21.06.2013 Views

Haliuzwi - Femina HIP

Haliuzwi - Femina HIP

Haliuzwi - Femina HIP

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

NGUVU ZA MWANAUME<br />

Jogoo halipandi mtungi?<br />

Ili watoto wasielewe wakubwa hupenda kusema ‘jogoo<br />

halipandi mtungi’! Hili ni tatizo la uume kutokusimama au<br />

Kiswahili sanifu, uhanithi. Watu wenye tatizo hili huchekwa<br />

na hivyo kufanya washindwe kutafuta ushauri wa kitaalamu.<br />

Kufanya hivyo ni kuwanyima haki yao ya msingi ya afya<br />

ya uzazi.<br />

Tuliteta na Dk Constantine Kibela na Dk Lugano Kiswaga wa<br />

Hospitali ya Wilaya ya Mkuranga kuhusu hili kwani tumekuwa<br />

tukipokea maswali lukuki ya wasomaji.<br />

Kulikoni jogoo kushindwa?<br />

“Hili ni tatizo ambalo mtu anaweza kuzaliwa nalo au<br />

kulipata katika kipindi chochote cha maisha yake.<br />

Linaweza kuwa la kudumu au la muda tu,” anasema<br />

Dk Constantine. Kumekuwa na uzushi kwamba kitovu<br />

cha mtoto kikiangukia kwenye uume mtoto atakuwa<br />

hanithi, jambo ambalo si kweli.<br />

Sababu za uhanithi:<br />

n Karibu 60% ya watu wenye tatizo hili hutokana na<br />

sababu za kisaikolojia, umri, matatizo ya kimazingira<br />

mfano: msongo wa mawazo kutokana na kukosa<br />

kazi, fedha, matatizo ya kifamilia, hofu ya kuambukizwa<br />

magonjwa, hofu ya kutumia kondom nk<br />

n Magonjwa sugu katika mwili, kwa mfano, ugonjwa<br />

wa ini, figo, kisukari, kifua kikuu nk<br />

n Matumizi yaliyokithiri ya dawa za kulevya au<br />

pombe<br />

n Vyakula tunavyokula vinaweza kusababisha uhanithi,<br />

kwani mrundikano wa mafuta katika mishipa<br />

ya damu unasababisha damu kushindwa kufika<br />

vizuri katika uume ili kuuwezesha kusimama.<br />

Tatizo hili halipaswi kuwa la mwanamume<br />

tu bali mwanamke anao<br />

uwezo wa kumsaidia mwenzi<br />

wake katika kutafuta ushauri na<br />

hata kumsaidia kuondoa hofu<br />

aliyonayo.<br />

Je, tatizo hili<br />

linatibika?<br />

Kitu muhimu ni kutambua<br />

chanzo cha tatizo lenyewe<br />

na kujitokeza kupata ushauri.<br />

Wanaume wengi wanashindwa<br />

kutafuta ushauri juu ya suala<br />

kama hili kwa kuona haya eti<br />

“mwanaume mzima ijulikane<br />

mi hanithi!” Wengine hufikia<br />

hatua ya kuigiza kama wana<br />

uhusiano wa kujamiiana<br />

ilimradi tu waonekane rijali.<br />

Kwa hisani ya TMEP,<br />

Mradi unaodhaminiwa na RFSU<br />

machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />

9

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!