MAGONJWA MAKUU YA KUKU, TIBA NA KINGA - Research Into Use
MAGONJWA MAKUU YA KUKU, TIBA NA KINGA - Research Into Use
MAGONJWA MAKUU YA KUKU, TIBA NA KINGA - Research Into Use
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
3.1.7 KoLIbASILoSI (coLIbAcILLoSIS)<br />
Maelezo<br />
Ni ugonjwa unaosababishwa na bakteria na hushambulia zaidi kuku na bata. Ugonjwa huu huathiri zaidi vifaranga.<br />
jinsi Ugonjwa Unavyoenea<br />
Dalili<br />
• Chanzo cha maambukizi ni maji na chakula kilichochafuliwa na kinyesi cha kuku wagonjwa. Bakteria<br />
wanaosababisha ugonjwa wameenea kila mahali hivyo kuweza kuchafua maji na chakula.<br />
• Vifaranga wanaweza kupata maambukizi wakiwa bado ndani ya yai kabla ya kuanguliwa.<br />
• Mayai machafu yenye bacteria ndiyo njia kuu ya kuambukiza vifaranga kupitia kitovu baada ya<br />
kutotolewa. Pia mayai yenye maganda dhaifu na makasha machafu ya kubebea mayai ni chanzo kingine<br />
cha maambukizi.<br />
• Kuku wanaonekana kuzubaa<br />
• Kuku wanatoa sauti ya chini chini<br />
• Kuku wanajikusanya karibu na taa inayotoa joto<br />
• Kuharisha na kinyesi kugandana katika njia ya haja<br />
• Ngozi ya kifuani ina uvimbe<br />
• Vifo vya vifaranga vinaweza kufikia asilimia 10, vifaranga walio totolewa inaweza kufika asilimia 50.<br />
Uchunguzi wa Mzoga<br />
Sehemu ya haja inaweza kuzibwa na kinyesi kilichokauka<br />
Njano ya yai kutapakaa tumboni, uchafu wenye rangi nyeupe au kijani, ukiwa na damu<br />
Uvimbe kwenye ini, utumbo na utandu wa tumboni<br />
20 Magonjwa Makuu Ya Kuku, Tiba Na Kinga