TAARIFA YA TATHMINI YA HALI YA VIWANDA - Tanzania Dairy ...
TAARIFA YA TATHMINI YA HALI YA VIWANDA - Tanzania Dairy ...
TAARIFA YA TATHMINI YA HALI YA VIWANDA - Tanzania Dairy ...
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
<strong>TAARIFA</strong> <strong>YA</strong> <strong>TATHMINI</strong> <strong>YA</strong> <strong>HALI</strong> <strong>YA</strong> <strong>VIWANDA</strong><br />
V<strong>YA</strong> KUSINDIKA MAZIWA TANZANIA OKTOBA 2006<br />
N.R. Mbwambo, C.M.D. Mutagwaba, M. Tsoxo na A.E. Temba<br />
1. UTANGULIZI<br />
Jukumu la kufanya mapitio lilitolewa na Katibu Mkuu, Wizara ya Maendeleo ya<br />
Mifugo. Madhumuni ya mapitio yalikuwa ni kutathmini hali ya viwanda vya<br />
kusindika maziwa ili kuweza kuandaa mikakati ya kuendeleza sekta. Jukumu<br />
lilitakiwa kuhusisha viwanda vyote yaani vinavyofanya kazi kwa sasa na ambavyo<br />
havifanyi kazi. Taarifa ya mapitio ilitakiwa kuainisha matatizo yanayovikabili<br />
viwanda na mapendekezo ya hali ya baadaye.<br />
2. NJIA ZA KUKUSAN<strong>YA</strong> TAKWIMU<br />
(i) Utambuzi wa viwanda:<br />
Kwa sasa hakuna orodha maalum na ya kuaminika inayoorodhesha<br />
viwanda vyote vya maziwa hapa nchini kwa hiyo njia kadhaa zilitumika<br />
nazo ni:<br />
(a) “Proceedings of the 4 th National <strong>Dairy</strong> Development Conference”,<br />
hususan mada ya, “The contribution of <strong>Dairy</strong> Industry to the<br />
National Economy, Poverty Alleviation and Household Food<br />
Security in <strong>Tanzania</strong>” ya Kurwijila, Ryoba na Kyomo, 2002.<br />
(b) Orodha ya Wanachama wa Chama cha Wasindikaji Maziwa<br />
<strong>Tanzania</strong> (TAMPA) na<br />
(c) “Proceedings of the 6 th National <strong>Dairy</strong> Development Conference”<br />
hususan mada ya “Value chain analysis and Socio-economic<br />
Assessment of the <strong>Dairy</strong> Industry in <strong>Tanzania</strong> iliyowasilishwa kwa<br />
pamoja na SCANAGRI na Business Care Services 2006.<br />
Vyanzo hivi vinaonekana kwa pamoja kutoa orodha ya kuaminika zaidi ya<br />
viwanda vya kusindika maziwa nchini kwa kuanzia.<br />
3. UKUSAN<strong>YA</strong>JI WA <strong>TAARIFA</strong> ZA AWALI.<br />
Iliandaliwa hojaji fupi na rahisi na kutumwa kwa barua-pepe kwenda kwa<br />
viwanda vilivyoorodheshwa kutumia njia iliyotajwa hapo juu (Kiambatanisho I).<br />
Aidha wenye viwanda/mameneja wa viwanda walihojiwa kwa simu. Njia ya simu<br />
ilisaidia sana kwa sababu viwanda vingi vilichukua muda mrefu kujibu barua<br />
pepe. Kwa viwanda vilivyopo Dar es Salaam mipango ya kuvitembelea<br />
iliandaliwa ambapo mahojiano ya kina ya ana kwa ana yalifanyika.<br />
4. MATOKEO <strong>YA</strong> AWALI<br />
1
Taarifa ya uwezo wa viwanda na hali halisi ilivyo sasa hivi inapatikana katika<br />
jedwali na.1. Inayonyesha kuwa hadi sasa hivi kuna viwanda 35 vyenye uwezo<br />
wa kusindika zaidi ya lita 1000 kwa siku kwa kila kimoja. Kati ya hivyo ni<br />
viwanda 28 tu ambavyo vinazalisha hadi sasa na vingine 7 ama vimefungwa au<br />
kusimamisha uzalishaji. Kuna baadhi ya viwanda vinatumia hadi zaidi ya 80% ya<br />
uwezo wake na vingine chini ya 16%. Kwa vile kuna viwanda visivyozalisha<br />
kabisa, wastani wa matumizi ya uwezo wa kusindika ni 12% tu.<br />
Uwezo wa jumla wa viwanda vyote ni kusindika, lita 428,500 kwa siku lakini hali<br />
halisi ni kusindika lita 52,330 kwa siku. Hali hii inaonyesha kuwa juhudi kubwa<br />
zinahitajika ili kuwezesha sekta ya viwanda vya maziwa kuwa na uwezo wa<br />
ushindani na kutoa mchango mkubwa kwenye uchumi wa taifa.<br />
5. MATATIZO <strong>YA</strong>NAYOATHIRI USINDIKAJI WA MAZIWA<br />
Matatizo yanayovikabili viwanda vya maziwa ni mengi na yanahitaji uchunguzi wa<br />
kina katika kila kiwanda ili kutoa ushauri kwa kila kiwanda husika, lakini matatizo<br />
yaliyotajwa na viwanda vyote ni kama yafuatayo:<br />
5.1 Ukosefu wa maziwa ya kutosha.<br />
Ingawa <strong>Tanzania</strong> inakadiriwa kuzalisha lita 1,400 milioni za maziwa kila mwaka<br />
kiasi cha maziwa yanayopatikana kwa ajili ya kusindika ni kidogo sana. Hali hii<br />
inatokana na maziwa mengi kuzalishwa na wafugaji wa jadi ambayo kiasi<br />
kikubwa kinatumika na wafugaji wenyewe, uzalishaji ni wa msimu na ukusanyaji<br />
ni mgumu. Wafugaji hawa ndio huzalisha 70% ya maziwa yote nchini.<br />
Upungufu wa maziwa ya kusindika ambao huwa zaidi wakati wa kiangazi<br />
unachangiwa na sababu nyingi ambazo ni:<br />
• Gharama kubwa na ugumu wa kukusanya maziwa ya wafugaji<br />
waliosambaa maeneo ya mbali<br />
• Ushindani na wachuuzi wadogo wadogo.<br />
• Faida ndogo kutokana na matumizi kidogo ya uwezo wa viwanda.<br />
• Uzalishaji wa msimu ambapo maziwa mengi hupatikana msimu wa mvua<br />
na kidogo sana wakati wa kiangazi na hivyo kushindwa kutosheleza<br />
2
Jedwali na. 1 Hali halisi ya viwanda vya kusindika Maziwa Mwezi Oktoba, 2006<br />
No. Mkoa Jina la kiwanda Hali ya sasa Uwezo wa<br />
kiwanda<br />
(lts)/siku<br />
Usindikaji<br />
kwa sasa<br />
(lts)/siku<br />
Matumizi<br />
ya uwezo<br />
(%)<br />
1 Dar es Salaam Royal <strong>Dairy</strong> Products Ltd Prod. suspended 90,000 0 0<br />
3 Azam <strong>Dairy</strong> Operating 3000<br />
4 Tommy <strong>Dairy</strong> Prod. suspended 15000 0 0<br />
5 Tan Dairies Operating 15000 4000 27<br />
6 Tanga Azania Dairies Ltd (Ex<br />
TDL)<br />
Operating 12,000 6000 50<br />
7 Tanga Fresh Operating 15000 14000 80<br />
8 Morani Operating 5000 1000 30<br />
9 Arusha Ex TDL New Northern<br />
Creamaries<br />
Operating 45000 2500 16<br />
10 International <strong>Dairy</strong> Products Operating 5000 1200 24<br />
11 Arusha <strong>Dairy</strong> Company Operating 5000 2000 40<br />
12 Kilimanjaro Nronga Women Operating 5000 2000 40<br />
13 West Kilimamnjaro Operating 1000 300 30<br />
14 Mboreni Women Operating 1000 200 20<br />
15 Marukeni Operating 1000 200 20<br />
16 Ng'uni Women Operating 1000 200 20<br />
17 Kalali Women Operating 1000 280 28<br />
18 Mara/Musoma Ex TDL Musoma <strong>Dairy</strong><br />
(Dr. Mazara)<br />
Closed 45000 0<br />
19 Ex TDL Utegi Plant<br />
(Otieno Igogo et.al)<br />
Closed 45000 0<br />
20 Baraki Sisters Operating 3000 2500 80<br />
21 New Mara Milk Operating 8000 4500 33<br />
22 Mwanza Victoria <strong>Dairy</strong> (Kishimba) Closed 45000 0<br />
23 Lake Side Closed 5000 0<br />
24 Kagera Kagera Milk (KADEFA) Operating 3000 350 12<br />
25 Kyaka Milk Plant Operating 1000 450 45<br />
26 Del Foods Operating 1000 250 25<br />
27 Mini Dairies (several) Operating 1800 1500 83<br />
28 Morogoro SUA Closed 3000 0<br />
29 Shambani Graduates Operating 700 250 36<br />
30 Tabora Ex TDL plant Closed 5000 0<br />
31 Coast Mojata Closed 6000 0<br />
32 Iringa ASAS <strong>Dairy</strong> Operating 12000 6500 54<br />
33 CEFA Njombe Milk<br />
Factory<br />
Operating 2,000 650 33<br />
34 Mbeya Ex TDL plant Closed/dismantle<br />
d<br />
16000 0<br />
35 Mbeya Maziwa Operating 1000 500 50<br />
JUMLA/<br />
WASTANI<br />
423,500 50,330 27<br />
3
wateja na hivyo wateja wengi kuhamia kwenye maziwa yanayotoka nje ya<br />
nchi.<br />
• Matumizi ya tecnolojia duni kama kutokuwa na uwezo wa kusindika<br />
maziwa kwa teknolojia ya UHT.<br />
5.2. Tatizo la soko.<br />
Matatizo ya soko yanatokana na sababu mbalimbali zikiwemo zifuatazo:<br />
• Sehemu kubwa ya jamii ya kitanzania kutokuwa na utamaduni wa<br />
kutumia maziwa. Matumizi ya maziwa kwa mtanzania kwa mwaka<br />
ni lita 39 tu. Mahitaji ya maziwa yakiongezeka yatavutia usindikaji.<br />
• Ushindani. Maziwa yaliyosindikwa ya <strong>Tanzania</strong> yanapatikana kwa<br />
msimu na kushindana na yanayotaka nje ya nchi yanayokuwapo<br />
muda wote na yanasindikwa kwa teknolojia ya UHT na hivyo<br />
kutohitaji jokofu kuyahifadhi.<br />
• Uhakika wa kupatikana. Kutokana na uzalishaji wa msimu<br />
upatikanaji wa maziwa ya hapa nchini hauna uhakika hivyo<br />
kupoteza wateja.<br />
• Usafiri – viwanda viko mbali na sehemu yanapopatikana maziwa au<br />
mbali na masoko makubwa na hivyo kuwa na gharama kubwa ya<br />
usafirishaji.<br />
• Kutokana na matatizo ya kutumia teknolojia duni maziwa ya hapa<br />
nchini hayafikii viwango vya ubora wa maziwa yanayoingizwa toka<br />
nchi za nje.<br />
• Kutokana na kutokuwa na vifaa vya kutosha vya usambazaji na<br />
miundombinu duni vijijini ukusanyaji na usambazaji huwa mgumu.<br />
5.3. Kutopatikana na Gharama kubwa ya vifaa vya kukusanyia<br />
maziwa:<br />
Hapa nchini hakuna viwanda vya kutengeneza vifaa vya kukusanyia<br />
maziwa kama makeni, matanki ya kupozea na kadhalika. Vifaa hivi<br />
huagizwa nchi za nje na vikifika bei yake inakuwa kubwa. Hali hii hufanya<br />
wasindikaji kushindwa kukusanya maziwa maeneo ya mbali na kiwanda.<br />
5.4. Ukosefu na gharama kubwa za pembejeo.<br />
Pembejeo zitumikazo kwenye usindikaji kama kimea (starter cultures) na<br />
vifungashio huagizwa toka nchi za nje na hivyo kufanya upatikanaji wake<br />
kuwa mgumu na bei kuwa ghali sana.<br />
4
5.5. Marufuku ya matumizi ya plastiki.<br />
Viwanda vyote vya maziwa hapa nchini hutumia vifungashio vya plastiki<br />
tu. Teknolojia ya kutumia vifungashio vya aina nyingine huhitaji mtaji<br />
mkubwa sana na pia huhitaji kiasi kukubwa cha maziwa. Aidha<br />
vifungashio vya plastiki hupunguza bei ya maziwa kwa mlaji na hivyo<br />
kuongeza matumizi ya maziwa. Ndiyo maana sehemu nyingi duniani sasa<br />
hivi wanahamia kwenye vifungashio vya plastiki hata kwa maziwa ya UHT.<br />
Kwa hiyo kupiga marufuku matumizi ya vifungashio vya plastiki kwenye<br />
maziwa ina maana ya kupiga marufuku usindikaji wa maziwa <strong>Tanzania</strong> na<br />
kutoa soko la <strong>Tanzania</strong> kwa maziwa ya nje. Aidha hali hii itafanya<br />
wafugaji wetu kukosa soko la uhakika wa maziwa yao na pia kuongeza<br />
matumizi ya maziwa yasiosindikwa ambayo siyo salama.<br />
5.6. Gharama kubwa za uwekezaji.<br />
Viwanda vya kusindika maziwa huhitaji mashine za gharama kubwa.<br />
Aidha msindikaji huhitaji mtaji mkubwa wa kuendeshea shughuli (working<br />
capital) ili aweze kuwalipa wafugaji hata kabla hajauza maziwa yake. Hii<br />
huhitaji mwekezaji apate mikopo wa riba ndogo na wa muda mrefu<br />
ambayo hapa nchini haipatikani.<br />
5.7. Matumizi ya teknolojia duni.<br />
Mahitaji ya mtaji mkubwa huwalazimisha wasindikaji hapa nchini kutumia<br />
teknolojia duni na hivyo kutoweza kutengeneza baadhi ya bidhaa kama<br />
UHT na kutoa bidhaa hafifu.<br />
5.8. Matatizo ya kimfumo na sera<br />
Katika kundi hili kuna matatizo kama urasimu katika vyombo vya kudhibiti<br />
ubora kama TBS, kuwa na vyombi vingi vya uthibiti, wadau<br />
kutoshirikishwa katika maandalizi ya sera, migogoro kati ya wafugaji na<br />
wasindikaji na vyama vya wadau visivyo imara.<br />
5.9. Matitizo mengineyo:<br />
Haya ni kama kipato kidogo cha wananchi, wawekezaji kuwa na miradi<br />
mingi kwa pamoja, sekta ya maziwa kutokuwa na mvuto kwa wawekezaji,<br />
ukosefu wa vyombo vya mikopo ya muda mrefu na riba ndogo na<br />
kutokuwa na maeneo maalum yenye miundombinu ya kutosha ya kujenga<br />
viwanda.<br />
6. MAPENDEKEZO <strong>YA</strong> NJIA ZA KUTATUA MATATIZO<br />
6.1. Kuongeza upatikanaji wa maziwa:<br />
Inapendekezwa kuongeza uzalishaji wa kila ng’ombe kwa kuboresha<br />
nasaba za ng’ombe wa maziwa, kuboresha mbinu za ulishaji, kuzuia na<br />
kutibu magonjwa na kuboresha matunzo kwa ujumla. Aidha kuna haja ya<br />
kuwekeza katika mashamba ya kati na makubwa ili kuongeza wingi wa<br />
maziwa kwenye eneo moja. Hii itahitaji serikali kushirikiana na wadau<br />
5
kuongeza upatikanaji wa ng’ombe bora wa maziwa, kufufua miradi ya<br />
kopa ng’ombe lipa ng’ombe, kuhamasisha uwekezaji katika mashamba<br />
makubwa, kuboresha miundombinu na upatikanaji wa mikopo nafuu na ya<br />
muda mrefu. Serikali pia ishirikiane na wadau kuimarisha vikundi vya<br />
wafugaji ili viwe na nguvu za kuweza kumiliki viwanda kama ilivyo kwa<br />
TDCU huko Tanga.<br />
6.2. Kupanua soko la ndani kwa:<br />
• Kuhamasiha jamii kutumia maziwa na hasa kulenga watoto na<br />
vijana kwa mipango ya maziwa mshuleni.<br />
• Kuwajengea wasindikaji uwezo wa kushindana kwa kuwawezesha<br />
kupata vifaa na teknolojia bora ili waweze kuzalisha bidhaa bora.<br />
Aidha serikali itatakiwa kulinda soko la ndani dhidi ya bidhaa<br />
zinazotelekezwa (damping).<br />
• Uhakika wa upatikanaji wa maziwa. Uhakika wa kupatikana<br />
maziwa ya kusindika kwa kipindi chote cha mwaka kutawezesha<br />
viwanda kuwatosheleza wateja muda wote na hivyo hawatahamia<br />
kwenye maziwa kutoka nje.<br />
• Kuboresha miundombinu kama barabara, umeme na upatikanaja<br />
wa vifaa na nyenzo za kukusanyia maziwa hata maeneo ya mbali<br />
6.3. Serikali kwa kushirikiana na wadu iwezeshe upatikanaji wa mashine, vifaa<br />
na mitambo kwa bei nafuu kwa kupunguzwa kodi, na kuagiza kwa wingi.<br />
Hii itawezesha viwanda kupata teknolojia ya kisasa.<br />
6.4. Pembejeo za gharama nafuu. Inapendekezwa serikali iondoe kodi<br />
zote kwenye pembejeo za usindikaji kama kimea (starter cultures)<br />
vifungashio n.k. Aidha kupitia TIC serikali ihamasishe uwekezaji kwenye<br />
viwanda vya mitambo na pembejeo za usindikaji hapa nchini.<br />
6.5. Kuondoa marufuku kwenye vifungushio vya plastiki. Vifungashio<br />
vya plastiki ndiyo pekee vinatumika hapa nchini kufungashia maziwa.<br />
Vifungashio mbadala vinahitaji uwekezaji mkubwa kwenye mitambo mipya<br />
na viwanda havina mtaji huo sasa. Aidha vifungshio mbadala ni ghali na<br />
hivyo vitapandisha bei ya maziwa kwa mlaji. Kama marufuku hii<br />
haitaondolewa usindikaji hapa nchini utakuwa umefungwa.<br />
6.6. Mitaji na gharama za uendeshaji. Kunahitajia kuwa na chombo cha<br />
mikopo ya uwekezaji kwenye sekta ya maziwa (<strong>Dairy</strong> Development Fund)<br />
kitakachotoa mikopo nafuu na ya muda mrefu (kama nchini India) aidha<br />
uanzishaji wa SACCOS unaweza kusaidia katika mikopo midogo midogo.<br />
Mazingira ya uwekezaji katika viwanda vya kutengeneza mitambo ya<br />
usindikaji na vifungshio hapa nchini yaboreshwe ili kuwavutia wawekezaji<br />
6
kwenye viwanda hivi. Aidha bidhaa za maziwa ziondolewe kodi ya VAT<br />
(Zero rating) kwa kipindi maalum kuwawezesha wasindikaji kujijengea<br />
uwezo wa ushindani kwenye soko la Afrika Mashariki.<br />
6.7. Kuboresha teknolojia ya usindikaji sambamba na kuongeza upatikanaji wa<br />
maziwa kuna haja na mafunzo kwa wafugaji na wa wasindikaji ili kuzalisha<br />
maziwa bora na kusindika bidhaa za aina mbalimbali na zenye ubora<br />
uaotakiwa.<br />
6.8. Kuboresha upatikanaji wa Taarifa na Takwimu.<br />
Kuna haja ya Serikali na Wadau kuanzisha mfumo wa kukusanya,<br />
kuchakata na kusambaza taarifa kuanzia vijijini kutumia maafisa ugani<br />
hadi Wizarani ili ziweze kuwa sahihi na kupatikana kwa haraka.<br />
6.9. Utatuzi wa maswala ya kisera.<br />
• Kuwepo uwajibikaji kwenye vyombo vya udhibiti na vyombo hivi<br />
madhumni yake, yawe ni kuwezesha na siyo kukwamisha.<br />
Inapendekezwa kuwa shughuli zote za udhibiti wa sekta ya maziwa<br />
zifanywe na Bodi ya Maziwa tofauti na sasa ambapo vyombo vingi<br />
hufanya hivyo;<br />
• Serikali iondoe kodi zote zenye kero kama ushuru unaotozwa na kila<br />
wilaya au zitozwe mara moja tu.<br />
• Wadau washirikishwe katika utayarishaji wa sera zinazohusu sekta ya<br />
maziwa.<br />
• Serkali itafute njia ya kuimarisha vyama vya kitaifa vya wadau (TAMPA,<br />
TAMPRODA) ili viwe kweli vya kitaifa na vyenye uwezo wa kushirkiana na<br />
Serikali kundeleza sekta.<br />
• Bodi ya Maziwa iliyoanzishwa kisheria iwezeshwe kufunya shughuli zake<br />
kwa kupewa rasilimali zinazotakiwa tofauti na sasa ambapo Bodi ipo kwa<br />
jina tu.<br />
• Uwepo mpango wa wafugaji wadogo kuzunguka mashamba makubwa<br />
(outgrowers scheme) ili nao wapate teknolojia toka kwenye mashamba<br />
makubwa.<br />
• Wahitimu vyuo vya mifugo na vyuo vikuu na wataamu wastaafu<br />
wawezeshwe kuwekeza kwenye sektka ya maziwa.<br />
• Serikali iwezeshe utafiti kufanyika katika sekta ya maziwa kuanzia kwenye<br />
uzalishaji hadi kwa mlaji.<br />
7
6.10 Utatuzi wa Matatizo mengineyo<br />
7. HITIMISHO<br />
• Miundumbinu iboreshwe ili kuwezesha maziwa kukusanywa toka maeneo<br />
ya mbali.<br />
• Bodi na vyama vya wadau wawezeshwe ili kutoa ushauri unaofaa ili<br />
wawekezaji waweze kushauriwa vizuri na pia kusimamia na kuondoa<br />
wawekezaji wasio na nia nzuri.<br />
Taarifa inaonyesha kuwa sekta ya usindikaji maziwa hapa nchini bado ni ndogo<br />
sana kulinganisha na nchi majirani. Ili sekta hii iweze kuhimili ushindani kutoka<br />
nje na kuweza kutoa mchango wake kwenye uchumi wa taifa juhudi kubwa<br />
hazina budi kufanyika na wadau wote pamoja na serikali. Matatizo yaliyotajwa ni<br />
kweli yapo na matokeo yake ni dhahiri katika viwanda vilivyosimamisha usindikaji<br />
na pia matumizi madogo ya uwezo wa viwanda vinavyoendelea kusindika.<br />
Matatizo haya ndiyo makubwa na yakitatuliwa yatawezesha sekta kukua kwa<br />
haraka na kutoa ushindani wa kutosha.<br />
Inapendekezwa kuwa njia zilizopendekezwa na wadau kutatua matatizo haya<br />
zijumuishwe kwenye mipango ya Bodi ya Maziwa na kwenye programu za<br />
utekelezaji wa sera ya maendeleo ya mifugo. Vyama vya Kitaifa vya wadau<br />
ambao ndiyo watekelezaji wakuu vipewe uwezo na vihusishwe kama wabia<br />
katika ngazi zote za utekelezaji. Aidha inapendekezwa kuwa, kwa vile<br />
haikuwezekana kufanya uchambuzi wa kina kwa kila kiwanda, uchambuzi huu<br />
uendelezwe hadi ngazi ya kila kiwanda na kila eneo ili kubaini na kuainisha<br />
matatizo ya kila kiwanda na hata kutoa ushauri kwa kila kiwanda na kutoa taarifa<br />
ya kina zaidi.<br />
8. MAREJEO<br />
1. K.R. Lusato, R. Ryoba na M.L. Kyomo, 2002. The contribution of <strong>Dairy</strong><br />
Industry to the National Economy, Poverty Alleviation and Household Food<br />
Security in <strong>Tanzania</strong>. In. Proceedings of the 4 th National <strong>Dairy</strong> Development<br />
Conference. 5 th – 6 th June 2002. AICC. Arusha <strong>Tanzania</strong>.<br />
2. UNDP/GSB – Value Chain Analysis and Socio economic Assessment of the<br />
<strong>Dairy</strong> Industry in <strong>Tanzania</strong>. Report presented by SCANAGRI and Business Care<br />
Services. In. Proceedings of the 6 th National <strong>Dairy</strong> Development Conference, 2 nd<br />
June 2006 Morogoro, <strong>Tanzania</strong>.<br />
Kiambatanisho na. 1<br />
DODOSO/QUESTIONNAIRE:<br />
INVENTORY REPORT ON MILK PROCESSING IN TANZANIA/<br />
8
<strong>TAARIFA</strong> <strong>YA</strong> <strong>TATHMINI</strong> <strong>YA</strong> MAENDELEO <strong>YA</strong> USINDIKAJI MAZIWA TANZANIA<br />
SECTION A/SEHEMU A: Company business profile/ Maelezo ya kiwanda.<br />
Fill the following table/<br />
Jaza jedwali lifuatalo<br />
Name/ x Designation/ x<br />
Jina:<br />
Cheo:<br />
Company name/ x Year of establishment /<br />
Jina la Kampuni<br />
Mwaka ulioanza<br />
Installed processing<br />
capacity (lts/day)/<br />
Uwezo wa kiwanda<br />
kusindika (lita/siku)<br />
Products processed in<br />
your factory/<br />
Aina ya bidhaa<br />
zinazosindikwa<br />
kiwandani kwako<br />
Employment (number<br />
of employees/<br />
Ajira (idadi ya<br />
wafanyakazi)<br />
x Actual (running)<br />
processing capacity<br />
(lts/day)/Uwezo<br />
halisi wa kiwanda<br />
kusindika (lita/siku)<br />
Maximum/<br />
Kiasi cha juu<br />
Minimum/<br />
Kiasi cha chini<br />
Type/Aina Amount (per year/<br />
Kiasi (kwa mwaka)<br />
x x<br />
x x<br />
x x<br />
x x<br />
x x<br />
x x<br />
Etc/n.k. Etc/n.k.<br />
Skilled labourers<br />
/Wataalam<br />
Unskilled labourers<br />
/Vibarua<br />
SECTION B/SEHEMU B: Problems/Matatizo<br />
What are the major problems facing your factory/business?<br />
Kiwanda/biashara yako/yenu inakumbana na matatizo gani?<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
x<br />
x<br />
x<br />
x<br />
x<br />
9
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………<br />
SECTION C/SEHEMU C: Solutions/Suluhisho<br />
What should be done to solve problems faced by your factory/business?<br />
Nini kifanyike kutatua matatizo yanayokabili kiwanda/biashara yako/yenu?<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………<br />
SECTION D/SEHEMU D: Opinion/Maoni<br />
What are your opinions on how milk processing business can develop?/<br />
Toa maoni yako kwa vipi vinwanda/bishara ya usindikaji maziwa iweze kuendelea?<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………………………………………………………………………………………………<br />
……………<br />
10