21.06.2013 Views

Haliuzwi - Femina HIP

Haliuzwi - Femina HIP

Haliuzwi - Femina HIP

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

TULICHOVUNA<br />

Tunajali VICOBA imetulia<br />

n Wakati wakisubiri wenzao kwa kikao, nasi<br />

‘tukawatwanga’ Si Mchezo! wapate ujumbe’<br />

“likuwa ni Jumatatu tuliiivu majira ya mchana.<br />

Kama tulivyokuwa tumekubaliana, mtu<br />

mmoja baada ya mwingine aliwasili katika kivuli<br />

cha mwembe na hatimaye tukajikuta tumetimia<br />

20. Penye wengi hapaharibiki neno, mmoja<br />

wetu alijitolea kuwa kiongozi wa muda, akatuongoza<br />

katika kuanzisha kikundi chetu”.<br />

Hivi ndivyo ilivyoazishwa Tunajali VICOBA, kikundi<br />

cha kuweka na kukopa cha wanakijiji wa Mwanambaya,<br />

Mkuranga. Kikundi hiki kilianzishwa Juni 28,<br />

2003 na hadi sasa kina wanachama 31, kama anavyosimulia<br />

Katibu wa kikundi hicho, Moshi Mfaume<br />

Manda.<br />

Enhe, mkutano uliendaje?<br />

Huo ulikuwa ni mkutano wetu wa kwanza.<br />

Alikuwepo Afisa Maendeleo wa Kata kushuhudia<br />

kinachoendelea. Tulijiundia katiba,<br />

kisha tukafanya uchaguzi wa viongozi. Tunao<br />

viongozi wanane, Mwenyekiti, Katibu,<br />

Mtunza Hazina, wahesabu fedha wawili na<br />

watunza funguo watatu.<br />

16 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />

n Kama kawa, wana sukari, sabuni ya maji<br />

(kwenye kidumu), midamida ikifika watauziana<br />

Mnapokutana mnafanya nini?<br />

Kila Alhamisi saa nane mchana tunakutana:<br />

l Mwenyekiti anafungua mkutano<br />

l Wanaodaiwa sabuni na sukari wanalipa<br />

madeni (ni mradi wa kikundi)<br />

l Tunachangia Mfuko wa Jamii (kila mwanachama<br />

anachangia sh 1,000 kwa mwezi)<br />

l Tunanunua hisa, yaani akiba (fedha) mtu<br />

anayoamua kuweka (bei ya hisa ni sh 500<br />

na mtu anaweza kununua hadi hisa 5 kwa<br />

wakati mmoja)<br />

l Waliokopeshwa fedha wanarejesha<br />

l Tunasoma barua za maombi ya mikopo<br />

(kama zipo)<br />

l Tunawakopesha wale ambao maombi yao<br />

yamepitishwa na kikundi<br />

l Tunauziana sukari na sabuni (kwa<br />

mkopo)<br />

l Katibu anasoma taarifa ya mapato na<br />

matumizi<br />

l Mwenyekiti anafunga kikao

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!