21.06.2013 Views

Haliuzwi - Femina HIP

Haliuzwi - Femina HIP

Haliuzwi - Femina HIP

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

STORI YANGU<br />

Mikopo imenitoa<br />

Naitwa Juma Kapute aka<br />

Chaudele, jina ambalo kwa<br />

Kizaramo linamaanisha<br />

kitindamimba. Kimanzichana<br />

ndo makazi yangu ingawa<br />

asili yangu ni Mngindo kutoka Lindi.<br />

Baada ya kuhitimu elimu ya msingi niliajiriwa<br />

katika mgahawa ambako nilipiga mzigo kwa<br />

miaka minne. Wakati huo nilikuwa nikitunza<br />

kiasi fulani cha mshiko katika mshahara wangu<br />

kila mwezi, hivyo nikawa nimedunduliza hadi<br />

Sh 140,000.<br />

Niliacha kazi na nikaitumia fedha hiyo<br />

kufungua mgahawa wangu na kwa kuwa kwa<br />

mapishi niko juu, pale mgahawani nilikuwa<br />

nikipiga mzigo mwenyewe, ingawa kwa sasa<br />

nasaidiana na mke wangu kwani tuna miradi<br />

mingine kibao.<br />

Niliendesha ‘kijiwe’ hicho huku nikiweka<br />

kiasi fulani cha faida benki, niliamua kujenga<br />

nyumba na kununua samani lakini nikawa na<br />

ndoto ya kupanua biashara.<br />

Wakaja watu wa FINCA ambao walikuwa<br />

wanatoa mikopo kwa wanawake, hivyo mke<br />

wangu alichangamkia mkopo ili afanye biashara<br />

ndogondogo. Kwa kuwa hatukuwa tumejipanga<br />

fresh tulishindwa kurejesha. Ilifika wakati<br />

wakaja kutunyang’anya vitu vyote ndani, hivyo<br />

ikabidi nitumie akiba ya benki kuokoa jahazi.<br />

4 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />

Ila sikukata tamaa, nilijiunga na Kasi Mpya<br />

SACCOS ili niendelee kufukuzia ndoto<br />

zangu. Nikalipa kiingilio kutokana na faida<br />

niliyokuwa nimeipata tena mgahawani<br />

baada ya sakata la FINCA, nikawa nanunua<br />

hisa kila mwezi hadi ikatimia Sh 70,000.<br />

Nikawa na uwezo wa kukopa sh 300,000<br />

ambazo nilizitumia kununulia mbao na<br />

kuziuza. Nikawa narejesha Sh 50,000 kila<br />

mwezi hadi nilipomaliza deni. Nilikuwa na<br />

mpango wa kukopa tena lakini ikatokea<br />

songombingo, SACCOS ikafa na viongozi<br />

wakasepa na mkwanja wote! Imebaki stori!<br />

Baadaye walikuja watu wa VICOBA,<br />

wakatuhamasisha nami nikachangamkia<br />

fursa kama kawa. Tuliunda kundi la watu

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!