08.01.2015 Views

MULIRU FARMERS CONSERVATION GROUP - Equator Initiative

MULIRU FARMERS CONSERVATION GROUP - Equator Initiative

MULIRU FARMERS CONSERVATION GROUP - Equator Initiative

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Empowered lives.<br />

Resilient nations.<br />

<strong>MULIRU</strong> <strong>FARMERS</strong><br />

<strong>CONSERVATION</strong> <strong>GROUP</strong><br />

Kenya<br />

Miradi ya <strong>Equator</strong><br />

Wanafijiji na Maendeleo Himili ya Jamii


MIRADI YA UNDP EQUATOR<br />

Kote duniani, jamiii zinazidi kubuni mbinu zinazonuiwa kuyakidhi mahitaji yao ya kila siku na ya kimazingira. Kuna kazi<br />

chache ambazo zimechapishwa za kuelezea kinagaubaga hizo mbinu bunifu na vile zilianzishwa,vile ziliathiri wakaaji wa<br />

sehemu mbali mbali na vile zimekuwa zikibadilika pindi wakati unapotita. Wachache wamejitokeza kuelezea wazi wazi juu<br />

ya miradi yao, na hata wale ambao wamefanya hivyo ni wakuu wa vijiji ambao wamefanya kuelezea kufaulu kwao.<br />

Mradi huu wa <strong>Equator</strong> Katika unadhamiria kujaza hili pengo kama njia moja ya kuadhimisha miaka kumi tangu kuanzishwa<br />

kwake. Masimulizi juu ya huu mradi ni baadhi tu ya mingi ambayo imefaulu na kushinda tuzo za <strong>Equator</strong> baada ya kukaguliwa<br />

na kutathiminiwa katika kitengo cha makundi ya kijamii yanayo hifadhi mazingira na kuinua maisha ya wanafijiji. Miradi hii<br />

inakusudiwa kuwa mifano ya kuiwa na kuwatia shime kuzungumzia ilivyofaulu ili kuhamasisha ulimwengu juu ya uhifadhi<br />

wa mazingira.<br />

Bonyeza katika ramani ya miradi ya <strong>Equator</strong> ili upate kupata habari zaidi<br />

Wahariri<br />

Mhariri Mkuu :<br />

Muhariri Meneja :<br />

Wahariri Waliochangia :<br />

Joseph Corcoran<br />

Oliver Hughes<br />

Dearbhla Keegan, Matthew Konsa, Erin Lewis, Whitney Wilding<br />

Wahandishi Waliochangia<br />

Edayatu Abieodun Lamptey, Erin Atwell, Toni Blackman, Jonathan Clay, Joseph Corcoran, Larissa Currado, Sarah Gordon, Oliver Hughes,<br />

Wen-Juan Jiang, Sonal Kanabar, Dearbhla Keegan, Matthew Konsa, Rachael Lader, Patrick Lee, Erin Lewis, Jona Liebl, Mengning Ma,<br />

Mary McGraw, Gabriele Orlandi, Juliana Quaresma, Peter Schecter, Martin Sommerschuh, Whitney Wilding, Luna Wu<br />

Uchoraji<br />

Oliver Hughes, Dearbhla Keegan, Matthew Konsa, Amy Korngiebel, Kimberly Koserowski, Erin Lewis, John Mulqueen, Lorena de la Parra,<br />

Brandon Payne, Mariajosé Satizábal G.<br />

Shukrani<br />

<strong>Equator</strong> ingependa kuwashukuru wanachama wa Muliru Farmers Conservation Group, haswa mwongozo na mchango wa James Ligare.<br />

Picha ni za Muliru Farmers Conservation Group, ramani ni za CIA World Factbook na Wikipedia. Masimulizi juu ya mradi huu yalitafsiriwa<br />

kwa Kiswahili na Dr. Ken Ramani.<br />

Nukuu Ziada<br />

United Nations Development Programme. 2012. Muliru Farmers Conservation Group, Kenya. <strong>Equator</strong> <strong>Initiative</strong> Case Study Series. New York,<br />

NY.


<strong>MULIRU</strong> <strong>FARMERS</strong><br />

<strong>CONSERVATION</strong> <strong>GROUP</strong><br />

Kenya<br />

MAELEZO KUHUSU MRADI HUU<br />

Kikundi cha wakulima wahifadhi wa Muliro ni shirika<br />

la kijamii linalopatikana karibu na msitu wa Kakamega<br />

magharibi mwa Kenya. Kikundi hiki hujipatia riziki kwa kuuza<br />

dawa ya kienyeji inayoitwa Naturab ambayo hutengenezwa<br />

kutokana na mti spesheli.<br />

Shughuli hizi za kikundi zimesaidia katika uhifadhi wa<br />

msitu wa Kakamega. Wengi wa wanachama wa kikundi hiki<br />

ni wanawake ambao huchuma riziki kwa kuuza dawa hii.<br />

Aidha, baadhi ya pesa zinazopatikana kutoka biashara hii<br />

hutumika kulipia utafiti kuhusu msitu huu na uhifadhi wake<br />

kwa kijumla.<br />

MUHTASARI<br />

ULISHINDA TUZO YA EQUATOR: Mwaka 2010<br />

ULIANZISHWA: Mwaka 1997<br />

ENEO: Mkoa wa Magharibi, Kenya<br />

WANAOFAIDI: Kaya 360<br />

MAZINGIRA: Msitu wa Kakamega<br />

YALIYOMO<br />

Historia na Mandhari 4<br />

Majukumu Makuu na Ubunifu 5<br />

Matokeo ya Kimazingira 7<br />

Matokeo ya Kijamii 7<br />

Jinsi ya Kudumisha Mradi Huu 8<br />

Maono 8<br />

Wahisani 8<br />

3


Historia na Mandhari<br />

Msitu wa Kakamega ndio msitu asilia ulionusurika kutokana<br />

na uharibifu wa kibinadamu. Msitu huu wenye miti aina tofauti<br />

hupatikana mkoa wa magharibi. Msitu huu ndio tegemeo la wakaaji<br />

wa eneo hilo. Wenyeji hutegemea msitu huu kwa mbao, kuni, chakula<br />

cha ng’ombe, miti ya ujenzi na miti ya kutengeneza dawa za kienyeji.<br />

Msitu huu ndo chanzo cha maji safi ya eneo hili pamoja na shughuli<br />

zote za kibiashara. Msitu Kakamega (kama ilivyo kawaida kwa msitu<br />

mingine nchini Kenya) huko karibu kuangamizwa na shughuli za<br />

kibinadamu kama vile: ukulima na ujenzi, mbao ,uchomaji makaa na<br />

utengenezaji wa madawa ya kienyeji. Idadi ya watu karibu na msitu<br />

inaendelea kuongezeka huku eneo la kilomita moja kukaliwa na<br />

watu takriban 1200. Hapa, kiwango cha umasikini ni cha juu huku<br />

watu 35,000 wakitegemea msitu huu.<br />

Kikundi hiki kina malengo manne makuu:<br />

i. Kuimarisha ukuzaji wa kibiashara wa Ocimum Kilimandschirium<br />

miongoni mwa wachochole wanoishi mkabala na msitu wa<br />

Kakamega<br />

ii. Kuunda na kutafutia soko bidhaa zinazotokana na mti huu<br />

ndiposa wakulima wa mashinani wajipatie mapato<br />

iii. Kuhamasisha wakulima kuhusu umuhimu wa kuutunza msitu<br />

wa Kakamega<br />

iv. Kuwakusanya majirani wa msitu huu ili kushiriki kikamilifu katika<br />

shughuli za kuhifadhi msitu huu.<br />

Kukuza na kuhifadhi mti wa dawa<br />

Baadhi ya miti inayopatikana katika msitu Kakamega ni Ocimum<br />

Kilimandscharicum. Tangu jadi mti huu umekuwa ukitumiwa na<br />

wenyeji kwa kutibu mafua na kikohozi. Mti huu huwa na mafuta<br />

yenye mnuko spesheli. Matawi yake yamekuwa yakichemshwa na<br />

kutumiwa kutibu magonjwa ya kupumua. Matumizi mengine ni<br />

kama: kufukuza mbu, kutengeneza asali (nyuki), viungo vya vyakula<br />

na kufukuza wadudu wanavamia ghala za mahindi.<br />

Kikundi cha Muliru kiliundwa mnamo mwaka wa 1997 kikiwa na lengo<br />

la kukuza mti wa Ocimum Kilimandscharicum ambao wangeutumia<br />

kama mbinu ya kuhifadhi msitu wa Kakamega na kuwapa kitega<br />

uchumi majirani wa msitu huu. Kikundi hiki kimechanganya elimu ya<br />

zamani na ile ya kisasa yakiteknolojia na sayansi na kupata washika<br />

dau wa kipekee - wakulima wa mashinani, asasi za utafiti na sekta<br />

ya kibinafsi – ili kuongeza ubora wa mti huu wa dawa. Kikundi hiki<br />

hushirikiana sako kwa bako na wakulima wa mashinani kuunda<br />

bidhaa tofauti tofauti kutokana na mti huu ambao huuzwa kwa<br />

kutumia nembo na jina la usajiri la Naturub. Naturub imesajiriwa<br />

kama dawa ya kutibu mafua, kikohozi, maumivu, kuumwa na<br />

wadudu na miteguko mbalimbali.<br />

4


Majukumu Makuu na Ubunifu<br />

Kikundi cha Muliru huwaleta pamoja majirani wa msitu Kakamega<br />

ili kupanda miche ya Ocimum Kilimanscharicum. Ukulima wa mti<br />

huu huwa biashara muhimu kwa wakulima waliotengwa wa eneo<br />

hii. Wakulima hufunzwa namna ya kutayarisha na kuvuna mti huu<br />

nyumbani mwao. Mti huu huvunwa kwa kukatia sehemu karibu na<br />

mizizi na kisha kuchuma matawi yake. Kitambo, utoaji wa mafuta<br />

ulifanyiwa nyumbani, lakini mnamo mwaka wa 2005, Muliru ilijenga<br />

mtambo wa kazi hiyo katikati mwa eneo hilo. Wakulima husaidiwa na<br />

kikundi kukusanya na kusafirisha matawi mitamboni. Hapa matawi<br />

hupimwa na kukaushwa. Matawi haya makavu hutengenezwa<br />

mafuta maalum ambayo huuzwa kwa nembo ya Naturub.<br />

Utengenezaji na uuzaji wa Naturub<br />

Tangu kuzinduliwa mtambo wa utengenezaji wa mti wa Ocimum<br />

tani 770 zimetengenezwa na kilo 700 za mafuta kidawa yametolewa.<br />

Aidha takriban vidonge 400,000 vya Naturub vimeuzwa mijini na<br />

mashinani kote nchini Kenya. Bidhaa hizi za Naturub zimekubaliwa<br />

vyema masokoni ingawa vimepata ushindani mkubwa kutoka<br />

bidhaa za kimataifa. Kipato cha mradi huu ni takribani dolla 70,000<br />

za kimarikani. Hivi sasa wakulilma kama 360 wanakuza mti huu<br />

mashambani mwao. Ukulima wa mti huu umeongezeka kwa<br />

kiwango kikubwa katika eneo hili.<br />

Uongozi<br />

Kikundi hiki kinaingozwa na bodi iliyoundwa na; mwenyekiti na<br />

naibu wa mwenyekiti, katibu na naibu wa katibu, mwekahazina,<br />

katibu mwandalizi na wanakamati wane, ambao uchaguliwa na<br />

vikundi vya wakulima kuhudumu kwa miaka fulani. Bodi ndiyo inayo<br />

usemi wa mwisho katika kikundi hiki cha Muliru. Jukumu kuu la bodi<br />

ni kuhakikisha kuwa maslahi ya wakulima yanazingatiwa na kupata<br />

ujira mwema wa mauzo yao. Kikundi kina nyapala mkuu ambaye<br />

anaendesha shughuli zote za kikundi hiki na kuripoti kwa bodi.<br />

Shirika hili lina vitengo kadha vyenye kushughulikia mambo tofauti<br />

tofauti; mfano, kitengo cha mauzo ambacho huijishughulisha na<br />

kuuza bidhaa za kikundi hiki katika maduka makuu nchini Kenya,<br />

kitengo hiki vile vile ushirikiana na makampuni ya kibinafsi ili<br />

kutangaza bidhaa za shirika hili. Mwisho kikundi huwa na vitengo<br />

vitatu katika ngazi ya mashinani. Mwakilishi wa vikundi vya<br />

wakulima ambaye hutoa maoni ya wakulima wakati wa mikutano.<br />

Ngazi ya pili, huwa na mwendesha mtambo ambaye husaidiwa na<br />

vijana tisa katika kutoa mafuta malighafi. Ngazi ya mwisho ni askari<br />

gongo mkuu ambaye hushirikiana na utawala wa mkoa ili kuchunga<br />

mali yote ya kikundi.<br />

Licha ya kukuza na kuuza bidhaa za Naturub, shirika hili la uhifadhi<br />

wa msitu huandaa warsha za kimasomo kwa wenyeji wa eneo hili<br />

wakiwafunza juu ya umuhimu wa kuyatunza mazingira na raslimali<br />

asilia kama misitu. Shirika hili hutayarisha miche ya miti asili ambayo<br />

hukabidhiwa wakulima ili kuipanda mashambani mwao.<br />

Ubunifu usiosahaulika wa kikundi hili ni ule wa kuanzisha mradi<br />

uliosajiri dawa, kuunda na kisha kuifanya biashara muhimu ya<br />

kunufaisha wakulima wachochole. Licha ya kuhimiza ukulima wa<br />

mti huu, kikundi kilienda hatua moja zaidi kwa kuanzisha mtambo<br />

uliomilikiwa na kuendeshwa na wakulima wenyewe. Isitoshe,<br />

wakulima wamepata ujira wa kudumu na kuinua viwango vya<br />

maisha yao.<br />

5


Fig. 1: Jendwali la Uongozi<br />

Bodi ya Usimamizi<br />

Nyapala Mkuu<br />

Kitengo cha Mafunzo<br />

Kitengo cha Uundaji<br />

Kitengo cha Mauzo<br />

Mwakilishi wa Wakulima<br />

Msimamizi wa Mtambo<br />

Askari gongo Mkuu<br />

Chanzo: Kikundi Cha Wakulima Wahifadhi Cha Muliru<br />

6


Matokeo<br />

MATOKEO YA KIMAZINGIRA<br />

Matokeo makuu ya mradi huu ni matumizi na uhifadhi mwema wa<br />

msitu Kakamega na vilevile kulinda takribani ndege 350 na mimea<br />

380 inayopatikana humo. Aidha, mradi huu umesaidia wenyeji kuwa<br />

na fikra chanya kuhusu uhifadhi wa msitu pamoja na miti - mradi<br />

huu vilevile umechukuliwa kama kielelezo chema cha uhifadhi wa<br />

msitu na, chama cha msitu cha jamii ya Mwileshi.<br />

Chama cha msitu cha jamii ya mwileshi<br />

Chama cha kitaifa kinachosimamia msitu (KWS) kiko mbioni<br />

kuhusisha jamii za mashinani katika uhifadhi wa misitu. Msitu<br />

wa Kakamega ulichaguliwa ili kufanyia majaribio hayo ambapo<br />

ushirikiano kati ya jamii za mashinani pamoja na kikundi cha Muliru<br />

wamepanda miche 10,000 mnamo Septemba 2010 pekee. Vyama<br />

hivi vilivyokusanywa pamoja hufunza jamii kuhusu umuhimu wa<br />

msitu na namna ya kuitunza misitu kwa jumla.<br />

Kubadili mtizamo kuhusu uhifadhi wa misitu<br />

Utafiti uliofanywa na kikundi cha MuIiru ,ukihusisha wakulima wa<br />

Ocimum 360 ulionyesha wazi kuwa wakulima asilimia 85 huhifadhi<br />

msitu. Matokeo kamili ya utafiti huo ni kama ifuatavyo; Asilimia 49 ya<br />

wakulima hao husambaza elimu ya uhifadhi wa misitu kwa wenzao,<br />

asilimia 59 wamepunguza ukusanyaji kuni , chakula cha ng’ombe na<br />

mbao msituni humo, asilimia 37 wamewakataza wanajamii wengine<br />

dhidi ya kutumia msitu vibaya na asilimia 5 ya wakulima wameripoti<br />

visa vya uwindaji haramu kwa utawala wa mkoa. Uvunaji wa Ocimum<br />

hauharibu mazingira, mimea ya Ocimum humea tena baada ya<br />

kukauka na hivyo jamii hupata kipato kisichoisha. Bidhaa za Naturub<br />

huwa na onyo na mawaidha ya kuhimiza uhifadhi wa mazingira.<br />

MATOKEO YA KIJAMII<br />

Kikundi cha Muliru kimetanda miongoni mwa wilaya 5<br />

zinazouzunguka msitu wa Kakamega ,na idadi ya watu ni kama2,500<br />

na wanachama wa kikundi wakiwa ni 360.Wengi wa watu katika<br />

eneo hili wametengwa kiuchumi na wengi ni wachochole walio na<br />

mashamba madogo mno yasiyoweza kuwakimu kimaisha. Kikundi<br />

hiki cha Muliru kimebadili hii hali kwa kuwapa wenyeji fursa ya kazi<br />

na njia ya kujipatia riziki. Takribani watu 8 wa eneo hili wamepata<br />

kazi ya kudumu mitamboni . Isitoshe takribani wakulima 900 wana<br />

kazi ya kulima mmea huu hadi sasa vidonge 400,000 vimeuzwa kote<br />

nchini hususan kwenye maduka makuu kama vile; Uchumi,Turskeys<br />

na Eastmat. Naturub vilevile hupatikana kwenye maduka ya dawa<br />

nchini Kenya. Wakulima hupata marupurupu yao mara tatu kwa<br />

mwaka na wameona kipato chao kikiongezeka kwa asilimia 300<br />

tangu mradi huu kuanzishwa.<br />

Faisa Nynginezo<br />

Kutokana na utafiti wa awali uliofanywa na kikundi hiki cha Muliru,<br />

kulipatikana faida nyinginezo kama; asilimia 31 ya wakulima hutumia<br />

hela walizozipata kutoka kwa mradi huu kuanzisha biashara ndogo<br />

ndogo na hivyo kuongezea kipato chao. Isitoshe , asilimia 83.5<br />

hutumia hela zao ili kununulia familia zao chakula . Asilimia 57 hulipia<br />

watoto karo ,asilimia 26 hujinunulia nguo, asilimia17.65 hutumia<br />

pesa hizo kukarabati nyumba zao. Wenyeji vilevile wamenufaika<br />

na elimu ya kibiashara wanaopewa na mashirika mengine. Mradi<br />

huu vilevile umeinua kiwango cha maisha ya wenyeji. Wakulima<br />

nao ni kati ya washika dau wa shirika hili . Wakulima kwa sasa wana<br />

ufahamu mkuu kuhusu kilimo, uwekaji pesa na kuhusu umuhimu<br />

wa mshikamano wa kijamii.<br />

Mradi huu aidha umehimiza usawa wa kijinsia ambapo jamii ya hapa<br />

imekubali ukweli kuwa uchumaji ni kazi ya mke na mume .Wanawake<br />

pia wanastahili kuchaguliwa kwenye nyadhifa za uongozi<br />

7


Jinsi ya Kudumisha Mradi Huu<br />

JINSI YA KUDUMISHA MRADI HUU<br />

Kikundi cha Muliru kilikua na mpango wa miaka kumi ya matumizi<br />

ya faida inayotokana na mauzo ya Naturub. Mpango wenyewe ulikua<br />

kama ufuatao; asilimia 10 kusaidia katika uhifadhi wa msitu wa<br />

Kakamega, asilimia 10 iingie kwenye mfuko wa maendeleo ya jamii<br />

inayozunguka msitu Kakamega, asilimia 60 kupewa wanachama wa<br />

kikundi cha Muliru, na asilimia 20 kuingia kwenye mfuko wa kusaidia<br />

utafiti. Kikundi kinachokisia kuwa shirika hili litajisimamia kifedha<br />

na kukua zaidi. Naturub ndiyo dawa pekee ya kienyeji kupata usajili<br />

wa kiserikali pamoja na shirika la madaktari linalosimamia dawa<br />

na sumu nchini. Upelelezi wa siri kuhusu Naturub umeonyesha<br />

kuwa dawa hii inazaa takribani shilingi million 100 kwa kila mwaka<br />

mijini. Kikundi cha Muliru kimetegemea mashirika ya nchini na<br />

kimataifa katika kufikia malengo yake. Muliru imewahi kushirikiana<br />

na kampuni kadhaa za matangazo na utangazaji katika kuendeleza<br />

malengo yake. Mashirika mengine ambayo yamefadhili Muliru ni<br />

kama chuo kikuu cha Nairobi, kituo cha dunia cha misitu, shirika la<br />

wanyama pori la Kenya (KWS) na mengineyo. Maono mengine ya<br />

kikundi ni kuongeza usalishaji, kutafuta masoko mengine ya nchini<br />

na kitaifa, kufanya utafiti zaidi kuhusu mmea huu kuwapa mafunzo<br />

zaidi wakulima na kuimarisha na kuhimiza wanawake na vijana<br />

kuunga mkono mradi huu.<br />

MAONO<br />

Budongo nchini Uganda. Kulingana na maoni ya kikundi cha Muliru,<br />

mafunzo yanayobadilishwa miongoni mwa watu wenye rika moja<br />

huzama na kueleweka zaidi<br />

WAHISANI<br />

• Kituo cha kimataifa cha uchunguzi wa Wadudu<br />

• Chuo Kikuu cha Nairobi<br />

• Shirika la Dunia la Misitu<br />

• Taasisi ya Utafiti waMisitu la Kenya [KEFRI]<br />

• Shirika la Wanyama Pori la Kenya [KWS]<br />

• Shirika la[GBDI]<br />

• Wakfu wa Ford<br />

• Wakfu wa Bio Vision<br />

• Wakifu wa Macarthur<br />

• Huduma za kiuduma za Kijerumani [DED]<br />

• PACT-Kenya/USAid<br />

• WHO Multilateral <strong>Initiative</strong> on Malaria/Research and Training in<br />

Tropical Diseases (TDR)<br />

Kikundi hiki kimebadilisha mawazo ya mradi na wanajamii wa nchi<br />

kama Uganda, Tanzania, Afrika kusini na Nigeria na vilevile jamii<br />

zingine za humu nchini. Zaidi ya watu 830 wametutembelea ndiposa<br />

wapate masomo ya moja kwa moja . Mafunzo yanayopatikana kutoka<br />

kwa mradi huu yamesambazwa kupitia kwa mihadhara ,uigizaji,<br />

utambaji na matembeleano. Isitoshe , mradi huu umeonyeshwa<br />

na kutangazwa na vyombo mbalimbali vya kimataifa kama redio<br />

na televisheni. Kutokana na utangazaji huo, mradi wetu umeigwa<br />

na jamii kadhaa mfano kikundi cha kuifadhi misitu cha mashariki<br />

ya Usambara nchini Tanzania na kikundi kinachohifadhi misitu ya<br />

8


MAREJELEO YA ZIADA<br />

• Muliru Farmers Conservation Group PhotoStory (Vimeo) vimeo.com/15780379<br />

• Video on Muliru Farmers Conservation Group (Vimeo) vimeo.com/43207923<br />

Masimulizi kuhusu miradi mingine, bonyeza hapa:<br />

<strong>Equator</strong> <strong>Initiative</strong><br />

Environment and Energy Group<br />

United Nations Development Programme (UNDP)<br />

304 East 45th Street, 6th Floor<br />

New York, NY 10017<br />

Tel: +1 646 781-4023<br />

www.equatorinitiative.org<br />

Mradi wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa ndio unaoendesha miradi ya maendeleo ya Umoja wa Mataifa kote ulimwenguni<br />

kwa kutoa mwito wa mageuzi na kuelekeza mataifa kwa maarifa, na malighafi ili kusaidia watu kujiimarisha kimaisha.<br />

Mradi huu wa <strong>Equator</strong> huleta pamoja Umoja wa Mataifa , serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali, wafanyibiashara na makundi ya<br />

mashinani ili kutambua na kuimaliza maendeleo himili kwa watu na jamii kwa jumla.<br />

©2012 Haki Zote ni za Mradi wa <strong>Equator</strong>

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!