You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
STORI YANGU<br />
Mikopo imenitoa<br />
Naitwa Juma Kapute aka<br />
Chaudele, jina ambalo kwa<br />
Kizaramo linamaanisha<br />
kitindamimba. Kimanzichana<br />
ndo makazi yangu ingawa<br />
asili yangu ni Mngindo kutoka Lindi.<br />
Baada ya kuhitimu elimu ya msingi niliajiriwa<br />
katika mgahawa ambako nilipiga mzigo kwa<br />
miaka minne. Wakati huo nilikuwa nikitunza<br />
kiasi fulani cha mshiko katika mshahara wangu<br />
kila mwezi, hivyo nikawa nimedunduliza hadi<br />
Sh 140,000.<br />
Niliacha kazi na nikaitumia fedha hiyo<br />
kufungua mgahawa wangu na kwa kuwa kwa<br />
mapishi niko juu, pale mgahawani nilikuwa<br />
nikipiga mzigo mwenyewe, ingawa kwa sasa<br />
nasaidiana na mke wangu kwani tuna miradi<br />
mingine kibao.<br />
Niliendesha ‘kijiwe’ hicho huku nikiweka<br />
kiasi fulani cha faida benki, niliamua kujenga<br />
nyumba na kununua samani lakini nikawa na<br />
ndoto ya kupanua biashara.<br />
Wakaja watu wa FINCA ambao walikuwa<br />
wanatoa mikopo kwa wanawake, hivyo mke<br />
wangu alichangamkia mkopo ili afanye biashara<br />
ndogondogo. Kwa kuwa hatukuwa tumejipanga<br />
fresh tulishindwa kurejesha. Ilifika wakati<br />
wakaja kutunyang’anya vitu vyote ndani, hivyo<br />
ikabidi nitumie akiba ya benki kuokoa jahazi.<br />
4 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />
Ila sikukata tamaa, nilijiunga na Kasi Mpya<br />
SACCOS ili niendelee kufukuzia ndoto<br />
zangu. Nikalipa kiingilio kutokana na faida<br />
niliyokuwa nimeipata tena mgahawani<br />
baada ya sakata la FINCA, nikawa nanunua<br />
hisa kila mwezi hadi ikatimia Sh 70,000.<br />
Nikawa na uwezo wa kukopa sh 300,000<br />
ambazo nilizitumia kununulia mbao na<br />
kuziuza. Nikawa narejesha Sh 50,000 kila<br />
mwezi hadi nilipomaliza deni. Nilikuwa na<br />
mpango wa kukopa tena lakini ikatokea<br />
songombingo, SACCOS ikafa na viongozi<br />
wakasepa na mkwanja wote! Imebaki stori!<br />
Baadaye walikuja watu wa VICOBA,<br />
wakatuhamasisha nami nikachangamkia<br />
fursa kama kawa. Tuliunda kundi la watu