28.02.2013 Views

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

<strong>JAMHURI</strong> <strong>YA</strong> <strong>MUUNGANO</strong> <strong>WA</strong> <strong>TANZANIA</strong><br />

WIZARA <strong>YA</strong> MAENDELEO <strong>YA</strong> MIFUGO NA UVUVI<br />

KANUNI ZA UFUGAJI BORA <strong>WA</strong> MIFUGO<br />

2000<br />

2009


<strong>JAMHURI</strong> <strong>YA</strong> <strong>MUUNGANO</strong> <strong>WA</strong> <strong>TANZANIA</strong><br />

WIZARA <strong>YA</strong> MAENDELEO <strong>YA</strong> MIFUGO NA UVUVI<br />

KANUNI ZA UFUGAJI BORA <strong>WA</strong> MIFUGO<br />

WIZARA <strong>YA</strong> MAENDELEO <strong>YA</strong> MIFUGO NA UVUVI<br />

S.L.P 9152<br />

DAR ES SAALAM MEI, 2009<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na kujiongezea<br />

kipato<br />

i


Kimetayarishwa na<br />

© Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi-Dar es salaam<br />

Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi<br />

S. L. P 9152<br />

Dar es Salaam - Tanzania<br />

Toleo la kwanza 2009<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na kujiongezea<br />

kipato<br />

ii


ORODHA <strong>YA</strong> VITABU VINGINE VILIVYOPO<br />

Vipo vitabu vingine ambavyo vimetayarishwa na Wizara kuwasaidia wafugaji, wanafunzi<br />

wa taaluma ya mifugo na wataalam wa mifugo wanaofanya shughuli za ugani. Vitabu<br />

hivyo ni:-<br />

Ufugaji Bora wa Nguruwe (Toleo la tatu) 2009<br />

Ufugaji Bora wa Kuku (Toleo la tano) 1997<br />

Ufugaji Bora wa Ng’ombe wa Nyama 2003<br />

Ufugaji Bora wa Ng’ombe wa Maziwa 2005<br />

Ufugaji Bora wa Kuku wa Kienyeji 2008<br />

Ufugaji Bora wa Nguruwe (Toleo la tatu) 2009<br />

Uzalishaji Bora wa Ngozi 2009<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na kujiongezea<br />

kipato<br />

iii


<strong>WA</strong>HARIRI<br />

Walioshiriki kuhariri kijitabu hiki cha Ufugaji Bora ni:-<br />

M. R. Bakuname Idara ya Utafiti, Mafunzo na huduma za Ugani<br />

E. S. Mngulwi Idara ya Utafiti, Mafunzo na huduma za Ugani<br />

H. L. N. Lyimo Idara ya Utafiti, Mafunzo na huduma za Ugani<br />

L. Asimwe Idara ya Uzalishaji Mifugo na Uendelezaji wa Miundombinu<br />

ya Masoko<br />

A. S. Bundala Idara ya Huduma za Afya ya Mifugo<br />

C. J. Ndomba Idara ya Uendelezaji Mifumo ya Ufugaji wa Asili<br />

M. I. Shawala Chuo cha Mafunzo ya Mifugo - Morogoro<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na kujiongezea<br />

kipato<br />

iv


SHUKRANI<br />

Shukrani ziwaendee watayarishaji wa kijitabu hiki ambao ni wataalam wa Kitengo cha<br />

Ugani na wataalam wengine wote wa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi na Ofisi<br />

ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kwa michango yao mbalimbali<br />

iliyowezesha kufanikisha kazi hii. Waandishi wamezingatia taarifa na takwimu toka<br />

vyanzo mbalimbali ambavyo vyote hivyo wanavitambua na kuvishukuru.<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na kujiongezea<br />

kipato<br />

v


<strong>YA</strong>LIYOMO<br />

SURA UKURASA<br />

JALADA i<br />

<strong>WA</strong>TA<strong>YA</strong>RISHAJI ii<br />

ORODHA <strong>YA</strong> VITABU VINGINE VILIVYOPO iii<br />

<strong>WA</strong>HARIRI iv<br />

SHUKURANI v<br />

<strong>YA</strong>LIYOMO vi<br />

DIBAJI viii<br />

UTANGULIZI ix<br />

SURA <strong>YA</strong> K<strong>WA</strong>NZA 1<br />

1.0 KANUNI ZA UFUGAJI <strong>WA</strong> NG’OMBE BORA 1<br />

1.1 Banda/Zizi la ng’ombe 1<br />

1.2 Uchaguzi wa ng’ombe wa kufuga 2<br />

1.2.1 Ng’ombe wa nyama 2<br />

1.2.2 Ng’ombe wa maziwa 2<br />

1.3 Utunzaji wa ndama 3<br />

1.4 Utunzaji wa ndama baada ya kuachishwa<br />

maziwa hadi kupevuka (miezi 12 – 18) 4<br />

1.5 Utunzaji wa ng’ombe wakubwa 5<br />

1.5.1 Upandishaji 5<br />

1.5.2 Dalili za ng’ombe jike anayehitaji 5<br />

kupandishwa<br />

1.5.3 Taratibu za uhimilishaji 6<br />

1.6 Matunzo ya ng’ombe mwenye mimba 6<br />

1.6.1 Dalili za ng’ombe anayekaribia kuzaa 6<br />

1.6.2 Matatizo yanayoweza kutokea wakati 6<br />

wa kuzaa<br />

1.7 Matunzo ya ng’ombe anayekamuliwa 7<br />

1.8 Utunzaji wa dume 7<br />

1.9 Uzalishaji wa mazao yatokanayo na ng’ombe 7<br />

1.9.1 Uzalishaji wa nyama 7<br />

1.9.2 Uzalishaji wa maziwa 8<br />

1.10 Ulishaji bora kwa misimu mbalimbali ya<br />

mwaka<br />

1.10.1 Hatua za kukabiliana na tatizo la<br />

8<br />

uhaba wa malisho<br />

1.10.2 Njia za kuhifadhi malisho 9<br />

1.10.3 Vyakula vya ziada 10<br />

1.11 Udhibiti na tiba ya magonjwa ya ng’ombe 10<br />

1.12 Kumbukumbu na takwimu muhimu 11<br />

SURA <strong>YA</strong> PILI 12<br />

2.0 KANUNI ZA UFUGAJI BORA <strong>WA</strong> MBUZI NA<br />

KONDOO<br />

12<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na kujiongezea<br />

kipato<br />

8<br />

vi


SURA UKURASA<br />

2.1 Zizi au banda la mbuzi/kondoo 12<br />

2.1.1 Vifaa vya kujengea na vipimo vya<br />

banda<br />

13<br />

2.2 Uchaguzi wa mbuzi/kondoo wa kufuga 14<br />

2.3 Utunzaji wa mbuzi/kondoo watoto 14<br />

2.3.1 Matunzo mengine 15<br />

2.4 Utunzaji wa mbuzi/kondoo wanaokua 15<br />

2.5 Utunzaji wa mbuzi/kondoo jike 16<br />

2.6 Utunzaji wa mbuzi/kondoo mwenye mimba 17<br />

2.7 Utunzaji wa mbuzi/kondoo anayenyonyesha 17<br />

2.8 Utunzaji wa dume la mbegu 17<br />

2.9 Matunzo mengine 17<br />

2.10 Udhibiti wa magonjwa ya mbuzi na kondoo 18<br />

2.11 Uzalishaji wa mazao ya mbuzi na kondoo 19<br />

2.11.1 Uzalishaji wa nyama 19<br />

2.11.2 Uzalishaji wa maziwa 19<br />

2.12 Utunzaji wa kumbukumbu za mifugo 19<br />

SURA <strong>YA</strong> TATU 21<br />

3.0 KANUNI ZA UFUGAJI BORA <strong>WA</strong> NGURUWE 21<br />

3.1 Banda la nguruwe 21<br />

3.2 Kuchagua nguruwe wa kufuga 22<br />

3.3 Utunzaji wa watoto wa nguruwe 22<br />

3.4 Utunzaji wa watoto wa nguruwe wiki 1 – 8 22<br />

3.5 Utunzaji wa nguruwe walioachishwa kunyonya 23<br />

3.6 Utunzaji wa nguruwe jike kutoka kupevuka<br />

hadi kuzaa<br />

24<br />

3.6.1 Kutunza nguruwe mwenye mimba 25<br />

3.6.2 Utunzaji wa nguruwe<br />

anayenyonyesha<br />

25<br />

3.7 Utunzaji wa dume 26<br />

3.8 Udhibiti wa afya na magonjwa ya nguruwe 26<br />

3.9 Uzalishaji wa mazao ya nguruwe 27<br />

3.10 Kuweka na kutunza kumbukumbu 27<br />

SURA <strong>YA</strong> NNE 28<br />

4.0 KANUNI ZA UFUGAJI BORA <strong>WA</strong> KUKU 28<br />

4.1 Banda la kuku 28<br />

4.1.1 Vifaa vinavyotumika kwa ujenzi wa<br />

banda<br />

29<br />

4.1.2 Ukubwa wa banda 29<br />

4.1.3 Vifaa na vyombo muhimu 29<br />

4.2 Kuchagua kuku bora wa kufuga 30<br />

4.2.1 Kuku wa asili 30<br />

4.2.2 Kuku wa kisasa 30<br />

4.2.3 Kuchagua jogoo 30<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na kujiongezea<br />

kipato<br />

vii


SURA UKURASA<br />

4.3 Mayai kwa ajili ya kutotoa vifaranga 31<br />

4.3.1 Uchaguzi wa mayai 31<br />

4.3.2 Utunzaji wa mayai 31<br />

4.4 Utunzaji wa kuku kwa makundi 31<br />

4.4.1 Kulea vifaranga kwa kutumia kuku 31<br />

4.4.2 Kulea vifaranga kwa kutumia bruda 32<br />

4.4.3 Kulea kuku wanaokua (wiki 7 - 20) 32<br />

4.4.4 Kuku wanaotaga 33<br />

4.5 Udhibiti na tiba dhidi ya magonjwa ya kuku 33<br />

4.5.1 Dalili za kuku mgonjwa 34<br />

4.6 Ufugaji wa aina nyingine za ndege 34<br />

4.7 Uzalishaji na masoko ya mazao ya kuku 34<br />

4.8 Utunzaji wa kumbukumbu 35<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na kujiongezea<br />

kipato<br />

viii


DIBAJI<br />

Tanzania ina idadi kubwa ya mifugo, ikiwemo takribani ng’ombe milioni 19.1, mbuzi<br />

13.5, kondoo milioni 3.6, nguruwe million 1.4, na kuku wa asili milioni 33, kuku wa<br />

kisasa milioni 20. Pamoja na kuwa na mifugo mingi kiasi hiki mchango wake katika pato<br />

la taifa bado ni mdogo 4.7% mwaka 2008 kutokana na ufugaji usiozingatia kanuni za<br />

ufugaji bora. Dira ya Sekta ya Mifugo ni kuwa, “Ifikapo mwaka 2025 kuwe na<br />

Sekta ya mifugo ambayo ni shirikishi na inayozingatia ufugaji wa kisasa,<br />

endelevu, inayoendeshwa kibiashara yenye mifugo bora na yenye tija kubwa,<br />

itakayoinua maisha ya Mtanzania kwa kutoa ajira, kuzalisha mali ghafi kwa<br />

ajili ya usindikaji, kuongeza pato la Taifa na kuhifadhi mazingira”. Ili kufikia<br />

malengo ya dira hii, Wizara imeweka mikakati mbalimbali, mojawapo ikiwa ni kuwapatia<br />

wafugaji elimu kuhusu ufugaji bora kupitia machapisho mbalimbali.<br />

Kijitabu hiki ni moja ya machapisho kinachoelezea kanuni za ufugaji bora wa mifugo<br />

hususan ng’ombe wa nyama na maziwa, mbuzi, kondoo, nguruwe na kuku. Kanuni hizi<br />

zimejikita katika uzalishaji, ujenzi wa mabanda, ulishaji bora wa mifugo na upatikanaji<br />

wa maji safi ya kutosha kwa kuzingatia makundi mbalimbali. Aidha kanuni zingine<br />

zilizoainishwa zinahusu udhibiti wa magonjwa na uzalishaji ili kukidhi mahitaji ya soko.<br />

Kuna uwezekano mkubwa kwa wafugaji kupata mafanikio makubwa kutokana na<br />

mifugo yao iwapo watazingatia kanuni hizi. Kanuni za ufugaji bora husaidia kuwaongoza<br />

wafugaji kufahamu mambo muhimu wanayotakiwa kufanya ili mifugo yao ikue vizuri,<br />

wapunguze vifo na kupata mazao mengi na yaliyo bora. Pia uzingatiaji wa kanuni hizi<br />

utampunguzia mfugaji gharama za uzalishaji ili kumwogezea kipato.<br />

Kijitabu hiki kimeandikwa kwa lugha nyepesi ili kuwawezesha watumiaji kukielewa<br />

vizuri. Ni matumaini yangu kuwa kijitabu kitakuwa cha manufaa kwa wafugaji na hasa<br />

pale ambapo kuna upungufu wa wataalamu wa ugani. Hata hivyo, kijitabu hiki<br />

hakichukui nafasi ya watalaam wa ugani hivyo wafugaji wanashauriwa kutumia<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na kujiongezea<br />

kipato<br />

ix


watalaam wa ugani kwa kadri inanavyowezekana. Pia ningependa kutoa mwito kwa<br />

wafugaji kujijengea tabia ya kusoma vitabu kujipatia elimu zaidi na teknolojia ya kisasa.<br />

C. Nyamrunda<br />

Katibu Mkuu 19 Agosti, 2009<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na kujiongezea<br />

kipato<br />

x


UTANGULIZI<br />

Nchini Tanzania zaidi ya asilimia 80 ya wananchi huishi vijijini na hujishughulisha na<br />

kilimo, ufugaji na uvuvi. Shughuli hizi ndizo uti wa mgongo wa taifa hili na zitaendelea<br />

kutegemewa katika kukuza uchumi. Ufugaji ni moja ya shughuli muhimu inayowapatia<br />

wananchi chakula na kipato ikizingatiwa kuwa asilimia 40 ya kaya za kilimo zipatazo<br />

milioni 4.8 hutegemea ufugaji. Mifugo ambayo inafugwa kwa wingi ni ng’ombe, mbuzi,<br />

kondoo, nguruwe na kuku.<br />

Pamoja na kuwa na mifugo mingi, ufugaji bado haujaweza kumwongezea mfugaji<br />

kipato na kuchangia pato la taifa kwa kiasi cha kuridhisha. Changamoto iliyopo mbele<br />

yetu ni kuongeza uzalishaji na tija ili kukidhi malengo ya Mkukuta, Dira ya Taifa ya<br />

Maendeleo 2025, Malengo ya Milenia 2015 na mwongozo wa Kilimo Kwanza. Sekta ya<br />

mifugo inayo nafasi kubwa katika kuchangia kufikia malengo haya kama kanuni za<br />

ufugaji bora zitazingatiwa.<br />

Madhumuni ya kutayarisha kijitabu hiki ni kuainisha kanuni za ufugaji bora unaozingatia<br />

ufugaji wa kisasa, endelevu, unaoendeshwa kibiashara ili kupata mifugo bora na yenye<br />

tija kubwa, itakayoinua maisha ya wananchi wanaotegemea ufugaji na kuhifadhi<br />

mazingira.<br />

Utayarishaji wa kijitabu hiki unatambua pia kuwepo kwa vitabu vingine vinavyoelezea<br />

kwa kina kuhusu ufugaji wa mifugo mbalimbali. Inatarajiwa kwamba kijitabu hiki<br />

kitatumiwa na wafugaji na wadau wengine kama nyenzo muhimu katika kuboresha<br />

uzalishaji wa mifugo nchini.<br />

Kijitabu hiki kinaainisha mambo ya kuzingatia katika ufugaji wa ng’ombe, mbuzi,<br />

kondoo, nguruwe na kuku wakati wa ujenzi wa mabanda, uchaguzi wa wanyama wa<br />

kufuga, na matunzo yao katika makundi mbalimbali. Aidha kanuni za udhibiti wa<br />

magonjwa, uzalishaji mazao ya mifugo yanayokidhi viwango na mahitaji ya soko na<br />

uwekaji wa kumbukumbu sahihi umeainishwa.<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na kujiongezea<br />

kipato<br />

xi


SURA <strong>YA</strong> K<strong>WA</strong>NZA<br />

1.0 KANUNI ZA UFUGAJI BORA <strong>WA</strong> NG’OMBE<br />

Ng’ombe wanafugwa kwa ajili ya nyama na maziwa lakini pia hutoa mazao<br />

mengine kama ngozi, mbolea na hutumika kama wanyama kazi. Zaidi ya asilimia<br />

95 ya ng’ombe wanaofugwa hapa nchini ni wa asili ambao huzalisha nyama na<br />

maziwa kwa kiwango kidogo ikilinganishwa na wale wachache walioboreshwa.<br />

Ng’ombe walioboreshwa wamegawanyika katika makundi mawili, wale<br />

wanaofugwa kwa ajili ya nyama na lingine kwa ajili ya maziwa. Ili kuwawezesha<br />

ng’ombe kuzalisha mazao bora ya nyama, maziwa na ngozi mfugaji anapaswa<br />

kufuata kanuni za ufugaji bora ambazo ni pamoja na:-<br />

i) Kwa ng’ombe wanaofugwa kwa mfumo wa ufugaji huria ni muhimu<br />

ardhi hiyo itunzwe kwa kuzingatia uwiano wa idadi ya ng’ombe na<br />

malisho.<br />

ii) Kujenga banda au zizi bora<br />

iii) Kuchagua koo/aina ya ng’ombe kulingana na lengo la uzalishaji (nyama<br />

au maziwa).<br />

iv) Kutunza makundi mbalimbali ya ng’ombe kulingana na umri na hatua<br />

ya uzalishaji<br />

v) Kumpa ng’ombe lishe sahihi kulingana na umri na mahitaji ya mwili.<br />

vi) Kudhibiti magonjwa ya ng’ombe kama inavyoshauriwa na mtaalam wa<br />

mifugo.<br />

vii) Kuvuna mifugo katika umri na uzito muafaka kulingana na mahitaji ya<br />

soko.<br />

viii) Kuzalisha maziwa, nyama na ngozi zinazokidhi viwango vya ubora na<br />

usalama.<br />

ix) Kutunza kumbukumbu za uzalishaji na matukio muhimu ya ufugaji.<br />

1.1 Mifumo ya Ufugaji<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

1


Ng’ombe wanaweza kufugwa katika mfumo wa ufugaji huria au kulishwa katika<br />

banda (ufugaji shadidi). Ufugaji huria huhitaji eneo kubwa la ardhi yenye malisho<br />

mazuri na vyanzo vya maji. Pamoja na kuwa na ufugaji huu, ni muhimu ardhi hiyo<br />

itunzwe kwa kuzingatia uwiano wa idadi ya ng’ombe na malisho. Ufugaji wa<br />

shadidi uzingatie uwepo wa banda bora na lishe sahihi<br />

Ufugaji Katika Mfumo Huria<br />

Ili mfugaji aweze kupata mazao mengi na bora katika ufugaji huria anapaswa<br />

kuzingatia yafuatayo:-<br />

• Atenge eneo la kutosha la kufugia kulingana na idadi ya ng’ombe alionao,<br />

• Atunze malisho ili yawe endelevu na yapatikane wakati wote,<br />

• Awe na eneo lenye maji ya kutosha; na<br />

• Atenganishe madume na majike ili kuzuia ng’ombe kuzaa bila mpangilio.<br />

Matunzo mengine ya ng’ombe yazingatie vigezo vingine muhimu kama umri, hatua<br />

ya uzalishaji na matumizi ya ng’ombe husika.<br />

1.2 Banda/Zizi Bora la ng’ombe .<br />

1.2.1 Banda Bora<br />

Banda lijengwe sehemu ya mwinuko mbali kidogo na makazi ya watu na liwe na<br />

sifa zifuatazo:-<br />

• Uwezo wa kumkinga ng’ombe dhidi ya mvua, upepo, jua kali na baridi,<br />

• Kuta imara zenye matundu au madirisha kwa ajili ya kuingiza hewa na<br />

mwanga wa kutosha,<br />

• Sakafu yenye mwinuko upande mmoja ili isiruhusu maji na uchafu<br />

kutuama,<br />

• Lijengwe katika hali ya kuruhusu kufanyiwa usafi kwa urahisi kila siku, na<br />

sakafu ngumu ya zege au udongo ulioshindiliwa na kuwekwa malalo,<br />

• Paa lisilovuja na,<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

2


• Liwe na sehemu za kulala ng’ombe wa makundi mbali mbali, sehemu ya<br />

kukamulia (kwa ng’ombe wa maziwa), stoo ya vyakula, sehemu ya kutolea<br />

huduma za kinga na tiba, eneo la kulishia na la maji ya kunywa.<br />

1.2.2 Zizi bora<br />

Zizi lijengwe sehemu ya mwinuko isiyoruhusu maji kutuama, mbali kidogo na<br />

makazi ya watu na liwe na sifa zifuatazo:-<br />

• Liweze kuhakikisha usalama wa ng’ombe,<br />

• Ukubwa wa zizi uzingatie idadi ya mifugo,<br />

• Liwe na sakafu ya udongo ulioshindiliwa vizuri na kufanyiwa usafi mara kwa<br />

mara;<br />

• Zizi la ndama liwe na paa; na<br />

• Lijengwe kwa vifaa madhubuti na visivyoharibu ngozi<br />

1.3 Uchaguzi wa koo na aina ya ng’ombe wa kufuga<br />

Kwa ufugaji wenye tija, mfugaji anashauriwa kuchagua koo na aina ya ng’ombe<br />

kwa kuzingatia malengo ya ufugaji (nyama au maziwa).<br />

1.3.1 Ng’ombe wa nyama<br />

Ng’ombe wanaofaa kufugwa kwa ajili ya uzalishaji nyama ni wale wanaokua kwa<br />

haraka na kuweka misuli mikubwa iliyojengeka vizuri. Baadhi ya koo zenye sifa<br />

hizo ni pamoja na Boran, Mpwapwa (nyama na maziwa), Charlolais, Aberdeen<br />

Angus, pamoja na chotara wao. Hata hivyo, nchini Tanzania ng’ombe aina ya Zebu<br />

(mfano Ufipa, Gogo, Masai, Sukuma, Tarime, Iringa red), Sanga (Ankole) na<br />

chotara wao ndio hutumika kama ng’ombe wa nyama.<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

3


1.3.2 Ng’ombe wa maziwa<br />

Sifa za ng’ombe wa maziwa ni zifuatazo:-<br />

Ng’ombe wa nyama aina ya Boran<br />

• Umbo lililopanuka kwa nyuma na kupungua kuelekea kichwani<br />

• Mgongo ulionyooka kuanzia mabegani kuelekea mkiani<br />

• Miguu mirefu iliyonyooka, minene yenye kuacha nafasi kwa ajili ya kiwele<br />

na kwato imara<br />

• Kiwele kiwe kikubwa chenye chuchu nne, ndefu, na unene wa wastani<br />

• Nafasi kati ya chuchu na chuchu iwe ya kutosha<br />

• Endapo ng’ombe anakamuliwa awe na kiwele kikubwa kilichoshikamana<br />

vizuri mwilini, na mishipa mikubwa kwenye kiwele iliyosambaa<br />

Aina ya ng’ombe wa maziwa wanaofugwa kwa wingi nchini ni pamoja na Friesian,<br />

Ayrshire, Jersey, Mpwapwa, Simmental na chotara watokanao na mchanganyiko<br />

wa aina hizo na Zebu.<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

4


Ng’ombe wa maziwa aina ya ‘Friesian’<br />

1.4 Utunzaji wa Makundi Mbalimbali ya Ng’ombe wa Maziwa<br />

Kulingana na Umri na Hatua ya Uzalishaji<br />

1.4.1 Utunzaji wa Ndama.<br />

Mfugaji anapaswa kutunza ndama vizuri kwa lengo la kupata ng’ombe wengi na<br />

bora kwa ajili ya maziwa. Mambo muhimu ya kuzingatia katika utunzaji wa ndama<br />

tangu kuzaliwa hadi kuachishwa maziwa ni pamoja na:<br />

• Kuhakikisha kuwa ndama anapakwa dawa ya kuzuia maambukizi ya viini<br />

vya magonjwa kupitia kwenye kitovu, kwa mfano dawajoto (Tincture of<br />

Iodine) mara baada ya kuzaliwa.<br />

• Ndama apatiwe maziwa ya awali yaani dang’a (colostrum) mara baada ya<br />

kuzaliwa kwa lengo la kupata kinga ya mwili dhidi ya magonjwa. Aidha,<br />

aendelee kunyonya maziwa hayo kwa muda wa siku 3-4;<br />

• Endapo jike aliyezaa amekufa au hatoi maziwa, apewe dang’a toka kwa<br />

ng’ombe mwingine kama yupo au dang’a mbadala, ambayo inaweza<br />

kutengenezwa kwa kuchanganya vitu vifuatavyo:<br />

� Lita moja ya maziwa yaliyokamuliwa wakati huo huo,<br />

� Lita moja ya maji yaliyochemshwa na kupozwa hadi kufikia joto la<br />

mwili,<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

5


� Kijiko kimoja cha chai cha mafuta ya samaki (cod liver oil),<br />

� Mafuta ya nyonyo vijiko vya chai 3, na<br />

� Yai moja bichi.<br />

Koroga mchanganyiko huo, weka katika chupa safi na ndama anyweshwe kabla<br />

haujapoa. Ndama anyweshwe mchanganyiko huo mara 2 kwa siku kwa muda wa<br />

siku 3 mfululizo na kila mara mchanganyiko uwe mpya. Wakati wa kunyweshwa,<br />

chupa iwekwe juu ya ulimi na kichwa cha ndama kiinuliwe juu kidogo ili asipaliwe;<br />

• Endapo ndama hawezi kunyonya, ng’ombe akamuliwe na ndama apewe<br />

maziwa kwa njia ya chupa kwa kuzingatia usafi wa maziwa na chupa,<br />

• Ndama aendelee kupewa maziwa kwa kiasi kama ilivyoonyeshwa kwenye<br />

Jedwali Na. 1,<br />

• Ndama aanze kuzoeshwa kula nyasi laini, pumba kidogo na maji safi wakati<br />

wote kuanzia wiki ya 2 baada ya kuzaliwa; na<br />

• Ndama aachishwe kunyonya au kupewa maziwa akiwa na umri wa miezi 3.<br />

Mfugaji ahakikishe kwamba ndama anayeachishwa kunyonya ana afya<br />

nzuri.<br />

Jedwali Na. 1: Kiasi cha Maziwa na Chakula Maalum kwa Ndama<br />

Umri (Wiki) Kiasi cha Maziwa kwa Kiasi cha chakula Maalum cha<br />

siku (lita)<br />

ndama kwa siku (kilo)<br />

1. 3.0 0.0<br />

2. 3.5 0.0<br />

3. 4.0 0.0<br />

4. 4.5 0.0<br />

5. 5.0 0.1<br />

6. 5.0 0.2<br />

7. 5.0 0.3<br />

8. 4.0 0.4<br />

9. 3.0 0.7<br />

10. 2.0 1.0<br />

11. 1.5 1.25<br />

12-16 0.75 1.5<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

6


Vyombo vinavyotumika kulishia ndama visafishwe vizuri kwa maji<br />

yaliyochemshwa, sabuni na kukaushwa.<br />

Matunzo mengine ya ndama ni pamoja na:-<br />

• Kuondoa pembe kati ya siku 3 hadi 14 mara zinapojitokeza ili kuzuia<br />

wanyama kuumizana na kuharibu ngozi,<br />

• Kukata chuchu za ziada kwa ndama jike,<br />

• Kuhasi ndama dume wasiozidi umri wa miezi 3 ambao hawatahitajika kwa<br />

ajili ya kuendeleza kizazi ili wakue haraka na kuwa na nyama nzuri,<br />

• Kuweka alama au namba za utambilisho kati ya siku ya kwanza na ya tano,<br />

mfano kuvalishwa hereni kwenye masikio, kwa ajili ya urahisi wa udhibiti<br />

wa umiliki na utunzaji kumbukumbu; na<br />

• Kuwapatia kinga dhidi ya maambukizi na tiba ya magonjwa wanapougua.<br />

Huduma hizi zifanyike chini ya maelekezo ya mtaalam wa mifugo.<br />

Utunzaji wa ndama baada ya kuachishwa maziwa hadi kupevuka (Miezi<br />

3 – 18)<br />

• Ndama baada ya kuachishwa maziwa apate malisho bora na chakula<br />

mchanganyiko kuanzia kilo 2 - 4 kwa siku kutegemea umri wake,<br />

• Ndama wanapofikia umri wa miezi 18, wachaguliwe wanaofaa kuendeleza<br />

kizazi, wasio na sifa nzuri waondolewe katika kundi.<br />

1.4.2 Utunzaji wa Mtamba<br />

Mtamba ni ng’ombe jike aliyefikisha umri wa kupandwa (wastani wa miezi 18)<br />

hadi anapozaa kwa mara ya kwanza. Ni muhimu kutunza vizuri mtamba ili<br />

kupata kundi bora la ng’ombe. Miezi 3 kabla ya kupandishwa mtamba<br />

apatiwe:-<br />

• Malisho bora,<br />

• Maji ya kutosha,<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

7


• Madini mchanganyiko; na<br />

• Chakula cha ziada kiasi cha kilo 2 – 3 kwa siku, ili kuchochea upevukaji<br />

na kuongeza uzito wa mwili.<br />

1.4.3 Utunzaji wa ng’ombe wakubwa<br />

Kundi la Mitamba<br />

Kundi hili linajumuisha ng’ombe wenye mimba, wanaokamuliwa na madume.<br />

Mfugaji anapaswa kutunza vizuri ng’ombe wake wakubwa kwa lengo la kumpatia<br />

mazao mengi na bora. Hili kundi kwa ujumla huhitaji malisho bora na maji safi ya<br />

kutosha kila siku. Mambo muhimu ya kuzingatia katika utunzaji wa ng’ombe<br />

wakubwa ni pamoja na:<br />

• Ng’ombe apatiwe majani makavu (hei) wastani wa kilo 10 au majani mabichi<br />

kilo 40 kwa siku kutegemeana na uzito. Iwapo malisho hayatoshi hususan<br />

wakati wa kiangazi, apewe masalia ya mazao (viwandani na mashambani)<br />

kama molasisi, mabua, maharage, mpunga n.k,<br />

• Ng’ombe apewe vyakula vya ziada (pumba, mashudu, madini mchanganyiko,<br />

unga wa mifupa na chokaa) kulingana na hatua na kiwango cha uzalishaji; na<br />

• Ng’ombe apatiwe kinga na tiba ya magonjwa kulingana na ushauri wa<br />

mtaalam wa mifugo.<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

8


Upandishaji<br />

Mfugaji anapaswa kumpandisha ng’ombe kwa umri na wakati muafaka ili kuepuka<br />

matatizo ya uzazi na pia kuhakikisha anapata ndama bora na maziwa mengi.<br />

Mambo muhimu ya kuzingatia ni pamoja na:<br />

• Mtamba apandishwe akiwa na umri wa miezi 17 -24 na uzito wa kilo 230 -<br />

300 kwa ng’ombe wa kigeni na umri wa miezi 30 – 36 na uzito wa kilo 200<br />

kwa ng’ombe wa asili. (Rejea Jedwali Na 2),<br />

• Ng’ombe aliyekwishazaa apandishwe siku 60 baada ya kuzaa; na<br />

• Siku 18 - 23 baada ya kupandishwa, ng’ombe achunguzwe kama ana dalili<br />

za joto ili apandishwe tena. Iwapo ng’ombe ataendelea kuonyesha dalili za<br />

joto baada ya kupandishwa mara tatu mfugaji apate ushauri wa mtaalam<br />

wa mifugo.<br />

Jedwali Na.2: Umri na Uzito wa Kupandisha Mtamba<br />

Aina ya Ng’ombe Uzito (Kg) Umri (Miezi)<br />

Friesian 240- 300 18 - 24<br />

Ayrshire 230 – 300 17 - 24<br />

Jersey 200 – 250 18 - 20<br />

Mpwapwa 200 – 250 18 - 20<br />

Chotara 230 - 280 18 – 24<br />

Boran 200 - 250 24 - 36<br />

Zebu 200 30 - 36<br />

Dalili za Ng’ombe Anayehitaji Kupandwa<br />

Ni muhimu mfugaji akazitambua dalili za ng’ombe anayehitaji kupandwa ili aweze<br />

kumpandisha kwa wakati. Dalili hizo ni pamoja na:-<br />

• Kupiga kelele mara kwa mara,<br />

• Kutotulia/kuhangaika,<br />

• Kutokwa na ute mweupe usiokatika ukeni,<br />

• Kupenda kupanda wenzake na husimama akipandwa na wenzake; na<br />

• Kunusanusa ng’ombe wengine<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

9


Ng’ombe akionyesha dalili za joto apandishwe baada ya masaa 12, kwa<br />

kuhimilisha au kwa kutumia dume bora (kwa mfano, akionyesha dalili asubuhi<br />

apandishwe jioni na akionyesha dalili jioni apandishwe asubuhi).<br />

Uhimilishaji<br />

Uhimilishaji ni njia ya kupandikiza mbegu kwa ng’ombe jike kwa kutumia mrija.<br />

Faida za uhimilishaji ni pamoja na kusambaza mbegu bora kwa haraka na kwa<br />

gharama nafuu, kupunguza gharama za kutunza dume na kudhibiti magonjwa ya<br />

uzazi.<br />

Ili mfugaji anufaike na huduma hii anapaswa kufanya yafuatayo:-<br />

• Kuchunguza kwa makini ng’ombe mwenye dalili za joto,<br />

• Kumjulisha mtaalamu wa uhimilishaji mapema ili kuwezesha zoezi hili<br />

kufanyika kwa wakati,<br />

• Kuchunguza kama ng’ombe atarudi kwenye joto siku ya 18- 23 baada ya<br />

kupandishwa; na<br />

• Ng’ombe aliyepandishwa apimwe mimba siku 60 hadi 90 baada ya<br />

kupandishwa.<br />

1.4.4 Matunzo ya Ng’ombe Mwenye Mimba<br />

Ng’ombe mwenye mimba huchukua miezi 9 hadi kuzaa. Katika kipindi hicho chote<br />

anastahili kupatiwa lishe bora na maji ya kutosha ili akidhi mahitaji ya ndama aliye<br />

tumboni na kutoa maziwa mengi baada ya kuzaa.<br />

Mambo ya kuzingatia ni pamoja na:<br />

• Ng’ombe apewe lishe bora na maji ya kutosha kipindi chote cha mimba,<br />

• Miezi 2 kabla ya kuzaa apewe kilo 2 za chakula cha ziada kwa siku,<br />

• Apewe kinga dhidi ya maambukizi na tiba ya magonjwa,<br />

• Ng’ombe anayekamuliwa aachishwe siku 60 kabla ya kuzaa; na<br />

• Ng’ombe anayekaribia kuzaa, hususan mtamba, azoeshwe kuingia kwenye<br />

sehemu ya kukamulia.<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

10


Dalili za Ng’ombe Anayekaribia Kuzaa<br />

Mfugaji anapaswa kufahamu dalili za ng’ombe anayekaribia kuzaa ili aweze<br />

kufanya maandalizi muhimu. Dalili hizo ni pamoja na:<br />

• Kujitenga kutoka kwa wenzake,<br />

• Kiwele kuongezeka ukubwa,<br />

• Chuchu kutoa maziwa zikikamuliwa,<br />

• Kutokwa na ute mwekundu na sehemu za uke kuvimba na kulegea,<br />

• Kuhangaika, kulala chini na kusimama; na<br />

• Kati ya saa moja hadi mbili kabla ya kuzaa sehemu ya uke hutokwa na maji<br />

mengi ambayo husaidia kulainisha njia ya ndama kupita.<br />

Huduma kwa Ng’ombe Anayezaa<br />

Ng’ombe anayezaa anahitaji uangalizi wa karibu ili kuhakikisha usalama wa<br />

ng’ombe na ndama anaezaliwa. Mambo ya kuzingatia ni pamoja na yafuatayo:<br />

• Sehemu ya kuzalia ng’ombe iandaliwe kwa kuwekwa nyasi kavu na laini na<br />

iwe safi,<br />

• Ng’ombe ahamishiwe sehemu iliyoandaliwa kwa ajili ya kuzaa mara baada<br />

ya dalili za kuzaa kuonekana; na<br />

• Ng’ombe aachwe azae mwenyewe bila usumbufu.<br />

Mfugaji apate ushauri/huduma kutoka kwa mtaalam iwapo matatizo yafuatayo<br />

yatajitokeza:-<br />

• Ng’ombe kushindwa kuzaa kwa masaa mawili hadi matatu baada ya<br />

chupa kupasuka,<br />

• Kondo la nyuma kushindwa kutoka masaa sita baada ya kuzaa<br />

• Kizazi kutoka nje; na<br />

• Ng’ombe kushindwa kusimama baada ya kuzaa.<br />

1.4.5 Matunzo ya Ng’ombe Anayekamuliwa<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

11


Ng’ombe anayekamuliwa anahitaji kupata chakula kwa ajili ya kujikimu na cha<br />

ziada kwa ajili ya uzalishaji wa maziwa. Ili kukidhi mahitaji ya uzalishaji wa<br />

maziwa ng’ombe:<br />

• Apewe chakula cha ziada kwa kiwango cha kilo 1 kwa kila lita 2-3 za<br />

maziwa anayotoa,<br />

• Apewe madini na virutubisho vingine kulingana na mahitaji,<br />

• Apewe maji mengi kwa vile ni ya muhimu katika kutengeneza maziwa,<br />

• Aachwe kukamuliwa siku 60 kabla ya kuzaa. Uachishwaji huu ufanywe<br />

taratibu ili ifikapo siku ya 60 kabla ya kuzaa ukamuaji usitishwe,<br />

• Baada ya kusitisha kukamuliwa, apewe kilo 2 za chakula cha ziada kwa siku<br />

hadi atakapozaa; na<br />

• Apatiwe kinga dhidi ya maambukizi ya magonjwa na tiba ya magonjwa<br />

kulingana na ushauri wa mtaalam wa mifugo.<br />

Uzalishaji wa maziwa<br />

Lengo la ufugaji wa ng’ombe wa maziwa ni kupata maziwa mengi, safi na salama<br />

pamoja na mazao yatokanayo na maziwa. Mambo muhimu ya kuzingatia ni:-<br />

• Sehemu ya kukamulia iwe safi na yenye utulivu,<br />

• Ng’ombe awe na afya nzuri, msafi, na kiwele kioshwe kwa maji safi ya<br />

uvuguvugu,<br />

• Mkamuaji awe msafi, kucha fupi na asiwe na magonjwa ya kuambukiza,<br />

• Inashauriwa mkamuaji asibadilishwe badilishwe,<br />

• Vyombo vya kukamulia viwe safi,<br />

• Muda wa kukamua usibadilishwe; na<br />

• Maziwa ya mwanzo kutoka kila chuchu yakamuliwe kwenye chombo<br />

maalum (strip cup) ili kuchunguza ugonjwa wa kiwele.<br />

1.5 Uchaguzi na Utunzaji wa Dume Bora la Mbegu<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

12


Dume ndilo linalojenga ubora wa kundi la ng’ombe katika masuala ya uzalishaji<br />

kutokana na uwezo wake wa kupanda majike wengi. Kwa wastani dume moja<br />

linaweza kupanda majike 20-25 wakati wa msimu wa uzalianaji (breeding season).<br />

Ili kundi la ng’ombe liwe bora, mambo yafuatayo yazingatiwe:<br />

• Chagua dume kutoka kwenye ukoo ulio bora kwa kuzingatia kumbukumbu<br />

za uzalishaji wa maziwa au nyama za wazazi wake,<br />

• Mfugaji apate ushauri wa mtaalam wa mifugo katika kuchagua dume bora,<br />

• Lisha dume malisho bora na maji safi ya kutosha. Pia apatiwe chakula cha<br />

ziada,<br />

• Katika ufugaji shadidi, dume la ng’ombe lifugwe kwenye banda imara lenye<br />

sehemu za kuwekea chakula, maji na kufanyia mazoezi,<br />

• Katika ufugaji huria, dume atengewe sehemu na kupatiwa chakula cha<br />

ziada,<br />

• Dume livalishwe pete puani kwa ajili ya kupunguza ukali na kuwezesha<br />

urahisi wa kumshika,<br />

• Dume apatiwe kinga na tiba ya magonjwa kulingana na ushauri wa<br />

mtaalam wa mifugo; na<br />

• Mfugaji apate ushauri wa mtaalam wa mifugo katika kuchagua dume bora.<br />

1.6 Utunzaji wa Ng’ombe wa Nyama<br />

Ng’ombe wengi wanaofugwa hapa nchini Tanzania ni wa asili ambao kwa kiwango<br />

kikubwa hutumika kwa ajili ya uzalishaji wa nyama. Hata hivyo uzalishaji wake wa<br />

nyama ni mdogo kutokana na kasi ndogo ya kukua na kuwa na uzito mdogo<br />

wakati wanapopevuka. Hali hii husababishwa na matunzo duni, kwa kuwa<br />

huchungwa/hulishwa kwa kutegemea malisho peke yake ambayo hayawezi<br />

kukidhi mahitaji ya viinilishe vinavyohitajika kwa ng’ombe.<br />

Ili kuongeza kasi ya ukuaji na kuongeza uzalishaji wa nyama, mfugaji anapaswa<br />

kufanya mambo yafuatayo:-<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

13


Ndama:<br />

• Wajengewe banda/boma imara, safi na lisilo na unyevunyevu ilikuepukana<br />

na magojwa kama kichomi na kuhara,<br />

• Waruhusiwe kunyonya kwa muda usiopungua miezi sita, pia wapatiwe<br />

majani laini kuanzia wanapofikia umri wa wiki mbili ili waanze kula<br />

mapema,<br />

• Wapatiwe maji masafi na yakutosha,<br />

• Ndama dume ambao hawatahitajika kwa ajili ya kuendeleza kizazi<br />

wahasiwe wakiwa na umri usiozidi miezi 3 ili wakue haraka na kuwa na<br />

nyama nzuri,<br />

• Wawekwe alama au namba za utambulisho kati ya siku ya kwanza na ya<br />

tano kwa ndama wote, mfano kuvalishwa hereni kwenye masikio, kwa ajili<br />

ya urahisi wa udhibiti wa umiliki na utunzaji kumbukumbu,<br />

• Ndama wachungwe eneo tofauti na ng’ombe wakubwa kuepuka<br />

maambukizi ya minyoo na magonjwa; na<br />

• Wapatiwe kinga dhidi ya maambukizi ya magonjwa na tiba wanapougua.<br />

Utunzaji wa ndama baada ya kuachishwa kunyonya hadi kupevuka<br />

(miezi 6 –24)<br />

Ndama wa umri huu anatakiwa apatiwe:<br />

• Malisho bora na maji safi ya kutosha wakati wote,<br />

• Vyakula vya ziada ili kukidhi mahitaji ya mwili (mifano ya vyakula<br />

mchanganyiko imeonyeshwa kwenye Jedwali Na. 3); na<br />

• Tiba na kinga dhidi ya magonjwa, hususan kinga ya kutupa mimba (S19)<br />

kwa ndama jike watakaotumika kuendeleza kundi.<br />

Katika kipindi cha miezi 6 hadi 24, mfugaji anashauriwa kuchagua ndama<br />

watakaoingizwa katika kundi la wazazi na wanaobaki wawe katika kundi la<br />

kunenepesha kwa ajili ya nyama.<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

14


Ng’ombe wa nyama mzazi<br />

Apatiwe:-<br />

• Malisho bora na maji safi ya kutosha wakati wote,<br />

• Vyakula vya ziada (mifano ya vyakula mchanganyiko iliyooneshwa kwenye<br />

Jedwali Na. 3), ili kukidhi mahitaji ya mwili,<br />

• Vyakula vya ziada kiasi kisichopungua kilo 2 kila siku miezi 2 kabla ya<br />

kuzaa,<br />

• Nafasi ya kunyonyesha ndama kwa miezi 6 mfululizo,<br />

• Tiba na kinga dhidi ya magonjwa; na<br />

• Apandishwe kwa kutumia dume bora au kwa kutumia njia ya uhimilishaji<br />

siku 60 baada ya kuzaa.<br />

Unenepeshaji wa Ng’ombe wa nyama<br />

Ng’ombe kwa ajili ya nyama anaweza kuchinjwa akiwa na umri wa kuanzia miezi 3<br />

kulingana na mahitaji ya soko. Kwa kawaida hapa Tanzania ng’ombe huchinjwa<br />

wakiwa na umri wa kuanzia miezi 18 kwa ng’ombe wa kigeni na zaidi ya miezi 36<br />

kwa ng’ombe wa asili.<br />

Ili mfugaji aweze kupata faida kutokana na ufugaji wa ng’ombe wa nyama<br />

anapaswa afanye yafuatayo:-<br />

• Afuge aina ya ng’ombe wanaokua na kukomaa haraka,<br />

• Anenepeshe ng’ombe kwa muda wa miezi 3 - 6 kabla ya kuchinjwa.<br />

unenepeshaji huongeza ubora wa nyama na kipato kwa mfugaji,<br />

• Awapatie chakula chenye mchanganyiko wenye viinilishe vya kutosha<br />

viinilishe vya kutia nguvu na joto mwilini viwe na uwiano mkubwa kuliko<br />

vingine (Jedwali Na 3),<br />

• Auze ng’ombe mara wanapofikisha umri na uzito unaohitajika katika<br />

soko ili kuepuka gharama za ziada.<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

15


Jedwali Na. 3. Mfano wa Mchanganyiko wa Chakula kwa Ajili ya<br />

Unenepeshaji<br />

Aina ya Chakula Kiasi kwa Kilo<br />

Majani makavu ya Mpunga/NganoHey 23.3<br />

Molasis 44.72<br />

Mahindi yaliyoparazwa 18.94<br />

Mashudu ya Alizeti/Pamba 11.4<br />

Madini mchanganyiko 0.7<br />

Chumvi 0.47<br />

Urea 0.47<br />

Jumla 100<br />

1.7 Uzalishaji na Uhifadhi wa Malisho Bora na Vyakula vya Ziada:<br />

Chakula kikuu cha ng’ombe ni nyasi. Vyakula vingine ni pamoja na miti malisho,<br />

mikunde na mabaki ya mazao. Ili kupata malisho misimu yote ya mwaka ni<br />

muhimu kuvuna na kuhifadhi malisho kipindi yanapopatikana kwa wingi.<br />

Inawezekana kupanda malisho mengi kuliko kiasi kinachohitajika msimu<br />

mmoja/wakati wa mvua, kuyavuna yanapofikia hatua ya kutoa maua na<br />

kuyahifadhi (mfano wa malisho yanayoweza kupandwa ni mabingobingo,<br />

guatemala, African fox-tail, desmodium, centrosema, lukina n.k). Malisho ya<br />

kupandwa ni vizuri yawe na mchanganyiko wa jamii ya nyasi, mikunde na miti<br />

malisho.<br />

Masalia ya Mazao Shambani<br />

Masalia ya mazao shambani kama vile mabua, magunzi, majani ya mikunde, viazi,<br />

ndizi, mpunga, na mengineyo yanaweza kukusanywa na kuhifadhiwa vizuri kama<br />

chakula cha ng’ombe.<br />

Malisho ya Miti na Matunda Yake<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

16


Malisho yatokanayo na miti ya malisho na matunda yake yanaweza kutumika<br />

kama malisho ya ng’ombe. Majani na matunda ya miti ya lukina, sesibania,<br />

migunga na mbaazi yanaweza kukaushwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya kulisha<br />

ng’ombe.<br />

1.7.1 Vyakula vya Ziada<br />

Ili kukidhi mahitaji ya viinilishe kulingana na kiwango cha uzalishaji, ng’ombe<br />

anatakiwa kupewa vyakula vya ziada. Vyakula hivyo vinatokana na mchanganyiko<br />

wa vyakula mbalimbali. Michanganyiko hii inategemeana na upatikanaji wa<br />

malighafi katika maeneo husika. Mifano ya mchanganyiko huo ni kama ifuatavyo:-<br />

Jedwali Na. 4: Mfano wa Kwanza wa Chakula cha Ziada<br />

Aina ya chakula Kiasi (kilo)<br />

Pumba za mahindi 47<br />

Mahindi yaliyoparazwa 20<br />

Mashudu ya alizeti/pamba 20<br />

Unga wa lukinaa 10<br />

Chokaa ya mifugo 2<br />

Chumvi 1<br />

Jumla 100<br />

Mfano wa pili wa chakula cha ziada ni tofali la kulamba lenye urea ambalo<br />

mchanganyiko wake ni:-<br />

Unga wa mahindi Kilo 1<br />

Pumba za mahindi Kilo 3<br />

Urea kilo 1<br />

Mashudu ya alizeti kilo 2<br />

Chumvi ya kawaida gramu 200<br />

Unga wa mifupa gramu 200<br />

Chokaa ya mifugo kilo 1.5<br />

Saruji kilo 1<br />

Mfugaji anatakiwa kuzingatia yafuatayo ili kupata tija katika ufugaji bora:-<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

17


• Kulisha mchanganyiko wa nyasi, mikunde na mchanganyiko wa madini na<br />

vitamini,<br />

• Kutenga maeneo kwa ajili ya kulisha ng’ombe kwa mzunguko pamoja na<br />

kupanda malisho katika mfumo huria na nusu huria; na<br />

• Kuvuna nyasi na mikunde inapofikia hatua ya kutoa maua na kuyahifadhi<br />

kwa matumizi wakati wa uhaba wa malisho, hususan wakati wa kiangazi.<br />

1.7.2 Njia za Kuhifadhi Malisho<br />

Malisho yanaweza kuhifadhiwa kwa kuyakausha (Hei) au kuyavundika (Saileji).<br />

Hei<br />

Hei ni majani yaliyohifadhiwa kwa kukaushwa baada ya kukatwa au kuachwa<br />

kukauka yakiwa shambani kwa matumizi ya baadaye. Katika kutengeneza hei<br />

yafuatayo yazingatiwe:<br />

Sileji<br />

• Vuna malisho yanapoanza kutoa maua,<br />

• Yaanikwe kwa siku 3 hadi 6 kutegemea aina ya malisho na hali ya<br />

hewa na yageuze mara 1 au 2 kwa siku ili yakauke vizuri,<br />

• Yafungwe katika marobota baada ya kukauka – inawezekana<br />

kutumia kasha la mbao lenye vipimo vifuatavyo:- Urefu sentimeta<br />

75, upana sentimeta 45, na kina sentimeta 35 au mashine na zana<br />

za kufunga marobota ya hei; na<br />

• Hifadhi marobota juu ya kichanja ili kuzuia maji yasiingie, unyevu na<br />

kuharibiwa na wadudu.<br />

Sileji ni majani yaliyokatwakatwa na kuvundikwa. Madhumuni ya kuyavundika ni<br />

kuyawezesha kubaki na ubora wake hadi wakati yatakapotumika. Katika<br />

kutengeneza sileji yafuatayo yazingatiwe:-<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

18


• Tengeneza sileji kwa kutumia majani yenye sukari nyingi kama<br />

mahindi au mabingobingo na mikunde , mabaki ya viwandani kama<br />

molasis,<br />

• Andaa shimo au mfuko wa plastiki kulingana na kiasi cha majani<br />

yaliyovunwa,<br />

• Vuna majani ya kuvundika katika umri wa kuanza kutoa maua.<br />

Endapo majani yaliyovunwa ni teketeke, yaachwe kwa siku moja<br />

yanyauke kupunguza kiwango cha maji,<br />

• Katakata majani uliyovuna katika vipande vidogovidogo,<br />

• Tandaza majani uliyokatakata ndani ya shimo au mfuko katika<br />

tabaka nyembamba na kushindilia ili kuondoa hewa yote,<br />

• Funika shimo ulilojaza majani kwa plastiki ikifuatiwa na udongo,<br />

• Sileji itakuwa tayari kutumika kuanzia siku 21; na<br />

• Sileji iliyofunguliwa kwa ajili ya matumizi ifunikwe haraka<br />

iwezekanavyo ili kuzuia kuharibika.<br />

Sileji inaweza kubaki na ubora katika shimo kwa muda mrefu kama haitafunguliwa<br />

na kuachwa wazi kwa muda mrefu.<br />

1.8 Udhibiti wa magonjwa ya ng’ombe<br />

Magonjwa huweza kusababishwa na matunzo hafifu, lishe duni na visababishi vya<br />

magonjwa kama vile protozoa, bakteria, virusi, riketsia na minyoo. Aidha, wadudu<br />

kama kupe na mbung’o wanasambaza visababishi vya magonjwa.<br />

Afya bora ya ng’ombe inatokana na kuzingatia mambo yafuatayo:-<br />

• Ndama apate maziwa ya awali (dang’a) ya kutosha kwa siku 3-4 baada ya<br />

kuzaliwa ili kuongeza kinga ya magonjwa mwilini,<br />

• Chovya kitovu cha ndama ndani ya madini joto (Tincture of Iodine) mara<br />

baada ya kuzaliwa kuzuia kuvimba kitovu. Ugonjwa huu huwapata ndama<br />

kutokana na kitovu kutokauka au kutohudumiwa ipasavyo mara baada ya<br />

ndama kuzaliwa. Kitovu huvimba na kutoa usaha, hukojoa kwa shida na<br />

wakati mwingine huvimba viungo,<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

19


• Ndama apewe dawa ya kuzuia minyoo kila baada ya miezi 3 kama<br />

atakavyoshauri mtaalam wa mifugo. Minyoo huwashambulia ndama zaidi<br />

hasa wale walioanza kula majani,<br />

• Zingatia usafi wa vyombo na banda, epuka kumpa ndama maziwa<br />

yaliyopoa na machafu ili kuzuia kuharisha,<br />

• Zingatia ujenzi wa mabanda kuruhusu mzunguko wa hewa ili kuzuia ndama<br />

kupata ugonjwa wa vichomi. Vichomi huwapata ndama wa umri wa miezi 5<br />

au zaidi wanaofugwa ndani katika mabanda machafu yasiyo na mzunguko<br />

wa hewa ya kutosha,<br />

• Ogesha ng’ombe kulingana na ushauri wa mtaalam wa mifugo ili kuua kupe<br />

wote wanaoleta magonjwa yatokanayo na kupe (ndigana kali na baridi,<br />

kukojoa damu na maji moyo) na mbung’o (ndorobo); na<br />

• Ng’ombe wapatiwe chanjo dhidi ya magonjwa mbalimbali. Chanjo muhimu<br />

ni za ugonjwa wa kutupa mimba, kimeta, ugonjwa wa miguu na midomo na<br />

chambavu.<br />

Mfugaji anashauriwa kutoa taarifa kwa mtaalamu wa mifugo anapoona<br />

ng’ombe wake ana baadhi ya dalili zifuatazo:-<br />

• Joto kali la mwili na manyoya kusimama,<br />

• amepunguza hamu ya kula,<br />

• amezubaa na kutoa machozi,<br />

• anasimama kwa shida na kusinzia,<br />

• anapumua kwa shida na pua kukauka,<br />

• anatokwa na kamasi nyingi,<br />

• anajitenga na kundi,<br />

• anakonda,<br />

• Anapunguza utoaji wa maziwa ghafla.<br />

1. 9 Kumbukumbu na Takwimu Muhimu<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

20


Kumbukumbu ni taarifa au maelezo sahihi yaliyoandikwa kuhusu matukio muhimu<br />

ya kila ng’ombe na shughuli zote zinazohusiana na ufugaji. Mfugaji anashauriwa<br />

kuweka kumbukumbu na takwimu muhimu katika shughuli zake za ufugaji wa<br />

ng’ombe. Kumbukumbu zinamsaidia mfugaji kujua mapato na matumizi na<br />

kufanya maamuzi sahihi kuhusu mifugo husika na mazao yake. Aidha,<br />

humwezesha kuweka mipango ya shughuli zake. Mfugaji anapaswa kuweka<br />

kumbukumbu muhimu zifuatazo:-<br />

• Uzazi (uhimilishaji na matumizi ya dume, tarehe ya kupandwa, kuzaa,<br />

kuachisha kunyonya)<br />

• kinga na tiba<br />

• utoaji wa maziwa<br />

• Ukuaji<br />

• Idadi ya ng’ombe kwa makundi – majike, ndama, mitamba, madume,<br />

maksai.<br />

• Kiasi na aina ya chakula<br />

• Mapato na matumizi<br />

• Kumbukumbu za manunuzi ya vifaa<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

21


SURA <strong>YA</strong> PILI<br />

2. 0 KANUNI ZA UFUGAJI BORA <strong>WA</strong> MBUZI NA KONDOO<br />

Mbuzi na kondoo wanaweza kufugwa kwa gharama nafuu na kuishi katika<br />

mazingira magumu kama ya maradhi na ukame ikilinganishwa na ng’ombe.<br />

Kutokana na umbile lao dogo wanaweza kufugwa katika eneo dogo na pia<br />

wanaweza kuhudumiwa na familia yenye nguvukazi na kipato kidogo. Uzao wa<br />

muda mfupi unamwezesha mfugaji kupata mbuzi/kondoo wengi kwa kipindi kifupi.<br />

Wanyama hao hufugwa kwa ajili ya nyama, maziwa, ngozi, sufu na mazao<br />

mengine kwa matumizi ya familia na kuongeza kipato. Ufugaji bora wa mbuzi na<br />

kondoo uzingatie kanuni zifuatazo:-<br />

i) Wafugwe kwenye banda au zizi bora,<br />

ii) Wachaguliwe kutokana na sifa za koo/aina na lengo la uzalishaji<br />

(nyama, maziwa au sufu),<br />

iii) Wapatiwe lishe sahihi kulingana na umri na mahitaji ya mwili,<br />

iv) Kuzingatia mbinu za kudhibiti magonjwa kama inavyoshauriwa na<br />

mtaalam wa mifugo,<br />

v) Kuweka na kutunza kumbukumbu sahihi za uzalishaji; na<br />

vi) Kuzalisha nyama, maziwa au sufu yenye ubora unaokidhi mahitaji ya<br />

soko<br />

Kondoo Mbuzi<br />

2.1 Zizi au Banda la Mbuzi/Kondoo<br />

Mbuzi/kondoo wanaweza kufugwa katika mifumo ya huria, shadidi na kwa<br />

kutumia njia zote mbili. Zizi hutumika katika mfumo huria ambapo mbuzi/kondoo<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na 22<br />

kujiongezea kipato


huchungwa wakati wa mchana na kurejeshwa zizini wakati wa usiku. Zizi bora ni<br />

lile lenye sifa zifuatazo:-<br />

• Lililo imara linaloweza kumkinga mbuzi/kondoo dhidi ya wanyama hatari na<br />

wezi,<br />

• Lililojengwa mahali pa mwinuko pasiporuhusu maji kutuama,<br />

• Ukubwa wa zizi uzingatie idadi na umri wa mifugo. Ni vema mbuzi/kondoo<br />

watengwe kulingana na umri wao; na<br />

• Liruhusu usafi kufanyika kwa urahisi.<br />

Pale ambapo mbuzi/kondoo wanafugwa kwa mfumo wa shadidi hufugwa katika<br />

banda wakati wote. Banda bora la mbuzi/kondoo linatakiwa kuwa na sifa<br />

zifuatazo:-<br />

• Imara, lenye uwezo wa kuwahifadhi kiafya na pia dhidi ya hali ya hewa<br />

hatarishi kwa mfano jua kali, upepo, baridi na mvua pamoja na wanyama<br />

hatari,<br />

• Lenye mwanga, hewa na nafasi ya kutosha inayoruhusu usafi kufanyika<br />

kwa urahisi,<br />

• Lijengwe sehemu isiyoruhusu maji kutuama na liwe mbali kidogo na<br />

nyumba ya kuishi watu. Pia ujenzi uzingatie mwelekeo wa upepo ili hewa<br />

kutoka bandani isiende kwenye makazi,<br />

• Liwe na sakafu ya kichanja chenye urefu wa mita 1 kutoka ardhini (Kwa<br />

banda la mbuzi),<br />

• Liwe na sehemu ya kuwekea chakula, maji na mahali pa kuweka jiwe la<br />

chumvichumvi; na<br />

• Liwe na vyumba tofauti kwa ajili ya majike na vitoto, mbuzi/kondoo<br />

wanaokua, wanaonenepeshwa na wanaougua.<br />

2.1.1 Vifaa vya Kujengea na Vipimo vya Banda<br />

Inashauriwa banda la mbuzi/kondoo lijengwe kwa kutumia vifaa vinavyopatikana<br />

kwa urahisi katika eneo husika. Ukubwa wa banda utategemea idadi ya<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

23


mbuzi/kondoo wanaofugwa humo na ukubwa wa umbo kama inavyoonekana<br />

kwenye Jedwali Na. 5<br />

Jedwali Na 5: Eneo la mbuzi/kondoo linalotakiwa<br />

Kundi la Mbuzi/Kondoo Eneo kwa Mnyama Mmoja<br />

(Mita 2 )<br />

Vitoto 0.3<br />

Wasio na mimba 1.5<br />

Wenye mimba 1.9<br />

Dume 2.8<br />

• Paa lijengwe kwa kutumia vifaa kama miti, mbao, na kuezekwa kwa nyasi,<br />

makuti, majani ya migomba, mabati au hata vigae kwa kutegemea uwezo<br />

wa mfugaji,<br />

• Kuta zijengwe kwa kutumia mabanzi, mbao, nguzo, wavu wa waya, fito na<br />

matofali. Kuta ziwe imara zinazoruhusu hewa na mwanga wa kutosha.<br />

Mlango uwe na ukubwa wa sentimita 60 x 150,<br />

• Sakafu inaweza kuwa ya udongo au zege. Sakafu ya kichanja inaweza<br />

kujengwa kwa kutumia miti, fito, mianzi, mbao au mabanzi na iweze<br />

kuruhusu kinyesi na mkojo kupita. Chumba cha majike na vitoto kiwe na<br />

nafasi ya sentimita 1.25 kati ya papi na papi, fito na fito au mti hadi mti.<br />

Chumba cha mbuzi/kondoo wakubwa iwe sentimita 1.9 kati ya mbao na<br />

mbao.<br />

2.2 Uchaguzi wa Mbuzi/Kondoo wa Kufuga<br />

Madhumuni ya kuchagua mbuzi au kondoo wa kufuga ni kuboresha uzalishaji na<br />

kuendeleza kizazi bora. Kuna aina nyingi za mbuzi/kondoo wanaoweza kufugwa<br />

kulingana na mazingira na mahitaji ya mfugaji. Uchaguzi hufanyika kwa kuangalia<br />

umbile, uzalishaji na kumbukumbu za wazazi kama vile umbo kubwa, ukuaji wa<br />

haraka, uwezo wa kutunza vitoto na kutoa maziwa mengi.<br />

Mbuzi wanaofaa kwa ajili ya maziwa ni aina ya Saanen, Norwegian na Toggenburg<br />

pamoja na chotara wao.<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

24


Mbuzi wanaofaa kwa ajili ya nyama ni Boer na chotara wao, mbuzi wa asili kama<br />

vile Pare white, Newala na Ujiji. Mbuzi aina ya Malya (Blended) wanafaa kwa ajili<br />

ya nyama na maziwa.<br />

Aidha, kondoo aina ya Black Head Persian (BHP), Masai red, Suffolk na Hampshire<br />

wanafaa kufugwa kwa ajili ya nyama. Merino na Lincoln hufugwa kwa ajili ya sufu,<br />

wakati Corriedale na Romney hufugwa kwa ajili ya nyama na sufu. Hapa Tanzania<br />

kondoo wanaopatikana kwa wingi ni Black Head Persian, Masai Red Dopper na<br />

kondoo wengine wa asili.<br />

Mbuzi/kondoo jike wanaofaa kwa ajili ya kuzalisha maziwa na nyama wawe na sifa<br />

zifuatazo:-<br />

• Historia ya kukua upesi, kuzaa (ikiwezekana mapacha) na kutunza vitoto<br />

vizuri,<br />

• Umbo la mstatili linaloashiria utoaji wa nyama nyingi; na<br />

• Asiwe na ulemavu wa aina yoyote<br />

Sifa za Ziada kwa Mbuzi wa Maziwa<br />

• Awe na miguu ya nyuma iliyo imara na iliyonyooka na yenye nafasi kwa ajili<br />

ya kiwele; na<br />

• Awe na kiwele kikubwa na chuchu ndefu zilizokaa vizuri<br />

Sifa za Dume<br />

Dume bora awe na sifa zifuatazo:-<br />

• Miguu iliyonyooka, imara na yenye nguvu,<br />

• Asiwe na ulemavu wa aina yoyote,<br />

• Mwenye uwezo na nguvu ya kupanda; na<br />

• Mwenye kokwa mbili zilizo kaa vizuri na zinazolingana<br />

Angalizo: Dume lichaguliwe kwa makini kwa sababu “dume ni nusu ya<br />

kundi”.<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

25


2.3 Utunzaji wa Vitoto vya Mbuzi/Kondoo<br />

Utunzaji huanza mara tu baada ya kuzaliwa.<br />

Mfugaji ahakikishe:-<br />

• Kitoto cha mbuzi/kondoo kinapata maziwa ya mwanzo (dang’a) ndani ya<br />

masaa 24 tangu kuzaliwa na kwa muda wa siku 3,<br />

• Kama kinanyweshwa maziwa, kipewe lita 0.7- 0.9 kwa siku. Maziwa haya, ni<br />

muhimu kwani yana viinilishe na kinga dhidi ya magonjwa,<br />

• Iwapo mama hatoi maziwa au amekufa, inashauriwa kutengeneza dang’a<br />

mbadala au kama kuna mbuzi/kondoo mwingine aliyezaa anaweza kusaidia<br />

kukinyonyesha kitoto hicho,<br />

• Kitoto cha mbuzi/kondoo kiendelee kunyonya kwa wiki 12 - 16. Wiki 2 baada<br />

ya kuzaliwa, pamoja na maziwa, kianze kupewa vyakula vingine kama nyasi<br />

laini na chakula cha ziada ili kusaidia kukua kwa tumbo. Aidha, kipewe maji<br />

wakati wote,<br />

• Vyombo vinavyotumika kulishia vinakuwa safi muda wote,<br />

• Kitoto cha mbuzi/kondoo kiachishwe kunyonya kikiwa na umri wa miezi 3 hadi<br />

4 kutegemea afya yake; na<br />

• Vitoto vipatiwe kinga na tiba ya magonjwa kulingana na ushauri wa mtaalam<br />

wa mifugo.<br />

2.3.1 Matunzo Mengine<br />

Utambuzi<br />

Mbuzi huwekewa alama ili atambulike kwa urahisi na kuwezesha utunzaji wa<br />

kumbukumbu zake. Shughuli hii hufanyika kwa mbuzi/kondoo akiwa na umri wa<br />

siku 3 - 14. Njia zitumikazo ni pamoja na:<br />

• Kuweka alama sikioni kwa kukata sehemu ndogo ya sikio,<br />

• Kumpa jina kwa wafugaji wenye mbuzi wachache,<br />

• Kumvisha hereni ya chuma au plastiki yenye namba kwenye sikio,<br />

• Kumvalisha mkanda wenye namba shingoni; na<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

26


• Kuweka namba kwa kuunguza sehemu ya ngozi ya mbuzi. Pale mfugaji<br />

anapotumia njia hii inashauriwa aweke alama kwenye eneo ambalo<br />

halitaathiri ubora wa ngozi<br />

Kuondoa vishina vya pembe<br />

Mbuzi/kondoo aondolewe vishina vya pembe akiwa na umri kati ya siku 3 hadi 14.<br />

Visipoondelewa hukua na kusababisha kuumizana na kuhitaji nafasi kubwa<br />

kwenye banda. Kazi hii ifanywe na mtaalam wa mifugo.<br />

Kuhasi<br />

Vitoto vya mbuzi/kondoo ambavyo havitatumika kwa ajili ya kuendeleza kizazi<br />

vihasiwe kabla ya kufikia umri wa miezi 3. Kazi hii ifanywe na mtaalam wa mifugo.<br />

2.4 Utunzaji wa Mbuzi/Kondoo wa Miezi 4 - 8<br />

Mbuzi wa miezi 4 mpaka 8 ni wale ambao wameacha kunyonya mpaka umri wa<br />

kupandishwa kwa mara ya kwanza. Mbuzi wa umri huu wana uwezo wa kula aina<br />

mbalimbali za malisho kama nyasi, mikunde, miti malisho na mabaki ya mazao<br />

wakati kondoo hupendelea zaidi nyasi fupi. Wakati wa kiangazi huhitaji kupatiwa<br />

chakula cha ziada au kupewa pumba za nafaka mbalimbali, mashudu ya alizeti,<br />

pamba na dengu, majani ya mikunde yaliyokaushwa, madini na vitamini.<br />

Katika ufugaji huria ni vema kuzingatia idadi ya mbuzi/kondoo inayoweza<br />

kuchungwa katika eneo, aina na hali ya malisho.<br />

Ili mbuzi/kondoo aweze kukua na kufikia uzito wa kuchinjwa/kupevuka mapema,<br />

mfugaji anapaswa kufuata kanuni za ufugaji bora zifuatazo:-<br />

• Kumpatia vyakula vya ziada kwa muda wa miezi 2 mfululizo kiasi cha kilo 0.2 –<br />

0.7 kwa siku kuanzia anapoachishwa kunyonya,<br />

• Kumpatia dawa ya kuzuia minyoo kila baada ya miezi 3 na kutoa kinga za<br />

magonjwa mengine kama itakavyoshauriwa na mtaalam wa mifugo,<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

27


• Kuchanja na kuogesha ili kuzuia magonjwa mbalimbali,<br />

• Kukata kwato mara zinapokuwa ndefu; na<br />

• Kuhasi madume yasiyotumika kuzalisha.<br />

2.5 Umri wa Kupandisha Mbuzi/Kondoo<br />

Mbuzi/kondoo wakitunzwa vizuri wanaweza kupandishwa wakiwa na umri wa<br />

miezi 8 hadi 12 kwa mbuzi/kondoo walioboreshwa na miezi 18 hadi 24 kwa mbuzi<br />

wa asili kutegemea afya yake. Hata hivyo, inashauriwa wapandishwe wanapofikia<br />

uzito wa kilo 12 au zaidi na wasipandishwe mbuzi/kondoo wa ukoo mmoja.<br />

Dalili za joto<br />

Mfugaji anashauriwa asimpandishe jike kabla hajafikisha umri wa kupandwa wa<br />

miezi 8 hadi 12 kwa mbuzi/kondoo walioboreshwa na miezi 18 hadi 24 kwa mbuzi<br />

wa asili hata kama ataonyesha dalili ya kuhitaji dume. Mbuzi/kondoo aliyezaa<br />

anaweza kupandishwa siku 30-60 baada ya kuzaa. Mbuzi/kondoo aliyeko kwenye<br />

joto huonyesha dalili zifuatazo:-<br />

• Hutingisha/huchezesha mkia,<br />

• Hupanda na kukubali kupandwa na wengine,<br />

• Hutoa ute mweupe ukeni,<br />

• Huhangaika mara kwa mara na kupiga kelele,<br />

• Hufuata madume,<br />

• Hamu ya kula hupungua,<br />

• Hukojoa mara kwa mara,<br />

• Uke huvimba na huwa mwekundu kuliko ilivyo kawaida; na<br />

• Kwa mbuzi anayekamuliwa hupunguza kiwango cha maziwa<br />

Mbuzi/kondoo apelekwe kwa dume mara tu dalili za joto zinapoonekana kwani<br />

joto hudumu kwa wastani wa siku 2 (saa 48). Chunguza tena dalili za joto baada<br />

ya siku 19 hadi 21 na kama dalili hazitaonekana tena kuna uwezekano mkubwa<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

28


kuwa mbuzi/kondoo amepata mimba. Mfugaji apange msimu mzuri wa<br />

mbuzi/kondoo kuzaa. Msimu mzuri ni mara baada ya mvua.<br />

2.6 Utunzaji wa Mbuzi/Kondoo Mwenye Mimba<br />

Kwa kawaida mbuzi/kondoo hubeba mimba kwa muda wa miezi 5. Utunzaji wa<br />

mbuzi/kondoo mwenye mimba ni muhimu kwani ndiyo chanzo cha kupata vitoto<br />

vyenye afya bora. Mfugaji anashauriwa kufuata kanuni zifuatazo:<br />

• Apatiwe vyakula vya ziada kilo 0.2 – 0.7 kwa siku ili kutosheleza mahitaji<br />

yake na kitoto kinachokua tumboni,<br />

• Apatiwe nyasi, miti malisho na mikunde mchanganyiko kilo 1.8 – 2.5 kwa<br />

siku.<br />

Dalili za Mbuzi/Kondoo Anayekaribia Kuzaa<br />

• Huhangaika kwa kulala na kuamka mara kwa mara,<br />

• Sehemu ya nje ya uke hulegea,<br />

• Hujitenga na kundi na hutafuta sehemu kavu na yenye kivuli,<br />

• Hupiga kelele; na<br />

• Hutokwa na ute mzito ukeni.<br />

Mfugaji akiona dalili hizi anashauriwa asimruhusu mbuzi/kondoo kwenda<br />

machungani, bali amtenge kwenye chumba maalum, ampatie maji ya kutosha na<br />

kumuandalia sehemu ya kuzalia.<br />

2.7 Utunzaji wa Mbuzi/Kondoo Anayenyonyesha<br />

Mbuzi/kondoo anayenyonyesha huhitaji chakula kingi zaidi ili kukidhi mahitaji ya<br />

mwili na kuzalisha maziwa kwa ajili ya kitoto/vitoto. Pamoja na nyasi, mikunde na<br />

majani ya miti malisho kilo 1.8 – 2.5 kwa siku ni muhimu apewe chakula cha<br />

nyongeza kilo 0.3 – 0.8 kwa kila lita ya maziwa inayoongezeka baada ya lita 2 na<br />

maji safi, salama na ya kutosha wakati wote.<br />

Taratibu za Kuzingatia Katika Ukamuaji wa Mbuzi wa Maziwa<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

29


Lengo la ufugaji wa mbuzi/kondoo wa maziwa ni kupata maziwa mengi, safi na<br />

salama pamoja na mazao yatokanayo na maziwa. Mambo muhimu ya kuzingatia<br />

ni:-<br />

• Sehemu ya kukamulia iwe safi na yenye utulivu,<br />

• Mbuzi/kondoo awe na afya nzuri, msafi, na kiwele kioshwe kwa maji safi ya<br />

uvuguvugu,<br />

• Mkamuaji asibadilishwe badilishwe awe msafi, mwenye kucha fupi na asiwe<br />

na magonjwa ya kuambukiza,<br />

• Vyombo vya kukamulia viwe safi; na<br />

• Maziwa ya mwanzo kutoka kila chuchu yakamuliwe kwenye chombo<br />

maalum (strip cup) ili kuchunguza ugonjwa wa kiwele.<br />

2.8 Utunzaji wa Dume Bora la Mbegu<br />

Dume bora la mbegu ni muhimu litunzwe ili liwe na uwezo wa kutoa mbegu bora,<br />

kupanda na kuzalisha. Dume bora huanza kupanda akiwa na umri kati ya miezi.8 -<br />

10 kwa mbuzi walioboreshwa. Katika msimu wa kupandisha dume moja liruhusiwe<br />

kupanda majike 40 hadi 50. Aidha, inashauriwa madume wenye umri wa miezi 8 –<br />

9 waruhusiwe kupanda majike ambao ndio mara ya kwanza kupandwa.<br />

Dume apatiwe:-<br />

• Malisho ya kutosha na vyakula vya ziada kiasi kisichopungua kilo 0.2 – 0.7<br />

kwa siku na maji ya kutosha,<br />

• Majani ya miti malisho, mikunde na nyasi mchanganyiko na mabaki ya<br />

mazao; na<br />

• Kilo 0.45 hadi 0.9 za chakula cha ziada za nyongeza kwa siku kulingana na<br />

uzito wake na wingi wa majike anayopanda.wiki 2 kabla na baada ya<br />

kuanza kupanda.<br />

2.9 Matunzo Mengine<br />

Kukata Mkia<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

30


Mara nyingine kondoo hukatwa mkia ili kuruhusu mtawanyiko mzuri wa mafuta<br />

katika misuli mwilini. Pia kondoo aliyekatwa mkia huwa msafi. Kazi hii ifanywe<br />

kama itakavyoshauriwa na mtaalam wa mifugo kwa kutumia vyombo maalum.<br />

Inashauriwa mkia ukatwe urefu wa sentimita 2.5 – 3.8 kutoka kwenye shina la<br />

mkia wakati kondoo akiwa na umri wa siku 3 mpaka mwezi 1.<br />

Kumnyoa Kondoo wa Sufu<br />

Sufu hunyolewa wakati kondoo akiwa hai au amechinjwa. Kwa kawaida<br />

hunyolewa miezi 6 hadi mwaka 1 ambapo sufu huwa imefikia urefu wa sentimita<br />

15 – 20. Vifaa vinavyotumika ni pamoja na mikasi au visu maalum. Uangalifu<br />

unahitajika wakati wa kunyoa ili ngozi ya kondoo isiharibike. Unyoaji ufanyike<br />

wakati wa kiangazi na siyo wakati wa mvua, kondoo akiwa na mimba au kipindi<br />

cha majani kutoa mbegu.<br />

2.10 Udhibiti wa Magonjwa ya Mbuzi na Kondoo<br />

Magonjwa husababishwa na vimelea jamii ya virusi, bakteria, protozoa na riketsia.<br />

Magonjwa mengine husababishwa na upungufu wa viinilishe, vitamini na protini.<br />

Dalili za mbuzi/kondoo mgonjwa ni pamoja na:-<br />

� Manyoya husimama,<br />

� Kuzubaa, kusinzia, kukohoa na kupiga chafya,<br />

� Kukosa hamu ya kula na kunywa maji,<br />

� Kujitenga na kundi,<br />

� Kuvimba taya la chini,<br />

� Kupumua kwa shida,<br />

� Kutokwa na machozi na makamasi,<br />

� Kuwa na upele au uvimbe kwenye sehemu ya mwili; na<br />

� Kutupa mimba.<br />

• Hatua za haraka za kumuona mtaalamu wa mifugo zichukuliwe iwapo<br />

baadhi ya dalili hizi zitaonekana,<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

31


• Mbuzi na kondoo wachanjwe dhidi ya magonjwa ya homa ya maapafu.<br />

Ugonjwa huu ni hatari sana na huenea kwa njia ya hewa na unaweza<br />

kusababisha vifo kati ya asilimia 60-100,<br />

• Kila baada ya miezi 6 mifugo ipatiwe kinga dhidi ya ugonjwa wa miguu na<br />

midomo na magonjwa mengine kama Kimeta, bonde la ufa, kutupa mimba<br />

na chambavu (BQ) zitolewe kulingana na ushauri wa mtalaam wa mifugo,<br />

• Kama kuna wanyama walioathirika watengwe kwenye kundi, wasisafirishwe<br />

au kuuzwa,<br />

• Mbuzi/kondoo wapatiwe dawa ya minyoo. Vitoto vya mbuzi/kondoo<br />

vipatiwe dawa ya minyoo vinapofikia umri wa mwezi 1. viendelee kupatiwa<br />

dawa ya minyoo kila mwezi hadi vinapofikia miezi 5 na baada ya hapo<br />

vipatiwe dawa ya minyoo kila baada ya miezi 3 - 4; na<br />

• Zingatia usafi wa banda ili kuwakinga na ugonjwa wa kuharisha na<br />

kuharisha damu na magonjwa mbalimbali.<br />

2.11 Utunzaji wa Kumbukumbu za Mifugo<br />

Kuweka kumbukumbu za mifugo ni muhimu katika uzalishaji kwa ajili ya kutambua<br />

kosaafu, gharama za utunzaji na faida. Pia, humsadia mfugaji kufanya maamuzi<br />

katika uendelezaji wa ufugaji wake. Mtalaamu wa mifugo pia anaweza kutumia<br />

kumbukumbu hizi ili kumsaidia mfugaji kuboresha ufugaji wake.<br />

Kumbukumbu muhimu zinazohitajika kutunzwa ni:-<br />

• Kumbukumbu za idadi na ukuaji wa wanyama waliopo, jinsi zao, uzito wa<br />

mbuzi/kondoo kwa kila mwezi ili kufuatilia ukuaji wake, tarehe ya<br />

kuachishwa kunyonya na idadi ya waliouzwa,<br />

• Kumbukumbu ya uzazi zinazoonyesha tarehe ya kuzaliwa, namba yake, jinsi<br />

yake, aina (breed), namba ya dume/jike, na uzito wa kuzaliwa,<br />

• Kumbukumbu za upandishaji zinazoonyesha namba ya mbuzi/kondoo<br />

anayepandwa, tarehe ya joto na ya kupandwa, namba ya dume lililotumika<br />

kupanda, tarehe ya joto la pili kama atarudia na tarehe ya kuzaa,<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

32


• Kumbukumbu za chanjo na matibabu zinazoonyesha namba ya<br />

mbuzi/kondoo, tarehe ya matibabu, aina ya chanjo au ugonjwa, dawa<br />

iliyotumika, idadi ya waliokufa na waliopona na jina la mtaalam aliyetibu,<br />

• Kumbukumbu za maziwa zinazoonyesha namba ya mbuzi/kondoo, tarehe<br />

ya kuzaa, kiasi cha maziwa kwa siku, na kiasi cha maziwa kwa kipindi chote<br />

cha kukamuliwa, tarehe ya kuacha kukamua na idadi ya siku alizokamuliwa,<br />

• Kumbukumbu za mapato na matumizi zinazoonyesha mapato na matumizi,<br />

vitu vilivyouzwa au kununuliwa kwa siku, kiasi cha fedha unachokuwa<br />

nacho kila wakati, kiasi cha fedha unachodai na kudaiwa.<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

33


SURA <strong>YA</strong> TATU<br />

3.0 KANUNI ZA UFUGAJI BORA <strong>WA</strong> NGURUWE<br />

Ufugaji wa nguruwe hapa nchini unaongezeka siku hadi siku kutokana na<br />

kuongezeka kwa walaji wa nyama ya nguruwe. Ili kufuga kwa faida ni vyema<br />

kufuata kanuni za ufugaji bora wa nguruwe.<br />

Nguruwe huweza kufugwa katika mfumo huria au wa ndani (shadidi). Katika<br />

mfumo huria, nguruwe huachwa huru kujitafutia chakula, hivyo ni lazima mfugaji<br />

awe na eneo au ardhi ya kutosha, eneo lililo jitenga mbali na makazi ya watu.<br />

Katika mfumo wa shadidi, nguruwe hufugwa ndani muda wote bila kutoka nje na<br />

kupewa chakula na maji kufuatana na mahitaji ya kila kundi.<br />

Nguruwe jike Nguruwe dume<br />

3.1 Banda la nguruwe<br />

Banda la nguruwe ligawanywe kulingana na makundi mbalimbali yanayofugwa.<br />

Aidha, liwe na sehemu ya stoo na ya kuchanganyia chakula. Banda bora linatakiwa<br />

kuwa na sifa zifuatazo:-<br />

• Lijengwe mahali pasipo na upepo mkali,<br />

• Kuta imara, zinazopitisha mwanga na hewa,<br />

• Liwe na sehemu ya kufanyia mazoezi,<br />

• Liwe kubwa la kutosha nguruwe kuchagua sehemu ya kupumzikia na sehemu<br />

ya mkojo na kinyesi,<br />

• Sakafu imara isiyoteleza, yenye mwinuko (2%) na isiyoruhusu maji kutuama;<br />

na<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

34


• Paa lisilovuja<br />

Vipimo vya wastani vya banda la nguruwe ni kama inavyoonyeshwa kwenye<br />

Jedwali Na. 6<br />

Jedwali Na.6: Nafasi Inayohitajika Kwa Makundi ya Nguruwe.<br />

Sehemu /Kundi Eneo kwa Nguruwe<br />

(Mita 2 )<br />

Chumba cha nguruwe mwenye mimba 1.28<br />

Sehemu ya mazoezi 3 hadi 4<br />

Chumba cha kuzalia pamoja na kreti 6.2<br />

Sehemu ya kunyonyeshea pamoja na sehemu<br />

10<br />

ya watoto<br />

Chumba cha wasionyonyesha:<br />

Sehemu ya kulala 0.4<br />

Sehemu ya mazoezi 0.9<br />

Nguruwe wanaokua (kilo 50 hadi 60) 0.73<br />

Nguruwe wenye uzito zaidi ya kilo 90 0.93<br />

Sehemu ya chakula kwa:<br />

Nguruwe wa kunenepesha 0.2 hadi 0.3<br />

Jike 0.35<br />

3.2 Kuchagua Nguruwe wa Kufuga<br />

Aina kuu za nguruwe wanaofugwa Tanzania ni nguruwe wa asili, Landrace,<br />

Hampshire, Large White, Saddleback na machotara wao. Ili kuweza kupata mazao<br />

mengi na bora ni muhimu kwa mfugaji kuchagua nguruwe wenye sifa zifuatazo:-<br />

Jike:<br />

• Awe na umbile la kumwezesha kubeba mimba na kuzaa kwa urahisi;<br />

• Awe na chuchu zisizopungua 10 – 14 na zilizojipanga vizuri;<br />

• Achaguliwe kutoka kwa wazazi wenye historia ya kuzaa watoto wengi,<br />

kutoa maziwa mengi na utunzaji mzuri wa watoto; na<br />

• Awe na miguu iliyonyooka, yenye nguvu na viungo imara.<br />

Dume:<br />

• Achaguliwe kutoka kwenye ukoo wenye historia ya kutokuwa na magonjwa<br />

au ulemavu,<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

35


• Awe na miguu imara, mchangamfu na mwenye afya bora,<br />

• Awe na umbile zuri na misuli imara itakayomwezesha kupanda majike bila<br />

matatizo,<br />

• Awe mwenye kokwa mbili zinazoonekana na zilizokamilika; na<br />

• Awe anayekua haraka.<br />

3.3 Utunzaji wa Watoto wa Nguruwe<br />

Watoto wa nguruwe hutunzwa kulingana na hatua ya ukuaji.<br />

• Mara baada ya kuzaliwa watoto wawekwe mahali penye joto la kutosha na<br />

wanyonye maziwa ya mwanzo. Maziwa hayo ni muhimu kwani yana<br />

viinilishe vya kujenga mwili, kuleta nguvu na kuongeza kinga dhidi ya<br />

magonjwa,<br />

• Kama mama amekufa mara baada ya kuzaa au anakataa kunyonyesha na<br />

hakuna nguruwe mwingine anayeweza kuwanyonyesha, watoto wapewe<br />

dang’a ya ng’ombe au dang’a mbadala,<br />

• Vitovu vikatwe na kuachwa sentimita 5 kwa kutumia vifaa safi, na kupaka<br />

dawa ya joto (Tincture of Iodine) ili kuzuia viini vya magonjwa kupitia<br />

kitovuni,<br />

• Wachomwe sindano ya madini ya chuma au kupaka madini ya chuma<br />

kwenye chuchu za mama wiki ya kwanza kwa kuwa maziwa na damu ya<br />

watoto haina kiasi cha kutosha cha madini hayo muhimu kwa kutengeneza<br />

damu mwilini. Kazi hii ifanywe na mtaalam wa mifugo; na<br />

• Meno anayozaliwa nayo yakatwe kwa kutumia mkasi mkali na safi. Meno<br />

hayo humuumiza mama anaponyonyesha. Kazi hii ifanywe na mtaalam wa<br />

mifugo.<br />

3.4 Utunzaji wa Watoto wa Nguruwe Wiki 1 - 8<br />

Wiki moja baada ya kuzaliwa watoto wa nguruwe wapatiwe huduma zifuatazo:-<br />

• Waendelee kupatiwa joto la kutosha hasa maeneo ya baridi kwa kutumia<br />

chanzo chochote cha joto kama umeme, taa ya chemli au mkaa,<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

36


• Wanyweshwe maji yenye madini ya chuma mililita 1.5 kwa kipindi cha<br />

mwezi mmoja au kuwapa nafasi ya kula udongo msafi au vidonge vyenye<br />

madini ya chuma pale ambapo njia ya sindano au ya kupaka chuchu<br />

haikuwezekana,<br />

• Walishwe chakula maalum cha kwanza cha watoto kidogo kidogo kuanzia<br />

siku ya 10 baada ya kuzaliwa na waendelee kupewa chakula hiki na maji ya<br />

kutosha mpaka siku ya kuachishwa kunyonya,<br />

• Watoto vidume ambao hawahitajiki kwa ajili ya kuzalisha wahasiwe wakiwa<br />

na umri kati ya wiki 3 hadi 6,<br />

• Wawekwe alama za utambulisho kabla ya kuwatenganisha na mama yao<br />

kwa kuwaweka namba kwenye masikio. Mfugaji anashauriwa kupata<br />

ushauri wa mtaalam wa mifugo kuhusu kuweka alama za utambulisho; na<br />

• Watoto waachishwe kunyonya kwa kutenganishwa na mama yao wakiwa<br />

na umri wa wiki 8 kwa kumhamishia mama kwenye chumba kingine na<br />

kuwaacha watoto kwenye chumba walichozaliwa.<br />

3.5 Utunzaji wa Nguruwe Walioachishwa Kunyonya<br />

Baada ya watoto wa nguruwe kuachishwa kunyonya ni muhimu kuzingatia<br />

yafuatayo:-<br />

• Hakikisha watoto wanapewa dawa ya minyoo, wanakingwa dhidi ya<br />

magonjwa na kutibiwa mara wanapougua,<br />

• Nguruwe walioachishwa kunyonya waanze kupewa chakula cha kukuza<br />

kama ilivyoainishwa katika Jedwali Na. 7.<br />

Jedwali Na. 7: Aina ya Chakula cha Kukuza Nguruwe<br />

Aina Kilo<br />

Pumba za mahindi 45<br />

Mahindi yaliyosagwa 30<br />

Mashudu ya pamba au Alizeti 15<br />

Dagaa 3<br />

Damu iliyokaushwa 5<br />

Madini 2<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

37


JUMLA 100<br />

• Badilisha chakula hatua kwa hatua kutoka chakula cha watoto kuingia<br />

chakula cha kukuza. Lisha sehemu 3 /4 ya chakula cha watoto na 1 /4 ya<br />

chakula cha kukuza kwa wiki ya kwanza, ongeza kufikia ½ kwa ½ wiki ya<br />

pili na ya tatu iwe 1 /4 ya chakula cha watoto na 3 /4 ya chakula cha kukuzia.<br />

Wiki ya 4 endelea kulisha chakula cha kukuza pekee.<br />

• Kiasi cha chakula kinachotakiwa kulishwa nguruwe wanaokua ni kama<br />

inavyoonyeshwa katika Jedwali Na. 7<br />

Jedwali Na. 7: Kiasi cha Chakula kwa Nguruwe Wanaokua<br />

Wiki Kiasi kwa siku (kilo)<br />

8 - 12 1.0<br />

12 -18 1.5<br />

18 -23 2.0<br />

23 -30 3.0<br />

• Chakula kigawanywe na kulishwa mara 2 kwa siku pamoja na maji safi ya<br />

kutosha wakati wote,<br />

• Usafi wa chumba, vifaa na mazingira ni muhimu ufanyike kila siku,<br />

• Viwepo vitu vya kuchezea kama minyororo au matairi mabovu ili watoto<br />

waweze kufanya mazoezi, kuondoa upweke na kupunguza kupigana; na<br />

• Mfugaji achague nguruwe kwa ajili ya kuendeleza uzalishaji wakiwa na umri<br />

wa miezi 3 au zaidi. Wale wasiohitajika kuendelea kufugwa wachinjwe kwa<br />

ajili ya nyama na mafuta wakifikia uzito wa kilo 60 hadi 90.<br />

3.6 Utunzaji wa Nguruwe Jike Kutoka Kupevuka Hadi Kuzaa<br />

Aina nyingi za nguruwe hupevuka wakiwa na umri wa miezi 5, hata hivyo si vema<br />

kumpandisha wakati huo kwa kuwa atakuwa hajakomaa vizuri kimaumbile.<br />

Inashauriwa kumpandisha atakapokuwa na umri wa miezi 8 hadi 9.<br />

• Kabla ya kupandishwa nguruwe jike apewe kilo 2.5 hadi 3.0 za chakula kwa<br />

siku,<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

38


• Nguruwe jike apelekwe kwa dume pale tu akioonyesha dalili za joto<br />

zifuatazo:-<br />

� Kutopenda kula chakula,<br />

� Kupiga kelele ovyo,<br />

� Kuhangaika kila mara,<br />

� Kupanda au kukubali kupandwa na nguruwe wenzake,<br />

� Sehemu ya uke kuvimba na kuwa nyekundu,<br />

� Kukojoa mara kwa mara na kutoa ute mweupe usiokatika ukeni; na<br />

� Kutulia anapokandamizwa mgongoni.<br />

Dalili hizi siyo lazima zionekane zote wakati mmoja hivyo ni muhimu mfugaji kuwa<br />

mwangalifu na ili aweze kuzitambua kwa urahisi, chumba cha majike<br />

yanayotarajiwa kupandwa kinatakiwa kiwe karibu na cha dume. Dalili hudumu kwa<br />

muda wa siku 2 hadi 3 hivyo nguruwe apandishwe mara anapokuwa kwenye joto<br />

na kurudia tena katika muda wa masaa 12.<br />

3.6.1 Kutunza Nguruwe Mwenye Mimba<br />

Mimba ya nguruwe huchukua miezi 3, wiki 3 na siku 3 (siku 114 hadi 119) hadi<br />

kuzaa.<br />

• Nguruwe jike mwenye mimba awekwe kwenye banda lenye nafasi, hewa na<br />

mwanga na eneo la kutosha kwa ajili ya mazoezi ya mwili. Nguruwe mwenye<br />

mimba anahitaji mazoezi zaidi ili kuimarisha miguu na misuli yake. Sehemu ya<br />

uzio isiwe na unyevu kuepuka magonjwa, ikiwezekana kuwe na kivuli cha<br />

kumkinga na jua kali,<br />

• Chumba cha kuzalia kiandaliwe wiki 2 hadi 3 kabla ya nguruwe kuzaa.<br />

Kiwekwe malalo na itengwe sehemu ambayo itahifadhi watoto wasilaliwe au<br />

kukanyagwa na mama yao,<br />

• Kiwe na sehemu ya kuweka chombo cha kuongezea joto, chakula na maji kwa<br />

ajili ya watoto,<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

39


• Nguruwe mwenye mimba anahitaji kupewa chakula kinacholeta nguvu na<br />

kujenga mwili. Katika mwezi wa 1 apewe kilo 2 hadi 2.5 kwa nguruwe<br />

mwenye afya nzuri, akiwa dhaifu apewe kilo 3 kwa kipindi cha wiki 3,<br />

• Kuanzia siku 60 kabla ya kuzaa alishwe kilo 3.5 za chakula kwa siku. Siku ya 3<br />

kabla ya kuzaa, chakula kipunguzwe hadi kufikia kilo 2 kwa siku. Siku ya kuzaa<br />

asipewe chakula, apewe maji tu,<br />

• Wiki 1 kabla ya kuzaa nguruwe aogeshwe vizuri kwa maji safi na sabuni. Baada<br />

ya kuogeshwa anyunyiziwe dawa ili kuzuia wadudu wa ngozi na apewe dawa<br />

ya minyoo; na<br />

• Anapokaribia kabisa kuzaa awekwe kwenye chumba cha uzazi.<br />

Dalili za Kuzaa<br />

Dalili za kuzaa zinapoonekana awepo mwangalizi ili aweze kutoa msaada kama<br />

utahitajika, hasa kwa nguruwe anayezaa kwa mara ya kwanza. Dalili za kuzaa ni:-<br />

• Kiwele na chuchu huongezeka ukubwa kwa kujaa maziwa,<br />

• Njia ya uke huvimba na kuwa nyekundu na mara nyingine hutoa maji<br />

mazito,<br />

• Nguruwe huhangaika na hupumua kwa nguvu,<br />

• Maziwa yanaweza kutoka yenyewe kwenye chuchu,<br />

• Hukojoa mara kwa mara,<br />

• Hukusanya majani na kuandaa mahali pa kuzalia; na<br />

• Tumbo linapwaya na baadhi ya majike hupoteza hamu ya kula.<br />

3.6.2 Utunzaji wa Nguruwe Anayenyonyesha<br />

Nguruwe anayenyonyesha anastahili kupatiwa matunzo muhimu kutokana na<br />

mahitaji ya mwili na utoaji wa maziwa. Ili kukidhi mahitaji hayo mfugaji anapaswa<br />

kuzingatia matunzo yafuatayo:-<br />

• Mara baada ya nguruwe kuzaa ahakikishe kondo la nyuma la uzazi limetoka<br />

lote, kwa kuhesabu vipande kulingana na idadi ya watoto. Endapo idadi<br />

haikulingana, unashauriwa kumwona mtaalam wa mifugo aliyekaribu.<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

40


• Apatiwe chakula kama inavyooneshwa katika Jedwali Na. 8<br />

Jedwali Na. 8: Kiwango cha Chakula kwa Siku<br />

Idadi ya siku baada ya kuzaa Kiasi cha chakula kwa siku (kilo/<br />

1 1<br />

2 2<br />

3 3<br />

4 - 8 4<br />

gram)<br />

Siku ya 9 na kuendelea 3 na gram 333 kwa kila mtoto<br />

Siku ya kuachisha kunyonya (siku ya<br />

60)<br />

• Apatiwe maji ya kutosha wakati wote; na<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

2<br />

• Apunguze chakula mpaka kilo 2 kwa siku anapomtenganisha nguruwe na<br />

watoto na amwongeze hadi kufikia kilo 3 kwa siku kutegemeana na afya ya<br />

nguruwe.<br />

Kumbuka nguruwe akilishwa chakula kingi, atanenepa sana na hatapata<br />

mimba kwa urahisi baadae na akibahatika kupata mimba huweza kuharibika.<br />

Akilishwa chakula kidogo hudhoofika, huzaa watoto dhaifu katika mimba<br />

zinazofuata na hutoa maziwa kidogo.<br />

3.7 Utunzaji wa Dume<br />

Nguruwe dume anaweza kutumika kwa kupanda jike akiwa na umri wa miezi 8<br />

hadi 9. Kwa umri huo anaruhusiwa kupanda jike 1 kwa wiki. Afikiapo miezi 10<br />

anaruhusiwa kupanda majike 2 hadi 3 kwa wiki. Akiwa na umri wa mwaka 1 au<br />

zaidi ana uwezo wa kupanda jike 1 kila siku kwa wiki 2 hadi 3 kisha apumzishwe<br />

kwa muda wa wiki 2. Dume mwenye uzito mkubwa asitumike kupanda jike dogo<br />

kwani anaweza kumvunja mgongo.<br />

41


Katika utunzaji wa dume bora la mbegu ni muhimu kuzingatia yafuatayo:<br />

• Dume aliyechaguliwa kwa ajili ya mbegu, atenganishwe na majike ili<br />

kuepusha kupanda wakati usiotakiwa,<br />

• Dume awe na eneo la mita za mraba 9.3 kwa ajili ya kupata mazoezi ya<br />

mwili,<br />

• Dume aogeshwe kwa dawa zinazoweza kuua wadudu na vimelea<br />

vinavyoweza kusababisha magonjwa,<br />

• Dume wa kupanda asinenepeshwe, hivyo alishwe chakula bora kiasi cha<br />

kilo 2 hadi 3 kwa siku na maji ya kutosha; na<br />

• Dume anayepanda majike chini ya mara 3 kwa wiki, alishwe kilo 2.5 za<br />

chakula na kama anapanda zaidi ya mara 3, alishwe kilo 3 kwa siku.<br />

3.8 Udhibiti wa Afya na Magonjwa ya Nguruwe<br />

Mfugaji anatakiwa kujali afya ya nguruwe ili kupunguza vifo na gharama za<br />

matibabu. Magonjwa yanayoshambulia nguruwe hapa nchini ni pamoja na Homa<br />

ya Nguruwe, Ukurutu, Kichomi, Ugonjwa wa Midomo na Miguu, Kimeta, Mafua,<br />

Ugonjwa wa kuhara hasa kwa nguruwe wachanga na minyoo. Dalili kuu za<br />

nguruwe mgonjwa ni:-<br />

• Hupoteza hamu ya kula<br />

• Kutochangamka<br />

• Kudhoofu<br />

• Kukonda<br />

• Kudumaa<br />

• Kujisuguasugua na kunyonyoka manyoya<br />

Mfugaji akiona mojawapo ya dalili hizo amwone mtalaam wa mifugo.<br />

3.10 Kuweka na Kutunza Kumbukumbu<br />

Kuweka kumbukumbu ni muhimu kwa ajili ya kufuatilia maendeleo ya uzalishaji na<br />

pia humsadia mfugaji kufanya maamuzi katika kuendeleza ufugaji wake.<br />

Kumbukumbu zinazowekwa zionyeshe:-<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

42


• Idadi ya nguruwe wanaofugwa kwa makundi mabalimbali<br />

• Kiasi cha chakula kinachohitajika kwa kila nguruwe<br />

• Uzito kila baada ya wiki 1 hasa kwa wale wanaofugwa kwa ajili ya nyama<br />

• Kumbukumbu za mapato na matumizi<br />

• Kumbukumbu za uzazi kwa nguruwe jike ni kama:<br />

� Aina ya nguruwe<br />

� Namba ya nguruwe<br />

� Tarehe ya kuzaliwa<br />

� Dume lililotumika<br />

� Tarehe ya kuzaa<br />

� Idadi ya waliozaliwa, wazima na waliokufa<br />

� Uzito wa watoto walipozaliwa, baada ya wiki 3 na baada ya wiki 8<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

43


SURA <strong>YA</strong> NNE<br />

4.0 KANUNI ZA UFUGAJI BORA <strong>WA</strong> KUKU.<br />

Kaya nyingi hapa nchini hujihusisha na ufugaji wa kuku kwa lengo la kujipatia<br />

chakula na kipato. Mazao yatokanayo na ufugaji wa kuku ni pamoja na mayai,<br />

nyama, mbolea na manyoya kwa ajili ya matumizi mbalimbali. Mifumo ya ufugaji<br />

kuku ambayo hutumika hapa nchini ni huria, nusu huria na shadidi. Ufugaji wa<br />

kuku utakuwa endelevu na wenye tija kwa kufuata kanuni za ufugaji bora<br />

zifuatazo:-<br />

• Kufuga kuku kwenye banda bora<br />

• Kuchagua kuku bora wa kufuga<br />

• Kutunza na kulisha kuku kulingana na hatua mbalimbali za ukuaji<br />

• Kudhibiti na kutibu magonjwa ya kuku<br />

• Kutunza kumbukumbu<br />

4. 1 Banda la kuku<br />

Kuku tafuta picha mbadala<br />

Kuku huhitaji banda bora ili wasiathirike na madhara mbalimbali. Banda bora la<br />

kuku linatakiwa kuwa na sifa zifuatazo:-<br />

• Imara, lenye uwezo wa kuwahifadhi kiafya na pia dhidi ya hali ya hewa<br />

hatarishi kwa mfano jua kali, upepo, baridi na mvua pamoja na wanyama<br />

hatari,<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

44


• Lenye mwanga, hewa na nafasi ya kutosha inayoruhusu usafi kufanyika kwa<br />

urahisi,<br />

• Lijengwe sehemu yenye mwinuko isiyotuama maji, isiyo na upepo mkali na iwe<br />

mbali kidogo na nyumba ya kuishi watu.<br />

• Liwe na vichanja kwa ajili ya kuku kupumzika na kulala<br />

• Liwe na sehemu ya kuwekea chakula, maji, kutagia, kuatamia na sehemu<br />

ya kulelea vifaranga<br />

• Liwe na nafasi ya kutosha kulingana na idadi ya kuku na kuweka vyombo<br />

vya chakula na maji<br />

• Kwenye mazingira ya joto banda liwe la ukuta mfupi na sehemu kubwa<br />

wazi yenye wavu hadi kufikia kwenye paa<br />

• Kwenye mazingira ya baridi banda liwe na ukuta mrefu unaokaribia paa na<br />

sehemu ndogo tu iwe wazi yenye wavu ili kupitisha hewa na mwanga<br />

4.1.1 Vifaa vinavyotumika kwa ujenzi wa banda<br />

Vifaa vya kujengea banda vizingatie gharama na upatikanaji wake katika eneo<br />

husika. Baadhi ya vifaa hivyo ni kama ifuatavyo:-<br />

• Sakafu Saruji, udongo, mbao, mianzi au fito<br />

• Kuta Fito, mabanzi, mbao, nguzo mianzi,udongo, matofali, mawe,<br />

mabati na wavu<br />

• Paa Nyasi, makuti, majani ya migomba, mabati na vigae.<br />

• Wigo Matofali, mbao, fito nguzo, mabanzi, mianzi, matete, wavu na<br />

mabati<br />

4.1.2 Ukubwa wa banda<br />

Ukubwa wa banda utategemea idadi ya kuku na aina ya kundi la kuku. Kuku<br />

wanahitaji nafasi tofauti kutegemea umri, aina, na njia ya ufugaji. Eneo la mita<br />

moja ya mraba linatosha kwa vifaranga 16 wa umri wa wiki 1 - 4. Hivyo banda<br />

lenye mita za mraba 16 linaweza kulea vifaranga 320 hadi wiki 4. Baada ya wiki 4<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

45


eneo hili liongezwe kutegemea aina ya kuku na njia inayotumika katika ufugaji<br />

kama inavyoonekana kwenye Jedwali Na. 9<br />

Jedwali Na 9: Eneo Linalohitajika Kufuga Kuku Kwenye Sakafu ya<br />

Umri wa kuku<br />

Matandazo Kutegemea na Umri na Aina ya Kuku<br />

Idadi ya kuku kwa mita 1 ya mraba<br />

Kuku wa mayai Kuku wa nyama<br />

Siku 1 hadi wiki 4 18 18<br />

Wiki ya 5 hadi ya 8 9 9<br />

Wiki ya 9 hadi 20 6 -<br />

Wiki 21 na kuendelea 3 - 4 -<br />

Angalizo:<br />

Mabanda yanayozungushiwa wigo kama ilivyo katika mfumo wa nusu huria, kuku<br />

mmoja huhitaji eneo la wazi lenye ukubwa wa mita za mraba 10. Mfano, kuku<br />

100 huhitaji eneo la mita za mraba 1000<br />

4. 1.3 Vifaa na Vyombo Muhimu<br />

Mfugaji anashauriwa kutumia vifaa na vyombo maalum ili kurahisisha na<br />

kuboresha utunzaji wa makundi mbalimbali ya kuku. Vifaa na vyombo<br />

vinavyohitajika kwa ajili ya kuwekea chakula na maji, kutagia mayai na kupumzikia<br />

vinapatikana kwenye maduka ya pembejeo za mifugo. Aidha, mfugaji anaweza<br />

kutengeneza mwenyewe kwa kutumia malighafi zilizopo kwenye mazingira yake.<br />

4.2 Kuchagua Kuku Bora wa Kufuga<br />

4.2.1 Kuku wa Asili<br />

Aina za kuku wa asili wanaopatikana hapa nchini ni pamoja na Kuchi (Kuza), Poni<br />

(Kishingo), Njachama, Kinyavu, Mbuni na Tongwe (Msumbiji). Mfugaji anaweza<br />

kuongeza uzalishaji kwa kuchagua kuku mwenye sifa zifuatazo:-<br />

• Uwezo wa kutaga mayai mengi (kati ya 15-20) katika mzunguko mmoja wa<br />

utagaji (Jedwali Na 10),<br />

• Uwezo wa kuatamia na kuangua vifaranga wengi,<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

46


• Uwezo wa kustahimili magonjwa,<br />

• Anayetoka maeneo yasiyo na magonjwa; na<br />

• Umbo kubwa na kukua haraka.<br />

Jedwali Na 10: Masuala ya Kuzingatia Wakati wa Kumchagua Kuku<br />

Mtagaji wa Kienyeji<br />

Viungo vya mwili Sifa<br />

Macho Maangavu, yenye wekundu kwa mbali na makubwa<br />

yamejaa kwenye soketi za macho.<br />

Mdomo Wenye rangi ya njano kwa mbali<br />

Kisunzu/upanga Chekundu, laini, kimelala kidogo upande na<br />

kinang’aa<br />

Shingo Iliyosimama<br />

Umbali kati ya kidari na<br />

nyonga<br />

Upana wa vidole 3-4 vya mpimaji<br />

Upana wa nyonga Upana wa vidole 3 vya mpimaji<br />

4.2.2 Kuku wa Kisasa<br />

Kuku bora wa kisasa kwa ajili ya mayai au nyama ni mwenye sifa zifuatazo:-<br />

• Uwezo wa kuanza kutaga wakiwa na umri mdogo (miezi 5 - 6) kutegemea na<br />

koo,<br />

• Umbo kubwa na anayekua haraka (kilo 1.5-2.0 kwa kipindi cha wiki 8-12)<br />

kutegemea na koo kwa kuku wa nyama,<br />

• Anayetaga mayai mengi (250 au zaidi) kwa kuku wa mayai kwa mwaka; na<br />

• Awe na uwezo wa kutaga katika umri wa miezi 6 - 8.<br />

4.2.3 Kuchagua Jogoo Bora wa Mbegu<br />

Jogoo wa mbegu anatakiwa awe na sifa zifuatazo:<br />

• Achaguliwe kutoka kwenye koo zenye sifa ya kutaga mayai mengi,<br />

• Mrefu, umbo kubwa, miguu imara na yenye nguvu,<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

47


• Awe machachari, ushawishi kwa mitetea na ari ya kupanda; na<br />

• Uwezo wa kupanda akiwa na umri wa miezi 7 – 10.<br />

4.3 Mayai kwa Ajili ya Kutotoa Vifaranga<br />

4.3.1 Uchaguzi wa Mayai<br />

Mayai kwa ajili ya kutotoa vifaranga yawe na sifa zifuatazo:-<br />

• Yaliyorutubishwa na jogoo,<br />

• Yasiwe na nyufa,<br />

• Yasiwe na maganda tepetepe,<br />

• Yasiwe na kiini kilichovunjika,<br />

• Yawe na ukubwa wa wastani; na<br />

• Yasiwe yamekaa zaidi ya wiki 2 baada ya kutagwa.<br />

4.3.2 Utunzaji wa Mayai<br />

Mayai ya kienyeji kwa ajili ya kutotoa vifaranga yatunzwe kwa kusimamishwa<br />

wima sehemu iliyochongoka ikiwa imeangalia chini kwa siku 3 za mwanzo na kisha<br />

yageuzwe ili sehemu iliyo butu iangalie chini. Mayai yahifadhiwe kwenye sehemu<br />

iliyo na ubaridi kidogo na giza.<br />

4.4 Utunzaji wa Kuku kwa Makundi<br />

4.4.1 Utunzaji wa Vifaranga<br />

Malezi bora ya vifaranga ni muhimu katika ufugaji wa kuku kwa sababu vifaranga<br />

hawana uwezo wa kustahimili mazingira wakiwa wenyewe mara wanapoanguliwa.<br />

Ukosefu wa malezi bora husababisha vifaranga kuwa dhaifu, kufa kwa wingi na<br />

hivyo kupunguza idadi ya kuku wa baadaye. Malezi ya vifaranga yanaweza<br />

kufanyika kwa kutumia kuku walezi au kutumia vifaa maalum.<br />

Kulea Vifaranga kwa Kutumia Kuku Mlezi<br />

Vifaranga wanaweza kulelewa na mama yao au kuku mlezi. Endapo kuku wengi<br />

wametotoa vifaranga kwa wakati mmoja, achaguliwe kuku mlezi aliye na uwezo<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

48


wa kulea vifaranga wengi kati ya waliototoa aendelee kulea na wengine waliototoa<br />

waachwe huru ili warudi kwenye mzunguko wa kutaga. Kuku mmoja anaweza<br />

kulea vifaranga 20 hadi 25. Mfugaji wa kuku, pamoja na kanuni nyingine,<br />

anapaswa kuzingatia yafuatayo:-<br />

• Kuku anayelea vifaranga atengewe chumba maalum, apewe maji ya<br />

kutosha na chakula chenye virutubishi muhimu,<br />

• Vifaranga wasiachiwe kutoka nje hadi watakapofika umri wa wiki 6,<br />

• Vifaranga watengwe na mama/mlezi baada ya wiki 4 kuruhusu mama<br />

aendelee na mzunguko wa kutaga; na<br />

• Katika maeneo yenye hali ya hewa ya ubaridi vifaranga wacheleweshwe<br />

kutenganishwa na mama/malezi hadi wiki ya 6 au mpaka waonekane<br />

wameota manyoya ya kutosha.<br />

Kulea Vifaranga kwa Kutumia Bruda<br />

Bruda ni chombo/sehemu iliyoandaliwa mahususi kwa ajili ya kuwapatia joto<br />

vifaranga badala ya mama/mlezi. Mfugaji anaweza kulea vifaranga wengi kwa<br />

kutumia bruda ambayo ni mduara unaoweza kutengenezwa kwa kutumia mbao,<br />

karatasi ngumu au kwa kuziba pembe za chumba. Aidha, njia hii hupunguza vifo<br />

vya vifaranga vinavyosababishwa na ndege au wanyama hatari, huruhusu kuku<br />

kutaga mapema zaidi na kuwa na mizunguko mingi ya utagaji (kwa kuku<br />

wanaoatamia). Vilevile, hurahisisha udhibiti wa magonjwa.<br />

Mfugaji anapaswa kufuata taratibu zifuatazo katika kulea vifaranga kwa kutumia<br />

bruda:-<br />

• Kuweka vifaa vya kuongeza joto kwa mfano taa ya umeme, chemli au jiko<br />

la mkaa. Zingatia kiwango cha joto katika bruda kinachohitajika. Wiki ya<br />

kwanza ni 35 o C, wiki ya pili ni 33 o C, wiki ya tatu ni 31 o C na wiki ya nne ni<br />

29 o C,<br />

• Kuchunguza mtawanyiko wa vifaranga ndani ya bruda ili kutathimini hali ya<br />

joto. Wakijikusanya kwenye chanzo cha joto, inaashiria kuwa baridi imezidi<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

49


hivyo joto liongezwe. Wakiwa mbali na chanzo cha joto maana yake joto<br />

limezidi hivyo joto lipunguzwe,<br />

• Bruda iwe na sakafu yenye malalo yatokanayo na maranda ya mbao au<br />

pumba za mpunga. Malalo yabadilishwe endapo yataonekana yameloana,<br />

• Bruda iwekwe vifaa vya maji na chakula. Maji na chakula kiwekwe kabla ya<br />

kuweka vifaranga,<br />

• Vifaa vya joto viwekwe ndani ya bruda masaa 6 kabla ya kuingia vifaranga,<br />

• Vifaranga walishwe chakula cha kuanzia gramu 12 - 15 kwa kipindi cha wiki<br />

ya kwanza na gram 15 - 21 kwa kipindi cha wiki ya 2. Katika wiki ya 3<br />

wapewe gramu 21 - 35 kwa kifaranga na chakula hicho kiwepo muda wote,<br />

• Vifaranga wapatiwe vitamini, madini na dawa za kinga (antibiotics); na<br />

• Vifaranga wapatiwe chanjo kulingana na maelekezo ya mtaalamu wa<br />

mifugo. Chanjo dhidi ya magonjwa muhimu kwa mfano, Marek’s (mara<br />

anapototolewa), Mdondo (siku ya 3 - 4 na kurudiwa baada ya siku ya 21 na<br />

kila baada ya miezi 3) na Gumboro (siku ya 7 na kurudia tena siku ya 21).<br />

Wapatiwe dawa ya minyoo (wiki ya 8) na Coccidiosis ( wiki ya 3 - 4)<br />

4.4.3 Kutunza Kuku Wanaokua (wiki 8 - 18)<br />

Utunzaji wa kundi hili unategemea mfumo unaotumika.<br />

Kuku Wanaofugwa Katika Mfumo Huria<br />

Kuku wanaofugwa katika mfumo huu wapatiwe matunzo bora yakiwemo<br />

yafuatayo;<br />

• Wapewe chakula cha ziada asubuhi kabla ya kutoka na wanaporudi kwenye<br />

banda. Chakula hicho kinaweza kugawanywa mara 2 kwa siku,<br />

• Wapatiwe maji safi na ya kutosha wakati wote; na<br />

• Wapatiwe chanjo na dawa kulingana na ushauri wa mtaalam wa mifugo.<br />

Kuku Wanaofugwa Katika Mfumo Shadidi<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

50


• Majogoo watenganishwe na mitetea katika wiki 7 hadi 10 ili kuzuia uzaliano<br />

usio na mpangilio,<br />

• Wapewe chakula cha kukuzia kuanzia wiki ya 8 - 15 gramu 55 - 60 na<br />

kuanzia wiki ya 16 gramu 65 - 80 kwa wanaofugwa mfumo huria na gram<br />

120- 125 kwa kuku kwa siku kwa wanaofugwa mfumo wa shadidi,<br />

• Kuku wa nyama wapatiwe chakula cha kuku wa nyama muda wote,<br />

• Wapatiwe maji safi ya kunywa kwa muda wote kwenye vyombo visafi,<br />

• Kuku wachunguzwe dalili zozote za ugonjwa ili waweze kupata tiba sahihi<br />

kutoka kwa mtaalamu wa mifugo,<br />

• Kuku wa wiki 9 - 20 wanahitaji nafasi ya mita za mraba 0.15 kwa kuku na<br />

wiki 21 au zaidi mita za mraba 0.2 kwa kuku,<br />

• Kuwe na vyombo maalum vya kutosha kwa ajili ya chakula na maji<br />

• Wafanyiwe usafi wa banda mara kwa mara ili kuzuia magonjwa<br />

yanayotokana na uchafu; na<br />

• Wakatwe midomo ili kuzuia kudonoana.<br />

4.4.4 Kuku Wanaotaga<br />

Mahitaji ya kuku wanaotaga ni tofauti na ya makundi mengine. Mambo ya<br />

kuzingatia kwa kuku wanaotaga ni pamoja na:-<br />

• Banda liwe na viota vya kutagia mayai (kiota 1 kwa kuku 3 - 5). Viota<br />

viwekwe bandani mara kuku watakapofikisha umri wa wiki 18 ili waanze<br />

kuzoea kuvitumia,<br />

• Wapatiwe chakula na maji safi wakati wote kwa kutumia vyombo maalum<br />

ambavyo ni visafi,<br />

• Kuku wasiotaga waondolewe kwenye kundi. Kuku hao huonekana wasafi na<br />

sehemu ya kutolea yai huwa ndogo na kavu, upanga wake kichwani (comb)<br />

huwa mdogo na mwekundu,<br />

• Wapewe dawa ya minyoo kila baada ya miezi 3,<br />

• Wawekewe fito au ubao mwembamba kama sehemu ya kupumzikia na<br />

mazoezi ili kuzuia kudonoana,<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

51


• Mayai yakusanywe mara 4 au zaidi kwa siku ili yasidonolewe na kuku,<br />

• Kuwe na malalo makavu na yabadilishwe mara yanapochafuka,<br />

• Vyombo vifanyiwe usafi kila siku ili kuzuia magonjwa; na<br />

• Watundikiwe majani mabichi aina ya mchicha, papai, alfaalfa, majani jamii<br />

ya mikunde ili kuboresha lishe.<br />

4.5 Udhibiti na Tiba Dhidi ya Magonjwa ya Kuku<br />

Kuku wanaopata lishe bora, kutunzwa vizuri na kupatiwa chanjo dhidi ya<br />

magonjwa yanayotokea mara kwa mara huwa na afya nzuri. Ni bora kuzuia<br />

magonjwa kuliko kutibu ili kupunguza vifo na gharama. Iwapo ugonjwa utatokea<br />

kuku wagonjwa watenganishwe na kuku wasio wagonjwa na wapatiwe tiba.<br />

Kanuni muhimu za kufuata ili kuzuia magonjwa ni:-<br />

• Banda liwe safi muda wote,<br />

• Kabla ya kuweka kuku, banda linyunyiziwe dawa ya kuua wadudu wa<br />

magonjwa mbalimbali,<br />

• Kuku wakaguliwe kila siku ili kubaini wagonjwa au wenye matatizo,<br />

kuwatenga na kutoa taarifa kwa mtaalam wa mifugo,<br />

• Kuku wapatiwe chanjo dhidi ya magonjwa mbalimbali,<br />

• Watu wasiohusika wasiingie eneo la kufugia kuku bila utaratibu,<br />

• Ndege na wanyama wengine wasifike eneo la kufugia kuku,<br />

• Banda la kufugia kuku litenganishwe na mabanda ya mifugo mingine,<br />

• Lango la kuingilia katika banda la kuku liwekewe dawa ya kukanyaga kwa<br />

wanaoingia ndani ili kuzuia kuingiza vimelea vya wadudu wa magonjwa; na<br />

• Vifaa vya chakula na maji viwe safi wakati wote.<br />

4.5.1 Dalili za Kuku Mgonjwa<br />

Dalili za ujumla zinazoonekana kwa kuku mgonjwa ni kama zifuatazo:-<br />

• Kuzubaa,<br />

• Kupoteza hamu ya kula,<br />

• Kujitenga na wenzake katika kundi; na<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

52


• Kupunguza au kusimama kutaga.<br />

Mfugaji anapoona mojawapo ya dalili hizo amwone mtaalam wa mifugo<br />

4.6 Ufugaji wa Aina Nyingine za Ndege<br />

Aina ya ndege wengine wanaofugwa hapa nchini ni pamoja na Bata maji, Bata<br />

bukini, Bata mzinga, Kanga na Njiwa. Ndege hao hufugwa kwa kiasi kidogo<br />

ukilinganisha na kuku kwa kuwa soko lao ni dogo. Utunzaji wao hautofautiani sana<br />

na kuku;<br />

• Wajengewe banda la kuishi ambalo ukubwa wake utategemea idadi ya<br />

ndege wanaofugwa,<br />

• Wapatiwe chakula chenye virutubisho na maji ya kunywa ya kutosha,<br />

• Wapatiwe kinga na tiba dhidi ya magonjwa,<br />

• Bata maji na Bata bukini wajengewe bwawa lenye nafasi ya kutosha kwa<br />

ajili ya kuogelea; na<br />

• Njiwa wajengewe viota sehemu ya juu kama kwenye mapaa ya nyumba.<br />

4.7 Utunzaji wa Kumbukumbu<br />

Utunzaji wa kumbukumbu ni muhimu sana katika ufugaji wa kuku na ndege<br />

wengine wafugwao ili kusaidia mfugaji kujua maendeleo ya ufugaji wake.<br />

Utaratibu wa kuweka kumbukumbu mara tukio linapotokea ni lazima ili kuepuka<br />

kusahau. Mfugaji ahakikishe anaweka kumbukumbu ambazo ni sahihi na<br />

zinazoeleweka.<br />

Aina za Kumbukumbu<br />

Kumbukumbu zinazopaswa kuwekwa ni pamoja na:-<br />

• Aina na idadi ya kuku waliopo kwenye kila kundi (mfano vifaranga, wanaokua,<br />

wanaotaga, majogoo),<br />

• Uzalishaji wa mayai kwa kundi la kuku waliopo,<br />

• Utotoaji wa vifaranga,<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

53


• Kinga na matibabu,<br />

• Mapato na matumizi,<br />

• Utagaji wa kila kuku na utunzaji (kwa kuku wa asili); na<br />

• Kumbukumbu za vifo.<br />

UFUGAJI UNAOTUMIA KANUNI BORA ZA UFUGAJI HUONGEZA TIJA NA<br />

KIPATO CHA MFUGAJI<br />

Zingatia kanuni za ufugaji bora ili kujihakikishia usalama wa chakula na<br />

kujiongezea kipato<br />

54

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!