18.02.2015 Views

Jinsi ya kudhibiti mbu katika mikorosho

Jinsi ya kudhibiti mbu katika mikorosho

Jinsi ya kudhibiti mbu katika mikorosho

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

1 2<br />

3<br />

JINSI YA KUDHIBITI MBU KATIKA<br />

MIKOROSHO<br />

1.0 Utangulizi.<br />

Kuna aina mbili za <strong>mbu</strong> wa korosho ambao<br />

huleta uharibifu mkubwa sana <strong>katika</strong> zao la<br />

korosho, hasa <strong>katika</strong> kanda <strong>ya</strong> kusini:<br />

♦ Mbu wa <strong>mikorosho</strong> (Helopeltis spp)<br />

♦ Mbu wa minazi (Pseudotheraptus wayii)<br />

1.1 Mbu wa Mikorosho (Helopeltis spp)<br />

Helopeltis ni wadudu jamii <strong>ya</strong> <strong>mbu</strong> wenye<br />

uwezo wa kuruka toka mkorosho hadi<br />

mwingine. Wadudu hawa wenye urefu wa<br />

milimita 5 - 10, wana mchanganyiko wa rangi<br />

<strong>ya</strong> njano, nyukundu na sehemu <strong>ya</strong> weusi<br />

kwenye mabawa (Picha 1). Wadudu hawa<br />

huchangamka na kurukaruka n<strong>ya</strong>kati za<br />

mchana, lakini asubuhi huwa watulivu<br />

kutokana na hali <strong>ya</strong> ubaridi.<br />

1.2. Mbu wa Minazi (Pseudotheraptus wayii)<br />

Mbu wa minazi wanafanana na wadudu<br />

waitwao kangambili ambao ni maarufu sana<br />

kwenye pamba na sufi. Wadudu hawa wana<br />

mchanganyiko wa rangi <strong>ya</strong> udongo na<br />

nyekundu na wana urefu wa milimita 14 - 15.<br />

Wadudu hawa wakiguswa hutoa harufu kali<br />

kama njia <strong>ya</strong> kujihami. Wanafahamika vizuri<br />

kwa majina <strong>ya</strong> kilugha kama vile “Nanoli”<br />

(Kimakonde); “Nandoli” (kimwera, ki<strong>ya</strong>o).<br />

2.0. Masha<strong>mbu</strong>lizi<br />

Aina hizi za <strong>mbu</strong> husha<strong>mbu</strong>lia maeneo<br />

machanga hasa majani, machipukizi, maua na<br />

tegu pia. Mbu hawa hutoboa eneo la<br />

masha<strong>mbu</strong>lizi kwa kutumia mwiba wa kwenye<br />

midomo <strong>ya</strong>o na kwa kufan<strong>ya</strong> hivyo, mate <strong>ya</strong>o<br />

yenye sumu huingia ndani <strong>ya</strong> mmea. Mate<br />

yenye sumu huleteleza makovu meusi <strong>katika</strong><br />

maeneo <strong>ya</strong> masha<strong>mbu</strong>lizi. Majani<br />

<strong>ya</strong>liyosha<strong>mbu</strong>liwa huweza kukunjamana,<br />

hatimaye kukauka. Machipukizi na maua<br />

<strong>ya</strong>naweza kudumaa <strong>ya</strong>siendelee na ukuaji,<br />

huku <strong>ya</strong>kibaki na makovu meusi.<br />

Penye masha<strong>mbu</strong>lizi makali <strong>ya</strong> <strong>mbu</strong> wa<br />

<strong>mikorosho</strong>, machipukizi kukauka pamoja na<br />

majani na kusababisha ugonjwa uitwao<br />

“debeki”. Ukaukaji huanza nchani na<br />

kuteremkia chini <strong>ya</strong> chipukizi. Mashada <strong>ya</strong><br />

maua <strong>ya</strong>liyosha<strong>mbu</strong>liwa hushindwa kuzaa<br />

kabisa. Miti iliyosha<strong>mbu</strong>liwa sana huonekana<br />

kama imebabuka na moto.<br />

Mbu wa minazi husha<strong>mbu</strong>lia pia tegu na<br />

mabibo machanga na kuacha makovu meusi<br />

yenye kuzama ndani kwenye ganda. Tegu<br />

zilizosha<strong>mbu</strong>liwa zikiwa changa sana,<br />

hubadilika rangi na kuwa nyeusi, husin<strong>ya</strong>a,<br />

kisha hupukutika chini. Pia baadhi <strong>ya</strong> korosho<br />

hizo huambatana na makovu.<br />

3.0. <strong>Jinsi</strong> <strong>ya</strong> Kuthibiti Mbu waharibifu.<br />

Mbu hawa wa aina zote mbili, pamoja na<br />

wadudu wa aina nyingine nyingi, wanaweza<br />

kuthibitiwa kwa njia mbili:<br />

3.1 Kutumia madawa<br />

Aina mbalimbali za madawa zimefanyiwa<br />

utafiti wa kina na kuonekana kwamba dawa<br />

aina <strong>ya</strong> KARATE ni bora kwa kuangamiza<br />

wadudu wa aina nyingi. Dawa hii hupuliziwa<br />

kutumia mashine za moto (Mist blower) au za<br />

kawaida (Knapsack sprayer) kutegemeana na<br />

ukubwa wa mkorosho. Kiwango<br />

kilichopendekezwa ni kuchangan<strong>ya</strong> mililita 3 -<br />

5 za dawa kwa lita moja <strong>ya</strong> maji kwa mti<br />

mkubwa. Upuliziaji unaanza mara baada <strong>ya</strong><br />

kuonekana masha<strong>mbu</strong>lizi na kurudia<br />

inapobidi. Matunda <strong>ya</strong>liyopuliziwa dawa<br />

<strong>ya</strong>situmike mpaka baada <strong>ya</strong> siku 21 (wiki 3).<br />

3.2 Kutumia uthibiti wa kibaolojia<br />

(Biological control).<br />

Pamoja na uwezo mkubwa wa kuthibiti na<br />

kuangamiza wadudu kwa kutumia madawa,<br />

lakini madawa ni <strong>ya</strong> gharama mno na <strong>ya</strong>na<br />

madhara sana <strong>katika</strong> mazingara yetu, ikiwa ni<br />

pamoja na kuua wadudu wenye manufaa kwa<br />

mazao yetu. Kwa ajili hiyo jitihada za kiutafiti<br />

zinafanyika ili kumsaidia mkulima kupunguza<br />

uwezekano wa kutumia madawa <strong>katika</strong> mazao.<br />

Utafiti wa kina umefanyika kuchunguza kama<br />

kuna wadudu aina nyingine ambao wanaweza<br />

kutumika kuangamiza wadudu waharibifu wa<br />

<strong>mikorosho</strong>. Hatimaye imeonekana kwamba<br />

wadudu aina <strong>ya</strong> Majimoto (Oecophylla<br />

longinoda) wanao uwezo mkubwa wa<br />

kuangamiza aina zote za <strong>mbu</strong> waharibifu wa<br />

<strong>mikorosho</strong>. Katika uchunguzi wetu, majimoto


4 5<br />

wameonekana mara nyingi tu wakikamata aina<br />

hizi za <strong>mbu</strong> wa <strong>mikorosho</strong> na kuwakokota hadi<br />

kwenye viota v<strong>ya</strong>o kwa ajili <strong>ya</strong> kufan<strong>ya</strong><br />

chakula. Baadhi <strong>ya</strong> viota vilivyowahi<br />

kufunguliwa, vimekutwa na mabaki <strong>ya</strong> sehemu<br />

<strong>ya</strong> mbalimbali za <strong>mbu</strong> hawa, kama vile<br />

mabawa, miguu, midomo nk.,<br />

Matokeo <strong>ya</strong> majaribio yetu <strong>ya</strong>meonyesha wazi<br />

kwamba <strong>mikorosho</strong> yenye majimoto wengi<br />

haisha<strong>mbu</strong>liwi na <strong>mbu</strong> wa <strong>mikorosho</strong>.<br />

Majimoto wakitanda kwenye machipukizi,<br />

maua au tegu hufan<strong>ya</strong> ulinzi mzuri sana dhidi<br />

<strong>ya</strong> masha<strong>mbu</strong>lizi <strong>ya</strong> <strong>mbu</strong> waharibifu. Kwa ajili<br />

hiyo majimoto hujulikana kama rafiki wa<br />

mkulima.<br />

NB: Pata nakala <strong>ya</strong>ko <strong>ya</strong> maelekezo (Na. 3)<br />

juu <strong>ya</strong> “Majimoto rafiki wa mkulima”<br />

A<br />

B<br />

C<br />

D<br />

UTAFITI NA MAENDELEO<br />

KANDA YA KUSINI<br />

JINSI YA<br />

KUDHIBITI MBU KATIKA<br />

MIKOROSHO<br />

Picha A: Mbu wa Mikorosho (Helopeltis spp)<br />

Picha B: Masha<strong>mbu</strong>lizi <strong>ya</strong> <strong>mbu</strong> wa Mikorosho<br />

Picha C: Mbu wa Minazi (P. wayii )<br />

Picha D: Masha<strong>mbu</strong>lizi <strong>ya</strong> <strong>mbu</strong> wa Minazi<br />

Imetolewa na<br />

KITUO CHA UTAFITI,<br />

NALIENDELE,<br />

S. L. P. 509,<br />

MTWARA

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!