MAGONJWA MAKUU YA KUKU, TIBA NA KINGA - Research Into Use
MAGONJWA MAKUU YA KUKU, TIBA NA KINGA - Research Into Use
MAGONJWA MAKUU YA KUKU, TIBA NA KINGA - Research Into Use
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Maelezo<br />
Minyoo huishi katika njia ya chakula kwenye kuku na wanyama. Minyoo inaweza kuwa na faida kwa mnyama au<br />
inaweza kuleta madhara. Minyoo mingi ya kuku husababisha madhara. Minyoo muhimu katika kuku ni aina ya<br />
Minyoo bapa na Minyooya Duara.<br />
3.4.1 MINYoo bAPA (TAPe WorM INfeSTATIoN)<br />
Maelezo<br />
Ni ugonjwa unaosababishwa na Minyoo Bapa ambayo hushambulia kuku, kanga na njiwa. Minyoo huathiri kuku<br />
na ndege wadogo na wakubwa ijapokuwa ndege wadogo wanaathirika zaidi.<br />
jinsi Ugonjwa Unavyoenea<br />
Dalili<br />
Tiba<br />
• Maambukizi huenea kupitia kinyesi cha kuku, ndege na wadudu wa kati (minyoo ya kwenye udongo,<br />
kombamwiko, na panzi).<br />
• Njia kuu ya maambukizi ni kupitia chakula na maji yaliyochafuliwa na wadudu wa kati wanaoneza<br />
minyoo.<br />
• Minyoo bapa (tegu) huishi tumboni na huweza kuziba utumbo na kusababisha kifo<br />
• Kuku kukonda na kutokukua vizuri<br />
• Kuku wanaonyesha ukosefu wa damu – macho na ndimi na sehemu zisizo na manyoya hupauka<br />
• Kuhara damu<br />
• Kwa kawaida vifo huwa vingi<br />
• Dawa za Minyoo – huwekwa kwenye maji au chakula.<br />
• Pata ushauri wa daktari.<br />
Magonjwa Makuu Ya Kuku, Tiba Na Kinga<br />
47