28.01.2015 Views

Frontier Tanzania Environmental Research REPORT 100

Frontier Tanzania Environmental Research REPORT 100

Frontier Tanzania Environmental Research REPORT 100

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

<strong>Frontier</strong> <strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong><br />

<strong>REPORT</strong> <strong>100</strong><br />

ELIMU YA MAZINGIRA YA BAHARI<br />

MUONGOZO WA MWALIMU<br />

<strong>Frontier</strong> <strong>Tanzania</strong><br />

February 2004


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

ii


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> Marine <strong>Research</strong> Programme<br />

<strong>REPORT</strong> <strong>100</strong><br />

Elimu ya mazingira ya bahari ya<br />

kitropiki<br />

Muongozo wa mwalimu<br />

Mumby, R., Fanning, E. Muruke, M. and St John, F. (eds)<br />

Kingereza Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mazingira Kiswahili<br />

Na Ushirika<br />

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibari<br />

Jumuiya ya Kuhifadhi Mazingira<br />

50-52 Rivingston Street<br />

London UK<br />

EC2A 3QP<br />

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam<br />

S. L. P. 35064<br />

Dar es Salaam<br />

<strong>Tanzania</strong><br />

Pemba 2004<br />

iii


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

Suggested Technical Report citation:<br />

<strong>Frontier</strong> <strong>Tanzania</strong> (2004). Marine environmental education: A Teacher’s Guide (Kiswahili). <strong>Frontier</strong><br />

<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong>. The Society for <strong>Environmental</strong> Exploration, London,<br />

UK, The University of Dar es Salaam, The Institute of Marine Science, Zanzibar, DfID Small Grants<br />

Scheme and the Ministry of Agriculture, Natural Resources, Environment and Co-operatives, Zanzibar.<br />

The <strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report Series is published by:<br />

The Society for <strong>Environmental</strong> Exploration<br />

50-52 Rivington Street<br />

London, EC2A 3QP<br />

United Kingdom<br />

Tel: +44 (0)20 7613 3061<br />

Fax: +44 (0)20 7613 2992<br />

Email: research@frontier.ac.uk<br />

Web Page: www.frontier.ac.uk<br />

ISSN 1479-1161 (Print)<br />

ISSN 1748-3670 (Online)<br />

ISSN 1748-5124 (CD-ROM)<br />

iv


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

© <strong>Frontier</strong> <strong>Tanzania</strong> 2004, 2005<br />

Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mazingira na Ushirika (MANREC)<br />

Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mazingira na Ushirika ni sehemu ya Serikali ya<br />

Mapinduzi ya Zanzibar. Idara ya Mazao ya Biashara, Matunda na misitu (DCCFF) ni<br />

sehemu ya wizara na inawajibika na muongozo wa uanzishaji wa sera ya misitu na<br />

maeneo tengefu, ikiwa ni pamoja na eneo tengefu la bahari la kisiwa cha Misali<br />

(MIMCA) visiwani Zanzibar.<br />

<strong>Frontier</strong> <strong>Tanzania</strong> (FT)<br />

<strong>Frontier</strong> <strong>Tanzania</strong> ni uhusiano kati ya shirika la kuchunguza mazingira na Chuo Kikuu<br />

cha Dar es Salaam. Shughuli za utafiti katika shirika hili zimeendelea tangu Julai 1989<br />

na zimehusisha watafiti toka <strong>Tanzania</strong> na nchi za nje. Utafiti unafanywa kwenye aina<br />

tofauti za mazingira yenye baolojia maalum na hadhi za uhifadhi. Maeneo<br />

yanayochunguzwa hujumuisha misitu, savana za kitropiki, uvuvi, miamba ya<br />

matumbawe, mikoko na nyasi za baharini.<br />

<strong>Frontier</strong> <strong>Tanzania</strong> Marine <strong>Research</strong> Programme (FT MRP)<br />

Huu ni mradi uliofanya utafiti wa kibahari, kisiwa cha Mafia (1989-1994), Songo<br />

Songo (1994-1995), na Mtwara (1996-2000). Mradi ulihamia Pemba ambayo ni<br />

sehemu ya Zanzibar mwaka 2001 ukilenga kisiwa cha Misali. <strong>Frontier</strong> <strong>Tanzania</strong><br />

inafanya kazi kwa kushirikiana na MANREC na Taasisi ya utafitu wa sayansi za bahari<br />

(IMS) katika utekelezaji wa shughuli zake.<br />

Chuo Kikuu cha Dar-es-salaam (UDSM)<br />

Chuo Kikuu cha Dar-es-salaam kilianzishwa Julai 1970 kama kitiuo cha mafunzo na<br />

utafiti katika sayansi za aina mbalimbali. Chuo kinatafiti mimea na wanyama wa<br />

<strong>Tanzania</strong> na kinafanya utafiti wa uimarishaji wa mazingira na matumizi endelevu ya<br />

maliasili za nchi.<br />

Shirika la kuchunguza mazingira (SEE)<br />

Shirika hili lilianzishwa mwaka 1989 na linafanya kazi isiyo ya kibiashara.<br />

Madhumuni ya Shirika hili ni kukuza, kuendeleza utafiti juu ya mazingira na<br />

kutekeleza miradi kwa vitendo itakayosaidia kuhifadhi mazingira na maliasili zake.<br />

Miradi iliyoanzishwa na kusimamiwa na Shirika hili hushirikisha pia wawakilishi wa<br />

kitaifa wa utafiti katika nchi husika.<br />

v


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

KWA MAWASILIANO ZAIDI<br />

Ministry of Agriculture Natural Resources<br />

Environment & Co-operatives<br />

P.O. Box 159, Zanzibar, <strong>Tanzania</strong><br />

Tel: +255 24 223 2840<br />

Fax: +255 24 223 0290<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong>: Head Quarters<br />

PO Box 9473, Dar es Salaam<br />

Tel: +255 22 2780 063<br />

Email: frontier@africaonline.com<br />

Department for Commercial Crops Fruits & Forestry<br />

PO Box 3526, Zazibar, <strong>Tanzania</strong><br />

Tel: +255 24 223 8628<br />

Fax: +255 24 223 6089<br />

Email: dccff@zanlink.com<br />

Dept. of Zoology & Marine Biology<br />

University of Dar es Salaam<br />

P.O. Box 35064, Dar es Salaam, <strong>Tanzania</strong><br />

Tel: +255 22 2410462<br />

E-mail: zoology@udsm.ac.tz<br />

The Institute for Marine Sciences<br />

University of Dar es Salaam<br />

P.O. Box 668, Zanzibar, <strong>Tanzania</strong><br />

Tel: +255 24 223 0741 / 2128 / 3472<br />

Fax: +255 24 223 3050<br />

Society for <strong>Environmental</strong> Exploration<br />

50-52 Rivington Street<br />

London, EC2A 3QP. U.K.<br />

Tel: +44 (0)20 7613 3061<br />

Fax: +44 (0)20 7613 2992<br />

E-mail: research@frontier.ac.uk<br />

Internet: www.frontier.ac.uk<br />

vi


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

Yaliyomo<br />

Utangulizi Kuhusu Elimu ya Mazingira na Muongozo Huu..............................ix<br />

Kwa nini tunataka Kuhifadhi Mazingira ya Bahari..........................................ix<br />

Maendeleo Endelevu..............................................................................................x<br />

Madhumuni ya FT MRP.......................................................................................xi<br />

Mpango wa Utafiti wa Bahari ..............................................................................xi<br />

Historia Ya FT MRP........................................................................................... xii<br />

SEHEMU YA KWANZA .......................................................................................1<br />

1. Utangulizi Kuhusu elimu ya mazingira ya bahari .........................................2<br />

2. Mikoko (Mikandaa) .........................................................................................3<br />

3. Eneo la maji kupwa na kujaa..........................................................................6<br />

4. Nyasi za Baharini ............................................................................................8<br />

5. Miamba ya Matumbawe.................................................................................10<br />

6. Uhusiano wa Mifumo ya Maisha ya Viumbe Hai Baharini........................13<br />

7. Mambo Unayopaswa na Usiyopaswa Kufanya Baharini ............................15<br />

8. Tishio Linaloyakabili Mazingira ya Bahari .................................................17<br />

SEHEMU YA PILI...............................................................................................19<br />

Shughuli zinazofanyika wakati wa ufundishaji..................................................19<br />

1. Masanamu ya kuchorwa................................................................................20<br />

2. Kusanifu matangazo (mabango)...................................................................21<br />

3. Chemsha bongo ya elimu ya mazingira........................................................22<br />

4. Mchezo wa taa za barabarani........................................................................25<br />

5. Kusema hapana kwa takataka ......................................................................27<br />

6. Mfumo wa ushirikiano wa chakula – 1 ........................................................29<br />

7. Mfumo / mtandao wa chakula (Uhusiano wa viumbe) 2.............................31<br />

8. Matembezi ya nyika hai .................................................................................34<br />

Marejeo .................................................................................................................36<br />

SHUKRANI:<br />

FT MRP inapenda kulishukuru shirika la kuchunguza mazingira (SEE) kwa kufadhili<br />

shughuli mbalimbali za Elimu ya Mazingira, wanafunzi na walimu walioshiriki<br />

katika shughuli hizo, kutoka skuli za Kangani, Fidel Castro na Mizingani, Wizara ya<br />

Elimu Afisi za Pemba hasa Mr Hussein (Afisa Kiongozi) kwa kutoa kibali cha<br />

kuendesha shughuli hizo. FT MRP pia inawashukuru Mr Ambakisye Simtoe kwa<br />

kuandaa shughuli za uelimishaji na kutafsiri muongozo huu, na Chuo Kikuu cha Dares-salaam<br />

kwa kusaidia shughuli za FT MRP za utafiti na watafiti wasaidizi wa kati<br />

ya mwaka 2001 na 2003.<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong><br />

vii


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

ACKNOWLEDGEMENTS<br />

This report is the culmination of the advice, co-operation, hard work and expertise of many<br />

people. In particular acknowledgments are due to the following:<br />

SOCIETY FOR ENVIRONMENTAL EXPLORATION<br />

Managing Director: Ms. Eibleis Fanning<br />

Programme Manager (Operations): Mr. Matthew Willson<br />

Programme Manager (<strong>Research</strong>): Ms. Nicola Beharrell<br />

Project Administration:<br />

Mr. Mike Lamb<br />

UDSM<br />

FT Co-ordinators:<br />

Dr. M. Muruke & Prof. K. M. Howell.<br />

FRONTIER-TANZANIA<br />

Project Co-ordinator: Ms. Carol Daniels<br />

<strong>Research</strong> Co-ordinator:<br />

Mr. Angus McVean<br />

Assistant <strong>Research</strong> Co-ordinators: Mr. Edward Mayhew, Ms. Ruth Mumby, Mr. Adam<br />

Pharoah<br />

<strong>Environmental</strong> Education Officer: Mr. Ambakisye Simtoe<br />

Dive Officer:<br />

Mr. Paulo Pizzolla<br />

Logistics Managers:<br />

Mr. Luke Gordon<br />

Boat Crew:<br />

Mr. Mussa Abdalah, Mr. Khashim Abdallah, Mr,<br />

Mzee Salum Seifu<br />

Security:<br />

Mr. Juma Mbaya Juma, Mr. Ali Osman Khamis, Mr.<br />

Sibouri Makame Kombo<br />

Cook:<br />

Mr. Ramadhani Juma Songoro<br />

<strong>Research</strong> Assistants:<br />

Ms. Alice Addison, Mr. Andrew Ashton, Ms.<br />

Katherine Barber, Mr. Matthew Bennett, Mr.<br />

Michael Brown, Ms. Hilary Cartwright-Taylor, Mr.<br />

Alasdair Cockburn, Ms. Charlotte Cranfield, Mr.<br />

Sharif Mohammed Faki, Mr. Christopher Faunce-<br />

Brown, Ms. Anna Franheim, Mr. Conrad Freese, Mr.<br />

Peter Nestory Gabagambi, Mr. Angus Galloway, Ms.<br />

Lydia Gaspare, Mr. Christopher Goatley, Ms.<br />

Eleanor Harrison, Ms. Jacqui Height, Mr. David<br />

Henderson, Ms. Frances, Ms. Lorraine Howe, Illsley,<br />

Ms. Louise Jary, Mr. Ben Jones, Mr. Ali Kitwana,<br />

Ms. Emilia Lascelles, Ms. Andrea Leedale, Ms.<br />

Helen Lofthouse, Mr. Edward Lousley, Mr. Chris<br />

Lovett, Ms. Christine McIntyre, Mr. Jacob Miller,<br />

Mr. Zahor Mohammed, Ms. Lauren Morgan, Mr.<br />

James Moss, Mr. Mathias Msafiri, Mr. Kevin<br />

Murphy, Ms. Olivia Palin, Mr. Adam Partington, Mr.<br />

Rashid Juma Rashid, Mr. David Roadknight, Mr.<br />

Andy Roddis, Mr. Peter Shunula, Mr. Julian Skeels,<br />

Ms. Rachael Smith, Ms. Eike Stubner, Ms. Elinor<br />

Thomas, Ms. Betty Vestberg, Ms. Rhiannon<br />

Williams,<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong><br />

viii


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

Local Staff<br />

Utangulizi Kuhusu Elimu ya<br />

Mazingira na Muongozo Huu<br />

Kwa miongo kadhaa elimu ya mazingira imekuwa ikifundishwa duniani kote kwa<br />

msisitizo mkubwa. Si muhimu kuwa imekuwa rasmi au la, lakini elimu ya mazingira<br />

imekuwa ikifundishwa kwa njia zote rasmi na zisizo rasmi kwa watu wa rika na<br />

mifumo tofauti. Elimu ya mazingira inapaswa kutoa msingi wa mabadiliko wa muda<br />

mrefu ambao unaweza kutumika katika maisha ya kila siku kwa kujiendeleza kiujuzi,<br />

matokeo ya kazi za vitendo na uwajibikaji binafsi.<br />

Katika kukabiliana na hali halisi na kwa njia sahihi, ni muhimu kwa muelimishaji<br />

kuielewa jamii husika na yanayoizunguka. Ni lazima ikumbukwe kuwa maarifa na<br />

mawazo kutoka katika jamii na tamaduni tofauti huwa havishabihiani pamoja. Hivyo<br />

mwelimishaji lazima awe na uwezo wa kubadilika na mwenye kupenda kujifunza ili<br />

kuwa na ujuzi unaohitajika kwa jamii husika. Waelimishaji wa mazingira lazima<br />

wahakikishe kuwa elimu inatolewa kwa njia sahihi ili kuongeza uwezo endelevu<br />

katika hifadhi ya mazingira.<br />

Mwongozo huu umeandaliwa kwa ajili ya waalimu na waelimishaji wengine wa<br />

elimu ya mazingira. Sehemu ya kwanza inatoa utangulizi wa mazingira ya bahari<br />

kufuatana na mgawanyiko wa mfumo wa maisha ya viumbe hai baharini; kwenye<br />

mikoko, maeneo ya maji kupwa na maji kujaa, nyasi za baharini na miamba ya<br />

matumbawe<br />

Sehemu ya pili ya mwongozo huu ina shughuli mbalimbali zinazoweza kufanyika<br />

wakati wa uelimishaji ili kusisitiza elimu ya mazingira kwa vitendo. Shughuli hizi si<br />

halisi lakini zinatoa mwongozo juu ya mwelekeo halisi wa mazingira ya bahari na<br />

shughuli za hifadhi. Ukitumika pamoja na vifaa vingine utakuwa msaada mkubwa<br />

kama kifundishio msaada. Izingatiwe kuwa baadhi ya maeneo ya mwongozo huu<br />

hayana tafsiri ya moja kwa moja ili kukidhi mahitaji ya jamii husika.<br />

Kwa nini tunataka Kuhifadhi<br />

Mazingira ya Bahari<br />

• Bahari inatoa rasilimali zitumikazo na watu waishio pwani.<br />

• Mazingira yanayozunguka bahari kama vile mikoko na nyasi za baharini<br />

zinahitajika kuhifadhiwa, kama kimojawapo kitaharibiwa kitaathiri kingine.<br />

• Kuongezeka kwa idadi ya watu, kunamaanisha kuongezeka kwa msukumo<br />

kwenye mazingira ya bahari, matokeo hayo yanahitajika kuwa endelevu ili kuwa<br />

na uhakika wa rasilimali za baadaye.<br />

• Mazingira mazuri ya bahari hutoa uhakika wa kuwepo kwa rasilimali za kutosha<br />

kwa jamii za pwani.<br />

• Mazingira mazuri ya bahari huwa kivutio kikubwa cha utalii na hivyo kukuza pato<br />

la Taifa.<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong><br />

ix


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

Maendeleo Endelevu<br />

Maendeleo endelevu ni hali ya mabadiliko ambayo huhusisha matumizi ya rasilimali,<br />

mielekeo ya uwekezaji, mzunguko wa maendeleo ya teknolojia, na mabadiliko ya<br />

kitaasisi yenye utulivu na mwelekeo wa kumsaidia binadamu kupata mahitaji yake<br />

kwa sasa na baadaye (Taarifa ya WCED, 1987).<br />

Hii haimaanishi kuwa bahari na ardhi visitumike kwa chakula na nishati, lakini ni<br />

kusema kwamba rasilimali hizi zitumike kwa sasa na kuwepo pia rasilimali za<br />

kutosha kwa vizazi vijavyo kwa viwango vilevile au vikubwa zaidi kuliko vya sasa.<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong><br />

x


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

Madhumuni ya FT MRP<br />

Mpango wa Utafiti wa Bahari<br />

Utafiti wa makazi na rasilimali za bahari hufanywa ili kutoa taarifa (Takwimu)<br />

muhimu kwa mwongozo wa matumizi ya rasilimali hizo kupitia uchoraji wa ramani<br />

zinaonyesha kiasi cha rasilimali na mgawanyiko wake kwenye maji yenye kina chini<br />

ya meta 30 na mifumo ya kimaisha ya viumbe hai iliyoko kwenye eneo la maji kupwa<br />

na maji kujaa. Takwimu hizi za msingi hutoa nafasi kwa utafiti yakinifu kufanyika.<br />

Hali za kibaologia, samaki waishio kwenye miamba ya matumbawe, idadi ya<br />

matumbawe na idadi ya wanyama wasio na uti wa mgongo vitafanyiwa utafiti kwa<br />

kutumia kielelezo cha hali ya juu kilichobuniwa na kufanyiwa marekebisho kwa<br />

miaka 12 ya kuwepo kwa FT MRP.<br />

Takwimu zinazokusanywa zitafanya kazi muhimu ya msingi katika kusimamia azma<br />

ya kuruhusu na kufanikisha madhumuni ya uongozi na utaratibu wa muda mrefu.<br />

Utafiti hufanywa na wafanyakazi wa FT MRP, watafiti wasaidizi toka mataifa<br />

mbalimbali na washirikishwaji toka taasisi mbalimbali kama vile Taasisi ya Sayansi<br />

za Bahari (IMS), Idara ya Mazao ya Biashara, Matunda na Misitu (DCCFF) na Idara<br />

ya Uvuvi na Rasilimali za Bahari (DFMR). Watafiti wote hufundishwa na<br />

kusimamiwa na wanabiologia ya bahari waliobobea .<br />

Vyanzo vya fedha vinapokuwa vizuri na vya uhakika, Vifaa vya kujifunzia hutolewa<br />

bure kwa washiriki kutoka <strong>Tanzania</strong>, wakati wanafunzi toka ng’ambo hujigharimia<br />

vitu vifuatavyo;<br />

• Cheti cha uzamiaji<br />

• Mafunzo ya utafiti wa bahari<br />

• Cheti cha BTEC ambacho ni sawa na cheti cha Darasa la 14 la uingereza<br />

Kuongeza ufahamu juu ya mazingira ya bahari<br />

• Mafunzo na majadiliano na wadau wa rasimali za bahari<br />

• Kuandaa na kugharimia siku za elimu ya mazingira kwa skuli za Pemba hasa zile<br />

zilizo kandokando ya bahari.<br />

FT MRP haikusudii kuzuia uvuvi Pemba. FT MRP inalengo la kufanya kazi na<br />

wavuvi waliopo, na mashirika yasiyo ya kiserikali kuhakikisha kuwa shughuli za<br />

uvuvi sasa na kwa vizazi vijavyo zinaendelea kuwa endelevu na samaki wa<br />

kutosha wanakuwepo.<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong><br />

xi


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

Historia Ya FT MRP<br />

Kisiwa cha Mafia 1989 – 1994<br />

Kisiwa cha Mafia kilitunukiwa kuwa eneo tengefu la Kibahari mwaka 1995 ikiwa ni<br />

matokeo ya kazi ya FT MRP iliyofanyika kati ya mwaka 1989 hadi 1994. Kwa sasa<br />

hifadhi hii inasimamiwa na Idara ya Hifadhi za Taifa la <strong>Tanzania</strong> kwa kushirikiana na<br />

WWF.<br />

Kisiwa cha Songo Songo 1994 – 1996<br />

Baada ya Utafiti Kisiwani Mafia kukamilika huku kukiwa na mafanikio makubwa,<br />

mradi wa FT MRP ulihamishiwa kisiwa kidogo cha Songosongo. Kisiwa hiki kina<br />

aina tofauti za matumbawe ambazo zilichunguzwa na kufanyiwa utafiti wa kina kisha<br />

ramani zikachorwa kuonyesha mpangilio wa rasilimali hizo, kazi iliyofanyika kwa<br />

muda wa miaka miwili. Vilevile kazi ya utafiti wa uvuvi iliyofanyika hapa ilikuwa ya<br />

muhimu zaidi kutokana na wavuvi wengi kukitumia kisiwa hiki kwa mapunziko<br />

mafupi kabla ya kupeleka samaki wao bara.<br />

Kilwa Kivinje 1997<br />

Ulikuwa ni mpango wa muda mfupi uliolenga maeneo ya maingilio ya mto Rufiji<br />

baharini. Taarifa juu ya aina mbalimbali za mikoko zilitumika kutengeneza ramani na<br />

matumizi yake yalichunguzwa kwa kina zaidi. Bahati mbaya eneo hilo lilikutwa likiwa<br />

limeathirika na mradi mkubwa wa ufugaji wa kamba. Madhara zaidi ya mradi huu<br />

yaelekea kusababishwa na kugeuzwa kwa hekta 20,000 za mikoko kuwa mabwawa ya<br />

kufugia kamba.<br />

Rasi za Mnazi, Mikindani na Mtwara 1997 – 2000<br />

Baada ya kutengeneza ramani ya ukanda wa kati wa Pwani ya <strong>Tanzania</strong>, FT MRP<br />

ilihamishia shughuli zake pwani ya kusini karibu ya mpaka wa Msumbiji. Mradi<br />

ulianza shughuli zake za utafiti Rasi ya Mnazi baada ya kushauriwa na Shirika la<br />

Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) ambapo ilipendekezwa kuanzishwa kwa eneo<br />

tengefu la kibahari. Baada ya hapo mradi ulihamia Rasi ya Mtwara mwaka 1998 na<br />

kufanya utafiti eneo lote la ukanda wa Pwani ya Kusini kuzunguka Wilaya ya Mtwara<br />

Mikindani.<br />

Wakati huo takwimu na taarifa juu ya uharibifu wa matumbawe uliosababishwa na<br />

mvua za El-Nino kusini mwa <strong>Tanzania</strong>. Kwa ujumla zilionyesha uharibifu mkubwa wa<br />

matumbawe na hasa katika pwani ya kusini mwa <strong>Tanzania</strong>. Kwa hiyo miradi zaidi<br />

ilianzishwa ili kurekebisha / kuondoa uharibifu na kuangalia utengamavu wa<br />

matumbawe. Miradi hii ilikamilika mwishoni mwa mwaka 2000.<br />

Kisiwa Cha Pemba 2001 – 2003<br />

FT MRP ilihamishia shughuli zake kisiwani Pemba mwezi wa pili mwaka 2001.<br />

Kisiwa cha Pemba kiko kaskazini mwa kisiwa cha Unguja na ni kimojawapo kati ya<br />

visiwa vikubwa viwili vinavyounda Zanzibar na kinatambulika Kimataifa kwa kuwa<br />

na rasilimali nyingi za bahari. Kwa pamoja Unguja na Pemba zina maeneo mengi<br />

yenye viumbe hai wa aina tofauti na wenye umuhimu mkubwa kimataifa (UNEP<br />

1989).<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong><br />

xii


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

Idadi na aina tofauti ya matumbawe iliyoripotiwa mwaka 1990 visiwani Zanizibar ni<br />

mara mbili zaidi ya ile iliyoripotiwa hapo mwanzo.<br />

Kwa pwani yote ya Africa mashariki na kati pwani ya Pemba ina mikoko mingi (Jean<br />

Veron, Pers comm.) ambayo ni moja ya maeneo makubwa ya uvuvi na hivyo kuwa<br />

chanzo kikubwa cha protini kwa wakazi wake. Mikoko ya Pemba kama ilivyo mingine<br />

yote ya <strong>Tanzania</strong> inahifadhiwa chini ya mpango maalumu wa hifadhi ili kupunguza<br />

madhara yanayosababishwa na binadamu.<br />

Mipango ya mwanzo ya FT MRP ililenga kwenye mpango wa hifadhi ya maeneo ya<br />

kisiwa cha Misali (MICA) ikiwa ni mipango ya miaka mitutu. FT MRP inafanya kazi<br />

kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mazingira na Ushirika Zanizibar<br />

(MANREC), Taasisi ya Sayansi za Bahari (IMS), Shirika la Kuhifadhi Mazingira ya<br />

Kisiwa cha Misali, (MICA), CARE – <strong>Tanzania</strong> na wadau asilia.<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong><br />

xiii


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

SEHEMU YA KWANZA<br />

1. Utangulizi Kuhusu elimu ya mazingira ya bahari<br />

2. Mikoko (Mikandaa)<br />

3. Eneo la maji kupwa na kujaa<br />

4. Nyasi za baharini<br />

5. Miamba ya Matumbawe<br />

6. Uhusiano wa Mifumo ya Maisha ya Viumbe Hai<br />

Baharini<br />

7. Mambo Unayopaswa na Usiyopaswa Kufanya<br />

Baharini<br />

8. Tishio Linaloyakabili Mazingira ya Bahari<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 1


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

1. Utangulizi Kuhusu elimu ya<br />

mazingira ya bahari<br />

Kihistoria, wakazi wa pwani wameyatumia mazingira ya bahari kujipatia chakula,<br />

vifaa vya ujenzi sehemu za kutabaruku na njia za usafirishaji. Kuongezeka kwa idadi<br />

ya watu, na kukua kwa sayansi na teknologia, kumesababisha ongezeko kubwa la<br />

matumizi ya bahari na mali asili zake na, upande mwingine kumekuwa na ongzeko la<br />

uharibifu wa mazingira na kupungua kwa rasilimali. Baadhi ya viumbe vimepotea na<br />

baadhi viko hatarini kupotea kama vile nyangumi na pomboo. Kwa hiyo hatua za<br />

haraka zinahitajika kuchukuliwa ambazo zitapelekea kuwekwa kwa taratibu na<br />

mwongozo madhubuti wa matumizi ya rasilimali za bahari upande mmoja, na<br />

kuhifadhi mazingira upande mwingine. Hivyo Elimu ya kutosha juu ya mazingira ya<br />

bahari na rasilimali zake inahitajika.<br />

Kabla ya menejimenti ya mazingira kufanyika ni muhimu kuelewa yaliyomo ndani ya<br />

mazingira ya bahari. Sura zifuatazo zinaelezea kwa ufupi yaliyomo kwenye mazingira<br />

ya bahari. Mazingira ya bahari ya kitropiki yanapatikana kati ya nyuzi 25 za latitudi<br />

pande zote mbili za ikweta. Ndani ya ukanda huu mdogo wa mazingira ya bahari<br />

duniani kote huwa katika mpangilio ufuatao toka nchi kavu kwenda baharini.<br />

• Misitu ya mikoko / mikandaa<br />

• Eneo la maji kupwa na kujaa<br />

• Nyasi za baharini<br />

• Miamba ya matumbawe<br />

Kila eneo lina uhusiano na jingine, mara nyingi hutegemeana ili viumbe hai viishi.<br />

Kutegemeana huko kumejadiliwa kwenye sehemu ya kwanza ya mwongozo huu,<br />

ambayo hutoa maelezo ya kila eneo kwa ufupi.<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 2


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

2. Mikoko (Mikandaa)<br />

2.1 Utangulizi<br />

Miti na vichaka vya mikoko hupatikana kati ya sehemu ya juu kabisa maji yanapojaa<br />

na sehemu ya chini kabisa maji yanapokupwa. Ni mimea ambayo hustawi vizuri<br />

kutokana na tabia maalum zinazoiwezesha kunawiri kwenye eneo hili, sifa hizo ni<br />

pamoja na kuwa na uwezo mkubwa wa kuvumiliwa kiwango kikubwa cha<br />

chumvichumvi ndani ya maji, kuwa na mizizi yenye sifa maalum ya kutoa chumvi<br />

ijulikanayo kama `pneumatophores` ambayo imejitokeza nje ya udongo hivyo<br />

kuruhusu uvutaji hewa rahisi kwenye tope lisilo na hewa (anoxic). Mpangilio wa aina<br />

za mikoko hutegemea uwezo wake kuvumilia chumvi chumvi ndani ya maji, aina ya<br />

udongo ilipomea na hali ya hewa.<br />

Mikoko hutumika kama chanzo cha nishati, miti ya kujengea na pia maeneo ya kuvua<br />

Samaki na shughuli zingine. Mikoko pia hutumika kama mazalio ya wanyama wa<br />

baharini, vifyonza virutubisho na kwenye mzunguko wa virutubisho hivyo, na pia<br />

huzuia mmomonyoko wa udongo pwani. (Semesi na Howell 1989).<br />

Mikoko ilipewa hadhi ya kulindwa <strong>Tanzania</strong> mwaka 1930, lakini kumekuwa na<br />

kutoelewana kati ya wanavijiji ambao wangependa kutumia maliasili zao na<br />

wanaohusika na kuzihifadhi. Imetokea mara nyingi kuwa wanakijiji hawakuruhusiwa<br />

kutumia mikoko wakati makampuni ya kibiashara yaliruhusiwa kufyeka mikoko kwa<br />

ajili ya kilimo cha mpunga, maeneo ya kutengeneza chumvi au maeneo ya kufugia<br />

samaki (Semesi na Howell 1989). Sheria zaidi zilizopitishwa Zanzibar mwaka 1968<br />

na <strong>Tanzania</strong> kwa ujumla mwaka 1991, kuzuia kukata mikoko kwa matumizi ya<br />

kibinadamu (Semesi 1998). Sheria hizi zilimaanisha kushabirisha matumizi ya kila<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 3


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

siku na mwongozo endelevu wa mfumo wa maisha ya viumbe hai (Semesi na Howell<br />

1989).<br />

2.2 Mikoko (mikandaa) ya <strong>Tanzania</strong><br />

Ukanda wa Pwani wa <strong>Tanzania</strong> una urefu wa Kilometer 800 na kati ya hizo km 600<br />

zina matumbawe, majani ya bahari na mikoko.<br />

• Moja kati ya maeneo yenye mikoko mingi kabisa Africa Mashariki ni eneo la mto<br />

Rufiji unapoingia baharini lenye ukubwa wa jumla ya Kilometa za mraba <strong>100</strong>0<br />

2.3 Mikoko ni nini<br />

• Mimea (miti / vichaka) inayovumilia mazingira ya chumvi inayopatikana eneo la<br />

bahari linalokupwa na kujaa maji<br />

• Mikoko hustawi kati ya eneo la kati na lile la chini kabisa maji yanapojaa na<br />

kupwa na mpangilio wa aina zake hutegemea muda wa maji kujaa<br />

• Mikoko ina sifa maalum zinazoiwezesha kuvumilia muongezeko na mabadiliko<br />

ya chumvichumvi ndani ya maji na hali ya kukosa hewa kwenye udongo<br />

• Kuna aina 60 za mikoko zinazostawi duniani kote, <strong>Tanzania</strong> inazo 10 kati ya hizo<br />

2.4 Hifadhi ya mikoko<br />

• Ni vigumu sana kulinda maeneo yote ya mikoko kwa kuwa mikoko imesambaa<br />

sehemu kubwa ya pwani ya <strong>Tanzania</strong><br />

• Elimu ya umuhimu wa mikoko na ushirikishwaji wananchi vinategemewa<br />

kusaidia utunzaji na matumizi mazuri ya mikoko ili iendelee kuwepo<br />

2.5 Tabia / Sifa maalum za mikoko<br />

Aina zote za mikoko zina tabia / sifa maalum zilizofanana zinazoiwezesha kuwepo<br />

maeneo ilipo.<br />

• `Pneumatophores’ (vikua) hii ni mizizi inayojitokeza nje ya udongo, hutokea sana<br />

kwenye maeneo yenye maji yaliyosimama<br />

• Viotea, hizi ni mbegu nene zenye uzito wa kutosha ambazo humea zingali kwenye<br />

mti mama hivyo huendelea kukua kwa haraka sana zinapoanguka kwenye tope<br />

• Ina uwezo wa kuvumilia kiasi kikubwa cha chumvi chumvi ndani ya maji, lakini<br />

kiwango kikubwa zaidi cha chumvichumvi hizo huweza kuiua mikoko<br />

• Ina uwezo wa kuzuia chumvichumvi kuingia kwenye mfumo wa mikoko<br />

• Majani yake yana ute wa nta juu yake na stomata zilizotumbukia ndani kupunguza<br />

upotevu wa maji baridi<br />

2.6 Kwa nini mikoko ni muhimu<br />

Mikoko huchuja takataka zilizo chini ya ardhi na kufyonza virutubisho kwa kutumia<br />

mizizi hivyo husaidia mzunguko wa virutubisho ambavyo huhitajika na viumbe<br />

vengine.<br />

• Huchuja matamahuruku na takataka kutoka nchi kavu hivyo huzilinda nyasi za<br />

baharini na matumbawe<br />

• Mizizi ya mikoko hufyonza maji baridi hivyo kupunguza kiwango cha maji hayo<br />

kinachoyafikia matumbawe ambacho kikizidi huweza kuyaharibu<br />

• Hupunguza mwendo kasi wa maji na hivyo kuruhusu lava na kamba kuishi salama<br />

• Pia ni makazi salama kwa viumbe mbalimbali<br />

• Chanzo cha chakula kwa binadamu – wanawake huvua samaki kwenye maeneo<br />

haya kwa matumizi ya nyumbani<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 4


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

• Chanzo cha nishati – hasa kwa jamii za pwani<br />

• Hutumika kujengea zio, nyumba, mitumbwi na madema n.k<br />

• Madawa asilia – Madawa ya kutibu magonjwa mbalimbali kama vile magonjwa<br />

ya tumbo na mikwaruzo<br />

• Ni kivutio kikubwa kwa watalii, kwa mfano misitu ya Jozani Unguja<br />

2.7 Ukataji / Uharibuifu wa mikoko<br />

• Ukataji wa mikoko kibiashara na matumizi ya kawaida sio endelevu na hasa<br />

inapokatwa bila uangalizi wowote<br />

• Mikoko hukatwa ili kuchoma mkaa na pia kupata maeneo ya uzalishaji wa chumvi<br />

• Upasuaji wa Mbao<br />

• Kilimo na ufugaji wa samaki<br />

• Umwagaji wa bidhaa za petroli na mabaki mengine<br />

• Matumizi ya kawaida (Uvuvi na nishati) husababisha madhara kidogo kuliko<br />

matumizi ya kibiashara<br />

• Madhara asilia kama vile milipuko ya Volkano na tufani huharibu mikoko pia.<br />

Athari zitokanazo na haya huwa ni kubwa mno hasa kama zitaambatana na<br />

uharibifu unaosababishwa na binadamu<br />

2.8 Matokeo ya kuharibu Mikoko<br />

• Kupungua kwa viumbe hai<br />

• Kuongezeka kwa mmomonyoko wa Pwani, miji iliyo karibu na pwani na mahoteli<br />

ya kitalii vyaweza kuathirika<br />

• Kuongezeka kwa matamahuruku kwenye matumbawe hupunguza uzalishaji na<br />

utalii<br />

• Chakula na nishati vitapungua na hivyo wanawake kulazimika kusafiri mbali<br />

kupata vitu hivyo<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 5


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

3. Eneo la maji kupwa na kujaa<br />

3.1 Utangulizi<br />

Eneo la maji kupwa na kujaa ni ukanda mwembamba, ni eneo ambalo hali ya ardhi<br />

yake hubadilika sana kuliko jingine lolote lile baharini, hivyo ni mazingira yenye<br />

taabu nyingi kwa viumbe wanaoishi hapo. Aidha mwendeleo wa kujaa na kupwa kwa<br />

maji umekuwa ukiviathiri viumbe hai ambao huhitaji uzoefu mkubwa wa mazingira<br />

haya ili viweze kuvumilia mabadiliko makubwa ya joto, chumvichumvi na mawimbi.<br />

Ingawa ni asilimia ndogo sana ya bahari yenye maji kupwa na kujaa duniani kote,<br />

eneo hili limekuwa na umuhimu mkubwa kutokana na kuwa na aina mbalimbali za<br />

viumbe hai. Pia kwa vile hufikika kwa urahisi na lina maliasili nyingi, sehemu nyingi<br />

huambatana na uvunaji mkubwa wa maliasili hizo.<br />

3.2 Umuhimu wake Kibaologia<br />

Eneo la maji kupwa na maji kujaa ni muhimu sana kwa kuwa chanzo kikubwa cha<br />

chakula kwa ajili ya jamii za pwani. Ukusanyaji wa makombe na uvuvi wa pweza na<br />

ngisi huzipatia jamii hizo vyanzo muhimu vya protini kama nyongeza kwa ile<br />

wanayoipata kwenye samaki. Maeneo haya pia huweza kuwa na mchanga au miamba.<br />

Mchanga wa Pwani ni kivutio kkikubwa cha watalii hivyo kuongezeka pato kwa taifa.<br />

Kwa mfano kisiwa cha Misali kina eneo hili kubwa ambalo huvutia watalii kulitumia<br />

kama sehemu ya kujifunza mengi na kupumzika (Kutabaruku).<br />

3.3 Uvunaji na uharibifu<br />

Kutokana na urahisi wa kufikika kwa eneo la maji kupwa na kujaa husababisha<br />

urahisi wa uvunaji wa maliasili zilizopo. Hivyo kama uvunaji huo hautazingatia<br />

taratibu za hifadhi na matumizi endelevu idadi ya viumbe hai inaweza kuathirika.<br />

Kwa kawaida mikuki na fimbo hutumika katika uvuvi wa pweza. Aina hii ya uvuvi<br />

yaweza kuwa endelevu ingawa bado kunahitajika takwimu sahihi ili kuepusha<br />

maamuzi yasiyoshabihiana na ukweli halisi. Kama idadi ya watalii itaongezeka juu ya<br />

kiwango kinachohitajika basi kuna uwezekano wa eneo hili kuathiriwa na shughuli<br />

mbalimbali kama vile kutembeatembea, kutupa taka na kuokota kombe, ambazo<br />

zaweza kuathiri mazingira aslilia.<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 6


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

3.4 Uhifadhi wake<br />

Uhifadhi ya maeneo haya hufanana ama na yale ya nchi kavu kwa upande moja au na<br />

yale ya bahari kwa upande mwinginehivyo uhifadhi wake huwamgumu, na hata<br />

katika utekelezaji wa mwongozo wa matumizi yake. Mara kwa mara kuna migongano<br />

juu ya idara ipi inahusika na uangalizi wa eneo hili. Pia kwa jinsi eneo hili<br />

linavyoonekana kama tupu hudhaniwa kuwa halina faida kwa viumbe wengi, mawazo<br />

ambayo sio sahihi.<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 7


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

4. Nyasi za Baharini<br />

4.1 Utangulizi<br />

Nyasi za baharini ni mimea ya nchi kavu ambayo imeweza kujijengea tabia ya kuishi<br />

baharini mpaka kina cha meta 50. Kuna aina 50 za majani ya baharini duniani kote,<br />

hupatikana zaidi kwenye maji kuanzia Antaktiki hadi <strong>Tanzania</strong>. Hufanana na nyasi za<br />

kawaida katika muonekano wake.<br />

4.2 Umuhimu wa majani ya baharini<br />

Majani haya huota kwenye maeneo tofauti kuanzia kwenye tope hadi kwenye miamba<br />

laini na yana uwezo wa kufunika meta moja ya mraba ambayo ya vikonyo vya nyasi<br />

4000 (Nybakken 2001). Vikonyo vya majani hayo huwa na mizizi imara ambayo<br />

huzashikilia vizuri hivyo kushinikiza mashapo sawia. Pia hutoa chakula kwa samaki,<br />

ulumba / ufuma na Kobe wa baharini. Mimea mingine ya baharini hujishikisha<br />

kwenye nyasi hizi. Samaki wadogo wadogo wanaokua hupata chakula, maeneo ya<br />

kujificha na makuzio. Hivyo nyasi za baharini ni makazi na maeneo muhimu ya uvuvi<br />

wa viumbe wadogo wadogo kama vile kamba.<br />

4.3 Manufaa / Matumizi / Uharibifu<br />

Hushikiza vizuri matamahuruku, hii huelezea umuhimu wa majani ya bahari kwa<br />

mfumo bora na imara wa maisha ya viumbe hai. Majani haya huweza kuharibiwa kwa<br />

njia nyingi.<br />

Njia asilia<br />

• Tufani kali<br />

• Mabadiliko ya kiasi cha chumvichumvi ndani ya maji kutokana na kuingia kwa<br />

maji baridi<br />

Binadamu<br />

• Maendelezo ya pwani pamoja na uchimbaji mchanga<br />

• Ujenzi wa mahoteli na viwanda huongeza kasi ya maji na hivyo waweza<br />

kusababishaa ongezeko kubwa la matamahuruku<br />

• Uchafuzi kutokana na umwagaji wa mafuta, maji taka na madawa<br />

• Utiaji nanga na uharibifu wa panga-boya<br />

• Uvuvi wa kupita kiasi<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 8


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

4.4 Matokeo / Madhara<br />

Ili kurudi katika hali ya kawaida baada ya kuharibiwa, nyasi za baharini huchukua<br />

muda wa miaka sita hadi mia moja kutegemea na ukubwa wa uharibifu uliotokea.<br />

Kwa hiyo uharibufu wowote huathiri mfumo mzima wa maisha ya viumbe hai<br />

baharini. Bila nyasi hizi mazalio na makuzio ya viumbe hai wengi yatakosekana na<br />

hivyo kupungua kwa idadi ya viumbe hivyo. Nyasi pia huzuia mashapo yasiyafikie<br />

matumbawe, hivyo kuondolewa kwake kutayaathiri matumbawe kwa kiasi kikubwa.<br />

4.5 Hifadhi yake<br />

Ni rahisi kuzihifadhi nyasi za baharini. Kinachohitajika ni kuweka vikwazo kwa<br />

waendeshaji / Wajenzi wa pwani ili kutoa nafasi kwa majani kustawi tena.<br />

Kwa vile nyasi hizi ni makazi ya aina mbalimbali za samaki na maeneo muhimu ya<br />

uvuvi, ni muhimu kuhakikisha kuwa maeneo hayo hayaharibiwi kwa faida ya wakazi<br />

wa pwani. Kama uharibifu ungalifanywa kwa nia ya kuwanufaisha wakazi wa pwani,<br />

basi manufaa hayo yangalikuwa ya muda mfupi tu. Manufaa yaweza kupatikana kwa<br />

maongozi endelevu. Ulinzi asilia unaotolewa na nyasi baharini kwa matumbawe<br />

hauwezi kufanywa na maumbo ya kuundwa na binadamu.<br />

Waendelezaji wa mahoteli wanaweza kuwa chanzo kikubwa cha uharibifu wa nyasi<br />

za baharini. Wajenzi hawa huziondoa nyasi kwa vile husadiki kuwa huleta<br />

muonekano mbaya wa eneo la hoteli kwa wageni na kwenye fukwe za mchanga. Ili<br />

kuzihifadhi, hatua madhubuti zinahitajika kuchukuliwa. Wenyeji wanahitaji<br />

kuelimishwa kuwa majani wasioyapenda yasipokuwepo fukwe na matumbawe<br />

ambayo watalii hulipia kuviona vitakuwa hatarini kutoweka.<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 9


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

5. Miamba ya Matumbawe<br />

5.1 Utangulizi<br />

Mara nyingi matumbawe huwa katika mkusanyiko ujulikanao kama “Koloni” la<br />

wanyama wenye uhai ambao huitaji mwanga wa jua na chakula kukua. Kila mnyama<br />

mmoja kwenye koloni huwa na uhusiano wa kufaidiana aina ya mwani ambayo<br />

huonekana kwa darubini tu. Uhusiano huu hufanyika kwa matumbawe kutoka madini<br />

ya chokaa ambayo ndio hutengeneza sehemu kubwa ya mfumo wa miamba ya<br />

matumbawe.<br />

Mimea hii midogodogo ndani ya matumbawe huishi kwa kuzaliana kwa kutumia<br />

mfumo wa mwanga wa jua na hewa ya kabondayoksaid toka kwenye matumbawe.<br />

Wakati huo huo matumbawe hupata hewa ya oksijeni na chakula kutoka kwenye<br />

mimea hii. Lakini pia kuna aina ya matumbawe (Yasiyojenga miamba) huweza kukua<br />

bila ya mimea hii, pia hayahitaji mwanga kukua hivyo hupatikana kwenye kina kirefu.<br />

Kwenye matumbawe pia kuna viumbe wanaotengeneza chokaa inayosaidia kujenga<br />

miamba. Viumbe hivi hujumuisha mwani wa kwenye matumbawe, matumbawe laini,<br />

na wanyama wasio na uti wa mgongo kama vile sponji na makombe madogo<br />

5.2 Umuhimu wa matumbawe<br />

Matumbawe ni muhimu kwa kuwa yanahifadhi aina nyingi za viumbe hai na kwamba<br />

ni chanzo muhimu cha chakula kwa mamilioni ya watu kupitia uvuvi wa samaki,<br />

makombe, na viumbe wengine. Pia huzuia mawimbi makubwa hivyo huyalinda<br />

mazingira ya pwani, fukwe na nchi kavu. Ili yaweze kustawi/kukua vizuri<br />

matumbawe yahahitaji mazingira maalum ambayo yamejadiliwa hapa chini.<br />

5.2.1 Joto<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 10


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

Kwa ukuaji mzuri, matumbawe huhitaji nyuzi joto kati ya 25-37 0 C kwa sababu hii<br />

matumbawe hupatikana ndani ya ukanda ulioko 25 0 kaskazini na 25 0 kusini ya Ikweta<br />

na kwenye kina kifupi cha maji.<br />

5.2.2 Mwanga wa kutosha<br />

• Mwanga husaidia mimea inayoishi kwenye matumbawe kufanya shughuli zake<br />

vizuri ambazo huongeza kasi ya ukuaji wa matumbawe na kuwepo kwa<br />

virutubisho vya kutosha<br />

• Matumbawe hupungua kwa kasi kadiri kina cha maji kinavyoongezeka hivyo<br />

kwenye kina cha meta 30 – 40 si rahisi kuyakuta<br />

5.2.3 Kutuama kwa mashapo / takataka<br />

• Kiasi kikubwa cha taka na matamahuruku kwenye maji hupunguza kiasi cha<br />

mwanga kinachoyafikia matumbawe na kuathiri uzalishaji wa chakula kwa<br />

kutumia mimea, hivyo kasi ya ukuaji huathirika pia<br />

• Utupaji wa taka huweza kutokea kwenye matumbawe na hili likitokea<br />

husababisha matumbawe kufa<br />

• Matumbawe hutumia nishati kubwa kuondoa uchafu<br />

5.2.4 Chumvi Chumvi<br />

• Mabadiliko kidogo tu ya chumvi ndani ya maji huweza kuathiri matumbawe.<br />

Hunawiri vizuri kwenye kiasi cha juu cha chumvi chumvi ndani ya maji, ukuaji<br />

wake hupungua au kusitishwa kabisa kiwango cha chumvi kinapopungua na<br />

hayaoti kabisa kwenye maji baridi kama vile kwenye maingilio ya mito Amazoni<br />

na Orinoko<br />

5.3 Uvunaji / uharibifu wa matumbawe<br />

• Matumbawe huharibiwa na aina yoyote mbaya ya uvuvi<br />

• Matumbawe huvunwa kwa ajili ya kutumika katika ujenzi, kama vivutio, na<br />

utengenezaji wa chokaa<br />

• Ukusanyaji wa makombe toka kwenye matumbawe<br />

• Ukataji wa mikoko – kwa ajili ya nishati, ujenzi na kwa kilimo na ufugaji<br />

• Uchafuzi kutokana na shughuli mbalimbali zinazofanywa na binadamu kama vile<br />

kilimo, maji taka, viwanda n.k<br />

• Utalii – uzamiaji, uogeleaji na utiaji nanga<br />

5.4 Hifadhi ya matumbawe<br />

Kwa vile matumbawe huishi na viumbe wengine wengi, ni muhimu kuwa waangalifu<br />

wakati wa kufanya hifadhi. Hii yaweza kufanywa kwa:<br />

• Kusitisha uvunaji wa matumbawe kwa ajili ya ujenzi na mapambo<br />

• Kuacha ukusanyaji wa makombe toka kwenye matumbawe<br />

• Kuzuia utiaji nanga kwenye matumbawe<br />

• Matumizi ya aina salama za uvuvi, kwa mfano kutembea juu ya matumbawe, na<br />

uvuvi wa mabomu na sumu havitakiwi<br />

• Ujenzi wa aina yoyote katika fukwe ni lazima uhakikishe kuwa hauathiri viumbe<br />

vya baharini<br />

Uangalizi wa matumbawe duniani kote unazingatiwa na unaelekea kuwa ni wenye<br />

mafanikio makubwa. Kisiwa cha Mafia nchini <strong>Tanzania</strong> kimefanywa kuwa eneo<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 11


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

tengefu la kibahari la jumla. Hii inamaanisha kuwa wakazi wa sehemu hiyo<br />

wanaruhusiwa kuvua lakini kwa mpango maalum unaoonyesha idadi na ukubwa wa<br />

samaki wanaopaswa kuvuliwa. Watalii wanaruhusiwa kufanya shughuli zao lakini<br />

mahoteli na vituo vyao vimewekewa mipaka maalum.<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 12


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

6. Uhusiano wa Mifumo ya Maisha<br />

ya Viumbe Hai Baharini<br />

6.1 Utangulizi<br />

Kuna uhusiano wa kimaisha / mazingira kati ya mikoko, nyasi za baharini na<br />

matumbawe. Hivyo ni muhimu kila mfumo kupewa kipaumbele katika hifadhi. Nyasi<br />

za baharini na mikoko huchuja uchafu / mashapo hivyo kuhakiki usalama wa<br />

matumbawe. Kwa upande wa pili matumbawe hupunguza kasi za mawimbi<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 13


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

maharibifu hivyo kuzuia uharibifu ambao ungeweza kutokea kwenye mikoko na nyasi<br />

za baharini.<br />

6.2 Mtazamo wa jumla<br />

Mpangilio ufuatao unaonyesha jinsi ambavyo kila eneo la bahari linavyofaidisha<br />

jingine.<br />

6.3 Mikoko<br />

• Huchuja matamahuruku na kufyonza virutubisho, hivyo huzipatia nyasi za<br />

baharini na matumbawe maji safi. Mashapo / uchafu vikizidi huua matumbawe<br />

• Huzuia mmomonyoko wa udongo kwenye fukwe<br />

• Hupunguza kiwango cha maji baridi kinachoyafikia matumbawe hivyo kupunguza<br />

mabadiliko ya chumvi chumvi ambayo huathiri matumbawe<br />

• Makuzio ya samaki wadogowadogo<br />

• Hupunguza kasi ya mawimbi hivyo huwezesha lava kuishi<br />

6.4 Nyasi za baharini na Maeneo ya maji kupwa na maji kujaa<br />

• Makulio ya samaki wadogowadogo<br />

• Hupunguza kasi ya mawimbi hiyo lava huweza kuishi<br />

• Huzuia mmomonyoko wa fukwe<br />

• Ni sehemu ambayo uozo mwingi hupatikana hivyo kuwa chanzo kikubwa cha<br />

chakula kwa viumbe vingi vya baharini<br />

• Huchuja / huzuia taka zisiyafikie matumbawe<br />

6.5 Matumbawe<br />

• Huzuia mawimbi makali kuyafikia majani ya baharini, mikoko na eneo<br />

linalokupwa na kujaa maji<br />

• Hutoa sehemu salama na imara kwa viumbe wa aina tofauti kuishi na kuzaliana<br />

• Aina ya viumbe wengi wanaopatikana kwenye matumbawe, huwezesha kuwa na<br />

mfumo mzuri wa mahusiano kibaologia (mahusiano yenye kufaidiana)<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 14


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

7. Mambo Unayopaswa na<br />

Usiyopaswa Kufanya Baharini<br />

7.1 Utangulizi<br />

Kutokana na kuongezeka kwa mahitaji ya maliasili za baharini kwa upande mmoja na<br />

haja ya matumizi endelevu kwa upande mwingine, kuna haja ya kuwa na njia salama<br />

za matumizi ya maliasili hizo. Kwa hiyo kila mdau analazimika kufahamu yampasayo<br />

na yasiompasa kufanya anapokuwa kwenye mazingira ya bahari. Taratibu zifuatazo<br />

zinapaswa kuzingatiwa na wadau wote, kwa nia ya kutunza mazingira na usalama<br />

binafsi, izingatiwe kuwa hizi ni sehemu tu ya taratibu zinazopaswa kuzingatiwa.<br />

7.2 Unapaswa<br />

• Kujua hali ya hewa kabla ya kwenda baharini<br />

• Uwe mwangalifu kwenye matumbawe<br />

• Kutia nanga mchangani<br />

• Kuchukua uchafu nyumbani<br />

• Kuacha matumbawe na vitu vingine kama ulivyovikuta<br />

• Kuipenda bahari na maliasili zake na kuzitunza<br />

7.3 Hupaswi<br />

• Kuogelea kwenye tufani, mawimbi makali au upepo mwingi<br />

• Kwenda kuzamia au kuogelea peke yako<br />

• Kuyasumbua au kuyachukua matumbawe au makombe (hai au Mafu)<br />

• Kugusa au kusimama kwenye matumbawe<br />

• Kutia nanga kwenye matumbawe<br />

• Kusababisha uchafuzi wa bahari<br />

• Kuvuna rasilimali yoyote kupita kiasi<br />

• Kutumia madawa ya aina yoyote baharini<br />

• Uvuvi wa kupita kiasi<br />

• Kuchimba mchanga pwani / ufukweni<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 15


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

• Kukata mikoko hovyo na kuchimba chambo kwenye mikoko<br />

7.4 ACHA!<br />

Kufanya shughuli yoyote inayoharibu mazingira ya bahari!<br />

7.5 ANZA!<br />

Kutumia njia salama kuvuna rasilimali za baharini ili kuhifadhi mazingira yake kwa<br />

ajili ya vizazi vijavyo.<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 16


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

8. Tishio Linaloyakabili Mazingira<br />

ya Bahari<br />

8.1 Utangulizi<br />

Maeneo ya bahari muhimu na yanayokabiliwa na tishio la uharibifu mkubwa ni<br />

mwamba wa matumbawe, mikoko, nyasi za baharini na maeneo ya maji kupwa na<br />

kujaa. Maeneo haya yanauhusiano wa kibaologia. Maeneo haya si muhimu tu kwa<br />

viumbe waishio baharini lakini pia ni muhimu kwa binadamu na hasa wakazi waishio<br />

pembezoni mwa bahari ambao uchumi na maisha yao hutegemea rasilimali za bahari.<br />

Hivyo kuna ulazima wa kuhifadhi mazingira ya bahari na maliasili zake.<br />

Tishio linalokabili mazingira ya bahari laweza kugawanywa sehemu mbili, tishio<br />

asilia na tishio linalotokana na binadamu.<br />

8.2 Tisho asilia linalohat arisha mazingira ya bahari<br />

1. Kiti cha Pweza chenye miiba (Acanthaster planci)<br />

Aina hii ya samaki ni hatari sana na hupatikana kwa wingi katika bahari ya pasifiki.<br />

Viumbe hivi chakula chao kikuu ni matumbawe, mara nyingi husababisha eneo<br />

kubwa la mwamba wa matumbane kuathirika na hata wakati mwingine kufa.<br />

2. Magonjwa<br />

Ugonjwa kama vile ‘blackland’ huvamia matumbawe na kuyabadilisha rangi yake na<br />

hata kuyaua kabisa.<br />

3. Matumbawe meupe<br />

Husababishwa na kuongezeka kwa jotoridi la maji ambapo mimea inayoishi na<br />

matumbawe hupoteza rangi na hivyo hushindwa kuzalisha chakula, hali hii hupelekea<br />

matumbawe kufa.<br />

4. Tufani na mawimbi yaendayo kasi<br />

Husababisha matumbawe, majani ya baharini, na mizizi ya mikoko (vikua) kufunikwa<br />

na takataka zinazotuama ambazo huathiri ukuaji, taka hizi zinapoongezeka huweza<br />

kusababisha vifo.<br />

8.3 Tishio linalotokana na binadamu<br />

1. Matumizi ya njia mbaya za uvuvi<br />

Uvuvi si lazima uwe mbaya na tishio kwa usalama wa mazingira ya bahari hasa<br />

unapokuwa katika hatua ya kuwa endelevu. Matatizo yanaweza kusababishwa na<br />

uvuvi wa kupita kiasi na kuvua samaki wachanga ambao ni tegemeo la baadaye. Aina<br />

zifuatazo za uvuvi ni tishio kubwa kwa mazingira ya bahari.<br />

- uvuvi wa kokolo / Juya<br />

- uvuvi wa mabomu / milipuko<br />

- uvuvi wa kigumi / neti za kojani<br />

- uvuvi wa sumu<br />

Njia hizi za uvuvi zinapaswa kuepukwa na kupingwa na kila mtu mwenye mapenzi<br />

mema na rasilimali za bahari na vizazi vya baadae.<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 17


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

2. Utupaji taka / uchafuzi<br />

Uchafuzi huathiri viumbe vya bahari na mazingira yao. Takataka nyingi ni sumu<br />

kama vile mafuta, uchafu wa majumbani, takataka na mabaki ya kwenye vyombo vya<br />

usafiri.<br />

3. Utiaji nanga<br />

Huharibu matumbawe, mara nyingi ni kutoka kwenye vyombo vya uvuvi na uzamiaji.<br />

Waweza kuzuia uharibifu kwa kuwa na vifaa vya kutilia nanga vinavyoelea au kuwa<br />

waangalifu wakati wa utiaji nanga.<br />

4. Wazamiaji<br />

Wasipokuwa waangalifu huweza kuharibu na hata kuua viumbe na mazingira ya<br />

baharini hasa kwenye mwamba wa matumbawe. Wazamiaji wanapaswa kuelimishwa<br />

juu ya uzamiaji salama.<br />

5. Biashara ya makome, makunguju, mabaragumu na makombe.<br />

Viumbe hawa wakiwa hai au wafu ni mapambo yanayopendwa. Lakini wokotaji wa<br />

vitu hivi waweza kuharibu mfumo wa usawa baharini, ni kwa sababu viumbe hivi<br />

huoza na kutengeneza miamba au mchanga wa ufukweni. Kama makombe mafu na<br />

matumbawe vitaondoshwa utengenezaji wa mchanga utasitika na kama makombe na<br />

matumbawe hai vitaondolewa viumbe wengine wataathirika pia kwa kukosa ama<br />

chakula au makazi.<br />

6. Ukataji mikoko hovyo<br />

Ukataji hovyo mikoko ni hatari sana kwa vile huharibu mandhari ya fukwe zetu,<br />

mazalio na makulio ya samaki. Mikoko pia huzuia mmonyoko wa ardhi na kuzuia<br />

uchafu kutoka nchi kavu kuyafikia matumbawe. Hivyo tunapaswa kuitunza mikoko<br />

na kuitumia kwa uangalifu.<br />

Hivyo ni jukumu la wadau kutumia rasilimali na mazingira ya bahari kwa<br />

uangalifu mkubwa ili kupunguza na hatimaye kuzuia kabisa tishio<br />

linaloyakabiri mazingira ya bahari.<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 18


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

SEHEMU YA PILI<br />

Shughuli zinazofanyika wakati wa<br />

ufundishaji<br />

1. Masanamu ya kuchorwa<br />

2. Kusanifu matangazo (mabango)<br />

3. Chemsha bongo ya elimu ya mazingira<br />

4. Mchezo wa taa za barabarani<br />

5. Kusema hapana kwa takataka<br />

6. Mfumo wa ushirikiano wa chakula – 1<br />

7. Mfumo / mtandao wa chakula (Uhusiano wa<br />

viumbe) 2<br />

8. Matembezi ya nyika hai<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 19


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

1. Masanamu ya kuchorwa<br />

1.1 Utangulizi<br />

Masanamu ya kuchorwa huwa ni mapambo yenye mvuto mkubwa kwa jamii, kama<br />

yakibuniwa vizuri huweza kuwa njia bora ya kufikisha ujumbe kwa jamii husika.<br />

Uhusiano wa maumbo na mazingira halisi ni muhimu sana ili kuleta mvuto na hisia<br />

juu ya ujumbe uliopo hivyo ni muhimu kuyazingatia haya wakati wa usanifu.<br />

1.2 Nini cha kufanya<br />

Sehemu ya kuweka masanamu inapaswa kuchunguzwa kabla ya ubunifu wa mchoro.<br />

Baada ya hilo sanamu inaweza kubuniwa na kuchorwa kwenye kuta za pembeni za<br />

skuli kwenye maeneo yanayoonekana kirahisi au katika kuta za zege vijijini. Kitu cha<br />

kuzingatia ni rangi zinunuliwe mapema na ziwe zinazoelekeana na aina ya mchoro,<br />

eneo unapochorwa na ujumbe uliokusudiwa.<br />

1.3 Vifaa<br />

Rangi za kawaida zinazotumika majumbani pamoja na vipakio, karatasi na kalamu<br />

1.4 Usanifu<br />

Chora mchoro kwenye karatasi ndogo na upake rangi, hii itawezesha tatizo lolote la<br />

mchoro kujulikana na kufuatiliwa mapema. Pia mchoro huo waweza kutumika kama<br />

mfano siku ya uchoraji mkubwa.<br />

1.5 Mawazo ya kisanifu<br />

Mchoro unaweza kuonyesha muonekano wa ndani ya maji, jinsi ya kutunza mazingira<br />

yanayoizuinguka jamii husika, Jambo lolote la kiulimwengu kama vile ukataji miti<br />

hovyo, viumbe vilivyo hatarini kupotea n.k. Mchoro unapaswa uwe na ujumbe wa<br />

kuihimiza jamii husika kuwa na mwelekeo wa kutunza mazingira.<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 20


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

2. Kusanifu matangazo (mabango)<br />

2.1 Lengo<br />

Kuwafanya washiriki kufikiria juu ya hali ya mazingira na jinsi wao binafsi<br />

wanavyoweza kuathirika. Kujenga mawazo juu ya mambo / mafunzo ya kila siku,<br />

kutoa mawazo yao katika usanifu kupitia vitabu, usanifu binafsi husaidia kujenga<br />

mawazo juu ya tangazo lililobuniwa. Kama unataka kazi hii iwe ni yenye mafanikio,<br />

hakikisha kuwa kuna mada rasmi itakayotoa ujumbe unaoonekana kwenye tangazo na<br />

washiriki wapewe nafasi ya kuchangia mawazo. Mfano ni matatizo gani yanayokabili<br />

mazingira ya bahari ama ni jinsi gani ukanda wa pwani unaweza kuhifadhiwa /<br />

kutunzwa. Toa nafasi ya majadiliano kwa kila mmoja kushiriki.<br />

2.2 Vifaa<br />

Karatasi<br />

Penseli / kalamu za rangi / rangi<br />

Maelezo ya kufuatisha<br />

2.3 Jinsi ya Kufanya<br />

Ruhusu washiriki kuunda mawazo ya kibunifu kwa kupitia vitabu. Mada<br />

ikishapatikana ubunifu waweza kuanza na baada ya kumaliza jadili na wabunifu<br />

kilichomo ndani ya mabango yao na wanategemea watu watapata tafsiri gani.<br />

2.4 Mawazo muhimu<br />

Ili kufanya mchezo wenye faida weka mada maalum ambayo washiriki watapaswa<br />

kuijadili. Kwa mfano kuna msukumo gani kwenye mazingira na namna gani fukwe<br />

zinaweza kutunzwa. Ruhusu mjadala ili kupata mlolongo wa maelezo. Kisha ruhusu<br />

washiriki kubuni mabango yenye ujumbe unaoendana na yaliyojadiliwa.<br />

2.5 Mawazo ya ziada<br />

Unaweza kuonyesha mchezo wa “coat of arms”. Wagawanye washirki katika<br />

makundi matatu, moja liwe picha zinazoonyesha mazingira yaliyoathirika, jingine<br />

picha zinazoonyesha vitu vilivyo sababisha uharibifu na la mwisho picha<br />

zinazoonyesha jinsi ya kubadilisha uharibifu wa mazingira uliotokea.<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 21


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

3. Chemsha bongo ya elimu ya<br />

mazingira<br />

3.1 Utangulizi<br />

Ni vizuri washiriki wakapewa changamoto juu ya uelewa wao. Kuwapa elimu / ujuzi<br />

kutahakikisha kuwa mawazo yanajengeka na kuimarika. Chemsha bongo ya<br />

mazingira yaweza kuhusisha mambo mapya au ya zamani. Kuwapa nafasi washiriki<br />

kwa uhuru zaidi bila hofu itarahisisha kujifunza na kukumbuka. Chemsha bongo<br />

yaweza kufanyika mara nyingi iwezekanavyo ili kukuza ufahamu juu ya mazingira.<br />

3.2 Lengo<br />

Kushirikisha timu zote kwenye mchezo hivyo kwanza unaanzia kwenye kona ya<br />

kwanza ya mbao kisha unaendelea mpaka mwisho. Kila sehemu ya mchezo ni lazima<br />

swali lijibiwe sawia ili kuendelea mbele na ili ujumbe uweze kuzingatiwa.<br />

3.3 Vifaa<br />

• daisi ya koro koro<br />

• ubao mpana<br />

• maswali<br />

• kalamu / rangi<br />

3.4 Jinsi ya kufanya<br />

Utengenezaji wa mchezo<br />

• Tengeneza ubao mdogo wenye vyumba (Mraba) toka mwanzo na hata mwisho<br />

(kama drafti)<br />

• Andika kwenye vyumba hivyo umepotea au rudi nyuma hatua moja, hii<br />

itauchangamsha mchezo<br />

• Wape vikadi kila timu zenye maumbo ya samaki au wanyama<br />

• Andaa maswali yanayoendana na umri wa washiriki<br />

Jinsi ya kucheza<br />

• Gawanya timu katika makundi mawili kisha weka hesabu zote mwanzo<br />

• Chagua timu inayoanza na uliza swali, jibu sahihi litapelekea timu hiyo kurusha<br />

daisi na kusonga mbele kwa nafasi zilizoamuliwa<br />

• Kuelekea kwenye mraba timu inapaswa kusubiri timu nyingine kujibu swali<br />

kwanza<br />

• Kama itatoa jibu sahihi itarusha pia daisi na kusonga mbele nafasi sawia<br />

• Kwa hiyo mchezo utaenda timu ya kwanza na kuendelea mbele na nyuma<br />

• Swali lisipopata jibu sahihi timu hairushi daisi na haisongi mbele, lazima wasubiri<br />

mzunguko wa pili<br />

3.5 Mawazo muhimu<br />

Hakikisha kuwa unazingatia amri za Umekosea na urudi nyuma hatua moja<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 22


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

3.6 Mawazo ya ziada<br />

Maswali yatoke kwenye mada tofauti kama vile, tishio, hatari, rasilimali, na wadau<br />

wa mazingira ya bahari. Vikadi vya maswali na miraba vipake rangi kiasikwamba<br />

mada husika, swali na mraba wake vifanane. Kwa mfano kama kadi ya swali la tishio<br />

linalokabili mazingira ya bahari ina rangi nyekundu, hili ndilo swali inabidi lijibiwe<br />

kama daisi itatua kwenye mraba wa rangi hiyo katika ubao.<br />

3.7 Maswali ya chemsha bongo<br />

S Taja aina moja ya uvuvi mbaya<br />

J Mabomu, Sumu, Kokolo<br />

S<br />

J<br />

S<br />

J<br />

S<br />

J<br />

S<br />

J<br />

S<br />

J<br />

S<br />

J<br />

S<br />

J<br />

S<br />

J<br />

S<br />

J<br />

Taja njia za uvuvi salama<br />

Madema, Ndoana<br />

Kwa nini watu wakitaka kutupa nanga lazima kuwa waangalifu<br />

Nanga inaweza kuharibu matumbawe<br />

Kipi chaweza kuoza haraka – Plastiki au bati<br />

Bati, Plastiki, huchukua miaka mingi sana kuoza na ikichomwa moto<br />

huongeza. Madawa yenye sumu hewani<br />

Kwanini hairuhusiwi kuokota kome ufukweni au kwenye matumbawe<br />

Zinapooza hutengeneza mchanga ambao ni muhimu katika kuweka hali nzuri<br />

ya fukwe, pia kome ni nyumba za baadhi ya viumbe kama vile kaa na pweza<br />

Kwanini hushauriwa kuweka bidhaa zote kwenye mfuko mmoja wa<br />

plastiki, na Kuutumia tena mfuko huo huo<br />

Kupunguza idadi ya mifuko ya plastiki, inamaana kupunguza uchafu kwenye<br />

makazi. Kutumia tena ule wa mwanzo itamaanisha kupunguza zaidi hivyo<br />

mazinira safi<br />

Kama una takataka na huna kwa kuzitupa, je utazitupa baharini<br />

Utatupa chini Au Utaweka mfukoni<br />

Utaziweka mfukoni hadi ukute shimo la taka<br />

Taja vitu vitano visivyotakiwa kuachwa kwenye ufukwe<br />

Plastiki, Vioo, Nyuma na taka kwa ujumla<br />

Mikoko inaisadiaje matumbawe<br />

Kwa kuzuia uchafu unaotoka nchi kavu usiyafikie matumbawe<br />

Kwa nini ni muhimu kwa wanabiologia ya bahari na wataalamu wa uvuvi<br />

Kuzungumza na maofisa wa uvuvi kujua aina na kiasi cha samaki<br />

kinachovuliwa <br />

Kuhakikisha kuwa aina fulani ya samaki haipotei kwa kuvuliwa sana, pia<br />

kujua kiasi Kilichopo na kilichovuliwa kutasaidia kumonita wavuvi<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 23


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

S<br />

J<br />

S<br />

J<br />

S<br />

J<br />

S<br />

J<br />

S<br />

J<br />

S<br />

J<br />

Kwanini hupaswi kununua kombe dukani<br />

Kombe wanaopatikana dukani ni wale waliochukuliwa toka kwenye<br />

Matumbawe wana uhusiano wa kibaolojia na matumbawe na viumb wengine.<br />

Hivyo kupungua kwa kombe kwaweza kuathiri ukuaji wa matumbawe<br />

Taja umuhimu wa majani ya baharini<br />

Huzuia mmomonyoko wa udongo hivyo huyalinda matumbawe, pia<br />

huwaficha samaki wadogowadogo wasiliwe na wakubwa<br />

Weka mpangilio huu wa chakula kwenye mnyororo kiti cha pweza<br />

chenye miiba, Binadamu ,baragumu , pweza na matumbawe<br />

Matumbawe – kiti chwa pweza chenye miiba- baragumu – pweza –binadamu<br />

Kwanini Elimu ya mazingira ni muhimu sana<br />

Elimu ya mazingira hutueleza jinsi tunavyoweza kuyatunza na kuyahifadhi<br />

mazingira yetu hivyo kurefusha maisha pia hufundisha madhara<br />

yatakayotokea tusipotunza mazingira<br />

Je mtu mmoja anaweza kuleta mabadiliko kwenye mazingira<br />

Ndiyo<br />

Taja njia tatu zinazoharibu matumbawe<br />

Utalii<br />

Ukusanyaji Kome<br />

Uzamiaji<br />

Utupaji nanga<br />

Uvuvi- nanga, mabomu, kigumi, sumu na uvuvi wa kutumia neti zenye<br />

matundu madogo sana (kojani nets)<br />

Sababu asilia – tufani na mawimbi makali<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 24


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

4. Mchezo wa taa za barabarani<br />

4.1 Lengo<br />

Kupima kumbukumbu za washiriki juu ya mambo waliojifunza siku za nyuma na siku<br />

ya mazingira. Pia kupima ufahamu wa mshiriki juu ya mazingira na uwezo wa<br />

kufikiria.<br />

4.2 Vifaa<br />

• Mifuniko mitatu ya plastiki ya duara (bluu, kijani, zambarau)<br />

• Karatasi na kalamu<br />

• Karatasi ngumu<br />

• Rangi (Njano, Kijani na Nyekundu)<br />

4.3 Jinsi ya kuandaa michezo<br />

• Tengeneza viboksi vidogo vitatu kwa kila kundi kwa kila kundi kimoja cha kijani,<br />

kimoja chekundu, na cha njano<br />

• Kijani – Salama / endelea<br />

• Nyekundu – hatari / zuia / acha<br />

• Njano – tahadhali / kuwa mwangalifu / tafakari<br />

• Kila kikundi huwa na viboksi vitatu vya aina zote<br />

• Tengeneza uwanja wa michezo ambao huwa na umbo la mraba, katikati huwekwa<br />

mifuniko mitatu ya duara yenye rangi tofauti<br />

• Andaa karatasi yenye maelezo ambayo yanaendana na rangi za viboksi (hatari,<br />

Salama na tahadhari)<br />

• Washiriki waweza kuwa kwenye makundi manne au zaidi<br />

4.4 Jinsi ya kucheza<br />

• Kila kundi hukaa pembe yake umbali sawia toka katikati<br />

• Maelezo husomwa kisha mwamuzi hutoa sekunde kadhaa kwa makundi kuamua<br />

kama ni hatari, tahadhari au salama<br />

• Kisha kwa haraka humpa mshiriki mmojawapo kisanduku husika, mwamuzi<br />

huhesabu moja, mbili, tatu – goo! kwa haraka mshiriki toka kila kundi atakimbia<br />

kuweka kisanduku katikati. Atakayeweka kwenye mfuniko wa bluu kisanduku<br />

sahihi kundi lake litapata alama tatu, kwenye kijani alama mbili na kwenye<br />

zambarau alama moja wa nne atapata sifuri kwa kuchelewa. Alama hutolewa kwa<br />

jibu sahihi tuu<br />

• Kama kuna mgongano wa majibu mwamuzi ataruhusu mjadala kidogo na kutoa<br />

jibu sahihi<br />

• Aina ya maelelezo itategemea rika ya washiriki<br />

• Badili nafasi ya mifuniko ktk kila baada ya swali moja<br />

4.5 Mawazo ya Ziada<br />

Endelea na sentensi zingine na fikiria ambazo zinaendana na rika na kiwango na<br />

uelewa wa washiriki na topiki inayofundishwa, waweza pia kutoa zawadi kwa<br />

washindi, zaweza kuwa vifaa vya shule na vitabu vya mazingira.<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 25


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

Team A<br />

Team B<br />

Rotate lids regularly<br />

Judge<br />

3 points 2 points<br />

Reader<br />

1 point<br />

Team D<br />

Referee<br />

Team C<br />

4.6 Mfano wa maelezo na majibu yake<br />

1. Kukata mikoko ovyo – Nyekundu<br />

2. Shughuli za uvuvi – Njano<br />

3. Utupaji taka – Njano<br />

4. Kukata miti ovyo – Nyekundu<br />

5. Kutumia mifuko ya plastiki ni kuzuri – Myekundu<br />

6. Kutia Nanga – Njano<br />

7. Uzoaji wa mchanga ufukweni – Nyekundu<br />

8. Umwagaji wa mafuta baharini – Nyekundu<br />

9. Utafiti wa kisayansi – Njano<br />

10. Kufanya kazi na <strong>Frontier</strong> – Kijani<br />

11. Kuchoma mkaa – Njano<br />

12. Kupandikiza mikoko – Kijani<br />

13. Ujenzi wa vituo vya Utalii – Njano<br />

14. Kuokota kome ufukweni – Nyekundu<br />

15. Uchomaji matumbawe kutengeneza chokaa – Nyekundu<br />

16. Uvuvi wa mabomu – Nyekundu<br />

17. Mbuyu ni aina mojawapo ya mikoko – Nyekundu<br />

18. Majani baharini si muhimu – Nyekundu<br />

19. <strong>Tanzania</strong> na Uingereza ni marafiki – Kijani<br />

20. Chips mayai ni chakula kizuri – Yeyote<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 26


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

5. Kusema hapana kwa takataka<br />

5.1 Utangulizi<br />

Ingawa kumekuwa na mambo mengi yanayoathiri mazingira lakini ni vigumu kujua<br />

ni lipi kati ya hayo litakuathiri wewe binafsi. Pia katika sehemu nyingi duniani watu<br />

hawana nguvu ya kutatua matatizo hayo kutokana na ukosefu wa fedha au kipato<br />

kidogo. Lakini pamoja na hilo watu ulimwenguni kote hushiriki katika matumizi ya<br />

bidhaa zinazosababisha uchafu kwa kiwango tofauti. Kwa mfano nchi nyingi hutumia<br />

mifuko ya plastiki kubebea mahitaji na hata kuhifadhi bidhaa. Baada ya kutumia<br />

mifuko hairudiwi tena bali hutupwa mbali kama uchafu. Plastiki, makopo, vioo na<br />

vyuma vyaweza kuwa hatari kwa watu na kuweza kuua wanyama kwa<br />

kuwasababishia vidonda au kwa kuvimeza.<br />

Katika nchi nyingi uzoaji wa taka ni kidogo kutokana na njia za usafiri kuwa duni.<br />

Kutokana na wakazi wengi huzichoma takataka na kuzifukia chini.<br />

Hii yaweza kuwa nzuri kwa vile inasaidia kupunguza taka lakini yaweza kuongeza<br />

tatizo watu wasipokuwa makini.<br />

Kama watu watatumia mifuko ya plastiki ile ile kwa kuikataa mipya inapokuwa si<br />

muhimu kuwa nayo, idadi ya plastiki na uchafu kwa ujumla waweza kupungua<br />

kwenye makazi. Na juu ya hili kama wanunuzi wa bidhaa watakuwa waangalifu na<br />

kuwa makini na wenye kiasi kwenye ununuzi wa bidhaa ingeweza kupunguza kasi ya<br />

uongezekaji wa taka kwenye makazi ya watu na wanyama. Kuwafahamisha watu juu<br />

ya nguvu waliyonayo juu ya taka kwa kuwahusisha katika mazoezi rahisi inaweza<br />

kusaidia watu kufikiria juu ya uwajibikaji.<br />

5.2 Lengo<br />

Andaa / buni eneo la mikoko lenye taka, Washiriki wanapaswa kutembea kutoka kiti<br />

kimoja hadi kingine bila ya kugusa ardhi kwa msaada wa daraja la mbao,<br />

wakikusanya taka na kuziweka kwenye pipa. Mchezo huu ni kama kituko lakini watu<br />

wanaweza kuulizwa kwamba wana maoni / hisia gani juu ya taka, kuufanya mchezo<br />

uwe mzuri zaidi. Pia hutakiwa kuelezea uchafu unaharibu mazingira yao kwa kiasi<br />

gani.<br />

Maoni yaweza kutolewa mwishoni mwa mchezo ni kwa jinsi gani mazingira mazuri<br />

yanaweza kufanywa na jinsi gani ya kuwa wawajibikaji.<br />

5.3 Vifaa<br />

• Viti 6-7<br />

• Mbao mbili<br />

• Pipa la taka<br />

• Karatasi<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 27


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

5.4 Jinsi ya kufanya<br />

• Kabla ya hapo tengeneza bango linaloonyesha madhara ya taka zinapokuwepo na<br />

jingine linaloonyesha faida za taka kutokuwepo ili iwasaidie washiriki kuelewa.<br />

Mfano wa madhara ya taka, kuchomwa plastiki huongeza kemikali zenye sumu<br />

hewani, taka ndogo zikimezwa na wanyama huwa hatari na pia taka hazipendezi<br />

kuziona. Faida za kutokuwa na taka ni pamoja na makazi safi ya kuishi, hali safi<br />

ya hewa na maisha salama<br />

• Tafuta eneo zuri la kuweka msitu wa kubuni wa mikoko<br />

• Panga viti vizuri ili kuruhusu washiriki kuweka mbao juu yake na kutembea<br />

upande mmoja hadi mwingine<br />

• Sambaza takataka kwa washiriki kuokota<br />

• Toa muda maalum kwa muokota taka kumaliza eneo lote la mikoko<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 28


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

6. Mfumo wa ushirikiano wa<br />

chakula – 1<br />

6.1 Utangulizi<br />

Viumbe hai wote wanauhusiano wa mzunguko wa nishati. Uhusiano huo hujulikana<br />

kama mfumo / mtandao wa ushirikiano wa chakula. Mimea iko chini / ngazi ya<br />

kwanza ya mfumo huo kama wazalishaji wa msingi. Kwa upande mwingine wanyama<br />

walao mimea wako katikati na juu yao ni wale wanyama walao nyama. Kutokana na<br />

kwamba wala nyama hula wanyama wenzao ambao wengi wao hula mimea, kuna<br />

usawa kati yao ambao huweza kuathiriwa na binadamu. Kwa mfano, idadi ya<br />

baragumu huongezeka haraka kukiwa na hali nzuri ya kimazingira, hivyo samaki<br />

wawalao pia huongezeka, lakini samaki wakiongezeka kupita kiasi hupelekea idadi ya<br />

baragumu kupungua na hivyo samaki wawalao pia huathirika.<br />

Wakazi wa pwani hutegemea samaki kwa mlo kamili na kujipatia kipato. Uvuvi<br />

mdogo mdogo hauna athari kwa mtandao wa chakula. Lakini uvuvi ukiongezeka sana<br />

kupita kiasi cha samaki basi samaki hao wataanza kupungua. Kupungua huko kwa<br />

samaki kunaweza kuathiri viumbe wengine.<br />

6.2 Lengo<br />

• Kujenga uelewa juu ya uhusiano kati ya Viumbe<br />

• Washiriki kuelewa madhara ya moja kwa moja na yasiyo ya moja kwa moja<br />

yanayoweza kusababishwa na binadamu kwenye mazingira baharini<br />

6.3 Jinsi ya kufanya<br />

• Buni mifumo / Mtandao wowote wa chakula (tumia mfumo huo hapo chini)<br />

• Uchore mfumo huo tayari kwa majadiliano<br />

• Tayarisha vipande vya karatasi zenye picha ya vitu vyote / viumbe vilivyoko<br />

kwenye mfumo huo<br />

• Mpe kila mshiriki picha / Mchoro kisha jadili mtandao / mfumo huo wa chakula<br />

na mahusiano kila kiumbe na chenzie<br />

• Washiriki wawe katika duara wakielekeaa upande mmoja na nyuso zao katikati<br />

• Athari zitokanazo na binadanu ziwe nje ya duara<br />

• Washiriki wajivute ndani ya duara na wakaribiane kiasi cha kutegemeana. Hili<br />

huitaji mazoezi<br />

• Mshiriki anayehusisha madhara yatokanayo na binadamu atamvuta mmoja wao<br />

kwa nguvu na kumwondoa kwenye duara, hilo litasababisha duara zima<br />

kuharibika.Hii huonyesha kitu halisi kinachoweza kutokea kwenye mtandao wa<br />

chakula<br />

• Hii ni njia rahisi kwa mshiriki kuona jinsi gani mfumo mzima na mtandao wa<br />

chakula huweza kubomoka kabisa ukiathiriwa na kitu chochote toka nje<br />

• Unaweza kurudiwa mara nyingi ili kutilia mkazo ujumbe uliopo. Kuhitimisha<br />

washiriki wanaweza kujadili kwa mjumuisho juu ya maada husika na<br />

kuzungumzia shughuli zozote wazifanyazo kila siku zenye athari kwenye mfumo<br />

mzima wa mtandao wa chakula<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 29


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 30


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

7. Mfumo/mtandao wa chakula<br />

(Uhusiano wa viumbe) 2<br />

7.1 Lengo<br />

• Kukuza ufahamu juu ya mahusiano ya viumbe hai na mazingira yao<br />

• Kuonyesha / kujifunza athari zitokanazo na binadamu kwenye mazingira haya<br />

7.2 Vifaa<br />

• Kalamu za kawaida na za rangi<br />

• Karatasi aina ya A4<br />

• vijiboksi vidogo (4 kwa kila kiumbe)<br />

• Karatasi aina ya A1 moja au mbili<br />

7.3 Jinsi ya kuandaa<br />

• Buni mfumo / mtandao wa chakula na uchole kwenye karatasi kubwa aina ya A1<br />

bila ya kuonyesha majina ya viumbe husika, ambayo yanaweza kuwakilishwa na<br />

namba<br />

• Chora picha zinazoelekeana na mchoro huo hapo juu kwenye karatasi au viboksi<br />

• Kama washiriki ni wengi wagawe kwenye makundi ya watu 4 au 5<br />

7.4 Jinsi ya kufanya<br />

• Tundika mchoro mkubwa kwenye ubao unakoweza kuonekana na kila mmoja<br />

• Wagawie wanafunzi picha<br />

• Kwa kujadiliana wape nafasi wanafunzi kuamua picha ipi inaelekeana na namba<br />

ipi kwenye mchoro<br />

• Baada ya kukamilisha upangaji wa picha zote kwenye mchoro jadiliana na<br />

wanafunzi madhara ya kuiharibu sehemu mojawapo katika mchoro huo<br />

• Husianisha mjadala na mazingira halisi na jadili shughuli zifanywazo na<br />

binadamu zinazoweza kuathiri mfumo huo<br />

7.5 Kwenye mchoro wa mfano ulioonyeshwa hapo chini namba zinawakilisha<br />

1. Papa – mla nyama<br />

2. Mcheche – mla nyama<br />

3. Ndege wa baharini<br />

4. Pweza – mla nyama<br />

5. Samaki – Kipepeo<br />

6. Samaki – Tembo<br />

7. Baragumu<br />

8. Kiti cha pweza chenye miiba<br />

9. Kamba<br />

10. Matumbawe<br />

11. Ufuma / ulumba<br />

12. Mwani<br />

13. Majani<br />

14. Majani ya baharini<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 31


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

7.6 Mawazo ya ziada<br />

Tumia viboksi kuonyesha mabadiliko ya usawa wa mfumo mzima. Weka viboksi 2<br />

katika kila hatua kwenye mchoro. Kisha waweza punguza kimoja sehemu mojawapo<br />

hii itapelekea kupungua kwa idadi ya viumbe husika na kuongezeka kwa viumbe<br />

walioko chini zaidi ya mfumo huo hivyo yaweza kuathiri mfumo mzima.<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 32


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

1<br />

2 3<br />

4<br />

5 6<br />

7 8<br />

9<br />

10 11<br />

12<br />

13<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 33


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

8. Matembezi ya nyika hai<br />

8.1 Utangulizi<br />

Unapofundisha ni muhimu kutumia rasilimali zote zilizopo na zinazofikika.<br />

Kutembea na kuangulia mazingira yaliyopo huleta hamasa zaidi kwa ulimwengu huu<br />

wa kushangaza. Kujifunza toka kwenye mazingira halisi zaidi kuliko kwenye vitabu<br />

humwezesha mwanafunzi yeyote kuielewa hali ilivyo na kukubaliana na mazingira<br />

hayo kwa moyo wa dhati.<br />

Kwa mfano mikoko huweza kuonekana kwa haraka haraka kama mimea isiyo na<br />

faida hivyo hutumika tu hovyo hovyo bila kujali, lakini ukichunguza kwa uangalifu<br />

zaidi utagundua kuna idadi kubwa ya viumbe kama vile ndege, kaa, kamba, kome na<br />

vinginevyoo vilivyojizoesha kuishi kwenye mazingira haya magumu ya mikoko.<br />

Hakikisha wanafunzi wanapata muda na nafasi ya kutosha kujifunza kwenye<br />

mazingira halisi na pia ruhusu maswali.<br />

8.2 Lengo<br />

• Kuelewa jinsi viumbe vinavyoishi katika mazingira yake na binadamu<br />

anavyoweza kuathiri mfumo huo. Kujifunza darasani mara nyingi humaanisha<br />

kuelewa tu bila kukubaliana na hali halisi kwenye mazingira husika<br />

• Kwa kuzungukwa na mazingira asilia yanayotumika kujifunza hurahisisha<br />

ufundishaji na kuwawezesha washiriki kupata ujumbe kirahisi. Kuweza kuona<br />

jinsi mshabihiano laini wa viumbe na mazingira yao ulivyo yaweza kukazia<br />

uelewa unaoendana na uwajibikaji kwa jinsi ambavyo binadamu anaathiri viumbe<br />

hivyo, hivyo kubadili mwelekeo<br />

8.3 Jinsi ya kufanya<br />

• Orodhesha mifumo yote ya kimazingira inavyoweza kutembelewa ambayo<br />

binadamu anaathiri viumbe hai wake, kama vile mikoko, majani ya baharini na<br />

maeneo ya maji kupwa na kujaa<br />

• Chunguza ni lipi linaendena na mada ya siku husika<br />

• Panga ni jambo gani ni muhimu liangaliwe wakati wa kutembelea mahali hapo,<br />

kwa mfano unataka kuona athari ya binadamu kwenye msitu wa karibu au ndege<br />

waishio kwenye mikoko<br />

• Hakikisha kuna muda wa kujiandaa kwa washiriki juu ya maada husika, hii<br />

itarahisisha matembezi hayo<br />

• Chukua kibeseni kipana cha kuangalizia wanyama na mimea midogo midogo na<br />

vifaa vingine muhimu, kutegemea na lililokusudiwa kuelekezwa<br />

Tafadhali hakikisha hakuna kiumbe chochote kitakachoumizwa na mara baada ya<br />

kujifunza kirudishwe kilipokuwa<br />

.<br />

8.4 Mahitaji muhimu<br />

• Vifaa vya utafiti na maendeleo juu ya mfumo mzima wa mazingira na viumbe hai<br />

unaotegemewa<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 34


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

8.5 Mfano<br />

Kutembelea msitu wa mikoko<br />

Mambo muhimu unayoweza kujifunza / kufundisha<br />

• Aina ya Mikoko iliyopo na mpangilio wake<br />

• Maeneo inapostawi mikoko baharini<br />

• Aina ya udongo ndani ya mikoko<br />

• Idadi ya mikoko kwenye eneo la mraba<br />

• Urefu na umri wa mikoko<br />

• Viumbe wengine waishio ndani ya mikoko<br />

• Aina mbalimbali za mizizi na inavyofanya kazi kuchuja uchafu na matamahuruku<br />

• Athari za binadamu kwenye mikoko<br />

• Kama imeathirika sana, waweza pia kufundisha upandikizaji wake na namna ya<br />

kufanya zoezi hilo kwa vitendo<br />

N.B<br />

kumbuka elimu kwa vitendo hutolewa ili kumwezesha mwanafunzi kuzingatia<br />

zaidi alivyojifunza, hivyo shirikisha zaidi wanafuzi katika vitendo. Kama<br />

mwalimu jiepushe kuhodhi mambo yote darasani.<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 35


Elimu ya mazingira ya bahari ya kitropiki: Muongozo wa mwalimu<br />

Marejeo<br />

Collins Concise English Dictionary 2000 (1982) Harpers Collins Publishers, Great<br />

Britain.<br />

Eade, D and Williams, S. (1995) The Oxfam Handbook of Development and Relief<br />

Volume 1. Oxfam (UK and Ireland)<br />

Nybakken, J.W. (2001) Marine Biology: An ecological approach. 5 th Edition. Moss<br />

Landing. Addison Wesley Longman.<br />

Semesi, A.K., and Howell, K. (1989) The Mangroves of the East African Region.<br />

UNEP, Nairobi. 45pp.<br />

Semesi, A.K., Mgaya, Y.D., Muruke, M.H.S., Francis, J., Mtolera, M. and Msuni, G.<br />

(1998) Coastal resources utilization and conservation issues in Bagamoyo, <strong>Tanzania</strong>.<br />

Ambio Vol 27 No. 8:635-644. Royal Swedish Academy of Sciences. P635-644.<br />

10pp.<br />

<strong>Frontier</strong>-<strong>Tanzania</strong> <strong>Environmental</strong> <strong>Research</strong> Report <strong>100</strong> 36

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!