21.06.2013 Views

Haliuzwi - Femina HIP

Haliuzwi - Femina HIP

Haliuzwi - Femina HIP

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

ISSN: 0856-8995<br />

KATUNI:<br />

machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />

<strong>Haliuzwi</strong><br />

MIKOPO<br />

imenitoa<br />

1


Mimi na mamsapu<br />

hatutaki utani!<br />

Tunadunduliza vijisenti<br />

vyetu taratiiibu.<br />

Wenyewe tumejiwekea<br />

malengo. Hata wewe<br />

unaweza.<br />

2 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />

Ndiyo,<br />

Bamsapu anatunza<br />

funguo, mie natunza<br />

kibubu. Mpo? Zama<br />

ndani ya toleo hili<br />

ujifunze kuhusu vikundi<br />

vya kuweka na kukopa<br />

na hata upatu! Watu<br />

wanafaidika bwana,<br />

asikwambie mtu!<br />

Si Mchezo! Huzalishwa na<br />

kusambazwa.<br />

Si Mchezo! husambazwa.<br />

Lilikozalishwa toleo hili.


<strong>Femina</strong><br />

<strong>HIP</strong><br />

Mhariri<br />

Majuka Ololkeri<br />

Pendo Mashulano<br />

Mwandishi<br />

Ng’orongo Nyamoni<br />

Washauri<br />

Betty Liduke<br />

Gaure Mdee<br />

Raphael Nyoni<br />

Mkurugenzi Mtendaji<br />

Dr. Minou Fuglesang<br />

Machapisho na Uzalishaji<br />

Amabilis Batamula<br />

Jiang Alipo<br />

Katuni na Usanifu<br />

BabaTau, Inc.<br />

Mpiga Chapa<br />

Jamana Printers Ltd<br />

Shughuli za Nje<br />

Constancia Mgimwa<br />

Nashivai Mollel<br />

Gloria Mkoloma<br />

Christine Bisangwa<br />

Rashid Kejo<br />

Usambazaji<br />

EAM Logistic Ltd<br />

<strong>Femina</strong> <strong>HIP</strong> na Washirika<br />

Si Mchezo! limefanyika kwa hisani<br />

kubwa ya Serikali za Sweden (Sida),<br />

Denmark (DANIDA) na Marekani<br />

kupitia USAID kama sehemu ya<br />

ufadhili wa PEPFAR kwa shirika la<br />

FHI360 mradi wa UJANA, PSI mradi<br />

wa HUSIKA pamoja na HIVOS. Toleo<br />

hili limefanyika kwa ushirikiano na<br />

JHU-CCP/TCCP na RFSU.<br />

Yaliyomo humu ndani ni jukumu la<br />

<strong>Femina</strong> <strong>HIP</strong> na hayawakilishi maoni<br />

au mitazamo ya wafadhili.<br />

Wasiliana nasi kwa:<br />

S.L.P. 2065, Dar es Salaam<br />

Simu: (22) 212 8265, 2126851/2<br />

Fax: (22) 2110842<br />

email: simchezo@feminahip.or.tz<br />

Si Mchezo! huchapishwa na<br />

<strong>Femina</strong> <strong>HIP</strong>.<br />

Sms: 0715 568222<br />

YALIYOMO<br />

4 Stori Yangu: Mikopo imenitoa<br />

6 Mambo mapya:<br />

8 Mambo ya Fedha: Zijue Vicoba<br />

10 Hadithi ya Picha: Mkopo wa ngoma!<br />

14 Je, Wajua: Kabla ya kukopa jipange<br />

16 Tulichovuna: Tunajali Vicoba imetulia!<br />

18 Chezasalama: Mwanamume wa ukweli...<br />

20 Burudani: Vinapanda bei<br />

22 Pasipo na Daktari: Minyoo bwana!<br />

23 Huduma: Walianza kama utani<br />

24 Katuni: Upatu unapogeuka Hupati!<br />

27 Ukweli wa Mambo: Yanawakuta wengi<br />

30 Ujana: Mila katika kupambana na VVU<br />

31 Ushauri<br />

TAHARIRI<br />

Mamboz? Najua umeitikia pouwaaaa! Katika ‘kulipika’ toleo<br />

hili la 59, tuliwazukia wakazi wa Mkuranga. Ingawa tuliweka<br />

kambi wilayani, mishemishe zetu zilikuwa Kimanzichana na<br />

kwingineko vijijini. Tulikula nao stori kibao kuhusu mambo ya<br />

fedha, vikundi vya kuweka na kukopa, hususan SACCOS na<br />

VICOBA. Hatukusahau hata ule ‘mchezo’ wetu maarufu, UPATU!<br />

Nakuacha uzame ndani, nisikuharibie utamu. Kila la kheri!<br />

Pendo<br />

Tuanzie<br />

buku mbili<br />

Ndo<br />

naandika<br />

hivyo..!<br />

“Mmh! sasa<br />

umaskini<br />

baibai”<br />

machi-aprili 2012 Si Si Mchezo!<br />

3


STORI YANGU<br />

Mikopo imenitoa<br />

Naitwa Juma Kapute aka<br />

Chaudele, jina ambalo kwa<br />

Kizaramo linamaanisha<br />

kitindamimba. Kimanzichana<br />

ndo makazi yangu ingawa<br />

asili yangu ni Mngindo kutoka Lindi.<br />

Baada ya kuhitimu elimu ya msingi niliajiriwa<br />

katika mgahawa ambako nilipiga mzigo kwa<br />

miaka minne. Wakati huo nilikuwa nikitunza<br />

kiasi fulani cha mshiko katika mshahara wangu<br />

kila mwezi, hivyo nikawa nimedunduliza hadi<br />

Sh 140,000.<br />

Niliacha kazi na nikaitumia fedha hiyo<br />

kufungua mgahawa wangu na kwa kuwa kwa<br />

mapishi niko juu, pale mgahawani nilikuwa<br />

nikipiga mzigo mwenyewe, ingawa kwa sasa<br />

nasaidiana na mke wangu kwani tuna miradi<br />

mingine kibao.<br />

Niliendesha ‘kijiwe’ hicho huku nikiweka<br />

kiasi fulani cha faida benki, niliamua kujenga<br />

nyumba na kununua samani lakini nikawa na<br />

ndoto ya kupanua biashara.<br />

Wakaja watu wa FINCA ambao walikuwa<br />

wanatoa mikopo kwa wanawake, hivyo mke<br />

wangu alichangamkia mkopo ili afanye biashara<br />

ndogondogo. Kwa kuwa hatukuwa tumejipanga<br />

fresh tulishindwa kurejesha. Ilifika wakati<br />

wakaja kutunyang’anya vitu vyote ndani, hivyo<br />

ikabidi nitumie akiba ya benki kuokoa jahazi.<br />

4 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />

Ila sikukata tamaa, nilijiunga na Kasi Mpya<br />

SACCOS ili niendelee kufukuzia ndoto<br />

zangu. Nikalipa kiingilio kutokana na faida<br />

niliyokuwa nimeipata tena mgahawani<br />

baada ya sakata la FINCA, nikawa nanunua<br />

hisa kila mwezi hadi ikatimia Sh 70,000.<br />

Nikawa na uwezo wa kukopa sh 300,000<br />

ambazo nilizitumia kununulia mbao na<br />

kuziuza. Nikawa narejesha Sh 50,000 kila<br />

mwezi hadi nilipomaliza deni. Nilikuwa na<br />

mpango wa kukopa tena lakini ikatokea<br />

songombingo, SACCOS ikafa na viongozi<br />

wakasepa na mkwanja wote! Imebaki stori!<br />

Baadaye walikuja watu wa VICOBA,<br />

wakatuhamasisha nami nikachangamkia<br />

fursa kama kawa. Tuliunda kundi la watu


30, tukachanga pesa ikafikia Sh<br />

105,000 na kila mmoja akanunua<br />

hisa kwa kadri awezavyo kwani<br />

aliyenunua hisa nyingi alikuwa<br />

na uwezo wa kukopa pesa nyingi<br />

pia.<br />

Wanasema ng’ombe wa maskini<br />

hazai na hata akizaa huzaa<br />

dume! Hawa nao baadaye<br />

walisepa na pesa za wanachama<br />

na hadi leo kesi iko mahakamani.<br />

Hapa napo nilikula hasara ya Sh<br />

52,000 hivi. Sikuchoka!<br />

Baadaye ilianzishwa SACCOS<br />

inaitwa Belita nikalipa kiingilio na michango<br />

nikawa mwanachama. Nilianza na mkopo wa<br />

Sh 50,000, nikaendelea kupanda na hivi majuzi<br />

nimekopa milioni nne. Narejesha bila tabu kwa<br />

kuwa nimewekeza fedha hizo katika biashara.<br />

Naishukuru mikopo maana imepanua biashara<br />

zangu, hivi sasa namiliki mkokoteni, baiskeli<br />

kumi, bajaj na nina mpango wa kuanza kujenga<br />

nyumba nyingine ya ukweli!<br />

Mkokoteni na baiskeli nakodisha, bajaj pia<br />

inakodishwa kubeba mazao na wagonjwa<br />

na nimepata tenda ya kusafirisha wanafunzi.<br />

Vyote hivi vinalipa kichizi!<br />

Mingo zote hizo zinaniwezesha kurejesha<br />

mkopo na kusomesha watoto wangu watatu<br />

na pesa ya kubadilisha<br />

mboga hainipigi chenga.<br />

Akaunti yangu ya benki<br />

nayo naendelea kuitunisha<br />

kwa faida inayobaki baada<br />

ya kutoa marejesho na<br />

matumizi.<br />

Nitaendelea kukopa,<br />

kuwekeza na kurejesha<br />

kwani mikopo ndiyo<br />

iliyonifikisha hapa. Cha<br />

muhimu ni malengo,<br />

nidhamu katika matumizi<br />

na marejesho na pia<br />

kujiwekea akiba benki.<br />

Nasema tena, NITAKOPA<br />

MPAKA KIELEWEKE!<br />

machi-aprili 2012 2012 Si Si Mchezo!<br />

5 5


MAMBO MAPYA<br />

Unapofika Kimanzichana<br />

ukiulizia watu maarufu<br />

eneo lile wa kwanza<br />

kutajwa ni msanii 20%!<br />

Nasi tukasema si vibaya<br />

‘tukimpaisha’ kwa staili ya<br />

pekee, tukatinga nyumbani<br />

kwao japo kupata picha na<br />

familia yake! Unamuona<br />

mrembo Jema? (wa kwanza<br />

kulia). Huyo ni mtoto wa<br />

20% na aliyeshika majarida<br />

ni mama mzazi wa msanii<br />

20%.<br />

Madogo hawa wanapiga bonge la ‘kolabo’ kulishambulia jukwaa!<br />

Ilikuwa ni katika sherehe za Mapinduzi ya Zanzibar huko Mkuranga<br />

ambapo mtoto Ramadhani Kasimu (aliyeshika ‘mic’) alikonga<br />

nyoyo za umati na wimbo “Naenda kusema kwa mama” wa msanii<br />

Asley. Huyo dogo mwingine pichani ni Jaffery A. Jaffery, alikwenda<br />

kutunza akanogewa akabaki uwanjani kumpiga tafu mwenzake!<br />

Naye alitunzwa ‘mshiko’ wa uhakika!<br />

6 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />

Kibubu bwana!<br />

Hahaha!<br />

Hiki kinaitwa kibubu. Inawezekana<br />

kili’batizwa’ jina hilo kwakuwa ‘hakisemi’,<br />

yaani hakionyeshi kilichomo<br />

ndani yake! Kibubu ni benki kiaina!<br />

Kinunue au kichongeshe uwe nacho<br />

nyumbani, ‘tupia’ humo fedha ndogondogo<br />

kila siku, jiti, bati, jero, buku<br />

na hata msimbazi kadri unavyozisaka.<br />

Baada ya mwaka au muda fulani uliojipangia,<br />

kivunje na utaona maajabu!<br />

Watu wamenunua mashamba kwa<br />

vibubu!


VICOBA, SACCOS<br />

wana mengi ya ziada<br />

Uzuri wa vikundi vya kuweka na kukopa<br />

ni zaidi ya ule tunaoweza kuufikiria kwa<br />

haraka. Kitendo cha kuwa pamoja kinawapa<br />

nafasi ya kufanya mambo mengi mengine<br />

yenye faida kwao binafsi na hata kwa jamii<br />

zinazowazunguka. Tumevitembelea sana<br />

vikundi hivi na tumejionea kwamba baadhi<br />

yao wanapokutana kwa shughuli zao<br />

za msingi, wanatumia mkusanyiko huo pia<br />

kupata elimu ya afya. Mashirika mbalimbali<br />

pia hutoa elimu ya mambo tofauti kwa<br />

vikundi hivi kwani si rahisi kuitoa kwa mtu<br />

mmojammoja. Hakuna anayeweza kubisha<br />

kwamba kuwa pamoja kuna faida lukuki.<br />

Cheza kwa stepu na kutumia nguvu kama<br />

Makhirikhiri ndio staili yake. Si mchezo! Jamaa<br />

naye ‘aliwabamba vya kutosha’ wananchi wa<br />

Mwalusembe kwa staili za kuvutia.<br />

machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />

7


8 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />

MAMBO YA FEDHA<br />

Vijue Vicoba<br />

Inawezekana wewe na jirani zako mnatamani kuanzisha chama cha kuweka na kukopa lakini hamjui<br />

hata pa kuanzia! Aliadina Peter Rwezaula, Afisa Maendeleo Mwandamizi wa Wilaya ya Mkuranga<br />

anatupiga ‘darasa’ kidogo kuhusu hili:<br />

“Vyama vya kuweka na kukopa viko vya aina nyingi ila maarufu zaidi ni Vicoba na Saccos. Taratibu zake<br />

hazitofautiani sana lakini kwa leo tutajikita katika Vicoba tu. Twende pamoja!<br />

VICOBA ni nini?<br />

Ni kifupi cha maneno ya kimombo, Village<br />

Community Bank, au kwa ‘kibantu’ chetu<br />

tunaweza kusema ‘Benki’ ya Wanakijiji.<br />

Jinsi ya kuanzisha Vicoba<br />

t Mnatakiwa kuwa kikundi cha watu kuanzia<br />

15 hadi 30.<br />

t Siku ya kwanza ya kukutana mnaweza kumualika<br />

Afisa Ushirika au Afisa Maendeleo<br />

ya Jamii ili kupata maelekezo zaidi.<br />

t Mtengeneze katiba (ni vizuri mpate<br />

msaada wa mtaalamu)<br />

t Wakati wa kutengeneza katiba mtakubaliana<br />

kuhusu kiingilio (ambacho hutolewa<br />

mara moja na hakirudishwi), thamani ya<br />

hisa, jinsi ya kununua n.k.<br />

t Chagueni viongozi wa muda (mtabadilisha<br />

viongozi kufuatana na katiba yenu)<br />

J<br />

Vinaendeshwaje?<br />

n Wanachama wanatakiwa wawe wananunua<br />

hisa lakini lazima kuwe na<br />

ukomo wa hisa anazoweza kumiliki<br />

mtu mmoja.<br />

n Kikundi kikutane angalau mara moja<br />

kwa wiki.<br />

n Ndani ya kikundi cha Vicoba inabidi<br />

muwe na vikundi vya watu watano<br />

watano ili kuwekeana udhamini wakati<br />

wa kukopa<br />

n Ni muhimu kuwa na mfuko wa jamii ili<br />

kusaidiana wakati wa matatizo kama<br />

misiba na mikopo ya dharura isiyo na<br />

riba<br />

n Kikundi cha Vikoba kiwe na sanduku<br />

la kuhifadhia fedha na washika funguo<br />

watatu kwa kufuli tatu.<br />

n Kila kikao wanachama wapewe taarifa<br />

ya akiba, mapato na matumizi.<br />

n Kikundi kikikua itabidi kiwe na akaunti<br />

benki ili kutunza fedha<br />

Kumbuka<br />

Ni kinyume cha sheria kwa<br />

mwanachama mmoja kumiliki<br />

zaidi ya moja ya tano ya hisa za<br />

chama na hairuhusiwi mtu kuwa<br />

mwanachama wa Vicoba mbili.


NGUVU ZA MWANAUME<br />

Jogoo halipandi mtungi?<br />

Ili watoto wasielewe wakubwa hupenda kusema ‘jogoo<br />

halipandi mtungi’! Hili ni tatizo la uume kutokusimama au<br />

Kiswahili sanifu, uhanithi. Watu wenye tatizo hili huchekwa<br />

na hivyo kufanya washindwe kutafuta ushauri wa kitaalamu.<br />

Kufanya hivyo ni kuwanyima haki yao ya msingi ya afya<br />

ya uzazi.<br />

Tuliteta na Dk Constantine Kibela na Dk Lugano Kiswaga wa<br />

Hospitali ya Wilaya ya Mkuranga kuhusu hili kwani tumekuwa<br />

tukipokea maswali lukuki ya wasomaji.<br />

Kulikoni jogoo kushindwa?<br />

“Hili ni tatizo ambalo mtu anaweza kuzaliwa nalo au<br />

kulipata katika kipindi chochote cha maisha yake.<br />

Linaweza kuwa la kudumu au la muda tu,” anasema<br />

Dk Constantine. Kumekuwa na uzushi kwamba kitovu<br />

cha mtoto kikiangukia kwenye uume mtoto atakuwa<br />

hanithi, jambo ambalo si kweli.<br />

Sababu za uhanithi:<br />

n Karibu 60% ya watu wenye tatizo hili hutokana na<br />

sababu za kisaikolojia, umri, matatizo ya kimazingira<br />

mfano: msongo wa mawazo kutokana na kukosa<br />

kazi, fedha, matatizo ya kifamilia, hofu ya kuambukizwa<br />

magonjwa, hofu ya kutumia kondom nk<br />

n Magonjwa sugu katika mwili, kwa mfano, ugonjwa<br />

wa ini, figo, kisukari, kifua kikuu nk<br />

n Matumizi yaliyokithiri ya dawa za kulevya au<br />

pombe<br />

n Vyakula tunavyokula vinaweza kusababisha uhanithi,<br />

kwani mrundikano wa mafuta katika mishipa<br />

ya damu unasababisha damu kushindwa kufika<br />

vizuri katika uume ili kuuwezesha kusimama.<br />

Tatizo hili halipaswi kuwa la mwanamume<br />

tu bali mwanamke anao<br />

uwezo wa kumsaidia mwenzi<br />

wake katika kutafuta ushauri na<br />

hata kumsaidia kuondoa hofu<br />

aliyonayo.<br />

Je, tatizo hili<br />

linatibika?<br />

Kitu muhimu ni kutambua<br />

chanzo cha tatizo lenyewe<br />

na kujitokeza kupata ushauri.<br />

Wanaume wengi wanashindwa<br />

kutafuta ushauri juu ya suala<br />

kama hili kwa kuona haya eti<br />

“mwanaume mzima ijulikane<br />

mi hanithi!” Wengine hufikia<br />

hatua ya kuigiza kama wana<br />

uhusiano wa kujamiiana<br />

ilimradi tu waonekane rijali.<br />

Kwa hisani ya TMEP,<br />

Mradi unaodhaminiwa na RFSU<br />

machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />

9


HADITHI YA PICHA<br />

10<br />

‘MKOPO WA NGOMA!’<br />

Mama Mwajei amejaliwa mtoto mmoja<br />

tu, hivyo anamlea kama mboni<br />

ya jicho! Siku ya siku imewadia,<br />

Mwajei kavunja ungo. Ndiyo! Kawa mkubwa<br />

sasa. Kawekwa ndani mwezi, sasa ni wakati wa<br />

kumtoa, wenyewe wanasema ‘kumkogesha maji’.<br />

Amepania kumfanyia bonge la sherehe, tatizo<br />

mshiko. Anafanyaje? Nini kinatokea? Fuatilia….<br />

Imeigizwa na Kimanzichana Vijana Troupe”<br />

Duh! Namie mwezi<br />

ujao nakamata kitita<br />

Sema usemavyo<br />

lakini hapa ngoma<br />

itachezeka na<br />

pombe zitanyweka<br />

mpaka kieleweke<br />

Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />

Hongera sana.<br />

Laki tano hiyo,<br />

hesabu<br />

Asante sana<br />

Naona hukataziki,<br />

sasa mie simo na<br />

utakuja kujuta<br />

Mama Mwajei ndo<br />

keshaamua, kila mtu<br />

anamshangaa<br />

Ama kweli<br />

tamaa mbele<br />

mauti nyuma!<br />

Si pale Kibisa Saccos mume<br />

wangu? Mikopo nje nje…<br />

Una akili sana<br />

waifu, kachukue<br />

tufanye biashara<br />

Mungu anipe<br />

nini mimi!<br />

Shughuli ya<br />

Mwajuma<br />

itaacha<br />

historia<br />

Alhamis mwamu, Ijumaa mbiga,<br />

Jmosi mkole, usiku wake rusharoho,<br />

Jpili mwali anatoka. Upo?<br />

Haya jirani, asante kwa<br />

mwaliko, tuko pamoja


Shost, mie nikipata tu<br />

mkopo namtoa mwanangu.<br />

Mzee nshamweka sawa<br />

Niliyopewa haitoshi kwa<br />

biashara. Mie naona<br />

tuitumie kumtoa mwajuma<br />

Chonde chonde!<br />

Itakutokea puani<br />

hiyo! Tena mie<br />

simo kabisaaa!<br />

He! Mumeo kakubali?<br />

Yaani mkopo<br />

umcheze mtoto?<br />

Maspika fanya manne<br />

kama hili. Sitaki<br />

muziki wa kitoto<br />

Usitie shaka,<br />

hapa umefika<br />

Hajakubali shost,<br />

nimemwongopea<br />

wa biashara<br />

Mmh! Hii akili au matope? Umcheze<br />

mtoto kwa mkopo? Utaulipaje?<br />

Ulisema ya biashara,<br />

leo unaniambia ya<br />

ngoma! Sitaki kusikia<br />

Mimi ndo<br />

niliyesaini<br />

na mimi ndo<br />

nitadaiwa<br />

na ndo<br />

nshaamua<br />

Ndo ushakuwa mkubwa, nakupatia<br />

ushanga mweupe na mwekundu,<br />

nitakueleza kazi zake…<br />

machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />

11


12<br />

Mungu mkubwa!<br />

Japo nina kazi<br />

ya kufagia lakini<br />

nimeacha historia<br />

Jamani, si<br />

mnisikilize<br />

kwanza?<br />

Huu mweupe unavaa<br />

ukiwa vizuri, yaani<br />

kama hauko hedhi…<br />

Hatujaja kwa<br />

mazungumzo. Lete<br />

chetu, vinginevyo<br />

tunazama ndani<br />

Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />

Leleleleleleeleleeeeeeeee<br />

Yeleleleleleleleee<br />

TAREHE YA MAREJESHO INANUKIA…<br />

Yaani Mwinyi, wewe wa<br />

kukataa kunikopesha<br />

elfu hamsini jamani!<br />

Aaaah, mkuki kwa<br />

nguruwe eenh? Wewe<br />

mbona nikikuomba<br />

‘vitu’ unabana?<br />

Jamaniii, mume wangu<br />

nitamwambia nini mie<br />

Ona sasa, ndo<br />

tushaaibika<br />

Halohalooooooooooo<br />

Maji ndo yamefika<br />

shingoni, anasaga vumbi<br />

kusaka marejesho<br />

Tupishe hukoooo<br />

Hivi angekufuata<br />

wewe msomaji<br />

katika hatua hii<br />

ungemshauri nini?


Anafurahi<br />

lakini mwisho<br />

wake utakuwa<br />

ni majonzi<br />

Mama Mwajei<br />

katimiza ndoto<br />

yake. Tuendelee!<br />

MAMBO YANAZIDI KUWA MAGUMU…<br />

Nipe thelathini<br />

kwa vyote<br />

Mmmh! Anauza bei<br />

ya kutupa! Sijui ana<br />

shida gani!<br />

Hii aibu tupu!<br />

Mwarabu<br />

mie leo<br />

nimeaibika<br />

mtaani!<br />

Nitafanya nini<br />

mie! Najuta<br />

kutokumsikiliza<br />

mume wangu!<br />

Nema<br />

Mwajuma<br />

nemaaaaaa<br />

Kapendezaaaaaa<br />

Fyokofyoko,<br />

unalia nini sasa,<br />

si nilikwambia!<br />

Jamani mwali<br />

wetu kapendeza<br />

hajapendezaaaaaa?<br />

SIKU YA SIKU IMEWADIA…<br />

Ana vitu<br />

chungu mzima,<br />

tukavibebe tu<br />

tuvinadi<br />

Ndiyo, haiwezekani<br />

mkopo achukue<br />

yeye, tulipe sie<br />

Nisamehe mume<br />

wangu, niko chini<br />

ya miguu yako…<br />

Hivi saa hizi ni usiku<br />

au mchana…?<br />

Mi mgeni mji<br />

huu, sijui<br />

Duh! Muziki wa ukweli,<br />

hajaleta nyenze.<br />

Twendeni jamani,<br />

hakuna kumlegezea<br />

Kama hukujifunza<br />

kwa kisa cha Mama<br />

Mwajei hujifunzi tena!<br />

Ni makosa kutumia<br />

mkopo kwa jambo<br />

ambalo halizalishi.<br />

machi-aprili 2012 Si Mchezo! 13


JE, WAJUA?<br />

Kabla ya kukopa jipange!<br />

Wa kucheka mmecheka, wa kusonya mmesonya,<br />

wa kugomba mmegomba, wa kubishana mmebishana<br />

lakini ukweli unabaki palepale kwamba hapa<br />

Mama Mwajei alichemka!<br />

Hebu tusemezane kidogo: hivi, inakuwaje unakubali furaha<br />

ya siku mbili-tatu ikusababishie majuto kwa miaka? Wapo<br />

waliochukua mkopo, wakafurahia jinsi mifuko ilivyoota ‘vijipu’<br />

ghafla, breki ya kwanza ikawa kilabuni ‘kujenga heshima’!<br />

Wapo pia waliochukua mkopo kwa ajili ya kujipatia ‘jiko’ jipya!<br />

Hawa nao tuwape pole!<br />

Katika sakata la Mama Mwajei tunaweza kuwalaumu na kuwachukia<br />

wanakikundi wenzake kwa kitendo cha kwenda<br />

‘kusafisha’ nyumba ya mwenzao, lakini ilikuwa ni haki kwao<br />

kufanya hivyo kwani vinginevyo lingegeuka kuwa ‘zengwe’ lao<br />

na wangepaswa kulipa fedha hiyo kwani wao ndio waliokuwa<br />

wadhamini wake.<br />

Nema<br />

Mwajuma<br />

nemaaaaaa<br />

Kapendezaaaaaa<br />

14 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />

Jamani mwali<br />

wetu kapendeza<br />

hajapendezaaaaaa?<br />

Ukweli ni huu<br />

Jamani, si<br />

mnisikilize<br />

kwanza?<br />

Mikopo si kitu kibaya na wala<br />

hatuna sababu ya kuiogopa kwani<br />

wapo wenzetu waliochukua<br />

mikopo wakawekeza katika<br />

biashara, wakajikwamua kiuchumi<br />

kama tulivyoona katika stori<br />

ya Juma Kaputi kwenye kurasa<br />

za Stori Yangu. Cha muhimu ni<br />

kujipanga na kuwa na malengo<br />

yenye tija.


Hatujaja kwa<br />

mazungumzo. Lete<br />

chetu, vinginevyo<br />

tunazama ndani<br />

Tufanyeje?<br />

Ufahamu<br />

n Fanya utafiti na uwe na ufahamu mzuri wa mradi<br />

unaotaka kuufanya kabla ya kuchukua mkopo<br />

n Ni muhimu kufungua akaunti benki ili uziweke fedha<br />

mara tu baada ya kuzipata kwa usalama wa fedha hizo<br />

na pia kuepuka kuwa nazo mfukoni au nyumbani ili<br />

usishawishike kuzitumia kwa mambo ambayo siyo<br />

uliyoyakusudia<br />

n Usimwamini kila mtu kwa ushauri kuhusu matumizi ya<br />

fedha kwani baadhi ya marafiki wanaweza kukushauri<br />

vibaya kwa kuwa ama wanafaidika na ‘matanuzi’<br />

utakayoyafanya au wangependa kukuona ukiumbuka.<br />

Mkopo, kama lilivyo jina lake, ni<br />

fedha ambayo utatakiwa kuirejesha.<br />

Katika vyama vya ushirika, kama<br />

SACCOS, VICOBA na hata katika taasisi<br />

nyingine za fedha, mkopo wowote<br />

utakaouchukua unapaswa kuurejesha<br />

ukiwa na kiasi fulani cha riba, hata kama<br />

utaurejesha baada ya wiki moja tu.<br />

Ili uweze kurejesha mkopo huo pamoja<br />

na riba ni lazima fedha hiyo iwekezwe<br />

katika mradi ambao utairuhusu ‘kutuna’<br />

ili hata utakapokuwa umeirejesha, kiasi<br />

fulani cha faida kibaki kwako kuendeleza<br />

huo mradi uliouanzisha.<br />

Unaporejesha fedha ya mkopo unatoa<br />

fursa kwa wenzako pia kuweza<br />

kukopeshwa na hatimaye watu wengi<br />

zaidi watajikwamua kutoka katika<br />

umaskini.<br />

Kumbuka<br />

J Usichukue mkopo bila<br />

mipango mizuri ya kuwekeza<br />

fedha hiyo<br />

SWALI:<br />

Nini kinasababisha<br />

baadhi ya watu kujikuta<br />

‘wakitumbua’ fedha ya<br />

mkopo?<br />

machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />

15


TULICHOVUNA<br />

Tunajali VICOBA imetulia<br />

n Wakati wakisubiri wenzao kwa kikao, nasi<br />

‘tukawatwanga’ Si Mchezo! wapate ujumbe’<br />

“likuwa ni Jumatatu tuliiivu majira ya mchana.<br />

Kama tulivyokuwa tumekubaliana, mtu<br />

mmoja baada ya mwingine aliwasili katika kivuli<br />

cha mwembe na hatimaye tukajikuta tumetimia<br />

20. Penye wengi hapaharibiki neno, mmoja<br />

wetu alijitolea kuwa kiongozi wa muda, akatuongoza<br />

katika kuanzisha kikundi chetu”.<br />

Hivi ndivyo ilivyoazishwa Tunajali VICOBA, kikundi<br />

cha kuweka na kukopa cha wanakijiji wa Mwanambaya,<br />

Mkuranga. Kikundi hiki kilianzishwa Juni 28,<br />

2003 na hadi sasa kina wanachama 31, kama anavyosimulia<br />

Katibu wa kikundi hicho, Moshi Mfaume<br />

Manda.<br />

Enhe, mkutano uliendaje?<br />

Huo ulikuwa ni mkutano wetu wa kwanza.<br />

Alikuwepo Afisa Maendeleo wa Kata kushuhudia<br />

kinachoendelea. Tulijiundia katiba,<br />

kisha tukafanya uchaguzi wa viongozi. Tunao<br />

viongozi wanane, Mwenyekiti, Katibu,<br />

Mtunza Hazina, wahesabu fedha wawili na<br />

watunza funguo watatu.<br />

16 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />

n Kama kawa, wana sukari, sabuni ya maji<br />

(kwenye kidumu), midamida ikifika watauziana<br />

Mnapokutana mnafanya nini?<br />

Kila Alhamisi saa nane mchana tunakutana:<br />

l Mwenyekiti anafungua mkutano<br />

l Wanaodaiwa sabuni na sukari wanalipa<br />

madeni (ni mradi wa kikundi)<br />

l Tunachangia Mfuko wa Jamii (kila mwanachama<br />

anachangia sh 1,000 kwa mwezi)<br />

l Tunanunua hisa, yaani akiba (fedha) mtu<br />

anayoamua kuweka (bei ya hisa ni sh 500<br />

na mtu anaweza kununua hadi hisa 5 kwa<br />

wakati mmoja)<br />

l Waliokopeshwa fedha wanarejesha<br />

l Tunasoma barua za maombi ya mikopo<br />

(kama zipo)<br />

l Tunawakopesha wale ambao maombi yao<br />

yamepitishwa na kikundi<br />

l Tunauziana sukari na sabuni (kwa<br />

mkopo)<br />

l Katibu anasoma taarifa ya mapato na<br />

matumizi<br />

l Mwenyekiti anafunga kikao


n Mida ya hisa ilipofika, kila<br />

mwanachama alinunua kadri ya<br />

uwezo wake<br />

Wanachama<br />

wanakopaje?<br />

z Anajaza fomu (tunazo)<br />

z Inasainiwa na wadhamini<br />

wawili ambao lazima wawe ni<br />

wanachama wa kikundi<br />

z Maombi yatasomwa mbele ya<br />

wanakikundi wote tunapokutana<br />

na yatajadiliwa<br />

z Ikipitishwa anakopeshwa, na<br />

kiwango cha juu ni mara tatu<br />

ya hisa alizonazo.<br />

z Anatakiwa kuanza kurejesha<br />

baada ya mwezi mmoja na<br />

katika miezi mitatu lazima awe<br />

amemaliza<br />

z Tunatoza riba ya asilimia 10 ya<br />

mkopo<br />

z Anayeshindwa kulipa tunachukua<br />

hisa zake zote pamoja<br />

na za wadhamini wake<br />

n Wanauziana sukari ili kutunisha mfuko.<br />

Ni kwa mkopo na wiki ijayo kila mmoja<br />

atapaswa kulipa!<br />

Mna vyanzo vingine vya mapato?<br />

n Tuna shamba la kikundi ambapo tunalima mihogo,<br />

matunda na mboga<br />

n Tuna mfuko wa jamii ambao tunachangia wenyewe<br />

kwa ajili ya kusaidia wenye matatizo na kugharamia<br />

shughuli za kikundi<br />

n Tunanunua sukari kwa jumla na kuuziana kwa rejareja<br />

n Tumepata mafunzo ya kutengeneza sabuni, hivyo<br />

tunatengeneza na kuuziana<br />

n Wachelewaji katika vikao tunawatoza faini ya sh 500,<br />

ili kutunisha mfuko<br />

Ujumbe?<br />

n Kikao kimefungwa, Mwenyekiti, Dora<br />

Danda na Katibu wake Moshi M. Manda<br />

wanaweka kumbukumbu sawa.<br />

Ndiyo. Vikundi vya kuweka na kukopa ni vizuri. Tumeshuhudia<br />

wanachama wenzetu wakianzisha biashara na hata kujenga<br />

nyumba za kisasa kwa kuweka na kukopa. Nanyi pia mnaweza<br />

kuanzisha!<br />

machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />

17


CHEZASALAMA<br />

Huyu ndiye mwanamume wa ukweli<br />

Edna anakonda kwa mawazo! Ana mtoto wa<br />

mchanga na angependa kusubiri japo kwa<br />

miaka mitatu kabla ya kuzaa mtoto mwingine.<br />

Hajui la kufanya. Amesikia stori nyingi za<br />

kutisha kutoka kwa ‘mashosti’ wake kuhusu njia<br />

za kisasa za uzazi wa mpango, hivyo anaogopa<br />

kuzitumia!<br />

Frank, mumewe Edna, yeye ana mtazamo tofauti.<br />

Amewahi kusoma kijitabu kinachoelezea vizuri<br />

njia za uzazi wa mpango na anafahamu kwamba<br />

stori alizozisikia mkewe hazina ukweli wowote.<br />

18 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />

“Twende kliniki mpenzi wangu. Tutapata maelezo<br />

yote na hofu yako itaondoka. Tutachagua njia inayotufaa<br />

na tutafurahia mapenzi yetu bila hofu,”<br />

Frank anamshawishi Edna na taratiibu wanambeba<br />

mtoto wao Alice na kuongozana kuelekea<br />

kliniki.<br />

Frank ni mwanamume wa kipekee mno! Anajali,<br />

anamhurumia mkewe na anaona umuhimu wa<br />

kutumia njia za uzazi wa mpango kwa faida yake<br />

mwenyewe, mkewe na hata watoto. Si mbabe, ni<br />

msikivu. Huyu ndiye mwanamume wa ukweli!


Faida za kutumia njia<br />

za uzazi wa mpango<br />

Kupanga uzazi kuna faida<br />

nyingi kwa mama, baba, watoto<br />

na familia kwa ujumla<br />

Kwa mama:<br />

n Itamsaidia kurejesha afya<br />

baada ya kujifungua<br />

n Inampa nafasi ya kutosha<br />

ya kuonyesha mapenzi kwa<br />

watoto na kwa mumewe<br />

n Inampa mama nafasi ya<br />

kuhudumia familia na<br />

kufanya shughuli za maendeleo<br />

Kwa watoto:<br />

t Mama mwenye<br />

afya huzaa watoto<br />

wenye afya<br />

t Watapata mapenzi<br />

na huduma<br />

ya wazazi kwa<br />

ukamilifu<br />

Kwa baba:<br />

n Anapunguza mzigo wa jukumu<br />

la kuihudumia familia<br />

n Inamsaidia kumudu mahitaji<br />

ya familia (elimu, chakula,<br />

malazi na mengineyo)<br />

n Inampa nafasi ya kutosha<br />

ya kuonyesha mapenzi kwa<br />

watoto na kwa mkewe<br />

n Anapata muda wa kuhudumia<br />

familia na kufanya<br />

shughuli za maendeleo<br />

Chukua hatua!<br />

n Panga pamoja na mpenzi wako,<br />

amueni lini mnataka kuzaa, watoto<br />

wangapi na wapishane kwa umri<br />

gani<br />

n Kwa ushauri wa mtaalam, kubalianeni<br />

njia ya uzazi wa mpango<br />

ambayo inawafaa.<br />

Ni haki na wajibu wa mwanamume<br />

kushiriki katika<br />

kupanga uzazi. Familia bora<br />

hujengwa na mwanamume<br />

na mwanamke pamoja<br />

machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />

19


BURUDANI<br />

Wimbo: Vinapanda bei<br />

Msanii: Blad Key<br />

Naamka asubuhi ee,<br />

jikoni kwangu kumelala<br />

paka<br />

Namfata mke wangu ee,<br />

amenuna eti anadai talaka<br />

Hataki tuongee,<br />

amenuna eti anataka<br />

kuondoka<br />

Anarudi kiijini,<br />

maisha ya dhiki yeye<br />

amechoka x2<br />

Mie nitafanya nini, na<br />

mfukoni sina hata senti<br />

Kipato changu cha chini,<br />

madukani vitu vinapanda<br />

bei x2<br />

We mama weee!!<br />

Kiitikio<br />

Vinapanda bei,<br />

Kila siku vitu vinapanda<br />

bei,we mama wee.<br />

Vinapanda bei,<br />

Kila siku vitu vinapanda bei<br />

anyokiee.<br />

20 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />

20 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />

Huu neneee<br />

Nimechelewa kazini, kwa<br />

sababu nauli iko juu<br />

Kutokana na hali duni,<br />

ikabidi nako niende kwa<br />

miguu<br />

Ile nafika kazini, bosi nae<br />

anakuja juu<br />

Anaanza nifokea, hali<br />

iliyofanya nibaki roho juu<br />

Mie nitafanya nini kipato<br />

changu hakikidhi mahitaji<br />

Hali ya maisha ni ngumu<br />

kila siku vitu vinapanda bei<br />

x2<br />

We mama weee!!<br />

Kiitikio<br />

Kibwagizo<br />

We we we we wee<br />

We mama we we we, we<br />

mama. x3


Baunsa noma!<br />

Mshikaji alienda kuiba kwa baunsa. Wakati J<br />

anatoka tu, ghafla akakutana nae. Baunsa<br />

akachukua vile vitu na kuvirudisha ndani<br />

halafu akamshika mkono kama ‘mwana’ vile<br />

na wakaanza kutembea. Mshikaji akajua labda<br />

anapelekwa polisi. Kufika kituo cha polisi<br />

cha kwanza wakapita, cha pili wakapita tena<br />

mmh! Mshikaji akaingiwa na hofu kufika kituo<br />

cha tatu baunsa akawa anapita tena, mshikaji<br />

akamuona afande nje akapiga kelele ‘‘afandee<br />

mimi mwiziii’’<br />

Toto nidhamu sifuri<br />

Mtoto: Baba niletee glasi ya maji!<br />

Baba:: We mtoto una kichaa nini? kachukue<br />

mwenyewe!<br />

Mtoto: Bwana niletee!<br />

Baba: Usinisumbue, ntakuja kukupiga makofi!<br />

Mtoto: Basi ukija kunipiga makofi njoo na glasi<br />

ya maji<br />

J<br />

Hajatulia!<br />

Siku moja, mama<br />

mwenye nyumba alikuwa<br />

akimuuliza msichana wake<br />

wa kazi kuhusu kuisha<br />

haraka kwa vijiti vya<br />

kuchokonoa meno.<br />

Mama:<br />

Hizi “toothpicks” mbona<br />

zimeisha haraka?<br />

Dada wa kazi:<br />

Mimi mwenyewe sijui<br />

labda uwaulize watoto<br />

wako, mimi huwa<br />

nikimaliza kutumia tu,<br />

nazirudisha kwenye kopo<br />

lake!<br />

Mama: Haaaa!!??<br />

J<br />

! ! !!<br />

Yataka moyo kuwa dokta….<br />

Mgonjwa:<br />

Dokta mimi nina tatizo la kusahau, yaani<br />

nikisema neno au ukiniambia hapo hapo<br />

nasahau kabisa.<br />

Dokta: Tatizo lako limekuanza lini?<br />

Mgonjwa: Tatizo gani tena?<br />

Dokta: ???**$!!!<br />

J<br />

machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />

21


Minyoo bwana!<br />

Hahahahaaaa! Watu bwana! Bila shaka umewahi<br />

kusikia mtu akisema eti binadamu lazima<br />

awe na minyoo! Eti minyoo ina kazi ya kulainisha<br />

chakula katika tumbo la binadamu!<br />

Dokta Lugano Kiswaga wa Hospitali ya<br />

Wilaya ya Mkuranga anasema huo ni uongo<br />

mtupu!<br />

“Minyoo iko ya aina nyingi na hakuna aina<br />

yoyote ya minyoo yenye faida katika mwili<br />

wa binadamu, ila huingia katika mwili wa binadamu<br />

au mnyama kwani ndiyo mazingira<br />

yanayoiwezesha kuzaliana,” anasema.<br />

Mh! Inaingiaje?<br />

“Kuna njia nyingi za kuingia ila kubwa ni<br />

kupitia chakula kisichosafishwa vizuri,<br />

nyingine ni kujipenyeza katika matundu<br />

madogomadogo ya ngozi ya mwanadamu,”<br />

anasema.<br />

“Ukila chochote bila kunawa mikono vizuri<br />

kwa sabuni na maji safi, unaweza kuingiza<br />

minyoo tumboni. Usipoosha vizuri matunda<br />

na mboga za majani zinazoliwa zikiwa<br />

mbichi, mfano kabichi, karoti, nyanya nk,<br />

unaweza kula minyoo”, anasema.<br />

“Minyoo inapopenya katika matundu ya<br />

ngozi, inakwenda katika mishipa ya damu,<br />

kisha kwenye moyo, halafu kwenye mapafu<br />

na hatimaye unaikohoa inaingia katika<br />

utumbo. Inapofika humo huweka makazi,<br />

ikakua, ikataga mayai, kisha ukayatoa mayai<br />

hayo kupitia haja kubwa, yanaanguliwa<br />

nje ya tumbo la binadamu na mzunguko<br />

hujirudia kama kawaida”, anasema.<br />

22 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />

PASIPO NA DAKTARI<br />

Utajuaje kama una minyoo?<br />

n Unaweza kuiona katika kinyesi<br />

n Kukohoa<br />

n Inatoboa utumbo, hivyo unaweza kuona<br />

damu kidogo katika kinyesi<br />

n Kuwashwa sana usiku sehemu ya haja kubwa<br />

(hasa kwa watoto)<br />

n Kukonda<br />

n Kukosa hamu ya kula<br />

n Upungufu wa damu<br />

n Ngozi kupauka<br />

n Ukuaji hafifu (kudumaa – hasa kwa watoto)<br />

Chonde chonde!<br />

Ukiona dalili hizi au hata baadhi yake, kamwone<br />

mtaalam wa afya kwa vipimo na ushauri kwani<br />

linaweza kuwa ni tatizo la minyoo, ambalo<br />

linaweza kuleta athari kubwa kwa binadamu,<br />

ikiwamo upungufu mkubwa<br />

wa damu na hata<br />

kifo! Usimeze dawa za<br />

minyoo bila ushauri wa<br />

daktari. J<br />

Kumbuka<br />

Zingatia usafi<br />

kujiepusha na<br />

magonjwa


HUDUMA<br />

Walianza kama utani!<br />

Siku moja wanawake 30 walikaa kikao ‘wakateta’<br />

jambo. Walichoka kuona jinsi janga la Ukimwi lilivyokuwa<br />

likienea kwa kasi katika jamii. Waliunda<br />

kikundi chao ‘wakakibatiza’ jina la JIMOWACO, yaani<br />

Jipeni Moyo Women and Community Organisation,<br />

kikundi ambacho leo hii ni gumzo kubwa Kisarawe na<br />

Mkuranga.<br />

Hawa, ni wanawake ambao waume zao walikuwa wakifanya<br />

kazi katika mgodi wa chokaa huko Kisarawe na hiyo<br />

ilikuwa ni mwaka 2003. Walichangishana pesa, wapo walioomba<br />

kwa waume zao, wapo waliovunja ‘vibubu’ vyao,<br />

ili mradi wazo lao lifanikiwe!<br />

Wako mbali!<br />

Leo hii JIMOWACO imesimama!<br />

Imeajiri wafanyakazi<br />

12 na tayari imefungua<br />

tawi wilayani Mkuranga,<br />

imeanzisha vikundi 20 vya<br />

kuweka na kukopa katika<br />

jamii, vikiwa na mchanganyiko<br />

wa watu waishio na<br />

VVU na wasio navyo. Wanatoa<br />

mahitaji ya shule na<br />

huduma za afya kwa watoto<br />

wapatao 7,093 na wanatoa<br />

huduma kwa watu<br />

waishio na VVU/Ukimwi<br />

wapatao 1,913 (Mkuranga)<br />

na 1,200 (Kisarawe)!<br />

Ama kweli hata mbuyu<br />

ulianza kama mchicha!<br />

Mambo sio mteremko!<br />

Wana malengo!<br />

“Tulipoanza tulikusudia kusadia<br />

yatima na wanaoishi katika<br />

mazingira hatarishi, wajane,<br />

na waishio na VVU/Ukimwi”,<br />

anasema Flaviana Mlaki, Mratibu<br />

wa Watoto-JIMOWACO.<br />

Mwananchi akifurahia msaada wa sare za<br />

shule kutoka JIMOWACO<br />

Pamoja na mafanikio makubwa waliyoyapata, Flaviana<br />

anasema vikwazo pia vipo:<br />

n Hawana uwezo wa kuwafikia watoto wote wanaohitaji<br />

huduma yao kwani ni wengi sana katika jamii.<br />

n Unyanyapaa nao bado upo na ni kikwazo kwa watu kujitokeza<br />

kwenda kupima VVU.<br />

n Licha ya elimu inayotolewa, maambukizi mapya bado<br />

yanajitokeza kwa kasi kwani waliokuwa wagonjwa baada<br />

ya kupata ahueni wanaendelea kuambukiza wengine.<br />

n Baadhi ya watu wanapougua kutokana na Ukimwi wanaamini<br />

wamerogwa, hivyo wanakwenda kwa waganga<br />

wa kienyeji.<br />

Wana ujumbe kwetu!<br />

JIMOWACO wanaamini kwamba<br />

hata wewe msomaji pamoja na watu<br />

waliokuzunguka mnaweza kuanzisha<br />

mkakati kama huu katika eneo lenu.<br />

Siri ya mafanikio ni subira, kujiamini<br />

na kupeana moyo!<br />

machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />

23


KATUNI<br />

upatu au hupati?<br />

Wanawake Mtaa wa Sita<br />

ni wachakarikaji haswa!<br />

Asiyeuza juisi anachoma<br />

maandazi, ili mradi mkono uende<br />

kinywani. Siku moja mwenzao,<br />

Mama Semeni, anapata wazo, ‘analiuza’<br />

kwa mashostito nao wanaingia<br />

‘line’. Songombingo linalotokea<br />

baadaye mmmmh, almanusura mtu<br />

asutwe kwa matarumbeta! Kulikoni?<br />

Sitaki kukumalizia utamu! Fuatilia!<br />

Michoro: babatau cartoons 2012<br />

BAADA YA WIKI MBILI<br />

24 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />

MCHEZO UMEANZA


machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />

25


26 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />

Ama kweli majuto<br />

ni mjukuu!<br />

Kijumbe ndo<br />

keshatoroka na<br />

fedha za mchezo,<br />

ameacha<br />

vumbi tu!<br />

Upatu ni<br />

mzuri. Tatizo<br />

wengi wetu<br />

tunaucheza<br />

kienyeji mno!


UKWELI WA MAMBO<br />

Yanawakuta wengi!<br />

Stori ya Mama Semeni<br />

na wenzake haichekeshi<br />

bali inasikitisha!<br />

Inawezekana hata wewe ama<br />

unacheza upatu au una mpango<br />

wa kucheza. Inawezekana<br />

umeapa kutokucheza tena<br />

upatu kwani yaliwahi kukukuta<br />

yaliyomkuta Mama Havinitishi<br />

na wenzake! Pole!<br />

Sio mchezo mbaya<br />

Upatu au ‘mchezo’ kama<br />

wengi wanavyouita,<br />

si jambo baya. Wengi<br />

‘wametoka’ kwa staili hii.<br />

Utaukuta mitaani, maofisini,<br />

kwa watu ambao ama<br />

wako katika ‘kijiwe’ kimoja<br />

au wanafanya biashara<br />

zinazofanana. Kwa kifupi ni<br />

jambo zuri. Ndiyo, kwani si<br />

kila mmoja ana uwezo wa<br />

kudunduliza vijisenti peke<br />

yake hadi mfuko utune.<br />

Zaidi ya kuwasaidia<br />

watu kuinua mitaji na<br />

kujikwamua kimaisha,<br />

‘mchezo’ huu unawasaidia<br />

watu kuishi kijamaa,<br />

yaani kufahamiana na<br />

kusaidiana katika matatizo<br />

mbalimbali ya kijamii,<br />

wengine wanasema ‘kufa na<br />

kuzikana’.<br />

Tatizo nini?<br />

Tumeshuhudia ngumi zikilika mitaani, watu<br />

wakiporomosheana matusi, wengine wakibubujikwa<br />

machozi baada ya ‘kuingia chaka’, ukiuliza kulikoni<br />

unaambiwa kijumbe ‘kasepa’ na fedha za wanakikundi!<br />

Yote haya yanatokea kwa sababu tunaucheza ‘mchezo’<br />

huu kienyeji mno, kama tunavyoona katika stori ya Mama<br />

Semeni na wenzake.<br />

Walipaswa wakutane, wafanye makubaliano ya kucheza<br />

‘mchezo’, kuwe na orodha ya wanachama iliyoandikwa<br />

na zamu za ‘kupokea’,<br />

wafanye uchaguzi wa<br />

‘kijumbe’ wajipangie<br />

masharti na kuwe<br />

na daftari la kusaini<br />

mwanachama<br />

anapowasilisha mchango<br />

na anapopokea.<br />

J Kumbuka<br />

Ni vizuri muwe ni kikundi<br />

cha watu mnaofahamiana<br />

vizuri kwa makazi, kipato<br />

na tabia, ili kuepusha<br />

mambo kwenda mrama.<br />

machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />

27


SAUTI YANGU<br />

Si Mchezo!<br />

<strong>Femina</strong> <strong>HIP</strong><br />

SLP 2065,<br />

DSM<br />

Acheni siasa, leteni<br />

maendeleo<br />

Nakereka sana na Baraza la Madiwani<br />

kugombana na Mkurugenzi wa<br />

Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga.<br />

Kila siku ni mifarakano isiyokuwa na<br />

tija. Mpaka sasa maendeleo hakuna<br />

na hatupigi hatua yoyote mbele.<br />

Miundombinu ni mibovu, hospitali ya<br />

wilaya hakuna chumba cha kuhifadhia<br />

maiti, vijana hawana ajira na maisha<br />

ni magumu kwa ujumla. Nawaomba<br />

viongozi hawa wakae pamoja na kutatua<br />

tofauti zao, washikamane na kutuletea<br />

maendeleo katika wilaya yetu.<br />

Saidi Juma Aina<br />

Mkuranga<br />

28 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />

Kama una chochote<br />

unachotaka kusema<br />

tuandikie ili upate<br />

fursa ya kuwaelimisha<br />

wengine<br />

Maoni yaliyotolewa katika ukurasa huu<br />

ni ya wasomaji, si lazima yalingane na<br />

msimamo wa <strong>Femina</strong> <strong>HIP</strong>.<br />

Wateja wengine<br />

wa saluni...<br />

Sipendi tabia ya baadhi ya wateja wanaokuja<br />

saluni kupata huduma za urembo wa nywele<br />

na nakshi nyingine. Wengi wanajisahau<br />

kwamba hili ni eneo la biashara na kazi.<br />

Wanajazana na kuanza kupiga umbea, wakati<br />

mwingine nafasi inakosekana kwa wateja<br />

wanaohitaji kupata huduma. Hii ni kero<br />

hapa kwetu na mbaya zaidi wanaume nao<br />

wanashiriki mambo haya. Jamani nendeni<br />

maeneo yenu mkafanye vijiwe vya umbea na<br />

majungu mtuache sisi tufanye kazi.<br />

Marium a.k.a Mama Zai<br />

Kimanzichana-Mkuranga<br />

Acheni kutudharau<br />

Kuna imani kwamba ukifanya<br />

kazi nyumba za kulala wageni<br />

maarufu kama guest house,<br />

baa au ukiwa mhudumu wa<br />

hoteli jamii inakuchukulia<br />

kama mhuni. Hii si sahihi hata<br />

kidogo kwani wanaofanya<br />

kazi hizi wanajiheshimu, kama<br />

yeyote yule anayefanya kazi<br />

katika sekta nyingine. Acheni<br />

kuwashikashika wahudumu.<br />

Jua kwamba wapo kazini na<br />

siyo sehemu ya kuendekeza<br />

mapenzi ya kulazimisha.<br />

Heshimu utu wao.<br />

Judith Macha<br />

Mkuranga-Pwani<br />

Wewe pia unaweza kulonga na vijana<br />

wenzako. Tuandike maoni,<br />

ushauri, vichekesho,maswali<br />

nk, weka anuani yako na tuma<br />

ukiambatanisha na picha yako<br />

kwa Mhariri, Jarida la Si Mchezo!,<br />

S.L.P 2065 Dar es Salaam.<br />

simchezo@feminahip.or.tz<br />

Au tumbukiza katika boksi la Si<br />

Mchezo! kama lipo katika eneo<br />

unaloishi.


januari-februari 2012 Si Mchezo! 29


Mila katika kupambana na VVU<br />

Unyago ni sehemu ya utamaduni wa watu wa Pwani<br />

ya Tanzania kumfundisha mtoto wa kike anapovunja<br />

ungo mambo muhimu yanayohusu afya ya uzazi, usafi<br />

na majukumu mengine yanayomhusu. Utamaduni huu<br />

umesaidia kwa kiasi kikubwa kuweka njia kwa watu<br />

wazima (manyakanga) kuwaandaa wasichana kwa<br />

maisha ya utu uzima. Mwisho wa mafunzo ya unyago<br />

wasichana ambao huitwa wali hutolewa nje kwa sherehe<br />

maalum ya kuhitimu ijulikanayo kama “kunema”.<br />

Hatua zimechukuliwa…<br />

Asasi isiyokuwa ya kiserikali ya PAYODE<br />

(Partnership for Youth Development)<br />

katika Halmashauri ya Mji wa Kibaha<br />

iliendesha mafunzo shirikishi kwa<br />

manyakanga kuhusu afya ya uzazi<br />

na kujikinga na maambukizi ya VVU.<br />

Mafunzo haya yalisaidia kuboresha uelewa<br />

wa manyakanga na kuwajengea stadi<br />

za kuingiza elimu hii ndani ya mafunzo<br />

ya unyago. Jumla ya manyakanga 40<br />

wamepata mafunzo kupitia PAYODE<br />

tangu mwaka 2008.<br />

30 Si Mchezo! machi-aprili 2012<br />

Watu wanasemaje?<br />

ZINDUKA<br />

Mtazamo uko hivi…<br />

Wasichana na wanawake<br />

wapo katika hatari zaidi ya<br />

kupata maambukizi ya VVU<br />

ikilinganishwa na wavulana<br />

na wanaume wa umri sawa na<br />

wao. Hata hivyo njia rahisi ya<br />

kuwafikia vijana hasa wasichana<br />

kwa shughuli za uelimishaji<br />

kuhusu ujana na makuzi bado ni<br />

changamoto kutokana na mila<br />

na desturi ya Mtanzania.<br />

Ushuhuda unaonyesha kuwa elimu ya unyago<br />

inayotolewa na manyakanga hawa waliopatiwa<br />

mafunzo imesaidia kupunguza tatizo la<br />

wasichana kuachishwa shule kwasababu ya<br />

ujauzito katika maeneo ya mradi. Jamii na<br />

serikali imefurahishwa na hatua ya PAYODE<br />

kutumia utamaduni wa watu wa Pwani kama<br />

njia chanya ya kufikishia wasichana elimu ya afya<br />

ya uzazi . “Natamani watoto wangu wangeliyajua<br />

haya yote kabla,” anasema mwenyekiti wa<br />

manyakanga, Mama Blandina Mbaji.


.<br />

USHAURI<br />

Swali<br />

Nina mpenzi ambaye tumekamilisha taratibu zote za ndoa, lakini kabla ya ndoa<br />

akapata ujauzito. Baada ya kuanza huduma za kliniki akaonekana ana maambukizi<br />

ya VVU, na mimi nilipopimwa nikawa salama. Je, mpenzi wangu huyu anafaa kuoa ?<br />

Ushauri tafadhali. Msomaji Si mchezo! Lindi-Pwani<br />

Kama mmepima na ukagundua<br />

mwenzio ana VVU usimuache.<br />

nendeni kwa mshauri nasaha<br />

atawashauri jinsi ya kumkinga<br />

mtoto na wewe mwenyewe<br />

usipate maambukizi na mtaishi<br />

kwa raha.<br />

Amosi<br />

wa Mkuranga<br />

Kama kweli unampenda<br />

mwenzi wako, nakushauri<br />

endelea kuwa naye kama<br />

rafiki yako wa karibu<br />

sana. Pia kuwa mshauri wake katika hali<br />

aliyonayo maana kuwa na VVU siyo kufa<br />

na urafiki au uhusiano usivunjike.<br />

Ibrahim Manjale,<br />

Mkuranga<br />

SWALI LA TOLEO LIJALO<br />

Pole kaka yangu, kama<br />

kweli hiyo mimba ni<br />

yako na unampenda<br />

mkeo nakushauri<br />

umuoe. Kuwa na<br />

VVU siyo mwisho wa<br />

mapenzi na hakuzuii<br />

kuendeleza mipango<br />

yenu. Nendeni<br />

kwenye kituo cha<br />

huduma na tiba kwa<br />

ushauri zaidi.<br />

Hamisi Nuru<br />

Jimowaco-Mkuranga<br />

Kuna binti tumependana na nimependa tabia zake. Yuko tayari<br />

kuoana nami lakini naogopa kwasababu nimetembea na dada<br />

yake ambaye kwa sasa ameolewa. Ila binti huyo sijafanya naye<br />

ngono, anasema mpaka tuoane. Naombeni ushauri wenu. Festo<br />

Mgaya, Songea.<br />

Nawapongeza kwa kupima. Yeyote anayeishi<br />

na VVU ana haki zote za kibinadamu<br />

ikiwa ni pamoja na kuoa/kuolewa, kuwa<br />

na familia n.k. Maamuzi ya kumuoa au<br />

kutokumuoa ni yako na yeye. Katika upimaji<br />

VVU kuna uwezekano kwa sasa ukawa<br />

salama lakini baada ya muda ukakutwa<br />

nawe hauko salama. Nenda katika kituo cha<br />

ushauri nasaha watakupa elimu ya kuishi<br />

na mke mwenye maambukizi ya VVU bila<br />

wewe kupata maambukizi na kupata watoto<br />

wasio na maambukizi.<br />

Asante<br />

Betty Liduke ni rafiki mkubwa<br />

wa vijana, hata wewe unaweza<br />

kulonga naye. Ni msambazaji<br />

mkubwa wa wa Jarida la Si<br />

Mchezo! Mkoani Njombe. Ni<br />

mshauri nasaha na ni mratibu<br />

wa kitengo cha udhibiti<br />

Ukimwi katika Kampuni ya<br />

TANWAT, Njombe.<br />

Mwandikie kupitia<br />

Jarida la Si Mchezo!<br />

Si Mchezo!<br />

S. L. P. 2065<br />

Dar es Salaam<br />

au tuma ujumbe mfupi wa<br />

maandishi kupitia namba<br />

0715 568222 na utuambie<br />

kama ungependa uchapishwe.<br />

machi-aprili 2012 Si Mchezo!<br />

31


32 Si Mchezo! machi-aprili 2012

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!