You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />
heshima, na kupokelewa mbele <strong>ya</strong> mkutano wa heshima sana katika ulimwengu. ... Roma<br />
ilikuwa ikishuka kutoka kitini chake, nailikuwa ni sauti la mtawa lililomushusha.”<br />
Mzaliwa mnyenyekevu Mtengenezaji akaonekanamwenye kutishwa na kufazaika.<br />
Wafalme wengi, wakamkaribia, na mmoja akamnongoneza “Musiwaogope wanaoua mwili<br />
lakini hawawezi kuua nafsi.” Mwengine akasema: “Na mutakapopelekwa mbele <strong>ya</strong> watawala<br />
na wafalme kwa ajili <strong>ya</strong>ngu, mtapewa kwa njia <strong>ya</strong> roho wa baba yenu lile mtakalo lisema.”<br />
Tazama Matayo 10:28, 18, 19.<br />
Ukim<strong>ya</strong> mwingi ukawa juu <strong>ya</strong> mkutano uliosongana. Ndipo afisa mmoja wa mfalme<br />
akasimama na, kushota kwa maandiko <strong>ya</strong> Luther, akauliza kwamba Mtengenezaji ajibu<br />
maswali mawili-ao ata<strong>ya</strong>kubali kwamba ni <strong>ya</strong>ke, na ao atakusudia kukana mashauri<br />
<strong>ya</strong>nayoandikwa humo. Vichwa v<strong>ya</strong> vitabu vilipokwisha kusomwa, Luther, kwa swali la<br />
kwanza, akakubali vitabu kuwa v<strong>ya</strong>ke. “Kwa swali la pili,” akasema, ningetenda bila busara<br />
kama ningejibu bila kufikiri. Ningehakikisha kidogo kuliko hali <strong>ya</strong> mambo inavyotaka, ao<br />
zaidi kuliko kweli inavyotaka. Kwa sababu hiyo ninaomba mfalme mtukufu, kwa<br />
unyenyekevu wote, unitolee wakati, ili nipate kujibu bila kukosa juu <strong>ya</strong> neno la Mungu.”<br />
Luther akasadikisha makutano kwamba hakutenda kwa hasira ao bila kufikiri. Utulivu<br />
huu, na kujitawala, isiyotazamiwa kwa mtu aliyejionyesha kuwa mgumu na asiyebadili shauri<br />
<strong>ya</strong>kamwezesha baadaye kujibu kwa busara na heshima ikashangaza maadui zake na kukemea<br />
kiburi chao.<br />
Kesho <strong>ya</strong>ke alipashwa kutoa jibu lake la mwisho. Kwa mda moyo wake ukadidimia.<br />
Maadui zake walionekana kwamba wangeshinda. Mawingu <strong>ya</strong>kakusanyika kando <strong>ya</strong>ke na<br />
<strong>ya</strong>kaonekana kumtenga na Mungu. Katika maumivu <strong>ya</strong> roho akatoa malalamiko <strong>ya</strong>le <strong>ya</strong><br />
kuhuzunisha sana, ambayo Mungu tu anaweza ku<strong>ya</strong>fahamu kabisa.<br />
“Ee Mwenyezi Mungu wa milele!” akapaza sauti; “kama ni kwa nguvu za ulimwengu huu<br />
tu ambapo napashwa kutia tumaini langu, yote imekwisha. ... Saa <strong>ya</strong>ngu <strong>ya</strong> mwisho imefika,<br />
hukumu <strong>ya</strong>ngu imekwisha kutangazwa. ... Ee Mungu, unisaidie juu <strong>ya</strong> hekima yote <strong>ya</strong><br />
ulimwengu. ... Mwanzo ni wako, ... na ni mwanzo wa haki na wa milele. Ee Bwana, unisaidie!<br />
Mungu mwaminifu na asiyebadilika, mimi si mtumainie mtu ye yote. ... Umenichagua kwa<br />
kazi hii. ... Simama kwa upande wangu, kwa ajili <strong>ya</strong> jina la mpendwa wako Yesu Kristo,<br />
anayekuwa mkingaji wangu, ngao <strong>ya</strong>ngu, na mnara wangu wa nguvu.”<br />
Lakini haikuwa hofu <strong>ya</strong> mateso, maumivu, wala mauti <strong>ya</strong>ke mwenyewe ambayo ilimlemea<br />
na hofu kuu. Alijisika upungufu wake. Katika uzaifu wake madai <strong>ya</strong> ukweli <strong>ya</strong>ngeweza kupata<br />
hasara. Si kwa usalama wake mwenyewe, bali kwa ajili <strong>ya</strong> ushindi wa injili alishindana na<br />
Mungu. Katika ukosefu wa usaada imani <strong>ya</strong>ke ikashikilia juu <strong>ya</strong> Kristo, Mkombozi mkuu.<br />
Hangeonekana pekee <strong>ya</strong>ke mbele <strong>ya</strong> baraza. Amani ikarudi kwa roho <strong>ya</strong>ke, na akafurahi<br />
kwamba aliruhusiwa kuinua Neno la Mungu mbele <strong>ya</strong> watawala wa mataifa.<br />
60