Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
TULICHOVUNA<br />
Tunajali VICOBA imetulia<br />
n Wakati wakisubiri wenzao kwa kikao, nasi<br />
‘tukawatwanga’ Si Mchezo! wapate ujumbe’<br />
“likuwa ni Jumatatu tuliiivu majira ya mchana.<br />
Kama tulivyokuwa tumekubaliana, mtu<br />
mmoja baada ya mwingine aliwasili katika kivuli<br />
cha mwembe na hatimaye tukajikuta tumetimia<br />
20. Penye wengi hapaharibiki neno, mmoja<br />
wetu alijitolea kuwa kiongozi wa muda, akatuongoza<br />
katika kuanzisha kikundi chetu”.<br />
Hivi ndivyo ilivyoazishwa Tunajali VICOBA, kikundi<br />
cha kuweka na kukopa cha wanakijiji wa Mwanambaya,<br />
Mkuranga. Kikundi hiki kilianzishwa Juni 28,<br />
2003 na hadi sasa kina wanachama 31, kama anavyosimulia<br />
Katibu wa kikundi hicho, Moshi Mfaume<br />
Manda.<br />
Enhe, mkutano uliendaje?<br />
Huo ulikuwa ni mkutano wetu wa kwanza.<br />
Alikuwepo Afisa Maendeleo wa Kata kushuhudia<br />
kinachoendelea. Tulijiundia katiba,<br />
kisha tukafanya uchaguzi wa viongozi. Tunao<br />
viongozi wanane, Mwenyekiti, Katibu,<br />
Mtunza Hazina, wahesabu fedha wawili na<br />
watunza funguo watatu.<br />
16 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />
n Kama kawa, wana sukari, sabuni ya maji<br />
(kwenye kidumu), midamida ikifika watauziana<br />
Mnapokutana mnafanya nini?<br />
Kila Alhamisi saa nane mchana tunakutana:<br />
l Mwenyekiti anafungua mkutano<br />
l Wanaodaiwa sabuni na sukari wanalipa<br />
madeni (ni mradi wa kikundi)<br />
l Tunachangia Mfuko wa Jamii (kila mwanachama<br />
anachangia sh 1,000 kwa mwezi)<br />
l Tunanunua hisa, yaani akiba (fedha) mtu<br />
anayoamua kuweka (bei ya hisa ni sh 500<br />
na mtu anaweza kununua hadi hisa 5 kwa<br />
wakati mmoja)<br />
l Waliokopeshwa fedha wanarejesha<br />
l Tunasoma barua za maombi ya mikopo<br />
(kama zipo)<br />
l Tunawakopesha wale ambao maombi yao<br />
yamepitishwa na kikundi<br />
l Tunauziana sukari na sabuni (kwa<br />
mkopo)<br />
l Katibu anasoma taarifa ya mapato na<br />
matumizi<br />
l Mwenyekiti anafunga kikao