Haliuzwi - Femina HIP
Haliuzwi - Femina HIP Haliuzwi - Femina HIP
ISSN: 0856-8995 KATUNI: machi-aprili 2012 Si Mchezo! Haliuzwi MIKOPO imenitoa 1
- Page 2 and 3: Mimi na mamsapu hatutaki utani! Tun
- Page 4 and 5: STORI YANGU Mikopo imenitoa Naitwa
- Page 6 and 7: MAMBO MAPYA Unapofika Kimanzichana
- Page 8 and 9: 8 Si Mchezo! machi-aprili 2012 MAMB
- Page 10 and 11: HADITHI YA PICHA 10 ‘MKOPO WA NGO
- Page 12 and 13: 12 Mungu mkubwa! Japo nina kazi ya
- Page 14 and 15: JE, WAJUA? Kabla ya kukopa jipange!
- Page 16 and 17: TULICHOVUNA Tunajali VICOBA imetuli
- Page 18 and 19: CHEZASALAMA Huyu ndiye mwanamume wa
- Page 20 and 21: BURUDANI Wimbo: Vinapanda bei Msani
- Page 22 and 23: Minyoo bwana! Hahahahaaaa! Watu bwa
- Page 24 and 25: KATUNI upatu au hupati? Wanawake Mt
- Page 26 and 27: 26 Si Mchezo! machi-aprili 2012 Ama
- Page 28 and 29: SAUTI YANGU Si Mchezo! Femina HIP S
- Page 30 and 31: Mila katika kupambana na VVU Unyago
- Page 32: 32 Si Mchezo! machi-aprili 2012
ISSN: 0856-8995<br />
KATUNI:<br />
machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />
<strong>Haliuzwi</strong><br />
MIKOPO<br />
imenitoa<br />
1
Mimi na mamsapu<br />
hatutaki utani!<br />
Tunadunduliza vijisenti<br />
vyetu taratiiibu.<br />
Wenyewe tumejiwekea<br />
malengo. Hata wewe<br />
unaweza.<br />
2 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />
Ndiyo,<br />
Bamsapu anatunza<br />
funguo, mie natunza<br />
kibubu. Mpo? Zama<br />
ndani ya toleo hili<br />
ujifunze kuhusu vikundi<br />
vya kuweka na kukopa<br />
na hata upatu! Watu<br />
wanafaidika bwana,<br />
asikwambie mtu!<br />
Si Mchezo! Huzalishwa na<br />
kusambazwa.<br />
Si Mchezo! husambazwa.<br />
Lilikozalishwa toleo hili.
<strong>Femina</strong><br />
<strong>HIP</strong><br />
Mhariri<br />
Majuka Ololkeri<br />
Pendo Mashulano<br />
Mwandishi<br />
Ng’orongo Nyamoni<br />
Washauri<br />
Betty Liduke<br />
Gaure Mdee<br />
Raphael Nyoni<br />
Mkurugenzi Mtendaji<br />
Dr. Minou Fuglesang<br />
Machapisho na Uzalishaji<br />
Amabilis Batamula<br />
Jiang Alipo<br />
Katuni na Usanifu<br />
BabaTau, Inc.<br />
Mpiga Chapa<br />
Jamana Printers Ltd<br />
Shughuli za Nje<br />
Constancia Mgimwa<br />
Nashivai Mollel<br />
Gloria Mkoloma<br />
Christine Bisangwa<br />
Rashid Kejo<br />
Usambazaji<br />
EAM Logistic Ltd<br />
<strong>Femina</strong> <strong>HIP</strong> na Washirika<br />
Si Mchezo! limefanyika kwa hisani<br />
kubwa ya Serikali za Sweden (Sida),<br />
Denmark (DANIDA) na Marekani<br />
kupitia USAID kama sehemu ya<br />
ufadhili wa PEPFAR kwa shirika la<br />
FHI360 mradi wa UJANA, PSI mradi<br />
wa HUSIKA pamoja na HIVOS. Toleo<br />
hili limefanyika kwa ushirikiano na<br />
JHU-CCP/TCCP na RFSU.<br />
Yaliyomo humu ndani ni jukumu la<br />
<strong>Femina</strong> <strong>HIP</strong> na hayawakilishi maoni<br />
au mitazamo ya wafadhili.<br />
Wasiliana nasi kwa:<br />
S.L.P. 2065, Dar es Salaam<br />
Simu: (22) 212 8265, 2126851/2<br />
Fax: (22) 2110842<br />
email: simchezo@feminahip.or.tz<br />
Si Mchezo! huchapishwa na<br />
<strong>Femina</strong> <strong>HIP</strong>.<br />
Sms: 0715 568222<br />
YALIYOMO<br />
4 Stori Yangu: Mikopo imenitoa<br />
6 Mambo mapya:<br />
8 Mambo ya Fedha: Zijue Vicoba<br />
10 Hadithi ya Picha: Mkopo wa ngoma!<br />
14 Je, Wajua: Kabla ya kukopa jipange<br />
16 Tulichovuna: Tunajali Vicoba imetulia!<br />
18 Chezasalama: Mwanamume wa ukweli...<br />
20 Burudani: Vinapanda bei<br />
22 Pasipo na Daktari: Minyoo bwana!<br />
23 Huduma: Walianza kama utani<br />
24 Katuni: Upatu unapogeuka Hupati!<br />
27 Ukweli wa Mambo: Yanawakuta wengi<br />
30 Ujana: Mila katika kupambana na VVU<br />
31 Ushauri<br />
TAHARIRI<br />
Mamboz? Najua umeitikia pouwaaaa! Katika ‘kulipika’ toleo<br />
hili la 59, tuliwazukia wakazi wa Mkuranga. Ingawa tuliweka<br />
kambi wilayani, mishemishe zetu zilikuwa Kimanzichana na<br />
kwingineko vijijini. Tulikula nao stori kibao kuhusu mambo ya<br />
fedha, vikundi vya kuweka na kukopa, hususan SACCOS na<br />
VICOBA. Hatukusahau hata ule ‘mchezo’ wetu maarufu, UPATU!<br />
Nakuacha uzame ndani, nisikuharibie utamu. Kila la kheri!<br />
Pendo<br />
Tuanzie<br />
buku mbili<br />
Ndo<br />
naandika<br />
hivyo..!<br />
“Mmh! sasa<br />
umaskini<br />
baibai”<br />
machi-aprili 2012 Si Si Mchezo!<br />
3
STORI YANGU<br />
Mikopo imenitoa<br />
Naitwa Juma Kapute aka<br />
Chaudele, jina ambalo kwa<br />
Kizaramo linamaanisha<br />
kitindamimba. Kimanzichana<br />
ndo makazi yangu ingawa<br />
asili yangu ni Mngindo kutoka Lindi.<br />
Baada ya kuhitimu elimu ya msingi niliajiriwa<br />
katika mgahawa ambako nilipiga mzigo kwa<br />
miaka minne. Wakati huo nilikuwa nikitunza<br />
kiasi fulani cha mshiko katika mshahara wangu<br />
kila mwezi, hivyo nikawa nimedunduliza hadi<br />
Sh 140,000.<br />
Niliacha kazi na nikaitumia fedha hiyo<br />
kufungua mgahawa wangu na kwa kuwa kwa<br />
mapishi niko juu, pale mgahawani nilikuwa<br />
nikipiga mzigo mwenyewe, ingawa kwa sasa<br />
nasaidiana na mke wangu kwani tuna miradi<br />
mingine kibao.<br />
Niliendesha ‘kijiwe’ hicho huku nikiweka<br />
kiasi fulani cha faida benki, niliamua kujenga<br />
nyumba na kununua samani lakini nikawa na<br />
ndoto ya kupanua biashara.<br />
Wakaja watu wa FINCA ambao walikuwa<br />
wanatoa mikopo kwa wanawake, hivyo mke<br />
wangu alichangamkia mkopo ili afanye biashara<br />
ndogondogo. Kwa kuwa hatukuwa tumejipanga<br />
fresh tulishindwa kurejesha. Ilifika wakati<br />
wakaja kutunyang’anya vitu vyote ndani, hivyo<br />
ikabidi nitumie akiba ya benki kuokoa jahazi.<br />
4 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />
Ila sikukata tamaa, nilijiunga na Kasi Mpya<br />
SACCOS ili niendelee kufukuzia ndoto<br />
zangu. Nikalipa kiingilio kutokana na faida<br />
niliyokuwa nimeipata tena mgahawani<br />
baada ya sakata la FINCA, nikawa nanunua<br />
hisa kila mwezi hadi ikatimia Sh 70,000.<br />
Nikawa na uwezo wa kukopa sh 300,000<br />
ambazo nilizitumia kununulia mbao na<br />
kuziuza. Nikawa narejesha Sh 50,000 kila<br />
mwezi hadi nilipomaliza deni. Nilikuwa na<br />
mpango wa kukopa tena lakini ikatokea<br />
songombingo, SACCOS ikafa na viongozi<br />
wakasepa na mkwanja wote! Imebaki stori!<br />
Baadaye walikuja watu wa VICOBA,<br />
wakatuhamasisha nami nikachangamkia<br />
fursa kama kawa. Tuliunda kundi la watu
30, tukachanga pesa ikafikia Sh<br />
105,000 na kila mmoja akanunua<br />
hisa kwa kadri awezavyo kwani<br />
aliyenunua hisa nyingi alikuwa<br />
na uwezo wa kukopa pesa nyingi<br />
pia.<br />
Wanasema ng’ombe wa maskini<br />
hazai na hata akizaa huzaa<br />
dume! Hawa nao baadaye<br />
walisepa na pesa za wanachama<br />
na hadi leo kesi iko mahakamani.<br />
Hapa napo nilikula hasara ya Sh<br />
52,000 hivi. Sikuchoka!<br />
Baadaye ilianzishwa SACCOS<br />
inaitwa Belita nikalipa kiingilio na michango<br />
nikawa mwanachama. Nilianza na mkopo wa<br />
Sh 50,000, nikaendelea kupanda na hivi majuzi<br />
nimekopa milioni nne. Narejesha bila tabu kwa<br />
kuwa nimewekeza fedha hizo katika biashara.<br />
Naishukuru mikopo maana imepanua biashara<br />
zangu, hivi sasa namiliki mkokoteni, baiskeli<br />
kumi, bajaj na nina mpango wa kuanza kujenga<br />
nyumba nyingine ya ukweli!<br />
Mkokoteni na baiskeli nakodisha, bajaj pia<br />
inakodishwa kubeba mazao na wagonjwa<br />
na nimepata tenda ya kusafirisha wanafunzi.<br />
Vyote hivi vinalipa kichizi!<br />
Mingo zote hizo zinaniwezesha kurejesha<br />
mkopo na kusomesha watoto wangu watatu<br />
na pesa ya kubadilisha<br />
mboga hainipigi chenga.<br />
Akaunti yangu ya benki<br />
nayo naendelea kuitunisha<br />
kwa faida inayobaki baada<br />
ya kutoa marejesho na<br />
matumizi.<br />
Nitaendelea kukopa,<br />
kuwekeza na kurejesha<br />
kwani mikopo ndiyo<br />
iliyonifikisha hapa. Cha<br />
muhimu ni malengo,<br />
nidhamu katika matumizi<br />
na marejesho na pia<br />
kujiwekea akiba benki.<br />
Nasema tena, NITAKOPA<br />
MPAKA KIELEWEKE!<br />
machi-aprili 2012 2012 Si Si Mchezo!<br />
5 5
MAMBO MAPYA<br />
Unapofika Kimanzichana<br />
ukiulizia watu maarufu<br />
eneo lile wa kwanza<br />
kutajwa ni msanii 20%!<br />
Nasi tukasema si vibaya<br />
‘tukimpaisha’ kwa staili ya<br />
pekee, tukatinga nyumbani<br />
kwao japo kupata picha na<br />
familia yake! Unamuona<br />
mrembo Jema? (wa kwanza<br />
kulia). Huyo ni mtoto wa<br />
20% na aliyeshika majarida<br />
ni mama mzazi wa msanii<br />
20%.<br />
Madogo hawa wanapiga bonge la ‘kolabo’ kulishambulia jukwaa!<br />
Ilikuwa ni katika sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar huko Mkuranga<br />
ambapo mtoto Ramadhani Kasimu (aliyeshika ‘mic’) alikonga<br />
nyoyo za umati na wimbo “Naenda kusema kwa mama” wa msanii<br />
Asley. Huyo dogo mwingine pichani ni Jaffery A. Jaffery, alikwenda<br />
kutunza akanogewa akabaki uwanjani kumpiga tafu mwenzake!<br />
Naye alitunzwa ‘mshiko’ wa uhakika!<br />
6 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />
Kibubu bwana!<br />
Hahaha!<br />
Hiki kinaitwa kibubu. Inawezekana<br />
kili’batizwa’ jina hilo kwakuwa ‘hakisemi’,<br />
yaani hakionyeshi kilichomo<br />
ndani yake! Kibubu ni benki kiaina!<br />
Kinunue au kichongeshe uwe nacho<br />
nyumbani, ‘tupia’ humo fedha ndogondogo<br />
kila siku, jiti, bati, jero, buku<br />
na hata msimbazi kadri unavyozisaka.<br />
Baada ya mwaka au muda fulani uliojipangia,<br />
kivunje na utaona maajabu!<br />
Watu wamenunua mashamba kwa<br />
vibubu!
VICOBA, SACCOS<br />
wana mengi ya ziada<br />
Uzuri wa vikundi vya kuweka na kukopa<br />
ni zaidi ya ule tunaoweza kuufikiria kwa<br />
haraka. Kitendo cha kuwa pamoja kinawapa<br />
nafasi ya kufanya mambo mengi mengine<br />
yenye faida kwao binafsi na hata kwa jamii<br />
zinazowazunguka. Tumevitembelea sana<br />
vikundi hivi na tumejionea kwamba baadhi<br />
yao wanapokutana kwa shughuli zao<br />
za msingi, wanatumia mkusanyiko huo pia<br />
kupata elimu ya afya. Mashirika mbalimbali<br />
pia hutoa elimu ya mambo tofauti kwa<br />
vikundi hivi kwani si rahisi kuitoa kwa mtu<br />
mmojammoja. Hakuna anayeweza kubisha<br />
kwamba kuwa pamoja kuna faida lukuki.<br />
Cheza kwa stepu na kutumia nguvu kama<br />
Makhirikhiri ndio staili yake. Si mchezo! Jamaa<br />
naye ‘aliwabamba vya kutosha’ wananchi wa<br />
Mwalusembe kwa staili za kuvutia.<br />
machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />
7
8 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />
MAMBO YA FEDHA<br />
Vijue Vicoba<br />
Inawezekana wewe na jirani zako mnatamani kuanzisha chama cha kuweka na kukopa lakini hamjui<br />
hata pa kuanzia! Aliadina Peter Rwezaula, Afisa Maendeleo Mwandamizi wa Wilaya ya Mkuranga<br />
anatupiga ‘darasa’ kidogo kuhusu hili:<br />
“Vyama vya kuweka na kukopa viko vya aina nyingi ila maarufu zaidi ni Vicoba na Saccos. Taratibu zake<br />
hazitofautiani sana lakini kwa leo tutajikita katika Vicoba tu. Twende pamoja!<br />
VICOBA ni nini?<br />
Ni kifupi cha maneno ya kimombo, Village<br />
Community Bank, au kwa ‘kibantu’ chetu<br />
tunaweza kusema ‘Benki’ ya Wanakijiji.<br />
Jinsi ya kuanzisha Vicoba<br />
t Mnatakiwa kuwa kikundi cha watu kuanzia<br />
15 hadi 30.<br />
t Siku ya kwanza ya kukutana mnaweza kumualika<br />
Afisa Ushirika au Afisa Maendeleo<br />
ya Jamii ili kupata maelekezo zaidi.<br />
t Mtengeneze katiba (ni vizuri mpate<br />
msaada wa mtaalamu)<br />
t Wakati wa kutengeneza katiba mtakubaliana<br />
kuhusu kiingilio (ambacho hutolewa<br />
mara moja na hakirudishwi), thamani ya<br />
hisa, jinsi ya kununua n.k.<br />
t Chagueni viongozi wa muda (mtabadilisha<br />
viongozi kufuatana na katiba yenu)<br />
J<br />
Vinaendeshwaje?<br />
n Wanachama wanatakiwa wawe wananunua<br />
hisa lakini lazima kuwe na<br />
ukomo wa hisa anazoweza kumiliki<br />
mtu mmoja.<br />
n Kikundi kikutane angalau mara moja<br />
kwa wiki.<br />
n Ndani ya kikundi cha Vicoba inabidi<br />
muwe na vikundi vya watu watano<br />
watano ili kuwekeana udhamini wakati<br />
wa kukopa<br />
n Ni muhimu kuwa na mfuko wa jamii ili<br />
kusaidiana wakati wa matatizo kama<br />
misiba na mikopo ya dharura isiyo na<br />
riba<br />
n Kikundi cha Vikoba kiwe na sanduku<br />
la kuhifadhia fedha na washika funguo<br />
watatu kwa kufuli tatu.<br />
n Kila kikao wanachama wapewe taarifa<br />
ya akiba, mapato na matumizi.<br />
n Kikundi kikikua itabidi kiwe na akaunti<br />
benki ili kutunza fedha<br />
Kumbuka<br />
Ni kinyume cha sheria kwa<br />
mwanachama mmoja kumiliki<br />
zaidi ya moja ya tano ya hisa za<br />
chama na hairuhusiwi mtu kuwa<br />
mwanachama wa Vicoba mbili.
NGUVU ZA MWANAUME<br />
Jogoo halipandi mtungi?<br />
Ili watoto wasielewe wakubwa hupenda kusema ‘jogoo<br />
halipandi mtungi’! Hili ni tatizo la uume kutokusimama au<br />
Kiswahili sanifu, uhanithi. Watu wenye tatizo hili huchekwa<br />
na hivyo kufanya washindwe kutafuta ushauri wa kitaalamu.<br />
Kufanya hivyo ni kuwanyima haki yao ya msingi ya afya<br />
ya uzazi.<br />
Tuliteta na Dk Constantine Kibela na Dk Lugano Kiswaga wa<br />
Hospitali ya Wilaya ya Mkuranga kuhusu hili kwani tumekuwa<br />
tukipokea maswali lukuki ya wasomaji.<br />
Kulikoni jogoo kushindwa?<br />
“Hili ni tatizo ambalo mtu anaweza kuzaliwa nalo au<br />
kulipata katika kipindi chochote cha maisha yake.<br />
Linaweza kuwa la kudumu au la muda tu,” anasema<br />
Dk Constantine. Kumekuwa na uzushi kwamba kitovu<br />
cha mtoto kikiangukia kwenye uume mtoto atakuwa<br />
hanithi, jambo ambalo si kweli.<br />
Sababu za uhanithi:<br />
n Karibu 60% ya watu wenye tatizo hili hutokana na<br />
sababu za kisaikolojia, umri, matatizo ya kimazingira<br />
mfano: msongo wa mawazo kutokana na kukosa<br />
kazi, fedha, matatizo ya kifamilia, hofu ya kuambukizwa<br />
magonjwa, hofu ya kutumia kondom nk<br />
n Magonjwa sugu katika mwili, kwa mfano, ugonjwa<br />
wa ini, figo, kisukari, kifua kikuu nk<br />
n Matumizi yaliyokithiri ya dawa za kulevya au<br />
pombe<br />
n Vyakula tunavyokula vinaweza kusababisha uhanithi,<br />
kwani mrundikano wa mafuta katika mishipa<br />
ya damu unasababisha damu kushindwa kufika<br />
vizuri katika uume ili kuuwezesha kusimama.<br />
Tatizo hili halipaswi kuwa la mwanamume<br />
tu bali mwanamke anao<br />
uwezo wa kumsaidia mwenzi<br />
wake katika kutafuta ushauri na<br />
hata kumsaidia kuondoa hofu<br />
aliyonayo.<br />
Je, tatizo hili<br />
linatibika?<br />
Kitu muhimu ni kutambua<br />
chanzo cha tatizo lenyewe<br />
na kujitokeza kupata ushauri.<br />
Wanaume wengi wanashindwa<br />
kutafuta ushauri juu ya suala<br />
kama hili kwa kuona haya eti<br />
“mwanaume mzima ijulikane<br />
mi hanithi!” Wengine hufikia<br />
hatua ya kuigiza kama wana<br />
uhusiano wa kujamiiana<br />
ilimradi tu waonekane rijali.<br />
Kwa hisani ya TMEP,<br />
Mradi unaodhaminiwa na RFSU<br />
machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />
9
HADITHI YA PICHA<br />
10<br />
‘MKOPO WA NGOMA!’<br />
Mama Mwajei amejaliwa mtoto mmoja<br />
tu, hivyo anamlea kama mboni<br />
ya jicho! Siku ya siku imewadia,<br />
Mwajei kavunja ungo. Ndiyo! Kawa mkubwa<br />
sasa. Kawekwa ndani mwezi, sasa ni wakati wa<br />
kumtoa, wenyewe wanasema ‘kumkogesha maji’.<br />
Amepania kumfanyia bonge la sherehe, tatizo<br />
mshiko. Anafanyaje? Nini kinatokea? Fuatilia….<br />
Imeigizwa na Kimanzichana Vijana Troupe”<br />
Duh! Namie mwezi<br />
ujao nakamata kitita<br />
Sema usemavyo<br />
lakini hapa ngoma<br />
itachezeka na<br />
pombe zitanyweka<br />
mpaka kieleweke<br />
Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />
Hongera sana.<br />
Laki tano hiyo,<br />
hesabu<br />
Asante sana<br />
Naona hukataziki,<br />
sasa mie simo na<br />
utakuja kujuta<br />
Mama Mwajei ndo<br />
keshaamua, kila mtu<br />
anamshangaa<br />
Ama kweli<br />
tamaa mbele<br />
mauti nyuma!<br />
Si pale Kibisa Saccos mume<br />
wangu? Mikopo nje nje…<br />
Una akili sana<br />
waifu, kachukue<br />
tufanye biashara<br />
Mungu anipe<br />
nini mimi!<br />
Shughuli ya<br />
Mwajuma<br />
itaacha<br />
historia<br />
Alhamis mwamu, Ijumaa mbiga,<br />
Jmosi mkole, usiku wake rusharoho,<br />
Jpili mwali anatoka. Upo?<br />
Haya jirani, asante kwa<br />
mwaliko, tuko pamoja
Shost, mie nikipata tu<br />
mkopo namtoa mwanangu.<br />
Mzee nshamweka sawa<br />
Niliyopewa haitoshi kwa<br />
biashara. Mie naona<br />
tuitumie kumtoa mwajuma<br />
Chonde chonde!<br />
Itakutokea puani<br />
hiyo! Tena mie<br />
simo kabisaaa!<br />
He! Mumeo kakubali?<br />
Yaani mkopo<br />
umcheze mtoto?<br />
Maspika fanya manne<br />
kama hili. Sitaki<br />
muziki wa kitoto<br />
Usitie shaka,<br />
hapa umefika<br />
Hajakubali shost,<br />
nimemwongopea<br />
wa biashara<br />
Mmh! Hii akili au matope? Umcheze<br />
mtoto kwa mkopo? Utaulipaje?<br />
Ulisema ya biashara,<br />
leo unaniambia ya<br />
ngoma! Sitaki kusikia<br />
Mimi ndo<br />
niliyesaini<br />
na mimi ndo<br />
nitadaiwa<br />
na ndo<br />
nshaamua<br />
Ndo ushakuwa mkubwa, nakupatia<br />
ushanga mweupe na mwekundu,<br />
nitakueleza kazi zake…<br />
machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />
11
12<br />
Mungu mkubwa!<br />
Japo nina kazi<br />
ya kufagia lakini<br />
nimeacha historia<br />
Jamani, si<br />
mnisikilize<br />
kwanza?<br />
Huu mweupe unavaa<br />
ukiwa vizuri, yaani<br />
kama hauko hedhi…<br />
Hatujaja kwa<br />
mazungumzo. Lete<br />
chetu, vinginevyo<br />
tunazama ndani<br />
Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />
Leleleleleleeleleeeeeeeee<br />
Yeleleleleleleleee<br />
TAREHE YA MAREJESHO INANUKIA…<br />
Yaani Mwinyi, wewe wa<br />
kukataa kunikopesha<br />
elfu hamsini jamani!<br />
Aaaah, mkuki kwa<br />
nguruwe eenh? Wewe<br />
mbona nikikuomba<br />
‘vitu’ unabana?<br />
Jamaniii, mume wangu<br />
nitamwambia nini mie<br />
Ona sasa, ndo<br />
tushaaibika<br />
Halohalooooooooooo<br />
Maji ndo yamefika<br />
shingoni, anasaga vumbi<br />
kusaka marejesho<br />
Tupishe hukoooo<br />
Hivi angekufuata<br />
wewe msomaji<br />
katika hatua hii<br />
ungemshauri nini?
Anafurahi<br />
lakini mwisho<br />
wake utakuwa<br />
ni majonzi<br />
Mama Mwajei<br />
katimiza ndoto<br />
yake. Tuendelee!<br />
MAMBO YANAZIDI KUWA MAGUMU…<br />
Nipe thelathini<br />
kwa vyote<br />
Mmmh! Anauza bei<br />
ya kutupa! Sijui ana<br />
shida gani!<br />
Hii aibu tupu!<br />
Mwarabu<br />
mie leo<br />
nimeaibika<br />
mtaani!<br />
Nitafanya nini<br />
mie! Najuta<br />
kutokumsikiliza<br />
mume wangu!<br />
Nema<br />
Mwajuma<br />
nemaaaaaa<br />
Kapendezaaaaaa<br />
Fyokofyoko,<br />
unalia nini sasa,<br />
si nilikwambia!<br />
Jamani mwali<br />
wetu kapendeza<br />
hajapendezaaaaaa?<br />
SIKU YA SIKU IMEWADIA…<br />
Ana vitu<br />
chungu mzima,<br />
tukavibebe tu<br />
tuvinadi<br />
Ndiyo, haiwezekani<br />
mkopo achukue<br />
yeye, tulipe sie<br />
Nisamehe mume<br />
wangu, niko chini<br />
ya miguu yako…<br />
Hivi saa hizi ni usiku<br />
au mchana…?<br />
Mi mgeni mji<br />
huu, sijui<br />
Duh! Muziki wa ukweli,<br />
hajaleta nyenze.<br />
Twendeni jamani,<br />
hakuna kumlegezea<br />
Kama hukujifunza<br />
kwa kisa cha Mama<br />
Mwajei hujifunzi tena!<br />
Ni makosa kutumia<br />
mkopo kwa jambo<br />
ambalo halizalishi.<br />
machi-aprili 2012 Si Mchezo! 13
JE, WAJUA?<br />
Kabla ya kukopa jipange!<br />
Wa kucheka mmecheka, wa kusonya mmesonya,<br />
wa kugomba mmegomba, wa kubishana mmebishana<br />
lakini ukweli unabaki palepale kwamba hapa<br />
Mama Mwajei alichemka!<br />
Hebu tusemezane kidogo: hivi, inakuwaje unakubali furaha<br />
ya siku mbili-tatu ikusababishie majuto kwa miaka? Wapo<br />
waliochukua mkopo, wakafurahia jinsi mifuko ilivyoota ‘vijipu’<br />
ghafla, breki ya kwanza ikawa kilabuni ‘kujenga heshima’!<br />
Wapo pia waliochukua mkopo kwa ajili ya kujipatia ‘jiko’ jipya!<br />
Hawa nao tuwape pole!<br />
Katika sakata la Mama Mwajei tunaweza kuwalaumu na kuwachukia<br />
wanakikundi wenzake kwa kitendo cha kwenda<br />
‘kusafisha’ nyumba ya mwenzao, lakini ilikuwa ni haki kwao<br />
kufanya hivyo kwani vinginevyo lingegeuka kuwa ‘zengwe’ lao<br />
na wangepaswa kulipa fedha hiyo kwani wao ndio waliokuwa<br />
wadhamini wake.<br />
Nema<br />
Mwajuma<br />
nemaaaaaa<br />
Kapendezaaaaaa<br />
14 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />
Jamani mwali<br />
wetu kapendeza<br />
hajapendezaaaaaa?<br />
Ukweli ni huu<br />
Jamani, si<br />
mnisikilize<br />
kwanza?<br />
Mikopo si kitu kibaya na wala<br />
hatuna sababu ya kuiogopa kwani<br />
wapo wenzetu waliochukua<br />
mikopo wakawekeza katika<br />
biashara, wakajikwamua kiuchumi<br />
kama tulivyoona katika stori<br />
ya Juma Kaputi kwenye kurasa<br />
za Stori Yangu. Cha muhimu ni<br />
kujipanga na kuwa na malengo<br />
yenye tija.
Hatujaja kwa<br />
mazungumzo. Lete<br />
chetu, vinginevyo<br />
tunazama ndani<br />
Tufanyeje?<br />
Ufahamu<br />
n Fanya utafiti na uwe na ufahamu mzuri wa mradi<br />
unaotaka kuufanya kabla ya kuchukua mkopo<br />
n Ni muhimu kufungua akaunti benki ili uziweke fedha<br />
mara tu baada ya kuzipata kwa usalama wa fedha hizo<br />
na pia kuepuka kuwa nazo mfukoni au nyumbani ili<br />
usishawishike kuzitumia kwa mambo ambayo siyo<br />
uliyoyakusudia<br />
n Usimwamini kila mtu kwa ushauri kuhusu matumizi ya<br />
fedha kwani baadhi ya marafiki wanaweza kukushauri<br />
vibaya kwa kuwa ama wanafaidika na ‘matanuzi’<br />
utakayoyafanya au wangependa kukuona ukiumbuka.<br />
Mkopo, kama lilivyo jina lake, ni<br />
fedha ambayo utatakiwa kuirejesha.<br />
Katika vyama vya ushirika, kama<br />
SACCOS, VICOBA na hata katika taasisi<br />
nyingine za fedha, mkopo wowote<br />
utakaouchukua unapaswa kuurejesha<br />
ukiwa na kiasi fulani cha riba, hata kama<br />
utaurejesha baada ya wiki moja tu.<br />
Ili uweze kurejesha mkopo huo pamoja<br />
na riba ni lazima fedha hiyo iwekezwe<br />
katika mradi ambao utairuhusu ‘kutuna’<br />
ili hata utakapokuwa umeirejesha, kiasi<br />
fulani cha faida kibaki kwako kuendeleza<br />
huo mradi uliouanzisha.<br />
Unaporejesha fedha ya mkopo unatoa<br />
fursa kwa wenzako pia kuweza<br />
kukopeshwa na hatimaye watu wengi<br />
zaidi watajikwamua kutoka katika<br />
umaskini.<br />
Kumbuka<br />
J Usichukue mkopo bila<br />
mipango mizuri ya kuwekeza<br />
fedha hiyo<br />
SWALI:<br />
Nini kinasababisha<br />
baadhi ya watu kujikuta<br />
‘wakitumbua’ fedha ya<br />
mkopo?<br />
machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />
15
TULICHOVUNA<br />
Tunajali VICOBA imetulia<br />
n Wakati wakisubiri wenzao kwa kikao, nasi<br />
‘tukawatwanga’ Si Mchezo! wapate ujumbe’<br />
“likuwa ni Jumatatu tuliiivu majira ya mchana.<br />
Kama tulivyokuwa tumekubaliana, mtu<br />
mmoja baada ya mwingine aliwasili katika kivuli<br />
cha mwembe na hatimaye tukajikuta tumetimia<br />
20. Penye wengi hapaharibiki neno, mmoja<br />
wetu alijitolea kuwa kiongozi wa muda, akatuongoza<br />
katika kuanzisha kikundi chetu”.<br />
Hivi ndivyo ilivyoazishwa Tunajali VICOBA, kikundi<br />
cha kuweka na kukopa cha wanakijiji wa Mwanambaya,<br />
Mkuranga. Kikundi hiki kilianzishwa Juni 28,<br />
2003 na hadi sasa kina wanachama 31, kama anavyosimulia<br />
Katibu wa kikundi hicho, Moshi Mfaume<br />
Manda.<br />
Enhe, mkutano uliendaje?<br />
Huo ulikuwa ni mkutano wetu wa kwanza.<br />
Alikuwepo Afisa Maendeleo wa Kata kushuhudia<br />
kinachoendelea. Tulijiundia katiba,<br />
kisha tukafanya uchaguzi wa viongozi. Tunao<br />
viongozi wanane, Mwenyekiti, Katibu,<br />
Mtunza Hazina, wahesabu fedha wawili na<br />
watunza funguo watatu.<br />
16 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />
n Kama kawa, wana sukari, sabuni ya maji<br />
(kwenye kidumu), midamida ikifika watauziana<br />
Mnapokutana mnafanya nini?<br />
Kila Alhamisi saa nane mchana tunakutana:<br />
l Mwenyekiti anafungua mkutano<br />
l Wanaodaiwa sabuni na sukari wanalipa<br />
madeni (ni mradi wa kikundi)<br />
l Tunachangia Mfuko wa Jamii (kila mwanachama<br />
anachangia sh 1,000 kwa mwezi)<br />
l Tunanunua hisa, yaani akiba (fedha) mtu<br />
anayoamua kuweka (bei ya hisa ni sh 500<br />
na mtu anaweza kununua hadi hisa 5 kwa<br />
wakati mmoja)<br />
l Waliokopeshwa fedha wanarejesha<br />
l Tunasoma barua za maombi ya mikopo<br />
(kama zipo)<br />
l Tunawakopesha wale ambao maombi yao<br />
yamepitishwa na kikundi<br />
l Tunauziana sukari na sabuni (kwa<br />
mkopo)<br />
l Katibu anasoma taarifa ya mapato na<br />
matumizi<br />
l Mwenyekiti anafunga kikao
n Mida ya hisa ilipofika, kila<br />
mwanachama alinunua kadri ya<br />
uwezo wake<br />
Wanachama<br />
wanakopaje?<br />
z Anajaza fomu (tunazo)<br />
z Inasainiwa na wadhamini<br />
wawili ambao lazima wawe ni<br />
wanachama wa kikundi<br />
z Maombi yatasomwa mbele ya<br />
wanakikundi wote tunapokutana<br />
na yatajadiliwa<br />
z Ikipitishwa anakopeshwa, na<br />
kiwango cha juu ni mara tatu<br />
ya hisa alizonazo.<br />
z Anatakiwa kuanza kurejesha<br />
baada ya mwezi mmoja na<br />
katika miezi mitatu lazima awe<br />
amemaliza<br />
z Tunatoza riba ya asilimia 10 ya<br />
mkopo<br />
z Anayeshindwa kulipa tunachukua<br />
hisa zake zote pamoja<br />
na za wadhamini wake<br />
n Wanauziana sukari ili kutunisha mfuko.<br />
Ni kwa mkopo na wiki ijayo kila mmoja<br />
atapaswa kulipa!<br />
Mna vyanzo vingine vya mapato?<br />
n Tuna shamba la kikundi ambapo tunalima mihogo,<br />
matunda na mboga<br />
n Tuna mfuko wa jamii ambao tunachangia wenyewe<br />
kwa ajili ya kusaidia wenye matatizo na kugharamia<br />
shughuli za kikundi<br />
n Tunanunua sukari kwa jumla na kuuziana kwa rejareja<br />
n Tumepata mafunzo ya kutengeneza sabuni, hivyo<br />
tunatengeneza na kuuziana<br />
n Wachelewaji katika vikao tunawatoza faini ya sh 500,<br />
ili kutunisha mfuko<br />
Ujumbe?<br />
n Kikao kimefungwa, Mwenyekiti, Dora<br />
Danda na Katibu wake Moshi M. Manda<br />
wanaweka kumbukumbu sawa.<br />
Ndiyo. Vikundi vya kuweka na kukopa ni vizuri. Tumeshuhudia<br />
wanachama wenzetu wakianzisha biashara na hata kujenga<br />
nyumba za kisasa kwa kuweka na kukopa. Nanyi pia mnaweza<br />
kuanzisha!<br />
machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />
17
CHEZASALAMA<br />
Huyu ndiye mwanamume wa ukweli<br />
Edna anakonda kwa mawazo! Ana mtoto wa<br />
mchanga na angependa kusubiri japo kwa<br />
miaka mitatu kabla ya kuzaa mtoto mwingine.<br />
Hajui la kufanya. Amesikia stori nyingi za<br />
kutisha kutoka kwa ‘mashosti’ wake kuhusu njia<br />
za kisasa za uzazi wa mpango, hivyo anaogopa<br />
kuzitumia!<br />
Frank, mumewe Edna, yeye ana mtazamo tofauti.<br />
Amewahi kusoma kijitabu kinachoelezea vizuri<br />
njia za uzazi wa mpango na anafahamu kwamba<br />
stori alizozisikia mkewe hazina ukweli wowote.<br />
18 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />
“Twende kliniki mpenzi wangu. Tutapata maelezo<br />
yote na hofu yako itaondoka. Tutachagua njia inayotufaa<br />
na tutafurahia mapenzi yetu bila hofu,”<br />
Frank anamshawishi Edna na taratiibu wanambeba<br />
mtoto wao Alice na kuongozana kuelekea<br />
kliniki.<br />
Frank ni mwanamume wa kipekee mno! Anajali,<br />
anamhurumia mkewe na anaona umuhimu wa<br />
kutumia njia za uzazi wa mpango kwa faida yake<br />
mwenyewe, mkewe na hata watoto. Si mbabe, ni<br />
msikivu. Huyu ndiye mwanamume wa ukweli!
Faida za kutumia njia<br />
za uzazi wa mpango<br />
Kupanga uzazi kuna faida<br />
nyingi kwa mama, baba, watoto<br />
na familia kwa ujumla<br />
Kwa mama:<br />
n Itamsaidia kurejesha afya<br />
baada ya kujifungua<br />
n Inampa nafasi ya kutosha<br />
ya kuonyesha mapenzi kwa<br />
watoto na kwa mumewe<br />
n Inampa mama nafasi ya<br />
kuhudumia familia na<br />
kufanya shughuli za maendeleo<br />
Kwa watoto:<br />
t Mama mwenye<br />
afya huzaa watoto<br />
wenye afya<br />
t Watapata mapenzi<br />
na huduma<br />
ya wazazi kwa<br />
ukamilifu<br />
Kwa baba:<br />
n Anapunguza mzigo wa jukumu<br />
la kuihudumia familia<br />
n Inamsaidia kumudu mahitaji<br />
ya familia (elimu, chakula,<br />
malazi na mengineyo)<br />
n Inampa nafasi ya kutosha<br />
ya kuonyesha mapenzi kwa<br />
watoto na kwa mkewe<br />
n Anapata muda wa kuhudumia<br />
familia na kufanya<br />
shughuli za maendeleo<br />
Chukua hatua!<br />
n Panga pamoja na mpenzi wako,<br />
amueni lini mnataka kuzaa, watoto<br />
wangapi na wapishane kwa umri<br />
gani<br />
n Kwa ushauri wa mtaalam, kubalianeni<br />
njia ya uzazi wa mpango<br />
ambayo inawafaa.<br />
Ni haki na wajibu wa mwanamume<br />
kushiriki katika<br />
kupanga uzazi. Familia bora<br />
hujengwa na mwanamume<br />
na mwanamke pamoja<br />
machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />
19
BURUDANI<br />
Wimbo: Vinapanda bei<br />
Msanii: Blad Key<br />
Naamka asubuhi ee,<br />
jikoni kwangu kumelala<br />
paka<br />
Namfata mke wangu ee,<br />
amenuna eti anadai talaka<br />
Hataki tuongee,<br />
amenuna eti anataka<br />
kuondoka<br />
Anarudi kiijini,<br />
maisha ya dhiki yeye<br />
amechoka x2<br />
Mie nitafanya nini, na<br />
mfukoni sina hata senti<br />
Kipato changu cha chini,<br />
madukani vitu vinapanda<br />
bei x2<br />
We mama weee!!<br />
Kiitikio<br />
Vinapanda bei,<br />
Kila siku vitu vinapanda<br />
bei,we mama wee.<br />
Vinapanda bei,<br />
Kila siku vitu vinapanda bei<br />
anyokiee.<br />
20 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />
20 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />
Huu neneee<br />
Nimechelewa kazini, kwa<br />
sababu nauli iko juu<br />
Kutokana na hali duni,<br />
ikabidi nako niende kwa<br />
miguu<br />
Ile nafika kazini, bosi nae<br />
anakuja juu<br />
Anaanza nifokea, hali<br />
iliyofanya nibaki roho juu<br />
Mie nitafanya nini kipato<br />
changu hakikidhi mahitaji<br />
Hali ya maisha ni ngumu<br />
kila siku vitu vinapanda bei<br />
x2<br />
We mama weee!!<br />
Kiitikio<br />
Kibwagizo<br />
We we we we wee<br />
We mama we we we, we<br />
mama. x3
Baunsa noma!<br />
Mshikaji alienda kuiba kwa baunsa. Wakati J<br />
anatoka tu, ghafla akakutana nae. Baunsa<br />
akachukua vile vitu na kuvirudisha ndani<br />
halafu akamshika mkono kama ‘mwana’ vile<br />
na wakaanza kutembea. Mshikaji akajua labda<br />
anapelekwa polisi. Kufika kituo cha polisi<br />
cha kwanza wakapita, cha pili wakapita tena<br />
mmh! Mshikaji akaingiwa na hofu kufika kituo<br />
cha tatu baunsa akawa anapita tena, mshikaji<br />
akamuona afande nje akapiga kelele ‘‘afandee<br />
mimi mwiziii’’<br />
Toto nidhamu sifuri<br />
Mtoto: Baba niletee glasi ya maji!<br />
Baba:: We mtoto una kichaa nini? kachukue<br />
mwenyewe!<br />
Mtoto: Bwana niletee!<br />
Baba: Usinisumbue, ntakuja kukupiga makofi!<br />
Mtoto: Basi ukija kunipiga makofi njoo na glasi<br />
ya maji<br />
J<br />
Hajatulia!<br />
Siku moja, mama<br />
mwenye nyumba alikuwa<br />
akimuuliza msichana wake<br />
wa kazi kuhusu kuisha<br />
haraka kwa vijiti vya<br />
kuchokonoa meno.<br />
Mama:<br />
Hizi “toothpicks” mbona<br />
zimeisha haraka?<br />
Dada wa kazi:<br />
Mimi mwenyewe sijui<br />
labda uwaulize watoto<br />
wako, mimi huwa<br />
nikimaliza kutumia tu,<br />
nazirudisha kwenye kopo<br />
lake!<br />
Mama: Haaaa!!??<br />
J<br />
! ! !!<br />
Yataka moyo kuwa dokta….<br />
Mgonjwa:<br />
Dokta mimi nina tatizo la kusahau, yaani<br />
nikisema neno au ukiniambia hapo hapo<br />
nasahau kabisa.<br />
Dokta: Tatizo lako limekuanza lini?<br />
Mgonjwa: Tatizo gani tena?<br />
Dokta: ???**$!!!<br />
J<br />
machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />
21
Minyoo bwana!<br />
Hahahahaaaa! Watu bwana! Bila shaka umewahi<br />
kusikia mtu akisema eti binadamu lazima<br />
awe na minyoo! Eti minyoo ina kazi ya kulainisha<br />
chakula katika tumbo la binadamu!<br />
Dokta Lugano Kiswaga wa Hospitali ya<br />
Wilaya ya Mkuranga anasema huo ni uongo<br />
mtupu!<br />
“Minyoo iko ya aina nyingi na hakuna aina<br />
yoyote ya minyoo yenye faida katika mwili<br />
wa binadamu, ila huingia katika mwili wa binadamu<br />
au mnyama kwani ndiyo mazingira<br />
yanayoiwezesha kuzaliana,” anasema.<br />
Mh! Inaingiaje?<br />
“Kuna njia nyingi za kuingia ila kubwa ni<br />
kupitia chakula kisichosafishwa vizuri,<br />
nyingine ni kujipenyeza katika matundu<br />
madogomadogo ya ngozi ya mwanadamu,”<br />
anasema.<br />
“Ukila chochote bila kunawa mikono vizuri<br />
kwa sabuni na maji safi, unaweza kuingiza<br />
minyoo tumboni. Usipoosha vizuri matunda<br />
na mboga za majani zinazoliwa zikiwa<br />
mbichi, mfano kabichi, karoti, nyanya nk,<br />
unaweza kula minyoo”, anasema.<br />
“Minyoo inapopenya katika matundu ya<br />
ngozi, inakwenda katika mishipa ya damu,<br />
kisha kwenye moyo, halafu kwenye mapafu<br />
na hatimaye unaikohoa inaingia katika<br />
utumbo. Inapofika humo huweka makazi,<br />
ikakua, ikataga mayai, kisha ukayatoa mayai<br />
hayo kupitia haja kubwa, yanaanguliwa<br />
nje ya tumbo la binadamu na mzunguko<br />
hujirudia kama kawaida”, anasema.<br />
22 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />
PASIPO NA DAKTARI<br />
Utajuaje kama una minyoo?<br />
n Unaweza kuiona katika kinyesi<br />
n Kukohoa<br />
n Inatoboa utumbo, hivyo unaweza kuona<br />
damu kidogo katika kinyesi<br />
n Kuwashwa sana usiku sehemu ya haja kubwa<br />
(hasa kwa watoto)<br />
n Kukonda<br />
n Kukosa hamu ya kula<br />
n Upungufu wa damu<br />
n Ngozi kupauka<br />
n Ukuaji hafifu (kudumaa – hasa kwa watoto)<br />
Chonde chonde!<br />
Ukiona dalili hizi au hata baadhi yake, kamwone<br />
mtaalam wa afya kwa vipimo na ushauri kwani<br />
linaweza kuwa ni tatizo la minyoo, ambalo<br />
linaweza kuleta athari kubwa kwa binadamu,<br />
ikiwamo upungufu mkubwa<br />
wa damu na hata<br />
kifo! Usimeze dawa za<br />
minyoo bila ushauri wa<br />
daktari. J<br />
Kumbuka<br />
Zingatia usafi<br />
kujiepusha na<br />
magonjwa
HUDUMA<br />
Walianza kama utani!<br />
Siku moja wanawake 30 walikaa kikao ‘wakateta’<br />
jambo. Walichoka kuona jinsi janga la Ukimwi lilivyokuwa<br />
likienea kwa kasi katika jamii. Waliunda<br />
kikundi chao ‘wakakibatiza’ jina la JIMOWACO, yaani<br />
Jipeni Moyo Women and Community Organisation,<br />
kikundi ambacho leo hii ni gumzo kubwa Kisarawe na<br />
Mkuranga.<br />
Hawa, ni wanawake ambao waume zao walikuwa wakifanya<br />
kazi katika mgodi wa chokaa huko Kisarawe na hiyo<br />
ilikuwa ni mwaka 2003. Walichangishana pesa, wapo walioomba<br />
kwa waume zao, wapo waliovunja ‘vibubu’ vyao,<br />
ili mradi wazo lao lifanikiwe!<br />
Wako mbali!<br />
Leo hii JIMOWACO imesimama!<br />
Imeajiri wafanyakazi<br />
12 na tayari imefungua<br />
tawi wilayani Mkuranga,<br />
imeanzisha vikundi 20 vya<br />
kuweka na kukopa katika<br />
jamii, vikiwa na mchanganyiko<br />
wa watu waishio na<br />
VVU na wasio navyo. Wanatoa<br />
mahitaji ya shule na<br />
huduma za afya kwa watoto<br />
wapatao 7,093 na wanatoa<br />
huduma kwa watu<br />
waishio na VVU/Ukimwi<br />
wapatao 1,913 (Mkuranga)<br />
na 1,200 (Kisarawe)!<br />
Ama kweli hata mbuyu<br />
ulianza kama mchicha!<br />
Mambo sio mteremko!<br />
Wana malengo!<br />
“Tulipoanza tulikusudia kusadia<br />
yatima na wanaoishi katika<br />
mazingira hatarishi, wajane,<br />
na waishio na VVU/Ukimwi”,<br />
anasema Flaviana Mlaki, Mratibu<br />
wa Watoto-JIMOWACO.<br />
Mwananchi akifurahia msaada wa sare za<br />
shule kutoka JIMOWACO<br />
Pamoja na mafanikio makubwa waliyoyapata, Flaviana<br />
anasema vikwazo pia vipo:<br />
n Hawana uwezo wa kuwafikia watoto wote wanaohitaji<br />
huduma yao kwani ni wengi sana katika jamii.<br />
n Unyanyapaa nao bado upo na ni kikwazo kwa watu kujitokeza<br />
kwenda kupima VVU.<br />
n Licha ya elimu inayotolewa, maambukizi mapya bado<br />
yanajitokeza kwa kasi kwani waliokuwa wagonjwa baada<br />
ya kupata ahueni wanaendelea kuambukiza wengine.<br />
n Baadhi ya watu wanapougua kutokana na Ukimwi wanaamini<br />
wamerogwa, hivyo wanakwenda kwa waganga<br />
wa kienyeji.<br />
Wana ujumbe kwetu!<br />
JIMOWACO wanaamini kwamba<br />
hata wewe msomaji pamoja na watu<br />
waliokuzunguka mnaweza kuanzisha<br />
mkakati kama huu katika eneo lenu.<br />
Siri ya mafanikio ni subira, kujiamini<br />
na kupeana moyo!<br />
machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />
23
KATUNI<br />
upatu au hupati?<br />
Wanawake Mtaa wa Sita<br />
ni wachakarikaji haswa!<br />
Asiyeuza juisi anachoma<br />
maandazi, ili mradi mkono uende<br />
kinywani. Siku moja mwenzao,<br />
Mama Semeni, anapata wazo, ‘analiuza’<br />
kwa mashostito nao wanaingia<br />
‘line’. Songombingo linalotokea<br />
baadaye mmmmh, almanusura mtu<br />
asutwe kwa matarumbeta! Kulikoni?<br />
Sitaki kukumalizia utamu! Fuatilia!<br />
Michoro: babatau cartoons 2012<br />
BAADA YA WIKI MBILI<br />
24 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />
MCHEZO UMEANZA
machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />
25
26 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />
Ama kweli majuto<br />
ni mjukuu!<br />
Kijumbe ndo<br />
keshatoroka na<br />
fedha za mchezo,<br />
ameacha<br />
vumbi tu!<br />
Upatu ni<br />
mzuri. Tatizo<br />
wengi wetu<br />
tunaucheza<br />
kienyeji mno!
UKWELI WA MAMBO<br />
Yanawakuta wengi!<br />
Stori ya Mama Semeni<br />
na wenzake haichekeshi<br />
bali inasikitisha!<br />
Inawezekana hata wewe ama<br />
unacheza upatu au una mpango<br />
wa kucheza. Inawezekana<br />
umeapa kutokucheza tena<br />
upatu kwani yaliwahi kukukuta<br />
yaliyomkuta Mama Havinitishi<br />
na wenzake! Pole!<br />
Sio mchezo mbaya<br />
Upatu au ‘mchezo’ kama<br />
wengi wanavyouita,<br />
si jambo baya. Wengi<br />
‘wametoka’ kwa staili hii.<br />
Utaukuta mitaani, maofisini,<br />
kwa watu ambao ama<br />
wako katika ‘kijiwe’ kimoja<br />
au wanafanya biashara<br />
zinazofanana. Kwa kifupi ni<br />
jambo zuri. Ndiyo, kwani si<br />
kila mmoja ana uwezo wa<br />
kudunduliza vijisenti peke<br />
yake hadi mfuko utune.<br />
Zaidi ya kuwasaidia<br />
watu kuinua mitaji na<br />
kujikwamua kimaisha,<br />
‘mchezo’ huu unawasaidia<br />
watu kuishi kijamaa,<br />
yaani kufahamiana na<br />
kusaidiana katika matatizo<br />
mbalimbali ya kijamii,<br />
wengine wanasema ‘kufa na<br />
kuzikana’.<br />
Tatizo nini?<br />
Tumeshuhudia ngumi zikilika mitaani, watu<br />
wakiporomosheana matusi, wengine wakibubujikwa<br />
machozi baada ya ‘kuingia chaka’, ukiuliza kulikoni<br />
unaambiwa kijumbe ‘kasepa’ na fedha za wanakikundi!<br />
Yote haya yanatokea kwa sababu tunaucheza ‘mchezo’<br />
huu kienyeji mno, kama tunavyoona katika stori ya Mama<br />
Semeni na wenzake.<br />
Walipaswa wakutane, wafanye makubaliano ya kucheza<br />
‘mchezo’, kuwe na orodha ya wanachama iliyoandikwa<br />
na zamu za ‘kupokea’,<br />
wafanye uchaguzi wa<br />
‘kijumbe’ wajipangie<br />
masharti na kuwe<br />
na daftari la kusaini<br />
mwanachama<br />
anapowasilisha mchango<br />
na anapopokea.<br />
J Kumbuka<br />
Ni vizuri muwe ni kikundi<br />
cha watu mnaofahamiana<br />
vizuri kwa makazi, kipato<br />
na tabia, ili kuepusha<br />
mambo kwenda mrama.<br />
machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />
27
SAUTI YANGU<br />
Si Mchezo!<br />
<strong>Femina</strong> <strong>HIP</strong><br />
SLP 2065,<br />
DSM<br />
Acheni siasa, leteni<br />
maendeleo<br />
Nakereka sana na Baraza la Madiwani<br />
kugombana na Mkurugenzi wa<br />
Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga.<br />
Kila siku ni mifarakano isiyokuwa na<br />
tija. Mpaka sasa maendeleo hakuna<br />
na hatupigi hatua yoyote mbele.<br />
Miundombinu ni mibovu, hospitali ya<br />
wilaya hakuna chumba cha kuhifadhia<br />
maiti, vijana hawana ajira na maisha<br />
ni magumu kwa ujumla. Nawaomba<br />
viongozi hawa wakae pamoja na kutatua<br />
tofauti zao, washikamane na kutuletea<br />
maendeleo katika wilaya yetu.<br />
Saidi Juma Aina<br />
Mkuranga<br />
28 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />
Kama una chochote<br />
unachotaka kusema<br />
tuandikie ili upate<br />
fursa ya kuwaelimisha<br />
wengine<br />
Maoni yaliyotolewa katika ukurasa huu<br />
ni ya wasomaji, si lazima yalingane na<br />
msimamo wa <strong>Femina</strong> <strong>HIP</strong>.<br />
Wateja wengine<br />
wa saluni...<br />
Sipendi tabia ya baadhi ya wateja wanaokuja<br />
saluni kupata huduma za urembo wa nywele<br />
na nakshi nyingine. Wengi wanajisahau<br />
kwamba hili ni eneo la biashara na kazi.<br />
Wanajazana na kuanza kupiga umbea, wakati<br />
mwingine nafasi inakosekana kwa wateja<br />
wanaohitaji kupata huduma. Hii ni kero<br />
hapa kwetu na mbaya zaidi wanaume nao<br />
wanashiriki mambo haya. Jamani nendeni<br />
maeneo yenu mkafanye vijiwe vya umbea na<br />
majungu mtuache sisi tufanye kazi.<br />
Marium a.k.a Mama Zai<br />
Kimanzichana-Mkuranga<br />
Acheni kutudharau<br />
Kuna imani kwamba ukifanya<br />
kazi nyumba za kulala wageni<br />
maarufu kama guest house,<br />
baa au ukiwa mhudumu wa<br />
hoteli jamii inakuchukulia<br />
kama mhuni. Hii si sahihi hata<br />
kidogo kwani wanaofanya<br />
kazi hizi wanajiheshimu, kama<br />
yeyote yule anayefanya kazi<br />
katika sekta nyingine. Acheni<br />
kuwashikashika wahudumu.<br />
Jua kwamba wapo kazini na<br />
siyo sehemu ya kuendekeza<br />
mapenzi ya kulazimisha.<br />
Heshimu utu wao.<br />
Judith Macha<br />
Mkuranga-Pwani<br />
Wewe pia unaweza kulonga na vijana<br />
wenzako. Tuandike maoni,<br />
ushauri, vichekesho,maswali<br />
nk, weka anuani yako na tuma<br />
ukiambatanisha na picha yako<br />
kwa Mhariri, Jarida la Si Mchezo!,<br />
S.L.P 2065 Dar es Salaam.<br />
simchezo@feminahip.or.tz<br />
Au tumbukiza katika boksi la Si<br />
Mchezo! kama lipo katika eneo<br />
unaloishi.
januari-februari 2012 Si Mchezo! 29
Mila katika kupambana na VVU<br />
Unyago ni sehemu ya utamaduni wa watu wa Pwani<br />
ya Tanzania kumfundisha mtoto wa kike anapovunja<br />
ungo mambo muhimu yanayohusu afya ya uzazi, usafi<br />
na majukumu mengine yanayomhusu. Utamaduni huu<br />
umesaidia kwa kiasi kikubwa kuweka njia kwa watu<br />
wazima (manyakanga) kuwaandaa wasichana kwa<br />
maisha ya utu uzima. Mwisho wa mafunzo ya unyago<br />
wasichana ambao huitwa wali hutolewa nje kwa sherehe<br />
maalum ya kuhitimu ijulikanayo kama “kunema”.<br />
Hatua zimechukuliwa…<br />
Asasi isiyokuwa ya kiserikali ya PAYODE<br />
(Partnership for Youth Development)<br />
katika Halmashauri ya Mji wa Kibaha<br />
iliendesha mafunzo shirikishi kwa<br />
manyakanga kuhusu afya ya uzazi<br />
na kujikinga na maambukizi ya VVU.<br />
Mafunzo haya yalisaidia kuboresha uelewa<br />
wa manyakanga na kuwajengea stadi<br />
za kuingiza elimu hii ndani ya mafunzo<br />
ya unyago. Jumla ya manyakanga 40<br />
wamepata mafunzo kupitia PAYODE<br />
tangu mwaka 2008.<br />
30 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />
Watu wanasemaje?<br />
ZINDUKA<br />
Mtazamo uko hivi…<br />
Wasichana na wanawake<br />
wapo katika hatari zaidi ya<br />
kupata maambukizi ya VVU<br />
ikilinganishwa na wavulana<br />
na wanaume wa umri sawa na<br />
wao. Hata hivyo njia rahisi ya<br />
kuwafikia vijana hasa wasichana<br />
kwa shughuli za uelimishaji<br />
kuhusu ujana na makuzi bado ni<br />
changamoto kutokana na mila<br />
na desturi ya Mtanzania.<br />
Ushuhuda unaonyesha kuwa elimu ya unyago<br />
inayotolewa na manyakanga hawa waliopatiwa<br />
mafunzo imesaidia kupunguza tatizo la<br />
wasichana kuachishwa shule kwasababu ya<br />
ujauzito katika maeneo ya mradi. Jamii na<br />
serikali imefurahishwa na hatua ya PAYODE<br />
kutumia utamaduni wa watu wa Pwani kama<br />
njia chanya ya kufikishia wasichana elimu ya afya<br />
ya uzazi . “Natamani watoto wangu wangeliyajua<br />
haya yote kabla,” anasema mwenyekiti wa<br />
manyakanga, Mama Blandina Mbaji.
.<br />
USHAURI<br />
Swali<br />
Nina mpenzi ambaye tumekamilisha taratibu zote za ndoa, lakini kabla ya ndoa<br />
akapata ujauzito. Baada ya kuanza huduma za kliniki akaonekana ana maambukizi<br />
ya VVU, na mimi nilipopimwa nikawa salama. Je, mpenzi wangu huyu anafaa kuoa ?<br />
Ushauri tafadhali. Msomaji Si mchezo! Lindi-Pwani<br />
Kama mmepima na ukagundua<br />
mwenzio ana VVU usimuache.<br />
nendeni kwa mshauri nasaha<br />
atawashauri jinsi ya kumkinga<br />
mtoto na wewe mwenyewe<br />
usipate maambukizi na mtaishi<br />
kwa raha.<br />
Amosi<br />
wa Mkuranga<br />
Kama kweli unampenda<br />
mwenzi wako, nakushauri<br />
endelea kuwa naye kama<br />
rafiki yako wa karibu<br />
sana. Pia kuwa mshauri wake katika hali<br />
aliyonayo maana kuwa na VVU siyo kufa<br />
na urafiki au uhusiano usivunjike.<br />
Ibrahim Manjale,<br />
Mkuranga<br />
SWALI LA TOLEO LIJALO<br />
Pole kaka yangu, kama<br />
kweli hiyo mimba ni<br />
yako na unampenda<br />
mkeo nakushauri<br />
umuoe. Kuwa na<br />
VVU siyo mwisho wa<br />
mapenzi na hakuzuii<br />
kuendeleza mipango<br />
yenu. Nendeni<br />
kwenye kituo cha<br />
huduma na tiba kwa<br />
ushauri zaidi.<br />
Hamisi Nuru<br />
Jimowaco-Mkuranga<br />
Kuna binti tumependana na nimependa tabia zake. Yuko tayari<br />
kuoana nami lakini naogopa kwasababu nimetembea na dada<br />
yake ambaye kwa sasa ameolewa. Ila binti huyo sijafanya naye<br />
ngono, anasema mpaka tuoane. Naombeni ushauri wenu. Festo<br />
Mgaya, Songea.<br />
Nawapongeza kwa kupima. Yeyote anayeishi<br />
na VVU ana haki zote za kibinadamu<br />
ikiwa ni pamoja na kuoa/kuolewa, kuwa<br />
na familia n.k. Maamuzi ya kumuoa au<br />
kutokumuoa ni yako na yeye. Katika upimaji<br />
VVU kuna uwezekano kwa sasa ukawa<br />
salama lakini baada ya muda ukakutwa<br />
nawe hauko salama. Nenda katika kituo cha<br />
ushauri nasaha watakupa elimu ya kuishi<br />
na mke mwenye maambukizi ya VVU bila<br />
wewe kupata maambukizi na kupata watoto<br />
wasio na maambukizi.<br />
Asante<br />
Betty Liduke ni rafiki mkubwa<br />
wa vijana, hata wewe unaweza<br />
kulonga naye. Ni msambazaji<br />
mkubwa wa wa Jarida la Si<br />
Mchezo! Mkoani Njombe. Ni<br />
mshauri nasaha na ni mratibu<br />
wa kitengo cha udhibiti<br />
Ukimwi katika Kampuni ya<br />
TANWAT, Njombe.<br />
Mwandikie kupitia<br />
Jarida la Si Mchezo!<br />
Si Mchezo!<br />
S. L. P. 2065<br />
Dar es Salaam<br />
au tuma ujumbe mfupi wa<br />
maandishi kupitia namba<br />
0715 568222 na utuambie<br />
kama ungependa uchapishwe.<br />
machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />
31
32 Si Mchezo! machi-aprili 2012