Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />
Waalimu hawa wa bidii wakajifan<strong>ya</strong> wenye kutawaliwa na maono, kuona kuwa kila<br />
mawazo na mvuto kama sauti <strong>ya</strong> Mungu. Wengine hata wakachoma Biblia zao. Mafundisho<br />
<strong>ya</strong> Munzer <strong>ya</strong>kakubaliwa na maelfu. Kwa upesi akatangaza kwamba kutii watawala, ilikuwa<br />
kutaka kumtumikia Mungu na Beliali. Mafundisho <strong>ya</strong> uasi <strong>ya</strong> Munzer <strong>ya</strong>kaongoza watu<br />
kuvunja mamlaka yote. Sherehe za kutisha za upinzani zikafuata, na mashamba <strong>ya</strong> Ujeremani<br />
<strong>ya</strong>kajaa na damu.<br />
Maumivu Makuu <strong>ya</strong> Roho Sasa Yakalemea Juu <strong>ya</strong> Luther<br />
Wana wa wafalme wa upande wa Papa wakatangaza kwamba uasi ulikuwa tunda <strong>ya</strong><br />
mafundisho <strong>ya</strong> Luther. Mzigo huu hakupashwa lakini kuleta huzuni kubwa kwa Mtengenezaji<br />
kwamba kisa cha kweli kilipaswa kuaibishwa kwa kuhesabiwa pamoja na ushupavu wa dini<br />
wa chini zaidi. Kwa upande mwengine, waongozi katika uasi walimchukia Luther. Hakukana<br />
madai <strong>ya</strong>o kwa maongozi <strong>ya</strong> Mungu tu, bali akawatangaza kuwa waasi juu <strong>ya</strong> mamlaka <strong>ya</strong><br />
serkali. Katika uhusiano wakamshitaki yeye kuwa mdai wa msingi.<br />
Roma ilitumainia kushuhudia muanguko wa Matengenezo. Na wakamlaumu Luther hata<br />
kwa ajili <strong>ya</strong> makosa ambayo alijaribu kwa bidii sana kusahihisha. Kundi la ushupavu, likadai<br />
kwa uongo kwamba lilitendewa <strong>ya</strong>siyo haki, wakapata huruma <strong>ya</strong> hesabu kubwa <strong>ya</strong> watu na<br />
kuzaniwa kuwa kama wafia dini. Kwa hiyo wale waliokuwa katika kupingana na<br />
Matengenezo wakahurumiwa na kusafishwa. Hii ilikuwa kazi <strong>ya</strong> roho <strong>ya</strong> namna moja <strong>ya</strong> uasi<br />
wa kwanza uliopatikana mbinguni.<br />
Shetani hutafuta kila mara kudangan<strong>ya</strong> watu na kuwaongoza kuita zambi kuwa haki na<br />
haki kuwa zambi. Utakatifu wa uongo, utakaso wa kuiga, ungali ukionyesha roho <strong>ya</strong> namna<br />
moja kama katika siku za Luther, kugeuza mafikara kutoka kwa Maandiko na kuongoza watu<br />
kufuata mawazo na maono kuliko sheria za Mungu. Kwa uhodari Luther akatetea injili kwa<br />
mashambulio. Pamoja na Neno la Mungu akapigana juu <strong>ya</strong> mamlaka <strong>ya</strong> man<strong>ya</strong>nganyi <strong>ya</strong><br />
Papa, wakati aliposimama imara kama mwamba kupinga ushupavu uliojaribu kujiunga na<br />
Matengenezo.<br />
Pande zote za upinzanihuweka pembeni Maandiko matakatifu, kwa faida <strong>ya</strong> hekima <strong>ya</strong><br />
kibinadamu kutukuzwa kawa chemchemi ama asili <strong>ya</strong> ukweli. Kufuata akili za kibinadamu<br />
kwa kusudi lakuabudu kama Mungu na kufan<strong>ya</strong> hii kanuni kwa ajili <strong>ya</strong> dini. Kiroma kinadai<br />
kuwa na uongozi wa Mungu ulioshuka kwa mustari usiovunjika toka kwa mitume na kutoa<br />
nafasi kwa ujinga na uchafu vifichwe chini <strong>ya</strong> agizo la “mitume”. Maongozi <strong>ya</strong>liyodaiwa na<br />
Munzer <strong>ya</strong>litoka kwa mapinduzi <strong>ya</strong> mawazo. Ukristo wa kweli hukubali Neno la Mungu kama<br />
jaribio la maongozi yote.<br />
Kwa kurudi kwake Wartburg, Luther akatimiza kutafsiri Agano Jip<strong>ya</strong>, na injili ikatolewa<br />
upesi kwa watu wa Ujeremani katika lugha <strong>ya</strong>o wenyewe. Ufasiri huu ukapokewa kwa furaha<br />
kubwa kwa wote waliopenda ukweli.<br />
74