Haliuzwi - Femina HIP

Haliuzwi - Femina HIP Haliuzwi - Femina HIP

feminahip.or.tz
from feminahip.or.tz More from this publisher
21.06.2013 Views

Mila katika kupambana na VVU Unyago ni sehemu ya utamaduni wa watu wa Pwani ya Tanzania kumfundisha mtoto wa kike anapovunja ungo mambo muhimu yanayohusu afya ya uzazi, usafi na majukumu mengine yanayomhusu. Utamaduni huu umesaidia kwa kiasi kikubwa kuweka njia kwa watu wazima (manyakanga) kuwaandaa wasichana kwa maisha ya utu uzima. Mwisho wa mafunzo ya unyago wasichana ambao huitwa wali hutolewa nje kwa sherehe maalum ya kuhitimu ijulikanayo kama “kunema”. Hatua zimechukuliwa… Asasi isiyokuwa ya kiserikali ya PAYODE (Partnership for Youth Development) katika Halmashauri ya Mji wa Kibaha iliendesha mafunzo shirikishi kwa manyakanga kuhusu afya ya uzazi na kujikinga na maambukizi ya VVU. Mafunzo haya yalisaidia kuboresha uelewa wa manyakanga na kuwajengea stadi za kuingiza elimu hii ndani ya mafunzo ya unyago. Jumla ya manyakanga 40 wamepata mafunzo kupitia PAYODE tangu mwaka 2008. 30 Si Mchezo! machi-aprili 2012 Watu wanasemaje? ZINDUKA Mtazamo uko hivi… Wasichana na wanawake wapo katika hatari zaidi ya kupata maambukizi ya VVU ikilinganishwa na wavulana na wanaume wa umri sawa na wao. Hata hivyo njia rahisi ya kuwafikia vijana hasa wasichana kwa shughuli za uelimishaji kuhusu ujana na makuzi bado ni changamoto kutokana na mila na desturi ya Mtanzania. Ushuhuda unaonyesha kuwa elimu ya unyago inayotolewa na manyakanga hawa waliopatiwa mafunzo imesaidia kupunguza tatizo la wasichana kuachishwa shule kwasababu ya ujauzito katika maeneo ya mradi. Jamii na serikali imefurahishwa na hatua ya PAYODE kutumia utamaduni wa watu wa Pwani kama njia chanya ya kufikishia wasichana elimu ya afya ya uzazi . “Natamani watoto wangu wangeliyajua haya yote kabla,” anasema mwenyekiti wa manyakanga, Mama Blandina Mbaji.

. USHAURI Swali Nina mpenzi ambaye tumekamilisha taratibu zote za ndoa, lakini kabla ya ndoa akapata ujauzito. Baada ya kuanza huduma za kliniki akaonekana ana maambukizi ya VVU, na mimi nilipopimwa nikawa salama. Je, mpenzi wangu huyu anafaa kuoa ? Ushauri tafadhali. Msomaji Si mchezo! Lindi-Pwani Kama mmepima na ukagundua mwenzio ana VVU usimuache. nendeni kwa mshauri nasaha atawashauri jinsi ya kumkinga mtoto na wewe mwenyewe usipate maambukizi na mtaishi kwa raha. Amosi wa Mkuranga Kama kweli unampenda mwenzi wako, nakushauri endelea kuwa naye kama rafiki yako wa karibu sana. Pia kuwa mshauri wake katika hali aliyonayo maana kuwa na VVU siyo kufa na urafiki au uhusiano usivunjike. Ibrahim Manjale, Mkuranga SWALI LA TOLEO LIJALO Pole kaka yangu, kama kweli hiyo mimba ni yako na unampenda mkeo nakushauri umuoe. Kuwa na VVU siyo mwisho wa mapenzi na hakuzuii kuendeleza mipango yenu. Nendeni kwenye kituo cha huduma na tiba kwa ushauri zaidi. Hamisi Nuru Jimowaco-Mkuranga Kuna binti tumependana na nimependa tabia zake. Yuko tayari kuoana nami lakini naogopa kwasababu nimetembea na dada yake ambaye kwa sasa ameolewa. Ila binti huyo sijafanya naye ngono, anasema mpaka tuoane. Naombeni ushauri wenu. Festo Mgaya, Songea. Nawapongeza kwa kupima. Yeyote anayeishi na VVU ana haki zote za kibinadamu ikiwa ni pamoja na kuoa/kuolewa, kuwa na familia n.k. Maamuzi ya kumuoa au kutokumuoa ni yako na yeye. Katika upimaji VVU kuna uwezekano kwa sasa ukawa salama lakini baada ya muda ukakutwa nawe hauko salama. Nenda katika kituo cha ushauri nasaha watakupa elimu ya kuishi na mke mwenye maambukizi ya VVU bila wewe kupata maambukizi na kupata watoto wasio na maambukizi. Asante Betty Liduke ni rafiki mkubwa wa vijana, hata wewe unaweza kulonga naye. Ni msambazaji mkubwa wa wa Jarida la Si Mchezo! Mkoani Njombe. Ni mshauri nasaha na ni mratibu wa kitengo cha udhibiti Ukimwi katika Kampuni ya TANWAT, Njombe. Mwandikie kupitia Jarida la Si Mchezo! Si Mchezo! S. L. P. 2065 Dar es Salaam au tuma ujumbe mfupi wa maandishi kupitia namba 0715 568222 na utuambie kama ungependa uchapishwe. machi-aprili 2012 Si Mchezo! 31

Mila katika kupambana na VVU<br />

Unyago ni sehemu ya utamaduni wa watu wa Pwani<br />

ya Tanzania kumfundisha mtoto wa kike anapovunja<br />

ungo mambo muhimu yanayohusu afya ya uzazi, usafi<br />

na majukumu mengine yanayomhusu. Utamaduni huu<br />

umesaidia kwa kiasi kikubwa kuweka njia kwa watu<br />

wazima (manyakanga) kuwaandaa wasichana kwa<br />

maisha ya utu uzima. Mwisho wa mafunzo ya unyago<br />

wasichana ambao huitwa wali hutolewa nje kwa sherehe<br />

maalum ya kuhitimu ijulikanayo kama “kunema”.<br />

Hatua zimechukuliwa…<br />

Asasi isiyokuwa ya kiserikali ya PAYODE<br />

(Partnership for Youth Development)<br />

katika Halmashauri ya Mji wa Kibaha<br />

iliendesha mafunzo shirikishi kwa<br />

manyakanga kuhusu afya ya uzazi<br />

na kujikinga na maambukizi ya VVU.<br />

Mafunzo haya yalisaidia kuboresha uelewa<br />

wa manyakanga na kuwajengea stadi<br />

za kuingiza elimu hii ndani ya mafunzo<br />

ya unyago. Jumla ya manyakanga 40<br />

wamepata mafunzo kupitia PAYODE<br />

tangu mwaka 2008.<br />

30 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />

Watu wanasemaje?<br />

ZINDUKA<br />

Mtazamo uko hivi…<br />

Wasichana na wanawake<br />

wapo katika hatari zaidi ya<br />

kupata maambukizi ya VVU<br />

ikilinganishwa na wavulana<br />

na wanaume wa umri sawa na<br />

wao. Hata hivyo njia rahisi ya<br />

kuwafikia vijana hasa wasichana<br />

kwa shughuli za uelimishaji<br />

kuhusu ujana na makuzi bado ni<br />

changamoto kutokana na mila<br />

na desturi ya Mtanzania.<br />

Ushuhuda unaonyesha kuwa elimu ya unyago<br />

inayotolewa na manyakanga hawa waliopatiwa<br />

mafunzo imesaidia kupunguza tatizo la<br />

wasichana kuachishwa shule kwasababu ya<br />

ujauzito katika maeneo ya mradi. Jamii na<br />

serikali imefurahishwa na hatua ya PAYODE<br />

kutumia utamaduni wa watu wa Pwani kama<br />

njia chanya ya kufikishia wasichana elimu ya afya<br />

ya uzazi . “Natamani watoto wangu wangeliyajua<br />

haya yote kabla,” anasema mwenyekiti wa<br />

manyakanga, Mama Blandina Mbaji.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!