JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - Tanzania Online Gateway
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - Tanzania Online Gateway JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - Tanzania Online Gateway
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA RIPOTI YA HUDUMA ZA AFYA TANZANIA BARA 2004 Imetayarishwa na: Idara ya Tiba Afya Makao Makuu P.O. Box 9083, DAR ES SALAAM June 2005
- Page 2 and 3: Yaliyomo Ukurasa Vifupisho 4 Utangu
- Page 4 and 5: VIFUPISHO ADB ADDO ARVs BADEA BF CC
- Page 6 and 7: 1.0 RIPOTI YA HUDUMA ZA AFYA MAKAO
- Page 8 and 9: • Kufanya ukarabati wa majengo ya
- Page 10 and 11: 2.2 Sera na Mipango o Kukamilisha u
- Page 12 and 13: • Umekwishakamilisha mpango wake
- Page 14 and 15: Katika kufanikisha mipango ya upati
- Page 16 and 17: Wizara pia ilizindua Mpango wa Taif
- Page 18 and 19: 2.3.4 Mpango wa Taifa wa Huduma za
- Page 20 and 21: Katika kipindi cha 2004/2005, watoa
- Page 22 and 23: Aidha, Wizara iliandaa na kusambaza
- Page 24 and 25: Mpaka sasa kati ya Halmashauri 113
- Page 26 and 27: 2.3.15 Mradi wa Uimarishaji Huduma
- Page 28 and 29: 2.4.3 Huduma za Afya ya Kinywa Kati
- Page 30 and 31: Matarajio ya Huduma ya Dawa, Vifaa
- Page 32 and 33: Matarajio ya Huduma za Utawala na W
- Page 34 and 35: • Kufuatilia, kutathmini na kutoa
- Page 36 and 37: kuzingatia kuwa, UKIMWI sasa ni tat
- Page 38 and 39: Katika mwaka wa fedha wa 2005/2006
- Page 40 and 41: Taasisi pia iliandaa mwongozo wa ki
- Page 42 and 43: Jangwa la Sahara na hatimaye kuonge
- Page 44 and 45: Utafiti wa Malaria Katika kipindi c
- Page 46 and 47: Pamoja na mafanikio mengi yaliyopat
- Page 48 and 49: 4.0 RIPOTI YA HUDUMA ZA AFYA MIKOA
- Page 50 and 51: 700.0 648 Mchoro 2: Kasi ya Vifo Vy
<strong>JAMHURI</strong> <strong>YA</strong> <strong>MUUNGANO</strong> <strong>WA</strong> <strong>TANZANIA</strong><br />
WIZARA <strong>YA</strong> AF<strong>YA</strong><br />
RIPOTI <strong>YA</strong> HUDUMA ZA AF<strong>YA</strong> <strong>TANZANIA</strong> BARA 2004<br />
Imetayarishwa na:<br />
Idara ya Tiba<br />
Afya Makao Makuu<br />
P.O. Box 9083,<br />
DAR ES SALAAM June 2005
Yaliyomo<br />
Ukurasa<br />
Vifupisho 4<br />
Utanguli 5<br />
1.1 Ripotiya Huduma za Aya Makao Makuu 2004/2005 6<br />
1.2 Dira/Mwelekeo (Vision ya Wizara) 6<br />
1.3 Majukumu ya Wizara ya Afya 6<br />
1.4 Azma (Mission) ya Wizara ya Afya 6<br />
1.5 Malengo ya Wizara ya Afya 6<br />
1.6 Maeneo yaliyopewa Kipaumbele 2004/2005 7<br />
1.7 Muhtasari wa kazi zilizopangwa kutekelezwa na Wizara ya Afya 2004/2005 8<br />
2.0 Utekelezaji wa Majukumu Afya Makao Makuu 2004/2005 9<br />
2.1 Mipango ya Maendeleo 9<br />
2.2 Sera na Mipango 10<br />
2.2.1 Mabadiliko katika Sekta ya Afya 10<br />
2.2.2 Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya 11<br />
2..2.3 Mfumo wa Taarifa za Uendeshaji wa Huduma za Afya 13<br />
2.3. Huduma za Kinga 14<br />
2.3.1 Udhibiti wa wa Magonjwa ya Kuambukiza 14<br />
2.3.2 Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Malaria 15<br />
2.3.3 Mpango wa Taifa wa Kifua Kikuu na Ukoma 16<br />
2.3.4 Mpango wa Taifa wa Kuzuia Upofu na Kudhibti Ugonjwa wa Usubi 18<br />
2.3.5 Huduma ya Elimu ya Afya kwa Umma 19<br />
2.3.6 Huduma ya Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto 19<br />
2.3.7 Mkakati wa Kutibu Magonjwa ya Watoto kwa Uwiano 20<br />
2.3.8 Mpango wa Taifa wa Chanjo 21<br />
2.3.9 Huduma ya Afya Shuleni 21<br />
2.3.10 Afya ya Mazingira 21<br />
2.3.11 Huduma za Afya Mipakani 22<br />
2.3.12 Afya katika Sehemu za Kazi 23<br />
2.3.13 Huduma za Afya Wilayani (District Health Services) 23<br />
2.3.14 UKIMWI 24<br />
2.3.15 Mradi wa Uimarishaji wa Huduma Muhimu za Afya 25<br />
2.4 Huduma za Tiba 26<br />
2.4.1 Huduma za Uchunguzi wa Magonjwa 26<br />
2.4.2 Huduma za Tiba Asili 27<br />
2.4.3 Hudma za Afya ya Kinywa 28<br />
2.4.4 Huduma za Afya ya Akili na Vita Dhidi ya Dawa za Kulevya 28<br />
2.4.5 Huduma za hospitali za Mshirika ya Kujitolea na Watu Binafsi 29<br />
2.4.6 Huduma ya Dawa, Vifaa na Vifaa Tiba 29<br />
2.4.7 Huduma za Kuzuia Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI kutoka kwa Mama kwenda kwa Mtoto 30<br />
2.4.8 Huduma ya Matibabu ya Nje ya Nchi 30<br />
2.5 Hudma ya Utawala na Utawala na Utumishi 31<br />
2.5.1 Idara ya Utawala 31<br />
2.6 Huduma ya Mafunzo ya Watumishi 32<br />
2.7 Ofisi ya Mganga Mkuu Kiongozi 34<br />
2.7.1 Huduma za Dharura na Maafa 34<br />
2.7.2 Ukaguzi wa Huduma za Afya 35<br />
2.7.3 Huduma za Uuguzi na Ukunga 35<br />
2.8 Uhasibu na Fedha 36<br />
2.8.1 Ukusanyaji wa Mapato 36<br />
2.8.2 Matumizi ya Fedha za kawaida 37<br />
2.8.3 Matumizi ya Fedha za Miradi ya Maendeleo 37<br />
3.0 Taasisi na Mamlaka zilizo chini ya Wizara ya Afya 39<br />
3.1 Taasisi ya Chakula na Lishe <strong>Tanzania</strong> (TFNC) 39<br />
3.2 Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali 40<br />
3.3 Mamlaka ya Chakula na Dawa 42<br />
3.4 Taasisi yaTaifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu 43<br />
3.5 Matatizo na changamoto 45<br />
3.6 Maeneo yaliyopewa kipaumbele mwaka 2005/2006 46<br />
4.0 Ripoti ya huduma za Afya Mikoa 48<br />
4.1 Utangulizi 48<br />
4.2 Mchanganuo wa Watu katika 48<br />
4.3 Mchanganuo wa hali ya Vifo vya Watoto na Mama wajawazito katika Mikoa 48<br />
4.4 Mchanganuo wa Maeneo ya kiutawala katika Mikoa 50<br />
4.5a Uwiano wa Wataalam wa Afya na Idadi ya Watu 50<br />
4.5b Uwiano wa Wataalam wa Afya ya Kinywa (Dental) na Idadi ya Watu 53<br />
4.6 Idadi ya Vituo vya kutolea Tiba na Umiliki wake 53<br />
4.7 Idadi ya vitanda vya kulaza wagonjwa kwa kufuata miliki ya Vituo vya kutolea tiba 56<br />
2
4.8 Watumishi wa Sekta ya Afya na Sehemu za Kazi 58<br />
4.9a Magari na Pikipiki 58<br />
4.9b Hadubini 59<br />
4.9c Mashine za X-ray 59<br />
4.9d Vifaa vya Utakasaji 60<br />
4.9e Vifaa vya Tiba ya Meno 60<br />
4.10 Magonjwa yanayotolewa Taarifa 61<br />
4.11 Magonjwa yaliyojitokeza kwa Wagonjwa wa Nje 64<br />
4.12 Magonjwa yaliyojitokeza kwa Wagonjwa Waliolazwa 66<br />
4.13 Taarifa ya Huduma Maalum 68<br />
4.14 Aina za X-ray zilizopigwa 69<br />
4.15 Huduma za Maabara 69<br />
4.16 Matokeo ya Vipimo vya Maabara 70<br />
4.17 Huduma za kliniki ya Meno 70<br />
4.18 Mahudhurio ya kliniki kwa Mama Wajawazito 71<br />
4.19 Mama wajawazito kujifungua 71<br />
4.20 Huduma kwa Mama waliojifungua 72<br />
4.21 Matatizo ya akinamama wakati wa kujifungua 72<br />
4.22 Sababu za Vifo vya Mama wajawazito 73<br />
4.23a Taarifa ya watoto waliozaliwa mmojammoja 74<br />
4.23b Taarifa ya Watoto waliozaliwa zaidi ya mmoja 74<br />
4.24 Idadi ya watoto chini ya mwaka mmoja waliopata chanjo 75<br />
4.25 Chanjo ya TT2+ kwa akinamama wajawazito 77<br />
4.26 Wateja wa uzazi wa mpango wanaoendelea na Huduma 77<br />
4.27 Watoto waliopata matone ya Vitamin A 78<br />
4.28 Kiwango cha Watoto wenye Utapiamlo Mkali 80<br />
4.29 Kiwango cha Kaya zenye vyoo vinavyokubalika na maji toka vyanzo salama 80<br />
4.30 Mapato na vyanzo vyake 81<br />
4.31 Fedha zilizotumika 82<br />
5.0 Ripoti ya Hospitali za Rufaa 84<br />
5.1 Utangulizi 84<br />
5.2 Ripoti ya huduma zilizotolewa 88<br />
5.2.1 Mahudhurio ya Nje 88<br />
5.2.2 Wagonjwa waliolazwa 89<br />
5.2.3 Magonjwa yaliyojitokeza kwa mahudhurio ya nje 89<br />
5.2.4 Magonjwa Kumi yaliyoongoza kwa Mahudhurio ya Nje 90<br />
5.2.5 Magonjwa yaliyojitokeza kwa Wagonjwa wa Ndani 91<br />
5.2.6 Magonjwa yaliyojitokeza kwa Wagonjwa waliolazwa Idara ya “Internal Medicine” 92<br />
5.2.7 Magonjwa yaliyojitokeza kwa Wagonjwa waliolazwa Wodi ya Upasuaji 92<br />
5.2.8 Huduma za Upasuaji 92<br />
5.2.9 Magonjwa ya Akinamama (Ggynaecology) 94<br />
5.2.10 Sababu za kulazwa Mama wajawazito 94<br />
5.2.11 Kujifungua Mama Wajawazito 95<br />
5.2.12 Aina ya kujifungua Mama Wajawazito 95<br />
5.2.13 Matokeo ya kujifungua Mama Wajawazito 96<br />
5.2.14 Sababu ya Vifo vya Mama Wajawazito 96<br />
5.2.15 Sababu za kulazwa na vifo wodi za watoto 97<br />
5.2.16 Sababu ya Vifo vya watoto wa umri chini ya mwaka mmoja 97<br />
5.2.17 Magonjwa ya Macho kwa waliolazwa 98<br />
5.2.18 Magonjwa ya Akili kwa waliolazwa 98<br />
5.2.19 Magonjwa ya Kinywa 99<br />
5.2.20 Idara ya Vipimo vya Maabara 99<br />
5.2.21 Takwamu za Damu Salama 100<br />
5.2.22 Takwimu za X-ray zilizopigwa 101<br />
5.2.23 Takwimu za kipimo cha Ultrasound 101<br />
5.2.24 Takwimu za kipimo cha CT Scan 102<br />
5.2.25 Takwimu za Watumishi 103<br />
5.2.26 Takwimu za Madaktari Bingwa 103<br />
5.2.27 Taarifa ya Fedha za Kuendesha Huduma 104<br />
5.3 Mafanikio na Matatizo katika Hospitali za Rufaa 105<br />
6.0 Ripoti za Hospitali za Huduma Maalum 107<br />
6.1 Hospitali ya Kibongoto 107<br />
6.2 Taasisi ya Tiba ya Magonjwa ya Mifupa MOI 107<br />
6.3 Hospitali ya Mirembe na Taasisi ya Mirembe 108<br />
6.4 Taasisi ya Saratani Ocean Road 109<br />
7.0 Ushirikiano na Nchi za Nje 110<br />
8.0 Shukrani 111<br />
3
VIFUPISHO<br />
ADB<br />
ADDO<br />
ARVs<br />
BADEA<br />
BF<br />
CCHP<br />
CHSB<br />
CDC<br />
CEDHA<br />
CHF<br />
CLP<br />
CUAMM<br />
DANIDA<br />
DDH<br />
DFID<br />
DOTS<br />
EEG<br />
EOP<br />
EPI<br />
EU<br />
HFGC<br />
GAVI<br />
GTZ<br />
ICU<br />
IDRC<br />
IMCI<br />
ITI<br />
JICA<br />
KCMC<br />
KfW<br />
MDRTB<br />
MDT<br />
MKUKUTA<br />
MOI<br />
MoU<br />
MSF<br />
MTUHA<br />
MUHUMA<br />
NACTE<br />
NEPHI<br />
NIMR<br />
OC<br />
OPD<br />
ORCI<br />
OREC<br />
OPET<br />
PHCI<br />
PMTCT<br />
DOTS<br />
PPM<br />
RHMT<br />
SAFI<br />
SAREC<br />
SDC<br />
SIDA<br />
SP<br />
STI<br />
S<strong>WA</strong>P<br />
TAMISEMI<br />
TALGWU<br />
TFDA<br />
TFNC<br />
TIKA<br />
TUGHE<br />
UKIMWI<br />
UNHCR<br />
UNDP<br />
UNFPA<br />
UNICEF<br />
USAID<br />
VAs<br />
VCT<br />
VVF<br />
WB<br />
WHO<br />
ZBTC<br />
African Development Bank<br />
Accredited Drug Dispensing Outlets<br />
Anti Retro Viral Drugs<br />
Bangue Arabe pour Development Economique en Afrique<br />
Basket Funds<br />
Comprehensive Council Health Plans<br />
Council Health Services Board<br />
Centre for Disease Control and Prevention<br />
Centre for Education in Health Development Arusha<br />
Community Health Fund (Mfuko wa Afya ya Jamii)<br />
Central Pathology Laboratory<br />
International College for Health Cooperation in Developing Countries<br />
Danish International Development Agency<br />
Designated District Hospital<br />
United Kingdom Department for International Development<br />
Directly Observed Treatment Short Course<br />
Electro Encephalogram<br />
Emergency Operational Plan<br />
Expanded Programme of Immunization<br />
European Union<br />
Health Facility Governing Committee<br />
Globed Fund for Vaccine Initiative<br />
Gesellschaft fuer Technische Zusammenarbeit<br />
Intensive Care Unit<br />
International Development Research Centre of Canada<br />
Integrated Management of Childhood Illnesses<br />
International Trachoma Initiate<br />
Japan International Cooperation Agency<br />
Kilimanjaro Christian Medical Centre<br />
German Bank for Development<br />
Multi Drug Resistant TB<br />
Multi Drugs Therapy<br />
Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini <strong>Tanzania</strong><br />
Muhimbili Orthopedic Institute<br />
Memorandum of Understanding<br />
Medicine Sans Frontieres<br />
Mfumo wa Taarifa za Uendeshaji wa Huduma za Afya<br />
Mradi wa Uimarishaji wa Huduma za Afya<br />
National Council for Technical Education<br />
National Essential Package of Health Interventions<br />
Institute for Medical Research<br />
Other Charges<br />
Out Patient Department<br />
Ocean Road Cancer Institute<br />
Organization of Petroleum Producing Countries<br />
Overseas Related Export Trade<br />
Primary Health Care Institute<br />
Prevention of Mother to Child Transmission<br />
Directly Observed Treatment Short Course<br />
Planned Preventive Maintenance<br />
Regional Health Management Team<br />
Sawazisha Kope, Anza Matibabu Mapema, Fanya Usafi wa Uso na Mwili Imarisha Mazingira<br />
Swedish Agency for Research Cooperation in Leading Countries<br />
Swiss Agency for Development and Cooperation<br />
Swedish International Development Authority<br />
Sulphurdoxine Pyrimethemine<br />
Sexually Transmitted Infections<br />
Sector Wide Approach Programme<br />
Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa<br />
<strong>Tanzania</strong> Local Government Workers Union<br />
<strong>Tanzania</strong> Food and Drug Authority<br />
<strong>Tanzania</strong> Food and Nutrition Centre<br />
Tiba kwa Kadi<br />
<strong>Tanzania</strong> Union for Government Health Employees<br />
Ukosefu wa Kinga Mwilini<br />
United Nations High Commission for Refugees<br />
United Nations Development Programme<br />
United Nations Fund for Population Activities<br />
United Nations Children Fund<br />
United States Agency for International Development<br />
Voluntary Agencies<br />
Voluntary Councelling and Testing<br />
Vesicle Vaganal Fistula<br />
World Bank<br />
Word Health Organization<br />
Zonal Blood Transfusion Centres<br />
4
Utangulizi<br />
Katika kipindi cha mwaka 2004/05, Huduma za Afya nchini ziliendelea kuimarika. Malengo<br />
yaliyowekwa katika kipindi hicho yalitekelezwa kwa ufanisi na vipaumbele vya Wizara pia<br />
vilifikiwa. Pamoja na mafanikio yaliyofikiwa katika kipindi hicho kulikuwa na tatizo la takwimu<br />
kutokamilika katika Sekta ya Afya. Kwa ujumla wake bado limeendelea kujitokeza katika<br />
uandikaji wa taarifa za mwaka za hospitali za Rufaa na Mikoa. Kutokana na hali hiyo bado ipo<br />
haja ya kuzingatia umakini katika kupata takwimu sahihi za utendaji kwani ndizo zitakazosaidia<br />
kutoa takwimu sahihi ya hali ya magonjwa na hali halisi ya Huduma za Afya Nchini. Matatizo<br />
yaliyojitokeza katika taarifa zetu za utendaji za mwaka yanatoa changamoto kwetu sisi watendaji<br />
tujipange upya katika kutekeleza majukumu yetu katika Sekta ya Afya. Aidha, takwimu<br />
zimeonyesha kushuka kwa viashiria vingi vya hali ya Afya katika taarifa za mwaka za Mikoa na<br />
Hospitali za Rufaa. Iwapo hapatakuwa na juhudi za kutosha za kurekebisha hali hiyo ni wazi<br />
kwamba hali ya Huduma ya Afya itazidi kushuka na hivyo kuathiri afya za wananchi. Kutokana<br />
na hali hiyo zinahitajika jitihada za kutosha za kujifunza kwa Mikoa/Hospitali iliyofanya vizuri ili<br />
kasoro zilizojitokeza ziweze kurekebishwa. Changamoto la tatizo la UKIMWI linataka kujipanga<br />
upya ili kutekeleza wajibu wetu katika kutoa huduma za afya kwa Watanzania.<br />
5
1.0 RIPOTI <strong>YA</strong> HUDUMA ZA AF<strong>YA</strong> MAKAO MAKUU 2004/2005<br />
1.1 Utangulizi<br />
Kwa mwaka 2004/2005 huduma za afya nchini ziliendelea kutolewa kwa kuzingatia sera,<br />
miongozo, mipango na mikakati mbalimbali iliyowekwa na Wizara ya Afya. Kazi<br />
zilizopangwa kufanyika katika kipind hiki zililenga dira, malengo na majukumu yaliyopewa<br />
kipaumbele. Vyote hivi ni mwendelezo wa utekelezaji wa mipango na mikakati iliyowekwa<br />
katika mwaka 2003/2004.<br />
1.2 Dira/Mwelekeo (Vision) ya Wizara<br />
Dira ya Wizara ya Afya ni “ Kutoa huduma za afya zenye ubora wa hali ya juu zinazofaa<br />
na zinazofikiwa na kutumiwa na wananchi wote kulingana na mahitaji yao kupitia<br />
mfumo wa afya ulio imara na endelevu”.<br />
1.3 Majukumu ya Wizara<br />
Ili kuiwezesha Wizara kufikia dira yake inatakiwa kutekeleza majukumu yafuatayo:-<br />
• Kusimamia Sera na kutayarisha miongozo ya Afya ya huduma za Kinga na Tiba<br />
• Kudhibiti kemikali na kuendesha uchunguzi wa kisayansi wa sababu za vifo<br />
• Kusimamia na kudhibiti ubora wa dawa, vifaa tiba, vipodozi na vyakula<br />
• Kuendeleza huduma za Tiba ya Asili<br />
• Kusimamia Mpango wa Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto<br />
• Ukaguzi wa huduma za afya<br />
• Kuandaa na kusimamia programu za mafunzo ya wataalamu wa afya na kuwaendeleza<br />
kitaaluma watumishi wa sekta ya afya<br />
• Kuinua kiwango cha ushirikiano kati ya Wizara, mashirika ya umma na dini, sekta<br />
binafsi, idara na miradi mbalimbali ya afya katika kuongeza na kuimarisha ubora wa<br />
huduma za afya<br />
• Kutafuta rasilimali na vyanzo vya kutosha vya fedha na kuhakikisha matumizi bora ya<br />
watumishi wa afya, fedha na vifaa<br />
• Kuongoza na kusimamia wakala za Serikali, taasisi na mashirika ya umma yaliyo chini<br />
ya Wizara ya Afya<br />
• Kushirikiana na jumuia za kimataifa katika kuimarisha huduma za Afya.<br />
1.4 Azma (Mission) ya Wizara ya Afya<br />
Azma ya Wizara ya Afya ni kutoa huduma za afya kulingana na mahitaji, kusimamia sera na<br />
kutayarisha miongozo sahihi inayowezesha upatikanaji wa wataalamu wa afya wenye ari na<br />
hamasa ili kuboresha afya hasa ya wale walio katika hatari ya kuugua zaidi.<br />
1.5 Malengo ya Wizara ya Afya<br />
• Kupunguza magonjwa na idadi ya vifo kwa makundi yanayoathirika zaidi hasa watoto<br />
wachanga, na walio chini ya miaka mitano, chipukizi ambao hawajafikisha umri wa<br />
kwenda shule na walio shuleni, vijana, watu wenye ulemavu, wazee na wanawake<br />
walio katika umri wa uzazi na kuongeza umri wa kuishi<br />
6
• Kuhakikisha kuwa huduma muhimu na za msingi za afya zinasaidiwa na kusimamiwa<br />
kwa utaratibu sahihi wa huduma za rufaa, utafiti, takwimu zenye mgawanyo wa kijinsia<br />
na kuwahusisha kikamilifu wananchi<br />
• Kufanya tathmini na kudhibiti usalama na ubora wa vyakula, dawa, kemikali na<br />
vipodozi ili kulinda afya ya wananchi wote na mazingira kwa ujumla<br />
• Kuzuia na kudhibiti magonjwa yanayoambukiza na yasiyoambukiza yakiwemo<br />
Malaria, Kifua Kikuu, Utapiamlo na yale mengine yanaohusiana na afya ya mazingira,<br />
afya kazini, matumizi ya kemikali<br />
• Kupanga mafunzo ya watumishi na kujitosheleza kwa wataalam wa afya wenye uwezo<br />
na ujuzi katika kada mbali mbali kwa kuzingatia uwiano wa kijinsia katika kutoa<br />
huduma za afya katika ngazi zote<br />
• Kuainisha mahitaji na kukarabati miundo mbinu ya afya kwa kuzingatia huduma<br />
zinazotolewa kwa watu wenye ulemavu na kuweka mfumo wa matengenezo ya<br />
majengo ya afya, mitambo na vifaa<br />
• Kufanya mapitio, kutayarisha, kuhamasisha, kueneza, kufuatilia na kutathmini sera ya<br />
afya, mipango na bajeti, miongozo, sheria za afya za viwango mbali mbali vya huduma,<br />
kanuni na taratibu zinazohakikisha huduma za afya zinatolewa kwa ubora unaotakiwa<br />
• Kuweka mazingira mazuri ya kazi na vitendea kazi kwa ajili ya kutoa huduma bora na<br />
muhimu za kiutendaji na utawala zenye kuzingatia jinsia.<br />
1.6 Maeneo yaliyopewa kipaumbele 2004/2005<br />
Maeneo yaliyopewa kipaumbele ni yale yaliyolenga katika kupunguza umasikini, magonjwa<br />
na vifo kwa wananchi wote, kuongeza umri wa kuishi na ubora wa maisha. Maeneo hayo<br />
yaliainishwa kama yafuatayo:-<br />
• Kuzipatia hospitali, vituo vya afya na zahanati dawa muhimu na vifaa vya hospitali<br />
• Kuimarisha huduma za hospitali za rufaa kwa kuzipatia vifaa vya hospitali, vifaa vya<br />
uchunguzi na dawa za maabara. Vifaa hivi huwawezesha waganga kugundua tatizo<br />
mapema na kutoa tiba sahihi<br />
• Udhibiti na uzuiaji wa Malaria<br />
• Kutoa mafunzo ya kitaalamu ya watarajali (pre-service) ya wataalam wa afya na ya<br />
kujiendeleza kwa kada zote za afya<br />
• Kuimarisha huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto, kwa kusambaza dawa za uzazi<br />
wa mpango, vifaa vya uzazi na kutoa mafunzo kwa waganga na wauguzi jinsi ya<br />
kutambua, kuainisha na kutoa tiba sahihi kwa magonjwa ya watoto kwa kupitia<br />
mpango wa uwiano wa kutibu magonjwa ya watoto (IMCI)<br />
• Kuimarisha huduma za chanjo kwa kununua dawa za chanjo, vifaa na vipuli kwa ajili<br />
ya mnyororo baridi<br />
• Udhibiti na uzuiaji wa kuenea kwa Kifua Kikuu na Ukoma<br />
• Kuboresha hali ya elimu ya lishe nchini<br />
• Kuimarisha afya na usafi wa mazingira nchini kote<br />
• Kuzipatia fedha hospitali Teule (DDH) na mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) ili<br />
kuongeza uwezo wa kutoa huduma kwa wananchi katika sehemu zisizo na vituo vya<br />
afya vya Serikali<br />
• Kutekeleza majukumu ya sekta ya afya katika kudhibiti ugonjwa wa UKIMWI<br />
• Kutumia matokeo ya utafiti yanayotolewa na taasisi mbalimbali za utafiti katika kutoa<br />
mapendekezo ya sera, miongozo na mipango mbali mbali ya afya<br />
• Kutoa mchango wa Serikali katika miradi yote inayopewa fedha na wahisani mbali<br />
mbali<br />
7
• Kufanya ukarabati wa majengo ya afya yaliyo katika hali mbaya na vifaa vya tiba na<br />
kuweka utaratibu wa kufanya matengenezo ya kinga (Planned Preventive Maintainance<br />
PPM)<br />
• Kufanya uchunguzi wa vyakula, dawa na kemikali, kutoa ushauri wa kitaalam na<br />
kutambua vyanzo vya vifo kwa kufanya uchunguzi wa kisayansi<br />
• Kusimamia na kudhibiti kemikali za viwandani na majumbani, utakaotekelezwa na<br />
Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali.<br />
1.7 Muhtasari wa kazi zilizopangwa kutekelezwa na Wizara ya Afya 2004/2005<br />
Katika kipindi hiki kazi zilizopangwa kutekelezwa na Wizara ya Afya kwa kutumia fedha za<br />
matumizi ya kawaida na miradi ya maendeleo, imefuata vipaumbele vilivyoanishwa hapo juu.<br />
Kazi hizo ni kama zifuatavyo:-<br />
• Kutoa dawa na vifaa vya hospitali kwa zahanati, vituo vya afya na hospitali katika<br />
ngazi zote ili kuiwezesha Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kutoa<br />
huduma muhimu za afya kwa wananchi<br />
• Kutoa ruzuku kwa hospitali za mashirika ya dini<br />
• Kusimamia, kufuatilia na kutathmini huduma za afya zitolewazo na Serikali za Mitaa,<br />
Mikoa, hospitali za Rufaa na Taifa<br />
• Kuimarisha huduma za chanjo, kuendeleza ubadilishaji wa mfumo wa uendeshaji wa<br />
majokofu ya chanjo kutoka matumizi ya mafuta ya taa kwenda katika matumizi ya gesi.<br />
Shughuli za chanjo zitaendelea kuimarishwa kote nchini<br />
• Kutekeleza mpango wa ukarabati na matengenezo ya hospitali za Mikoa na za Rufaa.<br />
Karakana Kuu za Kanda za vifaa na za ukarabati zitatumika kusaidia hospitali za<br />
Mikoa na Serikali za Mitaa kuanzisha uhakikimali na kuweka viwango kamili vya vifaa<br />
vya kutolea huduma za afya vinavyotumiwa na vituo vinavyotoa huduma za afya<br />
• Kufuatilia na kusimamia ubora na usalama wa chakula, dawa na vipodozi<br />
utakaotekelezwa na Mamlaka ya Taifa ya Chakula na Dawa (TFDA) kwa kutoa<br />
huduma za ukaguzi, usajili wa uzalishaji, majaribio na uchunguzi wa kimaabara wa<br />
sampuli ili kuhakikisha kuwa wazalishaji, wasafirishaji nje, waagizaji, wasambazaji na<br />
wauzaji wanazingatia ubora, viwango, taratibu na matendo ya utunzaji yanayokubalika<br />
• Kuzuia magonjwa ya kuambukiza na yasiyo ya kuambukiza hasa Malaria, UKIMWI,<br />
Kifua Kikuu na Utapiamlo. Hatua zitakazochukuliwa zitajumuisha uimarishaji na<br />
kuinua elimu ya afya na usimamizi wa kemikali<br />
• Kuweka kipaumbele katika utekelezaji wa mkakati mpya wa sekta ya afya wa<br />
kupambana na UKIMWI kwa kuhakikisha mpango huu unatekelezwa na kila idara<br />
umeingizwa katika mpango wa afya wa mwaka wa kila Halmashauri ya Wilaya.<br />
• Kutoa huduma za tiba kwa wagonjwa wa UKIMWI na magonjwa yanayoambatana<br />
nayo, kutoa ushauri nasaha na kupunguza unyanyapaa kwa walioathirika<br />
• Kutoa mafunzo kwa wataalamu mbalimbali wa afya juu ya tiba sahihi ya Malaria<br />
katika Wilaya zote nchini, uhamasishaji juu ya utumiaji wa vyandarua vyenye<br />
viuatilifu, utafiti wa usugu wa vimelea vya Malaria na tiba mseto<br />
• Kuhakikisha usalama wa damu, kuzuia maambukizi ya UKIMWI kwa mtoto toka kwa<br />
mama, kuhamasisha uzuiaji wa kuenea kwa UKIMWI kupitia ngono, uaminifu kwa<br />
mpenzi mmoja na matumizi ya kondom<br />
• Kuchukua hatua ambazo zitaongeza upatikanaji wa dawa za kupunguza makali ya<br />
UKIMWI kwa kushirikiana na wahisani na mifuko mbali mbali kama vile “Global<br />
Fund, The Bill and Melinda Gates Foundation”, “Clinton Foundation” na “President G.<br />
W. Bush Initiatives”<br />
8
• Kutekeleza mikakati ya pamoja ya kudhibiti maambukizi ya Kifua Kikuu na UKIMWI,<br />
kutoa dawa za Kifua Kikuu na Ukoma katika vituo vyote vya matibabu. Kufanya utafiti<br />
wa kitaifa wa Kifua Kikuu na kampeni za kutokomeza Ukoma<br />
• Kuendelea kutoa kipaumbele kwa magonjwa mengine kwa kutekeleza mipango na kazi<br />
zinazolenga utoaji wa huduma muhimu za afya kwa jamii, huduma za afya ngazi ya<br />
Wilaya na katika hospitali za Mikoa na Rufaa<br />
• Kuimarisha mipango ya mafunzo ya wataalamu na kuboresha mafunzo katika vyuo<br />
vyake ili kuhakikisha elimu inayotolewa na vyuo hivyo inakuwa bora zaidi. Kuweka<br />
mkazo zaidi katika mafunzo ya kujiendeleza ili kuwaongezea ujuzi na utaalamu<br />
wafanyakazi wa afya katika ngazi zote. Kuandaa mipango ya mafunzo endelevu ya<br />
wafanyakazi ambayo itatengenezwa kulingana na mahitaji ya kazi<br />
• Kukarabati majengo na vifaa vya kutolea huduma za afya na kukamilisha uchunguzi<br />
utakaosaidia uandaaji wa mpango wa maendeleo wa miaka 10 wa huduma za hospitali<br />
• Kukamilisha mapitio ya Sera ya Taifa ya Afya kwa kujumuisha maoni yaliyotolewa na<br />
wadau wengine wa afya<br />
• Kuwasilisha muswada wa sheria ya Afya ya Jamii katika Wizara ya Sheria na Mambo<br />
ya Katiba ili ukamilishwe na uwasilishwe bungeni<br />
• Kuimarisha ushirikiano na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa<br />
• Kutoa mafunzo ya huduma za dharura kwa wazazi kwa kufundisha waalimu 12 wa<br />
kitaifa na 80 kutoka Mikoani.<br />
2.0 UTEKELEZAJI <strong>WA</strong> MAJUKUMU AF<strong>YA</strong> MAKAO MAKUU 2004/2005<br />
2.1 Mipango ya Maendeleo<br />
Mwaka 2004/05 Wizara ya Afya ilitengewa kiasi cha shilingi 91,215,753,600/= kwa ajili ya<br />
utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Kati ya kiasi hicho, jumla ya shilingi 3,552,448,200/=<br />
zilitolewa na Serikali ya <strong>Tanzania</strong> na kiasi cha shilingi 87, 663, 305,400/= zilitoka kwa<br />
wahisani mbalimbali, wakiwemo wahisani wanaochangia Mfuko wa Pamoja wa Afya (Health<br />
Basket Fund). Fedha hizo zimetumika kutekeleza miradi ifuatayo: -<br />
• Ukarabati wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Wizara iliendelea kushirikiana na Benki ya<br />
Maendeleo ya Afrika (ADB) ili kukamilisha ukarabati mkubwa unaoendelea katika<br />
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Ukarabati huu unaenda sambamba na ununuzi na<br />
ufungaji wa vifaa mbalimbali kwa ajili ya Hospitali ya Taifa Muhimbili na hospitali za<br />
Manispaa za Ilala, Temeke na Kinondoni<br />
• Kuendeleza ujenzi wa wodi ya watoto (Paediatric Ward Complex)<br />
• Kuimarisha Hospitali Maalum na za Rufaa<br />
o Ukarabati wa majengo ya huduma ya wagonjwa wa nje, upasuaji, mfumo wa<br />
maji taka katika hospitali ya Meta mjini Mbeya, pamoja na ukarabati wa kijiji<br />
cha wagonjwa wa akili Isanga<br />
o Kutayarisha michoro kwa ajili ya ujenzi wa hosteli ya madaktari wanafunzi<br />
(Intern Doctors) na kukamilisha ujenzi wa chumba cha wagonjwa mahututi<br />
(ICU) katika hospitali ya Rufaa Mbeya<br />
o Ununuzi wa vifaa vya tiba kwa ajili ya hospitali za rufaa na maalum<br />
o Serikali imeweza kutoa mchango wake wote kama ilivyopangwa katika Taasisi<br />
ya Mifupa Muhimbili (MOI)<br />
o Serikali iliweza kukarabati majengo ya vyuo vya mafunzo ya afya nchini<br />
o Serikali imeweza kumalizia kutoa mchango wake wote (counterpart fund) ili<br />
kununua vifaa vya Taasisi ya Mifupa ya Muhimbili – MOI<br />
o Udhibiti wa magonjwa ya kuambukiza<br />
9
2.2 Sera na Mipango<br />
o Kukamilisha ujenzi wa jengo la ofisi za Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya<br />
Binaadamu (NIMR) Tukuyu<br />
o Kufanya ukarabati wa mifumo ya njia za umeme kwenye jengo la ofisi za<br />
Huduma za Mama na Mtoto Dar es Salaam<br />
o Kufanya ukarabati wa ofisi, mabweni na madarasa katika vyuo 33 vya afya<br />
vilivyo chini ya Wizara<br />
o Kuvipatia vituo vyote vya afya dawa na vifaa kwa ajili ya kukinga na kutibu<br />
magonjwa ya zinaa – STIs<br />
o Kukomboa na kusambaza dawa za ugonjwa wa Kifua Kikuu na Ukoma. Serikali<br />
imetoa mchango wake (counterpart funds) kwenye mradi kwa ajili ya kudhibiti<br />
magonjwa haya<br />
o Kutayarisha na kusambaza vitabu vya Mfumo wa Taarifa za Uendeshaji Huduma<br />
za Afya (MTUHA) nchi nzima.<br />
2.2.1 Mabadiliko katika Sekta ya Afya (Health Sector Reforms)<br />
Wizara kwa mwaka 2004/2005 ilifanikiwa kuhamasisha na kutoa mafunzo kwa Halmashauri<br />
za Wilaya 92 <strong>Tanzania</strong> Bara na kuziwezesha kuandaa na kupitisha Sheria ndogo ya kuanzisha<br />
Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF). Halmashauri hizo hazijumuishi Halmashauri kwa Wilaya 8<br />
ambazo ni mpya kwa kuwa Wizara bado inasubiri zipate mabaraza ya Madiwani, October<br />
2005.<br />
Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) unaendelea kuwa mkombozi kwa wananchi wenye kipato<br />
cha chini kwa kutoa unafuu wa matibabu kwa wale wanaojiunga na mfuko huo kwa<br />
kuwahakikishia upatikanaji wa dawa, vifaa tiba na vifaa muhimu. Wilaya za Mbinga, Igunga,<br />
Singida, Iramba, Songea na Iringa zimeendelea kuwa mfano.<br />
Wizara kwa kushirikiana na TAMISEMI na Halmashauri imeweza kuandaa na kusaini<br />
Mikataba ya CHF inayolenga kuwa na mwongozo wa matumizi bora ya fedha za CHF.<br />
Wizara itatumia mikataba ya CHF kulipia tele kwa tele kwa Halmashauri 30 zilizochanga<br />
kwa awamu mbili, yaani mwezi Oktoba 2004 Wizara ililipa shilingi millioni 400 na Juni<br />
2005 ililipa shilingi millioni 100.<br />
Wizara pia imehamasisha Halmashauri za Miji ya Moshi, Iringa, Mtwara na Jiji la Mwanza<br />
juu ya utaratibu wa kuchangia huduma za afya kabla ya kuugua kwa sekta isiyo rasmi katika<br />
maeneo ya mijini. Utaratibu huu unajulikana kwa jina la TIBA K<strong>WA</strong> KADI (TIKA). Mpango<br />
huu wa TIKA unafanana na CHF ya Halmashauri ya Wilaya na Mfuko wa Taifa wa Bima ya<br />
Afya ambapo kaya au watumishi wanachangia kabla ya kuugua na kupata matibabu ya<br />
mwaka mzima kwa kutumia KADI ya matibabu na hivyo kuzuia kutoa fedha taslimu ambazo<br />
zinaashiria mianya ya rushwa.<br />
Matarajio ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) Mwaka 2005/2006<br />
Mwaka 2005/06 Wizara inatarajia kutekeleza yafuatayo:<br />
• Kutoa mafunzo ya njia bora za kufanya makisio ya makusanyo<br />
• Kuhamasisha kwa ufasaha na ufanisi<br />
• Utunzaji na matumizi bora ya fedha za CHF<br />
10
• Kujenga msingi wa kudumu katika ngazi ya Kanda na Mikoa kwa kuvitumia vyuo vya<br />
kanda na kushauri Mikoa yote kuteua waratibu wa CHF wa Mikoa chini ya Kamati za<br />
uendeshaji huduma za afya za Mikoa, RHMT ili wawe kiungo kati ya Wizara, Kanda<br />
na Halmashauri<br />
• Kushauri Halmashari nazo ziwe na waratibu wa CHF.<br />
Pia, Wizara imepanga kuhamasisha na kuziwezesha Halmashauri zote za Miji/Manispaa/Jiji<br />
kuanzisha mpango wa Tiba kwa Kadi (TIKA) kwa kutunga sheria ndogo za TIKA na<br />
kuidhinishwa katika ngazi ya Halmashauri.<br />
2.2.2 Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya<br />
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya umeendelea kuimarisha shughuli zake na kuboresha<br />
huduma kwa wanachama wake. Mfuko huu sasa upo katika mwaka wake wa nne wa<br />
utekelezaji na sote tu mashahidi kuwa matatizo mengi ya awali yaliyotokana na uchanga wa<br />
Mfuko huu yamekuwa yakipatiwa ufumbuzi na kazi ya kuuboresha Mfuko huu inaendelea.<br />
Mwaka 2004/2005 Mfuko ulitekeleza yafuatayo:-<br />
• Ulisajili wanachama wapya 6,321 na hivyo kuufanya Mfuko kufikisha jumla ya<br />
wanachama 248,829 ikilinganishwa na wanachama 242,508 waliokuwepo kipindi cha<br />
2003/2004. Kati ya hao asilimia 56 ni wanaume na asilimia 44 ni wanawake. Juhudi<br />
zaidi za kusajili wanachama wapya zinaendelea kupitia ofisi za kanda pamoja na<br />
Makao Makuu ya Mfuko ili Watanzania wengi zaidi waendelee kunufaika na Mfuko<br />
huu<br />
• Idadi ya wanaonufaika na mpango huu imeongezeka kutoka 1,115,537 kipindi cha<br />
mwaka 2003/2004 hadi kufikia 1,144,614 katika mwaka 2004/2005. Hii ni sawa na<br />
asilimia nne (4%) ya Watanzania wote. Kundi la wazee nalo lipo ambapo wazee wenye<br />
umri wa zaidi ya miaka 60 walioandikishwa na watoto wao kama wategemezi ni<br />
468,148. Mfuko huu utaendelea kuangalia namna bora ya kuwajumuisha wazee wengi<br />
hasa kundi la wastaafu chini ya utaratibu huu<br />
• Umetengeneza jumla ya vitambulisho 949,153 kutokana na fomu zilizopokelewa. Hii<br />
ni asilimia 83.1 ya lengo la kutengeneza vitambulisho 1,142,378<br />
• Mahudhurio katika vituo vya matibabu yameongezeka kutoka wastani wa wanachama<br />
64,917 kwa mwezi katika mwaka 2003/2004 hadi kufikia wastani wa wanachama<br />
98,825 kwa mwezi katika mwaka 2004/2005. Jumla ya mahudhurio (Total attendance)<br />
tangu mwaka 2001 hadi Januari 2005 ilikuwa 1,991,977. Kati ya waliotibiwa asilimia<br />
62.5% ni walimu na asilimia 37% ni kundi la wanawake na watoto<br />
• Aidha, jumla ya shilingi bilioni 7.35 zimekwishalipwa kwa watoa huduma wa Serikali<br />
na wale wa asasi zisizo za Serikali tangu utaratibu huu ulipoanza kutumika miaka<br />
minne iliyopita, ikiwa ni marejesho kwa huduma walizotoa kwa wanachama<br />
• Jumla ya vituo 3,558 vya matibabu vilisajiliwa na Mfuko ili kuhudumia wanachama,<br />
ambapo asilimia 70 ya vituo hivi vipo vijijini. Kati ya vituo hivi vituo 519 vinamilikiwa<br />
na madhehebu ya dini na asasi zisizo za Serikali na maduka ya dawa ni 36<br />
yanamilikiwa na wamiliki binafsi<br />
• Umeweza kufanya tathmini ya uhai wa shughuli zake kwa kutumia wataalamu wake.<br />
Kwa upande wake Shirika la Kazi Duniani (ILO) limeipitia tathmini hiyo na kuridhika<br />
nayo. Utekelezaji wa tathmini hiyo utauwezesha uongozi wa mfuko kuboresha mafao<br />
mbalimbali pamoja na wigo wake, ikiwemo orodha ya madawa<br />
11
• Umekwishakamilisha mpango wake wa miaka 5 wa “Strategic Corporate Plan”<br />
unaoanza utekelezaji wake katika mwaka ujao wa fedha wa 2005/06. Mfuko utaweka<br />
kipaumbele vijijini katika mwaka wa kwanza wa utekelezaji wa mpango huo makini<br />
• Umetoa elimu kwa wadau 96,414 wakiwemo viongozi wa vyama vya wafanyakazi,<br />
watoa huduma na vilevile kwa vyombo vya habari<br />
• Umeimarisha ofisi zake saba za kanda kwa kuzipatia nyenzo, vifaa na madaraka zaidi.<br />
Katika kipindi hicho jumla ya watumishi 37 waliajiriwa katika Ofisi za Kanda, wengi<br />
wao wakiwa ni wakaguzi na hivyo kufanya Mfuko kuwa na watumishi 121 nchi nzima<br />
• Ulifanya zoezi la sensa kwa wanachama wake pamoja na ukaguzi wa vituo vya<br />
matibabu. Zoezi hili lilifanyika katika kanda ya mashariki na kanda ya ziwa na<br />
linaendelea katika kanda nyingine. Lengo kuu la zoezi hili, ni kuhakiki taarifa muhimu<br />
za wanachama hususan upande wa vitambulisho na upatikanaji wa huduma za<br />
matibabu hasa vijijini. Tathmini imeonyesha mafanikio makubwa katika kulipatia<br />
ufumbuzi tatizo la vitambulisho, kuimarisha na kuboresha zaidi huduma kwa<br />
wanachama<br />
• Umeweza kuimarisha shughuli zake kupitia teknolojia ya habari na mawasiliano<br />
ambapo shughuli nyingi sasa zinafanyika kupitia mfumo huo. Hii ni pamoja na<br />
kuziunganisha ofisi zote saba za kanda na Makao Makuu, kurahisisha uandaaji wa<br />
malipo kwa watoa huduma na mawasiliano ya haraka na wateja.<br />
Matarajio ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mwaka 2005/2006<br />
Mkakati utawekwa wa kutumia mbinu za soko ili kusajili waajiri wote wanaotakiwa<br />
kusajiliwa kisheria (k.m, Mashirika ya Umma na Taasisi za Umma) ikiwa ni katika kusajili<br />
wanachama wengi zaidi.<br />
Mfuko utaendelea na zoezi la sensa ya wanachama wake ili kutambua idadi yao, maeneo<br />
waishio na upatikanaji wa huduma za Afya katika maeneo husika. Zoezi hili pia linahusisha<br />
ujazaji wa fomu za uanachama kwa wanachama ambao walikuwa bado hawajajaza fomu za<br />
kujiandikisha na hivyo kutokuwa na vitambulisho. Zoezi hili limebaini kwamba asilimia<br />
kubwa ya wanachama wanaolalamikia kutokuwa na vitambulisho ukweli ni kuwa hawajajaza<br />
fomu za uanachama wala kuwasilisha picha.<br />
Mfuko umekwishaanza zoezi la ukaguzi wa watoa huduma wote kwa lengo la kuangalia<br />
huduma zitolewazo kwa wanachama, mazingira ya vituo, idadi ya wafanyakazi katika vituo,<br />
hali ya vifaa vya vipimo, tiba na vitendea kazi, majengo ya vituo, pamoja na mpangilio wa<br />
jinsi wagonjwa wa Mfuko wanavyohudumiwa. Lengo la zoezi la ukaguzi ni kuhakiki na<br />
kuboresha huduma za afya zitolewazo.<br />
Mfuko utaendelea na programu ya uelimishaji kwa kutumia mabango ambayo yanasambazwa<br />
katika maeneo ya vijijini ambako njia za mawasiliano ni hafifu. Mabango hayo yatachapisha<br />
ujumbe mbalimbali muhimu kuhusu Mfuko, kwa mfano, mafao yatolewayo na Mfuko, namna<br />
ya ujazaji wa fomu za uanachama, ujazaji wa fomu za madai, haki na wajibu wa Wanachama<br />
na Wadau wengine wa Mfuko.<br />
Programu maalum ya mafunzo kwa watoa huduma wa ngazi za vituo vya afya na zahanati<br />
ambako wanachama wengi wa Mfuko wanatibiwa itaendelea katika kipindi cha mwaka ujao<br />
wa fedha ili kujenga uwezo zaidi wa watoa huduma.<br />
12
Mfuko unatarajia kuingia katika awamu ya mwisho ya zoezi la kufunga mitambo ya mfumo<br />
wa kompyuta na mifumo habari katika ofisi zote za Mfuko. Mifumo na mtandao huu wa<br />
teknolojia ya habari (TEKNOHAMA) unatarajiwa kuongeza uwezo wa kufanya mawasiliano<br />
na watoa huduma na kurahisha taratibu na mchakato wa ulipaji madai na hivyo kupunguza<br />
ucheleweshaji na kero zilizokuwepo hapo awali.<br />
Mfuko unatarajia kuwekeza zaidi katika eneo la utoaji wa huduma za Mfuko katika ofisi za<br />
kanda kwa vile uzoefu wa uendeshaji wa ofisi za kanda uliokwishapatikana katika kipindi cha<br />
miaka miwili iliyopita umebaini mahitaji zaidi ya watumishi na vitendea kazi.<br />
Mfuko umekusudia kuandaa na kuanza kutekeleza Mkakati maalum wa miaka mitano (2005 -<br />
2009). Mkakati huu utaweka bayana na kuainisha maeneo ya msingi ambayo Mfuko utayapa<br />
kipaumbele katika kuhakikisha kuwa dira, dhamira na mipango ya Mfuko inatekelezwa kama<br />
ilivyopangwa.<br />
Mfuko unatarajia kufanya mapitio ya sera ya uwekezaji ya Mfuko, ili kuweza kuanzisha<br />
maeneo zaidi ya uwekezaji, mkakati unaolenga kuleta faida zaidi, pasipo kuwa na uwezekano<br />
mkubwa wa kupoteza fedha za wanachama.<br />
Ongezeko la akiba (Reserve) litauwezesha Mfuko kupanua uwigo wa mafao vikiwemo<br />
vipimo zaidi, miwani na muda mrefu zaidi wa kuhudumia wastaafu, ambavyo vitahitaji<br />
marekebisho ya sheria.<br />
Mfuko unakusudia kufanya marekebisho katika baadhi ya maeneo mfano, suala la mafao<br />
ambayo hayamo katika kitita cha mafao, (exclusions), wigo wa wanachama na uboreshaji wa<br />
mafao, ambavyo vinapendekezwa kuhamishiwa kutoka kwenye Sheria mama na kuwekwa<br />
katika Kanuni na Taratibu (Regulations), ili pindi vikihitaji kubadilishwa visiwe vinakuwa<br />
na mlolongo mrefu kama kurejeshwa Bungeni ambako huchukua muda mrefu.<br />
Lengo la marekebisho yote hayo ni kurekebisha mfumo wa utekelezaji na hivyo kuondoa<br />
kero mbalimbali zinazowasibu wanachama kwa vile baadhi ya malalamiko ya wanachama ni<br />
ya kweli lakini pamoja na dhamira ya Mfuko ya kuyashughulikia malalamiko hayo, sheria ya<br />
Mfuko bado hairuhusu maeneo hayo kujumuishwa.<br />
Lengo la baadaye la Mfuko ni kupanua uanachama ili kujumuisha wananchi wengi zaidi<br />
wakiwemo walio katika sekta ya ajira isiyo rasmi, ili kuboresha upatikanaji wa huduma bora<br />
ya Afya kwa wananchi wote.<br />
2.2.3 Mfumo wa Taarifa za Uendeshaji wa Huduma za Afya (MTUHA)<br />
Wizara imeendelea kutoa kipaumbele kwa upatikanaji wa takwimu katika sekta ya afya.<br />
Kumekuwapo na mikakati ya makusudi ili kuhakikisha kuwa takwimu zinazohitajika<br />
zinapatikana kwa ajili ya mipango, kutoa tathmini ya utoaji wa huduma za afya, kufuatilia<br />
utekelezaji wa mipango mbalimbali ya kisekta na kuboresha sera na miongozo mbalimbali ili<br />
kuhakikisha kwamba huduma zinatolewa katika ubora unaostahili.<br />
13
Katika kufanikisha mipango ya upatikanaji wa takwimu mikakati ifuatayo imetekelezwa<br />
katika mifumo inayotumika kupata takwimu:-<br />
• Mfumo wa Taarifa za Uendeshaji wa Huduma za Afya (MTUHA) umeendelea<br />
kuboreshwa katika ngazi ya Wilaya. Hii ni baada ya kuweka kompyuta na programu ya<br />
kuchambua takwimu hizo. Hii imesaidia kuongeza kasi ya upatiakanaji wa takwimu<br />
katika ngazi ya Wilaya, Mkoa na Taifa<br />
• Takwimu zinazopatikana kupitia mfumo wa kufanya tafiti mbalimbali nao<br />
umeimarishwa zaidi. Mafunzo yametolewa kwa viongozi waliomo kwenye Kamati za<br />
Afya za uendeshaji wa huduma Wilayani na Mikoani. Lengo kuu la mafunzo hayo<br />
lililikuwa kuwapa uwezo wa kimbinu wa kuandaa miswada ya kukusanya takwimu<br />
zilizo sahihi, kufanya utafiti, kuchambua takwimu zitokananzo na tafiti na kutumia<br />
matokeo ya fafiti ili kuboresha huduma ngazi ya Wilaya na Jamii kwa ujumla<br />
• Wizara imeendelea kuimarisha kitengo kinachoratibu takwimu za jamii ambazo<br />
zinakusanywa katika maeneo maalum hapa nchini. Takwimu hizi ndizo zinazotoa<br />
makadirio yanayoonyesha uzito wa matatizo ya magonjwa yanayoisibu jamii yetu<br />
• Mfumo wa mawasiliano ya kompyuta katika Makao Makuu ya Wizara yamekamilika.<br />
Hii itaboresha upatikanaji wa takwimu katika idara, sehemu na vitengo mbalimbali<br />
kuwa na kasi zaidi. Mtandao wa kompyuta kupitia mfumo huo umeanza kufanya kazi<br />
na huduma nyinginezo zitaongezwa kulingana na mahitaji.<br />
Matarajio ya Mfuko wa Taarifa za Uendeshaji wa Huduma za Afya mwaka 2005/2006<br />
Katika mwaka 2005/2006, Wizara inatarajia kuunganisha mfumo wa kompyuta uliopo makao<br />
Makuu ya Wizara na mifumo iliyopo mikoani na katika hospitali za mikoa na za rufaa. Lengo<br />
kuu ni kurahisisha ubadilishanaji wa taarifa mbalimbali zikiwemo takwimu za afya. Pia<br />
Wizara ipo mbioni kuanzisha tovuti yake kwa lengo la kuwapatia wananchi taarifa muhimu<br />
zinazohusu sekta ya afya.<br />
Pia, Wizara ipo mbioni kubadilisha nyenzo za kukusanya takwimu za afya za siku hadi siku.<br />
Mabadiliko hayo yanalenga kuhakikisha kuwa takwimu zinazokusanywa kutoka vituo vya<br />
kutolea tiba vinaingizwa kwenye kompyuta moja kwa moja badala ya kuandaa ripoti maalum<br />
inayopelekwa Wilayani kwa ajjili ya kuingizwa kwenye kompyuta<br />
Umuhimu wa takwimu kutoka katika jamii unazidi kuongezeka siku hadi siku. Kwa sababu<br />
hiyo mwaka 2005/2006 Wizara itaboresha huu mfumo ili vigezo vitakavyopatikana vitoe<br />
takwimu ya nchi nzima na sehemu muhimu za jamii. Lengo ni kupanua wigo wa maeneo ya<br />
kukusanya takwimu za aina hii.<br />
2.3 Huduma za Kinga Utekelezaji wa Majukumu mwaka 2004/2005<br />
2.3.1 Udhibiti wa Magonjwa ya Kuambukiza<br />
Pamoja na juhudi kubwa zinazochukuliwa za kupambana na magonjwa, tatizo la magonjwa<br />
ya kuambukiza limeendelea kuwepo nchini. Katika kipindi cha Juni 2004 hadi Aprili 2005<br />
kulikuwa na wagonjwa 3,462 wa kipindupindu na kati yao 93 walifariki ikilinganishwa na<br />
kipindi kama hicho 2003/2004 ambapo kulikuwa na wagonjwa 12,397 na vifo 217. Mikoa<br />
iliyoathirika zaidi na tatizo hili ni Dar es salaam, Morogoro, Tanga, Kigoma, Mbeya, Kagera,<br />
Arusha na Kilimanjaro. Ipo haja ya kuzingatia kanuni za afya bora ili kuondokana na<br />
ugonjwa huu unaotokana na uchafu.<br />
14
Tatizo la watu kuumwa na mbwa au wanyama wanaohisiwa kuwa na kichaa cha mbwa<br />
limekuwa likiongezeka kila mwaka. Mwaka 2004 watu 15,528 waliumwa na mbwa au<br />
wanyama wanaohisiwa kuwa na kichaa cha mbwa na kati yao watu 98 waliugua ambapo 78<br />
walifariki ikilinganishwa na mwaka 2003 ambapo watu 12,120 waliumwa na kati yao 56<br />
waliugua ambapo 47 walifariki. Wizara inashughulikia kinga ya kichaa cha mbwa, pia<br />
iliendelea kuwasiliana na Wizara ya Maji na Maendeleo ya Mifugo, Wizara ya Tawala za<br />
Mikoa na Serikali za Mitaa, Wizara ya Maliasili na Utalii, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa<br />
Serikali ili kuandaa mkakati wa kukabiliana na tatizo la watu kuumwa na wanyama<br />
wanaohisiwa kuwa na ugonjwa wa kichaa cha mbwa.<br />
Kutokana na kuanzishwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, wananchi wa nchi zetu tatu<br />
wamekuwa na uhuru zaidi wa kutembeleana, kwa hiyo Wizara inashirikiana na Wizara<br />
husika za Kenya na Uganda katika kupanua wigo wa ufuatiliaji na udhibiti wa magonjwa ya<br />
milipuko hasa sehemu za mipakani.<br />
Udhibiti wa Magonjwa yanayoenezwa na Wadudu (Vectors and Vector Borne Diseases)<br />
Katika kipindi cha mwaka 2004/2005 Wizara ikishirikiana na Taasisi ya Viuatilifu ya Arusha<br />
(TPRI) imefanya utafiti ili kupata viuatilifu (acaricides) vinavyofaa kuangamiza papasi<br />
wanaoleta homa ya papasi na matokeo ya utafiti huu yatakapokamilika yatatolewa kwa<br />
wadau. Aidha, wananchi katika mikoa husika wameendelea kuhamasishwa juu ya ujenzi wa<br />
nyumba bora na usafi wa mazingira ikiwa ni pamoja na matumizi ya vitanda ili kujiweka<br />
mbali na mazalio ya papasi.<br />
Matarajio ya Udhibiti wa Magonjwa ya Kuambukiza mwaka 2005/2006<br />
Ili kudhibiti magonjwa ya kuambukiza Wizara itaendelea kutoa mafunzo juu ya ufuatiliaji na<br />
udhibiti wa magonjwa kwa wataalam katika Wilaya 30. Wizara itaendelea na mapambano<br />
dhidi ya magonjwa yanayoenezwa na wadudu wanaoruka, wasioruka pamoja na wanyama<br />
(Vectors and vector borne diseases) kwa kufanya ufuatiliaji na usimamizi wa shughuli za<br />
udhibiti wa magonjwa hayo katika Wilaya 20.<br />
2.3.2 Mpango wa Taifa wa kudhibiti Malaria<br />
Ugonjwa wa malaria bado ni tatizo kubwa hapa nchini na linahitaji jitihada za pamoja katika<br />
kukabiliana nalo. Katika kipindi cha 2004/2005, Wizara ilitekeleza majukumu mbalimbali<br />
katika kukabiliana na ugonjwa wa Malaria. Utekelezaji huo ulihusu:-<br />
• kutoa mafunzo kwa wataalam mbalimbali wa afya kuhusu tiba sahihi,<br />
• uhamasishaji juu ya utumiaji wa vyandarua vyenye viuatilifu hasa kwa mama<br />
wajawazito na watoto chini ya umri wa miaka 5<br />
• utafiti wa usugu wa vimelea vya malaria<br />
• utafiti juu ya tiba ya mseto<br />
• utoaji wa tiba ya tahadhari kwa vipindi kwa mama wajawazito<br />
• tahadhari za kudhibiti milipuko ya malaria katika wilaya zenye milipuko ya malaria<br />
na uimarishaji wa udhibiti wa malaria ngazi ya jamii.<br />
Wizara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali inaendelea na uhamasishaji wa jamii katika<br />
kutumia vyandarua vyenye viuatilifu.<br />
15
Wizara pia ilizindua Mpango wa Taifa wa Hati Punguzo tarehe 22 Oktoba mwaka 2004,<br />
mpango ambao unawawezesha mama wajawazito na watoto walio chini ya umri wa miaka<br />
mitano kupata vyandarua vyenye viuatilifu kwa bei nafuu. Kwa hivi sasa, mpango wa Taifa<br />
wa Hati Punguzo unatekelezwa katika mikoa ya Dar-es-salaam, Dodoma, Morogoro, Tanga,<br />
Pwani, Kilimanjaro na Arusha. Mpango huu utajumuisha mikoa yote ya <strong>Tanzania</strong> Bara<br />
ifikapo mwishoni mwa mwaka 2005. Kufikia mwezi Mei mwaka 2005, mpango huu<br />
umeonyesha mafanikio makubwa katika utekelezaji kwani mama wajawazito wapatao<br />
100,000 wametumia Hati Punguzo kununulia vyandarua.<br />
Matarajio ya Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Malaria mwaka 2005/2006<br />
Mwaka huu Wizara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali iliadhimisha Siku ya Malaria<br />
Afrika iliyofanyika Kitaifa tarehe 25 Aprili, 2005 mkoani Singida. Kauli mbiu ya<br />
maadhimisho hayo ilikuwa “Tushirikiane kwa pamoja tushinde Malaria”. Kauli mbiu hii<br />
inakumbusha na kusisitiza umuhimu wa kuwashirikisha wadau wote katika Afya kupiga vita<br />
Malaria, hii ikiwa ni pamoja na jamii, Serikali kuu, Serikali za mitaa, wahisani mbalimbali,<br />
mashirika ya dini, watu binafsi nk.<br />
Pamoja na jitihada kubwa zinazofanyika ili kudhibiti ugonjwa wa Malaria nchini, kuna<br />
Wilaya 25 ambazo zipo katika hatari ya kupata milipuko ya ugonjwa wa malaria. Kwa hali<br />
hiyo, Wizara katika mwaka huu wa fedha imeandaa mikakati ya kuziweka wilaya zenye<br />
uwezekano wa kupata milipuko ya Malaria katika hali ya tahadhari ya kuweza kutabiri na<br />
kudhibiti milipuko hiyo.<br />
Wizara imeanza maandalizi ya kubadilisha matibabu ya Malaria kutoka dawa ya SP kwenda<br />
dawa ya mseto ya Artemether /Lumefantrine (ALU/Coartem). Maandalizi ya kubadili<br />
mwongozo wa matibabu, kuendesha mafunzo kwa watoa huduma za afya kuhusu tiba mpya<br />
na kuelimisha jamii yatafanyika. Matarajio ni kuanza kutumia dawa mseto ifikapo mwezi wa<br />
8, mwaka 2006.<br />
2.3.3 Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma<br />
Mwaka 2004 kumekuwa na ongezeko la usajili wa wagonjwa wa Kifua Kikuu toka 64,665<br />
mwaka 2003 hadi 65,644 mwaka 2004. Ongezeko hilo ni sawa na asilimia 1.5. Aidha,<br />
uponaji wa wagonjwa wa Kifua Kikuu pia umeongezeka kutoka asilimia 80.2 mwaka 2002<br />
hadi asilimia 82.5 mwaka 2003. Ongezeko hili ni la asilimia 2.8. Vilevile, idadi ya wagonjwa<br />
wa Kifua Kikuu wasiomaliza matibabu kama ilivyoelekezwa na wahudumu imepungua kwa<br />
asilimia 0.5.<br />
Kwa upande wa ugonjwa wa Ukoma, wagonjwa wamepungua kutoka 5,771 mwaka 2003<br />
hadi wagonjwa 5,602 mwaka 2004 ambalo ni punguzo la asilimia 3. Mafanikio haya<br />
yametokana na utekelezaji wa mikakati ya kudhibiti maradhi haya kwa kushirikisha jamii<br />
ambayo ni kuwatafuta, kuwatambua mapema na kutoa tiba kamilifu kwa wagonjwa chini ya<br />
usimamizi maalum unaoitwa ‘Directly Observed Treatment Short Course (DOTS)’ kwa ajili<br />
ya Kifua Kikuu na Multi -Drug Therapy (MDT) kwa ajili ya Ukoma.<br />
16
Katika kipindi cha Julai 2004 mpaka Juni 2005, Mpango wa Taifa wa Kifua Kikuu na<br />
Ukoma ulifanya ufuatiliaji wa watoto wa shule 1,048 waliobainika kuwa na uambukizo wa<br />
ugonjwa wa Kifua Kikuu katika mikoa ya Singida, Iringa, Mbeya, Kigoma na Kagera.<br />
Asilimia 48 ya watoto hao walipata uambukizo ndani ya kaya zao na jumla ya watoto 75<br />
yaani asilimia 3 walikuwa tayari na ugonjwa wa Kifua Kikuu (active TB) na walipewa dawa<br />
za matibabu.<br />
Kampeni za kutokomeza ugonjwa wa Ukoma Duniani zilifanyika katika mikoa ya Kagera,<br />
Rukwa na Tabora ambako jumla ya wagonjwa wapya 836 waligunduliwa na kuanzishiwa<br />
tiba. Aidha, katika juhudi za kurekebisha ulemavu (prevention and rehabilitation of<br />
disabilities) unaotokana na Ukoma, watu walioathirika na Ukoma wenye ulemavu 175<br />
walifanyiwa upasuaji wa aina mbalimbali na wengine 5,811 walipewa viatu maalum na watu<br />
37 walipewa miguu bandia. Vile vile, madaktari bingwa wa upasuaji 5 walipewa mafunzo<br />
rejea juu ya upasuaji wa wagonjwa waliopata ulemavu kutokana na Ukoma.<br />
Katika kipindi cha 2004/2005, jamii iliendelea kuelimishwa kwa kutumia njia mbalimbali<br />
ikiwa ni pamoja na kutoa matangazo kwa kutumia vyombo vya habari, kusambaza<br />
vipeperushi na mabango yenye ujumbe wa jinsi ya kutambua dalili, kujikinga na matibabu ya<br />
Kifua Kikuu na Ukoma. Aidha, dawa za kutosha za Kifua Kikuu na Ukoma ziliendelea<br />
kusambazwa katika mikoa, wilaya na vituo vyote vya matibabu. Dawa hizo zilitolewa kwa<br />
wagonjwa wote bila malipo.<br />
Matarajio ya Mpango wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma mwaka 2005/2006<br />
Katika kipindi cha 2005/06 Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma<br />
utaendeleza kampeni za kutokomeza Ukoma katika mikoa ya Ruvuma, Morogoro na Tanga.<br />
Aidha, shughuli za kurekebisha rejesta za wagonjwa wa Ukoma zitaendelea sambamba na<br />
kampeni za kutokomeza Ukoma ili kufikia lengo la kimataifa ifikapo Desemba mwaka 2005.<br />
Mpango utaendelea kuimarisha huduma za pamoja za kudhibiti Kifua Kikuu na UKIMWI na<br />
zile za kudhibiti Kifua Kikuu sugu ili kisienee nchini. Aidha, uagizaji na usambazaji wa dawa<br />
za kutosha za Kifua Kikuu na Ukoma katika vituo vyote vya matibabu nchini utafanywa.<br />
Sambamba na hili, Mpango utaendelea kuelimisha jamii kwa kutumia vipeperushi, mabango<br />
na kutoa habari kwa njia ya luninga na radio jinsi ya kujikinga na maambukizi, kutambua<br />
mapema na taratibu za kufuata wakati wa matibabu ya magonjwa ya Kifua Kikuu na Ukoma.<br />
Wizara inategemea kuanzisha huduma kwa wagonjwa wenye Kifua Kikuu sugu (Multi Drug<br />
TB) katika hospitali ya Kibong’oto iliyopo Wilayani Hai na kuanzisha mpango wa kutumia<br />
dawa za mseto zilizochanganywa pamoja (4 Fixed Dose Combinations) kutibu Kifua Kikuu<br />
katika Wilaya 6 za mwanzo za majaribio. Aidha, Wizara itaendelea na utekelezaji wa mpango<br />
wa pamoja wa kudhibiti uambukizo wa Kifua Kikuu na UKIMWI katika wilaya za Temeke,<br />
Korogwe na Iringa mjini.<br />
Bado jitihada za pamoja zinahitajika katika kuelimisha jamii kutambua dalili za Kifua Kikuu<br />
na Ukoma, kujitokeza kufanya uchunguzi na kuanza matibabu mapema ambayo hutolewa bila<br />
malipo katika vituo vya kutolea huduma za afya.<br />
17
2.3.4 Mpango wa Taifa wa Huduma za Macho na Kudhibiti Ugonjwa wa Usubi<br />
Katika kipindi cha mwaka 2004/2005 Wizara imetekeleza azimio la kimataifa la kutokomeza<br />
upofu unaozuilika duniani ifikapo mwaka 2020 (Vision 2020”) kwa kukamilisha na<br />
kuuzindua rasmi Mpango/Mkakati wa miaka mitano (2004-2008) wa Huduma za Macho<br />
Kitaifa. Mpango/Mkakati huu unatoa dira na mwelekeo wa Huduma za Macho katika jitihada<br />
za kudhibiti upofu ambao vyanzo vyake vikuu ni mtoto wa jicho, ukungu wa kioo cha jicho<br />
unaosababishwa na Trachoma, upungufu wa Vitamin A na Surua, presha ya macho, matatizo<br />
ya kuona yanayorekebishwa na lensi za miwani pamoja na Kisukari. <strong>Tanzania</strong> ni mojawapo<br />
ya mataifa ya kwanza kabisa kukamilisha Mpango Mkakati huu wa Kitaifa.<br />
Vilevile, katika kipindi hiki Wizara imeweza kutoa tiba ya ugonjwa wa Trachoma kwa<br />
kutumia dawa ya Zithromax kwa mtindo mpya unaoitwa “District Wide Approach” katika<br />
Wilaya 6 za Sikonge, Handeni, Dodoma vijijini, Tunduru, Magu na Ruangwa ambapo watu<br />
1,186,913 walitibiwa ikiwa ni juhudi za kutokomeza ugonjwa wa Trachoma ulimwenguni<br />
ifikapo mwaka 2020. Wizara pia imeandaa Mpango Mkakati wa miaka mitano (2004-2008)<br />
wa kudhibiti Ugonjwa wa Trachoma ambao unatoa dira na mwelekeo wa kuzuia upofu<br />
unaosababishwa na ugonjwa wa Trachoma, ugonjwa ambao unakadiriwa kuathiri takriban<br />
wilaya 50 hapa nchini.<br />
Ili kuharakisha utokomezaji wa upofu utokanao na Trachoma, Shirika la Afya Duniani<br />
limetoa mwongozo mpya wa utoaji wa dawa ya Zithromax inayotumika kutibu na kuzuia<br />
Trachoma, dawa inayotolewa kwa msaada na kampuni ya Pfizer kupitia Shirika la Kimataifa<br />
la kudhibiti Trachoma (International Trachoma Initiative). Mwongozo huu ulipelekea<br />
kufanyika kwa utafiti wa awali ili kuweza kujua kiwango cha ugonjwa huu katika ngazi ya<br />
wilaya. Wizara kwa msaada wa shirika la Kimataifa la kudhibiti Trachoma imefanikiwa<br />
kukamilisha utafiti huo katika Wilaya thelathini zenye ugonjwa huu. Utafiti huu bado<br />
unaendelea katika Wilaya 20 zilizobakia.<br />
<strong>Tanzania</strong> ni nchi ya kwanza kufanya utafiti huu kulingana na mwongozo mpya na<br />
inachukuliwa kama nchi ya mfano kwa nchi nyingine ambazo zina tatizo la ugonjwa huu<br />
kulingana na mafanikio yaliyojitokeza. Matokeo ya awali ya utafiti huu yameonyesha kuwa<br />
wilaya 26 kati ya 30 zina ugonjwa huu kwa kiwango cha zaidi ya asilimia 10.<br />
Mpango wa Taifa wa kudhibiti ugonjwa wa Usubi uliweza kugawa dawa ya Mectizan katika<br />
vijiji 650 vilivyopo katika Wilaya 14 ambazo ni Ulanga, Kilombero, Kilosa, Songea, Mbinga,<br />
Tunduru, Ludewa, Rungwe, Kyela, Muheza, Mvomero, Morogoro, Korogwe, na Lushoto.<br />
Jumla ya wananchi 2,948,862 walipatiwa dawa hii katika kipindi cha mwaka 2004/2005.<br />
Wizara inatarajia kugawa dawa ya Mectizan kwa wananchi wapatao 3,000,000 katika kipindi<br />
hiki.<br />
Malengo ya Mpango wa Taifa wa Huduma za Macho na Kudhibiti ugonjwa wa Usubi<br />
mwaka 2005/2006<br />
Katika kipindi cha 2005/2006 Wizara inatarajia kuongeza Wilaya 10 zaidi katika mpango wa<br />
kudhibiti ugonjwa wa Trachoma nchini kwa kutumia mtindo mpya wa “District Wide-<br />
Approach”. Jumla ya Wilaya 8 kati ya hizo zinatarajiwa kutolewa dawa ya Zithromax kwa<br />
wananchi wake.<br />
18
Wilaya zitakazojumuishwa katika mpango huo ni Kongwa, Kilosa, Meatu, Iramba, Singida<br />
vijijini, Igunga, Simanjiro na Mkuranga ambapo watu wapatao 2,300,000 wanatarajiwa<br />
kupatiwa matibabu ya ugonjwa wa Trachoma.<br />
Wizara inatarajia pia kugawa dawa ya “Mectizan” kwa ajili ya tiba ya ugonjwa wa Usubi<br />
(mass treatment) kwa wananchi wapatao 3,000,000 katika vijiji 690 vilivyoko katika Wilaya<br />
15 za Ulanga, Kilombero, Kilosa, Songea, Mbinga, Tunduru, Ludewa, Rungwe, Kyela,<br />
Muheza, Mvomero, Morogoro vijijini, Korogwe, Lushoto na Tunduru.<br />
23.5 Huduma ya Elimu ya Afya Kwa Umma<br />
Kwa mwaka 2004/2005, kazi ya kuelimisha na kuhamasisha jamii ishiriki katika kutambua na<br />
kutafuta ufumbuzi wa matatizo ya ki-afya yanayoisibu iliendelezwa. Aidha, Wizara<br />
inaendelea kukuza uwezo wa Kamati na Bodi za Afya za Wilaya ili ziweze kupanga,<br />
kutekeleza, kufuatilia na kutathmini huduma za Elimu ya Afya katika Jamii. Hii ni pamoja na<br />
kuwezesha Kamati na Bodi za Afya kubuni mikakati ya mawasiliano ya afya na kuandaa<br />
vielelezo vya afya vyenye uwezo wa kuleta mabadiliko yanayohitajika katika kuboresha afya<br />
ya jamii.<br />
Matarajio ya Huduma ya Elimu ya Afya kwa Umma mwaka 2005/2006<br />
Katika kipindi cha 2005/2006, Kitengo cha Elimu ya Afya kwa Umma kitaendelea<br />
kushirikiana na wadau mbali mbali kuelimisha wananchi mbinu za kubadili tabia na mitindo<br />
ya maisha inayohatarisha afya zao.<br />
Aidha, Kitengo cha Elimu ya Afya kwa Umma kitaimarisha uratibu na kupanua wigo wa<br />
shughuli za utoaji Elimu ya Afya kwa kushirikiana na vyombo mbalimbali vya habari<br />
vilivyopo katika jamii yetu, ikiwa ni pamoja na sanaa kwa maendeleo, ili kuweza kufikisha<br />
ujumbe wa afya kwa wananchi wengi.<br />
2.3.6 Huduma za Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto<br />
Katika kipindi cha 2004/2005, huduma maalum kwa wajawazito na watoto chini ya umri wa<br />
miaka mitano ziliendelea kutolewa bila malipo katika vituo vyote vya kutolea huduma vya<br />
Serikali. Huduma hizo ni pamoja na huduma kwa wanawake wajawazito, huduma za<br />
kujifungua, chanjo, matibabu kwa watoto wagonjwa wenye umri chini ya miaka 5 na uzazi<br />
wa mpango. Aidha, Wizara ilihakikisha upatikanaji na usambazaji wa dawa mbali mbali za<br />
uzazi wa mpango unafanyika nchini kwa kushirikiana na wahisani mbalimbali.<br />
Tathmini ya kina ya kutambua hali halisi ya uwezo wa vituo vyetu katika kukabiliana na<br />
dharura ya uzazi pamoja na rufaa imefanyika. Taarifa kamili itakuwa tayari Mwezi Julai<br />
2005. Matokeo yatatumika katika kuimarisha mikakati iliyopo ya kupunguza vifo<br />
vitokanavyo na uzazi ambapo wilaya zitakuwa ni watekelezaji wakuu. Aidha, tathimini ya<br />
kitaifa kuhusu hali halisi ya Afya ya Uzazi na Mtoto hapa nchini imefanyika (<strong>Tanzania</strong><br />
Demographic Health Survey) kwa kushirikiana na National Bureau of Statistics. Matokeo ya<br />
awali yatapatikana mwezi Septemba 2005. Tathmini hii itatupatia takwimu ya hali halisi ya<br />
sasa ya vifo vya wanawake vinavyotokana na uzazi kitaifa.<br />
19
Katika kipindi cha 2004/2005, watoa huduma na wakufunzi 130 walipata mafunzo rejea<br />
kuhusu uzazi wa mpango kutoka mikoa ya Dodoma, Kilimanjaro, Morogoro, Tanga, Lindi,<br />
Mbeya, Pwani na Mwanza. Pia, watoa huduma 100 kutoka mikoa ya Kilimanjaro, Dodoma,<br />
Tanga, Mtwara, Morogoro, Lindi, Mbeya, Mwanza na Pwani walipata mafunzo rejea ya<br />
utoaji huduma za wajawazito ikijumuisha matibabu ya tahadhari na kutoa kinga kwa<br />
wajawazito dhidi ya Malaria na upimaji wa ugonjwa wa Kaswende.<br />
Matarajio ya Huduma ya Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto mwaka 2005/2006<br />
Wizara ya Afya itaendelea kuboresha huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto bila malipo<br />
ikiwa ni huduma za matibabu kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano, chanjo, uzazi<br />
wa mpango, huduma kwa wanawake wajawazito ambao watahudhuria kliniki na kujifungua<br />
katika vituo vya kutolea huduma vya Serikali.<br />
Aidha, Wizara itaendelea kununua na kusambaza dawa za uzazi wa mpango nchi nzima kwa<br />
kushirikiana na wahisani. Wizara imetenga fedha kiasi cha shilingi billion 6.8 kwa ajili ya<br />
manunuzi hayo na usambazaji.<br />
Wizara imepanga kutoa mafunzo mbalimbali katika maeneo ya uzazi wa mpango (100), uzazi<br />
salama (80), Afya ya uzazi kwa vijana (40) kutoka katika mikoa ya Kilimanjaro, Dodoma,<br />
Tanga, Mtwara, Morogoro, Lindi, Mbeya, Mwanza na Pwani. Ufuatiliaji na usimamizi wa<br />
masuala ya afya ya uzazi, mama na mtoto utafanyika katika mikoa saba hapa nchini. Uhakiki<br />
wa utumiaji wa dawa za uzazi wa mpango katika maghala ya MSD makao makuu na Kanda<br />
(6), pamoja na zile za baadhi ya Wilaya katika Kanda zote saba za Afya ya Uzazi na Mtoto<br />
utafanyika ili kuboresha utunzaji wa dawa husika.<br />
2.3.7 Mkakati wa Kutibu Magonjwa ya Watoto kwa Uwiano (Intergrated Management of<br />
Childhood Illness-IMCI)<br />
Wizara ikishirikiana na wahisani iliendelea kutekeleza mkakati wa Udhibiti wa Magonjwa ya<br />
Watoto kwa Uwiano unaolenga kupunguza vifo vya watoto hasa vinavyotokana na Malaria,<br />
Kuharisha, Pneumonia, Surua na Utapiamlo.<br />
Katika kipindi cha 2004/2005, Wilaya 87 zimetekeleza mkakati wa IMCI. Jumla ya<br />
Wahudumu wa Afya 300 wamepata mafunzo kuhusu stadi za kumtibu mtoto. Wahudumu 40<br />
kutoka hospitali 7 wamepata mafunzo juu ya huduma ya dharura na kuboresha huduma kwa<br />
mtoto aliyezidiwa.<br />
Aidha, jamii imeendelea kuelimishwa juu ya mienendo inayoboresha afya ya mtoto.<br />
Mienendo hii inakazia lishe kwa mtoto, Makuzi ya Mwili na Akili, pamoja na Uzuiaji wa<br />
Magonjwa ya Watoto. Mafunzo haya yametolewa hadi ngazi ya kaya katika Wilaya 13.<br />
Matarajio ya Udhibiti wa Magonjwa ya Watoto kwa Uwiano (IMCI) mwaka 2005/2006<br />
Huduma za Afya na matibabu kwa watoto chini ya miaka mitano zitaendelea kuboreshwa<br />
katika ngazi zote. Wizara inatarajia kutoa mafunzo ya stadi za kutibu watoto kwa wahudumu<br />
wa afya na wakurufunzi 160. Mafunzo ya huduma ya dharura kwa wahudumu wa afya<br />
yatafanyika kwa wahudumu 30 na mafunzo ya wakurufunzi ngazi ya Taifa 50 na ngazi ya<br />
Wilaya 200 watapata mafunzo ya mienendo inayoboresha Afya ya Mtoto.<br />
20
2.3.8 Mpango wa Taifa wa Chanjo<br />
Huduma za chanjo zimeendelea kutolewa nchi nzima kwa watoto wanaostahili kupata chanjo<br />
hizo kama juhudi za serikali za kupunguza vifo na magonjwa ya watoto yanayozuilika kwa<br />
chanjo. Magonjwa hayo ni Kifua Kikuu, Dondakoo, Kifaduro, Pepopunda, Polio, Surua na<br />
Homa ya ini. Viwango vya chanjo vimeendelea kuongezeka vikilinganishwa na viwango vya<br />
mwaka uliopita DPT HB3 kutoka 89% hadi 91%, Measles toka 90% hadi 93% Polio toka<br />
92% hadi 93%, Kifua Kikuu kutoka 94% hadi 95%. Mafanikio haya yametokana na juhudi za<br />
serikali, jamii wadau mbalimbali pamoja na GAVI.<br />
Matarajio ya Mpango wa Taifa wa Chanjo mwaka 2005/2006<br />
Katika kipindi cha mwaka 2005/2006, Wizara ya Afya kwa kushirikiana na mikoa itaendelea<br />
kusimamia huduma za chanjo katika ngazi za Wilaya na itaendelea kutoa vitendea kazi na<br />
chanjo ili kuhakikisha watoto wote wanaostahili chanjo wanapata chanjo. Aidha, juhudi<br />
zitafanywa ili kutokomeza polio, kupunguza magonjwa ya surua, kufuta pepopunda kwa<br />
watoto wachanga na kupunguza vifo zitaendelea kuimarishwa. Wizara pia itaendelea kufanya<br />
tathmini ya magonjwa mengine yanayozuilika kwa chanjo ambazo hazijaanza kutumika hapa<br />
nchini.<br />
2.3.9 Huduma za Afya Shuleni<br />
Katika mwaka 2004/2005 Wizara ilisambaza Kadi za kupimia Afya za wanafunzi katika<br />
Manispaa za IIala, Temeke na Kinondoni. Waratibu wapatao 150 kutoka ngazi ya mkoa na<br />
wilaya walipatiwa mafunzo juu ya Udhibiti wa Magonjwa ya Kichocho na Minyoo mingine.<br />
Aidha, utafiti kuhusu ugonjwa wa Kichocho katika shule za msingi umefanyika katika<br />
Wilaya zote nchini.<br />
Matarajio ya Huduma za Afya Shuleni mwaka 2005/2006<br />
Katika mwaka 2005/2006, Wizara ya Afya inategemea kutoa mafunzo ya Huduma ya kwanza<br />
kwa Waratibu wa Afya Shuleni ngazi ya Wilaya, kuhamasisha Wilaya kuchangia katika<br />
kuchapisha kadi ya kupima afya za wanafunzi kwa shule za awali hadi sekondari. Utoaji wa<br />
dawa za Kichocho /Minyoo kwa wanafunzi pia utatekelezwa katika maeneo yaliyoathirika.<br />
2.3.10 Afya ya Mazingira<br />
Katika mwaka 2004/2005, Wizara imeimarisha udhibiti wa taka za hospitali (Health care<br />
Waste Management) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali pamoja na Chuo Kikuu cha Dar<br />
es Salaam kwa kuendesha mafunzo juu ya udhibiti taka za hospitali na ujenzi wa matanuru<br />
katika hospitali za Wilaya za Kilosa na Mahenge, Hospitali ya Ocean Road na Hospitali ya<br />
Rufaa ya Kibongoto. Aidha, Wizara imeboresha na kuinua hali ya Afya na Usafi wa<br />
Mazingira kwa kuendesha mashindano ya Afya na Usafi wa Mazingira nchini. Mashindano<br />
haya yalishirikisha Halmashauiri za Jiji la Mwanza, Manisipaa 12, Halmashauri za Miji 9 na<br />
Halmashauri 114 za Wilaya nchini.<br />
Ili kuinua kiwango cha usafi na ubora wa vyoo, kalibu (Moulds) za kutengenezea mabamba<br />
(slab) 560 zilitengenezwa na kusambazwa katika Wilaya za Rungwe, Bagamoyo, Kisarawe,<br />
Monduli na Mufindi pamoja na Mkoa wa Kigoma ili zitumike kujengea vyoo bora.<br />
21
Aidha, Wizara iliandaa na kusambaza miongozo ya utekelezaji wa huduma za Afya ya<br />
Mazingira nchini Miongozo na mikakati iliyoandaliwa ni pamoja na:-.<br />
• Mwongozo wa Mafunzo ya Mbinu Shirikishi Jamii katika kuboresha tabia za Afya na<br />
Usafi wa Mazingira<br />
• Mwongozo wa Udhibiti wa Taka (Waste Management Policy Guideline)<br />
• Mkakati wa Kitaifa wa Afya na Usafi wa Mazingira (National Environmental Health,<br />
Hygiene and Sanitation Strategy) mkakati huu unazingatia malengo ya kuondoa<br />
umaskini nchini pamoja na Malengo ya Maendeleo ya Milenia (Millenium<br />
Development Goals).<br />
Matarajio ya Afya ya Mazingira mwaka 2005/2006<br />
Katika kipindi cha 2005/2006, Wizara ya Afya inakusudia kuanzisha Vijiji bora kwa kila<br />
Mkoa ambavyo vitakidhi mahitaji yote ya kiafya. Tunatarajia kuanza na Wilaya tano kwa<br />
kuchagua Kijiji kimoja kila Wilaya. Aidha, Wizara itaendelea kushirikiana na Wizara mbali<br />
mbali, jumuia za kimataifa, mashirika yasiyokuwa ya kiserikali (NGOs) na jamii katika<br />
upangaji mipango mbinu shirikishi jamii ili kuboresha hali ya afya na usafi wa mazingira<br />
katika mikoa yote.<br />
Aidha, Wizara itaanza kutekeleza Mpango maalum wa Kudhibiti Taka za Hospitali (Health<br />
Care Waste Management) ili kudhibiti hali ya uambukizi wa maradhi kwa watoa huduma,<br />
wateja na jamii kwa jumla kwa vile mara nyingi taka zitokanazo na huduma za afya nchini<br />
zimekuwa zikionekana zikizagaa ovyo mahali zisipotakikana. Mpango huu utatekelezwa kwa<br />
muda wa miaka mitano 2005/06 – 2009/2010 katika mikoa yote. Mpango huu utaanza kwa<br />
kuzihusisha hospitali za Halmashauri zote za Wilaya, hospitali za mikoa na hospitali za rufaa<br />
nchini.<br />
Vilevile, itaratibu mapitio ya sheria ya ‘Drainage and Sewerage Ordinance Cap 259’ ya<br />
mwaka 1955 inayosimamia udhibiti wa maji taka nchini. Sheria hii ni ya zamani sana na<br />
imepitwa na wakati itapitiwa na kufanyiwa marekedisho yanayokidhi haja ya hali ilivyo kwa<br />
wakati huu.<br />
Katika kupima maendeleo ya Afya ya Mazingira Wizara itaendeleza mashindano ya Afya na<br />
Usafi wa Mazingira nchini, ambayo yataendelea kujumuisha halmashauri zote nchini (Jiji,<br />
Manisipaa, Mji na Wilaya). Lengo kuu la mashindano haya ni kushirikisha wananchi, sekta<br />
binafsi katika kuboresha hali ya usafi wa mazingira katika maeneo yao<br />
2.3.11 Huduma za Afya Mipakani<br />
Katika kuhakikisha kuwa udhibiti wa magonjwa ya kuambukiza kutoka nje ya nchi<br />
unaimarika, Wizara imeboresha huduma za Afya Mipakani ambapo maafisa wa Afya<br />
wamepata mafunzo mbalimbali ikiwemo jinsi ya kupambana na majanga. Pia, vituo<br />
vimeimarishwa kwa kuongeza vitendea kazi na kuajiri wataalam wa afya katika vituo vya<br />
Afya. Katika mwaka huu wa fedha, zaidi ya tani 5,470,000 za vyakula zilikaguliwa ambapo<br />
tani 40,800 ziliharibiwa baada ya kuthibitika kuwa hazifai kwa matumizi ya binadamu.<br />
22
Matarajio ya Huduma za Afya Mipakani mwaka 2005/2006<br />
Wizara itaendelea kuhakikisha kuwa magonjwa ya kuambukiza ya kimataifa yanadhibitiwa<br />
kwa kufuata sheria za Afya za Kimataifa. Vituo vya mipakani vitapatiwa nyenzo na vitendea<br />
kazi vya kisasa ikiwemo usafiri. Pia, udhibiti wa uingizwaji wa vyakula, dawa na vipodozi<br />
visivyokidhi viwango vya Afya utaimarishwa kwa kushirikiana na wadau wengine kwa<br />
Halmashauri zote nchini 113.<br />
2.3.12 Afya katika Sehemu za Kazi<br />
Kwa kuzingatia umuhimu wa Afya ya Wafanyakazi hususan maeneo ya viwanda, ujenzi na<br />
mashamba, Wizara imefanya uhamasishaji wa kamati za Halmashauri za Wilaya 48 juu ya<br />
uainishaji wa huduma za afya sehemu za kazi na huduma za afya ya msingi. Shughuli za<br />
usimamizi na ufuatiliaji wa afya sehemu za kazi zimefanyika katika Halmashauri 12. Aidha,<br />
mafunzo kwa wachimbaji wadogo wadogo 70 wa madini katika Mikoa ya Arusha na Mwanza<br />
yamefanyika.<br />
Matarajio ya Afya katika Sehemu za Kazi mwaka 2005/2006<br />
Kwa kutambua umuhimu wa afya ya wafanyakazi mahali pa kazi, Wizara imeweka mikakati<br />
ya kuwafikia na kuwahamasisha wafanyakazi wote juu ya madhara yatokanayo na kazi<br />
ifikapo 2015. Aidha Wizara imeweka mikakati endelevu inayotilia mkazo juu ya uzuiaji wa<br />
maambukizi ya UKIMWI mahali pa kazi. Ili kufikia azma hii madaktari 118 wa Halmashauri<br />
za Wilaya watapatiwa mafunzo juu ya uboreshaji wa afya ya wafanyakazi sehemu za kazi.<br />
2.3.13 Huduma za Afya Wilayani (District Health Services)<br />
Utekelezaji wa mabadiliko ya Sekta ya Afya ngazi ya Wilaya yalianza kutekelezwa kwa<br />
awamu tatu tofauti. Awamu ya kwanza ilikuwa kwa Halmashauri 37 kwa mwaka 2000,<br />
awamu ya pili 2002 Halmashauri 45 na awamu ya mwisho Halmashauri 31 na kufanya jumla<br />
ya Halmashauri za Wilaya, Jiji, Miji na Manispaa 113.<br />
Utekelezaji ulianza kwa kufundisha Halmashauri zote namna ya kuandaa Mipango<br />
Kambambe ya Afya ya Halmashauri (Comprehensive Council Health Plan) na kutayarisha<br />
taarifa za robo mwaka za utekelezaji zikihusu fedha na kazi halisi zilizotekelezwa (quarterly<br />
progress implementation reports – technical and financial). Mpaka sasa Halmashauri zote<br />
zinaandaa, kutekeleza na kutoa taarifa ya utekelezaji wa mipango hii kama ilivyopangwa.<br />
Mabadiliko yamekwenda sambamba na uundaji wa taasisi na miundo ya kuwezesha jamii<br />
kushiriki katika uendeshaji, umiliki na usimamizi wa huduma za afya. Vyombo hivyo ni<br />
Bodi za Huduma za Afya za Halmashauri na Kamati za Vituo vya Tiba. (Council Health<br />
Service Boards and Health Facility Governing Committees).<br />
Aidha, mpaka sasa Halmashauri zote 113 zimehamasishwa na kuridhia uundaji wa Bodi za<br />
afya na Kamati za Vituo vya Tiba. Hati Rasmi pamoja na Sheria Ndogo ya Mfuko wa Afya<br />
ya Jamii zipo katika ngazi ya utekelezaji kwa kuwa zikitoka Wilayani zinapelekwa mikoani<br />
ili kupitiwa na kuandikiwa barua na kupelekwa kwa Waziri mwenye dhamana na Serikali za<br />
Mitaa. Mwisho Katiba na Sheria kuandikwa kama Sheria na kutangazwa kwenye Gazeti la<br />
Serikali.<br />
23
Mpaka sasa kati ya Halmashauri 113 zilizohamasishwa ni Halmashauri 70 tu ambazo<br />
zimezindua Bodi za Huduma za afya na Kamati za vituo vya Tiba na zinafanyakazi. Wizara<br />
pia kwa mwaka jana ilibadilisha magari mapya 24 kwenye Halmshauri kwa ajili ya ufuatiliaji<br />
na usambazaji wa dawa na vifaa tiba na kinga kwenye vituo vya kutolea huduma.<br />
Matarajio ya Huduma za Afya Wilayani (District Health Services) mwaka 2005/2006<br />
Mwaka 2005/06 Wizara itakamilisha uzinduzi wa Bodi za Afya katika Halmashauri 63<br />
zilizobakia mara Sheria zao zitakapotangazwa kwenye Gazeti la Serikali. Sambamba na<br />
uzinduzi na uhamasishaji wa Bodi na Kamati za vituo vya Tiba, pia Halmashauri zitaendelea<br />
kuhamasishwa ili kuanzisha Mfuko wa Afya wa Jamii (Community Health Fund). Kwa vile<br />
hadi sasa Halmashauri za Wilaya 40 kati ya 113 zinatekeleza Mfuko wa Afya wa Jamii. Kwa<br />
kuwa Mfuko wa Afya wa Jamii unaendana na uzinduzi wa Bodi za Afya za Halmashauri<br />
inategemewa kwa mwaka wa 2005/06 kusaidia Halmashauri 73 zilizobakia ziwe zinatekeleza<br />
Mfuko huu.<br />
Wizara kwa mwaka 2005/06 itaendelea kutoa usimamizi wa kitaalam kwa Halmashauri juu<br />
ya uendeshaji wa huduma za afya katika ngazi ya Wilaya ili kuboresha huduma na kuendelea<br />
kubadilisha na kupeleka magari mapya 10 kwenye Halmashauri kwa ajili ya ufuatiliaji na<br />
usambazaji wa dawa na vifaa muhimu vya afya.<br />
Wizara itatoa mafunzo juu ya uainishaji wa MKUKUTA (NSGPR), Kitita cha Huduma<br />
Muhimu za Afya (NEPHI), Mpango wa Mabadiliko ya Afya wa miaka mitano (HSSP) na<br />
Mipango Kabambe ya Halmashauri CCHP). Aidha, mafunzo yatatolewa kwa timu za<br />
uandaaji Mipango ya Afya ya Halmashauri jinsi ya kutumia teknolojia ya kisasa ya kukotoa<br />
hesabu za bajeti za mipango ya Halmashauri (CCHP) kwa kulinganisha na mzigo wa<br />
magonjwa (Burden of Disease).<br />
2.3.14 UKIMWI<br />
Katika kukabiliana na janga hili la UKIMWI nchini, Wizara ilitekeleza Mkakati wa Sekta ya<br />
Afya wa Kudhibiti UKIMWI 2003-2006, ambao ni pamoja na Huduma ya Damu Salama,<br />
kutoa Ushauri Nasaha, Kufuatilia Mwenendo wa maambukizi ya Virusi vya UKIMWI katika<br />
Jamii, pamoja na Huduma ya Magonjwa ya Ngono (Sexually Transmitted Infections – STI).<br />
Mwaka 2004/05, kulikuwa na azma ya serikali ya kuanzisha mpango wa kitaifa wa kutoa<br />
dawa za kupunguza makali ya ugonjwa wa UKIMWI. Mpango huu uliweza kununua dawa<br />
kwa kutumia fedha zilizotengwa na Serikali. Hadi sasa wagonjwa wapatao 4,200<br />
wameanzishiwa dawa hizo katika vituo hivyo 32. Aidha, dawa zaidi zimeagizwa na<br />
zinategemewa kupokelewa hapa nchini kuanzia mwishoni wa mwezi April 2005. Dawa hizo<br />
zitatosha kuwaanzishia wagonjwa waliokusudiwa dawa wapatao 44,000.<br />
Aidha, katika kujenga uwezo wa hospitali wa kupima wagonjwa wa UKIMWI na kutambua<br />
hatua ya ugonjwa kwa lengo la kuanzisha matibabu, machine za Facs Count zinazopima<br />
viwango vya chembechembe za CD4 zipatazo 20 zimenunliwa na kusambazwa katika<br />
hospitali zote za rufaa na baadhi ya hospitali za mikoa. Mashine nyingine nane (8)<br />
zimeagizwa kwa ajili ya hospitali za mikoa iliyobakia.<br />
24
Aidha, mafunzo kwa wataalam wa afya ambao watatoa dawa za kupunguza makali ya<br />
UKIMWI kwa wagonjwa yametolewa kwa wataalam mbalimbali wa afya wapatao 492<br />
kutoka vituo 96 vya kutolea huduma za Afya. Vituo hivyo 96 vinajumuisha hospitali zote za<br />
rufaa na mikoa, baadhi ya hospitali za Wilaya, hospitali za Mashirika ya dini na Watu<br />
Binafsi. Huduma za kutoa madawa ya kupunguza makali ya ugonjwa wa UKIMWI<br />
zitaendelezwa kwa awamu kulingana na uwezo wa kifedha wa Serikali.<br />
Nchi yetu ina idadi kubwa ya watu wanaaohitaji dawa za kupunguza makali ya ugonjwa wa<br />
UKIMWI. Idadi hiyo ambayo inakisiwa kufikia watu 500,000 ni kubwa sana kulinganisha na<br />
uwezo. Serikali itaendelea kuongeza idadi ya wagonjwa wanaopata huduma hii kwa awamu<br />
mpaka wote wafikiwe.<br />
Matarajio ya Mpango wa kukabiliana na Ugonjwa wa UKIMWI mwaka 2005/2006<br />
Katika kuendelea kudhibiti ugonjwa wa UKIMWI na kutoa huduma kwa wale walioathirika<br />
na ugonjwa huu, Wizara mwaka 2005/2006 itaendelea kufuatilia mwenendo wa maambukizi<br />
ya virusi vya UKIMWI katika jamii kwa kufuatilia wajawazito katika kliniki 93 zilizopo<br />
kwenye mikoa 15 ya <strong>Tanzania</strong> Bara. Matokeo ya ufuatiliaji huu yatatoa picha kuhusu kuenea<br />
kwa virusi vya UKIMWI katika jamii na matokeo ya mikakati inayoendelea ya kudhibiti<br />
UKIMWI.<br />
Katika kipindi hiki, Wizara itakamilisha kuandaa utafiti wa kufuatilia usugu wa virusi vya<br />
UKIMWI kwa madawa yanayotumika hivi sasa kupunguza makali ya UKIMWI. Hivyo,<br />
ufuatiliaji wa usugu wa madawa ya kupunguza makali ya UKIMWI (HIV drug resistance<br />
threshold surveys) utaanzishwa katika mkoa wa Dar es Salaam ambapo dawa za kupunguza<br />
makali ya UKIMWI yalianza kutumika miaka kadhaa kabla ya serikali kuanza mpango wa<br />
kutoa dawa za kupunguza makali ya UKIMWI kwa wagonjwa wa UKIMWI.<br />
Matokeo yake yatasaidia katika kugundua dawa ambazo tayari Virusi vya UKIMWI<br />
vimekwisha kuwa sugu nazo kiasi kwamba haziwezi kupunguza makali ya ugonjwa wa<br />
UKIMWI na hivyo kusaidia wataalam kutoa maelekezo ya dawa zinazofaa.<br />
Wizara itanunua na kusambaza dawa za kupunguza makali ya UKIMWI katika vituo 180<br />
vilivyoteuliwa kutoa huduma hiyo kote nchini ili kuwafikia wagonjwa wapya 56,000 ili<br />
kufikia lengo jipya lililowekwa la kuwafikia wagonjwa 100,000 nchini kote ifikapo Juni<br />
2006. Vituo vipya vitakavyohusishwa katika mpango huu ni pamoja na hospitali zote za<br />
Wilaya na hospitali za binafsi ziliopo kwenye mikoa ya pembezoni na mikoa iliyo na<br />
viwango vya maamukizi ya UKIMWI zaidi ya asilimia saba.<br />
Huduma za ushauri nasaha na upimaji wa hiari zitaendelea kutolewa katika vituo 521<br />
vinavyotoa huduma ili kuweza kutoa ushauri nashaha kwa wagonjwa wote 100,000<br />
watakaokuwa kwenye tiba ya dawa za UKIMWI. Aidha, tutahakikisha mafunzo kwa<br />
wataalam wa kutoa huduma za dawa za kupunguza makali ya UKIMWI katika kila kituo<br />
yatatolewa na angalau watalam wanne ambao wameshapatiwa mafunzo wanakuwepo katika<br />
vituo vya huduma. Wizara itaendelea kutoa huduma za Magonjwa ya Zinaa katika mikoa<br />
yote 21 pamoja na kuelimisha jamii kuhusu ugonjwa wa UKIMWI hususan kuacha<br />
kuwanyanyapaa wagonjwa wa UKIMWI na kuzingatia matumizi sahihi ya dawa za<br />
kupunguza makali ya ugonjwa wa UKIMWI.<br />
25
2.3.15 Mradi wa Uimarishaji Huduma Muhimu za Afya (MUHUMA) TEHIP<br />
Mradi wa Uimarishaji Huduma Muhimu za Afya (MUHUMA) umekuwa ukitekelezwa katika<br />
Wilaya mbili za Morogoro vijijini na Rufiji toka Mwaka 1997 mpaka mwaka 2004 ulipofikia<br />
kikomo kama mradi. Utafiti umeonyesha kuwa kasi ya vifo imepungua katika Wilaya zote<br />
mbili kwa asilimia zaidi ya 55% kwa watoto chini ya miaka mitano na asilimia 18% kwa<br />
watu wazima. Kupungua huku kumeziweka Wilaya hizo mbili kwenye matumaini ya kufikia<br />
moja ya malengo ya milenia ya Umoja wa Mataifa ya kupunguza kasi ya vifo miongoni mwa<br />
watoto chini ya miaka mitano kwa theluthi mbili ifikapo mwaka 2015.<br />
Kufuatana na matokeo haya, Wizara ya Afya ikishirikiana na wadau wengine imeanza<br />
mikakati ya kupata fedha za kueneza mbinu na nyenzo zilizobuniwa na kufanyiwa kazi katika<br />
Wilaya hizo mbili katika Wilaya zote nchini. Dhana ni kuwa endapo nchi nzima itatekeleza<br />
yaliyofanywa Morogoro na Rufiji basi kasi ya vifo vya watoto wadogo na wakubwa<br />
itapungua na hivyo <strong>Tanzania</strong> kuwa miongoni mwa nchi za mwanzo kutekeleza mpango huo.<br />
2.4 Idara za Tiba Utekelezaji wa Majukumu mwaka 2004/2005<br />
2.4. 1 Huduma za Uchunguzi wa Magonjwa<br />
Mradi wa uimarishaji wa huduma za X-ray na Ultrasound ulikabidhiwa kwa Serikali kutoka<br />
kampuni ya “Philips Medical Systems” ya nchi ya Uholanzi ili tuweze kuuendeleza<br />
wenyewe. Makabidhiano hayo yalifanyika Jijini Mwanza katika hospitali ya Bugando tarehe<br />
22 Februari 2005, ambapo Mheshimiwa Rais alikabidhiwa mashine kubwa na maalum ya<br />
Ultrasound kutoka kwa mwakilishi wa Kampuni hiyo yenye thamani ya takriban fedha ya<br />
kitanzania shilingi milioni 88. Mashine nyingine ilipelekwa Zanzibar katika hospitali ya<br />
Mnazi mmoja tarehe 14 Machi, 2005. Aidha, Wizara iliagizwa kusimamia ukarabati na kinga<br />
ya matengenezo ya mashine hizo baada ya mradi kwisha ifikapo mwishoni mwa mwaka<br />
2005. Vilevile, Wizara imekamilisha taratibu zote za kupeleka Bungeni muswada wa sheria<br />
inayohusu usajili wa wanataaluma ya mionzi ili kuboresha huduma za mionzi.<br />
Kuhusu usimamizi na utekelezaji wa huduma za karakana zetu za Kanda, Wizara imeendelea<br />
kuziimarisha kwa kuzipatia vipuli, vifaa na nyenzo za utekelezaji wa matengenezo ya<br />
mashine hizo za kutolea huduma za Afya.<br />
Kuhusu uimarishaji wa maabara za hospitali ili ziweze kufuatilia wagonjwa wanaopatiwa<br />
dawa za kupunguza makali ya UKIMWI, Wizara imekwishaweka mashine 20 za kupima<br />
CD4 katika hospitali zote za rufaa na mikoa 16. Mashine nyingine 8 za CD4 na dawa zake<br />
zimeshawasili kwa ajili ya mikoa iliyobaki na hospitali za manispaa za Dar es Salaam.<br />
Vilevile, mashine kwa ajili ya vipimo vingine (Clinical Chemistry and Haematology) kwa<br />
ajili ya hospitlai 10 za mikoa na 13 za Wilaya zimegizwa. Vipimo hivyo ni kwa ajili ya<br />
kufuatilia athari za ARV (Toxicity follow up) kwa wagonjwa wanaotumia.<br />
Kuhusu huduma ya damu salama, ujenzi wa vituo vya kanda vya upatikanaji wa damu (Zonal<br />
Blood Transfusion Centres- ZBTC) umekamilika katika Kanda za Ziwa, Kasikazini na<br />
Nyanda za juu Kusini. Kwa upande wa Kanda ya Mashariki, ujenzi umeshaanza Dar es<br />
Salaam na kanda ya Kusini ujenzi haujaanza. Mwongozo wa huduma za damu salama<br />
umekamilika.<br />
26
Matarajio ya Huduma za Uchunguzi wa Magonjwa mwaka 2005/2006<br />
Wizara itaingia mkataba na Kampuni ya Philips Medical Systems katika kuhakikisha kuwa,<br />
mashine za X-ray, Ultrasound na vifaa vingine chini ya mradi wa kuimarisha huduma za<br />
uchunguzi wa magonjwa nchini zinadumu kwa miaka mingi. Katika mkataba huo mafunzo<br />
maalum hasa yale ya mashine zenye teknolojia ya hali ya juu hususan X-ray na Ultrasound<br />
yatatolewa kwa watumiaji, makandarasi na mafundi wetu waliopo kwenye karakana za<br />
Kanda.<br />
Mkataba huu utakuwa wa miaka 5 kuanzia Januari 2006 hadi Desemba 2010. Wizara pia<br />
itaendelea kuvifanyia matengenezo ya mara kwa mara vifaa tiba kupitia karakana za kanda<br />
kwa maeneo yote yanayotoa huduma ya afya kuanzia zahanati hadi hospitali za rufaa, kwa<br />
utaratibu utakaopangwa kwa ajili ya utekelezaji wake kufuatana na mwongozo wa Wizara juu<br />
ya uboreshaji na matengenezo ya vifaa tiba vya hospitali nchini.<br />
Wizara inakusudia kupeleka Bungeni muswada wa sheria inayohusu taaluma ya mionzi<br />
nchini katika mwaka 2005/06. Pia <strong>Tanzania</strong> imepewa heshima na nchi za Afrika ya kuwa<br />
mwenyeji wa kongamano la wanataaluma ya Radiologia kutoka Afrika mnamo mwezi<br />
Septemba, 2005.<br />
Wizara itaendelea kuimarisha huduma za maabara kwa kuagiza mashine nyingine, na vifaa<br />
vya maabara kwa ajili ya kufuatilia wagonjwa wanaopatiwa dawa za kusaidia kupunguza<br />
makali ya UKIMWI. Aidha, baadhi ya maabara zitaboreshwa kwa kufanyiwa ukarabati ili<br />
kukidhi mahitaji ya utoaji wa huduma hizo.<br />
Kuhusu huduma ya damu salama, Wizara itakamilisha ujenzi wa Kanda ya Mashariki pamoja<br />
na kuanza mipango ya ujenzi wa Kanda za Kusini (Mtwara) na Kati (Dodoma). Wakati huo<br />
Kanda za Ziwa, Nyanda za Juu Kusini na Kaskazini zitaanza kazi ya ukusanyaji wa damu<br />
salama katika hospitali zetu kwa kushirikiana na Shirika la Msalaba Mwekundu <strong>Tanzania</strong>.<br />
2.4.2 Huduma za Tiba Asili<br />
Mwaka 2002/2003 muswada wa Sheria ya Dawa, Tiba Asili na Tiba Mbadala, ulipitishwa na<br />
Bunge. Utekelezaji wa Sheria Namba 23 ya mwaka 2002 utaanza July 2005. Baraza la Tiba<br />
Asili na Tiba Mbadala tayari limekwisha teuliwa na mamlaka husika kwa mujibu wa Sheria<br />
hiyo.<br />
Wizara ya Afya imeandaa Kanuni na Miongozo ya usajili wa Waganga wa Tiba Asili na Tiba<br />
Mbadala. Usajili wa vituo vya kutolea huduma za Tiba Asili na Tiba Mbadala; nidhamu na<br />
maadili kwa Waganga wa Tiba Asili na Tiba Mbadala; usimamizi na usajili wa bidhaa<br />
nyinginezo za Asili zinazotumika kwa ajili ya afya ya binadamu.<br />
Matarajio ya Huduma za Tiba Asili mwaka 2005/2006<br />
Wizara itaendelea kuwaelimisha Waganga wa jadi na Wadau wa Tiba Asili na tiba mbadala<br />
ili kuielewa sheria ya tiba asili na tiba mbadala. Aidha, Wizara itaendelea na ufuatiliaji wa<br />
tiba asili na tiba mbadala likiwemo suala la utafiti.<br />
27
2.4.3 Huduma za Afya ya Kinywa<br />
Katika mwaka 2004/2005, Wizara ya Afya imefunga vifaa vya Tiba ya Meno (Dental Units)<br />
katika Halmashauri za Wilaya zifuatazo: Mbarali, Karatu, Ngorongoro, Simanjiro, Kiomboi,<br />
Morogoro Vijijini, Morogoro Manispaa, Mbozi, Hanang, Sikonge, Mpanda, Mvomero,<br />
Bariadi, Bukombe, Kilombero, Liwale, Njombe, Ludewa, Sengerema, Geita, Ukerewe,<br />
Misungwi, Newala, Mwanga na Kwimba. Pia, vifaa vilifungwa katika hospitali zifuatazo:<br />
Iringa, Bombo, Mawenzi, Mt. Meru na KCMC.<br />
Aidha dawa na vifaa muhimu vya tiba ya meno vilinunuliwa kwa ajili ya matumizi ya<br />
hospitali za mikoa na kwa ajili ya mafunzo vyuoni.<br />
Matarajio ya Huduma za Afya ya Kinywa mwaka 2005/2006<br />
Katika mwaka wa fedha 2005/2006 awamu ya pili ya ufungaji vifaa kwa kuzipatia kliniki za<br />
meno za Wilaya na Halmashauri viti (Dental Chairs), taa maalum (operating lights) na viti<br />
vya kukalia madaktari wa meno wanapofanya kazi (Operating Stools) utaanza.<br />
Wilaya/Halmashauri zitakazopatiwa vifaa hivyo ni:- Muheza, Korogwe, Chunya, Ileje,<br />
Mbeya Vijijini, Mbeya Manispaa, Mbarali, Rungwe, Kyela, Karatu, Ngorongoro, Simanjiro,<br />
Iramba, Morogoro Vijijini, Morogoro Manispaa, Mbozi, Hannang, Singida, Tabora, Sikonge,<br />
Mpanda, Musoma, Kigoma, Kilombero, Mvomero, Bariadi, Bukombe, Kishapu, Liwale,<br />
Njombe, Ludewa, Bukoba, Karagwe, Sengerema, Geita, Ukerewe, Misungwi, Newala,<br />
Mwanga, Kwimba, Dodoma Manispaa, Tarime, Bunda, Biharamulo, Tabora Manispaa, na<br />
Mbinga. Pia hospitali zifuatazo zitapatiwa vifaa hivyo; Kibosho, Mbeya Rufaa, Mawenzi, Mt.<br />
Meru, Bombo, Iringa, Dodoma, Mbeya Mkoa, Mirembe, Kilema, Bugando, Dareda, Ligula,<br />
Maweni, Singida na Bukoba.<br />
2.4.4 Huduma za Afya ya Akili na Vita dhidi ya Dawa za Kulevya<br />
Mwaka 2004/2005, Wizara imeendelea kusimamia uboreshaji wa huduma za afya ya akili<br />
ngazi ya msingi. Shughuli hizo zinaendelezwa katika mikoa ya Dar es Salaam, Manyara,<br />
Mtwara na Mwanza.<br />
Toleo rasmi la kwanza la vitabu vya Huduma ya Afya ya Akili ngazi ya Msingi<br />
vimechapishwa nakala 4,500 na kusambazwa kulingana na utaratibu wa kutoa mafunzo<br />
katika kila Mkoa.<br />
Matarajio ya Huduma za Afya ya Akili mwaka 2005/2006<br />
Kitengo kitaendelea na mipango ya kueneza huduma ya afya ya akili ngazi ya msingi kwa<br />
kushirikiana na wadau wa ndani na nje katika Mikoa ya Tanga, Arusha, Kilimanjaro,<br />
Manyara na Mwanza kwa kushirikiana na MEHATA na CORDAID na Mkoani Mtwara kwa<br />
kushirikiana na shirika la Basic Needs.<br />
Mpango wa kutoa Mafunzo kwa watoa huduma ngazi ya msingi utaendelea katika Mikoa ya<br />
Dar es Salaam na Manyara. Pia, Wizara inategemea kukamilisha uchapishaji wa mwongozo<br />
wa Sera ya Afya ya Akili.<br />
28
2.4.5 Huduma za Hospitali za Mashirika ya kujitolea, Makampuni na Watu Binafsi<br />
Katika mwaka 2004/2005, Hospitali mbili za Mashirika ya Dini (Karatu na Mugana)<br />
ziliombwa na Halmashauri za Wilaya ya Karatu na Bukoba Vijijini zitumike kama Hospitali<br />
Teule. Hospitali hizo tayari zimeanza kutumika kama hospitali Teule za Wilaya hizo. Ruzuku<br />
ilibakia kuwa TShs 30,000/= kwa kitanda kwa mwaka. Kulikuwa na ongezeko la vitanda 174<br />
kwa ajili ya kupewa Ruzuku.<br />
Jumla ya vituo vya kutolea huduma za afya vilivyosajiliwa mwaka 2004/2005 ni 53 ambavyo<br />
ni 73% kati ya 73 vilivyoombewa usajili.<br />
Matarajio ya Huduma za Hospitali za Mashirika ya kujitolea, Makampuni na Watu<br />
Binafsi mwaka 2005/2006<br />
Wizara itaanza kutumia “Service Agreement” katika kufanya makubaliano kati ya<br />
Halmashauri za Wilaya na wamiliki wa hospitali za mashirika ya dini. Vile vile, Wizara<br />
itajadili maombi ya Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kuhusu kutumia hospitali ya<br />
Tosamaganga kama hospitali Teule ya Wilaya hiyo.<br />
2.4.6 Huduma ya Dawa, Vifaa na Vifaa Tiba<br />
Mwaka 2004/05, kiasi cha Tshs. 35,175,356,000 zilitumika kununua dawa, vifaa na vifaa tiba<br />
kwa matumizi ya hospitali, Zahanati na Vituo vya Afya. Aidha, hospitali za Wilaya, Mikoa<br />
na Rufaa ziliendelea na utekelezaji wa uchangiaji wa gharama za dawa chini ya mfumo wa<br />
‘Capitalization of Hospital Pharmacies’ ambapo wananchi wanalipa nusu ya bei halisi ya<br />
dawa. Fedha kutokana na mauzo ya dawa ziliingizwa kwenye mfuko wa dawa (Drug<br />
Revolving Fund) kuwezesha hospitali hizo kununua dawa nyingine zilizohitajika.<br />
Mwaka 2004/2005, Zahanati mpya 526 na Vituo vya Aya 36 vilivyojengwa na Halmashauri<br />
na kwa nguvu za wananchi vilipewa masanduku ya dawa. Aidha, Zahanati 716 na vituo vya<br />
afya 88 katika Mikoa ya Kagera, Mara, Mwanza na Shinyanga vilianza kuagiza dawa na vifaa<br />
kwa kutumia mfumo wa Indent. Ili kurahisisha utoaji wa dawa na vifaa kwa mfumo huu,<br />
sehemu maalum imejengwa katika Bohari ya Mwanza kwa ajili ya kuhudumia Zahanati na<br />
Vituo vya Afya hivyo. Kutokana na hatua hiyo, Bohari ya Mwanza sasa imeondokana na<br />
mfumo wa usambazaji wa masanduku ya dawa.<br />
Wizara pia ilitoa mafunzo ya utekelezaji wa mfumo wa Indent kwa baadhi ya wajumbe wa<br />
Kamati za Uendeshaji wa Huduma za Afya katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Tanga.<br />
Wajumbe hawa watatoa mafunzo kwa watumishi katika Zahanati na Vituo vya Afya katika<br />
mikoa yao ili kuwezesha uagizaji wa dawa na vifaa kulingana na mahitaji na kwa kuzingatia<br />
mgao wa fedha na maradhi katika sehemu zao.<br />
Bohari ya Dawa iliendelea na usambazaji wa dawa na vifaa vya miradi misonge (vertical<br />
programmes) na vya misaada. Katika kipindi hicho, Bohari ya Dawa ilisambaza chanjo, dawa<br />
za kutibu Kifua Kikuu na Ukoma, Usubi, Uzazi wa Mpango, Matende, Ngirimaji na<br />
magonjwa ya mtegesheo kwa watu waishio na UKIMWI.<br />
29
Matarajio ya Huduma ya Dawa, Vifaa na Vifaa Tiba mwaka 2005/2006<br />
Katika mwaka wa fedha 2005/06, Wizara ya Afya imetengewa jumla ya Tshs.<br />
32,320,996,556 kwa ajili ya ununuzi wa dawa, vifaa na vifaa tiba kwa matumizi ya Zahanati,<br />
Vituo vya Afya na hospitali za Serikali na hospitali Teule kwa matumizi ya kawaida. Pia<br />
Serikali imetenga Tshs. 20,000,000,000 kwa ajili ya ununuzi na usambazaji wa dawa na vifaa<br />
tiba vya kupunguza makali ya UKIMWI.<br />
Wizara ya Afya kupitia Bohari ya Madawa, itasambaza dawa na vifaa katika Zahanati 3,500<br />
na Vituo vya Afya 400. Kati ya hivyo, Zahanati 175 na Vituo vya Afya 25 vitakuwa vipya<br />
vilivyojengwa na Halmashauri na nguvu za wananchi. Aidha, katika kuboresha usambazaji<br />
wa dawa, vifaa na vifaa tiba, Wizara ya Afya itaendesha majaribio ya mfumo ujulikanao<br />
kama Integrated Logistics System katika mikoa ya Dodoma na Iringa. Mfumo huu<br />
utawezesha Zahanati, Vituo vya Afya na hospitali kuagiza dawa na vifaa vya kawaida na vile<br />
vya miradi na misaada chini ya mfumo mmoja. Mfumo huu unatarajiwa kuiwezesha Wizara<br />
kukusanya takwimu za mahitaji na matumizi halisi ya dawa, vifaa na vifaa tiba.<br />
2.4.7 Huduma za kuzuia Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI kutoka kwa Mama kwenda<br />
kwa Mtoto<br />
Katika mwaka 2004/2005 wizara imesambaza huduma ya kuzuia maambukizi ya virusi vya<br />
ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mototo katika mikoa 9 zaidi ya <strong>Tanzania</strong> bara na<br />
kufanya huduma hii kupatikana katika hospitali zote za mikoa na 82 za Wilaya. Mikoa hiyo<br />
ni Lindi, Dodoma, Ruvuma, Rukwa, Kigoma, Mara, Shinyanga, Tanga na Singida.<br />
Vilevile, wizara inashirikiana na wadau mbalimbali ilikuweza kusambaza hudma hii katika<br />
hospitali na vituo vya kutolea huduma vinavyomilikiwa na mashirika ya dini.<br />
Wizara imeendelea na mpango wa kutoa dawa za kupunguza makali ya ugonjwa wa<br />
UKIMWI kwa akinamama wajawazito, wazazi wenzao na watoto wao. Mpango huu ambao<br />
unaitwa “MTCT –Plus” unaenda sambamba na mpango wa Taifa wa kutoa dawa za<br />
kupunguza makali ya UKIMWI (ART programe) na hivyo umeanza kutekelezwa katika vituo<br />
96 vilivyo katika mpango wa ART.<br />
Matarijio ya Huduma za kuzuia Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI kutoka kwa<br />
Mama kwenda kwa Mtoto mwaka 2005/2006<br />
Katika mwaka 2005/2006 Wizara ya Afya imepanga kupanua huduma ya kuzuia<br />
maambukizi ya virusi vya UKIMWI kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto (PMTCT) katika<br />
wilaya 20 zaidi ambazo hazina huduma hiyo na kufanya jumla ya wilaya 102 kuwa na<br />
huduma hii.<br />
Vile vile, Wizara itaendelea kuimarisha huduma ya “MTCT – Plus” ambayo imeanza<br />
kutolewa katika vituo vile 96 vilivyo katika mpango wa “ART Programme”.<br />
Lengo ni kuhakikisha akinamama wajawazito walioathirika na VVU na wenye vigezo vya<br />
kupata “ART” wapate huduma hiyo na wale ambao hawana vigezo wakisha jifungua<br />
waendelee kufuatiliwa na pindi watakapobainika kuwa wana vigezo wapatiwe huduma ya<br />
ART.<br />
30
2.4.8 Huduma ya Matibabu Nje ya Nchi<br />
Wizara imefanya mazungumzo na wahisani kutoka nje ya nchi ili kuanzisha hapa nchini<br />
huduma ya tiba ya magonjwa ambayo kwa sasa yanatibiwa nje ya nchi. Wahisani hao ni<br />
Serikali ya Japan na Serikali ya Watu wa China. Mipango hii imelenga kulipunguzia Taifa<br />
gharama za tiba nje ya nchi pamoja na kuwapunguzia wagonjwa maumivu wakati wakingojea<br />
kwa muda mrefu kwenda kutibiwa nje ya nchi kutokana na upungufu wa fedha.<br />
Matarajio ya Huduma ya Matibabu Nje ya Nchi mwaka 2005/2006<br />
Bajeti itaongezwa ili kuwezesha wagonjwa wengi zaidi kupelekwa kutibiwa nje ya nchi na<br />
kuendelea kutoa msaada kwa matibabu ya wagonjwa ambao badala ya kupelekwa kutibiwa<br />
nje ya nchi watatibiwa hapa nchini kwa vile wanashindwa kumudu gharama za matibabu<br />
hayo.<br />
Wizara itaendelea kushirikiana na mashirika na hospitali zinazoanzisha utoaji wa matibabu<br />
ambayo kwa sasa yanapatikana nje ya nchi, pamoja na Serikali ambazo zina mpango wa<br />
kusaidia nchi kuweza kutoa matibabu kama hayo.<br />
2.5 Huduma ya Utawala na Watumishi<br />
2.5.1 Idara ya Utawala Utekelezaji wa Majukumu mwaka 2004/2005<br />
Mwaka wa 2004/2005, Wizara ya Afya imeendelea kutekeleza Sera ya Menejimenti na Ajira<br />
katika Utumishi wa Umma ya Mwaka 1999, kwa kuajiri jumla ya Watumishi 148 wa kada<br />
mbalimbali za Afya. Aidha, katika kushughulikia maslahi na maendeleo ya watumishi ili<br />
kuimarisha utendaji kazi Wizara imewapandisha vyeo watumishi 6,587. Hili ni ongezeko la<br />
asilimia 65 ya lengo lililokuwa limewekwa la kuwapandisha vyeo watumishi 4,000.<br />
Watumishi wapatao 110 wa kada na ngazi tofauti walifanyiwa upekuzi (vetting) kwa<br />
madhumuni ya kuwawezesha kuelewa na kuzingatia misingi ya maadili mema katika<br />
utumishi wa Umma kwa mujibu wa Sheria, kanuni na taratibu zilizopo. Msisitizo mkubwa<br />
uliowekwa katika mafunzo hayo ulihusu suala zima la matumizi sahihi ya taarifa za Serikali<br />
na utii kwa Serikali. Aidha, Wizara iliendelea kutoa mafunzo ya jinsia kwa watumishi ili<br />
kuendelea kudumisha Utawala Bora ambapo jumla ya watumishi 744 walipatiwa mafunzo<br />
hayo.<br />
Pia Wizara ilitoa mafunzo kwa maafisa waandamizi na wa ngazi ya kati kuhusu<br />
misingi ya Utawala Bora na mapambano dhidi ya rushwa ili kuzuia matukio ya<br />
rushwa na kuziba mianya ya rushwa. Mafunzo haya yaliwahusisha Wakurugenzi wa<br />
Wizara ya Afya, Waganga Wakuu wa Mikoa, Waganga Wakuu wa Wilaya, Wakuu<br />
wa Vyuo vyote vya Afya nchini na Maafisa wengine. Jumla ya watumishi 1,169<br />
walipatiwa mafunzo hayo. Sambamba na mapambano dhidi ya rushwa, Wizara<br />
ilichapisha vijarida 850 vya Mkataba wa Huduma kwa Mteja na kuvisambaza kwa<br />
wadau. Lengo lilikuwa kuwafahamisha wateja wetu kuhusu mahusiano yetu na<br />
majukumu yetu kwao pamoja na haki na wajibu wao. Mkataba huu unaelekeza pia<br />
namna mteja anavyoweza kutuma malalamiko/maoni kuhusu huduma zetu.<br />
31
Matarajio ya Huduma za Utawala na Watumishi mwaka 2005/2006<br />
Wizara ya Afya itaendelea kutoa kipaumbele katika kuimarisha na kuboresha maslahi,<br />
maendeleo na utendaji kazi (Capacity building) kwa watumishi wake ili kuimarisha na<br />
kuongeza utoaji wa huduma za afya kwa wananchi watakaohitaji huduma hiyo muhimu.<br />
Malengo haya yatafikiwa kwa kuajiri watumishi wapya ili kuziba mapengo yaliyopo na<br />
kuwapandisha vyeo watumishi waliopo kwa kuzingatia sifa, vigezo na ikama iliyoidhinishwa.<br />
Ili kwenda sambamba na mabadiliko yanayoendelea kufanyika katika Sekta ya Afya, Wizara<br />
imejiwekea mpango wa kutoa mafunzo ya Huduma kwa Mteja kwa watumishi wake wote<br />
(customer care and Public ethics).Mafunzo haya yatawahusisha watumishi wapatao 3,336<br />
kutoka Makao Makuu ya wizara, Hospitali tatu za Rufaa, Vyuo vya Afya 108 pamoja na<br />
Kanda 6 za mafunzo. Mafunzo hayo yataendeshwa kwa awamu tatu.<br />
Aidha, Wizara imejipangia kuanzisha teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Information<br />
Communication Technology) ili kuimarisha na kuongeza utoaji wa huduma bora ya<br />
upatikanaji na upashanaji wa habari kwa haraka zaidi. Wizara tayari imeanza utoaji wa<br />
mafunzo kwa watumishi wake na itaendelea na mafunzo hayo ili kuwawezesha kumudu<br />
matumizi ya teknolojia hiyo.<br />
Kwa kutambua umuhimu wa mashirikiano na Mashirika ya Kimataifa na kwa kuzingatia Sera<br />
ya Utandawazi, Wizara ya Afya itaendelea kushirikiana na Taasisi zote muhimu ili kwenda<br />
sambamba na maendeleo ya kisasa.<br />
Viongozi wa Wizara na watendaji wake wakuu watahudhuria mikutano muhimu ili<br />
kujadiliana na kutolea maamuzi muhimu ya kimaendeleo na kuchangia uzoefu wa nchi yetu<br />
katika masuala mbalimbali ambayo tumeonyesha kuyamudu.<br />
2.6 Huduma ya Mafunzo ya Watumishi, Utekelezaji wa Majukumu mwaka 2004/05<br />
Katika kipindi cha mwaka 2004/2005 Wizara ilifanya yafuatayo:<br />
• Wanafunzi 2,803 walihitimu katika vyuo mbalimbali vya afya hapa nchini katika fani<br />
za Uuguzi na Sayansi za Afya. Aidha, jumla ya wanafunzi 214 walihitimu mafunzo<br />
ya Madaktari Tiba, Wafamasia, Madaktari wa meno katika ngazi ya Shahada katika<br />
vyuo vya Muhimbili, KCMC na Hubert Kairuki Memorial University. Madaktari 136<br />
walimaliza mafunzo ya “internship” na wanatarajia kupatiwa mafunzo ya kuwaandaa<br />
kufanya kazi (Inducton course) na kupangiwa vituo vya kazi sehemu mbalimbali<br />
nchini<br />
• Wizara imegharamia mafunzo ya muda mrefu ya watumishi 257 nje na ndani ya nchi<br />
ambao wanatarajiwa kumaliza mafunzo yao mwaka huu<br />
• Wizara imefanya mapitio kwa mitaala mitano katika vyuo vya Uguzi na Sayansi za<br />
Afya<br />
• Jumla ya vyuo 17 viliweza kufanyiwa ukarabati ambao utaendelea katika mwaka<br />
ujao wa 2005/2006 katika baadhi ya vyuo<br />
• Jumla ya vyuo 78 kati ya 93 vilivyokaguliwa na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi<br />
(NACTE) vilipata usajili wa baraza hilo<br />
• Wizara kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE)<br />
imeendelea kukagua vyuo vyote vinavyoendesha mafunzo katika fani ya Sayansi za<br />
Afya hapa nchini ili kupata usajili wa baraza hilo na kuviandaa kufikia hatua ya<br />
kupata ithibati (accreditation)<br />
32
• Wizara imetoa mafunzo kuhusu tiba ya kupunguza makali ya UKIMWI kwa<br />
watumishi 492 wakiwemo Madakatari, Wafamasia, Mafundi sanifu maabara,<br />
Wauguzi, watoa Ushauri nasaha na Wafauatiliaji wa wagonjwa majumbani (VCT<br />
counsellors and Home based care Providers). Vilevile, miongozo ya tiba ya ugonjwa<br />
wa UKIMWI na vijitabu vya kufundishia vilitengenezwa<br />
• Watumishi katika hospitali 68 wakiwemo Madaktari wafawidhi wa hospitali,<br />
Wauguzi waandamizi na Wafamasia walipata mafunzo ya kujiendeleza kuhusu<br />
matumizi sahihi ya madawa<br />
• Ukaguzi unaozingatia ubora wa viwango vya masomo, mafunzo ya vitendo na usafi<br />
wa mazingira ulifanyika katika vyuo 54 vilivyopo katika Kanda za Kaskazini,<br />
Mashariki, Kusini, Ziwa na Nyanda za juu Kusini<br />
• Wizara imekamilisha miongozo ya mafunzo ya Timu za Usimamizi katika ngazi ya<br />
Mkoa , Hospitali, Vituo vya Afya na Zahanati na kuanza mafunzo hayo kwa timu za<br />
mikoa kwa awamu<br />
• Wizara imeendesha mafunzo kwa timu za afya kwenye Sekretarieti za Mikoa. Lengo<br />
ni kuziimarisha timu hizi ziweze kuzisimamia na kuzisaidia Halmashauri za Wilaya<br />
kuboresha huduma wanazozitoa, matumizi ya rasilimali, utoaji taarifa na uzingatiaji<br />
wa viwango vya utoaji huduma. Katika mwaka huu timu za mikoa saba zilipatiwa<br />
mafunzo hayo.<br />
Kuhusu Mipango ya Watumishi mwaka 2004/2005 Wizara imefanya mambo yafuatayo:-<br />
• Imeendesha utafiti wa matumizi ya wataalam wanaohitimu katika Taasisi ya Elimu<br />
ya Afya ya Msingi (Tracer study)<br />
• Imeratibu vikao vya kamati ya wadau ya ufuatiliaji wa masuala ya maendeleo ya<br />
watumishi wa Sekta ya Afya<br />
• Imetoa mafunzo na maelekezo juu ya mfumo wa utunzaji wa takwimu za watumishi<br />
utumiao mfumo wa kompyuta kwa wahusika wakuu wa utunzaji wa takwimu za<br />
watumishi katika ngazi za Wilaya 15<br />
• Imefanya mapitio ya Sera ya watumishi katika Sekta ya Afya na kukamilisha<br />
mapitio ya Ikama ya watumishi katika Vyuo vya Afya.<br />
2.6.1 Matarajio ya Huduma ya Mafunzo ya Watumishi wa Afya mwaka 2005/2006<br />
Mwaka 2005/2006 Wizara inatarajia kufanya yafuatayo;<br />
• Wizara inatarajia kuvifanyia ukarabati vyuo vyake 27 ili kuviweka katika hali nzuri<br />
zaidi. Samabamba na hilo itaanzisha mafunzo ya Madaktari Wasaidizi katika<br />
kilichokuwa chuo cha Maafisa Tabibu Ifakara ambapo ukarabati mkubwa unaendelea<br />
hivi sasa<br />
• Wizara itafanya utafiti ili kupata mahitaji halisi ya mafunzo yanayohitajika sehemu<br />
ya kazi (Training Needs Assesmnt) yenye lengo la kupata maeneo yanayohitajika<br />
kutilia mkazo mafunzo kwa watumishi, ili kuboresha utoaji huduma zinazotolewa<br />
kwa wananchi<br />
• Wizara itaendesha mafunzo kwa timu za afya kwenye Sekretarieti za Mikoa. Lengo<br />
ni kuziimarisha timu hizi ziweze kuzisimamia na kuzisaidia Halmashauri za Wilaya<br />
kuboresha huduma wanazozitoa, matumizi ya rasilimali, utoaji taarifa na uzingatiaji<br />
wa viwango vya utoaji huduma. Katika mwaka 2005/2006 timu za mikoa 12<br />
zitapatiwa mafunzo hayo<br />
• Wizara itaendelea kufanya mapitio ya mitaala 4 ya Vyuo vya Sayansi ya Afya na<br />
uuguzi ili kuiboresha kulingana na mabadiliko yanayoendelea hivi sasa katika Sekta<br />
ya Afya<br />
33
• Kufuatilia, kutathmini na kutoa ushauri juu ya hali ya watumishi katika Sekta ya<br />
Afya kwa kushirikiana na mamlaka mbalimbali<br />
• Kuratibu vikao vya kamati ya Wadau ya kufuatialia masuala ya watumishi wa Sekta<br />
ya Afya<br />
• Kundesha mafunzo na maelekezo ya mfumo wa utunzaji takwimu za watumishi kwa<br />
kutumia kompyuta katika ngazi za Wilaya kwa zile Wilaya ambazo hazijapata<br />
mafunzo haya<br />
• Kuandaa mpango mkakati wa watumishi wa Sekta ya Afya<br />
• Kuendeleza utafiti wa matumizi ya wahitimu wa chuo cha CEDHA utafiti (Tracer<br />
Study), wenye lengo la kuboresha matumizi sahihi ya wataalam wanaohitimu katika<br />
chuo hicho.<br />
2.7 Ofisi ya Mganga Mkuu Kiongozi Utekelezaji wa Majukumu mwaka 2004/05<br />
2.7.1 Huduma za Dharura na Maafa<br />
Katika Kipindi cha mwaka 2004/2005, kazi zifuatazo zilitekelezwa:<br />
• Kuchapisha miongozo miwili ya utoaji wa Huduma za Dharura na Maafa yaani,<br />
“Health Sector Guidelines and Protocol on Emergency and Disaster Management” na<br />
“Emergency Operation Plan” (EOP) nakala 1,000 kila moja na kuzisambaza katika<br />
vituo vya kutolea huduma nchini<br />
• Kutoa mafunzo ya jinsi ya kukabiliana na Dharura na Maafa kwa watoa huduma ya<br />
afya katika Hospitali (First responders) ili kuongeza ufanisi katika kazi zao za kila<br />
siku<br />
• Kutoa mafunzo maalum ya jinsi ya kukabiliana na Dharura na Maafa kwa Kamati za<br />
Uendeshaji wa Huduma za Afya katika mikoa (RHMT), ili kuongeza ufanisi katika<br />
kusimamia kazi hiyo kwa watumishi katika hospitali<br />
• Kufanya upembuzi yakinifu katika hospitali za Kilimanjaro, Tanga, Arusha na<br />
Mbeya ili kutoa ushauri wa maandalizi ya jinsi ya kukabiliana na Dharura na Maafa,<br />
pindi yatokeapo.<br />
Matarajio ya Huduma za Dharura na Maafa mwaka 2005/2006<br />
Katika kipindi cha mwaka 2005/2006, kitengo kinakusudia kufanya kazi zifuatazo:<br />
• Kutembelea na kufanya ufuatiliaji (supportive supervision) katika Wilaya mbili (2)<br />
kwa kila mkoa, katika mikoa tisa ya <strong>Tanzania</strong> Bara kwa lengo la kufuatilia na<br />
kusimamia utoaji wa huduma za afya, ili kutoa ushauri na maelekezo ya kitaalam<br />
katika kuboresha huduma za afya hususani Dharura na Maafa<br />
• Kutoa mafunzo maalum ya jinsi ya kukabiliana na dharura na maafa kwa wajumbe<br />
40 wa Timu za Uendeshaji Huduma za Afya za Mikoa (RHMT), ili kuongeza ufanisi<br />
katika kusimamia utendaji wa kazi hiyo kwa watumishi katika hospitali zao<br />
• Kutoa mafunzo maalum ya jinsi ya kukabiliana na Dharura na Maafa kwa watumishi<br />
36 wa hospitali za hapa nchini (First responders) ili kuongeza ufanisi katika kazi za<br />
Dharura na Maafa katika hospitali za hapa nchini<br />
• Kuunda timu Maalum ya Kitaifa ya kukabiliana na Dharura na Maafa hapa nchini<br />
(National Rapid Response Team). Timu hii itapewa mafunzo maalum ya jinsi ya<br />
kukabiliana na Dharura na Maafa nchini, ili kuongeza ufanisi katika kazi zao za kila<br />
siku<br />
34
• Watumishi wawili wa kitengo cha Dharura na Maafa watapata mafunzo maalum ya<br />
muda mfupi nje au ndani ya nchi ya jinsi ya kukabiliana na Dharura na Maafa hapa<br />
nchini<br />
• Mtumishi mmoja wa kitengo cha Dharura na Maafa atapata mafunzo ya Shahada<br />
katika fani ya Uuguzi katika moja ya vyuo hapa nchini, ili kuongeza ufanisi katika<br />
kazi zake za kila siku katika kukabiliana na Dharura na Maafa hapa nchini<br />
• Kuendelea kufanya upembuzi yakinifu (Hazard Analysis and Vulnerability) ya jinsi<br />
ya kukabiliana na Dharura na Maafa nchini<br />
• Kuimarisha kitengo kwa kununua vitendea kazi pamoja na samani kwa ajili ya ofisi.<br />
Vifaa hivyo ni pamoja na kompyuta, meza n.k kwa lengo la kuongeza ufanisi wa kazi<br />
za kitengo cha Dharura na Maafa.<br />
2.7.2 Ukaguzi wa Huduma za Afya<br />
Mwaka 2004/2005, Wizara ilifanya kazi zifuatazo:-<br />
• Kupanga na kuzindua mwongozo wa mfumo wa kimataifa wa ubora wa huduma za<br />
afya<br />
• Kufanya mkutano na wadau kuhusu mwongozo wa kudhibiti na kuzuia maambukizo<br />
katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini<br />
• Kuandaa viwango na viashiria vya utoaji bora wa huduma<br />
• Kuandaa mwongozo wa kutathmini utendaji kazi kwa watumishi wa Afya<br />
• Kuandaa mwongozo kwa watumishi wa afya wa kujitathmini wao wenyewe kiutendaji<br />
kuhusiana na ubora wa huduma za afya wanazozitoa<br />
• Kuandaa mwongozo wa kutathmini utendaji kazi kwa watumishi wa Afya kuhusiana na<br />
ubora wa huduma za afya.<br />
Matarajio ya Ukaguzi wa Huduma za Afya mwaka 2005/2006<br />
Kitengo cha Ukaguzi wa utoaji wa huduma za Afya nchini kinategemea kutekeleza kazi<br />
zifuatazo, mwaka 2005/2006:<br />
• Kufanya usimamizi na ukaguzi katika Mikoa 8, Wilaya mbili kila mkoa<br />
• Kufundisha wataalam wa Taifa (National Trainers of Trainers) kuwawezesha<br />
kufundisha watumishi wengine katika kudhibiti maambukizo (Infection Prevention and<br />
Control IPC)<br />
• Kuendesha mafunzo juu ya udhibiti wa maambukizo (IPC), uboreshaji wa huduma za<br />
afya na mwongozo wa usimamizi na ukaguzi wa huduma za afya kwa Timu za<br />
Utendaji za Afya za Mikoa (Regional Health Management Teams) zote<br />
• Kuandaa na kuchapisha muongozo wa udhibiti wa maambukizo kwa watumishi wa<br />
Zahanati na Vituo vya Afya (Infection Prevention and Control for Health Centers and<br />
Dispensaries)<br />
• Kusambaza Mwongozo wa Kitaifa wa udhibiti wa maambukizo (National\Infection<br />
Prevention and Control Guidelines for Healthcare Services) na Mfumo wa Kitaifa wa<br />
Uboreshaji Huduma za Afya <strong>Tanzania</strong> (<strong>Tanzania</strong> Quality Improvement Framework).<br />
2.7.3 Huduma za Uuguzi na Ukunga<br />
Mwaka 2004/2005, Wizara ilitoa kipaumbele katika utoaji wa huduma za Uuguzi kwa<br />
wagonjwa walioathirika na Virusi vya UKIMWI. Hii ni pamoja na kutayarisha miongozo<br />
ya utoaji wa huduma za uuguzi kwa wagonjwa hao katika vituo vya kutolea huduma,<br />
kufanya tathmini ya kazi ya kutoa ushauri nasaha inayofanywa na wauguzi. Hii ni kwa<br />
35
kuzingatia kuwa, UKIMWI sasa ni tatizo kubwa mno katika vituo vyetu vya kutolea<br />
huduma bila kuwasahau watoa huduma wenyewe.<br />
Mafunzo ya uongozi wa wasimamizi wa huduma za Uuguzi na Ukunga yalitolewa kwa<br />
wasimamizi 16, ili kuwapa maarifa na stadi za usimamizi bora wa utowaji wa huduma<br />
katika vituo vya hospitali za mikoa na rufaa nchini.<br />
Matarajio ya Huduma za Uuguzi na Ukunga mwaka 2005/2006<br />
Mwaka wa 2005/2006, kitengo kinatarajia kutekeleza kazi zifuatazo;<br />
• Kuelimisha na kusambaza mwongozo wa utoaji wa huduma kwa watoa huduma<br />
kuhusu jinsi ya kujiepusha na kutoeneza maambukizi wakati wa kutoa huduma kwa<br />
walioathirika na UKIMWI nchini<br />
• Kuandaa mkakati kabambe wa utoaji huduma za uuguzi na ukunga wa miaka mitatu<br />
2005 - 2008, kwa kulingana na mkakati wa sera ya Wizara ya Afya ya kutoa huduna<br />
bora kwa kuzingatia MKUKUTA<br />
• Kufanya usimamizi na ushauri wa kitaaluma wa utoaji wa huduma za Uuguzi na<br />
Ukunga katika mikoa minane ya Mwanza, Pwani, Kilimanjaro, Shinyanga, Kagera,<br />
Dodoma, Arusha na Mbeya.<br />
• Kufuatilia kwa karibu watoa huduma hasa kwa kuzingatia malalamiko ya wananchi<br />
kuhusu lugha zisizofaa kwa kushirikiana na Baraza la Uuguzi na Ukunga<br />
• Kutoa mafunzo kwa maafisa wa Kitengo juu ya uendeshaji na usimamizi wa utoaji<br />
wa huduma za Uuguzi na Ukunga ili kuinua viwango vya ubora wa huduma<br />
zitolewazo nchini<br />
• Kuwawezasha kupata mafunzo maalum ya uendeshaji wa huduma za Uuguzi na<br />
Ukunga kwa maafisa wawili wa kitengo ndani na nje ya nchi, ili kuongeza ufanisi<br />
katika usimamiaji wa huduma za Uuguzi na Ukunga.<br />
2.8 Uhasibu na Fedha<br />
2.8.1 Ukusanyaji mapato kwa mwaka 2004/2005<br />
Wizara ilikuwa na lengo la kukusanya jumla ya Tsh. 496,504,000/= kutoka vyanzo<br />
mbalimbali vya mapato katika mwaka wa fedha wa 2004/05. Hadi kufikia tarehe 31 Machi,<br />
2005, Wizara ilikuwa imekusanya jumla ya Tsh. 609,344,885.11 ambazo zimetokana na<br />
makato ya kodi za nyumba za Serikali na Mashirika ya Umma, malipo ya ununuzi wa vitabu<br />
vya maombi ya Zabuni za Wizara na marejesho ya masurufu. Wizara inategemea kukusanya<br />
kiasi cha Tshs 34,101,356.68 kati ya tarehe 1 Aprili, 2005 hadi 30 Juni, 2005. Kiasi halisi<br />
kinachotegemewa kukusanywa kitakuwa kimevuka lengo la mapato yaliyokadiriwa. Hali hii<br />
imetokana na kiasi kikubwa cha marejesho ya masurufu. Aidha, mapato haya hayajumuishi<br />
fedha zinazotokana na makusanyo ya kuchangia gharama za huduma za afya. Fedha za<br />
uchangiaji hutumika kwenye hospitali zinakokusanywa ili kuboresha huduma zitolewazo kwa<br />
wananchi, kulingana na Sera ya Uchangiaji.<br />
Matarajio ya Ukusanyaji mapato mwaka 2005/2006<br />
Katika kipindi cha 2005/2006, Wizara ya Afya inatarajia kukusanya jumla ya Tshs<br />
598,005,000.00. Mapato haya yatatokana na kodi za nyumba za Serikali na Mashirika ya<br />
Umma zinazochangiwa na wafanyakazi, marejesho ya masurufu ya fedha za Serikali na<br />
malipo ya kununua makabrasha ya Zabuni za Wizara. Kwa kuzingatia utaratibu uliopo,<br />
36
mapato yanayotokana na makusanyo ya kuchangia gharama za huduma za afya<br />
hayajumuishwi katika makadirio haya.<br />
2.8.2 Matumizi ya fedha za Kawaida mwaka 2004/2005<br />
Mwaka wa fedha wa 2004/2005, Wizara ya Afya ilidhinishiwa jumla ya Tsh 195,800.00 kwa<br />
ajili yakugharamia utoaji wa huduma za afya. Kiasi cha Tsh 189.243,633,427.00 kati ya hizo<br />
zilitengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida ikijumuisha mishahara ya wafanyakazi wa<br />
Hospitali Teule (DDH), Hospitali ya Taifa Muhimbili, KCMC, Bugando na Taasisi zilizo<br />
chini ya Wizara. Kiasi kilichobaki cha Tsh. 6,642,499,373.00 kilitengwa kwa ajili ya<br />
mishahara ya watumishi wa Idara za Wizara ya Afya, Vyuuo vyote vinavyosimamiwa na<br />
Wizara na Hospitali za Kibong’oto, Mbeya Rufaa na Mirembe.<br />
Makadirio ya matumizi ya Kawaida katika mwaka 2005/2006<br />
Wizara ya Afya katika mwaka wa 2005/2006 inakadiria kutumia kiasi cha Tshs<br />
180,305,853,900.00 kwa ajili ya matumzi ya kawaida. Katika mwaka 2004/2005 Wizara<br />
ilitengewa jumla ya Tsh 104,465,379,200.00 kwa ajili ya matumzi ya kawaida. Hivyo kuna<br />
ongezeko la Tsh 75,840,474,700.00 ikilinganishwa na mwaka 2004/2005.<br />
Kati ya fedha hizo zilizotengwa kiasi cha Tsh 6,406,945,600.00 zitatumika kulipa mishahara<br />
ya watumishiwa Wizara ya Afya makao makuu, Hospitali za Mbeya Rufaa, Mirembe na<br />
Kibong’oto na Vyuo vyote vya mafunzo ya afya. Kiasi cha Tsh 173,898,908,300.00<br />
kilichosalia kimetengwa kwa ajili ya Matumzi mengineyo (OC) kwa ajili ya kazi za Idara za<br />
Wizara ya Afya na Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Afya. Kiasi hiki pia kinajumuisha<br />
mishahara ya Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Afya. Taasisi hizo ni pamoja na Taasisi ya<br />
Chakula na lishe (TFNC), Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Hospitali<br />
ya Taifa Muhimbili, Taasisi ya Mifupa (MOI), Taasisi ya Saratani – Ocean Road, Hositali<br />
Teule (District Designated Hospitals – DDH) na Hospitali za Mashirika ya kujitolea<br />
(Voluntary Agencies VA’s).<br />
2.8.3 Matumizi ya fedha za Miradi ya Maendeleo mwaka 2004/2005<br />
Jumla ya Tsh 66,416,700.00 zilitengwa kwa ajili ya utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo.<br />
Kati ya hizo Serikali ya <strong>Tanzania</strong> ilitenga jumla ya Tsh 3,552,448,200.00 na Tshs<br />
62,863,658,500.00 ni mchango wa Wahisani wanaosaidia Sekta ya Afya.<br />
Kiasi ambacho kilikuwa kimekwishatolewa na wahisani wa Mfuko wa Pamoja ni Tshs<br />
40,680,869,900.00 na fedha zilizo nje ya Mfuko wa Pamoja ni Tshs 4,697,565,032.25. Fedha<br />
zote zilizotolewa na wahisani zikijumuishwa pamoja zinafanya jumla ya Tsh<br />
48,930,883,132.25 ambayo ni sawa na asilimia 53.6 ya fedha zote zilizokisiwa kutolewa na<br />
Wahisani. Hadi tarehe 30 Aprili 2005, matumizi halisi kwa fedha zote za miradi ya<br />
maendeleo zikiwemo za Serikali pamoja na Wahisani ni Tsh 21,526,163,399.74.<br />
Makadirio ya Miradi ya Maendeleo mwaka 2005/2006<br />
37
Katika mwaka wa fedha wa 2005/2006 Wizara ya Afya inakadiria kutumia jumla ya Tshs<br />
90,862,748,400.00 kwa ajili ya utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo. Kati ya fedha hizo<br />
shilingi 5,000,000,000.00 ni kutoka Serekali ya <strong>Tanzania</strong> na kiasi cha shilingi<br />
85,862,748,400.00 ni kutoka Taasisi za Kimataifa zinazochangia Mfuko wa Pamoja wa Afya<br />
(Busket Fund) na wale walio nje ya mfuko.<br />
Fedha hizo zitatumika kutekeleza miradi ya maendeleo ifuatayo:<br />
• Kuendeleza ukarabati wa Hospitali ya Taifa Muhimbili na hospitali za Jiji la Dar es<br />
Salaam<br />
• Ukarabati wa wodi, maabara, chumba cha upasuaji na ujenzi wa hosteli ya madaktari<br />
walio katika mazoezi (Intern’s doctors) katika hospitali ya Rufaa Mbeya<br />
• Kuendeleza ukarabati wa wodi, nyumba za watumishi na jiko katika hospitali<br />
maalum ya Mirembe na Taasisi ya Isanga<br />
• Ukarabati wa wodi 6 za wagonjwa wa nje, nyumba za watumishi na wodi za<br />
wagonjwa wa Kifua Kikuu na ununuzi wa vifaa kwa ajili ya hospitali maalum ya<br />
Kifua Kikuu ya Kibongoto<br />
• Kuendeleza ujenzi wa wodi ya watoto katika hospitali ya Taifa Muhimbili<br />
• Kuendeleza michango ya Serekali (counterpart funds) kwa ajili ya kuendeleza<br />
ukarabati wa majengo ya Hospitali ya Taifa Muhimbili, ujenzi wa hospitali maalum<br />
hapa Dar es Salaam itakayojengwa kwa kushirikiana na Serekali ya <strong>Tanzania</strong> na<br />
TOKUSHUKAI na ujenzi wa hospitali ya Kanda ya Kusini, Mtwara<br />
• Kuendeleza ukamilishaji wa ujenzi wa maabara ya ubora (quality laboratory), Makao<br />
Makuu ya Wakala wa Mkemia Mkuu wa Serekali pamoja na ununuzi wa vifaa na<br />
kemikali kwa ajili ya maabara mpya ya Mwanza ambayo imekamilika hivi karibuni<br />
• Ukarabati wa vituo vya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu Amani, Gonja, Mwanza,<br />
Tukuyu na Dar es Salaam<br />
• Ukarabati wa jengo la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya litakalotumika kama ofisi<br />
• Kuendelea kukamilisha ukarabati wa vyuo vya afya 28<br />
• Kununua vifaa vya tiba kwa hospitali za Rufaa zote 6.<br />
38
3.0 RIPOTI ZA TAASISI NA MAMLAKA ZILIZO CHINI <strong>YA</strong> WIZARA <strong>YA</strong> AF<strong>YA</strong><br />
3.1 Taasisi ya Chakula na Lishe <strong>Tanzania</strong> (TFNC)<br />
Katika kipindi cha mwaka 2004/2005 Wizara ya Afya kupitia Taasisi yake ya Chakula na<br />
Lishe iliendelea kutoa ushauri wa kitaalam kwa Wilaya na kushirikiana na Taasisi na wadau<br />
mbali mbali katika kuboresha hali ya lishe ya jamii nchini.<br />
Katika juhudi za kudhibiti matatizo ya lishe, Taasisi iliendelea kuchukua hatua mbalimbali<br />
ikiwa ni pamoja na kuimarisha uwekaji wa madini joto kwenye chumvi katika Wilaya 25<br />
zenye wazalishaji chumvi wadogo kwa kuhamasisha viongozi wa Wilaya 285. Aidha, Taasisi<br />
ilitoa mafunzo kwa wakaguzi wa chumvi (maafisa afya na maafisa madini) wapatao 451 na<br />
kuunda timu za wakufunzi wa wazalishaji wa chumvi katika suala la uwekaji madini joto<br />
kwenye chumvi. Zoezi hilo lilihusisha Wilaya za Mtwara, Lindi, Kilwa, Rufiji, Mkuranga,<br />
Temeke, Kinondoni, Bagamoyo, Dodoma, Manyoni, Singida, Iramba, Kigoma, Njombe na<br />
Mbozi. Wilaya nyingine ni Tanga, Pangani, Muheza, Korogwe, Same, Mwanga, Meatu,<br />
Babati, Hanang na Karatu.<br />
Juhudi zilielekezwa katika Wilaya hizo kutokana na hali halisi kuwa sehemu kubwa ya<br />
chumvi inayozalishwa hapa nchini inatokana na wazalishaji wadogo katika maeneo hayo.<br />
Aidha, takwimu zinaonyesha kwamba kati ya hao wazalishaji wadogo ni asilimia 30 tu ndio<br />
wamekuwa wakiweka madini joto kwenye chumvi.<br />
Katika kuhakikisha kwamba chumvi yote inayozalishwa nchini inawekwa madini joto,<br />
Taasisi ya Chakula na Lishe sambamba na kutoa mafunzo na uhamasishaji ilisambaza vifaa<br />
mbalimbali vya kuwekea madini joto kwenye chumvi kwa wazalishaji. Vifaa hivyo ni pamoja<br />
na kilo 5,000 za madini joto na pampu 4,650 za kunyunyuzia madini joto kwenye chumvi na<br />
jumla ya vichupa 93,750 vya kemikali ya kupima uwepo wa madini joto kwenye chumvi<br />
(Iodine test solution). Taasisi iliendelea kuratibu utoaji wa matone ya Vitamini A kwa watoto<br />
wa umri kati ya miezi sita hadi miaka mitano na vidonge vya kutibu minyoo ya tumboni kwa<br />
watoto wa umri kati ya mwaka mmoja hadi miaka mitano katika mikoa yote <strong>Tanzania</strong> bara.<br />
Katika zoezi lililofanyika Desemba 2004, asilimia 93 ya watoto waliolengwa walipata matone<br />
ya Vitamini A na asilimia 90 walipata vidonge vya kutibu minyoo.<br />
Katika juhudi za kuendeleza lishe na afya ya mtoto, mkakati wa kitaifa wa kusimamia Lishe<br />
na Afya ya Mtoto chini ya umri wa miaka mitano umeandaliwa na kuzinduliwa. Aidha,<br />
mpango wa utekelezaji wa mkakati huu wa miaka mitano 2005 - 2009 umeandaliwa. Mkakati<br />
na Mpango wa Utekelezaji unaainisha vipengele muhimu kuhusu uimarishaji wa lishe ya<br />
mtoto na pia majukumu ya wadau kutoka sekta mbalimbali ikiwemo sekta binafsi. Mkakati<br />
huu utawezesha wadau kuchangia kikamilifu katika kuendeleza lishe na afya ya mtoto hasa<br />
wakati huu wa janga la UKIMWI.<br />
39
Taasisi pia iliandaa mwongozo wa kitaifa kuhusu lishe bora kwa wanaoishi na virusi vya<br />
UKIMWI. Jumla ya nakala 10,000 za mwongozo huo zilichapishwa na kusambazwa kwenye<br />
Wizara na taasisi husika, hospitali za rufaa, Mikoa na Wilaya, vyuo vya mafunzo na taasisi<br />
mbalimbali zinazoshughulika na tatizo la UKIMWI hapa nchini.<br />
Mpango wa Hospitali Rafiki wa Mama na Mtoto unaotekelezwa nchini toka mwaka 1992<br />
unalenga katika kuboresha hali ya afya na lishe ya watoto wachanga. Chini ya mpango huu<br />
hospitali zinatakiwa kutekeleza na kuboresha Huduma za Afya na Uzazi kwa wanawake<br />
wajawazito na waliojifungua.<br />
Katika kufuatilia Hospitali Rafiki wa Mama na Mtoto, hospitali 17 katika Wilaya za<br />
Shinyanga, Kasulu, Ndanda, Nyakahanga, Rubya, Biharamulo, Mugana, Magu na Meatu<br />
ziliweza kufanikiwa kuwa rafiki wa Mama na Mtoto kwa vigezo vya kimataifa. Hii inafanya<br />
<strong>Tanzania</strong> kuwa na hospitali 68 ambazo ni Rafiki wa Mama na Mtoto.<br />
Matarajio ya Taasisi ya Chakula na Lishe mwaka 2005/2006<br />
Katika kipindi cha mwaka 2005/2006, Taasisi itaendelea kuratibu shughuli za kitaifa za utoaji<br />
matone ya Vitamini A na vidonge vya kutibu minyoo kwa watoto walio na umri chini ya<br />
miaka mitano katika mikoa yote ya <strong>Tanzania</strong> bara. Wizara itaendelea kufuatilia na kutoa<br />
mafunzo na hamasa juu ya uwekaji wa madini joto kwenye chumvi ili kufikia lengo la<br />
asilimia 90 (au zaidi ya kaya zote nchini) linalopendekezwa na Shirika la Afya Duniani<br />
kwamba ziwe zinatumia chumvi yenye madini joto kutoka asilimia 84 ya hivi sasa.<br />
Taasisi pia itafanya utafiti kuhusu tatizo la upungufu wa damu kwa nchi nzima ili kuwa na<br />
takwimu sahihi za hali halisi ya tatizo hilo. Kupatikana kwa takwimu hizo kutasaidia katika<br />
kupanga mikakati na programu za kupunguza tatizo hili. Aidha, Taasisi itaandaa na<br />
kuchapisha vitabu zaidi kwa nia ya kutoa elimu kwa wananchi kuhusu lishe bora kwa wenye<br />
UKIMWI na kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu lishe bora ili kuepukana na<br />
magonjwa sugu yenye uhusiano na ulaji usiofaa kama vile kisukari, magonjwa ya mfumo wa<br />
damu na moyo, saratani na mengineyo.<br />
Ili kuzidi kuendeleza afya na lishe ya mtoto, Taasisi itaratibu mapitio ya Sheria Na. 10 ya<br />
mwaka 1978 inayosimamia uingizaji na uuzaji wa vyakula vya watoto wachanga, ili kuingiza<br />
vipengele vinavyohusiana na ulishaji wa mtoto na janga la UKIMWI. Sheria hii inadhibiti<br />
ubora wa vyakula vinavyoingizwa nchini toka nje na vile ambavyo vinazalishwa katika nchi<br />
yetu. Taasisi pia itaendelea kutoa ushauri wa kitaalam kwa Wilaya ili ziweze kupanga na<br />
kutekeleza programu na miradi inayolenga kuboresha lishe na afya za wananchi.<br />
3.2 Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali<br />
Katika kipindi cha mwka 2004/2005, Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali<br />
iliweza kufanya yafuatayo;<br />
• Kuendelea kutekeleza malengo yake ya kutoa huduma bora za kimaabara zinazohusu<br />
uchunguzi, ushauri wa kitaalam na utafiti katika nyanja za kemikali, vyakula, dawa,<br />
usalama wa mazingira na sayansi ya makosa ya jinai kwa wadau na wananchi kwa<br />
jumla<br />
• Uchunguzi jumla ya sampuli 3,934 na kutoa matokeo katika muda wa siku 14 kama<br />
ilivyoainishwa katika Mkataba wa Huduma kwa Mteja. Kati ya sampuli<br />
zilizochunguzwa, asilimia 82 zilifikia viwango vinavyokubalika kitaifa na kimataifa<br />
kwa matumizi ya binadamu na usalama wa mazingira. Mafanikio hayo yametokana na<br />
40
kununuliwa kwa mitambo ya kisasa na vifaa vya Maabara, wataalam kuongozewa ujuzi<br />
pamoja na kuzingatia maoni ya wateja<br />
• Uchunguzi wa sampuli 4,213 za dawa za kulevya (mihadharati) kutoka Idara, Asasi na<br />
waathirika ili kuainisha aina za dawa husika na matokeo ya uchunguzi na kukabidhiwa<br />
kwa mamlaka husika. Matokeo ya uchunguzi huo yamesaidia kuharakisha usikilizaji<br />
wa kesi na utoaji haki mahakamani na ushauri kwa Asasi hususan hospitali katika<br />
kusaidia kutoa tiba sahihi kwa waathirika<br />
• Kuendelea kutekeleza Sheria ya Usimamizi na Udhibiti wa Kemikali zitumikazo<br />
Viwandani na Majumbani “The Industrial and Consumer Chemicals (Management and<br />
Control) Act No. 3, 2003” ilioyoanza kutekelezwa Julai 2003, kwa lengo la kulinda<br />
afya za wananchi na mazingira<br />
• Kutoa elimu kwa umma kupitia vyombo vya habari, magazeti na vipeperushi kuhusu<br />
kemikali zilizopigwa marufuku duniani kutokana na athari za kiafya na mazingira.<br />
Sheria hii imesaidia kuzuia uwezekano wa nchi yetu kuwa jalala la kemikali hatari<br />
zinazoathiri afya, kuchafua vyanzo vya maji na mazingira<br />
• Imeshungulikia maombi 150 ya usajili wa kemikali kutoka kwa wadau <strong>Tanzania</strong> Bara<br />
na jumla ya vibali 365 vilitolewa kwa ajili ya uagizaji wa kemikali kutoka nje ya nchi<br />
• Kununua, kufunga na kuzindua mtambo wa DNA ambao unachunguza vinasaba (genes<br />
vya urithi na ukoo) katika maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali. Matokeo ya<br />
uchunguzi wa sampuli kwa kutumia mtambo huu umesaidia vyombo vya dola na<br />
mamlaka nyingine mfano, katika masuala ya kusingiziwa, kuiba au kubadilishana<br />
watoto hospitalini na hivyo kuondoa kero za wananchi. Pia husaidia kutambua vinasaba<br />
vya magonjwa ya kurithi na tafiti mbalimbali zinazohusiana na vimelea vya magonjwa,<br />
mimea na ugunduzi wa dawa za tiba mbadala. Aidha kumbukumbu za wahalifu<br />
zitahifadhiwa kwa kutumia mtambo huo na zitasaidia kutambua wanaofanya makosa<br />
mara kwa mara kwa kutumia majina bandia<br />
• Aidha, Maabara moja ya Kanda ya Ziwa Jijini Mwanza ilianzishwa ambayo imesaidia<br />
kuondoa kero ya kusafirisha sampuli na gharama kubwa inayohitajika kufika Dar es<br />
Salaam kufuatilia matokeo ya uchunguzi<br />
• Kupeleka wafanyakazi 17 kwa mafunzo ya muda mfupi na mrefu katika fani<br />
mablimbali ndani na nje ya nchi kwa kuzingatia usawa wa jinsia na vipaumbele<br />
• Kuzindua tovuti ya Wakala wa Mkemia Mkuu wa Serikali (www.gcla.go.tz) katika<br />
kuimarisha mawasiliano kati ya Wakala, wadau na jamii kwa ujumla ili kwenda<br />
sambamba na utandawazi.<br />
Matarajio ya Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serekali kwa mwaka<br />
2005/2006.<br />
Wakala inatarajia kufanya yafuatayo:-<br />
• Kutumia kwa makini rasilimali watu, fedha na vifaa katika kutekeleza Mkakati wa<br />
Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini <strong>Tanzania</strong><br />
• Kuchunguza jumla ya sampuli 4,631 ambapo asilimia kubwa itatokana na usajili<br />
wa kemikali na kuanzishwa kwa Maabara ya Kanda ya Ziwa Jijini Mwanza<br />
• Kupata wadau wengi wanaotarajia kujisajili kutokana na kuelimishwa kuhusu<br />
umuhimu wa sheria hii<br />
• Kutangaza kwa kutumia vyombo vya habari na mawasiliano umuhimu wa mtambo<br />
wa vinasaba katika kufanya tafifi mbalimbali kwa nchi za Afrika zilizo Kusini mwa<br />
41
Jangwa la Sahara na hatimaye kuongeza mapato ya Wakala kutokana na huduma<br />
zitakazotolewa<br />
• Kukamilisha uchambuzi yakinifu kwa ajili ya ujenzi wa Maabara ya Kanda ya<br />
Kaskazini mjini Arusha<br />
• Kuweka kipaumbele katika kuwasomesha wafanyakazi 19 katika maeneo<br />
yatakayosaidia kukuza uchumi na kupunguza umasikini wa kipato<br />
• Kuendelea kujitangaza kupitia tovuti yake ili huduma zake zifahamike kote<br />
ulimwenguni.<br />
3.3 Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA)<br />
Mamlaka hii ilianzishwa kwa sheria ya Chakula, Dawa na Vipodozi namba 1 ya mwaka 2003<br />
ili kusimamia udhibiti wa ubora, usalama na ufanisi wa vyakula, dawa, dawa za mitishamba,<br />
vipodozi na vifaa tiba.<br />
Katika kipindi cha 2004/2005, Mamlaka imeandaa rasimu ya kanuni/sheria ndogo zifuatazo:-<br />
• The <strong>Tanzania</strong> Food, Drugs and Cosmetics (Registration of pre-packed food)<br />
Regulations, 2004<br />
• The <strong>Tanzania</strong> Food, Drugs and Cosmetics (Cosmetics) Regulations, 2004<br />
• The <strong>Tanzania</strong> Food, Drugs and Cosmetics (Control of promotion of food)<br />
Regulations, 2004 na<br />
• The <strong>Tanzania</strong> Food, Drugs, and Cosmetics (Control of drug promotion) Regulation,<br />
2004.<br />
Aidha, mamlaka imeweza kuandaa miongozo ifuatayo:-<br />
• Mwongozo wa namna ya kushughulikia maombi ya usajili wa dawa<br />
• Mwongozo wa kutathmini maombi ya kutangaza bidhaa zinazodhibitiwa chini ya<br />
sheria ya Chakula, Dawa na Vipodozi ya mwaka 2003<br />
• Mwongozo wa kusajili vyakula nyongeza (food supplements).<br />
Jumla ya dawa 279 za binadamu, 12 za mifugo na 11 za vyakula zilisajiliwa. Mamlaka<br />
ilifanya kazi ya kutafuta taarifa za vyakula, vipodozi na dawa za miti shamba zinazozunguka<br />
sokoni bila kuthaminiwa na kusajiliwa kwa lengo la kutambua bidhaa hizo ili watengenezaji<br />
au waagizaji wake wahamasishwe kuleta maombi ya usajili. Jumla ya vyakula 5,066, vyakula<br />
nyongeza 126 na vipodozi 921 vilitolewa taarifa katika zoezi hilo. Vile vile, jumla ya maombi<br />
17 ya kusajili dawa za mitishamba yalipokelewa na yanaendelea kufanyiwa tathmini.<br />
Katika kuhakikisha kwamba bidhaa zilizo katika soko la <strong>Tanzania</strong> ni bora na salama,<br />
Mamlaka imefanya uchunguzi wa kimaabara kwa jumla ya sampuli 767, sampuli 608<br />
zilikidhi viwango na 159 hazikukidhi viwango. Bidhaa ambazo hazikukidhi viwango<br />
ziliondolewa sokoni na kwa zile zilizokuwa zinaombewa usajili, cheti cha kusajili<br />
hakikutolewa na hivyo kutoruhusiwa kuingizwa katika soko la <strong>Tanzania</strong>. Jumla ya aina 168<br />
ya vipodozi vyenye viambato vyenye sumu vilipigwa marufuku.<br />
Mamlaka imefanya ukaguzi katika jumla ya maduka 630 ya dawa, 70 ya vipodozi na maduka<br />
39 ya vyakula. Pia viwanda 183 vya ndani vya chakula na 72 (66 vya nje, na 6 vya ndani)<br />
vya dawa vilikaguliwa, na jumla ya maombi 3474 ya vibali vya kuingiza bidhaa nchini<br />
yalipokelewa. Vibali 1062 vya kuingiza vyakula kiasi cha tani 841,852.848 na vibali 2055<br />
vya kuingiza dawa vilitolewa.<br />
42
Mamlaka imefungua Ofisi za Kanda katika mikoa ya Mwanza na Arusha ili kusogeza<br />
huduma karibu na wananchi na mafunzo kuhusu sheria mpya katika Kanda za Kusini na<br />
Kaskazini yaliyofanyika kwa wadau 515.<br />
Katika kukabiliana na tatizo la ukiukwaji mkubwa wa sheria unaofanywa katika Maduka ya<br />
Dawa Baridi Mamlaka imeanzisha maduka 41 ya Dawa Muhimu (Accredited, Drug<br />
Dispensing Outlets – ADDO) mkoani Ruvuma katika vijiji na miji midogo ikiwa ni nyongeza<br />
kwa maduka 110 yaliyokwisha funguliwa tangu mpango uanzishwe mnamo mwezi Agosti<br />
2003.<br />
Tathmini ya mpango wa ADDO imefanyika na kuonyesha mafanikio makubwa katika kufikia<br />
malengo ya awali kuhusu mpango huo.<br />
Mwaka 2004/2005, kati ya matukio 42 ya madhara yaliyoshukiwa kutokana na matumizi ya<br />
dawa yametolewa taarifa kwa usahihi.<br />
Katika kushiriki vita dhidi ya UKIMWI Mamlaka imeendelea kuhakikisha kuwa dawa za<br />
kupunguza makali ya UKIMWI, zilizoingia nchini ni bora, salama na zina ufanisi uliofikia<br />
viwango vianvyotambulika.<br />
Katika kuelimisha wadau na kuboresha upashanaji habari, Mamlaka ilizindua tovuti yake<br />
mwaka 2004.<br />
Matarajio ya Mamlaka ya Chakula na Dawa mwaka 2005/2006<br />
Mamlaka ya Chakula na Dawa inatarajia kutekeleza yafuatayo:-<br />
• Kuendelea kusimamia ubora, usalama na ufanisi wa chakula, dawa, vipodozi, vifaa<br />
tiba n.k kwa kuimarisha mfumo wa usajili na ukaguzi ikiwa ni pamoja na ukaguzi wa<br />
viwanda vya nje na ndani, vituo vya mipakani na maeneo ya kufanyia biashara ya<br />
bidhaa hizo<br />
• Kuimarisha maabara kuu na zile ndogo zinazohamishika zilizopo vituo vya mipakani<br />
na mkoani ili ziwe na uwezo wa kupima vipimo mbali mbali kwa kuzingatia viwango<br />
vinvayokubalika vya bidhaa zinazosimamiwa na Mamlaka kwa kutumia zana za<br />
kisasa<br />
• Kuandaa miongozo na sheria ndogo ili kurahisisha utekelezaji wa Sheria Kuu, na<br />
kuboresha uelewa wa wadau<br />
• Kuendelea kutoa mafunzo kwa watumishi ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi zaidi<br />
ikiwa ni pamoja na kuimarisha na kutoa vitendea kazi kwa kulingana na teknolojia<br />
mpya<br />
• Mamlaka itaendelea kutoa elimu kwa wadau na wananchi wote kupitia vyombo vya<br />
habari na kupitia tovuti yake pamoja na kuendelea kutoa mafunzo mbalimbali<br />
• Ofisi za Kanda zitaendelea kufunguliwa kwa kadri bajeti itakavyoruhusu.<br />
3.4 Taasisi ya Utafiti wa Magojwa ya Binadamu (NIMR)<br />
Sheria ya Namba 23 ya mwaka 1979 inaitaka Taasisi kushughulikia masuala ya utafiti wa<br />
magonjwa ya binadamu. Mwaka 2004/2005, Taasisi ilishughulikia usimamizi, uratibu,<br />
udhibiti, uenezi, utangazaji wa matokeo na ukuzaji wa utafiti nchini. Magonjwa<br />
yaliyofanyiwa utafiti ni Malaria, Matende na Mabusha, Usubi, Kichocho, Minyoo ya Tumbo,<br />
Kuhara, Magonjwa ya Zinaa, Malale, Kifua Kikuu na UKIMWI.<br />
43
Utafiti wa Malaria<br />
Katika kipindi cha 2004/2005 tafiti mbalimbali za Malaria zimetoa matokeo ambayo<br />
yanaonyesha kuwa usugu wa vimelea vya Malaria kwa dawa ya SP unakua na umefikia<br />
asilimia kumi na tano (15%). Hatua hii ya usugu iliyofikiwa inahitaji mabadiliko ya tiba dhidi<br />
ya Malaria itakayoweka viwango vipya vya dawa za kutibu Malaria na kuweka bayana<br />
mabadiliko ya sera ya tiba ya Malaria. Kiutafiti pendekezo linalotolewa kukabiliana na usugu<br />
huu ni matumizi ya dawa mchanganyiko (combination therapy).<br />
Taasisi inafuatilia kuona kama kuna uwezekano wa mbu kuwa na usugu kwa madawa<br />
yanayotumika katika vyandarua hapa nchini. Ufuatiliaji huo umefanyika katika wilaya za<br />
Muheza, Tanga, Korogwe, Lushoto, Babati, Arumeru, Magu, Tabora, Kyela, Moshi, Ifakara,<br />
Kinondoni na Pangani.<br />
Ugonjwa wa Usubi<br />
Uchunguzi juu ya nguvu za sumu ya kuulia mazalia ya wadudu wanaosababisha Usubi<br />
ulifanyika katika Wilaya za Rungwe na Kyela. Matokeo yalionyesha mafanikio mazuri kwa<br />
kuua wadudu hao kama ilivyotarajiwa. Mbinu hii itatumika kuongeza kasi ya Mpango wa<br />
Taifa wa Kudhibiti Usubi.<br />
Utafiti wa Dawa Asilia<br />
Taasisi imefanya utafiti ili kutathmini kiwango cha dawa kinachopatikana katika mmea wa<br />
Artemisia Annua na pia kufanya utafiti katika ngazi ya kimaabara ya namna ya kutengeneza<br />
dawa itokanayo na mmea huo. Kutokana na utafiti huu, Taasisi imefanikiwa kupata mtiririko<br />
wa namna ya kutengeneza “Artemisinin” na baadaye kuibadilisha “Artemisinin” kuwa<br />
“Dihydro-artemisinin”, dawa inayofaa kwa kutibu Malaria. Aidha, kwa kushirikiana na kituo<br />
cha Munufu, Taasisi imeifanyia utafiti wa awali dawa ya Muhanse itumiwayo na wagonjwa<br />
wa UKIMWI na kuiona haina madhara ya kuhatarisha maisha ya mtumiaji pamoja na<br />
kwamba utafiti zaidi unahitajika.<br />
Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Matende<br />
Zoezi la “Mapping” kuangalia ukubwa wa tatizo la Matende limeonyesha kuwa <strong>Tanzania</strong> ina<br />
watu karibu milioni 30 ambao wapo katika hatari ya kupata ugonjwa wa Matende na<br />
Mabusha. Kati ya hao watu asilimia sita (6.6%) yaani milioni mbili tayari wameathirika na<br />
ugonjwa huu. Kimsingi asilimia 90% ya Wa-<strong>Tanzania</strong> wapo katika hatari ya kupata<br />
maambukizi ya ugonjwa wa Matende. Tathmini pia imegundua kwamba watu wenye<br />
vimelea vya ugonjwa wa Matende wapo katika Wilaya nchi isipokuwa Wilaya za Babati na<br />
Chunya<br />
Katika jitihada za kupambana na tatizo la Matende na Mabusha mwaka 2000 watu 38,000<br />
waliopewa dawa katika kisiwa cha Mafia na mwaka 2001 watu 700,000 katika mkoa wa<br />
Pwani. Katika mwaka 2002 idadi ya Watanzania waliopewa dawa ilifikia milioni mbili laki<br />
nne baada ya kuongezeka mkoa wa Mtwara. Mwaka 2003 kumekuwapo na ongezeko la watu<br />
wapatao milioni mbili na laki nne waliopatiwa dawa na kuifanya idadi ya Wa-<strong>Tanzania</strong><br />
waliopata tiba hiyo kuwa milioni nne na laki nne. Mwaka 2004 kulikuwa na ongezeko la<br />
watu laki tisa katika mkoa wa Tanga na hivyo kufanya watu walionufaika na mradi huu kuwa<br />
milioni tano. Mpango ulianza mwaka 2000 na umehusisha Wilaya 24.<br />
44
Upasuaji wa Mabusha au mishipa ya kushuka unaendelea katika mkoa wa Pwani hususan<br />
katika hospitali ya Wilaya ya Mafia na hospitali ya Wilaya ya Kibaha. Idadi iliyofikiwa ya<br />
waliopasuliwa katika Mkoa wa Pwani ni 2,000. Aidha, Mpango ulishirikiana na Mpango wa<br />
kutokomeza Usubi katika zoezi la usambazaji na unyweshaji wa dawa ya “Ivemectin” katika<br />
Wilaya za Lushoto, Korogwe na Muheza. Hatua hii iliongeza ufanisi mkubwa kwani asilimia<br />
kubwa ya watu walikunywa dawa na hivyo kufanya mipango yote miwili kufanikiwa.<br />
Kituo cha Kuimarisha Mikakati Thabiti ya Kudhibiti Malaria (CEEMI)<br />
Ujenzi wa jengo la Kituo cha Kuimarisha Mikakati Thabiti ya Kudhibiti Malaria (CEEMI)<br />
ulikamilika na jengo kufunguliwa rasmi na Mhe. Naibu Waziri wa Afya Dk. Hussein Mwinyi<br />
(MB) Septemba 16, 2004. Jengo hili linatumika kwa ushirika na Mpango wa Taifa wa<br />
kuthibiti Malaria. Ushirika huu umerahisisha kujenga mahusiano ya karibu na kuleta ufanisi<br />
katika kupiga vita dhidi ya Malaria nchini.<br />
Matarajio ya Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu mwaka 2005/2006<br />
Utafiti wa Malaria<br />
Taasisi inatarajia kufanya utafiti wa dawa mchanganyiko dhidi ya Malaria ili kuweza kutoa<br />
ushauri sahihi juu ya mchanganyiko huo wa dawa utakaoweza kukidhi haja na kupatikana<br />
kwa bei nafuu kwa jamii nzima ya Wa-tanzania. Aidha, Taasisi inatarajia kufanya majaribio<br />
ya madawa yatokanayo na miti shamba yanayoweza kuua au kufukuza mbu wa aina<br />
mbalimbali. Miti kadhaa imejaribiwa na ipo inayotia matumaini.<br />
Ugonjwa wa Usubi<br />
Utafiti utaendelea kwa lengo la kudhibiti usubi kwa njia ya kuua wadudu waambukizaji na<br />
kutathmini matokeo ya kazi hiyo katika kupunguza maambukizi ya Usubi. Pia, utafiti wa<br />
kupima kiwango cha Usubi katika jamii inayoishi kando kando ya mito inayonyunyiziwa<br />
dawa utafanyika.<br />
Utafiti wa Dawa Asilia<br />
Mwaka 2005/2006, Taasisi itafanya utafiti wa dawa za Malaria, viuatilifu kwa mbu na<br />
viluwiluwi wa mbu. Aidha, dawa nyingine zinazotumiwa na wagonjwa wa UKIMWI<br />
zitaendelea kufanyiwa utafiti kadiri nyenzo zitakavyoruhusu.<br />
Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Matende<br />
Inatarajiwa kuwa mpango huu utawafikia walengwa 2,800,000 katika Manispaa tatu za mkoa<br />
wa Dar-es-Salaam. Mikakati iliyowekwa ni pamoja na kuunda kamati mbalimbali za<br />
uhamasishaji (mabenki, wanahabari, asasi zisizo za kiserikali na Wizara mbalimbali)<br />
zitakazosaidia katika uhamasishaji wa zoezi la kunywa dawa za kinga dhidi ya Matende na<br />
Mabusha na kuwapatia wanafunzi wa shule vipeperushi vyenye kubeba ujumbe muhimu ili<br />
wavipeleke majumbani mwao.<br />
3.5 Matatizo na Changamoto<br />
45
Pamoja na mafanikio mengi yaliyopatikana bado kuna matatizo yanayoikabili Wizara.<br />
Matatizo hayo ni pamoja na:-<br />
• Uhaba wa wataalam wa Afya katika ngazi zote<br />
• Kuongezeka kwa uzito wa kazi katika hosptiali zote kutokana na ongezeko la<br />
wagonjwa wa UKIMWI<br />
• Kuibuka kwa magonjwa ya kuambukiza na yasiyo ya kuambukiza<br />
• Kupanda kwa gharama za ukomboaji, utunzaji na usambazaji wa vifaa na dawa kutoka<br />
MSD hadi mikoani na Wilayani<br />
• Uchakavu wa majengo ya kutolea huduma za Afya nchini (majengo ya hosptiali na<br />
vyuo vya mafunzo ya afya)<br />
• Kuendelea kwa maambukizi ya UKIMWI<br />
• Vifo vya akinamama vianvyotokana na uzazi na vifo vya watoto wachanga bado ni<br />
vingi<br />
• Uhaba wa vifaa muhimu vya hospitali na dawa<br />
• Upungufu wa rasilimali za kutosheleza mahitaji muhimu ya kisekta unaotokana na<br />
msukumo wa Kitaifa na Kimataifa kwa mfano fedha kwa ajili ya UKIMWI, Kifua<br />
Kikuu na Malaria.<br />
3.6 Maeneo yaliyopewa kipaumbele mwaka 2005/2006<br />
Malengo ya Wizara yameelekezwa katika maeneo muhimu yaliyotajwa katika<br />
Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini <strong>Tanzania</strong> (MKUKUTA) na<br />
yale yaliyopo katika Malengo ya Milenia. Maeneo yaliyopewa kipaumbele katika<br />
bajeti ya matumzi ya kawaida na ya maendeleo katika bajeti ya 2005/2006 ni haya<br />
yafuatayo:-<br />
• Kuhakikisha kuwa wafanyakazi wote walio chini ya Wizara ya afya wanalipwa<br />
mishahara na stahili zao<br />
• Kuimarisha huduma za afya zitolewazo na hospitali za Rufaa, Mikoa, Wilaya,<br />
Vituo vya Afya na Zahanati na kuhakikisha upatikanaji wa dawa muhimu<br />
pamoja na vifaa vya kutolea huduma<br />
• Kupunguza vifo vya watoto wachanga na vifo vya akinamama wajawazito<br />
• Kuimarisha huduma za chanjo, lishe na huduma za mama na mtoto na kudhibiti<br />
Malaria, Kifua Kikuu na Ukoma<br />
• Kutoa huduma kwa akinamama na kinababa baada ya umri wa uzazi (post<br />
Reproductive Age Services for Women and Men)<br />
• Kutoa huduma kwa akinamama wanaoathirika kutokana na matatizo<br />
yanayotokana na uzazi (Vesicle Vaginal Fistula – VVF)<br />
• Kupambana na jana la ugonwja wa UKIMWI na hasa katika kuboresha huduma<br />
za kinga ili kupunguza maambukizi pamoja na ununuzi wa dawa za kupugnuza<br />
makali ya UKIMWI<br />
• Kupambana na ugonjwa wa Ngirimaji, Matende na Usubi<br />
• Kuendeleza na kuimarisha mabadiliko katika Sekta ya Afya ikiwa ni pamoja na<br />
kufanya mapitio eneo la msamaha katika uchangiaji wa huduma za afya<br />
• Kuzipatia hospitali Teule (DDH) na Mashirika ya Kujitolea (VAs) rasilimali ili<br />
kuongeza uwezo wa kutoa huduma kwa wananchi katika sehemu zisizo na<br />
Vituo vya Afya vya umma<br />
46
• Kuimarisha huduma za afya za Halmashauri za Wilaya katika kuendesha<br />
huduma za afya kwa kutoa usafiri kwa ajili ya usimamizi, ufuatiliaji na<br />
usambazaji wa dawa na vifaa tiba<br />
• Kuongeza wafanyakazi wenye ujuzi katika taaluma mbalimbali na kutoa<br />
mafunzo ya kitaalam ya watarajali (pre-service), wataalam wa afya na ya<br />
kujiendeleza katika kada zote za afya<br />
• Kuinua ubora wa afya ya mazingira<br />
• Kuendeleza utafiti wa magonjwa ya binafamu<br />
• Kutoa mchango wa Serikali katika miradi yaote inayopewa fedha na wahisani<br />
mbalimbali<br />
• Kukamilisha ujenzi na ukarbati unaoendelea wa majengo ya hospitali na ya<br />
vyuo vya kutolea mafunzo ya afya vilivyo chini ya Wizara ya Afya<br />
• Kuendelea na ununuzi wa vifaa muhimu vya uchunguzi kwa hospitali za rufaa<br />
na maalum<br />
• Kufanya uchunguzi wa vyakula, dawa, kemikali na vipodozi, kutoa ushauri wa<br />
kitaalam na kutambua vyanzo vya vifo kwa kufanya uchunguzi wa kisayansi<br />
(forensic science)<br />
• Kusimamia na kudhibiti kemikali za viwandani na majumbani utakaotekelezwa<br />
na Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali<br />
• Ununuzi wa magari ya vyuo ambavyo havina magari kabisa<br />
• Ujenzi wa hosteli ya madaktari wanafunzi hspitali ya Rufaa Mbeya, Ukarabati<br />
wa wodi za wagonjwa hospitali ya Mirembe na ujenzi wa majengo ya hospitali<br />
ya Kibong’oto.<br />
47
4.0 RIPOTI <strong>YA</strong> HUDUMA ZA AF<strong>YA</strong> MIKOA<br />
4.1 Utangulizi<br />
Taarifa za huduma za afya nchini zinajumuisha zile zinazotoka Mikoani na Hospitali za<br />
Rufaa/Maalum ambazo zimekuwa zikitolewa katika vikao vya Waganga Wakuu wa Mikoa na<br />
Wakurugenzi wa Hospitali za Rufaa/Maalum. Lengo la ripoti hizi ni kutoa/kuonyesha hali<br />
halisi katika utoaji wa huduma ya afya katika sehemu hizo. Taarifa hizi zinaonyesha hali<br />
ilivyo katika maeneo ya watumishi, huduma, na mapato zikiainisha mafanikio, matatizo,<br />
mikakati ya kuendeleza mafanikio na kutatua mataizo yanayojitokeza.<br />
Kwa miaka kadhaa, watendaji katika ngazi ya Mikoa na Hospitali za Rufaa walikusanya<br />
takwimu mbalimbali kila mwaka. Hata hivyo ukusanyaji wa takwimu hizi haukufuata mfumo<br />
mmoja na hivyo ilikuwa vigumu kufanya majumuisho ya kitaifa na kufanya mlinganisho.<br />
Hata hivyo watendaji wachache wameendelea kutuma ripoti ambazo hazifanani kimfumo.<br />
Ili kuwa na uwiano na uelewa wa pamoja katika kutoa huduma ya afya kwa kuzingatia<br />
Mabadiliko katika Sekta ya Afya, Idara ya Tiba ilipewa jukumu la kuratibu uandaaji wa<br />
mwongozo utakaotumika kuandaa ripoti. Mwongozo wa mfumo huu umezingatia takwimu<br />
muhimu zinazorahisisha ufuatiliaji wa utendaji kitaifa na mfumo wa uwasilishaji wa takwimu<br />
hizo bila kuathiri ukamilifu na ubora na takwimu hizo.<br />
4.2 Mchanganuo wa Idadi ya watu katika Mikoa<br />
<strong>Tanzania</strong> bara ina idadi ya watu wapatao 34,718,009 kati ya hao akina mama wenye umri wa<br />
miaka 15 - 49 ni 34,718,009 (20%), watoto wa umri
Pwani 928325 216272 28206 709247<br />
Rukwa 1235046 245650 49739 25650<br />
Ruvuma 1145467 481340 49495 481340<br />
Singida 1170076 234017 46803 234017<br />
Shinyanga 2975594 580469 116638 541488<br />
Tabora 1479583 373915 74783 373916<br />
Tanga 1705214 306930 68209 358094<br />
Jumla Kitaifa 34,718,009 6,927,702 1,621,461 6,645,101<br />
4.3 Mchanganuo wa hali ya Vifo vya Watoto na Akinamama wajawazito katika Mikoa<br />
Kasi ya vifo vya watoto umri wa chini ya mwaka mmoja kati ya vizazi hai 1,000 ilikuwa ya<br />
juu kwa mikoa ya Tanga (255), Pwani (153), Mtwara (126) na Kagera (106). (Mchoro na. 1).<br />
Mchoro 1: Kasi ya Vifo Vya Watoto Umri Chini ya Mwaka 1<br />
Kasi ya vifo kati ya watoto 100<br />
300.0<br />
250.0<br />
200.0<br />
150.0<br />
100.0<br />
50.0<br />
0.0<br />
Tanga<br />
255<br />
153<br />
126<br />
106<br />
90<br />
Pwani<br />
Mtwara<br />
Kagera<br />
Morogoro<br />
90<br />
Shinyanga<br />
74<br />
Dar es Salaam<br />
73<br />
72<br />
60<br />
Iringa<br />
Lindi<br />
Mbeya<br />
Dodoma 56<br />
40<br />
Kilimanjaro<br />
37<br />
Mwanza<br />
36<br />
Arusha<br />
36<br />
Mara<br />
16<br />
Ruvuma<br />
8<br />
Manyara<br />
78<br />
Jumla Kitaifa, 2004<br />
Mikoa<br />
Kuhusu kasi ya vifo vya watoto miaka 5+, kati ya vizazi hai 1000 mikoa iliyoongoza ni<br />
Rukwa (648), Tanga (487), Pwani (396), Mtwara (212), Kagera (167) na Morogoro (140).<br />
(Mchoro na. 2).<br />
49
700.0<br />
648<br />
Mchoro 2: Kasi ya Vifo Vya Watoto Umri wa Miaka 5+<br />
Kasi ya vifo kati ya watoto 100<br />
600.0<br />
500.0<br />
400.0<br />
300.0<br />
200.0<br />
100.0<br />
487<br />
396<br />
212<br />
167<br />
142<br />
140<br />
100<br />
79<br />
70<br />
51<br />
43<br />
41<br />
41<br />
29<br />
27<br />
27<br />
21<br />
14<br />
6<br />
137<br />
0.0<br />
Rukwa<br />
Tanga<br />
Pwani<br />
Mtwara<br />
Kagera<br />
Ruvuma<br />
Morogoro<br />
Dar es Salaam<br />
Mbeya<br />
Dodoma<br />
Mwanza<br />
Tabora<br />
Iringa<br />
Lindi<br />
Kilimanjaro<br />
Arusha<br />
Manyara<br />
Shinyanga<br />
Kigoma<br />
Mara<br />
Jumla Kitaifa, 2004<br />
Mikoa<br />
Kuhusu vifo vya akinamama kwa sababu ya uzazi kasi kubwa ilikuwa kwa mikoa ya<br />
Morogoro (387), Manyara (328), Lindi (326), Kagera (266), Mbeya (265) na Tabora (261).<br />
(Mchoro na.3).<br />
400<br />
350<br />
387<br />
Mchoro 3: Kasi ya Vifo Vya Mama Wajawazito Katika Kila Mkoa<br />
328<br />
326<br />
Kasi ya vifo<br />
300<br />
250<br />
200<br />
150<br />
266<br />
265<br />
261<br />
257<br />
252<br />
221<br />
205<br />
189<br />
176<br />
166<br />
163<br />
156<br />
114<br />
113<br />
281<br />
253<br />
280<br />
200<br />
100<br />
67<br />
53<br />
50<br />
35<br />
0<br />
Morogoro<br />
Manyara<br />
Lindi<br />
Kagera<br />
Mbeya<br />
Tabora<br />
Mwanza<br />
Shinyanga<br />
Iringa<br />
Dodoma<br />
Mtwara<br />
Tanga<br />
Arusha<br />
Mara<br />
Ruvuma<br />
Kigoma<br />
Kilimanjaro<br />
Rukwa<br />
Pwani<br />
Dar es Salaam<br />
Jumla Kitaifa, 2001<br />
Jumla Kitaifa, 2002<br />
Jumla Kitaifa, 2003<br />
Jumla Kitaifa, 2004<br />
Mikoa<br />
4.4 Mchanganuo wa Maeneo ya Kiutawala katika Mikoa<br />
Kiutawala <strong>Tanzania</strong> Bara kuna Tarafa 550, Vijiji 10,478, na Kaya 5,598,655. (Jedwali na 2).<br />
Jedwali na 2: Mchanganuo wa Maeneo ya Kiutawala katika Mikoa<br />
Mikoa Idadi ya Vijiji Idadi ya Kaya Idadi ya Tarafa<br />
Arusha 315 184443 22<br />
Dar es Salaam 0 623939 10<br />
Dodoma 496 382914 26<br />
Iringa 720 357397 33<br />
Kagera 556 393808 25<br />
Kilimanjaro 492 249021 21<br />
Kigoma 238 210263 19<br />
50
Lindi 453 190761 28<br />
Manyara 300 199860 52<br />
Mara 444 259699 20<br />
Mbeya 963 483387 27<br />
Morogoro 817 141 30<br />
Mtwara 232 170 35<br />
Mwanza 715 368561 33<br />
Pwani 417 81 25<br />
Rukwa 436 222868 21<br />
Ruvuma 514 238659 22<br />
Singida 366 198589 21<br />
Shinyanga 868 369598 27<br />
Tabora 489 307503 20<br />
Tanga 647 356993 33<br />
Jumla Kitaifa 10478 55986655 550<br />
4.5a: Uwiano wa Wataalam wa Afya na Idadi ya Watu<br />
Mikoa yenye uwiano mzuri wa Madaktari na idadi ya watu ni Arusha (1:38,545), Pwani (1:<br />
42,196), Dar es Salaam (1:50,322) na Mara (1:58,120). Mikoa inayoongoza kwa kutokuwa na<br />
uwiano mzuri ni Rukwa na Mwanza (1:308,761 na 1:307,770). (Mchoro na. 4).<br />
Mchoro 4: Uwiano wa Daktari Mmoja na Idadi ya Watu Katika Kila Mkoa<br />
Mkoa<br />
Rukwa<br />
Mwanza<br />
Shinyanga<br />
Iringa<br />
Dodoma<br />
Mbeya<br />
Manyara<br />
Tabora<br />
Morogoro<br />
Lindi<br />
Kilimanjaro<br />
Mtwara<br />
Kigoma<br />
Kagera<br />
Tan ga<br />
Ruvuma<br />
Mara<br />
Dar es Salaam<br />
Pwani<br />
Arusha<br />
Jumla Kitaifa, 2004<br />
50,322<br />
42,196<br />
38,545<br />
65,950<br />
60,618<br />
58,731<br />
58,120<br />
132,500<br />
119,371<br />
116,190<br />
115,692<br />
115,692<br />
145,159<br />
143,159<br />
137,980<br />
168,179<br />
152,638<br />
254,037<br />
308,761<br />
307,770<br />
305,978<br />
- 50,000 100,000 150,000 200,000 250,000 300,000 350,000<br />
Idadi ya watu<br />
Kuhusu Madaktari Wasaidizi mikoa inayoongoza kwa kuwa na uwiano mzuri ni Mara (1:19,593),<br />
Arusha (1:22,381), Tanga (1:23,906) na Kilimanjaro (1:25,118). Mikoa inayoongoza kwa<br />
kutokuwa na uwiano mzuri ni Shinyanga (1:377,782), Pwani (1:197,552) na Mwanza (1:89,259).<br />
(Mchoro na. 5).<br />
51
Mchoro 5: Uwiano wa Daktari Msaidizi Mmoja na Idadi ya Watu Katika Kila Mkoa<br />
Mkoa<br />
Shinyanga<br />
Pwani<br />
Mwanza<br />
Kagera<br />
Tabora<br />
Manyara<br />
Dodoma<br />
Morogoro<br />
Mbeya<br />
Mtwara<br />
Kigoma<br />
Rukwa<br />
Dar es Salaam<br />
Lindi<br />
Ruvuma<br />
Iringa<br />
Kilimanjaro<br />
Tan ga<br />
Arusha<br />
Mara<br />
Jumla Kitaifa, 2004<br />
26,741<br />
25,118<br />
23,906<br />
22,381<br />
19,593<br />
38,595<br />
35,419<br />
34,816<br />
30,121<br />
47,513<br />
44,235<br />
44,235<br />
65,951<br />
57,264<br />
57,264<br />
53,690<br />
51,458<br />
67,145<br />
89,259<br />
197,552<br />
377,782<br />
- 50,000 100,000 150,000 200,000 250,000 300,000 350,000 400,000<br />
Idadi ya watu<br />
Mikoa yenye uwiano mzuri wa Afisa Tabibu na idadi ya watu ni Tanga (1:5,715), Arusha (1:<br />
5,930), Lindi (1:6,113) na Mara (1:6,210). Mikoa inayoongoza kwa kutokuwa na uwiano mzuri ni<br />
Pwani na Shinyanga (1:56,606 – 1:36,805). (Mchoro na. 6).<br />
Mchoro 6: Uwiano wa Afisa Tabibu (CO) Mmoja na Idadi ya Watu Katika Kila Mkoa<br />
Mkoa<br />
Pwani<br />
Shinyanga<br />
Dar es Salaam<br />
Mtwara<br />
Kigoma<br />
Morogoro<br />
Mwanza<br />
Dodoma<br />
Rukwa<br />
Kagera<br />
Tabora<br />
Manyara<br />
Iringa<br />
Kilimanjaro<br />
Ruvuma<br />
Mbeya<br />
Mara<br />
Lindi<br />
Arusha<br />
Tan ga<br />
Jumla Kitaifa, 2004<br />
12,966<br />
12,966<br />
12,029<br />
11,565<br />
10,989<br />
10,647<br />
9,956<br />
8,103<br />
8,103<br />
7,293<br />
7,093<br />
7,076<br />
6,913<br />
6,210<br />
6,113<br />
5,930<br />
5,715<br />
13,307<br />
23,056<br />
36,805<br />
56,606<br />
- 10,000 20,000 30,000 40,000 50,000 60,000<br />
Idadi ya watu<br />
Kuhusu Afisa Muuguzi mikoa inayoongoza kwa kuwa na uwiano mzuri ni Shinyanga (1:1226),<br />
Iringa (1:1,746), Ruvuma (1:1,932) na Arusha (1:2,234). Mikoa inayoongoza kwa kutokuwa na<br />
52
uwiano mzuri ni Morogoro (1:12,561), Mbeya (1:12,462) na Dar ea Salaam (1:9,054). (Mchoro<br />
na. 7).<br />
Mchoro 7: Uwiano wa Afisa Muuguzo (NO & TN) Mmoja na Idadi ya Watu Katika Kila Mkoa<br />
Mkoa<br />
Morogoro<br />
Mbeya<br />
Dar es Salaam<br />
Mtwara<br />
Kigoma<br />
Dodoma<br />
Kagera<br />
Mwanza<br />
Pwani<br />
Rukwa<br />
Mara<br />
Tabora<br />
Manyara<br />
Kilimanjaro<br />
Tan ga<br />
Lindi<br />
Arusha<br />
Ruvuma<br />
Iringa<br />
Shinyanga<br />
Jumla Kitaifa, 2004<br />
3,642<br />
3,609<br />
3,609<br />
3,504<br />
2,921<br />
2,723<br />
2,234<br />
1,932<br />
1,746<br />
1,226<br />
5,428<br />
5,221<br />
4,761<br />
4,491<br />
5,349<br />
9,054<br />
8,796<br />
8,796<br />
8,265<br />
12,561<br />
12,462<br />
- 2,000 4,000 6,000 8,000 10,000 12,000 14,000<br />
Idadi ya watu<br />
4.5b: Uwiano wa Wataalam wa Afya ya Kinywa (Dental) na Idadi ya Watu<br />
Mikoa ya Arusha na Dar es Salaam ndiyo yenye uwiano mzuri na wataalam wa Afya ya<br />
Kinywa wakati uwiano usio mzuri upo zaidi kwa mikoa ya Mwanza, Morogoro Mbeya na<br />
Tabora. (Jedwali na.3).<br />
Jedwali na 3: Uwiano wa Wataalam wa Afya ya Kinywa (Dental) na Idadi ya Watu<br />
Mikoa Madaktari wa<br />
Meno (DDS)<br />
Madaktari Wasaidizi<br />
wa Meno (ADO)<br />
Tabibu Meno<br />
(DTs)<br />
Fundi Sanifu<br />
Meno (DLTs)<br />
Arusha 1:277,530 1:231275 1:277,530 1:101724<br />
Dar es Salaam 1:258,419 1:339309 1:256,591 1:658584<br />
Dom 1:888,587 1:444,293 1:888,587 1:1,777,175<br />
Iringa 1:508,075 1:381055 1:27,017 1:524223<br />
Kagera 1:1,073,460 1:155794 1:450,566 1:14453<br />
Kilimanjaro 1:1,376,702 1:286100 1:698,351 1:1376702<br />
Kigoma 1:1,503,989 1:501,330 1:501330 0<br />
Lindi 1:417,697 1:412,651 1:206,326 0<br />
Manyara 1:128,138 1:64,079 42,713 0<br />
Mara 1:1,136,393 1:284,098 1:568,196 1:1,136,393<br />
Mbeya 1:277,547 1:119,004 1:156,542 1:299867<br />
Morogoro 1:1,852,504 1:231,563 1:168,409 1:926252<br />
Mtwara 1:174593 1:245,889 1:44,460 1:174593<br />
Mwanza 1:3,119,237 1:445,606 1:445,606 1:1559619<br />
Pwani 1:928,325 1:309,333 1:185,,665 0<br />
Rukwa 1:1,235,046 1:617,523 1:617,523 1:1235046<br />
Ruvuma 1:391542 1:293656 1:391542 1:1145467<br />
Singida 1:1170076 1:1170078 1:39003 0<br />
Shinyanga 1:2975594 1;991865 1;743899 0<br />
Tabora 1:1,479,583 1:429477 1:428253 0<br />
Tanga 1:424326 1:339460 1:242472 1:1697302<br />
Jumla Kitaifa<br />
4.5: Idadi ya Vituo vya kutolea Tiba na Umiliki wake<br />
53
Zipo Zahanati 4,678 nchini ambapo 3,109 (66%) zinamilikiwa na Serikali, 737 (15%)<br />
Mashirika ya Dini, 739 (16%) Watu Binafsi na 135 (3%) Mashirika ya Umma (Mchoro na 8).<br />
Mchoro 8: Umiliki wa Zahanati Katika <strong>Tanzania</strong><br />
Mashirika ya Umma<br />
3%<br />
Binafsi<br />
16%<br />
Mashirika ya Dini<br />
15%<br />
Serikali<br />
66%<br />
Mkoa wa Mwanza unaoongoza kwa kuwa na zahanati nyingi (336 ), ukifuatiwa na mikoa ya<br />
Kilimanjaro (332), Dar es Salaam (330), Mbeya (307) na Iringa (282). (Mchoro na 9).<br />
Mchoro 9: Jumla ya Zahanati ZoteKatika Kila Mkoa<br />
Mikoa<br />
Mwanz a<br />
Kilimanjaro<br />
DSM<br />
Mbeya<br />
Iringa<br />
Shinyanga<br />
Morogoro<br />
Dodoma<br />
Tan ga<br />
Kagera<br />
Tabora<br />
Kigoma<br />
Arusha<br />
Mara<br />
Rukwa<br />
Pwani<br />
Ruvuma<br />
Lindi<br />
Mtwara<br />
Singida<br />
Manyara<br />
139<br />
133<br />
155<br />
154<br />
152<br />
213<br />
207<br />
198<br />
196<br />
186<br />
184<br />
182<br />
240<br />
231<br />
249<br />
282<br />
272<br />
307<br />
336<br />
332<br />
330<br />
0 50 100 150 200 250 300 350<br />
Idadi<br />
Vituo vya Afya<br />
54
Vipo vituo vya Afya 491 nchini, ambapo vituo 333 (67%) vinamilikiwa na Serikali, 113<br />
(23%) Mashirika ya Dini, 10 (2%) Mashirika ya Umma na 37 (8%) Watu Binafsi. (Mchoro<br />
na. 10).<br />
Mchoro 10: Umiliki wa Vituo Vya Afya<br />
Mashirika ya Umma<br />
2%<br />
Binafsi<br />
8%<br />
Mashirika ya Dini<br />
23%<br />
Serikali<br />
67%<br />
Mkoa unayoongoza kwa kuwa na vituo vyingi vya afya ni Mkoa wa Mwanza ukifuatiwa<br />
na mikoa ya Iringa, Kilimanjaro na Morogoro. (Mchoro na 11).<br />
Mchoro 11: Idadi ya Vituo Vya Afya Katika kila Mkoa<br />
Mwanza<br />
Iringa<br />
34<br />
39<br />
Kilimanjaro<br />
32<br />
Morogoro<br />
31<br />
Kagera<br />
30<br />
Arusha<br />
29<br />
Rukwa<br />
28<br />
Mbe ya<br />
28<br />
Shinyanga<br />
27<br />
Mkoa<br />
Tan ga<br />
DSM<br />
Ruvuma<br />
21<br />
23<br />
25<br />
Dodoma<br />
21<br />
Mara<br />
Kigoma<br />
18<br />
20<br />
Pwani<br />
17<br />
Tabora<br />
15<br />
Singida<br />
15<br />
Lindi<br />
15<br />
Mtwara<br />
Manyara<br />
11<br />
14<br />
0 5 10 15 20 25 30 35 40<br />
Idadi<br />
Hospitali<br />
55
Hospitali zipo 217, ambapo 86 (38%) zinamilikiwa na Serikali, 88 (39%) Mashirika ya Dini,<br />
17 (7%) Mashirka ya Umma na 37 (16%) Watu Binafsi. (Mchoro na. 12).<br />
Mchoro 12: Umiliki wa Hospitali Katika Asilimia <strong>Tanzania</strong><br />
Mashirika ya Umma<br />
7%<br />
Binafsi<br />
16% Serikali<br />
38%<br />
Mashirika ya Dini<br />
39%<br />
Mchoro na. 13 unaonyesha umiliki wa vituo vyote vya kutolea tiba <strong>Tanzania</strong> Bara 2004.<br />
Mchoro 13: Umiliki wa Vituo Vyote Vya Kutolea Tiba, <strong>Tanzania</strong><br />
Mashirika ya Umma<br />
3%<br />
Binafsi<br />
15%<br />
Serikali<br />
65%<br />
Mashirika ya Dini<br />
17%<br />
4.7: Idadi ya vitanda vya kulaza wagonjwa kwa kufuata Miliki ya Vituo vya kutolea tiba<br />
Vituo vya Afya<br />
56
Uwezo wa vituo vya Afya kulaza wagonjwa nchini ni vitanda 10,184 na idadi ya vitanda<br />
vilivyopo ni 9,121 sawa na asilimia 86.8% ya uwezo wa kulaza. Kwa ujumla Mikoa ya<br />
Iringa, Tanga na Mwanza inaozongoza kwa kuwa na uwezo mkubwa wa kulaza wagonjwa.<br />
Wakati Mikoa ya Manyara, Arusha na Dar es Salaam ina uwezo mdogo. Serikali inaongoza<br />
kwa kuwa na uwezo mkubwa wa kulaza wagonjwa kwa (68.6%) ikifuatiwa na Mashirika ya<br />
Dini (30%), Watu Binafsi na (4.5%) Mashirika ya Umma (2%). (Jedwali na.4).<br />
Jedwali Na 4: Idadi ya Vitanda vya kulaza Wagonjwa kwa kufuata Miliki ya Vituo vya kutolea Tiba (Vituo vya Afya)<br />
Mikoa<br />
Idadi ya Vitanda Kwenye Vituo vya Huduma<br />
Jumla<br />
Serikali Mashirika ya Dini Mashirika ya Umma Binafsi<br />
Uwezo Vilivyopo* Uwezo Vilivyopo* Uwezo Vilivyopo* Uwezo Vilivyopo* Uwezo Vilivyopo*<br />
Arusha 127 132 188 268 8 8 70 70 293 478<br />
Dar es Salaam 126 84 100 100 0 15 40 50 216 249<br />
Dodoma 422 373 80 97 0 0 30 22 490 492<br />
Iringa 396 294 670 614 0 0 57 21 1123 929<br />
Kagera 298 295 180 145 0 0 16 25 549 410<br />
Kilimanjaro 405 453 33 58 0 5 18 53 356 569<br />
Kigoma 237 294 147 223 15 0 15 0 414 217<br />
Lindi 237 167 33 33 0 0 0 6 270 220<br />
Manyara 70 137 30 78 0 0 0 0 60 215<br />
Mara 260 201 100 104 25 14 50 50 435 369<br />
Mbeya 504 414 173 157 0 0 3 29 760 547<br />
Morogoro 390 297 50 30 52 29 30 0 406 362<br />
Mtwara 245 255 115 110 0 0 0 0 360 365<br />
Mwanza 777 497 96 96 0 0 35 35 858 177<br />
Pwani 216 15 0 16 247<br />
Rukwa 400 327 200 136 0 0 0 0 600 463<br />
Ruvuma 548 524 415 630 0 0 0 0 963 1154<br />
Singida 199 199 58 30 0 0 0 0 257 229<br />
Shinyanga 490 377 50 0 0 0 0 0 552 437<br />
Tabora 230 171 95 110 0 0 0 0 325 281<br />
Tanga 660 497 237 201 0 0 13 13 897 711<br />
Jumla Kitaifa 7021 6204 3050 3235 100 71 377 390 10184 9121<br />
Hospitali<br />
Uwezo wa Hospitali nchini kulaza wagonjwa ni vitanda 25,710 na idadi ya vitanda vilivyopo<br />
ni 25,641 ikiwa na vitanda 69 zaidi. Serikali inaongoza kwa kuwa na uwezo mkubwa wa<br />
kulaza wagonjwa (54.1%) ikifuatiwa na Mashirika ya Dini (39.9%), Watu Binafsi (4.8) na<br />
Mashirika ya Umma (1.5%). Mikoa yenye uwezo mkubwa ni Mwanza, Iringa na Dodoma na<br />
ile yenye uwezo mdogo ni Rukwa, Manyara na Kilimanjaro. (Jedwali na. 5).<br />
Jedwali Na 5: Idadi ya Vitanda vya kulaza Wagonjwa kwa kufuata Miliki ya Vituo vya kutolea Tiba (Hospitali)<br />
Mikoa<br />
Idadi ya Vitanda Kwenye Vituo vya Huduma<br />
Jumla<br />
Serikali Mashirika ya Dini Mashirika ya Umma Binafsi<br />
Uwezo Vilivyopo* Uwezo Vilivyopo* Uwezo Vilivyopo* Uweazo Vilivyopo* Uwezo Vilivyopo*<br />
Arusha 701 642 649 618 30 30 12 12 1192 1302<br />
Dar es Salaam 632 522 66 66 0 0 606 606 1184 1094<br />
Dodoma 1463 1329 580 330 0 0 0 0 2043 1659<br />
Iringa 925 745 990 961 150 40 235 85 2300 1831<br />
Kagera 305 192 580 690 0 0 60 60 1487 1300<br />
Kilimanjaro 542 873 320 1147 0 35 0 130 562 1735<br />
Kigoma 549 549 227 227 0 0 0 0 776 776<br />
Lindi 616 530 411 397 30 24 0 0 1057 951<br />
Manyara 545 454 200 530 0 0 0 0 404 1004<br />
Mara 769 769 285 262 0 0 0 0 1053 1031<br />
Mbeya 590 450 899 901 0 0 40 30 1529 1381<br />
Morogoro 520 527 778 790 135 135 73 73 1506 1525<br />
Mtwara 1010 877 350 300 0 0 0 0 1360 1177<br />
Mwanza 1087 854 1693 1693 0 0 20 20 2780 2508<br />
Pwani 498 100 213 0 811<br />
Rukwa 500 390 150 90 0 0 0 0 650 480<br />
Ruvuma 325 665 645 1015 0 0 0 0 970 1679<br />
Singida 630 444 995 912 0 0 0 0 1625 1356<br />
Shinyanga 1038 838 250 188 0 0 88 88 1376 1104<br />
Tabora 790 693 479 0 0 0 0 0 1269 1172<br />
57
Tanga 948 559 542 520 0 0 65 65 1557 1444<br />
Jumla Kitaifa 14160 13400 10444 10722 345 477 1199 1169 25710 25641<br />
Mkoa wa Dar es Salaam una uwiano mbaya wa kitanda kimoja na idadi ya watu (1:1,686),<br />
ukifuatiwa na Kigoma (1:1,205), Rukwa (1:1186) na Kagera (1:1,177). Mikoa iliyo na<br />
uwiano mzuri ni Iringa (1:540), Shinyanga (1:437) na Singida (1:229). Kitaifa uwiano huo ni<br />
1:928. (Mchoro na. 14).<br />
Mchoro 14: Uwiano wa Kitanda Kimoja kwa Idadi ya Watu Katika Kila Mkoa<br />
1,800<br />
1,686<br />
1,600<br />
1,400<br />
1,200<br />
1,205<br />
1,186<br />
1,177<br />
1,154<br />
1,091<br />
1,070<br />
Idadi ya Watu<br />
1,000<br />
800<br />
974<br />
929<br />
851<br />
837<br />
787<br />
759<br />
729<br />
724<br />
673<br />
598<br />
928<br />
600<br />
540<br />
400<br />
437<br />
200<br />
229<br />
-<br />
Dar es Salaam<br />
Kigoma<br />
Rukwa<br />
Kagera<br />
Tabora<br />
Ruvuma<br />
Mwanza<br />
Mbeya<br />
Mara<br />
Morogoro<br />
Manyara<br />
Pwani<br />
Mikoa<br />
Dodoma<br />
Tanga<br />
Mtwara<br />
Arusha<br />
Lindi<br />
Kilimanjaro<br />
Iringa<br />
Shinyanga<br />
Singida<br />
Jumla Kitaifa<br />
4.8: Watumishi wa sekta ya Afya na Sehemu za Kazi<br />
Jumla ya watumishi waliopo kwenye sekta ya afya mikoani ni 31,952 ambapo 23,874<br />
(74.7%) wameajiriwa Serikalini. Kwa ujumla Serikali ina upungufu wa watumishi 12,843<br />
ikiwa ni 40.2%. (Jedwali na 6).<br />
Jedwali Na 6: Watumishi wa sekta ya Afya na Sehemu za Kazi<br />
Sehemu ya Kazi<br />
Watumishi Serekali Mashirika ya Dini Mashirika ya Umma Mashirika Binafsi Jumla<br />
Waliopo Pungufu Waliopo Pungufu Waliopo Pungufu Waliopo Pungufu Waliopo Pungufu<br />
1 Medical Doctors 185 181 70 69 3 2 33 18 291 270<br />
2 Specialist Doctors 43 74 22 29 5 2 17 2 87 107<br />
3 Dental Surgeons 27 39 0 7 0 0 1 0 28 46<br />
4 Specialist Dental Surgeons 8 14 0 5 0 0 1 0 9 19<br />
5 Pharmacists 65 60 3 27 1 0 2 0 71 87<br />
6 Chemists 12 22 0 2 1 0 3 3 16 27<br />
7 Assistant Medical Officers 522 488 220 139 16 4 34 7 792 638<br />
8 Assistant Dental Officers 338 178 19 46 2 1 13 8 372 233<br />
9 Dental Therapists 307 115 29 49 13 2 15 10 364 176<br />
10 Clinical Officer 2186 2128 420 635 49 7 116 25 2771 2795<br />
11 Assistant Clinical Officers 998 417 119 22 1 0 18 6 1136 445<br />
12 Nursing Officers 1466 519 980 275 32 22 43 6 2521 822<br />
13 Nurse Tutors 506 348 60 19 47 10 10 0 623 377<br />
14 Trained Nurses 688 805 294 252 7 0 11 2 1000 1059<br />
15 Nurse Midwives 2225 1612 920 604 1 0 212 41 3358 2257<br />
16 Public H. Nurse B 1492 2259 76 398 3 0 20 4 1591 2661<br />
17 MCH Aides 1347 449 77 4 3 1 16 0 1443 454<br />
18 Medical Laboratory Technicians 274 144 44 67 0 5 17 10 335 226<br />
19 Radiographers 56 96 30 39 1 0 1 0 88 135<br />
20 Dental Technicians 74 113 6 31 0 0 0 0 80 144<br />
21 Optometry Technicians 19 83 11 26 0 0 0 0 30 109<br />
22 Orthopaedic Technicians 8 46 7 13 0 0 0 0 15 59<br />
23 Physiotherapists 49 84 14 26 1 0 1 0 65 110<br />
58
24 Chemical Laboratory Technicians 12 31 2 5 0 1 0 0 14 37<br />
25 Health Officers 676 358 12 24 3 2 8 0 699 384<br />
26 Pharmac. Technicians 144 297 31 35 4 8 0 0 179 340<br />
27 Medical Records Officers 135 232 65 84 0 1 4 14 204 331<br />
28 Lauderers 176 199 84 51 4 0 2 4 266 254<br />
29 Catering Officers 9 87 13 18 3 0 0 4 25 109<br />
30 Health Secretaries 57 99 29 34 2 0 0 3 88 136<br />
31 Wahudumu wa chumba cha maiti 111 87 35 43 6 2 28 3 180 135<br />
32 All Others 1814 243 777 77 37 21 132 9 2760 350<br />
33 Wahudumu Wauguzi 5961 449 1874 103 40 4 149 5 8024 561<br />
34 Wahudumu Maabara 1221 118 211 22 6 0 27 1 1465 141<br />
35 Wahudumu Meno 135 76 37 32 2 1 9 1 183 110<br />
36 Wahudumu Pharmacy 97 82 36 40 2 1 12 2 147 125<br />
37 Wahudumu X-ray 55 46 31 8 1 0 3 0 90 54<br />
38 Accounts Assistant 53 67 48 33 0 0 7 3 108 103<br />
39 Drivers 323 98 105 7 4 1 2 0 434 106<br />
Jumla ya Watumishi Kitaifa 23874 12843 6811 3400 300 98 967 191 31952 16532<br />
4.9a: Magari/Pikipiki<br />
Kuna jumla ya magari 733 ambapo asilimia 83.8 yanafanya kazi. Mikoa ya Mwanza na Mara<br />
inaongoza kwa kuwa na magari yanayofanya kazi (yote yanafanya kazi). Wakati Mikoa ya<br />
Rukwa na Iringa inaongoza kwa kuwa na magari mengi yasiofanya kazi asilimia 54 na 31.<br />
Kwa upande wa pikipiki Serikali ina pikipiki 433ambapo 90% ndizo zinazofanya kazi. Mikoa<br />
ya Kilimanjaro, Kigoma, Lindi na Rukwa pikipiki zote zinafanyakazi. Mkoa wa Iringa<br />
unaogoza kwa kuwa na pikipiki mbovu 35% ya pikipiki zote. (Jedwali na. 7).<br />
Jedwali na. 7: Magari/ Pikipiki<br />
Mikoa<br />
Hali ya Magari/Pikipiki<br />
Jumla<br />
Yanayofanya Kazi Yasiyofanya Kazi<br />
Magari Pikipiki Magari Pikipiki Magari Pikipiki<br />
Arusha 38 12 6 1 44 13<br />
Dar es Salaam 29 22 2 1 31 23<br />
Dodoma 24 24 7 2 31 26<br />
Iringa 32 24 15 13 47 37<br />
Kagera 25 14 3 2 28 16<br />
Kilimanjaro 29 24 9 0 38 24<br />
Kigoma 33 16 2 0 35 16<br />
Lindi 30 15 8 0 38 15<br />
Manyara 21 9 5 1 26 10<br />
Mara 23 10 0 1 23 11<br />
Mbeya 35 24 6 2 41 26<br />
Morogoro 40 53 4 2 44 55<br />
Mtwara 14 20 2 2 16 22<br />
Mwanza 26 30 0 4 26 34<br />
Pwani 32 0 2 34 0<br />
Rukwa 23 4 27 0 50 8<br />
Ruvuma 18 14 4 1 22 15<br />
Singida 27 24 9 3 36 27<br />
Shinyanga 35 22 4 0 39 22<br />
Tabora 30 19 2 4 32 23<br />
Tanga 47 10 5 0 52 10<br />
Jumla Kitaifa 611 390 122 39 733 433<br />
4.9b: Hadubini<br />
Kuna jumla ya hadubini 2,146 ambapo 80% zinafanya kazi. Mikoa yenye hadubini<br />
zinazofanya kazi kwa wingi ni Arusha na Dodoma. Mikoa yenye hadubini nyingi mbovu ni<br />
Rukwa na Lindi. (Jedwali na. 8).<br />
59
Jedwali na. 8: Hadubini<br />
Mikoa<br />
Hali ya Hadubini<br />
Jumla<br />
Zinazofanya Kazi<br />
Zisizofanya Kazi<br />
Arusha 102 9 111<br />
Dar es Salaam 75 16 91<br />
Dodoma 64 6 70<br />
Iringa 86 37 113<br />
Kagera 176 27 203<br />
Kilimanjaro 192 32 224<br />
Kigoma 92 12 104<br />
Lindi 30 15 54<br />
Manyara 51 16 116<br />
Mara 107 18 135<br />
Mbeya 52 14 66<br />
Morogoro 128 26 154<br />
Mtwara 60 16 76<br />
Mwanza 111 15 126<br />
Pwani 45 12 57<br />
Rukwa 23 21 44<br />
Ruvuma 70 13 83<br />
Singida 70 8 78<br />
Shinyanga 63 16 79<br />
Tabora 61 18 79<br />
Tanga 67 16 83<br />
Jumla Kitaifa 1,725 363 2146<br />
4.9c: Mashine za X-ray<br />
Kuna jumla ya mashine za X-ray 244 mikoani ambapo 83% zinafanyakazi. Mikoa<br />
inayoongoza kwa kuwa na mashine nyingi za X-ray zinazofanya kazi ni Da es Salaam na<br />
Arusha wakati mikoa yenye X-ray chache zinazofanya kazi ni Dodoma na Rukwa. (Jedwali<br />
na. 9).<br />
Jedwali na. 9: Mashine za X-ray s<br />
Mikoa<br />
Hali ya X-ray<br />
Jumla<br />
Zinazofanya Kazi Zisizofanya Kazi<br />
Arusha 16 5 21<br />
Dar es Salaam 28 2 30<br />
Dodoma 4 2 6<br />
Iringa 11 5 6<br />
Kagera 10 0 10<br />
Kilimanjaro 19 4 23<br />
Kigoma 6 2 8<br />
Lindi 10 4 14<br />
Manyara 5 0 5<br />
Mara 8 1 9<br />
Mbeya 8 3 11<br />
Morogoro 8 2 10<br />
Mtwara 6 2 8<br />
Mwanza 9 4 13<br />
Pwani 7 1 8<br />
Rukwa 5 3 8<br />
Ruvuma 7 3 10<br />
Singida 5 5 10<br />
Shinyanga 9 0 9<br />
Tabora 8 6 14<br />
Tanga 11 11<br />
Jumla Kitaifa 200 54 244<br />
4.9d: Vifaa vya Utakasaji<br />
Kuna jumla ya mashine za utakasaji 3,116 mikoani ambapo 87% zinafanyakazi. Mikoa ya<br />
Rukwa, Lindi na Kigoma inaongoza kwa kuwa na mashine nyingi zisizofanyakazi. (Jedwali<br />
na. 10).<br />
60
Jedwali na. 10: Vifaa vya Utakasaji<br />
Mikoa<br />
Hali ya Mashine za Utakasaji<br />
Jumla<br />
Zinazofanya Kazi<br />
Zisizofanya Kazi<br />
Arusha 34 17 51<br />
Dar es Salaam 199 27 226<br />
Dodoma 281 18 299<br />
Iringa 72 2 74<br />
Kagera 235 36 271<br />
Kilimanjaro 382 52 434<br />
Kigoma 11 5 16<br />
Lindi 23 12 35<br />
Manyara 24 5 29<br />
Mara 14 0 14<br />
Mbeya 520 83 613<br />
Morogoro 300 20 320<br />
Mtwara 96 4 100<br />
Mwanza 84 24 108<br />
Pwani 14 4 18<br />
Rukwa 86 53 139<br />
Ruvuma 15 5 20<br />
Singida 24 26 50<br />
Shinyanga 8 0 8<br />
Tabora 18 14 32<br />
Tanga 255 4 259<br />
Jumla Kimkoa 2,695 411 3,116<br />
4.9e: Vifaa vya Tiba ya Meno (Dental Unit and Chair)<br />
Jumla ya vifaa vya tiba ya meno ni 289 na vinavyofanyakazi ni 226 ambayo ni sawa na<br />
78.7%. Mikoa ambayo ina vifaa vingi visivyofanya kazi ni Dar es Salaam (40%), Dodoma<br />
(40%) na Kilimanajro (35.7%). (Jedwali na. 11).<br />
Jedwali na. 11: Vifaa vya Tiba ya Meno (Dental Unit and Chair)<br />
Mikoa<br />
Hali ya Vifaa<br />
Jumla<br />
Vinavyofanya Kazi<br />
Visivyofanya Kazi<br />
Arusha 15 1 16<br />
Dar es Salaam 15 10 25<br />
Dodoma 9 6 15<br />
Iringa 15 2 17<br />
Kagera 7 1 8<br />
Kilimanjaro 9 5 14<br />
Kigoma 6 4 10<br />
Lindi 6 4 10<br />
Manyara 5 1 6<br />
Mara 6 3 9<br />
Mbeya 14 5 19<br />
Morogoro 13 2 15<br />
Mtwara 6 2 8<br />
Mwanza 15 5 19<br />
Pwani 14 4 18<br />
Rukwa 4 0 4<br />
Ruvuma 12 2 14<br />
Singida 8 4 12<br />
Shinyanga 10 1 11<br />
Tabora 17 3 19<br />
Tanga 20 0 20<br />
Jumla Kitaifa 226 65 289<br />
4.10 Magonjwa yanayotolewa Taarifa<br />
61
Jumla ya wagonjwa 451,166 walitolewa taarifa kutoka Mikoa yote. Ugonjwa wa Dysentry<br />
uliongoza kwa kutolewa taarifa (22%) ukifuatiwa na Typhoid (17%), Meningitis (15%),<br />
Animal Bites (15%) na Measels (15%). (Mchoro na 15).<br />
Mchoro 15: Magonjwa Yaliyotolewa Taarifa Watu Wote, 2004<br />
Yellow Fever<br />
0%<br />
Acute Flaccid Paralysis<br />
Cholera<br />
0%<br />
2%<br />
Typhoid<br />
17%<br />
Dysentery<br />
22%<br />
Plague<br />
0%<br />
Animal Bites<br />
15%<br />
Meningitis<br />
15%<br />
Measles<br />
15%<br />
Louse Borne Typhus<br />
(Relapsing Fever)<br />
14%<br />
Kwa watu wa umri chini ya miaka mitano magonjwa yaliyotolewa taarifa ni Dysentry (85%),<br />
Typoid (5%), Cholera (4%) na Measles (1%). (Mchoro na. 16).<br />
Mchoro 16: Magonjwa Yaliyotolewa Taarifa Umri Miaka < 5, 2004<br />
Measles<br />
1%<br />
Meningitis<br />
3%<br />
Plague<br />
0%<br />
Animal Bites<br />
0%<br />
Typhoid<br />
5%<br />
Acute Flaccid Paralysis<br />
0%<br />
Yellow Fever<br />
0%<br />
Cholera<br />
4%<br />
Louse Borne Typhus<br />
(Relapsing Fever)<br />
2%<br />
Dysentery<br />
85%<br />
62
Kwa walio na umri wa miaka 5 na zaidi magonjwa yaliyotolewa taarifa zaidi ni<br />
Typhoid (18%), Animal Bites (16%), Meningitis (16%), Measles (16%), Dysentery<br />
(16%) na Relapsing Fever (16%). (Mchoro na 17).<br />
Mchoro 17: Magonjwa Yaliyotolewa Taarifa Umri Miaka 5+, 2004<br />
Yellow Fever<br />
Acute Flaccid Paralysis 0%<br />
0%<br />
Cholera<br />
2%<br />
Dys entery<br />
16%<br />
Typhoid<br />
18%<br />
Plague<br />
0%<br />
Animal Bites<br />
16%<br />
Louse Borne Typhus<br />
(Relapsing Fever)<br />
16%<br />
Meningitis<br />
16%<br />
Measles<br />
16%<br />
Vifo vilivyotokana na magonjwa yanayotolewa taarifa kwa watu wote ni kama<br />
inavyoonyeshwa kwenye Mchoro na. 18.<br />
Mchoro 18: Vifo Vitokanavyo na Magonjwa Yaliyotolewa Taarifa Umri Kwa Watu Wote, 2004<br />
Animal Bites<br />
16%<br />
Typhoid<br />
17%<br />
Acute Flaccid Paralysis<br />
Cholera 2%<br />
Dysentry<br />
3%<br />
10%<br />
Louse Borne Typhus<br />
(Relapsing Fever)<br />
10%<br />
Plague<br />
0%<br />
Measles<br />
10%<br />
Neonatal Tetanus<br />
16%<br />
Meningitis<br />
16%<br />
63
Kwa mwaka 2003 magonjwa yaliyoongoza kwa kutolewa taarifa yalikuwa Kuhara Damu<br />
(75%), Homa ya Matumbo (15%) na Kipindupindu (8%). (Mchoro na 19).<br />
Mchoro 19: Magonjwa Yaliyotolewa Taarifa Watu Wote, 2003<br />
Kichaa cha mbw a<br />
1%<br />
Kipindupindu<br />
8%<br />
Tauni<br />
0%<br />
Homa ya Matumbo<br />
15%<br />
Uti w a Mgongo<br />
1%<br />
Kuhara damu<br />
75%<br />
4.10 Magonjwa yaliyojitokeza kwa Wagonjwa wa Nje (OPD)<br />
Katika magonjwa yaliyojitokeza kwa wagonjwa wa umri chini ya miaka 5 wa OPD ni<br />
Malaria (39.4%), ARI (16.5%), Pneumonia (9.6%) na Diarrhoea Disease (7.1%). (Mchoro na<br />
20).<br />
64
Mchoro 20: Magonjwa 10 Yaliyojitokeza Zaidi kwa Wagonjwa wa Nje Umri < ya Miaka 5, 2004<br />
Malaria<br />
ARI<br />
16.5<br />
39.4<br />
Aina ya Magonjwa<br />
Pneumonia<br />
Diarrhoeal Disease<br />
Intestinal Worms<br />
Eye Infe cti on s<br />
Skin Infections<br />
Anaemia<br />
Minor surgical Conditions<br />
Ear Infections<br />
4.6<br />
3.9<br />
3.4<br />
2.5<br />
2.0<br />
1.5<br />
7.1<br />
9.6<br />
Ill Defined Symptoms (No diagnosis)<br />
2.0<br />
Other Diagnosis<br />
7.6<br />
0.0 5.0 10.0 15.0 20.0 25.0 30.0 35.0 40.0<br />
Idadi Katika Asilimia<br />
Kwa wagonjwa wenye umri wa miaka 5 na zaidi magonjwa yaliyoongoza ni Malaria<br />
(48.4%), ARI (10.6%), Intestinal Worms ( 4.5%) na Pneumonia (4.5%). (Mchoro na. 21).<br />
Mchoro 21: Magonjwa 10 Yaliyojitokeza Zaidi kwa Wagonjwa wa Nje Umri Miaka 5+, 2004<br />
Malaria<br />
ARI<br />
10.6<br />
48.4<br />
Aina ya Magonjwa<br />
Intestinal Worms<br />
Pneumonia<br />
Diarrhoeal Disease<br />
Minor surgical Conditions<br />
Eye In fe cti on s<br />
Anaemia<br />
Urinary Tract Infections<br />
Non-infectious Gastro-intest Disease<br />
4.5<br />
2.8<br />
2.3<br />
2.0<br />
1.9<br />
1.1<br />
4.5<br />
4.5<br />
Ill defined symptoms<br />
2.8<br />
Others Diagnosis<br />
14.7<br />
0.0 5.0 10.0 15.0 20.0 25.0 30.0 35.0 40.0 45.0 50.0<br />
Idadi Katika Asilimia<br />
Kuhusu Ugonjwa wa Malaria, wagonjwa wa nje wenye umri chini ya miaka 5 waliokuja na<br />
tatizo la ugonjwa huu walikuwa wengi kwa mikoa ya Mwanza (10.8%), Morogoro (9.3%),<br />
Dar eas Salaam (8.2) na Mbeya (7.8%). Mikoa iliyokuwa na mahudhurio ya chini ni Iringa<br />
(1.5%), Manyara (2.1%), Kilimanjaro (3.4%) na Lindi (3.5%). (Mchoro na.22).<br />
65
Mchoro 22: Wagonjwa Wa Nje wenye umri < miaka 5 Waliokuja na Tatizo la Malaria kwa kila mkoa,<br />
2004<br />
Mwanza<br />
10.8<br />
Morogoro<br />
9.3<br />
DSM<br />
8.2<br />
Mbeya<br />
7.8<br />
Tan ga<br />
7.4<br />
Kagera<br />
Dodoma<br />
5.8<br />
7.3<br />
Mikoa<br />
Tabora<br />
Mtwara<br />
Kigoma<br />
5.4<br />
5.5<br />
5.8<br />
Pwani<br />
Mara<br />
Rukwa<br />
3.8<br />
3.7<br />
5.0<br />
Arusha<br />
Lindi<br />
Kilimanjaro<br />
Manyara<br />
Iringa<br />
1.5<br />
2.1<br />
3.5<br />
3.4<br />
3.7<br />
0.0 2.0 4.0 6.0 8.0 10.0 12.0<br />
Idadi ya Wagonjwa Katika %<br />
Kwa wagonjwa wa nje wenye umri wa miaka 5 na zaidi waliokuja na tatizo la ugonjwa wa<br />
Malaria walikuwa wengi kwa mikoa ya Dar es Salaam (13.9%), Mwanza (11.9%), Tanga<br />
(8.5%) na Morogoro (7.6%). Mikoa iliyokuwa na mahudhurio ya chini kwa Malaria ni<br />
Rukwa (0.3%), Arusha (0.3%), Lindi (2.6%) na Manyara (3.0% ). (Mchoro na 23)).<br />
Mchoro 23: Wagonjwa wa Nje Umri Miaka 5+ Walikuja na Tatizo la Malaria Kwa Kila<br />
Mkoa,2004<br />
DSM<br />
13.9<br />
Mwanza<br />
11.9<br />
Tan ga<br />
8.5<br />
Morogoro<br />
Pwani<br />
Kilimanjaro<br />
Mara<br />
5.9<br />
7.6<br />
7.3<br />
7.3<br />
Mikoa<br />
Mbe ya<br />
Dodoma<br />
Kigoma<br />
Kagera<br />
3.9<br />
5.2<br />
5.7<br />
5.6<br />
Iringa<br />
3.8<br />
Mtwara<br />
Tabora<br />
Manyara<br />
Lindi<br />
Arusha<br />
Rukwa<br />
0.3<br />
0.3<br />
3.8<br />
3.5<br />
3.0<br />
2.6<br />
0.0 2.0 4.0 6.0 8.0 10.0 12.0 14.0<br />
Idadi Katika Asilimia<br />
4.10 Magonjwa yaliyojitokeza kwa Wagonjwa Waliolazwa<br />
Magonjwa yaliyojitokeza kwa wagonjwa waliolazwa wenye umri chini ya miaka mitano, ni<br />
Malaria (31.2%), ARI (18.1%), Diarrhoeal Diseases (7.6%), Pneumonia (5.8%) na Aanemia<br />
(4.8%). (Mchoro na 24).<br />
66
Mchoro 24: Magonjwa 10 Yaliyojitokeza Zaidi kwa Waliolazwa Umri < 5, 2004<br />
Magonjwa<br />
Malaria- Uncomplicated<br />
Acute Respiratory Infections<br />
Malaria- Severe, Complicated<br />
Diarrhoeal Diseases<br />
Pneumonia<br />
Anaemia<br />
Intestinal Worms<br />
Respiratory Disease (Nyinginezo)<br />
Tuberculosis<br />
Epilepsy<br />
Ill Defined Symtoms, no Diagnosis<br />
Other Diagnosis<br />
0.9<br />
0.7<br />
0.7<br />
2.4<br />
4.8<br />
4.0<br />
5.8<br />
7.6<br />
8.3<br />
15.5<br />
18.1<br />
31.2<br />
0.0 5.0 10.0 15.0 20.0 25.0 30.0 35.0<br />
Idadi Katika Asilimia<br />
Kwa wagonjwa waliolazwa wa umri wa miaka 5 na zaidi magonjwa yaliyoongoza ni<br />
Uncomplicated Malaria (40.1%), ARI (12.3%) Severe and Complicated Malaria (11.6%) na<br />
Diarrhoea diseases (7.1%). (Mchoro na. 25).<br />
Mchoro 25:Magonjwa 10 Yaliyojitokeza Zaidi kwa Waliolazwa Umri 5+, 2004<br />
Malaria- Uncomplicated<br />
40.1<br />
Acute Respiratory Infections<br />
12.3<br />
Malaria- Severe, Complicated<br />
11.6<br />
Diarrhoeal Diseases<br />
7.1<br />
Magonjwa<br />
Pneumonia<br />
Intestinal Worms<br />
Anaemia<br />
Tuberculosis<br />
3.9<br />
3.8<br />
2.5<br />
1.3<br />
HIV/AIDS<br />
1.0<br />
Urinary tract Infections (UTI)<br />
0.8<br />
Other Diagnosis<br />
14.9<br />
Ill Defined Symptoms, no Diagnosis<br />
0.9<br />
0.0 5.0 10.0 15.0 20.0 25.0 30.0 35.0 40.0 45.0<br />
Idadi Katika Asilimia<br />
Uncomplicated Malaria, Severe and Complicated Malaria, Anaemia pamoja na Pneumonia<br />
yaliongoza kati ya Magonjwa kumi yaliyosababisha vifo kwa watoto wenye umri chini ya<br />
miaka 5. (Mchoro na. 26).<br />
67
Mchoro 26: Magonjwa 10 Yaliyosababisha Vifo kwa Watoto Wenye Umri < ya Miaka 5, 2004<br />
Magonjwa<br />
Malaria- Uncomplicated<br />
Malaria- Severe, Complicated<br />
Anaemia<br />
Pneumonia<br />
Diarrhoeal Diseases<br />
Respiratory Disease (Nyinginezo)<br />
Peri-natal Conditions<br />
HIV/AIDS<br />
Epilepsy<br />
Severe Protein Ernegy Malnut.<br />
Other Diagnosis<br />
Ill Defined Symtoms, no Diagnosis<br />
1.1<br />
4.6<br />
3.9<br />
3.0<br />
2.8<br />
2.3<br />
2.2<br />
7.1<br />
11.8<br />
13.1<br />
23.2<br />
24.9<br />
0.0 5.0 10.0 15.0 20.0 25.0<br />
Idadi Katika Asilimia<br />
Kwa wagonjwa wa umri wa miaka 5 na zaidi vifo vyingi vilisababishwa na magonjwa ya<br />
Severe and Complicated Malaria (19.2%), HIV/AIDS (10.5%) na Uncomplicated Malaria<br />
(7.2%). (Mchoro na. 27).<br />
Mchoro 27: Magonjwa 10 Yaliyosababisha Vifo kwa Watu Wenye Umri Miaka 5+, 2004<br />
Magonjwa<br />
Other Diagnosis<br />
Ill Defined Symptoms, no Diagnosis<br />
Malaria- Severe, Complicated<br />
HIV/AIDS<br />
Malaria- Uncomplicated<br />
Tu bercu l os i s<br />
Pneumonia<br />
Neoplasms<br />
Anaemia<br />
Thyroid Diseases<br />
Cardiac Failure<br />
Diarrhoeal Diseases<br />
2.7<br />
2.6<br />
7.3<br />
7.2<br />
6.7<br />
6.2<br />
5.6<br />
5.3<br />
5.0<br />
10.5<br />
19.2<br />
21.6<br />
0.0 5.0 10.0 15.0 20.0 25.0<br />
Idadi Katika Asilimia<br />
4.13 Taarifa ya Huduma Maalum<br />
Huduma maaalum zilijumuisha upasuaji, kufunga uzazi (sterilization), blood transfusion, X-<br />
rays na ushauri nasaha. (Jedwali 12). mkoa wa Dodoma ulikuwa na Major Surgeries chache<br />
68
(904) kuliko mikoa yote wakati Mkoa wa Pwani ndio uliokuwa na Minor surgeries chache<br />
(1,134) kuliko yote. Sterilization kwa wanaume ilifanyika zaidi katika Mikoa ya Singida<br />
(7,260), Tabora (2,150), Kigoma (111) na Dar es Salaam (27). Mikoa ya Mtwara,<br />
Kilimanjaro na Manyara ilikuwa na Units chache zaidi za damu walizoongezewa wagonjwa<br />
kuliko mikoa mingine. Vilevile, mkoa wa Dodoma ulikuwa na idadi kidogo zaidi ya X-rays<br />
zilizopigwa wakati mikoa iliyopiga idadi kubwa ni Morogoro, Mwanza, Mbeya, Arusha na<br />
Iringa. Mikoa ya Kilimanjaro na Dodoma inatoa huduma kidogo zaidi za ushauri nasaha<br />
kuliko mingine. (Jedwali na 12).<br />
Jedwali na 12: Taarifa za Huduma Maalum<br />
Mikoa<br />
Major<br />
Surgeries<br />
Minor<br />
Surgeries<br />
Sterilization<br />
Blood Transfusions<br />
(Units)<br />
Idadi ya X-<br />
rays<br />
Counseling<br />
Services<br />
Wanaume Wanawake<br />
Arusha 4410 23435 7 779 1226 22499 11311<br />
Dar es Salaam 4294 70848 27 5646 43079 18496 18496<br />
Dodoma 904 3602 0 213 3018 3691 368<br />
Iringa 5067 12538 0 1141 5650 21667 10891<br />
Kagera 5096 14728 0 1027 6257 4097 6872<br />
Kilimanjaro 3187 12271 7 2108 1633 8029 216<br />
Kigoma 2925 19315 111 932 9197 4713 6822<br />
Lindi 3867 3825 0 814 4925 5534 2189<br />
Manyara 3418 11759 0 597 1996 4591 8891<br />
Mara 3234 3873 0 1310 11496 11389 6424<br />
Mbeya 4575 15275 3 924 4614 22609 23876<br />
Morogoro 5876 13728 0 196 6495 36331 10002<br />
Mtwara 1306 13465 0 416 1655 4566 603<br />
Mwanza 5121 5965 7 1067 16847 25364 11057<br />
Pwani 2336 1134 0 141 3055 6666 0<br />
Rukwa 1395 3147 0 844 6252 8896 1959<br />
Ruvuma 5661 12753 2 994 12078 17868 5676<br />
Singida 17845 673 4720 2540 6110 7825 1110<br />
Shinyanga 4717 13699 1 709 14654 15363 3606<br />
Tabora 2077 7256 2150 3543 13937 8604 5490<br />
Tanga 5169 9525 3 467 8428 9003 0<br />
Jumla Kitaifa 764180 272814 7038 26408 182603 267801 135859<br />
4.14 Aina ya X-ray zilizopigwa<br />
Kati ya Picha za X-ray zilizopigwa nyingi zilikuwa za Chest (37%), zikifuatiwa na<br />
Extremeties (33%), na Abdomen (15%). (Mchoro na. 28).<br />
69
Mchoro 28: Aina ya X-Ray Zilizopigwa 2004<br />
Abdomen<br />
15%<br />
Others<br />
4%<br />
Chest<br />
37%<br />
Pelvic<br />
3%<br />
Contrast Studies<br />
1%<br />
Skull<br />
3%<br />
Spine<br />
4%<br />
Extremeties<br />
33%<br />
4.14 Huduma za Maabara<br />
Kuhusu Huduma za Maabara, vipimo vilivyoongoza kwa wingi ni vipimo vya Damu (B/S)<br />
(45%) vikifuatiwa na Wekundu wa Damu (Hb) (19%), Mkojo (13%) na Choo kikubwa<br />
(12%). (Mchoro na. 29).<br />
Mchoro 29: Mchanganuo wa Huduma za Maabara, 2004<br />
Wingi wa Damu (Hb)<br />
19%<br />
Kaswende<br />
5%<br />
Sukari Kwenye Damu<br />
2%<br />
Damu<br />
45%<br />
Ngozi<br />
0%<br />
Makohozi<br />
4%<br />
Mkojo<br />
13%<br />
Choo<br />
12%<br />
4.16 Matokeo ya Vipimo vya Maabara<br />
Kati ya Vipimo vilivyopimwa vilivyoongoza kwa wingi ni Blood Slides (5,890,174),<br />
zikifuatiwa na Hb (2,194,096) pamoja na vipimo vya mkojo 1,013,392. (Jedwali na. 13).<br />
70
Jedwali 13: Matokeo ya Vipimo vya Maabara<br />
VIPIMO V<strong>YA</strong> DAMU B/S<br />
Jumla ya Vipimo 9263382<br />
Positive Malaria 4350210<br />
Positive Borellia 3461<br />
Positive others 3731<br />
VIPIMO V<strong>YA</strong> WEKUNDU <strong>WA</strong> DAMU (Hb)<br />
Jumla ya Vipimo 3194715<br />
HB chini ya 7.0g/L (50%) 545734<br />
VIPIMO V<strong>YA</strong> KASWENDE RPR/VORL<br />
Jumla ya Vipimo 544231<br />
Positive syphilis 68892<br />
VIPIMO V<strong>YA</strong> SUKARI KWENYE DAMU (B/Sugar)<br />
Jumla ya vipimo 344372<br />
Juu ya 10mmo/L (180mg/L) 64192<br />
VIPIMO V<strong>YA</strong> CHOO<br />
Jumla ya Vipimo 1508440<br />
Positive kwa H/worms 117943<br />
Positive kwa Ascaries 68202<br />
Positive kwa E. Histolytica 37640<br />
Positive Nyingine 68944<br />
VIPIMO V<strong>YA</strong> MKOJO<br />
Jumla ya Vipimo 1766116<br />
Positive kwa S. Haematobium 130723<br />
Positive kwa H. Vaginalis 19685<br />
Positive kwa Sugar 32159<br />
VIPIMO V<strong>YA</strong> MAKOHOZI<br />
Jumla ya Vipimo 448715<br />
Positive AFB 78504<br />
VIPIMO V<strong>YA</strong> PROTEIN KWENYE DAMU<br />
Jumla ya Vipimo 140671<br />
Positive Urea/Nitrogen 1301<br />
4.17 Huduma za kliniki ya Meno<br />
Kung’oa meno ndiyo tiba inayoongoza kwa asilimia 77 kati ya huduma za kinywa<br />
zinazotolewa. (Mchoro na. 30).<br />
Mchoro 30: Aina ya Tiba ya Meno<br />
Kuziba (Filling)<br />
10%<br />
Tiba Nyinginezo<br />
13%<br />
Kung’oa (Extraction)<br />
77%<br />
4.18 Mahudhurio ya Kliniki kwa Mama Wajawazito<br />
Matarajio ya mahudhurio ya kliniki kwa mama wajawazito yalikuwa 1,536,131. Jumla ya<br />
waliohudhurio ni 1,310,004 ikiwa ni pungufu kwa asilimia 14.7 ya matarajio. (Jedwali na. 13).<br />
71
Jedwali na 13: Mahudhurio ya Kliniki kwa Mama Wajawazito<br />
Mikoa Matarajio Mahudhurio kwa Mara ya<br />
Kwanza<br />
< wiki 20 Wiki 20+ Jumla ya Mahudhurio<br />
Arusha 55506 24641 27069 51710<br />
Dar es Salaam 106943 52216 52628 104844<br />
Dodoma 71046 40535 28509 69044<br />
Iringa 4782 17392 27859 45251<br />
Kagera 89923 37232 49691 86923<br />
Kilimanjaro 48000 21977 22132 44109<br />
Kigoma 59801 22831 35633 58464<br />
Lindi 24759 17609 983 18592<br />
Manyara 33245 12068 24333 36401<br />
Mara 59183 28201 28364 56565<br />
Mbeya 156329 36000 39864 75864<br />
Morogoro 74468 39377 40160 79537<br />
Mtwara 39074 20812 21168 41980<br />
Mwanza 124537 61354 71826 133180<br />
Pwani<br />
Rukwa 61748 16981 36960 53941<br />
Ruvuma 46985 21372 22113 43485<br />
Singida 45661 22104 26586 48690<br />
Shinyanga 240507 39639 71655 121279<br />
Tabora 123361 23342 52145 75487<br />
Tanga 70273 27493 37201 64694<br />
Jumla Kitaifa 1536131 583179 716879 1310040<br />
4.18 Kiwango cha wajawazito waliojifungulia kliniki<br />
Mikoa ya Kagera, Ruvuma na Lindi iliongoza kwa asilimia kubwa ya wajawazito<br />
waliojifungulia kliniki. (Mchoro na. 31).<br />
Mchoro 31: Kiwango cha Wajawazito Waliofungulia Kliniki<br />
Kagera<br />
Ruvuma<br />
Lindi<br />
Tan ga<br />
83.6<br />
78.0<br />
76.0<br />
96.0<br />
Arusha<br />
Iringa<br />
66.9<br />
75.0<br />
Mbeya<br />
63.1<br />
Tabora<br />
Mara<br />
61.0<br />
60.3<br />
Mikoa<br />
Mwanza<br />
Kigoma<br />
Dom<br />
Morogoro<br />
Shinyanga<br />
Singida<br />
Kilimanjaro<br />
51.4<br />
49.0<br />
47.0<br />
46.8<br />
42.7<br />
42.5<br />
59.2<br />
Rukwa<br />
Manyara<br />
35.0<br />
30.0<br />
Mtwara<br />
Avarage<br />
29.0<br />
57.5<br />
0.0 10.0 20.0 30.0 40.0 50.0 60.0 70.0 80.0 90.0 100.0<br />
Kiwango Katika Asilimia<br />
4.20 Huduma kwa Mama waliojifungua<br />
Jumla ya akinamama 976,858 walijifungulia katika vituo vya kutolea tiba. Asilimia 91.6<br />
walijifungua kwa njia ya kawaida. (Mchoro na 32).<br />
72
Mchoro 32: Taarifa za Kujifungua Wajawazito Katika Vituo Vya Kutolea Tiba<br />
Kupasuliwa(C/S)<br />
4.9%<br />
Njia Nyinginezo<br />
3.1%<br />
Vacuum<br />
0.4%<br />
Kawaida<br />
91.6%<br />
4.21 Matatizo ya Akina mama wakati wa kujifungua<br />
Tatizo kubwa ambalo liliwapata akina mama wakati wa kujifungua lilikuwa ni kutokwa na<br />
damu nyingi baada ya kujifungua (PPH). (Jedwali na.14).<br />
Jedwali na 14: Matatizo ya Akina Mama wakati wa Kujifungua<br />
Mikoa<br />
Kutokwa<br />
Damu Nyingi<br />
Kondo la Nyuma<br />
Kubaki<br />
Kuchanika Msamba<br />
(3rd degree)<br />
Matatizo<br />
Mengine<br />
APH PPH<br />
Arusha 37 100 83 3 171<br />
Dar es Salaam 89 4869 89 22 660<br />
Dodoma 1 55 35 4 69<br />
Iringa 7 97 51 22 99<br />
Kagera 58 266 137 16 116<br />
Kilimanjaro 62 168 51 7 159<br />
Kigoma 107 235 139 14 48<br />
Lindi 7 114 113 0 218<br />
Manyara 28 189 141 8 107<br />
Mara 0 78 97 0 100<br />
Mbeya 11 214 113 7 138<br />
Morogoro 160 126 72 11 1717<br />
Mtwara 8 111 69 3 33<br />
Mwanza 36 674 300 12 340<br />
Pwani 100 33 2 116 53<br />
Rukwa 2 18 59 5 26<br />
Ruvuma 15 171 57 5 522<br />
Singida 5 87 87 10 66<br />
Shinyanga 23 248 127 2 421<br />
Tabora 25 378 246 12 248<br />
Tanga 0 144 110 3 256<br />
Jumla Kitaifa 776 8288 2091 272 5501<br />
4.22 Sababu za Vifo vya Mama Wajawazito<br />
73
Sababu iliyoongoza mwaka 2004 kusababisha vifo vingi vya akinamama ni PPH (16%)<br />
ikifuatiwa na Puperial Sepsis (15%), Anaemia (12%), Eclampsia (10%) na Malaria (9%).<br />
(Mchoro na 34).<br />
Mchoro 34: Sababu zilizosababisha vifo vya akina mama waliojifungua mwaka 2004<br />
Other Diagnosis<br />
14%<br />
PPH<br />
16%<br />
Obstructed Labour<br />
4%<br />
Septicaemia<br />
3%<br />
Puerperial S epsis<br />
15%<br />
APH<br />
4%<br />
Ruptured Uterus<br />
6%<br />
HIV/AIDS<br />
8%<br />
Anaemia<br />
12%<br />
Malaria<br />
8%<br />
Eclampsia<br />
10%<br />
Kwa mwaka 2003 vifo vingi vilisababishwa na PPH (34%), Anaemia (10%), Puperial sepsis<br />
(7%), na Eclampsia (7%). (Mchoro na. 35).<br />
Mchoro 35: Sababu zilizosababisha vifo vya akina mama waliojifungua mwaka 2003<br />
HIV/AIDS<br />
5%<br />
Abraptid Placenta<br />
1%<br />
Others<br />
19%<br />
Ruptured Uteraus<br />
5%<br />
Chronic Infection<br />
1%<br />
PPH<br />
34%<br />
Unsafe Abotion<br />
0%<br />
Malaria<br />
5%<br />
Obstracted labour<br />
2%<br />
Anaemia<br />
10%<br />
APH<br />
2%<br />
Relapsing Fever<br />
0%<br />
Eclampsia<br />
7%<br />
EPH gestrois<br />
2%<br />
Puperal Sepsis<br />
7%<br />
4.23a Taarifa ya watoto waliozaliwa mmoja mmoja<br />
74
Kati ya watoto waliozaliwa mmojammoja watoto 792,549 walizaliwa hai ambapo watoto<br />
54,287 walikuwa na uzito < ya 2.5 kg .Watoto 4,302 walifariki kabla na baada ya masaa 24.<br />
Watoto 13,549 walizaliwa wafu (Jedwali na 15).<br />
Jedwali na 15: Taarifa za Watoto Waliozaliwa Mmojammoja<br />
Mikoa Waliozaliwa Hai Uzito wa Waliozaliwa Hai Waliozaliwa Wafu Waliozaliwa Hai Kisha<br />
(Still Births)<br />
Wakafa<br />
Waliopimwa Idadi < 2.5 kg Macerated Fresh Saa < 24 Saa 24+<br />
Arusha 25673 25673 1023 323 208 96 157<br />
DSM 81280 81280 4417 869 433 191 227<br />
Dom 36727 36301 639 151 101 49 19<br />
Iringa 14578 45578 2555 573 383 171 135<br />
Kagera 54481 40728 2534 444 276 104 61<br />
Kilimanjaro 36494 31930 1335 205 238 193 136<br />
Kigoma 54664 33781 2901 239 203 96 129<br />
Lindi 18982 18399 1316 196 139 77 37<br />
Manyara 15959 15524 999 224 132 82 85<br />
Mara 29316 29266 250 135 147 33 58<br />
Mbeya 37511 37067 2471 495 455 209 268<br />
Morogoro 35600 35749 5104 530 396 171 260<br />
Mtwara 27343 17819 1180 175 106 53 77<br />
Mwanza 71959 69976 6398 1546 357 182 159<br />
Pwani 25987 1785 247 159 29 28<br />
Rukwa 33699 33699 1372 257 64 0 0<br />
Ruvuma 37664 37664 4136 310 95 51 68<br />
Singida 25138 20901 764 207 114 52 18<br />
Shinyanga 53022 52946 1946 588 441 113 42<br />
Tabora 46706 35832 9101 459 250 176 78<br />
Tanga 29703 29436 2061 439 240 89 43<br />
Jumla Kitaifa 792486 729549 54287 8612 4937 2217 2085<br />
4.23b Taarifa ya Watoto waliozaliwa zaidi ya mmoja<br />
Kati ya watoto waliozaliwa zaidi ya mmoja, waliozaliwa hai walikuwa 120,225 ambapo<br />
watoto 753 walifariki kabla na baada ya masaa 24. Watoto waliozaliwa wafu ni 2,800.<br />
(Jedwali na. 16).<br />
Jedwali na. 16: Taarifa za watoto waliozaliwa zaidi ya mmoja<br />
Mikoa Waliozaliwa<br />
Hai<br />
Waliozaliwa Wafu (Still Births) Waliozaliwa Hai Kisha Wakafa (Still<br />
Births)<br />
Macerated Frsh Saa ≤24 Saa 24+<br />
Arusha 870 27 37 15 15<br />
Dar es Salaam 43285 222 109 32 1<br />
Dodoma 547 15 14 6 10<br />
Iringa 1073 29 26 34 20<br />
Kagera 1852 20 34 15 10<br />
Kilimanjaro 491 36 24 19 31<br />
Kigoma 1894 19 16 19 24<br />
Lindi 330 18 14 22 10<br />
Manyara 453 11 12 21 5<br />
Mara 177 15 21 5 2<br />
Mbeya 8577 168 175 17 9<br />
Morogoro 833 26 22 26 27<br />
Mtwara 322 99 46 3 8<br />
Mwanza 9061 226 87 58 23<br />
Pwani 358 12 8 47 12<br />
Rukwa 33711 322 127 0 0<br />
Ruvuma 632 43 26 15 18<br />
Singida 381 30 19 21<br />
Shinyanga 1889 170 110 52 7<br />
Tabora 12407 137 134 34 14<br />
Tanga 1082 51 43 13 19<br />
Jumla Kitaifa 120,225 1696 1104 474 279<br />
4.24 Idadi ya watoto chini ya mwaka mmoja waliopata chanjo<br />
75
Kuhusu chanjo ya BCG mikoa ya Lindi (121.3%), Mwanza (113.8%), Tanga (107%)<br />
iliongoza kwa viwango vikubwa kupita malengo. Mikoa ya Kilimanjaro, Manyara, na Iringa<br />
ilikuwa na viwango vidogo (90.5 – 94%). (Mchoro na. 36).<br />
Mchoro 36: Kiwango cha Chanjo ya BCG<br />
140.0<br />
Kiwango Katika Asilimia<br />
120.0<br />
100.0<br />
80.0<br />
60.0<br />
40.0<br />
121.3<br />
113.8<br />
107.0<br />
100.0<br />
99.4<br />
98.6<br />
98.5<br />
98.0<br />
97.0<br />
97.0<br />
97.0<br />
96.4<br />
96.0<br />
95.0<br />
95.0<br />
95.0<br />
94.0<br />
94.0<br />
92.4<br />
92.0<br />
90.5<br />
100.0<br />
90.1<br />
114.9<br />
20.0<br />
0.0<br />
Lindi<br />
Mwanza<br />
Tanga<br />
Mbeya<br />
Kagera<br />
Rukwa<br />
Mara<br />
Dar es Salaam<br />
Kigoma<br />
Pwani<br />
Shinyanga<br />
Arusha<br />
Dodoma<br />
Morogoro<br />
Mtwara<br />
Mikoa na Taifa<br />
Tabora<br />
Iringa<br />
Singida<br />
Ruvuma<br />
Manyara<br />
Kilimanjaro<br />
Total 2001<br />
Total 2002<br />
Total 2003<br />
Kwa chanjo ya DPT3 mkoa wa Kilimanjaro ulivuka lengo ambapo kiwango kilikuwa 109%,<br />
wakati mikoa ya Kigoma, Ruvuma, Tabora na Mtwara ilikuwa na viwango vya chini (79 –<br />
83%). (Mchoro na. 37).<br />
Mchoro 37: Kiwango cha Chanjo ya DPT3<br />
120.0<br />
109.0<br />
Kiwango Katika Asilimia<br />
100.0<br />
80.0<br />
60.0<br />
40.0<br />
95.9<br />
95.0<br />
94.1<br />
94.0<br />
93.6<br />
93.3<br />
92.7<br />
92.4<br />
91.0<br />
90.3<br />
90.0<br />
90.0<br />
90.0<br />
90.0<br />
89.0<br />
88.0<br />
83.0<br />
83.0<br />
82.6<br />
79.0<br />
94.8<br />
84.2<br />
105.9<br />
91.3<br />
20.0<br />
0.0<br />
Kilimanjaro<br />
Mara<br />
Dodoma<br />
Mwanza<br />
Morogoro<br />
Lindi<br />
Pwani<br />
Kagera<br />
Arusha<br />
Manyara<br />
Dar es Salaam<br />
Mbeya<br />
Rukwa<br />
Shinyanga<br />
Singida<br />
Iringa<br />
Tanga<br />
Mikoa na Taifa<br />
Mtwara<br />
Tabora<br />
Ruvuma<br />
Kigoma<br />
Total 2001<br />
Total 2002<br />
Total 2003<br />
Total 2004<br />
76
Kwa chanjo ya Polio mikoa ya Kilimanjaro, Lindi na Mwanza iliongoza kwa kuvuka<br />
malengo kwa kuwa na viwango vikubwa (104 – 109.8%), wakati mikoa ya Mtwara , Tabora,<br />
Pwani na Kigoma ilikuwa na viwango vya chini (83 – 85.6%). (Mchoro na. 38).<br />
Mchoro 38: Kiwango cha Chanjo ya Polio3<br />
120.0<br />
100.0<br />
109.8<br />
106.7<br />
104.0<br />
97.1<br />
96.9<br />
95.0<br />
94.0<br />
93.8<br />
93.0<br />
92.2<br />
92.0<br />
92.0<br />
91.0<br />
90.6<br />
89.1<br />
88.0<br />
88.0<br />
85.6<br />
85.6<br />
85.0<br />
83.0<br />
88.0<br />
108.5<br />
93.1<br />
Kiwango Katika Asilimia<br />
80.0<br />
60.0<br />
40.0<br />
49.0<br />
20.0<br />
0.0<br />
Kilimanjaro<br />
Lindi<br />
Mwanza<br />
Ruvuma<br />
Mara<br />
Dodoma<br />
Tanga<br />
Kagera<br />
Morogoro<br />
Arusha<br />
Manyara<br />
Rukwa<br />
Shinyanga<br />
Dar es Salaam<br />
Mbeya<br />
Iringa<br />
Mik oa na Taifa<br />
Singgida<br />
Kigoma<br />
Pwani<br />
Tabora<br />
Mtwara<br />
Total 2001<br />
Total 2002<br />
Total 2003<br />
Total 2004<br />
Kuhusu chanjo ya Surua mikoa iliyoongoza kwa kuvuka malengo ni Lindi, Tanga, Mwanza<br />
na Kilimanjaro (109 – 116.8%), wakati mikoa iliyokuwa na viwango vidogo ni Mtwara,<br />
Tabora na Pwani (78.4 – 87.8%). (Mchoro na. 39).<br />
Mchoro 39: Kiwango cha Chanjo ya Surua<br />
120.0<br />
116.8<br />
114.0<br />
113.9<br />
109.9<br />
100.0<br />
96.0<br />
96.0<br />
95.9<br />
94.0<br />
93.0<br />
91.0<br />
90.1<br />
90.0<br />
89.0<br />
88.8<br />
88.0<br />
88.0<br />
88.0<br />
87.8<br />
84.0<br />
78.4<br />
88.1<br />
86.0<br />
105.1<br />
95.2<br />
Kiwango Katika Asilimia<br />
80.0<br />
60.0<br />
40.0<br />
20.0<br />
0.0<br />
Lindi<br />
Tanga<br />
Mwanza<br />
Kilimanjaro<br />
DSM<br />
Rukwa<br />
Mara<br />
Dom<br />
Morogoro<br />
Singida<br />
Kagera<br />
Manyara<br />
Iringa<br />
Kigoma<br />
Arusha<br />
Mikoa na Taifa<br />
Mbeya<br />
Shinyanga<br />
Pwani<br />
Tabora<br />
Mtwara<br />
Total 2001<br />
Total 2002<br />
Total 2003<br />
Total 2004<br />
77
4.25 Chanjo ya TT2+ kwa akinamama wajawazito<br />
Mikoa ya Mwanza na Dar es Salaam iliongoza kwa Kiwango cha chanjo ya TT2+ kwa kuwa<br />
na viwango vikubwa (95.9 – 97.5) wakati mkoa uliokuwa na kiwango cha chini kabisa ni<br />
Pwani (26.1%). (Mchoro na. 40).<br />
Mchoro 40: Kiwango cha Chanjo ya TT2+<br />
Kiwango Katika Asilimia<br />
100.0<br />
90.0<br />
80.0<br />
70.0<br />
60.0<br />
50.0<br />
40.0<br />
30.0<br />
20.0<br />
26.1<br />
55.0<br />
66.7<br />
73.4<br />
74.0<br />
74.7<br />
77.0<br />
78.4<br />
78.4<br />
78.5<br />
80.0<br />
80.6<br />
85.1<br />
85.3<br />
86.0<br />
88.4<br />
90.6<br />
92.0<br />
92.0<br />
95.9<br />
97.5<br />
62.0<br />
61.0<br />
97.3<br />
78.8<br />
10.0<br />
0.0<br />
Pwani<br />
Tabora<br />
Kigoma<br />
Mbeya<br />
Manyara<br />
Rukwa<br />
Arusha<br />
Kilimanjaro<br />
Mtwara<br />
Ruvuma<br />
Morogoro<br />
Shinyanga<br />
Lindi<br />
Tanga<br />
Singida<br />
Iringa<br />
Kagera<br />
Dodoma<br />
Mara<br />
Dar ea Salaam<br />
Mwanza<br />
Total 2001<br />
Total 2002<br />
Total 2003<br />
Total 2004<br />
Mikoa na Taifa<br />
4.26 Wateja wa uzazi wa mpango wanaoendelea na Huduma<br />
Mkoa wa Tanga unaongoza kwa kuwa na akina mama wengi wanaoendelea na uzazi wa<br />
mpango (60.5%) ukifuatiwa na Mbeya. Mikoa yenye viwango vya chini ni Kagera (15.4%)<br />
na Mtwara (16.6%). Kitaifa akinamama wanaoendelea na uzazi wa mpango ni 36.9%.<br />
(Mchoro na. 41).<br />
Mchoro 41: Mama Wanaoendelea na Uzazi wa Mpango<br />
Tan ga<br />
Mbeya<br />
Ruvuma<br />
54.6<br />
65.5<br />
65.0<br />
Dar ea Salaam<br />
Kilimanjaro<br />
Dodoma<br />
Iringa<br />
Arusha<br />
48.0<br />
44.0<br />
43.0<br />
42.0<br />
53.7<br />
Mikoa na Taifa<br />
Morogoro<br />
Singida<br />
Mara<br />
Tabora<br />
Pwani<br />
Mwanza<br />
31.0<br />
30.5<br />
27.8<br />
36.0<br />
34.8<br />
40.0<br />
Lindi<br />
Manyara<br />
Kigoma<br />
25.4<br />
24.0<br />
21.1<br />
Shinyanga<br />
Mtwara<br />
Kagera<br />
Jumla Kitaifa,2004<br />
18.6<br />
16.6<br />
15.4<br />
36.9<br />
0.0 10.0 20.0 30.0 40.0 50.0 60.0 70.0<br />
Kiwango katika Asilimia<br />
78
Mkoa wa Rukwa unaongoza kwa kuwa na wateja wengi wapya wa uzazi wa mpango (28%)<br />
ukifuatiwa na mikoa ya Mara na Dar es Salaam (22.8%) kila mkoa. Mikoa yenye kiwango<br />
cha chini kabisa ni Manyara (5.2%) na Shinyanga (7.4%). Kitaifa wateja wapya wa uzazi wa<br />
mpango ni (15.7%). (Mchoro na. 42).<br />
Mchoro na. 42: Kiwango cha Wateja Wapya wa Uzazi wa Mpango<br />
Rukwa<br />
Mara<br />
Dar ea Salaam<br />
22.8<br />
22.8<br />
28.0<br />
Dodoma<br />
Mtwara<br />
Tabora<br />
18.0<br />
20.0<br />
22.0<br />
Mikoa na Taifa<br />
Ruvuma<br />
Lindi<br />
Mbeya<br />
Tan ga<br />
Arusha<br />
Mwanza<br />
Singida<br />
Morogoro<br />
17.4<br />
17.1<br />
15.6<br />
14.4<br />
14.0<br />
13.4<br />
13.0<br />
13.0<br />
Kigoma<br />
Kagera<br />
Kilimanjaro<br />
10.6<br />
10.1<br />
12.3<br />
Iringa<br />
8.0<br />
Shinyanga<br />
Manyara<br />
Jumla Kitaifa,2004<br />
5.2<br />
7.4<br />
15.7<br />
0.0 5.0 10.0 15.0 20.0 25.0 30.0<br />
Kiwango katika silimia<br />
4.27 Watoto waliopata matone ya Vitamin A<br />
Jumla ya watoto 2,277,173 wa umri wa miezi 6-11, walipata matone ya Vitamin A ambao ni<br />
asilimia 86.3 ya watoto wa umri huo. Mkoa wa Morogoro unaongoza kwa watoto wa umri wa<br />
miezi 6 – 11 waliopata matone ya Vitamini A (125%). Mkoa wa Manyara ulikuwa na<br />
kiwango cha chini (11%). Kitaifa asilimia 86.3 walipata matone ya Vitamin A. (Mchoro<br />
na.43).<br />
79
Mchoro 43: Watoto Umri Miezi 6 - 11 Waliopata Matone ya Vitamin A<br />
Morogoro<br />
125.0<br />
Kigoma<br />
123.2<br />
Pwani<br />
119.7<br />
Mara<br />
113.0<br />
Tanga<br />
Mtwara<br />
110.0<br />
102.0<br />
Mwanza<br />
Rukwa<br />
97.6<br />
96.3<br />
Mikoa na Taifa<br />
Kilimanjaro<br />
Lindi<br />
Arusha<br />
Ruvuma<br />
Dodoma<br />
Mbeya<br />
87.4<br />
86.0<br />
85.2<br />
93.2<br />
91.7<br />
91.3<br />
Tabora<br />
Dar es Salaam<br />
Shiinyanga<br />
Kagera<br />
Iringa<br />
Manyara<br />
16.9<br />
11.0<br />
33.3<br />
38.9<br />
77.5<br />
81.0<br />
Jumla Kitaifa, 2004<br />
86.3<br />
0.0 20.0 40.0 60.0 80.0 100.0 120.0 140.0<br />
Viwango Katika Asilimia<br />
Kwa watoto wa umri wa miaka 1 – 5 waliopata matone ya Vitamin A, kiwango cha Kitaifa<br />
kilikuwa ni 91.5%. Mkoa wa Mtwara uliongoza (125%) na Manyara ulikuwa wa mwisho<br />
(69%). (Mchoro na. 44).<br />
Mchoro 44: Watoto Umri Miaka 1 - 5 Waliopata Matone ya Vitamin A<br />
Mtwara<br />
125.0<br />
Tabora<br />
108.0<br />
Dodoma<br />
100.0<br />
Arusha<br />
98.2<br />
Kagera<br />
98.1<br />
Kigoma<br />
96.3<br />
Shinyanga<br />
95.6<br />
Mwanza<br />
Lindi<br />
93.1<br />
92.1<br />
Pwani<br />
90.9<br />
Mikoa na Taifa<br />
Kilimanjaro<br />
Tanga<br />
Mara<br />
Ruvuma<br />
Dar es Salaam<br />
Morogoro<br />
Mbeya<br />
89.0<br />
89.0<br />
88.5<br />
88.3<br />
85.0<br />
78.9<br />
90.4<br />
Iringa<br />
78.7<br />
Rukwa<br />
77.2<br />
Manyara<br />
69.0<br />
Jumla Kitaifa, 2001<br />
Jumla Kitaifa, 2002<br />
Jumla Kitaifa, 2003<br />
Jumla Kitaifa, 2004<br />
26.0<br />
87.0<br />
92.0<br />
91.5<br />
0.0 20.0 40.0 60.0 80.0 100.0 120.0 140.0<br />
Viwango Katika Asilimia<br />
80
4.28 Kiwango cha Watoto wenye Utapiamlo Mkali<br />
Jumla ya watoto 71,536 kati ya 2,121,767 waliopimwa walikuwa na Utapiamlo mkali sawa na<br />
asilimia 3.8 ya kiwango Kitaifa. Mkoa wa Morogoro uliongoza kwa kiwango kikubwa cha<br />
watoto wenye utapiamlo mkali (13.5%). Mikoa ya Iringa na Dodoma imekuwa na viwango<br />
vya chini vya watoto wenye utapiamlo mkali (0.8% – 0.9%). (Mchoro na. 45).<br />
Mchoro 45: Kiwango cha Utapiamlo Mkali<br />
14.0<br />
13.5<br />
12.0<br />
10.0<br />
4.4<br />
9.5<br />
10.1<br />
Asilimia<br />
8.0<br />
6.0<br />
5.2<br />
6.1<br />
4.0<br />
3.8<br />
3.3<br />
3.8<br />
4.0<br />
2.0<br />
2.4<br />
2.4<br />
1.6<br />
0.8<br />
0.9<br />
1.1<br />
1.1<br />
1.3<br />
1.7<br />
1.8<br />
2.0<br />
2.0<br />
2.0<br />
2.2<br />
2.2<br />
0.0<br />
Jumla Kitaifa, 2004<br />
Jumla Kitaifa, 2003<br />
Jumla Kitaifa, 2002<br />
Jumla Kitaifa, 2001<br />
Iringa<br />
Dodoma<br />
Kagera<br />
Kilimanjaro<br />
Arusha<br />
Singda<br />
Mwanza<br />
Manyara<br />
Mara<br />
Mbeya<br />
Dar es Salaam<br />
Mikoa na Taifa<br />
Pwani<br />
Ruvuma<br />
Mtwara<br />
Tabora<br />
Kigoma<br />
Shinyanga<br />
Rukwa<br />
Lindi<br />
Tanga<br />
Morogoro<br />
4.29 Kiwango cha Kaya zenye vyoo vinavyokubalika na maji toka vyanzo salama<br />
Kiwango cha Kaya zenye vyoo vinavyokubalika Kitaifa ni 64.8%. Mikoa iliyoongoza kwa<br />
kuwa na vyoo vinavyokubalika ni Shinyanga, Dar es Salaam na Iringa (80 – 84.4%). Mikoa<br />
iliyokuwa na viwango vya chini ni Tabora na Manyara (37 – 42%). (Mchoro na. 46).<br />
Mchoro 46: Kiwango cha Kaya Zenye Vyoo Vinavyokubalika<br />
Shinyanga<br />
83.4<br />
Dar es Salaam<br />
80.8<br />
Iringa<br />
80.0<br />
Tan ga<br />
77.3<br />
Dodoma<br />
77.0<br />
Arusha<br />
76.2<br />
Kiwango Katika Asilimia<br />
Ruvuma<br />
Mwanza<br />
Mbeya<br />
Singida<br />
Mtwara<br />
Morogoro<br />
Kigoma<br />
Lindi<br />
Pwani<br />
Rukwa<br />
71.5<br />
69.0<br />
67.0<br />
66.2<br />
65.1<br />
63.7<br />
62.7<br />
62.0<br />
61.6<br />
75.3<br />
Kilimanjaro<br />
55.8<br />
Mara<br />
54.0<br />
Manyara<br />
42.0<br />
Tabora<br />
37.0<br />
Jumla Kitaifa 2001<br />
Jumla Kitaifa, 2002<br />
63.0<br />
63.0<br />
Jumla Kitaifa, 2003<br />
65.0<br />
Jumla Kitaifa, 2004<br />
64.8<br />
0.0 10.0 20.0 30.0 40.0 50.0 60.0 70.0 80.0 90.0<br />
Mikoa na Taifa<br />
81
Kuhusu Kaya zinazopata maji toka vyanzo salama, mikoa ya Dodoma, Rukwa na Arusha<br />
inaongoza kwa viwango vya juu (62.8 – 84.2%). Kitaifa 53% ya Kaya hupata maji toka<br />
vyanzo salama. Mikoa ya Kigoma, Mtwara na Manyara ina viwango vya chini (32.8 – 39%).<br />
(Mchoro na. 47).<br />
Mchoro 47: Kiwango cha Kaya Zenye Vyanzo Vya Maji Salaama<br />
Kagera<br />
84.2<br />
Dodoma<br />
76.0<br />
Rukwa<br />
64.1<br />
Arusha<br />
62.8<br />
Ruvuma<br />
60.9<br />
Pwani<br />
60.0<br />
Tan ga<br />
59.0<br />
Iringa<br />
56.4<br />
Kiwango Katika Asilimia<br />
Mwanza<br />
Mbe ya<br />
Lindi<br />
Mara<br />
Kilimanjaro<br />
Shinyanga<br />
Morogoro<br />
Tabora<br />
39.2<br />
39.0<br />
43.1<br />
43.0<br />
47.4<br />
54.3<br />
54.0<br />
53.0<br />
Manyara<br />
39.0<br />
Mtwara<br />
35.9<br />
Singida<br />
Kigoma<br />
Jumla Kitaifa, 2001<br />
Jumla Kitaifa, 2002<br />
Jumla Kitaifa, 2003<br />
Jumla Kitaifa, 2004<br />
33.7<br />
32.8<br />
51.0<br />
52.0<br />
54.0<br />
53.0<br />
0.0 10.0 20.0 30.0 40.0 50.0 60.0 70.0 80.0 90.0<br />
Mikoa na Taifa<br />
4.30 Mapato na vyanzo vyake<br />
Mikoa mingi imetoa taarifa ya mapato na vyanzo vyake ikilinganishwa na miaka iliyopita.<br />
Kwa mwaka 2004 fedha nyingi zilikuwa za Serekali (OC 34% na PE 33%) zikifuatiwa na za<br />
Wahisani (Busket Fund) 23%. Mapato kutoka Halmashauri yalikuwa kidogo (1%). (Mchoro<br />
na. 48)).<br />
Mchoro 48: Vyanzo Mbalimbali vya Mapato, 2004<br />
Vyanzo vingine<br />
10%<br />
Cost Sharing<br />
4%<br />
Fe dha z a Halmashauri<br />
1%<br />
Community Health Fund<br />
1%<br />
Capitalization<br />
2%<br />
PE<br />
34%<br />
Basket Funds<br />
23%<br />
Miradi ya Maendeleo<br />
2%<br />
OC<br />
23%<br />
82
Mkoa ulioongoza kwa mapato ulikuwa ni Morogoro ukifuatiwa na Iringa, Mwanza, Arusha<br />
na Mbeya. Mikoa iliyokuwa na mapato ya chini zaidi ni Dodoma, Mtwara, Kigoma, Ruvuma<br />
na Lindi. (Mchoro na. 49).<br />
Mchoro 49: Jumla ya Mapato Kwa Kila Mkoa, 2004<br />
14,000,000,000<br />
12,000,000,000<br />
10,000,000,000<br />
8,000,000,000<br />
Tsh<br />
6,000,000,000<br />
4,000,000,000<br />
2,000,000,000<br />
-<br />
Dom<br />
Mtwara<br />
Kigoma<br />
Ruvuma<br />
Lindi<br />
Kagera<br />
Rukwa<br />
Tanga<br />
Kilima<br />
Shinyanga<br />
Mara<br />
Mikoa<br />
Pwani<br />
Tabora<br />
Manyara<br />
DSM<br />
Mbeya<br />
Arusha<br />
Mwanza<br />
Iringa<br />
Morogoro<br />
4.31 Fedha zilizotumika<br />
Fedha nyingi zilizotumika ziliwiana na upatikanaji wake kutoka vyanzo mbalimbali ambapo<br />
matumizi makubwa yalikuwa kwa ajili ya PE (32.5%). (Mchoro na. 50).<br />
Mchoro 50: Vyanzo vya Fedha Zilizotumika, 2004<br />
Fedha za Maendeleo<br />
1.7%<br />
Fedha za Halmashauri<br />
0.6%<br />
Vyanzo vingine<br />
6.4%<br />
Cost Sharing<br />
3.5%<br />
Community Health Fund<br />
0.4%<br />
Capitalization<br />
12.6%<br />
PE*<br />
32.5%<br />
Basket Funds<br />
21.3%<br />
OC<br />
21.0%<br />
83
Mkoa wa Morogoro umeongoza kwa kutumia fedha nyingi, ukifuatiwa na mikoa ya Iringa na<br />
Mwanza. Mikoa iliyotumia fedha kidogo zaidi ni Dodoma, Mwanza, Kigoma na Ruvuma.<br />
(Mchoro na 51).<br />
Mchoro 51: Kiasi cha Fedha kilichotumika, 2004<br />
9,000,000,000<br />
8,000,000,000<br />
7,000,000,000<br />
6,000,000,000<br />
5,000,000,000<br />
Tsh<br />
4,000,000,000<br />
3,000,000,000<br />
2,000,000,000<br />
1,000,000,000<br />
-<br />
Kagera<br />
Mtwara<br />
Dodoma<br />
Rukwa<br />
Manyara<br />
Kilimanjaro<br />
Pwani<br />
Lindi<br />
Mikoa<br />
Tabora<br />
Mara<br />
Mwanza<br />
Arusha<br />
Mbeya<br />
Iringa<br />
Morogoro<br />
84
5.0 RIPOTI ZA HOSPITALI ZA RUFAA<br />
5.1 Utangulizi<br />
Hospitali ya Rufaa Bugando (BMC)<br />
Hospitali ya Rufaa Bugando (Bugando Medical Centre) iliyopo Jijini Mwanza inatoa huduma<br />
za kirufaa kwa Kanda ya Ziwa. Inaendeshwa kwa makubaliano ya uendeshaji wa pamoja kati<br />
ya Serikali na Kanisa chini ya Baraza la Maaskofu wa Kikatoliki <strong>Tanzania</strong> ikiwa na Bodi ya<br />
Wadhamini na Kamati ya Utendaji.<br />
Utekelezaji wa maboresho ya huduma za afya uliendelea katika Hospitali ya Bugando katika<br />
mwaka wa 2004. Maboresho hayo yalilenga Ukarabati, Utoaji mafunzo, Utoaji wa Dawa za<br />
Kupunguza Makali ya UKIMWI (ARVs). Ujenzi wa Kituo cha Kanda cha kuhifadhi Damu<br />
salama (Zonal Blood Bank) pamoja na Huduma ya Kutembelea Hospitali (Outreach Services)<br />
Hospitali hii imefanya ukarabati wa ghorofa 5 za Jengo Kuu la Hospitali kwenye maeneo<br />
yanayotumika kwa kutoa huduma kwa wagonjwa. Ukarabati huo uliojumuisha Wodi ya<br />
Wazazi na Chumba cha upasuaji wa Wazazi uligharimu Tshs.142,153,250/= kwa msaada<br />
kutoka Japan/<strong>Tanzania</strong> Food Counterpart Fund<br />
Mafunzo mahali pa kazi yalitolewa kwa wafanyakazi wa hospitali wa vitengo mbalimbali ili<br />
kuboresha huduma zinazotolewa. Aidha, wafanyakazi 45 walipelekwa kwenye mafunzo ya<br />
kujiendeleza vyuoni. Ili kuinua kiwango cha elimu kwa wafanyakazi wasio na elimu ya<br />
sekondari hospitali imeanzisha masomo ya sekondari kwa Wauguzi na watumishi wengine ili<br />
waweze kujipatia elimu hiyo kwenye sehemu yao ya kazi.<br />
Hospitali ya Rufaa ya Bugando ilianza kutoa Dawa za Kupunguza makali ya UKIMWI<br />
mwezi Oktoba 2004. Wananchi wengi wamejitokeza na zoezi linaendelea vizuri. Wagonjwa<br />
1,000 wanahudhuria kliniki kati ya hao 300 ndio wapo kwenye matibabu ya dawa za<br />
kupunguza makali ya UKIMWI. Aidha, huduma za kuzuia maambukizi ya UKIMWI toka<br />
kwa mama kwenda kwa mtoto nazo zinaendelea kupanuka.<br />
Hospitali ya Rufaa ya Bugando imeendelea kukabiliwa na tatizo la upungufu mkubwa wa<br />
watumishi, hasa Madaktari. Kati ya jumla ya madaktari na madaktari bingwa 99 wanaotakiwa<br />
kuwepo, hospitali ina madaktari bingwa na madaktari wa kawaida 49 tu. Aidha, hospitali kwa<br />
sasa haina madaktari bingwa wa watoto na magonjwa ya akili.<br />
Hospitali ya Bugando imeanzisha mpango maalum kwa kuishirikiana na AMREF wa<br />
kupeleka madaktari bingwa kwenye hospitali za Mikoa ya Kagera, Kigoma, Shinyanga na<br />
Mwanza kila mwezi ili kutoa huduma za ubingwa.<br />
Katika eneo la hospitali pia vipo vyuo vya afya 6 na Chuo Kikuu Kishiriki cha Tiba chenye<br />
wanafunzi 35 (mwaka wa kwanza 25 na mwaka wa pili 10).<br />
Matarajio ya Hospitali ya Rufaa Bugando mwaka 2005/2006<br />
Katika mwaka 2005/06 Hospitali ya Rufaa Bugando itaendelea na juhudi zake za kuboresha<br />
huduma kwa kuendelea na ukarabati wa jengo la hospitali, kuimarisha utoaji wa huduma kwa<br />
wagonjwa na kuendelea na juhudi za kutafuta Madaktari Bingwa na wa kawaida, hasa katika<br />
fani ambazo hazina wataalam hao na zenye upungufu mkubwa.<br />
85
Kilimanjaro Christian Medical Centre (KCMC)<br />
Hospitali hii ya rufaa inamilikiwa na shirika la Msamaria Mwema na inaendeshwa kwa<br />
kushirikiana na Serekali ya <strong>Tanzania</strong>. Mwaka 2004/05 hospitali ya KCMC ilikamilisha<br />
awamu ya kwanza ya upanuzi wa jengo la Idara ya Wagonjwa wa Dharura. Jengo hili pia<br />
linatumika kwa huduma za wagonjwa wa nje, vipimo vya ubongo, mionzi, Famasia, kutunza<br />
kumbukumbu za wagonjwa na huduma ya afya kazini. Pia Jengo la Bio-Techonolojia kwa<br />
ajili ya utafiti wa Malaria lilizinduliwa.<br />
Aidha hospitali imepokea vifaa vipya kwa ajili ya Kitengo cha Endoscopy vyenye thamani ya<br />
shilingi milioni 300 pamoja na kununua mashine ya kufulia. Katika kipindi hicho hospitali<br />
ilianza uzalishaji wa hewa ya oxygen na hivyo kuondokana na gharama za ununuzi wa hewa<br />
hiyo na ina uwezo wa kutoa huduma kwa hospitali za mikoa ya Arusha, Kilimanjaro,<br />
Manyara na Tanga kwa malipo.<br />
Hospitali ya KCMC ilifanya upasuaji wa kwanza wa wagonjwa wa moyo 13. Upasuaji huo<br />
ulifanywa na madaktari wa hospitali hiyo kwa kushirikiana na madaktari kutoka Florida<br />
Merekani.<br />
Mwaka 2004/05, mafunzo ya uganga yaliendelea kuongezeka katika Chuo Kikuu cha Tiba<br />
(KCMC College) kama ifuatavyo, mwaka wa kwanza wanafunzi 38, wa pili 27, wa tatu 24,<br />
wa nne 26 na wa tano 15. Pia kumekuwepo na ongezeka la madaktari wanaochukua mafunzo<br />
ya ubingwa hadi kufikia 87.<br />
Matarajio ya Hospitali ya KCMC mwaka 2005/2006<br />
Mwaka 2005/06, hospitali ya KCMC inatarajia kuwapeleka madaktari wa upasuaji, nusu<br />
kaputi na wauguzi kwenye mafunzo ya muda mfupi ili kupata taaluma zaidi ya upasuaji wa<br />
moyo. Kwa kushirikiana na Harvad University Merekani, CIPRA/Duke University na<br />
London School of Hygiene and Tropical Medicine, hospitali itaendelea na utafiti wa<br />
magonjwa ya Malaria na UKIMWI.<br />
Hospitali itaimarisha huduma za wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kwa<br />
kuteua mratibu ambaye atahakikisha shughuli zote za mfuko zinaratibiwa. Aidha, itapanua<br />
huduma kwa wagonjwa wa UKIMWI kufuatia kukamilika kwa majengo ya wagonjwa wa<br />
nje.<br />
Aidha, Chuo Kikuu cha KCMC kinatarajia kuongeza nafasi za masomo ya udaktari ili<br />
kuongeza idadi yao hapa nchini kulingana na ufadhili wa Serekali.<br />
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH)<br />
Hii ni hospitali pekee ya Taifa chini ya Wizara ya Afya yenye Bodi ya Wadhamini na<br />
shughuli zake kusimamiwa na Mkurugenzi Mkuu Mtendaji. Majukumu ya hospitali hii ya<br />
rufaa ni pamoja na kutoa huduma za tiba za ngazi ya ubingwa (tertiary care ) na kufanya<br />
utafiti wa magonjwa.<br />
86
Taarifa ya ujenzi na ukarabati wa majengo mbalimbali ulioanza mwaka 2003/2004 ni kama<br />
ifuatavyo:<br />
Ujenzi wa jengo la watoto bado unaendelea, awamu ya kwanza ya ghorofa tatu<br />
umeshakamilika kwa kiasi kikubwa.<br />
Sehemu zilizokamilika zimeshaanza kutumika kama maabara, chumba cha wagonjwa<br />
mahututi, vyumba vya upasuaji, wodi za wagonjwa n.k. Wizara inafuatilia kibali cha<br />
kuendelea na ujenzi kwa kutumia mkandarasi yule yule kutoka Central Tender Board<br />
Mradi unaofadhiliwa na Benki ya Africa unaendelea vizuri ambapo jengo la Sewahaji<br />
limeshakamilika na linatumika. Kazi imeanza kwenye jengo la Kibasila, jengo la upasuaji na<br />
X-ray. Jengo la upasuaji katika kitengo cha akina mama litakamilika mwezi Mei na kuanza<br />
kutumika mwezi Juni 2005.<br />
Majengo mengine yaliyopo kwenye hatua za mwisho kukamilika ni pamoja na Karakana ya<br />
matengenezo, banda la mashine za kuchomea taka, nyumba ya kuhifadhia maiti, vibanda vya<br />
vituo vya umeme pamoja na majenereta. Njia za maji safi, maji taka, umeme na barabara zipo<br />
kwenye hatua nzuri. Pamoja na ukarabati unaoendelea pia mashine 10 mpya za ufuaji,<br />
mashine moja ya kutakasa vifaa na mashine ya kuchomea taka hatari zimefungwa na<br />
zinafanya kazi.<br />
Mradi unaofadhiliwa na Abbott Laboratories unahusu kukarabati maabara kuu, ujenzi wa<br />
jengo jipya la mapokezi OPD na kuwekewa vifaa vipya vya kufanyia kazi pamoja na kujenga<br />
ukuta kuzunguka eneo lote la Muhimbili. Mradi huu unatagemewa kukamilika mwezi Mei<br />
2005.<br />
Pamoja na hayo, mfadhili amegharamia ukarabati wa nyumba moja, jengo la usalama, paa la<br />
jengo la ufuaji, vifaa vya ulinzi kama radio call, mtandao wa mawasiliano,<br />
“Computerization” pamoja na ukarabati wa jengo la madaktari wanafunzi. Mategemeo ni<br />
kuwa, mwaka huu jengo la utawala litakarabatiwa, mtambo wa simu utawekwa na ujenzi wa<br />
jengo jipya la stoo ya kutunzia vifaa na madawa utaanza.<br />
Ujenzi wa jengo la ushauri nasaha umegharimiwa na Serikali ya <strong>Tanzania</strong>, JICA, na CDC.<br />
Jengo hili limeshakamilika na baadhi ya sehemu zimeanza kutumika.<br />
Matarajio ya Hospitali ya Rufaa Muhimbili mwaka 2005/2006<br />
Mwaka 2005/06 Hospitali ya taifa Muhimbili itaimarisha huduma za tiba kwa wananchi<br />
ikiwa ni pamoja na wagonjwa wa UKIMWI kulingana na mpango wa Taifa wa kudhibiti<br />
UKIMWI kwa kushirikiana na Centre for Disease Control (CDC) Merekani, Columbia<br />
University na Abbott/Axios.<br />
Ujenzi wa Jengo la wodi ya watoto utakamilishwa na baadhi ya vifaa vinavyohitajika<br />
vitanunuliwa ili kuliwezesha jengo hilo kufanya kazi. Aidha, ukarabati wa jengo la Kibasila ,<br />
upasuaji na X-ray utakamilika. Ukarabati wa majengo ya Mwaisela na Wazazi utaanza.<br />
Utengenezaji wa njia za maji safi, maji taka, umeme na barabara utaendelezwa. Ukarabati wa<br />
maabara kuu, ujenzi wa ukuta kuzunguka eneo la Muhimbili pamoja na jengo la mapokezi<br />
kwa msaada wa Abbott Laboratorie utakamilika.<br />
Pia hospitali inatarajia kuanza kutumia muundo mpya wa utumishi mwaka 2005/06.<br />
87
Hospitali ya Rufaa Mbeya (MRH)<br />
Hospitali hii ni hospitali ya rufaa chini ya Wizara ya Afya kwa Kanda ya Nyanda za Juu<br />
Kusini.<br />
Hospitali imegawanyika katika sehemu mbili, sehemu kuu ambayo ipo katikati ya mji wa<br />
Mbeya na kitengo cha magonjwa ya Akina Mama (obstetric and gynaecology) kilichopo eneo<br />
la Meta kilombeta 3 toka ilipo hospitali kuu. Pamoja na kutoa huduma za tiba za kirufaa,<br />
hushughulika na kufundisha wataalam mbalimbali wa afya na kufanya tafiti mbalimbali ili<br />
kubaini vyanzo vya matatizo. Hospitali ina Bodi ya Ushauri na inaendeshwa na Kamati ya<br />
Uongozi wa Hospitali.<br />
Mwaka wa fedha 2004/05 miradi ifuatayo ilitekelezwa:-<br />
• Ujenzi wa wodi ya wagonjwa mahututi (ICU) ambayo inatarajia kugharimu Sh.<br />
76,000,000/=<br />
• Ujenzi wa uzio wa ukuta katika eneo la kijiji cha ukarabati wa wagonjwa wa akili<br />
Uyole, kazi hiyo itafanywa kwa gharama ya Sh. 78,203,140/= -<br />
• Ununuzi wa mitambo ya nguvu za jua (Solar Heating System) kwa ajili ya hospitali<br />
ya Meta utagharimu Sh. 65,191,200<br />
• Michoro kwa ajili ya Ujenzi wa hosteli ya madaktari walio katika mazoezi na<br />
upanuzi wa jengo la maabara imekamilika na taratibu za kupata wakandarasi wa<br />
kufanya kazi hizo zinaendelea kufanywa<br />
• Ununuzi wa samani kwa ajili ya wodi ya wagonjwa mahututi unatekelezwa kupitia<br />
MSD<br />
• Ujenzi wa kituo cha mafunzo na matibabu ya wagonjwa wa UKIMWI na kufundishia<br />
wafanyakazi wa afya katika masuala ya kuwahudumia wagonjwa wa UKIMWI<br />
• Ujenzi wa jengo kwa ajili ya utafiti wa chanjo ya ugonjwa wa UKIMWI yaani<br />
“Vaccine Trial Center”. Mradi huu umefadhiliwa na Serikali ya Ujerumani.<br />
Matarajio ya Hospitali ya Mbeya Rufaa mwaka 2005/2006<br />
Mwaka 2005/06 Hospitali ya Rufaa Mbeya imepanga kufanya yafuatayo:<br />
• Kukamilisha ukarabati wa wodi za hospitali kuu<br />
• Kukamilisha ujenzi wa hosteli ya Intern doctors<br />
• Upanuzi wa maabara ya hospitali<br />
• Kuanza ujenzi wa kituo cha mafunzo, utafiti wa chanjo na matibabu ya ugonjwa wa<br />
UKIMWI<br />
• Kuimarisha sehemu ya kuhifadhia kumbukumbu za wagonjwa<br />
• Kuanza kutumia huduma kutoka sekta binafsi katika maeneo ya ulinzi, usafi wa nje<br />
na ufuaji nguo.<br />
88
5.2 Ripoti ya Huduma zilizotolewa hospitali za Rufaa mwaka 2004<br />
5.2.1 Mahudhurio ya Nje (OPD)<br />
Kwa mwaka 2004 mahudhurio ya nje (OPD) kwa kufuata umri yamekuwa ya idadi ndogo<br />
kwa Hospitali ya Bugando ikilinganishwa na hospitali nyingine (MNH, Mbeya Rufaa na<br />
KCMC). (Mchoro na. 1).<br />
Mchoro 1: Mahudhurio ya nje (OPD) kwa kufuata umri<br />
600000<br />
536175<br />
500000<br />
400000<br />
336661<br />
Idadi 300000<br />
263223<br />
195512<br />
200000<br />
100000<br />
72510<br />
40928<br />
100221<br />
6455<br />
62658 69113<br />
59675<br />
30642<br />
90317<br />
0<br />
Total Muhimbili KCMC Bugando Mbeya<br />
Hospital<br />
Miaka
5.2.2 Wagonjwa Waliolazwa (IPD)<br />
Jedwali namba 1 linaonyesha mahudhurio ya ndani (IPD) likijumuisha idadi ya vitanda,<br />
wagonjwa waliolazwa, utumiaji wa vitanda, wastani wa mgonjwa kukaa hospitalini na kasi<br />
ya vifo kwa idara katika hospitali za rufaa mwaka 2004. Hospitali ya MNH haikutoa<br />
takwimu hizi.<br />
Jedwali na. 1: Hali ya wodi na vitanda katika hospitali zote za rufaa nchini<br />
Idadi ya<br />
Idadi ya waliolazwa kwa Average Days of Bed occupancy Uwiano(%) wa<br />
No. Wodi/Idara<br />
vitanda mwaka<br />
stay in Hospitals rate<br />
vifo kwa Idara<br />
1 Internal Medicine 476 19338 9 63% 15%<br />
2 Upasuaji 410 12700 16 77% 6%<br />
3 Watoto 358 14767 7 53% 11%<br />
4 Neonatal 191 12119 9 66% 18%<br />
5 Orthopaedic 99 3407 7 77% 1%<br />
6 Macho (Eye) 147 4432 16 42% 0%<br />
7 ENT 47 2128 2 29% 1%<br />
8 Dental 7 486 0 0% 0%<br />
9 Psychiatry 152 2675 56 37% 2%<br />
10 Wazazi (Obstetrics) 460 41333 3 72% 3%<br />
11 Gynecology 161 8243 12 51% 3%<br />
12 Urology 94 3082 4 30% 5%<br />
13 Kifua kikuu (TB) 81 354 1 17% 16%<br />
14 ICU 53 643 11 44% 31%<br />
16 VVF 50 247 0 0% 0%<br />
17 VIP Ward 11 107 0 1% 0%<br />
Jumla 2004 2,797 126,061 9 39% 113%<br />
5.2.3 Magonjwa yaliyojitokeza kwa wingi kwa Mahudhurio ya Nje (OPD)<br />
Mchoro na 3 unaonyesha magonjwa yaliyojitokeza kwa wingi kwa mahudhurio ya nje (OPD)<br />
ni Malaria, Pneumonia, Diarrhoea Diseases, Anaemia, Hypertension na Dental Caries kwa<br />
hospitali za Bugando na Mbeya Rufaa. KCMC ni Malaria, ARI, UTI na Hypertension. Kwa<br />
Hospitali ya Taifa Muhimbili magonjwa yaliyoongoza ni Dental caries, Anaemia,<br />
Hypertension, BPH, Disorders of the Ear na UTI.<br />
90
Mchoro 3: Magonjw a yaliyojitokeza kw a w ingi kw a mahudhurio ya nje (OPD) katika Hospitali za Rufaa<br />
Mw aka 2004<br />
45<br />
40<br />
35<br />
30<br />
Idadi %<br />
25<br />
20<br />
15<br />
10<br />
5<br />
0<br />
Malaria<br />
Pneumonia<br />
ARI<br />
Diarrhoeal Diseases<br />
Hypertension<br />
UTI<br />
Ugonjwa<br />
Dental Caries<br />
Fractures<br />
Anaemia<br />
HIV/AIDS<br />
TB<br />
Bugando KCMC MNH Mbeya<br />
Kwa Hospitali ya Taifa Muhimbili, kwa mahudhurio ya OPD takwimu za magonjwa ya ARI<br />
na Diarrhoeal Diseases hazikupatikana wakati wa kuandaa hizi takwimu kutokana na baadhi<br />
ya kumbukumbu kutoonekana.<br />
5.2.4 Magonjwa Kumi yaliyoongoza kwa Mahudhurio ya Nje (OPD)<br />
Magonjwa yaliyoongoza kwa mahudhurio ya nje (OPD) kwa hospitali za rufaa bado ni<br />
Malaria, Pneumonia, Anaemia, Kifua Kikuu, Intestinal Worms, na ARI. (Mchoro na. 4).<br />
Mchoro 4: Magonjwa yaliyoongoza kwa mahudhurio ya nje (OPD)<br />
50<br />
45<br />
40<br />
35<br />
30<br />
Idadi % 25<br />
20<br />
15<br />
10<br />
5<br />
0<br />
Malaria<br />
Pneumonia<br />
Anaemia<br />
Pulmonary<br />
Tuberculosis<br />
Intestinal Worms<br />
ARI<br />
Magonjwa<br />
Diarrheal Diseases<br />
Fractures<br />
UTI<br />
Refractive Error<br />
91
5.2.5 Magonjwa yaliyojitokeza kwa Wagonjwa wa Ndani (IPD) kwa ujumla<br />
Magonjwa yaliyojitokeza zaidi kwa wagonjwa wa ndani (IPD) kwa ujumla kwa hospitali zote<br />
ni Labour pains, Malaria, Pneumonia, Fractures, HIV/AIDS, Anaemia na Hypertension.<br />
(Mchoro na. 5).<br />
Mchoro 5: Magonjwa yaliyoongoza kwa wagonjwa wa ndani (IPD)<br />
35<br />
30<br />
25<br />
Idadi %<br />
20<br />
15<br />
10<br />
`<br />
5<br />
0<br />
Labour pains<br />
Malaria<br />
Pneumonia<br />
Fractures<br />
HIV/AIDS<br />
PTB<br />
Magonjwa<br />
Anaemia<br />
Hypertension<br />
Diabetes Mellitus<br />
Heart Failure<br />
Bugando KCMC Muhimbili Mbeya<br />
5.2.6 Magonjwa yaliyojitokeza kwa Wagonjwa waliolazwa Idara ya “Internal Medicine”<br />
Magonjwa yaliyojitokeza zaidi kwa wagonjwa waliolazwa Idara ya Internal Medicine ni<br />
Malaria, Pneumonia, HIV/AIDS, na Hypertension. (Mchoro na. 6).<br />
7000<br />
Mchoro 6: Magonjwa yaliyoongoza kwa kulazwa na vifo vingi idara ya Internal Medicine<br />
6086<br />
6000<br />
5000<br />
4000<br />
idadi<br />
3000<br />
2447<br />
2439<br />
2000<br />
1000<br />
0<br />
481<br />
336<br />
792<br />
1404<br />
154<br />
1193<br />
233<br />
1039<br />
110<br />
985<br />
161<br />
785<br />
100<br />
772<br />
131<br />
741<br />
134<br />
Malaria<br />
Pneumonia<br />
HIV/AIDS<br />
Idadi<br />
Hypertension<br />
Vifo<br />
PTB<br />
Diarrhoea Diseases<br />
Magonjwa<br />
Diabetes<br />
Malignancies<br />
Anaemia<br />
CCF<br />
92
5.2.7 Magonjwa yaliyojitokeza kwa Wagonjwa waliolazwa Wodi ya Upasuaji<br />
Magonjwa yaliyojitokeza zaidi kwa wagojwa waliolazwa wodi ya upasuaji ni Fractures<br />
Injuries excluding fractures, dislocation, sprains and strains, Intestinal Obstruction, Hernias,<br />
Peptic Ulcer, Abdominal Malignancy, na Chest Trauma. (Mchoro na. 7).<br />
Mchoro 7: Magonjw a yaliyojitokeza kw a w ingi na vifo w odi za upasuaji<br />
Fractures<br />
Injury excluding fractures, dislocation, sprains and strains<br />
Intestinal Obstruction<br />
Hernias<br />
Peptic Ulcer Disease<br />
Idadi<br />
Abdominal Malignancy<br />
Portal Hypertention<br />
BPH<br />
Head injury<br />
Goiter<br />
Foreign body in the ENT<br />
Malignacy of genital organs<br />
0 100 200 300 400 500 600 700 800 900 1000<br />
Magonjwa<br />
5.2.8 Huduma za Upasuaji<br />
Wagonjwa<br />
Vifo<br />
Kwa hospitali zote za Rufaa vyumba vyote vya upasuaji ni “Non dedicated” na idadi ya<br />
upasuaji mkubwa na mdogo uliofanyika ni kama inavyoonekana katika Mchoro na. 8.<br />
Mchoro 8: Idadi ya vyumba vya upasuaji na aina ya upasuaji iliyofanyika<br />
9000<br />
8000<br />
7285<br />
8109<br />
7000<br />
6000<br />
5151<br />
5640<br />
5000<br />
idadi<br />
4000<br />
3000<br />
2515<br />
2000<br />
1000<br />
0<br />
5 9 14<br />
Idadi ya vyumba vya<br />
upasuaji<br />
Upasuaji Mkubwa<br />
1437<br />
529 629<br />
Aina ya upasuaji<br />
Upasuaji Mdogo<br />
1076<br />
Jumla ya upasuaji<br />
Bugando KCMC Muhimbili Mbeya<br />
93
Upasuaji mkubwa uliofanyika ulifanyika katika Idara za Obstetrics na Gynaecology (47%),<br />
Orthopedic (16%), General Surgery (14%) VVF/RVF (4%) na Opthalmology (2%). (Mchoro<br />
na. 9).<br />
Mchoro 9: Upasuaji Mkubwa uliofanyika<br />
Plasti Surgery<br />
0%<br />
Neurology<br />
0%<br />
Others<br />
0%<br />
VVF/RVF<br />
4%<br />
Ophthalmology<br />
2%<br />
General Surgery<br />
14%<br />
ENT<br />
9%<br />
Paediatic Surgery<br />
0%<br />
Orthopaedic<br />
16%<br />
Urology<br />
8%<br />
Obs and Gynnaecology<br />
47%<br />
Upasuaji mdogo uliofanyika ulikuwa Evacuation (20%), EUA (18%), Incision and Biopsy<br />
(14%), Reduction and PoP (8%) na Excision (8%). (Mchoro na. 10).<br />
Mchoro 10: Upasuaji mdogo uliofanyika<br />
UWSD<br />
5%<br />
Suprapubic Catheter<br />
4%<br />
Bougnage<br />
4%<br />
Oesophagascopy<br />
2%<br />
Anal Dilation<br />
1%<br />
Evacuation<br />
20%<br />
Circumcision<br />
4%<br />
Foreign Body Removal<br />
6%<br />
Screw and Pin removal<br />
6%<br />
EUA<br />
18%<br />
Excision<br />
8%<br />
Reduction and PoP<br />
8%<br />
Insision and Biopsy<br />
14%<br />
94
5.2.9 Magonjwa ya Akina Mama (Gynaecology)<br />
Magonjwa yaliyoongoza kwa magonjwa ya akina mama ni Pelvic Inflammatory Disease,<br />
Infertility na Uterine Fibroid kwa hospitali za Bugando na Mbeya Rufaa. Magonjwa ya<br />
Uterine fibroid, Carcinoma of the Cervix na Infertility yalioongoza kwa Hospitali ya KCMC.<br />
Kwa Hospitali ya Taifa Muhimbili ni Malignant Neoplasm, Ectopic Pregnancy, Infertility na<br />
Pelvic Inflammatory Disease. (Mchoro na. 11).<br />
Mchoro 11: Magonjwa ya akina mama (gynaecology)<br />
1600<br />
1400<br />
1200<br />
1000<br />
Idadi<br />
800<br />
600<br />
400<br />
200<br />
0<br />
Uterine Fibroid<br />
Infertility<br />
Adnexial Cyst<br />
Carcinoma of the<br />
Cervix<br />
Magonjwa<br />
Pelvic Inflammatory<br />
Disease<br />
Ovarian Tumors<br />
Genital Prolapse<br />
BUGANDO KCMC MNH MBE<strong>YA</strong><br />
5.2.10 Sababu za kulazwa Mama Wajawazito<br />
Sababu zilizoongoza katika kulazwa mama wajawazito ni Deliveries (89%), Abortions (6%),<br />
Malaria in Pregnancy (1%) na Ectopic Pregnancy (1%). (Mchoro na. 12).<br />
Mchoro 12: Sababu za kulazwa mama wajawazito<br />
Pelivic Inflamatory disease<br />
3%<br />
Malaria in pregnancy<br />
1%<br />
Hyperemesis gravidarum<br />
0%<br />
Anaemia<br />
0%<br />
Ectopic pregnancy<br />
1%<br />
Abortions<br />
6%<br />
Deliveries<br />
89%<br />
Takwimu za Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa magonjwa ya Malaria in Pregnancy, Pelvic<br />
Inflammatory Disease, na Ectopic Pregnancy hazikupatikana kwa kukosekana kwa<br />
kumbukumbu wakati takwimu zinaandaliwa.<br />
95
5.2.11 Kujifungua Mama Wajawazito<br />
Kuhusu kujifungua mama wajawazito zaidi ya asilimia 99 ya wale walioripotiwa<br />
walijifungulia hospitalini kwa hospitali zote. (Mchoro na. 13).<br />
Mchoro 13: Kujifungua Mama wajawazito<br />
BBAs<br />
1%<br />
TBAs<br />
0%<br />
Others (Taja)<br />
0%<br />
Hospitali<br />
99%<br />
Hospitali BBAs TBAs Others (Taja)<br />
5.2.12 Aina ya kujifungua Mama Wajawazito<br />
Kuhusu aina ya kujifungua mama wajawazito, wengi wa akina mama walijifungua kwa njia<br />
ya kawaida Spontaneous Vaginal Delivery ikifuatiwa na upasuaji (Caesarian Section) na<br />
Vacuum Extraction (Mchoro na. 14).<br />
Mchoro 14: Aina ya kujifungua mama wajawazito<br />
Forceps delivery<br />
0%<br />
Breech extraction<br />
2%<br />
Destructive procedures<br />
0%<br />
Others<br />
0%<br />
Vacuum extraction<br />
7%<br />
Caesarian section<br />
24%<br />
Spontaneous vaginal delivery<br />
67%<br />
Idadi ya akinamama waliojifungulia hospitali Bugando (5,451), KCMC (2,834), Muhimbili<br />
(11,530) na Mbeya (6,792) hailingani na idadi ya aina ya kujifungua kwa hospitali zote<br />
Bugando (6,989), KCMC (2,767), Muhimbili (11,414) na Mbeya (6,631). Hii ni kutokana na<br />
baadhi ya kumbukumbu kutopatikana.<br />
96
5.2.13 Matokeo ya kujifungua Mama Wajawazito<br />
Matokeo ya kujifungua akina mama wajawazito ni kuwa, akina mama 18,470 walijifungua<br />
kawaida na watoto 24,782 walizaliwa hai. Watoto 5,790 walikuwa na matatizo (Macerated<br />
Still Birth, Fresh Still Birth, Pre-term Babies na Underweight ≤ 2.5 kg. (Mchoro na. 15).<br />
Mchoro 15: Matokeo ya kujifungua mama wajawazito<br />
12000<br />
10000<br />
8000<br />
Idadi<br />
6000<br />
4000<br />
2000<br />
0<br />
Normal Deliveries<br />
Born Alive<br />
Macerated Still Birth<br />
Fresh Still Birth<br />
Pre-term Babies<br />
Under weight < 2.5<br />
kg<br />
Ruptured Uterus<br />
Aina ya matokeo<br />
BUGANDO KCMC MNH MBE<strong>YA</strong><br />
5.2.14 Sababu za Vifo vya Mama Wajawazito<br />
Tatizo la vifo vya akinamama wajawazito katika hospitali za rufaa bado ni kubwa kwa vile<br />
katika kipindi cha mwaka 2004 pekee hospitali zimeripoti jumla ya akinamama 533 walifariki<br />
kutokana na matatizo ya uzazi. Septicaemia iliongoza kwa 17%, PPH 15%, Pneuomonia<br />
11%, Eclampsia 10% na HIV/AIDS 5% kama inavyoonyeshwa katika Mchoro na. 16.<br />
Mchoro 16: Sababu za vifo mama wajawazito<br />
18<br />
17<br />
16<br />
15<br />
14<br />
12<br />
11<br />
10<br />
10<br />
Asilimia %<br />
8<br />
6<br />
8 7<br />
7<br />
6<br />
5<br />
4<br />
2<br />
3<br />
2 2 2 2 2<br />
2<br />
1 1<br />
0<br />
Septicaemia<br />
PPH<br />
Pneumonia<br />
Eclampsia<br />
Anaemia<br />
Obstructed Labour<br />
Malaria<br />
APH<br />
HIV/AIDS<br />
Pulmonary Oedema<br />
Meningitis<br />
Magonjwa<br />
Ruptured uterus<br />
Septic Abortion<br />
EPH Gestosis<br />
Puerperal Sepsis<br />
Unsafe Abortion<br />
Anaesthesis Accidents<br />
Others<br />
Kuhusu idadi ya vifo vya akina mama wajawazito, hospitali ya Bugando inaongoza kwa idadi<br />
kubwa. Sababu zilizoongoza kwa vifo vya akina mama wajawazito kwa hospitali zote ni<br />
Pneumonia, PPH, Malaria, Anaemia, Septecaemia pamoja na HIV/AIDS.<br />
97
5.2.15 Sababu za kulazwa na vifo wodi za watoto<br />
Sababu zilizoongoza kwa kulazwa na vifo kwa watoto kwa hospitali zote ni Malaria,<br />
Pneumonia, Diarrhoea, Malnutrition, PTB na Prematurity (Mchoro na. 17). Takwimu kutoka<br />
hospitali ya Taifa Muhimbili hazina ripoti ya ugonjwa ya Diarrhoea kwa vile wagonjwa<br />
hawapo na wodi 17 iliyokuwa ikitumiwa kwa ajili hiyo inatumika kwa wagonjwa wengine.<br />
Mchoro 17: Sababu za kulazwa watoto wodi za watoto<br />
PTB<br />
1%<br />
Dysentery<br />
1%<br />
Septicaemia<br />
2%<br />
Birth Asphyxia<br />
3%<br />
Gastroenteritis<br />
1%<br />
ARC<br />
1%<br />
Pre – maturity<br />
3%<br />
Malaria<br />
35%<br />
Malnutrition<br />
11%<br />
Paediatric AIDS<br />
3%<br />
Anaemia<br />
13%<br />
Acute Watery Diarrhoea<br />
12%<br />
Pneumonia<br />
14%<br />
5.2.16 Sababu ya Vifo vya Watoto wa umri chini ya mwaka mmoja<br />
Takwimu zilizokusanywa mwaka 2004 zinaonyesha kuwa sababu zilizoongoza kwa vifo<br />
vya watoto wa umri chini ya mwaka mmoja kwa hospitali zote ni:- Malaria,<br />
Pneumonia, Diarrhoea, Anaemia Pediatric AIDS na Malnutrition. Hospitali ya Taifa<br />
Muhimbili haikutoa takwimu kwa magonjwa ya Diarrhoea, Septicaemia, na Birth<br />
Asyphyxia kwa vile kumbukumbu hazikupatikana. (Mchoro na. 18).<br />
Mchoro 18: Vifo vya watoto chini ya mwaka mmoja<br />
25<br />
20<br />
Asilimia %<br />
15<br />
10<br />
5<br />
0<br />
Malaria<br />
Pneumonia<br />
Acute Watery<br />
Diarrhoea<br />
Anaemia<br />
Padiatric AIDS<br />
Malnutrition<br />
Pre – maturity<br />
PTB<br />
Magonjwa<br />
Septicaemia<br />
Birth Asphyxia<br />
Gastroenteritis<br />
ARC<br />
Others (Taja)<br />
Congenital<br />
Abnormalities<br />
98
5.2.17 Magonjwa ya Macho kwa waliolazwa<br />
Jumla ya wagonjwa 3079 walilazwa kwa magonjwa ya macho. Ugonjwa wa Cataract<br />
uliongoza kwa 70% ya wagonjwa wote ukifuatiwa na Trauma 12%, Trachoma 5%,<br />
Retinal/Optic disease 3% na mengine kama inavyoonyeshwa katika Mchoro na. 19.<br />
Mchoro 19; Waliolazwa magonjwa ya macho<br />
Trachoma<br />
0%<br />
Glaucoma<br />
5%<br />
Others<br />
1%<br />
Retinal/Optic Disease<br />
2%<br />
Corneal Ulcers<br />
3%<br />
Corneal perforation<br />
1%<br />
Uveitis<br />
1%<br />
Endophthalmitis<br />
1%<br />
Hyphaema<br />
1%<br />
Orbital Cellulitis<br />
1%<br />
Malignancy<br />
2%<br />
Trauma<br />
12%<br />
Cataract<br />
70%<br />
5.2.18 Magonjwa ya Akili kwa waliolazwa<br />
Jumla ya wagonjwa 1,095 waliripotiwa kulazwa kwa magonjwa ya akili na kati ya hao<br />
Non organic psyhcosis walikuwa 40%, Alcohol and Schizophrenia 29%, Manic depressive<br />
psychosis 23%, Drug abuse 17% na magonjwa mengine 4%. Hospitali ya KCMC haina wodi<br />
ya wagonjwa wa akili. (Mchoro na. 20).<br />
Mchoro 20: Magonjwa ya akili kwa waliolazwa<br />
Other Mental and behauvioral<br />
disorders<br />
4%<br />
Other unspecified disorders of<br />
the nervous system<br />
3%<br />
Mental deficiency<br />
0%<br />
Schizophrenia<br />
18%<br />
Alcohol and drugs abuse<br />
10%<br />
Epilepsy<br />
5%<br />
Organic brain syndrome<br />
2%<br />
Acute psychosis<br />
2%<br />
Non organic psycosis<br />
25%<br />
Senile Psycosis<br />
2%<br />
Manic depresive psychosis<br />
14%<br />
Alcoholic psychosis<br />
3%<br />
Psychoactive substance use<br />
disorders<br />
10%<br />
Depression<br />
2%<br />
99
5.2.19 Magonjwa ya Kinywa<br />
Katika kipindi cha mwaka 2004 jumla ya wagonjwa 14,780 waliripotiwa kupata huduma ya<br />
matibabu ya magonjwa ya kinywa na kati ya hao 72.8% walikuwa ni kwa ajili ya Dental<br />
Caries, 14.8% Gingivitis and other mucosal conditions, 2.7% Trauma na Periodontal disease<br />
pamoja na magonjwa mengine 7.2%. (Mchoro na. 21).<br />
Mchoro 21: Magonjwa ya kinywa<br />
Lymphadenopathy/Begign<br />
growth<br />
2%<br />
Abscesses<br />
1%<br />
Trauma<br />
7%<br />
Cancer (malignancies)<br />
3%<br />
Post Extraction Bleedind<br />
1%<br />
Cysts<br />
1%<br />
Gingivitis & other mucosal<br />
13%<br />
Ameloblastoma<br />
1%<br />
Scalling<br />
1%<br />
Others<br />
17%<br />
Periodontal disease<br />
7%<br />
Dental caries<br />
46%<br />
5.2.20 Idara ya Vipimo vya Maabara<br />
Idadi ya vipimo vya maabara kwa hospitali zote kwa idara ilikuwa kama inavyoonyeshwa<br />
kwenye Jedwali na 2 na Mchoro na 22.<br />
Jedwali na 2: Idara ya Vipimo vya Maabara<br />
BUGANDO KCMC MNH MBE<strong>YA</strong> RUFAA JUMLA<br />
Idadi Positve Idadi Positve Idadi Positve Idadi Positve Idadi Positive<br />
Clinical Chemistry 27027 2972 21650 3069 30367 5683 84727 6041<br />
Hematology 41278 27326 1528 95200 44651 19 208455 1547<br />
Microbiology 4226 1298 6802 76 3709 2664 574 17401 1948<br />
Serology 18736 3900 8486 1246 6160 17134 70 50516 5216<br />
Parasitology 30320 5260 14842 46 8990 18647 2849 72799 8155<br />
Histopathology 3051 0 7880 6681 4228 21840 0<br />
100
Mchoro na. 22 unaonyesha huduma mbalimbali zilizotolewa Idara ya Maabara katika<br />
hospitali zote za rufaa.<br />
Mchoro 22: Huduma mbalimbali zilizotolewa idara ya maabara<br />
100000<br />
90000<br />
80000<br />
70000<br />
60000<br />
Idadi<br />
50000<br />
40000<br />
30000<br />
20000<br />
10000<br />
0<br />
Bugando (Idadi) Bugando<br />
(Positive)<br />
KCM C (Idadi) KCM C<br />
M NH (Idadi) M NH<br />
(Positive)<br />
(Positive)<br />
Hospital<br />
M BE<strong>YA</strong> (Idadi) M BE<strong>YA</strong><br />
(Positive)<br />
Clinical Chemistry Hematology Microbiology Serology Parasitology Histopathology<br />
5.2.21: Takwimu za Damu Salama<br />
Hospitali ya Bugando ilioongoza katika huduma ya damu salama kwa kukusanya damu<br />
(Blood Donoted) units 4,451 ambapo units 4,420 walioongezwa wagonjwa. (Mchoro na. 23).<br />
Mchoro 23: Takwimu za Damu Salaama<br />
16000<br />
14000<br />
12000<br />
10000<br />
idadi<br />
8000<br />
6000<br />
4000<br />
2000<br />
0<br />
Blood Donated (Units) Blood Transfusion<br />
(Units)<br />
Blood Grouping (Units)<br />
huduma zilizotolewa<br />
Blood Grouping<br />
(Patients)<br />
Cross Matching (Units)<br />
BUGANDO KCMC MNH MBE<strong>YA</strong><br />
101
5.2.22: Takwimu za X-ray zilizopigwa<br />
Idadi kubwa ya X-ray zilizopigwa kwa hospitali zote ni Chest, Spine, Skull, Extremities pamoja<br />
na Abdomen. (Mchoro na. 24). Hospitali za Bugando, Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na<br />
Mbeya Rufaa hazikutoa idadi ya Contrast Studies zilizofanyika.<br />
Mchoro 24: Idadi ya X - ray zilizopigwa<br />
0 20 40 60 80<br />
Chest<br />
Extremeties<br />
Spine<br />
Skull<br />
Contrast studies<br />
Pelvis<br />
Abdomen<br />
Others (Taja)<br />
Legs<br />
Shoulder<br />
Hip Joint<br />
Femor<br />
Barium Studies<br />
Idadi %<br />
Magonjwa<br />
5.2.23 Tawimu za kipimo cha Ultrasound<br />
Katika mwaka 2004 jumla ya vipimo 26,139 vya ultrasound vilifanyika katika hospitali za<br />
rufaa. 51% ikiwa ni vya abdomen, 22% Obstetric, 13% Echocardiograms, 8% Pelivic na<br />
vingine kama inavyoonyeshwa kwenye Mchoro na. 25.<br />
Mchoro 25: Utra - sound zilizofanyika<br />
Brest<br />
0%<br />
Musculoskeletal<br />
1%<br />
Thyroid<br />
0%<br />
Urinary Tract<br />
3%<br />
All others<br />
1%<br />
Pelvic<br />
8% Echocardiograms<br />
13%<br />
Brain<br />
1%<br />
Eye<br />
0%<br />
Obstetrics<br />
22%<br />
Abdomen<br />
51%<br />
102
5.2.24 Takwimu za kipimo cha CT Scan<br />
Jumla ya vipimo mbalimbali 2915 vya CT- Scan vilivyofanyika kutoka kwa wagonjwa<br />
mbalimbali waliokuja kuomba huduma hii ikiwa 72% ni Brain, 17% Spine, 7% Abdomen na<br />
3% Chest kama inavyoonyeshwa katika Mchoro na.26.<br />
Mchoro 26: CT - Scan zilizofanyika<br />
Spine<br />
17%<br />
Chest<br />
3%<br />
Orbit<br />
Others Hip<br />
0%<br />
1% 0%<br />
Sinuses<br />
0%<br />
Pelvis<br />
0%<br />
Abdomen<br />
7%<br />
`<br />
Brain<br />
72%<br />
103
5.2.25 Takwimu za Watumishi<br />
Kutokana na idadi ya watumishi waliopo kwenye hospitali za rufaa ikilinganishwa na ikama<br />
pamoja na wale waliopo, upungufu mkubwa upo katika hospitali zote. Zaidi ni kwa kada za<br />
Specialist Doctors (214), Medical Doctors (113), Trained Nurses/Midwives (168), Nursing<br />
officers (678). Hospitali ya Taifa Muhimbili na KCMC pekee hazina Specialist Dental<br />
Surgeons, wanahitajika 8 kwa Hospitali ya Taifa Muhimbili na 2 kwa KCMC. (Jedwali na.<br />
3).<br />
Jedwali na. 3: Watumishi<br />
BUGANDO KCMC MNH MBE<strong>YA</strong> RUFAA<br />
Kada Ikama Waliopo Pungufu Ikama Waliopo Pungufu Ikama Waliopo Pungufu Ikama Waliopo Pungufu<br />
1 Specialist Doctors 16 15 35 117 53 65 142 54 88 43 14 26<br />
2 Medical Doctors 24 21 27 54 22 32 86 51 35 45 16 19<br />
3 Specialist Dental Surgeons 1 1 0 2 0 2 8 0 8 2 2 0<br />
4 Dental Surgeons 0 0 1 2 3 0 2 3 0 2 1 1<br />
5 Clinical psychologist 0 0 6 0 1 0 0 0 0 1 0 1<br />
6 Occupational therapist 0 0 1 17 7 10 9 3 6 1 0 1<br />
7 Pharmacists 6 6 0 6 5 1 13 14 0 4 3 1<br />
8 Chemists 0 0 0 2 0 2 0 0 0 1 0 1<br />
9 Assistant Medical Officers (Anaest) 1 1 7 7 6 1 0 0 0 0 20 0<br />
10 Assistant Dental Officers 2 1 1 0 1 0 0 0 0 2 1 1<br />
11 Nursing Officers 140 140 0 477 184 293 665 310 355 125 95 30<br />
12 Nurse Tutors 0 0 0 0 3 0 0 0 0 0 0 0<br />
13 Trained Nurses/Nurse Midwives 191 181 10 122 138 0 372 318 54 231 127 104<br />
14 Public Health Nurse B 0 0 0 6 0 6 0 0 0 4 4 0<br />
15 Medical Laboratory Technicians 25 23 2 32 15 17 24 15 9 25 12 13<br />
16 Radiographers 6 4 4 8 8 0 19 14 5 8 3 5<br />
17 Dental Technicians 1 1 0 4 1 3 4 2 2 2 0 2<br />
18 Optometry Technicians 2 2 0 7 3 4 2 5 0 6 2 4<br />
19 Orthopedic Technicians 2 2 0 8 7 1 0 0 0 6 1 5<br />
20 Physiotherapists 4 4 0 14 8 6 20 9 11 6 3 3<br />
21 Chemical Laboratory Technicians 0 0 0 0 0 0 14 0 14 2 0 2<br />
22 Health officers 0 0 1 4 0 4 0 0 0 1 0 1<br />
23 Medical Recorders 8 5 8 24 17 7 47 40 7 20 0 20<br />
24 Pharmaceutical Technicians 4 2 6 6 3 3 20 15 5 8 2 6<br />
25 Health Secretaries 2 2 0 2 3 0 0 0 0 2 1 1<br />
26 Accountants 8 8 0 12 20 0 6 6 0 2 1 0<br />
27 Administrative Officers 1 1 0 2 6 0 4 10 0 1 0 0<br />
28 All Others 7 7 5 0 0 0 0 0 0 113 104 0<br />
29 Director of finance and Planning 0 0 1 1 1 0 0 0 0 1 0 1<br />
30 Director of Adim. and HR 0 0 1 1 1 0 0 0 0 1 0 0<br />
31 Social wellfare officers 2 2 0 5 3 2 33 15 18 2 2 0<br />
32 Accounts clerks/Assistants 7 7 0 28 25 3 0 1 0 6 1 3<br />
33 Health Attendants 240 240 0 220 206 14 0 0 0 114 202 0<br />
34 Supplies officers 5 5 0 2 5 0 0 0 0 3 1 0<br />
35 Supplies assistants 2 2 4 12 7 5 0 0 0<br />
35 Others 465 561 0<br />
Jumla 2004 286 281 25 1669 1323 481 1490 885 617 273 314 31<br />
5.2.26 Takwimu za Madaktari Bingwa<br />
Kuna upungufu wa asilimia 55 ya Madaktari bingwa katika hospitali za rufaa ikilinganishwa<br />
na ikama. Takwimu zilizopatikana mwaka 2004 zinaonyesha kuwa kuna madaktari bingwa<br />
132 ikilinganishwa na ikama inayoonyesha madaktari bingwa 287 ambapo Hospitali ya Rufaa<br />
Mbeya ina upungufu mkubwa kwa 66%, Muhimbili 55%, Bugando 63% na KCMC 32%.<br />
(Mchoro na. 27).<br />
104
Mchoro 27: Takwimu za Madaktari Bingwa<br />
140<br />
132<br />
120<br />
100<br />
83<br />
Idadi<br />
80<br />
66<br />
60<br />
48<br />
49<br />
42<br />
47<br />
40<br />
31<br />
21<br />
19<br />
23<br />
16<br />
20<br />
0<br />
Muhimbili KCMC Bugando Mbeya<br />
Hospital<br />
Ikama Waliopo Upungufu<br />
5.2.27 Taarifa ya Fedha za Kuendeshea Huduma<br />
Kwa mwaka 2004/2005, Hospitali ya Taifa Muhimbili na Bugando zilipewa fedha kama<br />
zilivyoidhinishwa. Upungufu ulikuwa mdogo sana ambapo hospitali ya Bugando ilipewa pungufu<br />
kwa 0.5% na Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa 0.2%.<br />
Hospitali ya Mbeya Rufaa ilipewa fedha Tshs 2,490,060,610 pungufu kwa 62% ikilinganishwa na<br />
kiasi kilichoidhinishwa cha Tshs. 4,017,257,580. Hata hivyo hospitali ilipokea Tshs.<br />
1,724,769,966, kati ya hizi zilitumika Tshs. 1,156,572,757 na kubaki kiasi cha Tshs. 568,197,209.<br />
Hospitali ya KCMC ilipewa fedha Tshs. 2,756,548,318 ikiwa ni pungufu kwa 58.5 %<br />
ikilinganishwa na kiasi kilichoidhinishwa cha Tshs.4,711,396,122.<br />
Jumla ya fedha zilizoombwa, zilizopokelewa, upungufu na zilizotumika kwa hospitali zote za<br />
rufaa ni kama inavyoonyeshwa kwenye jedwali na. 4.<br />
Jedwali na. 4: Taarifa ya fedha za kuendeshea Huduma<br />
No. Maelezo Zilizoombwa Zilizopokelewa Upungufu Zilizotumika<br />
1 Ruzuku toka Serikali Kuu (OC) 16840558262 8353934576 2209173296 13550060785<br />
2 Ruzuku toka kwa Miradi ya Maendeleo 3798000000 1114462413 1883537587 1547264461<br />
3 Ruzuku toka Busket Fund 22000000 148000000 0 22000005<br />
4 Ruzuku ya dawa 3455015380 2717852082 139823461 3272846080<br />
5 Ruzuku ya vifaa vya Hospital 96000000 33115290 62884709 0<br />
6 Ruzuku ya Reagents na vifaa vya Maabara 48600000 33531363 15068636 0<br />
7 Ruzuku ya Dental Supplies 12000000 3794262 8205737 0<br />
8 Uchangiaji huduma za Afya 150000000 1047342030 33508237 287038225<br />
9 Capitalization 45415000 39741850 26797800 42249305<br />
10 Mishahara ya Wafanyakazi (PE) 25275644712 19681204219 153249133 25048935854<br />
Vyanzo vingine (Taja) 0 0 0 0<br />
11 Medical equipment 0 147520000 0 0<br />
12 Injection safety 28560000 17000000 11560000 0<br />
13 Blood Bank 35700400 25000000 10700400 0<br />
14 VAS 6422800 6422800 0 0<br />
15 PMTCT 0 5053000 0 0<br />
16 Axios 39340500 22032700 17307800 0<br />
17 IPPM 0 534337037 0 1068674079<br />
18 CT Scan 0 150556500 0 301113005<br />
19 Spec. Paed Lab 0 59515750 0 119031505<br />
20 Others 0 106558564 0 213117133<br />
Jumla 2004 45141860932 28648709517 2584038972 41437825166<br />
105
5.3 Mafanikio na Matatizo katika Hospitali za Rufaa<br />
Hospitali ya Rufaa Bugando<br />
Mafanikio<br />
Hospitali imepewa nafasi 10 za Wauguzi kati ya 20, nafasi 4 za Madaktari kati ya 12<br />
na nafasi 1 ya Madaktari Bingwa kati ya 6 zilizoombwa kwa mwaka 2004/2005.<br />
Hospitali ilipewa fedha toka Serikalini karibu sawa na kiasi kilichoidhinishwa.<br />
Matatizo<br />
Hospitali inakabiliwa na upungufu wa watumishi hasa katika kada za:<br />
• Anaesthesiologist<br />
• Paediatrician<br />
• Pathologist<br />
• Ajali na Dharua na<br />
• Magonjwa ya Akili<br />
Upo upungufu wa vyumba vya upasuaji kwa shughuli maalum za upasuaji<br />
Hospitali ya Rufaa Mbeya<br />
Mafanikio<br />
Hospitali ilipata fedha zote zilizoombwa kwa miradi ya Vit A Supplement toka<br />
UNICEF, PMTCT toka Wizarani na fedha kutoka Axios Foundation zilizotumika<br />
kukarabati jengo la OPD, kuendesha mafunzo ya kujikinga na maambukizi ya<br />
UKIMWI kwa watumishi na ununuzi wa dawa za kupunguza makali ya UKIMWI.<br />
Matatizo<br />
• Upo upungufu mkubwa wa watumishi katika kada za Uuguzi, Medical Records,<br />
Madaktari Bingwa wa Urology, Pediatric Surgery, ENT, Cordiothoracic<br />
Surgery, Plastic Surgery na Technologist<br />
• Reagents hazikupatikana kwa baadhi ya vipimo na ubora wa vipimo<br />
haukuridhisha kutokana na uhaba wa Technologist<br />
• Hakuna CT Scan<br />
• Mashine za kufua nguo za wagonjwa ni chakavu<br />
• Hospitali ilipewa fedha pungufu kwa 62% kulingana na kiasi kilichoidhinishwa.<br />
106
Hospitali ya Taifa Muhimbili<br />
Mafanikio<br />
• Hospitali ilipewa fedha karibu sawa na kiasi kilichoidhinishwa<br />
• Miradi ya maendeleo ya ujenzi na ukarabati ipo katika hatua nzuri<br />
• Wagonjwa wanalipa mara moja kwa huduma zote ikiwa ni katika kupunguza<br />
usumbufu<br />
• Nafasi za uongozi zimejazwa (Directors na Heads of Departments).<br />
Matatizo<br />
• Hospitali inakabiliwa na upungufu mkubwa wa watumishi katika kada za<br />
Specialist Doctors, Medical Doctors, Specialist Dental Surgeons, Nursing<br />
Officers, Trained Nurses/Midwives, Medical Lab. Technicians na<br />
Physiotherapists<br />
• Hospitali ilipewa fedha pungufu kwa 50% ikilinganishwa na kiasi<br />
kilichoainishwa kwenye bajeti<br />
• Wagonjwa wote hawapewi chakula, ni wale tu wa rufaa waliopokelewa na<br />
watoto.<br />
• Huduma zimekuwa zikitolewa kwa shida na kwa kiwango kidogo kutokana na<br />
ujenzi/ukarabati unaoendelea.<br />
107
6.0 RIPOTI ZA HOSPITALI ZA HUDUMA MAALUM<br />
6.1 Hospitali ya Kibong’oto<br />
Katika kipindi cha mwaka 2004, hospitali hii maalum kwa kutibu ugonjwa wa Kifua Kikuu<br />
ilihudumia wagonjwa wa nje 5,518, kati ya hao 2,178 walitibiwa ugonjwa wa Kifua Kikuu<br />
ambapo wenye umri chini ya miaka 5 walikuwa 174 na 2,004 wa umri wa miaka 5 na zaidi.<br />
Kuhusu wagonjwa wanaolazwa, hospitali ina vitanda 300, 256 vya wagonjwa wa Kifua<br />
Kikuu na 44 vya kawaida. Kasi ya kutumia kitanda ilikuwa 63% kwa Kifua Kikuu na 14%<br />
kawaida. Wastani wa kulaza wagonjwa kwa mwezi ni wagonjwa 90 kwa Kifua Kikuu na 30<br />
wa kawaida. Wastani wa siku kwa mgonjwa kukaa hospitali ulikuwa siku 60 kwa Kifua<br />
Kikuu na siku 5 kwa wagonjwa wa kawaida. Kasi ya vifo kutokana na ugonjwa wa Kifua<br />
Kikuu ilikuwa 14% na 15% kwa wagonjwa wa kawaida.<br />
Ugonjwa wa Kifua Kikuu ulioongoza katika magonjwa kwa mahudhurio ya nje (OPD) 49%<br />
ukifuatiwa na ARI (19%), na kwa wagonjwa wa ndani (IPD) Kifua Kikuu (59%) na ARI<br />
(12%) vile vile.<br />
Kuhusu huduma za maabara vipimo 39,462 vilifanyika, 35.2% ya vipimo hivyo ni Blood<br />
slide ikifuatiwa na Clinical haematology 17.2%<br />
Jumla ya X-rays 6,992 zilipigwa ambapo 50.4% zilikuwa za Kifua (Chest) ikifuatiwa na<br />
Upper Limbs 26%.<br />
Kwa mwaka 2004 hospitali ilikuwa na watumishi 183 kwa ujumla ikiwa na upungufu wa<br />
watumishi 92 ikilinganishwa na ikama ambayo ni watumishi 275. Upungufu mkubwa<br />
ulikuwa katika kada za Medical Doctors, Nurisng Officers, Trained Nurses/Midwives,<br />
Radiographers pamoja na Sanitary Labourer<br />
Katika kipindi hiki hospitali ilipokea fedha za kuendeshea huduma Tshs 860,411,848 zikiwa<br />
ni pungufu kwa kiasi cha Tshs 1,707,405,632 ikilinganishwa na kiasi kilichoidhinishwa cha<br />
Tshs 2,567,817,480.<br />
Matarajio ya Hospitali ya Kibongoto mwaka 2005/2006<br />
Mwaka 2005/06, hospitali itaendelea kutoa huduma za tiba kwa wagonjwa wa Kifua Kikuu<br />
na wagonjwa wengine. Hospitali pia itajenga maabara ya kuchunguza vimelea sugu vya<br />
Kifua Kikuu. Aidha, hospitali itakarabati mfumo wa maji taka, wodi tatu pamoja na nyumba<br />
tatu za watumishi.<br />
6.2 Taasisi ya Tiba ya Magonjwa ya Mifupa (MOI)<br />
Kwa kipindi cha mwaka 2004 Taasisi hii inayoshughulikia magonjwa ya mifupa, majeruhi na<br />
mishipa ya fahamu ilihudumia wagonjwa wa nje (OPD) 18669, wagonjwa 2050 wakiwa na<br />
umri chini ya miaka 5 na 16,619 wa umri wa miaka 5 na zaidi.<br />
Taasisi ina vitanda 167 ambapo wastani wa kulaza wagonjwa kwa mwezi ni wagonjwa 557<br />
ikiliganishwa na 548 mwaka 2003 na kasi ya vifo vya wagonjwa ilikuwa 4% ikilinganishwa<br />
na 4.7% mwaka 2003.<br />
108
Ugonjwa ulioongoza kwa mahudhurio ya nje (OPD) ulikuwa Degenerative diseases kwa 65%<br />
wakati ugonjwa uliongoza kwa wagonjwa wa ndani ni fractures of extremities (Upper and<br />
lower limbs) 33% ukifuatiwa na soft tissue injury 21%.<br />
Kuhusu huduma ya upasuaji mwaka 2004 idadi ya upasuaji uliofanyika ni 2011<br />
ikilinganishwa na 1174 mwaka 2003.<br />
Kati ya vipimo vya maabara 9440 vilifyofanyika 56% ni vya clinical haematology<br />
vikifuatiwa na 20% vya clinical chemistry.<br />
Taasisi kwa mwaka 2004 ilikusanya units za damu 102, wagonjwa 2069 waliongezewa damu,<br />
wagonjwa 1623 walitambuliwa makundi yao ya damu (Blood Groups), units 3447 zilifanyiwa<br />
mlinganisho wa makundi ya damu (Cros-matching) na wagonjwa 129 waliongezewa damu<br />
zao wenyewe (autodonation).<br />
Jumla ya X-rays 8386 zilipigwa, 56% kati ya hizi zilikuwa za extremities, 17% spine, 14%<br />
chest na 15% pelvic.<br />
Taasisi ilikuwa na jumla ya watumishi 386 ikiwa na upungufu wa watumishi 100 kulingana<br />
na ikama ambayo ni watumishi 486. Upungufu mkubwa upo katika kada za Senior Doctors,<br />
ICU Nurses, na Casuality Nurses.<br />
Kuhusu fedha za kuendeshea huduma kwa mwaka 2004, kulikuwa na upungufu katika<br />
kipengele kimoja tu cha Ruzuku toka Serikali Kuu (OC) kwa kiasi cha Tshs. 527,632,177<br />
kutokana na Tshs 1,400,000,000 zilizoidhinishwa ambapo zilipokelewa Tshs 872,367,883.<br />
Hapakuwa na upungufu kwa vyanzo vingine vya fedha kwa ujumla kwa vile Taasisi ilipokea<br />
Tshs 4,506,237,410 ikilinganishwa na Tshs 3,761,454,192 zilizoidhinishwa.<br />
Matarajio ya Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) mwaka 2005/2006<br />
Katika mwaka wa 2005/06 Taasisi inatarajia kutoa huduma kwa wagonjwa wa nje wapatao<br />
18,000 kati yao 8,460 (47%) ni wa kulipia na 9,540 ni wa kawaida. Katika kipindi hicho<br />
hicho pia jumla ya wagonjwa 6,560 wanategemewa kupatiwa huduma ya wagonjwa wa<br />
kulazwa, kati yao wagonjwa 760 (12%) watakuwa ni wa kulipia. Aidha, katika kipindi hicho<br />
wagonjwa 2,319 watapatiwa huduma ya upasuaji wa mifupa, ubongo na mishipa ya fahamu<br />
ambao kati yao wagonjwa 587 (25%) watakuwa wa kulipia.<br />
Taasisi pia imedhamiria kutoa tiba ya mazoezi ya viungo kwa wagonjwa wa nje na wa ndani<br />
kwa jumla ya mahudhurio (sessions) 24,200 na kutoa huduma ya viungo bandia 800, huduma<br />
za maabara kwa wagonjwa wa nje na ndani wapatao 15,700, kupiga picha (X-ray) kwa<br />
wagonjwa 20,200 na kuwahudumia wagonjwa mahututi 2,800.<br />
6.3 Hospitali ya Mirembe<br />
Hospitali hii hutuoa huduma za rufaa kwa wagonjwa wa magonjwa ya Akili. Katika mwaka<br />
2004 iliweza kutoa huduma ya wagonjwa wa nje 33,067 na waliolazwa 3,010. Kati ya<br />
wagonjwa waliolazwa wastani wa kukaa hospitali ulikuwa siku 4 kwa wagonjwa wa kawaida,<br />
na siku 31 kwa wagonjwa wa magonjwa ya Akili. Idadi ya vifo vilivyotokea katika mwaka<br />
2004 kwa kwa wagonjwa wa magonjwa ya akili ilikuwa asilima 4.4 ya idadi ya wagonjwa<br />
waliolazwa.<br />
109
Magonjwa ya Akili kumi yaliyoongoza kwa wagonjwa waliolazwa mwaka wa 2004 ni<br />
Schizophrenia 61%, Epilepsy 229 (8.4)%, Organic brain syndrome 134 (6%), Acute<br />
psychosis, Psychoactive substance use disorders 14% Depression, Alcoholic psychosis 2%<br />
Manic-depressive psychosis, Mania 0.7%, Senile dementia 1.4%, Acute Psychosis 0.9%,<br />
Mental deficiency 0.5% na Anxiety neurosis 0.4%<br />
Hospitali ya Mirembe pia hupokea wagonjwa wenye magonjwa ya kawaida na katika mwaka<br />
2004, magonjwa kumi yaliyojitokeza kwa mahudhulio ya nje (OPD) yalikuwa kama<br />
ifuatavyo: Malaria (2,668), Urinary Tract Infections (312), Diarrhoea Diseases (302), ARI<br />
(274), Hypertensions (242), Dental \Caries (208), Typhoid (661), Migrain Headache (227),<br />
Rheumatism (226) na PID (219).<br />
Taasisi ya Isanga<br />
Taasisi ya Isanga hutoa huduma kwa wagonjwa wa Akili wahalifu pamoja na huduma za<br />
kawaida kwa wagonjwa wa Akili. Jukumu pekee kwa Taasisi ya Isanga ni kuchunguza na<br />
kutoa taarifa ya hali ya Afya ya Akili aliyokuwa nayo mgonjwa wakati wa kutenda<br />
kosa/makosa yaliyomfanya achukuliwe hatua za kisheria.<br />
Taasisi ya Isanga ina vituo viwili vya kukarabati mienendo ya wagonjwa wa akili ambavyo ni<br />
Mirembe Annex na Kijiji cha Hombolo.<br />
Katika mwaka 2004/2005 Taasisi ya Isanga imekarabati wodi tatu pamoja na ukarabati wa<br />
mfumo wa maji taka Isanga.<br />
Matarajio ya Hospitali ya Mirembe na Taasisi ya Isanga mwaka 2005/2006<br />
Mwaka 2005/06 hospitali ya Mirembe na Taasisi ya Isanga imepanga kukarabati wodi tatu,<br />
kufanya maandalizi ya kujenga kituo cha walioathirika kwa utumiaji wa pombe na madawa<br />
ya kulevya, kukarabati nyumba za watumishi na kujenga wodi moja katika Taasisi ya Isanga.<br />
6.4 Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI)<br />
Taasisi hii maalum ya kutibu magonjwa ya Saratani kwa mwaka 2004 ilihudumia wagonjwa<br />
wa nje (OPD) 6,962 ambapo wagonjwa 2,947 walikuwa wa Saratani ya shingo ya uzazi na<br />
kati ya hao wagonjwa wapya walikuwa 992 na waliokuwa wakifuatiliwa ni 1,955. Wagonjwa<br />
4,015 walikuwa na Saratani za aina nyingine ambapo 1,874 kati yao ni wapya na 2,141<br />
walikuwa wakifuatiliwa.<br />
Kuhusu wagonjwa waliolazwa, Taasisi ina vitanda 122 ambapo wagonjwa 2,312 walilazwa<br />
mwaka 2004. Kasi ya kutumia vitanda ilikuwa 100% na wastani wa siku za kuwa hospitali<br />
ilikuwa siku 50 kwa wodi za wanawake, 120 wodi ya watoto na 30 wodi ya wanaume. Jumla<br />
ya vifo 187 vilitokea kutokana na magonjwa ya Saratani.<br />
Saratani ya shingo ya uzazi iliongoza kwa 34.6% ikifuatiwa na Kaposis Sarcoma 14%,<br />
Oesophagial carcinoma 8.1 %, Saratani ya matiti 8.0 % pamoja na Saratani za Head and Neck<br />
7.8% kati ya magonjwa kumi yaliyooongoza kwa magonjwa ya nje (OPD).<br />
Mwaka 2004 huduma za maabara zilizotolewa ni pamoja na vipimo vya Clinical Chemistry<br />
8,212 ambapo positive vilikuwa 2,073, Haematology 42, positive 29, Serology 11,498,<br />
positive 3,044 na Parasitology vipimo 4,961, positive vikiwa 1,477.<br />
110
Idadi ya X-rays zilizopigwa zilikuwa 2,332 ambapo Chest iliongoza kwa 71.9% ikifuatiwa na<br />
Barium meal/swallow 6.2%, Extremities 5.5% pamoja na Pelvis 4.9%.Vipimo vya Ultrsound<br />
vilikuwa 4,067 ambapo kipimo cha Abdomen/pelvis kilioongoza kwa 52.1% kikifuatiwa na<br />
Pelvis 18% pamoja na Abdomen 8.1%<br />
Tiba ya mionzi ilitolewa kwa wagonjwa 30,045 ambapo Shingo ya uzazi ilioongoza katika<br />
viungo vilivyotibiwa kwa 65%, ikifutiwa na Head and Neck 10.5% pamoja na Oesophagus<br />
6.3%.<br />
Kwa mwaka 2004, Taasisi ilikuwa na jumla ya watumishi 134 ikiwa na upungufu wa<br />
watumishi 111 ikilinganishwa na ikama ambayo ni watumishi 218. Upungufu mkubwa upo<br />
katika kada za Specialist Doctors ambapo 10 ndio wanahitajika, Medical Doctors 9, Nursing<br />
Officers 64 na Radiographers 12.<br />
Kuhusu Madaktari Bingwa, wapo madaktari 5 kukiwa na upungufu wa madaktari 14<br />
ikilinganishwa na ikama ambayo ni 18. Upungufu upo zadi kwa kada za General<br />
Surgeons/Onchologists 2, Physicians 5, Onchologists 3, Public Health Specialists 2 na<br />
Pathologist 1.<br />
Katika kipindi hiki Taasisi ilipewa fedha za kuendeshea huduma pungufu kwa 59.6% kwa<br />
vile ilipokea Tshs 1,552,369,335.30 ikilinganishwa na fedha zlizoidhinishwa Tshs.<br />
2,981,477,019.80.<br />
Matarajio ya Taasisi ya Saratani ya Ocean Road mwaka 2005/2006<br />
Katika mwaka 2005/2006, ili Taasisi ya Saratani iweze kuboresha huduma za wagonjwa wa<br />
Saratani ambao wamekuwa wakiongezeka mwaka hadi mwaka, itajitahidi kupata mashine<br />
mpya za matibabu, itakarabati na kuongeza wodi za wagonjwa katika awamu tatu ambapo<br />
awamu ya kwanza imepanga kutekelezwa na itagharimu Shilingi za Kitanzania milioni mia<br />
moja.<br />
7.0 Ushirikiano na Nchi za Nje<br />
Wizara ya Afya iliendelea kuwa na ushirikiano mzuri na wa karibu na nchi marafiki na<br />
mashirika ya kimataifa yenye moyo wa kusaidia sekta ya afya katika utoaji wa huduma za<br />
afya. Wizara ya Afya pia imepata ushirikiano mzuri na sekta nyingine hususan katika<br />
kuandaa Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umaskini <strong>Tanzania</strong> (MKUKUTA).<br />
Wizara pia imeendelea kuadhimisha siku za Afya za Kitaifa na Kimataifa<br />
Wizara inazishukuru nchi za Denmark, Uholanzi, Ujeremani, Uswisi na mashirika ya Benki<br />
ya Dunia, UNFPA, Development Cooperation of Ireland (DCI) kwa kutoa misaada yao<br />
kupitia Mfuko wa Pamoja wa Sekta ya Afya (Basket Funds) ambazo zimesaidia kwa kiasi<br />
kikubwa kuboresha huduma za afya ikiwa ni pamoja na kuendelea kutoa fedha za ukarabati<br />
wa zahanati na vituo vya afya nchini. Pia, nchi nyingine ni China, Cuba, Canada, Hispania,<br />
India, Ireland, Italia, Japan, Korea ya Kusini, Merekani, Misri, Sweden, Ufaransa na<br />
Uingereza ambazo zimeendelea kuisaidia sekta ya Afya.<br />
111
Vilevile Wizara imeshirikiana na Mashirika ya Kimataifa yafuatayo ; Jumuia ya Nchi za<br />
Ulaya (EU), Shirika la Kimataifa la Maendeleo (UNDP), Shirika la Afya Ulimwenguni<br />
(WHO), Shirika la Kuhudumia Watoto (UNICEF), Shirika la Umoja wa Mataifa la Uzazi wa<br />
Mpango (UNFPA), Shirika la Kimataifa la Kudhibiti UKIMWI (UNAIDS), Shirika la Umoja<br />
wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), Benki ya Dunia (WB), Benki ya Maendeleo<br />
ya Afrika (ADB), Benki ya Nchi za Kiarabu kwa ajili ya Maendeleo ya Uchumi wa Nchi za<br />
Afrika (BADEA) OPEC, na Madaktari Wasio na Mpaka (Medicin Sans Frontieres – MSF).<br />
Mashirika mengine ni mashirika ya maendeleo ya nchi mbali mbali ambayo ni CIDA<br />
(Canada), CUAMM (Italy), DANIDA (Denmark), DFID (Uingereza), GTZ (Ujeremani),<br />
IDRC (Ujeremani), IRELAND AID, JICA (Japan), KfW (Ujeremani), MISERIOR<br />
(Ujeremani), SAREC (Sweden), SDC (Uswisi), CDC (Marekani), SIDA (Sweden) na USAID<br />
(Marekani).<br />
Wafadhili wa miradi mbali mbali ni pamoja na International Eye Foundation, Merk, Pfizer,<br />
Hellen Keller Foundation, International Trochoma Initiative, Axios International, US<br />
President G.W. Bush Initiative, Bill Clinton Foundation, Bill and Melinda Gates Foundation,<br />
Abbot Laboratories, London School of Hygine and Tropical Medicine, John Hopkins<br />
University, Global Fund for HIV/AIDS, TB and Malaria na PMTCT-Plus University of<br />
Columbia.<br />
Mashirika yasiyo ya kiSerekali yalihusika katika kuchangia uimarishaji wa huduma za afya.<br />
Mashirika hayo ni Aga Khan Foundation, AMREF, Lions Club, Rotary International,<br />
BAK<strong>WA</strong>TA, CCBRT, CCT, ELCT , TEC, Msalaba Mwekundu, Shree Hindu Mandal,<br />
Hubert Kairuki Memorial Hospital, Regency Hospital, TPHA, German Leprosy Relief<br />
Association, MEHATA na TANESA.<br />
8.0 Shukrani<br />
Kwa wafuatao kwa kushiriki katika utayarishaji wa Ripoti ya Huduma za Afya <strong>Tanzania</strong><br />
mwaka 2004. Dr. H.J. Mosha MDS, Ph D (CDS – Retired), Dr. E. Mung’ong’o MD, MPH<br />
(Tiba MoH), Mr.J. Ihunyo DNM, ADHA, MHRH (Tiba MoH), Dr. A. Senkoro DDS, MPH<br />
(Ag. CDS MoH), Dr. E. Silayo DDS, MPH (MNH), Dr. J. Masalu DDS, MPH, Ph.D<br />
(MUCHS), Dr. A. Nyamihura DDS, MPH (Mafunzo ya Watumishi MoH), Ms. E. Bakari<br />
ADHA, MHRH (Kinga MoH), Mr. C. Mpandana DNM, BscN, MHA (Ofisi ya<br />
Mganga Mkuu Kiongozi), Mr. C. John Bsc. Statistics (PTMCT) na Mr. J. Rubona Bsc.<br />
Statistics, Msc. MD, Msc Computer Science (Mipango MoH).<br />
112