MULIRU FARMERS CONSERVATION GROUP - Equator Initiative
MULIRU FARMERS CONSERVATION GROUP - Equator Initiative
MULIRU FARMERS CONSERVATION GROUP - Equator Initiative
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Empowered lives.<br />
Resilient nations.<br />
<strong>MULIRU</strong> <strong>FARMERS</strong><br />
<strong>CONSERVATION</strong> <strong>GROUP</strong><br />
Kenya<br />
Miradi ya <strong>Equator</strong><br />
Wanafijiji na Maendeleo Himili ya Jamii
MIRADI YA UNDP EQUATOR<br />
Kote duniani, jamiii zinazidi kubuni mbinu zinazonuiwa kuyakidhi mahitaji yao ya kila siku na ya kimazingira. Kuna kazi<br />
chache ambazo zimechapishwa za kuelezea kinagaubaga hizo mbinu bunifu na vile zilianzishwa,vile ziliathiri wakaaji wa<br />
sehemu mbali mbali na vile zimekuwa zikibadilika pindi wakati unapotita. Wachache wamejitokeza kuelezea wazi wazi juu<br />
ya miradi yao, na hata wale ambao wamefanya hivyo ni wakuu wa vijiji ambao wamefanya kuelezea kufaulu kwao.<br />
Mradi huu wa <strong>Equator</strong> Katika unadhamiria kujaza hili pengo kama njia moja ya kuadhimisha miaka kumi tangu kuanzishwa<br />
kwake. Masimulizi juu ya huu mradi ni baadhi tu ya mingi ambayo imefaulu na kushinda tuzo za <strong>Equator</strong> baada ya kukaguliwa<br />
na kutathiminiwa katika kitengo cha makundi ya kijamii yanayo hifadhi mazingira na kuinua maisha ya wanafijiji. Miradi hii<br />
inakusudiwa kuwa mifano ya kuiwa na kuwatia shime kuzungumzia ilivyofaulu ili kuhamasisha ulimwengu juu ya uhifadhi<br />
wa mazingira.<br />
Bonyeza katika ramani ya miradi ya <strong>Equator</strong> ili upate kupata habari zaidi<br />
Wahariri<br />
Mhariri Mkuu :<br />
Muhariri Meneja :<br />
Wahariri Waliochangia :<br />
Joseph Corcoran<br />
Oliver Hughes<br />
Dearbhla Keegan, Matthew Konsa, Erin Lewis, Whitney Wilding<br />
Wahandishi Waliochangia<br />
Edayatu Abieodun Lamptey, Erin Atwell, Toni Blackman, Jonathan Clay, Joseph Corcoran, Larissa Currado, Sarah Gordon, Oliver Hughes,<br />
Wen-Juan Jiang, Sonal Kanabar, Dearbhla Keegan, Matthew Konsa, Rachael Lader, Patrick Lee, Erin Lewis, Jona Liebl, Mengning Ma,<br />
Mary McGraw, Gabriele Orlandi, Juliana Quaresma, Peter Schecter, Martin Sommerschuh, Whitney Wilding, Luna Wu<br />
Uchoraji<br />
Oliver Hughes, Dearbhla Keegan, Matthew Konsa, Amy Korngiebel, Kimberly Koserowski, Erin Lewis, John Mulqueen, Lorena de la Parra,<br />
Brandon Payne, Mariajosé Satizábal G.<br />
Shukrani<br />
<strong>Equator</strong> ingependa kuwashukuru wanachama wa Muliru Farmers Conservation Group, haswa mwongozo na mchango wa James Ligare.<br />
Picha ni za Muliru Farmers Conservation Group, ramani ni za CIA World Factbook na Wikipedia. Masimulizi juu ya mradi huu yalitafsiriwa<br />
kwa Kiswahili na Dr. Ken Ramani.<br />
Nukuu Ziada<br />
United Nations Development Programme. 2012. Muliru Farmers Conservation Group, Kenya. <strong>Equator</strong> <strong>Initiative</strong> Case Study Series. New York,<br />
NY.
<strong>MULIRU</strong> <strong>FARMERS</strong><br />
<strong>CONSERVATION</strong> <strong>GROUP</strong><br />
Kenya<br />
MAELEZO KUHUSU MRADI HUU<br />
Kikundi cha wakulima wahifadhi wa Muliro ni shirika<br />
la kijamii linalopatikana karibu na msitu wa Kakamega<br />
magharibi mwa Kenya. Kikundi hiki hujipatia riziki kwa kuuza<br />
dawa ya kienyeji inayoitwa Naturab ambayo hutengenezwa<br />
kutokana na mti spesheli.<br />
Shughuli hizi za kikundi zimesaidia katika uhifadhi wa<br />
msitu wa Kakamega. Wengi wa wanachama wa kikundi hiki<br />
ni wanawake ambao huchuma riziki kwa kuuza dawa hii.<br />
Aidha, baadhi ya pesa zinazopatikana kutoka biashara hii<br />
hutumika kulipia utafiti kuhusu msitu huu na uhifadhi wake<br />
kwa kijumla.<br />
MUHTASARI<br />
ULISHINDA TUZO YA EQUATOR: Mwaka 2010<br />
ULIANZISHWA: Mwaka 1997<br />
ENEO: Mkoa wa Magharibi, Kenya<br />
WANAOFAIDI: Kaya 360<br />
MAZINGIRA: Msitu wa Kakamega<br />
YALIYOMO<br />
Historia na Mandhari 4<br />
Majukumu Makuu na Ubunifu 5<br />
Matokeo ya Kimazingira 7<br />
Matokeo ya Kijamii 7<br />
Jinsi ya Kudumisha Mradi Huu 8<br />
Maono 8<br />
Wahisani 8<br />
3
Historia na Mandhari<br />
Msitu wa Kakamega ndio msitu asilia ulionusurika kutokana<br />
na uharibifu wa kibinadamu. Msitu huu wenye miti aina tofauti<br />
hupatikana mkoa wa magharibi. Msitu huu ndio tegemeo la wakaaji<br />
wa eneo hilo. Wenyeji hutegemea msitu huu kwa mbao, kuni, chakula<br />
cha ng’ombe, miti ya ujenzi na miti ya kutengeneza dawa za kienyeji.<br />
Msitu huu ndo chanzo cha maji safi ya eneo hili pamoja na shughuli<br />
zote za kibiashara. Msitu Kakamega (kama ilivyo kawaida kwa msitu<br />
mingine nchini Kenya) huko karibu kuangamizwa na shughuli za<br />
kibinadamu kama vile: ukulima na ujenzi, mbao ,uchomaji makaa na<br />
utengenezaji wa madawa ya kienyeji. Idadi ya watu karibu na msitu<br />
inaendelea kuongezeka huku eneo la kilomita moja kukaliwa na<br />
watu takriban 1200. Hapa, kiwango cha umasikini ni cha juu huku<br />
watu 35,000 wakitegemea msitu huu.<br />
Kikundi hiki kina malengo manne makuu:<br />
i. Kuimarisha ukuzaji wa kibiashara wa Ocimum Kilimandschirium<br />
miongoni mwa wachochole wanoishi mkabala na msitu wa<br />
Kakamega<br />
ii. Kuunda na kutafutia soko bidhaa zinazotokana na mti huu<br />
ndiposa wakulima wa mashinani wajipatie mapato<br />
iii. Kuhamasisha wakulima kuhusu umuhimu wa kuutunza msitu<br />
wa Kakamega<br />
iv. Kuwakusanya majirani wa msitu huu ili kushiriki kikamilifu katika<br />
shughuli za kuhifadhi msitu huu.<br />
Kukuza na kuhifadhi mti wa dawa<br />
Baadhi ya miti inayopatikana katika msitu Kakamega ni Ocimum<br />
Kilimandscharicum. Tangu jadi mti huu umekuwa ukitumiwa na<br />
wenyeji kwa kutibu mafua na kikohozi. Mti huu huwa na mafuta<br />
yenye mnuko spesheli. Matawi yake yamekuwa yakichemshwa na<br />
kutumiwa kutibu magonjwa ya kupumua. Matumizi mengine ni<br />
kama: kufukuza mbu, kutengeneza asali (nyuki), viungo vya vyakula<br />
na kufukuza wadudu wanavamia ghala za mahindi.<br />
Kikundi cha Muliru kiliundwa mnamo mwaka wa 1997 kikiwa na lengo<br />
la kukuza mti wa Ocimum Kilimandscharicum ambao wangeutumia<br />
kama mbinu ya kuhifadhi msitu wa Kakamega na kuwapa kitega<br />
uchumi majirani wa msitu huu. Kikundi hiki kimechanganya elimu ya<br />
zamani na ile ya kisasa yakiteknolojia na sayansi na kupata washika<br />
dau wa kipekee - wakulima wa mashinani, asasi za utafiti na sekta<br />
ya kibinafsi – ili kuongeza ubora wa mti huu wa dawa. Kikundi hiki<br />
hushirikiana sako kwa bako na wakulima wa mashinani kuunda<br />
bidhaa tofauti tofauti kutokana na mti huu ambao huuzwa kwa<br />
kutumia nembo na jina la usajiri la Naturub. Naturub imesajiriwa<br />
kama dawa ya kutibu mafua, kikohozi, maumivu, kuumwa na<br />
wadudu na miteguko mbalimbali.<br />
4
Majukumu Makuu na Ubunifu<br />
Kikundi cha Muliru huwaleta pamoja majirani wa msitu Kakamega<br />
ili kupanda miche ya Ocimum Kilimanscharicum. Ukulima wa mti<br />
huu huwa biashara muhimu kwa wakulima waliotengwa wa eneo<br />
hii. Wakulima hufunzwa namna ya kutayarisha na kuvuna mti huu<br />
nyumbani mwao. Mti huu huvunwa kwa kukatia sehemu karibu na<br />
mizizi na kisha kuchuma matawi yake. Kitambo, utoaji wa mafuta<br />
ulifanyiwa nyumbani, lakini mnamo mwaka wa 2005, Muliru ilijenga<br />
mtambo wa kazi hiyo katikati mwa eneo hilo. Wakulima husaidiwa na<br />
kikundi kukusanya na kusafirisha matawi mitamboni. Hapa matawi<br />
hupimwa na kukaushwa. Matawi haya makavu hutengenezwa<br />
mafuta maalum ambayo huuzwa kwa nembo ya Naturub.<br />
Utengenezaji na uuzaji wa Naturub<br />
Tangu kuzinduliwa mtambo wa utengenezaji wa mti wa Ocimum<br />
tani 770 zimetengenezwa na kilo 700 za mafuta kidawa yametolewa.<br />
Aidha takriban vidonge 400,000 vya Naturub vimeuzwa mijini na<br />
mashinani kote nchini Kenya. Bidhaa hizi za Naturub zimekubaliwa<br />
vyema masokoni ingawa vimepata ushindani mkubwa kutoka<br />
bidhaa za kimataifa. Kipato cha mradi huu ni takribani dolla 70,000<br />
za kimarikani. Hivi sasa wakulilma kama 360 wanakuza mti huu<br />
mashambani mwao. Ukulima wa mti huu umeongezeka kwa<br />
kiwango kikubwa katika eneo hili.<br />
Uongozi<br />
Kikundi hiki kinaingozwa na bodi iliyoundwa na; mwenyekiti na<br />
naibu wa mwenyekiti, katibu na naibu wa katibu, mwekahazina,<br />
katibu mwandalizi na wanakamati wane, ambao uchaguliwa na<br />
vikundi vya wakulima kuhudumu kwa miaka fulani. Bodi ndiyo inayo<br />
usemi wa mwisho katika kikundi hiki cha Muliru. Jukumu kuu la bodi<br />
ni kuhakikisha kuwa maslahi ya wakulima yanazingatiwa na kupata<br />
ujira mwema wa mauzo yao. Kikundi kina nyapala mkuu ambaye<br />
anaendesha shughuli zote za kikundi hiki na kuripoti kwa bodi.<br />
Shirika hili lina vitengo kadha vyenye kushughulikia mambo tofauti<br />
tofauti; mfano, kitengo cha mauzo ambacho huijishughulisha na<br />
kuuza bidhaa za kikundi hiki katika maduka makuu nchini Kenya,<br />
kitengo hiki vile vile ushirikiana na makampuni ya kibinafsi ili<br />
kutangaza bidhaa za shirika hili. Mwisho kikundi huwa na vitengo<br />
vitatu katika ngazi ya mashinani. Mwakilishi wa vikundi vya<br />
wakulima ambaye hutoa maoni ya wakulima wakati wa mikutano.<br />
Ngazi ya pili, huwa na mwendesha mtambo ambaye husaidiwa na<br />
vijana tisa katika kutoa mafuta malighafi. Ngazi ya mwisho ni askari<br />
gongo mkuu ambaye hushirikiana na utawala wa mkoa ili kuchunga<br />
mali yote ya kikundi.<br />
Licha ya kukuza na kuuza bidhaa za Naturub, shirika hili la uhifadhi<br />
wa msitu huandaa warsha za kimasomo kwa wenyeji wa eneo hili<br />
wakiwafunza juu ya umuhimu wa kuyatunza mazingira na raslimali<br />
asilia kama misitu. Shirika hili hutayarisha miche ya miti asili ambayo<br />
hukabidhiwa wakulima ili kuipanda mashambani mwao.<br />
Ubunifu usiosahaulika wa kikundi hili ni ule wa kuanzisha mradi<br />
uliosajiri dawa, kuunda na kisha kuifanya biashara muhimu ya<br />
kunufaisha wakulima wachochole. Licha ya kuhimiza ukulima wa<br />
mti huu, kikundi kilienda hatua moja zaidi kwa kuanzisha mtambo<br />
uliomilikiwa na kuendeshwa na wakulima wenyewe. Isitoshe,<br />
wakulima wamepata ujira wa kudumu na kuinua viwango vya<br />
maisha yao.<br />
5
Fig. 1: Jendwali la Uongozi<br />
Bodi ya Usimamizi<br />
Nyapala Mkuu<br />
Kitengo cha Mafunzo<br />
Kitengo cha Uundaji<br />
Kitengo cha Mauzo<br />
Mwakilishi wa Wakulima<br />
Msimamizi wa Mtambo<br />
Askari gongo Mkuu<br />
Chanzo: Kikundi Cha Wakulima Wahifadhi Cha Muliru<br />
6
Matokeo<br />
MATOKEO YA KIMAZINGIRA<br />
Matokeo makuu ya mradi huu ni matumizi na uhifadhi mwema wa<br />
msitu Kakamega na vilevile kulinda takribani ndege 350 na mimea<br />
380 inayopatikana humo. Aidha, mradi huu umesaidia wenyeji kuwa<br />
na fikra chanya kuhusu uhifadhi wa msitu pamoja na miti - mradi<br />
huu vilevile umechukuliwa kama kielelezo chema cha uhifadhi wa<br />
msitu na, chama cha msitu cha jamii ya Mwileshi.<br />
Chama cha msitu cha jamii ya mwileshi<br />
Chama cha kitaifa kinachosimamia msitu (KWS) kiko mbioni<br />
kuhusisha jamii za mashinani katika uhifadhi wa misitu. Msitu<br />
wa Kakamega ulichaguliwa ili kufanyia majaribio hayo ambapo<br />
ushirikiano kati ya jamii za mashinani pamoja na kikundi cha Muliru<br />
wamepanda miche 10,000 mnamo Septemba 2010 pekee. Vyama<br />
hivi vilivyokusanywa pamoja hufunza jamii kuhusu umuhimu wa<br />
msitu na namna ya kuitunza misitu kwa jumla.<br />
Kubadili mtizamo kuhusu uhifadhi wa misitu<br />
Utafiti uliofanywa na kikundi cha MuIiru ,ukihusisha wakulima wa<br />
Ocimum 360 ulionyesha wazi kuwa wakulima asilimia 85 huhifadhi<br />
msitu. Matokeo kamili ya utafiti huo ni kama ifuatavyo; Asilimia 49 ya<br />
wakulima hao husambaza elimu ya uhifadhi wa misitu kwa wenzao,<br />
asilimia 59 wamepunguza ukusanyaji kuni , chakula cha ng’ombe na<br />
mbao msituni humo, asilimia 37 wamewakataza wanajamii wengine<br />
dhidi ya kutumia msitu vibaya na asilimia 5 ya wakulima wameripoti<br />
visa vya uwindaji haramu kwa utawala wa mkoa. Uvunaji wa Ocimum<br />
hauharibu mazingira, mimea ya Ocimum humea tena baada ya<br />
kukauka na hivyo jamii hupata kipato kisichoisha. Bidhaa za Naturub<br />
huwa na onyo na mawaidha ya kuhimiza uhifadhi wa mazingira.<br />
MATOKEO YA KIJAMII<br />
Kikundi cha Muliru kimetanda miongoni mwa wilaya 5<br />
zinazouzunguka msitu wa Kakamega ,na idadi ya watu ni kama2,500<br />
na wanachama wa kikundi wakiwa ni 360.Wengi wa watu katika<br />
eneo hili wametengwa kiuchumi na wengi ni wachochole walio na<br />
mashamba madogo mno yasiyoweza kuwakimu kimaisha. Kikundi<br />
hiki cha Muliru kimebadili hii hali kwa kuwapa wenyeji fursa ya kazi<br />
na njia ya kujipatia riziki. Takribani watu 8 wa eneo hili wamepata<br />
kazi ya kudumu mitamboni . Isitoshe takribani wakulima 900 wana<br />
kazi ya kulima mmea huu hadi sasa vidonge 400,000 vimeuzwa kote<br />
nchini hususan kwenye maduka makuu kama vile; Uchumi,Turskeys<br />
na Eastmat. Naturub vilevile hupatikana kwenye maduka ya dawa<br />
nchini Kenya. Wakulima hupata marupurupu yao mara tatu kwa<br />
mwaka na wameona kipato chao kikiongezeka kwa asilimia 300<br />
tangu mradi huu kuanzishwa.<br />
Faisa Nynginezo<br />
Kutokana na utafiti wa awali uliofanywa na kikundi hiki cha Muliru,<br />
kulipatikana faida nyinginezo kama; asilimia 31 ya wakulima hutumia<br />
hela walizozipata kutoka kwa mradi huu kuanzisha biashara ndogo<br />
ndogo na hivyo kuongezea kipato chao. Isitoshe , asilimia 83.5<br />
hutumia hela zao ili kununulia familia zao chakula . Asilimia 57 hulipia<br />
watoto karo ,asilimia 26 hujinunulia nguo, asilimia17.65 hutumia<br />
pesa hizo kukarabati nyumba zao. Wenyeji vilevile wamenufaika<br />
na elimu ya kibiashara wanaopewa na mashirika mengine. Mradi<br />
huu vilevile umeinua kiwango cha maisha ya wenyeji. Wakulima<br />
nao ni kati ya washika dau wa shirika hili . Wakulima kwa sasa wana<br />
ufahamu mkuu kuhusu kilimo, uwekaji pesa na kuhusu umuhimu<br />
wa mshikamano wa kijamii.<br />
Mradi huu aidha umehimiza usawa wa kijinsia ambapo jamii ya hapa<br />
imekubali ukweli kuwa uchumaji ni kazi ya mke na mume .Wanawake<br />
pia wanastahili kuchaguliwa kwenye nyadhifa za uongozi<br />
7
Jinsi ya Kudumisha Mradi Huu<br />
JINSI YA KUDUMISHA MRADI HUU<br />
Kikundi cha Muliru kilikua na mpango wa miaka kumi ya matumizi<br />
ya faida inayotokana na mauzo ya Naturub. Mpango wenyewe ulikua<br />
kama ufuatao; asilimia 10 kusaidia katika uhifadhi wa msitu wa<br />
Kakamega, asilimia 10 iingie kwenye mfuko wa maendeleo ya jamii<br />
inayozunguka msitu Kakamega, asilimia 60 kupewa wanachama wa<br />
kikundi cha Muliru, na asilimia 20 kuingia kwenye mfuko wa kusaidia<br />
utafiti. Kikundi kinachokisia kuwa shirika hili litajisimamia kifedha<br />
na kukua zaidi. Naturub ndiyo dawa pekee ya kienyeji kupata usajili<br />
wa kiserikali pamoja na shirika la madaktari linalosimamia dawa<br />
na sumu nchini. Upelelezi wa siri kuhusu Naturub umeonyesha<br />
kuwa dawa hii inazaa takribani shilingi million 100 kwa kila mwaka<br />
mijini. Kikundi cha Muliru kimetegemea mashirika ya nchini na<br />
kimataifa katika kufikia malengo yake. Muliru imewahi kushirikiana<br />
na kampuni kadhaa za matangazo na utangazaji katika kuendeleza<br />
malengo yake. Mashirika mengine ambayo yamefadhili Muliru ni<br />
kama chuo kikuu cha Nairobi, kituo cha dunia cha misitu, shirika la<br />
wanyama pori la Kenya (KWS) na mengineyo. Maono mengine ya<br />
kikundi ni kuongeza usalishaji, kutafuta masoko mengine ya nchini<br />
na kitaifa, kufanya utafiti zaidi kuhusu mmea huu kuwapa mafunzo<br />
zaidi wakulima na kuimarisha na kuhimiza wanawake na vijana<br />
kuunga mkono mradi huu.<br />
MAONO<br />
Budongo nchini Uganda. Kulingana na maoni ya kikundi cha Muliru,<br />
mafunzo yanayobadilishwa miongoni mwa watu wenye rika moja<br />
huzama na kueleweka zaidi<br />
WAHISANI<br />
• Kituo cha kimataifa cha uchunguzi wa Wadudu<br />
• Chuo Kikuu cha Nairobi<br />
• Shirika la Dunia la Misitu<br />
• Taasisi ya Utafiti waMisitu la Kenya [KEFRI]<br />
• Shirika la Wanyama Pori la Kenya [KWS]<br />
• Shirika la[GBDI]<br />
• Wakfu wa Ford<br />
• Wakfu wa Bio Vision<br />
• Wakifu wa Macarthur<br />
• Huduma za kiuduma za Kijerumani [DED]<br />
• PACT-Kenya/USAid<br />
• WHO Multilateral <strong>Initiative</strong> on Malaria/Research and Training in<br />
Tropical Diseases (TDR)<br />
Kikundi hiki kimebadilisha mawazo ya mradi na wanajamii wa nchi<br />
kama Uganda, Tanzania, Afrika kusini na Nigeria na vilevile jamii<br />
zingine za humu nchini. Zaidi ya watu 830 wametutembelea ndiposa<br />
wapate masomo ya moja kwa moja . Mafunzo yanayopatikana kutoka<br />
kwa mradi huu yamesambazwa kupitia kwa mihadhara ,uigizaji,<br />
utambaji na matembeleano. Isitoshe , mradi huu umeonyeshwa<br />
na kutangazwa na vyombo mbalimbali vya kimataifa kama redio<br />
na televisheni. Kutokana na utangazaji huo, mradi wetu umeigwa<br />
na jamii kadhaa mfano kikundi cha kuifadhi misitu cha mashariki<br />
ya Usambara nchini Tanzania na kikundi kinachohifadhi misitu ya<br />
8
MAREJELEO YA ZIADA<br />
• Muliru Farmers Conservation Group PhotoStory (Vimeo) vimeo.com/15780379<br />
• Video on Muliru Farmers Conservation Group (Vimeo) vimeo.com/43207923<br />
Masimulizi kuhusu miradi mingine, bonyeza hapa:<br />
<strong>Equator</strong> <strong>Initiative</strong><br />
Environment and Energy Group<br />
United Nations Development Programme (UNDP)<br />
304 East 45th Street, 6th Floor<br />
New York, NY 10017<br />
Tel: +1 646 781-4023<br />
www.equatorinitiative.org<br />
Mradi wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa ndio unaoendesha miradi ya maendeleo ya Umoja wa Mataifa kote ulimwenguni<br />
kwa kutoa mwito wa mageuzi na kuelekeza mataifa kwa maarifa, na malighafi ili kusaidia watu kujiimarisha kimaisha.<br />
Mradi huu wa <strong>Equator</strong> huleta pamoja Umoja wa Mataifa , serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali, wafanyibiashara na makundi ya<br />
mashinani ili kutambua na kuimaliza maendeleo himili kwa watu na jamii kwa jumla.<br />
©2012 Haki Zote ni za Mradi wa <strong>Equator</strong>