Frontier Tanzania Environmental Research REPORT 100
Frontier Tanzania Environmental Research REPORT 100
Frontier Tanzania Environmental Research REPORT 100
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
<strong>Frontier</strong> <strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong><br />
<strong>REPORT</strong> <strong>100</strong><br />
ELIMU YA MAZINGIRA YA BAHARI<br />
MUONGOZO WA MWALIMU<br />
<strong>Frontier</strong> <strong>Tanzania</strong><br />
February 2004
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
ii
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> Marine <strong>Research</strong> Programme<br />
<strong>REPORT</strong> <strong>100</strong><br />
Elimu ya mazingira ya bahari ya<br />
kitropiki<br />
Muongozo wa mwalimu<br />
Mumby, R., Fanning, E. Muruke, M. and St John, F. (eds)<br />
Kingereza Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mazingira Kiswahili<br />
Na Ushirika<br />
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibari<br />
Jumuiya ya Kuhifadhi Mazingira<br />
50-52 Rivingston Street<br />
London UK<br />
EC2A 3QP<br />
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam<br />
S. L. P. 35064<br />
Dar es Salaam<br />
<strong>Tanzania</strong><br />
Pemba 2004<br />
iii
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
Suggested Technical Report citation:<br />
<strong>Frontier</strong> <strong>Tanzania</strong> (2004). Marine environmental education: A Teacher’s Guide (Kiswahili). <strong>Frontier</strong><br />
<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong>. The Society for <strong>Environmental</strong> Exploration, London,<br />
UK, The University of Dar es Salaam, The Institute of Marine Science, Zanzibar, DfID Small Grants<br />
Scheme and the Ministry of Agriculture, Natural Resources, Environment and Co-operatives, Zanzibar.<br />
The <strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report Series is published by:<br />
The Society for <strong>Environmental</strong> Exploration<br />
50-52 Rivington Street<br />
London, EC2A 3QP<br />
United Kingdom<br />
Tel: +44 (0)20 7613 3061<br />
Fax: +44 (0)20 7613 2992<br />
Email: research@frontier.ac.uk<br />
Web Page: www.frontier.ac.uk<br />
ISSN 1479-1161 (Print)<br />
ISSN 1748-3670 (Online)<br />
ISSN 1748-5124 (CD-ROM)<br />
iv
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
© <strong>Frontier</strong> <strong>Tanzania</strong> 2004, 2005<br />
Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mazingira na Ushirika (MANREC)<br />
Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mazingira na Ushirika ni sehemu ya Serikali ya<br />
Mapinduzi ya Zanzibar. Idara ya Mazao ya Biashara, Matunda na misitu (DCCFF) ni<br />
sehemu ya wizara na inawajibika na muongozo wa uanzishaji wa sera ya misitu na<br />
maeneo tengefu, ikiwa ni pamoja na eneo tengefu la bahari la kisiwa cha Misali<br />
(MIMCA) visiwani Zanzibar.<br />
<strong>Frontier</strong> <strong>Tanzania</strong> (FT)<br />
<strong>Frontier</strong> <strong>Tanzania</strong> ni uhusiano kati ya shirika la kuchunguza mazingira na Chuo Kikuu<br />
cha Dar es Salaam. Shughuli za utafiti katika shirika hili zimeendelea tangu Julai 1989<br />
na zimehusisha watafiti toka <strong>Tanzania</strong> na nchi za nje. Utafiti unafanywa kwenye aina<br />
tofauti za mazingira yenye baolojia maalum na hadhi za uhifadhi. Maeneo<br />
yanayochunguzwa hujumuisha misitu, savana za kitropiki, uvuvi, miamba ya<br />
matumbawe, mikoko na nyasi za baharini.<br />
<strong>Frontier</strong> <strong>Tanzania</strong> Marine <strong>Research</strong> Programme (FT MRP)<br />
Huu ni mradi uliofanya utafiti wa kibahari, kisiwa cha Mafia (1989-1994), Songo<br />
Songo (1994-1995), na Mtwara (1996-2000). Mradi ulihamia Pemba ambayo ni<br />
sehemu ya Zanzibar mwaka 2001 ukilenga kisiwa cha Misali. <strong>Frontier</strong> <strong>Tanzania</strong><br />
inafanya kazi kwa kushirikiana na MANREC na Taasisi ya utafitu wa sayansi za bahari<br />
(IMS) katika utekelezaji wa shughuli zake.<br />
Chuo Kikuu cha Dar-es-salaam (UDSM)<br />
Chuo Kikuu cha Dar-es-salaam kilianzishwa Julai 1970 kama kitiuo cha mafunzo na<br />
utafiti katika sayansi za aina mbalimbali. Chuo kinatafiti mimea na wanyama wa<br />
<strong>Tanzania</strong> na kinafanya utafiti wa uimarishaji wa mazingira na matumizi endelevu ya<br />
maliasili za nchi.<br />
Shirika la kuchunguza mazingira (SEE)<br />
Shirika hili lilianzishwa mwaka 1989 na linafanya kazi isiyo ya kibiashara.<br />
Madhumuni ya Shirika hili ni kukuza, kuendeleza utafiti juu ya mazingira na<br />
kutekeleza miradi kwa vitendo itakayosaidia kuhifadhi mazingira na maliasili zake.<br />
Miradi iliyoanzishwa na kusimamiwa na Shirika hili hushirikisha pia wawakilishi wa<br />
kitaifa wa utafiti katika nchi husika.<br />
v
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
KWA MAWASILIANO ZAIDI<br />
Ministry of Agriculture Natural Resources<br />
Environment & Co-operatives<br />
P.O. Box 159, Zanzibar, <strong>Tanzania</strong><br />
Tel: +255 24 223 2840<br />
Fax: +255 24 223 0290<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong>: Head Quarters<br />
PO Box 9473, Dar es Salaam<br />
Tel: +255 22 2780 063<br />
Email: frontier@africaonline.com<br />
Department for Commercial Crops Fruits & Forestry<br />
PO Box 3526, Zazibar, <strong>Tanzania</strong><br />
Tel: +255 24 223 8628<br />
Fax: +255 24 223 6089<br />
Email: dccff@zanlink.com<br />
Dept. of Zoology & Marine Biology<br />
University of Dar es Salaam<br />
P.O. Box 35064, Dar es Salaam, <strong>Tanzania</strong><br />
Tel: +255 22 2410462<br />
E-mail: zoology@udsm.ac.tz<br />
The Institute for Marine Sciences<br />
University of Dar es Salaam<br />
P.O. Box 668, Zanzibar, <strong>Tanzania</strong><br />
Tel: +255 24 223 0741 / 2128 / 3472<br />
Fax: +255 24 223 3050<br />
Society for <strong>Environmental</strong> Exploration<br />
50-52 Rivington Street<br />
London, EC2A 3QP. U.K.<br />
Tel: +44 (0)20 7613 3061<br />
Fax: +44 (0)20 7613 2992<br />
E-mail: research@frontier.ac.uk<br />
Internet: www.frontier.ac.uk<br />
vi
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
Yaliyomo<br />
Utangulizi Kuhusu Elimu ya Mazingira na Muongozo Huu..............................ix<br />
Kwa nini tunataka Kuhifadhi Mazingira ya Bahari..........................................ix<br />
Maendeleo Endelevu..............................................................................................x<br />
Madhumuni ya FT MRP.......................................................................................xi<br />
Mpango wa Utafiti wa Bahari ..............................................................................xi<br />
Historia Ya FT MRP........................................................................................... xii<br />
SEHEMU YA KWANZA .......................................................................................1<br />
1. Utangulizi Kuhusu elimu ya mazingira ya bahari .........................................2<br />
2. Mikoko (Mikandaa) .........................................................................................3<br />
3. Eneo la maji kupwa na kujaa..........................................................................6<br />
4. Nyasi za Baharini ............................................................................................8<br />
5. Miamba ya Matumbawe.................................................................................10<br />
6. Uhusiano wa Mifumo ya Maisha ya Viumbe Hai Baharini........................13<br />
7. Mambo Unayopaswa na Usiyopaswa Kufanya Baharini ............................15<br />
8. Tishio Linaloyakabili Mazingira ya Bahari .................................................17<br />
SEHEMU YA PILI...............................................................................................19<br />
Shughuli zinazofanyika wakati wa ufundishaji..................................................19<br />
1. Masanamu ya kuchorwa................................................................................20<br />
2. Kusanifu matangazo (mabango)...................................................................21<br />
3. Chemsha bongo ya elimu ya mazingira........................................................22<br />
4. Mchezo wa taa za barabarani........................................................................25<br />
5. Kusema hapana kwa takataka ......................................................................27<br />
6. Mfumo wa ushirikiano wa chakula – 1 ........................................................29<br />
7. Mfumo / mtandao wa chakula (Uhusiano wa viumbe) 2.............................31<br />
8. Matembezi ya nyika hai .................................................................................34<br />
Marejeo .................................................................................................................36<br />
SHUKRANI:<br />
FT MRP inapenda kulishukuru shirika la kuchunguza mazingira (SEE) kwa kufadhili<br />
shughuli mbalimbali za Elimu ya Mazingira, wanafunzi na walimu walioshiriki<br />
katika shughuli hizo, kutoka skuli za Kangani, Fidel Castro na Mizingani, Wizara ya<br />
Elimu Afisi za Pemba hasa Mr Hussein (Afisa Kiongozi) kwa kutoa kibali cha<br />
kuendesha shughuli hizo. FT MRP pia inawashukuru Mr Ambakisye Simtoe kwa<br />
kuandaa shughuli za uelimishaji na kutafsiri muongozo huu, na Chuo Kikuu cha Dares-salaam<br />
kwa kusaidia shughuli za FT MRP za utafiti na watafiti wasaidizi wa kati<br />
ya mwaka 2001 na 2003.<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong><br />
vii
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
ACKNOWLEDGEMENTS<br />
This report is the culmination of the advice, co-operation, hard work and expertise of many<br />
people. In particular acknowledgments are due to the following:<br />
SOCIETY FOR ENVIRONMENTAL EXPLORATION<br />
Managing Director: Ms. Eibleis Fanning<br />
Programme Manager (Operations): Mr. Matthew Willson<br />
Programme Manager (<strong>Research</strong>): Ms. Nicola Beharrell<br />
Project Administration:<br />
Mr. Mike Lamb<br />
UDSM<br />
FT Co-ordinators:<br />
Dr. M. Muruke & Prof. K. M. Howell.<br />
FRONTIER-TANZANIA<br />
Project Co-ordinator: Ms. Carol Daniels<br />
<strong>Research</strong> Co-ordinator:<br />
Mr. Angus McVean<br />
Assistant <strong>Research</strong> Co-ordinators: Mr. Edward Mayhew, Ms. Ruth Mumby, Mr. Adam<br />
Pharoah<br />
<strong>Environmental</strong> Education Officer: Mr. Ambakisye Simtoe<br />
Dive Officer:<br />
Mr. Paulo Pizzolla<br />
Logistics Managers:<br />
Mr. Luke Gordon<br />
Boat Crew:<br />
Mr. Mussa Abdalah, Mr. Khashim Abdallah, Mr,<br />
Mzee Salum Seifu<br />
Security:<br />
Mr. Juma Mbaya Juma, Mr. Ali Osman Khamis, Mr.<br />
Sibouri Makame Kombo<br />
Cook:<br />
Mr. Ramadhani Juma Songoro<br />
<strong>Research</strong> Assistants:<br />
Ms. Alice Addison, Mr. Andrew Ashton, Ms.<br />
Katherine Barber, Mr. Matthew Bennett, Mr.<br />
Michael Brown, Ms. Hilary Cartwright-Taylor, Mr.<br />
Alasdair Cockburn, Ms. Charlotte Cranfield, Mr.<br />
Sharif Mohammed Faki, Mr. Christopher Faunce-<br />
Brown, Ms. Anna Franheim, Mr. Conrad Freese, Mr.<br />
Peter Nestory Gabagambi, Mr. Angus Galloway, Ms.<br />
Lydia Gaspare, Mr. Christopher Goatley, Ms.<br />
Eleanor Harrison, Ms. Jacqui Height, Mr. David<br />
Henderson, Ms. Frances, Ms. Lorraine Howe, Illsley,<br />
Ms. Louise Jary, Mr. Ben Jones, Mr. Ali Kitwana,<br />
Ms. Emilia Lascelles, Ms. Andrea Leedale, Ms.<br />
Helen Lofthouse, Mr. Edward Lousley, Mr. Chris<br />
Lovett, Ms. Christine McIntyre, Mr. Jacob Miller,<br />
Mr. Zahor Mohammed, Ms. Lauren Morgan, Mr.<br />
James Moss, Mr. Mathias Msafiri, Mr. Kevin<br />
Murphy, Ms. Olivia Palin, Mr. Adam Partington, Mr.<br />
Rashid Juma Rashid, Mr. David Roadknight, Mr.<br />
Andy Roddis, Mr. Peter Shunula, Mr. Julian Skeels,<br />
Ms. Rachael Smith, Ms. Eike Stubner, Ms. Elinor<br />
Thomas, Ms. Betty Vestberg, Ms. Rhiannon<br />
Williams,<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong><br />
viii
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
Local Staff<br />
Utangulizi Kuhusu Elimu ya<br />
Mazingira na Muongozo Huu<br />
Kwa miongo kadhaa elimu ya mazingira imekuwa ikifundishwa duniani kote kwa<br />
msisitizo mkubwa. Si muhimu kuwa imekuwa rasmi au la, lakini elimu ya mazingira<br />
imekuwa ikifundishwa kwa njia zote rasmi na zisizo rasmi kwa watu wa rika na<br />
mifumo tofauti. Elimu ya mazingira inapaswa kutoa msingi wa mabadiliko wa muda<br />
mrefu ambao unaweza kutumika katika maisha ya kila siku kwa kujiendeleza kiujuzi,<br />
matokeo ya kazi za vitendo na uwajibikaji binafsi.<br />
Katika kukabiliana na hali halisi na kwa njia sahihi, ni muhimu kwa muelimishaji<br />
kuielewa jamii husika na yanayoizunguka. Ni lazima ikumbukwe kuwa maarifa na<br />
mawazo kutoka katika jamii na tamaduni tofauti huwa havishabihiani pamoja. Hivyo<br />
mwelimishaji lazima awe na uwezo wa kubadilika na mwenye kupenda kujifunza ili<br />
kuwa na ujuzi unaohitajika kwa jamii husika. Waelimishaji wa mazingira lazima<br />
wahakikishe kuwa elimu inatolewa kwa njia sahihi ili kuongeza uwezo endelevu<br />
katika hifadhi ya mazingira.<br />
Mwongozo huu umeandaliwa kwa ajili ya waalimu na waelimishaji wengine wa<br />
elimu ya mazingira. Sehemu ya kwanza inatoa utangulizi wa mazingira ya bahari<br />
kufuatana na mgawanyiko wa mfumo wa maisha ya viumbe hai baharini; kwenye<br />
mikoko, maeneo ya maji kupwa na maji kujaa, nyasi za baharini na miamba ya<br />
matumbawe<br />
Sehemu ya pili ya mwongozo huu ina shughuli mbalimbali zinazoweza kufanyika<br />
wakati wa uelimishaji ili kusisitiza elimu ya mazingira kwa vitendo. Shughuli hizi si<br />
halisi lakini zinatoa mwongozo juu ya mwelekeo halisi wa mazingira ya bahari na<br />
shughuli za hifadhi. Ukitumika pamoja na vifaa vingine utakuwa msaada mkubwa<br />
kama kifundishio msaada. Izingatiwe kuwa baadhi ya maeneo ya mwongozo huu<br />
hayana tafsiri ya moja kwa moja ili kukidhi mahitaji ya jamii husika.<br />
Kwa nini tunataka Kuhifadhi<br />
Mazingira ya Bahari<br />
• Bahari inatoa rasilimali zitumikazo na watu waishio pwani.<br />
• Mazingira yanayozunguka bahari kama vile mikoko na nyasi za baharini<br />
zinahitajika kuhifadhiwa, kama kimojawapo kitaharibiwa kitaathiri kingine.<br />
• Kuongezeka kwa idadi ya watu, kunamaanisha kuongezeka kwa msukumo<br />
kwenye mazingira ya bahari, matokeo hayo yanahitajika kuwa endelevu ili kuwa<br />
na uhakika wa rasilimali za baadaye.<br />
• Mazingira mazuri ya bahari hutoa uhakika wa kuwepo kwa rasilimali za kutosha<br />
kwa jamii za pwani.<br />
• Mazingira mazuri ya bahari huwa kivutio kikubwa cha utalii na hivyo kukuza pato<br />
la Taifa.<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong><br />
ix
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
Maendeleo Endelevu<br />
Maendeleo endelevu ni hali ya mabadiliko ambayo huhusisha matumizi ya rasilimali,<br />
mielekeo ya uwekezaji, mzunguko wa maendeleo ya teknolojia, na mabadiliko ya<br />
kitaasisi yenye utulivu na mwelekeo wa kumsaidia binadamu kupata mahitaji yake<br />
kwa sasa na baadaye (Taarifa ya WCED, 1987).<br />
Hii haimaanishi kuwa bahari na ardhi visitumike kwa chakula na nishati, lakini ni<br />
kusema kwamba rasilimali hizi zitumike kwa sasa na kuwepo pia rasilimali za<br />
kutosha kwa vizazi vijavyo kwa viwango vilevile au vikubwa zaidi kuliko vya sasa.<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong><br />
x
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
Madhumuni ya FT MRP<br />
Mpango wa Utafiti wa Bahari<br />
Utafiti wa makazi na rasilimali za bahari hufanywa ili kutoa taarifa (Takwimu)<br />
muhimu kwa mwongozo wa matumizi ya rasilimali hizo kupitia uchoraji wa ramani<br />
zinaonyesha kiasi cha rasilimali na mgawanyiko wake kwenye maji yenye kina chini<br />
ya meta 30 na mifumo ya kimaisha ya viumbe hai iliyoko kwenye eneo la maji kupwa<br />
na maji kujaa. Takwimu hizi za msingi hutoa nafasi kwa utafiti yakinifu kufanyika.<br />
Hali za kibaologia, samaki waishio kwenye miamba ya matumbawe, idadi ya<br />
matumbawe na idadi ya wanyama wasio na uti wa mgongo vitafanyiwa utafiti kwa<br />
kutumia kielelezo cha hali ya juu kilichobuniwa na kufanyiwa marekebisho kwa<br />
miaka 12 ya kuwepo kwa FT MRP.<br />
Takwimu zinazokusanywa zitafanya kazi muhimu ya msingi katika kusimamia azma<br />
ya kuruhusu na kufanikisha madhumuni ya uongozi na utaratibu wa muda mrefu.<br />
Utafiti hufanywa na wafanyakazi wa FT MRP, watafiti wasaidizi toka mataifa<br />
mbalimbali na washirikishwaji toka taasisi mbalimbali kama vile Taasisi ya Sayansi<br />
za Bahari (IMS), Idara ya Mazao ya Biashara, Matunda na Misitu (DCCFF) na Idara<br />
ya Uvuvi na Rasilimali za Bahari (DFMR). Watafiti wote hufundishwa na<br />
kusimamiwa na wanabiologia ya bahari waliobobea .<br />
Vyanzo vya fedha vinapokuwa vizuri na vya uhakika, Vifaa vya kujifunzia hutolewa<br />
bure kwa washiriki kutoka <strong>Tanzania</strong>, wakati wanafunzi toka ng’ambo hujigharimia<br />
vitu vifuatavyo;<br />
• Cheti cha uzamiaji<br />
• Mafunzo ya utafiti wa bahari<br />
• Cheti cha BTEC ambacho ni sawa na cheti cha Darasa la 14 la uingereza<br />
Kuongeza ufahamu juu ya mazingira ya bahari<br />
• Mafunzo na majadiliano na wadau wa rasimali za bahari<br />
• Kuandaa na kugharimia siku za elimu ya mazingira kwa skuli za Pemba hasa zile<br />
zilizo kandokando ya bahari.<br />
FT MRP haikusudii kuzuia uvuvi Pemba. FT MRP inalengo la kufanya kazi na<br />
wavuvi waliopo, na mashirika yasiyo ya kiserikali kuhakikisha kuwa shughuli za<br />
uvuvi sasa na kwa vizazi vijavyo zinaendelea kuwa endelevu na samaki wa<br />
kutosha wanakuwepo.<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong><br />
xi
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
Historia Ya FT MRP<br />
Kisiwa cha Mafia 1989 – 1994<br />
Kisiwa cha Mafia kilitunukiwa kuwa eneo tengefu la Kibahari mwaka 1995 ikiwa ni<br />
matokeo ya kazi ya FT MRP iliyofanyika kati ya mwaka 1989 hadi 1994. Kwa sasa<br />
hifadhi hii inasimamiwa na Idara ya Hifadhi za Taifa la <strong>Tanzania</strong> kwa kushirikiana na<br />
WWF.<br />
Kisiwa cha Songo Songo 1994 – 1996<br />
Baada ya Utafiti Kisiwani Mafia kukamilika huku kukiwa na mafanikio makubwa,<br />
mradi wa FT MRP ulihamishiwa kisiwa kidogo cha Songosongo. Kisiwa hiki kina<br />
aina tofauti za matumbawe ambazo zilichunguzwa na kufanyiwa utafiti wa kina kisha<br />
ramani zikachorwa kuonyesha mpangilio wa rasilimali hizo, kazi iliyofanyika kwa<br />
muda wa miaka miwili. Vilevile kazi ya utafiti wa uvuvi iliyofanyika hapa ilikuwa ya<br />
muhimu zaidi kutokana na wavuvi wengi kukitumia kisiwa hiki kwa mapunziko<br />
mafupi kabla ya kupeleka samaki wao bara.<br />
Kilwa Kivinje 1997<br />
Ulikuwa ni mpango wa muda mfupi uliolenga maeneo ya maingilio ya mto Rufiji<br />
baharini. Taarifa juu ya aina mbalimbali za mikoko zilitumika kutengeneza ramani na<br />
matumizi yake yalichunguzwa kwa kina zaidi. Bahati mbaya eneo hilo lilikutwa likiwa<br />
limeathirika na mradi mkubwa wa ufugaji wa kamba. Madhara zaidi ya mradi huu<br />
yaelekea kusababishwa na kugeuzwa kwa hekta 20,000 za mikoko kuwa mabwawa ya<br />
kufugia kamba.<br />
Rasi za Mnazi, Mikindani na Mtwara 1997 – 2000<br />
Baada ya kutengeneza ramani ya ukanda wa kati wa Pwani ya <strong>Tanzania</strong>, FT MRP<br />
ilihamishia shughuli zake pwani ya kusini karibu ya mpaka wa Msumbiji. Mradi<br />
ulianza shughuli zake za utafiti Rasi ya Mnazi baada ya kushauriwa na Shirika la<br />
Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) ambapo ilipendekezwa kuanzishwa kwa eneo<br />
tengefu la kibahari. Baada ya hapo mradi ulihamia Rasi ya Mtwara mwaka 1998 na<br />
kufanya utafiti eneo lote la ukanda wa Pwani ya Kusini kuzunguka Wilaya ya Mtwara<br />
Mikindani.<br />
Wakati huo takwimu na taarifa juu ya uharibifu wa matumbawe uliosababishwa na<br />
mvua za El-Nino kusini mwa <strong>Tanzania</strong>. Kwa ujumla zilionyesha uharibifu mkubwa wa<br />
matumbawe na hasa katika pwani ya kusini mwa <strong>Tanzania</strong>. Kwa hiyo miradi zaidi<br />
ilianzishwa ili kurekebisha / kuondoa uharibifu na kuangalia utengamavu wa<br />
matumbawe. Miradi hii ilikamilika mwishoni mwa mwaka 2000.<br />
Kisiwa Cha Pemba 2001 – 2003<br />
FT MRP ilihamishia shughuli zake kisiwani Pemba mwezi wa pili mwaka 2001.<br />
Kisiwa cha Pemba kiko kaskazini mwa kisiwa cha Unguja na ni kimojawapo kati ya<br />
visiwa vikubwa viwili vinavyounda Zanzibar na kinatambulika Kimataifa kwa kuwa<br />
na rasilimali nyingi za bahari. Kwa pamoja Unguja na Pemba zina maeneo mengi<br />
yenye viumbe hai wa aina tofauti na wenye umuhimu mkubwa kimataifa (UNEP<br />
1989).<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong><br />
xii
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
Idadi na aina tofauti ya matumbawe iliyoripotiwa mwaka 1990 visiwani Zanizibar ni<br />
mara mbili zaidi ya ile iliyoripotiwa hapo mwanzo.<br />
Kwa pwani yote ya Africa mashariki na kati pwani ya Pemba ina mikoko mingi (Jean<br />
Veron, Pers comm.) ambayo ni moja ya maeneo makubwa ya uvuvi na hivyo kuwa<br />
chanzo kikubwa cha protini kwa wakazi wake. Mikoko ya Pemba kama ilivyo mingine<br />
yote ya <strong>Tanzania</strong> inahifadhiwa chini ya mpango maalumu wa hifadhi ili kupunguza<br />
madhara yanayosababishwa na binadamu.<br />
Mipango ya mwanzo ya FT MRP ililenga kwenye mpango wa hifadhi ya maeneo ya<br />
kisiwa cha Misali (MICA) ikiwa ni mipango ya miaka mitutu. FT MRP inafanya kazi<br />
kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mazingira na Ushirika Zanizibar<br />
(MANREC), Taasisi ya Sayansi za Bahari (IMS), Shirika la Kuhifadhi Mazingira ya<br />
Kisiwa cha Misali, (MICA), CARE – <strong>Tanzania</strong> na wadau asilia.<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong><br />
xiii
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
SEHEMU YA KWANZA<br />
1. Utangulizi Kuhusu elimu ya mazingira ya bahari<br />
2. Mikoko (Mikandaa)<br />
3. Eneo la maji kupwa na kujaa<br />
4. Nyasi za baharini<br />
5. Miamba ya Matumbawe<br />
6. Uhusiano wa Mifumo ya Maisha ya Viumbe Hai<br />
Baharini<br />
7. Mambo Unayopaswa na Usiyopaswa Kufanya<br />
Baharini<br />
8. Tishio Linaloyakabili Mazingira ya Bahari<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 1
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
1. Utangulizi Kuhusu elimu ya<br />
mazingira ya bahari<br />
Kihistoria, wakazi wa pwani wameyatumia mazingira ya bahari kujipatia chakula,<br />
vifaa vya ujenzi sehemu za kutabaruku na njia za usafirishaji. Kuongezeka kwa idadi<br />
ya watu, na kukua kwa sayansi na teknologia, kumesababisha ongezeko kubwa la<br />
matumizi ya bahari na mali asili zake na, upande mwingine kumekuwa na ongzeko la<br />
uharibifu wa mazingira na kupungua kwa rasilimali. Baadhi ya viumbe vimepotea na<br />
baadhi viko hatarini kupotea kama vile nyangumi na pomboo. Kwa hiyo hatua za<br />
haraka zinahitajika kuchukuliwa ambazo zitapelekea kuwekwa kwa taratibu na<br />
mwongozo madhubuti wa matumizi ya rasilimali za bahari upande mmoja, na<br />
kuhifadhi mazingira upande mwingine. Hivyo Elimu ya kutosha juu ya mazingira ya<br />
bahari na rasilimali zake inahitajika.<br />
Kabla ya menejimenti ya mazingira kufanyika ni muhimu kuelewa yaliyomo ndani ya<br />
mazingira ya bahari. Sura zifuatazo zinaelezea kwa ufupi yaliyomo kwenye mazingira<br />
ya bahari. Mazingira ya bahari ya kitropiki yanapatikana kati ya nyuzi 25 za latitudi<br />
pande zote mbili za ikweta. Ndani ya ukanda huu mdogo wa mazingira ya bahari<br />
duniani kote huwa katika mpangilio ufuatao toka nchi kavu kwenda baharini.<br />
• Misitu ya mikoko / mikandaa<br />
• Eneo la maji kupwa na kujaa<br />
• Nyasi za baharini<br />
• Miamba ya matumbawe<br />
Kila eneo lina uhusiano na jingine, mara nyingi hutegemeana ili viumbe hai viishi.<br />
Kutegemeana huko kumejadiliwa kwenye sehemu ya kwanza ya mwongozo huu,<br />
ambayo hutoa maelezo ya kila eneo kwa ufupi.<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 2
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
2. Mikoko (Mikandaa)<br />
2.1 Utangulizi<br />
Miti na vichaka vya mikoko hupatikana kati ya sehemu ya juu kabisa maji yanapojaa<br />
na sehemu ya chini kabisa maji yanapokupwa. Ni mimea ambayo hustawi vizuri<br />
kutokana na tabia maalum zinazoiwezesha kunawiri kwenye eneo hili, sifa hizo ni<br />
pamoja na kuwa na uwezo mkubwa wa kuvumiliwa kiwango kikubwa cha<br />
chumvichumvi ndani ya maji, kuwa na mizizi yenye sifa maalum ya kutoa chumvi<br />
ijulikanayo kama `pneumatophores` ambayo imejitokeza nje ya udongo hivyo<br />
kuruhusu uvutaji hewa rahisi kwenye tope lisilo na hewa (anoxic). Mpangilio wa aina<br />
za mikoko hutegemea uwezo wake kuvumilia chumvi chumvi ndani ya maji, aina ya<br />
udongo ilipomea na hali ya hewa.<br />
Mikoko hutumika kama chanzo cha nishati, miti ya kujengea na pia maeneo ya kuvua<br />
Samaki na shughuli zingine. Mikoko pia hutumika kama mazalio ya wanyama wa<br />
baharini, vifyonza virutubisho na kwenye mzunguko wa virutubisho hivyo, na pia<br />
huzuia mmomonyoko wa udongo pwani. (Semesi na Howell 1989).<br />
Mikoko ilipewa hadhi ya kulindwa <strong>Tanzania</strong> mwaka 1930, lakini kumekuwa na<br />
kutoelewana kati ya wanavijiji ambao wangependa kutumia maliasili zao na<br />
wanaohusika na kuzihifadhi. Imetokea mara nyingi kuwa wanakijiji hawakuruhusiwa<br />
kutumia mikoko wakati makampuni ya kibiashara yaliruhusiwa kufyeka mikoko kwa<br />
ajili ya kilimo cha mpunga, maeneo ya kutengeneza chumvi au maeneo ya kufugia<br />
samaki (Semesi na Howell 1989). Sheria zaidi zilizopitishwa Zanzibar mwaka 1968<br />
na <strong>Tanzania</strong> kwa ujumla mwaka 1991, kuzuia kukata mikoko kwa matumizi ya<br />
kibinadamu (Semesi 1998). Sheria hizi zilimaanisha kushabirisha matumizi ya kila<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 3
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
siku na mwongozo endelevu wa mfumo wa maisha ya viumbe hai (Semesi na Howell<br />
1989).<br />
2.2 Mikoko (mikandaa) ya <strong>Tanzania</strong><br />
Ukanda wa Pwani wa <strong>Tanzania</strong> una urefu wa Kilometer 800 na kati ya hizo km 600<br />
zina matumbawe, majani ya bahari na mikoko.<br />
• Moja kati ya maeneo yenye mikoko mingi kabisa Africa Mashariki ni eneo la mto<br />
Rufiji unapoingia baharini lenye ukubwa wa jumla ya Kilometa za mraba <strong>100</strong>0<br />
2.3 Mikoko ni nini<br />
• Mimea (miti / vichaka) inayovumilia mazingira ya chumvi inayopatikana eneo la<br />
bahari linalokupwa na kujaa maji<br />
• Mikoko hustawi kati ya eneo la kati na lile la chini kabisa maji yanapojaa na<br />
kupwa na mpangilio wa aina zake hutegemea muda wa maji kujaa<br />
• Mikoko ina sifa maalum zinazoiwezesha kuvumilia muongezeko na mabadiliko<br />
ya chumvichumvi ndani ya maji na hali ya kukosa hewa kwenye udongo<br />
• Kuna aina 60 za mikoko zinazostawi duniani kote, <strong>Tanzania</strong> inazo 10 kati ya hizo<br />
2.4 Hifadhi ya mikoko<br />
• Ni vigumu sana kulinda maeneo yote ya mikoko kwa kuwa mikoko imesambaa<br />
sehemu kubwa ya pwani ya <strong>Tanzania</strong><br />
• Elimu ya umuhimu wa mikoko na ushirikishwaji wananchi vinategemewa<br />
kusaidia utunzaji na matumizi mazuri ya mikoko ili iendelee kuwepo<br />
2.5 Tabia / Sifa maalum za mikoko<br />
Aina zote za mikoko zina tabia / sifa maalum zilizofanana zinazoiwezesha kuwepo<br />
maeneo ilipo.<br />
• `Pneumatophores’ (vikua) hii ni mizizi inayojitokeza nje ya udongo, hutokea sana<br />
kwenye maeneo yenye maji yaliyosimama<br />
• Viotea, hizi ni mbegu nene zenye uzito wa kutosha ambazo humea zingali kwenye<br />
mti mama hivyo huendelea kukua kwa haraka sana zinapoanguka kwenye tope<br />
• Ina uwezo wa kuvumilia kiasi kikubwa cha chumvi chumvi ndani ya maji, lakini<br />
kiwango kikubwa zaidi cha chumvichumvi hizo huweza kuiua mikoko<br />
• Ina uwezo wa kuzuia chumvichumvi kuingia kwenye mfumo wa mikoko<br />
• Majani yake yana ute wa nta juu yake na stomata zilizotumbukia ndani kupunguza<br />
upotevu wa maji baridi<br />
2.6 Kwa nini mikoko ni muhimu<br />
Mikoko huchuja takataka zilizo chini ya ardhi na kufyonza virutubisho kwa kutumia<br />
mizizi hivyo husaidia mzunguko wa virutubisho ambavyo huhitajika na viumbe<br />
vengine.<br />
• Huchuja matamahuruku na takataka kutoka nchi kavu hivyo huzilinda nyasi za<br />
baharini na matumbawe<br />
• Mizizi ya mikoko hufyonza maji baridi hivyo kupunguza kiwango cha maji hayo<br />
kinachoyafikia matumbawe ambacho kikizidi huweza kuyaharibu<br />
• Hupunguza mwendo kasi wa maji na hivyo kuruhusu lava na kamba kuishi salama<br />
• Pia ni makazi salama kwa viumbe mbalimbali<br />
• Chanzo cha chakula kwa binadamu – wanawake huvua samaki kwenye maeneo<br />
haya kwa matumizi ya nyumbani<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 4
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
• Chanzo cha nishati – hasa kwa jamii za pwani<br />
• Hutumika kujengea zio, nyumba, mitumbwi na madema n.k<br />
• Madawa asilia – Madawa ya kutibu magonjwa mbalimbali kama vile magonjwa<br />
ya tumbo na mikwaruzo<br />
• Ni kivutio kikubwa kwa watalii, kwa mfano misitu ya Jozani Unguja<br />
2.7 Ukataji / Uharibuifu wa mikoko<br />
• Ukataji wa mikoko kibiashara na matumizi ya kawaida sio endelevu na hasa<br />
inapokatwa bila uangalizi wowote<br />
• Mikoko hukatwa ili kuchoma mkaa na pia kupata maeneo ya uzalishaji wa chumvi<br />
• Upasuaji wa Mbao<br />
• Kilimo na ufugaji wa samaki<br />
• Umwagaji wa bidhaa za petroli na mabaki mengine<br />
• Matumizi ya kawaida (Uvuvi na nishati) husababisha madhara kidogo kuliko<br />
matumizi ya kibiashara<br />
• Madhara asilia kama vile milipuko ya Volkano na tufani huharibu mikoko pia.<br />
Athari zitokanazo na haya huwa ni kubwa mno hasa kama zitaambatana na<br />
uharibifu unaosababishwa na binadamu<br />
2.8 Matokeo ya kuharibu Mikoko<br />
• Kupungua kwa viumbe hai<br />
• Kuongezeka kwa mmomonyoko wa Pwani, miji iliyo karibu na pwani na mahoteli<br />
ya kitalii vyaweza kuathirika<br />
• Kuongezeka kwa matamahuruku kwenye matumbawe hupunguza uzalishaji na<br />
utalii<br />
• Chakula na nishati vitapungua na hivyo wanawake kulazimika kusafiri mbali<br />
kupata vitu hivyo<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 5
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
3. Eneo la maji kupwa na kujaa<br />
3.1 Utangulizi<br />
Eneo la maji kupwa na kujaa ni ukanda mwembamba, ni eneo ambalo hali ya ardhi<br />
yake hubadilika sana kuliko jingine lolote lile baharini, hivyo ni mazingira yenye<br />
taabu nyingi kwa viumbe wanaoishi hapo. Aidha mwendeleo wa kujaa na kupwa kwa<br />
maji umekuwa ukiviathiri viumbe hai ambao huhitaji uzoefu mkubwa wa mazingira<br />
haya ili viweze kuvumilia mabadiliko makubwa ya joto, chumvichumvi na mawimbi.<br />
Ingawa ni asilimia ndogo sana ya bahari yenye maji kupwa na kujaa duniani kote,<br />
eneo hili limekuwa na umuhimu mkubwa kutokana na kuwa na aina mbalimbali za<br />
viumbe hai. Pia kwa vile hufikika kwa urahisi na lina maliasili nyingi, sehemu nyingi<br />
huambatana na uvunaji mkubwa wa maliasili hizo.<br />
3.2 Umuhimu wake Kibaologia<br />
Eneo la maji kupwa na maji kujaa ni muhimu sana kwa kuwa chanzo kikubwa cha<br />
chakula kwa ajili ya jamii za pwani. Ukusanyaji wa makombe na uvuvi wa pweza na<br />
ngisi huzipatia jamii hizo vyanzo muhimu vya protini kama nyongeza kwa ile<br />
wanayoipata kwenye samaki. Maeneo haya pia huweza kuwa na mchanga au miamba.<br />
Mchanga wa Pwani ni kivutio kkikubwa cha watalii hivyo kuongezeka pato kwa taifa.<br />
Kwa mfano kisiwa cha Misali kina eneo hili kubwa ambalo huvutia watalii kulitumia<br />
kama sehemu ya kujifunza mengi na kupumzika (Kutabaruku).<br />
3.3 Uvunaji na uharibifu<br />
Kutokana na urahisi wa kufikika kwa eneo la maji kupwa na kujaa husababisha<br />
urahisi wa uvunaji wa maliasili zilizopo. Hivyo kama uvunaji huo hautazingatia<br />
taratibu za hifadhi na matumizi endelevu idadi ya viumbe hai inaweza kuathirika.<br />
Kwa kawaida mikuki na fimbo hutumika katika uvuvi wa pweza. Aina hii ya uvuvi<br />
yaweza kuwa endelevu ingawa bado kunahitajika takwimu sahihi ili kuepusha<br />
maamuzi yasiyoshabihiana na ukweli halisi. Kama idadi ya watalii itaongezeka juu ya<br />
kiwango kinachohitajika basi kuna uwezekano wa eneo hili kuathiriwa na shughuli<br />
mbalimbali kama vile kutembeatembea, kutupa taka na kuokota kombe, ambazo<br />
zaweza kuathiri mazingira aslilia.<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 6
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
3.4 Uhifadhi wake<br />
Uhifadhi ya maeneo haya hufanana ama na yale ya nchi kavu kwa upande moja au na<br />
yale ya bahari kwa upande mwinginehivyo uhifadhi wake huwamgumu, na hata<br />
katika utekelezaji wa mwongozo wa matumizi yake. Mara kwa mara kuna migongano<br />
juu ya idara ipi inahusika na uangalizi wa eneo hili. Pia kwa jinsi eneo hili<br />
linavyoonekana kama tupu hudhaniwa kuwa halina faida kwa viumbe wengi, mawazo<br />
ambayo sio sahihi.<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 7
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
4. Nyasi za Baharini<br />
4.1 Utangulizi<br />
Nyasi za baharini ni mimea ya nchi kavu ambayo imeweza kujijengea tabia ya kuishi<br />
baharini mpaka kina cha meta 50. Kuna aina 50 za majani ya baharini duniani kote,<br />
hupatikana zaidi kwenye maji kuanzia Antaktiki hadi <strong>Tanzania</strong>. Hufanana na nyasi za<br />
kawaida katika muonekano wake.<br />
4.2 Umuhimu wa majani ya baharini<br />
Majani haya huota kwenye maeneo tofauti kuanzia kwenye tope hadi kwenye miamba<br />
laini na yana uwezo wa kufunika meta moja ya mraba ambayo ya vikonyo vya nyasi<br />
4000 (Nybakken 2001). Vikonyo vya majani hayo huwa na mizizi imara ambayo<br />
huzashikilia vizuri hivyo kushinikiza mashapo sawia. Pia hutoa chakula kwa samaki,<br />
ulumba / ufuma na Kobe wa baharini. Mimea mingine ya baharini hujishikisha<br />
kwenye nyasi hizi. Samaki wadogo wadogo wanaokua hupata chakula, maeneo ya<br />
kujificha na makuzio. Hivyo nyasi za baharini ni makazi na maeneo muhimu ya uvuvi<br />
wa viumbe wadogo wadogo kama vile kamba.<br />
4.3 Manufaa / Matumizi / Uharibifu<br />
Hushikiza vizuri matamahuruku, hii huelezea umuhimu wa majani ya bahari kwa<br />
mfumo bora na imara wa maisha ya viumbe hai. Majani haya huweza kuharibiwa kwa<br />
njia nyingi.<br />
Njia asilia<br />
• Tufani kali<br />
• Mabadiliko ya kiasi cha chumvichumvi ndani ya maji kutokana na kuingia kwa<br />
maji baridi<br />
Binadamu<br />
• Maendelezo ya pwani pamoja na uchimbaji mchanga<br />
• Ujenzi wa mahoteli na viwanda huongeza kasi ya maji na hivyo waweza<br />
kusababishaa ongezeko kubwa la matamahuruku<br />
• Uchafuzi kutokana na umwagaji wa mafuta, maji taka na madawa<br />
• Utiaji nanga na uharibifu wa panga-boya<br />
• Uvuvi wa kupita kiasi<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 8
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
4.4 Matokeo / Madhara<br />
Ili kurudi katika hali ya kawaida baada ya kuharibiwa, nyasi za baharini huchukua<br />
muda wa miaka sita hadi mia moja kutegemea na ukubwa wa uharibifu uliotokea.<br />
Kwa hiyo uharibufu wowote huathiri mfumo mzima wa maisha ya viumbe hai<br />
baharini. Bila nyasi hizi mazalio na makuzio ya viumbe hai wengi yatakosekana na<br />
hivyo kupungua kwa idadi ya viumbe hivyo. Nyasi pia huzuia mashapo yasiyafikie<br />
matumbawe, hivyo kuondolewa kwake kutayaathiri matumbawe kwa kiasi kikubwa.<br />
4.5 Hifadhi yake<br />
Ni rahisi kuzihifadhi nyasi za baharini. Kinachohitajika ni kuweka vikwazo kwa<br />
waendeshaji / Wajenzi wa pwani ili kutoa nafasi kwa majani kustawi tena.<br />
Kwa vile nyasi hizi ni makazi ya aina mbalimbali za samaki na maeneo muhimu ya<br />
uvuvi, ni muhimu kuhakikisha kuwa maeneo hayo hayaharibiwi kwa faida ya wakazi<br />
wa pwani. Kama uharibifu ungalifanywa kwa nia ya kuwanufaisha wakazi wa pwani,<br />
basi manufaa hayo yangalikuwa ya muda mfupi tu. Manufaa yaweza kupatikana kwa<br />
maongozi endelevu. Ulinzi asilia unaotolewa na nyasi baharini kwa matumbawe<br />
hauwezi kufanywa na maumbo ya kuundwa na binadamu.<br />
Waendelezaji wa mahoteli wanaweza kuwa chanzo kikubwa cha uharibifu wa nyasi<br />
za baharini. Wajenzi hawa huziondoa nyasi kwa vile husadiki kuwa huleta<br />
muonekano mbaya wa eneo la hoteli kwa wageni na kwenye fukwe za mchanga. Ili<br />
kuzihifadhi, hatua madhubuti zinahitajika kuchukuliwa. Wenyeji wanahitaji<br />
kuelimishwa kuwa majani wasioyapenda yasipokuwepo fukwe na matumbawe<br />
ambayo watalii hulipia kuviona vitakuwa hatarini kutoweka.<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 9
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
5. Miamba ya Matumbawe<br />
5.1 Utangulizi<br />
Mara nyingi matumbawe huwa katika mkusanyiko ujulikanao kama “Koloni” la<br />
wanyama wenye uhai ambao huitaji mwanga wa jua na chakula kukua. Kila mnyama<br />
mmoja kwenye koloni huwa na uhusiano wa kufaidiana aina ya mwani ambayo<br />
huonekana kwa darubini tu. Uhusiano huu hufanyika kwa matumbawe kutoka madini<br />
ya chokaa ambayo ndio hutengeneza sehemu kubwa ya mfumo wa miamba ya<br />
matumbawe.<br />
Mimea hii midogodogo ndani ya matumbawe huishi kwa kuzaliana kwa kutumia<br />
mfumo wa mwanga wa jua na hewa ya kabondayoksaid toka kwenye matumbawe.<br />
Wakati huo huo matumbawe hupata hewa ya oksijeni na chakula kutoka kwenye<br />
mimea hii. Lakini pia kuna aina ya matumbawe (Yasiyojenga miamba) huweza kukua<br />
bila ya mimea hii, pia hayahitaji mwanga kukua hivyo hupatikana kwenye kina kirefu.<br />
Kwenye matumbawe pia kuna viumbe wanaotengeneza chokaa inayosaidia kujenga<br />
miamba. Viumbe hivi hujumuisha mwani wa kwenye matumbawe, matumbawe laini,<br />
na wanyama wasio na uti wa mgongo kama vile sponji na makombe madogo<br />
5.2 Umuhimu wa matumbawe<br />
Matumbawe ni muhimu kwa kuwa yanahifadhi aina nyingi za viumbe hai na kwamba<br />
ni chanzo muhimu cha chakula kwa mamilioni ya watu kupitia uvuvi wa samaki,<br />
makombe, na viumbe wengine. Pia huzuia mawimbi makubwa hivyo huyalinda<br />
mazingira ya pwani, fukwe na nchi kavu. Ili yaweze kustawi/kukua vizuri<br />
matumbawe yahahitaji mazingira maalum ambayo yamejadiliwa hapa chini.<br />
5.2.1 Joto<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 10
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
Kwa ukuaji mzuri, matumbawe huhitaji nyuzi joto kati ya 25-37 0 C kwa sababu hii<br />
matumbawe hupatikana ndani ya ukanda ulioko 25 0 kaskazini na 25 0 kusini ya Ikweta<br />
na kwenye kina kifupi cha maji.<br />
5.2.2 Mwanga wa kutosha<br />
• Mwanga husaidia mimea inayoishi kwenye matumbawe kufanya shughuli zake<br />
vizuri ambazo huongeza kasi ya ukuaji wa matumbawe na kuwepo kwa<br />
virutubisho vya kutosha<br />
• Matumbawe hupungua kwa kasi kadiri kina cha maji kinavyoongezeka hivyo<br />
kwenye kina cha meta 30 – 40 si rahisi kuyakuta<br />
5.2.3 Kutuama kwa mashapo / takataka<br />
• Kiasi kikubwa cha taka na matamahuruku kwenye maji hupunguza kiasi cha<br />
mwanga kinachoyafikia matumbawe na kuathiri uzalishaji wa chakula kwa<br />
kutumia mimea, hivyo kasi ya ukuaji huathirika pia<br />
• Utupaji wa taka huweza kutokea kwenye matumbawe na hili likitokea<br />
husababisha matumbawe kufa<br />
• Matumbawe hutumia nishati kubwa kuondoa uchafu<br />
5.2.4 Chumvi Chumvi<br />
• Mabadiliko kidogo tu ya chumvi ndani ya maji huweza kuathiri matumbawe.<br />
Hunawiri vizuri kwenye kiasi cha juu cha chumvi chumvi ndani ya maji, ukuaji<br />
wake hupungua au kusitishwa kabisa kiwango cha chumvi kinapopungua na<br />
hayaoti kabisa kwenye maji baridi kama vile kwenye maingilio ya mito Amazoni<br />
na Orinoko<br />
5.3 Uvunaji / uharibifu wa matumbawe<br />
• Matumbawe huharibiwa na aina yoyote mbaya ya uvuvi<br />
• Matumbawe huvunwa kwa ajili ya kutumika katika ujenzi, kama vivutio, na<br />
utengenezaji wa chokaa<br />
• Ukusanyaji wa makombe toka kwenye matumbawe<br />
• Ukataji wa mikoko – kwa ajili ya nishati, ujenzi na kwa kilimo na ufugaji<br />
• Uchafuzi kutokana na shughuli mbalimbali zinazofanywa na binadamu kama vile<br />
kilimo, maji taka, viwanda n.k<br />
• Utalii – uzamiaji, uogeleaji na utiaji nanga<br />
5.4 Hifadhi ya matumbawe<br />
Kwa vile matumbawe huishi na viumbe wengine wengi, ni muhimu kuwa waangalifu<br />
wakati wa kufanya hifadhi. Hii yaweza kufanywa kwa:<br />
• Kusitisha uvunaji wa matumbawe kwa ajili ya ujenzi na mapambo<br />
• Kuacha ukusanyaji wa makombe toka kwenye matumbawe<br />
• Kuzuia utiaji nanga kwenye matumbawe<br />
• Matumizi ya aina salama za uvuvi, kwa mfano kutembea juu ya matumbawe, na<br />
uvuvi wa mabomu na sumu havitakiwi<br />
• Ujenzi wa aina yoyote katika fukwe ni lazima uhakikishe kuwa hauathiri viumbe<br />
vya baharini<br />
Uangalizi wa matumbawe duniani kote unazingatiwa na unaelekea kuwa ni wenye<br />
mafanikio makubwa. Kisiwa cha Mafia nchini <strong>Tanzania</strong> kimefanywa kuwa eneo<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 11
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
tengefu la kibahari la jumla. Hii inamaanisha kuwa wakazi wa sehemu hiyo<br />
wanaruhusiwa kuvua lakini kwa mpango maalum unaoonyesha idadi na ukubwa wa<br />
samaki wanaopaswa kuvuliwa. Watalii wanaruhusiwa kufanya shughuli zao lakini<br />
mahoteli na vituo vyao vimewekewa mipaka maalum.<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 12
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
6. Uhusiano wa Mifumo ya Maisha<br />
ya Viumbe Hai Baharini<br />
6.1 Utangulizi<br />
Kuna uhusiano wa kimaisha / mazingira kati ya mikoko, nyasi za baharini na<br />
matumbawe. Hivyo ni muhimu kila mfumo kupewa kipaumbele katika hifadhi. Nyasi<br />
za baharini na mikoko huchuja uchafu / mashapo hivyo kuhakiki usalama wa<br />
matumbawe. Kwa upande wa pili matumbawe hupunguza kasi za mawimbi<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 13
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
maharibifu hivyo kuzuia uharibifu ambao ungeweza kutokea kwenye mikoko na nyasi<br />
za baharini.<br />
6.2 Mtazamo wa jumla<br />
Mpangilio ufuatao unaonyesha jinsi ambavyo kila eneo la bahari linavyofaidisha<br />
jingine.<br />
6.3 Mikoko<br />
• Huchuja matamahuruku na kufyonza virutubisho, hivyo huzipatia nyasi za<br />
baharini na matumbawe maji safi. Mashapo / uchafu vikizidi huua matumbawe<br />
• Huzuia mmomonyoko wa udongo kwenye fukwe<br />
• Hupunguza kiwango cha maji baridi kinachoyafikia matumbawe hivyo kupunguza<br />
mabadiliko ya chumvi chumvi ambayo huathiri matumbawe<br />
• Makuzio ya samaki wadogowadogo<br />
• Hupunguza kasi ya mawimbi hivyo huwezesha lava kuishi<br />
6.4 Nyasi za baharini na Maeneo ya maji kupwa na maji kujaa<br />
• Makulio ya samaki wadogowadogo<br />
• Hupunguza kasi ya mawimbi hiyo lava huweza kuishi<br />
• Huzuia mmomonyoko wa fukwe<br />
• Ni sehemu ambayo uozo mwingi hupatikana hivyo kuwa chanzo kikubwa cha<br />
chakula kwa viumbe vingi vya baharini<br />
• Huchuja / huzuia taka zisiyafikie matumbawe<br />
6.5 Matumbawe<br />
• Huzuia mawimbi makali kuyafikia majani ya baharini, mikoko na eneo<br />
linalokupwa na kujaa maji<br />
• Hutoa sehemu salama na imara kwa viumbe wa aina tofauti kuishi na kuzaliana<br />
• Aina ya viumbe wengi wanaopatikana kwenye matumbawe, huwezesha kuwa na<br />
mfumo mzuri wa mahusiano kibaologia (mahusiano yenye kufaidiana)<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 14
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
7. Mambo Unayopaswa na<br />
Usiyopaswa Kufanya Baharini<br />
7.1 Utangulizi<br />
Kutokana na kuongezeka kwa mahitaji ya maliasili za baharini kwa upande mmoja na<br />
haja ya matumizi endelevu kwa upande mwingine, kuna haja ya kuwa na njia salama<br />
za matumizi ya maliasili hizo. Kwa hiyo kila mdau analazimika kufahamu yampasayo<br />
na yasiompasa kufanya anapokuwa kwenye mazingira ya bahari. Taratibu zifuatazo<br />
zinapaswa kuzingatiwa na wadau wote, kwa nia ya kutunza mazingira na usalama<br />
binafsi, izingatiwe kuwa hizi ni sehemu tu ya taratibu zinazopaswa kuzingatiwa.<br />
7.2 Unapaswa<br />
• Kujua hali ya hewa kabla ya kwenda baharini<br />
• Uwe mwangalifu kwenye matumbawe<br />
• Kutia nanga mchangani<br />
• Kuchukua uchafu nyumbani<br />
• Kuacha matumbawe na vitu vingine kama ulivyovikuta<br />
• Kuipenda bahari na maliasili zake na kuzitunza<br />
7.3 Hupaswi<br />
• Kuogelea kwenye tufani, mawimbi makali au upepo mwingi<br />
• Kwenda kuzamia au kuogelea peke yako<br />
• Kuyasumbua au kuyachukua matumbawe au makombe (hai au Mafu)<br />
• Kugusa au kusimama kwenye matumbawe<br />
• Kutia nanga kwenye matumbawe<br />
• Kusababisha uchafuzi wa bahari<br />
• Kuvuna rasilimali yoyote kupita kiasi<br />
• Kutumia madawa ya aina yoyote baharini<br />
• Uvuvi wa kupita kiasi<br />
• Kuchimba mchanga pwani / ufukweni<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 15
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
• Kukata mikoko hovyo na kuchimba chambo kwenye mikoko<br />
7.4 ACHA!<br />
Kufanya shughuli yoyote inayoharibu mazingira ya bahari!<br />
7.5 ANZA!<br />
Kutumia njia salama kuvuna rasilimali za baharini ili kuhifadhi mazingira yake kwa<br />
ajili ya vizazi vijavyo.<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 16
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
8. Tishio Linaloyakabili Mazingira<br />
ya Bahari<br />
8.1 Utangulizi<br />
Maeneo ya bahari muhimu na yanayokabiliwa na tishio la uharibifu mkubwa ni<br />
mwamba wa matumbawe, mikoko, nyasi za baharini na maeneo ya maji kupwa na<br />
kujaa. Maeneo haya yanauhusiano wa kibaologia. Maeneo haya si muhimu tu kwa<br />
viumbe waishio baharini lakini pia ni muhimu kwa binadamu na hasa wakazi waishio<br />
pembezoni mwa bahari ambao uchumi na maisha yao hutegemea rasilimali za bahari.<br />
Hivyo kuna ulazima wa kuhifadhi mazingira ya bahari na maliasili zake.<br />
Tishio linalokabili mazingira ya bahari laweza kugawanywa sehemu mbili, tishio<br />
asilia na tishio linalotokana na binadamu.<br />
8.2 Tisho asilia linalohat arisha mazingira ya bahari<br />
1. Kiti cha Pweza chenye miiba (Acanthaster planci)<br />
Aina hii ya samaki ni hatari sana na hupatikana kwa wingi katika bahari ya pasifiki.<br />
Viumbe hivi chakula chao kikuu ni matumbawe, mara nyingi husababisha eneo<br />
kubwa la mwamba wa matumbane kuathirika na hata wakati mwingine kufa.<br />
2. Magonjwa<br />
Ugonjwa kama vile ‘blackland’ huvamia matumbawe na kuyabadilisha rangi yake na<br />
hata kuyaua kabisa.<br />
3. Matumbawe meupe<br />
Husababishwa na kuongezeka kwa jotoridi la maji ambapo mimea inayoishi na<br />
matumbawe hupoteza rangi na hivyo hushindwa kuzalisha chakula, hali hii hupelekea<br />
matumbawe kufa.<br />
4. Tufani na mawimbi yaendayo kasi<br />
Husababisha matumbawe, majani ya baharini, na mizizi ya mikoko (vikua) kufunikwa<br />
na takataka zinazotuama ambazo huathiri ukuaji, taka hizi zinapoongezeka huweza<br />
kusababisha vifo.<br />
8.3 Tishio linalotokana na binadamu<br />
1. Matumizi ya njia mbaya za uvuvi<br />
Uvuvi si lazima uwe mbaya na tishio kwa usalama wa mazingira ya bahari hasa<br />
unapokuwa katika hatua ya kuwa endelevu. Matatizo yanaweza kusababishwa na<br />
uvuvi wa kupita kiasi na kuvua samaki wachanga ambao ni tegemeo la baadaye. Aina<br />
zifuatazo za uvuvi ni tishio kubwa kwa mazingira ya bahari.<br />
- uvuvi wa kokolo / Juya<br />
- uvuvi wa mabomu / milipuko<br />
- uvuvi wa kigumi / neti za kojani<br />
- uvuvi wa sumu<br />
Njia hizi za uvuvi zinapaswa kuepukwa na kupingwa na kila mtu mwenye mapenzi<br />
mema na rasilimali za bahari na vizazi vya baadae.<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 17
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
2. Utupaji taka / uchafuzi<br />
Uchafuzi huathiri viumbe vya bahari na mazingira yao. Takataka nyingi ni sumu<br />
kama vile mafuta, uchafu wa majumbani, takataka na mabaki ya kwenye vyombo vya<br />
usafiri.<br />
3. Utiaji nanga<br />
Huharibu matumbawe, mara nyingi ni kutoka kwenye vyombo vya uvuvi na uzamiaji.<br />
Waweza kuzuia uharibifu kwa kuwa na vifaa vya kutilia nanga vinavyoelea au kuwa<br />
waangalifu wakati wa utiaji nanga.<br />
4. Wazamiaji<br />
Wasipokuwa waangalifu huweza kuharibu na hata kuua viumbe na mazingira ya<br />
baharini hasa kwenye mwamba wa matumbawe. Wazamiaji wanapaswa kuelimishwa<br />
juu ya uzamiaji salama.<br />
5. Biashara ya makome, makunguju, mabaragumu na makombe.<br />
Viumbe hawa wakiwa hai au wafu ni mapambo yanayopendwa. Lakini wokotaji wa<br />
vitu hivi waweza kuharibu mfumo wa usawa baharini, ni kwa sababu viumbe hivi<br />
huoza na kutengeneza miamba au mchanga wa ufukweni. Kama makombe mafu na<br />
matumbawe vitaondoshwa utengenezaji wa mchanga utasitika na kama makombe na<br />
matumbawe hai vitaondolewa viumbe wengine wataathirika pia kwa kukosa ama<br />
chakula au makazi.<br />
6. Ukataji mikoko hovyo<br />
Ukataji hovyo mikoko ni hatari sana kwa vile huharibu mandhari ya fukwe zetu,<br />
mazalio na makulio ya samaki. Mikoko pia huzuia mmonyoko wa ardhi na kuzuia<br />
uchafu kutoka nchi kavu kuyafikia matumbawe. Hivyo tunapaswa kuitunza mikoko<br />
na kuitumia kwa uangalifu.<br />
Hivyo ni jukumu la wadau kutumia rasilimali na mazingira ya bahari kwa<br />
uangalifu mkubwa ili kupunguza na hatimaye kuzuia kabisa tishio<br />
linaloyakabiri mazingira ya bahari.<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 18
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
SEHEMU YA PILI<br />
Shughuli zinazofanyika wakati wa<br />
ufundishaji<br />
1. Masanamu ya kuchorwa<br />
2. Kusanifu matangazo (mabango)<br />
3. Chemsha bongo ya elimu ya mazingira<br />
4. Mchezo wa taa za barabarani<br />
5. Kusema hapana kwa takataka<br />
6. Mfumo wa ushirikiano wa chakula – 1<br />
7. Mfumo / mtandao wa chakula (Uhusiano wa<br />
viumbe) 2<br />
8. Matembezi ya nyika hai<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 19
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
1. Masanamu ya kuchorwa<br />
1.1 Utangulizi<br />
Masanamu ya kuchorwa huwa ni mapambo yenye mvuto mkubwa kwa jamii, kama<br />
yakibuniwa vizuri huweza kuwa njia bora ya kufikisha ujumbe kwa jamii husika.<br />
Uhusiano wa maumbo na mazingira halisi ni muhimu sana ili kuleta mvuto na hisia<br />
juu ya ujumbe uliopo hivyo ni muhimu kuyazingatia haya wakati wa usanifu.<br />
1.2 Nini cha kufanya<br />
Sehemu ya kuweka masanamu inapaswa kuchunguzwa kabla ya ubunifu wa mchoro.<br />
Baada ya hilo sanamu inaweza kubuniwa na kuchorwa kwenye kuta za pembeni za<br />
skuli kwenye maeneo yanayoonekana kirahisi au katika kuta za zege vijijini. Kitu cha<br />
kuzingatia ni rangi zinunuliwe mapema na ziwe zinazoelekeana na aina ya mchoro,<br />
eneo unapochorwa na ujumbe uliokusudiwa.<br />
1.3 Vifaa<br />
Rangi za kawaida zinazotumika majumbani pamoja na vipakio, karatasi na kalamu<br />
1.4 Usanifu<br />
Chora mchoro kwenye karatasi ndogo na upake rangi, hii itawezesha tatizo lolote la<br />
mchoro kujulikana na kufuatiliwa mapema. Pia mchoro huo waweza kutumika kama<br />
mfano siku ya uchoraji mkubwa.<br />
1.5 Mawazo ya kisanifu<br />
Mchoro unaweza kuonyesha muonekano wa ndani ya maji, jinsi ya kutunza mazingira<br />
yanayoizuinguka jamii husika, Jambo lolote la kiulimwengu kama vile ukataji miti<br />
hovyo, viumbe vilivyo hatarini kupotea n.k. Mchoro unapaswa uwe na ujumbe wa<br />
kuihimiza jamii husika kuwa na mwelekeo wa kutunza mazingira.<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 20
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
2. Kusanifu matangazo (mabango)<br />
2.1 Lengo<br />
Kuwafanya washiriki kufikiria juu ya hali ya mazingira na jinsi wao binafsi<br />
wanavyoweza kuathirika. Kujenga mawazo juu ya mambo / mafunzo ya kila siku,<br />
kutoa mawazo yao katika usanifu kupitia vitabu, usanifu binafsi husaidia kujenga<br />
mawazo juu ya tangazo lililobuniwa. Kama unataka kazi hii iwe ni yenye mafanikio,<br />
hakikisha kuwa kuna mada rasmi itakayotoa ujumbe unaoonekana kwenye tangazo na<br />
washiriki wapewe nafasi ya kuchangia mawazo. Mfano ni matatizo gani yanayokabili<br />
mazingira ya bahari ama ni jinsi gani ukanda wa pwani unaweza kuhifadhiwa /<br />
kutunzwa. Toa nafasi ya majadiliano kwa kila mmoja kushiriki.<br />
2.2 Vifaa<br />
Karatasi<br />
Penseli / kalamu za rangi / rangi<br />
Maelezo ya kufuatisha<br />
2.3 Jinsi ya Kufanya<br />
Ruhusu washiriki kuunda mawazo ya kibunifu kwa kupitia vitabu. Mada<br />
ikishapatikana ubunifu waweza kuanza na baada ya kumaliza jadili na wabunifu<br />
kilichomo ndani ya mabango yao na wanategemea watu watapata tafsiri gani.<br />
2.4 Mawazo muhimu<br />
Ili kufanya mchezo wenye faida weka mada maalum ambayo washiriki watapaswa<br />
kuijadili. Kwa mfano kuna msukumo gani kwenye mazingira na namna gani fukwe<br />
zinaweza kutunzwa. Ruhusu mjadala ili kupata mlolongo wa maelezo. Kisha ruhusu<br />
washiriki kubuni mabango yenye ujumbe unaoendana na yaliyojadiliwa.<br />
2.5 Mawazo ya ziada<br />
Unaweza kuonyesha mchezo wa “coat of arms”. Wagawanye washirki katika<br />
makundi matatu, moja liwe picha zinazoonyesha mazingira yaliyoathirika, jingine<br />
picha zinazoonyesha vitu vilivyo sababisha uharibifu na la mwisho picha<br />
zinazoonyesha jinsi ya kubadilisha uharibifu wa mazingira uliotokea.<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 21
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
3. Chemsha bongo ya elimu ya<br />
mazingira<br />
3.1 Utangulizi<br />
Ni vizuri washiriki wakapewa changamoto juu ya uelewa wao. Kuwapa elimu / ujuzi<br />
kutahakikisha kuwa mawazo yanajengeka na kuimarika. Chemsha bongo ya<br />
mazingira yaweza kuhusisha mambo mapya au ya zamani. Kuwapa nafasi washiriki<br />
kwa uhuru zaidi bila hofu itarahisisha kujifunza na kukumbuka. Chemsha bongo<br />
yaweza kufanyika mara nyingi iwezekanavyo ili kukuza ufahamu juu ya mazingira.<br />
3.2 Lengo<br />
Kushirikisha timu zote kwenye mchezo hivyo kwanza unaanzia kwenye kona ya<br />
kwanza ya mbao kisha unaendelea mpaka mwisho. Kila sehemu ya mchezo ni lazima<br />
swali lijibiwe sawia ili kuendelea mbele na ili ujumbe uweze kuzingatiwa.<br />
3.3 Vifaa<br />
• daisi ya koro koro<br />
• ubao mpana<br />
• maswali<br />
• kalamu / rangi<br />
3.4 Jinsi ya kufanya<br />
Utengenezaji wa mchezo<br />
• Tengeneza ubao mdogo wenye vyumba (Mraba) toka mwanzo na hata mwisho<br />
(kama drafti)<br />
• Andika kwenye vyumba hivyo umepotea au rudi nyuma hatua moja, hii<br />
itauchangamsha mchezo<br />
• Wape vikadi kila timu zenye maumbo ya samaki au wanyama<br />
• Andaa maswali yanayoendana na umri wa washiriki<br />
Jinsi ya kucheza<br />
• Gawanya timu katika makundi mawili kisha weka hesabu zote mwanzo<br />
• Chagua timu inayoanza na uliza swali, jibu sahihi litapelekea timu hiyo kurusha<br />
daisi na kusonga mbele kwa nafasi zilizoamuliwa<br />
• Kuelekea kwenye mraba timu inapaswa kusubiri timu nyingine kujibu swali<br />
kwanza<br />
• Kama itatoa jibu sahihi itarusha pia daisi na kusonga mbele nafasi sawia<br />
• Kwa hiyo mchezo utaenda timu ya kwanza na kuendelea mbele na nyuma<br />
• Swali lisipopata jibu sahihi timu hairushi daisi na haisongi mbele, lazima wasubiri<br />
mzunguko wa pili<br />
3.5 Mawazo muhimu<br />
Hakikisha kuwa unazingatia amri za Umekosea na urudi nyuma hatua moja<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 22
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
3.6 Mawazo ya ziada<br />
Maswali yatoke kwenye mada tofauti kama vile, tishio, hatari, rasilimali, na wadau<br />
wa mazingira ya bahari. Vikadi vya maswali na miraba vipake rangi kiasikwamba<br />
mada husika, swali na mraba wake vifanane. Kwa mfano kama kadi ya swali la tishio<br />
linalokabili mazingira ya bahari ina rangi nyekundu, hili ndilo swali inabidi lijibiwe<br />
kama daisi itatua kwenye mraba wa rangi hiyo katika ubao.<br />
3.7 Maswali ya chemsha bongo<br />
S Taja aina moja ya uvuvi mbaya<br />
J Mabomu, Sumu, Kokolo<br />
S<br />
J<br />
S<br />
J<br />
S<br />
J<br />
S<br />
J<br />
S<br />
J<br />
S<br />
J<br />
S<br />
J<br />
S<br />
J<br />
S<br />
J<br />
Taja njia za uvuvi salama<br />
Madema, Ndoana<br />
Kwa nini watu wakitaka kutupa nanga lazima kuwa waangalifu<br />
Nanga inaweza kuharibu matumbawe<br />
Kipi chaweza kuoza haraka – Plastiki au bati<br />
Bati, Plastiki, huchukua miaka mingi sana kuoza na ikichomwa moto<br />
huongeza. Madawa yenye sumu hewani<br />
Kwanini hairuhusiwi kuokota kome ufukweni au kwenye matumbawe<br />
Zinapooza hutengeneza mchanga ambao ni muhimu katika kuweka hali nzuri<br />
ya fukwe, pia kome ni nyumba za baadhi ya viumbe kama vile kaa na pweza<br />
Kwanini hushauriwa kuweka bidhaa zote kwenye mfuko mmoja wa<br />
plastiki, na Kuutumia tena mfuko huo huo<br />
Kupunguza idadi ya mifuko ya plastiki, inamaana kupunguza uchafu kwenye<br />
makazi. Kutumia tena ule wa mwanzo itamaanisha kupunguza zaidi hivyo<br />
mazinira safi<br />
Kama una takataka na huna kwa kuzitupa, je utazitupa baharini<br />
Utatupa chini Au Utaweka mfukoni<br />
Utaziweka mfukoni hadi ukute shimo la taka<br />
Taja vitu vitano visivyotakiwa kuachwa kwenye ufukwe<br />
Plastiki, Vioo, Nyuma na taka kwa ujumla<br />
Mikoko inaisadiaje matumbawe<br />
Kwa kuzuia uchafu unaotoka nchi kavu usiyafikie matumbawe<br />
Kwa nini ni muhimu kwa wanabiologia ya bahari na wataalamu wa uvuvi<br />
Kuzungumza na maofisa wa uvuvi kujua aina na kiasi cha samaki<br />
kinachovuliwa <br />
Kuhakikisha kuwa aina fulani ya samaki haipotei kwa kuvuliwa sana, pia<br />
kujua kiasi Kilichopo na kilichovuliwa kutasaidia kumonita wavuvi<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 23
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
S<br />
J<br />
S<br />
J<br />
S<br />
J<br />
S<br />
J<br />
S<br />
J<br />
S<br />
J<br />
Kwanini hupaswi kununua kombe dukani<br />
Kombe wanaopatikana dukani ni wale waliochukuliwa toka kwenye<br />
Matumbawe wana uhusiano wa kibaolojia na matumbawe na viumb wengine.<br />
Hivyo kupungua kwa kombe kwaweza kuathiri ukuaji wa matumbawe<br />
Taja umuhimu wa majani ya baharini<br />
Huzuia mmomonyoko wa udongo hivyo huyalinda matumbawe, pia<br />
huwaficha samaki wadogowadogo wasiliwe na wakubwa<br />
Weka mpangilio huu wa chakula kwenye mnyororo kiti cha pweza<br />
chenye miiba, Binadamu ,baragumu , pweza na matumbawe<br />
Matumbawe – kiti chwa pweza chenye miiba- baragumu – pweza –binadamu<br />
Kwanini Elimu ya mazingira ni muhimu sana<br />
Elimu ya mazingira hutueleza jinsi tunavyoweza kuyatunza na kuyahifadhi<br />
mazingira yetu hivyo kurefusha maisha pia hufundisha madhara<br />
yatakayotokea tusipotunza mazingira<br />
Je mtu mmoja anaweza kuleta mabadiliko kwenye mazingira<br />
Ndiyo<br />
Taja njia tatu zinazoharibu matumbawe<br />
Utalii<br />
Ukusanyaji Kome<br />
Uzamiaji<br />
Utupaji nanga<br />
Uvuvi- nanga, mabomu, kigumi, sumu na uvuvi wa kutumia neti zenye<br />
matundu madogo sana (kojani nets)<br />
Sababu asilia – tufani na mawimbi makali<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 24
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
4. Mchezo wa taa za barabarani<br />
4.1 Lengo<br />
Kupima kumbukumbu za washiriki juu ya mambo waliojifunza siku za nyuma na siku<br />
ya mazingira. Pia kupima ufahamu wa mshiriki juu ya mazingira na uwezo wa<br />
kufikiria.<br />
4.2 Vifaa<br />
• Mifuniko mitatu ya plastiki ya duara (bluu, kijani, zambarau)<br />
• Karatasi na kalamu<br />
• Karatasi ngumu<br />
• Rangi (Njano, Kijani na Nyekundu)<br />
4.3 Jinsi ya kuandaa michezo<br />
• Tengeneza viboksi vidogo vitatu kwa kila kundi kwa kila kundi kimoja cha kijani,<br />
kimoja chekundu, na cha njano<br />
• Kijani – Salama / endelea<br />
• Nyekundu – hatari / zuia / acha<br />
• Njano – tahadhali / kuwa mwangalifu / tafakari<br />
• Kila kikundi huwa na viboksi vitatu vya aina zote<br />
• Tengeneza uwanja wa michezo ambao huwa na umbo la mraba, katikati huwekwa<br />
mifuniko mitatu ya duara yenye rangi tofauti<br />
• Andaa karatasi yenye maelezo ambayo yanaendana na rangi za viboksi (hatari,<br />
Salama na tahadhari)<br />
• Washiriki waweza kuwa kwenye makundi manne au zaidi<br />
4.4 Jinsi ya kucheza<br />
• Kila kundi hukaa pembe yake umbali sawia toka katikati<br />
• Maelezo husomwa kisha mwamuzi hutoa sekunde kadhaa kwa makundi kuamua<br />
kama ni hatari, tahadhari au salama<br />
• Kisha kwa haraka humpa mshiriki mmojawapo kisanduku husika, mwamuzi<br />
huhesabu moja, mbili, tatu – goo! kwa haraka mshiriki toka kila kundi atakimbia<br />
kuweka kisanduku katikati. Atakayeweka kwenye mfuniko wa bluu kisanduku<br />
sahihi kundi lake litapata alama tatu, kwenye kijani alama mbili na kwenye<br />
zambarau alama moja wa nne atapata sifuri kwa kuchelewa. Alama hutolewa kwa<br />
jibu sahihi tuu<br />
• Kama kuna mgongano wa majibu mwamuzi ataruhusu mjadala kidogo na kutoa<br />
jibu sahihi<br />
• Aina ya maelelezo itategemea rika ya washiriki<br />
• Badili nafasi ya mifuniko ktk kila baada ya swali moja<br />
4.5 Mawazo ya Ziada<br />
Endelea na sentensi zingine na fikiria ambazo zinaendana na rika na kiwango na<br />
uelewa wa washiriki na topiki inayofundishwa, waweza pia kutoa zawadi kwa<br />
washindi, zaweza kuwa vifaa vya shule na vitabu vya mazingira.<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 25
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
Team A<br />
Team B<br />
Rotate lids regularly<br />
Judge<br />
3 points 2 points<br />
Reader<br />
1 point<br />
Team D<br />
Referee<br />
Team C<br />
4.6 Mfano wa maelezo na majibu yake<br />
1. Kukata mikoko ovyo – Nyekundu<br />
2. Shughuli za uvuvi – Njano<br />
3. Utupaji taka – Njano<br />
4. Kukata miti ovyo – Nyekundu<br />
5. Kutumia mifuko ya plastiki ni kuzuri – Myekundu<br />
6. Kutia Nanga – Njano<br />
7. Uzoaji wa mchanga ufukweni – Nyekundu<br />
8. Umwagaji wa mafuta baharini – Nyekundu<br />
9. Utafiti wa kisayansi – Njano<br />
10. Kufanya kazi na <strong>Frontier</strong> – Kijani<br />
11. Kuchoma mkaa – Njano<br />
12. Kupandikiza mikoko – Kijani<br />
13. Ujenzi wa vituo vya Utalii – Njano<br />
14. Kuokota kome ufukweni – Nyekundu<br />
15. Uchomaji matumbawe kutengeneza chokaa – Nyekundu<br />
16. Uvuvi wa mabomu – Nyekundu<br />
17. Mbuyu ni aina mojawapo ya mikoko – Nyekundu<br />
18. Majani baharini si muhimu – Nyekundu<br />
19. <strong>Tanzania</strong> na Uingereza ni marafiki – Kijani<br />
20. Chips mayai ni chakula kizuri – Yeyote<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 26
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
5. Kusema hapana kwa takataka<br />
5.1 Utangulizi<br />
Ingawa kumekuwa na mambo mengi yanayoathiri mazingira lakini ni vigumu kujua<br />
ni lipi kati ya hayo litakuathiri wewe binafsi. Pia katika sehemu nyingi duniani watu<br />
hawana nguvu ya kutatua matatizo hayo kutokana na ukosefu wa fedha au kipato<br />
kidogo. Lakini pamoja na hilo watu ulimwenguni kote hushiriki katika matumizi ya<br />
bidhaa zinazosababisha uchafu kwa kiwango tofauti. Kwa mfano nchi nyingi hutumia<br />
mifuko ya plastiki kubebea mahitaji na hata kuhifadhi bidhaa. Baada ya kutumia<br />
mifuko hairudiwi tena bali hutupwa mbali kama uchafu. Plastiki, makopo, vioo na<br />
vyuma vyaweza kuwa hatari kwa watu na kuweza kuua wanyama kwa<br />
kuwasababishia vidonda au kwa kuvimeza.<br />
Katika nchi nyingi uzoaji wa taka ni kidogo kutokana na njia za usafiri kuwa duni.<br />
Kutokana na wakazi wengi huzichoma takataka na kuzifukia chini.<br />
Hii yaweza kuwa nzuri kwa vile inasaidia kupunguza taka lakini yaweza kuongeza<br />
tatizo watu wasipokuwa makini.<br />
Kama watu watatumia mifuko ya plastiki ile ile kwa kuikataa mipya inapokuwa si<br />
muhimu kuwa nayo, idadi ya plastiki na uchafu kwa ujumla waweza kupungua<br />
kwenye makazi. Na juu ya hili kama wanunuzi wa bidhaa watakuwa waangalifu na<br />
kuwa makini na wenye kiasi kwenye ununuzi wa bidhaa ingeweza kupunguza kasi ya<br />
uongezekaji wa taka kwenye makazi ya watu na wanyama. Kuwafahamisha watu juu<br />
ya nguvu waliyonayo juu ya taka kwa kuwahusisha katika mazoezi rahisi inaweza<br />
kusaidia watu kufikiria juu ya uwajibikaji.<br />
5.2 Lengo<br />
Andaa / buni eneo la mikoko lenye taka, Washiriki wanapaswa kutembea kutoka kiti<br />
kimoja hadi kingine bila ya kugusa ardhi kwa msaada wa daraja la mbao,<br />
wakikusanya taka na kuziweka kwenye pipa. Mchezo huu ni kama kituko lakini watu<br />
wanaweza kuulizwa kwamba wana maoni / hisia gani juu ya taka, kuufanya mchezo<br />
uwe mzuri zaidi. Pia hutakiwa kuelezea uchafu unaharibu mazingira yao kwa kiasi<br />
gani.<br />
Maoni yaweza kutolewa mwishoni mwa mchezo ni kwa jinsi gani mazingira mazuri<br />
yanaweza kufanywa na jinsi gani ya kuwa wawajibikaji.<br />
5.3 Vifaa<br />
• Viti 6-7<br />
• Mbao mbili<br />
• Pipa la taka<br />
• Karatasi<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 27
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
5.4 Jinsi ya kufanya<br />
• Kabla ya hapo tengeneza bango linaloonyesha madhara ya taka zinapokuwepo na<br />
jingine linaloonyesha faida za taka kutokuwepo ili iwasaidie washiriki kuelewa.<br />
Mfano wa madhara ya taka, kuchomwa plastiki huongeza kemikali zenye sumu<br />
hewani, taka ndogo zikimezwa na wanyama huwa hatari na pia taka hazipendezi<br />
kuziona. Faida za kutokuwa na taka ni pamoja na makazi safi ya kuishi, hali safi<br />
ya hewa na maisha salama<br />
• Tafuta eneo zuri la kuweka msitu wa kubuni wa mikoko<br />
• Panga viti vizuri ili kuruhusu washiriki kuweka mbao juu yake na kutembea<br />
upande mmoja hadi mwingine<br />
• Sambaza takataka kwa washiriki kuokota<br />
• Toa muda maalum kwa muokota taka kumaliza eneo lote la mikoko<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 28
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
6. Mfumo wa ushirikiano wa<br />
chakula – 1<br />
6.1 Utangulizi<br />
Viumbe hai wote wanauhusiano wa mzunguko wa nishati. Uhusiano huo hujulikana<br />
kama mfumo / mtandao wa ushirikiano wa chakula. Mimea iko chini / ngazi ya<br />
kwanza ya mfumo huo kama wazalishaji wa msingi. Kwa upande mwingine wanyama<br />
walao mimea wako katikati na juu yao ni wale wanyama walao nyama. Kutokana na<br />
kwamba wala nyama hula wanyama wenzao ambao wengi wao hula mimea, kuna<br />
usawa kati yao ambao huweza kuathiriwa na binadamu. Kwa mfano, idadi ya<br />
baragumu huongezeka haraka kukiwa na hali nzuri ya kimazingira, hivyo samaki<br />
wawalao pia huongezeka, lakini samaki wakiongezeka kupita kiasi hupelekea idadi ya<br />
baragumu kupungua na hivyo samaki wawalao pia huathirika.<br />
Wakazi wa pwani hutegemea samaki kwa mlo kamili na kujipatia kipato. Uvuvi<br />
mdogo mdogo hauna athari kwa mtandao wa chakula. Lakini uvuvi ukiongezeka sana<br />
kupita kiasi cha samaki basi samaki hao wataanza kupungua. Kupungua huko kwa<br />
samaki kunaweza kuathiri viumbe wengine.<br />
6.2 Lengo<br />
• Kujenga uelewa juu ya uhusiano kati ya Viumbe<br />
• Washiriki kuelewa madhara ya moja kwa moja na yasiyo ya moja kwa moja<br />
yanayoweza kusababishwa na binadamu kwenye mazingira baharini<br />
6.3 Jinsi ya kufanya<br />
• Buni mifumo / Mtandao wowote wa chakula (tumia mfumo huo hapo chini)<br />
• Uchore mfumo huo tayari kwa majadiliano<br />
• Tayarisha vipande vya karatasi zenye picha ya vitu vyote / viumbe vilivyoko<br />
kwenye mfumo huo<br />
• Mpe kila mshiriki picha / Mchoro kisha jadili mtandao / mfumo huo wa chakula<br />
na mahusiano kila kiumbe na chenzie<br />
• Washiriki wawe katika duara wakielekeaa upande mmoja na nyuso zao katikati<br />
• Athari zitokanazo na binadanu ziwe nje ya duara<br />
• Washiriki wajivute ndani ya duara na wakaribiane kiasi cha kutegemeana. Hili<br />
huitaji mazoezi<br />
• Mshiriki anayehusisha madhara yatokanayo na binadamu atamvuta mmoja wao<br />
kwa nguvu na kumwondoa kwenye duara, hilo litasababisha duara zima<br />
kuharibika.Hii huonyesha kitu halisi kinachoweza kutokea kwenye mtandao wa<br />
chakula<br />
• Hii ni njia rahisi kwa mshiriki kuona jinsi gani mfumo mzima na mtandao wa<br />
chakula huweza kubomoka kabisa ukiathiriwa na kitu chochote toka nje<br />
• Unaweza kurudiwa mara nyingi ili kutilia mkazo ujumbe uliopo. Kuhitimisha<br />
washiriki wanaweza kujadili kwa mjumuisho juu ya maada husika na<br />
kuzungumzia shughuli zozote wazifanyazo kila siku zenye athari kwenye mfumo<br />
mzima wa mtandao wa chakula<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 29
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 30
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
7. Mfumo/mtandao wa chakula<br />
(Uhusiano wa viumbe) 2<br />
7.1 Lengo<br />
• Kukuza ufahamu juu ya mahusiano ya viumbe hai na mazingira yao<br />
• Kuonyesha / kujifunza athari zitokanazo na binadamu kwenye mazingira haya<br />
7.2 Vifaa<br />
• Kalamu za kawaida na za rangi<br />
• Karatasi aina ya A4<br />
• vijiboksi vidogo (4 kwa kila kiumbe)<br />
• Karatasi aina ya A1 moja au mbili<br />
7.3 Jinsi ya kuandaa<br />
• Buni mfumo / mtandao wa chakula na uchole kwenye karatasi kubwa aina ya A1<br />
bila ya kuonyesha majina ya viumbe husika, ambayo yanaweza kuwakilishwa na<br />
namba<br />
• Chora picha zinazoelekeana na mchoro huo hapo juu kwenye karatasi au viboksi<br />
• Kama washiriki ni wengi wagawe kwenye makundi ya watu 4 au 5<br />
7.4 Jinsi ya kufanya<br />
• Tundika mchoro mkubwa kwenye ubao unakoweza kuonekana na kila mmoja<br />
• Wagawie wanafunzi picha<br />
• Kwa kujadiliana wape nafasi wanafunzi kuamua picha ipi inaelekeana na namba<br />
ipi kwenye mchoro<br />
• Baada ya kukamilisha upangaji wa picha zote kwenye mchoro jadiliana na<br />
wanafunzi madhara ya kuiharibu sehemu mojawapo katika mchoro huo<br />
• Husianisha mjadala na mazingira halisi na jadili shughuli zifanywazo na<br />
binadamu zinazoweza kuathiri mfumo huo<br />
7.5 Kwenye mchoro wa mfano ulioonyeshwa hapo chini namba zinawakilisha<br />
1. Papa – mla nyama<br />
2. Mcheche – mla nyama<br />
3. Ndege wa baharini<br />
4. Pweza – mla nyama<br />
5. Samaki – Kipepeo<br />
6. Samaki – Tembo<br />
7. Baragumu<br />
8. Kiti cha pweza chenye miiba<br />
9. Kamba<br />
10. Matumbawe<br />
11. Ufuma / ulumba<br />
12. Mwani<br />
13. Majani<br />
14. Majani ya baharini<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 31
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
7.6 Mawazo ya ziada<br />
Tumia viboksi kuonyesha mabadiliko ya usawa wa mfumo mzima. Weka viboksi 2<br />
katika kila hatua kwenye mchoro. Kisha waweza punguza kimoja sehemu mojawapo<br />
hii itapelekea kupungua kwa idadi ya viumbe husika na kuongezeka kwa viumbe<br />
walioko chini zaidi ya mfumo huo hivyo yaweza kuathiri mfumo mzima.<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 32
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
1<br />
2 3<br />
4<br />
5 6<br />
7 8<br />
9<br />
10 11<br />
12<br />
13<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 33
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
8. Matembezi ya nyika hai<br />
8.1 Utangulizi<br />
Unapofundisha ni muhimu kutumia rasilimali zote zilizopo na zinazofikika.<br />
Kutembea na kuangulia mazingira yaliyopo huleta hamasa zaidi kwa ulimwengu huu<br />
wa kushangaza. Kujifunza toka kwenye mazingira halisi zaidi kuliko kwenye vitabu<br />
humwezesha mwanafunzi yeyote kuielewa hali ilivyo na kukubaliana na mazingira<br />
hayo kwa moyo wa dhati.<br />
Kwa mfano mikoko huweza kuonekana kwa haraka haraka kama mimea isiyo na<br />
faida hivyo hutumika tu hovyo hovyo bila kujali, lakini ukichunguza kwa uangalifu<br />
zaidi utagundua kuna idadi kubwa ya viumbe kama vile ndege, kaa, kamba, kome na<br />
vinginevyoo vilivyojizoesha kuishi kwenye mazingira haya magumu ya mikoko.<br />
Hakikisha wanafunzi wanapata muda na nafasi ya kutosha kujifunza kwenye<br />
mazingira halisi na pia ruhusu maswali.<br />
8.2 Lengo<br />
• Kuelewa jinsi viumbe vinavyoishi katika mazingira yake na binadamu<br />
anavyoweza kuathiri mfumo huo. Kujifunza darasani mara nyingi humaanisha<br />
kuelewa tu bila kukubaliana na hali halisi kwenye mazingira husika<br />
• Kwa kuzungukwa na mazingira asilia yanayotumika kujifunza hurahisisha<br />
ufundishaji na kuwawezesha washiriki kupata ujumbe kirahisi. Kuweza kuona<br />
jinsi mshabihiano laini wa viumbe na mazingira yao ulivyo yaweza kukazia<br />
uelewa unaoendana na uwajibikaji kwa jinsi ambavyo binadamu anaathiri viumbe<br />
hivyo, hivyo kubadili mwelekeo<br />
8.3 Jinsi ya kufanya<br />
• Orodhesha mifumo yote ya kimazingira inavyoweza kutembelewa ambayo<br />
binadamu anaathiri viumbe hai wake, kama vile mikoko, majani ya baharini na<br />
maeneo ya maji kupwa na kujaa<br />
• Chunguza ni lipi linaendena na mada ya siku husika<br />
• Panga ni jambo gani ni muhimu liangaliwe wakati wa kutembelea mahali hapo,<br />
kwa mfano unataka kuona athari ya binadamu kwenye msitu wa karibu au ndege<br />
waishio kwenye mikoko<br />
• Hakikisha kuna muda wa kujiandaa kwa washiriki juu ya maada husika, hii<br />
itarahisisha matembezi hayo<br />
• Chukua kibeseni kipana cha kuangalizia wanyama na mimea midogo midogo na<br />
vifaa vingine muhimu, kutegemea na lililokusudiwa kuelekezwa<br />
Tafadhali hakikisha hakuna kiumbe chochote kitakachoumizwa na mara baada ya<br />
kujifunza kirudishwe kilipokuwa<br />
.<br />
8.4 Mahitaji muhimu<br />
• Vifaa vya utafiti na maendeleo juu ya mfumo mzima wa mazingira na viumbe hai<br />
unaotegemewa<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 34
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
8.5 Mfano<br />
Kutembelea msitu wa mikoko<br />
Mambo muhimu unayoweza kujifunza / kufundisha<br />
• Aina ya Mikoko iliyopo na mpangilio wake<br />
• Maeneo inapostawi mikoko baharini<br />
• Aina ya udongo ndani ya mikoko<br />
• Idadi ya mikoko kwenye eneo la mraba<br />
• Urefu na umri wa mikoko<br />
• Viumbe wengine waishio ndani ya mikoko<br />
• Aina mbalimbali za mizizi na inavyofanya kazi kuchuja uchafu na matamahuruku<br />
• Athari za binadamu kwenye mikoko<br />
• Kama imeathirika sana, waweza pia kufundisha upandikizaji wake na namna ya<br />
kufanya zoezi hilo kwa vitendo<br />
N.B<br />
kumbuka elimu kwa vitendo hutolewa ili kumwezesha mwanafunzi kuzingatia<br />
zaidi alivyojifunza, hivyo shirikisha zaidi wanafuzi katika vitendo. Kama<br />
mwalimu jiepushe kuhodhi mambo yote darasani.<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 35
Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />
Marejeo<br />
Collins Concise English Dictionary 2000 (1982) Harpers Collins Publishers, Great<br />
Britain.<br />
Eade, D and Williams, S. (1995) The Oxfam Handbook of Development and Relief<br />
Volume 1. Oxfam (UK and Ireland)<br />
Nybakken, J.W. (2001) Marine Biology: An ecological approach. 5 th Edition. Moss<br />
Landing. Addison Wesley Longman.<br />
Semesi, A.K., and Howell, K. (1989) The Mangroves of the East African Region.<br />
UNEP, Nairobi. 45pp.<br />
Semesi, A.K., Mgaya, Y.D., Muruke, M.H.S., Francis, J., Mtolera, M. and Msuni, G.<br />
(1998) Coastal resources utilization and conservation issues in Bagamoyo, <strong>Tanzania</strong>.<br />
Ambio Vol 27 No. 8:635-644. Royal Swedish Academy of Sciences. P635-644.<br />
10pp.<br />
<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 36