Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />
Wapadri wakashtushwa kwa kufikiri kwamba watu wote wangeweza sasa kuzungumza<br />
pamoja nao Neno la Mungu na kwamba ujinga wao wenyewe ungehatarishwa. Roma ikaalika<br />
mamlaka <strong>ya</strong>ke yote kuzuia mwenezo wa Maandiko. Lakini kwa namna ilivyozidi kukataza<br />
Biblia, ndivyo hamu <strong>ya</strong> watu ikazidi kujua ni nini iliyofundishwa kwa kweli. Wote walioweza<br />
kusoma wakaichukua kwao na hawakuweza kutoshelewa hata walipokwisha kujifunza<br />
sehemu kubwa kwa moyo. Mara moja Luther akaanza utafsiri wa Agano la Kale.<br />
Maandiko <strong>ya</strong> Luther <strong>ya</strong>kapokewa kwa furaha sawasawa katika miji na katika vijiji. “Yale<br />
Luther na rafiki zake waliyoandika, wengine waka<strong>ya</strong>tawan<strong>ya</strong>. Watawa, waliposadikishwa juu<br />
<strong>ya</strong> uharamu wa kanuni za utawa, lakini wajinga sana kwa kutangaza neno la Mungu ...<br />
wakauzisha vitabu v<strong>ya</strong> Luther na rafiki zake. Ujeremani kwa upesi ukajaa na wauzishaji wa<br />
vitabu wajasiri.”<br />
Kujifunza Biblia Mahali Pote<br />
Usiku waalimu wa vyuo v<strong>ya</strong> vijiji wakasoma kwa sauti kubwa kwa makundi madogo<br />
<strong>ya</strong>liyokusanyika kando <strong>ya</strong> moto. Kwa juhudi yote roho zingine zikahakikishwa kwa ukweli.<br />
“Kuingia kwa maneno <strong>ya</strong>ko kunaleta nuru; kunamupa mujinga ufahamu.” Zaburi 119:130.<br />
Wakatoliki walioachia mapadri na watawa kujifunza Maandiko sasa wakawaalika kwa<br />
kuonyesha uwongo wa mafundisho map<strong>ya</strong>. Lakini, wajinga kwa Maandiko, mapadri na<br />
watawa wakashindwa kabisa. “Kwa huzuni,” akasema mwandishi mmoja mkatoliki, “Luther<br />
alishawishi wafuasi wake kwamba haikufaa kuamini maneno mengine isipokuwa Maandiko<br />
matakatifu.” Makundi <strong>ya</strong>kakusanyika kusikia mambo <strong>ya</strong> kweli <strong>ya</strong>liyotetewa na watu wa elimu<br />
ndogo. Ujinga wa hawa watu wakuu ukafunuliwa kwa kuonyesha uongo wa mabishano <strong>ya</strong>o<br />
kwa msaada wa mafundisho rahisi <strong>ya</strong> Neno la Mungu. Watumikaji, waaskari, wanawake, na<br />
hata watoto, wakajua Biblia kuliko mapadri na waalimu wenye elimu.<br />
Vijana wengi wakajitoa kwa kujifunza, kuchunguza Maandiko na kujizoeza wenyewe na<br />
kazi bora <strong>ya</strong> watu wa zamani. Walipokuwa na akili yenye juhudi na mioyo hodari, vijana<br />
hawa wakapata haraka maarifa ambayo kwa wakati mrefu hakuna mtu aliweza kushindana<br />
nao. Watu wakapata katika mafundisho map<strong>ya</strong> mambo ambayo <strong>ya</strong>lileta matakwa <strong>ya</strong> roho zao,<br />
na wakageuka kutoka kwa wale waliowalea kwa wakati mrefu na maganda <strong>ya</strong> bure <strong>ya</strong> ibada<br />
za sanamu na maagizo <strong>ya</strong> wanadamu.<br />
Wakati mateso <strong>ya</strong>lipoamshwa juu <strong>ya</strong> waalimu wa ukweli, wakafuata agizo hili la Kristo:<br />
“Na wakati wanapo watesa ninyi katika mji huu, kimbilieni kwa mji mwengine.” Matayo<br />
10:23. Wakimbizi wakapata mahali mlango karibu ulifunguka kwao, na waliweza kuhubiri<br />
Kristo, wakati mwengine ndani <strong>ya</strong> kanisa ao katika nyumba <strong>ya</strong> faragha ao mahali pa wazi.<br />
Kweli ikatawanyika kwa uwezo mkubwa usio wa kuzuia.<br />
Ni kwa bure watawala wa kanisa na wa serkali walitumia kifungo, mateso, moto, na<br />
upanga. Maelfu <strong>ya</strong> waaminifu wakatia muhuri kwa imani <strong>ya</strong>o kwa kutumia damu <strong>ya</strong>o, na<br />
75