21.06.2013 Views

Haliuzwi - Femina HIP

Haliuzwi - Femina HIP

Haliuzwi - Femina HIP

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

SAUTI YANGU<br />

Si Mchezo!<br />

<strong>Femina</strong> <strong>HIP</strong><br />

SLP 2065,<br />

DSM<br />

Acheni siasa, leteni<br />

maendeleo<br />

Nakereka sana na Baraza la Madiwani<br />

kugombana na Mkurugenzi wa<br />

Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga.<br />

Kila siku ni mifarakano isiyokuwa na<br />

tija. Mpaka sasa maendeleo hakuna<br />

na hatupigi hatua yoyote mbele.<br />

Miundombinu ni mibovu, hospitali ya<br />

wilaya hakuna chumba cha kuhifadhia<br />

maiti, vijana hawana ajira na maisha<br />

ni magumu kwa ujumla. Nawaomba<br />

viongozi hawa wakae pamoja na kutatua<br />

tofauti zao, washikamane na kutuletea<br />

maendeleo katika wilaya yetu.<br />

Saidi Juma Aina<br />

Mkuranga<br />

28 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />

Kama una chochote<br />

unachotaka kusema<br />

tuandikie ili upate<br />

fursa ya kuwaelimisha<br />

wengine<br />

Maoni yaliyotolewa katika ukurasa huu<br />

ni ya wasomaji, si lazima yalingane na<br />

msimamo wa <strong>Femina</strong> <strong>HIP</strong>.<br />

Wateja wengine<br />

wa saluni...<br />

Sipendi tabia ya baadhi ya wateja wanaokuja<br />

saluni kupata huduma za urembo wa nywele<br />

na nakshi nyingine. Wengi wanajisahau<br />

kwamba hili ni eneo la biashara na kazi.<br />

Wanajazana na kuanza kupiga umbea, wakati<br />

mwingine nafasi inakosekana kwa wateja<br />

wanaohitaji kupata huduma. Hii ni kero<br />

hapa kwetu na mbaya zaidi wanaume nao<br />

wanashiriki mambo haya. Jamani nendeni<br />

maeneo yenu mkafanye vijiwe vya umbea na<br />

majungu mtuache sisi tufanye kazi.<br />

Marium a.k.a Mama Zai<br />

Kimanzichana-Mkuranga<br />

Acheni kutudharau<br />

Kuna imani kwamba ukifanya<br />

kazi nyumba za kulala wageni<br />

maarufu kama guest house,<br />

baa au ukiwa mhudumu wa<br />

hoteli jamii inakuchukulia<br />

kama mhuni. Hii si sahihi hata<br />

kidogo kwani wanaofanya<br />

kazi hizi wanajiheshimu, kama<br />

yeyote yule anayefanya kazi<br />

katika sekta nyingine. Acheni<br />

kuwashikashika wahudumu.<br />

Jua kwamba wapo kazini na<br />

siyo sehemu ya kuendekeza<br />

mapenzi ya kulazimisha.<br />

Heshimu utu wao.<br />

Judith Macha<br />

Mkuranga-Pwani<br />

Wewe pia unaweza kulonga na vijana<br />

wenzako. Tuandike maoni,<br />

ushauri, vichekesho,maswali<br />

nk, weka anuani yako na tuma<br />

ukiambatanisha na picha yako<br />

kwa Mhariri, Jarida la Si Mchezo!,<br />

S.L.P 2065 Dar es Salaam.<br />

simchezo@feminahip.or.tz<br />

Au tumbukiza katika boksi la Si<br />

Mchezo! kama lipo katika eneo<br />

unaloishi.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!