You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
MAMBO MAPYA<br />
Unapofika Kimanzichana<br />
ukiulizia watu maarufu<br />
eneo lile wa kwanza<br />
kutajwa ni msanii 20%!<br />
Nasi tukasema si vibaya<br />
‘tukimpaisha’ kwa staili ya<br />
pekee, tukatinga nyumbani<br />
kwao japo kupata picha na<br />
familia yake! Unamuona<br />
mrembo Jema? (wa kwanza<br />
kulia). Huyo ni mtoto wa<br />
20% na aliyeshika majarida<br />
ni mama mzazi wa msanii<br />
20%.<br />
Madogo hawa wanapiga bonge la ‘kolabo’ kulishambulia jukwaa!<br />
Ilikuwa ni katika sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar huko Mkuranga<br />
ambapo mtoto Ramadhani Kasimu (aliyeshika ‘mic’) alikonga<br />
nyoyo za umati na wimbo “Naenda kusema kwa mama” wa msanii<br />
Asley. Huyo dogo mwingine pichani ni Jaffery A. Jaffery, alikwenda<br />
kutunza akanogewa akabaki uwanjani kumpiga tafu mwenzake!<br />
Naye alitunzwa ‘mshiko’ wa uhakika!<br />
6 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />
Kibubu bwana!<br />
Hahaha!<br />
Hiki kinaitwa kibubu. Inawezekana<br />
kili’batizwa’ jina hilo kwakuwa ‘hakisemi’,<br />
yaani hakionyeshi kilichomo<br />
ndani yake! Kibubu ni benki kiaina!<br />
Kinunue au kichongeshe uwe nacho<br />
nyumbani, ‘tupia’ humo fedha ndogondogo<br />
kila siku, jiti, bati, jero, buku<br />
na hata msimbazi kadri unavyozisaka.<br />
Baada ya mwaka au muda fulani uliojipangia,<br />
kivunje na utaona maajabu!<br />
Watu wamenunua mashamba kwa<br />
vibubu!