevu <strong>kwa</strong> Walimu kazini?” pia<br />
inalenga kuonesha umuhimu wa <strong>mafunzo</strong> <strong>kwa</strong> <strong>walimu</strong> kazini sambamba na kuwahamasisha <strong>walimu</strong><br />
kujua haki zao za msingi na kuzitetea ikiwa ni pamoja na haki ya kupata <strong>mafunzo</strong> kazini. Inamulika<br />
ushiriki wa wananchi katika upatikanaji wa elimu, wajibu wa wazazi kushiriki katika vikao na kutoa<br />
maoni na mapendekezo yao kuhusu maendeleo ya elimu <strong>kwa</strong> watoto wao na shule <strong>kwa</strong> ujumla,<br />
ili kufanikisha upatikanaji wa elimu <strong>bora</strong> nchini. Mhusika mkuu katika hadithi hii ni mtoto “Sadiki”<br />
anayetumika kuonesha harakati za kuleta mabadiliko katika shule yao, ambayo <strong>kwa</strong> muda mrefu ilikuwa<br />
ikifanya vibaya kutokana na wanafunzi kuwa na uelewa mdogo katika masomo. Hali hii ilisababishwa<br />
na <strong>walimu</strong> kutokuwa na mbinu mpya za ufundishaji kutokana na ukosefu wa <strong>mafunzo</strong> <strong>kwa</strong> <strong>walimu</strong><br />
kazini. Lakini baada ya <strong>walimu</strong> kuanza kupata <strong>mafunzo</strong> kazini, ufanisi katika shule ile ulibadilika <strong>kwa</strong><br />
kiwango kikubwa.<br />
4
Lete mawazo yako kuhusu kitabu hiki:<br />
Tarehe ya kupokea kitabu hiki ……………………………<br />
Jina…………………………………………………………...............<br />
Anwani ya Posta…………………………………………….........<br />
Namba ya simu……………………………………………………..<br />
Barua pepe……………………………………………………………<br />
Jinsi Mme / Mke<br />
Umri<br />
Kiwango cha <strong>Elimu</strong><br />
7 – 14 <strong>Elimu</strong> ya Msingi<br />
15 – 19 <strong>Elimu</strong> ya Sekondari<br />
20 – 30 Chuo<br />
31 – 40<br />
Zaidi ya 41<br />
1. Kitabu hiki kina habari muhimu?<br />
Ndiyo Hapana Kiasi<br />
2. Kitabu hiki kina manufaa?<br />
Ndiyo Hapana Kiasi<br />
3. Kitabu hiki kinaeleweka kiurahisi?<br />
Ndiyo Hapana Kiasi<br />
4. Kitabu hiki kinavutia?<br />
Ndiyo Hapana Kiasi<br />
5. Kitabu hiki kimeandi<strong>kwa</strong> vizuri?<br />
Ndiyo Hapana Kiasi<br />
6. Umependa michoro ya kitabu hiki?<br />
Ndiyo Hapana Kiasi<br />
40
Umependa nini kwenye kitabu hiki?<br />
Kitabu hiki kinawezaje kuboreshwa?<br />
Unategemea kutumiaje kitabu hiki?<br />
Mengineyo:<br />
Ukimaliza kujaza fomu hii itume <strong>kwa</strong>: Haki<strong>Elimu</strong>, Uchapishaji, SLP 79401, Dar es Salaam.<br />
41
Kuhusu kijitabu hiki<br />
Hali ya elimu katika kijiji cha Kisiwani ni mbaya. Kiwango cha ufaulu <strong>kwa</strong><br />
wanafunzi wa shule ya Msingi Ilaba kiko chini sana. Shule hii inakabiliwa<br />
na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na wanafunzi kutokufaulu<br />
kutokana na ukosefu wa <strong>walimu</strong> wenye taaluma ya kutosha kufundisha<br />
<strong>kwa</strong> kiwango kinachotakiwa, nyumba <strong>bora</strong> za <strong>walimu</strong>, pamoja na ukosefu<br />
wa vitabu vya kutosha. Hali halisi ya elimu katika shule ya msingi Ilaba<br />
inawachukiza sana wazazi wa kijiji cha Kisiwani. Mkutano unaitishwa shuleni<br />
<strong>kwa</strong> lengo la kujadili sababu za wanafunzi kushindwa kufanya vizuri katika<br />
masomo yao. Wazazi, wanafunzi pamoja na <strong>walimu</strong> wanahudhuria. Kila<br />
mmoja anatoa maoni yake kuhusu hali halisi ya elimu na kutoa mapendekezo<br />
ambayo yanafanyiwa kazi na hatimaye <strong>kwa</strong> pamoja wanafanikiwa kuleta<br />
mabadiliko ambayo yanasaidia kuleta elimu <strong>bora</strong> katika kijiji chao. Shule ya<br />
msingi Ilaba iliyokuwa ikifanya vibaya imebadilika na kuwa moja ya shule<br />
zinazofanya vizuri <strong>kwa</strong>ni idadi kubwa ya wanafunzi wanafanya vizuri katika masomo.<br />
Sadiki akiwa ni mwanafunzi wa Shule ya Msingi Ilaba ambaye pia anachukizwa na hali halisi ya maendeleo ya elimu katika shule yao. Ingawa<br />
ni mlemavu wa miguu, anafanya juhudi za makusudi <strong>kwa</strong> kuwahamasisha na kuwaongoza wenzake katika harakati za kuleta mabadiliko<br />
katika shule yao. Harakati hizi zinazaa matunda yanayorudisha tena matumaini mapya <strong>kwa</strong> wanafunzi, <strong>walimu</strong> na wananchi wa Kisiwani<br />
<strong>kwa</strong> ujumla. Kutokana na mafanikio hayo wazazi, <strong>walimu</strong> na wanafunzi katika kijiji cha Kisiwani wanadhamiria kushirikiana zaidi katika<br />
kuendeleza harakati za upatikanaji wa elimu <strong>bora</strong> na kuhakikisha shule yao inaendelea kuwa shule <strong>bora</strong> na ya kuigwa katika wilaya yao.<br />
Haki<strong>Elimu</strong> inafanya kazi kufikia usawa, u<strong>bora</strong>, haki za binadamu na demokrasia katika elimu <strong>kwa</strong><br />
kuwezesha jamii kubadili shule na mfumo wa sera za elimu,<br />
kuchochea mijadala yenye ubunifu na kuleta mabadiliko,<br />
kufanya utafiti yakinifu, kudadisi, kufanya uchambuzi na utetezi na<br />
kushirikiana na wadau kuendeleza manufaa ya pamoja na haki za jamii.<br />
SLP 79401 • Dar es Salaam • Tanzania<br />
Simu: (255 22) 2151852 au 3 • Faksi: (255 22) 2152449<br />
info@hakielimu.org • www.hakielimu.org