You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
30, tukachanga pesa ikafikia Sh<br />
105,000 na kila mmoja akanunua<br />
hisa kwa kadri awezavyo kwani<br />
aliyenunua hisa nyingi alikuwa<br />
na uwezo wa kukopa pesa nyingi<br />
pia.<br />
Wanasema ng’ombe wa maskini<br />
hazai na hata akizaa huzaa<br />
dume! Hawa nao baadaye<br />
walisepa na pesa za wanachama<br />
na hadi leo kesi iko mahakamani.<br />
Hapa napo nilikula hasara ya Sh<br />
52,000 hivi. Sikuchoka!<br />
Baadaye ilianzishwa SACCOS<br />
inaitwa Belita nikalipa kiingilio na michango<br />
nikawa mwanachama. Nilianza na mkopo wa<br />
Sh 50,000, nikaendelea kupanda na hivi majuzi<br />
nimekopa milioni nne. Narejesha bila tabu kwa<br />
kuwa nimewekeza fedha hizo katika biashara.<br />
Naishukuru mikopo maana imepanua biashara<br />
zangu, hivi sasa namiliki mkokoteni, baiskeli<br />
kumi, bajaj na nina mpango wa kuanza kujenga<br />
nyumba nyingine ya ukweli!<br />
Mkokoteni na baiskeli nakodisha, bajaj pia<br />
inakodishwa kubeba mazao na wagonjwa<br />
na nimepata tenda ya kusafirisha wanafunzi.<br />
Vyote hivi vinalipa kichizi!<br />
Mingo zote hizo zinaniwezesha kurejesha<br />
mkopo na kusomesha watoto wangu watatu<br />
na pesa ya kubadilisha<br />
mboga hainipigi chenga.<br />
Akaunti yangu ya benki<br />
nayo naendelea kuitunisha<br />
kwa faida inayobaki baada<br />
ya kutoa marejesho na<br />
matumizi.<br />
Nitaendelea kukopa,<br />
kuwekeza na kurejesha<br />
kwani mikopo ndiyo<br />
iliyonifikisha hapa. Cha<br />
muhimu ni malengo,<br />
nidhamu katika matumizi<br />
na marejesho na pia<br />
kujiwekea akiba benki.<br />
Nasema tena, NITAKOPA<br />
MPAKA KIELEWEKE!<br />
machi-aprili 2012 2012 Si Si Mchezo!<br />
5 5