You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
n Mida ya hisa ilipofika, kila<br />
mwanachama alinunua kadri ya<br />
uwezo wake<br />
Wanachama<br />
wanakopaje?<br />
z Anajaza fomu (tunazo)<br />
z Inasainiwa na wadhamini<br />
wawili ambao lazima wawe ni<br />
wanachama wa kikundi<br />
z Maombi yatasomwa mbele ya<br />
wanakikundi wote tunapokutana<br />
na yatajadiliwa<br />
z Ikipitishwa anakopeshwa, na<br />
kiwango cha juu ni mara tatu<br />
ya hisa alizonazo.<br />
z Anatakiwa kuanza kurejesha<br />
baada ya mwezi mmoja na<br />
katika miezi mitatu lazima awe<br />
amemaliza<br />
z Tunatoza riba ya asilimia 10 ya<br />
mkopo<br />
z Anayeshindwa kulipa tunachukua<br />
hisa zake zote pamoja<br />
na za wadhamini wake<br />
n Wanauziana sukari ili kutunisha mfuko.<br />
Ni kwa mkopo na wiki ijayo kila mmoja<br />
atapaswa kulipa!<br />
Mna vyanzo vingine vya mapato?<br />
n Tuna shamba la kikundi ambapo tunalima mihogo,<br />
matunda na mboga<br />
n Tuna mfuko wa jamii ambao tunachangia wenyewe<br />
kwa ajili ya kusaidia wenye matatizo na kugharamia<br />
shughuli za kikundi<br />
n Tunanunua sukari kwa jumla na kuuziana kwa rejareja<br />
n Tumepata mafunzo ya kutengeneza sabuni, hivyo<br />
tunatengeneza na kuuziana<br />
n Wachelewaji katika vikao tunawatoza faini ya sh 500,<br />
ili kutunisha mfuko<br />
Ujumbe?<br />
n Kikao kimefungwa, Mwenyekiti, Dora<br />
Danda na Katibu wake Moshi M. Manda<br />
wanaweka kumbukumbu sawa.<br />
Ndiyo. Vikundi vya kuweka na kukopa ni vizuri. Tumeshuhudia<br />
wanachama wenzetu wakianzisha biashara na hata kujenga<br />
nyumba za kisasa kwa kuweka na kukopa. Nanyi pia mnaweza<br />
kuanzisha!<br />
machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />
17