12.11.2012 Views

TAARIFA YA TATHMINI YA HALI YA VIWANDA - Tanzania Dairy ...

TAARIFA YA TATHMINI YA HALI YA VIWANDA - Tanzania Dairy ...

TAARIFA YA TATHMINI YA HALI YA VIWANDA - Tanzania Dairy ...

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

<strong>TAARIFA</strong> <strong>YA</strong> <strong>TATHMINI</strong> <strong>YA</strong> <strong>HALI</strong> <strong>YA</strong> <strong>VIWANDA</strong><br />

V<strong>YA</strong> KUSINDIKA MAZIWA TANZANIA OKTOBA 2006<br />

N.R. Mbwambo, C.M.D. Mutagwaba, M. Tsoxo na A.E. Temba<br />

1. UTANGULIZI<br />

Jukumu la kufanya mapitio lilitolewa na Katibu Mkuu, Wizara ya Maendeleo ya<br />

Mifugo. Madhumuni ya mapitio yalikuwa ni kutathmini hali ya viwanda vya<br />

kusindika maziwa ili kuweza kuandaa mikakati ya kuendeleza sekta. Jukumu<br />

lilitakiwa kuhusisha viwanda vyote yaani vinavyofanya kazi kwa sasa na ambavyo<br />

havifanyi kazi. Taarifa ya mapitio ilitakiwa kuainisha matatizo yanayovikabili<br />

viwanda na mapendekezo ya hali ya baadaye.<br />

2. NJIA ZA KUKUSAN<strong>YA</strong> TAKWIMU<br />

(i) Utambuzi wa viwanda:<br />

Kwa sasa hakuna orodha maalum na ya kuaminika inayoorodhesha<br />

viwanda vyote vya maziwa hapa nchini kwa hiyo njia kadhaa zilitumika<br />

nazo ni:<br />

(a) “Proceedings of the 4 th National <strong>Dairy</strong> Development Conference”,<br />

hususan mada ya, “The contribution of <strong>Dairy</strong> Industry to the<br />

National Economy, Poverty Alleviation and Household Food<br />

Security in <strong>Tanzania</strong>” ya Kurwijila, Ryoba na Kyomo, 2002.<br />

(b) Orodha ya Wanachama wa Chama cha Wasindikaji Maziwa<br />

<strong>Tanzania</strong> (TAMPA) na<br />

(c) “Proceedings of the 6 th National <strong>Dairy</strong> Development Conference”<br />

hususan mada ya “Value chain analysis and Socio-economic<br />

Assessment of the <strong>Dairy</strong> Industry in <strong>Tanzania</strong> iliyowasilishwa kwa<br />

pamoja na SCANAGRI na Business Care Services 2006.<br />

Vyanzo hivi vinaonekana kwa pamoja kutoa orodha ya kuaminika zaidi ya<br />

viwanda vya kusindika maziwa nchini kwa kuanzia.<br />

3. UKUSAN<strong>YA</strong>JI WA <strong>TAARIFA</strong> ZA AWALI.<br />

Iliandaliwa hojaji fupi na rahisi na kutumwa kwa barua-pepe kwenda kwa<br />

viwanda vilivyoorodheshwa kutumia njia iliyotajwa hapo juu (Kiambatanisho I).<br />

Aidha wenye viwanda/mameneja wa viwanda walihojiwa kwa simu. Njia ya simu<br />

ilisaidia sana kwa sababu viwanda vingi vilichukua muda mrefu kujibu barua<br />

pepe. Kwa viwanda vilivyopo Dar es Salaam mipango ya kuvitembelea<br />

iliandaliwa ambapo mahojiano ya kina ya ana kwa ana yalifanyika.<br />

4. MATOKEO <strong>YA</strong> AWALI<br />

1


Taarifa ya uwezo wa viwanda na hali halisi ilivyo sasa hivi inapatikana katika<br />

jedwali na.1. Inayonyesha kuwa hadi sasa hivi kuna viwanda 35 vyenye uwezo<br />

wa kusindika zaidi ya lita 1000 kwa siku kwa kila kimoja. Kati ya hivyo ni<br />

viwanda 28 tu ambavyo vinazalisha hadi sasa na vingine 7 ama vimefungwa au<br />

kusimamisha uzalishaji. Kuna baadhi ya viwanda vinatumia hadi zaidi ya 80% ya<br />

uwezo wake na vingine chini ya 16%. Kwa vile kuna viwanda visivyozalisha<br />

kabisa, wastani wa matumizi ya uwezo wa kusindika ni 12% tu.<br />

Uwezo wa jumla wa viwanda vyote ni kusindika, lita 428,500 kwa siku lakini hali<br />

halisi ni kusindika lita 52,330 kwa siku. Hali hii inaonyesha kuwa juhudi kubwa<br />

zinahitajika ili kuwezesha sekta ya viwanda vya maziwa kuwa na uwezo wa<br />

ushindani na kutoa mchango mkubwa kwenye uchumi wa taifa.<br />

5. MATATIZO <strong>YA</strong>NAYOATHIRI USINDIKAJI WA MAZIWA<br />

Matatizo yanayovikabili viwanda vya maziwa ni mengi na yanahitaji uchunguzi wa<br />

kina katika kila kiwanda ili kutoa ushauri kwa kila kiwanda husika, lakini matatizo<br />

yaliyotajwa na viwanda vyote ni kama yafuatayo:<br />

5.1 Ukosefu wa maziwa ya kutosha.<br />

Ingawa <strong>Tanzania</strong> inakadiriwa kuzalisha lita 1,400 milioni za maziwa kila mwaka<br />

kiasi cha maziwa yanayopatikana kwa ajili ya kusindika ni kidogo sana. Hali hii<br />

inatokana na maziwa mengi kuzalishwa na wafugaji wa jadi ambayo kiasi<br />

kikubwa kinatumika na wafugaji wenyewe, uzalishaji ni wa msimu na ukusanyaji<br />

ni mgumu. Wafugaji hawa ndio huzalisha 70% ya maziwa yote nchini.<br />

Upungufu wa maziwa ya kusindika ambao huwa zaidi wakati wa kiangazi<br />

unachangiwa na sababu nyingi ambazo ni:<br />

• Gharama kubwa na ugumu wa kukusanya maziwa ya wafugaji<br />

waliosambaa maeneo ya mbali<br />

• Ushindani na wachuuzi wadogo wadogo.<br />

• Faida ndogo kutokana na matumizi kidogo ya uwezo wa viwanda.<br />

• Uzalishaji wa msimu ambapo maziwa mengi hupatikana msimu wa mvua<br />

na kidogo sana wakati wa kiangazi na hivyo kushindwa kutosheleza<br />

2


Jedwali na. 1 Hali halisi ya viwanda vya kusindika Maziwa Mwezi Oktoba, 2006<br />

No. Mkoa Jina la kiwanda Hali ya sasa Uwezo wa<br />

kiwanda<br />

(lts)/siku<br />

Usindikaji<br />

kwa sasa<br />

(lts)/siku<br />

Matumizi<br />

ya uwezo<br />

(%)<br />

1 Dar es Salaam Royal <strong>Dairy</strong> Products Ltd Prod. suspended 90,000 0 0<br />

3 Azam <strong>Dairy</strong> Operating 3000<br />

4 Tommy <strong>Dairy</strong> Prod. suspended 15000 0 0<br />

5 Tan Dairies Operating 15000 4000 27<br />

6 Tanga Azania Dairies Ltd (Ex<br />

TDL)<br />

Operating 12,000 6000 50<br />

7 Tanga Fresh Operating 15000 14000 80<br />

8 Morani Operating 5000 1000 30<br />

9 Arusha Ex TDL New Northern<br />

Creamaries<br />

Operating 45000 2500 16<br />

10 International <strong>Dairy</strong> Products Operating 5000 1200 24<br />

11 Arusha <strong>Dairy</strong> Company Operating 5000 2000 40<br />

12 Kilimanjaro Nronga Women Operating 5000 2000 40<br />

13 West Kilimamnjaro Operating 1000 300 30<br />

14 Mboreni Women Operating 1000 200 20<br />

15 Marukeni Operating 1000 200 20<br />

16 Ng'uni Women Operating 1000 200 20<br />

17 Kalali Women Operating 1000 280 28<br />

18 Mara/Musoma Ex TDL Musoma <strong>Dairy</strong><br />

(Dr. Mazara)<br />

Closed 45000 0<br />

19 Ex TDL Utegi Plant<br />

(Otieno Igogo et.al)<br />

Closed 45000 0<br />

20 Baraki Sisters Operating 3000 2500 80<br />

21 New Mara Milk Operating 8000 4500 33<br />

22 Mwanza Victoria <strong>Dairy</strong> (Kishimba) Closed 45000 0<br />

23 Lake Side Closed 5000 0<br />

24 Kagera Kagera Milk (KADEFA) Operating 3000 350 12<br />

25 Kyaka Milk Plant Operating 1000 450 45<br />

26 Del Foods Operating 1000 250 25<br />

27 Mini Dairies (several) Operating 1800 1500 83<br />

28 Morogoro SUA Closed 3000 0<br />

29 Shambani Graduates Operating 700 250 36<br />

30 Tabora Ex TDL plant Closed 5000 0<br />

31 Coast Mojata Closed 6000 0<br />

32 Iringa ASAS <strong>Dairy</strong> Operating 12000 6500 54<br />

33 CEFA Njombe Milk<br />

Factory<br />

Operating 2,000 650 33<br />

34 Mbeya Ex TDL plant Closed/dismantle<br />

d<br />

16000 0<br />

35 Mbeya Maziwa Operating 1000 500 50<br />

JUMLA/<br />

WASTANI<br />

423,500 50,330 27<br />

3


wateja na hivyo wateja wengi kuhamia kwenye maziwa yanayotoka nje ya<br />

nchi.<br />

• Matumizi ya tecnolojia duni kama kutokuwa na uwezo wa kusindika<br />

maziwa kwa teknolojia ya UHT.<br />

5.2. Tatizo la soko.<br />

Matatizo ya soko yanatokana na sababu mbalimbali zikiwemo zifuatazo:<br />

• Sehemu kubwa ya jamii ya kitanzania kutokuwa na utamaduni wa<br />

kutumia maziwa. Matumizi ya maziwa kwa mtanzania kwa mwaka<br />

ni lita 39 tu. Mahitaji ya maziwa yakiongezeka yatavutia usindikaji.<br />

• Ushindani. Maziwa yaliyosindikwa ya <strong>Tanzania</strong> yanapatikana kwa<br />

msimu na kushindana na yanayotaka nje ya nchi yanayokuwapo<br />

muda wote na yanasindikwa kwa teknolojia ya UHT na hivyo<br />

kutohitaji jokofu kuyahifadhi.<br />

• Uhakika wa kupatikana. Kutokana na uzalishaji wa msimu<br />

upatikanaji wa maziwa ya hapa nchini hauna uhakika hivyo<br />

kupoteza wateja.<br />

• Usafiri – viwanda viko mbali na sehemu yanapopatikana maziwa au<br />

mbali na masoko makubwa na hivyo kuwa na gharama kubwa ya<br />

usafirishaji.<br />

• Kutokana na matatizo ya kutumia teknolojia duni maziwa ya hapa<br />

nchini hayafikii viwango vya ubora wa maziwa yanayoingizwa toka<br />

nchi za nje.<br />

• Kutokana na kutokuwa na vifaa vya kutosha vya usambazaji na<br />

miundombinu duni vijijini ukusanyaji na usambazaji huwa mgumu.<br />

5.3. Kutopatikana na Gharama kubwa ya vifaa vya kukusanyia<br />

maziwa:<br />

Hapa nchini hakuna viwanda vya kutengeneza vifaa vya kukusanyia<br />

maziwa kama makeni, matanki ya kupozea na kadhalika. Vifaa hivi<br />

huagizwa nchi za nje na vikifika bei yake inakuwa kubwa. Hali hii hufanya<br />

wasindikaji kushindwa kukusanya maziwa maeneo ya mbali na kiwanda.<br />

5.4. Ukosefu na gharama kubwa za pembejeo.<br />

Pembejeo zitumikazo kwenye usindikaji kama kimea (starter cultures) na<br />

vifungashio huagizwa toka nchi za nje na hivyo kufanya upatikanaji wake<br />

kuwa mgumu na bei kuwa ghali sana.<br />

4


5.5. Marufuku ya matumizi ya plastiki.<br />

Viwanda vyote vya maziwa hapa nchini hutumia vifungashio vya plastiki<br />

tu. Teknolojia ya kutumia vifungashio vya aina nyingine huhitaji mtaji<br />

mkubwa sana na pia huhitaji kiasi kukubwa cha maziwa. Aidha<br />

vifungashio vya plastiki hupunguza bei ya maziwa kwa mlaji na hivyo<br />

kuongeza matumizi ya maziwa. Ndiyo maana sehemu nyingi duniani sasa<br />

hivi wanahamia kwenye vifungashio vya plastiki hata kwa maziwa ya UHT.<br />

Kwa hiyo kupiga marufuku matumizi ya vifungashio vya plastiki kwenye<br />

maziwa ina maana ya kupiga marufuku usindikaji wa maziwa <strong>Tanzania</strong> na<br />

kutoa soko la <strong>Tanzania</strong> kwa maziwa ya nje. Aidha hali hii itafanya<br />

wafugaji wetu kukosa soko la uhakika wa maziwa yao na pia kuongeza<br />

matumizi ya maziwa yasiosindikwa ambayo siyo salama.<br />

5.6. Gharama kubwa za uwekezaji.<br />

Viwanda vya kusindika maziwa huhitaji mashine za gharama kubwa.<br />

Aidha msindikaji huhitaji mtaji mkubwa wa kuendeshea shughuli (working<br />

capital) ili aweze kuwalipa wafugaji hata kabla hajauza maziwa yake. Hii<br />

huhitaji mwekezaji apate mikopo wa riba ndogo na wa muda mrefu<br />

ambayo hapa nchini haipatikani.<br />

5.7. Matumizi ya teknolojia duni.<br />

Mahitaji ya mtaji mkubwa huwalazimisha wasindikaji hapa nchini kutumia<br />

teknolojia duni na hivyo kutoweza kutengeneza baadhi ya bidhaa kama<br />

UHT na kutoa bidhaa hafifu.<br />

5.8. Matatizo ya kimfumo na sera<br />

Katika kundi hili kuna matatizo kama urasimu katika vyombo vya kudhibiti<br />

ubora kama TBS, kuwa na vyombi vingi vya uthibiti, wadau<br />

kutoshirikishwa katika maandalizi ya sera, migogoro kati ya wafugaji na<br />

wasindikaji na vyama vya wadau visivyo imara.<br />

5.9. Matitizo mengineyo:<br />

Haya ni kama kipato kidogo cha wananchi, wawekezaji kuwa na miradi<br />

mingi kwa pamoja, sekta ya maziwa kutokuwa na mvuto kwa wawekezaji,<br />

ukosefu wa vyombo vya mikopo ya muda mrefu na riba ndogo na<br />

kutokuwa na maeneo maalum yenye miundombinu ya kutosha ya kujenga<br />

viwanda.<br />

6. MAPENDEKEZO <strong>YA</strong> NJIA ZA KUTATUA MATATIZO<br />

6.1. Kuongeza upatikanaji wa maziwa:<br />

Inapendekezwa kuongeza uzalishaji wa kila ng’ombe kwa kuboresha<br />

nasaba za ng’ombe wa maziwa, kuboresha mbinu za ulishaji, kuzuia na<br />

kutibu magonjwa na kuboresha matunzo kwa ujumla. Aidha kuna haja ya<br />

kuwekeza katika mashamba ya kati na makubwa ili kuongeza wingi wa<br />

maziwa kwenye eneo moja. Hii itahitaji serikali kushirikiana na wadau<br />

5


kuongeza upatikanaji wa ng’ombe bora wa maziwa, kufufua miradi ya<br />

kopa ng’ombe lipa ng’ombe, kuhamasisha uwekezaji katika mashamba<br />

makubwa, kuboresha miundombinu na upatikanaji wa mikopo nafuu na ya<br />

muda mrefu. Serikali pia ishirikiane na wadau kuimarisha vikundi vya<br />

wafugaji ili viwe na nguvu za kuweza kumiliki viwanda kama ilivyo kwa<br />

TDCU huko Tanga.<br />

6.2. Kupanua soko la ndani kwa:<br />

• Kuhamasiha jamii kutumia maziwa na hasa kulenga watoto na<br />

vijana kwa mipango ya maziwa mshuleni.<br />

• Kuwajengea wasindikaji uwezo wa kushindana kwa kuwawezesha<br />

kupata vifaa na teknolojia bora ili waweze kuzalisha bidhaa bora.<br />

Aidha serikali itatakiwa kulinda soko la ndani dhidi ya bidhaa<br />

zinazotelekezwa (damping).<br />

• Uhakika wa upatikanaji wa maziwa. Uhakika wa kupatikana<br />

maziwa ya kusindika kwa kipindi chote cha mwaka kutawezesha<br />

viwanda kuwatosheleza wateja muda wote na hivyo hawatahamia<br />

kwenye maziwa kutoka nje.<br />

• Kuboresha miundombinu kama barabara, umeme na upatikanaja<br />

wa vifaa na nyenzo za kukusanyia maziwa hata maeneo ya mbali<br />

6.3. Serikali kwa kushirikiana na wadu iwezeshe upatikanaji wa mashine, vifaa<br />

na mitambo kwa bei nafuu kwa kupunguzwa kodi, na kuagiza kwa wingi.<br />

Hii itawezesha viwanda kupata teknolojia ya kisasa.<br />

6.4. Pembejeo za gharama nafuu. Inapendekezwa serikali iondoe kodi<br />

zote kwenye pembejeo za usindikaji kama kimea (starter cultures)<br />

vifungashio n.k. Aidha kupitia TIC serikali ihamasishe uwekezaji kwenye<br />

viwanda vya mitambo na pembejeo za usindikaji hapa nchini.<br />

6.5. Kuondoa marufuku kwenye vifungushio vya plastiki. Vifungashio<br />

vya plastiki ndiyo pekee vinatumika hapa nchini kufungashia maziwa.<br />

Vifungashio mbadala vinahitaji uwekezaji mkubwa kwenye mitambo mipya<br />

na viwanda havina mtaji huo sasa. Aidha vifungshio mbadala ni ghali na<br />

hivyo vitapandisha bei ya maziwa kwa mlaji. Kama marufuku hii<br />

haitaondolewa usindikaji hapa nchini utakuwa umefungwa.<br />

6.6. Mitaji na gharama za uendeshaji. Kunahitajia kuwa na chombo cha<br />

mikopo ya uwekezaji kwenye sekta ya maziwa (<strong>Dairy</strong> Development Fund)<br />

kitakachotoa mikopo nafuu na ya muda mrefu (kama nchini India) aidha<br />

uanzishaji wa SACCOS unaweza kusaidia katika mikopo midogo midogo.<br />

Mazingira ya uwekezaji katika viwanda vya kutengeneza mitambo ya<br />

usindikaji na vifungshio hapa nchini yaboreshwe ili kuwavutia wawekezaji<br />

6


kwenye viwanda hivi. Aidha bidhaa za maziwa ziondolewe kodi ya VAT<br />

(Zero rating) kwa kipindi maalum kuwawezesha wasindikaji kujijengea<br />

uwezo wa ushindani kwenye soko la Afrika Mashariki.<br />

6.7. Kuboresha teknolojia ya usindikaji sambamba na kuongeza upatikanaji wa<br />

maziwa kuna haja na mafunzo kwa wafugaji na wa wasindikaji ili kuzalisha<br />

maziwa bora na kusindika bidhaa za aina mbalimbali na zenye ubora<br />

uaotakiwa.<br />

6.8. Kuboresha upatikanaji wa Taarifa na Takwimu.<br />

Kuna haja ya Serikali na Wadau kuanzisha mfumo wa kukusanya,<br />

kuchakata na kusambaza taarifa kuanzia vijijini kutumia maafisa ugani<br />

hadi Wizarani ili ziweze kuwa sahihi na kupatikana kwa haraka.<br />

6.9. Utatuzi wa maswala ya kisera.<br />

• Kuwepo uwajibikaji kwenye vyombo vya udhibiti na vyombo hivi<br />

madhumni yake, yawe ni kuwezesha na siyo kukwamisha.<br />

Inapendekezwa kuwa shughuli zote za udhibiti wa sekta ya maziwa<br />

zifanywe na Bodi ya Maziwa tofauti na sasa ambapo vyombo vingi<br />

hufanya hivyo;<br />

• Serikali iondoe kodi zote zenye kero kama ushuru unaotozwa na kila<br />

wilaya au zitozwe mara moja tu.<br />

• Wadau washirikishwe katika utayarishaji wa sera zinazohusu sekta ya<br />

maziwa.<br />

• Serkali itafute njia ya kuimarisha vyama vya kitaifa vya wadau (TAMPA,<br />

TAMPRODA) ili viwe kweli vya kitaifa na vyenye uwezo wa kushirkiana na<br />

Serikali kundeleza sekta.<br />

• Bodi ya Maziwa iliyoanzishwa kisheria iwezeshwe kufunya shughuli zake<br />

kwa kupewa rasilimali zinazotakiwa tofauti na sasa ambapo Bodi ipo kwa<br />

jina tu.<br />

• Uwepo mpango wa wafugaji wadogo kuzunguka mashamba makubwa<br />

(outgrowers scheme) ili nao wapate teknolojia toka kwenye mashamba<br />

makubwa.<br />

• Wahitimu vyuo vya mifugo na vyuo vikuu na wataamu wastaafu<br />

wawezeshwe kuwekeza kwenye sektka ya maziwa.<br />

• Serikali iwezeshe utafiti kufanyika katika sekta ya maziwa kuanzia kwenye<br />

uzalishaji hadi kwa mlaji.<br />

7


6.10 Utatuzi wa Matatizo mengineyo<br />

7. HITIMISHO<br />

• Miundumbinu iboreshwe ili kuwezesha maziwa kukusanywa toka maeneo<br />

ya mbali.<br />

• Bodi na vyama vya wadau wawezeshwe ili kutoa ushauri unaofaa ili<br />

wawekezaji waweze kushauriwa vizuri na pia kusimamia na kuondoa<br />

wawekezaji wasio na nia nzuri.<br />

Taarifa inaonyesha kuwa sekta ya usindikaji maziwa hapa nchini bado ni ndogo<br />

sana kulinganisha na nchi majirani. Ili sekta hii iweze kuhimili ushindani kutoka<br />

nje na kuweza kutoa mchango wake kwenye uchumi wa taifa juhudi kubwa<br />

hazina budi kufanyika na wadau wote pamoja na serikali. Matatizo yaliyotajwa ni<br />

kweli yapo na matokeo yake ni dhahiri katika viwanda vilivyosimamisha usindikaji<br />

na pia matumizi madogo ya uwezo wa viwanda vinavyoendelea kusindika.<br />

Matatizo haya ndiyo makubwa na yakitatuliwa yatawezesha sekta kukua kwa<br />

haraka na kutoa ushindani wa kutosha.<br />

Inapendekezwa kuwa njia zilizopendekezwa na wadau kutatua matatizo haya<br />

zijumuishwe kwenye mipango ya Bodi ya Maziwa na kwenye programu za<br />

utekelezaji wa sera ya maendeleo ya mifugo. Vyama vya Kitaifa vya wadau<br />

ambao ndiyo watekelezaji wakuu vipewe uwezo na vihusishwe kama wabia<br />

katika ngazi zote za utekelezaji. Aidha inapendekezwa kuwa, kwa vile<br />

haikuwezekana kufanya uchambuzi wa kina kwa kila kiwanda, uchambuzi huu<br />

uendelezwe hadi ngazi ya kila kiwanda na kila eneo ili kubaini na kuainisha<br />

matatizo ya kila kiwanda na hata kutoa ushauri kwa kila kiwanda na kutoa taarifa<br />

ya kina zaidi.<br />

8. MAREJEO<br />

1. K.R. Lusato, R. Ryoba na M.L. Kyomo, 2002. The contribution of <strong>Dairy</strong><br />

Industry to the National Economy, Poverty Alleviation and Household Food<br />

Security in <strong>Tanzania</strong>. In. Proceedings of the 4 th National <strong>Dairy</strong> Development<br />

Conference. 5 th – 6 th June 2002. AICC. Arusha <strong>Tanzania</strong>.<br />

2. UNDP/GSB – Value Chain Analysis and Socio economic Assessment of the<br />

<strong>Dairy</strong> Industry in <strong>Tanzania</strong>. Report presented by SCANAGRI and Business Care<br />

Services. In. Proceedings of the 6 th National <strong>Dairy</strong> Development Conference, 2 nd<br />

June 2006 Morogoro, <strong>Tanzania</strong>.<br />

Kiambatanisho na. 1<br />

DODOSO/QUESTIONNAIRE:<br />

INVENTORY REPORT ON MILK PROCESSING IN TANZANIA/<br />

8


<strong>TAARIFA</strong> <strong>YA</strong> <strong>TATHMINI</strong> <strong>YA</strong> MAENDELEO <strong>YA</strong> USINDIKAJI MAZIWA TANZANIA<br />

SECTION A/SEHEMU A: Company business profile/ Maelezo ya kiwanda.<br />

Fill the following table/<br />

Jaza jedwali lifuatalo<br />

Name/ x Designation/ x<br />

Jina:<br />

Cheo:<br />

Company name/ x Year of establishment /<br />

Jina la Kampuni<br />

Mwaka ulioanza<br />

Installed processing<br />

capacity (lts/day)/<br />

Uwezo wa kiwanda<br />

kusindika (lita/siku)<br />

Products processed in<br />

your factory/<br />

Aina ya bidhaa<br />

zinazosindikwa<br />

kiwandani kwako<br />

Employment (number<br />

of employees/<br />

Ajira (idadi ya<br />

wafanyakazi)<br />

x Actual (running)<br />

processing capacity<br />

(lts/day)/Uwezo<br />

halisi wa kiwanda<br />

kusindika (lita/siku)<br />

Maximum/<br />

Kiasi cha juu<br />

Minimum/<br />

Kiasi cha chini<br />

Type/Aina Amount (per year/<br />

Kiasi (kwa mwaka)<br />

x x<br />

x x<br />

x x<br />

x x<br />

x x<br />

x x<br />

Etc/n.k. Etc/n.k.<br />

Skilled labourers<br />

/Wataalam<br />

Unskilled labourers<br />

/Vibarua<br />

SECTION B/SEHEMU B: Problems/Matatizo<br />

What are the major problems facing your factory/business?<br />

Kiwanda/biashara yako/yenu inakumbana na matatizo gani?<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

x<br />

x<br />

x<br />

x<br />

x<br />

9


……………………………………………………………………………………………………<br />

……………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………<br />

SECTION C/SEHEMU C: Solutions/Suluhisho<br />

What should be done to solve problems faced by your factory/business?<br />

Nini kifanyike kutatua matatizo yanayokabili kiwanda/biashara yako/yenu?<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………<br />

SECTION D/SEHEMU D: Opinion/Maoni<br />

What are your opinions on how milk processing business can develop?/<br />

Toa maoni yako kwa vipi vinwanda/bishara ya usindikaji maziwa iweze kuendelea?<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………………………………………………………………………………………………<br />

……………<br />

10

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!