You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
NGUVU ZA MWANAUME<br />
Jogoo halipandi mtungi?<br />
Ili watoto wasielewe wakubwa hupenda kusema ‘jogoo<br />
halipandi mtungi’! Hili ni tatizo la uume kutokusimama au<br />
Kiswahili sanifu, uhanithi. Watu wenye tatizo hili huchekwa<br />
na hivyo kufanya washindwe kutafuta ushauri wa kitaalamu.<br />
Kufanya hivyo ni kuwanyima haki yao ya msingi ya afya<br />
ya uzazi.<br />
Tuliteta na Dk Constantine Kibela na Dk Lugano Kiswaga wa<br />
Hospitali ya Wilaya ya Mkuranga kuhusu hili kwani tumekuwa<br />
tukipokea maswali lukuki ya wasomaji.<br />
Kulikoni jogoo kushindwa?<br />
“Hili ni tatizo ambalo mtu anaweza kuzaliwa nalo au<br />
kulipata katika kipindi chochote cha maisha yake.<br />
Linaweza kuwa la kudumu au la muda tu,” anasema<br />
Dk Constantine. Kumekuwa na uzushi kwamba kitovu<br />
cha mtoto kikiangukia kwenye uume mtoto atakuwa<br />
hanithi, jambo ambalo si kweli.<br />
Sababu za uhanithi:<br />
n Karibu 60% ya watu wenye tatizo hili hutokana na<br />
sababu za kisaikolojia, umri, matatizo ya kimazingira<br />
mfano: msongo wa mawazo kutokana na kukosa<br />
kazi, fedha, matatizo ya kifamilia, hofu ya kuambukizwa<br />
magonjwa, hofu ya kutumia kondom nk<br />
n Magonjwa sugu katika mwili, kwa mfano, ugonjwa<br />
wa ini, figo, kisukari, kifua kikuu nk<br />
n Matumizi yaliyokithiri ya dawa za kulevya au<br />
pombe<br />
n Vyakula tunavyokula vinaweza kusababisha uhanithi,<br />
kwani mrundikano wa mafuta katika mishipa<br />
ya damu unasababisha damu kushindwa kufika<br />
vizuri katika uume ili kuuwezesha kusimama.<br />
Tatizo hili halipaswi kuwa la mwanamume<br />
tu bali mwanamke anao<br />
uwezo wa kumsaidia mwenzi<br />
wake katika kutafuta ushauri na<br />
hata kumsaidia kuondoa hofu<br />
aliyonayo.<br />
Je, tatizo hili<br />
linatibika?<br />
Kitu muhimu ni kutambua<br />
chanzo cha tatizo lenyewe<br />
na kujitokeza kupata ushauri.<br />
Wanaume wengi wanashindwa<br />
kutafuta ushauri juu ya suala<br />
kama hili kwa kuona haya eti<br />
“mwanaume mzima ijulikane<br />
mi hanithi!” Wengine hufikia<br />
hatua ya kuigiza kama wana<br />
uhusiano wa kujamiiana<br />
ilimradi tu waonekane rijali.<br />
Kwa hisani ya TMEP,<br />
Mradi unaodhaminiwa na RFSU<br />
machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />
9