Haliuzwi - Femina HIP
Haliuzwi - Femina HIP Haliuzwi - Femina HIP
26 Si Mchezo! machi-aprili 2012 Ama kweli majuto ni mjukuu! Kijumbe ndo keshatoroka na fedha za mchezo, ameacha vumbi tu! Upatu ni mzuri. Tatizo wengi wetu tunaucheza kienyeji mno!
UKWELI WA MAMBO Yanawakuta wengi! Stori ya Mama Semeni na wenzake haichekeshi bali inasikitisha! Inawezekana hata wewe ama unacheza upatu au una mpango wa kucheza. Inawezekana umeapa kutokucheza tena upatu kwani yaliwahi kukukuta yaliyomkuta Mama Havinitishi na wenzake! Pole! Sio mchezo mbaya Upatu au ‘mchezo’ kama wengi wanavyouita, si jambo baya. Wengi ‘wametoka’ kwa staili hii. Utaukuta mitaani, maofisini, kwa watu ambao ama wako katika ‘kijiwe’ kimoja au wanafanya biashara zinazofanana. Kwa kifupi ni jambo zuri. Ndiyo, kwani si kila mmoja ana uwezo wa kudunduliza vijisenti peke yake hadi mfuko utune. Zaidi ya kuwasaidia watu kuinua mitaji na kujikwamua kimaisha, ‘mchezo’ huu unawasaidia watu kuishi kijamaa, yaani kufahamiana na kusaidiana katika matatizo mbalimbali ya kijamii, wengine wanasema ‘kufa na kuzikana’. Tatizo nini? Tumeshuhudia ngumi zikilika mitaani, watu wakiporomosheana matusi, wengine wakibubujikwa machozi baada ya ‘kuingia chaka’, ukiuliza kulikoni unaambiwa kijumbe ‘kasepa’ na fedha za wanakikundi! Yote haya yanatokea kwa sababu tunaucheza ‘mchezo’ huu kienyeji mno, kama tunavyoona katika stori ya Mama Semeni na wenzake. Walipaswa wakutane, wafanye makubaliano ya kucheza ‘mchezo’, kuwe na orodha ya wanachama iliyoandikwa na zamu za ‘kupokea’, wafanye uchaguzi wa ‘kijumbe’ wajipangie masharti na kuwe na daftari la kusaini mwanachama anapowasilisha mchango na anapopokea. J Kumbuka Ni vizuri muwe ni kikundi cha watu mnaofahamiana vizuri kwa makazi, kipato na tabia, ili kuepusha mambo kwenda mrama. machi-aprili 2012 Si Mchezo! 27
- Page 1 and 2: ISSN: 0856-8995 KATUNI: machi-april
- Page 3 and 4: Femina HIP Mhariri Majuka Ololkeri
- Page 5 and 6: 30, tukachanga pesa ikafikia Sh 105
- Page 7 and 8: VICOBA, SACCOS wana mengi ya ziada
- Page 9 and 10: NGUVU ZA MWANAUME Jogoo halipandi m
- Page 11 and 12: Shost, mie nikipata tu mkopo namtoa
- Page 13 and 14: Anafurahi lakini mwisho wake utakuw
- Page 15 and 16: Hatujaja kwa mazungumzo. Lete chetu
- Page 17 and 18: n Mida ya hisa ilipofika, kila mwan
- Page 19 and 20: Faida za kutumia njia za uzazi wa m
- Page 21 and 22: Baunsa noma! Mshikaji alienda kuiba
- Page 23 and 24: HUDUMA Walianza kama utani! Siku mo
- Page 25: machi-aprili 2012 Si Mchezo! 25
- Page 29 and 30: januari-februari 2012 Si Mchezo! 29
- Page 31 and 32: . USHAURI Swali Nina mpenzi ambaye
UKWELI WA MAMBO<br />
Yanawakuta wengi!<br />
Stori ya Mama Semeni<br />
na wenzake haichekeshi<br />
bali inasikitisha!<br />
Inawezekana hata wewe ama<br />
unacheza upatu au una mpango<br />
wa kucheza. Inawezekana<br />
umeapa kutokucheza tena<br />
upatu kwani yaliwahi kukukuta<br />
yaliyomkuta Mama Havinitishi<br />
na wenzake! Pole!<br />
Sio mchezo mbaya<br />
Upatu au ‘mchezo’ kama<br />
wengi wanavyouita,<br />
si jambo baya. Wengi<br />
‘wametoka’ kwa staili hii.<br />
Utaukuta mitaani, maofisini,<br />
kwa watu ambao ama<br />
wako katika ‘kijiwe’ kimoja<br />
au wanafanya biashara<br />
zinazofanana. Kwa kifupi ni<br />
jambo zuri. Ndiyo, kwani si<br />
kila mmoja ana uwezo wa<br />
kudunduliza vijisenti peke<br />
yake hadi mfuko utune.<br />
Zaidi ya kuwasaidia<br />
watu kuinua mitaji na<br />
kujikwamua kimaisha,<br />
‘mchezo’ huu unawasaidia<br />
watu kuishi kijamaa,<br />
yaani kufahamiana na<br />
kusaidiana katika matatizo<br />
mbalimbali ya kijamii,<br />
wengine wanasema ‘kufa na<br />
kuzikana’.<br />
Tatizo nini?<br />
Tumeshuhudia ngumi zikilika mitaani, watu<br />
wakiporomosheana matusi, wengine wakibubujikwa<br />
machozi baada ya ‘kuingia chaka’, ukiuliza kulikoni<br />
unaambiwa kijumbe ‘kasepa’ na fedha za wanakikundi!<br />
Yote haya yanatokea kwa sababu tunaucheza ‘mchezo’<br />
huu kienyeji mno, kama tunavyoona katika stori ya Mama<br />
Semeni na wenzake.<br />
Walipaswa wakutane, wafanye makubaliano ya kucheza<br />
‘mchezo’, kuwe na orodha ya wanachama iliyoandikwa<br />
na zamu za ‘kupokea’,<br />
wafanye uchaguzi wa<br />
‘kijumbe’ wajipangie<br />
masharti na kuwe<br />
na daftari la kusaini<br />
mwanachama<br />
anapowasilisha mchango<br />
na anapopokea.<br />
J Kumbuka<br />
Ni vizuri muwe ni kikundi<br />
cha watu mnaofahamiana<br />
vizuri kwa makazi, kipato<br />
na tabia, ili kuepusha<br />
mambo kwenda mrama.<br />
machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />
27